Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo makusudi-ya-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo makusudi-ya-Mungu. Onyesha machapisho yote

Jumapili, 23 Juni 2019

Neno la Mungu | “Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II” Uendelezo wa Sehemu ya Kwanza

Neno la Mungu | “Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II” Uendelezo wa Sehemu ya Kwanza

Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”. Maudhui ya video hii:
Hakuna Awezaye Kuzuia Kazi Ambayo Mungu Anaamua Kufanya Kazi ya Usimamizi wa Mungu na Wokovu wa Wanadamu Yaanza na Ibrahimu Kumtoa Isaka Mungu Hajali Kama Binadamu Ni Mjinga—Anahitaji Tu Binadamu Awe Mkweli Binadamu Anapata Baraka za Mungu kwa Sababu ya Uaminifu na Utii Wake Kuwapata Wale Wanaomjua Mungu na Wanaoweza Kumshuhudia Ndilo Tamanio la Mungu Lisilobadilika
Mwenyezi Mungu alisema, Maneno na tabia iliyowasilishwa mbele na kufichuliwa na Mungu inawakilisha mapenzi Yake, na pia inawakilisha kiini Chake halisi. Wakati Mungu anapojihusisha na binadamu, haijalishi ni nini Anachosema au kufanya, au tabia gani Anayofichua, na haijalishi ni nini binadamu anaona kuhusu kiini cha Mungu na kile Anacho na alicho, vyote vinawasilisha mapenzi ya Mungu kwa binadamu. Licha ya kiwango ambacho binadamu anaweza kutambua, kufahamu, au kuelewa, vyote hivi vinawakilisha mapenzi ya Mungu—mapenzi ya Mungu kwa binadamu. Hili ni bila shaka! Mapenzi ya Mungu kwa binadamu ni vile Anavyohitaji watu kuwa, kile Anachohitaji wao kufanya, namna Anavyohitaji wao kuishi, na vile Anavyowahitaji kuweza kukamilisha kutimia kwa mapenzi ya Mungu. Je, mambo haya hayawezi kutenganishwa na kiini cha Mungu? Kwa maneno mengine, Mungu huwasilisha mbele tabia Yake na chote Alicho nacho na alicho wakati huohuo Akimtolea madai binadamu. Hakuna uongo, hakuna kusingizia, hakuna ufichaji, na wala hakuna kupiga chuku. Ilhali kwa nini binadamu hawezi kujua na kwa nini hajawahi kuweza kutambua waziwazi tabia ya Mungu? Na kwa nini hajawahi kutambua mapenzi ya Mungu? Kile ambacho kimefichuliwa na kuwasilishwa mbele na Mungu ndicho kile Mungu anacho Mwenyewe na maana yake, na kinaonyesha kila kipengele cha tabia Yake ya kweli—hivyo kwa nini binadamu hawezi kuona? Kwa nini binadamu hana uwezo wa kuwa na maarifa ya kina? Kunayo sababu muhimu ya haya. Na sababu yenyewe ni ipi? Tangu wakati wa uumbaji, binadamu hajawahi kumchukulia Mungu kama Mungu. Kwenye nyakati zile za mwanzo kabisa, haikujalisha ni nini Mungu alifanya kuhusiana na binadamu, yule binadamu ambaye ndiye tu alikuwa ameumbwa, binadamu alimchukulia yeye kuwa mwandani wake tu na wala si zaidi ya hapo, kama mtu wa kutegemewa, na hakuwa na maarifa yoyote wala uelewa wa Mungu. Hivi ni kusema, hakujua kwamba kile kilichowasilishwa mbele na Kiumbe huyu—Kiumbe huyu ambaye yeye alitegemea na kumwona kuwa mwandani wake—alikuwa kiini cha Mungu, na wala hakujua kwamba Kiumbe huyu ndiye anayetawala viumbe wote. Nikisema kwa urahisi, watu wa wakati huo hawakuwa na maarifa hata kidogo kumhusu Mungu. Hawakujua kwamba mbingu na nchi na mambo yote yalikuwa yameumbwa na Yeye na wala hawakujua ni wapi Alipotokea, na, zaidi hawakujua Yeye Alikuwa nani. Bila shaka, wakati huo Mungu hakumhitaji binadamu kumjua Yeye au kumfahamu Yeye au kuelewa kila kitu Alichofanya, au kufahamishwa kuhusu mapenzi Yake, kwani hizi zilikuwa nyakati za mapema zaidi baada ya uumbwaji wa wanadamu. Wakati Mungu alipoanza matayarisho ya kazi ya Enzi ya Sheria, Mungu alifanya mambo fulani kwa binadamu na pia Akaanza kutolea binadamu madai fulani, Akimwambia namna ya kutolea Mungu sadaka na namna ya kumwabudu. Ni wakati huo ndipo binadamu alipopata mawazo machache mepesi kuhusu Mungu, ni hapo tu ndipo alipojua tofauti kati ya binadamu na Mungu na kwamba Mungu Ndiye aliyewaumba wanadamu. Wakati binadamu alipojua kwamba Mungu alikuwa Mungu na binadamu alikuwa binadamu kukawa umbali fulani kati ya Yeye na Mungu, bado Mungu hakuhitaji kwamba binadamu awe na maarifa makuu au uelewa wa kina kumhusu Yeye. Hivyo basi, Mungu anayatoa mahitaji tofauti kwa binadamu kutokana na awamu na hali za kazi Yake. Mnaona nini katika haya? Ni kipengele kipi cha tabia ya Mungu unayoitambua? Je, Mungu ni wa kweli? Yale mahitaji ambayo Mungu anampa binadamu yanastahili? Kwenye nyakati za mapema kabisa kufuatia uumbaji wa wanadamu na Mungu, wakati ambao Mungu alikuwa bado hajatekeleza kazi ya ushindi na utimilifu wa binadamu, na Alikuwa hata bado hajaongea yale maneno mengi sana kwake, Alihitaji kidogo sana kutoka kwa binadamu. Licha ya kile ambacho binadamu alifanya na namna alivyotenda—hata kama alifanya mambo fulani yaliyomkosea Mungu—Mungu alimsamehe hayo yote, na akayapuuza. Kwa sababu Mungu Alijua kile Alichokuwa Amempa binadamu, na Alijua kile kilichokuwa ndani ya binadamu, basi Alijua kiwango cha mahitaji ambayo anafaa kudai kutoka kwa binadamu. Ingawaje kiwango cha mahitaji Yake kilikuwa cha chini sana wakati huo, hii haimaanishi kwamba tabia Yake haikuwa kuu, au kwamba hekima na uweza Wake yalikuwa si yoyote ila maneno matupu. Kwa binadamu, kunayo njia moja tu ya kujua tabia ya Mungu na Mungu Mwenyewe: kwa kufuata hatua za kazi ya usimamizi ya Mungu na wokovu wa wanadamu, na kuyakubali maneno ambayo Mungu anaongea akiyaelekeza kwa wanadamu. Kujua kile Mungu anacho na alicho, na kujua tabia ya Mungu, bado binadamu angemuuliza Mungu kumwonyesha nafsi Yake halisi? Binadamu hatafanya hivyo, na hathubutu kufanya hivyo, kwa kuweza kuifahamu tabia ya Mungu na kile Anacho na alicho, tayari binadamu atakuwa amemwona Mungu Mwenyewe wa kweli, na atakuwa tayari ameona nafsi Yake halisi. Haya ndiyo matokeo yasiyoepukika.
Kazi na mpango wa Mungu ulipokuwa ukiendelea mbele bila kusia, na baada ya Mungu kuanzisha agano la upinde wa mvua na binadamu kama ishara kwamba Hangewahi tena kuuangamiza ulimwengu kwa kutumia gharika, Mungu alikuwa na tamanio lililokuwa likiongezeka na kumsukuma kuwapata wale ambao wangeweza kuwa katika akili moja na Yeye. Hivyo, pia, Alikuwa na tamanio la haraka zaidi la kupata wale waliokuwa na uwezo wa kufanya mapenzi Yake duniani, na, isitoshe, kupata kundi la watu ambao wangeweza kuwa huru dhidi ya nguvu za giza, na kutoweza kuwa watumwa wa Shetani, na kuweza kuwa na ushuhuda kwake Yeye duniani. Kupata kundi la watu kama hawa kulikuwa ni tamanio la Mungu kwa muda mrefu, Alichokuwa akisubiria tangu wakati wa uumbaji. Hivyo basi, licha ya matumizi ya gharika na Mungu ili kuuangamiza ulimwengu, au agano Lake na binadamu, mapenzi ya Mungu, hali yake ya akili, mpango, na matumaini yote yalibakia yaleyale. Kile Alichotaka kufanya, ambacho Alikuwa ametamani kwa muda mrefu kabla ya uumbaji, kilikuwa kupata wale walio miongoni mwa wanadamu ambao Alitamani kuwapata—Kupata watu wa kundi hili ambao walioweza kufahamu na kujua tabia Yake, na kuyaelewa mapenzi Yake, kundi ambalo lingeweza kumwabudu Yeye. Watu kwenye kundi kama hili wanaweza kweli kuwa na ushuhuda kwake, na wao ndio, yaweza kusemekana, wasiri Wake.
Leo, hebu tuendelee kuzifuata nyayo za Mungu na kufuata nyayo za kazi Yake, ili tuweze kufichua fikira na mawazo ya Mungu, na kila kitu kinachomhusu Mungu, vyote ambavyo “vimehifadhiwa kwenye ghala” kwa muda mrefu. Kupitia mambo haya tutajua hatimaye tabia ya Mungu, kukielewa kiini cha Mungu, tutamruhusu Mungu kuingia kwenye mioyo yetu, na kila mmoja wetu ataweza kukaribia Mungu kwa utaratibu, na kupunguza umbali wetu na Mungu.
Sehemu ya kile tulichozungumzia wakati wa mwisho ilihusiana na kwa nini Mungu alianzisha agano na binadamu. Wakati huu, tutakuwa na ushirika kuhusu vifungo vya maandiko vilivyo hapa chini. Hebu tuanze kwa kuyasoma maandiko.

Jumatatu, 29 Aprili 2019

Maana ya Mateso na ni Mateso ya Aina Gani Ambayo Waumini wa Mungu Lazima Wastahimili

6. Maana ya Mateso na ni Mateso ya Aina Gani Ambayo Waumini wa Mungu Lazima Wastahimili

Maneno Husika ya Mungu:

Leo, watu wengi sana hawana ufahamu huo. Wao huamini kwamba mateso hayana thamani, wao hukanwa na ulimwengu, maisha yao ya nyumbani yamesumbuliwa, wao si wapendwa wa Mungu, na matazamio yao ni matupu. Kuteseka kwa watu wengine hufikia kiwango fulani, na fikira zao hugeukia kifo. Huu si upendo wa kweli kwa Mungu; watu kama hao ni waoga, hawana ustahamilivu, wao ni wadhaifu na wasio na nguvu! Mungu ana hamu ya mwanadamu kumpenda Yeye, lakini kadri mwanadamu anavyompenda Yeye, ndivyo kuteseka kwa mwanadamu huwa kwingi zaidi, na kadri mwanadamu anavyompenda Yeye, ndivyo majaribio ya mwanadamu huwa makubwa zaidi. Ikiwa unampenda Yeye, basi kila aina ya mateso yatakufika—na ikiwa humpendi, basi labda kila kitu kitaendelea kwa urahisi kwako, na kila kitu kinachokuzunguka kitakuwa kitulivu kwako. Unapompenda Mungu, utahisi kwamba mengi kandokando yako hayawezi kushindikana, na kwa sababu kimo chako ni kidogo sana utasafishwa; aidha, huwezi kumridhisha Mungu, na daima utahisi kwamba mapenzi ya Mungu ni ya juu sana, kwamba hayawezi kufikiwa na mwanadamu. Kwa sababu ya haya yote utasafishwa—kwa sababu kuna udhaifu mwingi ndani yako, na mengi yasiyoweza kuridhisha mapenzi ya Mungu, utasafishwa ndani. Lakini lazima muone kwa dhahiri kwamba utakaso hutimizwa tu kupitia usafishaji. Hivyo, katika siku hizi za mwisho lazima muwe na ushuhuda kwa Mungu. Haijalishi mateso yenu ni makubwa vipi, mnapaswa kuendelea hadi mwisho kabisa, na hata wakati wa pumzi yenu ya mwisho, bado lazima muwe waaminifu kwa Mungu, na kudhibitiwa na Mungu; huku pekee ndiko kumpenda Mungu kweli, na huu pekee ndio ushuhuda thabiti na mkubwa sana.

kutoka katika “Ni kwa Kupitia tu Majaribio ya Kuumiza Ndiyo Mnaweza Kujua Kupendeza kwa Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili

Usivunjike moyo, usiwe dhaifu, Nitakufichulia. Njia ya kwenda kwa ufalme sio laini hivyo, hakuna kitu kilicho rahisi hivyo! Unataka baraka zije kwa urahisi rahisi, sivyo? Leo kila mtu atakuwa na majaribio machungu ya kukumbana nayo, vinginevyo moyo wa upendo ulio nao Kwangu hautakuwa wenye nguvu zaidi na hutakuwa na upendo wa kweli Kwangu. Hata kama ni hali ndogo tu, kila mtu lazima azipitie, ni kwamba tu zinatofautiana kwa kiwango fulani. Hali hiyo ni moja ya baraka Zangu, ni wangapi hupiga magoti mbele Yangu mara kwa mara kuomba baraka Yangu? Watoto wapumbavu! Wewe daima huhisi kwamba maneno machache ya bahati huhesabika kama baraka Yangu, lakini huhisi kuwa uchungu ni moja ya baraka Zangu. Wale wanaoshiriki katika uchungu Wangu bila shaka watashiriki utamu Wangu. Hiyo ni ahadi Yangu na baraka Zangu kwenu.

kutoka katika “Sura ya 41” ya Matamko ya Kristo Mwanzoni katika Neno Laonekana katika Mwili

Wakati Mungu anafanya kazi ili kumsafisha mwanadamu, mwanadamu huteseka. Kadiri usafishaji wake ulivyo mkubwa, ndivyo upendo wake kwa Mungu ulivyo mkubwa zaidi na ndivyo nguvu za Mungu zinafichuliwa zaidi kwake. Kadiri usafishaji wa mwanadamu ulivyo wa kiwango cha chini, ndivyo upendo wake kwa Mungu ulivyo wa kiwango cha chini, na ndivyo nguvu za Mungu zinafichuliwa kwake kwa kiwango cha chini. Kadiri usafishaji wake na uchungu wake ulivyo mkubwa na zaidi yalivyo mateso yake, ndivyo upendo wake wa kweli kwa Mungu utakavyokuwa, ndivyo imani yake kwa Mungu itakavyokuwa ya kweli, na ndivyo maarifa yake ya Mungu yatakuwa ya kina. Katika uzoefu wako utaona kwamba wale ambao wanakabiliwa na usafishaji mkubwa na uchungu, na kushughulikiwa sana na kufundishwa nidhamu, wana upendo mkubwa kwa Mungu, na maarifa ya kina na elekevu ya Mungu. Wale ambao hawajapitia kushughulikiwa wanayo maarifa ya juu juu tu, na wanaweza tu kusema: “Mungu ni mzuri sana, Yeye huwapa watu neema ili waweze kumfurahia Yeye.” Kama watu wamepitia kushughulikiwa na kufundishwa nidhamu, basi hao wanaweza kuyazungumza maarifa ya kweli ya Mungu. Hivyo kazi ya Mungu katika mwanadamu ilivyo ya ajabu zaidi, ndivyo ilivyo ya thamani zaidi na ni muhimu zaidi. Kadiri inavyokosa kupenyeza kwako zaidi na kadiri isivyolingana na mawazo yako, ndivyo kazi ya Mungu inavyoweza kukushinda, kukupata, na kukufanya mkamilifu. Umuhimu wa kazi ya Mungu ni mkubwa sana! Kama Hangemsafisha mwanadamu kwa njia hii, kama Hangefanya kazi kulingana na njia hii, basi kazi ya Mungu haingekuwa na ufanisi na ingekuwa isiyo na maana. Hii ndiyo sababu ya umuhimu wa ajabu wa uteuzi Wake wa kundi la watu katika siku za mwisho. Hapo awali ilisemwa kuwa Mungu angelichagua na kulipata kundi hili. Kadiri ilivyo kuu kazi Anayofanya ndani yenu, ndivyo ulivyo mkubwa na safi upendo wenu kwa Mungu. Kadiri kazi ya Mungu ilivyo kuu zaidi, ndivyo mwanadamu anavyoweza kuonja hekima Yake na ndivyo maarifa ya mwanadamu Kwake yalivyo ya kina zaidi.

kutoka katika “Ni Lazima Wale Wanaofaa Kukamilishwa Wapitie Usafishaji” katika Neno Laonekana katika Mwili

Lazima uvumilie mateso kwa ajili ya ukweli, lazima ujitoe kwa ajili ya ukweli, lazima uvumilie udhalilishaji kwa ajili ya ukweli, na kupata ukweli zaidi lazima upate mateso zaidi. Hili ndilo unalopaswa kufanya. Msitupilie mbali ukweli kwa ajili ya maisha ya amani ya familia, na lazima msiipoteze heshima na uadilifu wa maisha kwa ajili ya starehe ya muda mfupi. Unapaswa kufuata yote ambayo ni ya kupendeza na mema, na unapaswa kufuata njia katika maisha ambayo ni ya maana zaidi. Kama wewe unaishi maisha ya kishenzi, na wala hufuati malengo yoyote, je, si huko ni kupoteza maisha Yako? Ni nini unachoweza kupata kutoka kwa maisha ya aina hii? Unapaswa kuziacha starehe zote za mwili kwa ajili ya ukweli mmoja, na hupaswi kutupilia mbali ukweli wote kwa ajili ya starehe ya muda mfupi. Watu kama hawa hawana uadilifu au heshima; hakuna maana ya kuwepo kwao!

kutoka katika “Matukio Aliyopitia Petro: Ufahamu Wake wa Adabu na Hukumu” katika Neno Laonekana katika Mwili

Wakati ambapo tunapokea hukumu ya maneno ya Mungu, hatupaswi kuogopa mateso, wala hatupaswi kuogopa maumivu; sembuse kuogopa kwamba maneno ya Mungu yataumiza mioyo yetu. Tunapaswa kusoma matamshi Yake zaidi kuhusu jinsi Anavyotuhukumu na kutuadibu na kufichua asili zetu potovu, na tunapokuwa tukisoma maneno ya Mungu, tunapaswa kujilinganisha mara kwa mara dhidi ya maneno hayo. Tuna upotovu huu wote; sote tunaweza kulingana nao. … Kwanza lazima tujue kuwa haijalishi ikiwa maneno yoyote Yake yanavutia kuyasikia, ikiwa yanatufanya tuhisi uchungu au utamu—lazima tuyakubali yote. Tunapaswa kuwa na mtazamo huu juu ya maneno ya Mungu. Mtazamo huu ni wa aina gani? Je, ni mtazamo wa kumcha Mungu? Wa uvumilivu? Au, ni mtazamo wa kuteseka? Nitawaambia, si wowote kati ya hii. Katika imani yetu, lazima tusisitize kwa uthabiti kwamba maneno ya Mungu ndiyo ukweli. Kwa kuwa kweli ndiyo ukweli, tunapaswa kuyakubali kwa busara. Bila kujali ikiwa tunaweza kutambua au kukubali au la, mtazamo wetu wa kwanza kuelekea maneno ya Mungu unapaswa kuwa ule wa kukubali kabisa.

kutoka katika “Umuhimu na Njia ya Kufuatilia Ukweli” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Kumpenda Mungu kunahitaji utafutaji wa mapenzi ya Mungu katika mambo yote, na kwamba ujisaili wewe mwenyewe kwa kina jambo lolote likikutokea, kujaribu kujua mapenzi ya Mungu na kujaribu kuona mapenzi ya Mungu ni yapi katika suala hili, Anataka ufanikishe nini, na ni jinsi gani utayajali mapenzi Yake? Kwa mfano: jambo fulani linafanyika linalokutaka uvumilie hali ngumu, wakati huo unapaswa ufahamu ni nini mapenzi ya Mungu, na ni jinsi gani unapaswa kuyajali mapenzi ya Mungu. Usijiridhishe mwenyewe: Jiweke kando kwanza. Hakuna kitu kilicho duni kuliko mwili. Ni lazima udhamirie kumridhisha Mungu, na ni lazima utekeleze wajibu wako. Katika mawazo kama hayo, Mungu atakupa nuru ya kipekee katika jambo hili, na moyo wako pia utapata faraja. Jambo lolote likikutendekea, liwe dogo au kubwa, ni sharti kwanza ujiweke pembeni na kuuona mwili kama kitu duni zaidi kuliko vitu vyote. Kadiri unavyouridhisha mwili zaidi, ndivyo unavyochukua uhuru zaidi; ukiuridhisha mara hii, wakati mwingine utataka zaidi, na jinsi hili linaendelea, ndivyo unapata kuupenda mwili hata zaidi. Mwili mara zote una tamaa kupita kiasi, mara zote mwili unakutaka uuridhishe, na kwamba uutosheleze kwa ndani, iwe ni katika chakula unachokula, unachokivaa, au kuwa na hasira katika matendo yako, au kuushawishi udhaifu na uzembe wako…. Kadiri unavyouridhisha mwili zaidi, ndivyo tamaa yake inaongezeka, na jinsi mwili unavyopotoka zaidi, hadi kufikia kiwango ambacho miili ya watu inahodhi dhana nzito, na kutomtii Mungu, na kujiinua, na kuanza kuishuku kazi ya Mungu. … Hivyo unafaa kuuasi mwili na usiutosheleze: “Mume wangu(mke), watoto, matarajio, ndoa, familia—hakuna hata moja kati ya haya ambalo ni la thamani! Moyoni mwangu mna Mungu pekee na nitajaribu kumridhisha Mungu kadiri ya uwezo wangu, na si kuuridhisha mwili.” Lazima uwe na azimio hili. Daima ukiwa na azimio hili, basi ukiuweka ukweli katika vitendo, na kujiweka kando, utaweza kufanya hivyo kwa juhudi kidogo.

kutoka katika “Kumpenda Mungu tu Ndiko Kumwamini Mungu Kweli” katika Neno Laonekana katika Mwili

Iwapo utapata uzima mbele za Mungu, na namna hatima yako itakavyokuwa, inategemea uasi wako dhidi ya mwili utakuwa wa namna gani. Mungu amekuokoa, na kukuteua na kukuamulia kabla, bado ikiwa leo hauko radhi kumridhisha, hauko radhi kuuweka ukweli katika vitendo, hauko radhi kuuasi mwili wako kwa moyo umpendao Mungu kwa dhati, hatimaye utajiangamiza mwenyewe, na kwa hivyo utapitia mateso mengi. Ikiwa mara zote unautosheleza mwili, Shetani atakumeza hatua kwa hatua, na kukuacha bila uzima, au upako wa Roho, hadi siku itafika ambayo ndani utakuwa giza. Ukiishi katika giza, utakuwa umetekwa nyara na Shetani, hutakuwa na Mungu tena moyoni mwako, na wakati ule utaukataa uwepo wa Mungu na kumwacha. Kwa hivyo, ikiwa unataka kumpenda Mungu, ni lazima ulipe gharama ya uchungu na kupitia shida. Hakuna haja ya hamasa za nje na shida, kusoma zaidi na kuzungukazunguka zaidi; badala yake, unafaa kuweka kando vitu vilivyomo ndani yako: mawazo kupita kiasi, maslahi ya kibinafsi, na masuala yako binafsi, dhana, na motisha. Hayo ndiyo mapenzi ya Mungu.

kutoka katika “Kumpenda Mungu tu Ndiko Kumwamini Mungu Kweli” katika Neno Laonekana katika Mwili

Mungu anawataka watu kuweka ukweli katika matendo kimsingi kushughulikia mambo yaliyo ndani yao, kushughulikiwa fikira zao, na dhana zao ambazo haziufuati moyo wa Mungu. Roho Mtakatifu huwagusa watu ndani ya mioyo yao, na kuwapa nuru na mwangaza. Kwa hivyo katika tukio lolote katika vita: Kila wakati watu wanapoweka ukweli katika vitendo, au kuweka mapenzi ya Mungu katika vitendo, huwa kuna vita vikali, na japokuwa mambo yanaweza kuonekana shwari katika miili yao, ila ndani ya mioyo yao kutakuwa na vita vya kufa na kupona—na ni baada tu ya hivi vita vikali, baada ya kutafakari kwa kina, ndipo ushindi au kushindwa kunaweza kuamuliwa. Mtu anashindwa kujua ama acheke au alie. Kwa sababu motisha nyingi ndani ya watu zina makosa, ama kwa sababu kazi kubwa ya Mungu inakinzana na dhana zao, watu wakiuweka ukweli katika vitendo vita vikali huzuka kisirisiri. Baada ya kuuweka huu ukweli katika vitendo, kisirisiri watu watakuwa wamemwaga machozi mengi sana ya huzuni kabla ya kuamua kumridhisha Mungu. Ni kwa sababu ya vita hivi watu huvumilia shida na usafishaji; huku ni kuteseka kwa kweli. Vita vikikukabili, kama unaweza kusimama kweli upande wa Mungu, utaweza kumridhisha. Kuteseka katika harakati ya kutenda ukweli hakuepukiki; ikiwa, wanapoweka ukweli katika vitendo, kila kitu ndani yao kingekuwa sawa, basi wasingehitaji kufanywa wakamilifu na Mungu, na kusingekuwa na vita, na hawangeteseka. Ni kwa sababu kuna mambo mengi ndani ya watu ndipo hawafai kutumiwa na Mungu, na tabia nyingi za uasi wa mwili, ndipo watu wanapaswa kujifunza funzo la kuasi dhidi ya mwili kwa kina zaidi. Huku ndiko Mungu anaita kuteseka ambako Alimtaka mwanadamu kushiriki Naye.

kutoka katika “Kumpenda Mungu tu Ndiko Kumwamini Mungu Kweli” katika Neno Laonekana katika Mwili

Katika imani yao kwa Mungu, kile ambacho watu hutafuta ni kupata baraka kwa ajili ya siku zijazo; hili ndilo lengo lao katika imani yao. Watu wote wana kusudi na tumaini hili, lakini upotovu ulio katika asili yao lazima uondolewe kupitia majaribu. Katika hali ambazo bado hujatakaswa, hizi ndizo hali ambamo lazima usafishwe—huu ni mpango wa Mungu. Mungu anakutengenezea mazingira, Akikulazimisha usafishwe hapo ili uweze kujua upotovu wako mwenyewe. Hatimaye, unafika hatua ambapo unaona heri kufa na kuziacha njama na tamaa zako, na kutii mamlaka na mipango ya Mungu. Kwa hiyo, kwa yeyote ambaye hana miaka kadhaa ya usafishaji na hajapitia kiwango fulani cha mateso, hataweza kujiondolea vifungo vya upotovu wa mwili katika mawazo na mioyo yake. Katika hali zozote zile ambazo bado ungali mtumwa wa Shetani, na katika hali zozote zile ambazo bado ungali na tamaa zako mwenyewe na matakwa yako mwenyewe, hizi ndizo hali ambamo unapaswa kuteseka. Ni kupitia mateso tu ndio watu wanaweza kupata mafunzo, kupata ukweli, na kuelewa mapenzi ya Mungu. Kwa kweli, ukweli mwingi unafahamika kwa kupitia majaribu makali. Hakuna anayeweza kufahamu mapenzi ya Mungu, kutambua uweza na busara ya Mungu, wala kuiona tabia ya haki ya Mungu anapokuwa katika mazingira ya utulivu na rahisi au wakati hali ni nzuri. Hilo halingewezekana!

kutoka katika “Namna ya Kumridhisha Mungu Katikati ya Majaribu” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Mungu hufanya kazi ndani ya kila mtu, na bila kujali mbinu Yake ni ipi, Anawatumia watu, vitu na mambo ya aina gani kufanya huduma, au maneno Yake yana sauti ya aina gani, Ana lengo moja tu la mwisho: kukuokoa. Kukuokoa kunamaanisha kukugeuza, na hivyo utakosaje kuteseka kidogo? Ni lazima upate kuteseka. Kuteseka huku kunaweza kuhusisha mambo mengi. Wakati mwingine, Mungu huibua watu, mambo, na vitu ambavyo viko karibu nawe ili kukufunua, kukuwezesha kujitambua, vinginevyo Yeye hukushughulikia moja kwa moja, kukupogoa, na kukufichua. Kama vile tu mtu aliye juu ya meza ya upasuaji–lazima upitie maumivu kiasi kwa ajili ya matokeo mazuri. Kama kila wakati Mungu anapokupogoa na kukushughulikia na kila wakati Anaibua watu, mambo, na vitu, hilo huchochea hisia zako na kukuongezea nguvu, basi kupitia hayo kwa njia hii ni sahihi, na utakuwa na kimo na utaingia katika uhalisi wa ukweli. Ikiwa, kila wakati unapopogolewa na kushughulikiwa, na kila wakati Mungu anapoinua mazingira yako, wewe huhisi maumivu au usumbufu wowote, na huhisi chochote kabisa, na kama huji mbele za Mungu kuelewa mapenzi Yake, wala huombi au kutafuta ukweli, basi wewe kweli ni mtu asiyejali kabisa! Watu ambao hawajali kabisa kamwe si hawatambui kiroho; kwa hiyo, Mungu hana njia ya kufanya kazi kwao. Mungu atasema: “Mtu huyu hajali kabisa na amepotoshwa sana. Nimemfanyia mambo mengi, nimetia bidii nyingi, lakini bado Siwezi kuuita moyo wake na Siwezi kuamsha roho yake. Jambo hili ni sumbufu na gumu sana.” Mungu akipanga mazingira, watu, vitu, na mambo fulani kwa ajili yako, Akikupogoa na kukushughulikia na ukijifunza kutokana na hili, ikiwa umejifunza kuja mbele za Mungu kutafuta ukweli, na, bila kujua, umetiwa nuru na kuangaziwa na kupata ukweli, ikiwa umepitia mabadiliko katika mazingira haya, umepata thawabu, na kupiga hatua, ukianza kuwa na ufahamu mdogo kuhusu mapenzi ya Mungu na kuacha kulalamika, basi yote haya yatamaanisha kuwa umesimama imara katikati ya majaribio ya mazingira haya, na umestahimili jaribio. Kwa hiyo, utakuwa umeshinda majaribu haya.

kutoka katika “Ili Kupata Ukweli, Lazima Ujifunze Kutoka kwa Watu, Mambo, na Vitu Vinavyokuzunguka” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Alhamisi, 25 Aprili 2019

Umuhimu wa Kazi ya Mungu ya Maneno

1. Umuhimu wa Kazi ya Mungu ya Maneno

Maneno Husika ya Mungu:
Katika Enzi ya Ufalme, Mungu anatumia neno ili kukaribisha enzi mpya, ili kubadilisha mbinu za kazi Yake, na kuweza kufanya kazi katika enzi nzima. Hii ndiyo kanuni ambayo kwayo Mungu hufanya kazi katika Enzi ya Neno. Alikuwa mwili ili kuweza kuzungumza kutoka mitazamo tofauti, kumwezesha binadamu kumwona Mungu kwa kweli, ambaye ni Neno linaloonekana katika mwili, na hekima Yake na maajabu. Kazi kama hiyo inafanywa ili kwa njia bora zaidi kutimiza shabaha za kumshinda binadamu, kumkamilisha binadamu, na kumwondoa binadamu. Hii ndiyo maana ya kweli ya kutumia neno ili kufanya kazi katika Enzi ya Neno. Kupitia katika neno, binadamu anajua kazi ya Mungu, tabia ya Mungu, kiini cha binadamu, na kile ambacho binadamu anastahili kuingia ndani yake. Kupitia katika neno, kazi yote ambayo Mungu angependa kufanya katika Enzi ya Neno inatimizwa. Kupitia katika neno, binadamu anafichuliwa, anaondolewa, na kujaribiwa. Binadamu ameliona neno, amelisikia neno, na akapata habari ya uwepo wa neno. Kutokana na haya, binadamu anaamini katika uwepo wa Mungu; binadamu anaamini katika uwezo na hekima za Mungu, pamoja na moyo wa upendo wa Mungu kwa binadamu na tamanio Lake la kumwokoa binadamu. Ingawa neno “neno” ni rahisi na la kawaida, neno kutoka kwenye kinywa cha Mungu mwenye mwili hutikisa dunia nzima; neno Lake hubadilisha moyo wa binadamu, fikira na tabia zee za binadamu, na sura nzee ya ulimwengu mzima. Kupitia enzi nyingi, Mungu pekee wa leo ndiye anayefanya kazi katika njia kama hiyo, na ni Yeye tu Anayeongea na kumwokoa binadamu hivyo. Kuanzia wakati huu kuendelea, binadamu huishi katika mwongozo wa neno, wakichungwa na kuruzukiwa na neno. Binadamu wote wanaishi katika ulimwengu wa neno, wanaishi katika laana na baraka za neno la Mungu, na hata kuna binadamu zaidi wanaoishi chini ya hukumu na kuadibu kwa neno. Maneno haya na kazi hii vyote ni kwa minajili ya wokovu wa binadamu, kwa minajili ya kutimiza mapenzi ya Mungu, na kwa minajili ya kubadilisha sura asilia ya ulimwengu wa uumbaji wa kale. Mungu aliuumba ulimwengu kwa neno, huwaongoza wanadamu kote ulimwenguni kwa neno, na pia hushinda na kuwaokoa binadamu kwa neno. Hatimaye, Yeye atatumia neno ili kuutamatisha ulimwengu mzima wa kale. Ni hapo tu ndipo mpango wa usimamizi unapokuwa mkamilifu kabisa. Katika Enzi nzima ya Ufalme, Mungu hutumia neno kufanya kazi Yake na kutimiza matokeo ya kazi Yake; Hafanyi maajabu au kutenda miujiza; Anafanya tu kazi Yake kupitia kwa neno. Kwa sababu ya neno, binadamu anastawishwa na kuruzukiwa; kwa sababu ya neno, binadamu hupokea maarifa na kupata uzoefu wa kweli. Binadamu katika Enzi ya Neno amepokea kwa kweli baraka za kipekee. Binadamu huwa hapati maumivu ya mwili na hufurahia tu ruzuku nyingi ya neno la Mungu; hawahitaji tena kutafuta au kushika safari, na kwa utulivu huona kuonekana kwa Mungu, wanamsikia Yeye akiongea binafsi, wanapokea ujazo Wake, na kumwona Yeye binafsi akifanya kazi Yake. Haya ndiyo mambo ambayo binadamu katika enzi zilizopita hawakuweza kufurahia, na hizi ndizo baraka ambazo wasingewahi kupokea.

kutoka katika “Enzi ya Ufalme Ndiyo Enzi ya Neno” katika Neno Laonekana katika Mwili

Wakati huo, Yesu alifanya kazi kubwa ambayo haikueleweka kwa wanafunzi Wake, na kusema mengi kwamba watu hawakuelewa. Hii ni kwa sababu, wakati huo, Hakutoa maelezo. Kwa hivyo, miaka kadhaa baada ya Yeye kuondoka, Mathayo aliunda kizazi chake, na wengine pia walifanya kazi kubwa ambayo ilikuwa ya mapenzi ya mwanadamu. Yesu hakuja kumkamilisha na kumpata mwanadamu, lakini kufanya awamu moja ya kazi: kuleta injili ya ufalme wa mbinguni na kukamilisha kazi ya kusulubiwa—na punde tu Yesu Aliposulubishwa, kazi Yake ilifika mwisho kamili. Lakini kwa awamu iliyoko sasa—kazi ya ushindi—maneno mengi zaidi lazima yasemwe, kazi nyingi zaidi lazima ifanywe, na lazima kuwe na hatua nyingi. Hivyo pia ni lazima siri za kazi ya Yesu na Yehova zitafichuliwa, ili wanadamu wote waweze kuwa na ufahamu na uwazi wa imani yao, kwa kuwa hii ni kazi ya siku za mwisho, na siku za mwisho ni mwisho wa kazi ya Mungu, wakati wa kuhitimisha kazi hii. Hii awamu ya kazi itakufafanulia sheria ya Yehova na ukombozi wa Yesu, na ni hasa ili uweze kuelewa kazi nzima ya mpango wa usimamizi wa Mungu wa miaka elfu sita, na kuelewa kusudi la kazi zote Alizozifanya Yesu na maneno Aliyoyasema, na hata upofu wako wa imani kwenye na katika ibada ya Biblia. Yote haya yatakuwezesha kujua. Wewe utakuja kufahamu kazi anayoifanya Yesu na kazi ya Mungu leo; utaelewa na kushuhudia ukweli wote, uzima, na njia. Katika awamu ya kazi Aliyoifanya Yesu, kwa nini Yesu Aliondoka bila kumaliza kazi ya Mungu? Kwa sababu awamu ya kazi ya Yesu haikuwa kazi ya kumalizia. Wakati Yeye Alisulubishwa msalabani, maneno Yake pia yalifika mwisho; baada ya kusulubiwa kwake, kazi Yake kwa hivyo ilimalizika. Awamu ya sasa ni tofauti. Ni baada tu ya maneno hayo kusemwa hadi mwisho na kazi nzima ya Mungu iwe imehitimika ndipo kazi yake itakapokuwa imemalizika. Wakati wa awamu ya kazi ya Yesu, kulikuwa na maneno mengi yaliyobakia bila kusemwa, au ambayo hayakuwa yameelezwa kikamilifu kwa ufasaha. Waama, Yesu hakujali Alichosema au kile ambacho hakusema, kwa kuwa huduma yake haikuwa huduma ya maneno; na hivyo baada ya Yeye kusulubishwa msalabani Aliondoka. Awamu hiyo ilikuwa hasa kwa ajili ya kusulubiwa, na ni tofauti na awamu ya sasa. Awamu ya kazi hii ni hasa kwa ajili ya kukamilisha, kufumbua, na kuleta kazi yote kwenye hitimisho. Kama maneno hayasemwi hadi tamati yake kabisa, hakutakuwa na mbinu ya kuhitimisha kazi hii, kwa kuwa awamu hii ya kazi yote inafikishwa mwisho na kukamilika kwa kutumia maneno. Wakati huo, Yesu Alifanya kazi kubwa isiyoeleweka na mwanadamu. Akaondoka kimyakimya, na leo bado kunao wengi wasioelewa maneno Yake, ambao ufahamu wao ni potofu lakini bado unaaminika nao kwamba ni sahihi, ambao hawajui kuwa wao si sahihi. Mwishoni, awamu hii ya sasa itafikisha kazi ya Mungu mwisho ulio kamilifu, na kutoa hitimisho Lake. Wote watakuja kufahamu na kujua mpango wa usimamizi wa Mungu. Dhana zilizo ndani ya mwanadamu, nia yake, fahamu yake potofu, dhana zake kuhusu kazi ya Yehova na Yesu, maoni yake kuhusu watu wa Mataifa mengine na michepuko yake ingine na makosa yake yatarekebishwa. Na mwanadamu ataelewa njia yote ya haki ya uzima, na kazi yote anayofanya Mungu, na ukweli wote. Wakati hayo yatafanyika, awamu hii ya kazi itafikia kikomo.

kutoka katika “Maono ya Kazi ya Mungu (2)” katika Neno Laonekana katika Mwili

Katika hatua hii ya mwisho ya kazi, matokeo yanapatikana kupitia kwa neno. Kupitia kwa neno, mwanadamu anaelewa mafumbo mengi na kazi ya Mungu katika vizazi vilivyopita; kupitia kwa neno, mwanadamu anapewa nuru na Roho Mtakatifu; kupitia kwa neno, mwanadamu anapata kuelewa mafumbo ambayo hayajawahi kuelezwa na vizazi vilivyopita, na pia kazi za manabii na, mitume wa enzi zilizopita, na kanuni ambazo walitumia kufanya kazi; kupitia kwa neno, mwanadamu anatambua tabia ya Mungu Mwenyewe, na pia uasi na pingamizi ya mwanadamu, na kujua dutu yao. Kupitia kwa hatua hizi za kazi na maneno yote yaliyonenwa, mwanadamu anatambua kazi ya Roho Mtakatifu, kazi ya mwili wa Mungu, na zaidi ya hayo, tabia Yake yote. Maarifa yako ya kazi ya usimamizi wa Mungu wa kupita miaka elfu sita ulitwaliwa kupitia kwa neno. Je, maarifa yako hayakuwa ya fikira zako za awali na mafanikio kwa kuyaweka kando pia yalipatikana kupitia neno? Katika hatua ya awali, Yesu Alifanya ishara na maajabu, lakini sio hivyo katika hatua hii. Je si kuelewa kwako kwa nini Hafanyi hivyo pia kulipatikana kupitia neno? Kwa hivyo, maneno yanenwayo katika hatua hii, yanashinda kazi iliyofanywa na mitume na manabii wa vizazi vilivyopita. Hata unabii uliotabiriwa na manabii haungeweza kupata matokeo haya.

kutoka katika “Fumbo la Kupata Mwili (4)” katika Neno Laonekana katika Mwili

Wakati wa siku za mwisho, Mungu Amekuja mahususi kwa ajili ya kuzungumza maneno Yake. Anazungumza kutokana na mtazamo wa Roho, kutokana na mtazamo wa mwanadamu, na kutokana na mtazamo wa nafsi ya tatu; Anazungumza kwa namna tofauti, Akitumia njia moja kwa kipindi fulani, na Anatumia njia za kuzungumza ili kubadilisha dhana za mwanadamu na kuondoa taswira ya Mungu yakini katika moyo wa mwanadamu. Hii ndiyo kazi kuu iliyofanywa na Mungu. Kwa sababu mwanadamu anaamini kwamba Mungu Amekuja kuponya wagonjwa, kutoa mapepo, kufanya miujiza, na kumpatia mwanadamu baraka za vitu, Mungu Anatekeleza hatua hii ya kazi—kazi ya kuadibu na hukumu—ili kuweza kuondoa mambo hayo kutoka katika dhana za mwanadamu, ili mwanadamu aweze kuuelewa uhalisia na ukawaida wa Mungu, na ili kwamba taswira ya Yesu iweze kuondolewa moyoni mwake na kuwekwa taswira mpya ya Mungu. Mara tu taswira ya Mungu ndani ya mwanadamu inapozeeka, basi inakuwa sanamu. Yesu alipokuja na kutekeleza hatua hii ya kazi, Hakuwakilisha Mungu kikamilifu. Alifanya baadhi ya ishara na maajabu, Alizungumza maneno kadhaa, na hatimaye Akasulubishwa, na Aliwakilisha upande mmoja wa Mungu. Hakuweza kuwakilisha yale yote ambayo ni ya Mungu, bali Alimwakilisha Mungu katika kufanya upande mmoja wa kazi ya Mungu. Hiyo ni kwa sababu Mungu ni mkuu, na ni wa ajabu sana, na Haeleweki, na kwa sababu Mungu Anafanya upande mmoja tu wa kazi Yake katika kila enzi. Kazi inayofanywa na Mungu katika enzi hii ni hasa ya kutoa maneno kwa ajili ya uzima wa mwanadamu, kuweka wazi hulka ya asili ya mwanadamu na tabia ya mwanadamu iliyoharibika, uondoaji wa dhana za kidini, fikra za kinjozi, mitazamo iliyopitwa na wakati, vilevile maarifa na utamaduni wa mwanadamu. Hii ni lazima iwekwe wazi na kusafishwa kupitia maneno ya Mungu. Katika siku za mwisho, Mungu Anatumia maneno na siyo ishara na maajabu ili kumfanya mwanadamu kuwa mkamilifu. Anatumia maneno Yake kumweka wazi mwanadamu, kumhukumu mwanadamu, kumwadibu mwanadamu, na kumkamilisha mwanadamu, ili katika maneno ya Mungu, mwanadamu aje kuona hekima na wema wa Mungu, na aje kuelewa tabia ya Mungu, ili kupitia maneno ya Mungu, mwanadamu aone matendo ya Mungu.

kutoka katika “Kuijua Kazi ya Mungu Leo” katika Neno Laonekana katika Mwili

Katika siku za mwisho, Mungu hasa hutumia neno kumfanya mwanadamu kuwa mkamilifu. Hatumii ishara na maajabu kumdhulumu mwanadamu, ama kumshawishi mwanadamu; hii haiweki wazi nguvu za Mungu. Iwapo Mungu angeonyesha tu ishara na maajabu, basi hakungekuwa na uwezo wa kuweka wazi ukweli wa Mungu, na hivyo haingewezekana kumfanya mwanadamu mkamilifu. Mungu hamfanyi mwanadamu mkamilifu kwa kutumia ishara na maajabu, ila Anatumia neno kunyunyizia na kumchunga mwanadamu, na baada ya haya kunapatikana utiifu kamili wa mwanadamu na ufahamu wa mwanadamu kuhusu Mungu. Hili ndilo lengo la kazi Anayofanya na maneno Anenayo. Mungu hatumii mbinu ya kuonyesha ishara na maajabu ili kumfanya mwanadamu kamili—Anatumia maneno, na Anatumia mbinu nyingi za kazi kumfanya mwanadamu kamili. Iwe ni usafishaji, kushughulikia, upogoaji, ama kupewa maneno, Mungu hunena kutoka taswira nyingi tofauti kumfanya mwanadamu kamili, na kumpa mwanadamu maarifa kuu ya kazi, hekima na ajabu ya Mungu.

kutoka katika “Yote Yanafanikishwa Kupitia kwa Neno la Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili

katika siku za mwisho, Mungu anapokuwa mwili, kimsingi Anatumia neno kukamilisha yote na kufanya yote yawe wazi. Katika maneno Yake pekee ndipo unaweza kuona kile Alicho; ni katika maneno Yake pekee ndiyo unaweza kuona kwamba yeye ni Mungu Mwenyewe. Mungu katika mwili Anapokuja duniani, hafanyi kazi nyingine ila kuongea maneno—hivyo basi hakuna haja ya kutumia uhakika; maneno yanatosha. Hii ni kwa sababu Amekuja kimsingi kufanya kazi hii, kumruhusu mwanadamu aone nguvu Zake na ukuu ulio kwenye neno Lake, kumruhusu mwanadamu kuona kupitia kwa maneno Yake jinsi Alivyojificha kwa unyenyekevu, na kumruhusu mwanadamu kujua ukamilifu Wake kupitia kwa maneno Yake. Kila kitu Alicho nacho na kile Alicho kiko katika maneno Yake, hekima Yake na ajabu yako katika maneno Yake. Katika hii ndipo unapofanywa kuona mbinu nyingi ambazo Mungu anatumia kuongea maneno Yake. Kazi ya Mungu nyingi katika wakati huu wote imekuwa kutoa, ufunuo, na kushughulika mwanadamu. Hatoi laana kwa mwanadamu kijuu juu, na hata Akifanya hivyo, ni kupitia kwa neno. Na hivyo, katika enzi hii ya Mungu kuwa mwili, usijaribu kuona Mungu akiponya wagonjwa na kufukuza mapepo tena, usijaribu kila mara kuona ishara—hakuna haja! Ishara hizo haziwezi kumfanya mwanadamu kamili! Kuongea wazi: Leo Mungu wa kweli Mwenyewe wa mwili Anaongea tu, na hatendi. Huu ni ukweli! Anatumia maneno kukufanya mkamilifu, na Anatumia maneno kukulisha na kukunyunyizia. Pia Anatumia maneno kufanya kazi, na Anatumia maneno badala ya uhakika kukufanya ujue ukweli Wake. Kama una uwezo wa kutazama aina hii ya kazi ya Mungu, basi itakuwa vigumu kuwa wa kutoonyesha hisia. Badala ya kulenga vitu vilivyo vibaya, mnapaswa tu kulenga yale yaliyo mazuri—hivyo ni kusema, bila kujali kama maneno ya Mungu yamekamilika au la, ama iwapo kuna majilio ya ukweli ama haupo, Mungu anamfanya mwanadamu kupata uzima kutoka kwa maneno Yake, na hii ndiyo ishara kuu kushinda zote, na hata zaidi, ni ukweli usiopingika. Huu ndio ushahidi bora wa kupata ufahamu kumhusu Mungu, na ni ishara hata kuu kushinda ishara. Maneno haya pekee yanaweza kumfanya mwanadamu kamili.

kutoka katika “Yote Yanafanikishwa Kupitia kwa Neno la Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili

Ingawa maneno Yangu yanaweza kuwa makali, yote yanasemwa kwa ajili ya wokovu wa mwanadamu, kwa kuwa Ninazungumza tu maneno na sio kuuadhibu mwili wa mwanadamu. Maneno haya humsababisha mwanadamu kuishi katika nuru, kujua kwamba mwanga upo, kujua kwamba mwanga ni wa thamani, hata zaidi kujua jinsi maneno haya yalivyo na manufaa kwa mtu, na kujua kwamba Mungu ni wokovu. Ingawa Nimesema maneno mengi ya kuadibu na hukumu, hayajafanywa kwako katika vitendo. Nimekuja kufanya kazi Yangu, kuzungumza maneno Yangu na, ingawa maneno Yangu yanaweza kuwa magumu, yanasemwa kwa hukumu ya upotovu na uasi wako. Madhumuni Yangu ya kufanya hili yanabaki kumwokoa mtu kutoka kwa utawala wa Shetani, kutumia maneno Yangu ili kumwokoa mwanadamu; Kusudi Langu sio kumdhuru mwanadamu kwa maneno Yangu. Maneno Yangu ni makali ili matokeo yaweze kupatikana kutoka katika Kazi Yangu. Ni katika kufanya kazi kwa njia hii tu ndipo mtu anaweza kujijua na anaweza kujitenga mbali na tabia yake ya uasi. Umuhimu mkubwa zaidi wa kazi ya maneno ni kuwaruhusu watu kuweza kutia katika matendo ukweli baada ya kuuelewa ukweli, kutimiza mabadiliko katika tabia yao, na kutimiza maarifa kuhusu wao wenyewe na kazi ya Mungu. Mbinu za kufanya kazi tu kupitia kwa kuongea ndizo zinazoweza kuleta mawasiliano kuhusu uhusiano kati ya Mungu na mwanadamu, maneno tu ndiyo yanayoweza kuelezea ukweli. Kufanya kazi kwa njia hii ndiyo mbinu bora zaidi ya kumshinda mwanadamu; mbali na matamko ya maneno, hakuna mbinu nyingine inayoweza kumpatia mwanadamu uelewa wa wazi zaidi wa ukweli na kazi ya Mungu, na hivyo basi katika awamu Yake ya mwisho ya kazi, Mungu anazungumza naye mwanadamu ili kuweza kuwa wazi kwa mwanadamu kuhusu ukweli na siri zote ambazo haelewi, na hivyo basi kumruhusu kufaidi njia ya kweli na uzima kutoka kwa Mungu na kisha kutosheleza mapenzi ya Mungu.

kutoka katika “Mnapaswa Kuweka Pembeni Baraka za Hadhi na Kuelewa Mapenzi ya Mungu kwa ajili ya Wokovu wa Mwanadamu” katika Neno Laonekana katika Mwili

Katika enzi hii, Mungu ataleta uhalisi huu miongoni mwenu ili kwamba kila binadamu aweze kuishi kwa kudhihirisha neno la Mungu, aweze kutia ukweli katika matendo, na kumpenda Mungu kwa dhati; kwamba binadamu wote waweze kutumia neno la Mungu kama msingi na uhalisi wao na kuwa na mioyo ya kumcha Mungu; na kwamba, kupitia kwa kutenda neno la Mungu, binadamu basi ataweza kutawala pamoja na Mungu. Hii ndiyo kazi ambayo Mungu atatimiza. Unaweza kuendelea na maisha bila ya kusoma neno la Mungu? Kuna wengi sasa wanaohisi kwamba hawawezi kukaa hata siku moja au mbili bila ya kusoma neno la Mungu. Lazima wasome neno Lake kila siku, na kama muda hauruhusu, kusikiliza neno Lake kunatosha. Hii ndiyo hisia ambayo Roho Mtakatifu anampa binadamu na hii ndiyo namna ambavyo Anaanza kumbadilisha binadamu. Yaani, Hutawala binadamu kupitia kwa maneno ili binadamu aweze kuingia katika uhalisi wa neno la Mungu. Iwapo, baada ya siku moja tu bila kula na kunywa neno la Mungu, unahisi giza na kiu na unaonakuwa halikubaliki, hili linaonyesha kwamba umeguswa na Roho Mtakatifu, na kwamba hajakupa kisogo. Basi wewe ndiye mmoja aliye katika mkondo huu. Hata hivyoiwapo baada ya siku moja au mbili bila kula na kunywa neno la Mungu huhisi chochote, na huna kiu, wala hujaguswa hata kidogo, hili linaonyesha kwamba Roho Mtakatifu amakupa kisogo. Hii inamaanisha, basi, kuwa hali iliyo ndani yako si sahihi; bado hujaingia katika Enzi ya Neno, na wewe ni mmoja aliyebaki nyuma. Mungu hutumia neno ili kumtawala binadamu; unahisi vyema ukila na kunywa neno la Mungu, na kama huhisi hivyo, hutakuwa na njia yoyote ya kufuata. Neno la Mungu linakuwa chakula cha binadamu na nguvu zinazomwendesha. Biblia inasema kwamba “Mwanadamu hataishi kwa mkate pekee, lakini kwa kila neno linalotoka kinywani mwa Mungu”. Hii ndiyo kazi ambayo Mungu ataikamilisha leo. Atafanikisha ukweli huu ndani yenu. Ikoje kwamba binadamu katika siku za kale angekaa siku nyingi bila ya kusoma neno la Mungu lakini angeendelea kula na kufanya kazi? Na kwa nini hali sivyo hivi sasa? Katika enzi hii, Mungu hutumia kimsingi neno ili kutawala yote. Kupitia kwa neno la Mungu, binadamu anahukumiwa na kukamilishwa, kisha hatimaye kupelekwa katika ufalme. Ni neno la Mungu tu linaloweza kuruzuku maisha ya binadamu, na ni neno la Mungu tu ndilo linaloweza kumpa binadamu nuru na njia ya kutenda, hasa katika Enzi ya Ufalme. Mradi tu kila siku unakula na kunywa neno Lake na huachi uhalisi wa neno la Mungu, Mungu ataweza kukukamilisha.

kutoka katika “Enzi ya Ufalme Ndiyo Enzi ya Neno” katika Neno Laonekana katika Mwili

Jumatatu, 22 Aprili 2019

“Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)” Sehemu ya Tatu

“Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)” Sehemu ya Tatu

Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”.
Maudhui ya video hii:
3. Mzunguko wa Uhai na Mauti wa Watu Wanaomfuata Mungu
Mwenyezi Mungu alisema, Baada ya hayo, hebu tuzungumzie mzunguko wa uhai na mauti wa wale wanaomfuata Mungu. Hili linawahusu, hivyo kuweni makini. Kwanza, fikiria kuhusu ni makundi gani ambamo watu wanaomfuata Mungu wanaweza kugawika. (Wateule wa Mungu na watendaji huduma.) Kuna mawili: wateule wa Mungu na watendaji huduma. Kwanza tutazungumza kuhusu wateule wa Mungu, ambao ni wachache. “Wateule wa Mungu” inarejelea nini? Baada ya Mungu kuumba vitu vyote na baada ya kuwepo wanadamu, Mungu alichagua kundi la watu ambao walimfuata, na wanaitwa tu “wateule wa Mungu.” Kuna mipaka maalum na umuhimu katika uchaguzi wa Mungu wa watu hawa. Mipaka ni kwamba kila wakati Mungu anafanya kazi muhimu ni lazima waje—ambacho ni kitu cha kwanza kati ya vinavyowafanya maalum. Na umuhimu wao ni gani? Kuchaguliwa kwao na Mungu kunamaanisha kuwa wana umuhimu mkubwa. Yaani, Mungu angelipenda kuwafanya hawa watu timilifu, na kuwafanya wakamilifu, na baada ya kazi Yake ya usimamizi kuisha, Atawachukua watu hawa. Je, umuhimu huu si mkubwa? Kwa hiyo, hawa wateule ni wa umuhimu mkubwa kwa Mungu, kwa kuwa ni wale ambao Mungu anakusudia kuwapata. Lakini watendaji huduma—vyema, hebu tuachane na uamuzi uliokwisha kufanywa na Mungu, na kwanza tuzungumzie asili yao. Maana ya kawaida ya “mtendaji huduma” ni mtu anayehudumu. Wanaohudumu ni wa kupita; hawahudumu kwa muda mrefu, au milele, ila wanaajiriwa au kuandikwa kwa muda mfupi. Wengi wao wanachaguliwa kutoka miongoni mwa wasioamini. Wajapo duniani ndipo inapoamriwa kwamba watachukua nafasi ya watendaji huduma katika kazi ya Mungu. Wanaweza kuwa walikuwa mnyama katika maisha yao yaliyopita, lakini pia wanaweza kuwa walikuwa mmoja wa wasioamini. Hiyo ndiyo asili ya watendaji huduma.
Hebu turejee kwa wateule wa Mungu. Wanapokufa, wateule wa Mungu huenda sehemu fulani tofauti kabisa na wasioamini na watu mbalimbali wenye imani. Ni sehemu ambayo wanaambatana na malaika na wajumbe wa Mungu, na ambayo inaendeshwa na Mungu binafsi. Japo katika sehemu hii, wateule wa Mungu hawawezi kumwona Mungu kwa macho yao wenyewe, si kama sehemu nyingine yoyote katika milki ya kiroho; ni sehemu ambayo hili kundi la watu huenda baada ya kufa. Wakifa, wao pia hupitia uchunguzi mkali kutoka kwa wajumbe wa Mungu. Na ni nini kinachochunguzwa? Wajumbe wa Mungu huchunguza njia zilizopitiwa na hawa watu katika maisha yao yote katika imani yao kwa Mungu, ikiwa waliwahi au hawakuwahi kumpinga Mungu wakati huo, au kumlaani, na ikiwa walitenda au hawakutenda dhambi mbaya au maovu. Uchunguzi huu unajibu swali la ikiwa mtu fulani ataondoka au atabaki. “Kuondoka” kunarejelea nini? Na “kubaki” kunarejelea nini? “Kuondoka” kunarejelea ikiwa, kulingana na mienendo yao, watabaki miongoni mwa madaraja ya wateule wa Mungu. “Kubaki” kunarejelea kuwa wanaweza kubaki miongoni mwa watu ambao wanafanywa na Mungu kuwa kamili katika siku za mwisho. Mungu ana mipango maalum kwa wale wanaobaki. Katika kila kipindi cha kazi Yake, Mungu atatuma watu kufanya kazi kama mitume au kufanya kazi ya kuyaamsha makanisa, au kuyahudumia. Lakini watu ambao wana uwezo wa kazi kama hizo hawapati miili mara kwa mara kama wasioamini, ambao wanazaliwa upya tena na tena; badala yake, wanarudishwa duniani kulingana na mahitaji na hatua ya kazi ya Mungu, na si wale wapatao mwili mara kwa mara. Je, kuna amri kuhusu ni lini wapate mwili? Je, wanakuja mara moja baada ya kila miaka michache? Je, wanakuja na hiyo haraka? Hawafanyi hivyo. Hii inategemea nini? Inategemea kazi ya Mungu, hatua ya kazi ya Mungu, na mahitaji Yake, na hakuna amri. Amri moja tu ni kwamba Mungu akifanya hatua ya mwisho ya kazi Yake katika siku za mwisho, wateule hawa wote watakuja. Wakija wote, hii itakuwa mara ya mwisho ambapo wanapata mwili. Na kwa nini hivyo? Hii inategemea matokeo yatakayopatikana katika hatua ya mwisho ya kazi ya Mungu—kwani katika hatua hii ya mwisho ya kazi, Mungu atawafanya wateule hawa kuwa kamili kabisa. Hili linamaanisha nini? Ikiwa, katika hii awamu ya mwisho, watu hawa watafanywa kuwa kamili, na kufanywa wakamilifu, basi hawatapata mwili kama awali; mchakato wa kuwa wanadamu utakamilika kabisa, sawa na mchakato wa kupata mwili. Hili linawahusu wale watakaobaki. Je, wale ambao hawawezi kubaki huenda wapi? Wasioweza kubaki wanakuwa na sehemu mwafaka ya kwenda. Kwanza kabisa kwa sababu ya maovu yao, makosa waliyofanya, na dhambi walizofanya, wao pia wanaadhibiwa. Baada ya kuadhibiwa, Mungu anawatuma miongoni mwa wasioamini; kulingana na hali ilivyo, Atafanya mpango wawe miongoni mwa wasioamini, vinginevyo miongoni mwa watu mbalimbali wenye imani. Yaani, wana chaguzi mbili: Moja ni labda waishi miongoni mwa watu wa dini fulani baada ya adhabu, na nyingine ni wawe wasioamini. Kama watakuwa wasioamini, basi watapoteza kila fursa. Lakini wakiwa watu wa imani—kwa mfano, wakiwa Wakristo—bado wangali na nafasi ya kurudi miongoni mwa madaraja ya wateule wa Mungu; kwa hili kuna uhusiano changamano sana. Kwa ufupi, ikiwa mmoja wa wateule wa Mungu atafanya kitu kitakachomkosea Mungu, wataadhibiwa sawa tu na watu wengine. Chukulia Paulo, kwa mfano, ambaye tulizungumzia awali. Paulo ni mfano wa wale wanaoadhibiwa. Je, mnapata picha ya yale ninayozungumzia? Je, mipaka ya wateule wa Mungu ni ya kudumu? (Kwa kiasi kikubwa ni ya kudumu.) Kiasi kikubwa chake ni cha kudumu, lakini sehemu ndogo si ya kudumu. Kwa nini hivyo? (Kwa sababu wametenda maovu.) Nimerejelea hapa mfano mmoja dhahiri: kutenda maovu. Wanapotenda maovu, Mungu hawataki, na wakati Mungu hawataki, anawatupa miongoni mwa makabila na aina mbalimbali za watu, kitu ambacho kinawaacha bila tegemeo na kufanya kurudi kwao kuwe kugumu. Haya yote yanahusu mzunguko wa uhai na mauti wa wateule wa Mungu.
Kinachofuata ni mzunguko wa uhai na mauti wa watendaji huduma. Tulisema asili za watendaji huduma ni gani? (Wengine walikuwa wasioamini, wengine walikuwa wanyama.) Hawa watendaji huduma walipata mwili baada ya kuwa wasioamini au wanyama. Na ujio wa hatua ya mwisho ya kazi, Mungu amechagua kundi la watu hawa kutoka kwa wasioamini, na ni kundi ambalo ni maalum. Nia ya Mungu ya kuchagua watu hawa ni kuhudumia kazi Yake. “Huduma” si neno la jamala kutamka, wala si kitu ambacho mtu yeyote angependa, lakini tunapaswa kuona ambao linawalenga. Kuna umuhimu maalum katika uwepo wa watendaji huduma wa Mungu. Hamna mwingine awezaye kuchukua nafasi yao, kwa kuwa walichaguliwa na Mungu. Na ni ipi nafasi ya watendaji huduma? Kuwahudumia wateule wa Mungu. Kwa ujumla, kazi yao ni kuihudumia kazi ya Mungu, kushirikiana na kazi ya Mungu, na kushirikiana na ukamilisho wa Mungu wa wateule Wake. Haijalishi kama wanafanya kazi ngumu, wanafanya kazi fulani, au wanajiandaa kufanya kazi fulani, ni yapi mahitaji ya Mungu kwa hawa watu? Je, anawadai sana kwa masharti Yake kwao? (La, Mungu anawataka wawe waaminifu.) Watendaji huduma pia wanapaswa kuwa waaminifu. Haijalishi asili zako, au kwa nini Mungu alikuchagua, ni lazima uwe mwaminifu: Ni lazima uwe mwaminifu kwa Mungu, kwa kile anachokuagiza, na vilevile kazi unayoiwajibikia na jukumu unalolifanya. Ikiwa watendaji huduma wanaweza kuwa waaminifu, na kumridhisha Mungu, basi hatima yao itakuwaje? Wataweza kubaki. Je, ni baraka kuwa mtendaji huduma anayebaki? Kubaki kunamaanisha nini? Hii baraka inamaanisha nini? Kihadhi, hawafanani na wateule wa Mungu, wanaonekana tofauti. Kwa hakika, hata hivyo, wakipatacho katika maisha haya siyo sawa na wakipatacho wateule wa Mungu? Angalau, katika haya maisha ni sawa. Hamlipingi hili, naam? Matamko ya Mungu, neema ya Mungu, riziki ya Mungu, baraka za Mungu—ni nani hafurahii vitu hivi? Kila mtu anafurahia wingi wa haya. Kitambulisho cha mtendaji huduma ni mtendaji huduma, lakini kwa Mungu, ni miongoni mwa vitu vyote Alivyoumba—tofauti ni kwamba tu nafasi yao ni ile ya watendaji huduma. Kama mmoja wa viumbe wa Mungu, kuna tofauti kati ya watendaji huduma na wateule wa Mungu? Kwa hakika, hakuna. Kwa mazungumzo ya kawaida, kuna tofauti, katika kiini kuna tofauti, kwa kurejelea nafasi wanazoshika kuna tofauti, ila Mungu hawabagui hawa watu. Hivyo ni kwa nini hawa watu wanatambuliwa kama watendaji huduma? Unapaswa kuelewa hili. Watendaji huduma wanatokana na wasioamini. Kutaja wasioamini kunatuambia kuwa maisha yao ya awali ni mabaya: Wote ni wakana Mungu, katika maisha yao ya nyuma walikuwa wakana Mungu, hawakumwamini Mungu, na walikuwa mahasimu wa Mungu, wa ukweli, na vitu vizuri. Hawakumwamini Mungu, hawakuamini kuwa kuna Mungu, hivi wana uwezo wa kuelewa maneno ya Mungu? Ni haki kusema kwamba, kwa kiwango kikubwa, hawana. Sawa tu na wanyama wasivyo na uwezo wa kuelewa maneno ya mwanadamu, watendaji huduma hawaelewi Mungu anasema nini, Anahitaji nini, kwa nini Ana mahitaji kama hayo—hawaelewi, hivi vitu havieleweki kwao, wanabaki bila nuru. Na kwa sababu hii, watu hawa hawana uhai tuliouzungumzia. Je, bila uhai, watu wanaweza kuelewa ukweli? Je, wana ukweli? Je, wana uzoefu na ufahamu wa maneno ya Mungu? (La.) Hizo ndizo asili za watendaji huduma. Lakini kwa kuwa Mungu anawafanya hawa watu watendaji huduma, bado kuna viwango Anavyohitaji wawe navyo; Hawadharau, na Hawachukulii kwa uzembe. Japo hawaelewi maneno yake, na hawana uhai, bado Mungu ni mwema kwao, na bado kuna viwango Anavyohitaji wawe navyo. Mmevizungumzia hivi viwango hivi karibuni: Kuwa mwaminifu kwa Mungu, na kufanya Asemacho. Katika huduma yako ni lazima uhudumu unapohitajika, na ni lazima uhudumu hadi mwisho. Kama unaweza kuhudumu hadi mwisho, ikiwa unaweza kuwa mtendaji huduma mwaminifu, unaweza kuhudumu hadi mwisho, na unaweza kukamilisha kazi upewayo na Mungu kikamilifu, basi utaishi maisha ya thamani, na utaweza kubaki. Ukitia bidii kidogo, ukijaribu kwa nguvu, ukiongeza maradufu jitihada zako za kumjua Mungu, ukiweza kuongea kidogo kuhusu ufahamu wa Mungu, ukiweza kumshuhudia Mungu, na zaidi, ukielewa kitu kuhusu mapenzi ya Mungu, ukiweza kushirikiana katika kazi ya Mungu, na ukiyazingatia kidogo mapenzi ya Mungu, basi wewe, mtendaji huduma, utapata bahati. Na hili litakuwa badiliko gani katika bahati? Hutaweza kubaki tu. Kutegemea tabia yako na malengo na juhudi zako binafsi, Mungu atakufanya mmoja wa wateule. Hii itakuwa bahati yako. Kwa watendaji huduma, ni nini kizuri kuhusu hili? Ni kwamba unaweza kuwa mmoja wa wateule wa Mungu. Inamaanisha nini ukiwa mmoja wa wateule wa Mungu? Inamaanisha kuwa hawatapata tena mwili kama wanyama au wasioamini. Je, hiyo ni habari njema? Ndiyo, na ni habari njema. Inamaanisha, watendaji huduma wanaweza kufinyangwa. Si kwamba kwa mtendaji huduma, Mungu akimpangia awali kuhudumu, daima atahudumu; si lazima iwe hivyo. Kutegemea tabia yake binafsi, Mungu atamtendea tofauti, na kumjibu tofauti.
Lakini kuna watendaji huduma ambao hawana uwezo wa kumtumikia Mungu hadi mwisho; wakati wa huduma yao, kuna wale ambao wanajitoa nusu na kutelekeza Mungu, kuna wale ambao hufanya mambo mengi mabaya, na hata wale ambao wanasababisha madhara makubwa na kufanya uharibifu mkubwa kwa Kazi ya Mungu, kuna hata watendaji huduma ambao humlaani Mungu, na kadhalika—na ni nini maana ya matokeo haya yasiyorekebishika? Matendo maovu yoyote kama hayo humaanisha kufikia mwisho kwa huduma yao. Kwa sababu matendo yako wakati wa huduma yamekuwa maovu sana, kwa sababu umevuka mipaka yako, wakati Mungu anaona huduma yako haijafikia kiwango Atakutoa ustahiki wa kutoa huduma, Hatakubali ufanye huduma, Atakutoa mbele ya macho Yake, na kutoka katika nyumba ya Mungu. Au ni kwamba hutaki kufanya huduma? Je, siku zote hutamani kufanya maovu? Je, siku zote wewe si mwaminifu? Sawa basi, kuna suluhisho rahisi: Utanyang'anywa ustahiki wako wa kuhudumu. Kwa Mungu, kunyang'anya mtendaji huduma ustahiki wa kufanya huduma kuna maana kuwa mwisho wa mtendaji huduma huyu umetangazwa, na hatakuwa anastahili kufanya huduma kwa Mungu tena, Mungu hahitaji huduma zake tena, na haijalishi ni vitu vipi vizuri atasema, maneno haya yatabaki ya bure. Mambo yanapofikia kiwango hiki, hii hali itakuwa isiyorekebishika; watendaji huduma kama hawa hawana njia ya kurudi nyuma. Na Mungu huwafanyia nini watendaji huduma kama hawa? Anawaachisha tu kutoa huduma? La! Je, Anawazuia tu wasibaki? Au anawaweka katika upande mmoja. Na kuwangoja wabadilike? Hafanyi hivyo. Kwa kweli Mungu hana upendo sana kwa watendaji huduma. Iwapo mtu ana aina hii ya mwelekeo katika huduma yake kwa Mungu, Mungu, kutokana na matokeo ya mwelekeo huu, Atawanyang’anya ustahiki wao wa kutoa huduma, na kwa mara nyingine kuwatupa tena miongoni mwa wasioamini. Na ni ipi hatima ya watendaji huduma waliorudishwa tena kati ya wasioamini? Ni sawa na ile ya wasioamini; kupata mwili kama wanyama na kupokea adhabu ya wasioamini katika ulimwengu wa kiroho. Na Mungu hatakuwa na maslahi ya kibinafsi katika adhabu yao, kwa kuwa hawana umuhimu wowote tena katika kazi ya Mungu. Huu si mwisho tu wa maisha yao ya imani kwa Mungu, ila mwisho wa hatima yao pia, kutangazwa kwa hatima yao. Kwa hiyo watendaji huduma wakihudumu vibaya, watapata matokeo wao wenyewe. Kama mtendaji huduma hana uwezo wa kufanya huduma hadi mwisho kabisa, au amenyang’anywa ustahiki wake wa kutoa huduma katikati ya njia, basi watatupwa miongoni mwa wasioamini—na kama watatupwa miongoni mwa wasioamini watashughulikiwa sawa na jinsi mifugo wanavyoshughulikiwa, sawa na watu wasio na akili au urazini. Ninapoielezea namna hiyo, unaelewa, naam?
Hivyo ndivyo Mungu anavyoushughulikia mzunguko wa uhai na mauti wa wateule wake na watendaji huduma. Mnajihisi vipi baada ya kusikia haya? Nimewahi kuzungumza kuhusu mada ambayo Nimeitaja sasa hivi, mada ya wateule wa Mungu na watendaji huduma? Kwa kweli Nimewahi, lakini hamkumbuki. Mungu ni mwenye haki kwa wateule wake na watendaji huduma. Kwa vyovyote vile Yeye ni mwenye haki, siyo? Kuna mahali popote unaweza kupata makosa? Wapo watu ambao watasema: “Kwa nini Mungu ni mvumilivu sana kwa wateule? Na kwa nini anawavumilia kidogo sana watendaji huduma?” Kuna yeyote angependa kuwatetea watendaji huduma? “Je, Mungu anaweza kuwapa watendaji huduma muda zaidi, na kuwa mstahimilivu na mvumilivu zaidi kwao?” Haya maneno yako sahihi? (Hapana, hayapo sahihi.) Na ni kwa nini hayapo sahihi? (Kwa kuwa tumeonyeshwa neema kweli kwa kufanywa kuwa watendaji huduma.) Watendaji huduma wameonyeshwa neema kwa kuruhusiwa kufanya huduma! Bila ya dhana “watendaji huduma,” na bila Kazi ya watendaji huduma, hawa watendaji huduma wangekuwa wapi? Miongoni mwa wasioamini, wakiishi na kufa pamoja na mifugo. Ni neema iliyoje wanayoifurahia leo, kuruhusiwa kuja mbele za Mungu, na kuja katika nyumba ya Mungu! Hii ni neema kubwa! Kama Mungu hakukupa nafasi ya kutoa huduma, usingekuwa na nafasi ya kuja mbele za Mungu. Kwa kusema machache, hata kama wewe ni Mbudha na umepata maisha ya milele, sanasana wewe ni mtumwa katika ulimwengu wa kiroho; hutaweza kamwe kumwona Mungu, au kusikia sauti Yake, au kusikia maneno Yake, au kuhisi upendo Wake na baraka Zake kwako, na hata isingewezekana kamwe kuonana na Yeye uso kwa uso. Kilicho tu mbele ya wafuasi wa Budha ni kazi rahisi. Hawawezi kamwe kumjua Mungu, na wanaitikia na kutii kiupofu tu, wakati ambapo watendaji huduma wanafaidi mengi sana katika hatua hii ya kazi. Kwanza, wanaweza kuonana na Mungu uso kwa uso, kusikia sauti Yake, kuyasikia maneno Yake, na kupitia neema na baraka Anazowapa watu. Zaidi ya hayo, wanaweza kufurahia maneno na ukweli unaotolewa na Mungu. Wanapata mengi zaidi! Mengi zaidi! Hivyo, kama mtendaji huduma, huwezi hata kufanya juhudi zilizo za kweli, je, Mungu bado atakuweka? Hawezi kukuweka. Hataki mengi kutoka kwako lakini hufanyi chochote Anachotaka vizuri, hujawajibika ipasavyo—na kwa hivyo, bila shaka, Mungu hawezi kukuweka. Hiyo ndiyo tabia ya haki ya Mungu. Mungu hakudekezi, lakini wala Hakubagui. Mungu anafanya kazi na kanuni hizo. Mungu hutekeleza mambo jinsi hii kwa watu na viumbe wote.
Inapokuja katika ulimwengu wa kiroho, kama viumbe mbalimbali waliomo watafanya kitu kibaya, kama hawafanyi kazi yao inavyostahili, Mungu pia ana sheria za peponi na amri zifaazo kuwashughulikia—hili halipingwi. Basi, katika maelfu kadhaa ya miaka ya kazi ya usimamizi ya Mungu, wasimamizi wengine ambao walifanya maovu wameangamizwa, wengine, leo, wangali wanazuiliwa na kuadhibiwa. Hili ndilo linafaa kukabiliwa na kila kiumbe aliye katika ulimwengu wa kiroho. Kama watafanya kitu kibaya au kutenda maovu, wanaadhibiwa—ambayo ni sawa na jinsi Mungu anatenda kwa wateule Wake na watendaji huduma. Na kwa hivyo, iwe ni katika ulimwengu wa kiroho au ulimwengu yakinifu, kanuni ambazo Mungu hutekeleza matendo hazibadiliki. Bila kujali kama unaweza kuona matendo ya Mungu au la, kanuni zao hazibadiliki. Daima, Mungu amekuwa na kanuni sawa kwa jinsi Anavyotekeleza matendo kwa vitu vyote na kuvishughulikia vitu vyote. Hili halibadiliki. Mungu atakuwa mkarimu kwa wale walio miongoni mwa wasioamini ambao angalau wanaishi ipasavyo, na kuwapa nafasi wale walio katika kila dini ambao wana tabia nzuri na hawatendi maovu, kwa kuwaruhusu kutekeleza wajibu wao katika vitu vyote vinavyosimamiwa na Mungu, na kufanya kile ambacho wanafaa kufanya. Vivyo hivyo, kati ya wale wanaomfuata Mungu, kati ya wateule Wake, Mungu habagui mtu yeyote kulingana na kanuni Zake hizi. Ni mwema kwa kila mtu anayeweza kumfuata kwa dhati, na kupenda kila mtu anayemfuata kwa dhati. Ni kwamba tu kwa aina hizi mbalimbali za watu—wasioamini, aina tofauti za watu wenye imani, na wateule wa Mungu—anachowazawadia wao ni tofauti. Chukulia wasioamini: hata kama hawamwamini Mungu, na Mungu huwaona kama mifugo, miongoni mwa kila kitu kila mmoja wao ana chakula, mahali pao wenyewe, na mzunguko wa kawaida wa uhai na mauti. Wanaotenda maovu wanaadhibiwa, na wanaofanya mazuri wanabarikiwa na hupokea wema wa Mungu. Hivyo ndivyo ilivyo? Kwa watu wenye imani, kama wanaweza kutii hasa maadili ya kidini, kizazi baada ya kizazi, basi baada ya hivi vizazi vyote Mungu hatimaye atatoa uamuzi Wake kwao. Vivyohivyo, kwa wewe leo, awe mmoja wa wateule wa Mungu au mtendaji huduma, Mungu vilevile atakuwazisha na kuamua mwisho wako kulingana na kanuni na amri za utawala ambazo Ameziweka. Miongoni mwa aina hizi kadhaa za watu—aina tofauti za watu wa imani, walio katika dini tofauti—je, Mungu amewapa nafasi ya kuishi? Uko wapi Uyahudi? Mungu ameingilia katika imani yao? Hajaingilia, siyo? Na vipi kuhusu Ukristo? Hajaingilia pia? Anawaruhusu kufuata mipangilio yao wenyewe, na Hasemi nao, au kuwapa nuru yoyote, na, zaidi ya hayo, Hawafichulii kitu chochote: “Kama unafikiria ni sahihi, basi amini hivyo!” Wakatoliki wanamwamini Maria, na kwamba ni kupitia kwa Maria ambapo habari zilimfikia Bwana Yesu; hiyo ndiyo aina yao ya imani. Na Mungu amewahi kurekebisha imani yao? Mungu huwapa uhuru, Mungu hawasikizi, na huwapa sehemu fulani ambapo wataishi. Na kwa Waisilamu na wafuasi wa Budha, je, Yuko hivyo pia? Ameweka mipaka kwa ajili yao, pia, na kuwaruhusu kuwa na mahali pao wenyewe pa kuishi, bila ya kuingilia imani zao. Yote yamepangwa vizuri. Na unaona nini katika haya yote? Kwamba Mungu ana mamlaka, lakini hatumii vibaya mamlaka Yake. Mungu hupanga vitu vyote katika mpangilio taratibu, na ni mwenye utaratibu, na katika hili busara na kudura Zake vinadhihirika.
Leo tumezungumzia mada mpya na maalum, ambayo inahusu masuala ya ulimwengu wa kiroho, ambayo ni sehemu mojawapo ya uendeshaji na utawala wa Mungu juu ya ulimwengu wa kiroho. Mlipokuwa hamyaelewi mambo haya, huenda mlisema; “Chochote kinachohusiana na haya ni mafumbo, na hayahusiani na kuingia kwetu katika uhai; mambo haya yametenganishwa na jinsi watu wanaishi hasa, na hatutaki kuyaelewa, wala hatutamani kuyasikia. Hayana uhusiano wowote na kumfahamu Mungu.” Sasa, mnafikiria kuna shida na aina hiyo ya mawazo? Ni sahihi? (La.) Mawazo kama hayo sio sahihi, na yana matatizo makubwa. Hii ni kwa sababu, kama unatamani kujua jinsi Mungu anatawala juu ya vitu vyote, huwezi tu kuelewa kile ambacho unaweza kuona na kile unachokipata kutoka kwa mawazo yako. Ni lazima pia ufahamu ya ulimwengu ule mwingine ambao hauonekani kwako, ambao umeunganishwa kwa njia isiyochanganulika na huu ulimwengu ambao unaweza kuuona. Haya yanahusu ukuu wa Mungu, yanahusu mada ya “Mungu ndiye chanzo cha uhai kwa vitu vyote”; ni taarifa kuhusu hayo. Bila ya hii taarifa, kungekuwepo na dosari na upungufu katika ufahamu kuhusu jinsi Mungu alivyo chanzo cha uhai kwa vitu vyote. Hivyo, kile ambacho tumeongea leo kinaweza kusemwa kuwa kimetamatisha yale tuliyoyaongelea kabla, pamoja na maudhui ya “Mungu ndiye chanzo cha uhai kwa vitu vyote.” Baada ya kuelewa haya, mna uwezo wa kumjua Mungu kupitia maudhui haya? Na kilicho muhimu zaidi ni kwamba leo, Nimewapitisha ujumbe muhimu sana: kuhusu watendaji huduma. Ninajua mnapenda sana kusikia mada kama hizi, kwamba mnayatilia maanani sana mambo haya, basi mnahisi mmeridhika na yale Nimezungumzia leo? (Ndiyo, tumeridhika.) Mwaweza kuwa hamvutiwi sana na vitu vingine, lakini haswa mnavutiwa na mazungumzo kuhusu watendaji huduma, kwa kuwa hii mada inagusia kila moyo wa mmoja wenu.

Jumapili, 17 Machi 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Hudumu kama Waisraeli Walivyofanya

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Hudumu kama Waisraeli Walivyofanya

Siku hizi watu wengi hawatilii maanani mafunzo yapi yanayopaswa kusomwa wakati wa upatano na wengine. Nimegundua kuwa wengi wenu hawawezi kujifunza mafunzo hata kidogo wakati wa ushirikiano na wengine. Wengi wenu mnashikilia maoni yenu mwenyewe, na wakati mnafanya kazi kanisani, unatoa maoni yako na yeye anatoa yake, moja uhusiano na mingine, bila kushirikiana kabisa. Mnajihusisha tu katika kutoa umaizi wenu wenyewe wa ndani, unaingia tu katika kuachilia huru “mizigo” ndani yenu, si kutafuta uzima hata kidogo. Inaonekana kwamba unafanya tu kazi hiyo kwa kutimiza wajibu, daima ukiamini kwamba unapaswa kufuata njia yako mwenyewe bila kujali jinsi watu wengine walivyo, na kwamba unapaswa kushiriki jinsi Roho Mtakatifu anavyokuongoza, bila kujali jinsi watu wengine walivyo. Hamna uwezo wa kugundua uwezo wa wengine, na hamuwezi kujichunguza. Njia yenu ya kupokea vitu ni yenye makosa sana. Inaweza kusemwa kwamba hata sasa bado mnaonyesha kujidai kwingi, kana kwamba ugonjwa huo wa zamani umerejea tena. Hamuwasiliani nyinyi kwa nyinyi ili kufikia uwazi kamili, kama ni matokeo gani yaliyopatikana kwa kuzuru kanisa hilo, au jinsi hali yako ya ndani ilivyokuwa wakati wa hivi karibuni, na kadhalika—ninyi hamuwasiliani tu kwa namna hii. Nyinyi kimsingi hamna mazoea kama vile kuacha dhana zenu wenyewe au kujitelekeza. Wale walio katika uongozi wanafikiri tu kuhusu kuwachangamsha ndugu na dada katika makanisa ya chini kwa njia ya ushirika wao, na wale wanaofuata wanajua tu kufuatilia peke yao. Kimsingi hamuelewi huduma ni nini au ushirikiano ni nini, na mnadhani tu kuhusu kuwa na dhamira nyinyi wenyewe kuulipiza upendo wa Mungu, wa kuwa na dhamira ya nyinyi wenyewe kuishi kwa kudhihirisha mtindo wa Petro, na si kuhusu kitu kingine chochote. Hata unasema, bila kujali jinsi watu wengine walivyo, hamtatii kwa upofu hata hivyo, na bila kujali watu wengine walivyo, ninyi wenyewe unatafuta ukamilifu na Mungu, na hiyo itatosha. Kwa kweli, dhamira yako hayajapata maonyesho thabiti katika uhalisi hata kidogo. Je! Hii sio aina yote ya tabia mnayoonyesha siku hizi. Kila mmoja wenu anashikilia imara utambuzi wenu wenyewe, na ninyi nyote mnataka kufanywa wakamilifu. Ninaona kwamba mmetumikia kwa muda mrefu sana na hamjaendelea sana, hasa katika somo hili la kufanya kazi pamoja kwa maelewano hamjaendelea kabisa! Kuenda kwenye makanisa unawasiliana kwa njia yako, na yeye anafanya ushirika kwa njia yake. Kuna uratibu wa upatanifu kwa nadra sana. Na watu walio chini ambao wanafuata wako namna hii hata zaidi. Ambayo ni kusema kwamba ni watu wachache sana miongoni mwenu wanaelewa kumtumikia Mungu ni nini, au jinsi mtu anapaswa kumtumikia Mungu. Mmechanganyikiwa, na kuchukulia masomo ya aina hii kama suala dogo sana, kwa kiasi kwamba watu wengi hawatekelezi tu kipengele hiki cha ukweli, wanafanya mabaya kwa kujua. Hata watu ambao wametumikia kwa miaka mingi kwa kweli wanapigana na kugombana. Je! Hiki si kimo chako halisi? Ninyi watu mnaohudumu pamoja kila siku ni kama Waisraeli ambao walimtumikia Mungu Mwenyewe katika hekalu kila siku. Inawezekanaje kuwa ninyi watu ambao ni kama makuhani hamjui jinsi ya kushirikiana na jinsi ya kutumikia?
Wakati ule, Waisraeli walimtumikia Yehova moja kwa moja hekaluni. Utambulisho wao ulikuwa ule wa kuhani. (Bila shaka si kila mtu alikuwa kuhani. Ni baadhi tu waliomtumikia Yehova katika hekalu ndio walikuwa na utambulisho wa makuhani). Wangevalia taji ambazo Yehova aliwapa (ambayo inamaanisha walifanya taji kulingana na matakwa ya Yehova, sio kwamba Yehova aliwapa taji moja kwa moja) na wakiwa wamevalia mavazi yao ya kikuhani ambayo Yehova aliwapa wangeingia katika hekalu wakiwa miguu mitupu kumtumikia Yehova moja kwa moja, tangu asubuhi hadi usiku. Utumishi wao kwa Yehova haukuwa usio na mipangalio au wa kutenda makosawapendavyo; yote ilikuwa kulingana na sheria, ambazo hakuna mtu aliyemtumikia Yehova moja kwa moja angeweza kukiuka. Wote walipaswa kufuata sheria hizi; vinginevyo, kuingia hekaluni kulikatazwa. Ikiwa yeyote kati yao alivunja sheria za hekalu, yaani, kama mtu yeyote aliasi amri za Yehova, ilikuwa lazima apate kutendewa kulingana na sheria zilizotolewa na Yehova, na hakuna mtu aliyeruhusiwa kupinga, na hakuna mtu aliyeruhusiwa kumtetea. Haijalishi ni miaka mingapi ambayo mtu huyo alimtumikia Mungu, wote walipaswa kufuata sheria. Hii ndio sababu makuhani wengi walivalia nguo za kikuhani kila wakati na kumtumikia Yehova kwa njia hii mwaka mzima, ingawa Yehova hakuwatendea kwa njia yoyote maalum, na hata walikwenda mbele ya madhabahu au hekalu maisha yao yote. Hivyo ndivyo ulivyokuwa uaminifu wao na utii wao. Haishangazi kwamba Yehova aliwabariki kwa njia hii; ilikuwa yote kutokana na uaminifu wao kwamba walipata kibali na kuyaona matendo yote ya Yehova. Wakati ule ambapo Yehova alifanya kazi katika Israeli, watu Wake waliochaguliwa, matakwa Yake juu yao yalikuwa makali sana. Wote walikuwa watiifu sana na walizuiliwa na sheria, ambazo zilitumika kuwalinda ili kwamba wamheshimu Yehova. Hizi zote zilikuwa amri za utawala za Yehova. Ikiwa miongoni mwa wale makuhani kulikuwa na yeyote ambaye hakuishika Sabato au ambaye alikiuka amri za Yehova na aligunduliwa na watu wa kawaida, huyo mtu angeletwa mara moja mbele ya madhabahu na kupigwa kwa mawe hadi kufa, na hivyo kutolewa kama dhabihu mbele ya “madhabahu ya mtu wa kawaida” ambayo Yehova alikuwa Ameanzisha. Haikuruhusiwa kuweka maiti zao katika hekalu au karibu na hekalu. Yehova hakukubali hilo. Ikiwa mtu alifanya hivyo, angetendewa kama wale ambao hutoa “dhabihu za kawaida,” na kutupwa katika shimo kubwa na kuuawa. Bila shaka, watu wote kama hao wangepoteza maisha yao, hakuna aliyeachwa hai. Kulikuwa hata na wale ambao walitoa “moto wa kawaida,” kwa maneno mengine, wale watu ambao hawakutoa dhabihu katika siku zilizotolewa na Yehova wangeteketezwa na moto wa Yehova pamoja na vitu vyao vya dhabihu, hawaruhusiwa kubaki juu ya madhabahu. Mahitaji kwa makuhani yalikuwa: Hawakuruhusiwa kuingia hekaluni, na hata ua wa nje wa hekalu, bila ya kwanza kuosha miguu yao; hakuna kuingia hekaluni ikiwa hujavalia vazi za kikuhani; hakuna kuingia hekaluni ikiwa hujavalia taji za kikuhani; hakuna kuingia hekaluni ikiwa umechafuliwa na maiti; hakuna kuingia hekaluni baada ya kuugusa mkono wa mtu asiye haki bila ya kwanza kuosha mikono yake mwenyewe; hakuna kuingia hekaluni baada ya mahusiano ya ngono na wanawake (hii haikuwa milele, kwa muda wa miezi mitatu tu), hawakuruhusiwa kuuona uso wa Yehova, wakati ulipokuwa umeisha, ikimaanisha kwamba ni baada ya miezi mitatu tu ndio wangeweza kuruhusiwa kuvaa mavazi safi ya kikuhani, na kuhudumu katika ua wa nje kwa siku saba kabla ya kuweza kuingia katika hekalu ili kuuona uso wa Yehova; waliruhusiwa kuvaa mavazi yote ya kikuhani ndani ya hekalu tu na hawaruhusiwa kuyavaa nje ya hekalu, ili kuepuka kulichafua hekalu la Yehova; iliwapasa wote waliokuwa makuhani kuwaleta wahalifu ambao wamekiuka sheria za Yehova mbele ya madhabahu ya Yehova ambako wangeuawa na watu wa kawaida, vinginevyo moto ungeanguka juu ya kuhani ambaye alishuhudia. Kwa hiyo walikuwa waaminifu kwa Yehova daima, kwa sababu sheria za Yehova zilikuwa kali juu yao, na hawangeweza kabisa kuthubutu kukiuka kikawaida amri Zake za utawala. Waisraeli walikuwa waaminifu kwa Yehova kwa sababu walikuwa wameuona moto Wake, walikuwa wameuona mkono ambao Yehova alitumia kuwaadibu watu, na pia kwa sababu hapo awali walimheshimu Yehova mioyoni mwao. Kwa hivyo kile walichopata sio moto wa Yehova tu; pia walipata utunzaji na ulinzi kutoka kwa Yehova, na kupata baraka za Yehova. Uaminifu wao ni kwamba walifuata maneno ya Yehova katika yale waliyofanya, bila mtu yeyote kuasi. Ikiwa mtu yeyote angekosa kutii, watu bado wangetekeleza maneno ya Yehova, na kuwaua wale wote waliokwenda kinyume na Yehova, bila njia yoyote ya kuficha. Hasa wale ambao walikiuka Sabato, wale waliokuwa na hatia ya uasherati, na wale walioiba sadaka kwa Yehova wangeadhibiwa vikali zaidi. Wale ambao walikiuka Sabato waliuawa kwa mawe nao (watu wa kawaida), au walipigwa viboko hadi kufa, bila yeyote kuachwa. Wale waliofanya vitendo vya uasherati, hata wale waliomtamani mwanamke mzuri, au wale waliokuwa na mawazo ya kiasherati baada ya kumwona mwanamke mwovu, au waliokuwa na tamaa ya kimapenzi baada ya kumwona mwanamke mwenye umri mdogo—kila mtu wa aina hii angeuawa. Ikiwa mwanamke mdogo yeyote ambaye hakuvaa nguo ya kufunika au utaji alimjaribu mwanaume katika kitendo cha tabia mbaya, mwanamke huyo angeuawa. Ikiwa ilikuwa ni kuhani (wale watu ambao walihudumu katika hekalu) ndiye aliyekiuka sheria za aina hii, angesulubiwa au kunyongwa. Hakuna mtu wa aina hii angeweza kuruhusiwa kuishi, na hakuna hata mtu mmoja angeweza kupata kibali mbele za Yehova. Jamaa za mtu wa aina hii hawangeruhusiwa kutoa dhabihu kwa Yehova mbele ya madhabahu kwa miaka mitatu baada ya kifo chake, na hawangeruhusiwa kugawana dhabihu ambazo Yehova aliwapa watu wa kawaida. Wakati tu ulipopita ndio wangeweka ng’ombe au kondoo wa daraja la juu kwenye madhabahu ya Yehova. Ikiwa kulikuwa na kosa lingine lolote, walipaswa kufunga kwa siku tatu mbele za Yehova, wakiomba neema Yake. Kuabudu kwao Yehova hakukuwa tu kwa sababu sheria za Yehova zilikuwa kali sana na za shuruti sana; badala yake ilikuwa ni kwa sababu ya neema ya Yehova, na pia ilikuwa kwa sababu walikuwa waaminifu kwa Yehova. Hivyo, huduma yao hadi leo imekuwa ya uaminifu vilevile, na hawajawahi kuvunja maombi yao mbele ya Yehova. Katika siku hizi watu wa Israeli bado wanapata utunzaji na ulinzi wa Yehova, na hata leo Yehova bado ni neema kati yao, na daima hukaa nao. Wote wanajua jinsi wanapaswa kumheshimu Yehova, na jinsi wanapaswa kumtumikia Yehova, na wote wanajua jinsi wanapaswa kuwa ili kupokea na kulindwa na Yehova, kwa sababu wote wanamcha Yehova mioyoni mwao. Siri ya mafanikio ya huduma yao yote si nyingine isipokuwa uchaji. Lakini nyinyi nyote mko namna gani leo? Je! Mnafanana na watu wa Israeli kwa vyovyote? Je! unafikiri kwamba huduma ya leo ni kama kufuata uongozi wa kielelezo mkubwa wa kiroho? Hamna tu uaminifu na uchaji wowote. Mnapokea neema nyingi, nyinyi ni sawa na makuhani wa Israeli, kwa sababu nyote mnamtumikia Mungu moja kwa moja. Ingawa hamuingii hekaluni, yale mnayopokea na mnayoona ni mengi zaidi kuliko kile ambacho makuhani waliomtumikia Yehova katika hekalu walipokea. Lakini bado mnaasi na mnapinga mara nyingi kuliko walivyofanya. Uchaji wenu ni mdogo sana, na hivyo mnapokea neema ndogo sana. Ingawa mnajitolea kidogo sana, mmepata mengi zaidi kuliko Waisraeli hao. Je! Huku sio kuwatendea nyinyi kwa wema? Wakati wa kazi katika Israeli, hakuna mtu angethubutu kumhukumu Yehova kama alivyotaka. Na nyinyi je? Kama si kwa sababu kazi Ninayofanya miongoni mwenu ni kuwashinda, Ningewezeje kuvumilia kutenda kwenu ovyo ovyo kuliaibisha kwa jina Langu? Ikiwa enzi mnayoishi ingekuwa Enzi ya Sheria, hakuna hata mmoja wenu angekuwa hai, kutokana na matendo yenu na maneno yenu. Uchaji wenu ni mdogo sana! Nyinyi daima mnanilaumu kwa kutowapa kibali kikubwa, na hata kusema kuwa sikuwapa maneno ya baraka ya kutosha, kwamba Nina laana tu kwenu. Je, hamjui kwamba kwa uchaji mdogo hivyo haiwezekani kwenu kukubali baraka Zangu? Je! Hamjui kwamba Mimi huwalaani mara kwa mara na kuwahukumu kwa sababu ya hali mbovu ya huduma yenu? Je, ninyi nyote mnajihisi kuwa mmekosewa? Ninawezaje kuwapa baraka Zangu kikundi cha watu ambao ni waasi na hawatii? Ninawezaje kutoa neema Yangu kwa watu ambao huleta aibu kwa jina Langu? Matendo kwa nyinyi watu tayari ni yenye huruma sana. Ikiwa Waisraeli wangekuwa waasi kama mlivyo leo, Ningalikuwa Nimewaangamiza muda mrefu uliopita. Ilhali Mimi siwatendei kwa vyovyote ila kwa huruma. Je! Huu sio wema? Je! Mnataka baraka nyingi zaidi kuliko hii? Wale pekee ambao Yehova anawabariki ni wale wanaomheshimu Yeye. Yeye huwaadibu wale wanaoasi dhidi Yake, Hamsamehei mtu yeyote kamwe. Je, si ninyi watu wa leo ambao hamjui jinsi ya kutumikia mko na haja zaidi ya kuadibiwa na hukumu, ili mioyo yenu iweze kurekebishwa kikamilifu? Je, kuadibiwa na hukumu ya aina hii sio baraka bora zaidi kwenu? Je! Sio ulinzi wenu bora? Bila hiyo, je, yeyote kati yenu angeweza kuvumilia moto wa Yehova unaochoma? Ikiwa kweli mngetumikia kwa uaminifu kama watu wa Israeli, je, hamngekuwa pia na neema kama rafiki yenu daima? Je, hangekuwa pia na furaha na neema ya kutosha? Je, nyote mnajua jinsi mnapaswa kutumikia?
Leo mahitaji ya nyinyi kufanya kazi pamoja kwa upatanifu ni sawa na jinsi Yehova alivyowataka Waisraeli kumtumikia. Vinginevyo, tamatisha tu huduma yenu. Kwa sababu nyinyi ni watu wanaomtumikia Mungu moja kwa moja, kwa kiwango cha chini zaidi mnapaswa kuweza kuwa waaminifu na watiifu katika huduma yenu, na lazima muweze wa kujifunza masomo kwa njia ya vitendo. Hasa wale wanaofanya kazi kanisani, je, yeyote kati ya ndugu na dada walio chini angethubutu kushughulika na nyinyi? Je, mtu yeyote angethubutu kuwaambia makosa yenu uso kwa uso? Mko juu ya yote, nyinyi kweli mnatawala kama wafalme! Hata hamjifunzi au kuingia katika somo la matendo kama hilo, na bado mnazungumza juu ya kumtumikia Mungu! Kwa sasa unaulizwa kuongoza makanisa kadhaa, na sio tu kwamba unakata tamaa mwenyewe, hata unashikilia mawazo na maoni yako, na kusema mambo kama “Nadhani jambo hili linafaa lifanyike kwa njia hii, kwani Mungu amesema kuwa hatupaswi kuzuiwa na wengine, na kwamba siku hizi hatupaswi kutii kwa upofu.” Kwa hiyo kila mmoja anashikilia maoni yake mwenyewe, na hakuna mtu anayemtii mwingine. Ingawa unafahamu wazi kwamba huduma yako iko katika shida kubwa, bado unasema, “Vile ninavyoona, yangu haiko mbali sana. Kwa hali yoyote sisi kila mmoja ana upande mmoja; unazungumza kuhusu yako, na mimi kuhusu yangu; unashiriki kuhusu maono yako na ninazungumza juu ya kuingia kwangu.” Huchukui jukumu kwa vitu vingi ambavyo vinapaswa kushughulikiwa, au unamudu tu, kila mtu akieleza maoni yake mwenyewe, kwa busara akilinda hali yake mwenyewe, sifa na uso wake. Hakuna mtu aliye tayari kujinyenyekesha, hakuna mtu atakayejitoa kwa ari kumrekebisha mwingine na kurekebishwa ili maisha yaendelee kwa haraka zaidi. Mara chache sana wakati mnafanya kazi pamoja hakuna yeyote kati yenu atasema, Ningependa kukusikia ukishiriki na mimi kuhusu kipengele hiki cha ukweli, kwa sababu bado nina tashwishi kukihusu. Au kusema: una uzoefu zaidi kuliko mimi juu ya jambo hili; unaweza kunipa mwelekeo fulani, tafadhali? Je, si hii ingekuwa njia nzuri ya kufanya hivyo? Nyinyi mlio kwenye viwango vya juu husikia ukweli mwingi, na kuelewa mengi kuhusu huduma. Ikiwa ninyi watu ambao mnaratibu kufanya kazi katika makanisa hamjifunzi kutoka kwa kila mmoja, na kuwasiliana, kufidia mapungufu ya kila mmoja, mnaweza kujifunza masomo kutoka wapi? Mnapokutana na chochote, mnapaswa kushirikiana na kila mmoja, ili maisha yenu yaweze kufaidika. Na mnapaswa kushirikiana kwa makini kuhusu mambo ya aina yoyote kabla ya kufanya maamuzi. Ni kwa kufanya hivyo tu ndio mnakuwa na jukumu kwa kanisa na si kuwa wazembe. Baada ya kutembelea makanisa yote, mnapaswa kukutana na kushiriki juu ya masuala yote mnayotambua na matatizo mnayokabiliwa nayo kazini, na kuwasiliana kuhusu nuru na mwanga ambao mmepokea—huu ni utaratibu wa lazima wa huduma. Lazima mfikie ushirikiano wa upatanifu kwa kusudi la kazi ya Mungu, kwa manufaa ya kanisa, na kwa kuwachochea ndugu na dada kuendelea. Unashirikiana pamoja naye na anashirikiana na wewe, kila mmoja akimbadilisha mwingine, mkifikia matokeo bora ya kazi, ili kutunza mapenzi ya Mungu. Huu tu ndio ushirikiano wa kweli, na watu kama hao tu ndio wana kuingia kwa kweli. Kunaweza kuwa na hotuba fulani isiyofaa wakati wa ushirikiano, lakini hiyo haijalishi. Shirikiana juu yake baadaye, na mpate ufahamu wa wazi kulihusu; msipuuze suala hilo. Baada ya aina hii ya ushirika unaweza kufidia mapungufu kwa ndugu na dada. Ni kwa kuenda kwa kina zaidi tu kwa namna hii katika kazi yako ndio unaweza kufikia matokeo bora. Kila mmoja wenu, kama watu wanaohudumu, lazima muweze kulinda maslahi ya kanisa katika yote mnayofanya, badala ya kuwa macho kwa maslahi yako mwenyewe. Haikubaliki kufanya pekee yako, pale ambapo unamdharau naye anakudharau. Watu wanaotenda kwa njia hii hawafai kumhudumia Mungu! Tabia ya mtu wa aina hii ni mbaya sana; hakuna hata kiasi kidogo cha ubinadamu bado kimebaki ndani yake. Yeye ni Shetani asilimia mia moja! Yeye ni mnyama! Hata sasa mambo kama haya bado yanatokea kati yenu, kwenda mpaka kushambuliana wakati wa ushirika, kutafuta visingizio kwa makusudi, kukasirika mkibishana juu ya jambo fulani dogo, hakuna mtu aliye radhi kujitenga, kila mtu akificha kilicho ndani kutoka kwa mwingine, akimwangalia mwingine na makini na kuwa macho. Je! Tabia ya aina hii ni huduma inayofaa kwa Mungu? Je, kazi kama hiyo yenu inaweza kuwakimu ndugu na dada? Sio tu kuwa huwezi kuwaongoza watu kwenye njia sahihi ya maisha, kwa kweli unaingiza tabia zako za upotovu ndani ya ndugu na dada. Je! Huwaumizi wengine? Dhamiri yako ni mbaya sana, iliyooza kabisa! Huingii katika ukweli, na huutii ukweli katika vitendo. Zaidi ya hayo, bila haya unaonyesha hadharani asili yako ya mbovu sana kwa watu wengine, huoni aibu hata kidogo! Ndugu na dada wamekabidhiwa kwako, lakini unawapeleka kuzimu. Je, si wewe ni mtu ambaye dhamiri yake imeoza? Huna aibu kabisa!
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Jumanne, 12 Machi 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Tabia Yako Ni Duni Sana!

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Tabia Yako Ni Duni Sana!

Ninyi nyote mmeketi katika viti vya kifahari, mkiwafundisha wale wa vizazi vijana ambao ni wa aina yenu, ukiwafanya waketi nawe. Je, mngekosaje kujua kwamba wale “watoto” wenu walikuwa tayari hawana pumzi, na kwamba hawakuwa na kazi Yangu zamani? Utukufu Wangu huangaza kutoka nchi ya Mashariki hadi nchi ya Magharibi, lakini wakati utukufu Wangu huenea mpaka mwisho wa dunia na wakati unapoanza kuinuka na kuangaza, Nitaondoa utukufu wa Mashariki na kuuletea Magharibi ili kwamba watu hawa wa giza katika Mashariki ambao wameniacha Mimi watakuwa bila mwanga unaong’aa kuanzia hapo kwendelea. Wakati huo, mtaishi katika bonde la kivuli. Ingawa watu leo ni wazuri mara mia zaidi kuliko awali, bado hawawezi kuyatosheleza mahitaji Yangu, na bado wao si ushahidi mtukufu Kwangu. Kwamba nyinyi mnaweza kuwa wazuri mara mia zaidi kuliko awali yote ni matokeo ya kazi Yangu—ni tunda la kazi Yangu duniani. Hata hivyo, bado Ninahisi maudhi kwa maneno na matendo yenu, na tabia yenu, na Ninahisi hasira ya ajabu sana kwa matendo yenu mbele Yangu, kwa maana hamna ufahamu wowote Wangu. Kwa hiyo mnawezaje kuwa walio hai kutoka kwa utukufu Wangu, na mnawezaje kuwa waaminifu kabisa kwa kazi Yangu ya baadaye? Imani yenu ni nzuri sana; mnasema kwamba mko radhi kutoa maisha yenu kwa kazi Yangu, kufanya chochote na kila kitu kwa ajili yake, lakini tabia yenu haijabadilika sana. Kumekuwa tu na maneno ya kiburi, na matendo yenu halisi ni duni sana. Inaonekana kwamba ulimi na midomo ya mtu iko mbinguni lakini miguu ya mtu iko mbali sana duniani, hivyo maneno na matendo yake na sifa yake bado yako katika hali mbaya sana. Sifa zenu tayari zimeharibiwa, mwenendo wenu unashuka hadhi, njia yenu ya kuzungumza ni ya chini, maisha yenu ni ya kudharauliwa, na hata ubinadamu wenu wote ni wa chini. Nyinyi ni wa mawazo finyu kwa watu na nyinyi hubishana juu ya kila kitu kidogo. Nyinyi hugombana juu ya sifa zenu na hadhi zenu wenyewe, hata kufikia kiasi kwamba mko radhi kushuka kuzimu, katika ziwa la moto. Maneno na matendo yenu ya sasa yanatosha kiasi kwamba Ninaweza kuamua kuwa nyinyi ni wenye dhambi. Mtazamo wenu juu ya kazi Yangu unatosha Kwangu kutambua kuwa nyinyi ni wale wadhalimu, na tabia zenu zote zinatosha kusema kuwa nyinyi ni roho chafu ambazo zimejaa machukizo. Maonyesho yenu na kile mnachofichua ni tosha kusema kuwa nyinyi ni watu ambao mmekunywa damu ya kutosha ya pepo wachafu. Wakati kuingia katika ufalme kunapozungumzwa hamfichui hisia zenu. Mnaamini kuwa jinsi mlivyo sasa kunatosha kwenu kuingia katika lango la ufalme Wangu wa mbinguni? Je, mnaamini kuwa mnaweza kupata kuingia katika nchi takatifu ya kazi na maneno Yangu bila maneno na vitendo vyenu kupitia majaribio Yangu? Ni nani anayeweza kwa ufanisi kuyadanganya macho Yangu mawili? Je, tabia zenu za mazungumzo ya kudharauliwa na duni, zawezaje kuepuka Mimi kuona? Maisha yenu yameamuliwa na Mimi kama maisha ya kunywa damu ya pepo hizo chafu na kula nyama ya pepo hao wachafu kwa sababu mnachukua sura yao mbele Yangu kila siku. Mbele Yangu tabia zenu zilikuwa mbaya hasa, hivyo, ni vipi Mimi singeweza kuchukizwa? Katika kile mnachosema kuna najisi ya pepo wachafu: Nyinyi hudanganya, huficha, na kujipendekeza kama wale tu wanaofanya uchawi, kama wale wanaodanganya na kunywa damu ya wasio wa haki. Maonyesho yote ya wanadamu ni madhalimu sana, hiyo watu wote wanawezaje kuwekwa katika nchi takatifu ambako wenye haki wapo? Je, unafikiri kwamba tabia hiyo yako ya kudharauliwa inaweza kukubainisha kama mtakatifu dhidi ya wale wadhalimu? Huo ulimi wako unaofanana na nyoka hatimaye utaangamiza mwili wako ambao huleta maangamizi na hufanya machukizo, na mikono yako hiyo ambayo imefunikwa na damu ya pepo wachafu pia itavuta roho yako kuzimu hatimaye, hiyo kwa nini usichukue fursa hii kuitakasa mikono yako iliyofunikwa na uchafu? Na kwa nini huchukui fursa hii kuukata ulimi wako huo ambao husema maneno maovu? Inawezekana kuwa uko radhi kuteseka chini ya moto wa kuzimu kwa sababu ya mikono yako miwili na ulimi wako na midomo? Mimi huilinda mioyo ya watu wote kwa macho Yangu mawili kwa sababu muda mrefu kabla ya kuwaumba wanadamu, Nilikuwa Nimeishika mioyo yao ndani ya mikono Yangu. Zamani Nilibaini moyo wa mwanadamu, kwa hiyo mawazo ya ndani ya moyo wa mwanadamu yanawezaje kuyaepuka macho Yangu? Na wanawezaje kuwepo mapema ili kuepuka kuchomwa kwa Roho Wangu?
Midomo yako ni yenye huruma zaidi kuliko njiwa lakini moyo wako ni mbaya zaidi kuliko nyoka ya kale, hata midomo yako ni mizuri kama mwanamke Mlebanoni, lakini moyo wako si mwema kama ule wa wanawake Walebanoni na hakika hauwezi kulinganishwa na uzuri wa Wakanaani. Moyo wako ni mdanganyifu sana. Ninachochukia ni midomo ya wadhalimu na mioyo ya wadhalimu pekee. Mahitaji Yangu kwa watu si ya juu kuliko watakatifu, ni vile tu kwamba Mimi huhisi chukizo kwa matendo maovu ya wadhalimu na Natumaini kwamba wadhalimu huenda waweze kuondoa kuchafuka kwao na kukimbia kutoka kwa mashaka yao ya sasa ili waweze kutofautishwa na wale wadhalimu, na kuishi na kuwa watakatifu pamoja na wale wenye haki. Nyinyi mko katika hali sawa na Mimi, lakini mmefunikwa na uchafu, hakuna hata mfano kidogo wa wanadamu walioumbwa hapo mwanzo ndani yenu, na kwa sababu kila siku mnaiga mfano wa hao pepo wachafu na mnafanya kile wanachokifanya na kusema kile wanachokisema, kila sehemu zenu na hata ndimi zenu na midomo yenu imelowa katika maji yao mabaya. Ni kwa kiwango ambacho mmefunikwa kabisa na hayo mawaa na hakuna sehemu hata moja ambayo inaweza kutumiwa kwa kazi Yangu. Ni jambo la kusikitisha sana! Mnaishi katika ulimwengu huu wa farasi na ng’ombe lakini bado kwa kweli hamjihisi kuwa na wasiwasi; na mmejaa furaha na nyinyi huishi kwa uhuru na kwa urahisi. Mnaogelea katika maji haya mabaya lakini kwa kweli hamjui kwamba mmeanguka katika mazingira haya. Kila siku unaafikiana na pepo wachafu na una shughuli na “kinyesi.” Uhai wako ni duni sana, lakini hujui kwamba bila shaka huendelei kuishi katika ulimwengu wa kibinadamu na kwamba humo ndani ya ufahamu wako mwenyewe. Je, hujui kwamba maisha yako yalikanyagwa na pepo wachafu zamani, kwamba tabia yako ilivunjiwa hadhi na maji machafu zamani? Je, unadhani kuwa unaishi katika paradiso ya kidunia, kwamba uko katikati ya furaha? Je, hujui kwamba umeishi maisha na pepo wachafu, na kwamba umeishi maisha na kila kitu ambacho wamekuandalia? Je, kuishi kwako kungewezaje kuwa na maana yoyote? Je, maisha yako yangewezaje kuwa na thamani yoyote? Umekuwa ukienda huku na huko kwa ajili ya wazazi wako pepo wachafu, hadi sasa, lakini hujui kwamba wale ambao wanakunasa mtegoni ni hao pepo wachafu, wazazi wako ambao walikuzaa na kukulea. Aidha, hujui kuwa uchafu wako hakika ulipewa wote na wao; yote unayojua ni kwamba wanaweza kukupa “ridhaa,” hawakuadibu, wala hawakuhukumu, na hasa hawakulaani. Hawajawahi kukulipukia kwa ghadhabu, lakini hukutendea kwa bashasha na kwa ukarimu. Maneno yao hulisha moyo wako na kukupendeza mno ili ukanganywe na bila kulitambua, unavutwa ndani na uko radhi kuwa wa huduma kwao, uwe mlango wao na kadhalika mtumishi wao. Huna malalamiko kamwe lakini uko radhi kutumiwa nao—unadanganywa nao. Kwa sababu hii, bila shaka huna majibizo yoyote kwa kazi ambayo Mimi hufanya—si ajabu kwamba wewe daima hutaka kuponyoka kwa siri kutoka kwa mikono Yangu, na si ajabu kwamba wewe daima hutaka kutumia maneno matamu ili kuidanganya fadhila Yangu. Inadhihirika kwamba tayari ulikuwa na mpango mwingine, mpangilio mwingine. Unaweza kuona sehemu ndogo ya vitendo Yangu, vitendo vya Mwenyezi, lakini hujui chembe ya hukumu na kuadibu kwangu. Hujui wakati kuadibu kwangu kulianza; unajua tu jinsi ya kunidanganya Mimi, lakini hujui kuwa Sivumilii ukiukaji na mwanadamu. Kwa kuwa tayari umeweka uamuzi wako kunitumikia Mimi, sitakuacha uende. Mimi ni Mungu mwenye wivu, na Mimi ni Mungu ambaye ana wivu kwa mwanadamu. Kwa kuwa tayari umewekelea maneno yako juu ya madhabahu, Sitakuvumilia wewe kuhudumia mabwana wawili. Je, ulifikiri ungepata upendo mwingine baada ya kuweka maneno yako juu ya madhabahu Yangu, baada ya kuyaweka mbele ya macho Yangu? Ningewezaje kuwaruhusu watu kunidanganya Mimi kwa njia hiyo? Je, ulidhani kwamba ungeweza kuweka nadhiri kikawaida, kula kiapo kunielekea Mimi na ulimi wako? Je, ungewezaje kula kiapo kunielekea kiti Changu cha enzi, Aliye Juu Zaidi? Je, ulifikiri kwamba viapo vyako vilikuwa tayari vimekufa? Nawaambia, hata kama miili yenu ikifa, viapo vyenu haviwezi kufa. Hatimaye, Nitawahukumu kwa msingi wa viapo vyenu. Lakini mnadhani kwamba mnaweza kuweka maneno yenu mbele Yangu ili kunivumilia Mimi na kwamba mioyo yenu inaweza kuwatumikia pepo wachafu na pepo wabaya. Je, hasira Yangu ingewezaje kuwavumilia hao watu mithili ya mbwa na nguruwe wanaonidanganya? Lazima Nitekeleze amri Zangu za kiutawala, na kuwapokonya kutoka kwa mikono ya pepo wachafu wale wote wenye fukuto, “wacha Mungu” ambao wanaamini katika Mimi “kunitumikia” Mimi kwa njia ya mpango, kuwa ng’ombe Wangu, kuwa farasi Wangu na kudhibitiwa na Mimi. Nitakufanya ushike uamuzi wako wa awali na kunitumikia Mimi tena. Siwezi kuvumilia kiumbe yeyote kunidanganya Mimi. Je, ulifikiria kwamba ungeweza kufanya maombi tu kiutukutu na kudanganya kiutukutu mbele Yangu? Je, ulifikiri kwamba Mimi sikuwa nimesikia au kuona maneno na matendo yako? Je, maneno yako na matendo yako yangekosaje kuwa katika mtazamo Wangu? Ningewezaje kuwaruhusu watu kunidanganya Mimi kwa njia hiyo?
Nimekuwa miongoni mwenu, Nimeshirikiana nanyi kwa majira kadhaa ya kuchipua na kwa majira kadhaa ya kupukutika, Nimeishi kati yenu kwa muda mrefu—ni kiasi gani cha tabia yenu ya kudharaulika kimeponyoka mbele ya macho Yangu? Maneno yenu hayo ya dhati daima yarudisha mwangwi ndani ya masikio Yangu; mamilioni na mamilioni ya matarajio yenu yamewekwa juu ya madhabahu Yangu—hayawezi hata kuhesabiwa. Lakini kwa kujitolea kwako na kile mnachokitumia, hakuna hata kidogo. Hakuna hata tone dogo la uaminifu wenu kwenye madhabahu Yangu. Yako wapi matunda ya imani yenu Kwangu? Mmepokea neema isiyo na mwisho kutoka Kwangu na mmeona mafumbo yasiyo na mwisho kutoka mbinguni, na Nimewaonyesha hata miale ya mbinguni lakini Sijawahi kuwa na moyo wa kuwachoma, na ni kiasi gani mmenipa Mimi kama malipo? Je, mko radhi kunipa Mimi kiasi gani? Kama umeshikilia chakula Nilichokupa, unageuka na kunitolea Mimi, hata ukisema kuwa ni kitu ambacho umepata kama malipo kwa jasho la kazi yako ngumu, kwamba unatoa yote uliyo nayo Kwangu. Je, unawezaje kukosa kujua kwamba “michango” yako Kwangu ni vitu vyote vilivyoibwa kutoka kwa madhabahu Yangu? Na sasa unavitoa Kwangu—si wewe unanidanganya Mimi? Unawezaje kukosa kujua kuwa vitu Ninavyovifurahia leo ni matoleo yote juu ya madhabahu Yangu, na sicho kile ulichokichuma kama malipo ya kazi yako ngumu halafu ukanitolea Mimi? Kwa kweli mnathubutu kunidanganya Mimi kwa njia hii, kwa hiyo ni kwa jinsi gani Ninaweza kuwasamehe? Ninawezaje kuvumilia hili zaidi? Nimewapa kila kitu. Nimewafungulia kila kitu, Nikakimu mahitaji yenu, na kuyafungua macho yenu, lakini bado mnanidanganya Mimi kwa njia hii, mkipuuza dhamiri yenu. Bila ubinafsi Nimewapa kila kitu, ili kwamba hata kama mnateseka, mmepata kutoka Kwangu kila kitu Nilichokileta kutoka mbinguni. Lakini hamna kujitolea kamwe, na hata kama mna mchango mdogo, mnalipa deni baada ya hapo. Je, si mchango wako utakuwa bure? Kile ambacho umenipa si chochote isipokuwa chembe moja ya mchanga, lakini kile ulichouliza kutoka Kwangu ni tani moja ya dhahabu. Je, si wewe unakuwa muhali? Ninafanya kazi miongoni mwenu. Hakuna kabisa dalili ya asilimia kumi ambayo Ninapaswa kupata, sembuse dhabihu za ziada. Zaidi ya hayo, asilimia kumi inayochangwa na wale ambao ni wacha Mungu inachukuliwa na wale waovu. Je, si nyinyi wote mmetawanyika kutoka Kwangu? Je, si nyinyi nyote mna uhasama na Mimi? Je, si nyinyi nyote mnaharibu madhabahu Yangu? Je, mtu wa aina hii anawezaje kuonekana kama hazina machoni Pangu? Je, si yeye ni nguruwe, mbwa ambao Ninawachukia? Ningewezaje kurejelea uovu wenu kama hazina? Kazi Yangu kwa kweli ni ya nani? Inawezekana kuwa tu ni ya kuwapiga nyinyi nyote ili kufichua mamlaka Yangu? Je, si maisha yenu yameshikiliwa na neno moja kutoka Kwangu? Ni kwa nini Ninatumia maneno tu kuwaagiza na Sijayageuza maneno kuwa ukweli ili kuwapiga haraka iwezekanavyo? Je, maneno Yangu na kazi Yangu ni ya kuwapiga wanadamu tu? Je, Mimi ni Mungu ambaye huwaua wasio na hatia bila ubaguzi? Hivi sasa, ni wangapi wenu ambao wako hapo mbele Yangu ambao wanatafuta njia sahihi ya maisha ya mwanadamu na nafsi zao nzima? Ni miili yenu tu iliyo mbele Yangu, lakini mioyo yenu iko huru, na iko mbali, mbali na Mimi. Kwa sababu hamjui kwa kweli kazi Yangu ni nini, kuna baadhi yenu ambao mnataka kuondoka Kwangu, mnaojitenga na Mimi, na mnataka kuishi katika mahali hapo pa raha ambapo hakuna kuadibu, hakuna hukumu. Je, hili ndilo watu wanatamani katika mioyo yao? Mimi hakika sikulazimishi. Njia yoyote utakayoichukua ni uchaguzi wako mwenyewe, na njia ya leo huenda sambamba na hukumu na laana, lakini nyote mnapaswa kujua kwamba kile Niliyowapa, iwe ni hukumu au kuadibu, zote ni zawadi bora kabisa Ninazoweza kuwapa, na vyote ni vitu ambavyo mnahitaji kwa dharura.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili