Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo kumjua-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo kumjua-Mungu. Onyesha machapisho yote

Jumapili, 20 Oktoba 2019

Matamshi ya Mungu | “Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo ya Kazi Yake” (Sehemu ya Pili)

Matamshi ya Mungu | “Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo ya Kazi Yake” (Sehemu ya Pili)

Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”. Maudhui ya video hii: Tembea katika Njia ya Mungu: Mche Mungu na Kuepuka Maovu Mungu Hutumia Majaribio Tofauti ili Kupima Kama Watu Humcha Mungu na Kujiepusha na Maovu Kutomcha Mungu na Kutojiepusha na Maovu ni Kumpinga Mungu
Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Jumatatu, 26 Agosti 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Ufahamu wako wa “Baraka” ni Upi

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Ufahamu wako wa “Baraka” ni Upi

Ingawa wale waliozaliwa katika enzi hii wametiishwa chini ya upotovu wa Shetani na mapepo wachafu sana, pia ni kweli kwamba wanaweza kupata wokovu mkuu kutokana na upotovu huu, hata mkubwa kuliko mifugo wanaotanda milima na tambarare na mali nyingi ya familia ambayo Ayubu alipata, na pia ni zaidi ya baraka ambayo Ayubu alipokea ya kumwona Yehova baada ya majaribu yake. Ilikuwa tu baada ya Ayubu kupitia jaribio la kifo ndipo angeweza kuyasikia maneno ya Yehova na angeweza kusikia sauti Yake ya mshindo kutoka mawinguni. Hata hivyo, hakuuona uso wa Yehova na hakujua tabia Yake. Kile Ayubu alipata kilikuwa tu mali ya kimwili ambayo hutoa furaha za mwili na watoto wazuri mno katika miji jirani pamoja na ulinzi kutoka kwa malaika wa mbinguni. Hakuwahi kumwona Yehova, na hata ingawa aliitwa mwenye haki, kamwe hakuijua tabia ya Yehova. Ingawa watu wa leo ni maskini kwa muda katika starehe za kimwili au wanapitia mazingira ya nje ya uhasama, Nimedhihirisha tabia Yangu ambayo Sikuwahi kuifunua kwa wanadamu katika vizazi vilivyopita, ambayo siku zote imekuwa siri, na miujiza Yangu kabla ya enzi kwa watu duni mno ambao pia Nimewapa wokovu mkuu, na hii ni mara ya kwanza ambayo Nimefanya hivyo. Sijawahi kufanya aina ya hii awali, na ingawa ninyi mko chini zaidi kuliko Ayubu, yale mmepata na yale mmeona yamemshinda Ayubu kwa mbali. Ingawa mmepitia kila aina ya mateso na maudhi, mateso hayo si kama majaribu ya Ayubu, lakini ni hukumu na kuadibu ambako watu wamepokea kwa sababu ya uasi na ukinzani wao, na kwa sababu ya tabia Yangu yenye haki. Ni hukumu yenye haki, kuadibu, na laana. Ayubu alikuwa mmoja wa Waisraeli, mmoja wa watu wenye haki aliyepokea upendo na rehema ya ajabu ya Yehova. Hakufanya vitendo viovu na hakumpinga Yehova; badala yake, alijitoa kwa Yehova kwa uaminifu, naye alitiishwa chini ya majaribu kwa sababu ya haki yake, na alipitia majaribu makali kwa sababu alikuwa mtumishi mwaminifu wa Yehova. Watu leo wako chini ya hukumu na laana Yangu kwa sababu ya uchafu na uovu wao. Ingawa mateso yao hayalingani kabisa na kile Ayubu alipitia wakati alipoteza mifugo wake, mali yake, watumishi wake, watoto wake, na wale walio wapendwa kwake wote, kile watu wanapitia ni usafishaji na uteketezaji mkali; kilicho kikubwa zaidi kuliko kile Ayubu alipitia ni kwamba aina hii ya jaribio haipunguzwi wala kuondolewa kwa sababu ya udhaifu wao, badala yake, ni ya muda mrefu hadi siku yao ya mwisho ya maisha. Hii ni adhabu, hukumu, laana—ni ya kuteketea bila huruma, na hata zaidi ni “urithi” wa wanadamu wa haki. Ni kile wanachostahili, na ni mahali pa maonyesho ya tabia Yangu yenye haki. Ni ukweli unaojulikana. Lakini yale watu wamepata yanapita sana yale wamevumilia sasa. Yale ambayo mmepitia ni vipingamizi tu kutokana na upumbavu, lakini mapato yenu ni mara mia zaidi ya mateso yenu. Kwa mujibu wa sheria za Israeli katika Agano la Kale, wale wote wanaonipinga Mimi, wale wote wanaonihukumu waziwazi, na wale wote wasioifuata njia Yangu lakini wanatoa sadaka zenye kukufuru Kwangu kwa ujasiri kwa hakika wataharibiwa kwa moto katika hekalu, au baadhi ya watu waliochaguliwa watawatupia mawe hadi kifo, na hata vizazi vyao vya nyumba yao wenyewe na jamaa zao wengine wa karibu watapitia laana Yangu, na katika dunia ijayo hawatakuwa huru, lakini watakuwa watumwa wa watumwa Wangu, Nami nitawaelekeza hadi uhamishoni miongoni mwa Mataifa nao hawataweza kurudi katika nchi yao. Kulingana na vitendo vyao, tabia zao, mateso yanayovumiliwa na watu leo si makubwa kama adhabu waliyopitia Waisraeli. Kusema kuwa kile mnachopitia sasa ni adhabu si bila sababu, na hii ni kwa sababu mmevuka mpaka kweli, na kama mngekuwa katika Israeli mngekuwa mmoja wa wenye dhambi milele na mngekatwa vipande vipande na Waisraeli muda mrefu uliopita na pia mngeteketezwa kwa moto kutoka mbinguni katika hekalu la Yehova. Na nini ambacho mmepata sasa? Nini ambacho mmepokea, nini ambacho mmefurahia? Nimedhihirisha tabia Yangu yenye haki ndani yenu, lakini muhimu zaidi ni kwamba Nimefunua uvumilivu Wangu kwa ukombozi wa mwanadamu. Mtu angesema kwamba yote ambayo Nimefanya ndani yenu ni kazi na uvumilivu, kwamba ni kwa ajili ya usimamizi Wangu, na hata zaidi ni kwa ajili ya starehe ya wanadamu.
Ingawa Ayubu alipitia majaribu kutoka kwa Yehova, alikuwa tu mtu mwenye haki aliyemwabudu Yehova, na hata alipokuwa akipitia majaribu hayo hakulalamika kumhusu Yeye, lakini alithamini sana kukutana kwake na Yehova. Watu wa leo hawathamini tu uwepo wa Yehova, bali humkataa, humchukia sana, hulalamika kumhusu, na hudhihaki uwepo Wake. Je, hamjapata zaidi ya kidogo? Je, mateso yenu kweli hayajakuwa makubwa sana? Je, baraka zenu hazijakuwa nyingi kuliko zile za Maria na Yakobo? Je, upinzani wenu haujakuwa hafifu? Inawezekana kuwa yale Nimehitaji kwenu, yale Nimeuliza kutoka kwenu yamekuwa makuu mno na mengi sana? Ghadhabu Yangu iliachiliwa huru tu juu ya wale Waisraeli walionipinga Mimi, si moja kwa moja juu yenu, lakini kile ambacho mmepata kimekuwa tu hukumu Yangu isiyo na huruma na mafichuzi pamoja na utakaso mkali usio na huruma. Licha ya haya watu bado wananipinga na kunikana Mimi bila hata chembe ya utii. Na hata kuna baadhi ya watu ambao hujitenga na Mimi na kunikataa; aina hiyo ya mtu si bora zaidi kuliko bendi ya Kora na Dathani wakimpinga Musa. Mioyo ya watu imekuwa migumu sana, na asili zao ni kaidi sana. Kamwe hawatabadili mienendo yao ya zamani. Wamejiweka wazi kama kahaba hadharani kwa matamshi Yangu, na maneno Yangu ni makali sana kwamba “hayana adabu”, yakiweka wazi asili za watu hadharani. Lakini watu huamkia tu kwa vichwa vyao, wanamwaga machozi machache, na kuwa na hisia za kusikitisha kidogo tu. Mara tu inapoisha, ni wakali kama mfalme wa wanyama wa pori katika milima na hawana utambuzi kabisa. Je, watu na aina hii ya tabia wanawezaje kujua kwamba wamefurahia baraka zaidi ya mara mia kuliko zile za Ayubu? Wanawezaje kugundua kwamba kile wanachokifurahia ni baraka ambazo zimeonekana katika enzi zote kwa nadra sana, ambazo hakuna mtu aliyewahi kuzifurahia awali? Dhamiri za watu zinawezaje kuhisi aina hii ya baraka ambayo hubeba adhabu? Kusema ukweli, chote Ninachohitaji kwenu ni ili muweze kuwa mifano kwa kazi Yangu na kuwa mashahidi kwa ajili ya tabia Yangu yote na matendo Yangu yote, na ili muweze kuwekwa huru kutokana na mateso ya Shetani. Lakini wanadamu daima huchukizwa na kazi Yangu na wanakuwa na uhasama kwake kimakusudi. Aina hiyo ya mtu anawezaje kutonichochea Mimi kurejesha sheria za Israeli na kuleta juu yake ghadhabu Yangu kwa ajili ya Israeli? Ingawa kuna wengi miongoni mwenu ambao ni “watiifu” Kwangu, kuna hata zaidi ambao wa namna ya “bendi ya Kora” Mara tu Nitakapoupata utukufu Wangu kamili, Nitachukua moto kutoka mbinguni na kuwateketeza hadi wawe majivu. Mnapaswa kujua kwamba Sitawaadibu watu kwa maneno Yangu tena, lakini kabla ya kuifanya kazi ya Israel, Nitaiteketeza kabisa ile namna ya “bendi ya Kora” wanaonipinga Mimi na ambao Nimewaondoa muda mrefu uliopita. Wanadamu hawatapata tena nafasi ya kunifurahia, lakini yote ambayo wataona yatakuwa ghadhabu na “moto” Wangu kutoka mbinguni. Nitafichua matokeo ya watu wote, na Nitawagawanya watu wote katika makundi mbalimbali. Nitaangalia kila tendo lao lenye uasi, na kisha kuimaliza kazi Yangu, ili matokeo ya watu yataamuliwa kulingana na uamuzi Wangu wakati wako duniani pamoja na mitazamo yao kunihusu. Wakati huo utakapofika, hakutakuwa na kitu kitakachoweza kubadilisha matokeo yao. Acha watu wafunue matokeo yao wenyewe! Acha Niyakabidhi matokeo ya watu kwa Baba wa mbinguni.
Soma Zaidi :Umeme wa Mashariki Unatoka Wapi?

Jumapili, 21 Julai 2019

Kupata Mwili Mara Mbili Kunakamilisha Umuhimu wa Kupata Mwili.

5. Kupata Mwili Mara Mbili Kunakamilisha Umuhimu wa Kupata Mwili

Maneno Husika ya Mungu:
Kupata mwili mara ya kwanza kulikuwa kumkomboa mwanadamu kutoka katika dhambi kupitia mwili wa Yesu, hivyo, Aliokoa mwanadamu kutoka kwa msalaba, lakini tabia potovu ya kishetani ilibaki ndani ya mwanadamu. Kupata mwili mara ya pili si kwa ajili ya kuhudumu tena kama sadaka ya dhambi ila ni kuwaokoa kamilifu wale waliokombolewa kutoka kwa dhambi. Hii inafanyika ili wale waliosamehewa wakombolewe kutoka kwa dhambi zao, na kufanywa safi kabisa, na kupata mabadiliko ya tabia, hivyo kujikwamua kutoka kwa ushawishi wa Shetani wa giza na kurudi mbele za kiti cha enzi cha Mungu. Hivyo tu ndivyo mwanadamu ataweza kutakaswa kikamilifu. Mungu Alianza kazi ya wokovu katika Enzi ya Neema baada ya Enzi ya Sheria kufika mwisho. Ni mpaka siku za mwisho tu ambapo Mungu Ametakasa binadamu kikamilifu kwa kufanya kazi ya hukumu na kuadibu mwanadamu kwa kuwa muasi, ndipo Mungu atakamilisha kazi Yake ya wokovu na kupumzika. Kwa hivyo, katika hatua tatu za kazi, ni mara mbili tu ndipo Mungu Alikuwa mwili ili kufanya kazi Yake kati ya mwanadamu Mwenyewe. Hiyo ni kwa sababu moja tu kati ya hatua tatu za kazi ni kuwaongoza wanadamu katika maisha yao, ilhali zingine mbili ni kazi ya wokovu. Mungu Anapokuwa mwili tu ndipo Atakapoishi pamoja na mwanadamu, kuzoea mateso ya dunia, na kuishi katika mwili wa kawaida. Katika hali hii tu ndipo Ataweza kumpatia mwanadamu wa uumbaji Wake neno la matendo wanalohitaji. Mwanadamu anapokea wokovu kamili kutoka kwa Mungu kwa sababu ya Mungu mwenye mwili, sio moja kwa moja kutoka kwa maombi yao kwenda mbinguni. Kwani mwanadamu ni mwenye mwili; mwanadamu hawezi kuona Roho wa Mungu na pia kutoweza kumkaribia. Kile tu mwanadamu anaweza kushiriki na mwili wa Mungu; kupitia Yeye tu ndipo mwanadamu ataweza kuelewa maneno yote, na ukweli wote, na kupokea wokovu kamili. Kupatikana kwa mwili mara ya pili kunatosha kumaliza dhambi za mwanadamu na kumtakasa mwanadamu. Hivyo, kupatikana kwa mwili mara ya pili kutafikisha tamati kazi yote ya Mungu mwenye mwili na kukamilisha umuhimu wa Mungu kupata mwili. Baada ya hapo, kazi ya Mungu mwenye mwili itakuwa imefika mwisho kabisa. Baada ya kupata mwili mara ya pili, hatakuwa mwili tena kwa kazi Yake. Kwani usimamizi Wake wote utakuwa umefika mwisho. Katika siku za mwisho, mwili Wake utakuwa umepata watu Wake teule kabisa, na yote mwanadamu katika siku za mwisho watakuwa wamegawanywa kulingana na aina yao. Hatafanya kazi ya wokovu tena, wala Hatarudi kuwa mwili ili kutekeleza kazi yoyote.

