Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Hukumu-na-Kuadibu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Hukumu-na-Kuadibu. Onyesha machapisho yote

Jumanne, 10 Septemba 2019

Tatizo Zito Sana: Usaliti (2)

Tatizo Zito Sana: Usaliti (2)

Mwenyezi Mungu alisema, Asili ya mwanadamu ni tofauti kabisa na kiini Changu; hii ni kwa kuwa asili potovu ya mwanadamu inatokana kabisa na Shetani na asili ya mwanadamu imemilikiwa na kupotoshwa na Shetani. Yaani, mwanadamu anaishi chini ya ushawishi wa uovu na ubaya wake. Mwanadamu hakui katika ulimwengu wa ukweli au mazingira matakatifu, na aidha haishi katika mwanga. Kwa hivyo, haiwezekani ukweli kumilikiwa kiasili katika asili ya kila mtu, na zaidi ya hayo, hawawezi kuzaliwa na kiini cha kumwogopa, kiini cha kumheshimu Mungu. Kinyume na hayo, wana asili inayompinga Mungu, isiyomtii Mungu, na isiyopenda ukweli. Asili hii ndilo tatizo Ninalotaka kuzungumzia—usaliti. Usaliti ni chanzo cha uasi wa kila mtu kwa Mungu. Hili ni tatizo lipatikanalo kwa mwanadamu tu na si Kwangu. Wengine watauliza swali la aina hii: Kwa kuwa wote wanaishi katika ulimwengu wa mwanadamu, ni kwa nini wanadamu wote wana asili inayomsaliti Mungu, lakini Kristo hana? Hili ni swali ambalo lazima lifafanuliwe kwenu waziwazi.
Kuishi kwa mwanadamu kunategemea kupata mwili kwa roho. Kwa maneno mengine, kila mtu anapata maisha ya kibinadamu ya mwili baada ya roho yake kupata mwili. Baada ya mwili wa mtu kuzaliwa, maisha hayo yanaendelea hadi kufikia mipaka ya juu zaidi ya mwili, yaani, wakati wa mwisho ambapo roho inaliacha umbo lake. Mchakato huu unajirudia tena na tena na roho ya mtu ikija na kwenda, ikija na kwenda, hivyo kudumisha maisha ya wanadamu wote. Uhai wa mwili vilevile ni uhai wa roho ya mwanadamu, na roho ya mwanadamu husaidia maisha ya mwili wa mwanadamu. Hiyo ni kusema, uhai wa kila mtu unatoka kwa roho zao; si miili yao ambayo ilikuwa na uhai kwanza. Kwa hivyo, asili ya wanadamu inatoka kwa roho zao; haitoki kwa miili yao. Roho ya kila mtu ndiyo tu inajua jinsi imepitia majaribu, mateso na uovu wa shetani. Mwili wa mwanadamu hauwezi kulifahamu hili. Vivyo hivyo, pasipo kujua mwanadamu anaendelea kuwa mchafu, mwovu na mbaya zaidi na zaidi, ilhali umbali baina Yangu na mwanadamu unaendelea kuongezeka hata zaidi, na siku za mwanadamu zinaendelea kuwa za giza hata zaidi. Roho za wanadamu zote ziko karibu na mikono ya Shetani. Kwa hivyo, ni dhahiri kuwa mwili wa mwanadamu pia umemilikiwa na Shetani. Ingekuwaje miili kama hii na wanadamu kama hawa wasimuasi Mungu na kupatana naye kiasili? Nilimtupa chini Shetani kwa sababu alinisaliti, basi wanadamu wangejinasua vipi kutoka katika hili? Hii ndiyo sababu asili ya mwanadamu ni usaliti. Ninaamini kuwa punde tu mnapoelewa hii mantiki vilevile mnapaswa kuwa na imani katika kiini cha Kristo! Mwili uliovaliwa na Roho wa Mungu ni mwili wa Mungu mwenyewe. Roho wa Mungu ni mkubwa, Yeye ni mwenyezi, mtakatifu, na mwenye haki—na vilevile ndivyo ambavyo mwili Wake ulivyo pia mkubwa, wenye uwezo, mtakatifu, na wenye haki. Mwili kama huo unaweza kufanya tu kile ambacho ni chenye haki na manufaa kwa mwanadamu, kile ambacho ni kitakatifu, chenye utukufu, na uweza, na hakiwezi kukifanya chochote ambacho kinakiuka ukweli au uadilifu na haki, isitoshe hata kile ambacho kinaasi dhidi ya Roho wa Mungu. Roho wa Mungu ni mtakatifu, na hivyo basi mwili Wake hauwezi kuharibiwa na Shetani; mwili Wake una kiini tofauti na ule mwili wa mwanadamu. Kwani ni mwanadamu, wala si Mungu, ambaye anaharibiwa na Shetani, na mwili wa Mungu usingeweza kuharibiwa na Shetani. Kwa hivyo, licha ya ukweli kwamba mwanadamu na Kristo wanakaa mahala pamoja, ni mwanadamu tu ndiye ambaye anatawaliwa, anatumiwa, na kutegwa na Shetani. Kinyume cha hayo, Kristo daima hapenyezwi na uovu wa Shetani, kwa kuwa Shetani hataweza kamwe kupaa hadi mahala pa aliye juu zaidi, na hataweza kumkaribia Mungu. Leo, nyote mnapaswa kuelewa kuwa ni mwanadamu tu, aliyepotoshwa na Shetani, ambaye ananisaliti, na kwamba daima tatizo hili halitakuwa linamhusu Kristo.
Roho zote ambazo zimepotoshwa na Shetani ziko chini ya udhibiti wa miliki ya Shetani. Ni wale tu wanaomwamini Kristo ndio waliotengwa kando, wakiokolewa kutoka katika kambi ya Shetani, na kuletwa katika ufalme wa leo. Watu hawa kamwe hawaishi chini ya ushawishi wa Shetani. Hata hivyo, asili ya mwanadamu bado imekita mizizi katika mwili wa mwanadamu. Hiyo ni kusema kwamba ijapokuwa roho zenu zimeokolewa, asili yenu bado ni ya mwonekano wake wa zamani na uwezekano kuwa mtanisaliti unabakia asilimia mia moja. Ndiyo maana kazi Yangu ni ya kudumu muda mrefu sana, kwa kuwa asili yenu ni isiyotikiswa kabisa. Sasa hivi nyote mnateseka jinsi mnavyoweza katika kutimiza wajibu wenu, lakini ukweli usiopingika ni huu: Kila mmoja wenu ana uwezo wa kunisaliti Mimi na kuirudia miliki ya Shetani, katika kambi yake, na kuyarudia maisha yenu ya zamani. Wakati huo haitawezekana kwenu kuwa hata na chembe ya utu au mwonekano wa binadamu kama mlionao sasa. Katika hali nzito, mtateketezwa, na zaidi mtalaaniwa milele, msipate mwili tena lakini muadhibiwe vikali. Hili ni tatizo lililowekwa mbele yenu. Ninawakumbusha kwa njia hii ili kwamba kwanza, kazi Yangu isiwe ya bure, na pili, nyote muweze kuishi katika siku za mwangaza. Kwa hakika, iwapo kazi Yangu ni bure si suala la umuhimu sana. Muhimu ni nyinyi muweze kuwa na maisha ya furaha na mustakabali mwema. Kazi Yangu ni kazi ya kuziokoa roho za watu. Roho yako ikiingia mikononi mwa Shetani, basi mwili wako hautakuwa na siku tulivu. Kama Ninaulinda mwili wako, basi roho yako kwa hakika itakuwa chini ya ulinzi Wangu. Ikiwa Ninakuchukia kwa kweli, basi mwili wako na roho yako vitaingia mara moja mikononi mwa Shetani. Unaweza kufikiri hali yako itakuwaje wakati huo? Kama siku moja maneno Yangu hatashindwa kuwashawishi, basi Nitawakabidhi nyote kwa Shetani awatese maradufu hadi wakati hasira Yangu imeyeyuka kabisa, ama Nitawaadhibu binafsi nyie binadamu msiokomboleka, kwa kuwa mioyo yenu ya kunisaliti haijawahi kubadilika.
Nyote sasa mnapaswa kujichunguza haraka iwezekanavyo kuona kwamba ni kiasi gani cha tabia zenu bado zinanisaliti Mimi. Ninasubiri kwa hamu jibu lenu. Msinipuuze mbali. Sifanyi mchezo kamwe na watu. Nikisema jambo basi bila shaka Nitalitenda. Natumaini nyinyi nyote mnaweza kuwa watu wa kuyachukulia kwa uzito maneno Yangu na msifikiri kwamba ni maneno ya riwaya za sayansi ya kubuni tu. Ninachokitaka ni matendo thabiti kutoka kwenu, si fikira zenu. Halafu, ni lazima mjibu maswali kama haya kutoka Kwangu: 1. Ikiwa kweli wewe ni mtendaji huduma, basi waweza kunitolea huduma kwa uaminifu, bila vitu vyovyote vizembe au hasi? 2. Ukigundua kuwa Sijawahi kukuthamini, je, bado utaweza kubaki na kunitolea huduma milele? 3. Kama ulitumia juhudi nyingi lakini bado Sikuchangamkii, je, utaweza kuendelea kunifanyia kazi katika uvunguvungu? 4. Ikiwa, baada ya wewe kutumia vitu fulani kwa ajili Yangu, Sijatimiza mahitaji yako madogomadogo, je, utavunjika moyo na kusikitishwa na Mimi au hata kuwa na ghadhabu na kunitusi? 5. Ikiwa daima umekuwa mwaminifu sana Kwangu na kunipenda, lakini unapitia mateso ya maradhi, umaskini wa maisha, na kutelekezwa na marafiki na jamaa au kupitia maafa mengine yoyote maishani, basi, uaminifu na mapenzi yako Kwangu yataendelea kuwepo? 6. Ikiwa hakuna lolote la lile unalofikiria moyoni mwako linalooana na Niliyotenda, basi utaitembeaje njia yako ya siku za usoni? 7. Ikiwa hupokei chochote ulichotarajia kupokea, je, waweza kuendelea kuwa mfuasi Wangu? 8. Kama hujawahi kuelewa kusudi na umuhimu wa kazi Yangu, basi waweza kuwa mtu mtiifu ambaye hatoi hukumu na hitimisho kiholela? 9. Unaweza kuyathamini maneno yote Niliyoyasema na kazi yote Niliyoifanya Nikiwa pamoja na wanadamu? 10. Unaweza kuwa mfuasi Wangu mwaminifu, kuwa radhi kuteseka kwa ajili Yangu hata kama hutapokea kitu chochote? 11. Unaweza kukosa kujali, kupanga, au kutayarisha kwa ajili ya njia yako ya usoni ya kuendelea kuishi kwako kwa ajili Yangu? Maswali haya ni mahitaji Yangu ya mwisho kwenu, na Natumaini nyote mnaweza kunijibu. Ukitimiza kitu kimoja au viwili kutoka kwa haya maswali, basi bado unahitaji kuendelea kutia bidii. Ikiwa huwezi kutimiza hata hitaji moja katika haya, basi wewe kwa kweli ni aina ya watu watakaotupwa kuzimu. Sina haja ya kusema zaidi kwa hao watu. Hii kwa hakika ni kwa sababu si watu ambao wanaweza kulingana nami. Ningewezaje kumweka mtu nyumbani Kwangu ambaye anaweza kunisaliti katika hali yoyote? Na kwa wale wanaoweza kunisaliti bado katika hali yoyote, Nitauchunguza utendaji wao kabla ya kufanya mipango mingine. Hata hivyo, alimradi ni watu wanaoweza kunisaliti Mimi, haijalishi ni katika hali gani, kamwe Sitaweza kusahau na Nitawakumbuka moyoni Mwangu huku Nikisubiri fursa ya kulipiza matendo yao maovu. Mahitaji Niliyoyaleta yote ni masuala ambayo kwayo mnapaswa kujikagua wenyewe. Natumaini nyote mnaweza kuyazingatia kwa uzito na kwamba hamshughuliki na Mimi kiuzembe. Hivi karibuni, Nitayachunguza majibu mliyonipa dhidi ya mahitaji Yangu. Kabla ya wakati huo, Sitahitaji kitu kingine zaidi kutoka kwenu na Sitawapatia onyo zaidi la dhati. Badala yake, Nitatekeleza mamlaka Yangu. Wale ambao wanapaswa kubakizwa watabakizwa, wale ambao wanapaswa kutuzwa watatuzwa, wale wanaopaswa kukabidhiwa kwa Shetani watakabidhiwa kwa Shetani, wale wanaopaswa kupokea adhabu kali watapokea adhabu kali, na wale ambao wanapaswa kuangamia watateketezwa. Kwa njia hiyo, kamwe hakutakuwepo na yeyote wa kunisumbua katika siku Zangu. Je, unayaamini maneno Yangu? Je, unaamini katika adhabu? Je, unaamini kwamba Nitawaadhibu wale waovu wote wanaonidanganya na kunisaliti? Je, ungependa siku hiyo ije mapema au ije baadaye? Je, wewe ni mtu anayeogopa sana adhabu, au mtu ambaye ni heri aniasi hata kama ataipitia adhabu? Siku hiyo ifikapo, unaweza kufikiria ikiwa utakuwa ukiishi katikati ya shangwe na vicheko, au katika kulia na kusaga meno yako? Ni hatima ya aina gani unatarajia utakuwa nayo? Je, umewahi kutafakari kwa uzito ikiwa unaniamini asilimia mia moja au una mashaka nami asilimia mia moja? Je, umewahi kutafakari kwa makini kuhusu matendo na mienendo yako itakuletea matokeo na hatima ya aina gani? Je, kweli unatumaini kuwa maneno Yangu yote yatatimizwa moja baada ya lingine, au una hofu sana kwamba maneno Yangu yatatimizwa moja baada ya lingine? Ikiwa unatumaini kwamba Ning’oe nanga mapema ili Nitimize maneno Yangu, basi unapaswa kuchukuliaje maneno na matendo yako mwenyewe? Ikiwa hutumainii kung’oa nanga Kwangu na hutumainii maneno Yangu yote yatimizwe mara moja, basi ni kwa nini hata unaniamini? Je, kweli unajua ni kwa nini unanifuata? Ikiwa ni kwa ajili ya kupanua mawanda yako tu, basi haina haja uyapitie malalamiko kama hayo. Ikiwa ni ili kwamba ubarikiwe na ukwepe maafa ya siku za usoni, basi ni kwa nini hujali mwenendo wako mwenyewe? Ni kwa nini hujiulizi mwenyewe kama unaweza kuyaridhisha mahitaji Yangu? Ni kwa nini pia hujiulizi mwenyewe kama unastahili kupokea baraka Zangu za siku za usoni?
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Jumatatu, 3 Juni 2019

Neno la Mungu | “Mwanadamu Mpotovu Hawezi Kumwakilisha Mungu”

Neno la Mungu | “Mwanadamu Mpotovu Hawezi Kumwakilisha Mungu”

