4. Adabu Takatifu Ambayo Waumini wa Mungu Wanapasa Kuwa Nayo
1. Fanya ibada za kiroho kila asubuhi kwa kusali na kusoma neno la Mungu kwa takriban nusu saa.
2. Tafuta madhumuni ya Mungu katika kila kitu kila siku ili uweze kuuweka ukweli katika matendo kwa usahihi zaidi.
3. Kuwa na ushirika na kila unayekutana naye, mkifunzana kutoka kwa uwezo wa kila mmoja ili nyote muweze kuendelea.
4. Kuwa na mtazamo wa matumaini kuhusu maisha, huku mara nyingi ikiimba nyimbo na sifa na utoe shukrani kwa ajili ya neema ya Mungu.
5. Usitegwe na dunia ya kilimwengu; jongea karibu na Mungu moyoni mwako kwa kawaida na usiingilie mambo ya wengine.
6. Weka hekima moyoni mwako na ukae mbali na uovu na sehemu zenye hatari.
7. Usibishane na watu, kuwa na ushirika kuhusu ukweli, na uelewane na wengine.
8. Kuwa radhi kufanya kila uwezalo kuwasaidia wengine, watulizie mashaka yao, na uwasaidie kutatua ugumu wao katika kuingia katika kumwamini Mungu.
9. Jifunze jinsi ya kutii wengine, usiwatawale watu na kuwalazimisha; waruhusu watu wapate faida kiasi katika kila kitu.
10. Mara nyingi mwabudu Mungu moyoni mwako, ukimwacha Awe na ukuu katika kila kitu na kumridhisha Yeye katika kila kitu.
Kanuni kumi za hapa juu za maisha na namna kumi za kuambatana na adabu takatifu yote ni vitu ambavyo watu wana uwezo wa kuvifanya. Watu wanaweza kuweka vitu hivi katika vitendo alimradi vinaeleweka na makosa ya mara kwa mara si magumu kusuluhisha. Bila shaka, watu fulani ambao ubinadamu wao ni mbaya zaidi wameondolewa katika hili.
kutoka katika Ushirika kutoka kwa Aliye Juu
Ubinadamu wa kufaa huashiria hasa kuwa na dhamiri, mantiki, unyoofu na heshima. Dhamiri na mantiki zinajumuisha kuonyesha ustahimilivu, kuwa na uvumilivu kwa wengine, kuwa mwaminifu, kutendea watu kwa hekima, na kuwa na upendo wa kweli kwa ndugu. Hizi ndizo sifa tano ambazo binadamu wa kufaa lazima wawe nazo.
Sifa ya kwanza ni kuwa na moyo wa ustahimilivu. Unamaanisha haijalishi dosari tunazoona ndani ya ndugu zetu, tunafaa kuwatendea vema, tukionyesha uvumilivu na uelewa. Hatupaswi kuwatenga au kuwashambulia kwa maneno. Tunapoona dosari au upotovu ukijifichua ndani ya watu wengine, tunafaa kukumbuka kuwa huu ni wakati wa kazi ya Mungu ya wokovu, kwa hivyo ni jambo la kawaida kwa wateule wa Mungu kufichua upotovu, na tunapaswa kuelewa. Mbali na hayo, tunahitaji kuangalia upotovu wetu sisi wenyewe, si lazima kuwa tunafichua upotovu wa kiwango cha chini kuliko wa watu wengine. Tunapaswa kuchukulia jinsi wengine wanavyofichua upotovu jinsi tunavyochukulia wetu kabisa. Kwa njia hiyo, tunaweza kuwastahimili wengine. Iwapo huwezi kustahimili watu wengine inamaanisha kuna shida na mantiki yako; inathibitisha kwamba huelewi ukweli na hujui kazi ya Mungu. Kutojua kazi ya Mungu kunamaanisha nini? Ni kutojua kwamba kazi ya Mungu bado haijakamilika na kwamba binadamu bado anaishi katika wakati wa kazi ya Mungu ya wokovu—bado hatujafanywa kuwa kamili. Kwa hivyo, kila mtu bila kuzuilika atafichua upotovu. Sasa kila mtu anaufuatilia ukweli kwa njia inayofaa, akipata kuelewa upotovu wake mwenyewe, na kupitia neno la Mungu. Kila mtu yuko kwenye kipindi cha kuingia katika ukweli na bado hajapata ukweli kikamilifu. Ni wakati tu watu wanapopata ukweli ndio tabia ya maisha yao itaanza kubadilika. Watu wanapoelewa jambo hili watakuwa na busara ya mtu wa kawaida, na basi watawatendea wengine na busara pia. Ikiwa watu hawana busara hawatawatendea wengine kwa busara.
Sifa ya pili ni kuonyesha uvumilivu kwa wengine. Kuwa mstahimilivu tu hakutoshi; lazima pia uwe mvumilivu. Wakati mwingine unaweza kuwa mstahimilivu na mwenye kuelewa tu, lakini haiwezekani kuepuka ndugu fulani kufanya jambo linaloweza kukusononesha au kukukosea. Katika hali kama hizo ni rahisi kwa tabia potovu ya binadamu kulipuka, kwa sababu sote tunapenda kupigana na kulinda fahari yetu, na sisi sote ni wenye ubinafsi na bure. Hivyo mtu akisema kitu kinachokusononesha au kufanya kitu kinachokukosea, unafaa kuwa mvumilivu. Uvumilivu pia unajumuishwa katika mawanda ya busara. Watu watakuza uvumilivu tu ikiwa wana busara. Lakini tunawezaje kuwa wavumilivu? Ukitaka kuwa mvumilivu kwa wengine, unahitaji kwanza kuwaelewa, “kumaanisha bila kujali anayesema kitu kinachokusononesha, unafaa kutambua hili: Maneno yake yamenisononesha. Alichosema kilionekana kufunua udhaifu wangu na kilionekana kunilenga mimi. Ikiwa maneno yake yananilenga mimi, anamaanisha nini anapoyasema? Je, anajaribu kunidhuru? Je, ananiona mimi kama adui yake? Je, ananichukia? Je, analipiza kisasi dhidi yangu? Mimi sijamkosea, kwa hivyo majibu ya maswali haya hayawezi kuwa ndiyo.” Kwa kuwa hiyo ndiyo hali, basi haijalishi kile alichosema ndugu huyu, yeye hakuwa na madhumuni ya kukusononesha au kukutendea kama adui yake. Hilo ni bila shaka. Aliposema maneno haya alikuwa anadhihirisha tu yale ambayo binadamu wa kawaida hufikiri, alikuwa anashiriki juu ya ukweli, kujadili maarifa, kufichua upotovu wa watu, au kukubali hali yake mwenyewe ya upotovu; bila shaka hakuwa anamlenga mtu yeyote yule kwa kujua. Kwanza unamwelewa, kisha hasira yako inaweza kutoweka, halafu unaweza kupata uvumilivu. Wengine watauliza: “Mtu akinishambulia kwa kujua na anilenge, na aseme mambo haya kwa makusudi ya kufanikisha kusudi fulani, basi nitawezaje kuwa mvumilivu?” Unapaswa kuwa mvumilivu jinsi hii: “Hata mtu akinishambulia kwa makusudi, bado nafaa kuwa mvumilivu. Hii ni kwa sababu yeye ni ndugu yangu na sio adui yangu, na bila shaka sio ibilisi, Shetani. Haiwezi kuepukika kwamba ndugu watafichua upotovu kiasi na kuwa na makusudi fulani katika mioyo yao. Hii ni kawaida. Napaswa kuelewa, na ninafaa kuhisi maono yake na kuwa mvumilivu.” Unapaswa kuwaza kwa njia hii, kisha usali kwa Mungu na kusema: “Mungu, mtu fulani ametoka kuumiza fahari yangu. Siwezi kukubali aibu hii; kila mara nataka kuwa mwenye hasira na kumshambulia. Huu kwa hakika ni ufichuzi wa upotovu. Nilikuwa nikidhani kuwa nilikuwa na upendo kwa wengine, lakini sasa kwa kuwa maneno ya mtu fulani yamenichoma moyoni siwezi kuvumilia. Nataka kumrudishia pia. Nataka kulipiza kisasi. Uko wapi upendo wangu? Je, hii yote si ni chuki tu? Bado niko na chuki moyoni mwangu! Mungu, jinsi Ulivyo na huruma kwetu na kutusamehe sisi dhambi zetu ndio jinsi tunavyofaa kuwa na huruma kwa wengine. Hatufai kuwa na kisasi dhidi ya wengine. Mungu, tafadhali nikinge, Usiache asili yangu ilipuke. Natamani kukutii Wewe na niishi kwenye upendo Wako. Tunampinga na kumkataa Kristo na Mungu sana katika kila kitu tukifanyacho, lakini Kristo bado Anakuwa mvumilivu nasi. Mungu anafanya hatua hii ya kazi Yake kwa uvumilivu mkubwa na upendo. Je, Kristo Alilazimika kuvumilia mateso, fedheha na kashfa kiasi gani? Ikiwa Kristo Alivumilia hayo, basi kiasi kidogo cha uvumilivu tunaofaa kuwa nao si kitu! Uvumilivu wetu umepungukiwa sana ukilinganishwa na ule wa Kristo….” Mara unapoomba kwa njia hii utajisikia ni kama wewe ni mpotovu mno, asiye wa maana kabisa, aliyepungukiwa katika kimo kabisa, na huo ndio wakati ambapo hasira yako itazimwa. Hivyo ndivyo unavyoweza kufikia uvumilivu.
Sifa ya tatu ni kuwatendea watu kwa uaminifu. Kuwa waaminifu kwa watu kuna maana kwamba bila kujali tunachofanya, iwe ni kuwasaidia wengine au kutoa huduma kwa ndugu zetu au kushiriki kuhusu ukweli, lazima tuzungumze kutoka moyoni. Zaidi ya hayo, usihubiri kile ambacho hujafanya. Wakati wowote ndugu wanahitaji msaada wetu tunapaswa kuwasaidia. Tunapaswa kutimiza wajibu wowote tunaohitaji kuutimiza. Kuwa mwaminifu, wala si muongo au wa kujidai. … Bila shaka, kuwa mtu mwaminifu kunahitaji hekima kiasi wakati unaposhughulika na watu fulani. Ukiona kwamba mtu fulani si wa kutegemewa kwa sababu upotovu wake ni wa kina kabisa, kama huwezi kumbaini na hujui anachoweza kufanya, basi unahitaji kuwa mwenye hekima na uepuke kumweleza kila kitu. Kuwa mtu mwaminifu kunahitaji maadili. Usizungumze kwa upofu kuhusu mambo usiyofaa kuwa ukizungumzia. Zaidi ya hayo, kuwa mtu mwaminifu kunahitaji kuongea na mantiki na usahihi. Watu wengine wanasisitiza kutenda uaminifu na kumfungulia mtu moyo licha ya shughuli nyingi alizo nazo. Huko ni kuwa mtu mwaminifu vipi? Je, huu sio upumbavu? Kuwa mtu wa kweli ni kutokuwa mjinga. Kunahusu kuwa mwerevu, wa kawaida na wazi, na usiyedanganya. Lazima uwe wa heshima na mwenye busara. Uaminifu hujengwa juu ya msingi wa busara. Hii ndiyo maana ya kuwa mwaminifu wakati unaposhughulika na watu, na kuwa mtu mwaminifu. Bila shaka, jambo muhimu sana kuhusu kuwa mtu mwaminifu ni kuwa mwaminifu kwa Mungu. Je, si lingekuwa tatizo kubwa kama wewe ni mtu mwaminifu mbele ya watu wengine tu, lakini wewe si mwaminifu mbele ya Mungu na umdanganye Yeye? Mkitafuta kuwa watu waaminifu mbele ya Mungu, basi kwa kawaida mtakuwa waaminifu mbele ya wengine. Iwapo huwezi kufanya hivyo mbele ya Mungu, basi kwa kweli huwezi kufanya hivyo mbele ya watu wengine. Haijalishi ni kipengele kipi cha ukweli au ni kitu kipi chema ambacho unaingia, lazima kwanza ukifanye mbele ya Mungu. Punde ambapo umepata matokeo mbele ya Mungu, kwa kiasili utaweza kuishi kwa kukidhihirisha mbele ya watu wengine. Usijichoshe kufanya hiki au kile mbele ya wengine, lakini kisha bila kujali ufanye chochote unachotaka mbele ya Mungu. Hili halitakuwa sawa. Jambo muhimu zaidi ni kulifanya mbele ya Mungu, ambaye huwajaribu binadamu na kuchunguza mioyo yao. Una uhalisi kwa hakika ikiwa unaweza kupita jaribio hili mbele ya Mungu. Huna uhalisi ikiwa huwezi kupita jaribio hili mbele ya Mungu—hii ndiyo kanuni ya kutenda ukweli.
Sifa ya nne ni kutendea watu kwa hekima. Baadhi ya watu husema: “Je, kuelewana na ndugu kunahitaji hekima?” Ndiyo, kunahitaji, kwa sababu kutumia hekima hutoa hata manufaa makubwa zaidi kwa ndugu zako. Baadhi watauliza: “Je, si kutumia hekima kwa ndugu ni kuwa mwenye hila?” Hekima si hila. Badala yake, ni kinyume kabisa na hila. Kutumia hekima kuna maana ya kuwa makini kwa jinsi unavyozungumza na ndugu wakati kimo chao ni kidogo, ikija kuwa wao wasiweze kukubali kile unachosema. Pia, kwa watu wenye kimo kidogo, hasa wale ambao hawana ukweli, wanaofichua upotovu fulani na kuwa na tabia fulani za upotovu, kama wewe ni wa kawaida na wazi sana na uwaambie kila kitu, inaweza kuwa rahisi kwao kuwa na kitu dhidi yako au kukutumia vibaya. Hivyo, ni lazima kwa kadiri uchukue tahadhari kiasi na uwe na mbinu fulani unapozungumza. Hata hivyo, kuwa na tahadhari dhidi ya watu hakumaanishi kutowasaidia au kutokuwa na upendo kwao—kunamaanisha tu kutowaambia mara moja baadhi ya mambo muhimu kuhusu nyumba ya Mungu, na kushiriki tu ukweli kwao. Kama wanahitaji msaada wa kiroho katika maisha, kama wanahitaji ruzuku ya na ukweli, lazima tufanye kila kitu tuwezalo ili kuwakidhi katika suala hili. Lakini iwapo wanauliza kuhusu hili na lile kuhusu nyumba ya Mungu, au hili na lile kuhusu viongozi na wafanyakazi wake, basi hakuna haja ya kuwaambia. Ukiwaambia, kuna uwezekano watafichua habari hii na hii itaathiri kazi ya nyumba ya Mungu. Kwa maneno mengine, ikiwa ni kitu ambacho hawafai kujua au kitu ambacho hawana haja ya kujua, basi usiwaruhusu kujua kukihusu. Kama ni kitu ambacho wanapaswa kujua, basi fanya kila uwezalo kuwafanya wajue kukihusu, kwa uthabiti na bila shaka. Kwa hivyo ni mambo yapi wanayopaswa kujua? Ufuatiliaji wa ukweli ndio watu wanapaswa kujua: Ni ukweli upi wanaopaswa kuwa nao, ni vipengele vipi vya ukweli wanafaa kuelewa, ni majukumu yapi wanapaswa kutimiza, ni majukumu yapi yanawafaa wao kutimiza, ni jinsi gani wanafaa kutimiza majukumu hayo, jinsi ya kuishi kwa kudhihirisha ubinadamu wa kawaida, jinsi ya kuishi maisha ya kanisa—haya yote ni mambo ambayo watu wanapaswa kujua. Kwa upande mwingine, masharti na kanuni za nyumba ya Mungu, kazi ya kanisa na hali za ndugu zako haviwezi kuwekwa wazi kwa kawaida kwa watu wa nje wala wasioamini katika familia yako. Hii ni kanuni ambayo ni lazima ifuatwe tunapotumia hekima. Kwa mfano, hupaswi kamwe kuzungumza kuhusu majina ya viongozi wako au wanapoishi. Ukizungumza kuhusu mambo haya, huwezi kujua wakati habari hii inaweza kufikia masikio ya watu wa nje, na mambo yanaweza kuwa ya taabu sana kama yatapishwa kwa baadhi ya wapelelezi wabaya au maajenti wa siri. Hili linahitaji hekima, na hii ndiyo maana nasema kuwa na hekima ni muhimu. Zaidi ya hayo, unapokuwa wa kawaida na wazi, kuna mambo fulani ya binafsi ambayo huwezi tu kumwambia mtu yeyote. Unafaa kupima kimo cha ndugu zako ili uone kama, baada ya kuwaeleza, wanaweza kuwa waovu na wafanye utani kuhusu kile unachosema, wakikusababishia matatizo baada ya hayo mambo kusambazwa, na hili likaharibu heshima yako. Hii ndiyo maana kuwa wa kawaida na wazi pia kunahitaji hekima. Hicho ndicho kiwango cha nne ambacho binadamu sawa lazima wamiliki—kutendea watu kwa hekima.
Sifa ya tano ni kuwa na upendo wa kweli kwa ndugu ambao hakika wanaamini katika Mungu. Hii inahusisha utunzaji kiasi, msaada halisi, na roho ya huduma. Tunapaswa hasa kuwa na ushirika zaidi na hao ndugu wanaofuatilia ukweli, na kuwapa ruzuku zaidi. Haijalishi kama wao ni waumini wapya au wamekuwa waumini kwa miaka kadhaa. Kuna kanuni moja hasa ya maisha ya kanisa: Watunze hasa wale ambao wanafuatilia ukweli. Shiriki na wao zaidi, wape ruzuku zaidi, na uwanyunyizie zaidi ili waweze kusaidiwa kuinuka haraka iwezekanavyo, kuwasaidia wakue katika maisha yao haraka wawezavyo. Kwa wale ambao hawafuatilii ukweli, kama itakuwa wazi kuwa hawaupendi ukweli baada ya kipindi cha unyunyizaji, basi hakuna haja ya kuweka juhudi kubwa kwao. Si lazima kwa sababu tayari umeshafanya kila kitu kiwezekanacho kwa mwanadamu. Inatosha kuwa umetimiza wajibu wako. … Unahitaji kuona ni nani unapaswa kulenga kazi yako kwake. Je, Mungu atawakamilisha wale wasiofuatilia ukweli? Kama Roho Mtakatifu hatafanya hivyo, basi kwa nini watu waendelee kufanya hilo kwa upofu? Huelewi kazi ya Roho Mtakatifu ilhali daima umejiamini sana—je, huo si upumbavu na ujinga wa binadamu? Hivyo, toa usaidizi zaidi kwa ndugu ambao kwa kweli wanaufuatilia ukweli, kwa sababu wao ni vyombo vya wokovu wa Mungu na wateule Wake walioamuliwa kabla. Tukishiriki kuhusu ukweli mara nyingi na watu hawa kwa moyo mmoja na mawazo na kusaidiana na kupeana ruzuku, mwishowe sisi wote tutapata wokovu. Wewe unayasaliti mapenzi ya Mungu usipojiunga na watu hawa. … Wale walio ndani ya kanisa walio na ubinadamu unaofaa wanapaswa kujiweka miongoni mwa wale ambao wanafuatilia ukweli, waingiliane kwa amani na watu hawa, na kwa njia ya ufuatiliaji wa ukweli hatua kwa hatua kujitumia kwa ajili ya Mungu kwa moyo na mawazo sawa. Kwa njia hiyo, wale wanaofuatilia ukweli wataokolewa na wewe pia utaokolewa, kwa sababu Roho Mtakatifu anafanya kazi kati ya wale wanaofuatilia ukweli. …
Ushirika ambao tumetoka kuwa nao ni juu ya vipengele vitano ambavyo binadamu wa kawaida lazima wamiliki. Kama una sifa hizi zote tano, utaweza kuingiliana kwa amani na ndugu zako, utapata nafasi yako katika kanisa, na utatimiza wajibu wako kwa njia bora zaidi kadri ya uwezo wako.