Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Jumapili, 17 Machi 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Hudumu kama Waisraeli Walivyofanya

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Hudumu kama Waisraeli Walivyofanya

Siku hizi watu wengi hawatilii maanani mafunzo yapi yanayopaswa kusomwa wakati wa upatano na wengine. Nimegundua kuwa wengi wenu hawawezi kujifunza mafunzo hata kidogo wakati wa ushirikiano na wengine. Wengi wenu mnashikilia maoni yenu mwenyewe, na wakati mnafanya kazi kanisani, unatoa maoni yako na yeye anatoa yake, moja uhusiano na mingine, bila kushirikiana kabisa. Mnajihusisha tu katika kutoa umaizi wenu wenyewe wa ndani, unaingia tu katika kuachilia huru “mizigo” ndani yenu, si kutafuta uzima hata kidogo. Inaonekana kwamba unafanya tu kazi hiyo kwa kutimiza wajibu, daima ukiamini kwamba unapaswa kufuata njia yako mwenyewe bila kujali jinsi watu wengine walivyo, na kwamba unapaswa kushiriki jinsi Roho Mtakatifu anavyokuongoza, bila kujali jinsi watu wengine walivyo. Hamna uwezo wa kugundua uwezo wa wengine, na hamuwezi kujichunguza. Njia yenu ya kupokea vitu ni yenye makosa sana. Inaweza kusemwa kwamba hata sasa bado mnaonyesha kujidai kwingi, kana kwamba ugonjwa huo wa zamani umerejea tena. Hamuwasiliani nyinyi kwa nyinyi ili kufikia uwazi kamili, kama ni matokeo gani yaliyopatikana kwa kuzuru kanisa hilo, au jinsi hali yako ya ndani ilivyokuwa wakati wa hivi karibuni, na kadhalika—ninyi hamuwasiliani tu kwa namna hii. Nyinyi kimsingi hamna mazoea kama vile kuacha dhana zenu wenyewe au kujitelekeza. Wale walio katika uongozi wanafikiri tu kuhusu kuwachangamsha ndugu na dada katika makanisa ya chini kwa njia ya ushirika wao, na wale wanaofuata wanajua tu kufuatilia peke yao. Kimsingi hamuelewi huduma ni nini au ushirikiano ni nini, na mnadhani tu kuhusu kuwa na dhamira nyinyi wenyewe kuulipiza upendo wa Mungu, wa kuwa na dhamira ya nyinyi wenyewe kuishi kwa kudhihirisha mtindo wa Petro, na si kuhusu kitu kingine chochote. Hata unasema, bila kujali jinsi watu wengine walivyo, hamtatii kwa upofu hata hivyo, na bila kujali watu wengine walivyo, ninyi wenyewe unatafuta ukamilifu na Mungu, na hiyo itatosha. Kwa kweli, dhamira yako hayajapata maonyesho thabiti katika uhalisi hata kidogo. Je! Hii sio aina yote ya tabia mnayoonyesha siku hizi. Kila mmoja wenu anashikilia imara utambuzi wenu wenyewe, na ninyi nyote mnataka kufanywa wakamilifu. Ninaona kwamba mmetumikia kwa muda mrefu sana na hamjaendelea sana, hasa katika somo hili la kufanya kazi pamoja kwa maelewano hamjaendelea kabisa! Kuenda kwenye makanisa unawasiliana kwa njia yako, na yeye anafanya ushirika kwa njia yake. Kuna uratibu wa upatanifu kwa nadra sana. Na watu walio chini ambao wanafuata wako namna hii hata zaidi. Ambayo ni kusema kwamba ni watu wachache sana miongoni mwenu wanaelewa kumtumikia Mungu ni nini, au jinsi mtu anapaswa kumtumikia Mungu. Mmechanganyikiwa, na kuchukulia masomo ya aina hii kama suala dogo sana, kwa kiasi kwamba watu wengi hawatekelezi tu kipengele hiki cha ukweli, wanafanya mabaya kwa kujua. Hata watu ambao wametumikia kwa miaka mingi kwa kweli wanapigana na kugombana. Je! Hiki si kimo chako halisi? Ninyi watu mnaohudumu pamoja kila siku ni kama Waisraeli ambao walimtumikia Mungu Mwenyewe katika hekalu kila siku. Inawezekanaje kuwa ninyi watu ambao ni kama makuhani hamjui jinsi ya kushirikiana na jinsi ya kutumikia?
Wakati ule, Waisraeli walimtumikia Yehova moja kwa moja hekaluni. Utambulisho wao ulikuwa ule wa kuhani. (Bila shaka si kila mtu alikuwa kuhani. Ni baadhi tu waliomtumikia Yehova katika hekalu ndio walikuwa na utambulisho wa makuhani). Wangevalia taji ambazo Yehova aliwapa (ambayo inamaanisha walifanya taji kulingana na matakwa ya Yehova, sio kwamba Yehova aliwapa taji moja kwa moja) na wakiwa wamevalia mavazi yao ya kikuhani ambayo Yehova aliwapa wangeingia katika hekalu wakiwa miguu mitupu kumtumikia Yehova moja kwa moja, tangu asubuhi hadi usiku. Utumishi wao kwa Yehova haukuwa usio na mipangalio au wa kutenda makosawapendavyo; yote ilikuwa kulingana na sheria, ambazo hakuna mtu aliyemtumikia Yehova moja kwa moja angeweza kukiuka. Wote walipaswa kufuata sheria hizi; vinginevyo, kuingia hekaluni kulikatazwa. Ikiwa yeyote kati yao alivunja sheria za hekalu, yaani, kama mtu yeyote aliasi amri za Yehova, ilikuwa lazima apate kutendewa kulingana na sheria zilizotolewa na Yehova, na hakuna mtu aliyeruhusiwa kupinga, na hakuna mtu aliyeruhusiwa kumtetea. Haijalishi ni miaka mingapi ambayo mtu huyo alimtumikia Mungu, wote walipaswa kufuata sheria. Hii ndio sababu makuhani wengi walivalia nguo za kikuhani kila wakati na kumtumikia Yehova kwa njia hii mwaka mzima, ingawa Yehova hakuwatendea kwa njia yoyote maalum, na hata walikwenda mbele ya madhabahu au hekalu maisha yao yote. Hivyo ndivyo ulivyokuwa uaminifu wao na utii wao. Haishangazi kwamba Yehova aliwabariki kwa njia hii; ilikuwa yote kutokana na uaminifu wao kwamba walipata kibali na kuyaona matendo yote ya Yehova. Wakati ule ambapo Yehova alifanya kazi katika Israeli, watu Wake waliochaguliwa, matakwa Yake juu yao yalikuwa makali sana. Wote walikuwa watiifu sana na walizuiliwa na sheria, ambazo zilitumika kuwalinda ili kwamba wamheshimu Yehova. Hizi zote zilikuwa amri za utawala za Yehova. Ikiwa miongoni mwa wale makuhani kulikuwa na yeyote ambaye hakuishika Sabato au ambaye alikiuka amri za Yehova na aligunduliwa na watu wa kawaida, huyo mtu angeletwa mara moja mbele ya madhabahu na kupigwa kwa mawe hadi kufa, na hivyo kutolewa kama dhabihu mbele ya “madhabahu ya mtu wa kawaida” ambayo Yehova alikuwa Ameanzisha. Haikuruhusiwa kuweka maiti zao katika hekalu au karibu na hekalu. Yehova hakukubali hilo. Ikiwa mtu alifanya hivyo, angetendewa kama wale ambao hutoa “dhabihu za kawaida,” na kutupwa katika shimo kubwa na kuuawa. Bila shaka, watu wote kama hao wangepoteza maisha yao, hakuna aliyeachwa hai. Kulikuwa hata na wale ambao walitoa “moto wa kawaida,” kwa maneno mengine, wale watu ambao hawakutoa dhabihu katika siku zilizotolewa na Yehova wangeteketezwa na moto wa Yehova pamoja na vitu vyao vya dhabihu, hawaruhusiwa kubaki juu ya madhabahu. Mahitaji kwa makuhani yalikuwa: Hawakuruhusiwa kuingia hekaluni, na hata ua wa nje wa hekalu, bila ya kwanza kuosha miguu yao; hakuna kuingia hekaluni ikiwa hujavalia vazi za kikuhani; hakuna kuingia hekaluni ikiwa hujavalia taji za kikuhani; hakuna kuingia hekaluni ikiwa umechafuliwa na maiti; hakuna kuingia hekaluni baada ya kuugusa mkono wa mtu asiye haki bila ya kwanza kuosha mikono yake mwenyewe; hakuna kuingia hekaluni baada ya mahusiano ya ngono na wanawake (hii haikuwa milele, kwa muda wa miezi mitatu tu), hawakuruhusiwa kuuona uso wa Yehova, wakati ulipokuwa umeisha, ikimaanisha kwamba ni baada ya miezi mitatu tu ndio wangeweza kuruhusiwa kuvaa mavazi safi ya kikuhani, na kuhudumu katika ua wa nje kwa siku saba kabla ya kuweza kuingia katika hekalu ili kuuona uso wa Yehova; waliruhusiwa kuvaa mavazi yote ya kikuhani ndani ya hekalu tu na hawaruhusiwa kuyavaa nje ya hekalu, ili kuepuka kulichafua hekalu la Yehova; iliwapasa wote waliokuwa makuhani kuwaleta wahalifu ambao wamekiuka sheria za Yehova mbele ya madhabahu ya Yehova ambako wangeuawa na watu wa kawaida, vinginevyo moto ungeanguka juu ya kuhani ambaye alishuhudia. Kwa hiyo walikuwa waaminifu kwa Yehova daima, kwa sababu sheria za Yehova zilikuwa kali juu yao, na hawangeweza kabisa kuthubutu kukiuka kikawaida amri Zake za utawala. Waisraeli walikuwa waaminifu kwa Yehova kwa sababu walikuwa wameuona moto Wake, walikuwa wameuona mkono ambao Yehova alitumia kuwaadibu watu, na pia kwa sababu hapo awali walimheshimu Yehova mioyoni mwao. Kwa hivyo kile walichopata sio moto wa Yehova tu; pia walipata utunzaji na ulinzi kutoka kwa Yehova, na kupata baraka za Yehova. Uaminifu wao ni kwamba walifuata maneno ya Yehova katika yale waliyofanya, bila mtu yeyote kuasi. Ikiwa mtu yeyote angekosa kutii, watu bado wangetekeleza maneno ya Yehova, na kuwaua wale wote waliokwenda kinyume na Yehova, bila njia yoyote ya kuficha. Hasa wale ambao walikiuka Sabato, wale waliokuwa na hatia ya uasherati, na wale walioiba sadaka kwa Yehova wangeadhibiwa vikali zaidi. Wale ambao walikiuka Sabato waliuawa kwa mawe nao (watu wa kawaida), au walipigwa viboko hadi kufa, bila yeyote kuachwa. Wale waliofanya vitendo vya uasherati, hata wale waliomtamani mwanamke mzuri, au wale waliokuwa na mawazo ya kiasherati baada ya kumwona mwanamke mwovu, au waliokuwa na tamaa ya kimapenzi baada ya kumwona mwanamke mwenye umri mdogo—kila mtu wa aina hii angeuawa. Ikiwa mwanamke mdogo yeyote ambaye hakuvaa nguo ya kufunika au utaji alimjaribu mwanaume katika kitendo cha tabia mbaya, mwanamke huyo angeuawa. Ikiwa ilikuwa ni kuhani (wale watu ambao walihudumu katika hekalu) ndiye aliyekiuka sheria za aina hii, angesulubiwa au kunyongwa. Hakuna mtu wa aina hii angeweza kuruhusiwa kuishi, na hakuna hata mtu mmoja angeweza kupata kibali mbele za Yehova. Jamaa za mtu wa aina hii hawangeruhusiwa kutoa dhabihu kwa Yehova mbele ya madhabahu kwa miaka mitatu baada ya kifo chake, na hawangeruhusiwa kugawana dhabihu ambazo Yehova aliwapa watu wa kawaida. Wakati tu ulipopita ndio wangeweka ng’ombe au kondoo wa daraja la juu kwenye madhabahu ya Yehova. Ikiwa kulikuwa na kosa lingine lolote, walipaswa kufunga kwa siku tatu mbele za Yehova, wakiomba neema Yake. Kuabudu kwao Yehova hakukuwa tu kwa sababu sheria za Yehova zilikuwa kali sana na za shuruti sana; badala yake ilikuwa ni kwa sababu ya neema ya Yehova, na pia ilikuwa kwa sababu walikuwa waaminifu kwa Yehova. Hivyo, huduma yao hadi leo imekuwa ya uaminifu vilevile, na hawajawahi kuvunja maombi yao mbele ya Yehova. Katika siku hizi watu wa Israeli bado wanapata utunzaji na ulinzi wa Yehova, na hata leo Yehova bado ni neema kati yao, na daima hukaa nao. Wote wanajua jinsi wanapaswa kumheshimu Yehova, na jinsi wanapaswa kumtumikia Yehova, na wote wanajua jinsi wanapaswa kuwa ili kupokea na kulindwa na Yehova, kwa sababu wote wanamcha Yehova mioyoni mwao. Siri ya mafanikio ya huduma yao yote si nyingine isipokuwa uchaji. Lakini nyinyi nyote mko namna gani leo? Je! Mnafanana na watu wa Israeli kwa vyovyote? Je! unafikiri kwamba huduma ya leo ni kama kufuata uongozi wa kielelezo mkubwa wa kiroho? Hamna tu uaminifu na uchaji wowote. Mnapokea neema nyingi, nyinyi ni sawa na makuhani wa Israeli, kwa sababu nyote mnamtumikia Mungu moja kwa moja. Ingawa hamuingii hekaluni, yale mnayopokea na mnayoona ni mengi zaidi kuliko kile ambacho makuhani waliomtumikia Yehova katika hekalu walipokea. Lakini bado mnaasi na mnapinga mara nyingi kuliko walivyofanya. Uchaji wenu ni mdogo sana, na hivyo mnapokea neema ndogo sana. Ingawa mnajitolea kidogo sana, mmepata mengi zaidi kuliko Waisraeli hao. Je! Huku sio kuwatendea nyinyi kwa wema? Wakati wa kazi katika Israeli, hakuna mtu angethubutu kumhukumu Yehova kama alivyotaka. Na nyinyi je? Kama si kwa sababu kazi Ninayofanya miongoni mwenu ni kuwashinda, Ningewezeje kuvumilia kutenda kwenu ovyo ovyo kuliaibisha kwa jina Langu? Ikiwa enzi mnayoishi ingekuwa Enzi ya Sheria, hakuna hata mmoja wenu angekuwa hai, kutokana na matendo yenu na maneno yenu. Uchaji wenu ni mdogo sana! Nyinyi daima mnanilaumu kwa kutowapa kibali kikubwa, na hata kusema kuwa sikuwapa maneno ya baraka ya kutosha, kwamba Nina laana tu kwenu. Je, hamjui kwamba kwa uchaji mdogo hivyo haiwezekani kwenu kukubali baraka Zangu? Je! Hamjui kwamba Mimi huwalaani mara kwa mara na kuwahukumu kwa sababu ya hali mbovu ya huduma yenu? Je, ninyi nyote mnajihisi kuwa mmekosewa? Ninawezaje kuwapa baraka Zangu kikundi cha watu ambao ni waasi na hawatii? Ninawezaje kutoa neema Yangu kwa watu ambao huleta aibu kwa jina Langu? Matendo kwa nyinyi watu tayari ni yenye huruma sana. Ikiwa Waisraeli wangekuwa waasi kama mlivyo leo, Ningalikuwa Nimewaangamiza muda mrefu uliopita. Ilhali Mimi siwatendei kwa vyovyote ila kwa huruma. Je! Huu sio wema? Je! Mnataka baraka nyingi zaidi kuliko hii? Wale pekee ambao Yehova anawabariki ni wale wanaomheshimu Yeye. Yeye huwaadibu wale wanaoasi dhidi Yake, Hamsamehei mtu yeyote kamwe. Je, si ninyi watu wa leo ambao hamjui jinsi ya kutumikia mko na haja zaidi ya kuadibiwa na hukumu, ili mioyo yenu iweze kurekebishwa kikamilifu? Je, kuadibiwa na hukumu ya aina hii sio baraka bora zaidi kwenu? Je! Sio ulinzi wenu bora? Bila hiyo, je, yeyote kati yenu angeweza kuvumilia moto wa Yehova unaochoma? Ikiwa kweli mngetumikia kwa uaminifu kama watu wa Israeli, je, hamngekuwa pia na neema kama rafiki yenu daima? Je, hangekuwa pia na furaha na neema ya kutosha? Je, nyote mnajua jinsi mnapaswa kutumikia?
Leo mahitaji ya nyinyi kufanya kazi pamoja kwa upatanifu ni sawa na jinsi Yehova alivyowataka Waisraeli kumtumikia. Vinginevyo, tamatisha tu huduma yenu. Kwa sababu nyinyi ni watu wanaomtumikia Mungu moja kwa moja, kwa kiwango cha chini zaidi mnapaswa kuweza kuwa waaminifu na watiifu katika huduma yenu, na lazima muweze wa kujifunza masomo kwa njia ya vitendo. Hasa wale wanaofanya kazi kanisani, je, yeyote kati ya ndugu na dada walio chini angethubutu kushughulika na nyinyi? Je, mtu yeyote angethubutu kuwaambia makosa yenu uso kwa uso? Mko juu ya yote, nyinyi kweli mnatawala kama wafalme! Hata hamjifunzi au kuingia katika somo la matendo kama hilo, na bado mnazungumza juu ya kumtumikia Mungu! Kwa sasa unaulizwa kuongoza makanisa kadhaa, na sio tu kwamba unakata tamaa mwenyewe, hata unashikilia mawazo na maoni yako, na kusema mambo kama “Nadhani jambo hili linafaa lifanyike kwa njia hii, kwani Mungu amesema kuwa hatupaswi kuzuiwa na wengine, na kwamba siku hizi hatupaswi kutii kwa upofu.” Kwa hiyo kila mmoja anashikilia maoni yake mwenyewe, na hakuna mtu anayemtii mwingine. Ingawa unafahamu wazi kwamba huduma yako iko katika shida kubwa, bado unasema, “Vile ninavyoona, yangu haiko mbali sana. Kwa hali yoyote sisi kila mmoja ana upande mmoja; unazungumza kuhusu yako, na mimi kuhusu yangu; unashiriki kuhusu maono yako na ninazungumza juu ya kuingia kwangu.” Huchukui jukumu kwa vitu vingi ambavyo vinapaswa kushughulikiwa, au unamudu tu, kila mtu akieleza maoni yake mwenyewe, kwa busara akilinda hali yake mwenyewe, sifa na uso wake. Hakuna mtu aliye tayari kujinyenyekesha, hakuna mtu atakayejitoa kwa ari kumrekebisha mwingine na kurekebishwa ili maisha yaendelee kwa haraka zaidi. Mara chache sana wakati mnafanya kazi pamoja hakuna yeyote kati yenu atasema, Ningependa kukusikia ukishiriki na mimi kuhusu kipengele hiki cha ukweli, kwa sababu bado nina tashwishi kukihusu. Au kusema: una uzoefu zaidi kuliko mimi juu ya jambo hili; unaweza kunipa mwelekeo fulani, tafadhali? Je, si hii ingekuwa njia nzuri ya kufanya hivyo? Nyinyi mlio kwenye viwango vya juu husikia ukweli mwingi, na kuelewa mengi kuhusu huduma. Ikiwa ninyi watu ambao mnaratibu kufanya kazi katika makanisa hamjifunzi kutoka kwa kila mmoja, na kuwasiliana, kufidia mapungufu ya kila mmoja, mnaweza kujifunza masomo kutoka wapi? Mnapokutana na chochote, mnapaswa kushirikiana na kila mmoja, ili maisha yenu yaweze kufaidika. Na mnapaswa kushirikiana kwa makini kuhusu mambo ya aina yoyote kabla ya kufanya maamuzi. Ni kwa kufanya hivyo tu ndio mnakuwa na jukumu kwa kanisa na si kuwa wazembe. Baada ya kutembelea makanisa yote, mnapaswa kukutana na kushiriki juu ya masuala yote mnayotambua na matatizo mnayokabiliwa nayo kazini, na kuwasiliana kuhusu nuru na mwanga ambao mmepokea—huu ni utaratibu wa lazima wa huduma. Lazima mfikie ushirikiano wa upatanifu kwa kusudi la kazi ya Mungu, kwa manufaa ya kanisa, na kwa kuwachochea ndugu na dada kuendelea. Unashirikiana pamoja naye na anashirikiana na wewe, kila mmoja akimbadilisha mwingine, mkifikia matokeo bora ya kazi, ili kutunza mapenzi ya Mungu. Huu tu ndio ushirikiano wa kweli, na watu kama hao tu ndio wana kuingia kwa kweli. Kunaweza kuwa na hotuba fulani isiyofaa wakati wa ushirikiano, lakini hiyo haijalishi. Shirikiana juu yake baadaye, na mpate ufahamu wa wazi kulihusu; msipuuze suala hilo. Baada ya aina hii ya ushirika unaweza kufidia mapungufu kwa ndugu na dada. Ni kwa kuenda kwa kina zaidi tu kwa namna hii katika kazi yako ndio unaweza kufikia matokeo bora. Kila mmoja wenu, kama watu wanaohudumu, lazima muweze kulinda maslahi ya kanisa katika yote mnayofanya, badala ya kuwa macho kwa maslahi yako mwenyewe. Haikubaliki kufanya pekee yako, pale ambapo unamdharau naye anakudharau. Watu wanaotenda kwa njia hii hawafai kumhudumia Mungu! Tabia ya mtu wa aina hii ni mbaya sana; hakuna hata kiasi kidogo cha ubinadamu bado kimebaki ndani yake. Yeye ni Shetani asilimia mia moja! Yeye ni mnyama! Hata sasa mambo kama haya bado yanatokea kati yenu, kwenda mpaka kushambuliana wakati wa ushirika, kutafuta visingizio kwa makusudi, kukasirika mkibishana juu ya jambo fulani dogo, hakuna mtu aliye radhi kujitenga, kila mtu akificha kilicho ndani kutoka kwa mwingine, akimwangalia mwingine na makini na kuwa macho. Je! Tabia ya aina hii ni huduma inayofaa kwa Mungu? Je, kazi kama hiyo yenu inaweza kuwakimu ndugu na dada? Sio tu kuwa huwezi kuwaongoza watu kwenye njia sahihi ya maisha, kwa kweli unaingiza tabia zako za upotovu ndani ya ndugu na dada. Je! Huwaumizi wengine? Dhamiri yako ni mbaya sana, iliyooza kabisa! Huingii katika ukweli, na huutii ukweli katika vitendo. Zaidi ya hayo, bila haya unaonyesha hadharani asili yako ya mbovu sana kwa watu wengine, huoni aibu hata kidogo! Ndugu na dada wamekabidhiwa kwako, lakini unawapeleka kuzimu. Je, si wewe ni mtu ambaye dhamiri yake imeoza? Huna aibu kabisa!
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Jumamosi, 16 Machi 2019

