Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo majaribio. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo majaribio. Onyesha machapisho yote

Jumapili, 14 Aprili 2019

Nilipitia Wokovu wa Mungu

Nilipitia Wokovu wa Mungu

Cheng Hao Mji wa Yongzhou, Mkoa wa Hunan
Wajibu ambao mimi na mke wangu tunatimiza kanisani ni kuhubiri injili. Muda mfupi uliopita, mke wangu alipandishwa cheo kuwa mkuu wa kundi la injili, huku mimi, kutokana na kiburi changu mwenyewe na utukutu wangu, nilipoteza kazi ya Roho Mtakatifu na kupelekwa nyumbani kutafakari juu ya matendo yangu. Kutokana na kwamba mimi na mke wangu tulianza kutimiza wajibu wetu wakati mmoja, lilikuwa jambo gumu kukubali kumuona akipandishwa cheo wakati nilifukuzwa kutoka kwa wajibu wangu. Machozi yalidondoka machoni mwangu nilipofikiri: “Mungu anatenganisha kila mmoja kwa jinsi yake na, kuzingatia kuwa nimefukuzwa, hii ni hakika kwamba nimefichuliwa na kuondoshwa. Aa! Nani angefikiri kwamba baada ya miaka yote hii, maisha yangu kama muumini yangeishia kwa kutofaulu kabisa. Yote ninayoweza kufanya sasa ni kusubiri adhabu yangu.” Kisha nikaenda nyumbani na moyo mzito. Kuanzia wakati huo kwendelea nikawa nimetatizika katika kushindwa na kujawa na suitafahamu na lawama kwa Mungu. Nilikuwa nimetumbukia katika giza bila matumaini.
Siku moja, nikapata vifungu viwili vinavyofuata vya neno la Mungu kwa bahati: “Sijawahi kusema kuwa hamkuwa na mategemeo, sembuse kwamba mlipaswa kuangamizwa au kupotea; je, Nimetangaza hadharani jambo hilo? Wewe husema kuwa huna tumaini, lakini si hili ni hitimisho lako? Je, si hii ni athari ya mawazo yako mwenyewe? Je, hitimisho lako lina maana?” (“Mnapaswa Kuweka Pembeni Baraka za Hadhi na Kuelewa Mapenzi ya Mungu kwa ajili ya Wokovu wa Mwanadamu” katika Neno Laonekana katika Mwili). “Huoni tabia ya Mungu yenye haki, na daima unamwelewa Mungu visivyo na kugeuza nia Zake, ambayo hukufanya daima uwe bila rajua na kupoteza matumaini. Je, hili si la kujiadhibu? … Huelewi kazi ya Mungu na huyaelewi mapenzi ya Mungu katu; hata zaidi, huelewi nia nzuri ambazo Mungu ameweka katika miaka Yake 6,000 za kazi ya usimamizi” (“Mapenzi ya Mungu ni Kuwaokoa Watu kwa Kiwango Kikubwa Sana Kinachowezekana” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo). Nikisoma vifungu hivi, nilitambua kwa mshangao: Mungu hazungumzi juu yangu? Mara tu nilipoarifiwa kwamba kanisa lilikuwa limenifukuza, nilikisia na kuhitimisha kuwa nilikuwa nimefichuliwa na kuondoshwa na kupoteza imani katika kutafuta ukweli. Niliishi katika hali ya kudumu ya uhasi na kutoelewana, kama nimekubali bila kulalamika kabisa kushindwa kwangu mwenyewe. Wakati huo, nilitazama moyoni mwangu, nikiuliza: “Je, unaelewa kwa kweli ni kwa nini umekutana na balaa hii? Je! Unaelewa kwa kweli mapenzi ya Mungu? Bila shaka hapana! Sielewi! Basi kwa nini nifanye makisio ya kishenzi na ufafanuzi kwa maneno usio na msingi? Je, si huku kulikuwa ni kuwa na kiburi sana, udanganyifu mno? Je, si nilikuwa nimejishusha katika mahali hapa pa mateso ya giza? Upumbavu jinsi gani, jinsi nilivyokuwa na upuuzi!” Kwa hiyo, nilikwenda mbele ya Mungu kwa sala, nikiomba nuru Yake ili nipate kufichua mapenzi Yake katika ufunuo huu wa hivi karibuni. Baadaye, niliona kifungu hiki cha neno la Mungu: “Yote Ayafanyayo ni mapenzi ya dhati kwako; Hana nia mbaya. Anawahukumu kwa sababu ya dhambi zenu, ili kwamba mweze kujichunguza wenyewe na kupokea wokovu mkubwa. Haya yote hufanywa kumfinyanga mwanadamu. Tangu mwanzo hadi mwisho, Mungu amekuwa Akifanya kila Awezalo kumwokoa mwanadamu, na hakika hayuko tayari kuwaangamiza kabisa wanadamu Aliowaumba kwa mikono Yake Mwenyewe. Sasa Amekuja miongoni mwenu kufanya kazi; je, huu si wokovu zaidi? Je, Angalikuchukia, Angaliendelea kufanya kazi ya kiwango hicho cha juu ili kukuongoza wewe Mwenyewe? Ni kwa nini Ateseke hivyo? Mungu hawachukii wala hana nia mbaya juu yenu. Mnapaswa kufahamu kuwa mapenzi ya Mungu ndiyo mapenzi ya kweli zaidi. Anawaokoa kupitia hukumu kwa sababu tu ya uasi wa mwanadamu; la sivyo, hawangepata wokovu. … Hana moyo wa kuwaacha mpotoshwe zaidi; wala Hana moyo wa kutaka kuwaona mkiishi mahala pachafu kama hapa, mkikandamizwa na Shetani apendavyo, Hana moyo wa kuwaacha mtumbukie Kuzimu. Anataka tu kulipata hili kundi lenu na kuwakomboa vilivyo. Hili ndilo kusudi kuu la kufanya kazi ya kushinda miongoni mwenu—ni kwa ajili ya wokovu tu” (“Ukweli wa Ndani wa Kazi ya Kushinda (4)” katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mungu ya dhati yaliufurahisha moyo wangu na kuniamsha kutoka kwa kuishiwa imani kwangu kulikokuwa kumetiwa ganzi. Kama ilivyobainika, ingawa hali yangu ilionekana kuwa ya kutia hofu kwa ukaguzi wa kwanza, ilikuwa ni Mungu kwa kweli akiniletea upendo Wake, na akinipa wokovu Wake. Haikuwa, kama nilivyofikiria, kwamba ningeondoshwa. Nilikuwa mwenye kiburi na mgumu—nikitimiza wajibu wangu kwa kuzembea na utundu bila kuwa na subira. Mungu hangevumilia kuniona nikiendelea kukanyagwa na Shetani. Hakuweza kuvumilia kuniona nikizidi kuzama chini zaidi na Yeye hasa hakuweza kuvumilia kuniona nikikabiliwa na adhabu kwa kuikosea tabia ya Mungu kupitia vitendo vya kiburi kisichozuilika. Hivyo, kupitia hukumu na kuadibiwa, Aliniletea wokovu, akanibariki kwa neema Yake ya kuokoa na kunisaidia kuyatoroka mishiko ya upotovu wa Shetani. Kufukuzwa kwa kanisa kulikuwa, kweli, wokovu mkuu mno wa Mungu. Jinsi nilivyozidi kuwa na kiburi, ndivyo Mungu alivyozidi kutengeneza mazingira ili kukabiliana na makosa yangu. Aliruhusu tamaa zangu kubaki bila kutimizwa ili moyo wangu uliokufa ganzi uanze kuhisi maumivu. Alitenda kupitia maumivu haya ili kunifanya kutafakari juu ya matendo yangu, kuelewa kiini cha asili yangu potovu na kutafuta ukweli ili kufanikisha mabadiliko katika tabia yangu. Hii ndiyo ile kazi halisi ya wokovu ambayo Mungu aliniletea. Yote aliyoyafanya yalikuwa ni utunzaji na upendo kwangu. Vinginevyo, bado ningekuwa naishi katika dhambi bila kujua isiyojali, bado nikitenda kwa uzembe, nikikatiza na kuingiliza kati kazi ya injili. Mwishowe, vitendo vyangu vingekuwa vimeikosea tabia ya Mungu na ningekuwa nimeondoshwa na Mungu. Wakati huu, nilikuja kuona kwamba wokovu wa Mungu ulikuwa halisi. Hakuna kitu cha uongo au kitupu kuhusu upendo wa Mungu—ni kweli na halisi. Mimi, hata hivyo, nilikosa kuona kazi ya Mungu na wokovu Wake. Nilikosa kutafuta nia yenye ari katika wokovu wa Mungu, badala yake nilijifafanua kupita kiasi mara kwa mara huku nikimwelewa Mungu visivyo na kumlaumu na kuishi kwa uzembe bila rajua. Nilikosa busara kiasi gani! Nilikuwa mtu asiyefaa kupokea hukumu ya Mungu na kuadibiwa.
Mungu mpendwa, asante! Kupitia uzoefu huu, ninatambua kwamba wokovu Wako ni wa kweli na hukumu Yako na kuadibu vimejaa upendo. Bila hukumu Yako na kuadibu, singewahi kamwe kujitazama kwa kweli. Ningendelea kuishi katika upotovu, hali yangu ikiendelea kuharibika, kukanyagwa na Shetani na hatimaye kubebwa naye. Kupitia uzoefu huu, nilitambua pia kuwa kiini Chako ni upendo na kwamba matendo Yako yote yanalenga kuwaokoa wanadamu. Mungu, ninaapa kujiwekeza kikamilifu katika kutafuta ukweli na kuanza upya. Bila kujali matokeo ni yapi, ninaapa kutimiza wajibu wangu wa kiumbe ili kuyaridhisha mapenzi Yako. Utukufu wote Uwe kwa Mwenyezi Mungu!

Ijumaa, 4 Januari 2019

Ni zipi tofauti muhimu kati ya Mungu mwenye mwili na hao watu ambao hutumiwa na Mungu?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu

5. Ni zipi tofauti muhimu kati ya Mungu mwenye mwili na hao watu ambao hutumiwa na Mungu?

Aya za Biblia za Kurejelea:
"Mimi nawabatiza na maji ili mtubu. Lakini yule ajaye baada ya mimi ni mwenye nguvu zaidi kuliko mimi, ambaye sistahili kuvichukua viatu vyake. Atawabatiza na Roho Mtakatifu, na moto" (MT 3:11).
Maneno Husika ya Mungu:
Kristo ni mwili uliovishwa na Roho wa Mungu. Mwili huu ni tofauti na wa mwanadamu yeyote aliye wa nyama. Tofauti hii ni kwa sababu Kristo sio wa mwili na damu bali ni mwili wa Roho. Anao ubinadamu wa kawaida na uungu kamili. Uungu Wake haujamilikiwa na mwanadamu yeyote. Ubinadamu Wake wa kawaida unaendeleza shughuli Zake zote za kawaida katika mwili, wakati uungu Wake unafanya kazi ya Mungu Mwenyewe. Basi iwe ubinadamu Wake au uungu, yote hujiwasilisha kwa mapenzi ya Baba wa mbinguni. Kiini cha Kristo ni Roho, yaani, uungu. Kwa hivyo, chemichemi Yake ni ile ya Mungu Mwenyewe; Dutu hii haitapinga kazi Yake Mwenyewe, na Yeye hangeweza kufanya kitu chochote kinachoharibu kazi Yake Mwenyewe, wala milele Yeye kutamka maneno yoyote ambayo yanakwenda kinyume na mapenzi Yake Mwenyewe. …
… Yote yanayomuasi Mungu yanatoka kwa Shetani; Shetani ni chanzo cha ubaya na uovu wote. Sababu kwamba mwanadamu anayo sifa sawa na ile ya Shetani ni kwa sababu mwanadamu amelagaiwa na kufinyangwa Shetani. Kristo hajawahi kupotoshwa na Shetani, hivyo Anazo tu tabia za Mungu na hakuna hata moja ya Shetani.
kutoka kwa "Kiini Cha Kristo ni Utiifu kwa Mapenzi ya Baba Wa Mbinguni" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kwa sababu ni mwanadamu mwenye kiini cha Mungu, Yuko juu ya wanadamu wote walioumbwa, juu ya mwanadamu yeyote anayeweza kutekeleza kazi ya Mungu. Kwa hivyo, miongoni mwa wale wote walio na umbo la binadamu kama Lake, miongoni mwa wale wote walio na ubinadamu, Yeye pekee ndiye Mungu mwenye mwili Mwenyewe—wengine wote ni wanadamu walioumbwa. Japokuwa wote wana ubinadamu, wanadamu walioumbwa si chochote zaidi ya wanadamu, ilhali Mungu mwenye mwili ni tofauti: katika mwili Wake, si tu kwamba ana ubinadamu ila pia muhimu zaidi Ana uungu.
kutoka kwa "Kiini cha Mwili Ulio na Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Uungu wa Kristo ni zaidi ya wanadamu wote, kwa hivyo Yeye Anayo mamlaka ya juu ya viumbe vyote vilivyoumbwa. Mamlaka haya ni uungu Wake, yaani, nafsi na tabia ya Mungu Mwenyewe, ambayo huamua utambulisho Wake.
kutoka kwa "Kiini Cha Kristo ni Utiifu kwa Mapenzi ya Baba Wa Mbinguni" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kwa kuwa Mungu ni mtakatifu na safi, na halisi na wa kweli, mwili Wake unatoka kwa Roho. Hili ni wazi, na bila shaka. Sio tu kuweza kushuhudia kwa Mungu Mwenyewe, bali pia kuweza kutekeleza kabisa mapenzi ya Mungu: huu ni upande mmoja wa dutu ya Mungu. Kwamba mwili unatoka kwa Roho na sura kuna maana kwamba mwili ambao Roho anajivisha ni tofauti kimsingi na mwili wa mwanadamu, na tofauti hii hasa iko ndani ya roho zao.
kutoka kwa "Ufafanuzi wa Tamko la Tisa" katika Neno Laonekana katika Mwili
Mwili uliovaliwa na Roho wa Mungu ni mwili wa Mungu mwenyewe. Roho wa Mungu ni mkubwa, Yeye ni mwenyezi, mtakatifu, na mwenye haki—na vilevile ndivyo ambavyo mwili Wake ulivyo pia mkubwa, wenye uwezo, mtakatifu, na wenye haki. Mwili kama huo unaweza kufanya tu kile ambacho ni chenye haki na manufaa kwa mwanadamu, kile ambacho ni kitakatifu, chenye utukufu, na uweza, na hakiwezi kukifanya chochote ambacho kinakiuka ukweli au uadilifu na haki, isitoshe hata kile ambacho kinaasi dhidi ya Roho wa Mungu. Roho wa Mungu ni mtakatifu, na hivyo basi mwili Wake hauwezi kuharibiwa na Shetani; mwili Wake una kiini tofauti na ule mwili wa mwanadamu. Kwani ni mwanadamu, wala si Mungu, ambaye anaharibiwa na Shetani, na mwili wa Mungu usingeweza kuharibiwa na Shetani. Kwa hivyo, licha ya ukweli kwamba mwanadamu na Kristo wanakaa mahala pamoja, ni mwanadamu tu ndiye ambaye anatawaliwa, anatumiwa, na kutegwa na Shetani. Kinyume cha hayo, Kristo daima hapenyezwi na uovu wa Shetani, kwa kuwa Shetani hataweza kamwe kupaa hadi mahala pa aliye juu zaidi, na hataweza kumkaribia Mungu. Leo, nyote mnapaswa kuelewa kuwa ni mwanadamu tu, aliyepotoshwa na Shetani, ambaye ananisaliti, na kwamba daima tatizo hili halitakuwa linamhusu Kristo.
kutoka kwa "Tatizo Zito Sana: Usaliti (2)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kwa sababu wanadamu ni, kwa hakika, binadamu, na wanaweza tu kuangalia kila kitu kutoka kwa mtazamo na kutoka katika kimo cha mtu. Hata hivyo, Mungu mwenye mwili ni tofauti kabisa na mtu aliyepotoka. Bila kujali ni vipi ambavyo mwili wa Mungu mwenye mwili ulivyo wa kawaida, ulivyo kama wengine, ulivyo wa chini, au hata namna ambavyo watu wanamdharau Yeye, fikira Zake na mwelekeo Wake kwa wanadamu ni mambo ambayo hakuna binadamu angeweza kufuatisha na wala hakuna binadamu angeweza kuiga. Siku zote Atawaangalia wanadamu kutoka kwa mtazamo wa uungu, kutoka katika kimo cha madaraka Yake kama Muumba. Siku zote Atawaona wanadamu kupitia katika kiini na akili ya Mungu. Hawezi kabisa kuwaona wanadamu kutoka katika kimo cha mtu wa kawaida na kutoka kwa mtazamo wa mtu aliyepotoka. Wakati watu wanapowaangalia wanadamu, wanawaangalia kwa mtazamo wa binadamu, na wanatumia mambo kama vile maarifa ya mwanadamu na masharti na nadharia za wanadamu kama kipimo. Hali hii imo ndani ya mawanda ya kile ambacho watu wanaweza kuona kwa macho yao; ni ndani ya upana ambao watu waliopotoka wanaweza kutimiza. Wakati Mungu anapowatazama wanadamu, Anawatazama kwa macho ya kiungu, na Anatumia kiini Chake na kile Alicho nacho na kile Alicho kama kipimo. Mawanda haya yanajumuisha mambo ambayo watu hawawezi kuona, na hapo ndipo Mungu mwenye mwili na wanadamu waliopotoka walivyo tofauti kabisa. Tofauti hii inaamuliwa na viini tofauti vya wanadamu na vya Mungu na ndivyo vinavyoamua utambulisho na nafasi zao pamoja na mtazamo na kimo ambacho wanaona mambo.
kutoka kwa "Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III" katika Neno Laonekana katika Mwili
Yeye ambaye Anafanya kazi katika Uungu Anawakilisha Mungu, ilhali wale wanaofanya kazi katika ubinadamu ni wanadamu wanaotumiwa na Mungu. Yaani, Mungu katika mwili ana utofauti halisi na wanadamu wanaotumiwa na Mungu. Mungu mwenye mwili Anaweza kufanya kazi ya Uungu, lakini wanadamu wanaotumiwa na Mungu hawawezi. Mwanzoni mwa kila enzi, Roho wa Mungu anaongea binafsi kuzindua enzi mpya na kuleta mwanadamu kwenye mwanzo mpya. Wakati Yeye Atamaliza mazungumzo Yake, itaashiria kwamba kazi ya Mungu katika Uungu imekamilika. Baada ya hapo, wanadamu wote hufuata mwongozo wa wale hutumiwa na Mungu kuingia katika uzoefu wa maisha.
kutoka kwa "Tofauti Muhimu Kati ya Mungu Aliyepata Mwili na Wanadamu Wanaotumiwa na Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Japo Mungu mwenye mwili Ana akili ya mwanadamu wa kawaida, kazi Yake haijatiwa doa na mawazo ya kibinadamu; Anafanya kazi katika kibinadamu na akili ya kawaida chini ya masharti ya awali kuwa atakuwa na ubinadamu na akili ya kawaida, na si na mawazo ya kawaida ya kibinadamu. Haijalishi mawazo ya mwili Wake ni bora kiasi gani, kazi Yake haionyeshi alama ya mantiki au kufikiria. Kwa maneno mengine, kazi Yake haiwazwi na akili ya mwili Wake, ila ni onyesho la moja kwa moja la kazi ya uungu katika ubinadamu Wake. Kazi yake yote ni huduma Anayostahili kutimiza, na haiwazwi hata chembe kwa akili Zake. Kwa mfano, kuponya wagonjwa, kufukuza mapepo na kusulubishwa hayakuwa mazao ya akili Zake za kibinadamu, yasingeweza kutimizwa na mwanadamu yeyote mwenye akili za kibinadamu. Vivyo hivyo, kazi ya ushindi ya leo ni huduma ambayo ni sharti itekelezwe na Mungu mwenye mwili, lakini si kazi ya mapenzi ya mwanadamu, ni kazi ambayo uungu Wake unapaswa kufanya, kazi ambayo hakuna mwanadamu wa mwili anaiweza.
kutoka kwa "Kiini cha Mwili Ulio na Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Tangu mwanzo, wanadamu ambao Mungu Ametumia wote wana mawazo ya kawaida na fikra. Wao wote wanajua jinsi ya kujiendesha na kushughulikia mambo ya maisha. Wanashikilia itikadi za kawaida za binadamu na kuwa na vitu vyote ambavyo wanadamu wa kawaida wanapaswa kuwa navyo. Wengi wao wana vipaji vya pekee na werevu wa kiasili. Kwa kufanya kazi kupitia wanadamu hawa, Roho wa Mungu Anakusanya na kutumia vipaji vyao, ambavyo ni zawadi yao Aliyowapa Mungu. Ni Roho wa Mungu Ndiye Anayeleta vipaji vyao katika kazi, na kuwasababisha kutumia uwezo wao kumhudumia Mungu. Hata hivyo, kiini cha Mungu hakina itikadi na hakina fikira. Hakiungani na mawazo ya binadamu na hata kinakosa vitu ambavyo binadamu wa kawaida huwa navyo. Yaani, Mungu hata hafahamu vizuri kanuni za maadili ya binadamu. Hivi ndivyo ilivyo Mungu wa leo Anapokuja duniani. Kazi Yake na maneno Yake hayajachafuliwa na nia au fikira za binadamu, bali ni dhihirisho la moja kwa moja la Roho, na Anafanya kazi moja kwa moja kwa niaba ya Mungu. Hii ina maana Roho huja kufanya kazi, ambayo Haweki ndani mawazo ya mwanadamu hata kidogo. Yaani, Mungu katika mwili Anajumuisha Uungu moja kwa moja, Hana mawazo ya binadamu au itikadi, na Haelewi kanuni za maadili ya binadamu. Kama kungekuwa na kazi ya Uungu tu (kumaanisha iwapo ingekuwa Mungu mwenyewe pekee ndiye Anayefanya kazi hiyo), kazi ya Mungu haingeweza kufanyika duniani. Kwa hivyo Mungu Anapokuja duniani, lazima Awe na wanadamu wachache Anaowatumia kufanya kazi katika ubinadamu pamoja na kazi Yake katika Uungu. Kwa maneno mengine, Yeye Anatumia kazi ya mwanadamu ili kusaidia kazi Yake takatifu. La sivyo, mwanadamu hangeweza kuja katika mawasiliano ya moja kwa moja na kazi ya Mungu.
kutoka kwa "Tofauti Muhimu Kati ya Mungu Aliyepata Mwili na Wanadamu Wanaotumiwa na Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kazi ya wanadamu wanaotumiwa pia ni kazi ya Roho Mtakatifu. Ni kwamba tu kazi ya Mungu ni dhihirisho kamili la Roho Mtakatifu, na hakuna tofauti, ilhali kazi ya wanadamu wanaotumiwa inachanganyika na mambo mengi ya kibinadamu, na wala sio udhihirishaji wa moja kwa moja wa Roho Mtakatifu, wala udhihirishaji kamili. … Roho Mtakatifu anapofanya kazi kwa wanadamu wanaotumika, karama zao na tabia zao halisi zinatumiwa pia na wala haziachwi. Tabia zao halisi zinatumiwa zote kwa ajili ya kutoa huduma kwa kazi. Tunaweza kusema kuwa Anafanya kazi kwa kutumia sehemu zilizopo za wanadamu ili kupata matokeo yatendayo kazi. Kinyume chake, kazi inayofanyika katika mwili uliopatikana ni kumdhihirisha moja kwa moja Roho na wala haichanganywi na akili na mawazo ya mwanadamu, haifikiwi na karama za mwanadamu, uzoefu wa mwanadamu au hali ya ndani ya mwanadamu.
kutoka kwa "Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Hakuna anayeishi katika mwili anayeweza kumwakilisha Mungu kwa njia ya moja kwa moja isipokuwa kama yeye ni binadamu anayetumiwa na Roho Mtakatifu. Hata hivyo, hata tabia ya mtu kama huyo na kile anachoishi kwa kudhihirishwa chote hakiwezi kuchukuliwa kwamba kinamwakilisha Mungu kabisa; inaweza kusemekana tu kwamba kile anachoishi kwa kudhihirishwa kinatawaliwa na Roho Mtakatifu. Tabia ya mtu kama huyo haiwezi kumwakilisha Mungu.
… Binadamu ni mfano halisi wa Shetani, na tabia ya mwanadamu haiwakilishi tabia ya Mungu. Baadhi ya wanadamu ni wenye tabia nzuri; Mungu anaweza kufanya baadhi ya kazi kupitia kwa tabia hiyo nayo kazi yao inatawaliwa na Roho Mtakatifu, ilhali tabia yao haiwezi kumwakilisha Mungu. Kazi ambayo Mungu hufanya ndani yao ni kule tu kufanya kazi na pamoja na kupanua kile ambacho tayari kimo ndani yao. Wawe ni manabii kutoka kwenye enzi zilizopita au binadamu wanaotumiwa na Mungu, hakuna yeyote anayeweza kumwakilisha Mungu kwa njia ya moja kwa moja. … binadamu yeyote aliye na asili ya dhambi hawezi kumwakilisha Mungu, na kwamba dhambi ya binadamu inamwakilisha Shetani. Hiyo ni kusema kwamba dhambi haimwakilishi Mungu na Mungu hana dhambi. Hata kazi inayofanywa ndani ya binadamu na Roho Mtakatifu inaweza tu kuchukuliwa kuwa imetawaliwa na Roho Mtakatifu na haiwezi kusemwa kwamba ilifanywa na binadamu kwa niaba ya Mungu. Kwa kadri ambavyo binadamu anahusika, si dhambi yake wala tabia yake inamwakilisha Mungu.
kutoka kwa "Mtu Mpotovu Hawezi Kumwakilisha Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Vitabu.

Jumamosi, 1 Septemba 2018

Swahili Christian Movie "Kutamani Sana" (3) - Nani Atanyakuliwa Kwanza Wakati Bwana Atakaporudi?

Swahili Christian Movie "Kutamani Sana" (3) - Nani Atanyakuliwa Kwanza Wakati Bwana Atakaporudi?

Wengi wa wale wanaomsadiki Bwana wanasadiki kwamba mradi tu wajitolee, wajitumie, na kutia bidii, bila shaka watakuwa miongoni mwa wale wa kwanza kunyakuliwa. Lakini je, kuna msingi wowote wa haya katika maneno ya Bwana? Bwana Yesu alisema, "But many that are first shall be last; and the last shall be first" (Mathayo 19:30). "Kondoo wangu huisikia sauti yangu" (Yohana 10:27). Ni wazi kwamba kama mtu anaweza kunyakuliwa au la kunaamuliwa na kama ataisikia sauti ya Bwana. Wale wanaoisikia kwanza sauti Yake na kukubali kuonekana Kwake na kazi ni wanawali wenye hekima, na watakuwa wa kwanza kunyakuliwa.
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, wafuasi wa Kristo

Jumatano, 11 Julai 2018

Christian Music Video Swahili "Hadithi ya Xiaozhen"(2): Kupigania Dhahabu

Christian Music Video Swahili "Hadithi ya Xiaozhen"(2): Kupigania Dhahabu

Xiaozhen alipopata kipande kikubwa cha dhahabu, aliwaita marafiki wake ili wagawane. Kile ambacho hakutambua ni kwamba mara tu watu wanapoona dhahabu, asili nzuri na mbaya ya mwanadamu hujiweka wazi …
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kwaya za Injili

Jumatatu, 5 Februari 2018

Katikati ya Maafa Niliiona Tabia ya Haki ya Mungu

7. Katikati ya Maafa Niliiona Tabia ya Haki ya Mungu

Li Jing, Beijing
7 Agosti, mwaka wa 2012
Siku hiyo, ilianza kunyesha asubuhi. Nilikwenda kwa mkutano nyumbani mwa ndugu mmoja, wakati mvua ilipoendelea kuongezeka zaidi na zaidi kwa uzito. Kufikia alasiri ilikuwa ikinyesha kana kwamba ilitoka mbinguni moja kwa moja. Wakati tulipomaliza mkutano wetu, mvua ilikuwa imeingia katika ua wa ndugu yangu, lakini kwa sababu nilikuwa na wasiwasi juu ya familia yangu, nilijitahidi kwenda nyumbani.