Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Yehova. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Yehova. Onyesha machapisho yote
Jumanne, 12 Desemba 2017
Kuhusu Biblia (1)
Mwenyezi Mungu alisema , Biblia inapaswa kuangaliwaje kuhusiana na imani kwa Mungu? Hili ni swali muhimu sana. Kwa nini tunawasiliana swali hili? Kwa sababu wakati ujao utaeneza injili na kupanua kazi ya Enzi ya Ufalme, na haitoshi tu kuweza kuzungumza juu ya kazi ya Mungu leo.
Ijumaa, 8 Desemba 2017
Kanisa la Mwenyezi Mungu | Wafaa Kujua Namna Ambavyo Ubinadamu Wote Umeendelea Hadi Siku ya Leo
Wafaa Kujua Namna Ambavyo Ubinadamu Wote Umeendelea Hadi Siku ya Leo
Mwenyezi Mungu alisema, Uzima wa kazi ya miaka 6,000 yote umebadilika kwa utaratibu kuambatana na nyakati. Mabadiliko katika kazi hii kumefanyika kulingana na hali zinazozunguka ulimwengu mzima. Kazi ya usimamizi ya Mungu imebadilika tu kwa utaratibu kulingana na mitindo ya kimaendeleo ya ubinadamu kwa ujumla; haikuwa imepangwa tayari mwanzoni mwa uumbaji. Kabla ya ulimwengu kuumbwa, au punde tu baada ya kuumbwa kwake, Yehova hakuwa amepanga bado awamu ya kwanza ya kazi, ile ya sheria; awamu ya pili ya kazi, ile ya neema; au awamu ya tatu ya kazi, ile ya kushinda, ambapo Angefanya kazi kwanza miongoni mwa kundi la watu—baadhi ya vizazi vya Moabu, na kuanzia hapa Angeweza kushinda ulimwengu mzima.
Ukaribisheni Urejeaji wa Bwana Yesu | Sifa na Ibada “Mungu Ameleta Utukufu Wake Mashariki”
Ukaribisheni Urejeaji wa Bwana Yesu | Sifa na Ibada “Mungu Ameleta Utukufu Wake Mashariki”
Mungu aliipa Israeli utukufu Wake kisha Akauhamisha mbali na pale,
na kuwaleta Waisraeli na kuwaleta watu wote Mashariki.
Mungu amewaelekeza wote kwenye mwanga
ili waweze kuungana tena na kuwa pamoja na mwanga,
wasilazimike kuutafuta tena, kuutafuta mwanga.
Mungu atawaacha wote wanaotafuta kuuona mwanga tena
na utukufu Aliokuwa nao katika Israeli,
kuona kwamba Mungu tayari ameshuka chini juu ya wingu jeupe miongoni mwa watu,
na kuona mawingu mengi meupe, na kuona vishada vya matunda,
kumwona Yehova Mungu wa Israeli, Mungu wa Israeli,
kumwona Mkuu wa Wayahudi, kumwona Masihi Aliyengojewa,
na kuonekana kamili kwa Yeye aliyeteswa na wafalme katika enzi zote.
Mungu atafanya kazi ya ulimwengu mzima na kufanya kazi kubwa,
akifichua utukufu Wake wote na matendo Yake yote kwa mwanadamu
katika siku za mwisho.
Mungu ataonyesha uso Wake uliojaa utukufu
kwa wale ambao wamemngoja Yeye kwa miaka mingi,
kwa wale ambao wametamani kumuona Yeye akija juu ya wingu jeupe,
kwa Israeli ambayo imemngoja Aonekane kwa mara nyingine tena,
kwa watu wote wanaomtesa Mungu.
Ili wote wajue kwamba Mungu kwa muda mrefu uliopita Ameuchukua utukufu Wake
na kuuleta katika Mashariki.
Hauko katika Uyahudi, kwa maana siku za mwisho tayari zimewadia!
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili
Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.
Kauli Maalum: Uzalishaji huu wa video ulitengenezwa kama mradi usio wa faida na Kanisa la Mwenyezi Mungu. Wahusika wanaoonekana katika uzalishaji huu wanafanya kwa msingi wa kutotafuta faida, na hawajalipwa kwa njia yoyote. Video hii isisambazwe kwa mtu mwingine kwa minajili ya faida, na ni matumaini yetu kwamba kila mtu atashiriki kuigawa na kuisambaza hadharani. Wakati unapoisambaza, tafadhali sisitiza chanzo chake. Bila ridhaa ya Kanisa la Mwenyezi Mungu, hakuna shirika, kundi la kijamii, au mtu binafsi anayeweza kubadilisha au kuhudhurisha visivyo maudhui ya video hii.