kutoka katika “Fumbo la Kupata Mwili (4)” katika Neno Laonekana katika Mwili

Yesu Alipokuwa Akifanya kazi Yake, maarifa ya mwanadamu juu Yake yalikuwa bado hayakuwa bayana na hayakuwa wazi. Mwanadamu aliamini kila wakati kuwa Alikuwa Mwana wa Daudi na kumtangaza kuwa nabii mkuu na Bwana mwema Aliyezikomboa dhambi za mwanadamu. Wengine, wakiwa na msingi wa imani, wakaponywa tu kwa kugusa vazi Lake; vipofu wakaona na hata wafu kurejeshwa katika uhai. Hata hivyo, mwanadamu hangeweza kutambua tabia potovu za kishetani zilizokita mizizi ndani yake na pia mwanadamu hakujua jinsi ya kuitoa. Mwanadamu alipokea neema nyingi, kama amani na furaha ya mwili, baraka ya familia nzima juu ya imani ya mmoja, na kuponywa magonjwa, na mengine mengi. Yaliyobaki ni matendo mema ya mwanadamu na kuonekana kwa kiungu; kama mwanadamu angeishi katika huo msingi, alichukuliwa kama muumini mzuri. Waumini hao tu ndio wangeingia mbinguni baada ya kifo, hii ina maana kuwa walikuwa wameokolewa. Lakini katika maisha yao, hawakuelewa kamwe njia ya maisha. Walitenda tu dhambi, na kisha kukiri kila wakati bila njia ya kuielekea tabia iliyobadilika; hii ndiyo ilikuwa hali ya mwanadamu katika Enzi ya Neema. Je mwanadamu amepokea wokovu kamili? La! Kwa hivyo, hatua ilipokamilika, bado kuna kazi ya hukumu na kuadibu. Hatua hii inamfanya mwanadamu kuwa safi kupitia neno ili kumpatia mwanadamu njia ya kufuata. Hatua hii haingekuwa na matunda ama ya maana kama ingeendelea na kukemea mapepo, kwani msingi wa dhambi wa mwanadamu haungetupwa mbali na mwanadamu angekoma tu baada ya msamaha wa dhambi. Kupitia kwa sadaka ya dhambi, mwanadamu amesamehewa dhambi zake, kwani kazi ya kusulubisha imefika mwisho na Mungu Ametawala juu ya Shetani. Lakini tabia potovu ya wanadamu bado imebaki ndani yao na mwanadamu anaweza kutenda dhambi na kumpinga Mungu; Mungu hajampata mwanadamu. Hiyo ndio sababu katika hatua hii ya kazi Mungu Anatumia neno kutangaza tabia potovu ya mwanadamu na kumuuliza mwanadamu kutenda kulingana na njia sahihi. Hatua hii ni ya maana zaidi kuliko zile za awali na pia yenye mafanikio zaidi, kwani wakati huu ni neno ambalo linatoa maisha moja kwa moja kwa mwanadamu na linawezesha tabia ya mwanadamu kubadilishwa kabisa; ni hatua ya kazi ya uhakika kabisa. Kwa hivyo, Mungu kupata mwili katika siku za mwisho imekamilisha umuhimu wa Mungu kupata mwili wa Mungu na kukamilisha usimamizi wa Mungu katika mpango wa kuokoa mwanadamu.

kutoka katika “Fumbo la Kupata Mwili (4)” katika Neno Laonekana katika Mwili

Mungu mwenye mwili wa kwanza Hakukamilisha kazi ya kupata mwili; Alikamilisha tu hatua ya kwanza ya kazi iliyokuwa lazima kwa Mungu kuifanya katika mwili. Kwa hivyo, ili kuimaliza kazi ya kupata mwili, Mungu Amerudi katika mwili kwa mara nyingine tena, Akiishi kulingana na ukawaida na uhalisia wote wa mwili, yaani, kuifanya kazi ya Mungu ijitokeze katika mwili wa kawaida kabisa, na kwa njia hiyo Anahitimisha kazi Aliyoiacha bila kukamilisha katika mwili. Mwili wa pili uliopatikana kimsingi ni sawa na ule wa kwanza, lakini ni halisi zaidi, wa kawaida kabisa kuliko ule wa kwanza. Kwa sababu hiyo, mateso unayoyapitia mwili wa pili uliopatikana ni makubwa kuliko yale ya ule wa kwanza, ila mateso haya ni kwa sababu ya huduma Yake katika mwili, ambayo ni tofauti na mateso ya mwanadamu mwovu. Vilevile yanachipuka kutokana na ukawaida na uhalisi wa mwili Wake. Kwa kuwa Anatekeleza huduma Yake katika mwili wa kawaida na halisi kabisa, mwili ni sharti upitie mateso mazito. Kadiri mwili ulivyo wa kawaida na halisi, ndivyo unateseka zaidi katika utekelezaji wa huduma Yake. Kazi ya Mungu inaonyeshwa katika mwili wa kawaida sana, mwili ambao si wa rohoni kamwe. Kwa kuwa mwili Wake ni wa kawaida, na ni lazima ubebe kazi ya kumwokoa mwanadamu, Anateseka hata zaidi kuliko ambavyo mwili wa rohoni unaweza kuteseka—mateso haya yote yanatokana na uhalisi na ukawaida wa mwili Wake. Kutokana na mateso yaliyopitiwa na hii miili miwili iliyopatikana wakati wa kutekeleza huduma Zao, mtu anaweza kuona kiini cha mwili uliopatikana. Kadiri mwili ulivyo wa kawaida, ndivyo Anapata mateso mazito Afanyapo kazi, kadri mwili unaofanya kazi unavyokuwa wa kweli, ndivyo maoni ya watu yanaendelea kuwa makali, na hatari zinazomkabili zinaendelea kuongezeka. Lakini, kadiri mwili ulivyo halisi, kadiri mwili unavyokuwa na hali kamili ya binadamu wa kawaida, ndivyo Anaweza zaidi kuifanya kazi ya Mungu katika mwili. Ulikuwa mwili wa Yesu ulioangikwa msalabani, mwili Wake Alioutoa kama kafara kwa dhambi; ni kupitia kwa mwili wenye ubinadamu wa kawaida ndipo Aliweza kumshinda Shetani na kumkomboa kabisa mwanadamu kutoka msalabani. Ni kupitia mwili kamili ndipo Mungu katika mwili mara ya pili Anatekeleza kazi ya ushindi na kumshinda Shetani. Ni mwili tu wa kawaida na halisi kabisa unaoweza kutekeleza kazi ya ushindi kwa ukamilifu wake na kutoa ushuhuda wa nguvu. Hii ni sawa na kusema kwamba kazi ya[a] kumshinda mwanadamu inafanywa kuwa bora kupitia uhalisia na ukawaida wa mwili wa Mungu, si kupitia miujiza mikuu na ufunuo. Huduma ya huyu Mungu mwenye mwili ni ya kunena na kwa njia hiyo inamshinda mwanadamu na kumfanya mkamilifu; kwa maneno mengine, kazi ya Roho Aliyejitokeza katika mwili, wajibu wa mwili, ni kunena na kupitia kwa hili kumshinda, kumfichua, kumfanya kuwa kamilifu, na kumwondoa mwanadamu kabisa. Kwa hivyo, ni katika kazi ya kushinda ambapo kazi ya Mungu katika mwili itatimiziwa kwa ukamilifu. Kazi ya ukombozi ya kwanza ilikuwa mwanzo tu wa kazi ya kupata mwili kwa Yesu; mwili unaofanya kazi ya kushinda utaikamilisha kazi nzima ya kupata mwili kwa Yesu. Kijinsia, mmoja ni mwanamke na mwingine ni mwanamume; kwa hili, maana ya kupata mwili kwa Mungu imekamilishwa. Mawazo mabaya ya mwanadamu kumhusu Mungu yameondolewa: Mungu Anaweza kuwa mwanamke na mwanamume, na kimsingi Mungu mwenye mwili Hana jinsia. Alimuumba mwanamume na mwanamke, na Hatofautishi kati ya hizi jinsia. Katika hatua hii ya kazi, Mungu Hafanyi ishara na miujiza, ili kwamba kazi iweze kutimiza matokeo yake kupitia kwa maneno. Sababu ya jambo hili, aidha, ni kwa maana kazi ya Mungu mwenye mwili mara hii si kuponya wagonjwa na kufukuza mapepo, ila kumshinda mwanadamu kupitia kunena, ikiwa na maana kwamba uwezo asili uliomo kwenye huu mwili uliopatikana wa Mungu ni kunena maneno na kumshinda mwanadamu, si kuponya wagonjwa na kufukuza mapepo. Kazi Yake katika ubinadamu wa kawaida si kutenda miujiza, si kuponya wagonjwa na kufukuza mapepo, ila ni kunena, na kwa hivyo Yesu kupata mwili kwa mara ya pili kunaonekana kwa watu kuwa kawaida zaidi ya mara ya kwanza. Watu wanaona kuwa Mungu kupata mwili si uongo; lakini huyu Mungu mwenye mwili ni tofauti na Yesu Aliyekuwa mwili, na japo wote ni Mungu wenye mwili, Hawako sawa kabisa. Yesu Alikuwa na ubinadamu wa desturi, ubinadamu wa kawaida, lakini Aliambatana na ishara nyingi na miujiza. Katika huyu Mungu mwenye mwili, macho ya mwanadamu hayataona ishara au miujiza, wala kuponya wagonjwa au kufukuza mapepo, wala kutembea juu ya bahari, wala kufunga kwa siku arobaini… Hafanyi kazi sawa na Aliyoifanya Yesu, si kwa kuwa mwili Wake kimsingi ni tofauti na ule wa Yesu, ila ni kwa sababu si huduma Yake kuponya wagonjwa na kufukuza mapepo. Haharibu kazi Yake mwenyewe, Havurugi kazi Yake mwenyewe. Kwa kuwa anamshinda mwanadamu kwa maneno Yake halisi, haina haja ya kumhini kwa miujiza, na kwa hivyo hii hatua ni kukamilisha kazi ya kupata mwili.

kutoka katika “Kiini cha Mwili Ulio na Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili

Kwa nini Ninasema kuwa maana ya kupata mwili haikukamilishwa katika kazi ya Yesu? Ni kwa sababu Neno halikuwa Mwili kikamilifu. Kilichofanywa na Yesu kilikuwa tu sehemu moja ya kazi ya Mungu katika mwili; Alifanya tu kazi ya ukombozi na Hakufanya kazi ya kumpata mwanadamu kikamilifu. Kwa sababu hii, Mungu Amekuwa mwili mara nyingine tena katika siku za mwisho. Hatua hii ya kazi, pia inafanywa katika mwili wa kawaida, ikifanywa na mwanadamu wa kawaida kabisa, ambaye ubinadamu wake haupiti mipaka ya ubinadamu. Kwa maneno mengine, Mungu Amekuwa mwanadamu kamili, na ni mtu ambaye utambulisho wake ni ule wa Mungu, mwanadamu kamili, mwili kamili, Ambaye Anatekeleza kazi. Katika jicho la mwanadamu, Yeye ni mwili tu ambao haujapita mipaka ya ubinadamu hata kidogo, mwanadamu wa kawaida kabisa Anayeweza kuzungumza lugha ya mbinguni, Ambaye Haonyeshi ishara za kimiujiza, Hafanyi miujiza, sembuse kuweka wazi ukweli wa ndani kuhusu dini katika kumbi kuu za mikutano. Kazi ya kupata mwili kwa mara ya pili inaonekana kwa wanadamu kuwa tofauti kabisa na ile ya kwanza, kiasi kwamba kazi hizi mbili zinaonekana kutokuwa na uhusiano wowote, na hakuna chochote katika kazi ya kwanza kinachoweza kuonekana wakati huu. Japo kazi ya kupata mwili kwa mara ya pili ni tofauti na ile ya kwanza, hili halithibitishi kuwa chanzo Chao si kimoja na sawa. Iwapo chanzo Chao ni kimoja inategemea aina ya kazi iliyofanywa na miili na si katika maumbo Yao ya nje. Katika hatua tatu za kazi Yake, Mungu Amekuwa mwili mara mbili, na mara zote kazi ya Mungu kuwa mwili inaanzisha enzi mpya, inaanzisha kazi mpya; kuwa mwili kwa mara ya kwanza na pili kunakamilishana. Macho ya wanadamu hayawezi kugundua kuwa hii miili miwili kwa kweli imetokana na chanzo kimoja. Ni wazi kwamba hili liko nje ya uwezo wa macho ya wanadamu au akili za wanadamu. Ila katika kiini Chao, ni miili sawa, kwani kazi Yao inatokana na Roho mmoja. Iwapo hii miili miwili inatokana na chanzo kimoja haiwezi kuamuliwa kutokana na enzi na sehemu Ilipozaliwa, au vigezo vingine kama hivyo, ila kwa kazi ya uungu iliyoonyeshwa Nayo. Kupata mwili wa pili hakufanyi kazi yoyote iliyofanywa na Yesu, kwani kazi ya Mungu haifuati makubaliano, lakini kila wakati inafungua njia mpya. Kupata mwili wa pili hakulengi kuongeza au kuimarisha maono ya kupata mwili wa kwanza katika akili za watu, ila kuutimiza na kuukamilisha, kuongeza kina cha wanadamu kumwelewa Mungu, kuvunja sheria zote ambazo zipo katika mioyo ya watu, na kufuta picha za uongo kuhusu Mungu mioyoni mwao. Ni wazi kuwa hakuna hatua yoyote ya kazi ya Mungu mwenyewe inaweza kumpa mwanadamu ufahamu kamili wa Mungu; kila mojawapo inatoa kwa sehemu tu, si ufahamu mzima. Japo Mungu Ameonyesha tabia Yake kikamilifu, kwa sababu ya upungufu wa ufahamu wa wanadamu, ufahamu wake kuhusu Mungu si kamili. Haiwezekani, kutumia lugha ya wanadamu, kueleza tabia nzima ya Mungu; basi hatua moja tu ya kazi Yake itamwelezaje Mungu kikamilifu? Anafanya kazi katika mwili kwa kujisetiri katika ubinadamu Wake wa kawaida, na mtu anaweza kumjua tu kupitia kwa maonyesho ya uungu Wake, si kupitia kwa umbo Lake la kimwili. Mungu Anakuja katika mwili kumruhusu mwanadamu Amjue kupitia kazi Zake mbalimbali, na hakuna hatua mbili za kazi Yake zinafanana. Ni kwa njia hii tu mwanadamu anaweza kuwa na ufahamu kamili wa kazi ya Mungu katika mwili, si kwa kujifunga katika kipengele kimoja tu.

kutoka katika “Kiini cha Mwili Ulio na Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili

Yesu alifanya hatua ya kazi ambayo ilitimiza tu kiini cha “Neno alikuwako kwa Mungu”: Ukweli wa Mungu ulikuwako kwa Mungu, na Roho wa Mungu alikuwa na mwili na alikuwa asiyetenganishwa kutoka Kwake, yaani, mwili wa Mungu mwenye mwili ulikuwa na Roho wa Mungu, ambalo ni thibitisho kuu zaidi kwamba Yesu mwenye mwili alikuwa aliyepata mwili wa kwanza wa Mungu. Hatua hii ya kazi ilitimiza maana ya ndani ya “Neno lapata mwili,” ilichangia kwenye maana ya kina zaidi ya “naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu,” na inakuruhusu wewe uamini kwa uthabiti maneno haya kwamba “Hapo mwanzo kulikuwako na Neno.” Ambalo ni kusema, wakati wa uumbaji Mungu alikuwa na maneno, Maneno Yake yalikuwa na Yeye na yasiyotenganishwa kutoka Kwake, na enzi ya mwisho inafanya nguvu na mamlaka ya maneno Yake yawe hata wazi zaidi, na kumkubalia mwanadamu kuyaona maneno Yake yote—kuyasikia maneno Yake yote. Hiyo ndiyo kazi ya enzi ya mwisho. Lazima uyajue mambo haya yote kabisa. Si suala la kuujua mwili, bali la kuujua mwili na Neno. Hiki ndicho kile unachotakiwa kushuhudia, kile ambacho kila mtu lazima akijue. Kwa sababu hii ni kazi ya kupata mwili kwa pili—na mara ya mwisho ambapo Mungu anapata mwili—inakamilisha kwa ukamilifu umuhimu wa kupata mwili, inatekeleza kabisa na kutoa kazi yote ya Mungu katika mwili, na kumaliza enzi ya Mungu kuwa katika mwili.

kutoka katika “Utendaji (4)” katika Neno Laonekana katika Mwili

Ikiwa katika hii hatua Mungu mwenye mwili Anapitia ugumu au Anatekeleza huduma Yake, Anafanya hivyo ili kukamilisha maana ya kupata mwili, kwani huku ndiko Mungu kupata mwili kwa mara ya mwisho. Mungu Anaweza kuwa mwili mara mbili tu. Hakuwezi kuwepo mara ya tatu. Kuwa mwili kwa mara ya kwanza Alikuwa ni wa kiume, wa pili ni wa kike, na kwa hivyo sura ya mwili wa Mungu imekamilika katika akili za mwanadamu; aidha, huku kuwa mwili mara mbili tayari kumemaliza kazi ya Mungu katika mwili. Mara ya kwanza, Mungu mwenye mwili Alikuwa na ubinadamu wa kawaida, ili kukamilisha maana ya kupata mwili. Mara hii vilevile Ana ubinadamu wa kawaida ila maana ya huku kupata mwili ni tofauti: ni kwa kina, na kazi Yake ni ya umuhimu mkubwa. Sababu ya Mungu kuwa mwili tena ni kukamilisha maana ya kupata mwili. Mungu Akiikamilisha kabisa hii hatua ya kazi Yake, maana nzima ya kupata mwili, yaani, kazi ya Mungu katika mwili, itakuwa imekamilika, na hakutakuwa na kazi nyingine ya kufanywa katika mwili. Yaani, tangu sasa Mungu Hatawahi tena kuja katika mwili kufanya kazi Yake.