Kumpenda Mungu tu Ndiko Kumwamini Mungu Kweli

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,

Kumpenda Mungu tu Ndiko Kumwamini Mungu Kweli

Mwenyezi Mungu alisema, Mnapotaka kumpenda na kumjua Mungu leo, kwa upande mmoja ni lazima mstahimili mateso, usafishaji, na kwa ule upande mwingine, ni lazima mgharamike. Hakuna funzo lililo kubwa kuliko lile la kumpenda Mungu, na inaweza kusemwa kuwa funzo ambalo watu hujifunza katika maisha yao yote ya imani ni jinsi ya kumpenda Mungu. Hii ni kusema, kama unamwamini Mungu ni lazima umpende Mungu. Ikiwa unamwamini tu Mungu lakini humpendi, hujapata ufahamu wa Mungu, na hujawahi kumpenda Mungu kwa upendo wa kweli utokao moyoni mwako, basi imani yako kwa Mungu ni bure; kama katika imani yako kwa Mungu humpendi Mungu, basi unaishi bure, na maisha yako yote ndiyo ya duni zaidi kwa maisha yote. Ikiwa katika maisha yako yote hujawahi kumpenda au kumtosheleza Mungu, basi kuna haja gani ya kuishi? Kuna haja gani ya imani yako kwa Mungu? Huku si kuharibu nguvu? Hii ni kusema, kama watu wanataka kuamini na kumpenda Mungu, ni sharti wagharamike. Badala ya kujaribu kuenenda kwa namna fulani kwa nje tu, wanapaswa watafute utambuzi wa kweli kutoka ndani ya mioyo yao. Ikiwa unapenda sana kuimba na kucheza lakini huwezi kuonyesha ukweli katika vitendo, unaweza kusemekana kwamba unampenda Mungu? Kumpenda Mungu kunahitaji utafutaji wa mapenzi ya Mungu katika mambo yote, na kwamba ujisaili wewe mwenyewe kwa kina jambo lolote likikutokea, kujaribu kujua mapenzi ya Mungu na kujaribu kuona mapenzi ya Mungu ni yapi katika suala hili, Anataka ufanikishe nini, na ni jinsi gani utayajali mapenzi Yake? Kwa mfano: jambo fulani linafanyika linalokutaka uvumilie hali ngumu, wakati huo unapaswa ufahamu ni nini mapenzi ya Mungu, na ni jinsi gani unapaswa kuyajali mapenzi ya Mungu. Usijiridhishe mwenyewe: Jiweke kando kwanza. Hakuna kitu kilicho duni kuliko mwili. Ni lazima udhamirie kumridhisha Mungu, na ni lazima utekeleze wajibu wako. Katika mawazo kama hayo, Mungu atakupa nuru ya kipekee katika jambo hili, na moyo wako pia utapata faraja. Jambo lolote likikutendekea, liwe dogo au kubwa, ni sharti kwanza ujiweke pembeni na kuuona mwili kama kitu duni zaidi kuliko vitu vyote. Kadiri unavyouridhisha mwili zaidi, ndivyo unavyochukua uhuru zaidi; ukiuridhisha mara hii, wakati mwingine utataka zaidi, na jinsi hili linaendelea, ndivyo unapata kuupenda mwili hata zaidi. Mwili mara zote una tamaa kupita kiasi, mara zote mwili unakutaka uuridhishe, na kwamba uutosheleze kwa ndani, iwe ni katika chakula unachokula, unachokivaa, au kuwa na hasira katika matendo yako, au kuushawishi udhaifu na uzembe wako… Kadiri unavyouridhisha mwili zaidi, ndivyo tamaa yake inaongezeka, na jinsi mwili unavyopotoka zaidi, hadi kufikia kiwango ambacho miili ya watu inahodhi dhana nzito, na kutomtii Mungu, na kujiinua, na kuanza kuishuku kazi ya Mungu. Kadiri unavyouridhisha mwili zaidi, ndivyo udhaifu wa mwili unavyokuwa mkubwa; daima utahisi kuwa hakuna anayekuonea huruma kwa udhaifu wako, daima utaamini kuwa Mungu amezidi sana, na utasema: Mungu anawezaje kuwa mkali namna hii? Ni kwa nini Hawezi kuwapa watu nafasi? Watu wakiudekeza sana mwili, na kuupenda kupindukia, basi watajiponza wao wenyewe. Ikiwa unampenda Mungu kwa dhati, na huuridhishi mwili, basi utaona kuwa kila anachokifanya Mungu ni chenye haki sana, na kizuri sana, na kwamba laana Yake kwa uasi wako na hukumu ya udhalimu wako ni haki. Zitakuwepo nyakati ambapo Mungu atakurudi na kukufundisha nidhamu, na kuanzisha mazingira ya kukukasirisha, na kukushurutisha uje mbele Zake—na daima utahisi kuwa anachokifanya Mungu ni cha ajabu. Hivyo utahisi kana kwamba hakuna uchungu mwingi, na kwamba Mungu anapendeza. Ukifuata udhaifu wa mwili, na kusema kwamba Mungu amezidi, basi daima utahisi uchungu na daima utahuzunika, na utakosa uwazi kuhusu kazi yote ya Mungu na itaonekana kana kwamba Mungu hana huruma kwa udhaifu wa mwanadamu, na Hatambui shida za mwanadamu. Hivyo utajihisi mnyonge na mpweke, kana kwamba umekumbwa na dhuluma kubwa, na wakati huo utaanza kulalama. Kadiri unavyoutosheleza udhaifu wa mwili, ndivyo unavyohisi kuwa Mungu anazidi, hadi inakuwa mbaya kiasi kwamba unaikana kazi ya Mungu, na kuanza kumpinga Mungu na kujaa uasi. Hivyo unafaa kuuasi mwili na usiutosheleze: “Mume wangu(mke), watoto, matarajio, ndoa, familia—hakuna hata moja kati ya haya ambalo ni la thamani! Moyoni mwangu mna Mungu pekee na nitajaribu kumridhisha Mungu kadiri ya uwezo wangu, na si kuuridhisha mwili.” Lazima uwe na azimio hili. Daima ukiwa na azimio hili, basi ukiuweka ukweli katika vitendo, na kujiweka kando, utaweza kufanya hivyo kwa juhudi kidogo. Inasemekana kuwa kulikuwepo na mkulima aliyeona nyoka barabarani aliyekuwa ameganda. Huyu mkulima alimchukua yule nyoka na kumweka kifuani mwake, na baada ya yule nyoka kuamka alimuuma yule mkulima hadi akafa. Miili ya wanadamu ni kama yule nyoka: asili yake ni kuyadhuru maisha yao—na ikipata mbinu yake kikamilifu, maisha yako yanapotea. Mwili ni wa Shetani. Kuna tamaa kupita kiasi ndani yake, hujithamini wenyewe, unafurahia faraja, na kushangilia burudani, kujiachilia katika uvivu na uzembe, na baada ya kuuridhisha kwa kiwango fulani mwishowe utakuangamiza. Hivi ni kusema, ukiuridhisha sasa, wakati mwingine utakuomba zaidi. Daima mwili una tamaa na matakwa kupita kiasi, na unajinufaisha kutokana na wewe kuutosheleza mwili na kukufanya uufurahie hata zaidi na kuishi katika starehe zake—na ikiwa hutaushinda, mwishowe utajipotosha. Iwapo utapata uzima mbele za Mungu, na namna hatima yako itakavyokuwa, inategemea uasi wako dhidi ya mwili utakuwa wa namna gani. Mungu amekuokoa, na kukuteua na kukuamulia kabla, bado ikiwa leo hauko radhi kumridhisha, hauko radhi kuuweka ukweli katika vitendo, hauko radhi kuuasi mwili wako kwa moyo umpendao Mungu kwa dhati, hatimaye utajiangamiza mwenyewe, na kwa hivyo utapitia mateso mengi. Ikiwa mara zote unautosheleza mwili, Shetani atakumeza hatua kwa hatua, na kukuacha bila uzima, au upako wa Roho, hadi siku itafika ambayo ndani utakuwa giza. Ukiishi katika giza, utakuwa umetekwa nyara na Shetani, hutakuwa na Mungu tena moyoni mwako, na wakati ule utaukataa uwepo wa Mungu na kumwacha. Kwa hivyo, ikiwa unataka kumpenda Mungu, ni lazima ulipe gharama ya uchungu na kupitia shida. Hakuna haja ya hamasa za nje na shida, kusoma zaidi na kuzungukazunguka zaidi; badala yake, unafaa kuweka kando vitu vilivyomo ndani yako: mawazo kupita kiasi, maslahi ya kibinafsi, na masuala yako binafsi, dhana, na motisha. Hayo ndiyo mapenzi ya Mungu.
Ushughulikiaji wa Mungu juu ya tabia za nje za watu ni sehemu moja ya kazi Yake; kwa mfano, kushughulikia ubinadamu wa watu wa nje, usiokuwa wa kawaida, au maisha na tabia zao, njia na desturi zao, na vilevile vitendo vyao vya nje, na hamasa zao. Lakini Anapowataka watu wauweke ukweli katika vitendo na wabadilishe tabia zao, kimsingi kinachoshughulikiwa hapa ni motisha na mawazo yaliyo ndani yao. Kushughulikia tabia zako za nje tu si kugumu; ni sawa na kukukataza kula vitu uvipendavyo, jambo ambalo ni rahisi. Kinachogusia dhana zilizo ndani yako, hata hivyo, si rahisi kukiachia: inakuhitaji uuasi mwili wako, na kulipa gharama, na kuteseka mbele za Mungu. Hii ndiyo hali hasa katika motisha za watu. Tangu wakati wa imani yao kwa Mungu mpaka leo, watu wamekuwa na motisha ambazo si sahihi. Wakati ambapo huweki ukweli katika vitendo, unahisi kuwa motisha zako ni sahihi, lakini jambo likikutokea, utaona kuwa kuna motisha nyingi ndani zisizo sahihi. Hivyo, Mungu akiwafanya watu kuwa wakamilifu, Anawafanya kugundua kuwa kuna dhana nyingi ndani yao ambazo zinawazuia kumfahamu Mungu. Ukitambua kuwa motisha zako zina makosa, kama unaweza kuacha kutenda kulingana na motisha na dhana zako, na unaweza kuwa na ushuhuda wa Mungu na kusimama imara katika msimamo wako kwa kila lifanyikalo kwako, hili linathibitisha kuwa umeuasi mwili wako. Ukiasi dhidi ya mwili wako, bila shaka kutakuwa na vita ndani yako. Shetani atajaribu kufanya watu kuifuata, atajaribu kuwafanya wafuate dhana za kimwili na kutekeleza maslahi ya kimwili—ila maneno ya Mungu yatawapa nuru watu na kuwaangazia kwa ndani, na wakati huu itakuwa juu yako ikiwa utamfuata Mungu au utamfuata Shetani. Mungu anawataka watu kuweka ukweli katika matendo kimsingi kushughulikia mambo yaliyo ndani yao, kushughulikiwa fikira zao, na dhana zao ambazo haziufuati moyo wa Mungu. Roho Mtakatifu huwagusa watu ndani ya mioyo yao, na kuwapa nuru na mwangaza. Kwa hivyo katika tukio lolote katika vita: Kila wakati watu wanapoweka ukweli katika vitendo, au kuweka mapenzi ya Mungu katika vitendo, huwa kuna vita vikali, na japokuwa mambo yanaweza kuonekana shwari katika miili yao, ila ndani ya mioyo yao kutakuwa na vita vya kufa na kupona—na ni baada tu ya hivi vita vikali, baada ya kutafakari kwa kina, ndipo ushindi au kushindwa kunaweza kuamuliwa. Mtu anashindwa kujua ama acheke au alie. Kwa sababu motisha nyingi ndani ya watu zina makosa, ama kwa sababu kazi kubwa ya Mungu inakinzana na dhana zao, watu wakiuweka ukweli katika vitendo vita vikali huzuka kisirisiri. Baada ya kuuweka huu ukweli katika vitendo, kisirisiri watu watakuwa wamemwaga machozi mengi sana ya huzuni kabla ya kuamua kumridhisha Mungu. Ni kwa sababu ya vita hivi watu huvumilia shida na usafishaji; huku ni kuteseka kwa kweli. Vita vikikukabili, kama unaweza kusimama kweli upande wa Mungu, utaweza kumridhisha. Kuteseka katika harakati ya kutenda ukweli hakuepukiki; ikiwa, wanapoweka ukweli katika vitendo, kila kitu ndani yao kingekuwa sawa, basi wasingehitaji kufanywa wakamilifu na Mungu, na kusingekuwa na vita, na hawangeteseka. Ni kwa sababu kuna mambo mengi ndani ya watu ndipo hawafai kutumiwa na Mungu, na tabia nyingi za uasi wa mwili, ndipo watu wanapaswa kujifunza funzo la kuasi dhidi ya mwili kwa kina zaidi. Huku ndiko Mungu anaita kuteseka ambako Alimtaka mwanadamu kushiriki Naye. Ukikumbana na shida, fanya hima na umwombe Mungu: Ee Mungu! Ninataka kukuridhisha, ninataka kustahimili mateso ya mwisho ili kuuridhisha moyo Wako, na bila kujali kuwa vikwazo ninavyokumbana navyo ni vikubwa kiasi gani, bado ni sharti nikuridhishe. Hata ikiwa ni kuyatoa maisha yangu yote, bado ni sharti nikuridhishe! Ukiomba na hili azimio utaweza kusimama imara katika ushuhuda wako. Kila wawekapo ukweli katika vitendo, kila wapitiapo usafishaji, kila wanapojaribiwa, na kila wakati kazi ya Mungu inapowashukia, watu wanapitia mateso makubwa. Haya yote ni mtihani wa watu, na kwa hivyo ndani yao wote mna vita. Hii ndiyo gharama hasa wanayolipa. Kusoma zaidi neno la Mungu na kuzungukazunguka zaidi, kwa namna fulani ni gharama. Ndiyo watu wanapaswa kufanya, ndio wajibu wao, na jukumu ambalo ni sharti walitimize, lakini ni lazima watu waweke kando yale yanayofaa kuwekwa kando. Ikiwa hamwezi, basi haijalishi mateso yako yatakuwa makubwa kiasi gani, na utazunguka kiasi gani, yote yatakuwa bure! Hivi ni kusema, ni mabadiliko ndani yako tu yanaweza kuamua iwapo mateso yako ya nje yana thamani. Tabia yako ya ndani ikibadilika na ikiwa umeweka ukweli katika vitendo, basi mateso yako yote ya nje yatapata kibali cha Mungu; ikiwa hakujakuwa na mabadiliko katika tabia yako ya ndani, basi haijalishi unateseka kiasi gani au unazungukazunguka kiasi gani nje, hakutakuwa na kibali kutoka kwa Mungu—na mateso ambayo hayajaidhinishwa na Mungu ni bure! Hivyo, kama gharama ambayo umelipa imedhinishwa na Mungu inaamuliwa na kama umekuwa na mabadiliko ndani yako au la, na kama unatia ukweli katika vitendo na kuasi dhidi ya motisha na dhana zako mwenyewe ili kupata ridhaa ya mapenzi ya Mungu, ufahamu wa Mungu, na uaminifu kwa Mungu. Haijalishi unazungukazunguka kiasi gani, ikiwa hujawahi kujua kuasi dhidi ya motisha zako, unatafuta tu matendo na hamasa za nje, na usitilie maanani maisha yako, basi taabu zako zitakuwa zimepita bure. Ikiwa una kitu unachotaka kusema katika mazingira fulani, ila kwa ndani huhisi ni sawa, kwamba hakina faida kwa ndugu na dada zako, na kinaweza kuwadhuru, basi na usikiseme, uchague kuumia kwa ndani, kwa kuwa haya maneno hayawezi kuridhisha mapenzi ya Mungu. Wakati huu, kutakuwa na vita ndani yako, lakini utakuwa tayari kuumia na kuviacha uvipendavyo, utakuwa radhi kustahimili haya mateso ili kumridhisha Mungu na ingawa utaumia kwa ndani, hutautosheleza mwili, na moyo wa Mungu utakuwa umeridhishwa, hivyo utafarijika kwa ndani. Kwa hakika huku ni kulipa gharama, na ndiyo gharama inayotakiwa na Mungu. Ukitenda kwa njia hii, kwa hakika Mungu atakubariki; ikiwa huwezi kulifanikisha hili, basi haijalishi unaelewa kiasi gani, au unaweza kunena vyema kiasi gani, yote haya hayatafaa kitu! Katika njia ya kumpenda Mungu, ikiwa unaweza kusimama upande wa Mungu anapopigana na Shetani, na usimgeukie Shetani, basi utakuwa umefanikisha mapenzi ya Mungu, na utakuwa umesimama imara katika ushuhuda wako.
Katika kila hatua ya kazi anayoifanya Mungu ndani ya watu, kwa nje inaonekana kama maingiliano kati ya watu, kana kwamba yalizaliwa kwa mipango ya wanadamu au kutokana na kuingilia kwa wanadamu. Ila kisirisiri, hatua ya kazi, na kila kitu kinachotendeka, ni pingamizi la Shetani kwa Mungu, na huhitaji watu kuwa imara katika ushuhuda wao kwa Mungu. Kwa mfano, tazama wakati Ayubu alijaribiwa: kisirisiri, Shetani alikuwa akiwekeana dau na Mungu, na kilichomtokea Ayubu kilikuwa ni matendo ya wanadamu, na kuingilia kwa wanadamu. Kuna pingamizi la Shetani kwa Mungu katika kila hatua ambayo Mungu anatenda ndani yenu—katika kila kitu kuna vita. Kwa mfano, ikiwa unawabagua ndugu na dada zako, utakuwa na maneno ambayo unataka kusema—maneno unayohisi huenda yasimpendeze Mungu—lakini usipoyasema, utahisi kutoridhika ndani, na kwa wakati huu vita vitazuka ndani yako: “Niseme au nisiseme?” Hivi ndivyo vita. Kwa hivyo, katika kila jambo unalopitia kuna vita, na wakati kuna vita ndani yako, kutokana na ushirikiano wako na kuteseka kwako, Mungu anafanya kazi ndani yako. Hatimaye unaweza kuliweka kando jambo lenyewe na ghadhabu yako inazimika. Hiyo ndiyo athari ya ushirika wako na Mungu. Kila kitu wafanyacho watu kinawahitaji kulipa gharama fulani katika juhudi zao. Bila taabu ya kweli, hawawezi kumridhisha Mungu, hata hawakaribii kumridhisha Mungu, na wanarusha tu maneno matupu! Je, haya maneno matupu yaweza kumridhisha Mungu? Wakati Mungu na Shetani wanapigana katika milki ya kiroho, utamridhishaje Mungu, na utasimamaje imara katika ushuhuda wako Kwake? Unapaswa kujua kuwa kila kitu unachokipitia ni majaribu makubwa na ndipo Mungu hukuhitaji kuwa na ushuhuda. Kwa nje yataonekana kama mambo madogo; lakini haya mambo yakitendeka huonyesha kama unampenda Mungu au la. Ikiwa unampenda, utaweza kusimama imara katika ushuhuda wako Kwake, na ikiwa hujaweka upendo Wake katika vitendo, hili linaonyesha kuwa wewe si Mtu ambaye anapenda kuuweka ukweli katika vitendo, kwamba huna ukweli, huna uzima, kuwa wewe ni makapi! Mambo huwatokea watu wakati Mungu anawataka wasimame imara katika ushuhuda wao Kwake. Hakuna kubwa lililokutendekea kwa sasa, na huna ushuhuda mkubwa, lakini kila chembe ya maisha yako ya kila siku inahusiana na ushuhuda kwa Mungu. Ikiwa utawavutia ndugu na dada zako, wanafamilia, na kila aliye karibu nawe; ikiwa siku moja wasioamini watakuja na wavutiwe na yote unenayo na utendayo, na kuona kuwa yote afanyayo Mungu ni ya ajabu, basi utakuwa umekuwa na ushuhuda. Ijapokuwa huna ufahamu na wewe si mwerevu sasa, kupitia kwa kufanywa mkamilifu na Mungu, unaweza kumridhisha na kuzingatia mapenzi Yake. Wengine wataona kazi Yake kubwa miongoni mwa wasio werevu. Watu huja kumjua Mungu na huwa washindi mbele ya Shetani na waaminifu kwa Mungu kwa kiwango fulani. Hakuna atakayekuwa na uthabiti kuliko hili kundi la watu. Huu utakuwa ushuhuda mkubwa zaidi. Ijapokuwa huwezi kufanya kazi kubwa, unaweza kumridhisha Mungu. Wengine hawawezi kuyaacha mawazo yao, ila wewe unaweza; wengine hawawezi kuwa na ushuhuda kwa Mungu wakati wa mapito yao ya kweli, ila unaweza kutumia hadhi na matendo yako ya kweli kulipia mapenzi ya Mungu na kuwa na ushuhuda mkubwa Kwake. Hili ndilo huhesabika kama mapenzi ya kweli kwa Mungu. Ikiwa huliwezi hili, basi hutoi ushuhuda miongoni mwa jamaa zako, miongoni mwa ndugu zako, miongoni mwa dada zako, au mbele ya walimwengu. Ikiwa huwezi kuwa na ushuhuda mbele ya Shetani, Shetani atakucheka, atakuchukulia kama mzaha, mwanasesere, mara kwa mara atakuchezea na kukughadhibisha. Majaribu mengi yatakupata siku za usoni—lakini ikiwa leo unampenda Mungu kwa moyo wa dhati, na ikiwa haijalishi ukubwa wa majaribu yaliyo mbele, bila kujali unachokipitia, unaweza kusimama imara katika ushuhuda wako, na kuweza kumridhisha Mungu, basi moyo wako utafarijiwa, na utakuwa jasiri hata majaribu utakayokabiliana nayo siku za usoni yawe makubwa kiasi gani. Hamwezi kuona ni nini kitatendeka siku za usoni; mnaweza tu kuridhisha Mungu katika hali ya leo. Hamwezi kufanya kazi yoyote kubwa, na unafaa kulenga kumridhisha Mungu kwa kuyapitia maneno yake katika maisha halisi, na kuwa na ushuhuda thabiti na mzito ambao unamtia aibu Shetani. Japo mwili wako hautaridhishwa na utateseka, utakuwa umemridhisha Mungu na kumletea aibu Shetani. Ikiwa daima unatenda hivi, Mungu atakufungulia njia mbele yako. Na siku moja, jaribio kubwa likija, wengine wataanguka chini, ila utaweza kuendelea kusimama imara: kwa sababu ya gharama uliyolipa, Mungu atakulinda ili usimame imara na usianguke. Kwa kawaida, ikiwa unaweza kuweka ukweli katika vitendo na kumridhisha Mungu kwa moyo ambao unampenda kweli, kwa hakika Mungu atakulinda wakati wa majaribu ya siku zijazo. Japokuwa wewe ni mpumbavu na mwenye kimo cha chini na usiye mwerevu, Mungu hatakubagua. Inategemea iwapo motisha zako ni za haki. Unaweza kumridhisha Mungu leo, iwapo uko makini na masuala madogo, unamridhisha Mungu kwa mambo yote, una moyo unaompenda Mungu kwa dhati, unampa Mungu moyo wa dhati, na japokuwa kuna baadhi ya mambo ambayo huwezi kuelewa, unaweza kwenda mbele za Mungu kurekebisha motisha zako, na kuyafuata mapenzi ya Mungu, na kufanya kila lipaswalo kumridhisha Mungu. Pengine ndugu na dada zako wataachana nawe, lakini moyo wako utakuwa unamridhisha Mungu, na hutatamani raha za mwili. Ikiwa daima unatenda kwa namna hii, utalindwa majaribu yakikusibu.
Majaribu haya yanailenga hali gani ya ndani ya watu? Yanalenga tabia ya uasi ndani ya watu ambayo haiwezi kumridhisha Mungu. Kuna mengi ambayo ni machafu ndani ya watu, na mengi ambayo ni ya unafiki, na kwa hivyo Mungu anawatia katika majaribu ili kuwasafisha. Lakini, ikiwa leo unaweza kumridhisha, basi majaribu ya siku zijazo yatakuwa ukamilifu kwako. Ikiwa leo, huwezi kumridhisha Mungu, basi majaribu ya siku za usoni yatakushawishi, na utaanguka bila kujua, na wakati huo hutaweza kujisaidia mwenyewe, kwani huendani na kazi ya Mungu, na huna kimo halisi. Na kwa hivyo, kama unataka kuweza kusimama imara katika siku za usoni, kumridhisha vyema Mungu, na kumfuata hadi mwisho, unapaswa kujenga msingi thabiti leo, unafaa kumridhisha Mungu kwa kutia ukweli katika vitendo kwa kila jambo, na kuzingatia mapenzi Yake. Iwapo daima unatenda kwa namna hii, kutakuwa na msingi ndani yako, na Mungu atahamasisha ndani yako moyo unaompenda, na Atakupa imani. Siku moja ambapo majaribu yatakuwa yamekukumba kwa kweli, ijapo utaumia, na kuhisi umedhulumiwa kwa kiwango fulani, na kuwa na huzuni kubwa, kana kwamba ulikuwa umekufa—ila mapenzi yako kwa Mungu hayatabadilika, na yataongezeka zaidi. Hizo ni baraka za Mungu. Ikiwa unaweza kumkubali Mungu na yote asemayo na atendayo leo kwa moyo mtiifu, basi kwa hakika utabarikiwa na Mungu, na kwa hivyo utakuwa mtu aliyebarikiwa na Mungu, na anayepokea ahadi Yake. Ikiwa leo hutendi, siku ambayo majaribu yatakukumba utakosa imani au moyo wenye mapenzi, na wakati huo jaribu litakuwa kishawishi; utatoswa ndani ya kishawishi cha Shetani na hutapata namna ya kuponyoka. Leo, unaweza kusimama imara jaribio dogo likikukabili, ila huenda usiweze kusimama imara siku ambayo jaribio kubwa litakukumba. Baadhi ya watu hujivuna, na kufikiri kwamba wako karibu na ukamilifu. Ikiwa huzami zaidi wakati huo, na kuridhika, basi utakuwa hatarini. Leo, Mungu hafanyi kazi ya majaribu makubwa, kwa kuonekana, kila kitu kiko salama, ila Mungu atakapokujaribu, utagundua kuwa umepungukiwa sana, kwani kimo chako ni kidogo mno, na huna uwezo wa kustahimili majaribu mazito. Ikiwa leo, hutasonga mbele, ukibaki katika hatua ile ile, basi dhoruba nzito ikija utaanguka. Mara nyingi inafaa mtazame udogo wa kimo chenu; mtapiga hatua kwa njia hii tu. Ikiwa unauona udogo wa ukomavu wako wakati wa majaribu tu, kwamba kimo chako ni dhaifu, kwamba kuna kidogo sana ndani yako ambacho ni halisi, na kwamba hutoshi kwa mapenzi ya Mungu—na kama utagundua haya wakati wa majaribu tu, utakuwa umechelewa mno.
Ikiwa hujui tabia ya Mungu, bila shaka utaanguka wakati wa majaribu, kwa kuwa hufahamu jinsi Mungu anavyowafanya watu kuwa wakamilifu, na ni kwa njia gani Huwafanya wakamilifu, na majaribu ya Mungu yakikushukia na yasilingane na mawazo yako, utashindwa kusimama imara. Upendo wa kweli wa Mungu ni tabia Yake kamili, na tabia kamili ya Mungu ikionyeshwa kwako, hili linakuletea nini mwilini mwako? Tabia ya haki ya Mungu ikionyeshwa kwako, bila shaka mwili wako utapata uchungu mkubwa. Iwapo hutapata haya maumivu, basi huwezi kufanywa mkamilifu na Mungu, wala huwezi kumpa Mungu mapenzi ya kweli. Mungu akikufanya mkamilifu kwa hakika atakuonyesha tabia Yake kamili. Tangu uumbaji hadi leo, Mungu hajawahi kuonyesha tabia Yake kamili—ila katika siku za mwisho Anaifichua kwa hili kundi la watu ambao Aliwateua awali na kuwachagua, na kwa kuwafanya watu wakamilifu, Anaiweka wazi tabia Yake, na kupitia kwayo Analifanya kamili kundi la watu. Huo ndio upendo wa kweli wa Mungu kwa watu. Kuyapitia mapenzi ya kweli ya Mungu kunawapasa watu wastahimili uchungu mkali, na kulipa gharama kubwa. Ni baada tu ya hili ndipo watapatikana na Mungu na waweze kutoa tena mapenzi ya kweli kwa Mungu, na ni hapo tu ndipo Moyo wa Mungu utaridhishwa. Ikiwa watu wanataka wafanywe wakamilifu na Mungu, na kama wanataka kufanya na mapenzi Yake, na kumpa Mungu mapenzi yao ya dhati kikamilifu, ni sharti wapitie mateso mengi na maumivu makali kutokana na hali hizo, kupata uchungu mkali kuliko mauti, hatimaye watashurutishwa kuirejesha mioyo yao ya kweli kwa Mungu. Ikiwa mtu anampenda Mungu kwa dhati au la, itafichuliwa wakati wa shida na usafishaji. Mungu hutakasa mapenzi ya watu, na hili vilevile hupatikana tu ndani ya shida na usafishaji.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Ijumaa, 15 Machi 2019

Matamshi ya Mungu | “Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III” Sehemu ya Saba

Matamshi ya Mungu | “Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III” Sehemu ya Saba

Mwenyezi Mungu anasema,“Kuonekana kwa Bwana Yesu kulifanikisha kujali Kwake kwingi kwa minajili ya wafuasi Wake katika ubinadamu na akakupokeza kwa mwili Wake wa kiroho,au unaweza kusema uungu Wake 。Kuonekana Kwake kuliwaruhusu watu kuwa na hali nyingine waliyopitia na hisia walizopitia zinazohusu kujali na utunzaji wa Mungu huku kukithibitisha kwa uthabiti kwamba Mungu Ndiye anayefungua enzi,anayeiendeleza enzi,na Yeye ndiye anayetamatisha enzi。Kupitia kwa Kuonekana Kwake Aliipatia nguvu imani ya watu wote,na kupitia kwa Kuonekana Kwake alithibitishia ulimwengu hoja kwamba Yeye ni Mungu Mwenyewe。Hali hii iliwapa wafuasi Wake uthibitisho wa milele,na kupitia kwa Kuonekana Kwake pia Aliweza kufungua awamu ya kazi Yake katika enzi mpya。“Tazama zaidi:Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Kumjua Mungu Ndiyo Njia ya Kumcha Mungu na Kuepuka Maovu”
Baada ya kushiriki kuhusu haya yote, je, mnao ufahamu wa kweli wa mapenzi ya Mungu? Mungu anaona tukio hili la usimamizi wa binadamu, wa kuwaokoa wanadamu, kama muhimu sana kuliko chochote kingine. Huyafanya mambo haya yote si kwa kutumia akili Zake tu, wala si kwa kutumia maneno Yake tu, na vilevile Yeye hafanyi hivi hususan kwa juujuu tu—Yeye huyafanya mambo haya yote kwa mpango, kwa viwango, na kwa mapenzi Yake. Ni wazi kwamba kazi hii ya kumwokoa binadamu imeshikilia umuhimu mkubwa kwa Mungu na hata binadamu. Haijalishi kazi ilivyo ngumu, haijalishi changamoto ni kubwa jinsi gani, haijalishi binadamu ni wanyonge jinsi gani, au binadamu amekuwa mwasi wa kweli, hakuna chochote kati ya haya ambacho ni kigumu kwa Mungu. Mungu hujibidiisha Mwenyewe, Akitumia jitihada Zake za bidii za kazi na kusimamia kazi ambayo Yeye Mwenyewe Anataka kutekeleza. Yeye pia Anapanga kila kitu na kuwatawala watu wote na kazi ambayo Anataka kukamilisha—hakuna chochote kati ya haya ambacho kimefanywa awali. Ndiyo mara ya kwanza Mungu ametumia mbinu hizi na kulipa gharama kubwa kwa minajili ya mradi huu mkubwa wa kusimamia na kumwokoa mwanadamu. Huku Mungu akiwa Anatekeleza kazi hii, hatua kwa hatua Anawaonyesha binadamu bila kuficha bidii Yake, kile Alicho nacho na kile Alicho, hekima na uweza, na kila dhana ya tabia Yake. Anafichua bila kuacha chochote haya yote kwa mwanadamu kidogo kidogo, Akifichua na kuonyesha mambo haya kwa namna ambayo Hajawahi kufanya awali. Kwa hivyo, katika ulimwengu mzima, mbali na watu ambao Mungu analenga kuwasimamia na kuwaokoa, hakujawahi kuwepo na viumbe vyovyote vilivyo karibu na Mungu, ambavyo vinao uhusiano wa karibu sana na Yeye. Katika moyo Wake, yule mwanadamu Anayetaka kumsimamia na kumwokoa ndiye muhimu zaidi, na Anamthamini mwanadamu huyu zaidi ya kitu kingine chochote; hata ingawa Amelipia gharama ya juu na ingawa Anaumizwa na kutosikilizwa bila kukoma na wao, Hakati tamaa na Anaendelea bila kuchoka katika kazi Yake bila ya malalamiko au majuto. Hii ni kwa sababu Anajua kwamba hivi karibuni au baadaye, binadamu siku moja wataitikia mwito Wake na kuguswa na maneno Yake, kutambua kwamba Yeye ndiye Bwana wa uumbaji, na kurudi upande Wake …
Baada ya kusikia haya yote leo, mnaweza kuhisi kwamba kila kitu ambacho Mungu anafanya ni kawaida sana. Yaonekana kwamba binadamu siku zote wamehisi mapenzi fulani ya Mungu kwao kutokana na matamshi Yake na pia kazi Yake, lakini siku zote kuna umbali fulani katikati ya hisia zao au maarifa yao na kile ambacho Mungu anafikiria. Kwa hivyo, Nafikiri ni muhimu kuwasiliana na watu wote kuhusu ni kwa nini Mungu alimuumba mwanadamu, na maelezo zaidi yanayoonyesha tamanio Lake la kuwapata watu aliokuwa Akitumainia. Ni muhimu kushiriki habari hii na kila mmoja, ili kila mmoja aweze kuwa wazi moyoni mwake. Kwa sababu kila fikira na wazo la Mungu, na kila awamu na kila kipindi cha kazi Yake vinafungamana ndani ya, na vyote hivi vimeunganishwa kwa karibu na, usimamizi Wake mzima wa kazi, unapoelewa fikira na mawazo ya Mungu, na mapenzi Yake katika kila hatua ya kazi Yake, ni sawa na ufahamu wa chanzo cha kazi ya mpango Wake wa usimamizi. Ni katika msingi huu ndipo ufahamu wako wa Mungu unapoanza kuwa wa kina. Ingawa kila kitu ambacho Mungu alifanya Alipoumba kwanza ulimwengu ambacho Nilitaja awali ni taarifa fulani tu kwa watu sasa na yaonekana kwamba hayana umuhimu sana katika utafutaji wa ukweli, katika mkondo wa kile ambacho utapitia kutakuwa na siku ambapo hutafikiria kuwa ni jambo rahisi sana kama mkusanyiko tu wa taarifa, wala kwamba ni kitu rahisi sana kama mafumbo fulani. Kwa kadri maisha yako yanavyoendelea na pale ambapo pana msimamo kidogo wa Mungu katika moyo wako, au unapokuja kuelewa waziwazi na kwa kina mapenzi Yake, utaweza kuelewa kwa kweli umuhimu na haja ya kile Ninachozungumzia leo. Haijalishi ni kwa kiwango kipi umeyakubali haya; ni muhimu kwamba uelewe na ujue mambo haya. Wakati Mungu anapofanya jambo, wakati Anapotekeleza kazi Yake, haijalishi kama amefanya na mawazo Yake au kwa mikono Yake, haijalishi kama ni mara ya kwanza ambapo Amelifanya au kama ni mara ya mwisho—mwishowe, Mungu anao mpango, na makusudio Yake na fikira Zake vyote vimo katika kila kitu Anachokifanya. Makusudio na fikira hizi vinawakilisha tabia ya Mungu, na vinaonyesha kile Alicho nacho na kile Alicho. Vitu hivi viwili—tabia ya Mungu na kile Alicho nacho na kile Alicho—lazima vieleweke na kila mmoja. Punde mtu anapoelewa tabia Yake na kile Alicho nacho na kile Alicho, ataanza kuelewa kwa utaratibu ni kwa nini Mungu anafanya kile Anachofanya na kwa nini Anasema kile Anachosema. Kutokana na hayo, anaweza kuwa na imani zaidi ya kumfuata Mungu, kuufuatilia ukweli, na kufuatilia mabadiliko katika tabia. Hivi ni kusema, ufahamu wa binadamu kuhusu Mungu na imani yake katika Mungu ni vitu viwili visivyoteganishwa.
Hata ingawa kile watu wanachosikia kuhusu au kupata ufahamu huo ni tabia ya Mungu, kile Alicho nacho na kile Alicho, kile wanachofaidi ni maisha yanayotoka kwa Mungu. Baada ya maisha haya kuhemshwa ndani yako, uchaji wako wa Mungu utakuwa mkubwa zaidi na zaidi, na kuvuna mavuno haya kunafanyika kwa kawaida sana. Kama hutaki kuelewa au kujua kuhusu tabia ya Mungu au kiini Chake, kama hutaki hata kutafakari juu ya mambo haya au kuyazingatia, Naweza kukuambia kwa hakika kwamba hiyo njia unayoifuatilia katika imani yako kwa Mungu haitawahi kukuruhusu kuyaridhisha mapenzi Yake au kupata sifa Zake. Zaidi ya hayo, huwezi kamwe kufikia wokovu—hizi ndizo athari za mwisho. Wakati watu hawamwelewi Mungu na hawajui tabia Yake, mioyo yao haiwezi kamwe kuwa wazi Kwake. Punde wanapomwelewa Mungu, wataanza kuelewa na kufurahia kile kilicho moyoni Mwake kwa kivutio na imani. Unapoelewa na kufurahia kile kilichomo ndani ya moyo wa Mungu, moyo wako utaanza kwa utaratibu, kidogokidogo, kuwa wazi Kwake. Wakati moyo wako unakuwa wazi Kwake, utahisi namna ambavyo mabadilishano yako na Mungu yatakavyokuwa ya aibu na duni, madai yako kutoka kwa Mungu na matamanio yako mengi binafsi. Moyo wako unapofunguka kwa kweli kwa Mungu, utaona kwamba moyo Wake ni ulimwengu usio na mwisho, na utaingia katika ulimwengu ambao hujawahi kuupitia awali. Katika ulimwengu huu hakuna kudanganya, hakuna udanganyifu, hakuna giza, hakuna maovu. Kunao ukweli wa dhati na uaminifu; kunayo nuru na uadilifu tu; kunayo haki na huruma. Umejaa upendo na utunzaji, umejaa rehema na uvumilivu, na kupitia katika ulimwengu huu utahisi shangwe na furaha ya kuwa hai. Mambo haya ndiyo ambayo Atakufichulia utakapoufungua moyo wako kwa Mungu. Hii dunia isiyo na kikomo imejaa hekima ya Mungu, na imejaa kudura Yake; umejaa pia upendo Wake na mamlaka Yake. Hapa unaweza kuona kila kipengele cha kile Mungu Alicho nacho na kile Alicho, ni nini kinachomletea Yeye shangwe, kwa nini Anakuwa na wasiwasi na kwa nini Anakuwa na huzuni, kwa nini Anakuwa na hasira…. Haya ndiyo ambayo kila mmoja anayeufungua moyo wake na kumruhusu Mungu kuingia ndani anaweza kuona. Mungu anaweza tu kuingia katika moyo wako kama utaufungua kwa ajili Yake. Unaweza kuona tu kile Mungu Alicho nacho na kile Alicho, na unaweza kuona tu mapenzi Yake kwako, kama Ameingia katika moyo wako. Wakati huo, utagundua kwamba kila kitu kuhusu Mungu ni chenye thamani, kwamba kile Alicho nacho na kile Alicho kina thamani sana ya kuthaminiwa. Ukilinganisha na hayo, watu wanaokuzunguka, vifaa na matukio katika maisha yako, hata wapendwa wako, mwandani wako, na mambo unayopenda, si muhimu sana. Ni madogo mno, na ni ya kiwango cha chini; utahisi kwamba hakuna chombo chochote cha anasa ambacho kitaweza kukuvutia tena, na vitu hivi haviwezi kukufanya kuvilipia gharama yoyote tena. Kwa unyenyekevu wa Mungu utaona ukubwa Wake na mamlaka Yake ya juu; aidha, katika jambo Alilofanya uliloliamini kuwa dogo mno, utaweza kuiona hekima Yake na uvumilivu Wake usio na mwisho, na utaiona subira Yake, uvumilivu Wake na ufahamu Wake kwako. Hili litazaa ndani yako upendo Kwake. Siku hiyo, utahisi kwamba mwanadamu anaishi katika ulimwengu mchafu, kwamba watu walio upande wako na mambo yanayokufanyikia katika maisha yako, na hata kwa wale unaopenda, upendo wao kwako, na ulinzi wao kama ulivyojulikana au kujali kwao kwako havistahili hata kutajwa—Mungu tu ndiye mpendwa wako na ni Mungu tu unayethamini zaidi. Wakati siku hiyo itawadia, Naamini kwamba kutakuwa na baadhi ya watu watakaosema: Upendo wa Mungu ni mkubwa na kiini Chake ni kitakatifu mno—ndani ya Mungu hakuna udanganyifu, hakuna uovu, hakuna wivu, na hakuna mabishano, lakini ni haki tu na uhalisi, na kila kitu Alicho nacho Mungu na kile Alicho vyote vinafaa kutamaniwa na binadamu. Binadamu wanafaa kujitahidi na kuwa na hamu ya kuvipata. Ni kwa msingi gani ndipo uwezo wa mwanadamu wa kutimiza haya umejengwa? Unajengwa kwa msingi wa ufahamu wa binadamu wa tabia ya Mungu, na ufahamu wao kuhusu kiini cha Mungu. Hivyo basi kuelewa tabia ya Mungu na kile Alicho nacho na kile Alicho, ni funzo la maisha yote kwa kila mtu na ni lengo la maisha yote linalofuatiliwa na kila mtu anayelenga kubadilisha tabia yake, na kutamani kumjua Mungu.
Tumezungumza tu kuhusu kazi yote ambayo Mungu amekamilisha, misururu ya mambo Aliyoyafanya kwa mara ya kwanza. Kila mojawapo ya mambo haya yanahusiana na mpango wa Mungu wa usimamizi na mapenzi ya Mungu. Yanahusiana pia na tabia binafsi ya Mungu na kiini Chake. Kama tunataka kuelewa bora zaidi kile Alicho nacho Mungu na kile Alicho, hatuwezi kukoma katika Agano la Kale au katika Enzi ya Sheria, lakini tunahitaji kusonga mbele pamoja na hatua ambazo Mungu alichukua katika kazi Yake. Hivyo basi, Mungu alipotamatisha Enzi ya Sheria na kuanza Enzi ya Neema, hatua zetu binafsi zimefika katika Enzi ya Neema—enzi iliyojaa neema na ukombozi. Katika enzi hii, Mungu tena Alifanya kitu cha muhimu sana kwa mara ya kwanza. Kazi katika enzi hii mpya kwa Mungu na hata kwa mwanadamu ilikuwa sehemu mpya ya kuanzia. Sehemu hii mpya ya kuanzia ilikuwa tena kazi mpya ambayo Mungu alifanya kwa mara ya kwanza. Kazi hii mpya ilikuwa kitu ambacho hakikuwahi kutokea awali ambacho Mungu alitekeleza na hakikufikirika na binadamu na viumbe vyote. Ni kitu ambacho kwa sasa kinajulikana kwa watu wote—hii ndiyo iliyokuwa mara ya kwanza Mungu aligeuka kuwa binadamu, mara ya kwanza Alianza kazi mpya kwa umbo la binadamu, Akiwa na utambulisho wa mwanamume. Kazi hii mpya ilionyesha kwamba Mungu alikuwa Amekamilisha kazi Yake katika Enzi ya Sheria, kwamba Asingefanya au kusema tena chochote chini ya sheria. Wala Asingewahi tena kuzungumza au kufanya chochote kwa mfano wa sheria au kulingana na kanuni au masharti ya sheria. Yaani, kazi Yake yote inayotokana na sheria ilisitishwa milele na isingeendelezwa, kwa sababu Mungu alitaka kuanza kazi mpya na kufanya mambo mapya, na mpango Wake kwa mara nyingine tena ulikuwa na sehemu mpya ya kuanzia. Hivyo basi, Mungu lazima Angemwongoza binadamu hadi katika enzi inayofuata.

Alhamisi, 14 Machi 2019

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Nne

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Nne

Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”. Maudhui ya video hii:
Uzao: Awamu ya Tano 
1. Mtu Hana Udhibiti wa Hatima ya Uzao Wake 
2. Baada ya Kulea Kizazi Kijacho, Watu Hufaidi Ufahamu Mpya wa Hatima Yao 
3. Kusadiki Katika Hatima si Kibadala cha Maarifa ya Ukuu wa Muumba 
4. Wale tu Wanaonyenyekea Ukuu wa Muumba Ndio Wanaweza Kupata Uhuru wa Kweli
Mwenyezi Mungu alisema,Mamlaka ya Mungu ni ya kipekee. Ndiyo maonyesho ya sifa ya, na hali halisi maalum ya, utambulisho wa Mungu Mwenyewe. Hakuna kiumbe ambacho kiliumbwa wala kile ambacho hakikuumbwa kinachomiliki maonyesho ya sifa kama hizi na hali halisi maalum; Muumba tu ndiye anayemiliki aina hii ya mamlaka. Hivyo ni kusema kwamba, ni Muumba tu—Mungu Yule wa kipekee—ambaye anaonyeshwa kwa njia hii na ndiye aliye na hali halisi hii. Kwa nini tuzungumzie mamlaka ya Mungu? Mamlaka ya Mungu Mwenyewe yanatofautiana vipi na mamlaka yaliyomo kwenye akili ya binadamu? Ni nini maalum sana kuyahusu? Na kunao umuhimu gani haswa kuyazungumzia hapa? Kila mmoja wenu lazima aweze kutilia maanani kwa umakinifu suala hili. Kwa watu wengi zaidi, “Mamlaka ya Mungu” ni fikira isiyoeleweka, ile ambayo ni ngumu sana kupata kuielewa, na mazungumzo yoyote kuihusu huenda yasizae matunda mazuri. Kwa hivyo lazima kutakuwepo na pengo kati ya maarifa ya mamlaka ya Mungu ambayo binadamu anaweza kumiliki, na hali halisi ya mamlaka ya Mungu. Ili kuliziba pengo hili, mtu lazima kwa utaratibu aweze kuelewa mamlaka ya Mungu kwa njia ya watu halisi-maishani, matukio, vitu au mambo muhimu yanayopatikana katika uwezo wa binadamu, na ambayo binadamu wanaweza kuyaelewa. Ingawaje kauli hii “Mamlaka ya Mungu” inaweza kuonekana kama isiyoeleweka, mamlaka ya Mungu kwa kweli si ya dhahania kamwe. Yeye yupo na binadamu kila dakika ya maisha yake, akimwongoza kila siku. Kwa hivyo, katika maisha ya kila siku ya kila mtu ataweza haswa kuona na kupitia dhana halisi ya mamlaka ya Mungu. Uhalisi huu ni ithibati tosha kwamba mamlaka ya Mungu kwa kweli yapo, na unakuruhusu kabisa kutambua na kuelewa hoja hii kwamba Mungu anamiliki mamlaka haya.
Mungu aliumba kila kitu, na baada ya kukiumba, Anao utawala juu ya kila kitu. Kuongezea kuwa na utawala juu ya kila kitu, pia anadhibiti kila kitu. Wazo hili linamaanisha nini “Mungu anadhibiti kila kitu”? Hali hii inaweza kuelezewa vipi? Hali hii inatumika vipi katika maisha halisi? Mnawezaje kuyajua mamlaka ya Mungu kwa kuelewa hoja hii kwamba “Mungu Anadhibiti kila kitu”? Kutoka kwenye kauli ile ile “Mungu anadhibiti kila kitu” tunafaa kuona kwamba kile ambacho Mungu anadhibiti si sehemu ya sayari, sehemu ya uumbaji, wala sehemu ya mwanadamu, lakini kila kitu: kuanzia kwa viumbe vile vikubwa hadi vile vidogovidogo, kuanzia kwa vile vinavyoonekana hadi visivyoonekana, kuanzia kwa nyota ulimwenguni hadi kwenye vitu vilivyo na uhai ulimwenguni, pamoja na viumbe vidogovidogo visivyoweza kuonekana kwa macho ya kawaida au viumbe vilivyo katika maumbo mengine. Huu ndio ufafanuzi hakika wa “kila kitu” ambacho Mungu “anadhibiti,” na ndio upana ambao Mungu anaonyesha ukuu Wake, urefu wa utawala na kanuni Yake.
Kabla ya binadamu hawa kujitokeza, viumbe vyote—sayari zote, nyota zote kule mbinguni—tayari vilikuwepo. Kwenye kiwango cha vitu vikubwa, vyombo hivi vya mbinguni vimekuwa vikizunguka mara kwa mara chini ya udhibiti wa Mungu, kwa uwepo wavyo wote, hata hivyo miaka mingi imepita. Ni sayari gani inaenda wapi na wakati gani haswa; ni sayari gani inafanya kazi gani, na lini; ni sayari gani inazunguka katika mzingo gani, na ni lini inatoweka au inabadilishwa—vitu hivi vyote vinasonga mbele bila ya kosa lolote dogo. Nafasi za sayari na umbali kati yazo ni masuala yanayofuata ruwaza maalum, ni masuala ambayo yanaweza kufafanuliwa kwa data yenye uhakika; njia ambazo zinasafiria, kasi na ruwaza ya mizingo yao, nyakati ambapo zinapatikana kwenye nafasi mbalimbali zinaweza kufafanuliwa kwa hakika na kufafanuliwa kwa sheria maalum. Kwa miaka na mikaka sayari zimefuata sheria hizi na hazijawahi kupotoka hata chembe. Hakuna nguvu inaweza kubadilisha au kutatiza mizingo yazo au ruwaza zao ambazo zinafuata. Kwa sababu sheria maalum zinazotawala mzunguko wazo na data yenye uhakika inayozifafanua iliamuliwa kabla na mamlaka ya Muumba, zinatii sheria hizi zenyewe, kulingana na ukuu na udhibiti wa Muumba. Kwenye kiwango cha mambo makubwamakubwa, si vigumu kwa binadamu kujua zaidi kuhusu ruwaza fulani, data fulani, pamoja na sheria au matukio fulani yasiyoeleweka au yasiyoelezeka. Ingawaje binadamu hawakubali kwamba Mungu yupo, haukubali hoja kwamba Muumba aliumba na anatawala kila kitu na zaidi ya yote hautambui uwepo wa mamlaka ya Muumba, wanasayansi wa kibinadamu, wanafalaki, nao wanafizikia wanachunguza na kugundua zaidi na zaidi kwamba uwepo wa kila kitu kwenye ulimwengu, na kanuni na ruwaza zinazoonyesha mzunguko wavyo, vinatawaliwa na kudhibitiwa na nishati nyeusi kubwa na isiyoonekana. Hoja hii inampa binadamu mshawasha wa kukubaliana na kutambua kwamba kunaye Mwenyezi aliye miongoni mwa ruwaza hizi za mzunguko, anayepangilia kila kitu. Nguvu zake si za kawaida, na ingawaje hakuna anayeweza kuona uso Wake wa kweli, Yeye hutawala na kudhibiti kila kitu kila dakika. Hakuna binadamu au nguvu zozote zile zinazoweza kuuzidi ukuu Wake. Huku binadamu akiwa amekabiliwa na hoja hii, lazima atambue kwamba sheria zinazotawala uwepo wa kila kitu haziwezi kudhibitiwa na binadamu, haziwezi kubadilishwa na yeyote; na wakati uo huo binadamu lazima akubali kwamba, binadamu hawezi kuelewa kikamilifu sheria hizi. Na hizi sheria hazitokei-kimaumbile lakini zinaamrishwa na Bwana na Mungu. Haya yote ni maonyesho na mamlaka ya Mungu yanayoonyesha kwamba mwanadamu anaweza kuelewa katika kiwango cha mambo makubwa.
Kwenye kiwango cha mambo madogomadogo, milima, mito, maziwa, bahari, na maeneo ya ardhi yote ambayo binadamu anatazama nchini, misimu yote ambayo yeye anapitia, mambo yote yanayopatikana kwenye ulimwengu, kukiwemo mimea, wanyama, vijiumbe na binadamu, vyote viko chini ya ukuu wa Mungu na vinadhibitiwa na Mungu Mwenyewe. Katika ukuu na udhibiti wa Mungu, vitu vyote vinakuwepo au vinatoweka kulingana na fikira Zake, maisha ya vitu hivi yanatawaliwa na sheria fulani, na vinakua na kuzaana kulingana nazo. Hakuna binadamu au kiumbe chochote kilicho juu ya sheria hizi. Kwa nini hali iko hivi? Jibu la pekee tu ni, kwa sababu ya mamlaka ya Mungu. Au, nikijibu kwa njia nyingine, kwa sababu ya fikira za Mungu na matamshi ya Mungu; kwa sababu Mungu Mwenyewe hufanya haya yote. Hivi ni kusema, ni mamlaka ya Mungu na ni akili ya Mungu ambayo iliunda sheria hizi; zitasonga na kubadilika kulingana na fikira Zake, na kusonga huku na mabadiliko haya yote yanafanyika au kutoweka kwa minajili ya mpango Wake. Hebu tuchukulie magonjwa ya mlipuko, kwa mfano. Yanazuka tu bila onyo, hakuna anayejua asili yake, au sababu maalum zinazoelezea ni kwa nini huwa yanafanyika, na kila wakati magonjwa ya mlipuko yanapofika mahali fulani, wale walio na bahati mbaya hawawezi kukwepa maafa. Sayansi ya binadamu inafafanua na kutuelewesha kwamba magonjwa ya mlipuko yanasababishwa na kuenea kwa vijiumbe maradhi vibaya au haribifu, na kasi yao, eneo lao, na mbinu ya kuenea kwake haiwezi kutabiriwa au kudhibitiwa na sayansi ya binadamu. Ingawaje binadamu huvipinga vijiumbe maradhi hivi kwa kila namna inayowezekana, huwa hauwezi kudhibiti ni watu gani au wanyama gani ambao wanaathiriwa kwa vyovyote vile wakati kunapokuwa na mkurupuko wa magonjwa mlipuko. Kitu cha pekee ambacho binadamu wanaweza kufanya ni kujaribu kuyazuia, kuyapinga, na kuyafanyia utafiti. Lakini hakuna anayejua chanzo asilia kinachoelezea mwanzo au mwisho wa magonjwa mlipuko yoyote ya kibinafsi, na hakuna anayeweza kuyadhibiti. Wakiwa wamekabiliwa na ongezeko na kuenea kwa magonjwa mlipuko, suala la kwanza ambalo binadamu hufanya ni kuunda chanjo, lakini mara nyingi magojwa mlipuko hayo hutoweka kabisa kabla ya hata chanjo kuwa tayari. Kwa nini magonjwa mlipuko hutoweka kabisa? Wengine husema kwamba viini vimeweza kudhibitiwa, wengine husema kwamba vimetoweka kabisa kwa sababu ya mabadiliko katika misimu…. Kuhusiana na ikiwa makisio haya ya kuchanganyikiwa ni kweli au la, sayansi haiwezi kutupa ufafanuzi wowote, na wala haitoi jibu lolote lenye uhakika. Kile ambacho binadamu wanakabiliwa nacho si makisio haya tu lakini pia ukosefu wa mwanadamu katika kuelewa na woga wa magonjwa mlipuko haya. Hakuna anayejua, baada ya kila kitu kuchambuliwa, ni kwa nini magonjwa mlipuko haya huanza au ni kwa nini huisha. Kwa sababu binadamu wanayo imani tu katika sayansi, unategemea pakubwa kwa sayansi hiyo, lakini hautambui mamlaka ya Muumba au kuukubali ukuu Wake, hautawahi kuwa na jibu.
Katika ukuu wa Mungu, mambo yote yapo na huangamia kwa sababu ya mamlaka Yake, kwa sababu ya usimamizi Wake. Baadhi ya mambo huja na kwenda polepole, na binadamu hawezi kutambua ni wapi yalitokea au kung’amua sheria ambazo mambo haya hufuata, sisemi hata kuelewa sababu za mambo haya kuja na kwenda. Ingawaje binadamu anaweza kushuhudia, kusikia, au kupitia yote yanayokuja na kuisha miongoni mwa mambo yote; ingawaje mambo haya yanao mwelekeo kwa binadamu, na ingawaje binadamu hung'amua kupitia kwa yaliyofichika akilini mwake, hali isiyokuwa ya kawaida, hali ya mara kwa mara au hata hali ya ajabu ya mambo mbalimbali, bado hajui chochote kuhusu mapenzi ya Muumba na akili Yake ambavyo vinaelezea mambo hayo. Kunazo hadithi nyingi zinazotokana na haya mambo yote, ukweli mwingi uliofichwa. Kwa sababu binadamu amepotoka na kwenda mbali na Muumba, kwa sababu hakubali hoja hii kwamba Mamlaka ya Muumba ndiyo hutawala mambo yote, hatawahi kujua kila kitu kinachofanyika katika ukuu Wake. Kwa sehemu nyingi zaidi, udhibiti na ukuu wa Mungu huzidi mipaka ya fikra ya binadamu, maarifa ya binadamu, kuelewa kwa binadamu, kuhusu kile ambacho sayansi ya binadamu inaweza kutimiza; uwezo wa binadamu walioundwa hauwezi kushindana nao. Baadhi ya watu husema “Kwa sababu hujashuhudia ukuu wa Mungu wewe mwenyewe, unawezaje kusadiki kwamba kila kitu kinatokana na mamlaka Yake?” Kuona si kuamini kila mara; kuona si kutambua na kuelewa kila mara. Kwa hivyo “sadiki” hutokea wapi? Ninaweza kusema kwa uhakika, “Sadiki inatokana na kiwango na kina cha kuelewa kwa watu kwa, na hali wanayopitia wao, uhalisi na chanzo kikuu cha mambo.” Kama unasadiki kwamba Mungu yupo, lakini huwezi kutambua, na wala huwezi kuelewa, hoja ya udhibiti wa Mungu na ukuu wa Mungu katika mambo yote, basi katika moyo wako hutawahi kukubali kwamba Mungu anayo mamlaka kama haya na kwamba mamlaka ya Mungu ni ya kipekee. Hutawahi kukubali kwa kweli Muumba kuwa Bwana wako, Mungu wako.
Sikiliza zaidi:

Jumanne, 12 Machi 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Tabia Yako Ni Duni Sana!

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Tabia Yako Ni Duni Sana!

Ninyi nyote mmeketi katika viti vya kifahari, mkiwafundisha wale wa vizazi vijana ambao ni wa aina yenu, ukiwafanya waketi nawe. Je, mngekosaje kujua kwamba wale “watoto” wenu walikuwa tayari hawana pumzi, na kwamba hawakuwa na kazi Yangu zamani? Utukufu Wangu huangaza kutoka nchi ya Mashariki hadi nchi ya Magharibi, lakini wakati utukufu Wangu huenea mpaka mwisho wa dunia na wakati unapoanza kuinuka na kuangaza, Nitaondoa utukufu wa Mashariki na kuuletea Magharibi ili kwamba watu hawa wa giza katika Mashariki ambao wameniacha Mimi watakuwa bila mwanga unaong’aa kuanzia hapo kwendelea. Wakati huo, mtaishi katika bonde la kivuli. Ingawa watu leo ni wazuri mara mia zaidi kuliko awali, bado hawawezi kuyatosheleza mahitaji Yangu, na bado wao si ushahidi mtukufu Kwangu. Kwamba nyinyi mnaweza kuwa wazuri mara mia zaidi kuliko awali yote ni matokeo ya kazi Yangu—ni tunda la kazi Yangu duniani. Hata hivyo, bado Ninahisi maudhi kwa maneno na matendo yenu, na tabia yenu, na Ninahisi hasira ya ajabu sana kwa matendo yenu mbele Yangu, kwa maana hamna ufahamu wowote Wangu. Kwa hiyo mnawezaje kuwa walio hai kutoka kwa utukufu Wangu, na mnawezaje kuwa waaminifu kabisa kwa kazi Yangu ya baadaye? Imani yenu ni nzuri sana; mnasema kwamba mko radhi kutoa maisha yenu kwa kazi Yangu, kufanya chochote na kila kitu kwa ajili yake, lakini tabia yenu haijabadilika sana. Kumekuwa tu na maneno ya kiburi, na matendo yenu halisi ni duni sana. Inaonekana kwamba ulimi na midomo ya mtu iko mbinguni lakini miguu ya mtu iko mbali sana duniani, hivyo maneno na matendo yake na sifa yake bado yako katika hali mbaya sana. Sifa zenu tayari zimeharibiwa, mwenendo wenu unashuka hadhi, njia yenu ya kuzungumza ni ya chini, maisha yenu ni ya kudharauliwa, na hata ubinadamu wenu wote ni wa chini. Nyinyi ni wa mawazo finyu kwa watu na nyinyi hubishana juu ya kila kitu kidogo. Nyinyi hugombana juu ya sifa zenu na hadhi zenu wenyewe, hata kufikia kiasi kwamba mko radhi kushuka kuzimu, katika ziwa la moto. Maneno na matendo yenu ya sasa yanatosha kiasi kwamba Ninaweza kuamua kuwa nyinyi ni wenye dhambi. Mtazamo wenu juu ya kazi Yangu unatosha Kwangu kutambua kuwa nyinyi ni wale wadhalimu, na tabia zenu zote zinatosha kusema kuwa nyinyi ni roho chafu ambazo zimejaa machukizo. Maonyesho yenu na kile mnachofichua ni tosha kusema kuwa nyinyi ni watu ambao mmekunywa damu ya kutosha ya pepo wachafu. Wakati kuingia katika ufalme kunapozungumzwa hamfichui hisia zenu. Mnaamini kuwa jinsi mlivyo sasa kunatosha kwenu kuingia katika lango la ufalme Wangu wa mbinguni? Je, mnaamini kuwa mnaweza kupata kuingia katika nchi takatifu ya kazi na maneno Yangu bila maneno na vitendo vyenu kupitia majaribio Yangu? Ni nani anayeweza kwa ufanisi kuyadanganya macho Yangu mawili? Je, tabia zenu za mazungumzo ya kudharauliwa na duni, zawezaje kuepuka Mimi kuona? Maisha yenu yameamuliwa na Mimi kama maisha ya kunywa damu ya pepo hizo chafu na kula nyama ya pepo hao wachafu kwa sababu mnachukua sura yao mbele Yangu kila siku. Mbele Yangu tabia zenu zilikuwa mbaya hasa, hivyo, ni vipi Mimi singeweza kuchukizwa? Katika kile mnachosema kuna najisi ya pepo wachafu: Nyinyi hudanganya, huficha, na kujipendekeza kama wale tu wanaofanya uchawi, kama wale wanaodanganya na kunywa damu ya wasio wa haki. Maonyesho yote ya wanadamu ni madhalimu sana, hiyo watu wote wanawezaje kuwekwa katika nchi takatifu ambako wenye haki wapo? Je, unafikiri kwamba tabia hiyo yako ya kudharauliwa inaweza kukubainisha kama mtakatifu dhidi ya wale wadhalimu? Huo ulimi wako unaofanana na nyoka hatimaye utaangamiza mwili wako ambao huleta maangamizi na hufanya machukizo, na mikono yako hiyo ambayo imefunikwa na damu ya pepo wachafu pia itavuta roho yako kuzimu hatimaye, hiyo kwa nini usichukue fursa hii kuitakasa mikono yako iliyofunikwa na uchafu? Na kwa nini huchukui fursa hii kuukata ulimi wako huo ambao husema maneno maovu? Inawezekana kuwa uko radhi kuteseka chini ya moto wa kuzimu kwa sababu ya mikono yako miwili na ulimi wako na midomo? Mimi huilinda mioyo ya watu wote kwa macho Yangu mawili kwa sababu muda mrefu kabla ya kuwaumba wanadamu, Nilikuwa Nimeishika mioyo yao ndani ya mikono Yangu. Zamani Nilibaini moyo wa mwanadamu, kwa hiyo mawazo ya ndani ya moyo wa mwanadamu yanawezaje kuyaepuka macho Yangu? Na wanawezaje kuwepo mapema ili kuepuka kuchomwa kwa Roho Wangu?
Midomo yako ni yenye huruma zaidi kuliko njiwa lakini moyo wako ni mbaya zaidi kuliko nyoka ya kale, hata midomo yako ni mizuri kama mwanamke Mlebanoni, lakini moyo wako si mwema kama ule wa wanawake Walebanoni na hakika hauwezi kulinganishwa na uzuri wa Wakanaani. Moyo wako ni mdanganyifu sana. Ninachochukia ni midomo ya wadhalimu na mioyo ya wadhalimu pekee. Mahitaji Yangu kwa watu si ya juu kuliko watakatifu, ni vile tu kwamba Mimi huhisi chukizo kwa matendo maovu ya wadhalimu na Natumaini kwamba wadhalimu huenda waweze kuondoa kuchafuka kwao na kukimbia kutoka kwa mashaka yao ya sasa ili waweze kutofautishwa na wale wadhalimu, na kuishi na kuwa watakatifu pamoja na wale wenye haki. Nyinyi mko katika hali sawa na Mimi, lakini mmefunikwa na uchafu, hakuna hata mfano kidogo wa wanadamu walioumbwa hapo mwanzo ndani yenu, na kwa sababu kila siku mnaiga mfano wa hao pepo wachafu na mnafanya kile wanachokifanya na kusema kile wanachokisema, kila sehemu zenu na hata ndimi zenu na midomo yenu imelowa katika maji yao mabaya. Ni kwa kiwango ambacho mmefunikwa kabisa na hayo mawaa na hakuna sehemu hata moja ambayo inaweza kutumiwa kwa kazi Yangu. Ni jambo la kusikitisha sana! Mnaishi katika ulimwengu huu wa farasi na ng’ombe lakini bado kwa kweli hamjihisi kuwa na wasiwasi; na mmejaa furaha na nyinyi huishi kwa uhuru na kwa urahisi. Mnaogelea katika maji haya mabaya lakini kwa kweli hamjui kwamba mmeanguka katika mazingira haya. Kila siku unaafikiana na pepo wachafu na una shughuli na “kinyesi.” Uhai wako ni duni sana, lakini hujui kwamba bila shaka huendelei kuishi katika ulimwengu wa kibinadamu na kwamba humo ndani ya ufahamu wako mwenyewe. Je, hujui kwamba maisha yako yalikanyagwa na pepo wachafu zamani, kwamba tabia yako ilivunjiwa hadhi na maji machafu zamani? Je, unadhani kuwa unaishi katika paradiso ya kidunia, kwamba uko katikati ya furaha? Je, hujui kwamba umeishi maisha na pepo wachafu, na kwamba umeishi maisha na kila kitu ambacho wamekuandalia? Je, kuishi kwako kungewezaje kuwa na maana yoyote? Je, maisha yako yangewezaje kuwa na thamani yoyote? Umekuwa ukienda huku na huko kwa ajili ya wazazi wako pepo wachafu, hadi sasa, lakini hujui kwamba wale ambao wanakunasa mtegoni ni hao pepo wachafu, wazazi wako ambao walikuzaa na kukulea. Aidha, hujui kuwa uchafu wako hakika ulipewa wote na wao; yote unayojua ni kwamba wanaweza kukupa “ridhaa,” hawakuadibu, wala hawakuhukumu, na hasa hawakulaani. Hawajawahi kukulipukia kwa ghadhabu, lakini hukutendea kwa bashasha na kwa ukarimu. Maneno yao hulisha moyo wako na kukupendeza mno ili ukanganywe na bila kulitambua, unavutwa ndani na uko radhi kuwa wa huduma kwao, uwe mlango wao na kadhalika mtumishi wao. Huna malalamiko kamwe lakini uko radhi kutumiwa nao—unadanganywa nao. Kwa sababu hii, bila shaka huna majibizo yoyote kwa kazi ambayo Mimi hufanya—si ajabu kwamba wewe daima hutaka kuponyoka kwa siri kutoka kwa mikono Yangu, na si ajabu kwamba wewe daima hutaka kutumia maneno matamu ili kuidanganya fadhila Yangu. Inadhihirika kwamba tayari ulikuwa na mpango mwingine, mpangilio mwingine. Unaweza kuona sehemu ndogo ya vitendo Yangu, vitendo vya Mwenyezi, lakini hujui chembe ya hukumu na kuadibu kwangu. Hujui wakati kuadibu kwangu kulianza; unajua tu jinsi ya kunidanganya Mimi, lakini hujui kuwa Sivumilii ukiukaji na mwanadamu. Kwa kuwa tayari umeweka uamuzi wako kunitumikia Mimi, sitakuacha uende. Mimi ni Mungu mwenye wivu, na Mimi ni Mungu ambaye ana wivu kwa mwanadamu. Kwa kuwa tayari umewekelea maneno yako juu ya madhabahu, Sitakuvumilia wewe kuhudumia mabwana wawili. Je, ulifikiri ungepata upendo mwingine baada ya kuweka maneno yako juu ya madhabahu Yangu, baada ya kuyaweka mbele ya macho Yangu? Ningewezaje kuwaruhusu watu kunidanganya Mimi kwa njia hiyo? Je, ulidhani kwamba ungeweza kuweka nadhiri kikawaida, kula kiapo kunielekea Mimi na ulimi wako? Je, ungewezaje kula kiapo kunielekea kiti Changu cha enzi, Aliye Juu Zaidi? Je, ulifikiri kwamba viapo vyako vilikuwa tayari vimekufa? Nawaambia, hata kama miili yenu ikifa, viapo vyenu haviwezi kufa. Hatimaye, Nitawahukumu kwa msingi wa viapo vyenu. Lakini mnadhani kwamba mnaweza kuweka maneno yenu mbele Yangu ili kunivumilia Mimi na kwamba mioyo yenu inaweza kuwatumikia pepo wachafu na pepo wabaya. Je, hasira Yangu ingewezaje kuwavumilia hao watu mithili ya mbwa na nguruwe wanaonidanganya? Lazima Nitekeleze amri Zangu za kiutawala, na kuwapokonya kutoka kwa mikono ya pepo wachafu wale wote wenye fukuto, “wacha Mungu” ambao wanaamini katika Mimi “kunitumikia” Mimi kwa njia ya mpango, kuwa ng’ombe Wangu, kuwa farasi Wangu na kudhibitiwa na Mimi. Nitakufanya ushike uamuzi wako wa awali na kunitumikia Mimi tena. Siwezi kuvumilia kiumbe yeyote kunidanganya Mimi. Je, ulifikiria kwamba ungeweza kufanya maombi tu kiutukutu na kudanganya kiutukutu mbele Yangu? Je, ulifikiri kwamba Mimi sikuwa nimesikia au kuona maneno na matendo yako? Je, maneno yako na matendo yako yangekosaje kuwa katika mtazamo Wangu? Ningewezaje kuwaruhusu watu kunidanganya Mimi kwa njia hiyo?
Nimekuwa miongoni mwenu, Nimeshirikiana nanyi kwa majira kadhaa ya kuchipua na kwa majira kadhaa ya kupukutika, Nimeishi kati yenu kwa muda mrefu—ni kiasi gani cha tabia yenu ya kudharaulika kimeponyoka mbele ya macho Yangu? Maneno yenu hayo ya dhati daima yarudisha mwangwi ndani ya masikio Yangu; mamilioni na mamilioni ya matarajio yenu yamewekwa juu ya madhabahu Yangu—hayawezi hata kuhesabiwa. Lakini kwa kujitolea kwako na kile mnachokitumia, hakuna hata kidogo. Hakuna hata tone dogo la uaminifu wenu kwenye madhabahu Yangu. Yako wapi matunda ya imani yenu Kwangu? Mmepokea neema isiyo na mwisho kutoka Kwangu na mmeona mafumbo yasiyo na mwisho kutoka mbinguni, na Nimewaonyesha hata miale ya mbinguni lakini Sijawahi kuwa na moyo wa kuwachoma, na ni kiasi gani mmenipa Mimi kama malipo? Je, mko radhi kunipa Mimi kiasi gani? Kama umeshikilia chakula Nilichokupa, unageuka na kunitolea Mimi, hata ukisema kuwa ni kitu ambacho umepata kama malipo kwa jasho la kazi yako ngumu, kwamba unatoa yote uliyo nayo Kwangu. Je, unawezaje kukosa kujua kwamba “michango” yako Kwangu ni vitu vyote vilivyoibwa kutoka kwa madhabahu Yangu? Na sasa unavitoa Kwangu—si wewe unanidanganya Mimi? Unawezaje kukosa kujua kuwa vitu Ninavyovifurahia leo ni matoleo yote juu ya madhabahu Yangu, na sicho kile ulichokichuma kama malipo ya kazi yako ngumu halafu ukanitolea Mimi? Kwa kweli mnathubutu kunidanganya Mimi kwa njia hii, kwa hiyo ni kwa jinsi gani Ninaweza kuwasamehe? Ninawezaje kuvumilia hili zaidi? Nimewapa kila kitu. Nimewafungulia kila kitu, Nikakimu mahitaji yenu, na kuyafungua macho yenu, lakini bado mnanidanganya Mimi kwa njia hii, mkipuuza dhamiri yenu. Bila ubinafsi Nimewapa kila kitu, ili kwamba hata kama mnateseka, mmepata kutoka Kwangu kila kitu Nilichokileta kutoka mbinguni. Lakini hamna kujitolea kamwe, na hata kama mna mchango mdogo, mnalipa deni baada ya hapo. Je, si mchango wako utakuwa bure? Kile ambacho umenipa si chochote isipokuwa chembe moja ya mchanga, lakini kile ulichouliza kutoka Kwangu ni tani moja ya dhahabu. Je, si wewe unakuwa muhali? Ninafanya kazi miongoni mwenu. Hakuna kabisa dalili ya asilimia kumi ambayo Ninapaswa kupata, sembuse dhabihu za ziada. Zaidi ya hayo, asilimia kumi inayochangwa na wale ambao ni wacha Mungu inachukuliwa na wale waovu. Je, si nyinyi wote mmetawanyika kutoka Kwangu? Je, si nyinyi nyote mna uhasama na Mimi? Je, si nyinyi nyote mnaharibu madhabahu Yangu? Je, mtu wa aina hii anawezaje kuonekana kama hazina machoni Pangu? Je, si yeye ni nguruwe, mbwa ambao Ninawachukia? Ningewezaje kurejelea uovu wenu kama hazina? Kazi Yangu kwa kweli ni ya nani? Inawezekana kuwa tu ni ya kuwapiga nyinyi nyote ili kufichua mamlaka Yangu? Je, si maisha yenu yameshikiliwa na neno moja kutoka Kwangu? Ni kwa nini Ninatumia maneno tu kuwaagiza na Sijayageuza maneno kuwa ukweli ili kuwapiga haraka iwezekanavyo? Je, maneno Yangu na kazi Yangu ni ya kuwapiga wanadamu tu? Je, Mimi ni Mungu ambaye huwaua wasio na hatia bila ubaguzi? Hivi sasa, ni wangapi wenu ambao wako hapo mbele Yangu ambao wanatafuta njia sahihi ya maisha ya mwanadamu na nafsi zao nzima? Ni miili yenu tu iliyo mbele Yangu, lakini mioyo yenu iko huru, na iko mbali, mbali na Mimi. Kwa sababu hamjui kwa kweli kazi Yangu ni nini, kuna baadhi yenu ambao mnataka kuondoka Kwangu, mnaojitenga na Mimi, na mnataka kuishi katika mahali hapo pa raha ambapo hakuna kuadibu, hakuna hukumu. Je, hili ndilo watu wanatamani katika mioyo yao? Mimi hakika sikulazimishi. Njia yoyote utakayoichukua ni uchaguzi wako mwenyewe, na njia ya leo huenda sambamba na hukumu na laana, lakini nyote mnapaswa kujua kwamba kile Niliyowapa, iwe ni hukumu au kuadibu, zote ni zawadi bora kabisa Ninazoweza kuwapa, na vyote ni vitu ambavyo mnahitaji kwa dharura.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Jumatatu, 11 Machi 2019

Gospel Music | "Yule Anayeshikilia Ukuu Juu ya Kila Kitu" | Musical Documentary (Swahili Subtitles)

Gospel Music | "Yule Anayeshikilia Ukuu Juu ya Kila Kitu" | Musical Documentary (Swahili Subtitles)

Kote katika ulimwengu mkubwa mno, sayari zote ya mbingu husogea kwa usahihi katika mizunguko yazo zenyewe. Chini ya mbingu, milima, mito, na maziwa vyote vina mipaka yavyo, na viumbe vyote huishi na kuzaana wakati wa misimu yote minne kulingana na sheria za maisha…. Hili lote limepangwa vizuri sana—je, kuna Mwenye Uwezo Mmoja anayepanga na kutawala yote haya? Tangu tuje katika ulimwengu huu tukilia tumeanza kutekeleza majukumu tofauti katika maisha. Sisi husogea kutoka kuzaliwa mpaka uzee mpaka kuugua hadi kifo, sisi husogea kati ya furaha na huzuni…. Wanadamu kwa kweli hutoka wapi, na kwa kweli tutaenda wapi? Ni nani huitawala jaala yetu? Kutoka nyakati za kale hadi siku za kisasa, mataifa makubwa yameibuka, nasaba za wafalme zimekuja na kwenda, na nchi na watu wamesitawi na kuangamia katika mikondo ya historia…. Kama tu sheria za asili, sheria za maendeleo ya wanadamu zina mafumbo yasiyo na kikomo. Ungependa kujua majibu kuyahusu? Filamu iitwayo Yule Ambaye Hushikilia Ukuu Juu ya Kila Kitu itakuongoza kufikia kiini cha jambo hili, ili kufichua mafumbo yote haya!
Mwenyezi Mungu alisema, Tangu unapoingia katika dunia hii ukilia, unaanza kutekeleza wajibu wako. Unachukua jukumu lako katika mpango wa Mungu na katika utaratibu wa Mungu. Unaanza safari ya maisha. Licha ya asili yako na licha ya safari iliyoko mbele yako, hakuna kitakachoepuka mpango na utaratibu ambao mbingu imeweka, na hakuna aliye na udhibiti wa hatima yake, kwa maana Anayetawala juu ya kila kitu ndiye tu Aliye na uwezo wa kazi hiyo. Tangu siku aliyoumbwa binadamu, Mungu amekuwa thabiti katika kazi Yake, kusimamia ulimwengu huu na kuelekeza mabadiliko na harakati ya mambo yote. Kama kila kiumbe, mwanadamu bila kujua anapata lishe ya utamu na mvua na umande kutoka kwa Mungu. Kama vitu vyote, mwanadamu bila kujua anaishi chini ya mpango wa mkono wa Mungu. Moyo na roho ya mwanadamu vimeshikwa katika mkono wa Mungu, na maisha yote ya mwanadamu yanatunzwa machoni mwa Mungu. Haijalishi kama unayaamini mambo haya au la, vitu vyote, vilivyo hai au vilivyokufa, vitahamishwa, vitabadilika, kufanywa vipya, na kutoweka kulingana na mawazo ya Mungu. Hivi ndivyo Mungu anavyotawala juu ya kila kitu.
Usiku uingiapo kwa utulivu, mwanadamu huwa hafahamu, kwani moyo wa mwanadamu hauwezi kujua jinsi giza linapokaribia au linakotoka. Usiku unapotoweka polepole, mwanadamu anakaribisha mwanga wa mchana, lakini moyo wa mwanadamu haufahamu ilikotoka nuru hii na jinsi gani nuru yenyewe imeliondoa giza la usiku. Mabadiliko kama haya ya kawaida ya mchana na usiku humpitisha mwanadamu katika kipindi kimoja baada ya kingine, kupita katika nyakati, wakati huu wote ikihakikisha kwamba kazi ya Mungu na mpango wake unafanywa wakati wa kila kipindi na katika nyakati zote. Mwanadamu alitembea kwa enzi nyingi na Mungu, lakini bado mwanadamu hafahamu kwamba Mungu ndiye kiongozi wa hatima ya mambo yote na viumbe hai au jinsi Mungu hupanga na kuelekeza mambo yote. Hili ni jambo ambalo limekwepa ufahamu wa binadamu tangu enzi za kale mpaka leo. Na juu ya ni kwa sababu ipi, sio kwa sababu njia za Mungu hazifahamiki, au kwa sababu mpango wa Mungu bado haujakamilika, lakini ni kwa sababu moyo na roho ya mwanadamu viko mbali sana na Mungu. Kwa hivyo, hata ingawa mwanadamu Anamfuata Mungu, bila kujua yeye hubaki katika huduma ya Shetani. Hakuna anayetafuta kwa ukamilifu nyayo au nafsi ya Mungu, na hakuna anayetaka kuwepo katika huduma na utunzaji wa Mungu. Badala yake, wao wako tayari kutegemea upotoshaji wa Shetani na yule mwovu ili kubadilishwa na dunia hii na kanuni za maisha ambazo watu waovu hufuata. Katika nafasi hii, moyo na roho za mwanadamu hutolewa kafara kwa shetani na kuwa riziki yake. Aidha, moyo wa binadamu na roho yake huwa mahali ambapo Shetani anaweza kuishi na kuufanya uwanja wake wa kuchezea. Kwa njia hii, mwanadamu kwa kutojua hupoteza ufahamu wake wa kanuni ya kuwa binadamu, na wa thamani na madhumuni ya kuwepo kwa binadamu. Sheria kutoka kwa Mungu na agano kati ya Mungu na mwanadamu huangamia hatua kwa hatua kutoka katika moyo wa mwanadamu mpaka mwishowe mwanadamu hawezi tena kuomba au kufuata na kumsikiza Mungu. Wakati upitapo, mwanadamu haelewi tena kwa nini Mungu alimuumba, wala haelewi maneno yanayotoka katika kinywa cha Mungu au kutambua kwamba yote hayo ni kutoka kwa Mungu. Mwanadamu huanza kupinga sheria na amri kutoka kwa Mungu; moyo na roho ya mwanadamu hufishwa. ... Mungu humpoteza mwanadamu Aliyemuumba pale mwanzo, na mwanadamu hupoteza mizizi ya mwanzo wake. Hii ni huzuni ya uanadamu. Kwa uhakika, tangu mwanzo mpaka sasa, Mungu alilifanya janga la wanadamu ambalo mwanadamu ni mhusika mkuu na mwaathiriwa, na hakuna hata mmoja anayeweza kupata jibu kuhusu nani ndiye mwelekezi wa hadithi hii ya janga.
Katika dunia hii kubwa, mabadiliko yasiyo hesabika yamefanyika, tena na tena. Hapana aliye na uwezo wa kuongoza binadamu isipokuwa Yeye ambaye Anatawala juu ya kila kitu katika ulimwengu. Hakuna yeyote hodari kwa kazi au kufanya maandalizi kwa ajili ya binadamu, wala aliye na uwezo wa kuwaongoza wanadamu kurejelea mwanga na ukombozi kutokana na ukosefu wa haki duniani. Mungu Analalamikia wakati ujao wa wanadamu, na Anahuzunishwa na kuanguka kwa mwanadamu. Anahisi huzuni kwa kuangamia kwa mwanadamu polepole na kwenda katika njia isiyo na upande wa kurudi. Mwanadamu ameuvunja moyo wa Mungu, akamkana na kumfuata yule mwovu. Hakuna waliowahi kuwa na mawazo kuhusu mwelekeo ambao mwanadamu wa aina hii atafuata. Ni kwa sababu hii haswa ndio kwamba hakuna ambaye ameona hasira ya Mungu. Hakuna anayetafuta njia ya kumpendeza Mungu au kujaribu kuwa karibu na Mungu. Kadhalika, hakuna anayetafuta kufahamu huzuni na maumivu ya Mungu. Hata baada ya kusikia sauti ya Mungu, binadamu anaendelea tu kwenye njia yake mbali na Mungu, kukwepa neema na huduma ya Mungu, na kuepuka ukweli wa Mungu, akiona ni afadhali auuze mwili wake kwa Shetani, adui wa Mungu. Na ni nani amewahi kuwa na mawazo yoyote ya jinsi gani Mungu atamtendea mwanadamu asiyetubu na ambaye amempuuza? Hakuna anayejua kwamba ukumbusho wa mara kwa mara na nasaha za Mungu ni kwa sababu Yeye anayo katika mikono yake maafa Aliyowaandalia yasiyokuwa ya kawaida, maafa ambayo yatakuwa magumu kwa mwili na nafsi ya mwanadamu kustahimili. Janga hili sio tu adhabu ya mwili bali ya roho pia. Lazima ujue hili: Mpango wa Mungu unapokataliwa na wakati kuwakumbusha kwake na nasaha hazileti mabadiliko, Atakuwa na hasira ya aina gani? Hii itakuwa kama kitu ambacho hakijawahi kushuhudiwa hapo awali au hata kusikika na viumbe vyovyote. Na hivyo Nasema, janga hili ni kubwa mno na kamwe hayatawahi kurudiwa. Hii ni kwa sababu uumbaji mmoja tu na wokovu mmoja wa mwanadamu ndio ulio ndani ya mpango wa Mungu. Hii ni mara ya kwanza na pia ni ya mwisho. Kwa hivyo, hakuna anayeweza kuelewa nia ya huruma na hamu ya Mungu kwa matarajio yake ya kuwaokoa wanadamu.
Mungu aliumba dunia hii na kuleta mwanadamu, kiumbe hai ambacho alitia uhai ndani yake. Baadaye, mwanadamu akaja kuwa na wazazi na jamaa na hakuwa mpweke tena. Tangu mwanadamu alipotua macho kwa mara ya kwanza katika dunia hii tunayoishi, ilibainika kuwa angeishi ndani ya utaratibu wa Mungu. Ni pumzi ya uhai kutoka kwa Mungu ndiyo hustawisha kila kiumbe hai katika ukuaji wake hadi kinapokomaa. Wakati wa mchakato huu, hakuna hata mmoja anayeamini kwamba mwanadamu huishi na kukua chini ya uangalizi wa Mungu. Badala yake, anashikilia kwamba mwanadamu hukua chini ya upendo na utunzaji wa wazazi wake, na kwamba ukuaji wake unaongozwa na silika ya maisha. Hii ni kwa sababu mwanadamu hajui aliyeleta maisha au kulikotoka maisha hayo, pia hafahamu jinsi silika ya maisha husababisha miujiza. Mwanadamu anajua tu kwamba chakula ndicho msingi wa kuendelea kwa maisha, kwamba uvumilivu ni chanzo cha kuwepo kwa maisha, na kwamba imani iliyomo akilini mwake ni utajiri wa maisha yake. Mwanadamu haihisi neema na riziki itokayo kwa Mungu. Mwanadamu huyatumia kwa uharibifu maisha aliyopewa na Mungu. ... Hapana hata mwanadamu mmoja ambaye Mungu Anamwangazia usiku na mchana amechukua jukumu la kuanza Kumwabudu. Mungu Anaendelea kufanya kazi kama Alivyopanga juu ya mwanadamu Akiwa hana matarajio yoyote kutoka kwa mwanadamu. Anafanya hivyo kwa matumaini kwamba siku moja, mwanadamu ataamka kutoka katika ndoto yake na ghafla kuelewa thamani na madhumuni ya maisha, kuelewa gharama Aliyopitia Mungu ili Ampe mwanadamu kila kitu alicho nacho, na kujua jinsi Mungu anavyotamani kwa ari mwanadamu ageuke na Kumrudia. Hakuna yeyote amewahi kufikiria juu ya siri ya asili na endelezo la maisha ya mwanadamu. Na bila shaka, Mungu tu Ambaye Anaelewa yote haya na kwa kimya huvumilia mapigo na maumivu kutoka kwa binadamu, ambaye alipokea kila kitu kutoka kwa Mungu bila shukurani. Binadamu huchukulia kila kitu kinacholetwa na maisha kimzaha, na tena kama "kama jambo lisilo na shaka," Mungu amesalitiwa, amesahaulika, na kukataliwa na binadamu. Je, mpango wa Mungu ni wa maana namna hii? Je mwanadamu, kiumbe hai ambaye alitoka katika mkono wa Mungu, ni wa maana namna hiyo? Mpango wa Mungu ni wa umuhimu kabisa; hata hivyo, maisha ya viumbe vya mkono wa Mungu vipo kwa ajili ya mpango Wake. Kwa hivyo, Mungu hawezi kuuharibu mpango wake kwa sababu ya chuki Yake kwa mwanadamu. Ni kwa ajili ya mpango Wake na pumzi aliyotoa ndiyo maana Mungu Hustahimili mateso yote, siyo kwa ajili ya mwili wa mwanadamu ila ni kwa sababu ya uhai wa mwanadamu. Mungu ana hamu ya kuchukua pumzi aliyopuliza ndani mwa mwanadamu, wala sio nyama za mwili. Huu ndio mpango wake.
Wote wanaokuja duniani lazima wapitie maisha na kifo, na wengi wamepitia mzunguko wa kifo na kuzaliwa upya. Wale wanaoishi watakufa hivi karibuni na wafu watarejea karibuni. Yote haya ni mwendo wa maisha uliopangwa na Mungu kwa kila kiumbe hai. Hata hivyo, njia hii na mzunguko huu ni ukweli ambao Mungu Anataka binadamu aone, kwamba maisha aliyopewa na Mungu hayana kikomo na hayazuiliwi na mwili, wakati, au nafasi. Hii ni siri ya maisha aliyopewa binadamu na Mungu na dhihirisho kwamba maisha yalikuja kutoka Kwake. Ingawa watu wengi wanaweza kosa kuamini kwamba maisha yalitoka kwa Mungu, binadamu bila ya kufahamu wanafurahia yote yatokayo kwa Mungu, iwe wanaamini au wanakana uwepo Wake. Iwapo siku moja Mungu kwa ghafla Atabadili moyo na Atake kurudisha yote yaliyomo duniani na kuchukua maisha Aliyotoa, basi yote duniani yataisha. Mungu Hutumia maisha Yake kukimu vitu vyote vilivyo hai na visivyo na uhai, na kuleta yote kwa utaratibu mzuri kwa mujibu wa madaraka na mamlaka Yake. Huu ni ukweli ambao hakuna anayeweza kuufahamu au kuuelewa kwa urahisi, na kweli hizi zisizoeleweka kwa fikira zetu ni dhihirisho halisi na ushahidi wa nguvu za Mungu katika maisha. Sasa hebu nikupe siri: Ukuu na nguvu ya uhai wa Mungu hauwezi kueleweka na kiumbe chochote. Hii ilikuwa hivyo awali, iko hivyo wakati huu, na itakuwa hivyo wakati ujao. Siri ya pili Nitakayotoa ni hii: chanzo cha uhai hutoka kwa Mungu, kwa viumbe vyote, haijalishi tofauti katika maumbile au muundo. Hata uwe kiumbe hai cha aina gani, huwezi kwenda kinyume na njia ya maisha ambayo Mungu ameweka. Katika hali yoyote, kile Napenda ni kuwa mwanadamu aelewe kwamba bila huduma, utunzaji, na utoaji wa Mungu, mwanadamu hawezi kupokea yote aliyokusudiwa kupokea, haijalishi juhudi au mapambano yake. Bila ruzuku ya uhai kutoka kwa Mungu, mwanadamu hupoteza maana ya thamani katika maisha na kupoteza madhumuni ya kusudi katika maisha. Mungu angewezaje kuruhusu mwanadamu anayepoteza thamani ya uhai wake kuishi hivyo bila ya kujali? Kisha tena, usisahau kwamba Mungu Ndiye chanzo cha maisha yako. Iwapo mwanadamu atashindwa kuthamini yote ambayo Mungu Amemfanyia, Mungu Hatachukua kile Alichotoa pekee, lakini zaidi ya hayo, mwanadamu atalipa mara mbili kufanya fidia kwa yote ambayo Mungu Ametumia.
Mei 26, 2003

Jumapili, 10 Machi 2019

Kuendeleza Ubora wa Tabia ni Kwa Ajili ya Kupokea Wokovu wa Mungu

Kuendeleza Ubora wa Tabia ni Kwa Ajili ya Kupokea Wokovu wa Mungu

Mwenyezi Mungu alisema, Kuendeleza ubora wa tabia ya watu kunahitaji kwamba muendeleze uwezo wenu wa kupokea. Hitaji la msingi kabisa kwenu ni kwamba myapokee waziwazi maneno yanayonenwa kwenu. Je, siyo imani iliyovurugika ikiwa unanifuata bila kufahamu kile Ninachosema? Ubora wenu wa tabia ni duni sana. Ni kwa sababu hammiliki uwezo wa kupokea kwamba hamna ufahamu hata mdogo wa kile kinachosemwa. Kwa hivyo, ni vigumu sana kutimiza matokeo yanayotamanika. Mambo mengi hayawezi kusemwa kwenu moja kwa moja na athari ya awali haiwezi kutimizwa. Kwa hiyo, kazi za ziada zinapaswa kuongezwa kwa kazi Yangu. Ni muhimu kuzindua kazi hii ya "kuinua ubora wa tabia ya watu" miongoni mwenu kwa sababu uwezo wenu wa kupokea, uwezo wa kuona mambo, na viwango vya maisha yenu ni maskini sana. Huu ndio mwelekeo unaohitajika; hakuna uchaguzi badili, na ni lazima ufanyike kwa namna hii ili sehemu ya matokeo iweze kutimizwa. Vinginevyo, maneno yote Ninayosema hayatafanikiwa, na hamngekumbukwa kama wenye dhambi? Je! Hamngekuwa wapotovu? Je, kazi hii inafanywa kwenu ni nini? Nini kinachohitajika kwenu? Je, hamjui? Mnapaswa kujua ubora wenu wenyewe wa tabia; hauwezi kufikia kile Ninachohitaji kamwe. Je, hii haicheleweshi kazi? Kwa ubora wa tabia na hulka yenu ya sasa, hakuna hata mmoja wenu ambaye anafaa kushuhudia kwa ajili Yangu, na hakuna mtu anayewezana na kazi ya kulichukua jukumu kubwa la kazi Yangu ya baadaye. Je, hamhisi aibu sana kuhusu hili? Itawezekanaje kuyakidhi matakwa Yangu yote kama hili linaendelea kutendeka? Unapaswa kufanya maisha yako yawe kamili na yenye thawabu. Usiruhusu muda upite bure. Hakuna thamani katika kufanya hivyo. Unapaswa kujua mambo ambayo inabidi kujiandaa nayo. Usijione kuwa mjuaji wa kila kitu. Hukaribii hata kidogo! Je! Kuna nini cha kuzungumzia ikiwa huna hata ufahamu wa kimsingi wa ubinadamu? Je, si vyote havingekuwa na maana? Hakuna hata mmoja kati yenu aliye na sifa zinazostahili kabisa kwa mintarafu ya kile Ninachohitaji kwa ubora wa tabia ya kibinadamu. Ni vigumu kupata mtu ambaye anafaa kutumiwa. Mnaamini ninyi ni watu ambao wanaweza kufanya kazi kubwa zaidi kwa ajili Yangu na kujitwika ukabidhi mkubwa kutoka Kwangu. Kwa kweli, hamjui jinsi hata ya kuingia katika masomo mengi mbele yenu, hivyo ingewezekanaje kuingia katika kweli za kina? Lazima kuingia kwenu kuwe kwenye utaratibu. Msifanye hivyo bila mpango. Hili si jambo la manufaa. Ingieni kutoka mwisho wenye kina kifupi—yasome maneno haya mstari kwa mstari hadi mfikie ufahamu na ubayana. Kila ndugu angalau anapaswa aweze kusoma. Usilitazame mara moja tu kwa haraka, na usilifanye kwa namna isiyo ya dhati. Kwa kawaida, unaweza pia kusoma baadhi ya kazi za kumbukumbu (kama vile sarufi au vitabu vya balagha). Hakuna haja ya kusoma vitabu vinavyoichochea akili yako sana (riwaya za mapenzi, ponografia, magazeti, au wasifu za watu mashuhuri), ambavyo husababisha madhara zaidi kuliko mema. Lazima uwe mweledi wa yote unayopaswa kuingia na unapaswa kufahamu. Madhumuni ya kuendeleza ubora wa tabia sio mengine ila kuwasaidia watu kujua asili yao wenyewe, utambulisho, hadhi au thamani. Nini jambo kuu ambalo makanisa hapa chini yanapaswa kuingia? Je, watu hawaongezi ubora wa tabia yao sasa? Ni muhimu kushikilia kuingia huku kwa kugeuka kuwa msomi; hakuwezi kuachiliwa huru! Kipengele kimoja ni kwamba lazima ninyi muelewe kwa nini ubora wa tabia ya watu unapaswa kuendelezwa, jinsi ubora wa tabia unaweza kuendelezwa, na vipengele vipi vya kuingia. Lazima muelewe maana ya ubinadamu wa kawaida, kwa nini kazi hii inapaswa kufanywa, na jinsi inapaswa kuratibiwa. Katika kuelimika, ni vipengele vipi vinayopaswa kufunzwa, na jinsi gani mtu anapaswa kuingia? Nyote mnapaswa kujua lengo la kuelimika ni nini. Je, sio kuyafahamu maneno ya Mungu na kuingia katika ukweli? Hali inayosambaa makanisani sasa ni ipi? Mkimwomba mtu apate kuelimika, anasahau kuhusu furaha ya maneno ya Mungu. Mkizungumza kuhusu ubinadamu wa kawaida, anashughulikia tu kuisafisha nyumba yake, kufagia sakafu au kupika, kusafisha jikoni na kununua vyombo vya kupika. Anajali tu kuhusu mambo haya na hajui jinsi ya kuishi maisha ya kanisa kwa kawaida. Vinginevyo anatafuta tu maneno katika kamusi na kujifunza maneno mapya, lakini hafanyi jambo lingine lolote siku nzima. Umepotoka ikiwa unabaki katika hali ya sasa. Basi kwa nini unaombwa kuingia katika maisha ya kiroho? Yote unayojifunza ni mambo haya ambayo hayawezi kukusaidia kufikia kile kinachohitajika kwako. Jambo la muhimu zaidi bado ni kuingia kwa maisha. Sababu ya kufanya kazi hii ni kutatua shida ambazo watu hukumbana nazo katika uzoefu wao. Kuinua ubora wa tabia kunakuwezesha kujua ubinadamu na kiini cha mwanadamu—kusudi kuu la kuyajua mambo haya ni ili maisha ya watu ya kiroho yaweze kukua na tabia yao iweze kubadilika. Unaweza kujua jinsi ya kuvaa na kupendeza; unaweza kuwa na utambuzi na hekima, na hata hivyo hatimaye, siku inapokuja kwako kuenda kazini, unashindwa kufanya hivyo. Unapaswa kujua, kwa hiyo, kile unapaswa kufanya pia wakati unainua ubora wako wa tabia. Kukubadilisha ni lengo. Kuinua ubora wa tabia ni jambo la ziada. Haitakubalika kama ubora wako wa tabia hauendelezwi. Ni vibaya hata zaidi ikiwa tabia yako haiwezi kubadilishwa. Moja bila ya nyingine haitoshi. Kuwa na ubinadamu wa kawaida hakumaanishi kwamba umekuwa na ushuhuda mkubwa sana. Kile kinachohitajika kwako si rahisi sana.
Wakati ambapo ubora wa tabia ya mtu umeendelea kiasi kwamba ana hisia na mtindo wa maisha ya ubinadamu wa kawaida na pia kuwa na kuingia kwa maisha, ni hapo tu ndipo ataweza kubadilika na kushuhudia. Siku ya kutoa ushuhuda inapofika, pia kuna haja ya kuzungumza kuhusu mabadiliko katika maisha ya binadamu na kuhusu ufahamu wa Mungu ndani. Mchanganyiko wa vipengele hivi viwili tu ndio ushahidi wa kweli na faida yako ya kweli. Haitakubalika ikiwa una mabadiliko tu katika ubinadamu kwa nje na huna ufahamu kwa ndani. Haitakubalika pia ikiwa una ufahamu na ukweli kwa ndani lakini hutilii maanani kuishi kulingana na ubinadamu wa kawaida. Kazi inayofanyika kwako leo sio kuwaonyesha wengine bali kukubadilisha. Unahitaji tu kuzingatia kujibadilisha. Unaweza kuandika na kusikiliza kila siku, lakini haitawezekana ikiwa hushiriki katika maeneo mengine ya maisha yako. Unapaswa kuwa na kuingia katika kila kipengele. Unapaswa kuwa na maisha ya kawaida ya mtakatifu. Akina dada wengi huvaa kama wanawake matajiri na kaka wanavaa kama waungwana matajiri au mabwana, wakipoteza kabisa ustahifu wa watakatifu. Kipengele kimoja ni kuinua ubora wa tabia ya mtu, ambacho kinaweza kufanikishwa kwa kawaida. Kipengele kingine cha umuhimu mkubwa ni kula na kunywa maneno ya Mungu. Je, haingekuwa kupoteza elimu ikiwa ubora wako wa tabia umeinuliwa lakini haukukutumiwa kwa sababu hukula na kunywa maneno ya Mungu? Lazima vipengele vyote viwili viunganishwe. Kwa nini maarifa ya Mungu yanatajwa katika majadiliano ya kile kinachohitajika kwako? Je, hii si kwa ajili ya matokeo ya kazi ya baadaye? Baada yako kushindwa, lazima uweze kushuhudia kutokana na uzoefu wako mwenyewe. Haitakubalika kama sura yako ya nje ni moja ya ubinadamu wa kawaida lakini huwezi kuonyesha uzoefu wako kupitia kinywa chako. Unapokuwa na maisha ya kawaida ya kiroho, unapaswa kufikia ubinadamu wa kawaida, na vipengele vingi vya ubinadamu wa kawaida vitaweza kufunzwa kwa dhahiri. Je, ungesema kwamba kufagia sakafu kunahitaji mafunzo maalum? Ikiwa unahitaji kutumia saa moja kufanya mazoezi jinsi ya kushikilia vijiti kwa kula, hiyo haikubaliki hata zaidi! Ubinadamu wa kawaida unashirikisha vipengele hivi: utambuzi, hisia, dhamiri na tabia. Iwapo unaweza kufanikisha ukawaida katika kila mojawapo ya vipengele hivi, ubinadamu wako uko katika kiwango kinachostahili. Unapaswa kuwa na mfanano wa binadamu wa kawaida na utende kama anayemwamini Mungu. Sio lazima ufikie viwango vya juu zaidi au kujishughulisha na diplomasia. Unapaswa tu kuwa mwanadamu wa kawaida, na hisia za kawaida za mtu, uweze kung’amua vitu, na kwa kiwango cha chini uonekane kama mwanadamu wa kawaida. Hiyo itakuwa imetosha. Kila kitu kinachohitajika kwako leo kiko katika uwezo wako, na huku si kukulazimisha ufanye kadri ya uwezo wako hata kidogo. Hakuna maneno yasiyo na maana au kazi isiyofaa yatatekelezwa kwako. Uovu wote ulioonyeshwa au kufichuliwa katika maisha yako lazima uondolewe. Ninyi mmepotoshwa na Shetani na mna sumu nyingi sana za Shetani. Yote ambayo yanahitajika kwako ni kuiepuka tabia hii potovu ya kishetani, si wewe kuwa mtu mwenye cheo cha juu, au mtu maarufu au mkuu. Hii haina maana. Kazi ambayo imefanyika kwenu inaafikiana na kile ambacho ni cha asili kwenu. Kuna mipaka ya kile Ninachohitaji kutoka kwa watu. Ikiwa watu wa leo wote wangeulizwa kutenda kama watu wa kada za Kichina, na kujizoeza toni ya sauti ya kada za Kichina, kujifunza katika namna ya kuzungumza ya viongozi wa serikali wenye cheo cha juu, au kujifunza kwa namna na sauti ya kuzungumza ya waandishi wa insha na waandishi wa riwaya, basi hili halingekubalika pia. Halingeweza kufikiwa. Kwa mujibu wa ubora wa tabia za watu hawa, wanapaswa angalau kuweza kuzungumza kwa hekima na busara na kuelezea mambo wazi. Ni wakati huo ndipo watakapoyatosheleza mahitaji. Kwa kiwango kidogo sana, utambuzi na hisia vinapaswa kufikiwa. Kwa sasa jambo kuu ni kuitupilia mbali tabia potovu ya kishetani. Lazima uutupilie mbali uovu unaouonyesha. Ikiwa hujavitupilia mbali hivi, unawezaje kugusia hisia na utambuzi wenye mamlaka mkubwa kabisa? Watu wengi wanaona kwamba enzi imebadilika. Hivyo hawajizoezi unyenyekevu au uvumilivu wowote, na pengine pia hawana upendo wowote au mwenendo mwema wa kitakatifu pia. Watu hawa ni wajinga mno! Je, wana kiwango chochote cha ubinadamu wa kawaida? Je, wanao ushuhuda wowote wa kuzungumziwa? Hawana utambuzi na hisia zozote kamwe. Bila shaka, vipengele fulani vya utendaji wa watu vilivyopotoka na vyenye makosa vinapaswa kurekebishwa. Kama vile maisha ya watu ya kiroho yasiyopindika au mwonekano wenye ganzi na upumbavu wa zamani—vitu hivi vyote vinapaswa kubadilika. Mabadiliko hayamaanishi kukuruhusu uwe mpotovu au kujiingiza katika mwili, au kusema chochote utakacho. Kuzungumza kiholela hakuwezi kukubalika! Kutenda kama mwanadamu wa kawaida ni kuzungumza kwa kueleweka. Ndiyo inamaanisha ndiyo, na la inamaanisha la. Kuwa mwenye ukweli kwa uhakika na uzungumze inavyofaa. Usilaghai, usidanganye. Inapaswa kujulikana ni mipaka gani mtu wa kawaida anaweza kufikia kuhusu mabadiliko ya tabia. Ikiwa hiyo haijulikani, hutaweza kuingia katika uhalisi.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili