Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Kazi-ya-Roho-Mtakatifu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Kazi-ya-Roho-Mtakatifu. Onyesha machapisho yote

Jumapili, 20 Oktoba 2019

Matamshi ya Mungu | “Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo ya Kazi Yake” (Sehemu ya Pili)

Matamshi ya Mungu | “Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo ya Kazi Yake” (Sehemu ya Pili)

Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”. Maudhui ya video hii: Tembea katika Njia ya Mungu: Mche Mungu na Kuepuka Maovu Mungu Hutumia Majaribio Tofauti ili Kupima Kama Watu Humcha Mungu na Kujiepusha na Maovu Kutomcha Mungu na Kutojiepusha na Maovu ni Kumpinga Mungu
Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Jumanne, 15 Oktoba 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Kutanafusi kwa Mwenye Uweza”

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Kutanafusi kwa Mwenye Uweza”

Mwenyezi Mungu anasema, “Wanadamu, walioacha ruzuku ya uzima kutoka kwa mwenye Uweza, hawajui kwa nini wanaishi, na bado wanaogopa kifo. Hukuna usaidizi, hakuna msaada, lakini bado wanadamu wanasita kufumba macho yao, wakiyakabili yote bila woga, wanaendeleza kwa muda mrefu kuishi kwa aibu ulimwenguni humu katika miili isiyokuwa na utambuzi wa nafsi. Unaishi hivyo, pasipo matumaini; anaishi hivyo, pasipo kuwa na lengo. Kuna aliye Mtakatifu tu katika hekaya atakayekuja kuwaokoa wale wanaoomboleza kwa maumivu na wanatamani sana majilio Yake. Imani hii haiwezi kutambulika kufikia sasa kwa watu ambao hawana utambuzi. Hata hivyo, watu bado wanaitaka sana. Mwenye Uweza ana rehema kwa watu hawa wanaoteseka sana. Wakati huo huo, Amechoshwa na watu hawa wasio na utambuzi, maana lazima Asubiri sana jibu kutoka kwa wanadamu. Anatamani kutafuta, kuutafuta moyo wako na roho yako. Anataka kukuletea chakula na maji na kukuzindua, ili usione kiu na kuhisi njaa tena. Unapokuwa umechoka na unapoanza kuona huzuni katika ulimwengu huu, usifadhaike, usilie. Mwenyezi Mungu, Mlinzi, atakaribisha kuwasili kwako wakati wowote.”

Alhamisi, 5 Septemba 2019

Neno la Mungu | “Ngurumo Saba Zatoa Sauti—Zikitabiri Kuwa Injili ya Ufalme Itaenea Kote Ulimwenguni”

Neno la Mungu | “Ngurumo Saba Zatoa Sauti—Zikitabiri Kuwa Injili ya Ufalme Itaenea Kote Ulimwenguni”

Mwenyezi Mungu anasema, “Wakati nuru ya Mashariki inapong'aa polepole tu ndipo giza kote duniani litaanza kugeuka na kuwa nuru, na hapo tu ndipo mwanadamu atatambua kwamba Nilishatoka Israeli zamani na Nimeanza kuchomoza upya Mashariki. Niliwahi kushuka Israeli na baadaye Niliondoka kutoka huko, Siwezi tena kuzaliwa Israeli kwa mara nyingine, kwa kuwa kazi Yangu inauongoza ulimwengu mzima na, zaidi ya hilo, umeme unamulika moja kwa moja kutoka Mashariki kwenda Magharibi. Hii ndiyo sababu Nimeshuka Mashariki na kuwaletea watu wa Mashariki Kanaani. Ningependa kuwaleta watu kutoka dunia nzima waje katika nchi ya Kanaani, na kwa hiyo Naendelea kutoa maneno Yangu katika nchi ya Kanaani ili kuudhibiti ulimwengu mzima. Kwa wakati huu,hakuna nuru katika dunia nzima isipokuwa katika Kanaani, na watu wote wamehatarishwa na njaa na baridi. Niliipa Israeli utukufu Wangu kisha Nikauchukua na baadaye Nikawaleta Waisraeli Mashariki, na vilevile ubinadamu wote Mashariki. Nimewaleta wote kwenye nuru ili waweze kuungana tena nayo, na kushirikiana na nuru , na wasilazimike kuitafuta tena.” Tazama zaidi: Maonyesho ya Mungu | "Mwanadamu Anaweza Kuokolewa tu Katikati ya Usimamizi wa Mungu"
Mimi Naeneza kazi Yangu katika nchi za Mataifa. Utukufu Wangu unamulika kotekote ulimwenguni; mapenzi Yangu yamo katika wanadamu yakitawanyika hapa na pale, wote wakiongozwa kwa mkono Wangu na kufanya kazi ambayo Nimewapa. Kuanzia wakati huu kuendelea, Nimeingia katika enzi mpya, kuwaleta watu wote katika ulimwengu mwingine. Niliporudi katika “nchi Yangu,” Nilianza sehemu nyingine tena ya kazi katika mpango Wangu wa asili, ili mwanadamu aje kunijua zaidi. Nauchukua ulimwengu katika ukamilifu wake na kuona kwamba[a] ni wakati muafaka wa kazi Yangu, kwa hiyo Naharakisha mbele na nyuma kufanya kazi Yangu mpya ndani ya mwanadamu. Hii ni enzi mpya, hata hivyo, na Nimeleta kazi mpya ili Niwachukue watu wapya wengi zaidi katika enzi mpya na kuachana na wengi wa wale Nitakaowaondoa. Katika taifa la joka kubwa jekundu, Nimetekeleza hatua ya kazi isiyoeleweka kwa wanadamu, kuwafanya kuyumba katika upepo, ambapo baadaye wengi wanabebwa kwa siri na upepo unaovuma. Kweli, huu ni “uwanja wa kupura” Ninaotaka kuusafisha; ni kile Ninachotamani na pia ni mpango Wangu. Kwa maana wengi waovu wameingia ndani kimya wakati Niko kazini, lakini Sina haraka ya kuwafukuza. Badala yake, Nitawatawanya wakati utakapofika. Ni baada ya hapo tu ndipo Nitakuwa chemchemi ya uzima, kuwakubalia wanaonipenda kweli wapokee kutoka Kwangu tunda la mtini na harufu ya yungiyungi. Katika nchi ambako Shetani huishi, nchi ya vumbi, hakuna dhahabu safi iliyobaki, ila ni mchanga tu, na kwa hiyo, Nikikabiliwa na hali hizi, Nafanya hatua hiyo ya kazi. Lazima ujue kwamba Ninachopata ni dhahabu safi, iliyosafishwa, wala si mchanga. Ni jinsi gani waovu wanaweza kubaki katika nyumba Yangu? Ninawezaje kuruhusu Mbweha kuwa vimelea ndani ya paradiso Yangu? Natumia kila mbinu inayoweza kufikiriwa kuvifukuza vitu hivi. Kabla ya mapenzi Yangu kufichuliwa, hakuna anayefahamu Ninachotaka kufanya. Nikichukua fursa hii, Ninawafukuza wale waovu, na wanalazimika kuondoka machoni Pangu. Hili ndilo Mimi huwafanyia waovu, lakini bado kutakuwa na siku ya wao kunifanyia huduma. Hamu ya watu kupata baraka ni kubwa mno; Kwa hivyo Ninageuza mwili Wangu na kuonyesha uso Wangu wa utukufu kwa nchi za Mataifa, ili watu wote waishi katika dunia yao wenyewe na kujihukumu, huku Naendelea kusema maneno ambayo Napaswa kuyasema na kuwaruzuku wanadamu wanachohitaji. Wakati wanadamu wanapata fahamu, Nitakuwa Nimeeneza kazi Yangu kitambo. Kisha Nitawaonyesha wanadamu mapenzi Yangu, na kuanza sehemu ya pili ya kazi Yangu juu ya wanadamu, kuwaruhusu watu wote wanifuate kwa karibu ili waambatane na kazi Yangu, na kuwaruhusu watu kufanya kila wawezalo kutekeleza nami kazi Ninayopaswa kufanya.
Kotekote katika ulimwengu Ninafanya kazi Yangu, na katika Mashariki, mashambulio ya radi yanapiga bila kukoma, yakiyatingisha mataifa yote na madhehebu. Ni sauti Yangu ndiyo imewaleta watu katika wakati wa sasa. Nitawasababisha watu wote kushindwa na sauti Yangu, kuingia katika mkondo huu, na kunyenyekea mbele Yangu, kwa maana Nilijirudishia utukufu Wangu kutoka duniani kote zamani na Nikautoa upya Mashariki. Ni nani asiyetamani kuuona utukufu Wangu? Ni nani asiyesubiri kwa hamu kurudi Kwangu? Ni nani asiye na kiu cha kuonekana Kwangu tena? Ni nani asiyetamani kuona kupendeza Kwangu? Ni nani hangetaka kuja kwenye nuru? Ni nani hangeuona utajiri wa Kanaani? Ni nani hangoji kwa hamu kurudi kwa Mkombozi? Ni nani asiyempenda kwa dhati Mwenyezi Mkuu? Sauti Yangu itaenea kotekote duniani; Ningependa, kuwazungumzia maneno mengi zaidi wateule wangu, Nikiwatazama. Kama radi yenye nguvu inayotingisha milima na mito, Nanena maneno Yangu kwa ulimwengu wote na kwa wanadamu. Hivyo maneno yaliyo kinywani Mwangu yamekuwa hazina ya mwanadamu, na watu wote wanayahifadhi maneno Yangu kwa upendo mkubwa. Umeme wa radi unaangaza kutoka Mashariki mpaka Magharibi. Maneno Yangu ni kiasi kwamba mwanadamu huchukia kuyaacha na pia huyaona kama yasiyoeleweka, lakini zaidi ya yote mwanadamu huyafurahia. Kama mtoto mchanga aliyezaliwa hivi karibuni, wanadamu wote wana uchangamfu na furaha, wakisherehekea kuja Kwangu. Kwa sauti Yangu, nitawaleta wanadamu wote mbele Yangu. Tangu hapo, Nitaingia rasmi katika jamii ya wanadamu ili waje kuniabudu. Kwa utukufu Ninaoutoa na maneno yaliyo kinywani Mwangu, Nitawafanya watu wote kuja mbele Yangu na kuona kwamba umeme unaangaza kutoka Mashariki na kwamba Mimi pia Nimeshuka kwenye “Mlima wa Mizeituni” wa Mashariki. Wataona kwamba Mimi tayari Nimekuwa duniani kwa muda mrefu, sio kama Mwana wa Wayahudi tena lakini kama Umeme wa Mashariki. Kwani Nimeshafufuka kitambo, na Nimeondoka miongoni mwa wanadamu, na kisha Nimeonekana tena miongoni mwa wanadamu Nikiwa na utukufu. Mimi ndiye Niliyeabudiwa enzi nyingi kabla ya wakati huu, na pia Mimi ni “mtoto mchanga” Aliyeachwa na Israeli enzi nyingi kabla ya wakati huu. Zaidi ya hayo, Mimi ndiye Mwenyezi Mungu mwenye utukufu wote wa enzi hii! Hebu wote waje mbele ya kiti Changu cha enzi ili waone uso Wangu mtukufu, wasikie sauti Yangu, na kuangalia matendo Yangu. Huu ndio ukamilifu wa mapenzi Yangu; ni mwisho na kilele cha mpango Wangu, na vilevile madhumuni ya usimamizi Wangu. Hebu kila taifa liniabudu Mimi, kila ulimi unikiri Mimi, kila mtu aniamini Mimi, na watu wote wawe chini Yangu!

Jumamosi, 31 Agosti 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Enzi ya Ufalme Ndiyo Enzi ya Neno” (Dondoo1)

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Enzi ya Ufalme Ndiyo Enzi ya Neno” (Dondoo1)

Mwenyezi Mungu anasema, “Katika Enzi ya Ufalme, Mungu anatumia neno ili kukaribisha enzi mpya, ili kubadilisha mbinu za kazi Yake, na kuweza kufanya kazi katika enzi nzima. Hii ndiyo kanuni ambayo kwayo Mungu hufanya kazi katika Enzi ya Neno. Alikuwa mwili ili kuweza kuzungumza kutoka mitazamo tofauti, kumwezesha binadamu kumwona Mungu kwa kweli, ambaye ni Neno linaloonekana katika mwili, na hekima Yake na maajabu. Kazi kama hiyo inafanywa ili kwa njia bora zaidi kutimiza shabaha za kumshinda binadamu, kumkamilisha binadamu, na kumwondoa binadamu. Hii ndiyo maana ya kweli ya kutumia neno ili kufanya kazi katika Enzi ya Neno. Kupitia katika neno, binadamu anajua kazi ya Mungu, tabia ya Mungu, kiini cha binadamu, na kile ambacho binadamu anastahili kuingia ndani yake. Kupitia katika neno, kazi yote ambayo Mungu angependa kufanya katika Enzi ya Neno inatimizwa. Kupitia katika neno, binadamu anafichuliwa, anaondolewa, na kujaribiwa. Binadamu ameliona neno, amelisikia neno, na akapata habari ya uwepo wa neno. Kutokana na haya, binadamu anaamini katika uwepo wa Mungu; binadamu anaamini katika uwezo na hekima za Mungu, pamoja na moyo wa upendo wa Mungu kwa binadamu na tamanio Lake la kumwokoa binadamu. Ingawa neno ‘neno’ ni rahisi na la kawaida, neno kutoka kwenye kinywa cha Mungu mwenye mwili hutikisa dunia nzima; neno Lake hubadilisha moyo wa binadamu, fikira na tabia zee za binadamu, na sura nzee ya ulimwengu mzima. Kupitia enzi nyingi, Mungu pekee wa leo ndiye anayefanya kazi katika njia kama hiyo, na ni Yeye tu Anayeongea na kumwokoa binadamu hivyo. Kuanzia wakati huu kuendelea, binadamu huishi katika mwongozo wa neno, wakichungwa na kuruzukiwa na neno. Binadamu wote wanaishi katika ulimwengu wa neno, wanaishi katika laana na baraka za neno la Mungu, na hata kuna binadamu zaidi wanaoishi chini ya hukumu na kuadibu kwa neno. Maneno haya na kazi hii vyote ni kwa minajili ya wokovu wa binadamu, kwa minajili ya kutimiza mapenzi ya Mungu, na kwa minajili ya kubadilisha sura asilia ya ulimwengu wa uumbaji wa kale. Mungu aliuumba ulimwengu kwa neno, huwaongoza wanadamu kote ulimwenguni kwa neno, na pia hushinda na kuwaokoa binadamu kwa neno. Hatimaye, Yeye atatumia neno ili kuutamatisha ulimwengu mzima wa kale. Ni hapo tu ndipo mpango wa usimamizi unapokuwa mkamilifu kabisa. Katika Enzi nzima ya Ufalme, Mungu hutumia neno kufanya kazi Yake na kutimiza matokeo ya kazi Yake; Hafanyi maajabu au kutenda miujiza; Anafanya tu kazi Yake kupitia kwa neno. Kwa sababu ya neno, binadamu anastawishwa na kuruzukiwa; kwa sababu ya neno, binadamu hupokea maarifa na kupata uzoefu wa kweli. Binadamu katika Enzi ya Neno amepokea kwa kweli baraka za kipekee. Binadamu huwa hapati maumivu ya mwili na hufurahia tu ruzuku nyingi ya neno la Mungu; hawahitaji tena kutafuta au kushika safari, na kwa utulivu huona kuonekana kwa Mungu, wanamsikia Yeye akiongea binafsi, wanapokea ujazo Wake, na kumwona Yeye binafsi akifanya kazi Yake. Haya ndiyo mambo ambayo binadamu katika enzi zilizopita hawakuweza kufurahia, na hizi ndizo baraka ambazo wasingewahi kupokea.”