Mwenyezi Mungu anasema, “Vitendo vyote na matendo ya Shetani vinaonyeshwa kupitia kwa binadamu. Sasa vitendo vyote na matendo yote ya binadamu ni maonyesho ya Shetani na hivyo basi haviwezi kumwakilisha Mungu. Binadamu ni mfano halisi wa Shetani, na tabia ya mwanadamu haiwezi kuiwakilisha tabia ya Mungu. Baadhi ya wanadamu ni wenye tabia nzuri; Mungu anaweza kufanya baadhi ya kazi kupitia kwa tabia hiyo nayo kazi yao inatawaliwa na Roho Mtakatifu. Ilhali tabia yao haiwezi kumwakilisha Mungu. Kazi ambayo Mungu hufanya ndani yao ni kule tu kufanya kazi na pamoja na kupanua kile ambacho tayari kimo ndani yao. Wawe ni manabii au binadamu wanaotumiwa na Mungu kutoka kwa enzi zilizopita, hakuna yeyote anayeweza kumwakilisha Mungu moja kwa moja.” “Kwani kiini cha binadamu ni tofauti na kile cha Mungu. Binadamu hawezi kamwe kuishi kwa kumdhihirisha Mungu, sembuse kuwa Mungu. Kile ambacho Roho Mtakatifu anamwelekeza binadamu kuishi kwa kudhihirisha ni kulingana tu na kile ambacho Mungu anahitaji kutoka kwa binadamu.”
Binadamu amekuwa akiishi katika funiko la ushawishi wa giza, huku akiwa amezuiliwa bila ya kuachiliwa na ushawishi wa Shetani. Nayo tabia ya binadamu, baada ya kutengenezwa na Shetani, inaendelea kuongezeka kuwa potovu. Mtu anaweza kusema kwamba binadamu huishi daima na tabia yake potovu ya kishetani, asiweze kumpenda Mungu kwa kweli. Kwa sababu ya hili, kama binadamu anataka kumpenda Mungu, lazima anyang'anywe kujidai kwake, kujigamba, kiburi, majivuno, na sifa nyingine kama hizo zinazomilikiwa na tabia ya Shetani. Vinginevyo, upendo wa binadamu ni upendo usio safi, ni upendo wa Shetani, na ule ambao hauwezi kabisa kupokea idhini ya Mungu. Kama binadamu hakamilishwi, kushughulikiwa, kuvunjwa, kupogolewa, kufundishwa nidhamu, kuadibiwa, au kusafishwa na Roho Mtakatifu moja kwa moja, hakuna yeyote anayeweza kumpenda Mungu kwa kweli. Ukisema kwamba sehemu ya tabia yako inamwakilisha Mungu na hivyo basi unaweza kumpenda Mungu kwa kweli, basi wewe ndiwe unayezungumza maneno ya kiburi na ni binadamu wa upuuzi. Binadamu kama hao ni malaika mkuu! Asili ya ndani ya binadamu haiwezi kumwakilisha Mungu kwa njia ya moja kwa moja. Lazima binadamu aiondoe asili yake ya ndani kupitia kwa ukamilifu wa Mungu, na kisha kupitia kutunza na kutosheleza mapenzi ya Mungu tu, na hata zaidi kupitia kwa kazi ya Roho Mtakatifu, ndipo kuishi kwa kudhihirishwa kwake kunaweza kuidhinishwa na Mungu. Hakuna anayeishi katika mwili anayeweza kumwakilisha Mungu kwa njia ya moja kwa moja isipokuwa kama yeye ni binadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu. Hata hivyo, hata kama huyu, tabia yake na kile anachoishi kwa kudhihirisha chote hakiwezi kuchukuliwa kwamba kinamwakilisha Mungu kabisa; inaweza kusemekana tu kwamba kile anachoishi kwa kudhihirishwa kinatawaliwa na Roho Mtakatifu. Tabia ya mtu kama huyo haiwezi kumwakilisha Mungu.
Ingawa tabia ya binadamu inaamrishwa na Mungu—hili halina shaka na linaweza kuchukuliwa kama jambo zuri—limetengenezwa na Shetani. Hiyo ndiyo maana tabia zote za binadamu kwa kweli ni tabia ya Shetani. Mtu anaweza kusema kuwa Mungu, katika tabia yake, ni mnyofu katika kutekeleza mambo, na kwamba yeye pia anatenda kwa njia hii; yeye pia an tabia kama hii, na hivyo basi anasema kwamba tabia yake inamwakilisha Mungu. Huyu ni binadamu wa aina gani? Je, tabia potovu ya kishetani inaweza kumwakilisha Mungu? Yeyote yule anayetangaza kwamba tabia yake ni wakilishi kwa Mungu, huyo mtu anamkufuru Mungu na kumtukana Roho Mtakatifu! Tukiangalia namna ambavyo Roho Mtakatifu hufanya kazi, kazi ambayo Mungu anafanya hapa ulimwenguni ni kwa ajili ya kushinda pekee. Hii ndiyo maana, nyingi ya tabia potovu za kishetani za binadamu bado hazijatakaswa, na ndiyo maana mienendo ya maisha ya binadamu bado ni taswira ya Shetani. Ndicho binadamu huamini kuwa chema a na kinawakilisha vitendo vya mwili wa binadamu au kwa usahihi zaidi, kinawakilisha Shetani na hakiwezi kumwakilisha Mungu kabisa. Hata kama binadamu tayari anampenda Mungu hadi kufikia kiwango ambacho anaweza kufurahia maisha ya mbinguni hapa ulimwenguni, anaweza kutamka kauli kama vile: “Eh Mungu! Siwezi kukupenda vya kutosha,” na kwamba amefikia eneo la juu zaidi, huwezi kusema kwamba anaishi kwa kumdhihirisha Mungu au kumwakilisha Mungu, kwani kiini cha binadamu ni tofauti na kile cha Mungu. Binadamu hawezi kamwe kuishi kwa kumdhihirisha Mungu, sembuse kuwa Mungu. Kile ambacho Roho Mtakatifu anamwelekeza binadamu kuishi kwa kudhihirisha ni kulingana tu na kile ambacho Mungu anahitaji kutoka kwa binadamu.

Jumanne, 23 Aprili 2019

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II Tabia ya Haki ya Mungu” Sehemu ya Kwanza

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II Tabia ya Haki ya Mungu” Sehemu ya Kwanza

Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”.
Maudhui ya video hii:
Kwa Kupinga Mungu kwa Ukaidi, Binadamu Anaangamizwa na Hasira za Mungu
Kupotoka kwa Sodoma: Kunakasirisha Binadamu, Kunaghadhibisha Mungu Sodoma Yaangamizwa kwa Kukosea Hasira za Mungu
Baada ya Ukinzani wa Mara kwa Mara wa Sodoma na Ukatili Wao Dhidi Yake, Mungu Anaufuta Kabisa
Mwenyezi Mungu alisema, Kupotoka kwa Sodoma: Kunakasirisha Binadamu, Kunaghadhibisha Mungu
Kwenye usiku huo, Lutu alipokea wajumbe wawili kutoka kwa Mungu na akawatayarishia karamu. Baada ya chajio, kabla hawajalala, watu kutoka kila pahali kwenye mji walizunguka makazi ya Lutu na kumwita nje Lutu. Maandiko yanawarekodi wakisema, “Wako wapi wale wanaume waliokuja kwako leo usiku? Walete kwetu, ili tupate kuwajua.” Ni nani aliyesema maneno haya? Alikuwa akiwaambia kina nani? Haya yalikuwa maneno ya watu wa Sodoma, walipiga mayowe nje ya makazi ya Lutu wakinuia kumwita Lutu. Je, unahisi vipi ukiyasikia maneno haya? Unaghadhibishwa? Je, maneno haya yanakuhuzunisha? Je, unabubujikwa na hasira kali? Je, Huoni kwamba maneno haya yananuka Shetani? Kupitia kwa maneno haya, unaweza kuhisi uovu na giza vilivyomo kwenye mji huu? Je, unaweza kuhisi ukatili na ushamba wa tabia za watu hawa kupitia kwa maneno yao? Je, unaweza kuhisi kina cha kupotoka kwao kupitia kwa tabia yao? Kupitia kwa maudhui ya hotuba yao, si vigumu kuona kwamba asili yao ya dhambi na tabia yao iliyopotoka ilikuwa imefikia kiwango kilichokuwa zaidi ya wao kuidhibiti. Isipokuwa Lutu, kila mtu katika mji huu hakuwa tofauti na Shetani; ule mtazamo tu wa mtu mwingine uliwafanya watu hawa kutaka kudhuru na kuwapotosha wao…. Mambo haya hayampatii tu mtu hisia ya asili potovu na ya kutisha ya mji huu, lakini pia yanamwonyesha harufu ya kifo iliyouzunguka mji huu; yanampa pia mtu hisia za dhambi na umwagikaji wa damu.
Alipojipata uso kwa uso na genge la majambazi waliojaa ukatili, watu waliokuwa wamejaa na maono ya kupotosha nafsi, Lutu aliitikia vipi? Kulingana na Maandiko: “Nawaomba … msitende maovu hivyo. Tazameni sasa, ninao mabinti wawili ambao ni mabikira; mniruhusu, nawaomba, niwalete nje kwenu, na mwafanyie mwonavyo kuwa vizuri katika macho yenu: ila kwa hawa wanaume msifanye chochote: kwani wamekuja chini ya kivuli cha paa langu.” Lutu alimaanisha yafuatayo katika maneno yake: Alikuwa radhi kuwatoa binti zake wawili ili kuwalinda wale wajumbe. Kutokana na akili razini, watu hawa wangekubali masharti ya Lutu na kuwaacha wale wajumbe wawili pekee; kwani hata hivyo, wajumbe hao walikuwa watu wageni kabisa kwao, watu ambao hawakuwa na chochote katu kuhusiana na wao; wajumbe hawa wawili walikuwa hawajawahi kudhuru masilahi yao. Hata hivyo, wakiwa na motisha ya asili yao ya dhambi, hawakuliwachia suala hili hapo. Badala yake, walizidisha tu jitihada zao. Hapa mojawapo ya mabishano yao yanaweza bila shaka kumpatia mtu maono zaidi kuhusu asili ya kweli na potovu ya watu hawa; wakati uo huo yanatujuza na kutufanya tuelewe sababu ya Mungu kutaka kuuangamiza mji huu.
Kwa hivyo walisema nini baadaye? Kama vile Biblia inavyosoma: “Toka. Na wakasema tena, Mtu huyu mmoja aliingia kwetu kukaa kwa muda, naye anatamani kuhukumu: sasa tutakushughulikia kwa njia mbaya zaidi, kuliko wao. Na wakamshinikiza sana mtu huyo, hadi Lutu, na wakawa karibu kuuvunja mlango.” Kwa nini walitaka kuuvunja mlango? Sababu ni kwamba walikuwa na hamu kubwa zaidi ya kuwadhuru wale wajumbe wawili. Wale wajumbe walikuwa wakifanya nini Sodoma? Kusudio lao la kuja hapo lilikuwa ni kumwokoa Lutu na familia yake; hata hivyo, watu wa mji huo walifikiri kimakosa kwamba walikuwa wamekuja kuchukua nyadhifa zao rasmi. Bila ya kuulizia kusudio lao, ilikuwa tu hali ya kujiamulia kufanya mambo kabla ya kujua ukweli wake, iliyoufanya mji huo kutaka kuwadhuru vibaya wajumbe hawa wawili; walitaka kuwadhuru watu wawili ambao hawakuhusiana kwa vyovyote vile na wao. Ni wazi kwamba watu wa mji huu walikuwa wamepoteza kabisa ubinadamu na akili zao razini. Kiwango cha wendawazimu wao na kukosa ustaarabu kwao kilikuwa tayari si tofauti na asili potovu ya Shetani ya kudhuru na kudanganya binadamu.
Walipowaamuru watu hawa watoke kwa Lutu, Lutu alifanya nini? Kutoka kwenye maandishi yanayofuata tunajua kwamba Lutu hakuwakabidhi wajumbe hawa kwa watu hawa. Je, Lutu aliwajua wajumbe hawa wawili wa Mungu? Bila shaka la! Lakini kwa nini aliweza kuwaokoa watu hawa wawili? Je, alijua ni nini walichokuwa wamekuja kufanya? Ingawaje hakujua kuhusu sababu yao ya kuja, alijua kwamba walikuwa ni watumishi wa Mungu, na kwa hivyo aliwapokea. Kwamba aliweza kuwaita watumishi hawa wa Mungu mabwana yaonyesha kwamba Lutu kwa kawaida alikuwa ni mfuasi wa Mungu, tofauti na wale wengine waliokuwa ndani ya Sodoma. Kwa hivyo, wakati wajumbe wa Mungu walipomjia, alihatarisha maisha yake binafsi ili kuwapokea watumishi hao wawili; aidha, aliwakabidhi binti zake wawili badala ya watumishi hao wawili ili kuwalinda watumishi hao. Hiki ndicho kitendo cha haki ya Lutu; vilevile ni onyesho linaloonekana waziwazi kuhusu asili na hali halisi ya Lutu, na ndiyo pia sababu ya Mungu kuwatuma watumishi Wake ili kumwokoa Lutu. Wakati alipokabiliwa na changamoto, Lutu aliwalinda watumishi hawa wawili bila kujali chochote kingine; alijaribu hata kufanya biashara ya kuwabadilisha binti zake wawili mradi tu watumishi hawa wapate usalama. Mbali na Lutu, kulikuwa na mtu yeyote mwingine ndani ya mji ambaye angefanya jambo kama hili? Kama vile hoja zinavyothibitisha—la! Kwa hivyo, ni wazi kabisa kwamba kila mtu katika Sodoma, isipokuwa Lutu, alikuwa mlengwa wa kuangamizwa pamoja na mlengwa aliyestahili kuangamizwa.

