Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo watu-wa-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo watu-wa-Mungu. Onyesha machapisho yote

Alhamisi, 23 Mei 2019

Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu | “Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja” sehemu ya kwanza

Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu | “Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja” sehemu ya kwanza

Mwenyezi Mungu anasema, “Kuingia rahani hakumaanishi kwamba mambo yote yatakoma kusonga, ama kwamba mambo yote yatakoma kuendelea, wala hakumaanishi kwamba Mungu atakoma kufanya kazi ama mwanadamu atakoma kuishi. Ishara ya kuingia rahani ni kama hii: Shetani ameangamizwa; wale watu waovu wanaomuunga mkono Shetani kwa kufanya maovu wameadhibiwa na kuondolewa; nguvu zote za uhasama kwa Mungu zimekoma kuwepo. Mungu kuingia rahani kunamaanisha kwamba Hatafanya tena kazi Yake ya wokovu wa binadamu. Binadamu kuingia rahani kunamaanisha kwamba binadamu wote wataishi ndani ya mwangaza wa Mungu na chini ya baraka Zake; hakutakuwa na upotovu wowote wa Shetani, wala maovu yoyote kutokea. Binadamu wataishi kama kawaida duniani, na wataishi chini ya ulinzi wa Mungu. Mungu na mwanadamu waingiapo rahani pamoja, kutamaanisha kwamba binadamu wameokolewa na kwamba Shetani ameangamizwa, kwamba kazi ya Mungu miongoni mwa mwanadamu imemalizika kabisa. Mungu hataendelea tena kufanya kazi miongoni mwa mwanadamu, na mwanadamu hataendelea tena kumilikiwa na Shetani. Kwa hivyo, Mungu hatakuwa shughulini tena, na mwanadamu hatakimbiakimbia tena; Mungu na mwanadamu wataingia rahani wakati huo huo.“
Kukaribia kwa mwisho wa kila kitu kunaonyesha mwisho wa kazi ya Mungu na kunaonyesha mwisho wa maendeleo ya binadamu. Hii inamaanisha kwamba binadamu kama walivyopotoshwa na Shetani wamefika mwisho wake wa maendeleo, na kwamba vizazi vya Adamu na Hawa vimeenea hadi mwisho wao binafsi, na pia inamaanisha kwamba haiwezekani kwa binadamu kama hawa, baada ya kupotoshwa na Shetani, kuendelea kustawi. Adamu na Hawa wa mwanzoni hawakuwa wamepotoshwa, lakini Adamu na Hawa waliofukuzwa kutoka Bustani ya Edeni walivurugwa na Shetani. Wakati Mungu na mwanadamu wanaingia rahani pamoja, Adamu na Hawa—waliofukuzwa kutoka Bustani ya Edeni—na vizazi vyao hatimaye watafika mwisho; binadamu wa baadaye bado watakuwa na vizazi vya Adamu na Hawa, lakini hawatakuwa watu wanaomilikiwa na Shetani. Badala yake, watakuwa watu waliookolewa na kutakaswa. Hawa watakuwa binadamu ambao wamehukumiwa na kuadibiwa, na walio watakatifu. Hawa watu hawatakuwa sawa na jamii ya binadamu kama ilivyokuwa awali; mtu anaweza kusema kwamba hao ni watu wa aina tofauti kabisa na Adamu na Hawa wa awali. Hawa watu watakuwa wamechaguliwa kutoka miongoni mwa wote waliopotoshwa na Shetani, na watakuwa ndio watu ambao hatimaye wamesimama imara wakati wa hukumu na kuadibu kwa Mungu, watakuwa kundi la mwisho la watu miongoni mwa wanadamu potovu. Kundi hili la watu ndilo tu litaweza kuingia katika raha ya mwisho pamoja na Mungu. Wanaoweza kusimama imara wakati wa kazi ya Mungu ya hukumu na kuadibu siku za mwisho—yaani, wakati wa kazi ya mwisho ya utakaso—watakuwa wale watakaoingia katika raha ya mwisho na Mungu; kwa hivyo, wanaoingia rahani wote watakuwa wametoka katika ushawishi wa shetani na kupokewa na Mungu baada tu ya kupitia kazi Yake ya mwisho ya utakaso. Hawa watu ambao hatimaye wamepokewa na Mungu wataingia katika raha ya mwisho. Kiini cha kazi ya Mungu ya kuadibu na hukumu ni kutakasa binadamu, na ni ya siku ya raha ya mwisho. Vinginevyo, binadamu wote hawataweza kufuata aina yao ama kuingia katika raha. Hii kazi ni njia ya pekee ya binadamu kuingia rahani. Kazi ya Mungu ya utakaso pekee ndiyo itatakasa udhalimu wa binadamu, na kazi Yake ya kuadibu na hukumu pekee ndiyo itadhihirisha hayo mambo yasiyotii miongoni mwa binadamu, hivyo kutenga wanaoweza kuokolewa kutoka wale wasioweza, na wale watakaobaki kutoka wale ambao hawatabaki. Kazi Yake itakapoisha, wale watu watakaobaki watatakaswa na kufurahia maisha ya pili ya binadamu ya ajabu zaidi duniani waingiapo ulimwengu wa juu wa binadamu; kwa maneno mengine, wataingia katika siku ya binadamu ya raha na kuishi pamoja na Mungu. Baada ya wasioweza kubaki kupitia kuadibu na hukumu, umbo zao halisi zitafichuliwa kabisa; baada ya haya wote wataangamizwa na, kama Shetani, hawatakubaliwa tena kuishi duniani. Binadamu wa baadaye hawatakuwa tena na aina yoyote ya watu hawa; watu hawa hawafai kuingia eneo la raha ya mwisho, wala hawafai kuingia siku ya raha ambayo Mungu na mwanadamu watashiriki, kwani ni walengwa wa adhabu na ni waovu, na si watu wenye haki. Walikuwa wamekombolewa wakati mmoja, na pia walikuwa wamehukumiwa na kuadibiwa; walikuwa pia wamemhudumia Mungu wakati mmoja, lakini siku ya mwisho itakapofika, bado wataondolewa na kuangamizwa kwa sababu ya uovu wao na kwa sababu ya kutotii na kutokombolewa kwao. Hawatakuwa tena katika ulimwengu wa baadaye, na hawatakuweko tena miongoni mwa jamii ya binadamu ya baadaye. Watenda maovu wote na yeyote na wote ambao hawajaokolewa wataangamizwa wakati watakatifu miongoni mwa binadamu wataingia rahani, bila kujali kama wao ni roho za wafu ama wale wanaoishi bado katika mwili. Bila kujali enzi ya hizi roho zitendazo maovu na watu watenda maovu, ama roho za watu wenye haki na watu wanaofanya haki wako, mtenda maovu yeyote ataangamizwa, na yeyote mwenye haki ataishi. Iwapo mtu ama roho inapokea wokovu haiamuliwi kabisa kulingana na kazi ya enzi ya mwisho, lakini inaamuliwa kulingana na iwapo wamempinga ama kutomtii Mungu. Kama watu wa enzi ya awali walifanya maovu na hawangeweza kuokolewa, bila shaka wangekuwa walengwa wa adhabu. Kama watu wa enzi hii wanafanya maovu na hawawezi kuokolewa, hakika wao pia ni walengwa wa adhabu. Watu wanatengwa kwa msingi wa mema na mabaya, sio kwa msingi wa enzi. Baada ya kutengwa kwa msingi wa mema na mabaya, watu hawaadhibiwi ama kutuzwa mara moja; badala yake, Mungu atafanya tu kazi Yake ya kuwaadhibu waovu na kuwatuza wema baada ya kufanya kazi Yake ya ushindi katika siku za mwisho. Kwa kweli, Amekuwa akitumia mema na mabaya kutenga binadamu tangu Afanye kazi Yake miongoni mwa binadamu. Atawatuza tu wenye haki na kuwaadhibu waovu baada ya kukamilika kwa kazi Yake, badala ya kuwatenga waovu na wenye haki baada ya kukamilika kwa kazi Yake mwishowe na kisha kufanya kazi Yake ya kuwaadhibu waovu na kuwatuza wazuri mara moja. Kazi Yake ya mwisho ya kuadhibu waovu na kuwatuza wazuri inafanywa kabisa ili kutakasa kabisa binadamu wote, ili Aweze kuleta binadamu watakatifu mno katika pumziko la milele. Hatua hii ya kazi Yake ni kazi Yake muhimu zaidi. Ni hatua ya mwisho ya kazi Yake yote ya usimamizi. Kama Mungu hangewaangamiza waovu lakini badala yake kuwaacha wabakie, basi binadamu wote bado hawangeweza kuingia rahani, na Mungu hangeweza kuleta binadamu katika ulimwengu bora. Kazi ya aina hii haingekuwa imekamilika kabisa. Atakapomaliza kazi Yake, binadamu wote watakuwa watakatifu kabisa. Mungu anaweza kuishi kwa amani rahani kwa namna hii pekee.
Watu leo hawawezi kutengana na mambo ya mwili; hawawezi kuacha starehe za mwili, wala hawawezi kuiacha dunia, pesa, ama tabia yao potovu. Watu wengi wanaendelea na shughuli zao kwa hali ya uzembe. Kwa kweli, hawa watu hawana Mungu mioyoni mwao hata kidogo; zaidi ya hayo, hawamchi Mungu. Hawana Mungu mioyoni mwao, na hivyo hawawezi kutambua yote anayofanya Mungu, na hawawezi kabisa kuamini maneno Azungumzayo kwa mdomo Wake. Watu hawa ni wa mwili sana, wamepotoshwa sana na hawana ukweli wowote, zaidi ya hayo, hawaamini kwamba Mungu anaweza kuwa mwili. Yeyote asiyemwamini Mungu wa mwili—yaani, yeyote asiyeamini kazi na hotuba ya Mungu anayeonekana na haamini Mungu anayeonekana lakini badala yake anaabudu Mungu asiyeonekana mbinguni—hana Mungu katika moyo wake. Ni watu wasiomtii na wanaompinga Mungu. Watu hawa hawana ubinadamu na fahamu, kusema chochote kuhusu ukweli. Kwa watu hawa Mungu anayeonekana na kushikika hawezi kuaminika zaidi, lakini Mungu asiyeonekana wala kushikika ni Mungu wa kuaminika na pia Anayefurahisha nyoyo zao. Wanachotafuta si ukweli wa uhalisi, wala si kiini cha kweli cha uhai, wala nia za Mungu; badala yake, wanatafuta msisimko. Mambo yoyote yanayoweza kuwaruhusu kufikia tamaa zao ni, bila shaka, imani na shughuli zao. Wamwamini Mungu tu ili kuridhisha tamaa zao, si kutafuta ukweli. Hawa watu si watenda maovu? Wanajiamini sana, na hawaamini kwamba Mungu aliye mbinguni atawaangamiza, hawa “watu wazuri.” Badala yake, wanaamini kwamba Mungu atawaruhusu kubaki na, zaidi ya hayo, Atawatuza vizuri sana, kwani wamemfanyia Mungu mambo mengi na kuonyesha kiwango kikubwa cha “uaminifu” Kwake. Kama wangemtafuta Mungu anayeonekana, wangelipiza kisasi mara moja dhidi ya Mungu na kukasirika wakati hawatapata tamaa zao. Hawa ni watu waovu wanaotaka kuridhisha tamaa zao; si watu wa uadilifu wanaosaka ukweli. Watu kama hao ni wale wanaojulikana kama waovu wanaomfuata Kristo. Wale watu wasioutafuta ukweli hawawezi kuamini ukweli. Hawawezi kabisa kutambua matokeo ya baadaye ya binadamu, kwani hawaamini kazi ama hotuba yoyote ya Mungu anayeonekana, na hawawezi kuamini hitimisho la baadaye la binadamu. Hivyo, hata wakimfuata Mungu anayeonekana, bado wanatenda maovu na hawatafuti ukweli, wala hawatendi ukweli Ninaohitaji. Wale watu wasioamini kwamba wataangamizwa kinyume ni kwamba ni wale watu watakaoangamizwa. Wote wanajiamini kuwa wajanja sana, na wanaamini kwamba wao wenyewe ndio wanaotenda ukweli. Wanafikiria mwenendo wao mbovu kuwa ukweli na hivyo wanauthamini. Hawa watu waovu wanajiamini sana; wanachukua ukweli kuwa mafundisho ya dini, na kuchukua vitendo vyao vibovu kuwa ukweli, na mwishowe watavuna tu walichopanda. Watu wanapojiamini zaidi na wanapokuwa na kiburi zaidi, ndipo hawawezi zaidi kupata ukweli; watu wanapomwamini Mungu wa mbinguni zaidi, ndipo wanampinga Mungu zaidi. Hawa ndio watu watakaoadhibiwa. Kabla ya binadamu kuingia rahani, iwapo kila aina ya mtu ataadhibiwa ama kutuzwa kutaamuliwa kulingana na iwapo wanatafuta ukweli, iwapo wanamjua Mungu, iwapo wanaweza kumtii Mungu anayeonekana. Waliomhudumia Mungu anayeonekana lakini bado hawamjui wala kumtii hawana ukweli. Watu hawa ni watenda maovu, na watenda maovu bila shaka wataadhibiwa; zaidi ya hapo, wataadhibiwa kulingana na mienendo yao mibovu. Mungu ni wa mwanadamu kumwamini, na pia Anastahili utii wa mwanadamu. Wale wanaomwamini tu Mungu asiye yakini na asiyeonekana ni wale wasiomwamini Mungu; zaidi ya hapo, hawawezi kumtii Mungu. Kama hawa watu bado hawawezi kumwamini Mungu anayeonekana wakati kazi Yake ya ushindi inakamilika, na pia wanaendelea kutomtii na kumpinga Mungu anayeonekana katika mwili, hawa wanaoamini isiyo yakini bila shaka, wataangamizwa. Ni kama ilivyo na wale miongoni mwenu—yeyote anayemtambua Mungu Aliyepata mwili kwa maneno lakini bado hatendi ukweli wa utii kwa Mungu Aliyepata mwili hatimaye ataondolewa na kuangamizwa, na yeyote anayemtambua Mungu anayeonekana na pia kula na kunywa ukweli ulioonyeshwa na Mungu anayeonekana lakini bado anamtafuta Mungu asiye yakini na asiyeonekana pia yeye ataangamizwa baadaye. Hakuna hata mmoja wa watu hawa anayeweza kubaki hadi wakati wa pumziko baada ya kazi ya Mungu kukamilika; hakuwezi kuwa yeyote kama watu hawa atakayebakia hadi wakati wa pumziko. Watu wenye pepo ni wale wasiotenda ukweli; asili yao ni ile inayompinga na kutomtii Mungu, na hawana nia hata kidogo za kumtii Mungu. Watu wote kama hao wataangamizwa. Iwapo una ukweli na iwapo unampinga Mungu hayo yanaamuliwa kulingana na asili yako, si kulingana na sura yako ama hotuba na mwenendo wako wa mara kwa mara. Asili ya kila mtu inaamua iwapo ataangamizwa; hii inaamuliwa kulingana na asili iliyofichuliwa na mienendo yao na kutafuta kwao ukweli. Miongoni mwa watu wanaofanya kazi sawa na pia kufanya kiasi sawa cha kazi, wale ambao asili yao ni nzuri na wanaomiliki ukweli ni watu wanaoweza kubaki, lakini wale ambao asili yao ya ubinadamu ni mbovu na wasiomtii Mungu anayeonekana ni wale watakaoangamizwa. Kazi ama maneno yoyote ya Mungu yanayoelekezwa kwa hatima ya binadamu yanahusiana na binadamu ipasavyo kulingana na asili ya kila mtu; hakutakuwa na ajali yoyote, na hakika hakutakuwa na kosa hata kidogo. Mtu anapofanya kazi tu ndipo hisia za binadamu ama maana itachanganywa ndani. Kazi anayofanya Mungu ndiyo inayofaa zaidi; hakika Hataleta madai ya uongo dhidi ya kiumbe yeyote. Sasa kuna watu wengi wasioweza kutambua hatima ya baadaye ya binadamu na ambao pia hawaamini maneno Nisemayo; wote wasioamini, pamoja na wasiotenda ukweli, ni mapepo!
Wanaotafuta na wasiotafuta sasa ni aina mbili tofauti ya watu, na wao ni aina mbili ya watu na hatima mbili tofauti. Wanaotafuta maarifa ya ukweli na kutenda ukweli ni watu ambao Mungu ataokoa. Wale wasiojua njia ya ukweli ni mapepo na adui; ni vizazi vya malaika mkuu na wataangamizwa. Hata wacha Mungu wanaomwamini Mungu asiye yakini—je, si mapepo pia? Watu wanaomiliki dhamiri nzuri lakini hawakubali njia ya ukweli ni mapepo; asili yao ni ile inayompinga Mungu. Wale wasiokubali njia ya ukweli ni wale wanaompinga Mungu, na hata kama watu hawa wanavumilia taabu nyingi, bado wataangamizwa. Wasio tayari kuiwacha dunia, wasioweza kuvumilia kutengana na wazazi wao, wasioweza kuvumilia kujiondolea raha zao za mwili, wote hawamtii Mungu na wote wataangamizwa. Yeyote asiyemwamini Mungu aliyepata mwili ni pepo; zaidi ya hayo, wataangamizwa. Wanaoamini lakini hawatendi ukweli, wasiomwamini Mungu aliyepata mwili, na wale ambao hawaamini kabisa kuwepo kwa Mungu wataangamizwa. Yeyote anayeweza kubaki ni mtu ambaye amepitia uchungu wa usafishaji na kusimama imara; huyu ni mtu ambaye kweli amepitia majaribio. Yeyote asiyemtambua Mungu ni adui; yaani, yeyote aliye ndani ama nje ya mkondo huu ambaye hamtambui Mungu aliyepata mwili ni adui wa Kristo! Shetani ni nani, mapepo ni nani, na nani ni maadui wa Mungu kama si wapinzani wasiomwamini Mungu? Wao si watu wasiomtii Mungu? Wao si watu wanaodai kwa maneno kuamini lakini hawana ukweli? Wao si wale watu wanaofuata tu kupata kwa baraka lakini hawawezi kumshuhudia Mungu? Bado unaweza kushiriki na wale mapepo leo na kusisitiza dhamiri na mapenzi na hawa mapepo; je, hii haichukuliwi kuwa kueneza nia nzuri kwa Shetani? Haichukuliwi kuwa kushiriki na mapepo? Kama watu bado hawawezi kutofautisha kati ya mazuri na maovu leo, na bado wanasisitiza kwa upofu mapenzi na huruma bila kwa njia yoyote kutamani kutafuta matakwa ya Mungu, na hawawezi kwa njia yoyote kuwa na moyo wa Mungu kama wao, mwisho wao utakuwa dhalili zaidi. Yeyote asiyemwamini Mungu wa mwili ni adui wa Mungu. Kama unaweza kusisitiza dhamiri na mapenzi kwa adui, je, hujakosa hisia ya haki? Kama unalingana na wale Ninaowachukia na kutokubaliana nao, na bado unasisitiza mapenzi na hisia za binafsi nao, basi wewe si asiyetii? Humpingi Mungu kimakusudi? Je, mtu kama huyu anamiliki ukweli? Ikiwa watu wanasisitiza dhamiri kwa adui, kusisitiza upendo kwa mapepo na kusisitiza huruma kwa Shetani, hawakatizi kazi ya Mungu kimakusudi? Wale watu wanaomwamini Yesu tu na hawamwamini Mungu aliyepata mwili wakati wa siku za mwisho na wale wanaodai kwa maneno kumwamini Mungu aliyepata mwili lakini wanafanya maovu wote ni adui wa Kristo, sembuse wale watu wasiomwamini Mungu. Hawa watu wote wataangamizwa. Kiwango ambacho mwanadamu anamhukumu mwanadamu kinatokana na tabia zake; aliye na mwenendo mzuri ni mtu mwenye haki, na aliye na mwenendo wa kuchukiza ni mwovu. Kiwango ambacho Mungu anamhukumu mwanadamu kinatokana na iwapo asili ya mtu inamtii Yeye; anayemtii Mungu ni mtu mwenye haki, na asiyemtii Mungu ni adui na mtu mwovu, bila kujali iwapo tabia ya mtu huyu ni nzuri ama mbaya, na bila kujali iwapo hotuba ya mtu huyu ni sahihi ama si sahihi. Watu wengine wanatamani kutumia matendo mazuri kupata hatima nzuri ya baadaye, na watu wengine wanataka kutumia hotuba nzuri kununua hatima nzuri. Watu wanaamini kimakosa kwamba Mungu anaamua matokeo ya mwanadamu kulingana na tabia ama hotuba yake, na kwa hivyo watu wengi watataka kutumia haya kupata fadhila ya muda mfupi kupitia udanganyifu. Watu ambao baadaye watasalimika kupitia pumziko wote watakuwa wamevumilia siku ya dhiki na pia kumshuhudia Mungu; wote watakuwa watu ambao wamefanya jukumu lao na wana nia ya kumtii Mungu. Wanaotaka tu kutumia fursa kufanya huduma ili kuepuka kutenda ukweli hawataweza kubaki. Mungu ana viwango sahihi vya mipangilio ya matokeo ya kila mtu; Hafanyi tu maamuzi haya kulingana na maneno na mwenendo wa mtu, wala Hayafanyi kulingana na tabia zao wakati wa kipindi kimoja cha muda. Hakika Hatakuwa na huruma na mwenendo wowote mbaya wa mtu kwa sababu ya huduma ya mtu ya zamani kwa Mungu, wala Hatamnusuru mtu kutokana na kifo kwa sababu ya gharama kwa Mungu ya mara moja. Hakuna anayeweza kuepuka adhabu ya uovu wake, na hakuna anayeweza kuficha tabia zake mbovu na hivyo kuepuka adhabu ya maangamizi. Kama mtu anaweza kweli kufanya jukumu lake, basi inamaanisha kwamba ni mwaminifu milele kwa Mungu na hatafuti tuzo, bila kujali iwapo anapokea baraka ama bahati mbaya. Kama watu wana uaminifu kwa Mungu waonapo baraka lakini wanapoteza uaminifu wao wasipoweza kuona baraka na mwishowe bado wasiweze kumshuhudia Mungu na bado wasiweze kufanya jukumu lao kama wapasavyo, hawa watu waliomhudumia Mungu wakati mmoja kwa uaminifu bado wataangamizwa. Kwa ufupi, watu waovu hawawezi kuishi milele, wala hawawezi kuingia rahani; watu wenye haki tu ndio mabwana wa pumziko. Baada ya binadamu kuingia katika njia sawa, watu watakuwa na maisha ya kawaida ya binadamu. Wote watafanya jukumu lao husika na kuwa waaminifu kabisa kwa Mungu. Watatoa kabisa kutotii kwao na tabia yao iliyopotoshwa, na wataishi kwa ajili ya Mungu na kwa sababu ya Mungu. Watakosa uasi na upinzani. Wataweza kabisa kumtii Mungu. Haya ndiyo maisha ya Mungu na mwanadamu na maisha ya ufalme, na ni maisha ya pumziko.
kutoka kwa Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja

Jumanne, 30 Aprili 2019

Adabu Takatifu Ambayo Waumini wa Mungu Wanapasa Kuwa Nayo

4. Adabu Takatifu Ambayo Waumini wa Mungu Wanapasa Kuwa Nayo

Maneno Husika ya Mungu:
Ni nini kinashirikishwa ndani ya ubinadamu wa kawaida? Utambuzi, hisia, dhamiri na tabia. Iwapo unaweza kufanikisha ukawaida katika kila mojawapo ya vipengele hivi, ubinadamu wako uko katika kiwango kinachostahili. Unapaswa kuwa na mfanano wa binadamu wa kawaida na utende kama anayemwamini Mungu. Sio lazima ufikie viwango vya juu zaidi au kujishughulisha na diplomasia. Unapaswa tu kuwa mwanadamu wa kawaida, na hisia za kawaida za mtu, uweze kung’amua vitu, na kwa kiwango cha chini uonekane kama mwanadamu wa kawaida. Hiyo itakuwa imetosha. Kila kitu kinachohitajika kwako leo kiko katika uwezo wako, na huku si kukulazimisha ufanye kadri ya uwezo wako hata kidogo. Hakuna maneno yasiyo na maana au kazi isiyofaa yatakayotekelezwa kwako. Uovu wote ulioonyeshwa au kufichuliwa katika maisha yako lazima uondolewe. Ninyi mmepotoshwa na Shetani na mna sumu nyingi sana za Shetani. Yote ambayo yanahitajika kwako ni kuiepuka tabia hii potovu ya kishetani, si wewe kuwa mtu mwenye cheo cha juu, au mtu maarufu au mkuu. Hii haina maana. Kazi ambayo imefanyika kwenu inaafikiana na kile ambacho ni cha asili kwenu. Kuna mipaka ya kile Ninachohitaji kutoka kwa watu. Ikiwa watu wa leo wote wangeombwa kutenda kama watu wa kada za Kichina, na kujizoeza toni ya sauti ya kada za Kichina, kujifunza katika namna ya kuzungumza ya viongozi wa serikali wenye cheo cha juu, au kujifunza kwa namna na sauti ya kuzungumza ya waandishi wa insha na waandishi wa riwaya, basi hili halingekubalika pia. Halingeweza kufikiwa. Kwa mujibu wa ubora wa tabia zenu, mnapaswa angalau kuweza kuzungumza kwa hekima na busara na kuelezea mambo wazi. Ni wakati huo ndipo mtakapoyatosheleza mahitaji. Kwa kiwango kidogo sana, utambuzi na hisia vinapaswa kufikiwa. Kwa sasa jambo kuu ni kuitupilia mbali tabia potovu ya kishetani. Lazima uutupilie mbali uovu unaouonyesha. Ikiwa hujavitupilia mbali hivi, unawezaje kugusia hisia na utambuzi wenye mamlaka mkubwa kabisa? Watu wengi wanaona kwamba enzi imebadilika. Hivyo hawajizoezi unyenyekevu au uvumilivu wowote, na pengine pia hawana upendo wowote au mwenendo mwema wa kitakatifu pia. Watu hawa ni wajinga mno! Je, wana kiwango chochote cha ubinadamu wa kawaida? Je, wanao ushuhuda wowote wa kuzungumziwa? Hawana utambuzi na hisia zozote kamwe. Bila shaka, vipengele fulani vya utendaji wa watu vilivyopotoka na vyenye makosa vinapaswa kurekebishwa. Kama vile maisha ya watu ya kiroho yasiyopindika ya zamani au mwonekano wao wenye ganzi na upumbavu—vitu hivi vyote vinapaswa kubadilika. Mabadiliko hayamaanishi kukuruhusu uwe mpotovu au kujiingiza katika mwili, kusema chochote utakacho. Kuzungumza kiholela hakuwezi kukubalika. Kutenda kama mwanadamu wa kawaida ni kuzungumza kwa kueleweka. Ndiyo inamaanisha ndiyo, na la inamaanisha la. Kuwa mwenye ukweli kwa uhakika na uzungumze inavyofaa. Usilaghai, usidanganye. Inapaswa kujulikana ni mipaka gani mtu wa kawaida anaweza kufikia kuhusu mabadiliko ya tabia. Ikiwa hiyo haijulikani, hutaweza kuingia katika uhalisi.
kutoka katika “Kuendeleza Ubora wa Tabia ni Kwa Ajili ya Kupokea Wokovu wa Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili
Katika tabia za watu wa kawaida hakuna uhalifu au udanganyifu, watu wana uhusiano wa kawaida kati yao, hawafanyi mambo pekee yao, na maisha yao si duni wala ya kufifia. Kwa hiyo, vilevile, Mungu huinuliwa miongoni mwa wote, maneno Yake hupenya miongoni mwa wanadamu, watu huishi katika amani kati yao na chini ya utunzaji na ulinzi wa Mungu, dunia imejaa upatanifu, bila kuingilia kwa Shetani, na utukufu wa Mungu huwa na umuhimu mkuu sana miongoni mwa wanadamu. Watu kama hao ni kama malaika: watakatifu, wa kusisimua, wasiolalamika kamwe kuhusu Mungu, na hutoa juhudi zao zote kwa utukufu wa Mungu duniani pekee.
kutoka katika “Sura ya 16” ya Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima katika Neno Laonekana katika Mwili
Nina matamanio mengi. Natamani mweze kutenda kwa njia inayofaa na yenye mwenendo mzuri, muwe waaminifu kutimiza wajibu wenu, muwe na ukweli na ubinadamu, muwe watu ambao wanaweza kuacha vitu vyote na kuyatoa maisha yao kwa ajili ya Mungu, na mengineyo. Matumaini haya yote yanatokana na upungufu wenu na upotovu na kutotii kwenu.
kutoka katika “Dhambi Zitampeleka Mwanadamu Jahanamu” katika Neno Laonekana katika Mwili
Watu ambao Mungu hutumia huonekana kwa nje kama watu wasio na akili na huonekana kama wasio na uhusiano wa kawaida na wengine, ingawa wao huzungumza na adabu, hawazungumzi kiholela, na wanaweza daima kuwa na moyo uliotulia mbele ya Mungu. Lakini ni mtu wa aina hiyo tu ndiye anatosha kutumiwa na Roho Mtakatifu. Mtu huyu asiye na akili anayezungumziwa na Mungu anaonekana kama asiye na uhusiano wa kawaida na wengine, na hana upendo wa kuelekea nje au matendo ya juu juu, lakini anapokuwa akieleza mambo ya kiroho anaweza kufungua roho yake na kwa kujinyima awatolee wengine mwangaza na nuru ambayo amepata kutoka kwa uzoefu wake wa hakika mbele za Mungu. Hivi ndivyo anavyodhihirisha upendo wake kwa Mungu na kuridhisha mapenzi ya Mungu. Wengine wote wanapokuwa wanamkashifu na kumdhihaki, ana uwezo wa kutoelekezwa na watu wa nje, matukio, au vitu, na bado anaweza kutulia mbele za Mungu. Mtu wa aina hii inavyooneka yuko na utambuzi wake mwenyewe wa pekee. Bila kujali wengine, moyo wake kamwe haumwachi Mungu. Wengine wanapokuwa wakizungumza kwa furaha na kwa vichekesho, moyo wake bado unasalia mbele za Mungu, kutafakari neno la Mungu au kusali kwa kimya kwa Mungu aliye moyoni mwake, akitafuta makusudi ya Mungu. Kamwe hafanyi udumishaji wa uhusiano wao na wengine lengo lake la msingi. Mtu wa aina hii inavyoonekana hana falsafa ya maisha. Kwa nje, mtu huyu ni mchangamfu, anayependwa, asiye na hatia, lakini pia anamiliki hisia ya utulivu. Huu ni mfano wa mtu ambaye Mungu anamtumia. Mambo kama falsafa ya maisha au “mantiki ya kawaida” hayawezi kupenya kwa mtu wa aina hii; mtu wa aina hii ameutoa moyo wake wote kwa neno la Mungu, ambaye anaonekana kuwa na Mungu tu katika moyo wake. Hii ni aina ya mtu ambaye Mungu anamrejelea kama mtu “bila mantiki,” naye tu ni mtu ambaye anatumiwa na Mungu. Alama ya mtu ambaye anatumiwa na Mungu ni: Haijalishi ni lini au wapi, moyo wake daima uko mbele za Mungu, na haijalishi jinsi gani wengine ni wenye anasa, jinsi gani wanavyoshiriki katika tamaa, wanajiingiza katika anasa za kimwili—moyo wake kamwe haumwachi Mungu, naye hafuatani na umati. Aina hii ya mtu pekee ndiye anafaa kwa ajili ya matumizi ya Mungu, naye hasa ni yule ambaye amekamilika na Roho Mtakatifu. Ikiwa huwezi kufikia hatua hii, basi hustahili kupatwa na Mungu, ili kukamilishwa na Roho Mtakatifu.
kutoka katika “Ni Muhimu Sana Kuanzisha Uhusiano wa Kufaa na Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili
Watu ambao wana ukweli ni wale ambao, katika matukio wanayopitia ya kweli, wanaweza kusimama imara katika ushuhuda wao, kusimama imara katika nafasi zao, kusimama katika upande wa Mungu, bila kurudi nyuma, na ambao wanaweza kuwa na uhusiano wa kawaida na watu wanaompenda Mungu, wale ambao, mambo yakishawatokea, wanaweza kumtii Mungu kabisa, na wanaweza kumtii Mungu hadi kifo. Matendo na ufunuo wako katika maisha halisi ndio ushuhuda wa Mungu, ni kuishi kwa kudhihirisha maisha ya mwanadamu na ushuhuda wa Mungu, na huku ni kufurahia upendo wa Mungu; unapopitia hadi kiwango hiki, matukio unayopitia yatakuwa yamekuwa na athari. Watu ambao wameuona upendo wa Mungu kwa kweli ni wale ambao wanaishi kwa kudhihirisha kwa kweli, ambao kila matendo yao yanapongezwa na wengine, ambao sura yao haipendezi lakini wanaoishi kwa kudhihirisha maisha ya utiifu wa hali ya juu, ambao wanawasiliana kwa karibu maneno ya Mungu na huelekezwa na Mungu, na kupata nuru kutoka kwa Mungu, ambao huweza kuongea mapenzi ya Mungu katika maneno yao, na wanawasiliana kwa karibu uhalisi, ambao huelewa zaidi kuhusu kuhudumu katika Roho, wanaongea kwa wazi, ambao ni wenye heshima na kuaminika, ambao hawakabiliki na wana tabia nzuri, ambao wanaweza kutii mipango ya Mungu na kusimama imara katika ushuhuda wakati mambo yanapowatokea, ambao wana utulivu bila kujali wanachokumbana nacho. Watu wengine wangali wachanga, lakini wanatenda kama mtu mzima; wamekomaa, wana ukweli, wanapendwa na wengine—na hawa ndio watu ambao wana ushuhuda, na ndio udhihirisho wa Mungu.
kutoka katika “Wanaompenda Mungu Wataishi Milele Katika Mwangaza Wake” katika Neno Laonekana katika Mwili
Madondoo ya Mahubiri na Ushirika kwa ajili ya Marejeo:
Mtu anayemwamini Mungu kwa hakika atatekeleza angalau vipengele hivi vitano vya maisha ya kiroho kila siku: kusoma neno la Mungu, kumwomba Mungu, kuwa na ushirika kuhusu ukweli, kuimba nyimbo na sifa, na kutafuta ukweli katika kila kitu. Ikiwa pia una maisha ya mikutano, utakuwa na furaha kuu zaidi. Mtu akiwa na uwezo wa jumla wa kupokea, kumaanisha anaweza kuelewa dhamira za Mungu baada ya kusoma maneno ya Mungu yeye mwenyewe, ataweza kuelewa ukweli, na kujua jinsi ya kutenda kulingana na ukweli, basi inaweza kusemwa kwamba mtu wa aina hii atafaulu katika imani yake. Iwapo mtu hana maisha ya kiroho ya aina hii, au iwapo maisha yake ya kiroho ni yasiyofaa kupindukia na yanaonekana tu mara chache sana, basi mtu huyo ni muumini aliyechanganyikiwa. Waumini waliochanganyikiwa hawawezi kupata matokeo mazuri kutoka kutimiza jukumu lao. Kuamini katika Mungu bila kuishi maisha ya kiroho ni kuwa na imani kwa maneno pekee; kwa watu kama hao, hakuna Mungu mioyoni mwao, sembuse uchaji wowote wa Mungu. Wanawezaje kuwa na mfano wa binadamu wa kufaa?
…………
Kuna vitu 10 vya kuzingatiwa na kuingiwa inapofikia kwa jinsi mtu wa kufaa anastahili kuwa:
1. Fuata adabu, jua masharti, na uwaheshimu wazee na kuwajali wadogo.
2. Kuwa na hali ya maisha inayofaa; iliyo na manufaa kwako mwenyewe na kwa wengine.
3. Valia kwa namna ya heshima na nyoofu; mavazi ya ajabu au ya urembo yamepigwa marufuku.
4. Usiwahi, kwa sababu yoyote ile, kuomba pesa kutoka kwa ndugu, na usitumie vitu vya watu wengine kama ni jambo la kawaida tu.
5. Kukutana na watu wa jinsia tofauti lazima kuwe na mipaka; vitendo vinahitajika kuwa vya heshima na vinyoofu.
6. Usibishane na watu; jifunze kuwasikiliza wengine kwa uvumilivu.
7. Dumisha usafi mzuri, lakini kwa kuzingatia hali halisi.
8. Jihusishe katika ushirika na uhusiano wa kufaa na wengine, jifunze kuwaheshimu na kuwa mwenye kuwajali watu, na pendaneni.
9. Fanya kila uwezalo kuwasaidia wale walio na mahitaji; usiitishe au kukubali vitu kutoka kwa watu wengine.
10. Usiwaruhusu wengine wakuhudumie; usiwaruhusu wengine wafanye kazi unayofaa kuwa ukifanya mwenyewe.
Masharti kumi ya hapo juu yanafaa kuwa ya msingi yanayofuatwa na waumini wote katika maisha yao, yeyote anayevunja masharti haya ni wa tabia duni. Unaweza kusema kuwa haya ni masharti ya nyumba ya Mungu na wale wanaoyaasi mara kwa mara bila shaka watatupwa kando.
Wale wote wanaoutafuta ukweli pia wanahitaji kufuata mienendo kumi mizuri ya watakatifu wa kale. Watu wanaoweka katika vitendo mara kwa mara na kudumisha haya bila shaka watapata thawabu kubwa za binafsi. Ni yenye manufaa makubwa mno kwa wanadamu.

Kanuni kumi za kuambatana na adabu takatifu:

1. Fanya ibada za kiroho kila asubuhi kwa kusali na kusoma neno la Mungu kwa takriban nusu saa.

2. Tafuta madhumuni ya Mungu katika kila kitu kila siku ili uweze kuuweka ukweli katika matendo kwa usahihi zaidi.

3. Kuwa na ushirika na kila unayekutana naye, mkifunzana kutoka kwa uwezo wa kila mmoja ili nyote muweze kuendelea.

4. Kuwa na mtazamo wa matumaini kuhusu maisha, huku mara nyingi ikiimba nyimbo na sifa na utoe shukrani kwa ajili ya neema ya Mungu.

5. Usitegwe na dunia ya kilimwengu; jongea karibu na Mungu moyoni mwako kwa kawaida na usiingilie mambo ya wengine.

6. Weka hekima moyoni mwako na ukae mbali na uovu na sehemu zenye hatari.

7. Usibishane na watu, kuwa na ushirika kuhusu ukweli, na uelewane na wengine.

8. Kuwa radhi kufanya kila uwezalo kuwasaidia wengine, watulizie mashaka yao, na uwasaidie kutatua ugumu wao katika kuingia katika kumwamini Mungu.

9. Jifunze jinsi ya kutii wengine, usiwatawale watu na kuwalazimisha; waruhusu watu wapate faida kiasi katika kila kitu.

10. Mara nyingi mwabudu Mungu moyoni mwako, ukimwacha Awe na ukuu katika kila kitu na kumridhisha Yeye katika kila kitu.

Kanuni kumi za hapa juu za maisha na namna kumi za kuambatana na adabu takatifu yote ni vitu ambavyo watu wana uwezo wa kuvifanya. Watu wanaweza kuweka vitu hivi katika vitendo alimradi vinaeleweka na makosa ya mara kwa mara si magumu kusuluhisha. Bila shaka, watu fulani ambao ubinadamu wao ni mbaya zaidi wameondolewa katika hili.

kutoka katika Ushirika kutoka kwa Aliye Juu

Ubinadamu wa kufaa huashiria hasa kuwa na dhamiri, mantiki, unyoofu na heshima. Dhamiri na mantiki zinajumuisha kuonyesha ustahimilivu, kuwa na uvumilivu kwa wengine, kuwa mwaminifu, kutendea watu kwa hekima, na kuwa na upendo wa kweli kwa ndugu. Hizi ndizo sifa tano ambazo binadamu wa kufaa lazima wawe nazo.

Sifa ya kwanza ni kuwa na moyo wa ustahimilivu. Unamaanisha haijalishi dosari tunazoona ndani ya ndugu zetu, tunafaa kuwatendea vema, tukionyesha uvumilivu na uelewa. Hatupaswi kuwatenga au kuwashambulia kwa maneno. Tunapoona dosari au upotovu ukijifichua ndani ya watu wengine, tunafaa kukumbuka kuwa huu ni wakati wa kazi ya Mungu ya wokovu, kwa hivyo ni jambo la kawaida kwa wateule wa Mungu kufichua upotovu, na tunapaswa kuelewa. Mbali na hayo, tunahitaji kuangalia upotovu wetu sisi wenyewe, si lazima kuwa tunafichua upotovu wa kiwango cha chini kuliko wa watu wengine. Tunapaswa kuchukulia jinsi wengine wanavyofichua upotovu jinsi tunavyochukulia wetu kabisa. Kwa njia hiyo, tunaweza kuwastahimili wengine. Iwapo huwezi kustahimili watu wengine inamaanisha kuna shida na mantiki yako; inathibitisha kwamba huelewi ukweli na hujui kazi ya Mungu. Kutojua kazi ya Mungu kunamaanisha nini? Ni kutojua kwamba kazi ya Mungu bado haijakamilika na kwamba binadamu bado anaishi katika wakati wa kazi ya Mungu ya wokovu—bado hatujafanywa kuwa kamili. Kwa hivyo, kila mtu bila kuzuilika atafichua upotovu. Sasa kila mtu anaufuatilia ukweli kwa njia inayofaa, akipata kuelewa upotovu wake mwenyewe, na kupitia neno la Mungu. Kila mtu yuko kwenye kipindi cha kuingia katika ukweli na bado hajapata ukweli kikamilifu. Ni wakati tu watu wanapopata ukweli ndio tabia ya maisha yao itaanza kubadilika. Watu wanapoelewa jambo hili watakuwa na busara ya mtu wa kawaida, na basi watawatendea wengine na busara pia. Ikiwa watu hawana busara hawatawatendea wengine kwa busara.

Sifa ya pili ni kuonyesha uvumilivu kwa wengine. Kuwa mstahimilivu tu hakutoshi; lazima pia uwe mvumilivu. Wakati mwingine unaweza kuwa mstahimilivu na mwenye kuelewa tu, lakini haiwezekani kuepuka ndugu fulani kufanya jambo linaloweza kukusononesha au kukukosea. Katika hali kama hizo ni rahisi kwa tabia potovu ya binadamu kulipuka, kwa sababu sote tunapenda kupigana na kulinda fahari yetu, na sisi sote ni wenye ubinafsi na bure. Hivyo mtu akisema kitu kinachokusononesha au kufanya kitu kinachokukosea, unafaa kuwa mvumilivu. Uvumilivu pia unajumuishwa katika mawanda ya busara. Watu watakuza uvumilivu tu ikiwa wana busara. Lakini tunawezaje kuwa wavumilivu? Ukitaka kuwa mvumilivu kwa wengine, unahitaji kwanza kuwaelewa, “kumaanisha bila kujali anayesema kitu kinachokusononesha, unafaa kutambua hili: Maneno yake yamenisononesha. Alichosema kilionekana kufunua udhaifu wangu na kilionekana kunilenga mimi. Ikiwa maneno yake yananilenga mimi, anamaanisha nini anapoyasema? Je, anajaribu kunidhuru? Je, ananiona mimi kama adui yake? Je, ananichukia? Je, analipiza kisasi dhidi yangu? Mimi sijamkosea, kwa hivyo majibu ya maswali haya hayawezi kuwa ndiyo.” Kwa kuwa hiyo ndiyo hali, basi haijalishi kile alichosema ndugu huyu, yeye hakuwa na madhumuni ya kukusononesha au kukutendea kama adui yake. Hilo ni bila shaka. Aliposema maneno haya alikuwa anadhihirisha tu yale ambayo binadamu wa kawaida hufikiri, alikuwa anashiriki juu ya ukweli, kujadili maarifa, kufichua upotovu wa watu, au kukubali hali yake mwenyewe ya upotovu; bila shaka hakuwa anamlenga mtu yeyote yule kwa kujua. Kwanza unamwelewa, kisha hasira yako inaweza kutoweka, halafu unaweza kupata uvumilivu. Wengine watauliza: “Mtu akinishambulia kwa kujua na anilenge, na aseme mambo haya kwa makusudi ya kufanikisha kusudi fulani, basi nitawezaje kuwa mvumilivu?” Unapaswa kuwa mvumilivu jinsi hii: “Hata mtu akinishambulia kwa makusudi, bado nafaa kuwa mvumilivu. Hii ni kwa sababu yeye ni ndugu yangu na sio adui yangu, na bila shaka sio ibilisi, Shetani. Haiwezi kuepukika kwamba ndugu watafichua upotovu kiasi na kuwa na makusudi fulani katika mioyo yao. Hii ni kawaida. Napaswa kuelewa, na ninafaa kuhisi maono yake na kuwa mvumilivu.” Unapaswa kuwaza kwa njia hii, kisha usali kwa Mungu na kusema: “Mungu, mtu fulani ametoka kuumiza fahari yangu. Siwezi kukubali aibu hii; kila mara nataka kuwa mwenye hasira na kumshambulia. Huu kwa hakika ni ufichuzi wa upotovu. Nilikuwa nikidhani kuwa nilikuwa na upendo kwa wengine, lakini sasa kwa kuwa maneno ya mtu fulani yamenichoma moyoni siwezi kuvumilia. Nataka kumrudishia pia. Nataka kulipiza kisasi. Uko wapi upendo wangu? Je, hii yote si ni chuki tu? Bado niko na chuki moyoni mwangu! Mungu, jinsi Ulivyo na huruma kwetu na kutusamehe sisi dhambi zetu ndio jinsi tunavyofaa kuwa na huruma kwa wengine. Hatufai kuwa na kisasi dhidi ya wengine. Mungu, tafadhali nikinge, Usiache asili yangu ilipuke. Natamani kukutii Wewe na niishi kwenye upendo Wako. Tunampinga na kumkataa Kristo na Mungu sana katika kila kitu tukifanyacho, lakini Kristo bado Anakuwa mvumilivu nasi. Mungu anafanya hatua hii ya kazi Yake kwa uvumilivu mkubwa na upendo. Je, Kristo Alilazimika kuvumilia mateso, fedheha na kashfa kiasi gani? Ikiwa Kristo Alivumilia hayo, basi kiasi kidogo cha uvumilivu tunaofaa kuwa nao si kitu! Uvumilivu wetu umepungukiwa sana ukilinganishwa na ule wa Kristo….” Mara unapoomba kwa njia hii utajisikia ni kama wewe ni mpotovu mno, asiye wa maana kabisa, aliyepungukiwa katika kimo kabisa, na huo ndio wakati ambapo hasira yako itazimwa. Hivyo ndivyo unavyoweza kufikia uvumilivu.

Sifa ya tatu ni kuwatendea watu kwa uaminifu. Kuwa waaminifu kwa watu kuna maana kwamba bila kujali tunachofanya, iwe ni kuwasaidia wengine au kutoa huduma kwa ndugu zetu au kushiriki kuhusu ukweli, lazima tuzungumze kutoka moyoni. Zaidi ya hayo, usihubiri kile ambacho hujafanya. Wakati wowote ndugu wanahitaji msaada wetu tunapaswa kuwasaidia. Tunapaswa kutimiza wajibu wowote tunaohitaji kuutimiza. Kuwa mwaminifu, wala si muongo au wa kujidai. … Bila shaka, kuwa mtu mwaminifu kunahitaji hekima kiasi wakati unaposhughulika na watu fulani. Ukiona kwamba mtu fulani si wa kutegemewa kwa sababu upotovu wake ni wa kina kabisa, kama huwezi kumbaini na hujui anachoweza kufanya, basi unahitaji kuwa mwenye hekima na uepuke kumweleza kila kitu. Kuwa mtu mwaminifu kunahitaji maadili. Usizungumze kwa upofu kuhusu mambo usiyofaa kuwa ukizungumzia. Zaidi ya hayo, kuwa mtu mwaminifu kunahitaji kuongea na mantiki na usahihi. Watu wengine wanasisitiza kutenda uaminifu na kumfungulia mtu moyo licha ya shughuli nyingi alizo nazo. Huko ni kuwa mtu mwaminifu vipi? Je, huu sio upumbavu? Kuwa mtu wa kweli ni kutokuwa mjinga. Kunahusu kuwa mwerevu, wa kawaida na wazi, na usiyedanganya. Lazima uwe wa heshima na mwenye busara. Uaminifu hujengwa juu ya msingi wa busara. Hii ndiyo maana ya kuwa mwaminifu wakati unaposhughulika na watu, na kuwa mtu mwaminifu. Bila shaka, jambo muhimu sana kuhusu kuwa mtu mwaminifu ni kuwa mwaminifu kwa Mungu. Je, si lingekuwa tatizo kubwa kama wewe ni mtu mwaminifu mbele ya watu wengine tu, lakini wewe si mwaminifu mbele ya Mungu na umdanganye Yeye? Mkitafuta kuwa watu waaminifu mbele ya Mungu, basi kwa kawaida mtakuwa waaminifu mbele ya wengine. Iwapo huwezi kufanya hivyo mbele ya Mungu, basi kwa kweli huwezi kufanya hivyo mbele ya watu wengine. Haijalishi ni kipengele kipi cha ukweli au ni kitu kipi chema ambacho unaingia, lazima kwanza ukifanye mbele ya Mungu. Punde ambapo umepata matokeo mbele ya Mungu, kwa kiasili utaweza kuishi kwa kukidhihirisha mbele ya watu wengine. Usijichoshe kufanya hiki au kile mbele ya wengine, lakini kisha bila kujali ufanye chochote unachotaka mbele ya Mungu. Hili halitakuwa sawa. Jambo muhimu zaidi ni kulifanya mbele ya Mungu, ambaye huwajaribu binadamu na kuchunguza mioyo yao. Una uhalisi kwa hakika ikiwa unaweza kupita jaribio hili mbele ya Mungu. Huna uhalisi ikiwa huwezi kupita jaribio hili mbele ya Mungu—hii ndiyo kanuni ya kutenda ukweli.

Sifa ya nne ni kutendea watu kwa hekima. Baadhi ya watu husema: “Je, kuelewana na ndugu kunahitaji hekima?” Ndiyo, kunahitaji, kwa sababu kutumia hekima hutoa hata manufaa makubwa zaidi kwa ndugu zako. Baadhi watauliza: “Je, si kutumia hekima kwa ndugu ni kuwa mwenye hila?” Hekima si hila. Badala yake, ni kinyume kabisa na hila. Kutumia hekima kuna maana ya kuwa makini kwa jinsi unavyozungumza na ndugu wakati kimo chao ni kidogo, ikija kuwa wao wasiweze kukubali kile unachosema. Pia, kwa watu wenye kimo kidogo, hasa wale ambao hawana ukweli, wanaofichua upotovu fulani na kuwa na tabia fulani za upotovu, kama wewe ni wa kawaida na wazi sana na uwaambie kila kitu, inaweza kuwa rahisi kwao kuwa na kitu dhidi yako au kukutumia vibaya. Hivyo, ni lazima kwa kadiri uchukue tahadhari kiasi na uwe na mbinu fulani unapozungumza. Hata hivyo, kuwa na tahadhari dhidi ya watu hakumaanishi kutowasaidia au kutokuwa na upendo kwao—kunamaanisha tu kutowaambia mara moja baadhi ya mambo muhimu kuhusu nyumba ya Mungu, na kushiriki tu ukweli kwao. Kama wanahitaji msaada wa kiroho katika maisha, kama wanahitaji ruzuku ya na ukweli, lazima tufanye kila kitu tuwezalo ili kuwakidhi katika suala hili. Lakini iwapo wanauliza kuhusu hili na lile kuhusu nyumba ya Mungu, au hili na lile kuhusu viongozi na wafanyakazi wake, basi hakuna haja ya kuwaambia. Ukiwaambia, kuna uwezekano watafichua habari hii na hii itaathiri kazi ya nyumba ya Mungu. Kwa maneno mengine, ikiwa ni kitu ambacho hawafai kujua au kitu ambacho hawana haja ya kujua, basi usiwaruhusu kujua kukihusu. Kama ni kitu ambacho wanapaswa kujua, basi fanya kila uwezalo kuwafanya wajue kukihusu, kwa uthabiti na bila shaka. Kwa hivyo ni mambo yapi wanayopaswa kujua? Ufuatiliaji wa ukweli ndio watu wanapaswa kujua: Ni ukweli upi wanaopaswa kuwa nao, ni vipengele vipi vya ukweli wanafaa kuelewa, ni majukumu yapi wanapaswa kutimiza, ni majukumu yapi yanawafaa wao kutimiza, ni jinsi gani wanafaa kutimiza majukumu hayo, jinsi ya kuishi kwa kudhihirisha ubinadamu wa kawaida, jinsi ya kuishi maisha ya kanisa—haya yote ni mambo ambayo watu wanapaswa kujua. Kwa upande mwingine, masharti na kanuni za nyumba ya Mungu, kazi ya kanisa na hali za ndugu zako haviwezi kuwekwa wazi kwa kawaida kwa watu wa nje wala wasioamini katika familia yako. Hii ni kanuni ambayo ni lazima ifuatwe tunapotumia hekima. Kwa mfano, hupaswi kamwe kuzungumza kuhusu majina ya viongozi wako au wanapoishi. Ukizungumza kuhusu mambo haya, huwezi kujua wakati habari hii inaweza kufikia masikio ya watu wa nje, na mambo yanaweza kuwa ya taabu sana kama yatapishwa kwa baadhi ya wapelelezi wabaya au maajenti wa siri. Hili linahitaji hekima, na hii ndiyo maana nasema kuwa na hekima ni muhimu. Zaidi ya hayo, unapokuwa wa kawaida na wazi, kuna mambo fulani ya binafsi ambayo huwezi tu kumwambia mtu yeyote. Unafaa kupima kimo cha ndugu zako ili uone kama, baada ya kuwaeleza, wanaweza kuwa waovu na wafanye utani kuhusu kile unachosema, wakikusababishia matatizo baada ya hayo mambo kusambazwa, na hili likaharibu heshima yako. Hii ndiyo maana kuwa wa kawaida na wazi pia kunahitaji hekima. Hicho ndicho kiwango cha nne ambacho binadamu sawa lazima wamiliki—kutendea watu kwa hekima.

Sifa ya tano ni kuwa na upendo wa kweli kwa ndugu ambao hakika wanaamini katika Mungu. Hii inahusisha utunzaji kiasi, msaada halisi, na roho ya huduma. Tunapaswa hasa kuwa na ushirika zaidi na hao ndugu wanaofuatilia ukweli, na kuwapa ruzuku zaidi. Haijalishi kama wao ni waumini wapya au wamekuwa waumini kwa miaka kadhaa. Kuna kanuni moja hasa ya maisha ya kanisa: Watunze hasa wale ambao wanafuatilia ukweli. Shiriki na wao zaidi, wape ruzuku zaidi, na uwanyunyizie zaidi ili waweze kusaidiwa kuinuka haraka iwezekanavyo, kuwasaidia wakue katika maisha yao haraka wawezavyo. Kwa wale ambao hawafuatilii ukweli, kama itakuwa wazi kuwa hawaupendi ukweli baada ya kipindi cha unyunyizaji, basi hakuna haja ya kuweka juhudi kubwa kwao. Si lazima kwa sababu tayari umeshafanya kila kitu kiwezekanacho kwa mwanadamu. Inatosha kuwa umetimiza wajibu wako. … Unahitaji kuona ni nani unapaswa kulenga kazi yako kwake. Je, Mungu atawakamilisha wale wasiofuatilia ukweli? Kama Roho Mtakatifu hatafanya hivyo, basi kwa nini watu waendelee kufanya hilo kwa upofu? Huelewi kazi ya Roho Mtakatifu ilhali daima umejiamini sana—je, huo si upumbavu na ujinga wa binadamu? Hivyo, toa usaidizi zaidi kwa ndugu ambao kwa kweli wanaufuatilia ukweli, kwa sababu wao ni vyombo vya wokovu wa Mungu na wateule Wake walioamuliwa kabla. Tukishiriki kuhusu ukweli mara nyingi na watu hawa kwa moyo mmoja na mawazo na kusaidiana na kupeana ruzuku, mwishowe sisi wote tutapata wokovu. Wewe unayasaliti mapenzi ya Mungu usipojiunga na watu hawa. … Wale walio ndani ya kanisa walio na ubinadamu unaofaa wanapaswa kujiweka miongoni mwa wale ambao wanafuatilia ukweli, waingiliane kwa amani na watu hawa, na kwa njia ya ufuatiliaji wa ukweli hatua kwa hatua kujitumia kwa ajili ya Mungu kwa moyo na mawazo sawa. Kwa njia hiyo, wale wanaofuatilia ukweli wataokolewa na wewe pia utaokolewa, kwa sababu Roho Mtakatifu anafanya kazi kati ya wale wanaofuatilia ukweli. …

Ushirika ambao tumetoka kuwa nao ni juu ya vipengele vitano ambavyo binadamu wa kawaida lazima wamiliki. Kama una sifa hizi zote tano, utaweza kuingiliana kwa amani na ndugu zako, utapata nafasi yako katika kanisa, na utatimiza wajibu wako kwa njia bora zaidi kadri ya uwezo wako.


kutoka katika “Jinsi ya Kujenga Maisha ya Kanisa na Maana ya Kujenga Maisha ya Kanisa” katika Mahubiri na Ushirika Kuhusu Kuingia Katika Maisha I

Jumapili, 28 Aprili 2019

Waumini katika Mungu Wanapasa Kujiandaa kwa Ajili ya Hatima Yao kwa Matendo Mema ya Kutosha

7. Waumini katika Mungu Wanapasa Kujiandaa kwa Ajili ya Hatima Yao kwa Matendo Mema ya Kutosha

Maneno Husika ya Mungu:

Huruma Zangu zinaonyeshwa kwa wale wanaonipenda Mimi na kujinyima wenyewe. Na adhabu inayoletwa kwa waovu ni thibitisho hasa la tabia Yangu ya haki na, zaidi sana, ushuhuda wa hasira Yangu. Msiba utakapokuja, njaa na baa litawakumba wale wote wanaopinga Mimi na watalia kwa uchungu. Wale wote ambao wametenda aina zote za uovu, lakini ambao wamenifuata kwa miaka mingi, hawataepuka kulipia dhambi zao; wao pia, wakijipata katika maafa, ambayo yameonekana kwa nadra katika mamilioni ya miaka, wataishi katika hali ya kila siku ya taharuki na woga. Na wale wafuasi Wangu ambao wamekuwa waaminifu Kwangu pekee watafurahi na kushangilia ukuu Wangu. Watakuwa na ridhaa isiyo na kifani na kuishi kwa raha ambayo Sijawahi kuwapa wanadamu. Kwa sababu Ninathamini matendo mema ya wanadamu na kuchukia matendo yao maovu. Tangu Nilipoanza kuwaongoza wanadamu, Nimekuwa Nikitamani kwa hamu kupata kikundi cha wanadamu ambao wanafikiria kama Mimi. Sijawahi kuwasahau wale ambao hawana fikira sawa na Zangu; Nimewachukia sana moyoni Mwangu, Nikisubiri tu nafasi kutoa adhabu kwa hao na kufurahia kuona hilo. Siku Yangu hatimaye imefika na siwezi kusubiri zaidi!

Kazi Yangu ya mwisho si kwa ajili ya kumwadhibu mwanadamu tu bali pia kwa ajili ya kupanga hatima ya mwanadamu. Aidha, ni kwa ajili ya kupokea shukrani kutoka kwa kila mtu kwa yale yote ambayo Nimefanya. Ninataka kila mtu aone kwamba yale yote ambayo Nimefanya ni sahihi na kwamba yote ambayo Nimefanya ni dhihirisho la tabia Yangu; si kwa uwezo wa mwanadamu, sembuse ulimwengu, ambao uliwaleta wanadamu. Kinyume na hili, mimi Ndiye Ninalisha kila kiumbe miongoni mwa vitu vyote. Bila uwepo Wangu, wanadamu wataangamia tu na kusumbuka kutokana na mashambulizi ya misiba. Hamna mwanadamu atakayeona uzuri wa jua na mwezi au dunia ya kijani kibichi; wanadamu watakumbana tu na usiku wenye baridi na bonde kali la uvuli wa mauti. Mimi tu Ndiye wokovu wa wanadamu. Mimi tu ndiye tumaini la wanadamu na zaidi ya hayo; Mimi tu Ndiye mwamba wa uwepo wa wanadamu wote. Bila Mimi, wanadamu watasimama kabisa mara moja. Bila mimi, wanadamu watakumbana na msiba mkuu na kukanyagwa na mapepo wa aina yote, hata kama hamna anayenisikiliza. Nimefanya kazi ambayo haiwezi kufanywa na yeyote yule ila mimi. tumaini Langu la pekee ni kwamba mwanadamu anaweza kunilipa kwa kutenda matendo kiasi mema. Ingawa wanaoweza kunilipa ni wachache, bado Nitahitimisha safari Yangu duniani na Nianze hatua ifuatayo ya kazi Yangu inayotokea, kwa sababu kukimbia kimbia Kwangu miongoni mwa wanadamu kwa miaka hii mingi imekuwa na matokeo mazuri, na Nimefurahishwa sana. Sijali kuhusu idadi ya watu ila kuhusu matendo yao mazuri. Kwa hali yoyote ile, Ninatumaini kwamba mtatayarisha matendo mema ya kutosha kwa ajili ya hatima yenu wenyewe. Huo ndio wakati Nitakaporidhika; la sivyo, hakuna yeyote miongoni mwenu atakayepuka maafa yatakayowafikia. Maafa haya hutoka Kwangu na bila shaka Mimi ndiye Niliyeyapanga. Ikiwa hamwezi kuonekana kuwa wema mbele Yangu, basi hamtaweza kuyaepuka maafa. Wakati wa majonzi, vitendo vyenu havikuchukuliwa kama vinavyofaa kabisa, kwa sababu imani na upendo wenu vilikuwa tupu, na mlijionyesha tu kuwa wenye woga au sugu. Kuhusu hili, Nitafanya hukumu ya mazuri au mabaya tu. Shaka Yangu inaendelea kuwa jinsi kila mmoja wenu hutenda na kujionyesha, kwa msingi ambao Nitatumia kufanya uamuzi kuhusu hatima yenu. Hata hivyo, ni sharti Niseme wazi kwamba: Sitawahurumia tena wale ambao hawakuwa waaminifu Kwangu kabisa wakati wa majonzi, kwa sababu huruma Yangu ina mipaka. Zaidi ya hayo, Simpendi yeyote yule ambaye amewahi kunisaliti Mimi, wala Sipendi kujihusisha na wale ambao hawawajali wenzao. Bila kujali huyo mtu ni nani, hii ndiyo tabia Yangu. Ni lazima Niwaambie hili: Yeyote atakayeuhuzunisha moyo Wangu hatapokea huruma kutoka Kwangu mara ya pili, na yeyote ambaye amekuwa mwaminifu Kwangu atadumu moyoni Mwangu milele.

kutoka katika “Unapaswa Kutayarisha Matendo Mema ya Kutosha kwa ajili ya Hatima Yako” katika Neno Laonekana katika Mwili

Natarajia tu kuwa katika hatua ya mwisho ya kazi Yangu, mnaweza kutekeleza kwa kujitokeza, kujitoa kikamilifu, na wala sio shingo upande tena. Bila shaka, Natarajia pia kuwa nyote muwe na hatima nzuri. Hata hivyo, bado Nina mahitaji Yangu ambayo ni kwenu nyinyi mfanye uamuzi bora kabisa katika kujitoa Kwangu pekee na moyo wa ibada ya mwisho. Kama mtu hana moyo huo wa ibada pekee, mtu huyo hakika atakwenda kuwa thamani ya Shetani, na Mimi Sitaendelea kumtumia. Nitamtuma nyumbani akatunzwe na wazazi wake.

kutoka katika “Juu ya Hatima” katika Neno Laonekana katika Mwili

Mnapaswa kufanya wajibu wenu wenyewe kwa kadri ya uwezo wenu kwa mioyo iliyo wazi na wima, na muwe tayari kufanya chochote kitakachohitajika. Kama mlivyosema, wakati siku itakuja, Mungu Hatamtendea mtu yeyote vibaya ambaye aliteseka au kulipa gharama kwa ajili Yake. Aina hii ya imani ni yenye thamani kuishikilia, na hampaswi kuisahau kamwe. Ni tu kwa njia hii Ninaweza kutuliza akili Yangu kuwahusu. Vinginevyo, Sitakuwa na uwezo wa kutuliza akili Yangu kuwahusu, na milele mtakuwa malengo ya chuki Yangu. Kama nyote mnaweza kufuata dhamiri zenu na kutoa yote kwa ajili Yangu, msiwache jitihada zozote kwa ajili ya kazi Yangu, na kutenga maisha ya jitihada za kazi ya injili Yangu, basi si moyo Wangu mara kwa mara utaruka kwa furaha kwa ajili yenu? Si Mimi Nitakuwa na uwezo wa kutuliza akili Yangu kuwahusu?

kutoka katika “Juu ya Hatima” katika Neno Laonekana katika Mwili

Kama kutafuta njia ya ukweli kunakufurahisha vyema, basi wewe ni yule anayeishi kila mara katika mwangaza. Kama wewe unafurahia kuwa mtoa huduma katika nyumba ya Mungu, ukifanya kazi kwa bidii na kwa makini bila kuonekana, siku zote ukitoa na katu hupokei, basi Nasema kwamba wewe ni mtakatifu mwaminifu, kwani hutafuti tuzo na unakuwa tu binadamu mwaminifu. Kama uko radhi kuwa wazi, kama uko radhi kutoa kila kitu ulichonacho, kama una uwezo wa kujitolea maisha yako kwa ajili ya Mungu na kuwa shahidi, kama wewe ni mwaminifu hadi kwa kiwango ambapo unajua tu kumridhisha Mungu na si kujifikiria au kuchukua chochote kwa ajili yako, basi Nasema kwamba watu kama hao ndio wanaostawishwa na mwangaza na wataishi milele katika ufalme.

kutoka katika “Maonyo Matatu” katika Neno Laonekana katika Mwili

Madondoo ya Mahubiri na Ushirika kwa ajili ya Marejeo:

Matendo mema ni ushahidi kwamba tumepata wokovu, na ni dhihirisho la kuingia kwetu katika ukweli na uhalisi wa neno la Mungu. Kama tumetayarisha matendo mengi mema, hilo linamaanisha kwamba tumekuwa watu wapya mbele za Mungu na kwamba tuna ushahidi wa kweli katika kipengele cha kuwa binadamu halisi. Matendo yetu mema ndiyo yanayoonyesha hasa kwamba tumetubu kwa kweli; ikiwa tumetayarisha matendo mengi mema, hili linamaanisha kuwa tuna mfano wa kweli wa mtu. Ikiwa umemwamini Mungu kwa miaka mingi lakini umefanya matendo mema machache, basi una mfano wa binadamu? Je, una dhamiri na mantiki? Je, wewe ni mtu anayelipiza upendo wa Mungu? Iko wapi imani yako ya kweli? Uko wapi moyo wako wa upendo na utii kwa Mungu? Ni uhalisi upi umeingia ndani? Huna chochote kati ya haya. Kwa hiyo, mtu asiyefanya matendo mema ni mtu asiyepokea chochote kutoka kwa imani yake kwa Mungu. Yeye ni mtu ambaye hajapata kabisa wokovu kutoka kwa Mungu, mtu ambaye upotovu wake ni wa kina sana na ambaye hajabadilika hata kidogo. Matendo mema kweli yanafafanua hili.

kutoka katika “Maana Muhimu ya Kuandaa Matendo Mema” katika Mahubiri na Ushirika Kuhusu Kuingia Katika Maisha II

Matendo mema ya kutosha ni yapi? Tunaweza kusema kwamba wajibu wowote ambao mtu anaweza au anapaswa kuutimiza katika uzoefu wake wa kazi ya Mungu, na kitu chochote ambacho Mungu anahitaji kutoka kwa mwanadamu—kama mwanadamu anaweza kufanya vitu hivi na anaweza kumridhisha Mungu, basi haya yote ni matendo mema Kama unaweza kuyatosheleza mahitaji ya Mungu, basi ni tendo jema. Kama una moyo wa ibada kwa Mungu wakati unapotimiza wajibu wako, basi ni tendo jema. Kama mambo unayoyafanya ni ya manufaa kwa watu waliochaguliwa na Mungu na kila mtu anafikiria kwamba unayoyafanya ni mazuri, basi ni tendo jema. Mambo yote ambayo dhamiri na mantiki ya mwanadamu huamini kuwa ni kulingana na madhumuni ya Mungu ni matendo mema. Mambo ambayo yanaweza kumridhisha Mungu na yana manufaa kwa watu wateule wa Mungu pia ni matendo mema. Kama mtu anaweza kufanya kila kitu ili kuyatayarisha haya matendo mema ambayo tumetoka kuzungumzia, hatimaye ataweza kuyatimiza, na hilo litamaanisha kuwa amekamilisha matendo mema ya kutosha. … Kila mtu sasa hutaka kutekeleza kazi yake na kufuatilia wokovu, lakini haitoshi tu kuwa na azimio na shauku. Mtu lazima aonyeshe tabia za utendaji na kuchukua hatua ya utendaji. Ni wajibu gani umetekeleza kwa ajili ya kuingia katika maisha ya watu wa Mungu wateule? Umefanya nini na ni thamani gani umelipa ili kuyaridhia matakwa ya Mungu? Umefanya nini ili kumridhisha Mungu na kulipa upendo Wake? Haya yote ni mambo ambayo inakubidi kuyatafakaria. Kama umefanya mambo mengi na kulipa thamani kubwa kwa ajili ya kuyaridhia matakwa ya Mungu na kwa ajili ya kuingia katika maisha na ukuaji wa watu wa Mungu wateule, basi inaweza kusemwa kuwa umeandaa matendo mema ya kutosha.

kutoka katika “Maana Muhimu ya Kuandaa Matendo Mema” katika Mahubiri na Ushirika Kuhusu Kuingia Katika Maisha II

Kwa kiwango cha chini, kutimiza kazi kiasi haitoshi peke yake kufanyiza kiasi cha kuridhisha cha matendo mema. Hivyo ni kusema, kutekeleza tu kiasi kidogo cha wajibu wako hakufikiriwi kuwa matendo mema ya kuridhisha hata kidogo. Matendo mema ya kuridhisha bila shaka sio rahisi kama watu wafikiriavyo. Kuandaa kiasi cha kuridhisha cha matendo mema huhitaji kujitumia kabisa kwa ajili ya Mungu. Aidha, kunahitaji kulipa kila thamani, na kuwa mwaminifu kwa agizo la Mungu tangu mwanzo hadi mwisho kwa imani nzuri; hii ndiyo njia ya pekee ya kuyaridhia matarajio ya Mungu.

Katika kutimiza wajibu wao kuna watu ambao kweli wamelipa thamani, wakafanya mambo ambayo yamesifiwa na Mungu, ambao wametekeleza wajibu wao kwa njia ambazo ni nzuri kabisa, za ajabu, za kupendeza na za kufanikiwa sana kiasi kwamba wanaweza kufikiriwa kuwa wametekeleza matendo mema. Baadhi ya ndugu na dada wamekwenda jela kwa sababu ya kutekeleza wajibu wao, ambao wamepitia maumivu mengi makali bila kumtii Shetani, na wamekuwa mashahidi. Kisha kuna watu ambao huthubutu kujiingiza hatarini bila kujali usalama wa kibinafsi au manufaa, ambao wamejitolea kufanya kazi za hatari kwa roho ya kufanya lililo la haki kwa ujasiri. Na kuna wale ndugu na dada ambao wanaweza kujitolea kwa kazi ya injili, na wanaweza kuvumilia fedheha katika kuhubiri injili ili kuwaokoa watu. Pia kuna wale wenye bidii katika kazi ya injili, wakivumilia shida bila malalamiko, wakiweka kando mambo ya kibinafsi na ya familia huku mawazo yao yakijawa na jinsi wanavyoweza kueneza injili ili kuwaleta watu zaidi mbele ya Mungu na kuyaridhisha mapenzi ya Mungu. Wote ambao wamejitolea kujitumia kabisa ili kumridhisha Mungu ni wale watu ambao tayari wamefanya matendo mema. Lakini bado wana umbali fulani kutoka kwa “matendo mema ya kuridhisha” ambayo Mungu hutaka. Watu wengi wameandaa tu matendo mema kiasi na hawajayaridhia kabisa matakwa ya Mungu. Hilo linatuhitaji kufanya tunaloweza ili kutimiza wajibu wetu na tuwe na bidii katika kuingia ndani kabisa ya ukweli ili kutekeleza matendo mema ya kuridhisha. Hili linatuhitaji tutafute kufanikisha matokeo bora sana ili kuuridhisha moyo wa Mungu, bila kujali ni wajibu gani tunaoutimiza. Hasa katika kueneza injili, bila kujali jinsi fedheha tunayopitia ilivyo kubwa au ni mateso kiasi gani tunayoyavumilia, mradi tunaweza kuwaleta watu zaidi kupata wokovu, ni lazima tuuchukue kama wajibu bila kujali gharama za kibinafsi. Huku tu ndio kutekeleza tendo bora sana. Kama watu wanaweza kutekeleza matendo zaidi yaliyo mema kama hili, hayo yanaweza kufikiriwa kuwa matendo mema ya kuridhisha. Hilo ndilo humletea Mungu furaha na shangwe mno, na watu kama hao kwa hakika watapokea sifa za Mungu. Mbali na hili, katika kutimiza wajibu wetu ni lazima pia tuwe makini na waangalifu sana, daima tukitafuta kujiboresha, na kutojiruhusu kuzembea hata kidogo. Ili kujitumia kwa ajili ya Mungu, ni lazima tuwe na kujitolea kwa uaminifu kabla tuweze kuyaridhisha mapenzi ya Mungu kabisa.

kutoka katika Ushirika kutoka kwa Aliye Juu

Chanzo: Tushughulikie Vipi Umeme wa Mashariki kwa Njia Inayolingana na Mapenzi ya Bwana?

Jumatano, 13 Februari 2019

Kanuni Kuu za Jinsi Wafanyakazi Hufanya Kazi

Sura ya 37. Kanuni Kuu za Jinsi Wafanyakazi Hufanya Kazi

Katika kazi yao, wafanyakazi wanapaswa kuzingatia mambo mawili: Moja ni kufanya kazi kabisa kulingana na kanuni zilizowekwa masharti na mipangilio ya kazi. Wafanyakazi hawapaswi kukiuka kanuni hizi, wasifanye kazi kulingana na mawazo yao wenyewe, na siyo kulingana na mapenzi yao. Wanapaswa kuonyesha uhusiano kwa kazi ya familia ya Mungu, na kuweka maslahi ya familia ya Mungu kwanza katika kila kitu wakifanyacho. Jambo jingine pia ni muhimu, na ni kwamba, katika kila kitu wakifanyacho, kuzingatia kufuata mwongozo wa Roho Mtakatifu, na kufanya kila kitu kwa ukali kulingana na neno la Mungu. Usipotii mwongozo wa Roho Mtakatifu au ikiwa kwa ukaidi unafuata mawazo yako mwenyewe na kufanya mambo kulingana na fikira zako mwenyewe, hili linafanya upinzani mkali sana kwa Mungu. Mama kwa mara kutotii kupata nuru na mwongozo wa Roho Mtakatifu huelekeza kwa mwisho kabisa. Hakuna jinsi ya kuendelea na kazi kama mtu amepoteza kazi ya Roho Mtakatifu, na ingawa mtu hufanya kazi, hakuna kitu kinachotimizwa. Ni kanuni hizi kuu mbili za kuzingatia wakati ukiwa kazini: Moja ni kufanya kazi kabisa kulingana na mipangilio kutoka hapo juu, na kufanya kazi na kanuni zilizowekwa na hayo ya hapo juu. Jambo jingine ni kufuata mwongozo kutoka kwa Roho Mtakatifu karibu. Mara tu mambo haya mawili yanapofahamika, ni vigumu kwa kazi kukosa kufikia matarajio yake. Kwa nyinyi ambao uzoefu wenu katika eneo hili bado ni kidogo, ridhaa yenu wenyewe hughushi kazi yenu zaidi. Wakati mwingine, hamuwezi kuelewa kupata nuru au mwongozo kutoka kwa Roho Mtakatifu karibu; kwa wengine, mnaonekana kuielewa, lakini huenda mnaipuuza. Wewe daima hufikiria au kufikia hitimisho kwa njia ya kibinadamu, kufanya kama unavyofikiria kuwa sahihi, bila kujali kabisa juu ya nia ya Roho Mtakatifu. Wewe huendelea na kazi yako tu kulingana na mawazo yako mwenyewe, ukiweka kando upataji wa nuru kutoka kwa Roho Mtakatifu. Hali kama hizo hutokea mara kwa mara. Mwongozo wa ndani kutoka kwa Roho Mtakatifu si wa kupita uwezo wa binadamu kamwe. Kwa kweli ni wa kawaida sana: Mfiko wa ndani wa roho yako unajua hii ndiyo njia sahihi ya kufanya hivyo, na kwamba hii ndiyo njia bora zaidi. Wazo kama hilo ni wazi sana; si matokeo ya kutafakari, na wakati mwingine huwezi kuelewa kikamilifu ni kwa nini kuifanya kwa njia hii. Hii mara nyingi si kitu kingine bali kupata nuru kutoka kwa Roho Mtakatifu. Hali kama hiyo ndiyo hutokea kwa kawaida kwa watu wengi sana. Roho Mtakatifu hukuongoza utende kwa njia sahihi zaidi. Siyo matokeo ya fikira zako, badala yake una hisia moyoni mwako na unang'amua kwamba hii ndiyo njia bora zaidi ya kufanya hivyo. Pengine hili ni kutoka kwa Roho Mtakatifu. Mapenzi ya mtu mara nyingi ni matokeo ya mfanyiko tendani wa mawazo yake na yamepakwa rangi na mawazo yake: Mapato yangu ni nini, jinsi nitakavyofaidika—haya ni sehemu ya chochote ambacho watu huamua kukifanya wenyewe. Mwongozo kutoka kwa Roho Mtakatifu hauna ughushi kama huo hata kidogo. Ni muhimu kuzingatia kwa makini mwongozo au kupata nuru kutoka kwa Roho Mtakatifu; hasa katika masuala muhimu unapaswa kuwa makini ili ulielewe. Watu ambao hufikiria mengi sana, ambao hupenda kufuata mawazo yao huenda wakaukosa. Wafanyakazi wazuri, wafanyakazi waangavu, huzingatia kazi ya Roho Mtakatifu. Watu wanaomtii Roho Mtakatifu humwogopa Mungu na kutafuta ukweli bila kuchoka. Ili kumridhisha Mungu na kumshuhudia Yeye, mtu anapaswa kuchunguza kazi yake mwenyewe kwa dalili za ughushi na madhumuni, na kujaribu kuona ni kiasi gani kilichomotishwa na matakwa ya kibinafsi, ni kiasi gani kilichotokana na kupatiwa nuru na Roho Mtakatifu, na ni kiasi gani kilicho cha kuambatana na neno la Mungu. Ni lazima daima na katika hali zote uyakague maneno na matendo yako. Kutenda kwa njia hii daima kutakuweka kwenye njia sahihi ya kumtumikia Mungu. Ni muhimu kuwa na ukweli mwingi chini ya amri yako ili kutimiza huduma kwa Mungu ambayo ni ya kupendeza nafsi Yake. Watu wana uwezo wa kutofautisha baada tu ya kuelewa neno la Mungu, na wanaweza kutambua kinachotoka kwa mapenzi yao wenyewe na vitu vinavyoonyesha motisha yao. Wanaweza kutambua uchafu wa wanadamu, na maana ya kutenda kulingana na ukweli. Ni hapo tu utakapojua jinsi ya kutii zaidi kwa usafi. Bila ukweli haiwezekani kwa watu kutofautisha. Mtu mpumbavu anaweza kumwamini Mungu maisha yake yote bila kujua maana ya kufichua upotovu, wala hajui kumpinga Mungu ni nini, kwa sababu yeye hana ukweli, wazo hili halipo katika akili yake. Hili ni kama kukarabati kifaa cha umeme. Je, mtu anawezaje kukitengeneza ikiwa hajui ni mzunguko umeme upi una kosa? Ndani yenu pia kuna mizunguko mingi. Wakati mwingine hitilafu iko katika malengo yenu, au ambako mapenzi yenu wenyewe yanahusika. Wakati mwingine hitilafu ni upotovu wa ufahamu wenu au ujuzi. Ama inaweza kuwa kutokana na kufuata mapenzi yenu wenyewe au kwa kuamini na kupotoshwa na wengine. Wakati mwingine nyinyi hufuata mwili mnapojaribu kulinda sifa zenu au hadhi. Hitilafu kama hizi hutokea mara kwa mara, hivyo kupeleka kazi mrama na kuleta hasara kwa kazi ya familia ya Mungu na maisha ya ndugu. Thamani ya kazi ya aina hii ni nini? Ni katizo, usumbufu, na uharibifu tu. Ili kutimiza kazi ambayo Mungu huwapa ni muhimu kuelewa kanuni hizi mbili. Ni lazima mshike kabisa mipango ya kazi kama ilivyoelezwa hapo juu, na lazima mzingatie kuutii mwongozo kutoka kwa Roho Mtakatifu. Ni wakati tu kanuni hizi mbili zinapofahamika ndipo kazi inapoweza kuwa ya kufaa na mapenzi ya Mungu yaridhishwe.
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu

Jumatatu, 17 Desemba 2018

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Kazi ya Mungu na Utendaji wa Mwanadamu" (Sehemu ya Pili)

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Kazi ya Mungu na Utendaji wa Mwanadamu" (Sehemu ya Pili)

Mwenyezi Mungu anasema, "Katika kila aina ya kazi ya Mungu kuna maono yanayofahamika na mwanadamu; maono yanayofuatwa na matarajio mwafaka ya Mungu kwa mwanadamu. Bila haya maono kama msingi, mwanadamu hawezi kuwa na uwezo wa utendaji na pia hangeweza kumfuata Mungu bila kuyumbayumba. Ikiwa mwanadamu hamjui Mungu au hayaelewi mapenzi ya Mungu, basi yote ayafanyayo ni bure na yasiyoweza kukubalika na Mungu. Hata mwanadamu awe na vipawa vingi kiasi gani, bado hawezi kujitenga na kazi ya Mungu na uongozi wa Mungu. Bila kujali uzuri na wingi wa matendo ya mwanadamu, bado hayawezi kuchukua nafasi ya kazi ya Mungu. Kwa hivyo basi, utendaji wa mwanadamu hauwezi kutenganishwa na maono katika hali yoyote ile. Wale ambao hawakubali maono mapya hawana vitendo vipya. Vitendo vyao havina uhusiano na ukweli kwani wanajifunga katika mafundisho ya dini na kufuata sheria zilizokufa; hawana maono mapya kabisa na kwa sababu hiyo hawatendi kulingana na enzi mpya. Wamepoteza maono na kwa kufanya hivyo wamepoteza kazi ya Roho Mtakatifu, hivyo basi kupoteza ukweli pia."

Ijumaa, 30 Novemba 2018

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Katika Imani Yako kwa Mungu Unapaswa Kumtii Mungu"

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Katika Imani Yako kwa Mungu Unapaswa Kumtii Mungu"

Mwenyezi Mungu anasema, "Jambo muhimu katika kumtii Mungu ni kuitambua nuru mpya, na kuweza kuikubali na kuiweka katika vitendo. Huu pekee ndio utii wa kweli. ... Kutoridhika na kuishi katikati ya neema za Mungu, kuwa na kiu ya ukweli, na kutafuta ukweli, na kunuia kuchumwa na Mungu—hii ndio maana ya kumtii Mungu katika hali ya utambuzi; hii ndiyo aina ya imani ambayo Mungu anataka."

Jumamosi, 24 Novemba 2018

Wimbo Mpya wa Dini | "Mungu Anapata Mwili ili tu Kumshinda Shetani na Kuwaokoa Binadamu"

Wimbo Mpya wa Dini | "Mungu Anapata Mwili ili tu Kumshinda Shetani na Kuwaokoa Binadamu"

Wakati wa kupata mwili kwa Mungu duniani, Anafanya kazi Yake miongoni mwa wanadamu. Kazi hii yote ina kusudi moja—kumshinda ibilisi Shetani. Atamshinda Shetani kumshinda mwanadamu, pia kupitia kukufanya mkamilifu.
Unapokuwa na ushuhuda mkubwa sana, hii pia itakuwa ishara ya kushindwa kwa Shetani. Mungu anapata mwili kumshinda Shetani na kuwaokoa wanadamu wote. Ili Shetani aweze kushindwa, mwanadamu kwanza anashindwa, kisha anakamilishwa.
Lakini kiini, huku akimshinda Shetani, Mungu anamwokoa mwanadamu toka mateso. Haijalishi kama hii kazi inafanyika Uchina au kote ulimwenguni, yote ni kwa ajili ya kumshinda Shetani na kumwokoa mwanadamu, aweze kuingia katika mapumziko. yote ni kwa ajili ya kumshinda Shetani Mungu anapata mwili kumshinda Shetani kuokoa wanadamu wote. Kupata mwili kwa Mungu katika mwili wa kawaida ni hasa kwa ajili ya kumshinda Shetani. Kazi ya Mungu huyu wa mwili ni kuwaokoa wanaompenda Mungu chini ya mbingu. Ni kwa sababu ya kuwashinda binadamu wote, na pia ni kwa sababu ya kumshinda Shetani.
Kiini cha kazi yote ya Mungu ni kumshinda Shetani kwa ajili ya wokovu wa mwanadamu. Mungu anapata mwili kumshinda Shetani na kuwaokoa wanadamu wote. Mungu anapata mwili kumshinda Shetani na kuwaokoa wanadamu wote, kuwaokoa wanadamu wote. Anawaokoa wanadamu wote. kuwaokoa wanadamu wote. Anawaokoa wanadamu wote.
kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumatatu, 12 Novemba 2018

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Ufafanuzi wa Tamko la Ishirini

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Ufafanuzi wa Tamko la Ishirini

Mungu aliwaumba wanadamu wote, na amewaongoza wanadamu wote mpaka leo. Hivyo, Mungu anajua yote yafanyikayo miongoni mwa wanadamu: Anajua uchungu ulio ndani ya ulimwengu wa mwanadamu, Anaelewa utamu ulio ndani ya ulimwengu wa mwanadamu, na kwa hiyo kila siku Yeye hufafanua hali za maisha za wanadamu wote, na, zaidi ya hayo, hushughulikia udhaifu na upotovu wa wanadamu wote. Si mapenzi ya Mungu kwamba wanadamu wote watupwe jahanamu, au kwamba wanadamu wote waokolewe. Kila mara huwa kuna kanuni kwa matendo ya Mungu, lakini hakuna anayeweza kuelewa sheria za yote Afanyayo. Watu wanapofahamu uadhama na ghadhabu ya Mungu, Mungu hubadilisha sauti mara moja kuwa ya huruma na upendo, lakini watu wanapokuja kujua huruma na upendo wa Mungu, Anaibadilisha sauti mara moja tena, Akiyafanya maneno Yake kuwa magumu kula kana kwamba ni kuku aliye hai. Katika maneno yote ya Mungu, mwanzo haujawahi kurudiwa kamwe, na maneno Yake yoyote hayajawahi kamwe kuzungumziwa kulingana na kanuni za matamko ya jana; hata sauti haifanani, wala hakuna uhusiano wowote katika maudhui—haya yote huwafanya watu wahisi wamekanganywa hata zaidi. Hii ni hekima ya Mungu, na ufichuzi wa tabia Yake. Yeye hutumia sauti na mtindo wa kunena Kwake kutawanya dhana za watu, ili kumtatiza Shetani, Akimnyang'anya Shetani nafasi ya kutia sumu matendo ya Mungu. Ajabu ya matendo ya Mungu husababisha akili za watu kuachwa zikiwa zimeshtushwa na maneno ya Mungu. Wanaweza kuupata mlango wao wa mbele kwa shida, au hata hawajui wakati wanaotarajiwa kula au kupumzika, hivyo wanatimiza kweli "kuacha kulala na kula ili kutumia rasilmali kwa ajili ya Mungu." Lakini hata wakati huu, Mungu bado haridhiki na hali za sasa, na kila mara huwa Amemkasirikia mwanadamu, Akimlazimisha kuonyesha moyo wake halisi. La sivyo, watu "wangetii" mara moja na kuwa wazembe, wakionyeshwa huruma kidogo tu na Mungu. Huu ni uduni wa mwanadamu; hawezi kubembelezwa, lakini lazima apigwe au alazimishwe ili asonge. "Kati ya wale wote Ninaowatazamia, hakuna mtu aliyewahi kunitafuta kwa makusudi na moja kwa moja. Wao wote huja mbele Zangu kwa kushawishiwa na wengine, wakiwafuata watu wengi, na hawana nia ya kulipa gharama au kutumia muda kustawisha maisha yao." Hivyo ndivyo hali za wote walio duniani zilivyo. Hivyo, bila kazi ya mitume au viongozi, watu wote wangekuwa wametawanyika kitambo sana, na kwa hiyo, kotekote katika enzi, hakujakuwa na ukosefu wa mitume na manabii.
Katika matamko haya, Mungu anazingatia kwa hali maalum kufanya muhtasari wa hali za maisha za wanadamu wote. Maneno kama "Maisha ya mwanadamu hayana joto hata kidogo, na hayana ladha wala mwanga wowote wa binadamu—lakini hajawahi kujizoeza nayo, akivumilia maisha yasiyo ya thamani ambayo yeye huenda hapa na pale akiharakisha kufanya mambo bila kufikia kitu chochote. Kwa haraka sana, siku ya kufa inakaribia, na mtu anakufa kifo cha uchungu." yote ni ya aina hii. Ni kwa nini Mungu ameongoza kuishi kwa wanadamu mpaka leo, na bado pia Anafichua utupu wa maisha katika ulimwengu wa mwanadamu? Na kwa nini Anafafanua maisha yote ya watu wote kama "kufika kwa haraka na kuondoka kwa haraka"? Huu, inaweza kusemwa, wote ni mpango wa Mungu, wote umeamuliwa na Mungu, na kwa hivyo, kwa namna moja unaashiria jinsi Mungu anadharau yote isipokuwa maisha katika uungu. Ingawa Mungu aliwaumba wanadamu wote, Hajawahi kamwe kufurahishwa na maisha ya wanadamu wote, na kwa hiyo Yeye huwaruhusu tu wanadamu waishi chini ya upotovu wa Shetani. Baada ya wanadamu kupitia mchakato huu, Atawaangamiza au kuwaokoa wanadamu, na hivyo mwanadamu atatimiza maisha duniani ambayo si matupu. Yote haya ni sehemu ya mpango wa Mungu. Na kwa hiyo, huwa kila mara kuna matamanio ndani ya fahamu ya mwanadamu, jambo ambalo limesababisha kutokuwa na mtu anayekufa kifo maasumu kwa furaha—lakini wale ambao tu hutimiza matamanio haya ni watu wa siku za mwisho. Leo, bado watu huishi katikati ya utupu usiogeuka na bado wanangoja matamanio haya yasiyoonekana: "Ninapoufunika uso Wangu kwa mikono Yangu, na kuwasukuma watu chini ya ardhi, mara moja wao hupungukiwa na pumzi, na ni vigumu waweze kuishi. Wao wote hunililia, wakiwa wenye hofu kwamba Nitawaangamiza, kwa maana wote wanatamani kutazama siku ambayo Nitatukuzwa." Hivyo ndivyo hali za watu zilivyo leo. Wote huishi katika "ombwe," bila "oksijeni," ambalo huwafanya kuwa na ugumu kupumua. Mungu hutumia matamanio ndani ya fahamu ya mwanadamu ili kuwasaidia wanadamu wote kuendelea kuishi; la sivyo, wote "wangeondoka nyumbani ili kuwa watawa wa kiume," kwa sababu hiyo wanadamu wote wangetoweka, na wangemalizika. Hivyo, ni kwa sababu ya ahadi ambayo Mungu alimpa mwanadamu ndio mwanadamu ameendelea kuishi mpaka leo. Huu ni ukweli, lakini mwanadamu hajawahi kugundua sheria hii, na kwa hiyo hajui ni kwa nini yeye "anahofu sana kwamba kifo kitamjia mara ya pili." Kwa kuwa ni binadamu, hakuna yeyote ambaye ana ujasiri wa kuendelea kuishi, wala hakuna yeyote ambaye amewahi kuwa na ujasiri wa kufa, na hivyo Mungu asema kwamba watu "hufa kifo cha uchungu." Hivyo ndivyo hali halisi miongoni mwa wanadamu ilivyo. Labda, katika matarajio yao, watu wengine wamekumbana na vizuizi na wakawaza juu ya kifo, lakini mawazo haya hayajawahi kufaulu; labda, wengine wamewaza juu ya kifo kwa sababu ya ugomvi wa familia, lakini wanawajali wapendwa wao, na wanabaki kutoweza kutimiza matamanio yao; na labda, wengine wamewaza juu ya kifo kwa sababu ya mapigo kwa ndoa yao, lakini hawako radhi kupitia hilo. Hivyo, watu hufa wakiwa na majonzi au majuto ya milele ndani ya mioyo yao. Hivyo ndivyo hali mbalimbali za watu wote zilivyo. Nikitazama juu ya ulimwengu mpana wa mwanadamu, watu huja na kwenda katika mkondo usiokuwa na mwisho, na ingawa wanahisi kwamba wangekuwa na raha zaidi kama wangekufa kuliko kuishi huku wakiendelea kusema maneno matupu, kamwe hakuna yeyote ambaye amewahi kuonyesha mfano kwa kufa na kufufuka, akawaambia walio hai namna ya kufurahia furaha ya kifo. Watu ni mafidhuli duni: Hawana haya wala kujiheshimu, nao daima hukosa kutimiza ahadi zao. Katika mpango Wake, Mungu alijaalia kikundi cha watu ambao wangefurahia ahadi Zake, na hivyo Mungu asema, "wengi wameishi katika mwili, na wengi wamekufa na wamezaliwa upya duniani. Hata hivyo kamwe hakuna yeyote kati yao aliyepata nafasi ya kufurahia baraka za ufalme leo." Wote ambao wanafurahia baraka za ufalme leo wamejaaliwa na Mungu tangu Alipouumba ulimwengu. Mungu alipanga ili roho hizi ziishi ndani ya mwili katika siku za mwisho, na hatimaye, Mungu atalipata kundi hili la watu, na kuwapangia kuwa Sinim. Kwa sababu, hususa, roho za watu hawa ni malaika, Mungu asema "Je, Nimetoweka kabisa katika roho ya mwanadamu?" Kwa kweli, watu wanapoishi katika mwili, wanabaki kutojua mambo ya ulimwengu wa kiroho. Kutokana na maneno haya rahisi hali ya moyo wa Mungu inaweza kuonekana: Maneno rahisi ya "mwanadamu kunipiga macho ya hadhari" yanaonyesha saikolojia ya Mungu isiyoelezeka kwa urahisi. Tangu wakati wa uumbaji mpaka leo, ndani ya moyo wa Mungu daima kumekuwa na majonzi yanayoandamana na ghadhabu na hukumu, kwani watu walio duniani hawana uwezo wa kuyajali mapenzi ya Mungu, kama tu asemavyo Mungu, "Mwanadamu ni kama kiumbe katili cha mlimani." Lakini Mungu asema pia, "Siku itawadia ambapo mwanadamu ataogelea kuja upande Wangu kutoka katikati ya bahari kuu, ili aweze kufurahia mali yote ya dunia na kuacha hatari ya kumezwa na bahari." Huu ndio ufanikishaji wa mapenzi ya Mungu, na pia unaweza kuelezwa kama mwelekeo usioepukika, na unaashiria ufanikishaji wa kazi ya Mungu.
Ufalme utakaposhuka duniani kabisa, watu wote watapata tena mfano wao wa asili. Hivyo, Mungu asema, "Nafurahia kutoka juu ya kiti Changu cha enzi, Naishi miongoni mwa nyota. Na malaika wananipa nyimbo mpya na dansi mpya. Udhaifu wao hausababishi machozi kutiririka nyusoni mwao tena. Sisikii tena, mbele Yangu, sauti za malaika wakilia, na hakuna tena anayeninung’unikia kuwa ana shida." Hili linaonyesha kwamba siku ambayo Mungu atapata utukufu kamili ndiyo siku ambayo mwanadamu atafurahia pumziko lake; watu hawakimbii huku na huko tena kutokana na usumbufu wa Shetani, dunia inaacha kuendelea mbele, na watu wanaishi katika pumziko—kwa kuwa idadi kubwa mno ya nyota angani zinafanywa upya, na jua, mwezi, na nyota, na kadhalika, na milima na mito yote iliyo mbinguni na duniani, vyote vinabadilishwa. Na kwa kuwa mwanadamu amebadilika, na Mungu amebadilika, kwa hiyo, pia, vitu vyote vinabadilika. Hili ndilo lengo la msingi la mpango wa usimamizi wa Mungu, na ule ambao utatimizwa hatimaye. Lengo la Mungu katika kuzungumza maneno haya yote ni hasa kwa mwanadamu kumjua Yeye. Watu hawaelewi amri za utawala za Mungu. Yote ambayo Mungu hufanya yametungwa na kupangwa na Mungu Mwenyewe, na Mungu hayuko radhi kumwacha mtu yeyote aingilie; badala yake, Yeye huwaruhusu watu kuona kwamba yote yamepangwa na Yeye na hayawezi kutimizwa na mwanadamu. Ingawa mwanadamu anaweza kuliona, au kuliona kuwa gumu kuwaza, yote yanadhibitiwa na Mungu pekee, na Mungu hatamani litiwe doa na wazo hata kidogo la mwanadamu. Mungu kwa kweli Hatawasamehe wowote wanaoshiriki, hata kwa kiasi kidogo; Mungu ni Mungu anayemwonea mwanadamu wivu, na inaonekana Roho wa Mungu hasa ni mwepesi wa kuhisi katika suala hili. Hivyo, yeyote aliye na nia hata kidogo ya kuingilia atazongwa mara moja na miale ya moto ya Mungu ya kuangamiza, ikimgeuza kuwa majivu ndani ya moto. Mungu hawaruhusu watu kuonyesha vipaji vyao jinsi wapendavyo, kwani wote walio na vipaji hawana uzima; hivi vipaji vya kudhaniwa humhudumia Mungu tu, na vinatokana na Shetani, na hivyo vinadharauliwa hasa na Mungu, Asiyeruhusu hili. Hata hivyo mara nyingi ni watu wasio na uhai ndio wanaweza kushiriki katika kazi ya Mungu, na, hata zaidi, kushiriki kwao huwa hakugunduliwi, kwani kunafichwa na vipaji vyao. Kotekote katika enzi, wale ambao wana vipawa hawajawahi kusimama imara, kwani hawana uzima, na hivyo wanakosa nguvu zozote za kupinga. Hivyo, Mungu asema, "Kama Sizungumzi waziwazi, mwanadamu kamwe hataacha kufanya upumbavu kamwe, na ataanguka katika kuadibu Kwangu bila kujua—kwa kuwa mwanadamu hanijui katika nafsi ya mwili Wangu." Wote ambao ni wa mwili na damu wanaongozwa na Mungu, lakini pia wanaishia katika kifungo cha Shetani, na kwa hiyo watu hawajawahi kuwa na uhusiano wa kawaida kati yao, kama ni kwa sababu ya tamaa, au kuabudu, au utaratibu wa mazingira yao. Mahusiano yasiyo ya kawaida kama hayo ndiyo Mungu anayachukua zaidi ya yote, na hivyo ni kwa sababu ya mahusiano kama hayo ndiyo maneno kama "Kile Ninachotaka ni viumbe vilivyo hai ambavyo vimejawa na uzima, si maiti ambazo zimegubika katika kifo. Kwa kuwa Ninaketi mezani pa ufalme, Nitatoa amri kwa watu wote duniani ili wapate ukaguzi Wangu" yanatoka kinywani mwa Mungu. Mungu anapokuwa juu ya ulimwengu mzima, kila siku Yeye huangalia kwa makini kila kitendo cha wale wa mwili na damu, na Hajawahi kumpuuza hata mmoja wao. Haya ni matendo ya Mungu. Na kwa hiyo, Nawasihi watu wote wachunguze fikira, mawazo, na matendo yao wenyewe. Siwataki muwe ishara ya aibu kwa Mungu, bali dhihirisho la utukufu wa Mungu, kwamba katika matendo, maneno, na maisha yenu yote, msiwe shabaha ya mizaha ya Shetani Haya ni matakwa ya Mungu kwa watu wote.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Vitabu.