Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Hukumu-ya-Kristo. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Hukumu-ya-Kristo. Onyesha machapisho yote
Jumapili, 2 Septemba 2018
Swahili Christian Movie "Kutamani Sana" (4) - Je, Ufalme wa Mbinguni uko Mbinguni au Ulimwenguni?
Septemba 02, 2018Dondoo-za-Filamu, Hukumu-ya-Kristo, Tafuta-Ufalme-wa-Mungu-Kwanza, VIDEONo comments
Watu wengi walio na imani kwa Bwana wanasadiki kwamba ufalme wa mbinguni uko mbinguni. Je, hivyo ndivyo ilivyo kwa kweli? Sala ya Bwana inasema: "Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe. Ufalme wako uje, Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni" (Mathayo 6:9-10). Kitabu cha Ufunuo kinasema, "Falme za dunia zimekuwa falme za Bwana wetu, na za Kristo wake" (Ufunuo 11:15). "Mji mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka kwa Mungu mbinguni, … maskani ya Mungu yako pamoja na wanadamu" (Ufunuo 21:2-3). Hivyo, ufalme wa mbinguni uko mbinguni au ulimwenguni?
Jumanne, 12 Desemba 2017
Kanisa la Mwenyezi Mungu | Matunda Machungu ya Kiburi
17. Matunda Machungu ya Kiburi | Kanisa la Mwenyezi Mungu
Hu Qing Jijini Suzhou, Mkoani Anhui
Nilipoona maneno ya Mungu yakisema: “Wale miongoni mwenu ambao huhudumu kama viongozi daima hutaka kuwa na ubunifu mkubwa, kuwa wazuri kuliko wengine, kupata hila mpya ili Mungu aweze kuona jinsi kweli mlivyo viongozi wakuu. … Nyinyi daima hutaka kuringa; si huu ni ufunuo kwa usahihi wa asili ya kiburi?” (“Bila Ukweli Ni Rahisi Kumkosea Mungu” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo), Nilifikiri mwenyewe: Nani ana ujasiri kama huo kujaribu kupata ujanja mpya ya ubunifu?