Jumapili, 17 Machi 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Hudumu kama Waisraeli Walivyofanya

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Hudumu kama Waisraeli Walivyofanya

Siku hizi watu wengi hawatilii maanani mafunzo yapi yanayopaswa kusomwa wakati wa upatano na wengine. Nimegundua kuwa wengi wenu hawawezi kujifunza mafunzo hata kidogo wakati wa ushirikiano na wengine. Wengi wenu mnashikilia maoni yenu mwenyewe, na wakati mnafanya kazi kanisani, unatoa maoni yako na yeye anatoa yake, moja uhusiano na mingine, bila kushirikiana kabisa. Mnajihusisha tu katika kutoa umaizi wenu wenyewe wa ndani, unaingia tu katika kuachilia huru “mizigo” ndani yenu, si kutafuta uzima hata kidogo. Inaonekana kwamba unafanya tu kazi hiyo kwa kutimiza wajibu, daima ukiamini kwamba unapaswa kufuata njia yako mwenyewe bila kujali jinsi watu wengine walivyo, na kwamba unapaswa kushiriki jinsi Roho Mtakatifu anavyokuongoza, bila kujali jinsi watu wengine walivyo. Hamna uwezo wa kugundua uwezo wa wengine, na hamuwezi kujichunguza. Njia yenu ya kupokea vitu ni yenye makosa sana. Inaweza kusemwa kwamba hata sasa bado mnaonyesha kujidai kwingi, kana kwamba ugonjwa huo wa zamani umerejea tena. Hamuwasiliani nyinyi kwa nyinyi ili kufikia uwazi kamili, kama ni matokeo gani yaliyopatikana kwa kuzuru kanisa hilo, au jinsi hali yako ya ndani ilivyokuwa wakati wa hivi karibuni, na kadhalika—ninyi hamuwasiliani tu kwa namna hii. Nyinyi kimsingi hamna mazoea kama vile kuacha dhana zenu wenyewe au kujitelekeza. Wale walio katika uongozi wanafikiri tu kuhusu kuwachangamsha ndugu na dada katika makanisa ya chini kwa njia ya ushirika wao, na wale wanaofuata wanajua tu kufuatilia peke yao. Kimsingi hamuelewi huduma ni nini au ushirikiano ni nini, na mnadhani tu kuhusu kuwa na dhamira nyinyi wenyewe kuulipiza upendo wa Mungu, wa kuwa na dhamira ya nyinyi wenyewe kuishi kwa kudhihirisha mtindo wa Petro, na si kuhusu kitu kingine chochote. Hata unasema, bila kujali jinsi watu wengine walivyo, hamtatii kwa upofu hata hivyo, na bila kujali watu wengine walivyo, ninyi wenyewe unatafuta ukamilifu na Mungu, na hiyo itatosha. Kwa kweli, dhamira yako hayajapata maonyesho thabiti katika uhalisi hata kidogo. Je! Hii sio aina yote ya tabia mnayoonyesha siku hizi. Kila mmoja wenu anashikilia imara utambuzi wenu wenyewe, na ninyi nyote mnataka kufanywa wakamilifu. Ninaona kwamba mmetumikia kwa muda mrefu sana na hamjaendelea sana, hasa katika somo hili la kufanya kazi pamoja kwa maelewano hamjaendelea kabisa! Kuenda kwenye makanisa unawasiliana kwa njia yako, na yeye anafanya ushirika kwa njia yake. Kuna uratibu wa upatanifu kwa nadra sana. Na watu walio chini ambao wanafuata wako namna hii hata zaidi. Ambayo ni kusema kwamba ni watu wachache sana miongoni mwenu wanaelewa kumtumikia Mungu ni nini, au jinsi mtu anapaswa kumtumikia Mungu. Mmechanganyikiwa, na kuchukulia masomo ya aina hii kama suala dogo sana, kwa kiasi kwamba watu wengi hawatekelezi tu kipengele hiki cha ukweli, wanafanya mabaya kwa kujua. Hata watu ambao wametumikia kwa miaka mingi kwa kweli wanapigana na kugombana. Je! Hiki si kimo chako halisi? Ninyi watu mnaohudumu pamoja kila siku ni kama Waisraeli ambao walimtumikia Mungu Mwenyewe katika hekalu kila siku. Inawezekanaje kuwa ninyi watu ambao ni kama makuhani hamjui jinsi ya kushirikiana na jinsi ya kutumikia?
Wakati ule, Waisraeli walimtumikia Yehova moja kwa moja hekaluni. Utambulisho wao ulikuwa ule wa kuhani. (Bila shaka si kila mtu alikuwa kuhani. Ni baadhi tu waliomtumikia Yehova katika hekalu ndio walikuwa na utambulisho wa makuhani). Wangevalia taji ambazo Yehova aliwapa (ambayo inamaanisha walifanya taji kulingana na matakwa ya Yehova, sio kwamba Yehova aliwapa taji moja kwa moja) na wakiwa wamevalia mavazi yao ya kikuhani ambayo Yehova aliwapa wangeingia katika hekalu wakiwa miguu mitupu kumtumikia Yehova moja kwa moja, tangu asubuhi hadi usiku. Utumishi wao kwa Yehova haukuwa usio na mipangalio au wa kutenda makosawapendavyo; yote ilikuwa kulingana na sheria, ambazo hakuna mtu aliyemtumikia Yehova moja kwa moja angeweza kukiuka. Wote walipaswa kufuata sheria hizi; vinginevyo, kuingia hekaluni kulikatazwa. Ikiwa yeyote kati yao alivunja sheria za hekalu, yaani, kama mtu yeyote aliasi amri za Yehova, ilikuwa lazima apate kutendewa kulingana na sheria zilizotolewa na Yehova, na hakuna mtu aliyeruhusiwa kupinga, na hakuna mtu aliyeruhusiwa kumtetea. Haijalishi ni miaka mingapi ambayo mtu huyo alimtumikia Mungu, wote walipaswa kufuata sheria. Hii ndio sababu makuhani wengi walivalia nguo za kikuhani kila wakati na kumtumikia Yehova kwa njia hii mwaka mzima, ingawa Yehova hakuwatendea kwa njia yoyote maalum, na hata walikwenda mbele ya madhabahu au hekalu maisha yao yote. Hivyo ndivyo ulivyokuwa uaminifu wao na utii wao. Haishangazi kwamba Yehova aliwabariki kwa njia hii; ilikuwa yote kutokana na uaminifu wao kwamba walipata kibali na kuyaona matendo yote ya Yehova. Wakati ule ambapo Yehova alifanya kazi katika Israeli, watu Wake waliochaguliwa, matakwa Yake juu yao yalikuwa makali sana. Wote walikuwa watiifu sana na walizuiliwa na sheria, ambazo zilitumika kuwalinda ili kwamba wamheshimu Yehova. Hizi zote zilikuwa amri za utawala za Yehova. Ikiwa miongoni mwa wale makuhani kulikuwa na yeyote ambaye hakuishika Sabato au ambaye alikiuka amri za Yehova na aligunduliwa na watu wa kawaida, huyo mtu angeletwa mara moja mbele ya madhabahu na kupigwa kwa mawe hadi kufa, na hivyo kutolewa kama dhabihu mbele ya “madhabahu ya mtu wa kawaida” ambayo Yehova alikuwa Ameanzisha. Haikuruhusiwa kuweka maiti zao katika hekalu au karibu na hekalu. Yehova hakukubali hilo. Ikiwa mtu alifanya hivyo, angetendewa kama wale ambao hutoa “dhabihu za kawaida,” na kutupwa katika shimo kubwa na kuuawa. Bila shaka, watu wote kama hao wangepoteza maisha yao, hakuna aliyeachwa hai. Kulikuwa hata na wale ambao walitoa “moto wa kawaida,” kwa maneno mengine, wale watu ambao hawakutoa dhabihu katika siku zilizotolewa na Yehova wangeteketezwa na moto wa Yehova pamoja na vitu vyao vya dhabihu, hawaruhusiwa kubaki juu ya madhabahu. Mahitaji kwa makuhani yalikuwa: Hawakuruhusiwa kuingia hekaluni, na hata ua wa nje wa hekalu, bila ya kwanza kuosha miguu yao; hakuna kuingia hekaluni ikiwa hujavalia vazi za kikuhani; hakuna kuingia hekaluni ikiwa hujavalia taji za kikuhani; hakuna kuingia hekaluni ikiwa umechafuliwa na maiti; hakuna kuingia hekaluni baada ya kuugusa mkono wa mtu asiye haki bila ya kwanza kuosha mikono yake mwenyewe; hakuna kuingia hekaluni baada ya mahusiano ya ngono na wanawake (hii haikuwa milele, kwa muda wa miezi mitatu tu), hawakuruhusiwa kuuona uso wa Yehova, wakati ulipokuwa umeisha, ikimaanisha kwamba ni baada ya miezi mitatu tu ndio wangeweza kuruhusiwa kuvaa mavazi safi ya kikuhani, na kuhudumu katika ua wa nje kwa siku saba kabla ya kuweza kuingia katika hekalu ili kuuona uso wa Yehova; waliruhusiwa kuvaa mavazi yote ya kikuhani ndani ya hekalu tu na hawaruhusiwa kuyavaa nje ya hekalu, ili kuepuka kulichafua hekalu la Yehova; iliwapasa wote waliokuwa makuhani kuwaleta wahalifu ambao wamekiuka sheria za Yehova mbele ya madhabahu ya Yehova ambako wangeuawa na watu wa kawaida, vinginevyo moto ungeanguka juu ya kuhani ambaye alishuhudia. Kwa hiyo walikuwa waaminifu kwa Yehova daima, kwa sababu sheria za Yehova zilikuwa kali juu yao, na hawangeweza kabisa kuthubutu kukiuka kikawaida amri Zake za utawala. Waisraeli walikuwa waaminifu kwa Yehova kwa sababu walikuwa wameuona moto Wake, walikuwa wameuona mkono ambao Yehova alitumia kuwaadibu watu, na pia kwa sababu hapo awali walimheshimu Yehova mioyoni mwao. Kwa hivyo kile walichopata sio moto wa Yehova tu; pia walipata utunzaji na ulinzi kutoka kwa Yehova, na kupata baraka za Yehova. Uaminifu wao ni kwamba walifuata maneno ya Yehova katika yale waliyofanya, bila mtu yeyote kuasi. Ikiwa mtu yeyote angekosa kutii, watu bado wangetekeleza maneno ya Yehova, na kuwaua wale wote waliokwenda kinyume na Yehova, bila njia yoyote ya kuficha. Hasa wale ambao walikiuka Sabato, wale waliokuwa na hatia ya uasherati, na wale walioiba sadaka kwa Yehova wangeadhibiwa vikali zaidi. Wale ambao walikiuka Sabato waliuawa kwa mawe nao (watu wa kawaida), au walipigwa viboko hadi kufa, bila yeyote kuachwa. Wale waliofanya vitendo vya uasherati, hata wale waliomtamani mwanamke mzuri, au wale waliokuwa na mawazo ya kiasherati baada ya kumwona mwanamke mwovu, au waliokuwa na tamaa ya kimapenzi baada ya kumwona mwanamke mwenye umri mdogo—kila mtu wa aina hii angeuawa. Ikiwa mwanamke mdogo yeyote ambaye hakuvaa nguo ya kufunika au utaji alimjaribu mwanaume katika kitendo cha tabia mbaya, mwanamke huyo angeuawa. Ikiwa ilikuwa ni kuhani (wale watu ambao walihudumu katika hekalu) ndiye aliyekiuka sheria za aina hii, angesulubiwa au kunyongwa. Hakuna mtu wa aina hii angeweza kuruhusiwa kuishi, na hakuna hata mtu mmoja angeweza kupata kibali mbele za Yehova. Jamaa za mtu wa aina hii hawangeruhusiwa kutoa dhabihu kwa Yehova mbele ya madhabahu kwa miaka mitatu baada ya kifo chake, na hawangeruhusiwa kugawana dhabihu ambazo Yehova aliwapa watu wa kawaida. Wakati tu ulipopita ndio wangeweka ng’ombe au kondoo wa daraja la juu kwenye madhabahu ya Yehova. Ikiwa kulikuwa na kosa lingine lolote, walipaswa kufunga kwa siku tatu mbele za Yehova, wakiomba neema Yake. Kuabudu kwao Yehova hakukuwa tu kwa sababu sheria za Yehova zilikuwa kali sana na za shuruti sana; badala yake ilikuwa ni kwa sababu ya neema ya Yehova, na pia ilikuwa kwa sababu walikuwa waaminifu kwa Yehova. Hivyo, huduma yao hadi leo imekuwa ya uaminifu vilevile, na hawajawahi kuvunja maombi yao mbele ya Yehova. Katika siku hizi watu wa Israeli bado wanapata utunzaji na ulinzi wa Yehova, na hata leo Yehova bado ni neema kati yao, na daima hukaa nao. Wote wanajua jinsi wanapaswa kumheshimu Yehova, na jinsi wanapaswa kumtumikia Yehova, na wote wanajua jinsi wanapaswa kuwa ili kupokea na kulindwa na Yehova, kwa sababu wote wanamcha Yehova mioyoni mwao. Siri ya mafanikio ya huduma yao yote si nyingine isipokuwa uchaji. Lakini nyinyi nyote mko namna gani leo? Je! Mnafanana na watu wa Israeli kwa vyovyote? Je! unafikiri kwamba huduma ya leo ni kama kufuata uongozi wa kielelezo mkubwa wa kiroho? Hamna tu uaminifu na uchaji wowote. Mnapokea neema nyingi, nyinyi ni sawa na makuhani wa Israeli, kwa sababu nyote mnamtumikia Mungu moja kwa moja. Ingawa hamuingii hekaluni, yale mnayopokea na mnayoona ni mengi zaidi kuliko kile ambacho makuhani waliomtumikia Yehova katika hekalu walipokea. Lakini bado mnaasi na mnapinga mara nyingi kuliko walivyofanya. Uchaji wenu ni mdogo sana, na hivyo mnapokea neema ndogo sana. Ingawa mnajitolea kidogo sana, mmepata mengi zaidi kuliko Waisraeli hao. Je! Huku sio kuwatendea nyinyi kwa wema? Wakati wa kazi katika Israeli, hakuna mtu angethubutu kumhukumu Yehova kama alivyotaka. Na nyinyi je? Kama si kwa sababu kazi Ninayofanya miongoni mwenu ni kuwashinda, Ningewezeje kuvumilia kutenda kwenu ovyo ovyo kuliaibisha kwa jina Langu? Ikiwa enzi mnayoishi ingekuwa Enzi ya Sheria, hakuna hata mmoja wenu angekuwa hai, kutokana na matendo yenu na maneno yenu. Uchaji wenu ni mdogo sana! Nyinyi daima mnanilaumu kwa kutowapa kibali kikubwa, na hata kusema kuwa sikuwapa maneno ya baraka ya kutosha, kwamba Nina laana tu kwenu. Je, hamjui kwamba kwa uchaji mdogo hivyo haiwezekani kwenu kukubali baraka Zangu? Je! Hamjui kwamba Mimi huwalaani mara kwa mara na kuwahukumu kwa sababu ya hali mbovu ya huduma yenu? Je, ninyi nyote mnajihisi kuwa mmekosewa? Ninawezaje kuwapa baraka Zangu kikundi cha watu ambao ni waasi na hawatii? Ninawezaje kutoa neema Yangu kwa watu ambao huleta aibu kwa jina Langu? Matendo kwa nyinyi watu tayari ni yenye huruma sana. Ikiwa Waisraeli wangekuwa waasi kama mlivyo leo, Ningalikuwa Nimewaangamiza muda mrefu uliopita. Ilhali Mimi siwatendei kwa vyovyote ila kwa huruma. Je! Huu sio wema? Je! Mnataka baraka nyingi zaidi kuliko hii? Wale pekee ambao Yehova anawabariki ni wale wanaomheshimu Yeye. Yeye huwaadibu wale wanaoasi dhidi Yake, Hamsamehei mtu yeyote kamwe. Je, si ninyi watu wa leo ambao hamjui jinsi ya kutumikia mko na haja zaidi ya kuadibiwa na hukumu, ili mioyo yenu iweze kurekebishwa kikamilifu? Je, kuadibiwa na hukumu ya aina hii sio baraka bora zaidi kwenu? Je! Sio ulinzi wenu bora? Bila hiyo, je, yeyote kati yenu angeweza kuvumilia moto wa Yehova unaochoma? Ikiwa kweli mngetumikia kwa uaminifu kama watu wa Israeli, je, hamngekuwa pia na neema kama rafiki yenu daima? Je, hangekuwa pia na furaha na neema ya kutosha? Je, nyote mnajua jinsi mnapaswa kutumikia?
Leo mahitaji ya nyinyi kufanya kazi pamoja kwa upatanifu ni sawa na jinsi Yehova alivyowataka Waisraeli kumtumikia. Vinginevyo, tamatisha tu huduma yenu. Kwa sababu nyinyi ni watu wanaomtumikia Mungu moja kwa moja, kwa kiwango cha chini zaidi mnapaswa kuweza kuwa waaminifu na watiifu katika huduma yenu, na lazima muweze wa kujifunza masomo kwa njia ya vitendo. Hasa wale wanaofanya kazi kanisani, je, yeyote kati ya ndugu na dada walio chini angethubutu kushughulika na nyinyi? Je, mtu yeyote angethubutu kuwaambia makosa yenu uso kwa uso? Mko juu ya yote, nyinyi kweli mnatawala kama wafalme! Hata hamjifunzi au kuingia katika somo la matendo kama hilo, na bado mnazungumza juu ya kumtumikia Mungu! Kwa sasa unaulizwa kuongoza makanisa kadhaa, na sio tu kwamba unakata tamaa mwenyewe, hata unashikilia mawazo na maoni yako, na kusema mambo kama “Nadhani jambo hili linafaa lifanyike kwa njia hii, kwani Mungu amesema kuwa hatupaswi kuzuiwa na wengine, na kwamba siku hizi hatupaswi kutii kwa upofu.” Kwa hiyo kila mmoja anashikilia maoni yake mwenyewe, na hakuna mtu anayemtii mwingine. Ingawa unafahamu wazi kwamba huduma yako iko katika shida kubwa, bado unasema, “Vile ninavyoona, yangu haiko mbali sana. Kwa hali yoyote sisi kila mmoja ana upande mmoja; unazungumza kuhusu yako, na mimi kuhusu yangu; unashiriki kuhusu maono yako na ninazungumza juu ya kuingia kwangu.” Huchukui jukumu kwa vitu vingi ambavyo vinapaswa kushughulikiwa, au unamudu tu, kila mtu akieleza maoni yake mwenyewe, kwa busara akilinda hali yake mwenyewe, sifa na uso wake. Hakuna mtu aliye tayari kujinyenyekesha, hakuna mtu atakayejitoa kwa ari kumrekebisha mwingine na kurekebishwa ili maisha yaendelee kwa haraka zaidi. Mara chache sana wakati mnafanya kazi pamoja hakuna yeyote kati yenu atasema, Ningependa kukusikia ukishiriki na mimi kuhusu kipengele hiki cha ukweli, kwa sababu bado nina tashwishi kukihusu. Au kusema: una uzoefu zaidi kuliko mimi juu ya jambo hili; unaweza kunipa mwelekeo fulani, tafadhali? Je, si hii ingekuwa njia nzuri ya kufanya hivyo? Nyinyi mlio kwenye viwango vya juu husikia ukweli mwingi, na kuelewa mengi kuhusu huduma. Ikiwa ninyi watu ambao mnaratibu kufanya kazi katika makanisa hamjifunzi kutoka kwa kila mmoja, na kuwasiliana, kufidia mapungufu ya kila mmoja, mnaweza kujifunza masomo kutoka wapi? Mnapokutana na chochote, mnapaswa kushirikiana na kila mmoja, ili maisha yenu yaweze kufaidika. Na mnapaswa kushirikiana kwa makini kuhusu mambo ya aina yoyote kabla ya kufanya maamuzi. Ni kwa kufanya hivyo tu ndio mnakuwa na jukumu kwa kanisa na si kuwa wazembe. Baada ya kutembelea makanisa yote, mnapaswa kukutana na kushiriki juu ya masuala yote mnayotambua na matatizo mnayokabiliwa nayo kazini, na kuwasiliana kuhusu nuru na mwanga ambao mmepokea—huu ni utaratibu wa lazima wa huduma. Lazima mfikie ushirikiano wa upatanifu kwa kusudi la kazi ya Mungu, kwa manufaa ya kanisa, na kwa kuwachochea ndugu na dada kuendelea. Unashirikiana pamoja naye na anashirikiana na wewe, kila mmoja akimbadilisha mwingine, mkifikia matokeo bora ya kazi, ili kutunza mapenzi ya Mungu. Huu tu ndio ushirikiano wa kweli, na watu kama hao tu ndio wana kuingia kwa kweli. Kunaweza kuwa na hotuba fulani isiyofaa wakati wa ushirikiano, lakini hiyo haijalishi. Shirikiana juu yake baadaye, na mpate ufahamu wa wazi kulihusu; msipuuze suala hilo. Baada ya aina hii ya ushirika unaweza kufidia mapungufu kwa ndugu na dada. Ni kwa kuenda kwa kina zaidi tu kwa namna hii katika kazi yako ndio unaweza kufikia matokeo bora. Kila mmoja wenu, kama watu wanaohudumu, lazima muweze kulinda maslahi ya kanisa katika yote mnayofanya, badala ya kuwa macho kwa maslahi yako mwenyewe. Haikubaliki kufanya pekee yako, pale ambapo unamdharau naye anakudharau. Watu wanaotenda kwa njia hii hawafai kumhudumia Mungu! Tabia ya mtu wa aina hii ni mbaya sana; hakuna hata kiasi kidogo cha ubinadamu bado kimebaki ndani yake. Yeye ni Shetani asilimia mia moja! Yeye ni mnyama! Hata sasa mambo kama haya bado yanatokea kati yenu, kwenda mpaka kushambuliana wakati wa ushirika, kutafuta visingizio kwa makusudi, kukasirika mkibishana juu ya jambo fulani dogo, hakuna mtu aliye radhi kujitenga, kila mtu akificha kilicho ndani kutoka kwa mwingine, akimwangalia mwingine na makini na kuwa macho. Je! Tabia ya aina hii ni huduma inayofaa kwa Mungu? Je, kazi kama hiyo yenu inaweza kuwakimu ndugu na dada? Sio tu kuwa huwezi kuwaongoza watu kwenye njia sahihi ya maisha, kwa kweli unaingiza tabia zako za upotovu ndani ya ndugu na dada. Je! Huwaumizi wengine? Dhamiri yako ni mbaya sana, iliyooza kabisa! Huingii katika ukweli, na huutii ukweli katika vitendo. Zaidi ya hayo, bila haya unaonyesha hadharani asili yako ya mbovu sana kwa watu wengine, huoni aibu hata kidogo! Ndugu na dada wamekabidhiwa kwako, lakini unawapeleka kuzimu. Je, si wewe ni mtu ambaye dhamiri yake imeoza? Huna aibu kabisa!
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Alhamisi, 7 Machi 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Onyo kwa Wale Wasioweka Ukweli katika Vitendo

