Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Filamu-za-Maisha-ya-Kanisa. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Filamu-za-Maisha-ya-Kanisa. Onyesha machapisho yote
Jumamosi, 2 Juni 2018
Swahili Christian Video "Kuzinduka" | Ni nini Maana ya Uzima?
Jina lake ni Chen Xi, na tangu akiwa mtoto elimu na ushawishi wa wazazi wake na shule yake zilimfanya yeye mara zote kutaka kwa tofauti na wengine na kutafuta kuwa juu ya wengine,kwa hivyo alikuwa na bidii katika masomo yake na kutia juhudi zote. Baada ya kumwamini Mungu Chen Xi alisoma maneno ya Mungu kwa wingi na akaja kuelewa kiasi fulani cha ukweli. Aliona kuwa njia pekee inayofaa katika maisha ni kumwamini na kumfuata Mungu na kuwa mtafutaji mwenye shauku, na alijitolea kwa dhati katika kutekeleza wajibu wake. Chen Xi alienda ughaibuni mwaka 2016 ili kutoroka harakati na mateso ya serikali ya Kikomunisti ya Kichina, na alihitaji kutumia Kiingereza wakati akifanya kazi yake ya kueneza injili na kutoa ushuhuda kwa kazi ya Mungu katika zile siku za mwisho. Alihisi kuheshimiwa, na kwamba alikuwa na talanta nadra. Kama vile alivyojazwa na kujiamini na alikuwa anafikiria kujitengenezea nafasi kanisani, aligundua kwamba ndugu na dada zake walishiriki ushirika kwa maneno ya Mungu kwa nuru na kwamba walikuwa na ufahamu zaidi wa Kiingereza kumliko. Yeye hakutaka kubaki nyuma, kwa hivyo ili kuwapita wengine na kutambuliwa na kupongezwa nao, alirudufu tena jitihada zake za kujifunza. Kipindi kidogo kilipita lakini bado hakuwafikia wengine. Chen Xi hakukubali ukweli huu na alijikuta akiishi kila siku kwa maumivu ya kujitahidi kwa ajili ya jina lake na faida yake binafsi. Yeye hakuwa na moyo wa kufuata ukweli au kuzingatia kuingia katika uzima, na alikuwa hasa hawezi kutekeleza wajibu wake vizuri. Alianguka kwa maono mabaya na kuvunjika moyo.... Ni wakati huo ndipo alikuja mbele za Mungu kwa sala na kusoma maneno Yake - hukumu na adhabu ya maneno Yake iliamsha nafsi yake na kumruhusu kuona wazi kiini cha sifa na hadhi pamoja na matokeo ya kufungwa na kuteswa na mambo haya. Alikuja kuelewa umuhimu wa kutekeleza wajibu wake, thamani ya kweli ya maisha, na maisha ya aina gani ndiyo ya furaha ya kweli. Kuanzia wakati huo alianza kuwa na malengo sahihi ya kufuata na kutokuwa chini ya fikira za uso au hadhi. Pia alianza kuzingatia kufuata ukweli na kutimiza wajibu wa kiumbe wa kulipa upendo wa Mungu …
Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.
Ijumaa, 1 Juni 2018
Latest Swahili Christian Video "Njia ya mwenendo wa Binadamu" | Hukumu ya Mungu iliniokoa
Latest Swahili Christian Video "Njia ya mwenendo wa Binadamu" | Hukumu ya Mungu iliniokoa
Tangu umri mdogo, wazazi wa Cheng Jianguang na walimu walimfundisha sheria kama vile "Uwiano ni hazina, uvumilivu ni wema," "Kunyamazia makosa ya rafiki wazuri hudumisha urafiki mzuri na wa muda mrefu," "Ingawa utaona makosa, ni vyema useme machache" zilikuwa ni nguzo za kudumisha uhusiano mzuri na watu wengine. Alichukua mafunzo haya kwa moyo, na kujifinza kamwe kutowakosea wengine katika matendo na mazungumzo yake, na daima kutunza uhusiano wake na wengine, hivi kumpatia sifa ya "mtu mzuri" kwa wale wliokuwa karibu naye. Baada ya kukubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika zile siku za mwisho, Cheng Jiangunag anajifunza kutoka kwa neno la Mungu kwamba ni kwa kutafuta ukweli na kuwa mtu mwaminifu pekee ndiyo anaweza kupata idhini ya Mungu na kupewa wokovu na Mungu, kwa hivyo anaapa kiapo kuwa mtu mwaminifu. Lakini, katika majukumu yake, yeye anazuiwa na tabia yake potovu, na anashindwa kujizuia kutenda kulingana na falsafa za kishetani za maisha: Wakati anapotambua kiongozi wa kanisa ambaye hatendi kulingana na ukweli katika kazi zake, ambayo inaathiri kazi ya kanisa, Cheng Jianguang anaamua kulinda uhusiano wake na kiongozi yule, na anashindwa kuwasilisha suala hilo upesi; wakati dada mmoja anapokuja kwake kutafuta jibu ambalo litamlazimu yeye kusimama imara na kulinda maslahi ya kanisa, Cheng Jianguang badala yake anachagua kusema uongo, kudanganya, na kukimbia kutoka kwa majukumu yake kwa sababu anaogopa kuwakosea wengine, kusababisha dada zake kukamatwa na serekali ya kikomunisti ya Kichina.... Alipokuwa akifunuliwa tena na tena na mambo ya kimsingi na kuhukumiwa na kufunuliwa katika neno la Mungu, Cheng Jianguang anakuja kuelewa kwamba mantiki na sheria ambazo yeye hutenda ni sumu za kishetani na kwamba jinsi anavyoishi ni tabia ya kishetani. Anakuja kuona kuwa kiini cha kuwa mtu wa ndio ni kile cha mtu mdanganyifu, mtu ambaye Mungu huchukia kabisa na kudharau, na huyo mtu wa ndio asipotubu na kubadikika, yeye bila shaka hataepuka kukataliwa na kuondolewa na Mungu. Anakuja pia kuelewa kwamba ni kwa kuwa mtu mwaminifu pekee ndipo anaweza kuwa mtu mzuri kila mara. Hivyo, yeye anajitahidi kutafuta ukweli na kuwa mtu mwaminifu, na chini ya uongozi wa neno la Mungu, hatimaye anafanikiwa kuishi kwa kudhihirisha mfano wa mtu mwaminifu na kutembea katika njia ya wokovu na Mungu.
Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.