Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Kutafakari-kwa-Kikristo. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Kutafakari-kwa-Kikristo. Onyesha machapisho yote

Alhamisi, 18 Julai 2019

Maneno ya Mungu | “Mnapaswa Kuzingatia Matendo Yenu”

Maneno ya Mungu | “Mnapaswa Kuzingatia Matendo Yenu”

Mwenyezi Mungu anasema, “Katika maisha yenu ya kila siku, mnaishi katika hali na mazingira yasiyo na ukweli ama fahamu nzuri. Hamna rasilimali ya uwepo na pia hamna msingi wa Kunijua au kujua ukweli. Imani yenu imejengwa tu juu ya ujasiri usio dhahiri au kwenye ibada za kidini na ujuzi kulingana na mafundisho ya kidini kabisa. Kila siku Ninatazama mienendo yenu na kuchunguza nia yenu na matunda yenu maovu. Sijawahi kumpata mmoja ambaye kwa kweli aliweka moyo wake na roho yake kwenye madhabahu Yangu, ambayo hayajawahi kusonga. Kwa hivyo, Singependa kuyamwaga bure maneno yote ambayo Nina nia ya kumwelezea mwanadamu wa aina hii. Moyoni Mwangu, Ninapanga kuikamilisha kazi Yangu iliyosalia tu na kuleta wokovu kwa mwanadamu ambaye Sijamwokoa bado. Hata hivyo, Ningependa wale wote wanaonifuata wapokee wokovu Wangu na ukweli ambao neno Langu linaweka katika mwanadamu. Natumaini kuwa siku moja unapofumba macho yako, utauona ulimwengu ambamo manukato yametanda hewani na vijito vya maji ya uhai vinatiririka, na wala sio dunia baridi isiyoonekana vizuri ambapo giza limetanda angani na ambamo vilio vya kughadhabisha havikomi.”
Kila siku, fikira na matendo ya kila mmoja yanachunguzwa na Yeye na, katika wakati uo huo, wamo katika matayarisho ya siku zao zinazofuata. Hii ni njia ambayo lazima kila mtu aliye hai aipitie na ambayo Nimeamulia kabla kila mmoja. Hakuna anayeweza kuepuka hili na hakuna atakayepata upendeleo. Nimezungumza maneno yasiyohesabika na zaidi ya yote Nimefanya kazi kubwa mno. Kila siku, Ninatazama vile kila mwanadamu kiasili anafanya yote ambayo anafaa kufanya kulingana na asili yake na vile inavyoendelea. Bila kujua, wengi tayari wamo katika “njia sahihi”, ambayo Niliiweka kwa ufunuo wa mwanadamu wa kila aina. Tayari Nimemweka kila aina ya mwanadamu katika mazingira tofauti tofauti, na katika sehemu zao, kila mmoja amekuwa akionyesha tabia zake za asili. Hakuna mtu wa kuwafunga, hakuna mtu wa kuwatongoza. Wako huru katika nafsi yao yote na lile wanalolieleza linakuja kwa wepesi. Kuna kitu kimoja tu ambacho huwaweka katika nidhamu, na hayo ni maneno Yangu. Kwa hivyo, kuna idadi ya wanadamu husoma tu maneno Yangu shingo upande ili mwisho wao usiwe ule wa mauti, lakini kamwe hawaweki maneno Yangu katika matendo. Kwa upande mwingine, wanadamu wengine huona ugumu kuvumilia siku bila maneno Yangu kuwaelekeza na kuwapa, kwa hivyo wao hushikilia maneno Yangu kiasili wakati wote. Muda unavyopita, wao basi hugundua siri ya maisha ya mwanadamu, hatima ya mwanadamu na thamani ya kuwa na utu. Mwanadamu si zaidi ya haya katika uwepo wa maneno Yangu, na Mimi huruhusu tu mambo yachukue mkondo wake. Sifanyi chochote kinachomlazimisha mwanadamu kuishi kulingana na maneno Yangu kama msingi wa kuwepo kwake. Na kwa hivyo wale wasiokuwa na dhamiri au thamani katika kuwepo kwao hutazama kwa kimya mambo yanavyoenda kisha wanayatupa maneno Yangu kando kwa ujasiri na kufanya vile wanavyopenda. Wanaanza kuchoshwa na ukweli na mambo yote yatokayo Kwangu. Isitoshe, wao huchoka kukaa katika nyumba Yangu. Wanadamu hawa hukaa katika nyumba Yangu kwa ufupi tu kwa ajili ya hatima zao na kuepuka adhabu, hata kama wanafanya huduma. Lakini nia zao huwa hazibadiliki, wala matendo yao. Hii huendeleza zaidi hamu zao za Baraka, hamu za njia moja kwenda katika ufalme ambako wanaweza kubakia milele, na pia njia ya kuingia mbingu ya milele. Jinsi wanavyotamani zaidi siku Yangu ije hivi karibuni, ndivyo wanavyohisi zaidi kuwa ukweli umekuwa kizingiti, kizuizi njiani mwao. Wanangoja kwa hamu kuingia katika ufalme ili wafurahie daima baraka za ufalme wa mbinguni, bila kutaka kuufuata ukweli ama kukubali hukumu na kuadibu, na zaidi ya yote, bila kuhitaji kuishi kwa utumishi katika nyumba Yangu na kufanya vile Ninavyoamuru. Wanadamu hawa hawaingii katika nyumba Yangu kuukamilisha moyo unaotaka kujua ukweli wala kufanya kazi pamoja na uongozi Wangu. Lengo lao tu ni wawe miongoni mwa wale ambao hawataangamizwa katika enzi inayofuata. Kwa hivyo nyoyo zao hazijawahi kuujua ukweli wala kujua jinsi ya kuukubali ukweli. Hii ndiyo sababu wanadamu wa aina hii hawajawahi kutia vitendoni ukweli au kujua undani wa ufisadi wao, ilhali wameishi katika nyumba yangu kama “wajakazi” mpaka mwisho. Wanangoja “kwa uvumilivu” kuja kwa siku Yangu, na hawachoki wanaporushwa huku na kule na hali ya kazi Yangu. Haijalishi bidii zao ni kubwa namna gani au ni gharama gani wamelipa, hakuna atakayeona kuwa wameteseka kwa ajili ya ukweli ama kujitoa kwa ajili Yangu. Katika mioyo yao, wanangoja kwa hamu siku ambayo Nitakomesha enzi nzee, na zaidi ya hayo, wanangoja kwa hamu kujua jinsi nguvu na mamlaka Yangu ni kuu. Kile hawajawahi kimbilia kufanya ni kujibadilisha na kufuata ukweli. Wanapenda kile kinachonichosha na kuchoshwa na kile ninachopenda. Wanangoja kwa hamu kile Ninachokuwa na kinyongo nacho lakini wakati uo huo wanaogopa kupoteza kile Ninachochukia. Wanaishi katika dunia hii yenye maovu ila hawajawahi kuwa na chuki nayo na wana hofu sana kuwa Nitaiangamiza dunia hii. Nia walizo nazo zinakanganya: Wanapendezwa na dunia hii Ninayochukia, na kwa wakati uo huo wanangoja kwa hamu Niiharibu dunia hii hivi karibuni. Kwa njia hii, wataepuka mateso ya uharibifu na wabadilishwe kuwa watawala wa enzi mpya kabla hawajapotoshwa kutoka katika njia ya kweli. Hii ni kwa sababu hawapendi ukweli na wanahofia kila kitu kitokacho Kwangu. Huenda ikawa watakuwa “watu watiifu” kwa muda mfupi kwa minajili ya kutopoteza baraka, lakini fikira zao za kungoja baraka kwa hamu na woga wao wa kuangamia na kuingia katika ziwa la moto haziwezi kukingwa kuonekana. Siku Yangu inapokaribia, hamu zao zinazidi kuimarika. Na vile janga lilivyo kubwa, ndivyo wanavyopoteza tumaini wasijue watakapoanzia ili kunifanya Nifurahi na kuzuia wasipoteze baraka ambazo wamezingoja kwa muda mrefu. Pindi mkono Wangu unapoanza kazi yake, wanadamu hawa wana hamu kuchukua hatua kuhudumu kama watangulizi. Wanafikiri tu kusonga kwa nguvu mpaka mstari wa mbele wa majeshi, wakiwa na woga mwingi kuwa Sitawaona. Wanafanya na kusema kile wanachodhani ni ukweli, bila kujua kuwa vitendo na matendo yao hayajawahi na umuhimu kwa ukweli, na kuwa hutatiza na kuingilia tu mipango Yangu. Hata ingawa wanaweza kuwa wameweka juhudi nyingi na wanaweza kuwa wa kweli katika ridhaa na nia zao kustahimili ugumu, kila wanachokifanya hakihusiani na Mimi , kwa maana Sijaona hata mara moja kwamba matendo yao yametoka kwa nia njema, na zaidi ya hayo, Sijawaona kama wameweka kitu chochote kwenye madhabahu Yangu. Hayo ndiyo matendo yao mbele Yangu kwa miaka hii mingi.
Mwanzoni, Nilitaka kuwapa ukweli zaidi, lakini kwa sababu mtazamo wenu kwa ukweli ni baridi sana na isiyojali, Nimesalimu amri. Sipendi kuona jitihada Zangu zikipotea bure, na pia Sipendi kuona watu wakishika maneno Yangu na ilhali katika kila sehemu wanafanya yale ya Kunipinga Mimi, kunidhuru Mimi, na kunikufuru. Kwa sababu ya mtazamo wenu na utu wenu, Ninawapa sehemu kidogo tu ya maneno yaliyo muhimu zaidi kwenu kama jaribio Langu kwa wanadamu. Ni mpaka sasa ndiyo Naweza thibitisha kwa hakika kwamba uamuzi na mipango Niliyoweka ni kulingana na yale mnayohitaji na kuwa mtazamo Wangu kwa wanadamu uko sawa. Miaka yenu mingi ya matendo mbele Yangu imenipa jibu ambalo Sijawahi kupata hapo awali. Na swali la jibu hili ni: “Mtazamo wa mwanadamu mbele ya ukweli na Mungu wa ukweli ni upi?” Juhudi ambazo Nimemwagia mwanadamu ni dhihirisho la kiini Changu cha kumpenda mwandamu, na vitendo na matendo ya mwanadamu mbele Yangu pia yamedhihirisha kiini cha mwanadamu cha kuchukia ukweli na kunipinga Mimi. Katika wakati wote Mimi hujali wale wote ambao wamenifuata, lakini hakuna wakati ambao wale wanaonifuata wameweza kupokea neno Langu; hawana uwezo kabisa wa kukubali hata maoni yanayotoka Kwangu. Hili ndilo hunihuzunisha zaidi ya yote. Hakuna anayeweza kunielewa na, zaidi ya hayo, hakuna anayeweza kunikubali, hata ingawa mtazamo Wangu ni wa kweli na maneno Yangu ni ya upole. Wote wanafanya kazi Niliyowaaminia kuifanya kulingana na nia yao ya asili; hawatafuti nia Zangu, wala kuuliza maombi Yangu. Bado wanadai kuwa Wananihudumia kwa uaminifu, wakati huu wote wakiwa wananiasi. Wengi wanaamini kuwa ukweli usiokubalika nao au ukweli ambao hawawezi kutia vitendoni sio ukweli. Kwa watu kama hawa, ukweli Wangu unakuwa kitu cha kukataliwa na kutupiliwa kando. Kwa wakati uo huo Ninakuwa mmoja anayetambuliwa na mwanadamu kwa neno tu kama Mungu, lakini pia kuchukuliwa kama mtu wa nje asiyekuwa ukweli, njia na uhai. Hakuna anyejua ukweli huu: Maneno yangu ndio ukweli usiobadilika milele. Mimi Ndiye msambazaji wa binadamu na kiongozi wa pekee wa mwanadamu. Thamani na maana ya maneno Yangu haibainishwi na kama yanakubaliwa au kutambuliwa na mwanadamu, ila ni kwa kiini cha maneno yenyewe. Hata kama hakuna mtu hata mmoja duniani anaweza kupokea maneno Yangu, thamani ya maneno Yangu na usaidizi wake kwa mwanadamu hayapimiki na mwanadamu yeyote. Kwa hivyo, Ninapokumbwa na wanadamu wengi wanaoasi, kukataa au kudharau kabisa maneno Yangu, msimamo Wangu ni huu tu: Wacha wakati na ukweli uwe shahidi Wangu na uonyeshe kuwa maneno Yangu ndiyo ukweli, njia na uhai. Wacha vionyeshe kuwa yote Niliyosema ni ya ukweli, na kuwa ni yale ambayo mwanadamu lazima apewe, na, zaidi ya yote, yale ambayo mwanadamu anafaa akubali. Nitawaruhusu wote wanaonifuata wajue ukweli huu: Wote wasioyakubali maneno Yangu kikamilifu, wale wasioyaweka maneno Yangu katika vitendo, wale wasiopata sababu ndani ya maneno Yangu, na wale wasiopata wokovu kwa sababu ya maneno Yangu, ni wale ambao wamehukumiwa na maneno Yangu na, zaidi ya hayo, wamepoteza wokovu Wangu, na fimbo Yangu haitaondoka kamwe miongoni mwao.
Aprili 16, 2003
Zaidi: Asili na Maendeleo ya Kanisa la Mwenyezi Mungu

Jumatatu, 15 Julai 2019

Sura ya 13. Maana ya Utendaji wa Watu Kuamua Matokeo Yao

Sura ya 13. Maana ya Utendaji wa Watu Kuamua Matokeo Yao

1. Hakuna Ambaye Angeokolewa iwapo Mungu Angeangalia Tu Maonyesho ya Asili ya Watu
Kwa sasa, utendaji wa watu unaamua matokeo yao, lakini huu utendaji ni upi? Je, unaujua? Nyinyi mnaweza kufikiri kwamba hili linarejelea tabia ya watu iliyopotoka ikijionyesha kazini mwao, lakini halimaanishi lile. Utendaji huu unanena kuhusu ikiwa unaweza kuweka ukweli kwenye vitendo au la na ikiwa unaweza kusalia mwaminifu na kujizatiti unapotenda wajibu wako au la, na vilevile mtazamo wako wa kumwamini Mungu, msimamo wako kwa Mungu, uamuzi wako wa kuteseka kwa ajili ya ugumu, mtazamo wako kwa kukubali hukumu na kupogolewa, kiwango chako cha mabadiliko na idadi ya dhambi kubwa. Haya yote yanachangia katika utendaji wako. Utendaji huu haumaanishi kiwango cha mwisho cha kufichua tabia yako iliyopotoshwa, lakini badala yake umefanikiwa kwa kiasi gani katika imani yako kwa Mungu. Iwapo matokeo ya watu yangeamuliwa kulingana na maonyesho ya asili yao, basi hakuna mtu ambaye angeokolewa. Je, hii ingekuwaje haki ya Mungu? Ikiwa wewe ni kiongozi, asili yako itajionyesha zaidi, na yeyote ambaye atajionyesha zaidi hatakuwa na uhakika sana wa kusalia. Kama hii ingeamua matokeo ya watu, basi kadiri watu wangezidi kutenda kazi katika kiwango cha juu, ndivyo wangezidi kumalizika haraka; kadiri wangezidi kuwa katika kiwango cha juu, ndivyo wangezidi kuonyesha asili yao katika kiasi kikubwa. Kama hali ingekuwa hivi, basi ni nani ambaye angethubutu kutekeleza wajibu wake? Kwa njia hii, je, haingekuwa kwamba wale ambao hawatekelezi wajibu wao wangeokolewa wote?
Utendaji huu unahusiana na ikiwa wewe ni mwaminifu na umejitoa kwa Mungu au la, ikiwa una upendo kwake au la, ikiwa unaweka ukweli kwenye matendo au la na vilevile ni katika kiwango gani ambacho umebadilika. Ni kulingana na utendaji huu kwamba hukumu yako inaamuliwa; si kulingana na kiwango cha upotovu wa tabia yako kinachojionyesha. Ukifikiria jinsi hii, umetafsiri vibaya mapenzi ya Mungu. Asili yote ya wanadamu ni sawa, ni vile tu kuna ubaya na uzuri wa ubinadamu. Hata usipoonyesha, asili yako bado ni sawa na yule anayeonyesha. Mungu Anajua vyema kilicho katika undani wa mwanadamu. Huhitaji kuficha chochote — Mungu huchunguza mioyo ya watu na mawazo. Ikiwa upotovu wako mwingi unafichuliwa wakati unapofanya kazi katika kiwango cha juu, Mungu atauona; ikiwa hutafanya kazi na usifichuliwe, je, Mungu hajui kuuhusu? Je, huku si kuamini uongo wako? Ukweli ni kwamba Mungu Anajua asili yako nje na ndani, bila kujali ulipo. Mungu Anajua vyema wale wote wanaofanya kazi yao, lakini je, si pia Ajua wale wasiofanya? Watu wengine hudhani kuwa hao viongozi walio kwenye hadhi ya juu wanachimba makaburi yao tu, kwa sababu upotovu wao mwingi utajifichua na kuonekana na Mungu pasi na kuepuka. Je, ungefichuliwa sana vile iwapo hawangeifanya kazi? Kufikiria kwa jinsi hii ni kwa upuzi! Ikiwa Mungu hauoni, basi si Hataweza kuuhukumu? Kama hali ingekuwa ile, je, haingekuwa kwamba wale ambao hawafanyi kazi wangesalia wote? Kulingana na kuelewa kwa mwanadamu, Mungu hangeona mabadiliko ya wale ambao hufanya kazi, bila kujali mabadiliko hayo ni makuu kiasi gani; Mungu Angewahukumu tu kulingana na maonyesho yao ya upotovu. Kinyume na hayo, Mungu hangewahukumu wale ambao wanaonyesha machache, licha ya kubadilika kwa kiasi kidogo. Je, unaamini kuwa hii ni haki ya Mungu? Je, mtu yeyote anaweza kusema kuwa Mungu ni mwenye haki iwapo Angefanya hili? Je, huku sio kutafasiri kubaya kwako ambako kunapelekea kuelewa kwa Mungu kubaya? Basi, je, imani yako kwa Mungu si ni ya uongo? Je, huku si kuamini kuwa Mungu sio mwenye haki daima? Je, si imani kama ile ni kufuru kwa Mungu? Ikiwa huna kitu chochote kilicho hasi na lolote jema halifichuliwi pia, bado huwezi kuokolewa. Jambo kuu ambalo huamua matokeo ya watu ni utendaji wao mwema. Lakini, hakuwezi kuwa na kitu hasi sana vilevile—kama ni kikuu kiasi cha kuleta maafa au adhabu, basi wote wataangamizwa. Kama kungekuwa jinsi mnavyofikiria, wale walio wafuasi wa kiwango cha chini wangepata wokovu mwishowe, na wale ambao ni viongozi wangekwisha. Una wajibu ambao lazima uutekeleze; lakini unapoutekeleza wajibu huo, utafichua upotovu wako licha yako mwenyewe, ni kama unakwenda kwa gilotini. Kama matokeo ya watu yangeamuliwa na asili yao, hakuna yeyote ambaye angeokolewa—kama hali kweli ingekuwa hii, basi, je, haki ya Mungu ingekuwa wapi? Haingeonekana kabisa. Nyinyi nyote mmeelewa mapenzi ya Mungu visivyo.
2. Utendaji Huu ni Kwa Ajili ya Kazi ya Mungu kwa Watu
Acheni niwape mfano: Katika shamba la miti ya matunda, mwenyewe hunyunyuzia maji na kutia mbolea, kisha husubiri matunda. Miti ambayo inazaa matunda ni mizuri na inahifahdiwa; ile ambayo haizai matunda bila shaka ni mibaya na haitahifadhiwa. Fikiria hali hii: Mti unazaa matunda, lakini una ugonjwa, na baadhi ya matawi mabaya yanahitaji kupogolewa. Je, mtu huu unapaswa kuhifadhiwa? Unapaswa kuhifadhiwa, na utakuwa mzuri baada ya kupogolewa na kutibiwa. Fikiria hali nyingine: Mti hauna maradhi, lakini hauna matunda—mti kama huu haufai kuhifadhiwa. Je, huku “kuzaa matunda” kunamaanisha nini? Kuna maana ya kazi ya Mungu kuwa na athari. Mungu anapofanya kazi kwa watu, asili yao haina vingine ila kujionyesha, na kwa ajili ya upotovu wa Shetani hawataepuka kuwa na dhambi, lakini katikati ya haya kazi ya Mungu ndani yao itazaa matunda. Ikiwa Mungu haoni hivyo, lakini Anaona tu asili ya mwanadamu ikionyeshwa, basi ule hautaitwa wokovu wa mwanadamu. Tunda la watu kuokolewa linadhihirishwa hasa katika kutekeleza wajibu kwao na kuweka ukweli kwenye matendo. Mungu huangalia kiwango cha watu cha mafanikio katika sehemu hizo na pia ukubwa wa dhambi zao. Hali hizi mbili zinachangia katika kuamua matokeo yao na ikiwa watasalia au la. Mathalani, watu wengine walikuwa wapotovu sana, wakijitolea kabisa kwa miili yao, na wala sio kwa familia ya Mungu. Hawakutumia rasilmali kwa ajili ya Mungu hata kidogo, lakini sasa wanatekeleza wajibu wao kwa shauku na wako na moyo mmoja na Mungu—kwa huu matazamo, je, kumekuwa na mabadiliko? Haya ni mabadiliko. Ni mabadiliko haya ambayo Mungu Anataka. Pia, watu wengine walipenda kusambaza mawazo walipokuwa nayo, lakini sasa wanapokuwa na mawazo mengine, wanaweza kuwa watiifu na kufuatilia ukweli, bila kuyasambaza au kufanya kinyume na Mungu. je, kumekuwa na mabadiliko? Naam! Watu wengine wanaweza kuwa wamepinga wakati mmoja waliposhughulikiwa na kupogolewa tena, lakini sasa wanapopogolewa na kushughulikiwa, wanaweza kujifahamu. Baada ya kuyakubali, wanapitia mabadiliko ya kweli—je, hii si athari? Naam! Hata hivyo, bila kujali mabadiliko yako ni makuu kiasi gani, asili yako haiwezi kubadilishwa kwa mara moja. Haiwezekani kutofichua dhambi zozote, lakini ikiwa kuingia kwako kutafanywa kwa kawaida, hata kwa uasi mwingine, utakuwa na ufahamu wake wakati huo. Ufahamu huu unaweza kukuletea mabadiliko ya mara moja na hali yako itaimarika na kuwa nzuri zaidi na zaidi. Unaweza kuwa na dhambi mara moja au mbili, lakini sio kila mara. Haya ni mabadiliko. Haimaanishi kwamba mtu aliyebadilika kwa kitengo fulani hana dhambi zozote tena; huo sio ukweli. Aina hii ya mabadiliko ina maana kuwa mtu aliyepitia kazi ya Mungu anaweza kuweka ukweli mwingi kweye vitendo na anaweza kutenda baadhi ya yale ambayo Mungu anahitaji. Dhambi zao zitapungua na kuwa chache zaidi na zaidi na matukio ya kuasi yatakuwa machache na madogo. Unaweza kuona kutokana na haya kuwa kazi ya Mungu imekuwa na athari; kile ambacho Mungu anataka ni kujionyesha kama huku ambako matokeo haya yamefanikishwa kwa watu. Hivyo, jinsi ambavyo Mungu Anashughulikia matokeo ya watu na Anavyomtendea mtu ni yenye haki kabisa, mwafaka na isiyo na mapendeleo. Unahitaji tu kutia bidii katika kutumia rasilmali yako kwa ajili ya Mungu, kuweka moyo wako wote katika kutenda ukweli ambayo unapaswa bila kusita, na Mungu hawezi kukutendea isiyo haki. Ebu fikiria: je, wale wanaoweka ukweli kwenye vitendo wanaweza kuadhibiwa na Mungu? Watu wengi wanashuku tabia ya Mungu yenye haki na wanachelea kuwa bado wataadhibiwa ikiwa wataweka ukweli kwenye vitendo; wanaogopa kuwa Mungu hataona uaminifu wao na kujitolea kwao. Watu wengine wanakuwa wa kutoonyesha hisia baada ya kupogolewa na kushughulikiwa; wanahisi wanyonge kiasi cha kutotekeleza wajibu wao na wanapoteza uaminifu wao na kujitolea kwao. Kwanini hivi? Hili kwa kiasi ni kwa ajili ya watu kukosa ufahamu kuhusu kiini cha matendo yao ambayo hupelekea kutokubali kupogolewa na kushughulikiwa. Pia kwa kiasi ni kwa ajili ya watu kutoelewa umuhimu wa kushughulikiwa na kupogolewa, wakiamini hilo kuwa ishara ya kuamuliwa kwa matokeo yao. Kwa sababu hiyo, kimakosa watu huamini kuwa wakiwa na uaminifu fulani na kujitolea kwa Mungu, basi hawawezi kushughulikiwa na kupogolewa; wakishughulikiwa, haiwezi kuwa haki ya Mungu. Kutoelewa kama huku kunawafanya wengi kutoaminika na kutojitolea kwa Mungu. Hakika, yote ni kwa sababu watu ni waongo sana; hawataki kupitia ugumu—wanataka kupata baraka kwa njia rahisi. Hawana ufahamu wa haki ya Mungu. Si kwamba Mungu hajafanya lolote la haki ama kwamba hatafanya lolote la haki, ni tu kwamba watu daima hawafikiri kwamba Anayofanya Mungu ni haki. Machoni pa wanadamu, kama kazi ya Mungu haipatani na mapenzi ya mwanadamu ama kama si matarajio yao, ina maana kuwa Yeye si mwenye haki. Watu kamwe hawatambui wakati kile wanachofanya si sahihi ama haiambatani na ukweli; katu hawatambui kwamba wanampinga Mungu. Kama Mungu hangewashughulikia ama kuwapogoa watu kwa ajili ya dhambi zao na wala kuwakaripia kwa sababu ya makosa yao, lakini daima angekuwa mtulivu, kamwe bila kuwakasirisha, daima bila kuwakosea, na daima bila kufunua makovu yao, lakini angewakubalia kula na kuwa na wakati mzuri na Yeye, basi watu hawangelalamika kuwa Mungu sio mwenye haki. Wangesema kuwa Mungu ni mwenye haki kwa unafiki. Kwa hivyo, watu bado hawaamini kuwa kile ambacho Mungu Anahitaji ni utendaji wao baada ya kubadilishwa kwao. Je, Mungu angekuwa vipi na uhakika kama wangeendelea na hayo? Kama Mungu angewasuta watu kidogo, hawangeamini tena kuwa Yeye huona utendaji wao baada ya mabadiliko. Wangeacha kuamini kuwa Yeye ni mwenye haki, na hawangekuwa na radhi kubadilishwa. Kama watu wangeendelea na hali hii, wangehadaiwa na mawazo yao wenyewe.
Soma Zaidi: Imani za Kimsingi za Kanisa la Mwenyezi Mungu