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Onyo kwa Wale Wasioweka Ukweli katika Vitendo

Wale miongoni mwa ndugu na dada ambao daima hueneza ubaya wao ni vibaraka wa Shetani na hulivuruga kanisa. Watu hawa lazima siku moja wafukuzwe na kuondolewa. Katika Imani yao kwa Mungu, ikiwa watu hawana moyo wa kumcha Mungu ndani yao, ikiwa hawana moyo ambao ni mtiifu kwa Mungu, basi hawatashindwa tu kufanya kazi yoyote ya Mungu, lakini kinyume na hayo watakuwa watu wanaovuruga kazi ya Mungu na wanaomuasi Mungu. Wakati mtu anayeamini Mungu hamtii Mungu ama kumcha Mungu lakini badala yake anamwasi Yeye, basi hii ndiyo aibu kuu zaidi kwa muumini. Ikiwa usemi na mwenendo wa muumini daima havina mpango na bila kizuizi kama asiyeamini, basi huyu muumini ni mwovu zaidi kumpiku asiyeamini; yeye ni ibilisi halisi. Wale walio kanisani ambao wanaeneza matamshi yao yenye sumu, wale miongoni mwa ndugu na dada ambao wanasambaza uvumi, kuchochea utengano na kufanya magenge wanapaswa kufukuzwa kutoka kanisani. Lakini watu hawa wamezuiwa kwa kuwa sasa ni enzi tofauti ya kazi ya Mungu, kwa sababu wamehukumiwa kuwa vyombo vya kuondolewa. Wale waliopotoshwa na Shetani wote wana tabia iliyopotoka. Lakini ilhali baadhi ya watu wana tu tabia iliyopotoka kuna wengine wasio jinsi hii, ya kuwa hawana tu tabia za kishetani zilizopotoka, lakini asili zao pia ni mbovu kupita kiasi. Yote anayoyafanya mtu huyu na kusema hayaonyeshi tu tabia yake ya kishetani, bali yeye mwenyewe ni ibilisi Shetani halisi. Anachofanya ni kuvuruga na kukatiza kazi ya Mungu, kuvuruga maisha ya kuingia ya ndugu na dada, na kuharibu maisha ya kawaida ya kanisa. Mbwa mwitu hawa waliovalia ngozi ya kondoo lazima waondolewe nje siku moja, na mtu lazima awe na mtazamo usiojizuia kwa vibaraka hawa wa Shetani; mtu lazima awe na mtazamo wa kuachwa kwao. Ni katika kufanya hili pekee ndipo mtu atakaweza kusimama upande wa Mungu na wale wasioweza kufanya hili wako katika ushirika na Shetani. Mungu daima yumo mioyoni mwa wale wanaomwamini Mungu kwa kweli na daima wana moyo wa kumcha Mungu, moyo wa kumpenda Mungu. Wale wanaomwamini Mungu lazima wayafanye mambo kwa moyo wa uangalifu na wenye busara, na yote wanayoyafanya yanapasa kulingana na matakwa ya Mungu na yaweze kuuridhisha moyo wa Mungu. Hawapaswi kuwa wabishi, wakifanya watakavyo, hayo hayafai katika utaratibu mtakatifu. Watu hawawezi kuipunga bendera ya Mungu kwa madaha na kucharuka kila mahali, wakijishau na kutapeli kotekote; kutenda haya ni tendo la uasi la juu zaidi. Familia zina masharti na mataifa yana sheria, hivyo ni kwa kiasi gani zaidi ndiyo familia ya Mungu ina viwango vikali? Je, si pia ina amri za usimamiaji? Watu wana uhuru wa kutenda watakayo, lakini amri za usimamizi za Mungu haziwezi kubadilishwa kwa hiari. Mungu ni Mungu asiyewaruhusu watu kumkosea Yeye na Mungu ni Mungu anayewauwa watu—je, watu hawajui hili tayari?
Kila moja ya kanisa lina watu wanaolivuruga kanisa, watu wanaokatiza kazi ya Mungu. Watu hawa wote ni Shetani wanaojifanya katika familia ya Mungu. Mtu wa aina hii ni mjuzi wa kuiga, akija mbele Yangu kwa heshima, akitikisa vichwa kwa kukubali na kuinama, akitenda kama mbwa wengi walio hafifu, akijitolea “yote” yake ili kufikia malengo yake mwenyewe, lakini akionyesha sura yake mbaya mbele ya ndugu. Anapomwona mtu akiuweka ukweli katika vitendo anamshambulia na kumtenga, na anapomwona mtu mbaya kumpiku yeye mwenyewe, anamsifu mno na kujipendekeza kwake, wakitenda kama viongozi wa kiimla kanisani. Inaweza kusemwa kuwa mengi ya makanisa yana aina hii ya “nyoka mwovu wa ndani,” aina hii ya “mbwa wa kupakata” kati yao. Wanatembea kwa siri kwa pamoja, wakikonyezeana na kuashiriana, na hakuna hata mmoja wao anayeweka ukweli katika vitendo. Yeyote aliye na sumu zaidi ndiye “ibilisi mkuu,” na yeyote aliye na hadhi ya juu zaidi huwaongoza, akipeperusha bendera yao juu zaidi. Watu hawa wanakuwa huru na kufanya wanachotaka kanisani, wakieneza ubaya wao, wakiachilia kifo, wakifanya watakavyo, wakisema wanachopenda, bila anayedhubutu kuwakomesha, wakijawa na tabia za kishetani. Punde tu wanapoanza kusababisha usumbufu, hewa ya kifo inaingia ndani ya kanisa. Wale wanaoweka ukweli katika vitendokatika kanisa wanaachwa na wanashindwa kufikia uwezo wao, ilhali wale wanaovuruga kanisa na kusambaza kifo wanakuwa huru na kufanya wanachotaka kanisani. Cha ziada ni, watu wengi huwafuata. Aina hii ya kanisa iko chini ya udhibiti wa Shetani na ibilisi ni mfalme wao. Iwapo watu wa kanisa hawataamka na kuwafukuza hao ibilisi wakuu, basi pia watakuja kuangamia siku moja. Kuanzia leo na kuendelea hatua lazima zichukuliwe dhidi ya kanisa la aina hii. Ikiwa wale wanaoweza kuuweka ukweli mdogo katika vitendo hawajihusishi na utafutaji, basi kanisa hilo litapigwa marufuku. Ikiwa hakuna mtu yeyote kanisani aliye radhi kuuweka ukweli katika vitendo, hakuna yeyote anayeweza kuwa shahidi kwa Mungu, basi kanisa hilo linapasa kutengwa kabisa, na miunganisho yao na makanisa mengine kukatizwa. Hili linaitwa kuzika kifo, na kumfukuza Shetani. Iwapo kuna nyoka kadhaa waovu wa ndani katika kanisa, na vilevile nzi wadogo wanaowafuata wale wasio na ufahamu kabisa, ikiwa wale wa kanisa bado hawawezi kutoa vifungu na ushawishi wa nyoka hawa baada ya wao kuona ukweli, basi hawa wajinga wataondolewa mwishoni. Ingawa nzi hawa wadogo wanaweza kuwa hawajafanya lolote baya, wao ni wenye hila hata zaidi, wadanganyifu hata zaidi na wenye kukwepa hata zaidi na kila mtu aliye namna hii ataondolewa. Hakuna yeyote atakayeachwa! Wale walio wa Shetani watarudishwa kwa Shetani, ilhali wale walio wa Mungu hakika watakwenda kutafuta ukweli; hili linaamuliwa na asili zao. Acheni wale wote wanaomfuata Shetani waangamie! Hakuna huruma watakayoonyeshwa watu hawa. Acheni wale wanaofuata ukweli wapate utoaji na muwakubalie kufurahia neno la Mungu hadi mioyo yao itosheke. Mungu ni mwenye haki; Yeye hawatendei watu kwa udhalimu. Ikiwa wewe ni ibilisi basi hutakuwa na uwezo wa kuuweka ukweli katika vitendo. Ikiwa wewe ni mtu anayetafuta ukweli basi ni wazi kuwa hutatekwa nyara na Shetani—hili halina tashwishi yoyote.
Wale wasiotafuta kuendelea daima wanataka wengine wawe wabaya na watepetevu kama wao wenyewe, wale wasioweka ukweli katika vitendo wanawaonea gere wale wanaotenda ukweli. Wale wasioweka ukweli katika vitendo daima wanataka kuwadanganya wale wapumbavu na wasio na ufahamu. Mambo ambayo watu hawa wanaeneza yanaweza kukufanya usawijike, kuteleza kwenda chini, kuwa na hali isiyokuwa ya kawaida na kujawa na kiza ndani yako; yanaweza kukufanya usogezwe mbali na Mungu, na yanakufanya uuthamini mwili na kujihusisha na tamaa. Wale ambao hawapendi ukweli, ambao daima humshughulikia Mungu kwa uzembe hawana maarifa ya binafsi, na tabia zao huwashawishi watu kufanya dhambi na kuasi Mungu. Hawaweki ukweli katika vitendo wala kuwaruhusu wengine kutenda ukweli. Wanathamini dhambi na hawana chuki kwao wenyewe. Hawajifahamu wenyewe na huwakomesha wengine kujifahamu wenyewe, na huwakomesha wengine kuwa na matamanio ya kujua ukweli. Wale wanaowadanganya hawawezi kuona mwangaza na huanguka gizani, hawajijui wenyewe, na ukweli kwao si wazi na wanakuwa mbali zaidi na zaidi na Mungu. Hawaweki ukweli katika vitendo na huwakomesha wengine kutenda ukweli, wakiwaleta watu hao wajinga mbele yao. Badala ya kusema kuwa wanamwamini Mungu ingekuwa vyema kusema kuwa wanawaamini mababu zao, kwamba kile wanachoamini ni sanamu zilizo mioyoni mwao. Ingekuwa vyema kwa wale watu wanaosema kuwa wanamfuata Mungu kufungua macho yao watazame vizuri waone ni nani wanayemwamini hasa: Je, ni Mungu unayemwamini hakika, ama Shetani? Ikiwa unajua kuwa unayemwamini si Mungu ila sanamu zako mwenyewe, basi ni vyema kabisa usiseme kuwa wewe ni muumini. Ikiwa hakika hujui unayemwamini ni nani, basi, pia, ni vyema kabisa usiseme kuwa wewe ni muumini. Kusema hivi kutakuwa kukufuru! Hakuna anayekushurutisha umwamini Mungu. Msiseme kuwa mnaniamini Mimi, kwa kuwa Niliyasikia maneno hayo hapo kale wala Sitamani kuyasikia tena, kwa kuwa mnachoamini ni sanamu zilizo katika mioyo yenu na nyoka waovu wa ndani walio miongoni mwenu. Wale wanaotikisa vichwa vyao wanaposikia ukweli, wanaotabasamu sana wanaposikia mazungumzo ya kifo ni watoto wa Shetani, na wote ni vyombo vya kuondolewa. Kuna watu wengi kanisani ambao hawana ufahamu, na jambo la uongo linapotendeka wanasimama tu upande wa Shetani. Wanapoitwa vibaraka wa Shetani wanahisi kuwa wamekosewa sana. Wanasemekana kuwa hawana ufahamu, lakini daima wanasimama upande usiokuwa na ukweli. Hakujakuwa na wakati muhimu ambapo wamesimama upande wa ukweli, hakuna wakati mmoja ambapo wamesimama na kutetea mjadala juu ya ukweli, kwa hivyo je, hawana ufahamu? Kwa nini daima wanasimama upande wa Shetani? Kwa nini hawasemi neno lolote la haki ama lenye maantiki kwa ukweli? Je, hali hii kweli imetokana na kuchanganyikiwa kwao kwa ghafla? Kadri mtu anapokuwa na ufahamu mdogo, ndivyo anavyozidi kushindwa kusimama upande wa ukweli. Je, hili linaonyesha nini? Je, halionyeshi kuwa wale wasio na ufahamu wanapenda uovu? Je, halionyeshi kuwa wale wasio na ufahamu ni watoto waaminifu wa Shetani? Je, ni kwa nini daima wanaweza kusimama upande wa Shetani na kuzungumza lugha moja naye? Kila neno na tendo lao, na maonyesho yao yanathibitisha vya kutosha kuwa wao sio wapenzi wa ukweli kwa namna yoyote, lakini badala yake wao ni watu wanaochukia ukweli. Kwamba wanaweza kusimama upande wa Shetani kunadhihirisha kuwa hakika Shetani anawapenda ibilisi hawa wadogo wanaopigana kwa ajili ya Shetani katika maisha yao yote. Je, taarifa hizi za kweli si wazi sana? Ikiwa hakika wewe ni mtu unayependa ukweli, basi kwa nini huwezi kuwaheshimu wale wanaotenda ukweli, na mbona unawafuata mara moja wale wasioweka ukweli katika vitendo punde tu wanapokuwa na mabadiliko ya sura? Je, hili ni tatizo la aina gani? Sijali iwapo una ufahamu au la, sijali kwamba umelipa gharama kuu kiasi gani, sijali kuwa nguvu zako ni kuu kiasi gani na sijali ikiwa wewe ni nyoka mwovu wa ndani ama kiongozi anayepeperusha bendera. Ikiwa nguvu zako ni kuu basi ni kwa ajili tu ya usaidizi wa nguvu za Shetani; ikiwa hadhi yako iko juu, basi ni kwa sababu kuna wengi waliokuzunguka wasiotenda ukweli; ikiwa hujafukuzwa basi ni kwa kuwa sasa sio wakati wa kazi ya kufukuza, bali ni wakati wa kazi ya kuondoa. Hakuna haraka ya kukufukuza sasa. Ninahitaji tu kusubiri siku ifike ambayo utakuwa umeshaondolewa ili Nikuadhibu. Yeyote asiyeweka ukweli katika vitendo ataondolewa!
Wale wanaomwamini Mungu kwa kweli ni wale walioradhi kuweka neno la Mungu kwenye matendo, na ni wale walioradhi kutenda ukweli. Wale wanaoweza kwa kweli kuwa shahidi kwa Mungu pia ni wale walioradhi kuweka neno Lake kwenye matendo, na ni wale ambao kwa kweli wanaweza kusimama upande wa ukweli. Wale wanaotumia hila na wale wanaotenda yasio haki wote ni watu wasiokuwa na ukweli na wote huleta aibu kwa Mungu. Wale walio kanisani wanaohusika na mabishano ni vibaraka wa Shetani, na ni mfano mwema wa Shetani. Mtu wa aina hii ni mwovu sana. Wale wasio na ufahamu na wasio na uwezo wa kusimama upande wa ukweli wanahifadhi nia mbovu na kufifisha ukweli. Watu hawa hata zaidi ni mawakilishi kamili wa Shetani; wamepita hali ya ukombozi na ni wazi mno kuwa wao wote ni vitu vya kuondolewa. Wale wasioweka ukweli katika vitendo hawapaswi kuruhusiwa kusalia katika familia ya Mungu, wala wale wanaobomoa kanisa kwa maksudi. Lakini sasa Sifanyi kazi ya kufukuza. Watafichuliwa tu na kuondolewa mwishoni. Hakuna kazi nyingine ya bure itakayofanywa kwa watu hawa; wale walio wa Shetani hawana uwezo wa kusimama upande wa ukweli, ilhali wale wanaotafuta ukweli wanaweza kusimama upande wa ukweli. Wale wasioweka ukweli katika vitendo hawastahili kusikia njia ya kweli na hawastahili kuwa na ushuhuda kwa ukweli. Kimsingi ukweli si kwa ajili ya masikio yao lakini badala yake unazungumzwa kwa ajili ya masikio ya wale wanaoutenda. Kabla ya mwisho wa kila mtukufichuliwa, wale wanaovuruga kanisa na kukatiza kazi kwanza wataachwa upande moja. Pindi kazi itakapokamilika, watu hawa watafunuliwa mmoja baada ya mwingine kabla ya kuondolewa. Wakati wa kutoa ukweli, Siwatilii maanani kwa sasa. Ukweli wote unapofichuliwa kwa mwanadamu watu hao wanapasa kuondolewa, kwa kuwa huo pia utakuwa wakati ambapo watu wataainishwa kulingana na aina yao. Kwa sababu ya werevu wao mdogo, wale wasio na ufahamu watakuja kuangamia mikononi mwa watu waovu na watapotoshwa na watu waovu na watashindwa kurudi. Watu hawa wanapasa kushughulikiwa kwa njia hii, kwa kuwa hawaupendi ukweli, kwa sababu hawana uwezo wa kusimama upande wa ukweli, kwa sababu wanawafuata watu waovu, wanawaunga mkono watu waovu, na kwa sababu wanashirikiana na watu waovu na kumuasi Mungu. Wanajua vema kuwa watu hao waovu wananururisha uovu lakini wanafanya mioyo yao kuwa migumu na kuwafuata, wakienda kinyume na ukweli. Je, watu hawa wasioweka ukweli katika vitendo lakini wanaofanya mambo ya uharibifu na ya chukizo wote si wanafanya maovu? Ingawa kuna wale miongoni mwao ambao wanajipa mtindo wenyewe kama “wafalme” na wale wanaofuata msururu nyuma yao, je, asili yao ya kuasi Mungu si ni sawa yote? Je, wanaweza kutoa sababu gani kuwa Mungu hawaokoi? Je, wanaweza kutoa sababu gani kuwa Mungu si mwenye haki? Je, si ni uovu wao wenyewe ambao umewaangamiza? Je, si ni uasi wao ambao utawavuta hadi jahanamu? Wale wanaoweka ukweli katika vitendo mwishowe wataokolewa na kufanywa wakamilifu kwa kupitia ukweli. Wale wasioweka ukweli katika vitendo mwishowe watakaribisha maangamizi kwa kupitia ukweli. Hii ndio miisho inayowasubiri wale wanaoweka ukweli katika vitendo na wale wasioutenda. Ninawashauri wale ambao hawana mpango wa kuweka ukweli katika vitendo watoke kanisani haraka iwezekanavyo ili kuepuka kutenda dhambi nyingi zaidi. Wakati utakapofika, hata majuto yatakuwa yamechelewa, na hasa wale wanaofanya magenge na kufanya migawanyiko, na wale nyoka waovu wa ndani katika kanisa lazima watoke haraka sana. Watu hawa ambao ni wenye asili ya mbwa mwitu mwovu hawana uwezo wa mabadiliko, ni heri watoke kanisani kwa nafasi inayopatikana mwanzo, wasiweze kuyavuruga maisha mazuri ya ndugu na dada tena, na hivyo kuepuka adhabu ya Mungu. Nyinyi ambao mlienda pamoja nao mtafanya vema kutumia nafasi hii kutafakari juu yenu wenyewe. Je, mtawafuata waovu nje ya kanisa, ama kusalia na kufuata kwa uaminifu wote? Lazima uzingatie jambo hili kwa makini. Ninawapa nafasi moja zaidi ya kuchagua. Ninalisubiri jibu lenu.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Jumatatu, 25 Februari 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Umuhimu wa Kuukoa Uzao wa Moabu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Umuhimu wa Kuukoa Uzao wa Moabu

Katika miaka hii miwili hadi mitatu ya kazi, kile kilichopaswa kutimizwa katika kazi ya hukumu iliyofanyika juu yenu kimetimizwa kimsingi. Watu wengi wamesahau matarajio na kudura yao ya baadaye. Hata hivyo, inapotajwa kuwa ninyi ni uzao wa Moabu, wengi wenu huchukizwa sana—nyuso zenu hubadilika, vinywa vyenu hupinda, na macho yenu hukodolea. Hamuwezi kabisa kuamini kwamba ninyi ni uzao wa Moabu. Moabu ilifukuzwa hadi nchi hii baada ya kulaaniwa. Ukoo wa wana wa Moabu umerithishwa mpaka leo, na ninyi nyote ni uzao wake. Hakuna kitu ambacho Ninaweza kufanya—nani aliyekusababisha uzaliwe katika nyumba ya Moabu? Ninakuhurumia na Siko radhi uwe hivi, lakini ukweli hauwezi kubadilishwa na watu. Wewe ni uzao wa Moabu, na Siwezi kusema kuwa wewe ni uzao wa Daudi. Haijalishi wewe ni uzao wa nani, bado wewe ni mmoja wa viumbe. Ni kwamba tu wewe ni kiumbe wa cheo cha chini—wewe ni kiumbe wa kuzaliwa katika hali duni. Viumbe vyote lazima vipitie kazi yote ya Mungu, vyote ni vyombo vya kushinda Kwake, na lazima vyote viione tabia Yake yenye haki, na kupitia hekima na kudura Yake. Sasa wewe ni uzao wa Moabu na lazima uikubali hukumu hii na kuadibu, hivyo kama hungekuwa uzao wa Moabu, basi pia hungehitaji kukubali hukumu na kuadibu huku? Unapaswa kutambua hili! Kwa kweli, kufanya kazi kwa uzao wa Moabu kwa sasa ni kwa thamani sana na kwenye umuhimu sana. Maadam kazi imefanywa kwenu, ina umuhimu mkubwa mno. Kama kazi ingefanywa kwa uzao wa Hamu haingeweza kuwa muhimu kwa sababu wao hawajazaliwa katika hali duni kama hiyo na kuzaliwa kwao sio sawa na Moabu. Uzao wa mwana wa pili wa Nuhu Hamu umelaaniwa tu—hawakuja kutokana na uasherati. Ni kwamba tu wao ni wa hali ya chini, kwa sababu Nuhu aliwalaani na wao ni watumishi wa watumishi. Wanayo hali ya chini, lakini thamani yao ya asili haikuwa chini. Tukizungumza kuhusu Moabu, watu wanajua kwamba awali alikuwa na hali ya chini kwa sababu alizaliwa kutokana na uasherati. Ingawa nafasi ya Loti ilikuwa ya juu sana, Moabu alizaliwa na Lutu na binti yake. Ingawa Loti alikuwa mtu mwenye haki, Moabu bado alikuwa chombo cha laana. Moabu alikuwa wa thamani ya chini na alikuwa na cheo cha chini, na hata kama hakuwa amelaaniwa alikuwa wa uchafu, hivyo alikuwa tofauti na Hamu. Hakukubali na alipinga, aliasi dhidi ya Yehova, ndiyo sababu alianguka katika maeneo yenye giza zaidi. Kufanya kazi sasa kwa uzao wa Moabu ni kuwaokoa wale ambao wameanguka katika giza zaidi. Ingawa walikuwa wamelaaniwa, Mungu yuko tayari kupata utukufu kutoka kwao. Hii ni kwa sababu hapo awali, wote walikuwa watu waliomkosa Mungu mioyoni mwao—kuwafanya tu kuwa wale wanaomtii na kumpenda Yeye ni ushindi wa kweli, na matunda hayo ya kazi ni ya thamani sana na yenye kuridhisha zaidi. Huku tu ni kupata utukufu—huu ndio utukufu ambao Mungu anataka kuupata katika siku za mwisho. Ingawa watu hawa ni wa nafasi ya chini, sasa wanaweza kupata wokovu mkubwa mno, ambao kwa kweli ni kupandishwa hadhi na Mungu. Kazi hii ni ya maana sana, na ni kwa njia ya hukumu ndipo Anawapata watu hawa. Yeye hawaadhibu kwa makusudi, lakini Amekuja kuwaokoa. Kama bado angekuwa Anafanya kazi ya kushinda katika Israeli wakati wa siku za mwisho ingekuwa ni bure; hata kama ingezaa matunda, haingekuwa na thamani yoyote au umuhimu wowote mkubwa, na Yeye hangeweza kupata utukufu wote. Anafanya kazi kwenu, yaani, wale ambao wameanguka katika maeneo yenye giza zaidi, wao walio nyuma zaidi kimaendeleo. Watu hawa hawakiri kuwa kuna Mungu na kamwe hawajapata kujua kwamba kuna Mungu. Viumbe hawa wamepotoshwa na Shetani hadi kiwango ambapo wamemsahau Mungu. Wamepofushwa na Shetani na hawajui kabisa kwamba kuna Mungu mbinguni. Katika mioyo yenu nyote mnaabudu sanamu, mnamwabudu Shetani—je, si ninyi ni watu wa hali ya chini zaidi, watu walio nyuma zaidi kimaendeleo? Ninyi ni wa hali ya chini kabisa ya mwili, mnakosa uhuru wowote wa kibinafsi, na mnapitia shida pia. Ninyi pia ni watu mlio katika ngazi ya chini kabisa katika jamii hii, bila hata uhuru wa imani. Huu ni umuhimu wa kufanya kazi kwenu. Kufanya kazi kwenu sasa, uzao wa Moabu, sio kuwafedhehesha kwa makusudi, lakini ni kufichua umuhimu wa kazi. Ni kuwainua sana. Ikiwa mtu ana mantiki na utambuzi, atasema: “Mimi ni uzao wa Moabu. Kweli sistahili kuinuliwa kukuu huku na Mungu ambako nimepokea sasa, au baraka hizi nyingi. Kwa mujibu wa yale ninayofanya na kusema, na kulingana na hali na thamani yangu—sistahili kabisa hizo baraka nyingi kutoka kwa Mungu. Waisraeli wana upendo mkubwa kwa Mungu, na neema wanayoifurahia imefadhiliwa kwao na Yeye, lakini hali yao ni ya juu zaidi kuliko yetu. Abrahamu alijitolea sana kwa Yehova, na Petro alijitolea sana kwa Yesu—ibada yao ilishinda yetu kwa mara mia, na kwa msingi wa matendo yetu hatufai kabisa kufurahia neema ya Mungu.” Huduma ya watu hawa nchini China haiwezi kuletwa mbele za Mungu hata kidogo. Ni fujo kamili tu, na kwamba sasa mnafurahia neema nyingi za Mungu ni kuinuliwa na Mungu kabisa! Je, ni wakati upi mmeitafuta kazi ya Mungu? Je, mmeyatoa maisha yenu kwa Mungu lini? Ni wakati gani mmeiacha familia yako kwa urahisi, wazazi wenu, na watoto wenu? Hakuna hata mmoja wenu aliyelipa gharama kubwa! Kama haingekuwa kwa Roho Mtakatifu kukufanya uonekane, wangapi wenu wangeweza kutoa dhabihu kila kitu? Ni kwa sababu tu mmelazimishwa na kushurutishwa ndipo mmefuata hadi leo. Upendo wenu uko wapi? Utiifu wenu uko wapi? Kulingana na matendo vyenu, mngepaswa kuangamizwa muda mrefu uliopita—kufagiliwa mbali kungepaswa kufanywa kwenu. Mna haki gani ya kufurahia baraka nyingi mno—ninyi hamstahili kabisa! Nani kati yenu amebuni njia yake mwenyewe? Ni nani kati yenu ameipata njia ya ukweli mwenyewe? Ninyi nyote ni wavivu na walafi, fidhuli msio na maana ambao mnasherehekea katika faraja kwa tamaa! Mnafikiri ninyi ni wakubwa sana? Je, nini mlicho nacho cha kujivunia? Hata kama Singesema ninyi ni uzao wa Moabu, je, asili yenu, mahali penu pa kuzaliwa ni ya fahari sana? Hata kama Singesema ninyi ni uzao wake, je, si ninyi nyote ni uzao wa Moabu kwa kweli? Ukweli wa mambo unaweza kubadilishwa? Je, kufichua asili yenu sasa kunaenda dhidi ya ukweli wa mambo? Angalieni jinsi mlivyo wanyonge, maisha yenu, na tabia—je, hamjui kwamba ninyi ni wa chini kabisa kati ya walio chini miongoni mwa wanadamu? Nini mlicho nacho cha kujisifia? Angalia nafasi yenu katika jamii. Je, si mko katika kiwango cha chini kabisa? Je, mnadhani kwamba Nimenena vibaya? Ibrahimu alimtoa Isaka. Nini ambacho mmetoa? Ayubu ilitoa kila kitu. Nini ambacho mmetoa? Watu wengi sana wameyatoa maisha yao, wakafa, wakamwaga damu yao ili kutafuta njia ya kweli. Je, mmelipa gharama hiyo? Kwa kulinganisha, hamna sifa zinazostahili hata kidogo kufurahia neema hiyo kubwa, kwa hivyo ni sawa kusema leo kwamba ninyi ni uzao wa Moabu? Msijione kuwa wakuu sana. Huna chochote cha kujisifia. Wokovu mkubwa kama huo, neema hiyo kubwa imepewa kwenu bure. Hamjatoa chochote, lakini mmeifurahia neema bure. Je, hamuoni haya? Je, njia hii ya ukweli ni jambo ambalo ninyi wenyewe mlipata kupitia kutafuta? Je, si ni Roho Mtakatifu aliyewalazimisha kuikubali? Kamwe humkuwa na moyo wa kutafuta na hasa hamkuwa na mioyo ya kuutafuta ukweli, ya kuutamani ukweli. Mmekuwa tu mkistarehe na kuufurahia, na mmeupata ukweli huu bila jitihada kwa upande wenu. Mna haki gani ya kulalamika? Je, unadhani kuwa wewe ni wa thamani kubwa zaidi? Ikilinganishwa na wale ambao walitoa dhabihu maisha yao na kumwaga damu yao, nini mnachopaswa kulalamikia? Kuwaangamiza hivi sasa litakuwa ni jambo linalotarajiwa! Kando na kutii na kufuata, hamna chaguzi zingine. Ninyi hasa hamstahili! Wengi wa wale kati yenu waliitwa, lakini kama mazingira hayangewalazimisha au kama hamngeitwa, hamngekuwa tayari kabisa kutokea wazi. Nani yuko tayari kutelekeza mambo kwa namna hii? Ni nani yuko tayari kuacha anasa za mwili? Ninyi nyote ni watu ambao husherehekea kwa ulafi katika faraja na kutafuta maisha ya anasa! Mmepata baraka nyingi mno—nini kingine mnacho cha kusema? Mna malalamiko yapi? Mmefurahia baraka nyingi mno na neema kuu mno mbinguni, na kazi sasa imefichuliwa kwenu ambayo haikuwahi kufanywa duniani awali. Je, si hii ni baraka? Kwa sababu mmempinga na kuasi dhidi ya Mungu, sasa mmepitia kuadibu kiasi hiki. Kwa sababu ya kuadibu huku mmeziona rehema na upendo wa Mungu, na hata zaidi mmeziona haki na utakatifu Wake. Kwa sababu ya kuadibu huku na kwa sababu ya uchafu wa wanadamu, mmeiona nguvu kuu ya Mungu, na mmeuona utakatifu na ukuu Wake. Je, si huu ni ukweli adimu mno? Je! Si haya ni maisha yenye maana? Kazi ambayo Mungu hufanya ina maana tele! Hivyo nafasi yenu ilivyo chini zaidi, ndivyo inavyoonyesha zaidi kuinuliwa na Mungu, na ndivyo inavyothibitisha zaidi jinsi kazi Yake ilivyo na thamani kwenu leo. Ni hazina yenye thamani mno hasa! Haiwezi kupatikana popote pengine, na kwa muda mrefu hakuna mtu aliyefurahia wokovu mkubwa hivi. Ukweli kwamba nafasi yenu ni ya chini inaonyesha jinsi wokovu wa Mungu ulivyo mkuu, na inaonyesha kwamba Mungu ni mwaminifu kwa wanadamu—Yeye huokoa, sio kuangamiza.
Watu wa Uchina hawajawahi kumwamini Mungu na hawajawahi kumhudumia Yehova, hawajawahi kumhudumia Yesu. Yote wanayofanya ni kusujudu, kufukiza uvumba, kuchoma sanamu ya Mungu ya karatasi, na kumwabudu Buddha. Wao wanaabudu sanamu tu—wote ni waasi mno, hivyo jinsi nafasi ya watu ilivyo ya chini zaidi, ndivyo inavyoonyesha zaidi kwamba kile Mungu hupata kutoka kwenu ni utukufu hata zaidi. Kutoka kwa mtazamo wa watu fulani, wangesema: “Mungu, ni kazi gani Unayofanya? Wewe, Mungu mwenye fahari sana, Mungu mtakatifu mno, ulikuja katika nchi yenye uchafu? Je, Unajidharau sana hivyo? Sisi ni wachafu sana, lakini Uko radhi kuwa pamoja nasi? Uko tayari kuishi kati yetu? Sisi ni wa cheo cha chini sana, lakini Uko radhi kutufanya kuwa kamili? Na Ungetutumia sisi kama mifano na vielelezo? “Ninasema: Huelewi mapenzi Yangu! Huelewi kazi ambayo Nataka kufanya wala huelewi tabia Yangu. Huwezi kufikia umuhimu wa kazi ambayo Ninaenda kufanya. Je, kazi Yangu ingepatana na mawazo ya kibinadamu? Kulingana na mawazo ya kibinadamu, Ningelazimika kuzaliwa katika nchi nzuri ili kuonyesha kwamba mimi ni wa hali ya juu, kuonyesha kwamba Mimi ni wa thamani kubwa, na kuonyesha uheshimiwa, utakatifu, na ukuu Wangu. Kama Ningezaliwa mahali ambapo pananitambua, katika familia ya ngazi ya juu, na kama Ningekuwa wa cheo na hadhi ya juu, basi Ningetendewa vizuri sana. Hiyo haingekuwa na manufaa kwa kazi Yangu, hivyo je, wokovu mkuu mno bado ungeweza kufichuliwa? Wote wanaoniona Mimi wangenitii, na hawangenajisiwa na uchafu. Nilipaswa kuzaliwa katika mahali pa aina hii. Hivyo ndivyo ninyi mnaamini. Lakini litafakari: Je! Mungu alikuja duniani kwa ajili ya raha, au kwa ajili ya kazi? Kama Ningefanya kazi katika aina ya mahali hapo rahisi, mahali penye starehe, je, Ningepata utukufu Wangu kamili? Je, Ningeweza kuvishinda viumbe Vyangu vyote? Mungu alipokuja duniani Yeye hakuwa wa ulimwengu na Yeye hakuwa mwili ili apate kuufurahia ulimwengu. Mahali ambapo kufanya kazi kungefichua tabia Yake vizuri sana na pawe mahali pa maana zaidi ni mahali Alipozaliwa. Kama ni nchi takatifu au yenye uchafu, na bila kujali Anapofanya kazi, Yeye ni mtakatifu. Kila kitu duniani kiliumbwa na Yeye; Ni kwamba tu kila kitu kimepotoshwa na Shetani. Hata hivyo, vitu vyote bado ni Vyake; vyote viko mikononi Mwake. Kuja Kwake katika nchi yenye uchafu kufanya kazi ni kufichua utakatifu Wake; Yeye hufanya hivi kwa ajili ya kazi Yake, yaani, Yeye huvumilia aibu kubwa kufanya kazi kwa njia hii ili kuwaokoa watu wa nchi hii yenye uchafu. Hii ni kwa ajili ya ushuhuda na ni kwa ajili ya wanadamu wote. Kile aina hii ya kazi inawaruhusu watu kuona ni haki ya Mungu, na ina uwezo zaidi wa kuonyesha mamlaka ya juu kabisa ya Mungu. Ukuu na uadilifu Wake vinaonyeshwa kupitia wokovu wa kundi la watu wa hali ya chini ambao hakuna mtu anayewapenda. Kuzaliwa katika nchi yenye uchafu haimaanishi kabisa kuwa Yeye ni duni; inawaruhusu tu viumbe vyote kuuona utukufu Wake na upendo wake wa kweli kwa wanadamu. Zaidi Anavyofanya kwa njia hii, zaidi inavyofichua upendo Wake safi zaidi kwa mwanadamu, upendo wake usio na dosari. Mungu ni mtakatifu na mwenye haki. Hata ingawa Alizaliwa katika nchi yenye uchafu, na ingawa Anaishi na watu hao ambao wamejawa uchafu, kama vile Yesu alivyoishi na wenye dhambi katika Enzi ya Neema, si kazi Yake yote kwa ajili ya kuishi kwa wanadamu wote? Je, si yote ni ili mwanadamu aweze kuupata wokovu mkuu? Miaka elfu mbili iliyopita Aliishi na wenye dhambi kwa miaka kadhaa. Hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya ukombozi. Leo, Anaishi na kikundi cha watu wachafu, wa hali ya chini. Hii ni kwa ajili ya wokovu. Je, si kazi Yake yote ni kwa ajili yenu, wanadamu hawa? Kama haingekuwa ili kuwaokoa wanadamu, kwa nini Angeishi na kuteswa pamoja na wenye dhambi kwa miaka mingi sana baada ya kuzaliwa horini? Na kama haingekuwa ili kuwaokoa wanadamu, kwa nini Angeurudia mwili kwa mara ya pili, kuzaliwa katika nchi hii ambako mapepo hukusanyika, na kuishi na watu hawa ambao wamepotoshwa kwa kina na Shetani? Je, si Mungu ni mwaminifu? Ni aina gani ya kazi Yake ambayo haijakuwa kwa ajili ya wanadamu? Ni aina gani ambayo haijakuwa kwa ajili ya kudura yako? Mungu ni mtakatifu! Hili haliwezi kubadilika. Yeye hanajisiwi na uchafu, ingawa Amekuja katika nchi yenye uchafu; yote haya yanamaanisha tu kwamba upendo wa Mungu kwa wanadamu ni wenye kuwajali wengine sana, mateso na aibu Anayoyavumilia ni makubwa sana! Kwa ajili yenu nyote, na kwa ajili ya kudura yenu, Yeye hupitia aibu kubwa sana. Je, hamjui hivyo? Yeye hawaokoi watu wakuu au wana wa familia tajiri na zenye uwezo, lakini Yeye huwaokoa hasa wale ambao ni wa hali za chini na wanaodharauliwa na wengine. Je, si haya yote ni utakatifu Wake? Je, si haya yote ni haki Yake? Afadhali Azaliwe katika nchi yenye uchafu na kuteseka aibu yote kwa ajili ya kuishi kwa wanadamu wote. Mungu ni halisi sana—Hafanyi kazi ya uwongo. Je, si kila hatua ya kazi Yake imefanyika kwa utendaji hivi? Ingawa watu wote wanamkashifu na kusema kuwa Anakaa mezani pamoja na wenye dhambi, ingawa watu wote wanamdhihaki na kusema kuwa Anaishi na wana wa uchafu, na watu wa hali ya chini sana, bado Anajitolea bila ubinafsi, na bado Anakataliwa kwa njia hii kati ya wanadamu. Je, si mateso Anayoyahimili ni makubwa zaidi kuliko yenu? Je, si kazi Yake ni zaidi ya gharama ambayo mmelipa? Mlizaliwa katika nchi ya uchafu lakini mmepata utakatifu wa Mungu. Mlizaliwa katika nchi ambako mapepo hukusanyika lakini mmepokea ulinzi mkubwa. Je, mna uchaguzi gani mwingine? Ni malalamiko yapi mliyo nayo? Je, si mateso ambayo Amevumilia ni makubwa zaidi kuliko mateso ambayo mmevumilia? Amekuja duniani na hajawahi kufaidi furaha za ulimwengu wa kibinadamu. Anayachukia mambo hayo. Mungu hakuja duniani kufurahia manufaa ya kibinadamu kutoka kwa mwanadamu, wala haikuwa kufurahia mambo mazuri ya wanadamu kula na kuvalia. Hazingatii mambo haya; Alikuja duniani kuteseka kwa ajili ya mwanadamu, si kufurahia mambo mazuri ya kidunia. Alikuja kuteseka, Alikuja kufanya kazi, na kukamilisha mpango Wake wa usimamizi. Hakuchagua mahali pazuri, kuishi katika ubalozi au hoteli ghali mno, wala Hana watumishi kadhaa kumtumikia. Kutokana na kile mmeona, hamjui kama Alikuja kufanya kazi au kufurahia? Je, macho yenu hayafanyi kazi? Amewapa kiasi gani? Kama Angezaliwa katika mahali pazuri Angeweza kuupata utukufu? Je, Angeweza kufanya kazi? Je! Huko kungekuwa na umuhimu wowote? Angeweza kuwashinda kabisa wanadamu? Angeweza kuwaokoa watu kutoka katika nchi ya uchafu? Kulingana na mawazo ya kibinadamu, “Mungu, kwa kuwa Wewe ni mtakatifu, kwa nini Ulizaliwa katika mahali penye uchafu mno kama hapa? Unatuchukia na kutukirihi sisi wanadamu wachafu; Unachukia upinzani wetu na uasi wetu, hivyo kwa nini Unaishi nasi? Wewe ni Mungu mkuu sana—hungeweza kuzaliwa tu popote, lakini ilibidi uzaliwe katika nchi hii yenye uchafu? Unatuadibu na kutuhukumu kila siku na Unajua wazi kwamba sisi ni uzao wa Moabu, basi kwa nini bado Unaishi kati yetu? Kwa nini Ulizaliwa katika familia ya uzao wa Moabu? Kwa nini Ulifanya hivyo? “Aina hii ya ufahamu wenu inakosa mantiki! Ni aina hii ya kazi tu ambayo inawaruhusu watu kuuona ukuu Wake, unyenyekevu na kujificha Kwake. Yuko tayari kutoa kila kitu kwa ajili ya kazi Yake, na Amevumilia mateso yote kwa ajili ya kazi Yake. Anafanya kwa ajili ya wanadamu, na hata zaidi kumshinda Shetani ili viumbe vyote viweze kutii chini ya utawala Wake. Hii tu ni kazi ya maana, yenye thamani. Kama uzao wa Yakobo ungezaliwa nchini China, katika kipande hiki cha ardhi, na wote walikuwa ninyi nyote, basi umuhimu wa kazi iliyofanyika kwenu ingekuwa nini? Shetani angesema nini? Shetani angesema: “Walikuwa wakikuogopa Wewe, lakini hakuna mtu aliyeirithisha kwa muda mrefu. Hata hivyo, mababu zao walikuogopa; Walikutii tangu mwanzo na hawana historia ya kukusaliti. Ni kwamba tu baada ya kipindi cha muda hiyo haikurithishwa tena. Wao si wenye giza kabisa, wa hali ya chini kabisa, au walio nyuma zaidi kimaendeleo kati ya wanadamu. Walikukiri tangu mwanzo. Hakuna umuhimu wa kuifanya kwa njia hiyo! Ikiwa inafanyika hivi kwa kweli, nani atakayeridhishwa na kazi hii? “Kati ya ulimwengu wote, watu wa Kichina ni watu walio nyuma zaidi kimaendeleo. Wamezaliwa na hali ya chini na uadilifu duni, ni wapumbavu na wenye ganzi, nao ni watovu wa adabu na waliofifia. Wameloweshwa na tabia za kishetani, wachafu na waasherati. Mnayo haya yote. Kwa mintarafu ya tabia hizi potovu, baada ya kazi hii kukamilika watu watazitupilia mbali na wataweza kutii kikamilifu na kufanywa kuwa kamili. Tunda tu kutoka kwa aina hii ya kazi ndilo huitwa ushuhuda kati ya viumbe! Je, unaelewa kile kinachoitwa ushuhuda? Je, ushuhuda unapaswa kutolewaje? Aina hii ya kazi imewafanya kuwa foili[a] pamoja na vyombo vya huduma, na hata zaidi, mmekuwa vyombo vya wokovu. Leo ninyi ni watu wa Mungu na baadaye mtakuwa mifano na vielelezo. Katika kazi hii, mnajitwisha majukumu mbalimbali, na hatimaye mtakuwa vyombo vya wokovu. Watu wengi ni hasi kwa sababu ya hili; Je, si wao ni vipofu kabisa? Huwezi kuona chochote waziwazi! Je, cheo hiki tu kinakuzidi? Je, unaelewa kile kinachotajwa kama tabia ya Mungu yenye haki? Je, unaelewa wokovu ni nini? Je, unaelewa upendo wa Mungu ni nini? Huna uaminifu! Unapoona jina zuri unafurahi. Usipoona jina zuri hukubali nawe unarudi nyuma. Wewe ni nini? Hufuati njia ya kweli! Afadhali uache kutafuta mara moja. Ni jambo la aibu! Jambo dogo sana linakuzidi. Je, si hii ni ishara ya aibu?
Afadhali uweze kujijua kiasi. Usijione kuwa mkuu sana, wala usiwazie kwenda mbinguni. Tafuta tu kushindwa hapa duniani kwa kufanya wajibu ipasavyo! Usifikiri kuhusu ndoto hizo zisizo halisi ambazo hazipo. Mtu akisema jambo kama: “Ingawa mimi ni wa uzao wa Moabu, niko tayari kujitahidi kumpata Mungu, na katika siku zijazo nitamkana babu yangu wa zamani! Alinizaa na pia alinikandamiza, na hadi sasa nimekuwa nikiishi tu katika giza. Leo Mungu ameniachilia na hatimaye nimeiona mbingu. Kupitia kwa ufunuo wa Mungu hatimaye nimeona kwamba mimi ni wa uzao wa Moabu. Awali nilikuwa gizani, na sikujua kwamba Mungu amefanya kazi nyingi sana; yote ni kwa sababu nimepofushwa na Shetani huyu wa zamani. Nitamkana na kumuaibisha kabisa.” Haya ni maneno kutoka kwa mtu mwenye hamu ya kupata, mwenye ujasiri. Hivyo mna ujasiri? Licha ya ukweli kwamba mna mfano wa mwanadamu, mnashindwa kustahimili kasi zaidi kuliko mtu mwingine yeyote, nanyi ni wepesi zaidi wa kuathirika kuhusiana na suala hili. Mara tu inapotajwa kwamba ninyi ni uzao wa Moabu, midomo yenu inapinda kwa kuibibidua. Je! Si hii ni tabia ya nguruwe? Haina maana. Mko tayari kutoa dhabihu maisha yenu kwa ajili ya umaarufu na bahati yenu! Huko tayari kuwa uzao wa Moabu, lakini sivyo ulivyo? Ninasema leo kwamba wewe uko hivyo, na lazima ukiri jambo hilo. Siendi kinyume na ukweli. Watu wengine ni hasi kwa sababu ya jambo hili, lakini wewe ni hasi kuhusu nini? Je, si wewe pia ndiye mtoto wa joka kubwa jekundu? Je, ni udhalimu kusema kwamba wewe ni uzao wa Moabu? Angalia kile unachoishi kwa kudhihirisha, ndani na nje. Kutoka kichwani hadi mguuni, hakuna kitu cha kujisifia. Uasherati, uchafu, upofu, upinzani, uasi—si haya yote ni sehemu ya tabia yako? Daima wewe huishi ndani ya nchi ya uasherati nawe hufanya uovu wote. Unadhani kuwa wewe ni mtakatifu wa ajabu sana, lakini hebu yalinganishe mambo ambayo umeyafanya. Unafurahishwa sana na matokeo yako—nini ulicho nacho cha kujisifia? wewe ni kama wanyama, huna ubinadamu! Mnaafikiana na wanyama, mnaishi ndani ya uovu, dhana za kiasherati. Je! Mnakosa kiasi gani? Mnakubali kwamba ninyi ni watoto wa joka kubwa jekundu, na mko tayari kufanya huduma, lakini baadaye inaposemekana kuwa wewe ni uzao wa Moabu unakuwa hasi. Je! Si huu ni ukweli? Sawasawa na ulivyozaliwa na mama na baba yako, haijalishi jinsi walivyo wabaya, bado ulizaliwa na wao. Hata ukipata mama wa kambo na kuondoka katika nyumba hiyo, je, si wewe bado ni mtoto wa wazazi wako wa mwanzo? Je! Ukweli huo unaweza kubadilishwa? Je, nimekupachika tu jina kwa kubahatisha? Watu wengine wanasema: "Je! Si ungenipa tu jina lingine?” Ninasema: “Je, unaonaje Nikikupa jina la foili[a]?" Hawataki kuwa foili[a] pia. Basi unataka kuwa nini? Foili[a], watendaji huduma—si ninyi mko hivi? Ungechagua nini kingine? Je, si wewe ni mtu aliyezaliwa katika nchi ya joka kubwa jekundu? Haijalishi ni kiasi gani unasema kuwa wewe ni mwana wa Daudi, haikubaliani na ukweli. Je, hili ni jambo ambalo wewe mwenyewe ulichagua? Je, unaweza tu kutumia jina zuri kujitaja kwa kubahatisha? Je! Si watoto wa joka kubwa jekundu waliozungumziwa zamani ni nyinyi, kundi hili la watu waliopotoshwa? Watendaji huduma waliotajwa—je, si wao pia ni nyinyi, watu hawa waliopotoshwa? Vielelezo vilivyoshindwa, mifano iliyotajwa— si hivi pia ni nyinyi, watu hawa? Njia ya kukamilishwa—si hilo linasemwa kwa ajili yenu? Wale ambao wanaadibiwa na kuhukumiwa ni nyinyi, na si wale wanaokamilishwa baadaye watakuwa baadhi ya wale miongoni mwenu? Je, jina hili lina maana? Ninyi ni wapumbavu sana kiasi kwamba hamuwezi hata kuona kitu hicho kidogo kwa dhahiri? Hujui nani ni uzao wa nani, lakini Niko dhahiri kulihusu. Nawaambieni. Ikiwa unaweza kulitambua leo hivyo ni vizuri. Usijidhalilishe kila wakati. Zaidi unavyokuwa hasi na kurudi nyuma, ndivyo inavyoonyesha zaidi kwamba wewe ni uzao wa Shetani. Kuna mtu ambaye, unapomtaka asikilize wimbo, anasema: “Je, uzao wa Moabu hutumia vinasasauti? Sitausikiliza; Mimi sistahili!” Ukimtaka aimbe, anasema: “Ikiwa uzao wa Moabu unaimba, Je, Mungu yuko radhi kusikiliza? Mungu ananichukia. Nina aibu sana kwenda mbele za Mungu na siwezi kushuhudia Kwake. Sitaimba kabisa, Mungu asije akakasirika Anapousikia.” Je! Si hii ni njia hasi ya kulishughulikia? Kama mmoja wa viumbe, ulizaliwa katika nchi ya uasherati na wewe ni mtoto wa joka kubwa jekundu, uzao wa Moabu; unapaswa kumkana babu yako wa zamani na kumkana Shetani wa zamani. Huyu tu ndiye mtu anayemtaka Mungu kwa kweli.