Jumatano, 24 Julai 2019

Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu | “Mungu Ndiye Bwana wa Viumbe Vyote”

Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu | “Mungu Ndiye Bwana wa Viumbe Vyote”

Mwenyezi Mungu anasema, “Kwa kweli, Mungu ni Bwana wa mambo yote. Yeye ndiye Mungu wa viumbe vyote. Yeye si Mungu wa Waisraeli pekee, na Yeye si Mungu wa Wayahudi pekee; Yeye ni Mungu wa viumbe vyote. … Kazi Yake ya awali ilifanywa Yudea, ndani ya eneo la Israeli; katika mataifa yasiyo ya Kiyahudi Hakufanya kazi yoyote ya uzinduzi wa enzi hata kidogo. Hatua ya mwisho ya kazi Yake haifanywi tu miongoni mwa watu wa mataifa yasiyo ya Kiyahudi; hata zaidi ya hayo, inafanywa miongoni mwa watu waliolaaniwa. Jambo hili moja ndio ushahidi unaoweza zaidi kumwaibisha Shetani; hivyo, Mungu “anakuwa” Mungu wa viumbe vyote ulimwenguni na kuwa Bwana wa vitu vyote, Anayeabudiwa na kila kiumbe mwenye uhai .” Tazama zaidi: Gospel Music | "Yule Anayeshikilia Ukuu Juu ya Kila Kitu"| Musical Documentary (Swahili Subtitles)
Je, hizi zote si dhana za binadamu? Mungu aliunda mbingu na dunia yote na vitu vyote, na kuumba viumbe vyote; Angewezaje kuzuia kazi Yake ndani ya Israeli peke yake? Katika hali hiyo, kungekuwa na haja gani ya Yeye kuumba viumbe Vyake vyote? Aliiumba dunia nzima; Ametekeleza mpango Wake wa usimamizi wa miaka elfu sita sio tu ndani ya Israeli lakini pia na kila mtu ulimwenguni. Bila kujali kama anaishi Uchina, Amerika, Uingereza ama Urusi, kila mtu ni wa ukoo wa Adamu; wote wameumbwa na Mungu. Hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuondoka katika mawanda ya viumbe wa Mungu, na hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuepuka utambulisho wa “ukoo wa Adamu.” Wote ni viumbe wa Mungu, na wote ni wa ukoo wa Adamu; pia ni wazawa wapotovu wa Adamu na Hawa. Sio tu Waisraeli ambao ni viumbe wa Mungu, lakini ni watu wote; hata hivyo, wengine miongoni mwa viumbe wamelaaniwa, na wengine wamebarikiwa. Kuna mambo mengi ya kupendeza kuwahusu Waisraeli; Mungu awali alikuwa akifanya kazi nao kwa sababu walikuwa watu wapotovu kwa kiasi kidogo zaidi. Wachina ni dhaifu wakilinganishwa nao, na hawawezi hata kutumaini kulingana nao; hivyo, Mungu awali alifanya kazi miongoni mwa watu wa Israeli, na hatua ya pili ya kazi Yake ilifanywa tu Yudea. Kwa sababu hii, watu huunda dhana nyingi na kanuni nyingi. Kwa kweli, iwapo Angetenda kulingana na dhana za binadamu, Mungu angekuwa tu Mungu wa Waisraeli; kwa njia hii Asingeweza kupanua kazi Yake katika mataifa yasiyo ya Kiyahudi, kwa sababu Angekuwa tu Mungu wa Waisraeli badala ya Mungu wa viumbe vyote. Unabii ulisema kuwa jina la Yehova lingekuwa kubwa katika mataifa yasiyo ya Kiyahudi na kuwa jina la Yehova lingeenezwa kwa mataifa yasiyo ya Kiyahudi—mbona ulisema hivi? Iwapo Mungu angekuwa Mungu wa Waisraeli tu, basi Angefanya kazi tu Israeli. Zaidi ya hayo, Asingepanua kazi hii, na Asingefanya huu unabii. Kwa sababu Alifanya huu unabii, Angehitaji kuipanua kazi Yake hadi mataifa yasiyo ya Kiyahudi na hadi kila taifa na mahali. Kwa sababu Alisema hili, basi Angefanya hivyo. Huu ndio mpango Wake, kwani Yeye ndiye Bwana aliyeumba mbingu na dunia na vitu vyote, na Mungu wa viumbe vyote. Bila kujali iwapo Anafanya kazi na Waisraeli ama katika Yudea nzima, kazi Anayoifanya ni kazi ya ulimwengu mzima na kazi ya binadamu wote. Kazi Anayoifanya leo katika taifa la joka kubwa jekundu—katika taifa lisilo la Kiyahudi—bado ni kazi ya binadamu wote. Israeli inaweza kuwa kituo cha kazi Yake duniani; vivyo hivyo, Uchina pia inaweza kuwa kituo cha kazi Yake miongoni mwa mataifa yasiyo ya Kiyahudi. Je, sasa Hajatimiza unabii kwamba “jina la Yehova litakuwa kubwa katika mataifa yasiyo ya Kiyahudi”? Hatua ya kwanza ya kazi Yake miongoni mwa mataifa yasiyo ya Kiyahudi inahusu kazi hii Anayoifanya katika taifa la joka kuu jekundu. Kwa Mungu mwenye mwili kufanya kazi katika nchi hii na kufanya kazi miongoni mwa hawa watu waliolaaniwa hasa inaenda kinyume na dhana za binadamu; hawa watu ni wa chini zaidi na wasio na thamani yoyote. Hawa wote ni watu ambao Yehova alikuwa amewaacha mwanzoni. Watu wanaweza kuachwa na watu wengine, lakini wakiachwa na Mungu, hawa watu hawatakuwa na hadhi, na watakuwa na thamani ya kiwango cha chini zaidi. Kama sehemu ya viumbe, kumilikiwa na Shetani ama kuachwa na watu wengine yote mawili ni mambo machungu, lakini sehemu ya viumbe ikiachwa na Bwana wa viumbe, hii inaashiria kwamba hadhi yake iko katika kiwango cha chini kabisa. Wazawa wa Moabu walilaaniwa, na walizaliwa ndani ya nchi hii isiyo na maendeleo; bila shaka, wazawa wa Moabu ni watu walio na hadhi ya chini zaidi chini ya ushawishi wa giza. Kwa sababu hawa watu walimiliki hadhi ya chini zaidi zamani, kazi inayofanywa miongoni mwao inaweza kabisa kuzivunja dhana za binadamu, na pia ni kazi yenye faida kubwa zaidi kwa mpango Wake mzima wa usimamizi wa miaka elfu sita. Ili Afanye kazi miongoni mwa watu hawa ni kitendo kinachoweza zaidi kuzivunja dhana za binadamu; Akiwa na hili Anazindua enzi; na hili Anavunja dhana zote za binadamu; Akiwa na hili Anatamatisha kazi ya Enzi nzima ya Neema. Kazi Yake ya awali ilifanywa Yudea, ndani ya eneo la Israeli; katika mataifa yasiyo ya Kiyahudi Hakufanya kazi yoyote ya uzinduzi wa enzi hata kidogo. Hatua ya mwisho ya kazi Yake haifanywi tu miongoni mwa watu wa mataifa yasiyo ya Kiyahudi; hata zaidi ya hayo, inafanywa miongoni mwa watu waliolaaniwa. Jambo hili moja ndio ushahidi unaoweza zaidi kumwaibisha Shetani; hivyo, Mungu “anakuwa” Mungu wa viumbe vyote ulimwenguni na kuwa Bwana wa vitu vyote, Anayeabudiwa na kila kiumbe mwenye uhai.
Kwa sasa bado kuna watu wengine wasioelewa ni aina gani ya kazi mpya ambayo Mungu amezindua. Mungu amefanya mwanzo mpya katika mataifa yasiyo ya Kiyahudi na Ameanza enzi nyingine na kuzindua kazi nyingine, na Anafanya kazi miongoni mwa ukoo wa Moabu. Je, hii si kazi Yake mpya kabisa? Hakuna yeyote katika enzi zote aliyeipitia kazi hii, wala hakuna aliyeisikia, sembuse kuithamini. Hekima ya Mungu, ajabu ya Mungu, kutoeleweka kwa Mungu, ukubwa wa Mungu, utakatifu wa Mungu vinategemea hatua hii ya kazi katika siku za mwisho, ili kuibuka wazi. Je, hii si kazi mpya inayovunja dhana za binadamu? Bado kuna wale wanaofikiria hivi: “Kwa sababu Mungu alimlaani Moabu na kusema kuwa Angewaacha wazawa wa Moabu, Angeweza kuwaokoaje sasa?” Hao ni wale watu kutoka mataifa yasiyo ya Kiyahudi waliolaaniwa na kulazimishwa nje ya Israeli; Waisraeli waliwaita “mbwa wasio wa Kiyahudi.” Kwa mtazamo wa kila mtu, wao sio mbwa wasio wa Kiyahudi pekee, lakini mbaya hata zaidi, ni wana wa maangamizi; kwa maneno mengine, wao si wateule wa Mungu. Ingawa awali walikuwa wamezaliwa ndani ya eneo la Israeli, wao siyo sehemu ya watu wa Israeli; wao pia walifukuzwa kwenda kwa mataifa yasiyo ya Kiyahudi. Wao ndio watu wa chini zaidi. Ni kwa sababu hasa wao ni watu wa chini zaidi miongoni mwa binadamu ndio Mungu anatekeleza kazi Yake ya kuzindua enzi mpya miongoni mwao, kwani wao ni wawakilishi wa binadamu wapotovu. Kazi ya Mungu haikosi uchaguzi ama madhumuni, kazi Anayoifanya miongoni mwa watu hawa leo pia ni kazi inayofanywa miongoni mwa viumbe. Nuhu alikuwa sehemu ya viumbe, kama walivyo wazawa wake. Yeyote duniani aliye na mwili na damu ni sehemu ya viumbe. Kazi ya Mungu imeelekezwa kwa viumbe wote; haitekelezwi kulingana na kama mtu amelaaniwa baada ya kuumbwa. Kazi Yake ya usimamizi imeelekezwa kwa viumbe wote, sio wale wateule wasiolaaniwa. Kwa sababu Mungu anataka kutekeleza kazi Yake miongoni mwa viumbe Vyake, kwa hakika Ataifanya hadi kukamilika kwa mafanikio; Atafanya kazi miongoni mwa hao watu walio na manufaa kwa kazi Yake. Kwa hivyo, Anavunja mikataba yote ya kufanya kazi miongoni mwa watu; Kwake, maneno “kulaaniwa,” “kuadibu” na “kubarikiwa” hayana maana! Wayahudi ni wazuri hasa, na wateule wa Israeli sio wabaya pia; ni watu wenye ubora mzuri wa tabia na ubinadamu mzuri. Awali Yehova alizindua kazi Yake miongoni mwao na Akafanya kazi Yake ya awali, lakini ingekuwa bila maana kama Angewatumia kama wapokeaji wa kazi Yake ya ushindi sasa. Ingawa wao pia ni sehemu ya viumbe na wana vipengele vingi vyema, ingekuwa bila maana kutekeleza hatua hii ya kazi miongoni mwao. Asingeweza kumshinda yeyote, wala Asingeweza kushawishi viumbe wote. Huu ndio umuhimu wa uhamisho wa kazi Yake kwa watu hawa wa taifa la joka kubwa jekundu. Maana ya ndani zaidi hapa ni ya uzinduzi Wake wa enzi, ya kuvunja Kwake kwa kanuni zote na dhana zote za mwanadamu na pia kwa kumaliza Kwake kazi ya Enzi nzima ya Neema. Kama kazi Yake ya sasa ingefanywa miongoni mwa Waisraeli, ikifika wakati ambao mpango Wake wa usimamizi wa miaka elfu sita kukamilika, kila mtu angeamini kuwa Mungu ni Mungu tu wa Waisraeli, kuwa Waisraeli tu ndio wateule wa Mungu, kuwa Waisraeli tu ndio wanaostahili kurithi baraka na ahadi za Mungu. Katika siku za mwisho, Mungu anapata mwili katika taifa lisilo la Kiyahudi la joka kubwa jekundu; Ametimiza kazi ya Mungu kama Mungu wa viumbe wote; Amekamilisha kazi Yake yote ya usimamizi, na Atamaliza sehemu kuu ya kazi Yake kwa taifa la joka kubwa jekundu. Kiini cha hatua hizi tatu za kazi ni wokovu wa mwanadamu—ambao ni, kufanya viumbe wote vimwabudu Bwana wa viumbe. Hivyo basi, kila hatua ya kazi hii ni muhimu sana; Mungu hatafanya chochote kisicho na maana ama thamani. Kwa upande mmoja, hatua hii ya kazi inajumuisha kuzindua enzi na kukamilisha enzi mbili za awali; kwa upande mwingine inajumuisha kuvunja dhana zote za mwanadamu na njia ya zamani ya imani ya mwanadamu na maarifa. Kazi ya enzi mbili za awali ilifanywa kulingana na dhana tofauti za binadamu; hatua hii, hata hivyo, inafuta kabisa dhana za binadamu, na hivyo kuwashinda binadamu kikamilifu. Kwa kutumia ushindi wa ukoo wa Moabu na kutumia kazi iliyotekelezwa miongoni mwa ukoo wa Moabu, Mungu atawashinda binadamu wote katika ulimwengu mzima. Huu ndio umuhimu wa kina zaidi wa hatua hii ya kazi Yake, na ndicho kipengele cha thamani ya hatua hii ya kazi Yake. Hata kama sasa unajua kuwa hadhi yako ni ya chini na kuwa una thamani ya chini, bado utahisi kwamba umekutana na jambo linalofurahisha sana: Umerithi baraka kubwa, ukapata ahadi kubwa, na unaweza kamilisha hii kazi kubwa ya Mungu, na unaweza kuuona uso wa kweli wa Mungu, kujua tabia Yake ya asili, na kufanya mapenzi ya Mungu. Hatua mbili za awali za kazi ya Mungu zilifanywa Israeli. Iwapo hatua hii ya kazi Yake katika siku za mwisho bado ingefanywa miongoni mwa Waisraeli, viumbe wote havingeamini kwamba Waisraeli tu ndio waliokuwa wateule, lakini pia mpango wa usimamizi wa Mungu wote haungefikia athari iliyotaka. Wakati ambapo hatua hizi mbili za kazi Yake zilifanywa Israeli, hakuna kazi yoyote mpya iliyokuwa imefanywa na hakuna kazi yoyote ya Mungu ya kuzindua enzi ilikuwa imewahi kufanywa katika mataifa yasiyo ya Kiyahudi. Hatua hii ya kazi ya kuzindua enzi inafanywa kwanza katika mataifa yasiyo ya Kiyahudi, na zaidi ya hayo, inafanywa kwanza miongoni mwa ukoo wa Moabu; hii imezindua enzi mpya. Mungu amevunja maarifa yoyote yaliyo ndani ya dhana za binadamu na hajaruhusu yoyote yaendelee kuwa hai. Katika kazi Yake ya kushinda Amevunja dhana za binadamu, hiyo njia ya zamani, ya maarifa ya binadamu, Anaruhusu watu waone kuwa kwa Mungu hakuna kanuni, kwamba hakuna kitu kizee kumhusu Mungu, kwamba kazi Anayoifanya ni ya uhuru kabisa, ni huru kabisa, kwamba Yeye yuko sahihi katika chochote Anachofanya. Ni lazima utii kikamilifu kazi yoyote Anayoifanya miongoni mwa viumbe. Kazi yoyote Anayoifanya ni ya maana na inafanywa kulingana na mtazamo Wake na maarifa Yake na sio kulingana na chaguo za watu na dhana za watu. Anafanya yale mambo yaliyo na manufaa kwa kazi Yake; kama kitu hakina manufaa kwa kazi Yake, Hatakifanya, hata kiwe kizuri vipi! Anafanya kazi na kuchagua mpokeaji na eneo la kazi Yake kulingana na maana na madhumuni ya kazi Yake. Hafuati kanuni za zamani, wala Hafuati fomula nzee; badala yake, Anapanga kazi Yake kulingana na umuhimu wa kazi; mwishowe, Anataka kufikia matokeo yake ya kweli na madhumuni yanayotarajiwa. Iwapo huelewi mambo haya sasa, kazi hii haitatimiza matokeo yoyote kwako.

Jumamosi, 6 Julai 2019

Sura ya 30. Kumtumikia Mungu Mtu Anapaswa Kutembea Njia ya Petro

Sura ya 30. Kumtumikia Mungu Mtu Anapaswa Kutembea Njia ya Petro

Mwenyezi Mungu alisema, Watu wengi hawawezi kuainisha ni watu gani wana ukweli, watu gani hawana ukweli na watu gani husema mambo yaliyo na ukweli. Unapoulizwa kueleza ni nini maana ya "ukweli," huwezi kueleza kwa wazi. Lakini mara tu mtu anaposema kitu, unasema: “Mtazamo wake ni wa kweli. Maneno ayasemayo yanaonyesha ufahamu wa utendaji uliopatikana kupitia kwa uzoefu.” Unaelewa mara tu unapowasikia wakizungumza. Kwa ninyi hapa mlio wapya, Nikiwauliza ni nini maana ya 'uhalisi,' hamtaweza tu kunijibu, lakini pia hamtaweza kueleza tofauti kati ya mtu anayezungumza uhalisi na mtu anayezungumza mafundisho ya dini. Hili halisemwi kuwadunisha ninyi, ni tu kwamba hamna uzoefu. Tazama wale wakongwe wa kanisa; ingawa washawishi wengine wa kufanya mengi huenda wakawakanganya na vitu wasivyoweza haswa kutambua sababu sahihi, bado wanajua kwamba wanachosema watu hao si sahihi. Wanaweza kutambua ni watu gani wanazungumza mafundisho ya dini, na watu gani wanazungumza uhalisi. Ninyi, kwa hali yoyote, hata bado hamjababia. Hili halisemwi kuwashushia hadhi, kwa hivyo msione vibaya kwa sababu ya hili. Hii ni njia ya kawaida ya uzoefu ambayo kila mtu ni lazima apitie. Kila mtu ni lazima apitie miaka mingi ya kunyunyiziwa maji, kufanyiwa uchunguji, kusikiliza, kuhisi, kutambua na kupitia kabla ya kufahamu polepole lakini kwa kina uzoefu wa maisha, kabla ya kuvuka lango na kufungua macho yao. Ukizungumza tu mafundisho ya dini na kusikia mafundisho ya dini, ikiwa huwezi kutambua masuala yanayohusu uhalisi na usiwe na utambuzi, basi macho yako hayajafunguliwa; bado tu hayajafunguliwa. Ni nini maana ya "macho yako hayajafunguliwa"? Inamaanisha bado hujavuka lango, na huo ni ukweli. Inamaanisha kwamba hujavuka lango panapohusiana na ukweli. Jitazameni sasa. Labda unaweza kufanya kazi ya uchungaji, kuwasaidia wengine, kutoa msaada na kutumia, au kufanya mambo mengine ya desturi katika familia ya Mungu. Lakini wewe hasa huna uhalisi, wala hutakuwa hasa na utambuzi wowote wa kufikia uhalisi au kufikia nyaraka na mafundisho ya dini. Labda hamjaridhishwa na hili, mpaka siku moja mtu fulani aje anayezungumza mafundisho ya dini, aliye na maneno ya kushawishi, na kisha huenda mtamkweza. Na wakati mtu yule aliye na uhalisi wa kweli ajapo, aliye kimya, asiyetoa sauti, basi huenda mtamdharau. Mara mnapofanya hivi, wakati huo mtajua kimo chenu wenyewe kiko wapi. Ndio, kimo cha mwanadamu, ufahamu wa mtu kuhusu uhalisi na wa mtu mwenyewe, uzoefu wa mtu kuhusu kweli, ufahamu wa mtu kuhusu Mungu—mambo haya yote hutokana na uzoefu, hutokana na kuishi siku baada ya siku, hili ni wazi na dhahiri. Vitu hivi bila shaka havitokani na kusoma wala kutoka kwa mambo mangapi uliyoyasikia. "Nina mambo haya, nimeyasikia na ninayakumbuka. Kiwango changu cha maarifa kiko juu sana, mimi ni mwanafunzi wa chuo, ninafanya kazi fulani, ninachunguza jambo fulani, na mimi huyajua mambo mara tu niyasikiapo." Unaweza kutumia maarifa uliyojifunza kusikia falsafa, siasa au fasihi. Lakini huwezi kuyatumia hapa, hayana maana! Tuna nini hapa, basi? Maarifa uliyojifunza huenda yakakusaidia kujua maneno yaliyoandikwa ya ukweli au kuhusu vile yameelezwa vizuri zaidi kuliko wengine, lakini wewe si bora kuliko wengine inapohusu wewe kuupitia ukweli; huna heri kuhusiano na hilo. Mnalikubali hili, sivyo? Hamchunguzi masuala ya uzoefu wa maisha na mnakosa mambo mengi sana. Lakini kwa ninyi ambao mna maarifa fulani, ambao sasa mko katika nafasi ya heri ya kuwa kiongozi juu ya watu wengine, ambao mko kazini mara kwa mara na ambao hukutana na wakongwe wa kanisa walio katika viwango vya juu, na ambao hufanya kazi fulani maalum, mnaweza kuendelea haraka zaidi. Mnaweza kuendelea haraka sana kuliko vile wale wakongwe wa kanisa wangeweza hapo awali, haraka na ufahamu wenu wa uhalisi, na hali yoyote ya ukweli na kwa kujifahamu wenyewe. Labda hamtatembea katika njia inayopinda au labda ninyi pia mtahitajika kupatwa na vipingamizi fulani. Hali ya kila mtu ni tofauti, hali zao ni tofauti. Watu wengine wanahitajika kupatwa na vipingamizi fulani kabla ya kuweza kupitia mabadiliko makuu. Na kisha kuna watu wengine ambao hawahitaji kupatwa na vipingamizi vikubwa, lakini hugundua njia wanayopaswa kutembea na upotovu wao wenyewe katika mambo yanayotendeka kandokando yao, na wao hupata ujuzi fulani katika watu, mambo na vitu vilivyo kandokando yao—huyu ni mtu anayeendelea upesi sana kwa kulinganisha.
Hivyo mnapaswa kuzingatia nini sasa? Ikiwa mtazingatia tu kuyafanyia kazi na kujishughulisha na mambo ya ukingoni, basi maendeleo yenu yatacheleweshwa. Mnapoamini katika Mungu, maendeleo yenu binafsi maishani ni muhimu zaidi na ni ya maana zaidi. Huenda ukajiandaa tu na mafundisho ya dini, au na uwezo wa kufanya kazi, au huenda ukafanya jambo fulani kwa kutumia mbinu fulani nzuri sana, au kwa hekima; mambo haya yote ni ya kufuata, ingawa bado huwezi kuendelea bila hayo. Suala kuu la imani yako kwa Mungu ni kwamba lazima uujue ukweli kabisa, upitie ukweli na uwe na ufahamu fulani wa ukweli, na uweze kuwa na moyo mtiifu na kutosheleza mapenzi ya Mungu mbele Yake. Iwapo unaamini katika Mungu lakini kadri unavyoamini, ndivyo uhusiano wako na Mungu unaenda mrama, ndivyo unavyosonga mbali zaidi na Mungu na ndivyo unavyokuwa na sehemu nyingi ndani yako zinazopingana na ukweli, basi hilo linathibitisha kwamba imani yako haikuongozi kuendelea, kwamba Roho Mtakatifu hajakushughulikia, na kwamba umepotea na umevuka mipaka. Iwapo unaamini kwa kipindi fulani na kisha unakuwa na ufahamu fulani wa uhalisi, kujifahamu kwa kiasi fulani, na ufikirie umeelewa mambo fulani ya uhalisi, basi hili linathibitisha kwamba unafahamu mambo ya kiroho, macho yako yamefunguka na unatembea katika njia sahihi. Kuna wakongwe wengine sasa ambao wamefuata kwa miaka miwili au mitatu, ambao hata hawajababia, ambao ni waasi na wasiozuiwa na ambao hujitayarisha kupokea baraka, ambao wanajitayarisha kufurahia utajiri wao mzuri baada ya kazi kukamilishwa. Hata bado hawajababia kulingana na uzoefu wa maisha, na hawana uhusiano wenye upatanifu na Mungu hata kidogo. Ni vyema kuwa nao kwa kipindi kifupi, na watatii shingo upande, na hawatathubutu kutoa sauti ikiwa wana dhana. Lakini baada ya muda fulani kupita, mara tu wanapoanza kupinga, wanakuwa vyombo vya kuangamia. Kila mtu yuko juu ya ardhi hatari, na hili ni jambo la kuogofya. Ikiwa unamwamini Mungu na unatembea kwenye njia sahihi, basi imani yako ni muafaka na utapata baraka. Ikiwa utaenda kombo, ukitembea kwenye njia isiyo sahihi au njia isiyonyooka, usipoendelea mbele, usipoendelea mbele kwa uwezo wako wote, basi utaangamia na utapata adhabu.
Watu wana njia mbili za imani katika Mungu: Moja ni kuweza kumwamini Mungu kabisa; na nyengine ni kumuasi Mungu na kumpinga Yeye. Hizi ndizo njia mbili pekee. Haiwezekani kwamba humpingi Mungu lakini pia humtii Yeye; hili haliwezekani. Ikiwa humtii Mungu na huna ufahamu halisi, basi unaweza tu kuwa mkaidi na muasi. Huenda usionyeshe uasi kwa mambo unayosema, na huenda usimpinge Yeye waziwazi kwa silaha zilizochukuliwa, lakini bado moyo wako ni mkaidi. Au iwapo huulizwi kufanya jambo, huenda ukahisi umejawa na upendo kwa Mungu na kuhisi uko karibu sana na Mungu. Lakini mara tu unapoulizwa kufanya jambo, basi ukaidi wako, kiburi chako, kujidai kwako na mambo yako ya Shetani hufichuliwa; mara tu yanapofichuliwa, basi ukaidi wako unakuwa wa kweli. Je, si hivyo? Huenda ukaichukulia imani yako kwa Mungu kama tu "Mimi nimebarikiwa kwa kuamini katika Mungu na baadaye nitakuwa chombo cha baraka Zake. Mimi ni mshirika wa familia ya Mungu na mimi nimeinuliwa na Mungu; mimi ni mtu aliyekwezwa na Mungu. Nimebarikiwa na Mungu ni mwema kwangu." Lakini ikiwa unliona kwa njia hii, kuna maana gani? Kuna maana gani kupiga makelele kwa maneno haya matupu yanayorudiwarudiwa? Jambo kuu sasa ni iwapo unaweza kuokolewa au la, iwapo unatembea kwa njia sahihi ya maisha au la, iwapo Mungu anakusifu katika imani yako au la, iwapo Mungu anakubali kuwa kwako mshirika wa familia ya Mungu au la, na iwapo Mungu anakukubali au la; ni hayo tu ndiyo yanaweza kuchukuliwa kama kuwa makini katika imani yako kwa Mungu. Imani ya kipumbavu, kama vile "Ah, Mungu ni mwema kwangu, Mungu hunifadhili, nimebarikiwa na mimi hufanikiwa kila mahali. Tazama, Mungu ameniinua na kunifanya kuwa kiongozi katika familia Yake. Nimekuwa na bahati sana na nyota yangu imekuwa ikiinuka tangu nilipokuja katika familia ya Mungu." Kuringia tu jambo la aina hii hakuna maana. Ni tupu; lisilo na maana! Ikiwa umepewa nafasi lakini huishikilii upesi, basi ilitolewa bure, na hakutakuwa na maana hata ukipewa nafasi nyingi kiasi gani. Shikilia upesi mambo fulani ya kweli, na halisi. Baadhi ya waumini wakongwe husema: "Ah, nimebarikiwa! Mimi nimebarikiwa na mimi ni mtu aliyebarikiwa zaidi katika dunia yote, katika ulimwengu wote!" Haingekusaidia hata ungekuwa malaika; huwezi tu kusema mambo ya aina hii, ni lazima ushikilie upesi mambo ya kweli. Hasa ninyi ambao mumeamini katika Mungu kwa muda mfupi tu na mmepata uzoefu kidogo kutokana na kufanya mambo, ambao hamkupitia zile hatua za kazi hapa mwanzo, na ambao mlikuja mwisho kabisa—je, uko tayari kuwa na uhakika kabisa ili baadaye uweze kuokolewa? Je, uko tayari? Huko tayari, sivyo? Ikiwa huko tayari kuwa na uhakika kabisa kuhusu jambo hilo, basi uko katika nafasi hatari!
Ikiwa huelewi ni nini maana ya kumhudumia Mungu au nini maana ya kutii Mungu, na unaelewa kidogo sana namna ya kumwabudu Mungu au jinsi watu wanapaswa kuamini katika Mungu; iwapo hujashikilia mambo haya na huyafahamu katika moyo wako, basi utaenda mrama kwa urahisi sana na utamuasi Mungu kwa urahisi sana. Kama wale walioanguka hapa awali waliosema: "Roho Mtakatifu na atufunulie mambo haya!" Ninyi nyote sasa mnaona jambo hili kwa dhahiri. Wakati huo hawakuwa na nia yoyote ya kufanya chochote kibaya na kumuasi Mungu, na walijua kwmba Mungu alikuwa amewainua na kwamba ni lazima wafanye kazi kwa bidii. Ilhali hawakutembea kwenye njia sahihi, wakifikiria tu kwamba Mungu alikuwa amewainua, kwamba walitaka kufanya kazi kwa bidii, na kufanya kazi nzuri ya kuwa wachungaji wa wale waliokuwa chini yao kanisani; walidhani chochote kile ambacho waliokuwa juu yao waliwataka wafanye, wangefanya. Hawakuwa wameshika mambo ya utendaji na hakika walikuwa wanafanya mambo bila kutambua, wakitegemea ushupavu wao wenyewe. Walipokuwa hawatumiwi tena, walikasirika sana na kusema: "Mungu ni mwenye haki. Roho na afichue hili! Imani yangu haiko katika mwanadamu, iko katika Mungu." Hawakupanga awali kusema maneno haya, hivyo yalisemwa bila hiari? Sababu yake ilikuwa gani? Ilikuwa ni kwa sababu mwanadamu hamchi Mungu na hamfahamu Yeye. Unaona kwamba watu wengine husema mambo mengine ambayo ni ya upumbavu na ujinga, na wao husamehewa. Wao husamehewa kwa ajili ya ujinga wao na kile ambacho wajibu wao ulikuwa hakichunguzwi. Mbona hali si hiyo kwa watu wengine? Kwa sababu walisema mambo yaliyokuwa mazito sana: "Wewe ni Mungu, lakini bado sitakutii Wewe." Watu hawa ni wapinga Kristo; wao humuasi Mungu na hawakubali ukweli. Watu wengine ni wapumbavu na wajinga. Ni sawa kuonyesha upumbavu wako na ujinga mara moja au mara mbili; lakini ukikosea amri za Mungu za usimamizi au ukikosea tabia ya Mungu, basi utakuwa matatani. Tazama njia ambayo Petro alitembea. Alipata nuru kutoka kwa Roho Mtakatifu hapo mwanzo na alizungumza na Yesu, akisema: "Wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu aishiye." Mara tu Roho Mtakatifu alipokuwa amempa nuru, wakati huo alipata ujuzi fulani na moyo wake ulijazwa nuru. Hata kama wakati huo hakuwa na ufahamu wa kina, lakini alitafuta kumfahamu Mungu, na akatembea kwenye njia sahihi ya kumhudumia Mungu. Kumhudumia Mungu ni jambo la hatari zaidi, na pia ni jambo la utukufu zaidi. Kwa sababu wanadamu ni wakaidi na wapotovu, mara tu wanapopotea, wao humalizika. Watu humhudumia Mungu, sio watu wengine; kumhudumia Mungu ni jambo la hatari. Petro alitembea katika njia hiyo na alikuwa na imani hii. Na je, kuhusu Paulo? Hakukubali kwamba Yesu alikuwa Kristo. Alimuwinda bila kukoma na, baada ya kuangushwa chini, bado Paulo hakutambua kwamba Mungu alikuwa Bwana wa vitu vyote, wala vile wanadamu wanapaswa kumtii Yeye. Hakuwa na akili ya kawaida ya kufikiria, lakini kuanzia mwanzo hadi mwisho alihodhi fikira za kiburi: "Ninakupa Wewe kiasi hiki kwa hivyo unapaswa kunipa kiasi hicho; ninatumia rasilimali kiashi hiki, kwa hivyo Wewe unapaswa kunituza kiasi hicho na kunipa kiasi hicho cha mshahara." Kazi yake ilikuwa chini ya utawala wa fikira za aina hii wakati huo wote. Hivyo hakuwahi kuwa na moyo wa kumheshimu Mungu, hakuwahi kuwa na moyo wa kumcha Mungu. Angalia toni ya maneno yake: "Nimepigana vita"—Nimepigana vita Ulivyonifanya nipigane; "Nimemaliza kazi yangu"—Nimekimbia kwenye njia uliyoniambia nikimbie; "Nimeidumisha imani"—je, hukunifanya niidumishe?" Nimeidumisha, kwa hivyo taji ya utukufu haipaswi kuhifadhiwa kwa ajili yangu? Je, hakunena na toni ya aina hii? Bila shaka hangeweza kuzungumza waziwazi namna hii katika waraka. Alizungumza kitasifida na kimafumbo, lakini maneno yake yalianza kutoka kwa dhana hizi. Ni nini kilifanyika mwishowe? Yeye bado aliadhibiwa, au sivyo? Mnatakiwa kuona dhahiri vile wanadamu wanapaswa kuchagua kwenye njia ya kumhudumia Mungu, kwenye njia ya kuamini katika Mungu. Ni njia zipi za kumhudumia Mungu ni za njia za Paulo? Ni njia zipi za kuamini ni za njia ya Paulo? Ni jinsi gani njia ya kumcha Mungu ya kumhudumia Mungu kama ya Petro inaweza kutimizwa? Kuna njia ambayo viumbe wa Mungu wanapaswa kutembea ili kumwabudu Yeye; njia hiyo ni lazima ichaguliwe sawasawa na malengo yenu ni lazima yawe dhahiri. Usiwe mpumbavu, lakini tembea kwa bidii na kusimama juu ya ardhi imara, na maono yaliyo dhahiri kikamilifu. Ni hatari wewe kutembea kwenda mbele katika njia ya kipumbavu na ina hakikisha kwamba siku moja utakosea amri za usimamizi za Mungu au kuanza kunung'unika.
Je, mna hakika kuhusu asili gani au hali gani ndani ya wanadamu huwaongoza kwa urahisi sana katika uangamiaji, bila kujali ikiwa ni kiongozi au mfuasi? Je, unajua kuhusu asili ya kawaida ya wanadamu? Ukawaida wa asili ya wanadamu ni kumsaliti Mungu; kila mtu na watu wote wanaweza kumsaliti Mungu. Je, kutoamini pekee sio kumsaliti Mungu? Je, kumsaliti Mungu ni nini? Ni mambo gani yanamaanisha kumsaliti Mungu? Ni lazima ufahamu kiini cha wanadamu kimeumbwa na nini; ni lazima uelewe hili na kufahamu mzizi wa mambo hayo. Udhaifu wako wa mauti, hasira, njia mbaya, tabia mbaya au adabu mbaya—mambo haya yote ni ya juujuu. Ukiyashika tu mambo haya kwa kukaza na kiini chako kibakie kisichofumbuliwa, basi bado utatembea kwenye njia isiyonyooka na bado utamuasi Mungu. Je, sivyo? Ninyi bado kila mara tu mnababia na kukamata utondoti hafifu. Mwanadamu anaweza kumsaliti Mungu wakati wowote au mahali popote na hili ni tatizo kubwa. Labda wakati huu unaweza kumpenda Mungu kwa kiwango kikubwa, kutumia rasilimali nyingi kwa ajili ya Mungu, kuwa mwaminifu hasa; labda wakati huu unaweza kuwa wa akili hasa na kuwa na dhamiri. Lakini huenda kukaja na wakati na mahali ambapo kitu fulani kitakuongoza kumsaliti Mungu. Tuseme kwamba mtu fulani ni wa akili hasa wakati huu; Roho Mtakatifu anamshughulikia, ana uzoefu fulani wa utendaji, amebeba mzigo, yeye hutekeleza jukumu lake kwa uaminifu na ana imani thabiti sana. Basi tuseme Mungu angefanya jambo fulani la kumsikitisha, jambo alilodhani si sahihi. Dhana zingeinuka ndani yake wakati huo, mara moja angekuwa mbaya, na angepoteza shauku na kuwa ovyoovyo katika kazi yake, na angeachana na maombi, akisema, "Ni nini ambacho ninaombea? Mungu hapaswi kufanya jambo hili! Ninawezaje kuomba?" Nguvu zake zingeisha na shauku yake ya maombi ingeipotea. Hii inaitwa nini? Je, hili sio dhihirisho la usaliti? Katika wakati wowote au mahali popote, mwanadamu anaweza kumwacha Mungu, kumkana Mungu na kumshutumu Mungu—je, haya yote si usaliti? Hili ni jambo la kuogofya. Tazama, unadhani kwamba sasa huna dhana zozote na unaweza kumtii Mungu wakati mwingi, kwamba unaposhughulikiwa na kupogolewa hutamwacha Mungu. Ilhali unaweza bado kumsaliti Mungu wakati wowote au mahali popote. Ni lazima ufahamu vilivyo asili ya mwanadamu. Bila shaka, baadhi ya watu wakati mwingine watakuwa na dhamiri fulani, na hao watakuwa watu ambao asili zao ni nzuri kwa kulinganisha. Wengine watakuwa na ubinadamu wa uovu, na asili zao zitakuwa mbaya. Lakini haijalishi iwapo mtu yeyote anasema ubinadamu wako ni mzuri au mbaya, au iwapo ubora wako ni mzuri au mbaya, asili ya kawaida ni kwamba unaweza kumsaliti Mungu. Asili ya mwanadamu ni kumsaliti Mungu, hivyo watu wangeweza kumsaliti Mungu kama hawangekuwa wamepotoshwa? Bado mnafikiri sasa: "Asili za watu ambao wamepotoshwa na Shetani zitamsaliti Mungu kwa hivyo hakuna ninachoweza kufanya. Nitahitajika tu kubadilika polepole." Je, bado mnawaza kwa njia hii? Basi Niambieni, je, watu wangeweza kumsaliti Mungu ikiwa hawangekuwa wamepotoshwa? Watu wangeweza pia kumsaliti Mungu ikiwa hawangekuwa wamepotoshwa. Wanadamu walipoumbwa walipewa hiari, walikuwa wadhaifu sana, na hawakuwa na moyo ambao ungeweza kumfikia Mungu kwa kweli au uliogeuka kumwelekea Mungu kwa kweli: Mungu ni Muumba wetu na sisi ni viumbe Wake. Wanadamu hakuwa na moyo huu. Wanadamu hawakuwa na ukweli ndani yao wala chochote ambacho kingeweza kuwasaidia kumwabudu Mungu. Mungu aliwapa hiari ili kwamba wanadamu waweze kufikiria, lakini wanadamu hawakujua Mungu ni nani na hawakufahamu jinsi ya kumwabudu Mungu. Hawakuwa na kitu kama hiki ndani yao. Hata kama hungepotoshwa, bado ungeweza tu kumsaliti Mungu. Kwa nini ni hivi? Shetani hukushawishi ili umfuate yeye na kumsaliti Mungu. Wewe uliumbwa na Mungu lakini humfuati Yeye. Badala yake unamfuata Shetani. Je, wewe si msaliti basi? Wasaliti husaliti. Wewe unafahamu kwelikweli kiini hiki, au sivyo? Hivyo wanadamu wanaweza kumsaliti Mungu wakati wowote na katika mahali popote. Ni wakati tu wanadamu watakapoishi kikamilifu ndani ya ufalme wa Mungu na ndani ya nuru ya Mungu, wakati Shetani atakuwa ameangamizwa na hakuna tena ushawishi wowote, hapo tu ndipo wanadamu hawataweza tena kumsaliti Mungu. Wakati bado kuna ushawishi, wanadamu badow wanaweza kumsaliti Mungu; hivyo inasemekana kwamba wanadamu hawana thamani. Bado unafikiria: "Sasa nimepata mambo fulani. Nina mambo fulani ambayo hayamsaliti Mungu, lakini yaliyo na upatanifu na Mungu. Siwezi kufikiriwa kuwa kioo kinachong'aa, lakini angalau kama chupa ya udongo. Siwezi kufikiriwa kuwa dhahabu, lakini labda shaba nyekundu." Unajistahi mwenyewe kwa hali ya juu sana. Je, unajua mwanadamu ni kitu cha aina gani? Mwanadamu anaweza kumsaliti Mungu wakati wowote au mahali popote na hafikii hata thamani ya peni moja. Kama tu alivyosema Mungu: "Rundo la mavi ya mbwa, wakatili na mafidhuli." Watu hufikiria: "Mimi si fidhuli! Mimi si fidhuli kamwe! Kwa nini nisiweze kuelewa jambo hili? Kwa nini sijalipitia? Ikiwa sijapotoshwa, basi siwezi kumsaliti Mungu." Kuna mifano ya hili, na kuna ukweli. Ninachowaambia sasa hakikosi msingi. Mambo haya yote ni kuwaonyesha ninyi, kuwaridhisha ninyi; ni kwa njia hii pekee ndio mnaweza kufikia ufahamu wa upotovu wenu wenyewe na kutatua tatizo la usaliti. Hakutakuwa tena na usaliti wowote ndani ya wanadamu katika ufalme, wanadamu wataishi chini ya utawala wa Mungu na Shetani hatakuwa na utawala juu yao, na wanadamu wataishi huru na hawatahitaji kuwa na wasiwasi, wakidhani, "Je, naweza kumsaliti Mungu?" Hakutakuwa na haja ya kuwa na wasiwasi; haitakuwa na maana! Baadaye, inaweza kutangazwa kwamba humtakuwa na chochote ndani yenu kinachomsaliti Mungu. Lakini sasa, mambo hayajakuwa sawa, kwani kiini cha wanadamu ni kile kinachoweza kumsaliti Mungu wakati wowote na katika mahali popote. Sio kwamba utamsaliti Mungu kwa sababu ya hali fulani mbaya, au kwamba bila hali yoyote mbaya au bila mtu yeyote kukulazimisha basi hutamsaliti Mungu. Unaweza bado kumsaliti Mungu hata iwapo hakuna anayekulazimisha; hili ni tatizo la kiini potovu cha wanadamu, na ni tatizo la asili yao. Ona jinsi unavyopumua tu sasa, jinsi hujafanya chochote, hujasonga, hujafikiria chochote, na ilhali hiyo asili inayomsaliti Mungu iko ndani yako—je, hii ni sahihi? Kwa nini? Kwa sababu wanadamu wana usaliti ndani yao na Mungu hayuko ndani yao. Roho ya wanadamu na nafsi ya wanadamu havina sehemu ya Mungu ndani yao. Hivyo, unaweza kumsaliti Mungu wakati wowote au katika mahali popote. Angalia, malaika ni tofauti. Hawana tabia ya Mungu, wala hawana kiini cha Mungu. Lakini wanaweza kumtii Mungu kikamilifu kwa sababu waliumbwa na Mungu sanasana kumhudumia Yeye na wao hutumwa kila mahali; wao ni mali ya Mungu. Wanadamu, kwa hali yoyote, waliumbwa kuishi duniani na hawakuumbwa na akili ya kumwabudu Mungu. Wanadamu wana uwezo wa kumsaliti Mungu na ni vyombo vinavyoweza kutumiwa au kupiganiwa na mtu yeyote. Wao ni wa thamani duni! Kwamba wanadamu wana asili hii imefichuliwa ili watu waweze kupata ufahamu wa jambo hili na wao wenyewe. Kutokana na hali hii, watu wanaweza kuanza kubadilika, na kuanzia hapa wanaweza kutafuta njia ya utendaji. Kufahamu ni katika mambo gani unaweza kumsaliti Mungu na ni kasoro gani unahitaji kurekebisha ili usimsaliti Mungu, utafikia hatua ambapo hutamsaliti tena Mungu katika hali nyingi na utaepuka kumsaliti Yeye katika nyingi ya hali hizo. Iwapo baadaye utamsaliti Mungu au la haitakuwa juu yako. Safari yako ya maisha itafikia mwisho wake, na itafikia wakati huo ambapo kazi ya Mungu itafanyika, lakini iwapo baadaye utamsaliti Mungu au la hautakuwa wajibu wako. Kwa nini hilo lilisemwa wakati huu tu? Kabla ya wanadamu kupotoshwa na Shetani, alikuja na akawashawishi wanadamu, na hapo basi waliweza kumsaliti Mungu. Baada ya Shetani kuangamizwa, je, wanadamu wakati huo hawatamsaliti Mungu tena? Wakati huo haujafika bado. Kwa hivyo wanadamu bado wana tabia potovu ya kishetani ndani yao, na wanaweza kumsaliti Mungu wakati wowote na mahali popote. Mara tu uzoefu wako wa maisha unapofikia hatua fulani, vitu vingi ndani yako vinavyomsaliti Mungu vitatupiliwa mbali. Wewe wakati huo utakuwa na vitu vingi vizuri, utaweza kutekeleza kujizuia na utaweza kujitawala mwenyewe. Hutakuwa na uwezo wa kumsaliti Mungu tena kwa wingi wa wakati huo, na baada ya Shetani kuangamia utapitia mabadiliko kamili. Hatua hii ya kazi ni kutatua sasa usaliti wa wanadamu na kutatua ukaidi wa wanadamu. Baadaye watu hawatamsaliti Mungu kwani Shetani atakuwa ameangamizwa, na hili haliwahusu wanadamu hata kidogo. Je, unafahamu? Kufahamu asili ya wanadamu ya kusaliti kunaanzia hapa: Ni mambo gani ni ya asili inayomsaliti Mungu, ni mambo gani ni sehemu ya kuonyesha usaliti, jinsi wanadamu wanapaswa kuingia na jinsi wanapaswa kufahamu. Kiini hiki cha wanadamu bado kiko ndani yao, wao bado wanaweza kumsaliti Mungu wakati wowote au mahali popote, na bado wanaweza kufanya mambo ambayo hawafikirii kuwa ni ya kumsaliti Mungu. Wanadamu wanaweza kumsaliti Mungu wakati wowote na mahali popote, hiyo ni kusema kwamba wanadamu hawana hali ya kujitawala, kwani Shetani amewamiliki. Unaweza bado kumsaliti Mungu hata kama hujapotoshwa, achilia mbali wakati huu ambapo umejazwa na tabia potovu ya kishetani. Wewe unaweza hata zaidi kumsaliti Mungu wakati wowote na mahali popote. Sasa unahitajika kutupilia mbali tabia potovu, ili kwamba hayo mambo yaliyo ndani yako yanayomsaliti Mungu yatapungua zaidi na zaidi, na utakuwa na nafasi nyingi zaidi mbele ya Mungu kumruhusu Yeye kukukamilisha na kukukubali. Ikiwa utapata uzoefu mwingi kuhusu wokovu wa Mungu katika mambo yote, utakamilishwa wakati wa hatua hii. Hivyo, ikiwa kitu fulani cha Shetani, au pepo mchafu, atakuja kukudanganya na kukusumbua, unaweza basi kutumia utambuzi wako, au sivyo? Kwa njia hii, tabia yako ya usaliti itapungua, na hiki ni kitu ambacho kitahemshwa ndani yako katika siku za baadaye. Wanadamu walipoumbwa kwa mara ya kwanza, hawakuwa na akili hii, wala hawakufahamu ibada ya Mungu, jinsi ya kumtii Mungu au usaliti wa Mungu ni nini. Shetani alikuja kuwashawishi wanadamu na wakamfuata, walimsaliti Mungu, na wakawa wasaliti kwa Mungu. Hii ni kwa sababu wanadamu hawakuwa na uwezo wa kutambua mema na mabaya, hawakuwa na akili ya kumwabudu Mungu, wala hawakuwa na ufahamu wowote kwamba Mungu alikuwa Muumba au ufahamu wowote wa jinsi wanadamu wanapaswa kumwabudu Mungu. Katika siku za baadaye, Mungu kuwafinyanga wanadamu sasa ni kufanya kweli hizi (ufahamu wa kiini cha Mungu na tabia Yake...) ndani ya wanadamu, ili kwamba waweze kufahamu hali hizi na wawe kiwango fulani cha kujitawala na hali hizi. Yaani, kadiri uzoefu wako unavyokuwa wa kina, ndivyo utakavyomfahamu Mungu na ndivyo utapunguza kuwa na mambo yanayomsaliti Mungu. Kadiri unavyokuwa na mambo yanayopatana na Mungu, ndivyo utakavyoweza kumshinda Shetani, kadiri unavyokuwa na hali ya kujitawala, ndivyo utakavyoweza kuishi kwa kudhihirisha maisha ya kweli. Baadhi ya watu huuliza: "Wanadamu wana kiini cha upotovu ndani yao na wanaweza kumsaliti Mungu wakati wowote na mahali popote; ni vipi ambavyo Mungu anaweza kusema bado Amewafanya wanadamu kuwa wakamilifu?" Kufanywa mkamilifu ni kumfahamu Mungu kupitia kwa uzoefu, na pia ni kufahamu asili yao wenyewe, kujua jinsi ya kumwabudu Mungu na kumtii Mungu, kuweza kutambua kati ya kazi ya Mungu na kazi ya wanadamu, na kutambua tofauti kati ya kazi ya Roho Mtakatifu na kazi ya pepo wachafu kupitia kwa uzoefu. Pia ni kuwa na ufahamu wa jinsi Shetani ibilisi humuasi Mungu, jinsi wanadamu humuasi Mungu, uumbaji ni nini na Muumba ni nani. Ninyi mnafahamu mambo haya, au sivyo? Haya yote ni mambo waliyopewa wanadamu kupitia kwa kazi ya Mungu katika siku za baadaye. Hivyo, wale watakaofanywa wakamilifu mwishowe watabeba uzito zaidi na watakuwa na thamani zaidi kuliko wale wa hapo mwanzo ambao hawakuwa wamepitia upotovu. Kwa sababu kuna mambo mengine ambayo yameongezwa ndani ya wanadamu na mambo mengine ambayoyamehemshwa ndani yao, watu wanaofanywa wakamilifu mwishowe watakuwa na hali ya kujitwala kuliko Adamu na Hawa wa wakati huo, na watafahamu ukweli zaidi wa jinsi ya kumwabudu Mungu na kumtii Yeye; watafahamu zaidi jinsi ya kuwa binadamu. Adamu na Hawa hawakujua mambo haya na nyoka alikuja kuwashawishi na wakala tunda kutoka kwa mti wa kufahamu mema na mabaya. Mwishowe walijua aibu, na wakaendelea kutojua jinsi ya kumwabudu Mungu, na wakawa wapotovu zaidi na zaidi, hadi wakati huu. Hili ni jambo la kina kabisa, na hakuna yeyote katika ubinadamu potovu anayeweza kulifahamu kabisa. Wanadamu bado wanaweza kumsaliti Mungu wakati wowote na mahali popote kwa sababu ya silika za mwili wao. Ilhali, mwishowe, Mungu atawakamilisha wanadamu na kuwaingiza katika hatua inayofuata; hili ni jambo ambalo watu huona ni vigumu kulifahamu.
Kwa nini wanadamu wanahitajika kumfahamu Mungu? Ikiwa wanadamu hawatamfahamu Mungu au hawatafahamu hali hii ya ukweli, basi watatumiwa kwa urahisi sana na kudanganywa na pepo wachafu. Mara tu wanapofahamu ukweli, basi haitakuwa rahisi kwao kudanganywa na kutumiwa na pepo wachafu. Lakini ikiwa, baada ya wewe kupata ufahamu huu, na ukaendelea kufanya jambo unalojua kwamba ni kukosea amri za usimamizi za Mungu au linafanywa kwa kuasi Mungu, basi hutaweza kukombolewa. Wewe uko katika hali gani wakati huu? Maadamu sasa mna tumaini moja, bila kujali iwapo Mungu anakumbuka mambo ya zamani au la, mnapaswa kudumisha fikira hizi: Ni lazima nitafute badiliko katika tabia yangu, nitafute kumfahamu Mungu, kutodanganywa na Shetani tena na kutofanya chochote kinacholeta aibu kwa jina la Mungu. Ni sehemu gani kuu huamua iwapo mtu sasa ana thamani yoyote, iwapo ataokolewa au la na iwapo ana tumaini yoyote au la? Nazo ni, baada ya wewe kusikia mahubiri, iwapo unaweza kupokea ukweli au la, iwapo unaweza kutekeleza ukweli huo au la na iwapo unaweza kubadilika au la. Hizi ni sehemu muhimu. Ikiwa utahisi tu majuto, ikiwa utaenda tu kufanya mambo na kuendelea kufikiria kwa njia hiyo hiyo ya zamani, na ukose kuwa na ufahamu wowote kabisa kuhusu jambo hili lakini badala yake uwe mbaya zaidi na zaidi, basi utakosa tumaini na unapaswa kutangazwa kuwa asiye na thamani. Kadiri unavyomfahamu Mungu, na kadiri unavyojifahamu, basi ndivyo utakavyoweza kujitawala mwenyewe. Kadiri unavyoweza kupenya katika asili yako mwenyewe kwa ufahamu, ndivyo utakavyoweza kujitawala mwenyewe. Baada ya wewe kujumlisha uzoefu wako, hutawahi tena kushindwa katika jambo hili. Kwa kweli kabisa, kila mtu ana madoa fulani juu yake ambayo hayajachunguzwa tu. Kila mtu anayo, wengine wana madogo, wengine wana makubwa; wengine huongea waziwazi, na wengine huficha nia zao na kufanya kazi kwa siri. Kila mtu anayo; Baadhi ya watu hufanya mambo ambayo watu wengine wanajua kuyahusu na baadhi ya watu hufanya mambo ambayo watu wengine hawajui kuyahusu. Kuna mawaa juu ya kila mtu na yote yanafichua tabia fulani za upotovu, kama vile kiburi au majivuno, au wao hufanya dhambi fulani, au makosa fulani au kupotoka katika kazi zao, au wanaonyesha kiasi kidogo cha ukaidi. Haya yote ni mambo ya kusamehewa kwani ni mambo ambayo mtu yeyote aliyepotoka hawezi kuepuka. Ilhali yanapaswa kuepukika mara tu unapofahamu ukweli. Na hakutakuwa tena na haja ya wewe kusumbuliwa mara kwa mara na mambo yaliyofanyika katika siku za zamani. Badala yake, inafaa kuhofiwa kwamba bado hutabadilika hata baada ya kupata kufahamu, eti utajua kwamba si sahihi kufanya kitu na bado uendelee kukifanya, na kwamba utaendelea kufanya kitu fulani hata baada ya kuambiwa kwamba ni kibaya. Watu hawa hawawezi kukombolewa.

Ijumaa, 14 Juni 2019

Unafaa Utofautishe Vipi Kati ya Kazi ya Roho Mtakatifu na Kazi ya Pepo Wabaya?

2. Unafaa Utofautishe Vipi Kati ya Kazi ya Roho Mtakatifu na Kazi ya Pepo Wabaya?

Maneno Husika ya Mungu:
Kazi ya Roho Mtakatifu ni kuhusu kuwasaidia watu kupata faida; ni kuwaadilisha watu; hakuna kazi ambayo haiwanufaishi watu. Haijalishi kama ukweli ni wa kina au usio wa kina, na haijalishi tabia ya wale wanaopokea ukweli huo ilivyo, chochote ambacho Roho Mtakatifu Anafanya, yote hayo huwanufaisha watu.
kutoka kwa "Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Mwenyezi Mungu alisema, Kazi ya Roho Mtakatifu ni aina ya mwongozo wa kimatendo na kupata nuru kwa hali nzuri. Haiwaruhusu watu kuwa baridi. Huwaletea faraja, huwapa imani na uamuzi na kuwawezesha kufuatilia kufanywa kamili na Mungu. Wakati Roho Mtakatifu hufanya kazi, watu wanaweza kuingia kwa vitendo; wao si baridi wala hawalazimishwi, lakini ni wa kimatendo. Wakati Roho Mtakatifu hufanya kazi, watu wana faraja na wenye radhi, na wako tayari kutii, na wana furaha kujinyenyekeza, na hata ingawa wana maumivu na ni dhaifu ndani, wana uamuzi wa kushirikiana, wanateseka kwa furaha, wanaweza kutii, na hawajatiwa doa na mapenzi ya mwanadamu, hawajatiwa doa na fikira ya mwanadamu, na hakika hawajatiwa doa na tamaa na motisha za mwanadamu. Wakati watu wanapitia kazi ya Roho Mtakatifu, ndani yao ni watakatifu hasa. Wale ambao wanamiliki kazi ya Roho Mtakatifu huishi kwa kudhihirisha upendo wa Mungu, upendo wa kaka na dada zao, na kufurahia vitu ambavyo Mungu hufurahia na kuchukia vitu ambavyo Mungu huchukia. Watu ambao wanaguswa na kazi ya Roho Mtakatifu wana ubinadamu wa kawaida, na wanamiliki ubinadamu na daima hufuatilia ukweli. Wakati Roho Mtakatifu hufanya kazi ndani ya watu, hali zao huwa nzuri zaidi na zaidi, na ubinadamu wao unakuwa wa kawaida zaidi na zaidi, na ingawa ushirikiano wao mwingine unaweza kuwa mpumbavu, motisha zao ziko sahihi, kuingia kwao ni kwa hali nzuri, hawajaribu kukatiza, na hakuna nia mbaya ndani yao. Kazi ya Roho Mtakatifu ni ya kawaida na ya kweli, Roho Mtakatifu hufanya kazi kwa mwanadamu kulingana na amri za maisha ya kawaida ya mwanadamu, na Yeye huwapa nuru na kuongoza watu kulingana na ufuatiliaji halisi wa watu wa kawaida. Wakati Roho Mtakatifu hufanya kazi kwa watu, Yeye huwaongoza na kuwapa nuru kulingana na mahitaji ya watu wa kawaida, Anawakimu kwa msingi wa mahitaji yao, na Yeye huwaongoza na kuwapa nuru kwa hali nzuri kwa msingi wa kile ambacho wanakosa, na kwa upungufu wao; wakati Roho Mtakatifu hufanya kazi, kazi hii inalingana na amri za maisha ya kawaida ya mwanadamu, na ni katika maisha halisi pekee ndio watu wanaweza kuona kazi ya Roho Mtakatifu. Iwapo, katika maisha yao ya kila siku, watu wako katika hali nzuri na wana maisha ya kawaida ya kiroho, basi wanamiliki kazi ya Roho Mtakatifu. Katika hali kama hiyo, wakati wanakula na kunywa maneno ya Mungu wana imani, wakati wanaomba wanatiwa moyo, wakati kitu kinawafanyikia wao si baridi, na wakati kinawafanyikia wanaweza kuona masomo ambayo Mungu anawahitaji kujifunza, na hawako baridi, ama dhaifu, na ingawa wana ugumu wa kweli, wako tayari kukubali mipango yote ya Mungu.
…………
Ni kazi ipi hutoka kwa Shetani? Katika kazi inayotoka kwa Shetani, maono ndani ya watu si yakini na ni dhahania, na hawana ubinadamu wa kawaida, motisha za vitendo vyao si sahihi, na ingawa wanataka kumpenda Mungu, daima kuna lawama ndani yao, na lawama hizi na fikira daima zinaingilia katindani yao, zikizuia kukua kwa maisha yao, na kuwasitisha kuwa na hali za kawaida mbele ya Mungu. Ambayo ni kusema, punde tu kuna kazi ya Shetani ndani ya watu, mioyo yao haiwezi kuwa kwa amani mbele ya Mungu, na hawajui cha kufanya, kuona mkutano kunawafanya kutaka kuhepa, na hawawezi kufumba macho yao wakati wengine wanaomba. Kazi ya roho waovu huharibu uhusiano wa kawaida kati ya mwanadamu na Mungu, na huvuruga maono ya awali ya watu na njia ambayo maisha yao yameingia, katika mioyo yao hawawezi kamwe kumkaribia Mungu, daima mambo hufanyika ambayo huwasababishia vurugu na kuwatia pingu, na mioyo yao haiwezi kupata amani, kuacha upendo wao wa Mungu bila nguvu, na kuwafanya kusononeka. Hayo ndiyo maonyesho ya kazi ya Shetani. Kazi ya Shetani inadhihirishwa katika yafuatayo: kutoweza kushikilia msimamo na kuwa na ushuhuda, kukusababisha kuwa mtu ambaye ana makosa mbele ya Mungu, na ambaye hana uaminifu kwa Mungu. Kwa kuingilia kwa Shetani, unapoteza upendo na uaminifu kwa Mungu ndani yako, unaondolewa uhusiano wa kawaida na Mungu, hufuatilii ukweli, ama kujiendeleza, unarudi nyuma, na kuwa baridi, unajipendeza, unaachia uenezaji wa dhambi, na huchukii dhambi; zaidi ya hayo, kuingilia kwa Shetani kunakufanya mpotovu, kunasababisha mguso wa Mungu kutoweka ndani yako, na kunakufanya kulalamika kuhusu Mungu na kumpinga Yeye, kukufanya uwe na shaka na Mungu, na hata kuna hatari ya wewe kumwacha Mungu. Hii yote ni kazi ya Shetani.
kutoka kwa "Kazi ya Roho Mtakatifu na Kazi ya Shetani" katika Neno Laonekana katika Mwili
Ikiwa ni kazi ya Roho Mtakatifu, mwanadamu anakuwa wa kawaida kabisa, na ubinadamu wake unakuwa wa kawaida kabisa. Mwanadamu ana maarifa mengi ya tabia yake, ambayo yameharibiwa na Shetani, na asili ya mwanadamu, na ana shauku kubwa ya kuuelewa ukweli. Ni sawa na, kusema, maisha ya mwanadamu yanakuwa na kukua, na Atabia ya upotovu ya mwanadamu inakuwa na uwezo wa mabadiliko zaidi na zaidi—yote hiyo ni maana ya Mungu kuwa maishi ya mwanadamu. Kama njia haiwezi kufunua vitu hivyo ambavyo ni asili ya mwanadamu, haiwezi kubadilisha atabia ya mwanadamu, na, zaidi ya hayo, hauwezi kumleta mbele ya Mungu au kumpa uelewa wa kweli juu ya Mungu, na hata kufanya ubinadamu wake kuwa duni zaidi na hisia zake kuwa si za kawaida zaidi, basi njia hii itakuwa si njia ya kweli, na inaweza kuwa ni kazi ya roho mchafu, au njia ya zamani. Kwa ufupi, haiwezi kuwa kazi ya sasa ya Roho Mtakatifu.
kutoka kwa "Ni Wale tu Wanaomjua Mungu na Kazi Yake ndio Wanaoweza Kumridhisha Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Mambo yanayotokana na Mungu hukusababisha kuwa wazi zaidi kuhusu maono, na hukusababisha kusogea karibu na karibu zaidi na Mungu, ukishiriki upendo na ndugu kwa bidii; unakuwa na uwezo wa kutilia maanani mzigo wa Mungu, na moyo wako umpendao Mungu haupungui; kuna njia mbele yako kuitembea. Mambo ambayo hutokana na Shetani hukusababisha kupoteza maono na vyote ulivyokuwa navyo awali vimetoweka; unajitenga na Mungu, huna upendo kwa ndugu nawe una moyo wa chuki. Unakuwa mwenye kukata tamaa, hutaki tena kuishi maisha ya kanisa, na moyo wako umpendao Mungu hauko tena. Hii ni kazi ya Shetani na pia ni matokeo ambayo yameletwa na kazi ya roho mbaya.
kutoka kwa Matamshi na Ushuhuda wa Kristo Mwanzoni
Wakati Roho Mtakatifu hufanya kazi ili kuwapa watu nuru, Yeye kwa ujumla kuwapa ufahamu wa kazi ya Mungu, na ya kuingia kwao ya kweli na hali ya ukweli, na pia Huwapa azimio, huwaruhusu kuelewa kusudi la hamu la Mungu na mahitaji yake kwa ajili ya mtu leo, Huwapa azimio la kufungua njia zote. Hata wakati ambapo watu wanapitia umwagaji damu na sadaka ni lazima watende kwa ajili ya Mungu, na hata kama wanakumbana na mateso na dhiki, lazima bado wampende Mungu, na wasiwe na majuto, na lazima wawe shahidi kwa Mungu. Azimio la aina hii ni misisimko ya Roho Mtakatifu, na kazi ya Roho Mtakatifu—lakini jua kwamba hujamilikiwa na misismko kama hii kila wakati.
kutoka kwa "Utendaji (1)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Watu wengine husema kwamba Roho Mtakatifu anafanya kazi ndani yao nyakati zote. Hili haliwezekani. Ikiwa wangesema kwamba Roho Mtakatifu yuko nao kila mara, hilo lingekuwa la kweli. Ikiwa wangesema kwamba fikira na hisi zao ni za kawaida nyakati zote, hilo pia lingekuwa la kweli, na lingeonyesha kwamba Roho Mtakatifu yuko nao. Ikiwa unasema kwamba Roho Mtakatifu anafanya kazi ndani yako kila mara, kwamba unapata nuru kutoka kwa Mungu na kuguswa na Roho Mtakatifu kila wakati, na unapata ufahamu mpya kila wakati, basi hili si la kawaida. Ni la rohoni kabisa! Bila tashwishi yoyote, watu hao ni pepo wabaya! Hata wakati ambapo Roho wa Mungu huja ndani ya mwili, kuna nyakati ambapo lazima Apumzike, na lazima Ale—sembuse wewe. Wale ambao wamemilikiwa na pepo wabaya huonekana kutokuwa na udhaifu wa mwili. Wanaweza kutelekeza na kuacha kila kitu, wao ni wasiohemkwa, wenye uwezo wa kustahimili mateso, wao hawahisi uchovu hata kidogo sana, kana kwamba wamevuka mipaka ya mwili. Je, hili silo la rohoni kabisa? Kazi ya pepo mwovu ni ya rohoni, na mambo haya ni yasiyofikiwa na mwanadamu. Wale wasioweza kutofautisha huwa na wivu wanapoona watu kama hao, na husema kwamba imani yao katika Mungu ni thabiti sana, na nzuri sana, na kwamba wao huwa si wadhaifu kamwe. Kwa kweli, hili ni dhihirisho la kazi ya pepo mwovu. Hiyo ni kwa sababu watu wenye hali ya kawaida huwa na udhaifu wa binadamu usioepukika; hii ni hali ya kawaida ya wale walio na kuwepo kwa Roho Mtakatifu.
kutoka kwa "Utendaji (4)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Wanaweza kuzungumza kutoka ndani mwako au ndani ya sikio lako, au la sivyo wanaweza kuyachanganya mawazo na akili yako, wanazuia kuguswa kwa Roho Mtakatifu ili usiweze kuuhisi, na baada ya hapo wanaanza kukuingilia, kuzifanya fikira zako ziwe zilizochanganyikiwa na akilia yako iwe iliyovurugika, na kukufanya usiyekuwa na utulivu na usiye thabiti. Hivyo ndivyo ilivyo kazi ya roho wabaya.
Wanaweza kuzungumza kutoka ndani mwako au ndani ya sikio lako, au la sivyo wanaweza kuyachanganya mawazo na akili yako, wanazuia kuguswa kwa Roho Mtakatifu ili usiweze kuuhisi, na baada ya hapo wanaanza kukuingilia, kuzifanya fikira zako ziwe zilizochanganyikiwa na akilia yako iwe iliyovurugika, na kukufanya usiyekuwa na utulivu na usiye thabiti. Hivyo ndivyo ilivyo kazi ya roho wabaya.
kutoka kwa "Maana ya Mungu Kuupitia Uchungu wa Dunia" katika Neno Laonekana katika Mwili
Unaweza kuhisi roho yako mwenyewe? Unaweza kugusa roho yako? Unaweza kuhisi roho yako inafanya nini? Hujui, siyo? Ikiwa unaweza kuhisi na kugusa vitu fulani kama hiki, basi ni roho nyingine ndani yako inafanya kitu kwa nguvu—ikidhibiti vitendo na maneno yako. Ni kitu kisichohusiana na wewe, kisicho cha wewe. Wale wenye roho ovu wana uzoefu wa kina na hili.
kutoka kwa "Jinsi ya kuelewa Umoja wa Mwili wa Mungu na Roho" katika Neno Laonekana katika Mwili
Leo kunao baadhi ya pepo wabaya wanaofanya kazi kupitia kwa mambo yasiyo ya ulimwenguni humu ili kumpotosha mwanadamu; hilo si chochote bali ni uigaji kwa upande wao, kumpotosha mwanadamu kupitia kwa kazi ambayo kwa sasa haifanywi na Roho Mtakatifu. Pepo wengi wabaya huiga ufanyaji wa miujiza na uponyaji wa magonjwa; si chochote ila kazi ya pepo wabaya, kwani Roho Mtakatifu hafanyi tena kazi kama hiyo leo. Wale wote wanaokuja baadaye na wanaoiga kazi ya Roho Mtakatifu—ni pepo wabaya.
kutoka kwa "Fumbo la Kupata Mwili (1)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Ushirika wa Mtu:
Kazi ya Roho Mtakatifu huwaruhusu watu kuuelewa ukweli, huwaruhusu kujua kiini potovu cha Shetani, na huwapa maarifa ya kweli kuhusu kile Mungu anacho na Alicho. Athari zake zote ni nzuri kwa ujumla. Leo, tunajua ukweli ni nini, kwamba ukweli unatoka kwa Mungu, kwamba mambo mazuri yanatoka kwa Mungu, kile kinachofaa kumilikiwa na watu wenye ubinadamu wa kawaida, kile ambacho ni mapenzi ya Mungu, na kile ambacho ni maisha ya kweli. Mambo haya yote ni mazuri, na uhalisi wa mambo mazuri ni ukweli. Hivi ndivyo athari ya kazi ya Mungu ilivyo, na tunaielewa tu kutokana na kupata nuru na uangazaji wa Roho Mtakatifu. Kazi ya pepo wabaya haiwezi kuwapa watu maarifa ya mambo mazuri. Unafaa kuwa wazi na kujua kwamba watu ambao pepo wabaya hufanya kazi ndani yao hawaelewi wala kuufahamu ukweli wowote. Kazi ya pepo wabaya inaweza tu kuwafanya watu kuwa waovu zaidi na zaidi, inaweza kuleta tu giza zaidi na zaidi ndani ya mioyo yao, kuzifanya tabia zao kuwa potovu zaidi na zaidi, na hali yao kuzoroteka zaidi na zaidi, na hatimaye kuishia katika kuteseka milele na kuangamia. Kazi ya Roho Mtakatifu huwafanya watu kuwa wa kawaida zaidi na zaidi, huwapa ufahamu mkubwa zaidi wa ukweli na siku zote huwapa imani kubwa zaidi kwa Mungu, na wanaweza kumtii Mungu zaidi na zaidi. Hatimaye, huwaruhusu kumjua kabisa Mungu na kumwabudu Mungu. Hii ndiyo athari ya kazi ya Roho Mtakatifu, na ni kinyume kabisa cha kazi ya pepo wabaya.
kutoka kwa "Kujua Kazi ya Roho Mtakatifu Kuna Umuhimu Mkubwa kwa Wokovu wa Mwanadamu" katika Mahubiri na Ushirika juu ya Kuingia Katika Maisha (II)
Hapa chini, hebu tuangalie baadhi ya utofauti mwingine waziwazi kati ya kazi mbalimbali za pepo wabaya na kazi ya Roho Mtakatifu, na namna ambavyo zinaonyeshwa kwa njia mahususi. Roho Mtakatifu huwachagua watu wanaofuatilia ukweli, na walio na dhamiri na mwelekeo, na wanaomiliki uadilifu. Hawa ndio aina ya watu ambao Roho Mtakatifu hufanya kazi ndani yao. Pepo wabaya huchagua watu ambao ni wajanja na wa kipuuzi, wasiopenda ukweli, na wasio na dhamiri wala mwelekeo. Watu kama hao ndio pepo wabaya hufanya kazi ndani yao. Ni nini tunachoona tunapolinganisha wale waliochaguliwa kwa kazi ya Roho Mtakatifu, na wale waliochaguliwa kwa kazi ile ya pepo wabaya? Tunaweza kuona kwamba Mungu ni mtakatifu, na mwenye haki, kwamba wale wanaochaguliwa na Mungu huutafuta ukweli, na wanayo dhamiri na mwelekeo, kwamba wanao uadilifu na wanapenda kile ambacho ni haki. Wale wanaochaguliwa na pepo wabaya ni wajanja, ni wachoyo na wenye dharau, hawaupendi ukweli, hawana dhamiri na mwelekeo, na hawautafuti ukweli. Pepo wabaya huchagua tu mambo mabaya na wale watu ambao si wa kweli, ambapo tunaona ya kwamba pepo wabaya wanapenda uovu na giza, kwamba wanawakimbia wale wanaoutafuta ukweli, na ni wepesi wa kuwamiliki wale ambao wako kombo na ni wajanja, wale ambao wanavutiwa na udhalimu, na wanaorogwa kwa urahisi. Wale ambao pepo wabaya huchagua kufanyia kazi ndani yao hawawezi kuokolewa, na wanaondolewa na Mungu. Ni lini, na ni katika mazingira gani, ndipo pepo wabaya hufanya kazi? Wao hufanya kazi wakati watu wamesonga mbali na Mungu na kuasi dhidi ya Mungu. Kazi ya pepo wabaya huwaroga watu, na hufanya hivyo kwa kuchukua fursa ile wanapotenda dhambi. Wakati watu wako katika hali yao dhaifu zaidi, hasa wanapokuwa katika maumivu makuu ndani ya mioyo yao, wakati wanapohisi vibaya na wakiwa wamechanganyikiwa, pepo mbaya huchukua fursa hii kujiingiza ndani polepole ili kuwaroga na kuwapotosha, kuleta kutoelewana kati yao na Mungu. Kunao wakati wa kazi ya Roho Mtakatifu: Wakati watu wanapomwita Mungu, wakati mioyo yao inapomgeukia Mungu, wanapomhitaji Mungu, wanapotubu kwa Mungu, na wanapoutafuta ukweli, basi ndipo Roho Mtakatifu huanza kufanya kazi ndani yao. Tazama namna ambavyo kila dhana ya kazi ya Roho Mtakatifu ilivyo ili kumwokoa mwanadamu, namna Anavyotafuta fursa za kumwokoa mwanadamu, ilhali pepo wabaya hutafuta fursa za kuwapotosha na kuwalaghai watu. Pepo wabaya wanayo dharau na ni waovu, ni wenye kudhuru kwa siri na wabaya, kila kitu wanachofanya kinalenga katika kumpotosha mwanadamu, na kumdhuru mwanadamu, na kumteketeza yeye. Wakati watu wanapohitaji msaada, wanapomtafuta Mungu kwa dharura, wanapohitaji wokovu wa Mungu, na wanapotaka kusonga karibu na Mungu ndani ya mioyo yao, Roho Mtakatifu hujitokeza kwao na kufanya kazi ya wokovu. Mungu ni upendo, na pepo wabaya ni chuki—hili liko wazi kwako, sivyo? Kile tu ambacho pepo wabaya hufanya ni ili kuwezesha kumteketeza na kumpotosha mwanadamu, na kile tu ambacho Roho Mtakatifu hufanya ni kwa upendo na wokovu wa mwanadamu. Athari ya kazi ya Roho Mtakatifu ni kuwatakasa watu, kuwaokoa dhidi ya kupotoka kwao, kuwaruhusu kujijua na kumjua Shetani, kuweza kuasi dhidi ya Shetani, kuweza kuufuatilia ukweli, na hatimaye kuishi kwa kudhihirisha mfanano wa mwanadamu. Pepo wabaya hupotosha, hutia najisi, na kuwafunga watu, huwaweka ndani zaidi ya dhambi, na kuwasababishia maumivu makubwa zaidi katika maisha yao, na hivyo wakati pepo wabaya wanapofanya kazi ndani ya watu, watu hao wamo hatarini; hatimaye, wanateketezwa na Shetani, jambo ambalo ni matokeo ya kazi ya pepo wabaya. Athari ya kazi ya Roho Mtakatifu ni kuweza hatimaye kuwaokoa watu, kuwafanya kuishi kwa kudhihirisha maisha halisi, kuwa huru na kukombolewa kabisa, na kupokea baraka za Mungu. Tazama: Pepo wabaya humweka mwanadamu katika giza, humpeleka kwenye shimo la kuzimu; Roho Mtakatifu humchukua mwanadamu kutoka kwenye giza, na kumpeleka kwenye mwangaza, na hadi kwenye uhuru. Kazi ya Roho Mtakatifu huwapa watu nuru na kuwaongoza watu, Huwapa fursa mbalimbali, na wanapokuwa wanyonge na dhambi Yeye huwapa faraja. Huwaruhusu watu kujijua, huwaruhusu kuufuatilia ukweli, na Halazimishi watu kufanya mambo, lakini Huwaacha kujichagulia njia yao wao wenyewe, na hatimaye Huwapeleka kwenye mwangaza. Pepo wabaya huwalazimisha watu kufanya mambo na kuwaamrisha hapa na pale. Kila kitu wanachosema ni uongo na kinawaroga watu, kuwadanganya na kuwafunga; pepo wabaya hawawapatii watu uhuru, hawawaruhusu kuchagua, huwalazimisha kufuata barabara ya maangamio, na hatimaye kuwaingiza ndani ya dhambi zaidi na zaidi, na kuwasababishia kifo. Hebu tazama watu hao waovu, wale watu waovu: Wanawakokota wengine hadi kwenye uharibifu, wanawavuta kwenye uhalifu, na kuwavuta kwa ghafla kwenye maeneo ya kuchezea kamari. Hatimaye, baada ya wao kuziharibu familia za watu na kuwafarakanisha na dunia, wanafurahi, kazi yao imekamilika, na wametimiza nia yao. Je, hawa ni mashetani, sivyo? Ilhali wale ambao ni wazuri kwa kweli na wanamcha Mungu wanawaongoza watu kuwa karibu zaidi na Mungu, na kuwaongoza katika imani ya Mungu, katika ufahamu wa ukweli, katika kuyafuatilia maisha halisi, na hatimaye kuwafanya kuishi kwa kudhihirisha mfanano wa mwanadamu. Utofautishi kati ya mambo haya mazuri na mabaya ni wazi vipi! Katika kulinganisha kanuni, mbinu, na athari ya mwisho ya kazi ya Roho Mtakatifu na ile ya pepo wabaya, tunaona kwamba Mungu humwokoa mwanadamu, humpenda mwanadamu, na humpa mwanadamu ukweli, kwamba Yeye humchukua mwanadamu na kumweka kwenye mwangaza, na hatimaye humruhusu mwanadamu kubarikiwa na kuwa mtu halisi na kuishi kwa kudhihirisha maisha ya ukweli. Shetani humpotosha mwanadamu, humfunga mwanadamu, hujaribu kumteketeza mwanadamu, na hatimaye humwongoza mwanadamu katika kuteseka milele na kuangamia. Kupitia kujua kazi ya Roho Mtakatifu, tunaweza kutambua kazi ya pepo wabaya na kuujua ukweli wa upotoshwaji wa mwanadamu na Shetani. Leo, katika imani yetu kwa Mungu tunafahamu kile tunachofaa kufuatilia, kwamba Mungu ni mzuri, na kwamba tunafaa kumjua Mungu, kumwabudu Mungu, na kumtii Mungu. Tunayo malengo katika maisha yetu, na tunalo tumaini la wokovu. Hizi ndizo athari za kazi ya Roho Mtakatifu. Leo, kama ungeulizwa kusema Shetani ni nini, ungeweza kusema? Tabia potovu ya Shetani inaonyeshwa kwa njia gani? Tabia ya Shetani ni yenye maovu, yenye kudhuru kwa siri, yenye makosa, mbovu, yenye dharau, yenye kushikilia maovu yote, na yenye sumu kabisa. Kila kitu ambacho Mungu anacho na Alicho ni nini? Ni hali ya kuwa mwenye haki, utakatifu, heshima, kudura, hekima, na rehema na upendo. Ile hisia ambayo Shetani huwapatia watu ni ya kuchukiza na iliyolaaniwa. Ile hisia ambayo Mungu huwapatia watu ni ya kukaribishwa, uzuri na kuheshimiwa.
kutoka kwa "Kujua Kazi ya Roho Mtakatifu Kuna Umuhimu Mkubwa kwa Wokovu wa Mwanadamu" katika Mahubiri na Ushirika juu ya Kuingia Katika Maisha (II)
Ni nini athari ya kazi ya Roho Mtakatifu kwa mwanadamu? Humruhusu mwanadamu kuyaelewa maneno ya Mungu, na ukweli, na humruhusu mwanadamu kumjua Mungu na kujijua. Ukweli unao athari maradufu. Kwa upande mmoja, kuufahamu ukweli huwapatia watu maarifa ya Mungu, kwani ukweli ndio kiini cha maisha ya Mungu, ni kile Mungu anacho na Alicho, ni uhalisi wa mambo mazuri, na unawakilisha tabia na maisha ya Mungu—na hivyo basi ni sahihi kabisa kusema kwamba, kwa kuuelewa ukweli, tunafaidi ufahamu fulani wa Mungu. Wakati uo huo, ukweli unaweka pia wazi kupotoka kwetu, na hivyo basi wale wote wanaouelewa ukweli wanayo maarifa ya kweli kujihusu, na wameona wazi kabisa picha yao ya kweli na picha ya kweli ya Shetani. Kila kitu kinawekwa wazi kwa ukweli. Ni nini athari ya ufahamu wa ukweli kupitia kazi ya Roho Mtakatifu? Kwa upande mmoja, tunakijua kiini chetu potovu, tunamwona kwamba mwanadamu ni maskini, wa kuhurumiwa, kipofu, aliye na uchi, aliyepotoka, mwovu, mchoyo na mwenye dharau, kwamba hana mfanano hata kidogo wa mwanadamu wa kweli, kwamba hayuko tofauti hata kidogo na Shetani, kwamba asili yake na kiini chake vyote viko sawa na Shetani. Je, hii si athari ya ufahamu wa ukweli? Hakuna chochote ambacho si sahihi kuhusu haya. Isitoshe, kwa mtazamo huu tuko wazi kabisa kuhusu athari za kazi ya Roho Mtakatifu. Kazi ya Roho Mtakatifu inayo pia athari nyingine nyingi. Kazi ya Roho Mtakatifu inaweza kuwapa watu imani ya kweli: Kila mojawapo ya maombi yetu kwa Mungu hutufanya kuhisi kwamba imani yetu kwa Mungu imeongezeka, na kwamba ni kweli zaidi. … Si ukweli hata kidogo kusema kwamba kunazo sehemu nyingi katika kazi ya Roho Mtakatifu, na mitazamo mingi ya athari zake. … kazi ya Roho Mtakatifu hutupatia maarifa ya kweli ya tabia ya Mungu, ya kudura na hekima ya Mungu, ya uchanganuzi Wake wa kina wa mioyo yetu, na hutupatia maarifa ya matendo ya ajabu na hali isiyofikirika kuhusu Mungu. Hivyo, pia, ndivyo inavyoturuhusu kujua na kushikilia kudura ya Mungu na utawala wake dhidi ya vyote.
kutoka kwa "Kujua Kazi ya Roho Mtakatifu Kuna Umuhimu Mkubwa kwa Wokovu wa Mwanadamu" katika Mahubiri na Ushirika juu ya Kuingia Katika Maisha (II)
Wale ambao pepo wabaya hufanya kazi ndani yao hugeuka na kuwa wabaya na wazi na wenye kufanya jeuri wakati wanapoongea na kuwaambia watu ni nini cha kufanya. Baadhi yao hata hukiuka tabia njema na maadili ya ubinadamu wa kawaida. Maneno yao na vitendo vyao huroga na kuingilia kati watu, asili ya maneno hayo na vitendo hivyo ni mbovu na ya kuchukiza, na wanapotosha watu, na kuwadhuru watu, na hawana manufaa yoyote kwao. Punde tu pepo mbaya anapoonekana ndani ya mtu, wanahisi woga na wasiwasi, na kunakuwa na dharura kuu katika vitendo vyao, ni kana kwamba wanalipuka kwa kutokuwa wastahimilivu. Kuonekana kwake huwafanya watu kuhisi hasa kwa njia isiyo ya kawaida, na hakuna manufaa yoyote hata kidogo kwa wengine. Maonyesho makuu ya kazi ya pepo wabaya: Onyesho la kwanza ni kuwaelekeza watu kufanya hivi au vile, kuwaambia kufanya mambo, au kuwaelekeza kuongea unabii wa uongo. Onyesho la pili ni kuongea kwa mbinu ile ijulikanayo kama ya "ndimi" ambayo hakuna anayeielewa; hata wasemaji wenyewe hawawezi kuelewa kile wanachosema, na baadhi yao wanaweza "kuifasiri." Onyesho la tatu ni pale ambapo watu siku zote wanaupokea ufunuo, unaofanyika kwa uradidi fulani. Kwa wakati mmoja wataelekezwa kufanya kitu kimoja, na kwa wakati mwingine wataambiwa kufanya kitu kingine, na wanaishi katika wasiwasi usioisha. Onyesho la nne: watu ambao pepo mbaya anafanya kazi ndani yao wanayo hamu ya kufanya hiki au kile, na hawawezi kusubiri—licha ya kama kitu hicho kinakubaliwa katika mazingira yao au la. Huwa hata wanatoka nje kwenye giza la usiku; mwenendo wao si wa kawaida kamwe. Onyesho la tano: watu ambao pepo mbaya anafanya kazi ndani yao huwa hasa wenye majivuno na kiburi, kila kitu wanachosema ni cha kushusha hadhi na kuamrisha, hawawezi kuuongea ukweli wowote, anawaacha watu wakiwa wamekasirika, na kuwalazimisha watu kuingia kwenye taabu kama pepo. Onyesho la sita: watu ambao pepo mbaya anafanya kazi ndani yao hawana ufahamu kiasi kidogo cha mipangilio kutoka juu, isitoshe hawaelewi kanuni za kazi; wanamkenulia Mungu, wanajaribu kuwadanganya watu, na matendo yao mabaya yanatatiza mpangilio wa kawaida wa kanisa. Onyesho la saba: watu ambao pepo mbaya anafanya kazi ndani yao mara nyingi hujifanya kuwa watu wengine bila sababu, au vinginevyo wametumwa na mtu, kuwafanya watu kuyasikiliza maneno yao, na hakuna anayeweza kujua namna walivyofikia hapo. Onyesho la nane: watu ambao pepo mbaya anafanya kazi ndani yao mara nyingi hawana urazini, na hawauelewi ukweli; kwa kawaida, wanakosa welekevu wa kuelewa, na hawana kule kupewa nuru na Roho Mtakatifu. Watu hugundua kwamba kile wanachoelewa hasa si cha kawaida, na si sahihi kabisa. Onyesho la tisa: watu ambao pepo mbaya anafanya kazi ndani yao ni wenye makuu kabisa na wasio na urazini, hawamtukuzi Mungu wala kumtolea ushuhuda kamwe, hawawezi kuuongea ukweli wowote, na kile wanachofanya na kusema tu huwa kinawashambulia watu, kinawafunga, na kuwawekea mipaka, mpaka pale ambapo mioyo yao imeshughulikiwa, na wao kupigwa na kugeuzwa kuwa wabaya na wasioweza kujiokoa, huku nao wakiwa na furaha kisirisiri—ambayo ndiyo nia kuu ya kazi ya pepo wabaya. Onyesho la kumi: watu ambao wamepagawa na pepo wabaya—maisha yao yana kasoro kabisa, mtazamo wao mkali, na maneno yao hasa hayana urafiki, ni kana kwamba wao ni pepo ambaye ameingia ulimwenguni humu. Hakuna nidhamu katika maisha yao ya kila siku, hawana uthabiti kabisa, wao hawatabiriki kama vile wale wanyama wasiofugwa, wanyama mwitu, na watu wanawaona kuwa wanaweza kupingika kabisa. Hayo ndiyo maonyesho ya watu waliofungwa na mashetani. Watu ambao wamepagawa na pepo wabaya mara nyingi hasa wanakuwa wenye chuki na kujitenga na wale ambao Roho Mtakatifu anafanya kazi ndani yao na wanaoweza kuuongea ukweli. Ndivyo inavyokuwa mara nyingi kwamba watu wanapokuwa bora zaidi, ndipo wanapotaka kuwashambulia na kuwashutumu, ilhali watu wanapokosa mwelekeo na kuchanganyikiwa zaidi, ndipo wanapofanya kadri wanachoweza kuwalaghai na kuwavisha kilemba cha ukoka, na hasa wao kuwa radhi kujihusisha nao. Kazi ya pepo wabaya hugeuza nyeusi ikawa nyeupe, na kuyafanya mazuri kuwa mabaya na mabaya kuwa mazuri. Hayo ndiyo matendo ya pepo wabaya.
kutoka kwa "Maonyesho Makuu ya Kazi ya Pepo Wabaya" katika Ushirikiano Kutoka kwa wa Juu
Roho yoyote ambayo kazi yake inajionyesha katika hali isiyo ya ulimwenguni humu ni pepo mbaya, na kazi na matamko ya roho yoyote inayotekeleza kazi isiyo ya ulimwenguni humu ndani ya watu ni kazi ya pepo mbaya; mbinu hizi zote ndizo ambazo pepo wabaya hufanya kazi na si za kawaida na za humu ulimwenguni, na zinaonyeshwa kimsingi kwa njia sita zifuatazo:
1. Udhibiti wa moja kwa moja wa uneni wa watu, jambo ambalo linaonyesha waziwazi kwamba pepo mbaya anazungumza, na wala si watu wenyewe wanaozungumza kwa kawaida;
2. Hisia kwamba pepo mbaya anawaelekeza watu na kuwaamuru kufanya hiki na kile;
3. Watu ambao, wakati wakiwa kwenye chumba, wanaweza kujua wakati mtu yuko karibu kuingia ndani;
4. Watu ambao mara nyingi wanazisikia sauti zikiwazungumzia na ambazo wengine hawawezi kuzisikia;
5. Watu ambao wanaweza kuona na kusikia mambo ambayo wengine hawawezi;
6. Watu ambao siku zote wanafadhaishwa, na wanajizungumzia wenyewe, na hawawezi kuwa katika mazungumzo ya kawaida au utangamano na watu.
Wale wote ambao pepo mbaya anafanya kazi ndani yao bila kuepukika wanayo maonyesho haya sita. Wao hawana urazini, siku zote wako katika hali ya taharuki, hawawezi kutangamana na watu kwa njia ya kawaida, ni kana kwamba wao hawashawishiki kwa lolote lile, na kuna jambo lililojitenga na lisilo lao. Watu kama hao wamepagawa na pepo mbaya au wanaye pepo mbaya anayefanya kazi ndani yao, na kazi yote ya pepo wabaya inajionyesha na si ya ulimwenguni humu. Hii ndiyo kazi inayotambulika kwa haraka zaidi kuhusu pepo wabaya. Wakati pepo mbaya anapompagaa mtu, anacheza nao kiasi cha kwamba wanaathirika kabisa. Wanakosa urazini, kama zuzu, hali ambayo inathibitisha kwamba kiini cha mambo ni kuwa, pepo wabaya ni pepo waovu wanaopotosha na kuteketeza watu. Matamko ya pepo wabaya ni rahisi kuyatambua: Matamko yao yanaonyesha kikamilifu kiini chao cha uovu, yapo palepale, yamevurugika, na yananuka, yanarishai harufu ya kifo. Kwa watu walio na uhodari mzuri, maneno ya pepo wabaya huwafanya kuhisi utupu na kutovutiwa, yasiyorekebisha maadili, yasiyo na chochote ila uongo na maneno yasiyo na maana, wanahisi wakiwa wamevurugika na wanaona ugumu kuelewa yote haya, kama zigo la upuuzi. Huu ni baadhi ya upuuzi unaotambulika kwa haraka zaidi kuhusu pepo wabaya. Kuwaroga watu, baadhi ya wale pepo wabaya wa "kiwango cha juu" hujifanya kuwa Mungu au Kristo wanapoongea, huku wengine wakijifanya kuwa malaika au watu maarufu. Wanapoongea, pepo hawa wabaya ni stadi katika kuiga maneno au kauli fulani za Mungu, au sauti ya Mungu, na watu wasiouelewa ukweli wanadanganywa kwa urahisi na pepo kama hawa wabaya wa "kiwango cha juu." Watu wa Mungu waliochaguliwa lazima wawe wazi kwamba, kiini cha mambo ni kwamba, pepo wabaya ni waovu na wasio na aibu, na hata kama wao ni pepo wabaya wa "kiwango cha juu," wao hawana ukweli kabisa. Pepo wabaya, zaidi ya yote, ni pepo wabaya, kiini cha pepo wabaya ni uovu, na wenye sampuli moja na Shetani.
kutoka kwa "Jinsi ya Kutambua Upumbavu na Uongo wa Roho Waovu, Makristo wa Uongo, na Wapinga Kristo" katika Kumbukumbu za Kihistoria za Ushirika na Mipangilio ya Kazi ya Kanisa (II)
Kila kitu ambacho pepo wabaya hufanya si cha ulimwenguni humu kabisa, wao huelekeza moja kwa moja watu kufanya hiki au kile, huwaamuru moja kwa moja kufanya hiki na kile, huwalazimisha kwa njia ya moja kwa moja kufanya mambo—haya ndiyo maonyesho ya kazi ya pepo wabaya. Kazi ya Roho Mtakatifu haijawahi kuwalazimisha watu kufanya hiki au kile, haijawahi kuwaamuru watu huku na kule, haijawahi kukosa kuwa ya ulimwenguni humu, haijawahi kutumia mbinu zisizo za ulimwenguni humu kuwaelekeza watu kufanya mambo, siku zote imefichwa ndani kabisa ya watu, na inawagusa kupitia kwa dhamiri yao ili kuwafanya kuuelewa ukweli na maneno ya Mungu, na baadaye hutumia dhamiri kuwafanya kuuweka ukweli ule katika matendo. Hii ndiyo mbinu ambayo Roho Mtakatifu hufanyia kazi. Roho Mtakatifu hajawahi kuwalazimisha wala kuwashurutisha watu, Hajawahi kufanya chochote kisicho cha ulimwenguni humu au chenye maonyesho, na Haelekezi watu waziwazi. Tunajua nini kutoka kwa haya? Tunajua kwamba kazi ya Roho Mtakatifu ni nyenyekevu na fiche, na hasa fiche, na hakuna yoyote yake imefichuliwa. Mungu ni mwenye kudura na anashikilia utawala dhidi ya vitu vyote, lakini Roho Mtakatifu hamwambii mwanadamu kwa njia ya moja kwa moja, "Aisee, unafaa kufanya hivi au vile." Roho Mtakatifu hajawahi kuchukua hatua namna hii; Yeye hukugusa, kwa kutumia upendo Yeye hukugusa, na Yeye ni mtulivu sana, kiasi cha kwamba huhisi kama mtu anakugusa—lakini kwenye kina cha moyo wako unahisi kwamba unafaa kuchukua hatua kwa njia fulani, na kwamba ni sahihi na bora kufanya hivyo. Tazama namna ambavyo Mungu alivyo mzuri! Tazama tena sura mbovu na ya kuhurumiwa ya wale waliopagawa na pepo wabaya, tazama ambavyo, pindi wanapokutana na watu, wanasema, "Leo roho amenielekeza kusema hivi, ameniambia kufanya vile, amenifanya kufanya hivi," angalia namna ambavyo wakati mwingine wanavyoamka kwenye usiku wa giza kueneza injili, au kuomba, au kusema namna ambavyo wameguswa na lazima watimize wajibu wao. Tazama namna, punde watu wanapofungwa na pepo mbaya, yeye huwasababishia mateso mabaya, na kuwafanya kusambaratika, tazama namna ambavyo hawajui ni lini watakula au kufanya mambo, namna ambavyo maisha yao yamebadilika na kuwa kombo. Wakati ambapo pepo wabaya wanafanya kazi ndani ya watu, wao huwazungusha huku na kule, na kuwaacha wakiwa wamechoka na hoi. Hatimaye, wanaambulia patupu: Hakuna mabadiliko katika tabia yao ya maisha, wangali bado wamepotoka kama walivyokuwa awali, wale ambao kwa kawaida walikuwa na majivuno na makuu wangali bado na majivuno na makuu, na wale waliokuwa wajanja na wakujitia mapuuza wangali wajanja na walewale wa kujitia mapuuza. Kazi ya pepo wabaya huwapotosha watu, na kuwaacha wakiwa si wa kawaida kiakili. Kutoka kwenye utaratibu wa utendaji wa pepo wabaya, tunaona tu namna ambavyo wana dharau, uovu, mapuuza, na ujinga. Hafanyi chochote ila kuwanyanyasa na kuwapotosha watu, kwa sababu ya haya wanachukiwa na kulaaniwa na watu, wanaosema kwamba wao ni wabaya. Hivyo, kazi ya pepo wabaya inamwakilisha Shetani—hakuna kosa katika haya. Yeyote aliyewaona watu ambao pepo wabaya hufanya kazi ndani yao, au wale waliopagawa na Shetani, anajua tu namna wanavyochukiza, walivyo na mapuuza, uovu, na walivyojaa upotovu. Je, mnayaona haya? Je, mnayaona baadhi yake, sivyo? Je, mmeona kwamba pepo wabaya wanaumiliki ukweli? Je, pepo wabaya wanao upendo wowote kwa wanadamu? Kutoka kwenye kazi ya pepo wabaya, inaweza kuonekana kwamba hawana ukweli hata kidogo, na kwamba asili yao ni ya uovu kabisa. Baada ya kuona namna ambavyo pepo wabaya wanavyowapotosha watu, umeona namna ambavyo Shetani hupotosha watu—ni ukweli kabisa. Kwa sababu pepo wote wabaya wanashirikiana na Shetani, kwani wote wanamfuata Shetani, na ndio washiriki, marafiki, na washirikishi wa Shetani, wamekuwa na Shetani tangu hapo zama za kale. Shetani aliwaongoza pepo hawa wote wabaya katika kuasi dhidi ya Mungu na akaangushwa hapa ulimwenguni. Je, pepo mbaya angeweza—pepo mbaya asiye na ukweli na mwenye kuasi kabisa Mungu katika asili yake—kuuleta ukweli wowote kwa mtu anapompagaa? Anaweza kuyaleta mabadiliko katika tabia zao? Bila shaka, la.
kutoka kwa "Kujua Kazi ya Roho Mtakatifu Kuna Umuhimu Mkubwa kwa Wokovu wa Mwanadamu" katika Mahubiri na Ushirika juu ya Kuingia Katika Maisha (II)