Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo dutu-ya-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo dutu-ya-Mungu. Onyesha machapisho yote

Ijumaa, 24 Mei 2019

Imani za Kimsingi za Kanisa la Mwenyezi Mungu

Imani za Kimsingi za Kanisa la Mwenyezi Mungu

(1) Mafundisho ya Kanisa la Mwenyezi Mungu
Mafundisho ya Ukristo yanatoka kwa Biblia, na mafundisho ya Kanisa la Mwenyezi Mungu yanatoka kwa ukweli wote ulioonyeshwa na Mungu tangu wakati wa uumbaji wakati wa kazi ya Enzi ya Sheria, Enzi ya Neema, na Enzi ya Ufalme. Hiyo ni kusema, Agano la Kale, Agano Jipya, na Biblia ya Enzi ya Ufalme–Neno Laonekana Katika Mwili–zilizoonyeshwa Bwana Yesu aliyekurudi wa siku za mwisho, Mwenyezi Mungu, ni imani za msingi na mafundisho ya Kanisa la Mwenyezi Mungu. Agano la Kale linarekodi kazi ya Yehova Mungu ya kuagiza sheria na amri na kuyaongoza maisha ya mwanadamu wakati wa Enzi ya Sheria; Agano Jipya linarekodi kazi ya ukombozi iliyofanywa na Bwana Yesu wakati wa Enzi ya Neema; na Neno Laonekana Katika Mwili yote ni ukweli kwa ajili ya utakaso na wokovu wa wanadamu ulioonyeshwa na Mwenyezi Mungu wakati wa Enzi ya Ufalme, pamoja na maelezo ya kazi ya hukumu ya Mungu wakati wa siku za mwisho. Biblia ya kweli ni matamko yote ya Mungu wakati wa hatua tatu za kazi, na imani za msingi za Kanisa la Mwenyezi Mungu ni matamko yote ya Mungu wakati wa hatua tatu za kazi, yaani, ukweli wote ulioonyesha na Mungu wakati wa hatua hizi tatu za kazi. Maandiko matatu Matakatifu ndiyo imani za msingi na mafundisho ya Kanisa la Mwenyezi Mungu.
Ukristo ulizaliwa na kazi ya Bwana Yesu katika Enzi ya Neema, lakini Bwana Yesu Kristo unaomwamini alifanya tu kazi ya ukombozi tu katika Enzi ya Neema. Kwa sababu Bwana Yesu mwenye mwili alisulubiwa na alitumika kama sadaka ya dhambi ya mwanadamu, kumwokoa mtu kutoka kwa mikono ya Shetani na kumtoa kutoka kwa hukumu na laana ya sheria, mtu alikuwa aje tu mbele ya Mungu na kukiri dhambi zake na kutubu ili kusamehewa dhambi zake na kufurahia neema karimu na baraka nyingi zilizofadhiliwa na Mungu. Hii ilikuwa kazi ya ukombozi iliyofanywa na Bwana Yesu. Ingawa dhambi za mwanadamu zilisamehewa na ukombozi wa Bwana Yesu, mtu hakufutiwa asili yake ya dhambi, alikuwa bado amefungwa na kudhibitiwa nayo, na hangeweza kuepuka kufanya dhambi na kumpinga Mungu kwa kuwa mwenye kiburi na majivuno, akijitahidi kuwa na umaarufu na pato, kuwa na wivu na mgomvi, kusema uongo na kuwadanganya watu, kufuata mienendo miovu ya ulimwengu, na kadhalika. Mwanadamu hakuwa amejikomboa kutoka kwa utumwa wa dhambi na kuwa mtakatifu, na hivyo Bwana Yesu alitabiri mara nyingi kwamba angekuja tena kutekeleza kazi ya hukumu ya siku za mwisho, akisema: “Tazama, Naja upesi” (Ufunuo 22:12). “Na iwapo mtu yeyote atayasikia maneno yangu, na asiyaamini, Mimi sitamhukumu: kwa kuwa mimi sikuja ili niihukumu dunia, bali kuiokoa dunia. Yeye ambaye ananikataa mimi, na hayakubali maneno yangu, ana yule ambaye anamhukumu: neno hilo ambalo nimelisema, ndilo hilo ambalo litamhukumu katika siku ya mwisho” (Yohana 12:47-48). Pia imeandikwa katika Waraka wa Kwanza wa Petro kwamba “Kwa maana muda umekuja ambao lazima hukumu ianze katika nyumba ya Mungu” (1 Petro 4:17). Mwenyezi Mungu, Kristo wa siku za mwisho, ni Bwana Yesu aliyerejea. Yeye ameonyesha ukweli wote kwa ajili ya utakaso na wokovu wa binadamu, Ametekeleza kazi ya hukumu akianzia kwa nyumba ya Mungu, na Ametimiza kikamilifu unabii wa Biblia. Neno Laonekana Katika Mwili kilivyoonyeshwa na Mwenyezi Mungu ni “neno ambalo Roho aliyaambia makanisa” (Ufunuo 2:7) iliyotabiriwa katika Kitabu cha Ufunuo, na ni maelezo ya kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho. Kazi ya hukumu inayofanywa na Mwenyezi Mungu ni hatua ya mwisho ya kazi ya Mungu ya wokovu wa wanadamu, na pia ni hatua yake ya msingi na muhimu. Kama mtu anataka kuokolewa na Mungu na kuingia katika ufalme wa mbinguni, ni lazima akubali kazi ya Mungu ya hukumu, na katika hili kumetimizwa maneno ya Bwana Yesu: “Na kukawa na kelele saa sita ya usiku, Tazama, anakuja bwana arusi; ondokeni nje ili kumkaribisha” (Mathayo 25:6). “Tazama, nimesimama mlangoni, na kupiga hodi: mtu yeyote akisikia sauti yangu, na aufungue mlango, Mimi nitaingia kwake, na nitakula na yeye, na yeye na Mimi” (Ufunuo 3:20). Ni kama tu mtu anakubali na kupitia hukumu na kuadibiwa kwa maneno ya Mungu anapoweza kufahamu utakatifu na haki ya Mungu, kujua kiini na asili ya upotovu wa mwanadamu na Shetani na ukweli wake wa kweli, kwa kweli kutubu mbele ya Mungu, kujiondolea mwenyewe dhambi zote, kufanikisha utakatifu, kuwa yule anayemtii Mungu na kumwabudu Mungu, na kuchumwa na Mungu. Ni hapo tu atakapokuwa na sifa kamili kuzirithi ahadi na baraka za Mungu, na kupata hatima nzuri.
Mafundisho ya Kanisa la Mwenyezi Mungu yanatoka kwa ukweli wote ulioonyeshwa na Mungu katika hatua Zake tatu za kazi, ambayo ina maana kwamba yanatoka kwa maneno ya Mungu yaliyoandikwa katika Biblia na kutoka Neno Laonekana Katika Mwili. Mungu alianza kazi ya kumwokoa mwanadamu kufuatia kuumba Kwake dunia, na mpango wa usimamizi Wake kwa wokovu wa binadamu hautakamilika hadi Yeye amalize kazi ya hukumu kuanzia kwa nyumba ya Mungu katika siku za mwisho. Kutoka kwa maneno na ukweli wote ambao Mungu ameuelezea katika hatua tatu za kazi, tunaweza kikamiifu kuona kwamba, iwe ni kazi ya Mungu kufanyika kwa kutumia mtu hapo mwanzo wakati wa Enzi ya Sheria, au kazi Yake Alipokuwa mwili mara mbili katika Enzi ya Neema na Enzi ya Ufalme, yote ni matamko na maonyesho ya ukweli ya Roho mmoja; katika kiini, ni Mungu mmoja ambaye hunena na kufanya kazi. Kwa hiyo, mafundisho ya Kanisa la Mwenyezi Mungu yanatoka kwa Biblia na kutoka Neno Laonekana Katika Mwili.
(2) Kuhusu Neno Laonekana Katika Mwili
Neno Laonekana Katika Mwili ni matamshi ya kibinafsi ya Mwenyezi Mungu, Kristo wa siku za mwisho, na ni ukweli wote ambao Mungu ameuonyesha ili kumtakasa na kumwokoa mwanadamu wakati wa kazi Yake ya hukumu ya siku za mwisho. Ukweli huu ni maonyesho ya moja kwa moja ya Roho Mtakatifu, ufunuo wa maisha na kiini cha Mungu, na maonyesho ya tabia ya Mungu na kile Anacho na alicho. Ndizo njia ya pekee ambayo mtu anaweza kupitia ili kumjua Mungu na kutakaswa na kuokolewa. Maneno yanayoonyeshwa na Mwenyezi Mungu ni kanuni kuu ya vitendo vya mtu na mwenendo, na hakuna methali za juu zaidi kwa maisha ya mwanadamu.
Wakristo wa Kanisa la Mwenyezi Mungu husoma maneno ya Mungu katika Neno Laonekana Katika Mwili kila siku, kama vile tu Wakristo wa Ukristo husoma Biblia. Wakristo wote huchukua maneno ya Mungu kama mwongozo wa maisha yao na kama methali ya juu mno kuliko zote katika maisha. Katika Enzi ya Neema, Wakristo wote walisoma Biblia na kusikiliza mahubiri ya Biblia. Mabadiliko yalitokea hatua kwa hatua katika tabia za watu, na walifanya dhambi chache zaidina zaidi. Kadhalika, kupitia kusoma kwa maneno ya Mwenyezi Mungu na ushirika wa maneno ya Mungu, Wakristo wa Kanisa la Mwenyezi Mungu hatua kwa hatua huelewa ukweli na kuachana na utumwa wa dhambi, hawatendi tena dhambi na kumpinga Mungu, na kuwa wa ulingano na Mungu. Ukweli unathibitisha kwamba ni kwa kusoma maneno Mungu tu ndipo mtu anapoweza kutakaswa na kubadilishwa na kuishi kwa kudhihirisha picha ya mtu halisi. Huu ni ukweli ambao hakuna yeyote anayeweza kuukana. Maneno ya Mungu yaliyoandikwa katika Biblia yalionyeshwa Mungu alipofanya kazi katika Enzi ya Sheria na Enzi ya Neema, wakati Neno Laonekana Katika Mwili ni maneno yanayoonyeshwa na Mungu katika kazi ya siku za mwisho. Chanzo cha yote mawili ni kutoka kwa Roho Mtakatifu. Maneno na kazi ya Mwenyezi Mungu zimetimiza unabii katika Biblia kikamilifu, na Mwenyezi Mungu ni Bwana Yesu aliyerudi, kama vile tu Bwana Yesu alivyosema: “Bado ningali nayo mengi ya kuwaambieni, lakini hivi sasa hamwezi kuyavumilia. Hata hivyo, wakati yeye, Roho wa ukweli, atakapokuja, atawaongoza hadi kwenye ukweli wote: kwa maana hatazungumza juu yake mwenyewe; bali chochote atakachosikia, atakinena: na atawaonyesha mambo yajayo” (Yohana 16:12-13). Hiyo, pia, ilitabiriwa katika Kitabu cha Ufunuo kwamba, “Yeye aliye na sikio, na alisikie neno ambalo Roho aliyaambia makanisa” (Ufunuo 2:7). “Na nikaona katika mkono wa kuume wa yule aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi kitabu ambacho kiliandikwa ndani na nyuma, kilichofungwa kwa mihuri saba. … tazama, Simba wa kabila la Yuda, Shina la Daudi, ameshinda apate kukifungua kile kitabu, na kuifungua ile mihuri saba” (Ufunuo 5:1, 5).
Leo, sisi sote tumeona ukweli mmoja: Maneno yote yanayoonyeshwa na Mwenyezi Mungu ni ukweli, na yana mamlaka na nguvu–ni sauti ya Mungu. Hakuna anayeweza kukana au kubadilisha hili. Neno Laonekana Katika Mwili chapatikana bila vizuizi kwenye mtandao kwa watu wa nchi na maeneo yote kutafuta na kuchunguza. Hakuna yeyote ambaye huthubutu kukataa kwamba hayo ni maneno ya Mungu, au kwamba ni ya ukweli. Maneno ya Mungu yanaendesha ubinadamu mzima kuendelea mbele, watu wameanza hatua kwa hatua kuamka katikati ya maneno ya Mungu, na wao wanaendelea hatua kwa hatua kuelekea kuukubali ukweli na maarifa ya ukweli. Enzi ya Ufalme ni enzi ambapo maneno ya Mwenyezi Mungu hutawala duniani. Kila moja ya maneno ya Mungu litatimizwa na kukamilishwa. Kama tu vile waumini wote katika Mungu hukiri Biblia leo, watu ambao wanaamini katika Mungu watakiri hivi karibuni kwamba Neno Laonekana Katika Mwili ni maneno ya Mungu katika siku za mwisho. Leo, Neno Laonekana Katika Mwili ni msingi wa imani za Kanisa la Mwenyezi Mungu, na kwa hakika utakuwa msingi wa kuwepo kwa wanadamu wote katika enzi ijayo.
(3) Kuhusu Majina ya Mungu na Hatua Tatu za Kazi ya Mungu
Kufuatia upotovu wake na Shetani, mwanadamu huishi chini ya miliki ya Shetani na upotovu wake umeongezeka kwa kina kuliko wakati uliopita. Mwanadamu hawezi kujiokoa, na huhitaji wokovu wa Mungu. Kwa mujibu wa mahitaji ya wanadamu wapotovu, Mungu amefanya hatua tatu za kazi katika Enzi ya Sheria, katika Enzi ya Neema, na katika Enzi ya Ufalme. Katika Enzi ya Sheria, Mungu alifanya kazi ya kuagiza sheria na amri na kuongoza maisha ya mwanadamu. Katika Enzi ya Neema, Mungu alipata mwili, juu ya msingi wa kazi Yake katika Enzi ya Sheria, akatekeleza kazi ya kusulubiwa na kumkomboa mwanadamu kutoka kwa dhambi. Katika Enzi ya Ufalme, Mungu kwa mara nyingine tena amepata mwili na, juu ya msingi wa kazi ya ukombozi katika Enzi ya Neema, hutekeleza kazi ya hukumu kuanzia kwa nyumba ya Mungu, huonyesha ukweli wote wa kwa ajili ya utakaso na wokovu wa mwanadamu, na hutuletea njia pekee kwa ajili ya ufuatiliaji wa utakaso na wokovu. Ni kama tu tukichuma hali halisi ya ukweli kama maisha yetu, tukiwa wale ambao humtii na kumwabudu Mungu, tutakapokuwa na sifa kamili kuongozwa katika ufalme wa Mungu na kupokea ahadi na baraka za Mungu. Hatua tatu za kazi ya Mungu ya wokovu wa mwanadamu zimeunganika kwa karibu, kila hatua ni ya lazima, kila moja huenda juu mno na kuwa na kina zaidi ya ile ya mwisho, zote ni kazi ya Mungu mmoja, na ni hatua hizo tatu tu za kazi ya Mungu ambazo ni kazi kamili ya wokovu wa wanadamu.
Majina matatu–Yehova, Yesu, na Mwenyezi Mungu–ni majina tofauti ambayo Mungu ameyachukua katika Enzi ya Sheria, Enzi ya Neema, na Enzi ya Ufalme. Mungu huchukua majina tofauti kwa sababu kazi Yake inatofautiana katika enzi tofauti. Mungu hutumia jina jipya kuanza enzi mpya na kuwakilisha kazi ya enzi hiyo. Jina la Mungu lilikuwa Yehova katika Enzi ya Sheria, na Yesu katika Enzi ya Neema. Mungu hutumia jina jipya–Mwenyezi Mungu–katika Enzi ya Ufalme, akitimiza unabii katika Kitabu cha Ufunuo: “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Filadelfia andika… Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, na nitaliandika jina la Mungu wangu juu yake, na jina la mji wa Mungu wangu, ambao ni Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu: na nitaliandika juu yake jina langu jipya” (Ufunuo 3:7, 12). “Mimi ndiye Alfa na Omega, Mwanzo na tena mwisho, Akasema Bwana, ambaye yuko, na ambaye alikuweko, na ambaye atakuja, Mwenyezi” (Ufunuo 1:8). Ingawa majina ya Mungu na kazi katika enzi hizo tatu ni tofauti, kuna Mungu mmoja tu katika kiini, na chanzo ni kimoja.
Kazi ya Mungu ya kumwokoa mwanadamu hasa hushirikisha hatua tatu za kazi. Yeye ametumia majina tofauti katika kila enzi, lakini kiini cha Mungu hakibadiliki kamwe. Hatua tatu za kazi hufanywa na Mungu mmoja; hivyo, Yehova, Yesu, na Mwenyezi Mungu ni Mungu yule yule mmoja. Yesu alikuwa ni kuonekana kwa Yehova, na Mwenyezi Mungu ni Bwana Yesu aliyerudi, na hivyo Mwenyezi Mungu ni Mungu mmoja wa kweli ambaye aliziumba mbingu na ardhi na vitu vyote, huamrisha vitu vyote, na hushikilia ukuu juu ya kila kitu, na Yeye ndiye yule wa milele na Muumba pekee.
Katika hatua tatu za kazi ya kumwokoa mwanadamu, Mungu ameifichua tabia Yake yote kwa mwanadamu, akituruhusu tuone kwamba tabia ya Mungu si huruma na upendo tu, lakini pia haki, uadhama, na ghadhabu, kwamba kiini Chake ni utakatifu na haki, na ni ukweli na upendo, kwamba tabia ya Mungu na mamlaka na nguvu za Mungu hazimilikiwi na kiumbe chochote kilichoumbwa au kisichoumbwa. Tunaamini kuwa maneno yote ambayo Mungu ameyasema tangu wakati wa uumbaji hadi mwisho wa dunia ni ukweli. Mbingu na dunia zitapita, lakini maneno ya Mungu kamwe hayatatoweka, na kila mojawapo litatimizwa!

Jumapili, 21 Aprili 2019

Kwa Nini Mungu Anaitwa kwa Majina Tofauti katika Enzi Tofauti?

2. Kwa Nini Mungu Anaitwa kwa Majina Tofauti katika Enzi Tofauti?

Maneno Husika ya Mungu:
Katika kila enzi, Mungu Anafanya kazi mpya na huitwa kwa jina jipya; Je, anawezaje kufanya kazi sawa katika enzi tofauti? Itakuwaje Yeye kugandamana na yale ya zamani? Jina la Yesu lilichukuliwa kuwa la kazi ya ukombozi, hivyo bado Yeye Anaweza kuitwa kwa jina moja wakati Atarudi katika siku za mwisho? Je, bado Yeye Atafanya kazi ya ukombozi? Ni kwa nini Yehova na Yesu ni kitu kimoja, ilhali wanaitwa kwa majina tofauti katika enzi hizi tofauti? Je, si kwa sababu enzi za kazi Yao ni tofauti? Jina moja linawezaje kumwakilisha Mungu kwa ukamilifu wake? Kwa njia hii, lazima Mungu aitwe kwa jina tofauti katika enzi tofauti, lazima atumie jina kubadilisha enzi na kuwakilisha hiyo enzi, kwa kuwa hakuna jina moja linaweza kumwakilisha Mungu mwenyewe kikamilifu. Na kila jina linaweza tu kuwakilisha kipengele cha wakati cha tabia ya Mungu katika enzi fulani; yote linahitaji kufanya ni kuwakilisha kazi Yake. Kwa hivyo, Mungu Anaweza kuchagua jina lolote ambalo linafaa tabia yake kuwakilisha enzi nzima.
kutoka kwa "Maono ya Kazi ya Mungu (3)" katika Neno Laonekana katika Mwili
"Yehova" ni jina ambalo Nilichukua wakati wa kazi Yangu kule Uyahudi, na linamaanisha Mungu wa Wayahudi (Wateule wa Mungu) Anayeweza kumhurumia mwanadamu, kumlaani mwanadamu, na kuyaongoza maisha ya mwanadamu. Lina maana Mungu Anayemiliki nguvu kuu na Amejawa na hekima. … Hivyo ni kusema, Yehova pekee ndiye Mungu wa watu wa Uyahudi waliochaguliwa, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, Mungu wa Musa na Mungu wa Wayahudi wote. Na sasa katika enzi hii, Wayahudi wote isipokuwa kabila la Uyahudi wanamwabudu Yehova. Wanatoa kafara Kwake kwa madhabahu, na kumtumikia wakivaa mavazi ya kikuhani hekaluni. Wanachotumainia ni kuonekana tena kwa Yehova. … Jina Yehova ni jina mahsusi la Wayahudi walioishi chini ya sheria. Katika kila enzi na kila hatua ya kazi, jina Langu haliwi bila msingi, lakini lina umuhimu wakilishi: Kila jina linawakilisha enzi moja. "Yehova" Anawakilisha Enzi ya Sheria, na ni jina la heshima kwa Mungu Aliyeabudiwa na Wayahudi.
kutoka kwa "Mwokozi Amerudi Tayari Juu ya 'Wingu Jeupe'" katika Neno Laonekana katika Mwili
Wakati wa Enzi ya Sheria, kazi ya kumwelekeza mwanadamu ilifanyika katika Jina la Yehova, na awamu ya kwanza ya kazi ilifanyika duniani. Kazi ya awamu hii ilikuwa ni kujenga hekalu na madhabahu, na kutumia sheria kuwaongoza watu wa Israeli na kufanya kazi miongoni mwao. Kwa kuongoza watu wa Israeli, Alizindua kituo cha kazi Yake hapa duniani. Kwa msingi huu, Yeye Alipanua kazi yake nje ya Israeli, ambayo ni kusema kwamba, kuanzia Israeli, Aliendeleza kazi yake nje, ili vizazi vya baadaye walikuja kujua polepole kwamba Yehova Alikuwa Mungu, na kuwa Yehova Alikuwa Ameumba mbingu na nchi na vitu vyote, Alitengeneza viumbe vyote. Yeye Alieneza kazi yake kupitia kwa watu wa Israeli. Nchi ya Israeli ilikuwa ya mahali takatifu pa kwanza pa kazi ya Yehova hapa duniani, na kazi ya Mungu ya hapo mwanzoni ilikuwa kote katika nchi ya Israeli. Hiyo ilikuwa kazi ya Enzi ya Sheria.
kutoka kwa "Maono ya Kazi ya Mungu (3)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Jina la Yesu liliashiria mwanzo wa Enzi ya Neema. Wakati Yesu Alianza kufanya huduma Yake, Roho Mtakatifu Alianza kutoa ushuhuda kwa jina la Yesu, na jina la Yehova halikuzungumziwa tena, na badala yake Roho Mtakatifu Alianza kazi mpya hasa kwa jina la Yesu. Ushuhuda wa wale waliomwamini Yeye ulitolewa kwa ajili ya Yesu Kristo, na kazi waliyoifanya walifanya pia kwa ajili ya Yesu Kristo. Hitimisho Enzi ya Sheria ya Agano la Kale lilimaanisha kuwa kazi iliyofanywa hasa kutumia jina la Yehova ilikuwa imefikia kikomo. Baada ya hii, jina la Mungu halikuwa Yehova tena; badala yake Yeye Aliitwa Yesu, na kutoka hapa Roho Mtakatifu Alianza kazi hasa kwa kutumia jina la Yesu.
kutoka kwa "Maono ya Kazi ya Mungu (3)" katika Neno Laonekana katika Mwili
"Yesu" ni Imanueli, na lina maana sadaka ya dhambi iliyojawa na upendo, Amejawa na huruma, na Anamkomboa mwanadamu. Alifanya kazi ya Enzi ya Neema, na Anawakilisha Enzi ya Neema, na Anaweza tu kuwakilisha sehemu moja tu ya mpango wa usimamizi. … Yesu pekee ndiye Mkombozi wa wanadamu. Yeye ni sadaka ya dhambi ambayo ilimkomboa mwanadamu kutoka kwa dhambi. Ambayo ni kusema, jina la Yesu lilitoka katika Enzi ya Neema, na kuwepo kwa ajili ya kazi ya wokovu katika Enzi ya Neema. Jina la Yesu liliwepo ili kuwezesha watu wa Enzi ya Neema kuzaliwa upya na kuokolewa, na ni jina mahsusi la wokovu wa binadamu wote. Kwa hivyo jina Yesu linawakilisha kazi ya wokovu, na kuashiria Enzi ya Neema. … "Yesu" Anawakilisha Enzi ya Neema, na ni jina la Mungu wa wale wote waliokombolewa katika Enzi ya Neema.
kutoka kwa "Mwokozi Amerudi Tayari Juu ya 'Wingu Jeupe'" katika Neno Laonekana katika Mwili
Wakati wa Enzi ya Neema, jina la Mungu lilikuwa ni Yesu, ambalo lina maana kuwa Mungu Alikuwa Mungu ambaye Alimwokoa mwanadamu, na ya kwamba Alikuwa Mungu wa rehema na wa upendo. Mungu Alikuwa na mwanadamu. Upendo wake, huruma yake, na wokovu wake uliandamana na kila mtu. Mwanadamu angeweza tu kupata amani na furaha, kupokea baraka zake, kupokea neema yake kubwa na nyingi, na kupokea wokovu wake iwapo mwanadamu angekubali jina lake na akubali uwepo wake. Kupitia kusulubiwa kwa Yesu, wale wote ambao walimfuata Yeye walipokea wokovu na walisamehewa dhambi zao.
kutoka kwa "Maono ya Kazi ya Mungu (3)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kwa hivyo, enzi ya mwisho—enzi ya siku za mwisho—itakapofika, jina langu litabadilika tena. Sitaitwa Yehova, au Yesu, na wala sio Masiha, lakini nitaitwa Mwenyezi Mungu Mwenyewe mwenye nguvu, na chini ya jina hili Nitaleta enzi nzima kufikia tamati. Nilijulikana kama Yehova wakati mmoja. Niliitwa pia Masiha, na watu wakaniita Yesu Mwokozi pia wakati mmoja kwa sababu walinipenda na kuniheshimu. Lakini leo Mimi sio Yehova au Yesu Ambaye watu walimfahamu nyakati zilizopita—Mimi ni Mungu Ambaye Amerejea katika siku za mwisho, Mungu Ambaye ataleta enzi kufika mwisho. Mimi ni Mungu Mwenyewe Ambaye Anainuka katika kingo za dunia, Nimejawa na tabia Yangu nzima, na Nimejawa na mamlaka, heshima na utukufu. Watu hawajawahi kushirikiana na Mimi, hawajawahi kunifahamu, na wamekosa ufahamu kuhusu tabia Yangu. Tangu uumbaji wa dunia hadi leo, hapana hata mtu mmoja ambaye Ameniona. Huyu ni Mungu Ambaye ametokea kwa mwanadamu katika siku za mwisho lakini Amejificha kati ya mwanadamu. Anaishi kati ya mwanadamu, wa kweli na halisi, kama jua iwakayo na moto unaochoma, Aliyejaa nguvu na kujawa mamlaka. Hakuna hata mtu mmoja au kitu ambacho hakitahukumiwa na maneno Yangu, wala mtu hata mmoja au kitu ambacho hakitatakaswa kupitia moto unaowaka. Hatimaye, mataifa yote yatabarikiwa kwa sababu ya maneno Yangu, na pia kupasuliwa kwa vipande kwa sababu ya maneno Yangu. Kwa njia hii, watu wote katika siku za mwisho wataona kuwa Mimi ndiye Mwokozi Aliyerejea, Mimi ndiye Mungu Mwenyezi Ambaye Ninatamalaki juu ya binadamu wote, na Nilikuwa sadaka ya dhambi kwa mwanadamu wakati mmoja, lakini katika siku za mwisho Ninakuwa pia miale ya Jua Linalochoma vitu vyote, na pia Jua la haki Linalofichua vitu vyote. Hivyo ndivyo ilivyo kazi Yangu ya siku za mwisho. Nilichukua jina hili na Ninamiliki tabia hii ili watu wote wapate kuona kuwa Mimi ni Mungu mwenye haki, na Mimi ni jua linachoma, na moto unaowaka. Ni hivyo ili watu wote waniabudu, Mungu pekee wa kweli, na ili waone uso Wangu wa kweli: Mimi sio tu Mungu wa Wayahudi, wala Mimi sio Mkombozi tu—Mimi ni Mungu wa viumbe vyote katika mbingu na dunia na bahari.
kutoka kwa "Mwokozi Amerudi Tayari Juu ya 'Wingu Jeupe'" katika Neno Laonekana katika Mwili
Wengine wanasema kwamba jina la Mungu halibadiliki, hivyo, mbona basi jina la Yehova likawa Yesu? Ilitabiriwa kuja kwa Masihi, hivyo mbona basi mwanadamu kwa jina Yesu alikuja? Mbona jina la Mungu lilibadilika? Kazi kama hiyo haikufanyika muda mrefu uliopita? Hawezi Mungu leo kufanya kazi mpya? Kazi ya jana inaweza kubadilishwa, na kazi ya Yesu inaweza kufuata baada ya hiyo ya Yehova. Haiwezi kazi ya Yesu kurithiwa na kazi ingine? Ikiwa jina la Yehova linaweza kubadilishwa kuwa Yesu, basi jina la Yesu haliwezi kubadilishwa pia? Hii si ya ajabu, na watu wanafikiria hivyo[a] tu kwa sababu ya akili zao rahisi. Mungu daima atakuwa Mungu. Bila kujali mabadiliko ya kazi Yake na jina Lake, tabia na maarifa Yake hayabadiliki milele. Ikiwa unaamini kwamba Mungu anaweza tu kuitwa na jina Yesu, basi unajua machache sana. Unathubutu kudai kwamba Yesu milele ni jina la Mungu, kwamba Mungu milele na daima atajulikana kwa jina Yesu, na kwamba haya hayatabadilika? Unathubutu kudai kwa uhakika ni jina la Yesu lililohitimisha Enzi ya Sheria na pia kuhitimisha enzi ya mwisho? Nani anaweza kusema kwamba neema ya Yesu inaweza kuhitimisha enzi?
kutoka kwa "Ni Jinsi Gani Mwanadamu Aliyemfafanua Mungu katika Dhana Zake Anaweza Kupokea Ufunuo wa Mungu?" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kama kazi ya Mungu katika kila enzi ni sawa daima, naye daima anaitwa kwa jina sawa, ni jinsi gani basi mwanadamu atamjua Yeye? Mungu lazima aitwe Yehova, na mbali na Mungu kuitwa Yehova, yeyote ambaye ataitwa jina jingine si Mungu. Ama kwa njia nyingine Mungu Anaweza tu kuitwa Yesu, na Mungu hawezi kuitwa jina lingine isipokuwa Yesu; na mbali na Yesu, Yehova si Mungu, na wala Mwenyezi Mungu si Mungu. Mwanadamu anaamini kuwa ni ukweli Mungu ni mwenye uweza, lakini Mungu ni Mungu pamoja na mwanadamu; Sharti aitwe Yesu, kwa kuwa Mungu yu pamoja na mwanadamu. Kufanya hili ni kufuata mafundisho, na kumshurutisha Mungu kwenye eneo fulani. Kwa hivyo, kazi ambayo Mungu hufanya katika kila awamu, jina ambalo Yeye huitwa, na mfano ambao yeye anatwaa, na kila awamu ya kazi yake mpaka leo, havifuati kanuni hata moja, na hayakabiliwi na kikwazo chochote. Yeye ni Yehova lakini pia ni Yesu, na vile vile ni Masihi, na Mwenyezi Mungu. Kazi yake inaweza kubadilika polepole, na kuna mabadiliko sambamba katika jina lake. Hamna jina moja ambalo linaweza kumwakilisha Yeye kikamilifu, lakini majina yote ambayo Yeye huitwa yanaweza kumwakilisha Yeye, na kazi ambayo Amefanya katika kila enzi inawakilisha tabia yake.
kutoka kwa "Maono ya Kazi ya Mungu (3)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kila wakati ambao Mungu Atawasili hapa duniani, Yeye Atabadilisha jina lake, jinsia yake, mfano wake, na kazi yake; Yeye harudii kazi yake, na Yeye daima yu mpya na kamwe si wa zamani. Wakati Alikuja hapo awali, Aliitwa Yesu; Je, anaweza bado kuitwa Yesu anapokuja tena wakati huu? … Kuna wale ambao wanasema kuwa Mungu habadiliki. Hiyo ni sahihi, lakini inaashiria mabadiliko ya tabia ya Mungu na pia kiini chake. Mabadiliko ya jina lake na kazi hayathibitishi ya kuwa kiini chake kimebadilika; kwa maneno mengine, Mungu siku zote Atakuwa Mungu, na hii kamwe haitabadilika. Iwapo utasema kuwa kazi ya Mungu daima inabaki vile vile, basi Angekuwa na uwezo wa kumaliza mpango wake wa usimamizi wa miaka elfu sita? Wewe hujua tu kwamba Mungu habadiliki milele, lakini je, unajua kuwa Mungu ni mpya milele na kamwe si wa zamani?
kutoka kwa "Maono ya Kazi ya Mungu (3)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Na kwa hivyo, kila wakati Mungu Anapokuja, anaitwa kwa jina moja, Yeye anawakilisha enzi moja, na Yeye anafungua njia mpya; na kwa kila njia mpya, Yeye huchukua jina jipya, ambalo inaonyesha kuwa Mungu daima ni mpya na wala si wa zamani, na ya kwamba kazi yake daima inasonga mbele. Historia inasonga mbele daima, na kazi ya Mungu inasonga mbele daima. Ili mpango wa usimamizi wa Mungu wa miaka elfu sita ufike upeo wake, lazima uendelee kusonga mbele. Kila siku ni sharti Yeye afanye kazi mpya, kila mwaka lazima Yeye afanye kazi mpya, ni sharti Yeye afungue njia mpya, sharti aanzishe enzi mpya, aanzishe kazi mpya na kubwa zaidi, na ni sharti alete majina mapya na kazi mpya.
kutoka kwa "Maono ya Kazi ya Mungu (3)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Siku itawadia ambapo Mungu hataitwa Yehova, Yesu, au Masihi—Yeye Ataitwa tu Muumba. Wakati huo, majina yote ambayo Alichukua hapa duniani yatafikia kikomo, kwa kuwa kazi yake hapa duniani itakuwa imefika mwisho, na baada ya hapo Mungu hatakuwa na jina. Wakati mambo yote yatakuja kuwa chini ya utawala wa Muumba, kwa nini umwite kwa jina sahihi ila bado halijakamilika? Je, bado unatafuta jina la Mungu sasa? Je, bado unathubutu kusema kuwa Mungu Anaitwa tu Yehova? Je, bado unathubutu kusema kuwa Mungu Anaweza tu kuitwa Yesu? Je, unaweza kubeba dhambi ya kumkufuru Mungu?
kutoka kwa "Maono ya Kazi ya Mungu (3)" katika Neno Laonekana katika Mwili

Jumamosi, 20 Aprili 2019

Mwenyezi Mungu Ndiye Mungu Mmoja wa Kweli Anayetawala Juu ya Vitu Vyote.

1. Mwenyezi Mungu Ndiye Mungu Mmoja wa Kweli Anayetawala Juu ya Vitu Vyote.

Maneno Husika ya Mungu:
Wanadamu hawajui ni nani Mkuu wa kila kitu katika ulimwengu huu, aidha hajui mwanzo na mustakabali wa wanadamu. Wanadamu wanaishi tu, bila budi, katikati ya hii sheria. Hakuna anayeweza kuiepuka wala kuibadilisha kwani katika vitu vyote na katika mbingu kuna Mmoja kutoka milele hadi milele ambaye ni Mkuu wa kila kitu. Ni Yeye ambaye Hajawahi kuonekana na mwanadamu, ambaye wanadamu hawajawahi kumjua, ambaye wanadamu hawajawahi kuamini kuwepo Kwake, na bado ni Yeye Aliyewapulizia pumzi mababu wa wanadamu na kuwapa wanadamu uhai. Ni Yeye ndiye Huruzuku na kustawisha wanadamu kwa kuishi kwao, na huwaongoza wanadamu hadi siku ya leo. Aidha, Yeye na Yeye pekee ni wa kutegemewa na wanadamu ili kuendelea kuishi. Ni Mkuu wa kila kitu na Hutawala viumbe vyote vyenye uhai chini ya dunia. Huamrisha misimu yote minne, na ni Yeye huita upepo, jalidi, theluji na mvua. Huwapa wanadamu mwangaza wa jua na huleta machweo ya jioni. Ni Yeye Aliyeumba mbingu na ardhi, Akampa mwanadamu milima, maziwa na mito na kila kitu kilicho na uhai ndani yake. Matendo Yake yamo kila mahali, nguvu Zake ziko kila mahali, busara Zake ziko kila mahali na mamlaka Yake yako kila mahali. Kila mojawapo ya hizi sheria na kanuni ni mfano mzuri wa matendo Yake, na kila mojawapo inafichua hekima na mamlaka Yake. Nani anayeweza kujiondoa kutoka kwa ukuu Wake? Na ni nani anayeweza kujitoa mwenyewe katika njia Zake? Kila kitu kinaishi chini ya uangalizi Wake, zaidi ya hayo, kila kitu huishi chini ya ukuu Wake. Matendo na nguvu Zake huwaacha wanadamu bila chaguo ila kutambua ukweli kwamba ni Yeye pekee Anayeishi na Ana ukuu juu ya kila kitu. Hakuna kitu chochote ila Yeye kinachoweza kuamuru dunia, wala kuwajibikia wanadamu bila kukoma. Bila kujali kama unaweza kutambua vitendo vya Mungu, bila kujali kama unaamini katika kuwepo kwa Mungu, hakuna shaka kuwa hatima yako inaegemea katika mipango ya Mungu, na hakuna shaka kuwa Mungu atakuwa na ukuu juu ya kila kitu. Uwepo na utawala Wake haviwezi kutabiriwa ikiwa vinatambulika na kufahamika na binadamu au la. Ni Yeye pekee Anayejua kuhusu yaliyopita ya mwanadamu, yaliyomo na yanayojiri, na Yeye pekee ndiye mwamuzi wa hatima ya wanadamu. Haijalishi kama unaukubali huu ukweli, haitachukua muda mrefu kabla mwanadamu kushuhudia haya yote kwa macho yake mwenyewe, na huu ni ukweli ambao hivi karibu Mungu Ataudhihirisha.
kutoka kwa "Mwanadamu Anaweza Kuokolewa Tu Katikati ya Usimamizi wa Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Njia ya maisha si kitu ambacho kinaweza kumilikiwa na mtu yeyote tu, wala hakipatikani kwa urahisi na wote. Hiyo ni kwa sababu maisha yanaweza kuja tu kutoka kwa Mungu, ambayo ni kusema, Mungu Mwenyewe tu ndiye Anamiliki mali ya maisha, hakuna njia ya maisha bila Mungu Mwenyewe, na hivyo Mungu tu ndiye chanzo cha uzima, na kijito cha maji ya uzima kinachotiririka nyakati zote. Kutoka Alipoumba dunia, Mungu amefanya kazi kubwa inayoshirikisha uhai wa maisha, Amefanya kazi kubwa ambayo huletea mwanadamu maisha, na Amelipa gharama kubwa ili mtu aweze kupata uzima, kwa kuwa Mungu Mwenyewe ni uzima wa milele, na Mungu Mwenyewe ni njia ambayo kwayo mtu hufufuliwa. Mungu kamwe hajawahi kosa kwa moyo wa mwanadamu, na Anaishi miongoni mwa binadamu wakati wote. Amekuwa nguvu ya kuendesha maisha ya mwanadamu, chanzo cha kuwepo kwa binadamu, na amana ya fahari ya kuwepo kwa binadamu baada ya kuzaliwa. Husababisha binadamu kuzaliwa upya, na kumwezesha kwa ushupavu kuishi kwa kila jukumu lake. Kwa sababu ya uwezo Wake, na nguvu ya maisha Yake yasiyopungua, binadamu ameishi kwa kizazi baada ya kizazi, ambapo nguvu ya uhai wa Mungu umekuwa uti wa mgongo wa kuwepo kwa binadamu, na ambayo Mungu amelipa gharama ambayo hakuna mtu wa kawaida amewahi kulipa. Nguvu za Mungu za maisha zinaweza kutawala juu ya nguvu zozote; zaidi ya hayo, inazidi mamlaka yoyote. Maisha Yake ni ya milele, nguvu zake za ajabu, na nguvu Zake za maisha si rahisi kuzidiwa na kiumbe yeyote au nguvu za adui. Nguvu za maisha ya Mungu zipo, na hung'aa mwangaza wake ulio mzuri sana, bila ya kujali muda au mahali. Maisha ya Mungu, huishi milele bila kubadilika katika kusumbuka kwa mbingu na nchi. Mambo yote hupita, lakini maisha ya Mungu hubaki, kwa maana Mungu ni chanzo cha kuwepo kwa mambo yote, na mizizi ya kuwepo kwao. Asili ya maisha ya mwanadamu hutoka kwa Mungu, kuwepo kwa mbingu ni kwa sababu ya Mungu, na kuwepo kwa ardhi kunatokana na nguvu ya uhai wa Mungu. Hakuna kitu kinachomiliki nguvu kinachoweza kuzidi ukuu wa Mungu, na hakuna kitu chenye nguvu kinachoweza kuvunja mipaka ya mamlaka ya Mungu. Kwa njia hii, bila kujali wao ni nani, kila mtu lazima ajiwasilishe kwa utawala wa Mungu, kila mtu lazima aishi chini ya amri za Mungu, na hakuna mtu anayeweza kutoroka kutoka katika utawala Wake.
kutoka kwa "Ni Kristo Wa Siku za Mwisho Pekee Ndiye Anayeweza Kumpa Mwanadamu Njia ya Uzima wa Milele" katika Neno Laonekana katika Mwili
Mungu aliumba dunia hii na kuleta mwanadamu, kiumbe hai ambacho alitia uhai ndani yake. Baadaye, mwanadamu akaja kuwa na wazazi na jamaa na hakuwa mpweke tena. Tangu mwanadamu alipotua macho kwa mara ya kwanza katika dunia hii tunayoishi, ilibainika kuwa angeishi ndani ya utaratibu wa Mungu. Ni pumzi ya uhai kutoka kwa Mungu ndiyo hustawisha kila kiumbe hai katika ukuaji wake hadi kinapokomaa. Wakati wa mchakato huu, hakuna hata mmoja anayeamini kwamba mwanadamu huishi na kukua chini ya uangalizi wa Mungu. Badala yake, anashikilia kwamba mwanadamu hukua chini ya upendo na utunzaji wa wazazi wake, na kwamba ukuaji wake unaongozwa na silika ya maisha. Hii ni kwa sababu mwanadamu hajui aliyeleta maisha au kulikotoka maisha hayo, pia hafahamu jinsi silika ya maisha husababisha miujiza. Mwanadamu anajua tu kwamba chakula ndicho msingi wa kuendelea kwa maisha, kwamba uvumilivu ni chanzo cha kuwepo kwa maisha, na kwamba imani iliyomo akilini mwake ni utajiri wa maisha yake. Mwanadamu haihisi neema na riziki itokayo kwa Mungu. Mwanadamu huyatumia kwa uharibifu maisha aliyopewa na Mungu.
kutoka kwa "Mungu Ndiye Chanzo cha Uhai wa Mwanadamu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Majaliwa ya mwanadamu inadhibitiwa na mikono ya Mungu. Wewe huna uwezo wa kujidhibiti mwenyewe: Licha ya mwanadamu yeye mwenyewe daima kukimbilia na kujishughulisha, anabakia bila uwezo wa kujidhibiti. Kama ungejua matarajio yako mwenyewe, kama ungeweza kudhibiti majaliwa yako mwenyewe, ingekuwa wewe bado ni kiumbe? Kwa kifupi, bila kujali jinsi Mungu hufanya kazi, kazi yote yake ni kwa ajili ya mwanadamu. Chukua, kwa mfano, mbingu na nchi na vitu vyote ambavyo Mungu aliviumba ili kumhudumia mwanadamu: mwezi, jua, na nyota ambazo Yeye alimuumbia mwanadamu, wanyama na mimea, majira ya machipuko, majira ya joto, vuli na baridi, na kadhalika—yote ni kwa ajili ya kuwepo kwa mwanadamu.
kutoka kwa "Kurejesha Maisha ya Kawaida ya Mwanadamu na Kumpeleka Kwenye Hatima ya Ajabu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Tangu unapoingia katika dunia hii ukilia, unaanza kutekeleza wajibu wako. Unachukua jukumu lako katika mpango wa Mungu na katika utaratibu wa Mungu. Unaanza safari ya maisha. Licha ya asili yako na licha ya safari iliyoko mbele yako, hakuna kitakachoepuka mpango na utaratibu ambao mbingu imeweka, na hakuna aliye na udhibiti wa hatima yake, kwa maana Anayetawala juu ya kila kitu ndiye tu Aliye na uwezo wa kazi hiyo. Tangu siku aliyoumbwa binadamu, Mungu amekuwa thabiti katika kazi Yake, kusimamia ulimwengu huu na kuelekeza mabadiliko na harakati ya mambo yote. Kama kila kiumbe, mwanadamu bila kujua anapata lishe ya utamu na mvua na umande kutoka kwa Mungu. Kama vitu vyote, mwanadamu bila kujua anaishi chini ya mpango wa mkono wa Mungu. Moyo na roho ya mwanadamu vimeshikwa katika mkono wa Mungu, na maisha yote ya mwanadamu yanatunzwa machoni mwa Mungu. Haijalishi kama unayaamini mambo haya au la, vitu vyote, vilivyo hai au vilivyokufa, vitahamishwa, vitabadilika, vitafanywa vipya, na kutoweka kulingana na mawazo ya Mungu. Hivi ndivyo Mungu anavyotawala juu ya kila kitu.
Usiku uingiapo kwa utulivu, mwanadamu huwa hafahamu, kwani moyo wa mwanadamu hauwezi kujua jinsi giza linapokaribia au linakotoka. Usiku unapotoweka polepole, mwanadamu anakaribisha mwanga wa mchana, lakini moyo wa mwanadamu haufahamu ilikotoka nuru hii na jinsi gani nuru yenyewe imeliondoa giza la usiku. Mabadiliko kama haya ya kawaida ya mchana na usiku humpitisha mwanadamu katika kipindi kimoja baada ya kingine, kupita katika nyakati, wakati huu wote ikihakikisha kwamba kazi ya Mungu na mpango wake unafanywa wakati wa kila kipindi na katika nyakati zote. Mwanadamu alitembea katika enzi nyingi na Mungu, lakini bado mwanadamu hafahamu kwamba Mungu ndiye kiongozi wa hatima ya mambo yote na viumbe hai na pia hafahamu jinsi Mungu hupanga na kuongoza mambo yote. Hili ni jambo ambalo limekwepa ufahamu wa binadamu tangu enzi za kale mpaka leo.
kutoka kwa "Mungu Ndiye Chanzo cha Uhai wa Mwanadamu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Tangu wakati wa uumbaji, nilianza uamuzi wa mapema na uteuzi wa kundi hili la watu—lenu nyinyi, kundi hili leo. Tabia yako, uhodari, umbo, ukomavu, familia uliyozaliwa ndani, kazi yako, ndoa—kila kitu chako, hata rangi ya nywele zako, ngozi yako, na tarehe yako ya kuzaliwa—vyote hivi vimepangiliwa kwenye mkono Wangu. Chochote unachofanya na yeyote unayekutana naye kila siku vyote vinategemea mpangilio Wangu, sisemi chochote kuhusu kitakachokuleta mbele yangu Mimi leo, ambacho hasa ni maudhui ya mpangilio Wangu. Usijisababishie mahangaiko wewe mwenyewe, lakini endelea kwa utulivu.
kutoka Matamshi na Ushuhuda wa Kristo Mwanzoni
Tangu Alipoanza uumbaji wa viumbe vyote, nguvu za Mungu zilianza kuonyeshwa na zikaanza kufichuliwa, kwani Mungu alitumia maneno kuumba vitu vyote. Haijalishi ni njia gani Alitumia, haijalishi ni kwa nini Aliviumba, viumbe vyote viliumbwa na kusimama imara na kuwepo kwa sababu ya matamshi ya Mungu, na haya ndiyo mamlaka ya kipekee ya Muumba. Kwenye muda kabla ya mwanadamu kuumbwa ulimwenguni, Muumba alitumia nguvu na mamlaka Yake kuumba viumbe vyote kwa minajili ya mwanadamu, na Akatumia mbinu za kipekee kutayarisha mazingira yanayofaa kuishi mwanadamu. Kwa yote Aliyoyafanya, ilikuwa ni kwa kumtayarishia mwanadamu ambaye hivi karibuni angepokea pumzi Zake. Hivi ni kusema kwamba, kwenye muda ule kabla ya mwanadamu kuumbwa, mamlaka ya Mungu yalionyeshwa kupitia kwenye viumbe vyote tofauti na mwanadamu, na vitu vikubwa kama vile mbingu, nuru, bahari, na ardhi, na vile vilivyo vidogo kama vile wanyama na ndege, pamoja na wadudu na vijiumbe vyote vya kila aina, zikiwemo vimelea mbalimbali visivyoonekana kwa macho ya kawaida. Kila mojawapo kilipewa maisha kwa matamshi ya Muumba, na kila kiumbe mojawapo kilizaana kwa sababu ya matamshi ya Muumba na kila kimojawapo kiliishi chini ya ukuu wa Muumba kwa sababu ya matamshi ya Muumba. Ingawaje hawakupokea pumzi za Muumba, bado walionyesha maisha na nguvu walizopewa na Muumba kupitia kwa mifumo na miundo yao mbalimbali; ingawaje hawakupokea uwezo wa kuongea aliopewa mwanadamu na Muumba, kila kimojawapo kilipokea njia ya kuelezea maisha yao ambayo walipewa na Muumba, na ambayo ilitofautiana na ile lugha ya Mwanadamu. Mamlaka ya Muumba hayatoi tu nguvu za maisha kwenye vifaa vinavyoonekana kuwa tuli, ili visiwahi kutoweka, lakini, vilevile, hupatia silika ya kuzaana na kuongezeka kwa kila kiumbe hai, ili visiwahi kutoweka, na ili kizazi baada ya kizazi, vitaweza kupitisha sheria na kanuni za kuishi walizopewa na Muumba. Namna ambavyo Muumba anatilia mkazo mamlaka Yake haikubaliani kwa lazima na mtazamo wa mambo makubwamakubwa au madogomadogo, na haiwekewi mipaka ya umbo lolote; Anaweza kuamuru utendaji mambo katika ulimwengu na kushikilia ukuu juu ya maisha na kifo cha viumbe vyote, na, vilevile, Anaweza kushughulikia viumbe vyote ili viweze kumhudumia Yeye; Anaweza kusimamia kazi zote za milima, mito, na maziwa, na kutawala viumbe vyote ndani yake, na, zaidi ya hayo, Anaweza kutoa kile ambacho kinahitajika na viumbe vyote. Haya ndiyo maonyesho ya mamlaka ya pekee ya Muumba miongoni mwa viumbe vyote mbali na mwanadamu. Maonyesho kama hayo si tu ya maisha tunayoishi, na hayatawahi kusita, au kupumzika, na hayawezi kubadilishwa au kuharibiwa na mtu yeyote au kitu chochote, wala hayawezi kuongezwa au kupunguzwa na mtu yeyote au kitu chochote—kwani hamna kile kinachoweza kubadilisha utambulisho wa Muumba, na, hivyo basi, mamlaka ya Muumba hayawezi kubadilishwa na kiumbe chochote kilichoumbwa, na hayawezi kufikiwa na kiumbe chochote-ambacho hakikuumbwa.
kutoka kwa "Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee I" katika Neno Laonekana katika Mwili
Hatima za binadamu na zile za ulimwengu zimeingiliana kwa ndani na ukuu wa Muumba, zimefungamanishwa na haziwezi kutenganishwa na mipango ya Muumba; na hatimaye, haziwezi kutenganishwa na mamlaka ya Muumba. Kupitia kwenye sheria za mambo yote binadamu huja kuelewa mipango ya Muumba na ukuu Wake; kupitia kwenye sheria za namna ya kuishi ambazo anaona katika utawala wa Muumba; kutoka kwenye hatima za mambo yote anapata hitimisho kuhusu njia ambazo Muumba huonyesha ukuu Wake na kuvidhibiti; na kwenye mzunguko wa maisha ya binadamu na mambo yote ambayo binadamu kwa kweli hupitia ile mipango na mipangilio ya Muumba kwa mambo yote na kwa viumbe vyote vilivyo hai na anashuhudia kwa kweli namna ambavyo mipango na mipangilio hiyo inavyozidi sheria zote za nchi, kanuni, na taasisi, mamlaka na nguvu zote nyingine. Kwa mujibu wa haya, binadamu wanashawishiwa kutambua kwamba, ukuu wa Muumba hauwezi kukiukwa na kiumbe chochote kilichoumbwa, kwamba hakuna nguvu zinazoweza kuharibu au kubadilisha matukio na mambo yaliyoamuliwa kabla na Muumba. Ni kupitia kwenye sheria na kanuni hizi takatifu ambapo binadamu na viumbe vyote wanaweza kuishi na kuzalisha, kizazi baada ya kizazi. Je, huu si mfano halisi wa mamlaka ya Muumba?
kutoka kwa "Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III" katika Neno Laonekana katika Mwili
(Fungu Lililochaguliwa la Neno la Mungu)
Mungu Anaongoza Majaliwa ya Wanadamu Wote
Kama washiriki wa jamii ya binadamu na Wakristo wamchao Mungu, ni jukumu na wajibu wa sisi wote kutoa akili na mwili wetu kwa kutimiza agizo la Mungu, kwani uhai wetu wote ulitoka kwa Mungu, na upo kwa sababu ya ukuu wa Mungu. Kama akili zetu na miili yetu si kwa ajili ya agizo la Mungu na si kwa sababu ya kusudi la haki la mwanadamu, basi nafsi zetu hazina thamani kwa wale waliokufa kishahidi kwa ajili ya agizo la Mungu, na thamani ndogo zaidi kwa Mungu, aliyetupa kila kitu.
Mungu aliumba dunia hii, Aliumba mwanadamu huyu, na zaidi ya hayo Alikuwa muasisi wa utamaduni wa zamani wa Giriki na ustaarabu wa binadamu. Ni Mungu tu anayemfariji huyu mwanadamu, na ni Mungu tu anayemtunza mwanadamu huyu usiku na mchana. Ukuaji na maendeleo ya binadamu hayatengani na ukuu wa Mungu, na historia na mustakabali wa mwanadamu ni zisizochangulika kutoka kwa miundo ya Mungu. Kama wewe ni Mkristo wa kweli, basi hakika utaamini kwamba kupanda na kushuka kwa nchi ama taifa lolote hufanyika kulingana na miundo ya Mungu. Mungu pekee hujua majaliwa ya nchi ama taifa, na Mungu pekee hudhibiti mwendo wa huyu mwanadamu. Iwapo mwanadamu anataka kuwa na majaliwa mazuri, iwapo nchi inataka kuwa na majaliwa mazuri, basi lazima mwanadamu ampigie Mungu magoti kwa ibada, atubu na kukiri mbele ya Mungu, la sivyo majaliwa na hatima ya mwanadamu hayataepuka kumalizika kwa janga.
Angalia nyuma wakati wa safina ya Nuhu: Wanadamu walikuwa wapotovu sana, walikuwa wamepotea kutoka katika baraka za Mungu, hawakuwa wanatunzwa na Mungu tena, na walikuwa wamepoteza ahadi za Mungu. Waliishi gizani, bila mwangaza wa Mungu. Hivyo wakawa waasherati kwa asili, wakajiachilia katika mkengeuko wa kutisha. Watu kama hao hawangeweza tena kupokea ahadi za Mungu; hawakufaa kushuhudia uso wa Mungu, wala kusikia sauti ya Mungu, kwani walikuwa wamemwacha Mungu, kuweka kando yote Aliyowapa, na kusahau mafunzo ya Mungu. Mioyo yao ilipotea mbali zaidi na zaidi na Mungu, na ilivyofanya hivyo, wakawa wapotovu zaidi ya mantiki na ubinadamu wote na wakazidi kuwa waovu. Hivyo walikaribia kifo zaidi, na kukabiliwa na ghadhabu na adhabu ya Mungu. Ni Nuhu tu aliyemwabudu Mungu na kuepukana na uovu, na hivyo aliweza kusikia sauti ya Mungu, na kusikia maelekezo ya Mungu. Alijenga safina kulingana na maelekezo ya neno la Mungu, na kukusanya aina yote ya viumbe hai. Na kwa njia hii, wakati kila kitu kilikuwa kimetayarishwa, Mungu aliangamiza dunia. Nuhu tu na wanachama saba wa familia yake walinusurika maangamizi, kwani Nuhu alimwabudu Yehova na kuepukana na uovu.
Kisha angalia enzi ya sasa: Hawa watu wenye haki kama Nuhu, ambao wangeweza kumwabudu Mungu na kuepuka uovu, wamekoma kuwepo. Lakini bado Mungu ana fadhili kwa mwanadamu huyu, na Anamsamehe mwanadamu wakati huu wa enzi ya mwisho. Mungu anawatafuta wanaomtaka Yeye ajitokeze. Anawatafuta wale wanaoweza kuyasikia maneno Yake, wale ambao hawajasahau agizo Lake na wanatoa mioyo na miili yao Kwake. Anawatafuta wale walio watiifu kama watoto wachanga mbele Yake, na hawampingi. Kama hujazuiliwa na nguvu zozote katika ibada yako Kwake, basi Mungu atakutazama na neema, na kukupea baraka Zake. Kama wewe ni wa daraja la juu, wa sifa ya heshima, aliyemiliki maarifa mengi, mmiliki wa mali nyingi, na kuungwa mkono na watu wengi, lakini mambo haya hayakuzuii kuja mbele za Mungu kuukubali wito Wake na agizo Lake, kufanya kile Mungu anachokuambia ufanye, basi yote unayoyafanya yatakuwa yenye umuhimu zaidi duniani na yenye haki zaidi ya binadamu. Ukiukataa wito wa Mungu kwa sababu ya hadhi yako na malengo yako mwenyewe, yote utakayoyafanya yatalaaniwa na hata kudharauliwa na Mungu. Labda wewe ni rais, ama mwanasayansi, ama mchungaji, ama mzee, lakini bila kujali ukuu wa ofisi yako, ukitegemea maarifa yako na uwezo katika shughuli zako, basi daima utakuwa wa kushindwa na kamwe utanyimwa baraka za Mungu, kwa sababu Mungu hakubali chochote unachofanya, na Hakubali kwamba kazi yako ni yenye haki, wala kukubali kwamba unafanya kazi kwa msaada wa mwanadamu. Atasema yote unayofanya, ni ya kutumia maarifa na nguvu za mwanadamu kumvulia mwanadamu ulinzi wa Mungu na kumnyima baraka za Mungu. Atasema kuwa unamwongoza mwanadamu kuelekea gizani, kuelekea kifo, na kuelekea mwanzo wa kuwepo bila mipaka ambapo mwanadamu amempoteza Mungu na baraka Zake.
Kutoka wakati mwanadamu kwanza alikuwa na sayansi ya jamii, akili yake ilishughulishwa na sayansi na maarifa. Kisha sayansi na maarifa vikawa vyombo vya kutawala mwanadamu, na hapakuwa tena na nafasi ya kutosha kumwabudu Mungu, na hapakuwa tena na mazingira mazuri ya kumwabudu Mungu. Nafasi ya Mungu ikashuka hata chini zaidi moyoni mwa mwanadamu. Dunia moyoni mwa mwanadamu bila nafasi ya Mungu ni giza, tupu bila matumaini. Na hivyo kukatokea wanasayansi wa jamii, wataalamu wa historia na wanasiasa wengi kueleza nadharia ya sayansi ya jamii, nadharia ya mageuko ya binadamu, na nadharia nyingine zinazopinga ukweli kwamba Mungu alimuumba mwanadamu, kujaza moyo na akili ya mwanadamu. Na kwa njia hii, wanaoamini kwamba Mungu aliumba kila kitu wanakuwa wachache zaidi, na wale wanaoamini nadharia ya mageuko wanakuwa hata wengi kwa nambari. Watu zaidi wanachukulia rekodi za kazi ya Mungu na maneno Yake wakati wa enzi ya Agano la Kale kuwa hadithi na hekaya. Kwa mioyo yao, watu wanakuwa wasiojali heshima na ukubwa wa Mungu, kwa imani kwamba Mungu yupo na anatawala kila kitu. Kusalia kwa mwanadamu na majaliwa ya nchi na mataifa si muhimu kwao tena. Mwanadamu anaishi katika dunia tupu akijishughulisha tu na kula, kunywa, na ufuatiliaji wa furaha. … Watu wachache wanashughulika kutafuta Afanyapo Mungu kazi Yake leo, ama kutafuta jinsi Anavyoongoza na kupanga majaliwa ya mwanadamu. Na kwa njia hii, ustaarabu wa ubinadamu bila fahamu ukawa huwezi kukutana na matakwa ya mwanadamu hata zaidi, na hata kuna watu zaidi wanaohisi kwamba, kuishi kwa dunia kama hii, wanayo furaha ya chini kuliko watu walioenda. Hata watu wa nchi zilizokuwa na ustaarabu wa juu wanaeleza malalamiko haya. Kwani bila mwongozo wa Mungu, bila kujali jinsi viongozi na wanasosiolojia wanatafakari kuhifadhi ustaarabu wa binadamu, haina mafanikio. Hakuna anayeweza kujaza utupu kwa moyo wa mwanadamu, kwani hakuna anayeweza kuwa uhai wa mwanadamu, na hakuna nadharia ya kijamii inayoweza kumwokoa kutokana na utupu unaomtesa. Sayansi, maarifa, uhuru, demokrasia, wasaa wa mapumziko, faraja, haya yote ni mapumziko ya muda, Hata na mambo haya, mwanadamu hataepuka kufanya dhambi na kuomboleza udhalimu wa jamii. Mambo haya hayawezi kupunguza tamaa ya mwanadamu na hamu ya kuchunguza. Kwa sababu mwanadamu aliumbwa na Mungu na kafara na uchunguzi usio na sababu wa mwanadamu vitamwongoza tu kwa dhiki zaidi. Mwanadamu daima atakuwa katika hali ya hofu isiyoisha, hatajua jinsi ya kuukabili mustakabali wa wanadamu, ama jinsi ya kuikabili njia iliyo mbele. Mwanadamu atakuja hata kuogopa sayansi na elimu, na kuhofia hata zaidi utupu ulio ndani yake sana. Duniani humu, bila kujali kama unaishi katika nchi huru ama isiyo na haki za binadamu, huwezi kabisa kuponyoka majaliwa ya mwanadamu. Kama wewe ni kiongozi ama anayeongozwa, huwezi kabisa kuponyoka hamu ya kuchunguza majaliwa, siri na majaliwa ya mwanadamu. Chini ya hayo, huna uwezo wa kutoroka hisia ya utupu inayotatiza. Matukio kama haya, yaliyo kawaida kwa wanadamu wote, yanaitwa matukio ya kijamii na wanasosiolojia, lakini hakuna mtu mkubwa anayeweza kuja mbele kutatua shida kama hizi. Mwanadamu, hata hivyo, ni mwanadamu. Nafasi na maisha ya Mungu hayawezi kubadilishwa na mwanadamu yeyote. Mwanadamu hahitaji tu jamii iliyo na haki, ambapo kila mtu analishwa vyema na ana uhuru na usawa, lakini wokovu wa Mungu na Yeye kuwapa uhai. Wakati tu mwanadamu atapokea wokovu wa Mungu na kupatiwa uhai na Yeye ndipo mahitaji, hamu ya kuchunguza, na utupu wa kiroho wa mwanadamu utaweza kutatuliwa. Iwapo watu wa nchi ama taifa hawawezi kupokea wokovu na utunzaji wa Mungu, basi nchi ama taifa kama hilo litatembelea njia inayoelekea uharibifuni, inayoelekea gizani, na litaangamizwa na Mungu.
Labda nchi yako inafanikiwa sasa, lakini ukiruhusu watu wako kupotea kutoka kwa Mungu, basi nchi yako itazidi kujipata bila baraka za Mungu. Ustaarabu wa nchi yako utazidi kukanyagiwa chini, na kabla ya muda mrefu watu watamwasi Mungu na kulaani Mbingu. Na hivyo majaliwa ya nchi pasipo kujua yataletwa kwa uharibifu. Mungu ataziinua nchi zenye nguvu ili kukabiliana na nchi hizo zilizolaaniwa na Mungu, na anaweza hata kuzifuta kutoka uso wa dunia. Kupanda na kushuka kwa nchi ama taifa kunategemea kama viongozi wao wanamwabudu Mungu, na kama wanawaongoza watu wao karibu na Mungu na kumwabudu. Lakini, kwa hii enzi ya mwisho, kwa sababu wale wanaomtafuta Mungu kwa kweli na kumwabudu wanazidi kuwa wachache, Mungu anaweka fadhili ya pekee juu ya nchi ambapo Ukristo ni dini ya serikali. Anazikusanya pamoja kuunda kambi ya haki kiasi ya dunia, wakati nchi zikanazo Mungu ama zile zisizomwabudu Mungu wa kweli zinakuwa wapinzani wa kambi ya haki. Kwa njia hii, Mungu hana tu mahali miongoni mwa wanadamu pa kufanyia kazi Yake, lakini pia Anapata nchi zinazoweza kutumia mamlaka ya haki, ili kulazimisha mipaka na vikwazo kwa nchi hizo zinazompinga Mungu. Lakini licha ya hayo, bado hakuna watu zaidi wanaokuja mbele kumwabudu Mungu, kwa sababu mwanadamu amepotea mbali sana kutoka Kwake, na Mungu hajakuwa kwa mawazo ya mwanadamu kwa muda mrefu. Kunabakia tu duniani nchi zinazotumia haki na kupinga udhalimu. Lakini hii ni mbali na matakwa ya Mungu, kwani hakuna kiongozi wa nchi yoyote atamruhusu Mungu kuongoza watu wake, na hakuna chama cha kisiasa kitakachokusanya pamoja watu wake kumwabudu Mungu; Mungu amepoteza mahala Pake halali kwa mioyo ya nchi zote, taifa, chama tawala, na hata kwa moyo wa kila mtu. Ingawa nguvu za haki ziko kwa dunia hii, utawala ambapo Mungu hana mahali kwa moyo wa mwanadamu ni dhaifu. Bila baraka ya Mungu, uwanja wa kisiasa utaanguka katika vurugu na wenye kuweza kudhuriwa na mashambulizi. Kwa mwanadamu, kuwa bila baraka ya Mungu ni kama kukosa mwanga wa jua. Bila kujali jinsi viongozi wanafanya mchango kwa watu wao kwa uangalifu, bila kujali idadi ya mikutano ya haki wanadamu wanafanya pamoja, hakuna kati ya hii itakayorejesha mambo ama kubadilisha majaliwa ya mwanadamu. Mwanadamu anaamini kuwa nchi ambapo watu wanalishwa na kuvalishwa nguo, ambapo watu wanaishi kwa amani, ni nchi nzuri, na iliyo na uongozi mzuri. Lakini Mungu hafikirii hivyo. Anaamini kuwa nchi ambapo hakuna mtu anayemwabudu ndiyo Atakayoiangamiza. Njia ya mwanadamu ya kufikiria ni tofauti kabisa na ya Mungu. Kama mkuu wa nchi hamwabudu Mungu, basi majaliwa ya nchi hii itakuwa ya kutisha, na nchi haitakuwa na majaliwa.
Mungu hashiriki katika siasa za mwanadamu, lakini majaliwa ya nchi ama taifa inadhibitiwa na Mungu, Mungu anadhibiti dunia hii na ulimwengu mzima. Majaliwa ya mwanadamu na mpango wa Mungu yanashikamana kwa undani, na hakuna mwanadamu, nchi ama taifa limetolewa kwa mamlaka ya Mungu. Iwapo mwanadamu anatamani kujua majaliwa yake, basi lazima aje mbele ya Mungu. Mungu atawafanya wanaomfuata na kumwabudu kufanikiwa, na Atashusha na kuwaangamiza wale wanaompinga na kumkataa.
Kumbuka tukio katika Biblia ambapo Mungu aliangamiza Sodoma, na fikiria pia jinsi mke wa Loti alivyokuwa nguzo ya chumvi. Fikiria nyuma jinsi watu wa Ninawi walitubu dhambi zao kwa gunia na majivu, na kumbuka kilichofuata baada ya Wayahudi kumsulubisha Yesu miaka 2,000 iliyopita. Wayahudi walitolewa Israeli na kukimbilia nchi duniani kote. Wengi waliuwawa, na taifa lote la Kiyahudi lilikabiliwa na uharibifu wa kipekee. Walimsulubisha Mungu—wakafanya uhalifu wa kuchukiza—na kuchochea tabia ya Mungu. Walifanywa kulipa kwa ajili ya walichofanya, walifanywa kukubali matokeo ya vitendo vyao. Walimlaani Mungu, walimkataa Mungu, na hivyo walikuwa na majaliwa moja pekee: kuadhibiwa na Mungu. Haya ndiyo matokeo machungu na maafa ambayo viongozi wao waliletea nchi na taifa lao.
Leo, Mungu amerudi duniani kufanya kazi Yake. Atasimama kwanza kwa mkutano mkubwa wa viongozi madikteta: Uchina, ngome kali ya ukanaji Mungu. Mungu amepata kundi la watu kwa hekima na nguvu Zake. Wakati huu, Anawindwa na chama tawala cha Uchina kwa kila namna na kukabiliwa na mateso makubwa, bila mahala pa kupumzisha kichwa Chake na kutoweza kupata makazi. Licha ya haya, Mungu bado anaendelea kufanya kazi Aliyonuia kufanya: Anatamka sauti Yake na kueneza injili. Hakuna anayeweza kuelewa uweza wa Mungu. Uchina, nchi inayomchukulia Mungu kama adui, Mungu hajawahi kukoma kazi Yake. Badala yake, watu zaidi wamekubali kazi na neno Lake, kwani Mungu anafanya yote Awezayo kuokoa kila mshiriki wa ubinadamu. Tunaamini hakuna nchi ama nguvu inayoweza kuzuia yale anayotaka kutimiza Mungu. Wale wanaozuia kazi ya Mungu, wanaopinga neno la Mungu, kuvuruga na kudhoofisha mpango wa Mungu hatimaye wataadhibiwa na Mungu. Anayeasi kazi ya Mungu atatumwa kuzimu; nchi yoyote inayoasi kazi ya Mungu itaangamizwa; taifa lolote linaloinuka kupinga kazi ya Mungu litafutwa kutoka dunia hii, na litakoma kuwepo. Nahimiza watu wa mataifa, nchi na hata viwanda vyote kusikiza sauti ya Mungu, kutazama kazi ya Mungu, kuzingatia majaliwa ya mwanadamu, hivyo kumfanya Mungu kuwa mtakatifu zaidi, wa heshima zaidi, wa juu zaidi na chombo cha pekee cha kuabudu miongoni mwa wanadamu, na kuruhusu wanadamu wote kuishi chini ya baraka za Mungu, kama tu ukoo wa Ibrahimu ulivyoishi chini ya ahadi ya Yehova, na kama tu Adamu na Hawa, walioumbwa awali na Mungu, walivyoishi kwa Bustani ya Edeni.
Kazi ya Mungu ni kama mawimbi yanayotapakaa kwa nguvu. Hakuna anayeweza kumweka kizuizini, na hakuna anayeweza kusimamisha nyayo Zake. Wale tu wanaosikiza maneno Yake kwa makini, na wanaomtafuta na kuwa na kiu naye, wanaweza kufuata nyayo Zake na kupokea ahadi Zake. Wasiofanya hivyo watakabiliwa na maafa makuu na adhabu inayostahili.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Jumatano, 27 Februari 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kusudi la Kuwasimamia Binadamu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kusudi la Kuwasimamia Binadamu

Ikiwa watu wanaweza kweli kuielewa kikamilifu njia sahihi ya maisha ya binadamu na vilevile kusudi la usimamizi wa Mungu wa binadamu, wasingeshikilia mategemeo yao ya baadaye na majaliwa yao binafsi kama hazina mioyoni mwao. Wasingetamani tena kuwatumikia wazazi wao ambao ni wabaya zaidi kuliko nguruwe na mbwa. Je, mategemeo ya baadaye na majaliwa ya mwanadamu si kabisa kile kinachodaiwa nyakati za sasa kuwa “wazazi” wa Petro? Yamekuwa kama tu mwili na damu ya mwanadamu. Je, hatima, mategemeo ya baadaye ya mwili yatakuwa ni kumwona Mungu wakati ukiwa hai, au kwa roho kukutana na Mungu baada ya kifo? Je, mwili kesho utaishia katika tanuu kubwa kama katika taabu, au utakuwa katika kuteketezwa kwa moto? Je, maswali kama haya yanayohusu iwapo mwili wa mwanadamu utahimili taabu au mateso ni habari kubwa sana ambayo kila mtu sasa katika mkondo huu ambaye ana ubongo na akili yake iko sawa anahangaika zaidi nayo? (Hapa, kuhimili mateso hurejelea kupokea baraka; kuteseka humaanisha kwamba majaribu ya siku zijazo ni yenye manufaa kwa hatima ya mwanadamu. Taabu hurejelea kushindwa kusimama imara, au kudanganywa; au, humaanisha kwamba mtu anakabiliana na hali ya hatari ya bahati mbaya katikati ya majanga na maisha yake yanakuwa magumu kuendelea nayo, na kwamba hakuna hatima nzuri kwa roho.) Watu wanajitayarisha na mantiki timamu lakini pengine kile wanachofikiri hakifanani kabisa na kile ambacho mantiki yao inapaswa kutayarishwa nayo. Hii ni kwa sababu ni wajinga kiasi na wanafuata vitu bila kufikiri. Wote wanapaswa kuwa na uelewe wa kina wa kile ambacho wanapaswa kuingia kwacho, na kwa mahususi wanapaswa kutatua kile wanachopaswa kuingia kwacho wakati wa mateso (yaani, wakati wa utakasaji wa tanuu), na kile wanachopaswa kutayarishwa nacho katika jaribu la moto. Usiwatumikie wazazi wako siku zote (kumaanisha mwili) ambao ni sawa na nguruwe na mbwa, na ni wabaya zaidi kuliko chungu na wadudu. Kuna haja gani ya kuteseka juu ya hilo, kufikiri sana, kuutesa ubongo wako? Mwili si wako, bali upo katika mikono ya Mungu ambaye Hakudhibiti wewe pekee bali pia Anamwamuru Shetani. (Kwa asili ilimaanisha kuwa ulikuwa wa Shetani. Kwa kuwa Shetani pia yupo mikononi mwa Mungu, ingeweza kuwekwa hivyo tu. Maana inashawishi zaidi kusema namna hiyo—inamaanisha kuwa wanadamu hawapo chini ya miliki ya Shetani kabisa, bali wapo mikononi mwa Mungu.) Unaishi chini ya mateso ya mwili, lakini je, mwili ni wako? Upo chini ya udhibiti wako? Kwa nini usumbuke kufikiri sana juu ya hilo? Kwa nini usumbuke sana kumsihi Mungu kwa ajili ya mwili wako uliooza ambao umeshahukumiwa zamani sana na kulaaniwa, vilevile kutiwa najisi na roho wachafu? Kwa nini usumbuke siku zote kwa kushikilia washirika wa Shetani karibu na moyo wako? Huna wasiwasi kwamba mwili unaweza kuharibu mategemeo yako halisi ya baadaye, matumaini mazuri, na hatima ya kweli ya maisha yako?
Njia ya leo si rahisi kuitembea. Mtu anaweza kusema kwamba ni vigumu kuipitia na ni adimu sana katika enzi zote. Hata hivyo, nani angeweza kufikiri kuwa mwili wa mwanadamu pekee unatosha kumwangamiza mara moja? Kazi leo hakika ni ya thamani kama vile mvua wakati wa majira ya kuchipua na ni ya thamani kama wema wa Mungu kwa mwanadamu. Hata hivyo, ikiwa mwanadamu hajui kusudi la kazi Yake leo au kuelewa kiini cha mwanadamu, inawezekanaje tunu na thamani yake vizungumziwe? Mwili si wa wanadamu wenyewe, hivyo kwa kweli hakuna mtu anayeweza kuona waziwazi hatima yake itakuwa wapi. Hata hivyo, unapaswa kujua vizuri kwamba Mungu wa uumbaji Atawarudisha binadamu, ambao waliumbwa, katika nafasi yao ya asili, na kurejesha sura yao ya asili kutoka wakati wa kuumbwa kwao. Atachukua tena kikamilifu pumzi Aliyompuliza ndani ya binadamu, na kuchukua tena mifupa na mwili wake na kurudisha vyote kwa Bwana wa viumbe. Atabadilisha na kufanya upya binadamu kikamilifu, na kuchukua tena kutoka binadamu urithi wote ambao kwa asili haukuwa wa binadamu, bali ulikuwa wa Mungu. Hatamkabidhi tena binadamu urithi huo. Maana hakuna hata kitu kimoja kati ya hivyo vilikuwa vya binadamu kwa asili. Atavichukua vyote tena—huu si uporaji usio wa haki, bali unakusudiwa kuirejesha mbingu na dunia katika hali yake ya asili, na kubadilisha na kumfanya upya binadamu. Hii ni hatima inayofaa kwa mwanadamu, ingawa pengine si kuichukua tena baada ya kuuadibu mwili kama watu wanavyofikiri. Mungu hataki mifupa ya mwili baada ya maangamizi yake, bali vitu vya asili katika mwanadamu ambavyo mwanzo vilikuwa vya Mungu. Hivyo, hatawaangamiza binadamu au kuuondoa kabisa mwili wa binadamu, maana mwili wa binadamu si mali binafsi ya mwanadamu. Badala yake, ni kiungo cha Mungu, ambaye anasimamia binadamu. Angewezaje kuuangamiza mwili wa binadamu ili Yeye “afurahi”? Je, wakati huu, kwa kweli umeachana na kila kitu cha huo mwili wako ambao hauna thamani hata ya senti moja? Kama ungeweza kuelewa asilimia thelathini ya kazi ya siku za mwisho (asilimia thelathini tu, yaani, kuifahamu kazi ya Roho Mtakatifu leo, vilevile kazi ya neno Mungu hufanya katika siku za mwisho), basi usingeweza kuendelea “kuutumikia” au “kuwa” na upendo kwa mwili wako kama unavyofanya leo, ambao umepotoka kwa miaka mingi. Unapaswa kuelewa kwa kina kwamba binadamu sasa wameendelea kwa hali ambayo haijawahi kutokea na hawataendelea tena kusonga mbele kama magurudumu ya historia. Mwili wako wa udongo umeshafunikwa na nzi tangu zamani, hivyo unawezaje kuwa na nguvu ya kurudisha nyuma magurudumu ya historia ambayo Mungu ameyawezesha kuendelea hadi siku hii ya leo? Unawezaje kufanya saa ya siku za mwisho ambayo ni kama bubu ipige tena na kuendelea kusogeza mikono yake kwa upande wa kulia? Unawezaje kuubadilisha upya ulimwengu ambao unaonekana kama umefunikwa na ukungu mzito? Je, mwili wako unaweza kufufua milima na mito? Je, mwili wako, ambao una kazi ndogo tu, unaweza kweli kurejesha ulimwengu wa binadamu ambao umekuwa ukiutamani? Unaweza kweli kuwaelimisha wadhuria wako kuwa “binadamu”? Unaelewa sasa? Mwili wako unamilikiwa na nini hasa? Makusudi halisi ya Mungu ya kumfinyanga mwanadamu, ya kumkamilisha mwanadamu, na ya kumbadilisha mwanadamu hayakuwa kukupatia nchi nzuri ya asili au kuleta pumziko la amani kwa mwili wa mwanadamu. Badala yake, ilikuwa ni kwa ajili ya utukufu Wake na ushuhuda Wake, kwa furaha bora ya binadamu hapo baadaye, na ili kwamba hivi karibuni waweze kufurahia pumziko. Bado, si kwa ajili ya mwili wako, maana mwanadamu ni mtaji wa usimamizi wa Mungu na mwili wa mwanadamu ni kiungo tu. (Mwanadamu ni kitu chenye roho na mwili, wakati mwili ni kitu kiharibikacho tu. Hii humaanisha kwamba mwili ni chombo kwa ajili ya mpango wa usimamizi.) Unapaswa kujua kwamba kuwakamilisha wanadamu, kuwatimiza wanadamu, na kuwapata wanadamu hakujaleta kitu chochote zaidi ya mapanga na maangamizi kwa mwili wao, na kumeleta mateso yasiyokoma, kuungua kwa moto, hukumu zisizokuwa na huruma, kuadibu, na laana, na vilevile majaribu yasiyokuwa na mipaka. Hicho ni kisa cha ndani na ukweli wa kazi ya kumsimamia binadamu. Hata hivyo, vitu hivi vyote vimelengwa dhidi ya mwili wa binadamu, na mikuki yote ya uhasama bila huruma inaelekezwa kwenye mwili wa binadamu (maana kwa asili binadamu hakuwa na hatia). Hayo yote ni kwa ajili ya utukufu na ushuhuda Wake, na kwa ajili ya usimamizi Wake. Hii ni kwa sababu kazi Yake si tu kwa ajili ya binadamu, bali ni kwa ajili ya mpango wote na kutimiza mapenzi Yake ya asili Alipomuumba binadamu. Kwa hiyo, pengine asilimia tisini ya kile ambacho watu wanapitia ni mateso na majaribu ya moto, lakini kuna siku chache sana tamu na za furaha au hata hakuna kabisa ambazo mwili wa mwanadamu umekuwa ukitamani, na hata hawawezi kufurahia nyakati za furaha katika mwili wakishinda jioni nzuri pamoja na Mungu. Mwili ni mchafu, hivyo kile ambacho mwili wa mwanadamu unakiona au unakifurahia si chochote bali ni adabu ya Mungu ambayo haipendwi na mwanadamu, na ni kana kwamba ulikuwa unakosa mantiki ya kawaida. Hii ni kwa sababu Atadhihirisha tabia Yake ya haki ambayo haipendwi na mwanadamu, haivumilii makosa ya mwanadamu, na huchukia kabisa maadui. Mungu hufichua waziwazi tabia Yake yote kupitia njia yoyote iwezekanayo, na hivyo Akihitimisha kazi ya vita Vyake na Shetani vya miaka elfu sita—kazi ya wokovu wa binadamu wote na maangamizi ya Shetani wa zamani!
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Jumamosi, 2 Februari 2019

Namna ya Kumridhisha Mungu katikati ya Majaribu

Sura ya 59. Namna ya Kumridhisha Mungu katikati ya Majaribu

Ninaibua maswali machache kwa tafakari yenu: Tangu mara ya mwisho tuliposema kwamba kutakuwa na miaka saba mingine ya majaribu makubwa, iwe ni kwa dhiki au majanga, je, mmegundua kusudi la Mungu kupitia kwa hayo? Ni asili gani ya binadamu mnaweza kuona katika mijibizo na mitazamo ya watu kwa miaka hii saba ya majaribu? Hili litachanganuliwa vipi? Fikirieni hilo. Ninazungumzia asili ya binadamu katika kila ushirika, kufikia chanzo, kuchanganua asili ya binadamu, na kuchanganua kiini. Ni juu yenu basi kuwasiliana ufahamu wenu kuhusu hizi mada.

Mnapaswa kuelewa kusudi la Mungu na ni lazima muijue asili ya binadamu kupitia hii miaka saba ya majaribu. Kwa hakika, kila sentensi ya Mungu ina kusudi Lake, ambamo mmefichwa ukweli. Bila kujali ni suala gani linafanyiwa ushirika, au ni ukweli gani unaoenyeshwa, ndani yake mna njia ambayo watu wanapaswa kupitia, matakwa ya Mungu kwa watu, na kusudi la Mungu kwa wanaomtafuta. Katika haya mazungumzo ya majaribu, dhiki, na hatimaye mateso, matakwa kwa watu na kusudi la Mungu pia vimo ndani. Watu, bila shaka, wanaonyesha hisia kwa mitazamo yao, kwa kuwa watu hawajaundwa kwa mbao; wako hai, na wanaonyesha hisia kwa kila kitu. Je, kuna maana kuchanganua ni hali gani za asili ya binadamu zinawakilishwa katika hisia za watu? Ina maana kushiriki kuihusu? Uchanganuzi utasaidia watu kuliona hilo wazi, kulijua wao wenyewe, na kujua vyema kabisa mioyoni mwao ili kwamba hatimaye wawe na njia mwafaka ya kuchagua. Ikiwa mtu amekanganyikiwa na hajui kusudi la Mungu, haelewi ukweli, na ana ufahamu mdogo kuhusu matakwa ya Mungu kwake na wajibu anaopaswa kutekeleza, au njia gani anapaswa kutembea, pengine mtu wa aina hii hatasimama imara. Kwa hivyo, inapaswa kujulikana ni njia gani inapaswa kutumiwa baadaye wakati wa majaribu mbalimbali.

Kila wakati majaribu ya miaka saba yanapotajwa, kuna watu wengi wanaohisi vibaya sana na kuvunjika moyo kusiko kwa kawida, na kuna watu wengine ambao hulalamika, na kuna mchanganyiko wa hisia. Ni dhahiri kutokana na hizi hisia kwamba watu sasa wanahitaji majaribu haya, wanahitaji aina hii ya dhiki na utakasaji. Watu humwamini Mungu kwa nia ya kutaka kupata baraka siku zijazo. Watu wote wana kusudi na tumaini hili. Hata hivyo, upotovu ndani ya asili ya binadamu ni lazima uondolewe kupit majaribu. Katika hali yoyote usiyoipita, ni katika hizi hali ambamo ni lazima usafishwe—huu ni mpango wa Mungu. Mungu anakutengenezea mazingira, Akikulazimisha usafishwe hapo ili ujue upotovu wako mwenyewe. Hatimaye unafika hatua ambapo unaona heri kufa na kuziacha njama na tamaa zako, na kutii mamlaka na mipango ya Mungu.

Hivyo ikiwa watu hawana miaka kadhaa ya usafishaji, ikiwa hawana kiwango fulani cha mateso, hawataweza kuepuka utumwa wa upotovu wa mwili katika mawazo na mioyo yao. Katika hali zozote zile bado ungali mtumwa wa Shetani, katika hali zozote bado ungali na tamaa zako mwenyewe, matakwa yako mwenyewe—ni katika hali hizi ambamo unapaswa kuteseka. Mafunzo yanaweza kupatikana tu katika mateso, yaani, kuweza kupata ukweli, na kuelewa kusudi la Mungu. Kwa kweli, ukweli mwingi unafahamika katika uzoefu wa majaribu makali. Hakuna asemaye kuwa kusudi la Mungu linajulikana, kwamba uweza na busara Yake vinafahamika, kwamba tabia ya haki ya Mungu inaonekana katika mazingira ya utulivu au katika hali zinazofaa. Hilo haliwezekani!

Mungu ametayarisha mazingira mwafaka ambamo Anawafanya watu kuwa wakamilifu, ila haijulikani kwa yeyote ni kwa nini Mungu anaweza kutaka kuwajaribu watu, kuwatakasa. Nyinyi nyote mnasema, “Mungu anawependaje wanadamu kwamba Anaweza kutayarisha miaka saba ya majaribu kuwatakasa watu na kuwafanya safi! Ni mvumilivu kiasi gani! Ni mwenye kuonyesha huruma kiasi gani!” Haina haja uyaseme haya, kila mmoja anaelewa mafundisho, lakini kwa hakika hakuna yeyote anayeifahamu hali halisi Je, miaka saba ya Mungu ya majaribu, miaka saba ya kazi ni ya nini? Bila shaka, inahitajika ili kwamba kazi Yake ifanyike. Hata bila kukuokoa, bado kuna upendo, sawa? Anapokuokoa, unasema, “Haya ni mapenzi aliyonayo Mungu kwetu, hii ni huruma Yake.” Je, Asingekuwa ametayarisha hii miaka saba ya majaribu, na kukamilisha kazi mara moja, bado kusingekuwepo upendo? Je, ingelikuwa miaka miwili ya majaribu, au mwaka mmoja, au siku ingalifika mara moja, je, hayo yasingekuwa mapenzi na huruma? Si kama unavyodhani: Miaka saba ya majaribu ni utakaso wa Mungu kwetu, ni kiwango Anachotupenda: ni lazima tutii. Unasema haya wakati tu hakuna njia nyingine. Hili linadhihirisha nini? Linadhihirisha uhasi, linadhihirisha lawama, na linadhihirisha kukosa njia mbadala na kukata tamaa. Mungu alisema kwamba kutakuwa na miaka saba mingine. Wacha iwe miaka saba basi. Kisha unakurupuka na kusema maneno mazuri: Mungu, Unatupenda; Mungu, ni kwa ajili ya kututakasa. Bila miaka saba ya majaribu, je, huo usingelikuwa mwisho wetu? Kusingelikuwa na fursa. Watu wengine wanatamani kubarikiwa sasa hivi. Hiyo inaweza kuwa faida halisi! Mtu kama huyo hajali kitu kingine chochote kile. Mtu kama huyu hafai hata kwa senti moja. Kuna kazi ya vitendo katika hii miaka saba. Je, haijasemwa awali kwamba maneno mengine ni njia, lakini vilevile ni ukweli? Hakuna kipengele ambacho ni maneno tu bila matendo. Kila kipengele kina dhima. Aidha, kama aionavyo mwanadamu, takribani kila kipengele kina njia, lakini njia hii si ya kukurairai, si ya kukudanganya. Badala yake ni mazingira ya kweli, hali halisi Hakuna njia mwafaka kuliko hii. Baada ya kusikia maneno haya, watu wengine hufikiri: Ikiwa ni kama usemavyo, hii miaka saba inapoisha, ni nani anaweza kutambua umesalia muda kiasi gani! Kutokana na mijibizo ya watu inaonekana kuwa asili ya binadamu imewekwa kwa namna kwamba baada ya kukumbana na majaribu ya mateso, kupokea uchungu mwilini, anataka kuuepuka na kuukataa. Hakuna hata mtu mmoja hujitokeza na kuchukua hatua ya kudai: Mungu, nipe majaribu fulani ya kuteseka, nipatie dhiki fulani. Mungu, nipatie taabu zaidi. Hili linadhihirisha kuwa kiasilia watu hawapendi ukweli. Iwe ni kusudi la Mungu au la, au inafaidi watu vipi, haijalishi ni nzuri kiasi gani, watu wote hukataa hali yoyote inayoiletea miili yao machungu au ile isiyoafiki matamanio yao. Kuna watu wasemao: “Sipingi. Nilifanya uamuzi zamani kuyatoa maisha yangu yote kwa Mungu. Nina furaha kabisa haijalishi ni miaka mingapi, na nitamtumikia Mungu kwa moyo. Sina lawama. Haijalishi ninakumbana na majaribu gani, haijalishi ninakutana na mateso gani, iwe ni kutelekezwa na familia au maumivu ya ugonjwa, nitafuata hadi mwisho.” Huku kutokuwa na lawama kwako pia ni aina ya hali hasi, kwa sababu kila wakati unapokumbana na kitu chochote, kila wakati unaposemewa maneno, kwa hakika huelewi maana iliyo ndani. Hii “sina mjibizo” unayoisema kwa hivyo si kingine bali ni kutojali, njia wakati ambapo hakuna njia nyingine. Hakuna jingine la kufanya ila hili, kwa hivyo unajilazimisha kufuata hata wakati ambapo hauko radhi. Kwa vyovyote vile hakuna awezaye kufaulu kuepuka miaka saba ya majaribu. Hata hivyo, hii ni tofauti na wewe kutaka kutoroka. Ungetamani kuepuka lakini huwezi. Hili ni jambo la asili ya mwanadamu. Lifikirie. Je, ndivyo ilivyo? Watu wengine wanahisi: Nilipokumbana na tukio kama hili miaka kumi iliyopita, daima nilifuata, na niliteseka sana, kwa hivyo ninaweza kuendelea kuvumilia kwa miaka michache. Kutafuta kwenu kwa kusudi la Mungu kumekanganyikiwa na hamjakutilia maanani. Hivyo, ikiwa kwa ndani hujayatii mapenzi ya Mungu, basi umeyasaliti na kukana mapenzi ya Mungu. Ijapokuwa huna hali hii, na hujafanya jambo hili, hizi dalili, haya mambo yaliyo ndani yako, yanamkana Mungu, kwa sababu unachokifiria na kutarajia kwa ndani sicho Mungu anachokihitaji. Aidha kwa hakika humsifu Mungu kutoka ndani ya moyo wako kwa yote Anayohitaji kutoka kwako na yote Anayofanya, iwe ni njia, au kile ulichoambiwa.

Na kwa kila kitu Mungu ambacho anawataka watu wafanye, chochote Mungu alichowapangia watu kulingana na mahitaji yao, asili ya binadamu ni kukikataa, kukosa kukikubali. Haijalishi unautangaza vipi msimamo wako, au iwe una ufahamu kidogo, kwa vyovyote vile, ufahamu wako wa mafundisho hauwezi kutatua kilicho katika asili yako. Kwa hivyo ninasema kwamba watu wengi wanazungumzia vitu vizuri katika mafundisho, na kusema maneno ya juujuu kuyastahimili. Hatimaye, japo, katika maombi wanasema: Nimepitia kwa ufanisi miaka mingi sana. Miaka saba si miaka mingi na wala si miaka michache. Tazama ninavyozeeka, jinsi afya yangu ilivyoharibika, na kwamba sina familia nzuri. Nimeandamana na Wewe miaka hii yote, nifanya bidii hata bila malipo, nimechoka ijapokuwa sijafanya kazi kwa bidii. Hata kama Utaipunguza hata kwa miaka michache, nifanyie hisani mara hii moja! Unajua udahaifu wa watu… Kwa kuomba maneno haya, ni kama kuna utiifu kidogo. Wanaendelea kusema “Unajua udhaifu wa watu”; kuna maana nyingine ndani ya maneno haya, ambayo ni kusema, Unajua udhaifu wa binadamu, basi ni kwa nini inachukua muda mrefu kiasi hiki? Je, hii si hali iliyo ndani mwa watu? Kwa hivyo, mnahisi mnafahamu vitu vingi, tayari mmevikubali, na kuonekana mmefahamu ukweli, lakini kwa hakika bado mnaukataa ukweli, na kwenda kinyume cha ukweli. Vitu mnavyovifanya haviambatani na ukweli. Japo kijuujuu hamjafanya vitendo viovu, na hamjatamka kitu chochote kibaya, hii imejikita tu kwa kutovunja amri za utawala, kwa kutoikosea tabia ya Mungu. Hujaelewa kusudi Lake na hata hivyo hauko tayari kulipokea. Hukubaliani na Yeye kufanya mambo kwa njia hii. Unafikiri: Iwapo nitaifanya kazi hii, sitapoteza muda na nitaikamilisha kazi hii kwa muda mfupi iwezakanavyo, ili kwamba niwasaidie watu wa Mungu kuepuka mateso zaidi kutoka kwa joka kuu jekundu, kuzuia kupotea kwa watu wengi zaidi, kuepuka mateso yangu. Je, hili si wazo walilonalo watu? Watu mioyoni mwao wanatumaini kufika kwa ufalme wa Mungu, na kuangamia kwa haraka kwa ulimwengu wa Shetani. Ni neema kubwa ikiwa neno moja la Mungu litawabadilisha. Mitazamo ya ndani ya watu, matamanio yao makubwa kwa hakika hayatekelezi kusudi la Mungu, na kimsingi hakuna kiini cha kutii. Hili pia linagusa ule msemo: Asilimia mia moja ya kile kilicho ndani ya asili ya binadamu ni usaliti. Kwa hivyo, kwa kulichanganua hili au lile tukio lenu, kwa kulichanganua hili suala, lile wazo, au ile hisia, iwe unaikabili kwa njia hasi, au unalalamika, ikiwa hujali au umenyamaza bila kusema neno, kuna ukinzani katika haya yote. Haya yote ni usaliti. Je, huu uchanganuzi ni sahihi? Nisingalichanganua hili, kungekuwepo na watu wanaohisi: Ninaweza kudhaniwa kuwa mtu mzuri. Ningekumbana na jambo hili miaka michache iliyopita, bila shaka ningelalamika, ikiwezekana ningerudi nyuma, lakini sasa silalamiki. Hulalamiki, lakini je una uelewa? Je, uelewa wako mdogo unajumuisha uelewa wa kweli? Kuna ukweli ndani yake? Je, uelewa wako unalingana na kusudi la Mungu? Je, umepata kibali cha Mungu? Je, una kiini cha kumtii Mungu? Je, uko radhi na tayari kumtii Mungu? Kama sivyo, basi bila shaka unakinzana na Mungu. Inawezekana kwamba hali yako ya moyo sasa hivi ni nzuri, na hujihisi vibaya, au kwa sababu sasa hivi umewekwa katika kufanya kazi. Ikiwa siku moja utatumwa nyumbani, na utakapokuwa katika giza la hali mbaya ya moyo, hata hivyo, kilicho ndani ya moyo wako kitafichuliwa. Kuna watu wengine wenye kimo kidogo, wenye muda mfupi wa uzoefu ambao wanaweza kugeuka na kukimbia, kurudi ulimwenguni. Kwa hakika, katika uchanganuzi wa mwisho, mjibizo wowote ule ulionao, unakataa mazingira aliyokupangia Mungu. Asili ya watu ya kumsaliti Mungu inafichuliwa kila mahali. Ikiwa hili lisingechanganuliwa, watu wasingejijua kwa kina ipasavyo. Watu wakikumbana na kitu chochote, wote wanamsaliti Mungu na wanakosa kumtii. Mijibizo ya baadhi yenu ni kutotaka, au hisia za malalamiko, uhasi na huzuni, na mnasema: Kwa ndani, binadamu hapendi ukweli, na huku kutopenda si kingine bali ni usaliti. Bado haitoshi kama mnazungumza namna hii tu, na hamjachanganua hadi kwenye kina cha kiini. Mnasema kwamba kutopenda ukweli ni usaliti, lakini kwa kweli, hili si sahili hivyo Mmelichanganua vipi? Hamjielewi nyinyi wenyewe. Unaweza usijue hiyo ni hali gani uliyonayo, na huwezi kutofautisha mazuri na mabaya, ikiwa ni usaliti au la, na hujijui wazi wewe mwenyewe iwe umetii au la. Hamuwezi kuchanganua kabisa asili zenu wenyewe. Kila mara mnapokumbana na jambo fulani mnashindwa kujua namna ya kwenda mbele. Hatimaye, utakapokumbana na jaribu, je, utaweza kulitambua kusudi la Mungu? Utalifafanua hili vipi? Unapaswa kutembea katika njia gani? Ni mantiki gani au ni ukweli gani unapaswa kuwa nao ili kukidhi kusudi la Mungu? Kama kiwango cha chini zaidi, ni lazima uwe na mtazamo chanya. Je, mmeyawazia maswali haya?

Zamani watu wengine walikuwa na mawazo kuhusu anachokifanya Mungu mwenye mwili. Ushirika uliofuata ulisababisha kuwepo na ukweli usiohitaji uthibitisho. Ukweli huu usiohitaji uthibitisho ni: Binadamu wanapaswa kukiri kuwa yote anayofanya Mungu ni sahihi, kuwa yote ni muhimu. Kama binadamu hawataelewa wanapaswa hata hivyo kutii na si kupinga. Kama binadamu wana mawazo ni lazima wataaibika. Je, watu wanakumbuka maneno haya? Kila mara wanapokabiliana na kitu, wanajisemea wao wenyewe: Kwa namna yoyote usiwe na mawazo, kwa namna yoyote usiyahukumu. Kuna maana katika kila kitu anachokifanya Mungu. Ijapokuwa hatuwezi kuelewa kwa sasa, siku moja tutapata aibu. Wanazishikilia tu sheria kama hii. Sheria ya aina hii, hata hivyo, yaweza kusuluhisha matatizo kadhaa ya waumini ambao wamekanganyikiwa. Kwa mtu aliye na uelewa haya maneno yatasaidia kuelewa maana ya vitu vingi, na kutumia hii sheria kila mara hali inaposhuhudiwa yaweza kuweka wazi mambo mengi. Ni nini kinachofanyika kama hakuna umaizi? Mtu anaweza tu kutii sheria, na katika kufanya hivyo anaweza pia kulindwa na kuzuia kukiuka amri za utawala, si kueneza maafa. Sheria hii ina manufaa! Sio ati haina maana! Katika sehemu mbalimbali sheria hii imesomwa kwa moyo. Wengine huiandika madaftarini, au kuiandika kwenye jalada la kitabu, na kuisoma kila wakati wanapofungua kitabu, huku wakiikariri. Wanaikariri wanapoomba. Kufanya hivyo kuna manufaa kadhaa. Watu wengine hawathubutu kufanya mambo kwa kubahatisha, na wana uchaji mdogo mioyoni mwao. Ila kulingana na watu wengi, hawana uelewa wa kweli wa hali chanya, na kuna vitu vingi sana vilivyo hasi. Ijapokuwa inaonekana kuwa mnajihisi vyema kabisa na hamjaacha kufanya kazi, kuna vitu vingi hasi kwa kweli kati yenu, na hakuna vitu chanya. Kuna mijibizo mingi sana kanisani kuhusu mambo kama haya. Je, mmejaribu kujijumuishia nyinyi wenyewe? Kama vitu vya aina hii vingekabiliwa tena, mngemkataa Mungu au kumsaliti Mungu? Kuna baadhi ya watu ambao labda wametambua, "Binadamu hana uwezo wa kuielewa asili yake mwenyewe. Bila shaka sitajaribu kukataa tena, na lazima niwe makini. Lazima niombe kila siku!” Huu sio mpango wa uhakika. Nimegundua kuwa huwa mnapata aibu, na mara nyingi mnasema: "Ah, nitafanya nini kuhusu hii asili ya binadamu? Siwezi kuisuluhisha mimi mwenyewe, na siwezi kuielewa. Kwa kweli sina haki ya kujisimamia mimi mwenyewe. Sijui ninaweza kufanya nini siku moja. Ninaogopa sana. Kumwamini Mungu lazima kufanyike kwa makini mno. Uzembe wowote waweza kusababisha maafa, na hilo laweza kuwa jambo baya mno. Hata sijijui, siwezi kujitegemea..." Ingawa watu wanaosema haya mara kwa mara huwa wanajielewa kwa kiasi fulani, wana uelewa kidogo mno kuhusu ukweli. Wanachanganyikiwa kila mara wanapokumbana na kitu chochote. Wanapatwa na wasiwasi, wanahisi uoga, na hawana njia yoyote ile wanapopatwa na chochote kile. Wakati huu umeshinda miaka saba ya majaribu, na hujasababisha maafa, na hujakiuka amri za utawala, lakini je, waweza kuwa na uhakika kuhusu wakati ujao? Wawezaje kuyashinda haya yote bila kizuizi? Unaona kuwa umeyashinda masaibu kwa urahisi sana, kwa kujificha hapa na pale. Ulijificha kwa mwaka mmoja au nusu mwaka hadi yakaisha. Wanadamu wanaweza kujificha, lakini asili ya binadamu ni kitu ambacho hakiwezi kufichika. Je, hakupaswi kuwa na ukweli uisohitaji thibitisho unaohusiana na hili, pia? Katika kila majaribu ya Mungu kuna nia nzuri. Kwa kila tukio linaloshuhudiwa kuna ukweli ambao mtu anapaswa kuwa nao ili kusimama imara. Jiandaeni na ukweli ili kukabiliana na majaribu tofauti tofauti kwa sasa, na hamtaogopa bila kujali miaka ya majaribu hapo mbeleni. Lazima muwe na ujasiri. Kutii mipango ya Mungu kamwe hakuwezi kuwa na dosari. Njia daima itakuwa na matumaini. Mwawezaje kuwa wakamilifu bila majaribu kadhaa? Bila majaribu, hakuna shahidi. Ni vipi basi mtamridhisha Mungu? Majaribu yatawaletea baraka za Mungu. Ni kwa kumfuata tu Mungu hadi mwisho ndipo mtu aweza kuingia katika ufalme. Kumbuka: nyinyi nyote mna fungu katika dhiki, ufalme, na uvumilivu wa Kristo.


kutoka kwa Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Vitabu.