Mwanzoni nilipowapa nafasi ya watu wa Mungu mlikuwa mnaruka juu chini—mliruka kwa furaha zaidi kuliko mtu yeyote. Lakini ilikuwaje mara Niliposema kuwa ninyi ni uzao wa Moabu? Ninyi nyote mlishindwa kustahimili! Ungesema kimo chenu kipo wapi? Dhana yenu ya nafasi ni nzito sana! Wengi hawawezi kujiinua. Wengine huenda kufanya biashara, na wengine huenda kazini. Mara tu Ninaposema kwamba ninyi ni uzao wa Moabu nyote mnataka kukimbia. Je, huku ndiko kushuhudia kwa Mungu ambako huwa mnapigia kelele wakati wote? Je! Shetani ataridhishwa kwa njia hii? Si hii ni alama ya aibu? Ni faida gani kuwa na nyinyi? Ninyi nyote ni taka! Ni mateso ya namna gani ambayo mmestahimili, lakini mnahisi kuwa mmetendewa mabaya sana? Mnafikiri kwamba mara tu Mungu amewatesa hadi kiwango fulani Atafurahi, kana kwamba Mungu alikuja kuwahukumu kimakusudi, na baada ya kuwahukumu na kuwaangamiza, kazi Yake itakuwa imekamilika. Je, ni hivyo ndivyo Nimesema? Je, si hii ni kwa sababu ya upofu wenu? Je! Ni kwamba ninyi wenyewe hamjitahidi kufanya vizuri au kwamba Ninawahukumu kwa makusudi? Sijawahi kufanya hivyo—hilo ni jambo ambalo mlilifikiria wenyewe. Sijafanya kazi kwa njia hiyo kabisa, wala Sina nia hiyo. Kama Ningetaka kuwaangamiza kwa kweli, je, Ningehitaji kuteseka sana hivyo? Ningetaka kuwaangamiza kwa kweli, Ningehitaji kuzungumza nanyi kwa dhati? Mapenzi Yangu ni haya: wakati ambapo Nimewaokoa ndipo Nitakapoweza kupumzika. Zaidi mtu alivyo wa hali ya chini, ndivyo alivyo chombo cha wokovu wangu zaidi. Zaidi mwezavyo kuingia kiutendaji, ndivyo Nitakavyofurahia zaidi. Zaidi mnavyoshindwa kustahimili ndivyo Ninavyofadhaika zaidi. Daima mnataka kuingia kwa mwendo wa furaha kuelekea kiti cha enzi, lakini Nitawaambieni, hiyo sio njia ya kuwaokoa kutokana na uchafu. Njozi ya kukaa kwa kiti cha enzi haiwezi kukufanya kuwa mkamilifu; hiyo si kweli. Nasema kuwa wewe ni uzao wa Moabu, kisha unakuwa na huzuni. Unasema: “Unataka niende kuzimu. Sitakuwa na ushuhuda Kwako au kuteswa kwa ajili Yako.” Je, si kufanya kwako hivi ni kunipinga Mimi? Je, hili ni la manufaa kwako? Nimekupa neema nyingi sana—umesahau? Moyo wa Mungu ambao ni kama tu mama mwenye upendo umegeuka kuwa maji baridi kwa sababu yako na kuwa barafu. Je! Shetani atakuachilia huru? Ikiwa hushuhudii Kwangu Sitakuhimiza lakini unapaswa kujua kwamba hatimaye utakuwa lengo la maangamizo. Ikiwa Siwezi kupata ushuhuda ndani yako, Nitaupata kwa watu wengine. Hilo halina maana Kwangu, lakini mwishowe utalijutia, na wakati huo utakuwa umeanguka gizani muda mrefu uliopita. Basi nani atakayeweza kukuokoa? Usifikiri kwamba kazi haiwezi kufanyika bila wewe. Hakungekuwa na wengi sana pamoja na wewe, na hakungekuwa na wachache sana bila wewe. Usijione kuwa mheshimiwa sana. Ikiwa hutaki kunifuata, hiyo inaonyesha tu kwamba wewe ni muasi, na hakuna kitu cha kutamanisha ndani yako. Ikiwa wewe ni msemaji mzuri, si hivyo ni kwa sababu tu umejiandaa na maneno Niliyoyaleta kupitia kwa kazi Yangu? Nini ulicho nacho cha kujisifia? Usiruhusu mawazo yako yafikie hitimisho lisilo la msingi! Ikiwa Siwezi kupata utukufu kutoka kwenu, uzao huu wa Moabu, Nitachagua kikundi cha pili, na cha tatu cha uzao wa Moabu kufanya kazi mpaka Nipate utukufu. Ikiwa huko radhi kuwa na ushuhuda Wangu, basi toka nje! Sitakulazimisha! Usifikiri kwamba Nitashindwa kusonga hatua bila ninyi. Kupata vyombo vinavyofaa kwa kazi Yangu katika nchi hii ya China hakuhitaji jitihada. Hakuna kitu kingine chochote kinachoweza kupatikana katika nchi hii—watu wachafu, wapotovu bila shaka wako kila mahali na kazi Yangu inaweza kufanyika popote. Usiwe na kiburi sana! Bila kujali wewe ni mwenye kiburi vipi, je, si bado wewe ni mtoto aliyezaliwa kutokana na uzinzi? Angalia thamani yako, na ni chaguo gani lingine ulilo nalo? Kukukubali tu kuishi ni kuinuliwa kukubwa, kwa hivyo ni nini unajivunia? Kama haingekuwa kwa ajili ya kazi Yangu kukomesha enzi, je, si ungekuwa umeanguka katika majanga ya kawaida na maafa ya kibinadamu zamani sana? Je! Unaweza bado kuishi kwa raha sana? Bado daima unabishana kuhusu suala hili. Tangu Niliponena kuhusu uzao wa Moabu umekuwa ukibibidua midomo wakati wote. Hufanyi uchunguzi, husomi, na unamchukia kila mtu. Unapowaona watu wengine wakifanya uchunguzi unawavuruga na kusema mambo ya kuwavunja moyo. Una ujasiri! Unasema: “Uzao wa Moabu unajifunza nini? Sitajifunza kwa ajili Yake. "Je, si hili ni jambo ambalo mnyama angesema? Je, hata unafikiriwa kuwa mwanadamu? Nimesema mambo mengi kwako, lakini haijafanikisha chochote. Je, Nimefanya kazi hii yote bure? Je, Nimesema maneno haya yote bure? Kama ungekuwa mbwa bado ungeutikisa mkia wako; mtu wa aina hiyo siye hata sawa na mbwa! Wakati mwingine unabibidua midomo, wakati mwingine unatazama kwa shaka—je, kazi hii yote iliyofanyika kwako ilikuwa ya bure? Mara tu Ninaponena kuhusu uzao wa Moabu, watu wengine hujishusha hadhi kimakusudi. Wanavaa tofauti kuliko hapo awali nao ni wachafu sana kisai kwamba hawaonekani kama watu, nao hunung’unika: “Mimi ni uzao wa Moabu, sifai kitu. Hata hivyo hakuna kitu kizuri ndani yangu na sitaki kupata baraka zozote. Kwa vyovyote, hivi ndivyo ilivyo. Je, uzao wa Moabu unaweza kufanywa kuwa mkamilifu? "Mara tu Ninaponena kuhusu uzao wa Moabu, watu wengi hawana matumaini tena, na kusema: “Mungu anasema kwamba sisi ni uzao wa Moabu—hii inaonyesha nini? Kwa kuchunguza toni ya sauti Yake, hakuna uwezekano wa ukombozi! Hakuna upendo katika maneno Yake. Je! Si sisi ni malengo ya maangamizo? “Je! Umesahau kile kilichosemwa hapo awali? Leo neno “uzao wa Moabu” ni jambo pekee ambalo umekumbuka? Kwa kweli, maneno mengi ni kwa ajili ya kufikia kitu, lakini pia yanafichua ukweli wa mambo. Watu wengi hawaliamini. Huko tayari kuteseka kwa njia hiyo kwa ajili Yangu. Unaogopa kifo na daima unataka kutoroka. Ikiwa unataka kwenda Sitakulazimisha kukaa, lakini ni lazima Nikweleze wazi jambo moja: Usiishi maisha yote bure, na usisahau mambo yote Nilivyokwambia zamani. Kama mmoja wa viumbe unapaswa kutekeleza wajibu wa mmoja wa viumbe. Usifanye mambo dhidi ya dhamiri yako; unachopaswa kufanya ni kujitolea kwa Bwana wa uumbaji. Uzao wa Moabu pia ni sehemu tu ya uumbaji, ni kwamba tu wamelaaniwa. Chochote kitokeacho, bado wewe ni mmoja wa viumbe. Ikiwa unasema: “Ingawa mimi ni uzao wa Moabu, nimefurahia neema nyingi ya Mungu mbeleni, hivyo ni lazima niwe na dhamiri. Nitakiri tu lakini sitafikiri sana kulihusu. Hata kama nitateseka ndani ya mkondo huu, nitateseka mpaka mwisho. Kama mimi ni wa uzao wa Moabu basi iwe hivyo! Bado nitafuata hadi mwisho. “Ikiwa unasema hivi, basi huko mbali sana. Lazima ufuate mpaka mwisho. Ukikimbia kwa kweli huna matumaini ya baadaye — umeingia kwenye barabara ya maangamizo.
Ni vizuri kuwafanya muelewe asili yenu, na kuwafanya muuelewe ukweli wa mambo ni wenye manufaa kwa kazi. Vinginevyo, matokeo ambayo yanapaswa kufanikishwa hayatafanikishwa. Hii ni sehemu ya kazi ya kushinda, na ni hatua muhimu katika kazi. Huo ni ukweli. Kufanya kazi hii ni kuziamsha roho za watu, kuamsha hisia za dhamiri zao na kuwaruhusu watu kupata wokovu huu mkubwa. Ikiwa mtu ana dhamiri, anapoona kwamba yeye ni wa hali ya chini anapaswa hasa kumshukuru Mungu. Anayashika maneno Yake kwa nguvu, anaishika kwa nguvu neema ambayo Amempa, na hata kulia kwa uchungu na kusema: “Nafasi yetu ni ya chini sana na hatujapata chochote duniani. Hakuna mtu kutuheshimu, watu hawa wa hali ya chini. Tunateswa katika mazingira yetu ya nyumbani, waume zetu hutukana, wake zetu hutushutumu, watoto wetu hutudharau, na tunapokuwa wazee, binti zetu wakwe pia hututesa. Hakika hatujateseka kidogo, na kwamba sasa tunafurahia upendo mkuu wa Mungu ni furaha sana! Kama haungekuwa wokovu wa Mungu kwetu, tungewezaje kung’amua mateso ya kibinadamu? Je, si bado tungekuwa tumepakazwa matope katika dhambi hii? Je, huku si Mungu kutuinua? Mimi ni mmoja wa watu duni kabisa na Mungu ameniinua juu sana. Hata kama nitaangamia bado lazima niulipize upendo Wake. Mungu anaweza kutuheshimu na kunena uso kwa uso nasi, watu duni mno, na hata kama Yeye huniadibu—ninaweza kusema nini? Je, si kuadibu pia ni kuinua Kwake? Hata ikiwa ninaadibiwa bado naweza kuiona nguvu Yake kuu. Siwezi kuwa bila dhamiri—lazima niulipize upendo Wake. Siwezi kuwa muasi sana dhidi ya Mungu. Yeye hunena nami uso kwa uso na Hunifundisha kwa kuushika mkono wangu. Yeye huniandalia kila kitu, Huishi pamoja nami, na Huteseka pamoja nami.” Nafasi ya Mungu na hadhi Yake si sawa na ya watu, lakini mateso Yake ni sawa, na kile Anachokula na kuvaa ni sawa, ni watu wote tu humheshimu—hii ndiyo tofauti pekee. Je, si kila kitu kingine ambacho kinafurahiwa ni sawa? Hivyo mna haki gani kuwa na mengi ya kusema kulihusu? Mungu amevumilia mateso makubwa mno na kufanya kazi kubwa sana, na nyinyi—mlio chini kuliko mchwa, kuliko wadudu—mmepata kuinuliwa pakubwa leo. Ikiwa huwezi kuulipiza upendo wa Mungu, dhamiri yako iko wapi? Watu wengine hunena kutoka mioyoni mwao na kusema: “Kila wakati nikifikiri kuondoka kutoka kwa Mungu macho yangu yanajawa na machozi nami nahisi kuhukumiwa na dhamiri yangu. Mimi ni mwenye kuwiwa kwa Mungu. Siwezi kufanya hivi. Siwezi kuwa namna hiyo Kwake. Ningekufa na kufa kwangu kuipe kazi Yake utukufu, nitaridhika kupita kiasi. Vinginevyo, hata nikiishi sitahisi amani. “Sikiliza maneno haya—huu ndio wajibu ambao kiumbe anapaswa kutimiza. Ikiwa mtu anakuwa na maono haya ndani yake kila mara, atahisi kuwa dhahiri na starehe ndani yake; atakuwa na uhakika wa mambo haya. Utasema: “Mungu haniumizi na Hanifedheheshi kimakusudi wala Haniaibishi. Ingawa Ananena kwa ukali kwa kiasi fulani na huuchoma moyo, ni kwa ajili yangu mwenyewe. Ingawa Ananena kwa ukali namna hiyo, bado Ananiokoa, na Yeye bado ni mwenye huruma kwa udhaifu wangu. Hanihukumu na ukweli. Naamini kwamba Mungu ni wokovu.” Ikiwa kweli una maono haya, hutafikia kiwango cha kukimbia. Katika dhamiri yako, unaweza kuhisi kuwa umekosea, unaweza kuhisi shutuma, kwamba hupaswi kumtendea Mungu kwa namna hiyo. Unafikiri kuhusu neema yote uliyoipata, maneno yote ambayo umeyasikia—je, unaweza kuyasikiliza bure? Haijalishi ni nani anakimbia, wewe huwezi. Watu wengine hawaamini, lakini lazima wewe uamini. Watu wengine wanamtelekeza Mungu, lakini lazima wewe umtetee Mungu na kushuhudia Kwake. Wengine humkashifu Mungu, lakini wewe huwezi. Haijalishi jinsi Mungu asivyo na huruma kwako, bado unapaswa kumtendea vyema. Unapaswa kuulipiza upendo Wake na lazima uwe na dhamiri, kwa sababu Mungu hana hatia. Kuja Kwake duniani kutoka mbinguni kufanya kazi miongoni mwa wanadamu kulikuwa aibu kubwa tayari. Yeye ni mtakatifu bila uchafu hata kidogo. Kuja kwenye nchi ya uchafu—ni fedheha kiasi gani ambayo Amevumilia? Kufanya kazi ndani yenu ni kwa ajili yenu. Ikiwa huna dhamiri katika kumtendea Yeye, ingekuwa bora kufa kifo cha mapema!
Hivi sasa, watu wengi wanakosa kipengele hiki cha maono na hawawezi kabisa kuielewa kazi hii na hawajui nini Mungu anataka hasa kukamilisha kupitia kazi hii. Hasa wale waliokanganyika—ni kama wameingia katika matata mengi na kutunduwazwa baada ya zamu chache. Ukifafanua kikamilifu lengo la mpango wa usimamizi wa Mungu kwao, basi hiyo haingekuwa hivyo. Watu wengi hawawezi kulielewa, na wanaamini kwamba kazi ya Mungu ni kuwatesa watu. Hawaelewi hekima na maajabu ya kazi Yake, na hawaelewi kwamba kazi Yake ni kufichua nguvu Yake kuu, na hata zaidi ni kuwaokoa wanadamu. Hawaoni yote hayo, wao huona tu kama wana matumaini yoyote, na kama wataweza kuingia mbinguni. Wanasema: Kazi ya Mungu daima ni ya mzunguko; kama ungetufanya tu tuione hekima Yako moja kwa moja hiyo ingekuwa vizuri. Hupaswi kututesa kwa njia hii. Tunakosa sana katika ubora wa tabia na hatuyafahamu mapenzi Yako. Ingekuwa vizuri sana kama Ungenena na kutenda tu moja kwa moja. Unatufanya tukisie, lakini hatuwezi. Ingekuwa vizuri kama Ungeharakisha na kuturuhusu tuuone utukufu Wako. Nini haja ya kufanya mambo kwa njia ya mzunguko? “Kile mnachokosa sana sasa ni dhamiri. Zingatieni hili zaidi na fungueni macho yenu wazi kabisa ili muone nani hasa anayefanya hatua kwa hatua kwa kazi. Msifikie uamuzi upesi bila kutafakari. Sasa umeelewa zaidi kwa juujuu njia ya maisha unayopaswa kupitia. Bado kuna kiasi kikubwa cha ukweli ambacho unapaswa kupitia, na siku inapokuja ambapo unaweza kuuelewa kikamilifu, hutasema hivyo tena, wala hutalalamika. Wala hutaufafanua bila uzito. Utasema: "Mungu ni mwenye busara sana, mtakatifu sana. Yeye ni mwenye nguvu sana!"
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili