Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Video-ya-Injili. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Video-ya-Injili. Onyesha machapisho yote

Jumatatu, 30 Julai 2018

Video ya Injili 2018 | "Kutoka Kinywani mwa Mauti" | Mungu Amenipa Fursa ya Pili Katika Maisha

Video ya Injili 2018 | "Kutoka Kinywani mwa Mauti" | Mungu Amenipa Fursa ya Pili Katika Maisha

Liu Zhen, mwenye umri wa miaka 78, ni mke wa nyumbani wa kawaida wa mashambani. Baada ya kumwamini Mungu, alihisi furaha isiyo na kisawe na kusoma maneno Yake na kuimba nyimbo za kumsifu siku zote, na mara nyingi kukusanyika pamoja na ndugu zake kushirikiana juu ya ukweli. ... Hata hivyo, mambo mazuri hayadumu. Anakamatwa na kuteswa na serikali ya Kikomunisti ya China, ikimtia katika shida mbaya sana. Polisi wanampeleka kwenye kituo cha polisi kwa ajili ya kuhojiwa mara tatu, na kumwonya asimwamini Mungu tena. Wanamchunguza na kwenda nyumbani kwake ili kumtisha. Chini ya shinikizo la serikali ya Kikomunisti ya China, mumewe, mwanawe, na mkwe wake pia wanapinga na kuzuia imani yake kwa Mungu. Kupitia maumivu haya, anamtegemea na kumtazamia Mungu kwa kweli, na maneno Yake yanampa imani na nguvu, yakimruhusu kusimama imara kati ya mateso na dhiki. Katika kilele cha mateso yake wakati hajiwezi kabisa, anamlilia Mungu kwa dharura. Anasikia sala yake na kumfungulia njia. Jioni moja, ghafla anapoteza fahamu na hawezi kuamshwa. Daktari anasema kuwa hawezi kuokolewa na anaiambia familia yake ijiandae kwa ajili ya kuaga kwake, lakini baada ya masaa 18, kimiujiza anaamka. Muujiza huu wa Mwenyezi Mungu unawashangaza wale walio karibu na yeye na kumfungulia njia mpya. ... Baada ya uzoefu huu, Liu Zhen anakuja kuelewa kwa undani kwamba maisha ya watu hayana uhakika, na hakuna yeyote kati yetu anayeweza kuyadhibiti—ni Mungu pekee ndiye Anayetawala jaala ya watu na ana maisha yetu, mauti, mafanikio, na bahati mbaya mikononi Mwake. Pia anakuja kupata uzoefu kwamba ni Mungu pekee ndiye ambaye Aliyepo kwa ajili yetu, daima Yuko karibu kutusaidia, na ni Yeye tu tunayeweza kumwamini na kumtegemea!
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Video ya Injili