Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Jumatano, 31 Oktoba 2018

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Je, Umekuwa Hai Tena?"

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Je, Umekuwa Hai Tena?"

Mwenyezi Mungu anasema, "Ikiwa watu wanatamani kuwa viumbe hai, na kuwa na ushuhuda wa Mungu, na kuthibitishwa na Mungu, wanapaswa kukubali wokovu wa Mungu, wanapaswa kuwa watiifu katika hukumu na kuadibu Kwake, na wanapaswa kukubali kwa furaha kushughulikiwa na kupogolewa na Mungu. Baada ya hapo ndipo wataweza kuweka katika matendo ukweli wote unaohitajika na Mungu, na baada ya hapo ndipo wataweza kupata wokovu wa Mungu, na kuwa viumbe hai kabisa. Walio hai wanaokolewa na Mungu, wamehukumiwa na kuadibiwa na Mungu, wapo tayari kujitoa wenyewe na wana furaha kutoa maisha yao kwa Mungu, na wapo tayari kujitoa maisha yao yote kwa Mungu. Pale ambapo walio hai watachukua ushuhuda wa Mungu ndipo Shetani ataweza kuaibishwa, ni walio hai tu ndio wanaweza kueneza kazi ya injili ya Mungu, ni walio hai tu ndio wanaoupendeza moyo wa Mungu, ni walio hai tu ndio watu halisi."
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumanne, 30 Oktoba 2018

Mashahidi wa Kristo wa Siku za Mwisho | Jinsi ya kuelewa kwamba Kristo ndiye ukweli, njia, na uzima?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, hekima ya Mungu

Mashahidi wa Kristo wa Siku za Mwisho | 8. Jinsi ya kuelewa kwamba Kristo ndiye ukweli, njia, na uzima?

I. Ni Lazima Mtu Ashuhudie Kipengele cha Ukweli Kuhusu Kupata Mwili kwa Mungu
8. Jinsi ya kuelewa kwamba Kristo ndiye ukweli, njia, na uzima?
Aya za Biblia za Kurejelea:
"Mwanzoni kulikuwa na Neno, na Neno alikuwa na Mungu, na Neno alikuwa Mungu. Hivyo ndivyo alivyokuwa mwanzoni na Mungu" (YN. 1:1-2).
"Na Neno alifanywa kuwa mwili, na akakaa kati yetu, (nasi tukautazama utukufu wake, utukufu kama ule wa Mwana wa pekee aliyezaliwa na Baba,) aliyejawa neema na ukweli" (YN. 1:14).
"Mimi ndiye njia, ukweli na uhai: hakuna mwanadamu ayaje kwa Baba, bali kwa njia yangu" (YN. 14:6).
"Maneno ninayoongea kwenu ni roho, na ni uhai" (YN. 6:63).
Maneno Husika ya Mungu:
Ukweli unatoka katika ulimwengu wa mwanadamu, na bado ukweli katika mwanadamu unapitishwa na Kristo. Unaanzia kwa Kristo, yaani, kutoka kwa Mungu mwenyewe, na hauwezi kufikiwa na mwanadamu.
kutoka kwa "Mafanikio au Kushindwa Kunategemea Njia Ambayo Mwanadamu Hutembea" katika Neno Laonekana katika Mwili
"Mwanzoni kulikuwa na Neno, na Neno alikuwa na Mungu, na Neno alikuwa Mungu, na Neno likawa mwili." Hii (kazi ya kuonekana kwa Neno katika mwili) ni kazi ambayo Mungu atatimiza katika siku za mwisho, na ni sura ya mwisho ya mpango Wake mzima wa uongozi, kwa hivyo Mungu lazima Aje duniani na kudhihirisha maneno Yake katika mwili.
kutoka kwa "Yote Yanafanikishwa Kupitia kwa Neno la Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Katika Enzi ya Ufalme, Mungu anatumia neno ili kukaribisha enzi mpya, ili kubadilisha mbinu za kazi Yake, na kuweza kufanya kazi katika enzi nzima. Hii ndiyo kanuni ambayo Mungu hufanyia kazi katika Enzi ya Neno. Alikuwa mwili ili kuweza kuzungumza kutoka mitazamo tofauti, kumwezesha binadamu kumwona Mungu kwa kweli, ambaye ni Neno linaloonekana katika mwili, na hekima Yake na maajabu. Kazi kama hiyo inafanywa ili kwa njia bora zaidi kutimiza shabaha za kumshinda binadamu, kumfanya binadamu kuwa mtimilifu, na kumwondoa binadamu. Hii ndiyo maana ya kweli ya kutumia neno ili kufanya kazi katika Enzi ya Neno. Kupitia kwenye neno, binadamu anajua kazi ya Mungu, tabia ya Mungu, kiini cha binadamu, na kile ambacho binadamu anastahili kuingia ndani chake. Kupitia neno, kazi yote ambayo Mungu hupenda kufanya katika Enzi ya Neno inatimizwa. Kupitia neno, binadamu anafichuliwa, anaondolewa, na kujaribiwa. Binadamu ameliona neno, amelisikia neno, na akapata habari ya uwepo wa neno. Kutokana na haya, binadamu anaamini katika uwepo wa Mungu; binadamu anaamini katika uwezo na hekima za Mungu, pamoja na moyo wa upendo wa Mungu kwa binadamu na tamanio Lake la kumwokoa binadamu. Ingawa neno "neno" ni rahisi na kawaida, neno kutoka kwenye kinywa cha Mungu kuwa mwili hutikisa dunia nzima; neno Lake hubadilisha moyo wa binadamu, fikira na tabia zee za binadamu, na sura nzee ya ulimwengu mzima. Kupitia enzi nyingi, Mungu pekee wa leo ndiye anayefanya kazi katika njia kama hiyo, na ni Yeye tu Anayeongea na kumwokoa binadamu hivyo. Baadaye, binadamu huishi katika mwongozo wa neno, akichungwa na kujazwa na neno; wanaishi katika ulimwengu wa neno, wanaishi katika laana na baraka za neno la Mungu, na hata zaidi kuishi chini ya na hukumu na kuadibu kwa neno. Maneno haya na kazi hii vyote ni kwa minajili ya wokovu wa binadamu, kutimiza mapenzi ya Mungu, kubadilisha sura asilia wa ulimwengu wa uumbaji wa kale. Mungu aliuumba ulimwengu kwa neno, huwaongoza wanadamu kote ulimwenguni kwa neno, hushinda na kuwaokoa binadamu kwa neno. Hatimaye, Yeye atatumia neno ili kuutamatisha ulimwengu mzima wa kale. Ni hapo tu ndipo mpango wa usimamizi unapokuwa mkamilifu kabisa.
kutoka kwa "Enzi ya Ufalme Ndiyo Enzi ya Neno" katika Neno Laonekana katika Mwili
Leo Mungu Amekuwa mwili kimsingi ili kukamilisha kazi ya "Neno kuonekana katika mwili," kutumia neno kumfanya mwanadamu kamili, na kumfanya mwanadamu kukubali ushughulikiaji wa neno na usafishaji wa neno. Katika maneno Yake, anakufanya kupata kupewa na kupata uzima; katika maneno Yake, unaona kazi Yake na matendo. Mungu Anatumia neno kukuadibu na kukutakasa, na hivyo ukipata ugumu wa maisha, ni pia kwa sababu ya neno la Mungu. Leo, Mungu hafanyi kazi kwa kutumia mambo ya hakika, ila ni kwa maneno. Baada tu ya neno Lake kuja juu yako ndipo Roho Mtakatifu Atafanya kazi ndani yako na kukufanya upate uchungu ama uhisi utamu. Ni neno la Mungu pekee ndilo linaloweza kukuleta katika hali halisi, na ni neno la Mungu pekee ndilo linaloweza kukufanya mkamilifu. Kwa hivyo, angalau lazima uelewe kuwa kazi inayofanywa na Mungu katika siku za mwisho kimsingi ni kutumia neno Lake kumfanya kila mwanadamu kamili na kumwongoza mwanadamu. Kazi yote Anayofanya ni kupitia kwa neno; Hatumii ukweli kuadibu. … Kwa hivyo, katika siku za mwisho, Mungu anapokuwa mwili, kimsingi Anatumia neno kukamilisha yote na kufanya yote yawe wazi. Katika maneno Yake pekee ndipo unaweza kuona kile Alicho; ni katika maneno Yake pekee ndiyo unaweza kuona kwamba yeye ni Mungu Mwenyewe. Mungu katika mwili Anapokuja duniani, hafanyi kazi nyingine ila kuongea maneno—hivyo basi hakuna haja ya kutumia uhakika; maneno yanatosha. Hii ni kwa sababu Amekuja kimsingi kufanya kazi hii, kumruhusu mwanadamu aone nguvu Zake na ukuu ulio kwenye neno Lake, kumruhusu mwanadamu kuona kupitia kwa maneno Yake jinsi Alivyojificha kwa unyenyekevu, na kumruhusu mwanadamu kujua ukamilifu Wake kupitia kwa maneno Yake. Kila kitu Alicho nacho na kile Alicho kiko katika maneno Yake, hekima Yake na ajabu yako katika maneno Yake. Katika hii ndipo unapofanywa kuona mbinu nyingi ambazo Mungu anatumia kuongea maneno Yake. … Leo Mungu wa kweli Mwenyewe wa mwili Anaongea tu, na hatendi. Huu ni ukweli! Anatumia maneno kukufanya mkamilifu, na Anatumia maneno kukulisha na kukunyunyizia. Pia Anatumia maneno kufanya kazi, na Anatumia maneno badala ya uhakika kukufanya ujue ukweli Wake. Kama una uwezo wa kutazama ukweli huu wa kazi ya Mungu, basi itakuwa vigumu kuwa wa kutoonyesha hisia.
kutoka kwa "Yote Yanafanikishwa Kupitia kwa Neno la Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Na bado ni huyu mtu wa kawaida aliyefichika kati ya watu ndiye anayefanya kazi hii mpya ya kutuokoa. Yeye hafafanui chochote kwetu, wala hatuelezi ni sababu gani Amekuja. Yeye tu, anafanya kazi anayotarajia kufanya, na kwa mujibu wa mpango Wake. Maneno Yake na matamshi Yake yanazidi kuja kwa wingi. Kuanzia kufariji, kuonya, kukumbusha, na kupeana onyo mpaka kukaripia na kufundisha nidhamu; kuanzia kutumia sauti ya upole mpaka kutumia maneno makali na ya adhimu—yote yanatia huruma na hofu kwa mwanadamu. Kila kitu Anachosema kinatufikia kwetu na kulenga siri zilizofichwa ndani yetu, maneno Yake huchoma mioyo yetu, huchoma nafsi zetu, na hutuacha tukiwa na aibu na wanyonge. …
Pasipo sisi kujua, huyu mtu asiye muhimu ametuelekeza katika hatua baada ya hatua ya kazi ya Mungu. Sisi hupitia majaribu tele, na hukabiliwa na kurudi kusikohesabika, na tunajaribiwa na kifo. Tunajifunza haki ya Mungu na adhama ya tabia Yake, na kufurahia, upendo na huruma Zake, tunakuja kufahamu nguvu za Mungu ambazo ni kubwa na hekima Yake, tunashuhudia uzuri wa Mungu, na kutazama hamu Yake ya kumwokoa mwanadamu. Kwa maneno ya huyu mtu wa kawaida, tunakuja kujua asili na kiini cha Mungu, tunakuja kufahamu mapenzi ya Mungu, tunakuja kujua asili ya mwanadamu na kiini cha mwanadamu, na tunapata kuona njia ya wokovu na ukamilifu. Maneno yake hutufanya sisi tufe, na kutufanya kuzaliwa upya; maneno yake hutufariji, na ilhali pia hutuacha tukiwa tumejawa na hatia na hisia ya kuwa wadeni; maneno yake hutuletea furaha na amani, lakini pia maumivu makubwa. Wakati mwingine sisi ni kama wanakondoo wa kuchinjwa kwenye mikononi Yake; wakati mwingine sisi ni kama kipenzi cha roho yake na kufurahia upendo wake na huba yake; wakati mwingine sisi ni kama adui wake, waliofanywa majivu na ghadhabu yake katika macho yake. Sisi ni wanadamu waliookolewa Naye, sisi ni funza machoni pake, na sisi ni wanakondoo waliopotea ambao Yeye hufikiria kuhusu kuwapata mchana na usiku. Yeye ni mwenye huruma kwetu, anatudharau, yeye hutuinua, yeye hutufariji na kutuhimiza, yeye hutuongoza, yeye hututia nuru, yeye huturudi na kutufundisha nidhamu, na Yeye hata hutulaani. Yeye hujitia wasiwasi usiku na mchana kwa ajili yetu, Yeye hutulinda na kututunza usiku na mchana, na hatuachi kamwe, na Yeye hutoa utunzaji Wake wote kwetu na hulipia gharama yoyote kwa ajili yetu. Miongoni mwa maneno ya mwili huu mdogo na wa kawaida, tumefurahia ukamilifu wa Mungu, na kuona hatima ambayo Mungu ametupa. …
Matamshi ya mungu yanaendelea, na Yeye hutumia mbinu mbalimbali na mitazamo kutuonya na kutuelekeza tutakachofanya na kueleza sauti ya moyo Wake. Maneno Yake hubeba nguvu ya maisha, na hutuonyesha njia tunayopasa kutembea, na yanatuwezesha kujua ukweli ni nini. Tunaanza kuvutiwa na maneno Yake, tunaanza kuzingatia sauti Yake na jinsi anavyoongea, na bila hiari tunaanza kuwa na hamu ya sauti ya moyo wa huyu mwanadamu asiye wa ajabu. Yeye hufanya juhudi za mchwa kwa ajili yetu, anapoteza usingizi na hamu ya chakula kwa ajili yetu, analia kwa ajili yetu, anashusha pumzi kwa ajili yetu, anaugua magonjwa kwa ajili yetu, anadhalilishwa kwa ajili ya wokovu na hatima yetu, na moyo Wake huvuja damu na kulia kwa ajili ya uasi na kufa ganzi kwetu. Utu kama huu na umiliki Wake haupo kwa upeo wa binadamu wa kawaida, na hauwezi kumilikiwa na yeyote aliyepotoka. Ana uvumilivu na subira isiyomilikiwa na mtu wa kawaida, na upendo Wake haumilikiwi na kiumbe yeyote aliyeumbwa. Hakuna mtu mbali na Yeye anayeweza kujua mawazo yetu yote, au kufahamu asili yetu ama kiini chetu, ama kuhukumu uasi wetu na upotovu wa binadamu, ama kusema nasi na kufanya kazi kati yetu kama hivi kwa niaba ya Mungu wa mbinguni. Hakuna mtu ila Yeye anayeweza kumiliki mamlaka, hekima, na heshima ya Mungu; tabia ya Mungu na kile Anacho na alicho yametoka, kwa ukamilifu wao, kutoka Kwake. Hakuna mtu mbali na Yeye ambaye anaweza kutuonyesha njia na kutuletea mwangaza. Hakuna yeyote ila Yeye anayeweza kutufichulia siri ambazo Mungu hajatufunulia tangu uumbaji hadi leo. Hamna yeyote isipokuwa Yeye ambaye anaweza kutuokoa kutokana utumwa wa shetani ama upotovu wa tabia yetu potovu Yeye huwakilisha Mungu, na kuonyesha sauti ya moyo wa Mungu, ushawishi wa Mungu, na maneno ya hukumu ya Mungu, yote ambayo huelekezwa kwa mwanadamu. Ameanza enzi mpya, nyakati mpya, na akaleta mbingu na nchi mpya, kazi mpya, na ametuletea matumaini, na akamaliza maisha ambayo si dhahiri, na akatuwezesha kikamilifu kuona njia ya wokovu. Ameshinda ubinadamu wetu wote, na kupata mioyo yetu. Tangu wakati huo na kuendelea, akili zetu zinapata ufahamu, na nafsi zetu huonekana kufufuka: Huyu mwanadamu wa kawaida asiyekuwa na umuhimu, ambaye huishi kati yetu na kwa muda amekuwa akikataliwa na sisi—Je, si Yeye ni Bwana Yesu, ambaye daima huwa kwa mawazo yetu, na ambaye tunamtamani usiku na mchana? Ni Yeye! Ni Yeye Kweli! Yeye ni Mungu wetu. Yeye ndiye kweli, njia, na uzima! Yeye ameturuhusu kuishi tena, na kuona nuru, na kusimamisha mioyo yetu kuhangaika. Tumerudi nyumbani mwa Mungu, tumerejea mbele ya kiti chake cha enzi, tuko uso kwa uso pamoja na Yeye, tumeshuhudia uso wake, na tumeona barabara iliyo mbele.
kutoka kwa "Kutazama Kuonekana kwa Mungu katika Hukumu na Kuadibu Kwake" katika Neno Laonekana katika Mwili
Maneno yangu ndio ukweli usiobadilika milele. Mimi Ndiye msambazaji wa binadamu na kiongozi wa pekee wa mwanadamu. Thamani na maana ya maneno Yangu haibainishwi na kama yanakubaliwa au kutambuliwa na mwanadamu, ila ni kwa kiini cha maneno yenyewe. Hata kama hakuna mtu hata mmoja duniani anaweza kupokea maneno Yangu, thamani ya maneno Yangu na usaidizi wake kwa mwanadamu hayapimiki na mwanadamu yeyote. Kwa hivyo, Ninapokumbwa na wanadamu wengi wanaoasi, kukataa au kudharau kabisa maneno Yangu, msimamo Wangu ni huu tu: Wacha wakati na ukweli uwe shahidi Wangu na uonyeshe kuwa maneno Yangu ndiyo ukweli, njia na uhai. Wacha vionyeshe kuwa yote Niliyosema ni ya ukweli, na kuwa ni yale ambayo mwanadamu lazima apewe, na, zaidi ya yote, yale ambayo mwanadamu anafaa akubali. Nitawaruhusu wote wanaonifuata wajue ukweli huu: Wote wasioyakubali maneno Yangu kikamilifu, wale wasioyaweka maneno Yangu katika vitendo, wale wasiopata sababu ndani ya maneno Yangu, na wale wasiopata wokovu kwa sababu ya maneno Yangu, ni wale ambao wamehukumiwa na maneno Yangu na, zaidi ya hayo, wamepoteza wokovu Wangu, na fimbo Yangu haitaondoka kamwe miongoni mwao.
kutoka kwa "Mnapaswa Kuzingatia Matendo Yenu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Neno limepata mwili na Roho wa kweli amepatikana katika mwili—kwamba ukweli wote, uzima, na njia umekuja katika mwili, na Roho amewasili duniani na katika mwili kwa kweli. Ingawa, kijuujuu, hili linaonekana ni tofauti na utungaji mimba kwa Roho Mtakatifu, katika kazi hii mnaweza kuona kwa dhahiri zaidi kwamba Roho tayari amepatikana katika mwili, na, zaidi ya hayo, kwamba Neno limepata mwili, na Neno limeonekana katika mwili, na unaweza kufahamu maana ya kweli ya maneno haya: Hapo mwanzo kulikuwako na Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Zaidi ya hayo, lazima ufahamu maneno ya leo ni Mungu, na lazima utazame maneno yakipata mwili. Huu ni ushuhuda bora zaidi unaoweza kuwa nao. Hili linathibitisha kwamba una ufahamu wa kweli wa Mungu kupata mwili—wewe huwezi tu kumjua na kumchambua Yeye, lakini pia unajua kwamba njia unayoifuata leo ni njia ya uzima, na njia ya ukweli. Yesu alifanya hatua ya kazi ambayo ilitimiza tu kiini cha "Neno alikuwako kwa Mungu": Ukweli wa Mungu ulikuwako kwa Mungu, na Roho wa Mungu alikuwa na mwili na alikuwa asiyetenganishwa kutoka Kwake, yaani, mwili wa Mungu mwenye mwili ulikuwa na Roho wa Mungu, ambalo ni thibitisho kuu zaidi kwamba Yesu mwenye mwili alikuwa aliyepata mwili wa kwanza wa Mungu. Hatua hii ya kazi ilitimiza maana ya ndani ya "Neno lapata mwili," ilichangia kwenye maana ya kina zaidi ya "naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu," na inakuruhusu wewe uamini kwa uthabiti maneno haya kwamba "Hapo mwanzo kulikuwako na Neno." Ambalo ni kusema, wakati wa uumbaji Mungu alikuwa na maneno, Maneno Yake yalikuwa na Yeye na yasiyotenganishwa kutoka Kwake, na enzi ya mwisho inafanya nguvu na mamlaka ya maneno Yake yawe hata wazi zaidi, na kumkubalia mwanadamu kuyaona maneno Yake yote—kuyasikia maneno Yake yote. Hiyo ndiyo kazi ya enzi ya mwisho. Lazima uyajue mambo haya yote kabisa. Si suala la kuujua mwili, bali la kuujua mwili na Neno. Hiki ndicho kile unachotakiwa kushuhudia, kile ambacho kila mtu lazima akijue. Kwa sababu hii ni kazi ya kupata mwili kwa pili—na mara ya mwisho ambapo Mungu anapata mwili—inakamilisha kwa ukamilifu umuhimu wa kupata mwili, inatekeleza kabisa na kutoa kazi yote ya Mungu katika mwili, na kumaliza enzi ya Mungu kuwa katika mwili.
kutoka kwa "Utendaji (4)" katika Neno Laonekana katika Mwili
(Fungu Lililochaguliwa la Neno la Mungu)
Ni Kristo wa Siku za Mwisho Pekee Ndiye Anayeweza Kumpa Mwanadamu Njia ya Uzima wa Milele
Njia ya maisha si kitu ambacho kinaweza kumilikiwa na mtu yeyote tu, wala hakipatikani kwa urahisi na wote. Hiyo ni kwa sababu maisha yanaweza kuja tu kutoka kwa Mungu, ambayo ni kusema, Mungu Mwenyewe tu ndiye Anamiliki mali ya maisha, hakuna njia ya maisha bila Mungu Mwenyewe, na hivyo Mungu tu ndiye chanzo cha uzima, na kijito cha maji ya uzima kinachotiririka nyakati zote. Kutoka Alipoumba dunia, Mungu amefanya kazi kubwa inayoshirikisha uhai wa maisha, Amefanya kazi kubwa ambayo huletea mwanadamu maisha, na Amelipa gharama kubwa ili mtu aweze kupata uzima, kwa kuwa Mungu Mwenyewe ni uzima wa milele, na Mungu Mwenyewe ni njia ambayo kwayo mtu hufufuliwa. Mungu kamwe hajawahi kosa kwa moyo wa mwanadamu, na Anaishi miongoni mwa binadamu wakati wote. Amekuwa nguvu ya kuendesha maisha ya mwanadamu, chanzo cha kuwepo kwa binadamu, na amana ya fahari ya kuwepo kwa binadamu baada ya kuzaliwa. Husababisha binadamu kuzaliwa upya, na kumwezesha kwa ushupavu kuishi kwa kila jukumu lake. Kwa sababu ya uwezo Wake, na nguvu ya maisha Yake yasiyopungua, binadamu ameishi kwa kizazi baada ya kizazi, ambapo nguvu ya uhai wa Mungu umekuwa uti wa mgongo wa kuwepo kwa binadamu, na ambayo Mungu amelipa gharama ambayo hakuna mtu wa kawaida amewahi kulipa. Nguvu za Mungu za maisha zinaweza kutawala juu ya nguvu zozote; zaidi ya hayo, inazidi mamlaka yoyote. Maisha Yake ni ya milele, nguvu zake za ajabu, na nguvu Zake za maisha si rahisi kuzidiwa na kiumbe yeyote au nguvu za adui. Nguvu za maisha ya Mungu zipo, na hung'aa mwangaza wake ulio mzuri sana, bila ya kujali muda au mahali. Maisha ya Mungu, huishi milele bila kubadilika katika kusumbuka kwa mbingu na nchi. Mambo yote hupita, lakini maisha ya Mungu hubaki, kwa maana Mungu ni chanzo cha kuwepo kwa mambo yote, na mizizi ya kuwepo kwao. Asili ya maisha ya mwanadamu hutoka kwa Mungu, kuwepo kwa mbingu ni kwa sababu ya Mungu, na kuwepo kwa ardhi kunatokana na nguvu ya uhai wa Mungu. Hakuna kitu kinachomiliki nguvu kinachoweza kuzidi ukuu wa Mungu, na hakuna kitu chenye nguvu kinachoweza kuvunja mipaka ya mamlaka ya Mungu. Kwa njia hii, bila kujali wao ni nani, kila mtu lazima ajiwasilishe kwa utawala wa Mungu, kila mtu lazima aishi chini ya amri za Mungu, na hakuna mtu anayeweza kutoroka kutoka katika utawala Wake.
Pengine, sasa, unataka kupokea maisha, au labda unataka kupata ukweli. Vyovyote vilivyo, unataka kumpata Mungu, kumpata Mungu unayeweza kutegemea, na ambaye anaweza kukupa uzima wa milele. Ukitaka kupata uzima wa milele, lazima kwanza uelewe chanzo cha uzima wa milele, na lazima kwanza ujue Mungu yuko wapi. Tayari nilishasema Mungu pekee ndiye maisha yasiyobadilika, na Mungu tu ndiye aliye na njia ya maisha. Kwa kuwa maisha Yake ni imara, hivyo ni ya milele; kwa kuwa Mungu tu ndiye njia ya maisha, basi Mungu Mwenyewe ni njia ya uzima wa milele. Kwa hivyo, lazima kwanza uelewe aliko Mungu, na jinsi ya kupata njia hii ya uzima wa milele. Hebu sasa tushiriki kwa masuala haya mawili tofauti.
Kama kweli unataka kupata njia ya uzima wa milele, na kama wewe unayo tamaa katika utafutaji wako kwa ajili yake, basi kwanza ulijibu swali hili: Mungu yuko wapi leo? Labda utajibu kwamba Mungu anaishi mbinguni, bila shaka—Hangeishi katika nyumba yako? Labda unaweza kusema, kawaida Mungu anaishi kati ya mambo yote. Au unaweza kusema kwamba Mungu anaishi katika moyo wa kila mtu, au kwamba Mungu yuko katika ulimwengu wa kiroho. Mimi sipingi lolote kati ya haya, lakini lazima nifafanue suala hilo. Sio sahihi kabisa kusema kwamba Mungu anaishi katika moyo wa mwanadamu, wala si makosa kabisa. Hiyo ni kwa sababu, miongoni mwa waumini katika Mungu, kuna wale ambao imani yao ni ya kweli na wale ambao imani yao ni uongo, kuna wale ambao Mungu anawakubali na wale ambao hawakubali, kuna wale ambao humfurahisha na wale ambao ni chukizo, na kuna wale ambao Yeye huwafanya kamili na wale ambao hupunguza. Na hivyo mimi Nasema kwamba Mungu Anaishi tu katika nyoyo za watu wachache, na watu hawa bila shaka ni wale ambao kweli wanaamini katika Mungu, wale ambao Mungu anawakubali, wale ambao humpendeza, na wale ambao Yeye huwafanya kamili. Wao ni wale wanaoongozwa na Mungu. Kwa kuwa wanaongozwa na Mungu, kwa hivyo ni watu ambao tayari wamesikia na kuona njia ya Mungu ya uzima wa milele. Wale ambao imani yao kwa Mungu ni ya uongo, wale ambao hawajaidhinishwa na Mungu, wale ambao wanadharauliwa na Mungu, wale ambao wamechujwa na Mungu—wamefungwa katika kukataliwa na Mungu, wamefungwa kubaki bila njia ya maisha, na wamefungwa kubaki wajinga wa kujua aliko Mungu. Kwa upande mwingine, wale ambao Mungu anaishi katika nyoyo zao wanajua aliko Mungu. Wao ni watu wale ambao Mungu huwapa njia ya uzima wa milele, na ni wale wanaomfuata Mungu. Je, unajua, sasa, aliko Mungu? Mungu yupo katika moyo wa mtu na upande wa mtu. Hayupo tu katika ulimwengu wa kiroho, na juu ya mambo yote, lakini hata zaidi Yupo duniani ambapo mwanadamu huishi. Na hivyo kufika kwa siku za mwisho kumechukua hatua ya kazi ya Mungu katika sehemu mpya. Mungu ana ukuu juu ya mambo yote katika ulimwengu, na Yeye ni uti wa mgongo wa mwanadamu katika moyo wake, na zaidi ya hayo, Yeye yuko miongoni mwa wanadamu. Ni kwa njia hii pekee Anaweza kuleta njia ya maisha kwa binadamu, na kumleta mwanadamu katika njia ya maisha. Mungu amekuja duniani, na Anaishi kati ya wanadamu, ili wanadamu wanaweza kupata njia ya maisha, na hivyo binadamu anaweza kuwepo. Wakati huo huo, Mungu pia huamuru mambo yote katika ulimwengu, ili wapate kushirikiana na usimamizi Wake miongoni mwa wanadamu. Na hivyo, kama wewe unakiri tu kwamba Mungu yuko mbinguni na katika moyo wa mwanadamu, lakini usikiri ukweli wa kuwepo kwa Mungu miongoni mwa watu, basi kamwe hutapata uzima, na kamwe hutapata njia ya kweli.
Mungu Mwenyewe ni maisha, na kweli, na uzima Wake na ukweli hutawala. Wale ambao hawana uwezo wa kupata ukweli kamwe hawatapata uzima. Bila mwongozo, msaada, na utoaji wa kweli, nanyi tu mtapata barua, mafundisho, na zaidi sana, kifo. Maisha ya Mungu ni ya milele, na ukweli wake na maisha hupatana. Kama huwezi kupata chanzo cha ukweli, basi huwezi kupata lishe ya maisha; kama huwezi kupata starehe ya maisha, basi utakuwa hakika huna ukweli, na hivyo mbali na mawazo na dhana, ukamilifu wa mwili wako hautakuwa chochote ila mwili, mwili wako unaonuka. Ujue kwamba maneno ya vitabu hayahesabiki kama maisha, kumbukumbu za historia haziwezi kupokelewa kama ukweli, na mafundisho ya siku za nyuma hayawezi kutumika kama sababu ya maneno ya sasa anayosema Mungu. Kinachoonyeshwa tu na Mungu anapokuja duniani na kuishi miongoni mwa binadamu ni ukweli, maisha, mapenzi ya Mungu, na njia Yake ya sasa ya kufanya kazi. Kama wewe utatumia rekodi ya maneno yaliyosemwa na Mungu wakati wa enzi zilizopita leo, basi wewe ni mtafutaji wa mambo ya kale, na njia bora ya kukueleza wewe ni mtaalamu wa urithi wa kihistoria. Kwa sababu wewe daima unaamini katika athari ya kazi ambayo Mungu alifanya katika nyakati zilizopita, amini tu katika kivuli cha Mungu alichowacha awali Alipokuwa Akifanya kazi miongoni mwa wanadamu, na kuamini tu kwa njia ambayo Mungu aliwapa wafuasi wake katika nyakati za zamani. Huamini katika mwelekeo wa kazi ya Mungu leo, huamini katika uso wa utukufu wa Mungu leo, na huamini katika njia ya sasa ya kweli iliyotolewa na Mungu. Na hivyo wewe ni mwotaji wa mchana ambaye hana ufahamu kamwe na hali ya mambo ya sasa. Kama sasa bado wewe unafuata maneno yasiyokuwa na uwezo wa kuleta maisha kwa binadamu, basi wewe ni kipande cha ukuni uliokauka kisicho na matumaini[a], kwa maana wewe ni mwenye kushikilia ukale mno, asiyeweza kutiishwa kwa urahisi, huwezi kusikiza wosia!
Mungu aliyepata mwili Anaitwa Kristo, na hivyo Kristo ambaye Anaweza kuwapa binadamu ukweli anaitwa Mungu. Hakuna kitu kikuu kuliko hiki, Kwa kuwa Anayo hali ya Mungu, na ana tabia za Mungu, na hekima katika kazi Yake, ambayo haiwezi kupatikana kwa binadamu. Wale wanaojiita Kristo, walakini hawawezi kufanya kazi ya Mungu, ni matapeli. Kristo sio tu udhihirisho wa Mungu duniani, badala yake, mwili hasa ulioigwa na Mungu kufanya na kutimiza kazi Yake kati ya wanadamu. Mwili huu si ule unaoweza kubadilishwa na mtu yeyote tu, lakini ambao unaweza kutosha kufanya kazi ya Mungu duniani, na kueleza tabia ya Mungu, na pia kumwakilisha Mungu, na kumpa binadamu maisha. Hivi karibuni au baadaye, wale Kristo bandia wataanguka wote, ingawa wanadai kuwa Kristo, hawana chochote cha hali ya Kristo. Na hivyo mimi nasema kwamba hali halisi ya Kristo haiwezi kuelezwa na mwanadamu, bali inajibiwa na kuamuliwa na Mungu Mwenyewe. Kwa njia hii, kama kweli unataka kutafuta njia ya maisha, lazima kwanza ukiri kuwa ni kwa kuja duniani ndipo Anazirejesha njia za maisha kwa binadamu, na lazima kukiri ni katika siku za mwisho Yeye anakuja duniani kuhifadhia njia ya maisha kwa mwanadamu. Haya sio ya wakati wa nyuma; yanatendeka leo.
Kristo wa siku za mwisho huleta uzima, na huleta kudumu kwa njia ya kweli na ya milele. Ukweli huu ni njia ambayo binadamu atapata uzima, na njia pekee ambayo mtu atamjua Mungu na kuidhinishwa na Mungu. Kama hutatafuta njia ya maisha inayotolewa na Kristo wa siku za mwisho, basi kamwe hutapata kibali cha Yesu, na kamwe hutastahili kuingia lango la ufalme wa mbinguni, maana wewe ni kikaragosi na mfungwa wa historia. Wale ambao wanadhibitiwa na kanuni, na maandiko, na waliofungwa na historia kamwe hawataweza kupata maisha, na kamwe hawataweza kupata njia ya daima ya maisha. Hayo ni kwa sababu walio nayo ni maji machafu yaliyolala palepale kwa maelfu ya miaka, badala ya maji ya uzima yanayotiririka kutoka kwenye kiti cha enzi. Wale ambao hawajaruzukiwa maji ya uzima daima watabakia maiti, vitu vya kuchezewa na Shetani, na wana wa Jehanamu. Je, basi jinsi gani wanaweza kumtazama Mungu? Kama wewe kamwe hujaribu kushikilia kwenye siku zilizopita, jaribu tu kuweka mambo kama yalivyo kwa kusimama kwa utulivu, na wala hujaribu kubadili hali kama ilivyo na kuacha historia, basi wewe hutakuwa daima dhidi ya Mungu? Hatua za kazi ya Mungu ni kubwa na zenye nguvu, kama kufurika kwa mawimbi na mngurumo wa radi—ilhali wewe unakaa na kwa uvivu ukisubiri uharibifu, na kujikita katika upumbavu wako na kutofanya chochote. Kwa njia hii, jinsi gani unaweza kuchukuliwa kama mtu anayefuata nyayo za Mwanakondoo? Jinsi gani unaweza kuhalalisha Mungu unayeshikilia kama Mungu ambaye ni daima mpya na si kamwe wa zamani? Na jinsi gani maneno ya vitabu vyako vya manjano yanaweza kukubeba hadi enzi mpya? Yanawezaje kukuongoza katika kutafuta hatua za kazi ya Mungu? Na jinsi gani yanaweza kukuchukua wewe kwenda mbinguni? Unayoshikilia mikononi ni barua ambazo zisizoweza kukuondolea kitu ila furaha ya muda mfupi, sio ukweli unaoweza kukupa maisha. Maandiko unayosoma ni yale tu ambayo yanaweza kuimarisha ulimi wako, sio maneno ya hekima ambayo yanaweza kukusaidia kujua maisha ya binadamu, wala njia inayoweza kukuongoza kwa ukamilifu. Je, si tofauti hii hukupa sababu kwa ajili ya kutafakari? Je, si inakuruhusu kuelewa siri zilizomo ndani? Je, una uwezo wa kujiwasilisha mwenyewe mbinguni kukutana na Mungu? Bila kuja kwa Mungu, je, unaweza kujichukua mwenyewe kwenda mbinguni kufurahia pamoja na familia ya Mungu? Je, wewe bado unaota sasa? Basi, Napendekeza sasa acha kuota, na kuangalia Anayefanya kazi sasa, na Anayefanya kazi ya kuwaokoa binadamu siku za mwisho. Kama huwezi, wewe kamwe hutapata ukweli, na kamwe hutapata uzima.
Wale ambao wanataka kupata uzima bila kutegemea ukweli wa neno la Kristo ni watu wafidhuli mno duniani, na wale ambao hawawezi kukubali njia ya maisha inayoletwa na Kristo wamepotea ndotoni. Na hivyo nasema kwamba watu ambao hawakubali Kristo wa siku za mwisho watadharauliwa milele na Mungu. Kristo ni lango la binadamu kwa ufalme katika siku za mwisho, ambayo hakuna anayeweza kupita bila Yeye. Hakuna anayeweza kukamilishwa na Mungu ila kwa njia ya Kristo. Unaamini katika Mungu, na hivyo ni lazima ukubali neno Lake na kutii njia Yake. Lazima usifikiri juu ya kupata baraka tu bila kupokea ukweli, au kukubali utoaji wa maisha. Kristo Anakuja katika siku za mwisho ili wale wote ambao kweli wanaamini katika Yeye waweze kupata maisha. Kazi Yake ni kwa ajili ya kuhitimisha enzi ya zamani na kuingia enzi mpya, na ni njia ambayo lazima ichukuliwe na wale wote ambao wataingia enzi mpya. Kama huna uwezo wa kumtambua Yeye, na badala yake kumhukumu, kulikufuru jina Lake au hata kumtesa Yeye, basi wewe umefungwa kuchomwa milele, na kamwe hutaingia katika ufalme wa Mungu. Kwa maana Kristo Mwenyewe ni onyesho la Roho Mtakatifu, onyesho la Mungu, Yule ambaye Mungu amemkabidhi kufanya kazi Yake hapa duniani. Na hivyo nasema kwamba kama huwezi kukubali yote yanayofanywa na Kristo wa siku za mwisho, basi unakufuru Roho Mtakatifu. Adhabu ambayo lazima ishuhudiwe na wale ambao wanakufuru Roho Mtakatifu ni hasa dhahiri kwa wote. Nawaambia tena kwamba kama mtampinga Kristo wa siku za mwisho, na kumkanusha, basi hakuna mtu ambaye anaweza kubeba matokeo ya hilo kwa niaba yako. Aidha, tangu siku hii na kuendelea huwezi kuwa na nafasi nyingine ya kupata kibali cha Mungu; hata kama utajaribu kujikomboa mwenyewe, kamwe tena hutautazama uso wa Mungu. Kwa kuwa unachopinga si binadamu, unachokataa si jambo dogo, bali ni Kristo. Je, unafahamu ghadhabu ya matokeo haya? Wewe hujafanya makosa madogo, bali umetenda uhalifu wa kutisha. Na hivyo Nashauri kila mtu kutoweka wazi meno yenu mbele ya ukweli, au kufanya shutuma bila ya kujali, kwa kuwa ni ukweli tu unaoweza kukuletea maisha, na hakuna kitu isipokuwa ukweli kinachoweza kukuruhusu kuzaliwa upya na kutazama uso wa Mungu.
kutoka kwa "Neno Laonekana katika Mwili"
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumatatu, 29 Oktoba 2018

Neno la Mungu | "Wale Waliofanywa Kuwa Watimilifu Ndio tu Wanaoweza Kuishi Maisha Yenye Maana"

Neno la Mungu | "Wale Waliofanywa Kuwa Watimilifu Ndio tu Wanaoweza Kuishi Maisha Yenye Maana"

Mwenyezi Mungu anasema, "Wale waliofanywa kuwa watimilifu hawawezi tu kuwa watiifu baada ya kushindwa, lakini wanaweza pia kuwa na maarifa na kubadilisha tabia yao. Wanamjua Mungu, wamepitia njia ya Mungu mwenye upendo, na wamejazwa na ukweli. Wanajua namna ya kupitia kazi ya Mungu, wanaweza kuteseka kwa ajili ya Mungu, na wanayo mapenzi yao wenyewe. … Kufanywa kuwa watimilifu kunarejelea wale ambao, baada ya kukamilika kwa kazi ya ushindi, wanaweza kufuatilia ukweli na kufaidika kutoka kwa Mungu. Kunaashiria wale ambao, baada ya kukamilika kwa kazi ya ushindi, wanasimama imara katika majaribio na wanaishi kwa kudhihirisha ukweli."
Soma Zaidi: Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumapili, 28 Oktoba 2018

Swahili Christian Video "Bwana Anakuja Kwa Namna Gani Hasa?" | The Son of Man Has Come to Earth

Swahili Christian Video "Bwana Anakuja Kwa Namna Gani Hasa?" | The Son of Man Has Come to Earth

Katika siku za mwisho, hali ya moyo ya Wakristo wanaongoja kurudi kwa Bwana Yesu inakuwa kali sana, lakini ni kwa vipi, hasa, Bwana atarudi? Baadhi wanasema, "Bwana Yesu atakuja na mawingu." Wengine wanasema, "Unabii unaotabiri kurudi Kwake nao unasema, 'Tazama, mimi nakuja kama mwizi' (Ufu 16:15). 'Bali kwanza lazima apitie mambo mengi, na akataliwe na kizazi hiki' (Luka 17:25). 'Na kukawa na kelele saa sita ya usiku, Tazama, anakuja bwana arusi; ondokeni nje ili kumkaribisha' (Mat 25:6). Kama anakuja na mawingu kwa kila mmoja kumwona, tunaelezaje fumbo la Yeye kuja kwa siri, kuteseka, na kukataliwa, pamoja na kusema kwamba wengine watashuhudia kuhusu kurudi Kwake?" Bwana atatokeaje kwetu? Mchezo wa kuchekesha Bwana Anakujaje Hasa unajaribu kusuluhisha mashaka yetu kuhusu jambo hili.
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumamosi, 27 Oktoba 2018

Filamu za Kikristo | "Mazungumzo" | Christian Testimony of Overcoming Satan

Filamu za Kikristo | "Mazungumzo" | Christian Testimony of Overcoming Satan

Jiang Xinyi na Wakristo wengine walikamatwa na serikali ya CCP; wao huwatesa Wakristo kwa ukatili ili kutwaa fedha za kanisa na kuwakamata viongozi zaidi wa kanisa. Kisha, ili kuwalazimisha kuikataa imani yao, wao huzindua kampenii moja baada ya nyingine ya kuwatia kasumba, lakini kwa uongozi wa maneno ya Mungu, wao huweza kuyashinda mateso na udanganyifu wote wa Shetani. Wao hutegemea ukweli kushiriki katika vita vikali na serikali ya CCP …
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Ijumaa, 26 Oktoba 2018

Swahili Gospel Movie Segment "Mungu Anashikilia Ukuu Juu Ya Majaliwa ya Kila Nchi na Watu Wote"

Swahili Gospel Movie Segment "Mungu Anashikilia Ukuu Juu Ya Majaliwa ya Kila Nchi na Watu Wote"

Milki ya kale ya Kirumi na Milki ya zamani ya Uingereza zilikuwa na mafanikio na nguvu kwa haraka sana na kisha kufifia kuelekea kudhoofika na uharibifu. Sasa, Marekani limekuwa taifa kubwa lisilobishaniwa la ulimwengu na pia lina jukumu lisilofidika la kudumisha na kuimarisha hali ya ulimwengu. Ni mafumbo ya aina gani hasa yaliyofichika kuhusiana na kuinuka na kuanguka kwa mataifa? Ni nani aliye na mamlaka juu ya majaliwa ya kila nchi na watu wote? Sehemu hii ya ajabu kutoka kwa filamu ya Kikristo, "Yule Anayeshikilia Ukuu Juu ya Kila Kitu", itakufichulia majibu haya.
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Alhamisi, 25 Oktoba 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Ujana Uliotumiwa Bila Majuto

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ukatili Mateso

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Ujana Uliotumiwa Bila Majuto

Xiaowen, Chongqing
"Upendo ni hisia safi, safi bila ya dosari. Tumia moyo wako, tumia moyo wako kupenda na kuhisi na kutunza. Upendo hauweki masharti au vikwazo au umbali. Tumia moyo wako, tumia moyo wako kupenda na kuhisi na kutunza. Ukipenda hudanganyi, kunung'unika, kutelekeza, kutarajia kupata malipo" ("Upendo safi bila Dosari" katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Wimbo huu wa neno la Mungu siku moja ulinisaidia kupitia maumivu ya maisha ya muda mrefu yaliorefuka bure gerezani ambao ulidumu miaka 7 na miezi 4. Ingawa serikali ya CCP ilininyang'anya miaka mizuri zaidi ya ujana wangu, nimepata ukweli halisi na wa thamani zaidi kutoka kwa Mwenyezi Mungu na kwa hiyo sina malalamiko au majuto.
Mnamo mwaka wa 1996 nilipokea kukuzwa na Mungu na kukubali wokovu wa Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho. Kupitia kusoma maneno ya Mungu na kukusanyika katika ushirika, nilidhihirisha kwamba yote ambayo Mungu amesema ni ukweli, ambayo ni tofauti kabisa na maarifa na nadharia zote za dunia hii mbovu. Neno la Mwenyezi Mungu ni methali ya juu zaidi kwa maisha. Kilichofanya nisisimke zaidi kilikuwa kwamba ningeweza kuwa wa kawaida na wazi na kuzungumza kwa uhuru juu ya chochote na ndugu wa kiume na wa kike. Sikuwa na haja hata kidogo ya kujilinda dhidi ya lawama au kushindwa kwa akili na watu wakati wa kuingiliana nao. Nilihisi faraja na furaha ambayo sikuwahi kuhisi awali; kwa kweli niliipenda familia hii. Hata hivyo, si muda mrefu ulipita kabla sijasikia kwamba nchi hii haikuwaruhusu watu kumwamini Mwenyezi Mungu. Jambo hili lilinifanya kuchanganyikiwa kabisa, kwa sababu neno Lake liliwaruhusu watu kumwabudu Mungu na kuitembea njia sahihi ya maisha; liliwaruhusu watu kuwa waaminifu. Kama kila mtu angemwamini Mwenyezi Mungu, basi ulimwengu wote ungekuwa na amani. Kwa kweli sifahamu: Kumwamini Mungu kulikuwa ndiko shughuli ya haki zaidi; kwa nini serikali ya CCP ilitaka kutesa na kupinga kumwamini Mwenyezi Mungu kiasi kwamba ingewakamata waumini Wake? Niliwaza: Bila kujali ni vipi serikali ya CCP inatutesa au ni jinsi gani maoni ya umma ya kijamii ni makubwa, nimeamua kuwa hii ndiyo njia sahihi ya maisha na mimi kwa hakika nitaitembelea hadi mwisho!
Baada ya haya, nilianza kutekeleza wajibu wangu katika kanisa wa kusambaza vitabu vya neno la Mungu. Nilijua kwamba kutimiza wajibu huu katika nchi hii ambayo ilimpinga Mungu ilikuwa hatari sana na ningeweza kukamatwa wakati wowote. Lakini nilijua pia kuwa kama sehemu ya uumbaji wote, ulikuwa ni misheni yangu katika maisha wa kutumia kila kitu kwa ajili ya Mungu na kutimiza wajibu wangu; lilikuwa ni jukumu ambalo sikuweza kulikwepa. Nilipokuwa tu nikianza kushirikiana na Mungu kwa imani, siku moja mnamo Septemba mwaka wa 2003, nilikuwa njiani kuwapelekea ndugu fulani wa kiume na wa kike vitabu vya neno la Mungu na nilikamatwa na watu kutoka kwa Ofisi ya Usalama wa Taifa ya mjini.
Katika Ofisi ya Usalama wa Taifa, nilihojiwa tena na tena na sikujua jinsi ya kujibu; nilimlilia Mungu kwa haraka: "Ee Mwenyezi Mungu, nakuuliza Wewe unipe hekima Yako, na unipe maneno ambayo napaswa kuzungumza ili nisikusaliti Wewe na niweze kuwa shahidi kwa ajili Yako." Wakati huo, nilimlilia Mungu kila siku; Sikuthubutu kumwacha Mungu, nilimwomba tu Mungu anipe akili na hekima ili niweze shughulikia polisi hao waovu. Shukrani kwa Mungu kwa kunichunga na kunilinda; kila wakati nilipohojiwa, ama nilikuwa nikitema mate, au nilikuwa na kwikwi mfululizo na sikuweza kuzungumza. Katika kuona kazi ya ajabu ya Mungu, nikaamua kwa dhati: Kuwa waziwazi! Wanaweza kuchukua kichwa changu, wanaweza kuchukua maisha yangu, lakini kabisa hawatanifanya kumsaliti Mungu leo kamwe! Ninapoweka azimio langu kwamba ningependa kuhatarisha maisha yangu kuliko kumsaliti Mungu kama Yuda, Mungu alinipa "endelea" kwa kila namna: Kila wakati nilipohojiwa, Mungu angenilinda na kuniruhusu nipitie majaribu. Ingawa sikusema chochote, serikali ya CCP ilinishtaki kwa "kutumia dhehebu bovu kuangamiza utekelezaji wa sheria" na kunihukumu kifungo cha miaka 9 katika jela! Niliposikia hukumu ya mahakama, sikuwa na huzuni kwa sababu ya ulinzi wa Mungu, wala sikuwaogopa; badala yake, niliwadharau. Wakati watu hao walikuwa wakitangaza hukumu, nilisema kwa sauti ya chini: "Huu ni ushahidi kwamba serikali ya CCP inampinga Mungu!" Baadaye, maafisa wa usalama wa umma walikuja tu kuchunguza jinsi mtazamo wangu ulivyokuwa, na nikawaambia kwa utulivu: "Miaka tisa ni nini? Wakati utakapofika kwangu kutoka, bado nitakuwa mshiriki wa Kanisa la Mwenyezi Mungu; ikiwa huniamini, subiri tu na kuona! Lakini unapaswa kukumbuka, kesi hii wakati mmoja ilikuwa katika mikono yenu!" Mtazamo wangu kwa kweli uliwashangaza; waliinua vidole gumba vyao juu na kusema tena na tena: "Umekuwa mahiri sana! Tunakustahi! Wewe ni mjeuri kuliko Dada Jiang! [a] Hebu tukutane wakati utakapotoka, na tutakupa chakula cha jioni!" Wakati huo, nilihisi kwamba Mungu alipata utukufu na moyo wangu ulipendezwa. Mwaka huo nilipohukumiwa, nilikuwa na umri wa miaka 31 tu.
Jela za China ni kuzimu duniani, na maisha ya muda mrefu ya gereza yalinifanya kuona kabisa unyama wa kweli wa Shetani na kiini chake cha kishetani ambacho kimekuwa adui kwa Mungu. Polisi wa China huwa hawafuati utawala wa sheria, lakini badala yake hufuata utawala wa uovu. Gerezani, polisi binafsi huwa hawawashughulikii watu, lakini huwachochea wafungwa kufanya vurugu ili kutiisha wafungwa wengine. Hawa polisi waovu pia hutumia mbinu za aina zote kuyafungia mawazo ya watu; kwa mfano, kila mtu anayeingia anapaswa kuvaa sare sawa za mfungwa zilizo na nambari maalum ya mfululizo, ni sharti anyolewe nywele zao kulingana na matakwa ya gereza, ni lazima avae viatu vilivyoidhinishwa na jela, anapaswa kutembelea vijia ambavyo gereza limemruhusu kutembelea, na anapaswa kutembea mwendo wa askari kwa kasi iliyoruhusiwa na gereza. Bila kujali kama ni majira ya kuchipua, majira ya joto, majira ya kupukutika kwa majani au majira ya baridi, ikiwa kuna mvua au kuna jua, au kama ni siku ya baridi kali, wafungwa wote wanapaswa kufanya kama walivyoamriwa bila ya uchaguzi wowote. Kila siku tulihitajika kukusanyika angalau mara 15 kupangwa na kuimba nyimbo za sifa kwa serikali ya CCP angalau mara tano; tulikuwa pia na kazi za kisiasa, yaani, walitufanya tujifunze sheria za gereza na katiba, na walitufanya kufanya mtihani kila baada ya miezi sita. Kusudi la hili lilikuwa ni kututia kasumba. Pia wangeyapima bila mpango maalum maarifa yetu ya masomo na sheria za jela. Polisi wa gereza walitutesa sio kiakili tu, wao pia walituharibu kimwili kwa unyama kamili: nilipaswa kufanya kazi ngumu kwa zaidi ya saa kumi kwa siku, kama tumesokomezwa pamoja na watu wengine mia kadhaa katika kiwanda chembamba tukifanya kazi za mikono. Kwa sababu kulikuwa watu wengi sana katika nafasi ndogo kiasi hicho, na kwa sababu kelele ya kutatanisha ya mashine ilikuwa kila mahali, bila kujali mtu alikuwa na afya kiasi gani, mwili wake ungepata uharibifu mkubwa kama angekaa hapo kwa muda. Nyuma yangu kulikuwa na mashine ya kutoboa matundu na kila siku ilitoboa mashimo mfululizo. Sauti ya kunguruma iliyopitisha ilikuwa isiyovumilika na baada ya miaka michache, nilipata ugonjwa hatari wa kutosikia. Hata leo hii sijapata nafuu. Kitu kilichokuwa kibaya zaidi kwa watu kilikuwa vumbi na uchafuzi wa mazingira katika kiwanda hicho. Baada ya kuchunguzwa, watu wengi walipatikana wakiwa wameambukizwa kifua kikuu na uvimbe wa koromeo. Aidha, kutokana na muda mrefu wa kukaa kitako hapo kufanya kazi ya mikono, ilikuwa haiwezekani kusogea hapa na pale na watu wengi waliambukizwa ugonjwa hatari wa bawasiri. Serikali ya CCP iliwachukulia wafungwa kama mashine za kutengeneza pesa; hawakuwa na mazingatio hata kidogo ya kama mtu aliishi au alikufa. Waliwafanya watu kufanya kazi tangu asubuhi na mapema mpaka usiku kabisa. Mara nyingi nilikuwa nimechoka sana kiasi kwamba sikuweza kuendelea kimwili. Haikuwa hii tu, nilipaswa pia nishughulike na aina zote za mitihani ya nasibu bali na kazi zangu za kila wiki za kisiasa, kazi za mikono, na kazi za umma, nk. Kwa hiyo, kila siku nilikuwa katika hali ya wasiwasi wa hali ya juu; hali yangu ya kiakili ilikuwa ikinyoshwa daima, na nilikuwa na wasiwasi zaidi kwamba singeweza kuwafikia wengine kama ningezembea hata kidogo, na kwa hiyo ningeadhibiwa na polisi wa gereza. Katika mazingira ya aina hiyo, kumaliza siku moja salama haikuwa kazi rahisi kufanya.
Nilipoanza tu kumaliza kifungo changu, sikuweza kustahimili aina hii ya kuharibiwa kikatili na polisi wa gereza. Aina zote za kazi ngumu ya mikono na shinikizo la kiitikadi lilifanya kupumua kuwe kugumu, sembuse kuwa ilibidi niwe na mawasiliano ya aina yote na wafungwa. Nilibidi pia kuvumilia dhuluma na matusi ya polisi wa kishetani wa gereza na wafungwa …. Niliteswa mara kwa mara na kuwekwa taabuni. Mara kadhaa, nilizama katika hali ya kukata tamaa, hasa nilipofikiria urefu wa hukumu yangu ya miaka tisa, nilihisi mshindo wa kutojiweza kwa kuhuzunisha na sikujua ni mara ngapi nililia—kiasi kwamba nilifikiria kujiua ili kujiweka huru kutoka kwa maumivu niliyokuwa nayo. Kila wakati nilipokuwa na huzuni kupita kiasi na sikuweza kujifadhili, ningeomba kwa haraka na kumlilia Mungu na Mungu angenipatia nuru na kuniongoza: “Bado huwezi kufa. Sharti ukaze ngumi yako na kuendelea kuishi kwa ari; lazima uishi maisha kwa ajili ya Mungu. Watu wanapokuwa na ukweli ndani yao basi wanakuwa na azimio hili na kamwe hawatamani kufa tena; kifo kinapokutisha, utasema, ‘Ee Mungu, siko radhi kufa; bado sikufahamu! Bado sijalipiza upendo Wako! … Lazima niwe na ushuhuda mzuri wa Mungu. Lazima nilipize upendo wa Mungu. Baada ya hapo, haijalishi jinsi nitakavyokufa. Kisha, nitakuwa nimeishi maisha ya kutosheleza. Bila kujali ni nani mwengine anayekufa, sitakufa sasa; lazima niendelee kuishi kwa ushupavu’” (“Jinsi ya Kujua Asili ya Mwanadamu” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo). Maneno ya Mungu yalikuwa kama maono laini na latifu ya mama yangu akiutuliza moyo wangu mpweke. Yalikuwa pia kama baba yangu akitumia mikono miwili kuyafuta kwa uangalifu machozi kutoka kwa uso wangu kwa upendo. Moja kwa moja, mkondo wa vuguvugu na nguvu zilikurupuka kupitia moyo wangu. Ingawa nilikuwa nikiteseka kimwili katika jela la giza, kujaribu kujiua hakukuwa mapenzi ya Mungu. Singeweza kumshuhudia Mungu na pia ningekuwa kichekesho cha Shetani. Ingekuwa ushuhuda kama ningetoka hai kutoka gereza hili lenye pepo baada ya miaka tisa. Maneno ya Mungu yalinipa ujasiri wa kuendelea na maisha yangu na nikafanya azimio moyoni mwangu: Haijalishi matatizo gani yaliyo mbele yangu, kwa uangalifu nitaendelea kuishi; nitaishi kwa ujasiri na nguvu na hakika nitashuhudia kuridhika kwa Mungu.
Mwaka nenda mwaka rudi, kazi ya kuzidi kiasi ilisababisha mwili wangu kudhoofika hatua kwa hatua. Baada ya kukaa kitako kwa muda mrefu katika kiwanda ningeanza kutoa jasho maridhawa na bawasiri zangu zingevuja damu zilipokuwa kali vya kutosha. Kutokana na upungufu wangu mkali wa damu, mara kwa mara ningehisi kizunguzungu. Lakini gerezani, kumwona daktari si jambo rahisi kufanya; kama polisi wa gereza walikuwa wamefurahi, wangenipa dawa za bei nafuu. Kama hawakuwa na furaha, wangesema nilikuwa nikijifanya mgonjwa ili kuepuka kazi. Ningevumilia mateso ya ugonjwa huu na kuyazuilia machozi yangu. Baada ya kazi ya siku kutwa ningekuwa nimechoka kabisa. Niliukokota mwili wangu mchovu hadi kwa chumba changu kidogo cha gereza na nilitaka kupata mapumziko, lakini sikuwa hata na chembe ya ya nguvu ya kupata usingizi madhubuti: Ama polisi wa gereza walikuwa wakiniita katikati ya usiku kufanya kitu fulani, au niliamshwa na kelele ya kunguruma iliyopigwa na polisi wa gereza. … Mara kwa mara nilichezewachezewa nao na kuteseka vibaya sana. Aidha, nililazimika kustahimili kutendewa kinyama na polisi hawa wa gereza. Nilikuwa kama mkimbizi nikilala sakafuni au ushorobani, au hata kando ya choo. Nguo nilizoziosha hazikuwa kavu, lakini zilikuwa zimefungwa pamoja na nguo za wafungwa wengine ili kukaushwa. Kuosha nguo katika majira ya baridi kulikuwa kwa kukatisha tamaa hasa, na watu wengi waliambukizwa ugonjwa wa baridi yabisi kwa sababu ya kuvaa mavazi manyevu kwa vipindi virefu vya wakati. Gerezani, haikuchukua muda mrefu kwa watu wenye afya kuwa goigoi na bozi, wadhaifu kimwili au kujawa magonjwa. Mara kwa mara tulikula majani ya mboga ya zamani, yaliyokaushwa na ambayo yalikuwa yamepitwa na msimu. Kama ulitaka kula kitu bora zaidi, basi ulilazimika kununua chakula ghali huko gerezani. Ingawa watu walifanywa kujifunza sheria gerezani, hakukuwa na sheria huko; polisi wa gereza ndio waliokuwa sheria na kama mtu yeyote angewaudhi, walipata sababu ya kukuadhibu—hata kwa kiasi kwamba waliweza kukuadhibu bila sababu yoyote. Hata la kudharauliwa zaidi ni kwamba walichukulia waumini wa Mwenyezi Mungu kuwa wahalifu wa kisiasa, wakisema kuwa uhalifu wetu ulikuwa mbaya zaidi kuliko mauaji na kuchoma mali. Kwa hiyo, walinichukia hasa na walinidhibiti kikamilifu, na kunitesa kikatili sana. Aina hii ya tabia mbovu ni ushahidi usiobadilika wa tabia potovu ya madikteta, upinzani kwa Mbinguni, na kuwa na uadui na Mungu! Baada ya kuvumilia mateso ya kikatili ya gereza, moyo wangu mara kwa mara ulijazwa na hasira ya haki: Ni sheria gani kumwamini Mungu na kumwabudu Mungu hukiuka? Ni uhalifu gani kumfuata Mungu na kuitembea njia sahihi ya maisha? Wanadamu waliumbwa na mikono ya Mungu na kumwamini Mungu na kumwabudu Mungu ni sheria ya mbingu na dunia; ni sababu gani serikali ya CCP iliyo nayo ya kuzuia kwa nguvu na kusumbua hili? Kwa dhahiri ni tabia yake potovu na upinzani kwa Mbingu; huwa inajiweka yenyewe dhidi ya Mungu katika kila kipengele, huwa inashikiza kitambulisho cha kupinga maendeleo kwa waumini wa Mwenyezi Mungu na hututesa kwa ukali na kutuharibu. Huwa inajaribu kuwaondosha waumini wote wa Mwenyezi Mungu kwa dharuba moja kali. Si huku ni kubadilisha weusi na weupe na kuwa mpinga maendeleo kikamilifu? Kwa hasira huipinga Mbingu na ina uhasama na Mungu; hatimaye ni lazima ipitie adhabu ya haki ya Mungu! Kila mahali kuna upotovu, lazima kuwe na hukumu; kila mahali kuna dhambi, lazima kuwe na adhabu. Hii ni sheria ya Mungu ya mbinguni iliyoamuliwa kabla, hakuna mtu anayeweza kuitoroka. Uhalifu muovu wa serikali CCP umepanda kwa anga, na itapitia maangamizo ya Mungu. Kama tu Mungu alivyosema: “Mungu ameichukia sana jamii hii ya giza toka zamani. Anasaga meno Yake, Akitamani kumkanyaga mwovu huyu, joka wa zamani mwenye chuki, ili kwamba asiinuke tena, na hatamnyanyasa tena mwanadamu; Hatasamehe matendo yake ya zamani, Hatavumilia udanganyifu wake kwa mwanadamu, atalipiza kisasi kwa kila kosa alilofanya katika enzi zote; Mungu hatamhurumia hata kidogo huyu kiongozi wa uovu wote, Atamharibu kabisa” (“Kazi na Kuingia (8)” katika Neno Laonekana katika Mwili).
Katika gereza hili la pepo, nilikuwa duni kuliko mbwa wa kutangatanga machoni mwa polisi hawa maovu; hawakunipiga na kunikemea tu, lakini polisi hawa waovu mara kwa mara na kwa ghafla wangeingia kwa vishindo na kutawanya matandiko yangu na vitu vyangu vya kibinafsi kuwa takataka. Pia, wakati wowote ambapo ghasia fulani zilifanyika katika ulimwengu wa nje, watu walio gerezani ambao ni wasimamizi wa masuala ya kisiasa wangenitafuta na kudadisi maoni yangu kuhusu matukio haya na kwa kawaida wangenishambulia kuhusu ni kwa nini niliitembea njia ya kumwamini Mungu. Kila wakati nilipokabiliwa na aina hii ya kuhojiwa, ningekuwa na wasiwasi, kwa sababu sikujua mpango upi muovu waliokuwa nao kwangu. Moyo wangu daima ulikuwa ukimwomba Mungu kwa haraka na kulilia msaada na mwongozo kupitia wakati wa kilele cha hatari hii. Siku baada ya siku, mwaka baada ya mwaka, dhuluma, unyonywaji, na ukandamizwaji viliniumiza kwa mateso yasiyosemeka: Kila siku nilipewa kazi ya mikono iliyozidi na majukumu ya kisiasa ya kuchusha, ya kuchosha, nilisumbuliwa pia na ugonjwa wangu na juu ya yote, nilidhoofika akili. Lilinifikisha kwenye ukingo wa kusambaratika. Hasa wakati nilipoona mfungwa wa makamo wa kike amejinyonga kutoka kwa dirisha usiku wa manane kwa sababu hakuweza kuvumilia mateso ya kinyama ya polisi hawa waovu, na mfungwa mwingine mzee wa kike aliyekufa kutokana matibabu ya ugonjwa wake yaliyocheleweshwa, nilizama katika shida zile zile zilizosonga na tena nikaanza kutafakari kujiua. Nilihisi kuwa kifo kilikuwa ndiyo aina bora ya faraja. Lakini nilijua kwamba huko kungekuwa kumsaliti Mungu na singeweza kufanya hivyo. Sikuwa na chaguo jingine lolote ila kuvumilia maumivu yote na kuitii mipango ya Mungu. Lakini mara tu nilipofikiri juu ya hukumu yangu ndefu, na kufikiri juu ya nilivyokuwa mbali na kupata uhuru, nilihisi kuwa hakuna maneno yaliyoweza kuelezea maumivu yangu na kukata tamaa kwangu; nilihisi kuwa sikuweza kuendelea kuhimili hili na kwamba sikujua ni muda gani ningeweza kusimama imara. Ni mara ngapi sikuweza kufanya chochote ila kujifunika kwa mfarishi wangu usiku wa manane na kulia, nikimuomba na kumsihi Mwenyezi Mungu na kumwambia Yeye kuhusu maumivu yote yaliyokuwa kwa mawazo yangu. Katika wakati wa maumivu yangu mengi na kutojiweza, niliwaza: Mimi ninateseka leo ili nipate kujitenga na upotovu na kupokea wokovu wa Mungu. Shida hizi ndizo ninazopaswa kupitia, na ambazo ni lazima nipitie. Mara tu nilipofikiria hili, sikuhisi uchungu tena; Badala yake, nilihisi kuwa kulazimishwa kuingia gerezani kwa sababu ya imani yangu kwa Mungu, na kupitia shida ili kupata wokovu lilikuwa jambo la thamani na umuhimu mkubwa mno; mateso haya yalikuwa ya thamani sana! Bila kujua, dhiki ya moyo wangu ilibadilika kuwa furaha na sikuweza kuzuia hisia zangu; nilianza kuimba bila kufungua mdomo wimbo wa uzoefu niliokuwa na uzoefu nao moyoni mwangu uitwao "Maisha Yetu si ya Bure": "Maisha yetu si ya bure", mateso yetu yana maana. Maisha yetu si ya bure, hatutakubali kughairi bila kujali ni jinsi gani maisha yalivyo magumu. Maisha yetu si ya bure, sisi hupata fursa nzuri ya kumjua Mungu. Maisha yetu si ya bure, sisi tunaweza kutumia rasilmali kwa ajili ya Mungu mkuu. Ni nani aliyebarikiwa kutuliko? Ni nani mwenye bahati kutuliko? Ee, kile ambacho Mungu hutupa kinazidi vyote vya vizazi vilivyopita; tunapaswa kuishi kwa ajili ya Mungu na tunapaswa kumlipa Mungu kwa sababu ya upendo Wake mkubwa." Niliurudia wimbo huo ndani ya moyo wangu na nilivyozidi kuimba ndani ya moyo wangu, ndivyo nilivyozidi kutiwa moyo; nilivyozidi kuimba, ndivyo nilivyozidi kuhisi kuwa nilikuwa na nguvu na furaha. Sikuweza kujizuia kuapa mbele ya Mungu: "Ee, Mwenyezi Mungu, ninakushukuru Wewe kwa faraja Yako na kunitumainisha ambavyo vimenisababisha kuwa tena na imani na ujasiri wa kuendelea kuishi. Umeniruhusu kujisikia kwamba Wewe kweli ni Bwana wa maisha yangu na Wewe ni nguvu ya maisha yangu. Ingawa nimefungwa mahali hapa pa kusikitisha sana, siko peke yangu, kwa sababu Umekuwa pamoja nami daima kupitia siku hizi za giza; Umenipa imani tena na tena na umenipa motisha kuendelea. Ee Mungu, kama ninaweza kutoka nje ya hapa siku moja na kuishi kwa uhuru, basi nitatimiza wajibu wangu na sitauumiza moyo Wako tena wala kujifanyia mipango mwenyewe. Ee Mungu, bila kujali jinsi siku zijazo zilivyo ngumu au zilivyo za shida, niko radhi kukutegemea Wewe kwendelea kuishi na nguvu!"
Gerezani, mara kwa mara nilikumbuka siku za nyuma tukiwa na ndugu zangu wa kiume na wa kike; huo ulikuwa wakati mzuri sana! Kila mtu alishangilia na kucheka, na pia tulikuwa na migogoro, lakini yote haya yalikuwa kumbukumbu nzuri. Lakini kila wakati nilipotafakari juu ya nyakati ambapo kwa uzembe nilifanya kazi zangu za zamani, nilihisi kuwa na hatia sana na mwenye kuwiwa. Nilifikiri juu ya migogoro niliyokuwa nayo na ndugu zangu wa kiume na wa kike kwa sababu ya tabia yangu ya kiburi; nilihisi kuwa na wasiwasi hasa na mwenye kujuta. Kila wakati hili lilipotokea, ningeangua kilio na kimya kimya ningeimba wimbo mashuhuri katika moyo wangu: “Ninajuta sana, Ninajuta sana, nimepoteza muda mwingi sana wa thamani. Muda husonga mbele milele na ni majuto tu ambayo hubaki. … Kwa ajili ya kuwiwa kwangu kwa zamani na nitaanza upya na imani na kujivunia. Mungu anipa fursa nyingine, na kwa uvumilivu Wake nitafanya uchaguzi wangu mpya. Nitafurahia siku hii hasa, kutenda ukweli, kutekeleza wajibu wangu vizuri inavyowezekana, na hivyo kumridhisha Mungu. Moyo wa Mungu una wasiwasi, umejaa matarajio. Kwa hiyo sitavunja moyo Wake tena" ("Ninajuta sana" katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Katika maumivu yangu na kujilaumu, mara kwa mara nilimwomba Mungu moyoni mwangu: Ee Mungu! Kwa hakika nimepungukiwa na Wewe mno; kama Utaliruhusu, niko radhi kutafuta kukupenda Wewe. Baada ya kuondoka gerezani, bado nitakuwa tayari kutimiza wajibu wangu na nitakuwa radhi kuanza tena! Nitaufidia upungufu wangu wa zamani! Wakati wa muda wangu gerezani, nilikuwa nimewakosa hasa wale ndugu wa kiume na wa kike niliokuwa nikiwasiliana nao asubuhi na usiku; kwa kweli nilitaka kuwaona, lakini katika gereza hili la pepo ambalo nilikuwa nimefungiwa, tamaa hii ilikuwa ombi lisilowezekana. Hata hivyo, mara kwa mara ningewaona ndugu hawa wa kiume na wa kike katika ndoto zangu; niliota kwamba tulikuwa tunasoma neno la Mungu pamoja na kuwasiliana ukweli pamoja. Tulikuwa na furaha na wachangamfu.
Wakati wa tetemeko kubwa la ardhi la Wenchuan la mwaka wa 2008, gereza tulimokuwa tulifungiwa ndani lilitetemeshwa na mimi nilikuwa mtu wa mwisho kuhama eneo hilo wakati huo. Katika siku hizo kulikuwa na mitikisiko midogo baada ya tetemeko ambayo haikusita. Wafungwa wote na polisi wa gereza waliogopa sana na kuwa na wasiwasi kiasi kwamba hawakuweza kuendelea. Lakini moyo wangu ulikuwa hasa mtulivu na imara, kwa sababu nilijua kwamba hili lilikuwa ni neno la Mungu likitimia; kulikuwa ni kuwasili kwa ghadhabu kali ya Mungu. Wakati wa tetemeko hilo moja katika miaka mia, neno la Mungu liliulinda moyo wangu daima; ninaamini kwamba maisha na kifo cha mwanadamu vyote vi mikononi mwa Mungu. Bila kujali jinsi Mungu anavyofanya hivyo, niko radhi kuitii mipango ya Mungu. Hata hivyo, kitu cha pekee kilichonifanya kuhuzunika ni kama ningekufa, basi singepata tena fursa ya kutimiza wajibu wangu kwa Bwana wa viumbe, singekuwa na fursa tena ya kuufidia upendo wa Mungu, na singeweza kuwaona ndugu zangu wa kiume na wa kike. Lakini, wasiwasi wangu ulikuwa uliozidi; Mungu alikuwa nami daima na alinipa ulinzi mkubwa sana, ambao uliniruhusu kuendelea kuishi baada ya tetemeko la ardhi na kuishi kwa amani wakati wa tetemeko!
Mnamo Januari ya mwaka wa 2011, niliachiliwa mapema, ambako hatimaye kulimaliza maisha yangu ya utumwa gerezani. Katika kupata uhuru wangu, moyo wangu ulikuwa na msisimko mkubwa: Ninaweza kurudi kanisani! Ninaweza kuwa pamoja na ndugu zangu wa kiume na wa kike! Maneno hayakuweza kuelezea hali yangu ya kihisia ya akili. Kile ambacho sikutarajia ni kwamba baada ya kurudi nyumbani, binti yangu hakunijua, na jamaa na marafiki zangu walinitazama kwa mtazamo wa pekee; wote walijitenga nami na hawangeingiliana nami. Watu waliokuwa karibu nami hawakunielewa au kunikaribisha. Wakati huu, ingawa sikuwa gerezani nikidhulumiwa na kuteswa, mitazamo ya dharau, dhihaka, na kuachwa vilifanya kuwe vigumu kustahimili. Nilikuwa dhaifu na hasi. Sikuweza kujizuia kutafakari juu ya siku za nyuma: wakati tukio lilipotendeka, nilikuwa na umri wa miaka thelathini na mmoja tu; wakati nilipotoka gerezani, majira nane ya baridi na majira saba ya joto yalikuwa yamepita. Ni mara ngapi ambapo Mungu alikuwa amepanga watu, mambo na vitu wakati wa upweke wangu na kutojiweza ili kunisaidia; ni mara ngapi maneno ya Mungu yalinifariji katika maumivu yangu na kukata tamaa kwangu; ni mara ngapi nilipotaka kufa Mungu alinipa uwezo wa kuwa na ujasiri wa kuendelea kuishi …. Katika kipindi hicho cha miaka mirefu ya mchungu, ni Mungu aliyeniongoza hatua kwa hatua nje ya bonde la kivuli cha mauti hadi kuendelea kuishi kwa ushupavu. Katika kukabili shida hii sasa, nilikuwa hasi na dhaifu na nilikuwa nimemsikitisha Mungu. Kwa kweli nilikuwa mwoga na mtu asiyeweza ambaye alikuwa alikuwa na asante ya punda! Katika kufikiria hili, moyo wangu ulishutumiwa vikali; sikuweza kujizuia kufikiri juu ya kiapo nilichofanya na Mungu wakati nilipokuwa gerezani: "Kama ninaweza kutoka nje ya hapa siku moja na kuishi kwa uhuru, basi bado nitatimiza wajibu wangu. Siko tayari kuumiza tena moyo wa Mungu na sitajifanyia mipango mwenyewe tena!" Niliwazia kiapo hiki na kutafakari juu ya hali niliyokuwa nayo wakati nilipofanya kiapo kwa Mungu. Machozi yaliyatia ukungu kuona kwangu na polepole nikaimba wimbo mmoja wa neno la Mungu:
Kwa hiari yangu mwenyewe mimi humfuata Mungu. Sijali kama Yeye ananitaka au la. Natafuta kumpenda Yeye, kwa udhabiti kumfuata Yeye. Nitampata Yeye, na kutoa maisha yangu Kwake.
I. Mapenzi ya Mungu yatimizwe. Moyo wangu utolewe kwa Mungu kikamilifu. Bila kujali Mungu anafanya nini au Anachonipangia, nitaendelea kufuata, nikitafuta kumpata Yeye. Kwa hiari yangu mwenyewe ninamfuata Mungu. Sijali kama Yeye ananitaka au la. Natafuta kumpenda Yeye, kwa udhabiti kumfuata Yeye. Mimi nitampata, na kutoa maisha yangu kwake.
II. Ukitamani kusimama na kutimiza mapenzi ya Mungu, ukitaka kumfuata Yeye mpaka mwisho, kuweka msingi imara, tenda ukweli katika vitu vyote. Hili humpendeza Mungu na Yeye ataimarisha upendo wako. Kwa hiari yangu mwenyewe mimi humfuata Mungu. Sijali kama Yeye ananitaka au la. Natafuta kumpenda Yeye, kwa udhabiti kumfuata Yeye. Nitampata Yeye, na kutoa maisha yangu Kwake.
III. Unapokabiliwa na majaribu, unahuzunika na kuteseka. Lakini, kwa ajili ya kumpenda Mungu, ungevumilia kila shida, kuacha maisha yako na kila kitu. Kwa hiari yangu mwenyewe mimi humfuata Mungu. Sijali kama Yeye ananitaka au la. Natafuta kumpenda Yeye, kwa udhabiti kumfuata Yeye. Nitampata Yeye, na kutoa maisha yangu Kwake. ("Sitapumzika Mpaka Nimpate Mungu" katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya)
Baada ya muda wa ibada za kiroho na urekebishaji, kwa haraka nilitoka nje ya uhasi wangu chini ya kunurishwa kwa Mungu na nikajirudisha kwenye safu za kutimiza wajibu wangu.
Hata kama miaka bora zaidi ya ujana wangu ilitumika gerezani; katika miaka hii saba na miezi minne nilipopitia shida kwa sababu ya imani yangu katika Mungu, sina malalamiko na sina majuto, kwa sababu ninaelewa ukweli fulani na nimepitia upendo wa Mungu. Nahisi kuwa kuna maana na thamani kwa mateso yangu; hili ni jambo la pekee la utukufu na neema ambazo Mungu alinitengenezea, hili ni pendeleo langu! Hata kama jamaa na marafiki zangu hawanielewi, na hata kama binti yangu hanijui, hakuna mtu, jambo au kitu kitakachoweza kunitenga na uhusiano wangu na Mungu; hata kama nikifa, siwezi kumwacha Mungu.
Upendo Safi Bila Dosari ndio wimbo niliopenda sana kuuimba gerezani; sasa, nataka kutumia matendo yangu halisi kutoa upendo safi zaidi kwa Mungu!
kutoka kwa Ushuhuda wa Washindi
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Vitabu.

Jumatano, 24 Oktoba 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Nguvu ya Maisha Ambayo Haiwezi Kuzimwa Kamwe

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki,

Kanisa la Mwenyezi Mungu | 2.Nguvu ya Maisha Ambayo Haiwezi Kuzimwa Kamwe

Dong Mei, Mkoa wa Henan
Mimi ni mtu wa kawaida. Niliishi maisha ya kawaida. Kama wengi wanaotamani sana mwanga, nilijaribu njia nyingi kutafuta maana ya kweli ya uwepo wa wanadamu, nikijaribu kuyapa maisha yangu umuhimu zaidi. Mwishowe, juhudi zangu zote zilikuwa bure. Lakini baada ya kuwa na bahati ya kutosha kukubali kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho, mabadiliko ya muujiza yalitokea katika maisha yangu. Yalileta rangi zaidi katika maisha yangu, na nilikuja kuelewa kwamba ni Mungu pekee ni Mtoa wa kweli wa roho na maisha ya wanadamu. Nilikuwa na furaha kwamba hatimaye nilikuwa nimepata njia sahihi ya maisha. Hata hivyo, huku nikitekeleza wajibu wangu wakati mmoja nilikamatwa kiharamu na kuteswa kikatili na serikali ya CCP. Kutoka kwa hili, safari ya maisha yangu ilipata uzoefu ambao kamwe sitasahau ...
Siku moja mnamo Desemba 2011 takribani saa moja asubuhi, mimi na kiongozi mwingine wa kanisa ulikuwa tukitekeleza hesabu ya mali ya kanisa wakati zaidi ya maafisa kumi wa polisi ghafla waliingia. Mmoja wa hawa polisi waovu alitukurupia na kusema kwa kelele: “Msisonge!” Baada ya kuona kilichokuwa kikitokea, kichwa changu kilishtuka. Kisha, polisi waovu walituchungquza kama magaidi waliokuwa wakitekeleza wizi. Pia walipekua kila chumba, walivigeuza shelabela kwa haraka sana. Mwishowe, walipata mali fulani ya kanisa, kadi tatu za benki, risiti za kuweka pesa, kompyuta, simu za rununu, na kadhalika. Waliyachukua yote ngawira, na kisha walituchukua sisi wanne kwa kituo cha polisi.
Alasiri, polisi waovu waliwaleta ndani dada wengine watatu ambao walikuwa wamewakamata. Walitufungia sisi saba katika chumba na hawakuacha tuzungumze, wala hawakuturuhusu tulale usiku ulipofika. Baada ya kuona dada wakifungiwa ndani na mimi, na kufikiri kuhusu ni kiasi gani cha pesa ambacho kanisa lilipoteza, nilikuwa nimezuzuliwa na wasiwasi. Yote ambayo ningefanya ni kuomba kwa dharura kwa Mungu: Ee Mungu! Huku nikikabiliwa na hali ya aina hii, sijui la kufanya. Tafadhali linda moyo wangu na kuufanya mtulivu. Baada ya kuomba, nilifikiri maneno ya Mungu: “Usiogope, mambo kama haya yanapofanyika katika kanisa, yote yanaruhusiwa na Mimi. Simama na kuwa sauti Yangu. Kuwa na imani kwamba mambo na vitu vyote vinaruhusiwa na kiti Changu cha enzi na vyote vina nia zangu ndani yavyo” (Matamshi na Ushuhuda wa Kristo Mwanzoni). “Unapaswa kujua kwamba vitu vyote katika mazingira yaliyokuzunguka yako hapo kwa ruhusa Yangu, Napanga yote. Ona kwa dhahiri na kuridhisha moyo Wangu katika mazingira ambayo Nimekupa” (Matamshi na Ushuhuda wa Kristo Mwanzoni). Maneno ya Mungu yalizima hofu kubwa moyoni mwangu. Nilitambua kwamba, leo, hii hali imenipata kwa ruhusa ya Mungu, na kwamba wakati ulikuwa umewadia ambapo Mungu alitaka nimshuhudie. Baada ya kuelewa mapenzi ya Mungu, nilimwomba Mungu na kusema: “Ee Mungu! Nataka kutii utaratibu na mipango Yako na kusimama imara katika ushuhuda Kwako—lakini mimi ni wa kimo kidogo, na naomba kwamba Unipe imani na nguvu, na kunilinda katika kusimama imara.”
Asubuhi iliyofuata, walitutenga na kutuhoji. “Najua wewe ni kiongozi wa kanisa. Tumekuwa tukiwafuatia ninyi watu kwa miezi mitano,” alisema mmoja wa polisi waovu kwa maringo. Nilipomsikia akieleza kwa utondoti kila kitu ambacho walikuwa wamefanya kunifuatia, nilitetemeka kwaa woga. Katika akili yangu, nilifikiri, Polisi waovu kweli waliweka matayarisho mengi katika kutukamata. Kwa kuwa tayari wanajua mimi ni kiongozi wa kanisa, hakuna jinsi wataniacha niende. Mara moja niliweka azimio langu mbele ya Mungu: Afadhali nife badala ya kumsaliti Mungu na kuwa Yuda. Baada ya kuona kuwa kuhoji kwao hakukuwa kunazaa matunda yoyote, walimpa mtu kazi ya kunitazama na kutoniacha nilale.
Katika siku ya tatu ya mahojiano, mkuu wa polisi waovu aliwasha kompyuta na kunifanya nisome taarifa zilizomsingizia Mungu. Kwa kuona kwamba sikuguswa, baada ya hapo alinihoji kwa makini kuhusu fedha za kanisa. Niligeuza kichwa changu kwa upande mmoja na kumpuuza. Hili lilimfanya kukasirika sana na alianza kutukana. “Haijalishi usiposema lolote—tunaweza kukuzuia bila mwisho, na kukutesa wakati wowote ule tunaotaka,” alinitisha kwa ukali. Katikati ya usiku huo, polisi walianza mateso yao. Walivuta mkono wangu mmoja nyuma ya bega langu na mwingine juu kutoka kwa mgongo wangu. Walifinya mgongo wangu na miguu yao, kwa nguvu walitia pingu vifundo pamoja. Ilikuwa uchungu sana kiasi kwamba nilipiga yowe kwa maumivu—mifupa na nyama katika mabega yangu zilihizi kana kwamba zingepasuka. Ningeweza tu kupiga magoti bila kusonga na kichwa changu kikiwa sakafuni. Nilifikiri mayowe yangu yangewafanya watulize makali kwangu, lakini badala yake waliweka kikombe cha chai kati ya pingu na mgongo wangu, jambo ambalo lilizidisha tena maumivu. Mifupa katika mwili wangu wa juu ilihisi kana kwamba ilikuwa imevunjwa nusu. Nilihisi uchungu sana hivi kwamba sikuthubutu kupumua nje na jasho baridi ilitiririka usoni pangu. Punde tu nilipohisi kwamba singevumilia uchungu tena, mmoja wa polisi waovu alichukua fursa hii kuniambia: “Tupe tu jina na tutakuachilia uende mara moja.” Wakati huo, nilimwita Mungu aulinde moyo wangu. Mara moja nilifikiri maneno ya wimbo wa uzoefu wa maisha: “Mungu mwenye mwili hupitia maumivu. Je, mimi, mtu huyu mpotovu, napaswa kuteseka kiasi gani zaidi? Nikikubali ushawishi wa giza, nawezaje kukutana na Mungu? ...Afadhali nivumilie taabu zote, na kufidia huzuni kubwa ya Mungu” (“Kusubiri Habari Njema Kutoka kwa Mungu” katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Wimbo ulinipa nguvu. Ndiyo—Mungu mwenye mwili amepitia uchungu huo wote kwa ajili ya wokovu wetu, nami, mtu huyu aliyepotoshwa kwa kina na Shetani, lazima niteseke hata zaidi. Iwapo ningekubali kushindwa na Shetani kwa sababu singeweza kuvumilia uchungu, ningewezaje kukabiliana na Mungu wakati wowote tena? Kufikiri hili kulinipa nguvu, na nikakua mgumu mara nyingine tena. Polisi waovu walinitesa kwa takriban saa moja. Walipoondoa pingu, mwili wangu mzima ulianguka bila nguvu sakafuni. “Usipoongea tutafanya hilo tena!” walinipigia kelele. Niliwatazama na kutosema chochote. Moyo wangu ulijawa na chuki kwa polisi hawa waovu. Mmoja wa polisi waovu alisonga mbele kutia pingu tena. Huku nikifikiri uchungu mkali sana ambao nilikuwa nimeupita karibuni, niliendelea kumwomba Mungu moyoni mwangu. Kwa mshangao wangu, alipojaribu kuvuta mikono yangu nyuma ya mgongo wangu hangeweza kuisogeza. Haikuwa uchungu sana, pia. Alikuwa akijaribu kwa nguvu sana hivi kwamba kichwa chake chote kilikuwa kimejaa jasho—lakini bado hangeweza kutia pingu. “Una nguvu mwingi!” alitweta kwa hasira. Nilijua kwamba huyu alikuwa Mungu akinijali, kwamba Mungu alikuwa akinipa nguvu. Shukrani iwe kwa Mungu!
Kufika alfajiri kulikuwa vigumu. Bado nilikuwa na kiwewe nilipofikiri nyuma jinsi polisi waovu walikuwa wamenitesa. Pia walinitisha, wakiniambia kwamba iwapo singesema chochote, wangelazimika kunipeleka ndani sana ya milimani na kuniua. Baadaye, walipokamata waumini wengine, wangesema nililisaliti kanisa—wangechafua jina langu, na kuwafanya ndugu wengine wa kanisa wanichukie na kunikana. Kufikiri hilo, moyo wangu ulizidiwa na mawimbi ya majonzi na kutojiweza. Nilijipata nikihisi mwoga na mnyonge. Akilini mwangu nilifikiri: Afadhali nife. Kwa njia hiyo sitakuwa Yuda na kumsaliti Mungu, wala sitakanwa na ndugu zangu. Pia nitaepuka uchungu wa mateso ya mwili. Kwa hivyo nilingoja hadi wakati ambapo polisi waovu waliokuwa wakinilinda hawakuwa wakitia makini na kuupiga kichwa changu kwa nguvu sana dhidi ya ukuta—lakini yote yaliyotokea ilikuwa kwamba kichwa changu kiliona kizunguzungu, sikufa. Wakati huo, maneno ya Mungu yalinipa nuru kutoka ndani: “katika siku hizi za mwisho lazima muwe na ushuhuda kwa Mungu. Haijalishi mateso yenu ni makubwa vipi, mnapaswa kuendelea hadi mwisho kabisa, na hata wakati wa pumzi yenu ya mwisho, bado lazima muwe waaminifu kwa Mungu, na kwa rehema ya Mungu; huku pekee ndiko kumpenda Mungu kweli, na huu pekee ndio ushuhuda thabiti na mkubwa sana” (Kutoka kwa “Ni kwa Kupitia tu Majaribio ya Kuumiza Ndiyo Mnaweza Kujua Kupendeza kwa Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili). “Wengine wanapokuelewa vibaya, unaweza kumwomba Mungu na kusema: ‘Ee Mungu! Siombi kwamba wengine wanivumilie, wala kwamba wanisamehe. Naomba tu kwamba niweze kukupenda moyoni mwangu, kwamba niwe na uhakika moyoni mwangu, na kwamba dhamiri yangu ni safi. Siombi kwamba wengine wanisifu, au kuniheshimu, ninatafuta tu kukuridhisha kutoka moyoni mwangu’” (Kutoka kwa “Ni kwa Kupitia Usafishaji tu Ndiyo Mwanadamu Anaweza Kumpenda Mungu kwa Kweli” katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mungu yaliondoa huzuni kutoka kwa moyo wangu. Ndiyo—Mungu huwataka watu wenye azimio, watu ambao wanaweza kumshuhudia Mungu mbele ya Shetani, watu ambao wanaweza kustahimili hadi mwisho kabisa na kufuata mipango yote ya Mungu bila kujali jinsi taabu wanayopitia ilivyo kubwa. Hata zaidi, Mungu huona mioyo ya ndani kabisa ya watu. Iwapo polisi wakinisingizia, hata kama ndugu wengine kwa kweli wanielewe visivyo na kunikataa kwa sababu hawajui kile kilichotendeka kwa kweli, naamini kwamba nia za Mungu ni nzuri; Mungu anajaribu imani na upendo wangu Kwake, na napaswa kufuatilia kumfanya Mungu kuridhika. Baada ya kubaini njama janja za Shetani, ghafla nilihisi mwenye fedheha na aibu. Niliona kwamba imani yangu kwa Mungu ilikuwa ndogo sana. Sikuwa nimeweza kusimama imara baada ya kupitia uchungu kidogo, na nilikuwa nimefikiri kutoroka na kuepuke mipango ya Mungu kupitia kifo. Watu wanapomwacha Mungu, wanaishi katika giza. Lengo la polisi waovu katika kuzungumza maneno haya ya tishio lilikuwa kunifanya nimkane Mungu. Na isingekuwa ulinzi wa Mungu, ningedanganywa na njama zao janja. Nilipokuwa nikitafakari maneno ya Mungu, moyo wangu ulijawa na mwanga. Sikutaka tena kufa, ila kuishi maisha mazuri, na kutumia kile ambacho kweli niliishi kwa kudhihirisha kumshuhudia Mungu na kumletea Shetani aibu.
Polisi hao wawili waovu waliopewa kazi ya kunilinda waliuliza mbona nilikuwa nimegongesha kichwa changu dhidi ya ukuta. Nilisema kwa sababu polisi hao wengine walikuwa wamenipiga. “Kimsingi tunafanya kazi kupitia elimu. Usijali—sitawaacha wakupige tena,” mmoja wao alisema kwa tabasamu. Baada ya kusikia maneno yake ya faraja, nilifikiri: Hawa watu wawili si wabaya; tangu nikamatwe wamekuwa wazuri kabisa kwangu. Kwa hilo, nililegeza tahadhari yangu. Lakini wakati huo, maneno ya Mungu yalikuja ghafla moyoni mwangu: “Nyakati zote, watu Wangu wanapaswa kujihadhari dhidi ya hila danganyifu za Shetani, walinde lango la nyumba Yangu kwa ajili Yangu, … kitu ambacho kitawazuia kuingia katika mtego wa Shetani, wakati mtakapokuwa na majuto ya kuchelewa sana” (“Tamko la Tatu” la Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mungu yalinipa kumbusho la wakati wa kufaa, yakinionyesha kwamba njama janja za ibilisi ni nyingi, na napaswa kuwa hadhari dhidi ya ibilisi hawa wakati wote. Sikutarajia hata kidogo kwamba punde wangefichua tabia zao halisi. Mmoja wa polisi waovu alianza kumkashifu Mungu, huku mwingine aliketi chini kando yangu alinipapasa mguu wangu, akinitazama kwa jicho la husuda na kuuliza kuhusu fedha za kanisa. Jioni, alipoona kwamba nilikuwa nikisinzia, alianza kupapasa kifua changu. Baada ya kuona kwamba walikuwa wamefichua tabia yao halisi, nilijawa na hasira. Ni sasa tu nilipoona waliodhaniwa polisi wa watu walikuwa tu wahuni na wadhalimu. Haya yalikuwa mambo mabaya yenye kustahili dharau, ambayo wangeweza kufanya. Kama matokeo, niliweza tu kumwomba Mungu kwa dharura ili anilinde kutokana na madhara yao.
Katika siku kadhaa zilizofuata, polisi waovu hawakunihoji tu kwa makini kuhusu kanisa, lakini pia walichukua zamu kunitazama ili kwamba nisilale. Baadaye, walipoona jinsi sikuwa nimewapa chochote, polisi hao wawili waovu waliokuwa wakinihoji walizidi kwa ghadhabu. Mmoja wao alinishambulia vikali, akinizaba kofi usoni, akinipiga kwa vishindo mara kadhaa. Uso wangu uliwasha, ulianza kuvimba, na mwishowe ukawa wenye ganzi sana kiasi kwamba singehisi chochote. Kwa sababu maswali yao hayakuwa yamezaa matunda yoyote kutoka kwangu, jioni moja mkuu wa polisi waovu alinipigia unyende na kusema, “Unahitaji kuanza kufungua mdomo wako. Unajaribu subira yangu—siamini kwamba hakuna chochote tunaweza kufanya na wewe. Nimekutana na watu wengi wagumu zaidi kukuliko. Tusipokuwa wakali kwako, hutatii katu!!” Alitoa amri na polisi waovu kadhaa walianza kunitesa. Jioni, chumba cha mahojiano kilikuwa cha huzuni na cha kuogofya—nilihisi kana kwamba nilikuwa jahanamu. Walinifanya nichutame sakafuni na kufunga mikono yangu katikati ya magoti na miguu yangu. Kisha, waliingiza kifimbo cha mbao katikati ya mapindi ya mikono yangu na nyuma ya magoti yangu, wakilazimisha mwili wangu wote kupinda juu. Kisha walikiinua kifimbo na kukiweka katikati ya meza mbili, wakiuacha mwili wangu wote ukining’inia hewani na kichwa changu kikiwa juu chini. Punde waliponiinua juu, kichwa changu kilipata kizunguzungu na niliona vigumu kupumua. Ilihisi kana kwamba nilikuwa nikisongwa. Kwa sababu nilikuwa nilining’inishwa hewani juu chini uzito wangu wote ulikuwa ukiangukia vifundo vyangu. Mwanzoni, ili kukomesha pingu kuukata mwili wangu, nilifumbata mikono yangu pamoja kwa kukaza, nikaupinda mwili wangu, na kujaribu kwa nguvu kadiri nilivyoweza kubaki katika hali hiyo. Lakini nguvu yangu ilipungua polepole. Mikono yangu iliteleza kutoka kwa vifundo vya miguu hadi kwa magoti yangu, na pingu ilikata kwa kina katika mwili wangu, ikiniacha na uchungu mkubwa sana. Baada ya kuning’inia hivi kwa takribani nusu saa, ilihisi kana kwamba damu yote katika mwili wangu ilikuwa imejikusanya kichwani mwangu. Uvimbe mchungu katika kichwa changu na macho ulifanya yahisi kana kwamba yalikuwa karibu kulipuka. Makato ya kina yalikuwa yamechimbwa katika vifundo vyangu, na mikono yangu ilikuwa imevimba sana kiasi kwamba ilionekana kama mikate miwili. Nilihisi nilikuwa ukingoni mwa kifo. “Siwezi kuvumilia tena, niweke chini!” nilipaza sauti kwa kukata tamaa. “Hakuna anayeweza kukuokoa ila wewe mwenyewe. Tuambie tu jina na tutakuacha uteremke chini,” alisema mmoja wa polisi waovu kwa ukali. Mwishowe, waliona kwa kweli nilikuwa katika taabu na waliniweka chini. Walinilisha glukosi kiasi na kuanza kunihoji tena. Nililala bila nguvu kama matope ardhini, macho yangu yakifumbwa kwa kukaza, nikiwa siwatilii makini. Bila kutarajia, polisi waovu waliniinua hewani tena. Bila nguvu ya kushikilia kwa mikono yangu, sikuwa na lingine ila kuacha pingu ijitie ndani katika vifundo vyangu, makali yaliyochongoka yakikata mwili wangu. Wakati huo, ilikuwa uchungu sana nilitoa yowe la kuhuzunisha sana. Sikuwa na nguvu ya kuendelea kupigana na kupumua kwangu kulikuwa kumekua kwa kina kifupi sana. Ilionekana kana kwamba wakati ulikuwa umesimama. Nilihisi kwamba nilikuwa nikiyumbayumba ukingoni mwa kifo. Nilipofikiri kwamba wakati huu kweli ningekufa, nilitaka kumwambia Mungu maneno yaliyokuwa moyoni mwangu kabla ya maisha yangu kuisha: “Ee Mungu! Wakati huu, ambapo kweli niko ukingoni mwa kifo, nahisi woga— lakini hata kama kweli nikifa leo, bado nitasifu haki Yako. Ee Mungu! Katika safari yangu fupi ya maisha, nakushukuru kwa kunichagua nirudi nyumbani kutoka kwa dunia hii ya dhambi, kunizuia kuzurura, nikiwa nimepotea, na kuniruhusu kuishi milele katika kumbatio Lako kunjufu. Ee Mungu, nimefurahia upendo Wako sana—na ilhali sasa tu, wakati maisha yangu yako karibu kuisha, ndipo nagundua kwamba sijatunza upendo Wako. Nyakati nyingi nimekufanya kuwa na huzuni na masikitiko; mimi ni kama mtoto mjinga anayejua tu kufurahia upendo wa mama yake, ilhali hajawahi kufikiria kuulipiza. Sasa tu ambapo niko karibu kupoteza maisha yangu ndipo naelewa kwamba ni lazima nitunze upendo Wako, na ni sasa tu ndipo najuta kukosa nyakati nyingi nzuri. Sasa, ninachojuta zaidi ni kwamba sijaweza kukufanyia lolote na unanidai mengi sana, na kama bado naweza kuishi, kwa hakika nitafanya kila niwezalo kutekeleza wajibu wangu, kufidia kile Unachonidai. Wakati huu, naomba tu kwamba Unipe nguvu, kuniruhusu kutowahi tena kuogopa kifo, na kuwa mwenye nguvu katika kile ninachokabili....” Tone baada ya tone la machozi lilianguka kutoka kwa paji la uso wangu. Usiku ulikuwa kimya kiasi cha kuogofya. Sauti ya pekee ilikuwa saa kubwa ikipiga ta-ta, kana kwamba kuhesabu sekunde ambazo zilisalia za maisha yangu. Hapo ndipo kitu cha muujiza kilifanyika: Nilihisi kana kwamba mwanga wa jua wa vuguvugu ulikuwa ukiniangazia, na polepole niliacha kuhisi uchungu mwilini mwangu. Maneno ya Mungu nguruma akilini mwangu: “Tangu unapoingia katika dunia hii ukilia, unaanza kutekeleza wajibu wako. Unachukua jukumu lako katika mpango wa Mungu na katika utaratibu wa Mungu. Unaanza safari ya maisha. Licha ya asili yako na licha ya safari iliyoko mbele yako, hakuna kitakachoepuka mpango na utaratibu ambao mbingu imeweka, na hakuna aliye na udhibiti wa hatima yake, kwa maana Anayetawala juu ya kila kitu ndiye tu Aliye na uwezo wa kazi hiyo” (Kutoka kwa “Mungu Ndiye Chanzo cha Uhai wa Mwanadamu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Ndiyo—Mungu ndiye chanzo cha maisha yangu, Mungu hutawala kudura yangu, na lazima nijiachilie mikononi mwa Mungu na kujiweka katika matumizi Yake. Kutafakari maneno ya Mungu kulinipa hisia ya kufurahisha, tulivu moyoni mwangu, kana kwamba nilikuwa nikijinyoosha katika kumbatio kunjufu la Mungu. Nilijipata nikilala. Wakiwa na woga kwamba ningekufa, polisi waovu waliniweka chini na kwa haraka walinipa glukosi kiasi na maji. Katika kukaribia kwangu kifo, nilikuwa nimetazama matendo ya muujiza ya Mungu.
Siku iliyofuata, polisi waovu walishinda jioni nzima wakiniinua juu tena na tena. Walinihoji kuhusu mahali ambapo pesa za risiti ambazo walikuwa wamechukua ngariwa zilikuwa. Wakati huo wote, sikusema chochote—ilhali bado hawakukata tamaa. Ili kupata pesa za kanisa, walitumia kila njia yenye kustahili dharau kunitesa. Wakati huo, maneno ya Mungu yalirudia rudia moyoni mwangu: “Maelfu ya miaka ya chuki ikiwa imejaa kifuani, milenia ya dhambi imeandikwa katika moyo–inawezekanaje hii isichochee chuki? Kumlipiza Mungu, kuuondoa kabisa uadui wake, usimwache kutangatanga tena, na usimruhusu kufanya fujo zaidi kama anavyotaka! Sasa ndio wakati: Mwanadamu ana muda mrefu tangu akusanye nguvu zake zote, amejitolea nguvu zake zote, amelipa kila gharama, kwa hili, kuchana uso uliojificha wa pepo hili na kuwafanya watu, ambao wamepofushwa na kuvumilia kila aina ya mateso na taabu, kuinuka kutoka katika maumivu na kurudi kwa Shetani huyu wa zamani” (Kutoka kwa “Kazi na Kuingia (8)” katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mungu yalinipa nguvu na imani kubwa. Ningepigana hadi kufa na Shetani, na hata kama ningekufa, ningesimama imara katika ushuhuda wangu kwa Mungu. Nikitiwa msukumo na maneno ya Mungu, bila kujua nilisahau uchungu. Kwa njia hii, kila wakati waliniinua juu, maneno ya Mungu yalinitia msukumo na kunipa motisha, na hivyo kadiri walivyonibeba juu mara nyingi, ndivyo nilivyoweza kubaini asili yao zaidi—ambayo ilikuwa ya ibilisi waovu—na ndivyo azimio langu kusimama imara katika ushuhuda wangu na kumridhisha Mungu lilivyokuwa kubwa zaidi. Mwishowe, wote walichoshwa na mimi. “Watu wengi sana hawawezi kuvumilia kutundikwa hivi kwa nusu saa, lakini amevumilia wakati huu wote—kwa kweli yeye ni sugu!” Niliwasikia wakitoa mawazo. Kwa kusikia maneno haya, nilijawa na msisimko. Akilini mwangu, nilifikiri: Mungu msaada wangu, huwezi kunivunja moyo. Mbali na mateso ya mwili, wakati wa siku na usiku zangu tisa katika kituo cha polisi polisi waovu pia walininyima usingizi. Kila wakati nilipofunga macho yangu na kuanza kusinzia, wangepiga vifimbo vyao dhidi ya meza, au sivyo wangenifanya nisimame na kukimbia huku na kule, au sivyo kunipigia kelele tu, wakijaribu kunihuzunisha na kuvunja akili yangu. Baada ya siku tisa, wakiona kwamba hawakuwa wamefikia lengo lao, polisi bado hawakukata tamaa. Walinipeleka katika hoteli, ambapo walitia pingu mikono yangu mbele ya miguu yangu, kisha wakaingiza kifimbo cha mbao katikati ya mapindi ya mikono na miguu yangu, nikilazimika kuketi mwili wangu ukiwa umepinda juu sakafuni. Walinifanya nibaki katika hali hii nikiketi sakafuni kwa siku kadhaa zilizofuata, ambayo ilisababisha pingu kuukata mwili wangu. Mikono na vifundo vyangu vilivimba na kubadilika rangi kuwa zambarau, na kikalio changu kilihisi uchungu sana sikuthubutu kukisugua ama kukishika; ilihisi kama nilikuwa nikikalia sindano. Siku moja, mmoja wa viongozi wa polisi waovu, akiona kwamba mahojiano yangu hayakuwa yamezaa matunda, alitembea kunifikia akiwa amekasirika sana na kunizaba kofi kwa nguvu usoni—kwa nguvu kiasi cha kutosha kulegeza meno yangu mbili.
Mwishowe, wakuu wawili kutoka kwa Idara ya Usalama wa Umma ya Mkoa walikuja. Punde walipowasili, waliondoa pingu, wakanisaidia kwenda kwa kochi, na kunipa kikombe cha maji. “Umekuwa na wakati mgumu kwa siku chache zilizopita—lakini usilitilie moyoni, walikuwa wakifuata tu amri,” walisema kwa unafiki. Unafiki wao ulinifanya niwachukie sana kiasi kwamba nilisaga meno yangu. Pia walijaribu kutumia Biblia kunileta upande wao, na kuwasha kompyuta na kunionyesha ushahidi usio kweli. Walisema maneno mengi ambayo yalishutumu na kufukuru dhidi ya Mungu. Moyoni mwangu, nilihisi kukasirishwa. Nilitaka kubishana nao, lakini nilijua kwamba kufanya hivyo kungewafanya tu kukufuru dhidi ya Mungu kwa wayowayo hata zaidi. Wakati huu, nilihisi kweli jinsi taabu aliyopitia Mungu mwenye mwili ilivyokuwa kubwa, na jinsi Mungu alivyovumilia fedheha nyingi kwa ajili ya kumwokoa mwanadamu. Kilicho zaidi, niliona uhafifu na kustahili dharau kwa ibilisi hawa waovu. Moyoni mwangu, kwa siri niliapa kwamba ningejiondoa kabisa kwa Shetani na milele kuwa mwaminifu kwa Mungu. Baadaye, bila kujali jinsi walivyojaribu kunidanganya, niliendelea kufunga mdomo wangu na sikusema chochote. Baada ya kuona kuwa maneno yao hayakuwa na athari yoyote, wakuu hao wawili waliondoka tu kwa hasira.
Katika kipindi cha siku na usiku kumi katika hoteli, waliendelea kunitia pingu, wakinifanya kuchuchumaa sakafuni nikishika miguu yangu. Nikikumbuka tangu nilipokamatwa, nilikuwa nimeishi siku na usiku kumi na tisa katika kituo cha polisi na hoteli. Ulinzi wa upendo wa Mungu ulikuwa umeniruhusu nilale kidogo, lakini polisi waovu hawakuwa wameniruhusu kulala wakati huo wote; ningefunga macho tu kwa muda na wangefanya chochote kilichohitajika kuniweka macho—kupiga meza, kunipiga teke kwa nguvu, kunipigia kelele, kuniamuru nikimbie huku na kule, na kadhalika. Kila wakati ningeshtuliwa, moyo wangu ungetwanga kifuani mwangu, na ningehisi woga sana. Hilo, likiongezwa kwa mateso ya mara kwa mara ya polisi waovu, na nguvu yangu iliishia kupunguka kabisa, mwili wangu wote ulikuwa umevimba na usiotulia, na niliona kila kitu vikiwa mbili mbili. Ningejua kulikuwa na watu mbele yangu wakiongea, lakini sauti ya milio yao ingeonekana kana kwamba ilikuwa ikitoka mbali sana. Zaidi ya hayo, mijibizo yangu ilianza kuwa ya polepole sana. Kwa mimi kustahimili hili kwa kiasi fulani kulikuwa yote kwa sababu ya nguvu kuu ya Mungu! Kama alivyosema Mungu: “Husababisha binadamu kuzaliwa upya, na kumwezesha kwa ushupavu kuishi kwa kila jukumu lake. Kwa sababu ya uwezo Wake, na nguvu ya maisha Yake yasiyopungua, binadamu ameishi kwa kizazi baada ya kizazi, ambapo nguvu ya uhai wa Mungu umekuwa uti wa mgongo wa kuwepo kwa binadamu…. Nguvu za Mungu za maisha zinaweza kutawala juu ya nguvu zozote; zaidi ya hayo, inazidi mamlaka yoyote. Maisha Yake ni ya milele, nguvu zake za ajabu, na nguvu Zake za maisha si rahisi kuzidiwa na kiumbe yeyote au nguvu za adui” (Kutoka kwa “Ni Kristo Wa Siku za Mwisho Pekee Ndiye Anayeweza Kumpa Mwanadamu Njia ya Uzima wa Milele” katika Neno Laonekana katika Mwili). Moyoni mwangu, nilitoa shukrani na sifa ya uaminifu kwa Mungu: Ee Mungu! Unatawala vitu vyote, matendo Yako ni yasiyokadirika, Wewe pekee ni mwenyezi, Wewe ni nguvu ya maisha isiyozimika, Wewe ni chemichemi ya maji hai kwa maisha yangu. Katika hali hii maalum, nimetazama nguvu Yako maalum na mamlaka. Mwishowe, polisi waovu hawakupata majibu kwa maswali yao kutoka kwangu, na walinituma hadi katika kituo cha kuzuia.
Njiani kuelekea katika kituo cha kuzuia, polisi wawili waliniambia: “Umefanya vizuri sana. Ninyi watu huenda mkawa katika kituo cha kuzuia, lakini ninyi ni watu wazuri. Kuna aina nyingi hapo: wauza madawa, wauaji, malaya—utaona utakapowasili.” “Kwa kuwa unajua sisi ni watu wazuri, mbona mnatukamata? Je, serikali haiongei kuhusu uhuru wa dini?” niliuliza. “Hiyo ni Chama cha Kikomunisti inawadanganya. Chama hicho hutupa riziki yetu, kwa hivyo lazima tufanye kinachosema. Hatuna chuki kwako ama kuwa na kitu chochote dhidi yako. Tulikukamata tu kwa sababu unamwamini Mungu,” mmoja wa polisi alisema. Baada ya kusikia hili, nilikumbuka kila kitu nilichokuwa nimepitia. Singeweza kuzuia kukumbuka maneno ya Mungu: “Uhuru wa dini? Haki halali na matakwa ya wananchi? Zote hizo ni njama za kufunika dhambi!” (Kutoka kwa “Kazi na Kuingia (8)” katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mungu yaliulenga kiini cha suala, yakiniruhusu kuona kwa kweli sura ya kweli ya serikali ya CCP na jinsi inavyojaribu kupata heshima ambayo haistahili; kwa juu juu, inapeperusha bendera ya uhuru wa dini, lakini kwa siri inakamata, kukandamiza, na kushambulia wale wanaomwamini Mungu pande zote za nchi na kupora pesa za kanisa—yote ambayo huweka wazi asili yake ya yenye dhambi ya kuchukiza, ya shetani.
Nikiwa katika kituo cha kuzuia, kulikuwa na nyakati ambapo nilikuwa dhaifu na katika maumivu. Lakini maneno ya Mungu yaliendelea kunipa moyo, kunipa nguvu na imani, kuniruhusu kuelewa kwamba ingawa Shetani alikuwa ameniondolea uhuru wa mwili, mateso yalikuwa yameniongeza, yakinifundisha kumtegemea Mungu wakati wa mateso ya hao ibilisi waovu, kuniruhusu kuelewa maana ya kweli ya ukweli mwingi, kuona thamani ya ukweli, na kuongeza azimio langu na motisha ya kufuatilia ukweli. Nilikuwa tayari kuendelea kumtii Mungu, na kupitia yote ambayo Mungu alikuwa amenipangia. Kama matokeo, nilipokuwa nikifanya kazi katika kituo cha kuzuia, niliimba nyimbo na kwa kimya nilifikiri kuhusu upendo wa Mungu. Nilihisi kwamba moyo wangu ulikuwa umekuja karibu na Mungu, na sikuona tena siku zikiwa chungu ama za kudhikisha sana.
Wakati wa kipindi hiki, polisi waovu walinihoji mara mingi zaidi. Nilimshukuru Mungu kwa kuniongoza katika kushinda mateso yao mara kwa mara tena. Baadaye polisi waovu waliondoa pesa zote kutoka kwa kadi zangu tatu za benki. Kutazama bila kujiweza peza za kanisa zikichukuliwa na polisi waovu kuliuvunja moyo wangu. Moyo wangu ulijawa na chuki kwa hili kundi lafi, ovu la ibilisi, na nilitamani sana ufalme wa Kristo kuwasili punde. Mwishowe, licha ya kutokuwa na ushahidi wowote, walinihukumu mwaka mmoja na miezi mitatu ya kuelimishwa tena kupitia kazi kwa ajili ya “kuvuruga utulivu wa umma.”
Baada ya kuteswa kikatili na serikali ya CCP, kwa kweli nilikuwa nimeonja upendo na wokovu wa Mungu kwangu, na nilikuja kufahamu ukuu na uweza wa Mungu na matendo Yake ya muujiza, nilikuwa nimeona mamlaka na nguvu ya maneno ya Mungu. Aidha kwa kweli nilikuwa nimemdharau Shetani. Katika kipindi hicho cha mateso, maneno ya Mungu yalikuwa yameandamana na mimi kupitia mchana na usiku za kudhikisha, maneno ya Mungu yalikuwa yameniruhusu kubaini njama janja za Shetani na kutoa ulinzi wa wakati wa kufaa. Maneno ya Mungu yalikuwa yamenifanya kuwa mwenye nguvu na ujasiri, yakiniruhusu kushinda mateso yao katili mara kwa mara tena. Maneno ya Mungu yalikuwa yamenipa nguvu na imani, yalikuwa yamenipa ujasiri wa kupigana na Shetani hadi mwisho kabisa.... Shukrani ziwe kwa Mungu! Mwenyezi Mungu ndiye ukweli, njia na uzima! Daima nitamfuata Mwenyezi Mungu hadi mwisho kabisa!
kutoka kwa Ushuhuda wa Washindi