kutoka katika “Kiini cha Mwili Ulio na Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili

(Fungu Lililochaguliwa la Neno la Mungu)

Kupata Mwili Mara Mbili Kunakamilisha Umuhimu wa Kupata Mwili

Kila hatua ya kazi iliyofanywa na Mungu ina umuhimu wake mkubwa. Yesu alipokuja zamani, Alikuwa mwanaume, lakini Mungu anapokuja wakati huu Yeye ni mwanamke. Kutokana na hili, unaweza kuona kwamba Mungu aliwaumba mwanaume na mwanamke kwa ajili ya kazi Yake na Kwake hakuna tofauti ya jinsia. Roho Wake anapowasili, Anaweza kuchukua mwili wowote kwa matakwa Yake na mwili huo unaweza kumwakilisha Yeye. Uwe wa kiume au kike, unaweza kumwakilisha Mungu alimradi tu ni mwili Wake wa nyama. Kama Yesu angeonekana kama kike alipokuja, kwa maneno mengine, iwapo mtoto wa kike, sio wa kiume, angezaliwa kwa njia ya Roho Mtakatifu, hatua hiyo ya kazi ingekuwa imekamilika pia. Kama hali ingekuwa hivyo, basi hatua ya leo ya kazi ingelazimika kukamilishwa badala yake na mwanaume, lakini kazi ingekamilika pia. Kazi inayofanywa katika hatua hizi zote ni muhimu kwa kiwango sawa; hakuna hatua yoyote ya kazi inayojirudia au kupingana na nyingine. Wakati huo, Yesu alipokuwa akifanya kazi Yake aliitwa Mwana wa pekee, na “Mwana” inaashiria jinsia ya kiume. Basi kwa nini Mwana wa pekee halikutajwa katika hatua hii? Hii ni kwa sababu mahitaji ya kazi yamelazimisha badiliko la jinsia ambayo ni tofauti na ile ya Yesu. Kwa Mungu hakuna tofauti ya jinsia. Kazi Yake inafanywa kama Anavyotaka na katika kufanya kazi Yake hazuiliwi na kitu chochote kile, lakini hasa yupo huru. Hata hivyo, kila hatua ya kazi ina umuhimu wake mkubwa. Mungu alipata mwili mara mbili, na ni dhahiri kwamba kupata mwili Kwake katika siku za mwisho ni mara ya mwisho. Amekuja kufichua matendo Yake yote. Ikiwa katika hatua hii Hakupata mwili ili Yeye binafsi afanye kazi kwa ajili ya mwanadamu kushuhudia, mwanadamu milele angeshikilia fikra kwamba Mungu ni wa kuime tu, na si wa kike. Kabla ya hili, wanadamu wote waliamini kwamba Mungu angeweza kuwa tu mwanaume na kwamba mwanamke hawezi kuitwa Mungu, maana wanadamu wote walimchukulia mwanamume kuwa na mamlaka juu ya mwanamke. Waliamini kwamba hakuna mwanamke anayeweza kuchukua mamlaka, bali ni mwanamume tu. Aidha hata walisema kwamba mwanamume alikuwa ni mkuu wa mwanamke na kwamba mwanamke anapaswa kumtii mwanaume na asimshinde. Iliposemwa hapo nyuma kwamba mwanamume alikuwa mkuu wa mwanamke, ilielekezwa kwa Adamu na Hawa ambao walikuwa wamedanganywa na yule nyoka, na wala sio kwa mwanamume na mwanamke kama walivyoumbwa na Yehova hapo mwanzo. Bila shaka, mwanamke anapaswa kumtii na kumpenda mume wake, na mume anapaswa kujifunza kuilisha na kuiruzuku familia yake. Hizi ni sheria na kanuni zilizowekwa na Yehova ambazo kwazo wanadamu wanapaswa kuzifuata katika maisha yao ya hapa duniani. Yehova alimwambia mwanamke “Ashiki yako itakuwa kwa mume wako, na atatawala juu yako.” Alisema hivyo tu ili kwamba wanadamu (yaani, mwanamume na mwanamke) waweze kuishi maisha ya kawaida chini ya utawala wa Yehova, na tu ili kwamba maisha ya wanadamu yaweze kuwa na mfumo na yasipoteze mwelekeo. Kwa hivyo, Yehova alitengeneza kanuni zinazofaa ya namna ambavyo mwanamume na mwanamke wanavyopaswa kutenda, lakini hili lilihusu tu viumbe wote wanaoishi duniani na halikuhusiana na mwili wa Mungu wa nyama. Inawezekanaje Mungu awe sawa na viumbe Wake? Maneno Yake yalielekezwa tu kwa wanadamu wa viumbe Wake; Alianzishia mwanamume na mwanamke kanuni ili wanadamu waweze kuishi maisha ya kawaida. Hapo mwanzo, Yehova alipoumba wanadamu, Aliwaumba wanadamu wa aina mbili, mwanamume na mwanamke; na kwa hiyo, kuna mgawanyo wa kike na kiume katika miili Yake. Hakuamua juu ya kazi Yake kulingana na maneno aliyozungumza kwa Adamu na Hawa. Mara mbili Alipopata mwili kuliamuliwa kwa kuzingatia kabisa mawazo Yake alipowaumba wanadamu kwa mara ya kwanza, yaani, Alikamilisha kazi ya kupata Kwake mwili mara mbili, kwa msingi wa mwanamke na mwanamume kabla ya wao kupotoshwa. Ikiwa wanadamu wangechukua maneno yaliyozungumzwa na Yehova kwa Adamu na Hawa, ambao walikuwa wamedanganywa na yule nyoka, na kuyatumia katika kazi ya mwili wa Mungu, je, si Yesu pia angepaswa kumpenda mke Wake kama Alivyotakiwa? Je, kwa njia hii, Mungu bado ni Mungu? Na ikiwa ni hivyo, je, bado Angeweza kukamilisha kazi Yake? Ikiwa ni vibaya kwa mwili wa Mungu kuwa mwanamke, je, basi lisingekuwa kosa kubwa sana pia kwa Mungu kumuumba mwanamke? Ikiwa mwanadamu bado anaamini kwamba Mungu kupata mwili kama mwanamke ni vibaya, je, basi Yesu, ambaye hakuoa na hivyo hakuweza kumpenda mke Wake, angekuwa na makosa kama kupata mwili wa sasa? Kwa kuwa unatumia maneno yaliyozungumzwa na Yehova kwa Hawa ili kupima ukweli wa Mungu kupata mwili leo, basi unapaswa kutumia maneno ya Yehova kwa Adamu kumhukumu Bwana Yesu ambaye alipata mwili katika Enzi ya Neema. Je, hawa wawili sio sawa? Kwa kuwa unampima Bwana Yesu kulingana na mwanamume ambaye hakuwa amedanganywa na yule nyoka, basi hupaswi kuhukumu ukweli wa kupata mwili leo hii kulingana na mwanamke ambaye alikuwa amedanganywa na yule nyoka. Hili si haki! Ikiwa umefanya hukumu ya namna hiyo, inathibitisha kukosa urazini kwako. Yehova alipopata mwili mara mbili, jinsia ya mwili Wake ilikuwa inahusiana na mwanamume na mwanamke ambaye hakuwa amedanganywa na yule nyoka; Alipata mwili mara mbili kulingana na mwanamume na mwanamke ambaye hakuwa amedanganywa na yule nyoka. Usifikiri kwamba uanaume wa Yesu ulikuwa sawa na uanaume wa Adamu ambaye alidanganywa na yule nyoka. Hahusiani naye kabisa, na ni wanaume wawili wa asili tofauti. Hakika haiwezi kuwa kwamba uanaume wa Yesu unathibitisha Yeye ni mkuu wa wanawake wote lakini sio mkuu wa wanaume wote? Je, Yeye si Mfalme wa Wayahudi wote (ikiwa ni pamoja na wanaume na wanawake)? Yeye ni Mungu Mwenyewe, sio tu mkuu wa mwanamke bali mkuu wa mwanamume pia. Yeye ni Bwana wa viumbe vyote, na mkuu wa viumbe vyote. Unawezaje kuamua uanaume wa Yesu kuwa ishara ya mkuu wa mwanamke? Huku si kukufuru? Yesu ni mwanamume ambaye hajapotoshwa. Yeye ni Mungu; Yeye ni Kristo; Yeye ni Bwana. Anawezaje kuwa mwanamume kama Adamu ambaye alipotoshwa? Yesu ni mwili uliovaliwa na Roho wa Mungu aliye mtakatifu sana. Unawezaje kusema kuwa Yeye ni Mungu aliye na uanaume wa Adamu? Kama ni hivyo, kazi yote ya Mungu haingekuwa si sahihi? Je, Yehova angeweza kuuweka ndani ya Yesu uanaume wa Adamu ambaye alidanganywa na yule nyoka? Je, si kupata mwili kwa wakati huu ni tukio jingine la kazi ya Mungu mwenye mwili ambaye ni tofauti kijinsia na Yesu lakini aliye kama Yeye katika asili? Bado unathubutu kusema kwamba Mungu mwenye mwili hawezi kuwa mwanamke kwa kuwa mwanamke ndiye aliyedanganywa kwanza na yule nyoka? Bado unathubutu kusema kwamba, kwa kuwa mwanamke ndiye mwenye najisi sana na ni chanzo cha upotovu wa wanadamu, Mungu hawezi kabisa kupata mwili kama mwanamke? Bado unathubutu kuendelea kusema kwamba “mwanamke siku zote atamtii mwanamume na hawezi kamwe kudhihirisha au kumwakilisha Mungu moja kwa moja”? Hukuelewa hapo nyuma; lakini sasa bado unaweza kuendelea kukufuru kazi ya Mungu, hususan mwili wa nyama wa Mungu? Kama huwezi kuona hili kwa uwazi kabisa, ni vizuri zaidi ukawa makini na ulimi wako, la sivyo upumbavu na ujinga wako ufichuliwe na ubaya wako uwekwe wazi. Usidhani kwamba unaelewa kila kitu. Nakueleza kwamba yote uliyokwishayaona na kuyapitia hayakutoshelezi wewe kuelewa hata sehemu ndogo kabisa ya mpango Wangu wa usimamizi. Hivyo kwa nini basi unakuwa mwenye kiburi sana? Talanta ndogo hiyo uliyonayo na maarifa kidogo hayo uliyonayo hayatoshelezi kutumika na Yesu hata katika sekunde moja ya kazi Yake! Je, una uzoefu kiasi gani hasa? Yale uliyoyaona na yote uliyoyasikia katika maisha yako yote na yale uliyoyafikiria ni kidogo kuliko kazi Ninayoifanya kwa muda mfupi sana! Ni bora usichambue na kutafuta kosa. Haijalishi una kiburi kiasi gani, wewe bado ni kuimbe tu mdogo kuliko mchwa! Vyote vilivyomo katika tumbo lako ni vichache zaidi ya vile vilivyomo katika tumbo la mchwa! Usifikiri kwamba kwa kuwa tu umepata uzoefu na ukubwa kiasi, unaweza kuashiria kwa shauku na kuzungumza kwa majivuno. Je, uzoefu wako na ukubwa wako sio matokeo ya maneno Niliyoyazungumza? Je, unaamini kwamba yalikuwa mbadala wa kufanya kwako kazi kwa bidii na kutokwa jasho? Siku hii, unaona kuwa nimepata mwili, na kwa sababu ya hili pekee unajawa na dhana nyingi hizo, na kutoka kwalo unakuwa na fikira nyingi isiyohesabika. Isingekuwa kwa kupata mwili Kwangu, bila kujali talanta ulizo nazo ni za ajabu kiasi gani, usingekuwa na dhana hizi nyingi; na. Si fikira zako zinatoka hapa? Kama si kupata mwili kwa Yesu mara hiyo ya kwanza, je, hata ungejua kuhusu kupata mwili? Je, si kwa sababu ya maarifa yako kutoka kwa kupata mwili mara ya kwanza ndio una ufidhuli kuthubutu kuhukumu kupata mwili kwa mara ya pili? Kwa nini ukuchunguze badala ya kuwa mfuasi mtiifu? Wakati umeingia katika mkondo huu na kuja mbele ya Mungu mwenye mwili, je, Angekuruhusu kuchunguza hili? Ni sawa kwako kuchunguza historia ya familia yako, lakini ukijaribu kuchunguza “historia ya familia” ya Mungu, inawezekanaje Mungu wa leo akuruhusu kufanya uchunguzi kama huo? Je, wewe si kipofu? Je, hujiletei dharau kwako mwenyewe?

Ikiwa tu kazi ya Yesu ingefanywa bila kukamilishwa na kazi katika hatua hii ya siku za mwisho, basi mwanadamu milele angeshikilia fikira kwamba Yesu tu ndiye Mwana wa pekee wa Mungu, yaani, Mungu ana mwana mmoja tu, na kwamba yeyote anayekuja baada yake akiwa na jina jingine hawezi kuwa Mwana pekee wa Mungu, sembuse Mungu Mwenyewe. Mwanadamu ana fikira kwamba yeyote ambaye anajitoa sadaka kwa ajili ya dhambi au yule ambaye anachukua mamlaka kwa niaba ya Mungu na anayewakomboa wanadamu wote ni Mwana wa Mungu wa pekee. Kuna baadhi ambao wanaamini kwamba alimradi Yeye anayekuja ni mwanamume, Anaweza kuchukuliwa kuwa ni Mwana wa Mungu wa pekee na mwakilishi wa Mungu, na hata kuna wale wanaosema kwamba Yesu ni Mwana wa Yehova, Mwana Wake wa pekee. Je, hii kweli siyo tu fikira iliyopita kiasi ya mwanadamu? Ikiwa hatua hii ya kazi haingefanywa katika enzi ya mwisho, basi wanadamu wote wangekuwa gizani sana kumhusu Mungu. Ingekuwa ni hivyo, mwanamume angejidhania kuwa ni wa juu sana kuliko mwanamke, na wanawake hawangeweza kamwe kuinua vichwa vyao juu na hivyo, hakuna mwanamke angeweza kuokolewa. Watu siku zote wanaamini kwamba Mungu ni mwanamume, na aidha kwamba siku zote Amemchukia mwanamke na asingempa wokovu. Ingekuwa ni hivyo, isingekuwa ukweli kwamba wanawake wote walioumbwa na Yehova na pia ambao wamepotoshwa, wasingeweza kuwa na fursa ya kuokolewa? Je, basi isingekuwa bure kwa Yehova kumuumba mwanamke, yaani, kumuumba Hawa? Na je, mwanamke asingeangamia milele? Kwa hiyo, hatua ya kazi katika siku za mwisho inafanywa ili kuwaokoa wanadamu wote, sio mwanamke tu Ikiwa kunaye anayefikiria kwamba ikiwa Mungu angepata mwili kama kike, ingekuwa kwa ajili ya kumwokoa mwanamke pekee, basi mtu huyo bila shaka angekuwa mpumbavu!

Kazi inayofanywa kwa sasa imesukuma mbele kazi ya Enzi ya Neema; yaani, kazi katika mpango mzima wa usimamizi wa miaka elfu sita imesonga mbele. Ingawa Enzi ya Neema imeisha, kazi ya Mungu imeendelea mbele. Kwa nini Ninasema mara kwa mara kwamba hatua hii ya kazi inajengwa juu ya Enzi ya Neema na Enzi ya Sheria? Hii ina maana kwamba kazi ya siku hii ni mwendelezo wa kazi iliyofanyika katika Enzi ya Neema na maendeleo ya kazi iliyofanyika katika Enzi ya Sheria. Hatua hizi tatu zinaingiliana kwa karibu na kuunganika moja kwa inayofuata kwa karibu. Kwa nini pia Ninasema kwamba hatua hii ya kazi inajengwa juu ya ile iliyofanywa na Yesu? Tuseme kwamba hatua hii haingejengwa juu ya kazi iliyofanywa na Yesu, ingebidi kusulubiwa kwingine kufanyike katika hatua hii, na kazi ya ukombozi ya hatua iliyopita ingelazimika kufanywa upya tena. Hii isingekuwa na maana yoyote. Kwa hiyo, sio kwamba kazi imekamilika kabisa, bali ni kwamba enzi imesonga mbele, na kiwango cha kazi kimewekwa juu kabisa kuliko kilivyokuwa kabla. Inaweza kusemwa kwamba hatua hii ya kazi imejengwa juu ya msingi wa Enzi ya Sheria na kwenye mwamba wa kazi ya Yesu. Kazi hii inajengwa hatua kwa hatua, na hatua hii sio mwanzo mpya. Ni muungano tu wa hatua tatu za kazi ndio unaweza kuchukuliwa kuwa mpango wa usimamizi wa miaka elfu sita. Kazi ya hatua hii inafanywa kwa msingi wa kazi ya Enzi ya Neema. Ikiwa hatua hizi mbili za kazi hazikuhusiana, kwa nini basi kusulubiwa hakurudiwi katika hatua hii? Kwa nini Sibebi dhambi za mwanadamu, lakini badala yake Naja kumhukumu na kumwadibu mwanadamu moja kwa moja? Ikiwa kazi Yangu ya kumhukumu na kumwadibu mwanadamu na kuja Kwangu saa hii si kwa njia ya Roho Mtakatifu na hakukufuata kusulubiwa, basi Nisingekuwa na sifa zinazostahili kumhukumu na kumwadibu mwanadamu. Kazi katika hatua inajenga kabisa juu ya kazi katika hatua iliyotangulia. Hiyo ndiyo maana ni kazi kama hii tu ndiyo inaweza kumleta mwanadamu katika wokovu hatua kwa hatua. Yesu pamoja na Mimi tunatoka kwa Roho Mmoja. Ingawa miili Yetu haina uhusiano, Roho Zetu ni moja; ingawa kile Tunachofanya na kazi Tulizo nazo hazifanani, kwa asili Tunafanana; Miili Yetu ina maumbo tofauti, lakini hii ni kwa sababu ya mabadiliko ya enzi na mahitaji tofauti ya kazi Yetu; huduma Zetu hazifanani, hivyo kazi Tunayoileta na tabia Tunayoifichua kwa mwanadamu pia ni tofauti. Ndiyo maana kile ambacho mwanadamu anakiona na kukielewa leo hii si kama kile cha wakati uliopita; ni hivyo kwa sababu ya mabadiliko ya enzi. Ingawa jinsia na maumbo ya miili Yao ni tofauti, na kwamba hawakuzaliwa katika familia moja, sembuse katika kipindi kimoja, hata hivyo Roho Zao ni moja. Ingawa miili Yao haina uhusiano wa damu au kimwili kwa namna yoyote ile, haipingiki kwamba Wao ni Mungu kupata mwili katika vipindi viwili tofauti vya nyakati. Ni ukweli usiopingika kwamba Wao ni miili ya nyama ya Mungu, ingawa hawatoki katika ukoo mmoja na hawatumii lugha moja ya binadamu (mmoja alikuwa mwanamume aliyezungumza lugha ya Wayahudi na mwingine ni mwanamke anayezungumza Kichina pekee). Ni kwa sababu hizi ndiyo Wameishi katika nchi tofauti kufanya kazi ambayo inampasa kila mmoja kufanya, na katika nyakati tofauti vilevile. Licha ya ukweli kwamba Wao ni Roho moja, wakiwa na asili inayofanana, hakuna mfanano wa wazi kabisa kati ya ngozi za nje za miili Yao. Wanashiriki tu ubinadamu sawa, lakini sura ya nje ya miili Yao na kuzaliwa Kwao hakufanani. Mambo haya hayana athari katika kazi Zao au maarifa aliyonayo mwanadamu juu Yao, maana, kimsingi, Wao ni Roho moja na hakuna anayeweza kuwatenganisha. Ingawa Hawana uhusiano wa damu, nafsi Zao zote zinaongoza Roho Zao, ambazo zinawapa kazi tofauti katika nyakati tofauti, na miili Yao kwa ukoo tofauti. Roho wa Yehova si baba wa Roho wa Yesu na Roho wa Yesu si mwana wa Roho wa Yehova: Ni Roho moja. Vile vile Kama vile Mungu mwenye mwili wa leo na Yesu. Ingawa Hawahusiani kwa damu, ni Wamoja; hii ni kwa sababu Roho Zao ni moja. Mungu anaweza kufanya kazi ya rehema na wema, vilevile na ile kazi ya hukumu ya haki na kumwadibu mwanadamu, na ile ya kuleta laana kwa mwanadamu; na hatimaye, Anaweza kufanya kazi ya kuuharibu ulimwengu na kuwaadhibu waovu. Je, hafanyi haya yote Mwenyewe? Je, hii si kudura ya Mungu? Aliweza kutangaza sheria kwa ajili ya mwanadamu na kumpa amri, na aliweza pia kuwaongoza Waisraeli wa awali katika kuishi maisha yao duniani na kuwaongoza kujenga hekalu na madhabahu, Akiwatawala Waisraeli wote. Kwa kutegemea mamlaka Yake, Aliishi pamoja na Waisraeli duniani kwa miaka elfu mbili. Waisraeli hawakuthubutu kumwasi; wote walimheshimu Yehova na walifuata amri Zake. Hii ilikuwa Kazi iliyofanywa kwa kutegemea mamlaka Yake na kudura Yake. Kisha, katika Enzi ya Neema, Yesu alikuja kuwakomboa wanadamu wote walioanguka (sio Waisraeli pekee). Alionyesha rehema na wema kwa mwanadamu. Yesu ambaye mwanadamu alimwona katika Enzi ya Neema Alikuwa amejazwa na wema na siku zote Alikuwa mwenye upendo kwa mwanadamu, maana Alikuwa amekuja kuwakomboa wanadamu kutoka dhambini. Aliweza kuwasamehe wanadamu dhambi zao hadi pale ambapo kusulubiwa Kwake kuliwakomboa wanadamu kutoka dhambini kabisa. Wakati huo, Mungu alionekana kwa mwanadamu kwa rehema na wema; yaani, Alijitoa sadaka kwa ajili ya mwanadamu na Alisulubiwa kwa ajili ya dhambi za mwanadamu ili kwamba ziweze kusamehewa milele. Alikuwa mwenye rehema, mwenye huruma, mwenye upendo na mstahimilivu. Na wale wote waliomfuata Yesu katika Enzi ya Neema nao pia walitafuta kuwa wastahimilivu na wenye upendo katika mambo yote. Walistahimili mateso kwa muda mrefu, na hawakuwahi kulipiza kisasi hata walipopigwa, kulaaniwa au kupigwa mawe. Lakini haya hayawezi kuwa hivyo tena katika hatua ya mwisho. Vivyo hivyo, hata ingawa Roho Zao zilikuwa moja, kazi ya Yesu na Yehova hazikufanana kabisa. Kazi ya Yehova haikuwa kwa ajili ya kukamilisha enzi bali kuiongoza, kukaribisha maisha ya wanadamu duniani. Hata hivyo, kazi sasa ni kuwashinda wale walio katika mataifa yasiyo ya Wayahudi na ambao wamepotoshwa sana, kuongoza sio tu familia ya China bali ulimwengu mzima. Inaweza kuonekana kwako kwamba kazi hii inafanywa Uchina pekee, lakini kwa kweli imekwishaanza kusambaa katika nchi za ughaibuni. Ni kwa nini wageni mara kwa mara wanatafuta njia ya kweli? Hiyo ni kwa sababu Roho tayari amekwishaanza kazi, na maneno yanayonenwa sasa yanaelekezwa kwa watu ulimwenguni kote. Na hili, nusu ya kazi tayari inafanywa. Kutoka kuumbwa kwa dunia hadi sasa, Roho wa Mungu ameendeleza hii kazi kubwa, na aidha Amefanya kazi tofauti katika enzi tofauti, na katika mataifa tofauti. Watu wa kila enzi wanaiona tabia Yake tofauti, ambayo kwa asili inafichuliwa kupitia kazi tofauti Anazozifanya. Yeye ni Mungu, aliye mwingi wa rehema na wema; Yeye ni sadaka ya dhambi kwa ajili ya mwanadamu na mchungaji wa mwanadamu; lakini pia Yeye ni hukumu, kuadibu, na laana kwa mwanadamu. Angeweza kumwongoza mwanadamu kuishi duniani kwa miaka elfu mbili na pia Angeweza kuwaokoa wanadamu waliopotoka kutoka dhambi. Leo, pia Anaweza kuwashinda wanadamu ambao hawamjui na kuwafanya wawe chini ya miliki Yake, ili kwamba wote wajinyenyekeze kwake kikamilifu. Mwishowe, Atachoma yote ambayo si safi na ambayo ni dhalimu ndani ya wanadamu katika ulimwengu mzima, ili kuwaonyesha kwamba Yeye si Mungu wa Rehema, na upendo tu, si Mungu wa hekima, na maajabu tu, si Mungu mtakatifu tu, bali, hata zaidi ni Mungu anayemhukumu mwanadamu. Kwa waovu miongoni mwa wanadamu, Yeye ni mwenye kuchoma, kuhukumu na kuadhibu; kwa wale ambao wanapaswa kukamilishwa, Yeye ni mateso, usafishaji, na majaribu, na vilevile faraja, ruzuku, utoaji wa maneno, kushughulika na kupogoa. Na kwa wale ambao wanaondolewa, Yeye ni adhabu na vilevile malipo. Niambie, je, Mungu si mwenye enzi? Anaweza kufanya kazi yoyote na yote, sio tu kusulubiwa kama ulivyokuwa ukifikiri. Unamfikiria Mungu kuwa ni wa chini sana! Je, unaamini kwamba chote Anachoweza kufanya ni kukomboa wanadamu wote kupitia kusulubiwa kwako pekee? Na baada ya hilo, utamfuata mbinguni kula tunda kutoka mti wa uzima na kunywa kutoka mto wa uzima? … Je, inaweza kuwa rahisi hivyo? Niambie, umekamilisha nini? Je, una uzima wa Yesu? Ni kweli ulikombolewa naye, lakini kusulubiwa kulikuwa ni kazi ya Yesu Mwenyewe. Ni wajibu gani umeukamilisha kama mwanadamu? Una uchaji Mungu wa nje pekee lakini huielewi njia Yake. Hivyo ndivyo unavyomdhihirisha? Ikiwa hujapata maisha ya Mungu au kuona tabia Yake yote ya haki, basi huwezi kudai kuwa mtu aliye na uzima, na hustahili kupitia katika lango la ufalme wa mbinguni.

Mungu si Roho pekee, Anaweza pia kuwa mwili: aidha, Yeye ni mwili wa utukufu. Yesu, ingawa hamjamwona, alishuhudiwa na Waisraeli, yaani, Wayahudi wa wakati huo. Mwanzoni alikuwa mwili wa nyama, lakini baada ya kusulubiwa, Aligeuka mwili wa utukufu. Yeye ni Roho anayezunguka mambo yote na Anaweza kufanya kazi katika kila mahali. Anaweza kuwa Yehova, au Yesu au Masihi; hatimaye, Anaweza pia kuwa Mwenyezi Mungu. Yeye ni haki, hukumu, na kuadibu; Yeye ni laana na ghadhabu, lakini pia Yeye ni rehema na wema. Kazi zote ambazo Amezifanya zinaweza kumwakilisha. Unasema Yeye ni Mungu ni wa aina gani? Hutaweza kuelezea kabisa. Yote unayoweza kusema ni: “Kuhusu Mungu ni wa aina gani, siwezi kuelezea.” Usihitimishe kwamba Mungu milele ni Mungu wa rehema na wema, kwa sababu tu Yeye alifanya kazi ya ukombozi katika hatua moja. Je, unaweza kuwa na uhakika kwamba Yeye ni Mungu wa rehema na upendo pekee? Ikiwa Yeye ni Mungu wa rehema na mwenye upendo, kwa nini Ataikomesha enzi katika siku za mwisho? Kwa nini Ataleta chini majanga mengi sana? Ikiwa ni kama unavyofikiri, kwamba Yeye ni Mungu wa rehema na upendo kwa mwanadamu hadi mwisho kabisa, hata hadi katika enzi ya mwisho, basi kwa nini atatuma chini majanga kutoka mbinguni? Ikiwa Anampenda mwanadamu kama Anavyojipenda na kama Anavyompenda Mwanawe wa pekee, basi kwa nini Atatuma chini mapigo na mvua ya mawe kutoka mbinguni? Kwa nini Anamruhusu mwanadamu kuteseka na njaa na ndwele ya kufisha? Kwa nini anamruhusu mwanadamu kuteseka majanga haya? Hakuna yeyote kati wenu anayethubutu kusema Yeye ni Mungu wa aina gani, na hakuna anayeweza kuelezea. Je, unaweza kuwa na uhakika kwamba Yeye ni Roho? Je, unathubutu kusema kuwa Yeye ni mwili wa Yesu pekee? Na unathubutu kusema kuwa Yeye ni Mungu ambaye milele atasulubiwa kwa ajili ya mwanadamu?

kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Alhamisi, 18 Julai 2019

Maneno ya Mungu | “Mnapaswa Kuzingatia Matendo Yenu”

Maneno ya Mungu | “Mnapaswa Kuzingatia Matendo Yenu”

Mwenyezi Mungu anasema, “Katika maisha yenu ya kila siku, mnaishi katika hali na mazingira yasiyo na ukweli ama fahamu nzuri. Hamna rasilimali ya uwepo na pia hamna msingi wa Kunijua au kujua ukweli. Imani yenu imejengwa tu juu ya ujasiri usio dhahiri au kwenye ibada za kidini na ujuzi kulingana na mafundisho ya kidini kabisa. Kila siku Ninatazama mienendo yenu na kuchunguza nia yenu na matunda yenu maovu. Sijawahi kumpata mmoja ambaye kwa kweli aliweka moyo wake na roho yake kwenye madhabahu Yangu, ambayo hayajawahi kusonga. Kwa hivyo, Singependa kuyamwaga bure maneno yote ambayo Nina nia ya kumwelezea mwanadamu wa aina hii. Moyoni Mwangu, Ninapanga kuikamilisha kazi Yangu iliyosalia tu na kuleta wokovu kwa mwanadamu ambaye Sijamwokoa bado. Hata hivyo, Ningependa wale wote wanaonifuata wapokee wokovu Wangu na ukweli ambao neno Langu linaweka katika mwanadamu. Natumaini kuwa siku moja unapofumba macho yako, utauona ulimwengu ambamo manukato yametanda hewani na vijito vya maji ya uhai vinatiririka, na wala sio dunia baridi isiyoonekana vizuri ambapo giza limetanda angani na ambamo vilio vya kughadhabisha havikomi.”
Kila siku, fikira na matendo ya kila mmoja yanachunguzwa na Yeye na, katika wakati uo huo, wamo katika matayarisho ya siku zao zinazofuata. Hii ni njia ambayo lazima kila mtu aliye hai aipitie na ambayo Nimeamulia kabla kila mmoja. Hakuna anayeweza kuepuka hili na hakuna atakayepata upendeleo. Nimezungumza maneno yasiyohesabika na zaidi ya yote Nimefanya kazi kubwa mno. Kila siku, Ninatazama vile kila mwanadamu kiasili anafanya yote ambayo anafaa kufanya kulingana na asili yake na vile inavyoendelea. Bila kujua, wengi tayari wamo katika “njia sahihi”, ambayo Niliiweka kwa ufunuo wa mwanadamu wa kila aina. Tayari Nimemweka kila aina ya mwanadamu katika mazingira tofauti tofauti, na katika sehemu zao, kila mmoja amekuwa akionyesha tabia zake za asili. Hakuna mtu wa kuwafunga, hakuna mtu wa kuwatongoza. Wako huru katika nafsi yao yote na lile wanalolieleza linakuja kwa wepesi. Kuna kitu kimoja tu ambacho huwaweka katika nidhamu, na hayo ni maneno Yangu. Kwa hivyo, kuna idadi ya wanadamu husoma tu maneno Yangu shingo upande ili mwisho wao usiwe ule wa mauti, lakini kamwe hawaweki maneno Yangu katika matendo. Kwa upande mwingine, wanadamu wengine huona ugumu kuvumilia siku bila maneno Yangu kuwaelekeza na kuwapa, kwa hivyo wao hushikilia maneno Yangu kiasili wakati wote. Muda unavyopita, wao basi hugundua siri ya maisha ya mwanadamu, hatima ya mwanadamu na thamani ya kuwa na utu. Mwanadamu si zaidi ya haya katika uwepo wa maneno Yangu, na Mimi huruhusu tu mambo yachukue mkondo wake. Sifanyi chochote kinachomlazimisha mwanadamu kuishi kulingana na maneno Yangu kama msingi wa kuwepo kwake. Na kwa hivyo wale wasiokuwa na dhamiri au thamani katika kuwepo kwao hutazama kwa kimya mambo yanavyoenda kisha wanayatupa maneno Yangu kando kwa ujasiri na kufanya vile wanavyopenda. Wanaanza kuchoshwa na ukweli na mambo yote yatokayo Kwangu. Isitoshe, wao huchoka kukaa katika nyumba Yangu. Wanadamu hawa hukaa katika nyumba Yangu kwa ufupi tu kwa ajili ya hatima zao na kuepuka adhabu, hata kama wanafanya huduma. Lakini nia zao huwa hazibadiliki, wala matendo yao. Hii huendeleza zaidi hamu zao za Baraka, hamu za njia moja kwenda katika ufalme ambako wanaweza kubakia milele, na pia njia ya kuingia mbingu ya milele. Jinsi wanavyotamani zaidi siku Yangu ije hivi karibuni, ndivyo wanavyohisi zaidi kuwa ukweli umekuwa kizingiti, kizuizi njiani mwao. Wanangoja kwa hamu kuingia katika ufalme ili wafurahie daima baraka za ufalme wa mbinguni, bila kutaka kuufuata ukweli ama kukubali hukumu na kuadibu, na zaidi ya yote, bila kuhitaji kuishi kwa utumishi katika nyumba Yangu na kufanya vile Ninavyoamuru. Wanadamu hawa hawaingii katika nyumba Yangu kuukamilisha moyo unaotaka kujua ukweli wala kufanya kazi pamoja na uongozi Wangu. Lengo lao tu ni wawe miongoni mwa wale ambao hawataangamizwa katika enzi inayofuata. Kwa hivyo nyoyo zao hazijawahi kuujua ukweli wala kujua jinsi ya kuukubali ukweli. Hii ndiyo sababu wanadamu wa aina hii hawajawahi kutia vitendoni ukweli au kujua undani wa ufisadi wao, ilhali wameishi katika nyumba yangu kama “wajakazi” mpaka mwisho. Wanangoja “kwa uvumilivu” kuja kwa siku Yangu, na hawachoki wanaporushwa huku na kule na hali ya kazi Yangu. Haijalishi bidii zao ni kubwa namna gani au ni gharama gani wamelipa, hakuna atakayeona kuwa wameteseka kwa ajili ya ukweli ama kujitoa kwa ajili Yangu. Katika mioyo yao, wanangoja kwa hamu siku ambayo Nitakomesha enzi nzee, na zaidi ya hayo, wanangoja kwa hamu kujua jinsi nguvu na mamlaka Yangu ni kuu. Kile hawajawahi kimbilia kufanya ni kujibadilisha na kufuata ukweli. Wanapenda kile kinachonichosha na kuchoshwa na kile ninachopenda. Wanangoja kwa hamu kile Ninachokuwa na kinyongo nacho lakini wakati uo huo wanaogopa kupoteza kile Ninachochukia. Wanaishi katika dunia hii yenye maovu ila hawajawahi kuwa na chuki nayo na wana hofu sana kuwa Nitaiangamiza dunia hii. Nia walizo nazo zinakanganya: Wanapendezwa na dunia hii Ninayochukia, na kwa wakati uo huo wanangoja kwa hamu Niiharibu dunia hii hivi karibuni. Kwa njia hii, wataepuka mateso ya uharibifu na wabadilishwe kuwa watawala wa enzi mpya kabla hawajapotoshwa kutoka katika njia ya kweli. Hii ni kwa sababu hawapendi ukweli na wanahofia kila kitu kitokacho Kwangu. Huenda ikawa watakuwa “watu watiifu” kwa muda mfupi kwa minajili ya kutopoteza baraka, lakini fikira zao za kungoja baraka kwa hamu na woga wao wa kuangamia na kuingia katika ziwa la moto haziwezi kukingwa kuonekana. Siku Yangu inapokaribia, hamu zao zinazidi kuimarika. Na vile janga lilivyo kubwa, ndivyo wanavyopoteza tumaini wasijue watakapoanzia ili kunifanya Nifurahi na kuzuia wasipoteze baraka ambazo wamezingoja kwa muda mrefu. Pindi mkono Wangu unapoanza kazi yake, wanadamu hawa wana hamu kuchukua hatua kuhudumu kama watangulizi. Wanafikiri tu kusonga kwa nguvu mpaka mstari wa mbele wa majeshi, wakiwa na woga mwingi kuwa Sitawaona. Wanafanya na kusema kile wanachodhani ni ukweli, bila kujua kuwa vitendo na matendo yao hayajawahi na umuhimu kwa ukweli, na kuwa hutatiza na kuingilia tu mipango Yangu. Hata ingawa wanaweza kuwa wameweka juhudi nyingi na wanaweza kuwa wa kweli katika ridhaa na nia zao kustahimili ugumu, kila wanachokifanya hakihusiani na Mimi , kwa maana Sijaona hata mara moja kwamba matendo yao yametoka kwa nia njema, na zaidi ya hayo, Sijawaona kama wameweka kitu chochote kwenye madhabahu Yangu. Hayo ndiyo matendo yao mbele Yangu kwa miaka hii mingi.
Mwanzoni, Nilitaka kuwapa ukweli zaidi, lakini kwa sababu mtazamo wenu kwa ukweli ni baridi sana na isiyojali, Nimesalimu amri. Sipendi kuona jitihada Zangu zikipotea bure, na pia Sipendi kuona watu wakishika maneno Yangu na ilhali katika kila sehemu wanafanya yale ya Kunipinga Mimi, kunidhuru Mimi, na kunikufuru. Kwa sababu ya mtazamo wenu na utu wenu, Ninawapa sehemu kidogo tu ya maneno yaliyo muhimu zaidi kwenu kama jaribio Langu kwa wanadamu. Ni mpaka sasa ndiyo Naweza thibitisha kwa hakika kwamba uamuzi na mipango Niliyoweka ni kulingana na yale mnayohitaji na kuwa mtazamo Wangu kwa wanadamu uko sawa. Miaka yenu mingi ya matendo mbele Yangu imenipa jibu ambalo Sijawahi kupata hapo awali. Na swali la jibu hili ni: “Mtazamo wa mwanadamu mbele ya ukweli na Mungu wa ukweli ni upi?” Juhudi ambazo Nimemwagia mwanadamu ni dhihirisho la kiini Changu cha kumpenda mwandamu, na vitendo na matendo ya mwanadamu mbele Yangu pia yamedhihirisha kiini cha mwanadamu cha kuchukia ukweli na kunipinga Mimi. Katika wakati wote Mimi hujali wale wote ambao wamenifuata, lakini hakuna wakati ambao wale wanaonifuata wameweza kupokea neno Langu; hawana uwezo kabisa wa kukubali hata maoni yanayotoka Kwangu. Hili ndilo hunihuzunisha zaidi ya yote. Hakuna anayeweza kunielewa na, zaidi ya hayo, hakuna anayeweza kunikubali, hata ingawa mtazamo Wangu ni wa kweli na maneno Yangu ni ya upole. Wote wanafanya kazi Niliyowaaminia kuifanya kulingana na nia yao ya asili; hawatafuti nia Zangu, wala kuuliza maombi Yangu. Bado wanadai kuwa Wananihudumia kwa uaminifu, wakati huu wote wakiwa wananiasi. Wengi wanaamini kuwa ukweli usiokubalika nao au ukweli ambao hawawezi kutia vitendoni sio ukweli. Kwa watu kama hawa, ukweli Wangu unakuwa kitu cha kukataliwa na kutupiliwa kando. Kwa wakati uo huo Ninakuwa mmoja anayetambuliwa na mwanadamu kwa neno tu kama Mungu, lakini pia kuchukuliwa kama mtu wa nje asiyekuwa ukweli, njia na uhai. Hakuna anyejua ukweli huu: Maneno yangu ndio ukweli usiobadilika milele. Mimi Ndiye msambazaji wa binadamu na kiongozi wa pekee wa mwanadamu. Thamani na maana ya maneno Yangu haibainishwi na kama yanakubaliwa au kutambuliwa na mwanadamu, ila ni kwa kiini cha maneno yenyewe. Hata kama hakuna mtu hata mmoja duniani anaweza kupokea maneno Yangu, thamani ya maneno Yangu na usaidizi wake kwa mwanadamu hayapimiki na mwanadamu yeyote. Kwa hivyo, Ninapokumbwa na wanadamu wengi wanaoasi, kukataa au kudharau kabisa maneno Yangu, msimamo Wangu ni huu tu: Wacha wakati na ukweli uwe shahidi Wangu na uonyeshe kuwa maneno Yangu ndiyo ukweli, njia na uhai. Wacha vionyeshe kuwa yote Niliyosema ni ya ukweli, na kuwa ni yale ambayo mwanadamu lazima apewe, na, zaidi ya yote, yale ambayo mwanadamu anafaa akubali. Nitawaruhusu wote wanaonifuata wajue ukweli huu: Wote wasioyakubali maneno Yangu kikamilifu, wale wasioyaweka maneno Yangu katika vitendo, wale wasiopata sababu ndani ya maneno Yangu, na wale wasiopata wokovu kwa sababu ya maneno Yangu, ni wale ambao wamehukumiwa na maneno Yangu na, zaidi ya hayo, wamepoteza wokovu Wangu, na fimbo Yangu haitaondoka kamwe miongoni mwao.
Aprili 16, 2003
Zaidi: Asili na Maendeleo ya Kanisa la Mwenyezi Mungu

Jumatatu, 15 Julai 2019

Sura ya 13. Maana ya Utendaji wa Watu Kuamua Matokeo Yao

Sura ya 13. Maana ya Utendaji wa Watu Kuamua Matokeo Yao

1. Hakuna Ambaye Angeokolewa iwapo Mungu Angeangalia Tu Maonyesho ya Asili ya Watu
Kwa sasa, utendaji wa watu unaamua matokeo yao, lakini huu utendaji ni upi? Je, unaujua? Nyinyi mnaweza kufikiri kwamba hili linarejelea tabia ya watu iliyopotoka ikijionyesha kazini mwao, lakini halimaanishi lile. Utendaji huu unanena kuhusu ikiwa unaweza kuweka ukweli kwenye vitendo au la na ikiwa unaweza kusalia mwaminifu na kujizatiti unapotenda wajibu wako au la, na vilevile mtazamo wako wa kumwamini Mungu, msimamo wako kwa Mungu, uamuzi wako wa kuteseka kwa ajili ya ugumu, mtazamo wako kwa kukubali hukumu na kupogolewa, kiwango chako cha mabadiliko na idadi ya dhambi kubwa. Haya yote yanachangia katika utendaji wako. Utendaji huu haumaanishi kiwango cha mwisho cha kufichua tabia yako iliyopotoshwa, lakini badala yake umefanikiwa kwa kiasi gani katika imani yako kwa Mungu. Iwapo matokeo ya watu yangeamuliwa kulingana na maonyesho ya asili yao, basi hakuna mtu ambaye angeokolewa. Je, hii ingekuwaje haki ya Mungu? Ikiwa wewe ni kiongozi, asili yako itajionyesha zaidi, na yeyote ambaye atajionyesha zaidi hatakuwa na uhakika sana wa kusalia. Kama hii ingeamua matokeo ya watu, basi kadiri watu wangezidi kutenda kazi katika kiwango cha juu, ndivyo wangezidi kumalizika haraka; kadiri wangezidi kuwa katika kiwango cha juu, ndivyo wangezidi kuonyesha asili yao katika kiasi kikubwa. Kama hali ingekuwa hivi, basi ni nani ambaye angethubutu kutekeleza wajibu wake? Kwa njia hii, je, haingekuwa kwamba wale ambao hawatekelezi wajibu wao wangeokolewa wote?
Utendaji huu unahusiana na ikiwa wewe ni mwaminifu na umejitoa kwa Mungu au la, ikiwa una upendo kwake au la, ikiwa unaweka ukweli kwenye matendo au la na vilevile ni katika kiwango gani ambacho umebadilika. Ni kulingana na utendaji huu kwamba hukumu yako inaamuliwa; si kulingana na kiwango cha upotovu wa tabia yako kinachojionyesha. Ukifikiria jinsi hii, umetafsiri vibaya mapenzi ya Mungu. Asili yote ya wanadamu ni sawa, ni vile tu kuna ubaya na uzuri wa ubinadamu. Hata usipoonyesha, asili yako bado ni sawa na yule anayeonyesha. Mungu Anajua vyema kilicho katika undani wa mwanadamu. Huhitaji kuficha chochote — Mungu huchunguza mioyo ya watu na mawazo. Ikiwa upotovu wako mwingi unafichuliwa wakati unapofanya kazi katika kiwango cha juu, Mungu atauona; ikiwa hutafanya kazi na usifichuliwe, je, Mungu hajui kuuhusu? Je, huku si kuamini uongo wako? Ukweli ni kwamba Mungu Anajua asili yako nje na ndani, bila kujali ulipo. Mungu Anajua vyema wale wote wanaofanya kazi yao, lakini je, si pia Ajua wale wasiofanya? Watu wengine hudhani kuwa hao viongozi walio kwenye hadhi ya juu wanachimba makaburi yao tu, kwa sababu upotovu wao mwingi utajifichua na kuonekana na Mungu pasi na kuepuka. Je, ungefichuliwa sana vile iwapo hawangeifanya kazi? Kufikiria kwa jinsi hii ni kwa upuzi! Ikiwa Mungu hauoni, basi si Hataweza kuuhukumu? Kama hali ingekuwa ile, je, haingekuwa kwamba wale ambao hawafanyi kazi wangesalia wote? Kulingana na kuelewa kwa mwanadamu, Mungu hangeona mabadiliko ya wale ambao hufanya kazi, bila kujali mabadiliko hayo ni makuu kiasi gani; Mungu Angewahukumu tu kulingana na maonyesho yao ya upotovu. Kinyume na hayo, Mungu hangewahukumu wale ambao wanaonyesha machache, licha ya kubadilika kwa kiasi kidogo. Je, unaamini kuwa hii ni haki ya Mungu? Je, mtu yeyote anaweza kusema kuwa Mungu ni mwenye haki iwapo Angefanya hili? Je, huku sio kutafasiri kubaya kwako ambako kunapelekea kuelewa kwa Mungu kubaya? Basi, je, imani yako kwa Mungu si ni ya uongo? Je, huku si kuamini kuwa Mungu sio mwenye haki daima? Je, si imani kama ile ni kufuru kwa Mungu? Ikiwa huna kitu chochote kilicho hasi na lolote jema halifichuliwi pia, bado huwezi kuokolewa. Jambo kuu ambalo huamua matokeo ya watu ni utendaji wao mwema. Lakini, hakuwezi kuwa na kitu hasi sana vilevile—kama ni kikuu kiasi cha kuleta maafa au adhabu, basi wote wataangamizwa. Kama kungekuwa jinsi mnavyofikiria, wale walio wafuasi wa kiwango cha chini wangepata wokovu mwishowe, na wale ambao ni viongozi wangekwisha. Una wajibu ambao lazima uutekeleze; lakini unapoutekeleza wajibu huo, utafichua upotovu wako licha yako mwenyewe, ni kama unakwenda kwa gilotini. Kama matokeo ya watu yangeamuliwa na asili yao, hakuna yeyote ambaye angeokolewa—kama hali kweli ingekuwa hii, basi, je, haki ya Mungu ingekuwa wapi? Haingeonekana kabisa. Nyinyi nyote mmeelewa mapenzi ya Mungu visivyo.
2. Utendaji Huu ni Kwa Ajili ya Kazi ya Mungu kwa Watu
Acheni niwape mfano: Katika shamba la miti ya matunda, mwenyewe hunyunyuzia maji na kutia mbolea, kisha husubiri matunda. Miti ambayo inazaa matunda ni mizuri na inahifahdiwa; ile ambayo haizai matunda bila shaka ni mibaya na haitahifadhiwa. Fikiria hali hii: Mti unazaa matunda, lakini una ugonjwa, na baadhi ya matawi mabaya yanahitaji kupogolewa. Je, mtu huu unapaswa kuhifadhiwa? Unapaswa kuhifadhiwa, na utakuwa mzuri baada ya kupogolewa na kutibiwa. Fikiria hali nyingine: Mti hauna maradhi, lakini hauna matunda—mti kama huu haufai kuhifadhiwa. Je, huku “kuzaa matunda” kunamaanisha nini? Kuna maana ya kazi ya Mungu kuwa na athari. Mungu anapofanya kazi kwa watu, asili yao haina vingine ila kujionyesha, na kwa ajili ya upotovu wa Shetani hawataepuka kuwa na dhambi, lakini katikati ya haya kazi ya Mungu ndani yao itazaa matunda. Ikiwa Mungu haoni hivyo, lakini Anaona tu asili ya mwanadamu ikionyeshwa, basi ule hautaitwa wokovu wa mwanadamu. Tunda la watu kuokolewa linadhihirishwa hasa katika kutekeleza wajibu kwao na kuweka ukweli kwenye matendo. Mungu huangalia kiwango cha watu cha mafanikio katika sehemu hizo na pia ukubwa wa dhambi zao. Hali hizi mbili zinachangia katika kuamua matokeo yao na ikiwa watasalia au la. Mathalani, watu wengine walikuwa wapotovu sana, wakijitolea kabisa kwa miili yao, na wala sio kwa familia ya Mungu. Hawakutumia rasilmali kwa ajili ya Mungu hata kidogo, lakini sasa wanatekeleza wajibu wao kwa shauku na wako na moyo mmoja na Mungu—kwa huu matazamo, je, kumekuwa na mabadiliko? Haya ni mabadiliko. Ni mabadiliko haya ambayo Mungu Anataka. Pia, watu wengine walipenda kusambaza mawazo walipokuwa nayo, lakini sasa wanapokuwa na mawazo mengine, wanaweza kuwa watiifu na kufuatilia ukweli, bila kuyasambaza au kufanya kinyume na Mungu. je, kumekuwa na mabadiliko? Naam! Watu wengine wanaweza kuwa wamepinga wakati mmoja waliposhughulikiwa na kupogolewa tena, lakini sasa wanapopogolewa na kushughulikiwa, wanaweza kujifahamu. Baada ya kuyakubali, wanapitia mabadiliko ya kweli—je, hii si athari? Naam! Hata hivyo, bila kujali mabadiliko yako ni makuu kiasi gani, asili yako haiwezi kubadilishwa kwa mara moja. Haiwezekani kutofichua dhambi zozote, lakini ikiwa kuingia kwako kutafanywa kwa kawaida, hata kwa uasi mwingine, utakuwa na ufahamu wake wakati huo. Ufahamu huu unaweza kukuletea mabadiliko ya mara moja na hali yako itaimarika na kuwa nzuri zaidi na zaidi. Unaweza kuwa na dhambi mara moja au mbili, lakini sio kila mara. Haya ni mabadiliko. Haimaanishi kwamba mtu aliyebadilika kwa kitengo fulani hana dhambi zozote tena; huo sio ukweli. Aina hii ya mabadiliko ina maana kuwa mtu aliyepitia kazi ya Mungu anaweza kuweka ukweli mwingi kweye vitendo na anaweza kutenda baadhi ya yale ambayo Mungu anahitaji. Dhambi zao zitapungua na kuwa chache zaidi na zaidi na matukio ya kuasi yatakuwa machache na madogo. Unaweza kuona kutokana na haya kuwa kazi ya Mungu imekuwa na athari; kile ambacho Mungu anataka ni kujionyesha kama huku ambako matokeo haya yamefanikishwa kwa watu. Hivyo, jinsi ambavyo Mungu Anashughulikia matokeo ya watu na Anavyomtendea mtu ni yenye haki kabisa, mwafaka na isiyo na mapendeleo. Unahitaji tu kutia bidii katika kutumia rasilmali yako kwa ajili ya Mungu, kuweka moyo wako wote katika kutenda ukweli ambayo unapaswa bila kusita, na Mungu hawezi kukutendea isiyo haki. Ebu fikiria: je, wale wanaoweka ukweli kwenye vitendo wanaweza kuadhibiwa na Mungu? Watu wengi wanashuku tabia ya Mungu yenye haki na wanachelea kuwa bado wataadhibiwa ikiwa wataweka ukweli kwenye vitendo; wanaogopa kuwa Mungu hataona uaminifu wao na kujitolea kwao. Watu wengine wanakuwa wa kutoonyesha hisia baada ya kupogolewa na kushughulikiwa; wanahisi wanyonge kiasi cha kutotekeleza wajibu wao na wanapoteza uaminifu wao na kujitolea kwao. Kwanini hivi? Hili kwa kiasi ni kwa ajili ya watu kukosa ufahamu kuhusu kiini cha matendo yao ambayo hupelekea kutokubali kupogolewa na kushughulikiwa. Pia kwa kiasi ni kwa ajili ya watu kutoelewa umuhimu wa kushughulikiwa na kupogolewa, wakiamini hilo kuwa ishara ya kuamuliwa kwa matokeo yao. Kwa sababu hiyo, kimakosa watu huamini kuwa wakiwa na uaminifu fulani na kujitolea kwa Mungu, basi hawawezi kushughulikiwa na kupogolewa; wakishughulikiwa, haiwezi kuwa haki ya Mungu. Kutoelewa kama huku kunawafanya wengi kutoaminika na kutojitolea kwa Mungu. Hakika, yote ni kwa sababu watu ni waongo sana; hawataki kupitia ugumu—wanataka kupata baraka kwa njia rahisi. Hawana ufahamu wa haki ya Mungu. Si kwamba Mungu hajafanya lolote la haki ama kwamba hatafanya lolote la haki, ni tu kwamba watu daima hawafikiri kwamba Anayofanya Mungu ni haki. Machoni pa wanadamu, kama kazi ya Mungu haipatani na mapenzi ya mwanadamu ama kama si matarajio yao, ina maana kuwa Yeye si mwenye haki. Watu kamwe hawatambui wakati kile wanachofanya si sahihi ama haiambatani na ukweli; katu hawatambui kwamba wanampinga Mungu. Kama Mungu hangewashughulikia ama kuwapogoa watu kwa ajili ya dhambi zao na wala kuwakaripia kwa sababu ya makosa yao, lakini daima angekuwa mtulivu, kamwe bila kuwakasirisha, daima bila kuwakosea, na daima bila kufunua makovu yao, lakini angewakubalia kula na kuwa na wakati mzuri na Yeye, basi watu hawangelalamika kuwa Mungu sio mwenye haki. Wangesema kuwa Mungu ni mwenye haki kwa unafiki. Kwa hivyo, watu bado hawaamini kuwa kile ambacho Mungu Anahitaji ni utendaji wao baada ya kubadilishwa kwao. Je, Mungu angekuwa vipi na uhakika kama wangeendelea na hayo? Kama Mungu angewasuta watu kidogo, hawangeamini tena kuwa Yeye huona utendaji wao baada ya mabadiliko. Wangeacha kuamini kuwa Yeye ni mwenye haki, na hawangekuwa na radhi kubadilishwa. Kama watu wangeendelea na hali hii, wangehadaiwa na mawazo yao wenyewe.
Soma Zaidi: Imani za Kimsingi za Kanisa la Mwenyezi Mungu

Jumamosi, 6 Julai 2019

Sura ya 30. Kumtumikia Mungu Mtu Anapaswa Kutembea Njia ya Petro

Sura ya 30. Kumtumikia Mungu Mtu Anapaswa Kutembea Njia ya Petro

Mwenyezi Mungu alisema, Watu wengi hawawezi kuainisha ni watu gani wana ukweli, watu gani hawana ukweli na watu gani husema mambo yaliyo na ukweli. Unapoulizwa kueleza ni nini maana ya "ukweli," huwezi kueleza kwa wazi. Lakini mara tu mtu anaposema kitu, unasema: “Mtazamo wake ni wa kweli. Maneno ayasemayo yanaonyesha ufahamu wa utendaji uliopatikana kupitia kwa uzoefu.” Unaelewa mara tu unapowasikia wakizungumza. Kwa ninyi hapa mlio wapya, Nikiwauliza ni nini maana ya 'uhalisi,' hamtaweza tu kunijibu, lakini pia hamtaweza kueleza tofauti kati ya mtu anayezungumza uhalisi na mtu anayezungumza mafundisho ya dini. Hili halisemwi kuwadunisha ninyi, ni tu kwamba hamna uzoefu. Tazama wale wakongwe wa kanisa; ingawa washawishi wengine wa kufanya mengi huenda wakawakanganya na vitu wasivyoweza haswa kutambua sababu sahihi, bado wanajua kwamba wanachosema watu hao si sahihi. Wanaweza kutambua ni watu gani wanazungumza mafundisho ya dini, na watu gani wanazungumza uhalisi. Ninyi, kwa hali yoyote, hata bado hamjababia. Hili halisemwi kuwashushia hadhi, kwa hivyo msione vibaya kwa sababu ya hili. Hii ni njia ya kawaida ya uzoefu ambayo kila mtu ni lazima apitie. Kila mtu ni lazima apitie miaka mingi ya kunyunyiziwa maji, kufanyiwa uchunguji, kusikiliza, kuhisi, kutambua na kupitia kabla ya kufahamu polepole lakini kwa kina uzoefu wa maisha, kabla ya kuvuka lango na kufungua macho yao. Ukizungumza tu mafundisho ya dini na kusikia mafundisho ya dini, ikiwa huwezi kutambua masuala yanayohusu uhalisi na usiwe na utambuzi, basi macho yako hayajafunguliwa; bado tu hayajafunguliwa. Ni nini maana ya "macho yako hayajafunguliwa"? Inamaanisha bado hujavuka lango, na huo ni ukweli. Inamaanisha kwamba hujavuka lango panapohusiana na ukweli. Jitazameni sasa. Labda unaweza kufanya kazi ya uchungaji, kuwasaidia wengine, kutoa msaada na kutumia, au kufanya mambo mengine ya desturi katika familia ya Mungu. Lakini wewe hasa huna uhalisi, wala hutakuwa hasa na utambuzi wowote wa kufikia uhalisi au kufikia nyaraka na mafundisho ya dini. Labda hamjaridhishwa na hili, mpaka siku moja mtu fulani aje anayezungumza mafundisho ya dini, aliye na maneno ya kushawishi, na kisha huenda mtamkweza. Na wakati mtu yule aliye na uhalisi wa kweli ajapo, aliye kimya, asiyetoa sauti, basi huenda mtamdharau. Mara mnapofanya hivi, wakati huo mtajua kimo chenu wenyewe kiko wapi. Ndio, kimo cha mwanadamu, ufahamu wa mtu kuhusu uhalisi na wa mtu mwenyewe, uzoefu wa mtu kuhusu kweli, ufahamu wa mtu kuhusu Mungu—mambo haya yote hutokana na uzoefu, hutokana na kuishi siku baada ya siku, hili ni wazi na dhahiri. Vitu hivi bila shaka havitokani na kusoma wala kutoka kwa mambo mangapi uliyoyasikia. "Nina mambo haya, nimeyasikia na ninayakumbuka. Kiwango changu cha maarifa kiko juu sana, mimi ni mwanafunzi wa chuo, ninafanya kazi fulani, ninachunguza jambo fulani, na mimi huyajua mambo mara tu niyasikiapo." Unaweza kutumia maarifa uliyojifunza kusikia falsafa, siasa au fasihi. Lakini huwezi kuyatumia hapa, hayana maana! Tuna nini hapa, basi? Maarifa uliyojifunza huenda yakakusaidia kujua maneno yaliyoandikwa ya ukweli au kuhusu vile yameelezwa vizuri zaidi kuliko wengine, lakini wewe si bora kuliko wengine inapohusu wewe kuupitia ukweli; huna heri kuhusiano na hilo. Mnalikubali hili, sivyo? Hamchunguzi masuala ya uzoefu wa maisha na mnakosa mambo mengi sana. Lakini kwa ninyi ambao mna maarifa fulani, ambao sasa mko katika nafasi ya heri ya kuwa kiongozi juu ya watu wengine, ambao mko kazini mara kwa mara na ambao hukutana na wakongwe wa kanisa walio katika viwango vya juu, na ambao hufanya kazi fulani maalum, mnaweza kuendelea haraka zaidi. Mnaweza kuendelea haraka sana kuliko vile wale wakongwe wa kanisa wangeweza hapo awali, haraka na ufahamu wenu wa uhalisi, na hali yoyote ya ukweli na kwa kujifahamu wenyewe. Labda hamtatembea katika njia inayopinda au labda ninyi pia mtahitajika kupatwa na vipingamizi fulani. Hali ya kila mtu ni tofauti, hali zao ni tofauti. Watu wengine wanahitajika kupatwa na vipingamizi fulani kabla ya kuweza kupitia mabadiliko makuu. Na kisha kuna watu wengine ambao hawahitaji kupatwa na vipingamizi vikubwa, lakini hugundua njia wanayopaswa kutembea na upotovu wao wenyewe katika mambo yanayotendeka kandokando yao, na wao hupata ujuzi fulani katika watu, mambo na vitu vilivyo kandokando yao—huyu ni mtu anayeendelea upesi sana kwa kulinganisha.
Hivyo mnapaswa kuzingatia nini sasa? Ikiwa mtazingatia tu kuyafanyia kazi na kujishughulisha na mambo ya ukingoni, basi maendeleo yenu yatacheleweshwa. Mnapoamini katika Mungu, maendeleo yenu binafsi maishani ni muhimu zaidi na ni ya maana zaidi. Huenda ukajiandaa tu na mafundisho ya dini, au na uwezo wa kufanya kazi, au huenda ukafanya jambo fulani kwa kutumia mbinu fulani nzuri sana, au kwa hekima; mambo haya yote ni ya kufuata, ingawa bado huwezi kuendelea bila hayo. Suala kuu la imani yako kwa Mungu ni kwamba lazima uujue ukweli kabisa, upitie ukweli na uwe na ufahamu fulani wa ukweli, na uweze kuwa na moyo mtiifu na kutosheleza mapenzi ya Mungu mbele Yake. Iwapo unaamini katika Mungu lakini kadri unavyoamini, ndivyo uhusiano wako na Mungu unaenda mrama, ndivyo unavyosonga mbali zaidi na Mungu na ndivyo unavyokuwa na sehemu nyingi ndani yako zinazopingana na ukweli, basi hilo linathibitisha kwamba imani yako haikuongozi kuendelea, kwamba Roho Mtakatifu hajakushughulikia, na kwamba umepotea na umevuka mipaka. Iwapo unaamini kwa kipindi fulani na kisha unakuwa na ufahamu fulani wa uhalisi, kujifahamu kwa kiasi fulani, na ufikirie umeelewa mambo fulani ya uhalisi, basi hili linathibitisha kwamba unafahamu mambo ya kiroho, macho yako yamefunguka na unatembea katika njia sahihi. Kuna wakongwe wengine sasa ambao wamefuata kwa miaka miwili au mitatu, ambao hata hawajababia, ambao ni waasi na wasiozuiwa na ambao hujitayarisha kupokea baraka, ambao wanajitayarisha kufurahia utajiri wao mzuri baada ya kazi kukamilishwa. Hata bado hawajababia kulingana na uzoefu wa maisha, na hawana uhusiano wenye upatanifu na Mungu hata kidogo. Ni vyema kuwa nao kwa kipindi kifupi, na watatii shingo upande, na hawatathubutu kutoa sauti ikiwa wana dhana. Lakini baada ya muda fulani kupita, mara tu wanapoanza kupinga, wanakuwa vyombo vya kuangamia. Kila mtu yuko juu ya ardhi hatari, na hili ni jambo la kuogofya. Ikiwa unamwamini Mungu na unatembea kwenye njia sahihi, basi imani yako ni muafaka na utapata baraka. Ikiwa utaenda kombo, ukitembea kwenye njia isiyo sahihi au njia isiyonyooka, usipoendelea mbele, usipoendelea mbele kwa uwezo wako wote, basi utaangamia na utapata adhabu.
Watu wana njia mbili za imani katika Mungu: Moja ni kuweza kumwamini Mungu kabisa; na nyengine ni kumuasi Mungu na kumpinga Yeye. Hizi ndizo njia mbili pekee. Haiwezekani kwamba humpingi Mungu lakini pia humtii Yeye; hili haliwezekani. Ikiwa humtii Mungu na huna ufahamu halisi, basi unaweza tu kuwa mkaidi na muasi. Huenda usionyeshe uasi kwa mambo unayosema, na huenda usimpinge Yeye waziwazi kwa silaha zilizochukuliwa, lakini bado moyo wako ni mkaidi. Au iwapo huulizwi kufanya jambo, huenda ukahisi umejawa na upendo kwa Mungu na kuhisi uko karibu sana na Mungu. Lakini mara tu unapoulizwa kufanya jambo, basi ukaidi wako, kiburi chako, kujidai kwako na mambo yako ya Shetani hufichuliwa; mara tu yanapofichuliwa, basi ukaidi wako unakuwa wa kweli. Je, si hivyo? Huenda ukaichukulia imani yako kwa Mungu kama tu "Mimi nimebarikiwa kwa kuamini katika Mungu na baadaye nitakuwa chombo cha baraka Zake. Mimi ni mshirika wa familia ya Mungu na mimi nimeinuliwa na Mungu; mimi ni mtu aliyekwezwa na Mungu. Nimebarikiwa na Mungu ni mwema kwangu." Lakini ikiwa unliona kwa njia hii, kuna maana gani? Kuna maana gani kupiga makelele kwa maneno haya matupu yanayorudiwarudiwa? Jambo kuu sasa ni iwapo unaweza kuokolewa au la, iwapo unatembea kwa njia sahihi ya maisha au la, iwapo Mungu anakusifu katika imani yako au la, iwapo Mungu anakubali kuwa kwako mshirika wa familia ya Mungu au la, na iwapo Mungu anakukubali au la; ni hayo tu ndiyo yanaweza kuchukuliwa kama kuwa makini katika imani yako kwa Mungu. Imani ya kipumbavu, kama vile "Ah, Mungu ni mwema kwangu, Mungu hunifadhili, nimebarikiwa na mimi hufanikiwa kila mahali. Tazama, Mungu ameniinua na kunifanya kuwa kiongozi katika familia Yake. Nimekuwa na bahati sana na nyota yangu imekuwa ikiinuka tangu nilipokuja katika familia ya Mungu." Kuringia tu jambo la aina hii hakuna maana. Ni tupu; lisilo na maana! Ikiwa umepewa nafasi lakini huishikilii upesi, basi ilitolewa bure, na hakutakuwa na maana hata ukipewa nafasi nyingi kiasi gani. Shikilia upesi mambo fulani ya kweli, na halisi. Baadhi ya waumini wakongwe husema: "Ah, nimebarikiwa! Mimi nimebarikiwa na mimi ni mtu aliyebarikiwa zaidi katika dunia yote, katika ulimwengu wote!" Haingekusaidia hata ungekuwa malaika; huwezi tu kusema mambo ya aina hii, ni lazima ushikilie upesi mambo ya kweli. Hasa ninyi ambao mumeamini katika Mungu kwa muda mfupi tu na mmepata uzoefu kidogo kutokana na kufanya mambo, ambao hamkupitia zile hatua za kazi hapa mwanzo, na ambao mlikuja mwisho kabisa—je, uko tayari kuwa na uhakika kabisa ili baadaye uweze kuokolewa? Je, uko tayari? Huko tayari, sivyo? Ikiwa huko tayari kuwa na uhakika kabisa kuhusu jambo hilo, basi uko katika nafasi hatari!
Ikiwa huelewi ni nini maana ya kumhudumia Mungu au nini maana ya kutii Mungu, na unaelewa kidogo sana namna ya kumwabudu Mungu au jinsi watu wanapaswa kuamini katika Mungu; iwapo hujashikilia mambo haya na huyafahamu katika moyo wako, basi utaenda mrama kwa urahisi sana na utamuasi Mungu kwa urahisi sana. Kama wale walioanguka hapa awali waliosema: "Roho Mtakatifu na atufunulie mambo haya!" Ninyi nyote sasa mnaona jambo hili kwa dhahiri. Wakati huo hawakuwa na nia yoyote ya kufanya chochote kibaya na kumuasi Mungu, na walijua kwmba Mungu alikuwa amewainua na kwamba ni lazima wafanye kazi kwa bidii. Ilhali hawakutembea kwenye njia sahihi, wakifikiria tu kwamba Mungu alikuwa amewainua, kwamba walitaka kufanya kazi kwa bidii, na kufanya kazi nzuri ya kuwa wachungaji wa wale waliokuwa chini yao kanisani; walidhani chochote kile ambacho waliokuwa juu yao waliwataka wafanye, wangefanya. Hawakuwa wameshika mambo ya utendaji na hakika walikuwa wanafanya mambo bila kutambua, wakitegemea ushupavu wao wenyewe. Walipokuwa hawatumiwi tena, walikasirika sana na kusema: "Mungu ni mwenye haki. Roho na afichue hili! Imani yangu haiko katika mwanadamu, iko katika Mungu." Hawakupanga awali kusema maneno haya, hivyo yalisemwa bila hiari? Sababu yake ilikuwa gani? Ilikuwa ni kwa sababu mwanadamu hamchi Mungu na hamfahamu Yeye. Unaona kwamba watu wengine husema mambo mengine ambayo ni ya upumbavu na ujinga, na wao husamehewa. Wao husamehewa kwa ajili ya ujinga wao na kile ambacho wajibu wao ulikuwa hakichunguzwi. Mbona hali si hiyo kwa watu wengine? Kwa sababu walisema mambo yaliyokuwa mazito sana: "Wewe ni Mungu, lakini bado sitakutii Wewe." Watu hawa ni wapinga Kristo; wao humuasi Mungu na hawakubali ukweli. Watu wengine ni wapumbavu na wajinga. Ni sawa kuonyesha upumbavu wako na ujinga mara moja au mara mbili; lakini ukikosea amri za Mungu za usimamizi au ukikosea tabia ya Mungu, basi utakuwa matatani. Tazama njia ambayo Petro alitembea. Alipata nuru kutoka kwa Roho Mtakatifu hapo mwanzo na alizungumza na Yesu, akisema: "Wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu aishiye." Mara tu Roho Mtakatifu alipokuwa amempa nuru, wakati huo alipata ujuzi fulani na moyo wake ulijazwa nuru. Hata kama wakati huo hakuwa na ufahamu wa kina, lakini alitafuta kumfahamu Mungu, na akatembea kwenye njia sahihi ya kumhudumia Mungu. Kumhudumia Mungu ni jambo la hatari zaidi, na pia ni jambo la utukufu zaidi. Kwa sababu wanadamu ni wakaidi na wapotovu, mara tu wanapopotea, wao humalizika. Watu humhudumia Mungu, sio watu wengine; kumhudumia Mungu ni jambo la hatari. Petro alitembea katika njia hiyo na alikuwa na imani hii. Na je, kuhusu Paulo? Hakukubali kwamba Yesu alikuwa Kristo. Alimuwinda bila kukoma na, baada ya kuangushwa chini, bado Paulo hakutambua kwamba Mungu alikuwa Bwana wa vitu vyote, wala vile wanadamu wanapaswa kumtii Yeye. Hakuwa na akili ya kawaida ya kufikiria, lakini kuanzia mwanzo hadi mwisho alihodhi fikira za kiburi: "Ninakupa Wewe kiasi hiki kwa hivyo unapaswa kunipa kiasi hicho; ninatumia rasilimali kiashi hiki, kwa hivyo Wewe unapaswa kunituza kiasi hicho na kunipa kiasi hicho cha mshahara." Kazi yake ilikuwa chini ya utawala wa fikira za aina hii wakati huo wote. Hivyo hakuwahi kuwa na moyo wa kumheshimu Mungu, hakuwahi kuwa na moyo wa kumcha Mungu. Angalia toni ya maneno yake: "Nimepigana vita"—Nimepigana vita Ulivyonifanya nipigane; "Nimemaliza kazi yangu"—Nimekimbia kwenye njia uliyoniambia nikimbie; "Nimeidumisha imani"—je, hukunifanya niidumishe?" Nimeidumisha, kwa hivyo taji ya utukufu haipaswi kuhifadhiwa kwa ajili yangu? Je, hakunena na toni ya aina hii? Bila shaka hangeweza kuzungumza waziwazi namna hii katika waraka. Alizungumza kitasifida na kimafumbo, lakini maneno yake yalianza kutoka kwa dhana hizi. Ni nini kilifanyika mwishowe? Yeye bado aliadhibiwa, au sivyo? Mnatakiwa kuona dhahiri vile wanadamu wanapaswa kuchagua kwenye njia ya kumhudumia Mungu, kwenye njia ya kuamini katika Mungu. Ni njia zipi za kumhudumia Mungu ni za njia za Paulo? Ni njia zipi za kuamini ni za njia ya Paulo? Ni jinsi gani njia ya kumcha Mungu ya kumhudumia Mungu kama ya Petro inaweza kutimizwa? Kuna njia ambayo viumbe wa Mungu wanapaswa kutembea ili kumwabudu Yeye; njia hiyo ni lazima ichaguliwe sawasawa na malengo yenu ni lazima yawe dhahiri. Usiwe mpumbavu, lakini tembea kwa bidii na kusimama juu ya ardhi imara, na maono yaliyo dhahiri kikamilifu. Ni hatari wewe kutembea kwenda mbele katika njia ya kipumbavu na ina hakikisha kwamba siku moja utakosea amri za usimamizi za Mungu au kuanza kunung'unika.
Je, mna hakika kuhusu asili gani au hali gani ndani ya wanadamu huwaongoza kwa urahisi sana katika uangamiaji, bila kujali ikiwa ni kiongozi au mfuasi? Je, unajua kuhusu asili ya kawaida ya wanadamu? Ukawaida wa asili ya wanadamu ni kumsaliti Mungu; kila mtu na watu wote wanaweza kumsaliti Mungu. Je, kutoamini pekee sio kumsaliti Mungu? Je, kumsaliti Mungu ni nini? Ni mambo gani yanamaanisha kumsaliti Mungu? Ni lazima ufahamu kiini cha wanadamu kimeumbwa na nini; ni lazima uelewe hili na kufahamu mzizi wa mambo hayo. Udhaifu wako wa mauti, hasira, njia mbaya, tabia mbaya au adabu mbaya—mambo haya yote ni ya juujuu. Ukiyashika tu mambo haya kwa kukaza na kiini chako kibakie kisichofumbuliwa, basi bado utatembea kwenye njia isiyonyooka na bado utamuasi Mungu. Je, sivyo? Ninyi bado kila mara tu mnababia na kukamata utondoti hafifu. Mwanadamu anaweza kumsaliti Mungu wakati wowote au mahali popote na hili ni tatizo kubwa. Labda wakati huu unaweza kumpenda Mungu kwa kiwango kikubwa, kutumia rasilimali nyingi kwa ajili ya Mungu, kuwa mwaminifu hasa; labda wakati huu unaweza kuwa wa akili hasa na kuwa na dhamiri. Lakini huenda kukaja na wakati na mahali ambapo kitu fulani kitakuongoza kumsaliti Mungu. Tuseme kwamba mtu fulani ni wa akili hasa wakati huu; Roho Mtakatifu anamshughulikia, ana uzoefu fulani wa utendaji, amebeba mzigo, yeye hutekeleza jukumu lake kwa uaminifu na ana imani thabiti sana. Basi tuseme Mungu angefanya jambo fulani la kumsikitisha, jambo alilodhani si sahihi. Dhana zingeinuka ndani yake wakati huo, mara moja angekuwa mbaya, na angepoteza shauku na kuwa ovyoovyo katika kazi yake, na angeachana na maombi, akisema, "Ni nini ambacho ninaombea? Mungu hapaswi kufanya jambo hili! Ninawezaje kuomba?" Nguvu zake zingeisha na shauku yake ya maombi ingeipotea. Hii inaitwa nini? Je, hili sio dhihirisho la usaliti? Katika wakati wowote au mahali popote, mwanadamu anaweza kumwacha Mungu, kumkana Mungu na kumshutumu Mungu—je, haya yote si usaliti? Hili ni jambo la kuogofya. Tazama, unadhani kwamba sasa huna dhana zozote na unaweza kumtii Mungu wakati mwingi, kwamba unaposhughulikiwa na kupogolewa hutamwacha Mungu. Ilhali unaweza bado kumsaliti Mungu wakati wowote au mahali popote. Ni lazima ufahamu vilivyo asili ya mwanadamu. Bila shaka, baadhi ya watu wakati mwingine watakuwa na dhamiri fulani, na hao watakuwa watu ambao asili zao ni nzuri kwa kulinganisha. Wengine watakuwa na ubinadamu wa uovu, na asili zao zitakuwa mbaya. Lakini haijalishi iwapo mtu yeyote anasema ubinadamu wako ni mzuri au mbaya, au iwapo ubora wako ni mzuri au mbaya, asili ya kawaida ni kwamba unaweza kumsaliti Mungu. Asili ya mwanadamu ni kumsaliti Mungu, hivyo watu wangeweza kumsaliti Mungu kama hawangekuwa wamepotoshwa? Bado mnafikiri sasa: "Asili za watu ambao wamepotoshwa na Shetani zitamsaliti Mungu kwa hivyo hakuna ninachoweza kufanya. Nitahitajika tu kubadilika polepole." Je, bado mnawaza kwa njia hii? Basi Niambieni, je, watu wangeweza kumsaliti Mungu ikiwa hawangekuwa wamepotoshwa? Watu wangeweza pia kumsaliti Mungu ikiwa hawangekuwa wamepotoshwa. Wanadamu walipoumbwa walipewa hiari, walikuwa wadhaifu sana, na hawakuwa na moyo ambao ungeweza kumfikia Mungu kwa kweli au uliogeuka kumwelekea Mungu kwa kweli: Mungu ni Muumba wetu na sisi ni viumbe Wake. Wanadamu hakuwa na moyo huu. Wanadamu hawakuwa na ukweli ndani yao wala chochote ambacho kingeweza kuwasaidia kumwabudu Mungu. Mungu aliwapa hiari ili kwamba wanadamu waweze kufikiria, lakini wanadamu hawakujua Mungu ni nani na hawakufahamu jinsi ya kumwabudu Mungu. Hawakuwa na kitu kama hiki ndani yao. Hata kama hungepotoshwa, bado ungeweza tu kumsaliti Mungu. Kwa nini ni hivi? Shetani hukushawishi ili umfuate yeye na kumsaliti Mungu. Wewe uliumbwa na Mungu lakini humfuati Yeye. Badala yake unamfuata Shetani. Je, wewe si msaliti basi? Wasaliti husaliti. Wewe unafahamu kwelikweli kiini hiki, au sivyo? Hivyo wanadamu wanaweza kumsaliti Mungu wakati wowote na katika mahali popote. Ni wakati tu wanadamu watakapoishi kikamilifu ndani ya ufalme wa Mungu na ndani ya nuru ya Mungu, wakati Shetani atakuwa ameangamizwa na hakuna tena ushawishi wowote, hapo tu ndipo wanadamu hawataweza tena kumsaliti Mungu. Wakati bado kuna ushawishi, wanadamu badow wanaweza kumsaliti Mungu; hivyo inasemekana kwamba wanadamu hawana thamani. Bado unafikiria: "Sasa nimepata mambo fulani. Nina mambo fulani ambayo hayamsaliti Mungu, lakini yaliyo na upatanifu na Mungu. Siwezi kufikiriwa kuwa kioo kinachong'aa, lakini angalau kama chupa ya udongo. Siwezi kufikiriwa kuwa dhahabu, lakini labda shaba nyekundu." Unajistahi mwenyewe kwa hali ya juu sana. Je, unajua mwanadamu ni kitu cha aina gani? Mwanadamu anaweza kumsaliti Mungu wakati wowote au mahali popote na hafikii hata thamani ya peni moja. Kama tu alivyosema Mungu: "Rundo la mavi ya mbwa, wakatili na mafidhuli." Watu hufikiria: "Mimi si fidhuli! Mimi si fidhuli kamwe! Kwa nini nisiweze kuelewa jambo hili? Kwa nini sijalipitia? Ikiwa sijapotoshwa, basi siwezi kumsaliti Mungu." Kuna mifano ya hili, na kuna ukweli. Ninachowaambia sasa hakikosi msingi. Mambo haya yote ni kuwaonyesha ninyi, kuwaridhisha ninyi; ni kwa njia hii pekee ndio mnaweza kufikia ufahamu wa upotovu wenu wenyewe na kutatua tatizo la usaliti. Hakutakuwa tena na usaliti wowote ndani ya wanadamu katika ufalme, wanadamu wataishi chini ya utawala wa Mungu na Shetani hatakuwa na utawala juu yao, na wanadamu wataishi huru na hawatahitaji kuwa na wasiwasi, wakidhani, "Je, naweza kumsaliti Mungu?" Hakutakuwa na haja ya kuwa na wasiwasi; haitakuwa na maana! Baadaye, inaweza kutangazwa kwamba humtakuwa na chochote ndani yenu kinachomsaliti Mungu. Lakini sasa, mambo hayajakuwa sawa, kwani kiini cha wanadamu ni kile kinachoweza kumsaliti Mungu wakati wowote na katika mahali popote. Sio kwamba utamsaliti Mungu kwa sababu ya hali fulani mbaya, au kwamba bila hali yoyote mbaya au bila mtu yeyote kukulazimisha basi hutamsaliti Mungu. Unaweza bado kumsaliti Mungu hata iwapo hakuna anayekulazimisha; hili ni tatizo la kiini potovu cha wanadamu, na ni tatizo la asili yao. Ona jinsi unavyopumua tu sasa, jinsi hujafanya chochote, hujasonga, hujafikiria chochote, na ilhali hiyo asili inayomsaliti Mungu iko ndani yako—je, hii ni sahihi? Kwa nini? Kwa sababu wanadamu wana usaliti ndani yao na Mungu hayuko ndani yao. Roho ya wanadamu na nafsi ya wanadamu havina sehemu ya Mungu ndani yao. Hivyo, unaweza kumsaliti Mungu wakati wowote au katika mahali popote. Angalia, malaika ni tofauti. Hawana tabia ya Mungu, wala hawana kiini cha Mungu. Lakini wanaweza kumtii Mungu kikamilifu kwa sababu waliumbwa na Mungu sanasana kumhudumia Yeye na wao hutumwa kila mahali; wao ni mali ya Mungu. Wanadamu, kwa hali yoyote, waliumbwa kuishi duniani na hawakuumbwa na akili ya kumwabudu Mungu. Wanadamu wana uwezo wa kumsaliti Mungu na ni vyombo vinavyoweza kutumiwa au kupiganiwa na mtu yeyote. Wao ni wa thamani duni! Kwamba wanadamu wana asili hii imefichuliwa ili watu waweze kupata ufahamu wa jambo hili na wao wenyewe. Kutokana na hali hii, watu wanaweza kuanza kubadilika, na kuanzia hapa wanaweza kutafuta njia ya utendaji. Kufahamu ni katika mambo gani unaweza kumsaliti Mungu na ni kasoro gani unahitaji kurekebisha ili usimsaliti Mungu, utafikia hatua ambapo hutamsaliti tena Mungu katika hali nyingi na utaepuka kumsaliti Yeye katika nyingi ya hali hizo. Iwapo baadaye utamsaliti Mungu au la haitakuwa juu yako. Safari yako ya maisha itafikia mwisho wake, na itafikia wakati huo ambapo kazi ya Mungu itafanyika, lakini iwapo baadaye utamsaliti Mungu au la hautakuwa wajibu wako. Kwa nini hilo lilisemwa wakati huu tu? Kabla ya wanadamu kupotoshwa na Shetani, alikuja na akawashawishi wanadamu, na hapo basi waliweza kumsaliti Mungu. Baada ya Shetani kuangamizwa, je, wanadamu wakati huo hawatamsaliti Mungu tena? Wakati huo haujafika bado. Kwa hivyo wanadamu bado wana tabia potovu ya kishetani ndani yao, na wanaweza kumsaliti Mungu wakati wowote na mahali popote. Mara tu uzoefu wako wa maisha unapofikia hatua fulani, vitu vingi ndani yako vinavyomsaliti Mungu vitatupiliwa mbali. Wewe wakati huo utakuwa na vitu vingi vizuri, utaweza kutekeleza kujizuia na utaweza kujitawala mwenyewe. Hutakuwa na uwezo wa kumsaliti Mungu tena kwa wingi wa wakati huo, na baada ya Shetani kuangamia utapitia mabadiliko kamili. Hatua hii ya kazi ni kutatua sasa usaliti wa wanadamu na kutatua ukaidi wa wanadamu. Baadaye watu hawatamsaliti Mungu kwani Shetani atakuwa ameangamizwa, na hili haliwahusu wanadamu hata kidogo. Je, unafahamu? Kufahamu asili ya wanadamu ya kusaliti kunaanzia hapa: Ni mambo gani ni ya asili inayomsaliti Mungu, ni mambo gani ni sehemu ya kuonyesha usaliti, jinsi wanadamu wanapaswa kuingia na jinsi wanapaswa kufahamu. Kiini hiki cha wanadamu bado kiko ndani yao, wao bado wanaweza kumsaliti Mungu wakati wowote au mahali popote, na bado wanaweza kufanya mambo ambayo hawafikirii kuwa ni ya kumsaliti Mungu. Wanadamu wanaweza kumsaliti Mungu wakati wowote na mahali popote, hiyo ni kusema kwamba wanadamu hawana hali ya kujitawala, kwani Shetani amewamiliki. Unaweza bado kumsaliti Mungu hata kama hujapotoshwa, achilia mbali wakati huu ambapo umejazwa na tabia potovu ya kishetani. Wewe unaweza hata zaidi kumsaliti Mungu wakati wowote na mahali popote. Sasa unahitajika kutupilia mbali tabia potovu, ili kwamba hayo mambo yaliyo ndani yako yanayomsaliti Mungu yatapungua zaidi na zaidi, na utakuwa na nafasi nyingi zaidi mbele ya Mungu kumruhusu Yeye kukukamilisha na kukukubali. Ikiwa utapata uzoefu mwingi kuhusu wokovu wa Mungu katika mambo yote, utakamilishwa wakati wa hatua hii. Hivyo, ikiwa kitu fulani cha Shetani, au pepo mchafu, atakuja kukudanganya na kukusumbua, unaweza basi kutumia utambuzi wako, au sivyo? Kwa njia hii, tabia yako ya usaliti itapungua, na hiki ni kitu ambacho kitahemshwa ndani yako katika siku za baadaye. Wanadamu walipoumbwa kwa mara ya kwanza, hawakuwa na akili hii, wala hawakufahamu ibada ya Mungu, jinsi ya kumtii Mungu au usaliti wa Mungu ni nini. Shetani alikuja kuwashawishi wanadamu na wakamfuata, walimsaliti Mungu, na wakawa wasaliti kwa Mungu. Hii ni kwa sababu wanadamu hawakuwa na uwezo wa kutambua mema na mabaya, hawakuwa na akili ya kumwabudu Mungu, wala hawakuwa na ufahamu wowote kwamba Mungu alikuwa Muumba au ufahamu wowote wa jinsi wanadamu wanapaswa kumwabudu Mungu. Katika siku za baadaye, Mungu kuwafinyanga wanadamu sasa ni kufanya kweli hizi (ufahamu wa kiini cha Mungu na tabia Yake...) ndani ya wanadamu, ili kwamba waweze kufahamu hali hizi na wawe kiwango fulani cha kujitawala na hali hizi. Yaani, kadiri uzoefu wako unavyokuwa wa kina, ndivyo utakavyomfahamu Mungu na ndivyo utapunguza kuwa na mambo yanayomsaliti Mungu. Kadiri unavyokuwa na mambo yanayopatana na Mungu, ndivyo utakavyoweza kumshinda Shetani, kadiri unavyokuwa na hali ya kujitawala, ndivyo utakavyoweza kuishi kwa kudhihirisha maisha ya kweli. Baadhi ya watu huuliza: "Wanadamu wana kiini cha upotovu ndani yao na wanaweza kumsaliti Mungu wakati wowote na mahali popote; ni vipi ambavyo Mungu anaweza kusema bado Amewafanya wanadamu kuwa wakamilifu?" Kufanywa mkamilifu ni kumfahamu Mungu kupitia kwa uzoefu, na pia ni kufahamu asili yao wenyewe, kujua jinsi ya kumwabudu Mungu na kumtii Mungu, kuweza kutambua kati ya kazi ya Mungu na kazi ya wanadamu, na kutambua tofauti kati ya kazi ya Roho Mtakatifu na kazi ya pepo wachafu kupitia kwa uzoefu. Pia ni kuwa na ufahamu wa jinsi Shetani ibilisi humuasi Mungu, jinsi wanadamu humuasi Mungu, uumbaji ni nini na Muumba ni nani. Ninyi mnafahamu mambo haya, au sivyo? Haya yote ni mambo waliyopewa wanadamu kupitia kwa kazi ya Mungu katika siku za baadaye. Hivyo, wale watakaofanywa wakamilifu mwishowe watabeba uzito zaidi na watakuwa na thamani zaidi kuliko wale wa hapo mwanzo ambao hawakuwa wamepitia upotovu. Kwa sababu kuna mambo mengine ambayo yameongezwa ndani ya wanadamu na mambo mengine ambayoyamehemshwa ndani yao, watu wanaofanywa wakamilifu mwishowe watakuwa na hali ya kujitwala kuliko Adamu na Hawa wa wakati huo, na watafahamu ukweli zaidi wa jinsi ya kumwabudu Mungu na kumtii Yeye; watafahamu zaidi jinsi ya kuwa binadamu. Adamu na Hawa hawakujua mambo haya na nyoka alikuja kuwashawishi na wakala tunda kutoka kwa mti wa kufahamu mema na mabaya. Mwishowe walijua aibu, na wakaendelea kutojua jinsi ya kumwabudu Mungu, na wakawa wapotovu zaidi na zaidi, hadi wakati huu. Hili ni jambo la kina kabisa, na hakuna yeyote katika ubinadamu potovu anayeweza kulifahamu kabisa. Wanadamu bado wanaweza kumsaliti Mungu wakati wowote na mahali popote kwa sababu ya silika za mwili wao. Ilhali, mwishowe, Mungu atawakamilisha wanadamu na kuwaingiza katika hatua inayofuata; hili ni jambo ambalo watu huona ni vigumu kulifahamu.
Kwa nini wanadamu wanahitajika kumfahamu Mungu? Ikiwa wanadamu hawatamfahamu Mungu au hawatafahamu hali hii ya ukweli, basi watatumiwa kwa urahisi sana na kudanganywa na pepo wachafu. Mara tu wanapofahamu ukweli, basi haitakuwa rahisi kwao kudanganywa na kutumiwa na pepo wachafu. Lakini ikiwa, baada ya wewe kupata ufahamu huu, na ukaendelea kufanya jambo unalojua kwamba ni kukosea amri za usimamizi za Mungu au linafanywa kwa kuasi Mungu, basi hutaweza kukombolewa. Wewe uko katika hali gani wakati huu? Maadamu sasa mna tumaini moja, bila kujali iwapo Mungu anakumbuka mambo ya zamani au la, mnapaswa kudumisha fikira hizi: Ni lazima nitafute badiliko katika tabia yangu, nitafute kumfahamu Mungu, kutodanganywa na Shetani tena na kutofanya chochote kinacholeta aibu kwa jina la Mungu. Ni sehemu gani kuu huamua iwapo mtu sasa ana thamani yoyote, iwapo ataokolewa au la na iwapo ana tumaini yoyote au la? Nazo ni, baada ya wewe kusikia mahubiri, iwapo unaweza kupokea ukweli au la, iwapo unaweza kutekeleza ukweli huo au la na iwapo unaweza kubadilika au la. Hizi ni sehemu muhimu. Ikiwa utahisi tu majuto, ikiwa utaenda tu kufanya mambo na kuendelea kufikiria kwa njia hiyo hiyo ya zamani, na ukose kuwa na ufahamu wowote kabisa kuhusu jambo hili lakini badala yake uwe mbaya zaidi na zaidi, basi utakosa tumaini na unapaswa kutangazwa kuwa asiye na thamani. Kadiri unavyomfahamu Mungu, na kadiri unavyojifahamu, basi ndivyo utakavyoweza kujitawala mwenyewe. Kadiri unavyoweza kupenya katika asili yako mwenyewe kwa ufahamu, ndivyo utakavyoweza kujitawala mwenyewe. Baada ya wewe kujumlisha uzoefu wako, hutawahi tena kushindwa katika jambo hili. Kwa kweli kabisa, kila mtu ana madoa fulani juu yake ambayo hayajachunguzwa tu. Kila mtu anayo, wengine wana madogo, wengine wana makubwa; wengine huongea waziwazi, na wengine huficha nia zao na kufanya kazi kwa siri. Kila mtu anayo; Baadhi ya watu hufanya mambo ambayo watu wengine wanajua kuyahusu na baadhi ya watu hufanya mambo ambayo watu wengine hawajui kuyahusu. Kuna mawaa juu ya kila mtu na yote yanafichua tabia fulani za upotovu, kama vile kiburi au majivuno, au wao hufanya dhambi fulani, au makosa fulani au kupotoka katika kazi zao, au wanaonyesha kiasi kidogo cha ukaidi. Haya yote ni mambo ya kusamehewa kwani ni mambo ambayo mtu yeyote aliyepotoka hawezi kuepuka. Ilhali yanapaswa kuepukika mara tu unapofahamu ukweli. Na hakutakuwa tena na haja ya wewe kusumbuliwa mara kwa mara na mambo yaliyofanyika katika siku za zamani. Badala yake, inafaa kuhofiwa kwamba bado hutabadilika hata baada ya kupata kufahamu, eti utajua kwamba si sahihi kufanya kitu na bado uendelee kukifanya, na kwamba utaendelea kufanya kitu fulani hata baada ya kuambiwa kwamba ni kibaya. Watu hawa hawawezi kukombolewa.