Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Jumanne, 7 Mei 2019

Tofauti Kati Ya Kumfuata Mungu na Kuwafuata Watu

5. Tofauti Kati Ya Kumfuata Mungu na Kuwafuata Watu

Maneno Husika ya Mungu:
Kilicho na umuhimu mkuu katika kumfuata Mungu ni kwamba kila kitu kinapaswa kuwa kwa kadri ya maneno ya Mungu leo: Kama unafuatilia kuingia katika uzima au kutimiza mapenzi ya Mungu, kila kitu kinapaswa kulenga maneno ya Mungu leo. Kama kile ambacho unawasiliana kwa karibu na kufuatilia hakilengi maneno ya Mungu leo, basi wewe ni mgeni kwa maneno ya Mungu, na umeondolewa kabisa katika kazi ya Roho Mtakatifu. Kile ambacho Mungu hutaka ni watu ambao huzifuata nyayo Zake. Haijalishi vile ulichoelewa awali ni cha ajabu na safi, Mungu hakitaki, na kama huwezi kuweka kando vitu hivyo, basi vitakuwa kizuizi kikubwa mno kwa kuingia kwako katika siku za baadaye. Wale wote ambao wanaweza kufuata nuru ya sasa ya Roho Mtakatifu wamebarikiwa. Watu wa enzi zilizopita pia walifuata nyayo za Mungu, ilhali hawangeweza kufuata mpaka leo; hii ndiyo baraka ya watu wa siku za mwisho. Wale ambao wanaweza kufuata kazi ya sasa ya Roho Mtakatifu, na ambao wanaweza kuzifuata nyayo za Mungu, kiasi kwamba wamfuate Mungu popote Awaongozapo—hawa ni watu ambao wamebarikiwa na Mungu. Wale wasiofuata kazi ya sasa ya Roho Mtakatifu hawajaingia katika kazi ya maneno ya Mungu, na haijalishi wanafanya kazi kiasi gani, au mateso yao ni makubwa vipi, au wanakimbia hapa na pale kiasi gani, hakuna linalomaanisha chochote kwa Mungu kati ya hayo, na Yeye hatawasifu.

kutoka katika “Jua Kazi Mpya Zaidi ya Mungu na Fuata Nyayo za Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili

Watu wengi hawapati shangwe ndani ya ukweli, na vile vile katika hukumu. Badala yake, wao hupata furaha kwa nguvu na mali; watu kama hawa huchukuliwa kama wenye dharau. Wanatafuta tu madhehebu yaliyo na ushawishi duniani na wahubiri na waalimu wanaotoka katika seminari. Hata ingawa wameikubali njia ya ukweli, bado wako na shaka ndani yao na hawawezi kujitolea kikamilifu. Wanazungumzia kujinyima kwa sababu ya Mungu, lakini macho yao yamelenga tu wahubiri wakuu na waalimu, na Kristo anasukumwa pembeni. Mioyo yao imejaa umaarufu, mali na utukufu. Hawaamini kamwe kuwa mtu wa kawaida tu anaweza kuwashinda wengi vile, kwamba mtu asiye wa kutambulika kwa macho tu anaweza kukamilisha watu. Hawaamini kuwa hawa watu wasio na sifa, walio kwenye vumbi na vilima vya samadi ni watu waliochaguliwa na Mungu. Wanaamini kuwa kama watu wale wangekuwa vyombo vya wokovu Wake Mungu, basi mbingu na ardhi zitageuzwa juu na chini na watu wote watacheka kupindukia. Wanaamini kuwa iwapo Mungu atawachagua watu wasio na sifa yoyote wafanywe viumbe kamili, basi wao walio na sifa watakuwa Mungu Mwenyewe. Maoni yao yamechafuliwa na kutoamini; hakika, mbali na kutoamini, wao ni wanyama wasio na maana. Kwa maana wao wanathamini tu nyadhifa, hadhi kuu na mamlaka; wanachokithamini sana ni makundi makuu na madhehebu makuu. Hawana heshima hata kidogo kwa wale wanaoongozwa na Kristo; wao ni wasaliti tu waliomgeuka Kristo, kuugeuka ukweli na uhai.

Unachopendezwa nacho sio unyenyekevu wa Kristo, ila ni wale wachungaji wa uongo wenye umaarufu. Hupendi maarifa au kupendeza kwa Kristo, bali unapenda wale watukutu wanaojihusisha na ulimwengu mchafu. Unauchekelea uchungu wa Kristo asiyekuwa na pahali pa kulaza kichwa Chake, na badala yake unatamani maiti zinazokamata sadaka na kuishi katika uasherati. Hauko tayari kupokea mateso pamoja na Kristo, lakini unakimbilia mikononi mwa wapinzani wa Kristo hata ingawa wanakupa nyama za mwili pekee, barua na udhibiti pekee. Hata sasa, moyo wako bado unawaendea wao, sifa zao, hadhi zao, na ushawishi wao. Ilhali unazidi kuchukua mtazamo ambapo unaona kazi ya Kristo kuwa ngumu sana kukubali na huko tayari kuikubali. Hii ndiyo maana Ninasema hauna imani ya kumkubali Kristo. Sababu iliyokufanya Umfuate mpaka leo hii ni kuwa ulilazimishwa. Moyoni mwako milele mna picha nyingi refu; huwezi kusahau kila neno lao na matendo yao, au maneno yao ya ushawishi na mikono. Wao ni, katika moyo wenu, wakuu milele na tena mashujaa milele. Lakini hivi sivyo ilivyo na Kristo wa leo hii. Yeye moyoni mwako kamwe Hana umuhimu na kamwe Hastahili heshima. Kwa maana Yeye ni wa kawaida sana, mwenye ushawishi mdogo zaidi na Yuko mbali na ukuu.

kutoka katika “Je, Wewe Ni Muumini wa Kweli wa Mungu?” katika Neno Laonekana katika Mwili

Madondoo ya Mahubiri na Ushirika kwa ajili ya Marejeo:

Kumfuata Mungu humaanisha kumsikiliza Mungu katika kila kitu, kuitii mipango yote ya Mungu, kutenda kulingana na maneno ya Mungu, na kuyakubali yote yatokayo kwa Mungu. Kama unamwamini Mungu, basi unapaswa kumfuata Mungu; lakini, bila kulitambua, wakati wanapomwamini Mungu watu wengi huwafuata watu, ambalo ni jambo la mzaha na la kuhuzunisha. Kusema kwa kweli, yeyote watu wanayemfuata ni yule wanayemwamini. Ingawa watu wengine humwamini Mungu kwa jina tu, mioyoni mwao hakuna Mungu; katika mioyo yao, wao huwaabudu viongozi wao. Kuwasikiliza viongozi wa fulani, na kwenda hata kiasi cha kuikataa mipango ya Mungu, ni onyesho la kumwamini Mungu lakini kuwafuata watu. Kabla ya hawajapata ukweli, imani ya kila mtu imevurugika na kuchanganyikiwa kama hili. Wao hata hawajui kabisa maana ya kumfuata Mungu, na wanashindwa kusema tofauti kati ya kumfuata Mungu na kuwafuata watu. Wao huamini tu kwamba yeyote anayesema mafundisho mema, na ya juu, ni baba au mama yao; kwao, yeyote aliye na maziwa ni mama yao, na yeyote aliye na nguvu ni baba yao. Hivyo ndivyo jinsi wanavyosikitisha. Inaweza kusemwa kuwa, kwa hatua tofauti tofauti, hii ndiyo hali ya kiroho ya watu wengi.

Inamaanisha nini kumfuata Mungu? Na unawezaje kutia hilo katika vitendo? Kumfuata Mungu hakuhusishi tu kumwomba Mungu na kumsifu Mungu; kilicho muhimu zaidi ni kula na kunywa maneno ya Mungu na kuishi kulingana na maneno ya Mungu, kutenda kulingana na ukweli, kutafuta njia ya kupata uzoefu wa maisha katikati ya maneno ya Mungu, kukubali agizo la Mungu, kutekeleza kila moja ya wajibu wako vizuri, na kuitembea njia iliyo mbele yako kama unavyoongozwa na Roho Mtakatifu. Hasa, katika nyakati muhimu, wakati matatizo makuu yanapokufika, kuna hata haja kubwa zaidi ya kutafuta maana ya Mungu, kuwa na hadhari ya kudanganywa na mafundisho ya mwanadamu, na kutokuwa chini ya udhibiti wa mtu yeyote. “Kile kitokacho kwa Mungu mimi hukitii na kukifuata, lakini ikiwa kinatoka kwa mapenzi ya mwanadamu mimi hukikataa kwa uthabiti; wakati kile kinachohubiriwa na viongozi au wafanyakazi kina mgongano na mipango ya Mungu, basi mimi bila shaka humfuata Mungu na kuwakataa watu. Kama kina makubaliano kamili na mipango na mapenzi ya Mungu, basi naweza kukisikiliza.”

Inamaanisha nini kuwafuata watu? Kuwafuata watu inamaanisha mtu huwafuata wafanyakazi au viongozi anaowaabudu. Mungu hana nafasi kubwa katika mioyo yaomoyo wake; yeye hutundika kidokezo akisema anamwamini Mungu, na katika kila kitu anachofanya yeye ni kujifananisha na watu au kuwaiga. Hasa wakati ni jambo kuu, anawaacha watu kuamua, anawaacha watu waongoze jaala yao, yeye mwenyewe hatafuti maana ya Mungu, na anashindwa kutambua maneno yanayosemwa na watu. Mradi anachokisikia kinaonekana kuwa cha maana, basi bila kujali kama kinapatana na ukweli bado yeye hukikubali na kukisikiliza. Haya ni maonyesho ya kuwafuata watu. Imani ya watu kama hao katika Mungu haina kanuni, hakuna ukweli katika matendo yao, wao husikiliza mtu yeyote anayesema jambo la maana, na hata vijimungu vyao vikichukua njia mbaya, wao huvifuata mpaka mwisho. Mungu Akivilaani vijimungu vyao, basi watakuwa na dhana juu ya Mungu, na kushikilia kikiki vijimungu vyao. Sababu zao ni kwamba “tunapaswa kumsikiliza yeyote aliye na madaraka juu yetu; nguvu ya karibu ni bora kuliko nguvu ya juu.” Hii ni mantiki duni, upumbavu mtupu, lakini huo ndio upumbavu wa hao ambao huwafuata watu. Wale wanaowafuata watu hawana ukweli. Ni wale tu ambao humfuata Mungu wanaoamini kweli katika Mungu; Wale wanaowafuata watu huabudu sanamu, wamekuwa wakidanganywa na watu, na katika mioyo yao hakuna Mungu wala ukweli.

kutoka katika Ushirika kutoka kwa Aliye Juu

Watu wengi humwamini Mungu lakini hawajui ni nini maana ya kumtii Mungu, na hufikiri kwamba kuwasikiliza viongozi wao katika vitu vyote ni sawa na kumtii Mungu. Maoni kama haya ni ya upuuzi kabisa, kwa sababu chanzo cha utii wao si sahihi. Wao hudhukuru kuwasikiliza viongozi wao kuwa ni kumtii Mungu. Kumwamini Mungu kulingana na maoni haya ni kumwamini Mungu kwa jina tu; kwa uhakika, watu hawa huwaamini watu. …

Tunapomwamini Mungu, Mungu anapaswa kushikilia mahali pa kuongoza katika mioyo yetu, tunapaswa kusalimisha uongozi kwa Mungu katika mambo yote, tunapaswa kutafuta maana ya Mungu katika kila kitu, vitendo vyetu vinapaswa kulingana na maneno ya Mungu, na kwa mujibu wa mwongozo wa Roho Mtakatifu, na tunapaswa kutii yote yatokayo kwa Mungu. Ukiwasikiliza watu, basi hili linathibitisha kwamba Mungu hana mahali moyoni mwako, kwamba ni watu pekee walio na mahali katika moyo wako. Hakuna kilicho muhimu zaidi kwa watu kuliko kufuatilia ukweli na kuyaelewa mapenzi ya Mungu. Ikiwa huzingatii kuyatafuta malengo ya Mungu na kuyafahamu mapenzi ya Mungu, basi wako si utii wa kweli. Haijalishi ni sahihi jinsi gani wanavyosikika, ikiwa daima wewe huwasikiliza watu, basi kwa kiini wewe huwasikiliza watu–ambako si sawa na kumtii Mungu. Kwa kweli, kama wale wanaomwamini Mungu wanaweza kuelewa maana ya Mungu moja kwa moja kutoka kwa maneno Yake, ikiwa wanaweza kupata njia yao wenyewe ya kutenda katika maneno Yake, na huwasiliana ukweli kwa karibu, na kuuelewa ukweli, kwa maneno Yake, baada ya hayo wao waiweke katika vitendo, na ikiwa kwa wakati muhimu, wanaweza kuomba zaidi, na kutafuta uongozi wa Roho Mtakatifu, na kutii malengo ya Roho Mtakatifu, hivi kweli ni kumtii Mungu. Wale wanaomtii Mungu hutafuta njia katika maneno ya Mungu, matatizo yao hutatuliwa katika maneno ya Mungu, na wao hufanya kazi katikati ya uongozi wa Roho Mtakatifu; hivi kweli ni kumtii Mungu. Wale ambao husikiliza viongozi wao katika kila kitu wana hakika ya kupotea mbali na Mungu katika mioyo yao. Zaidi ya hayo, hawana amani mbele ya Mungu, sio wale wanaoishi mbele ya Mungu na kutafuta ukweli, hawana uhusiano na Mungu, na kanuni ya matendo yao ni kumsikiliza yeyote anayesema mambo halisi–mradi ni kiongozi, watatii. Vitendo kama hivyo ni vya dhihaka. Hawana ukweli wala uwezo wa kutofautisha, na wanaweza tu kudhibitisha kilicho sawa au kibaya kulingana na mawazo yao au akili, kwa hiyo jinsi gani wanaweza kujua kama kinafanana na ukweli? Kama wao huamini Mungu kulingana na maoni hayo, basi katika maisha yao yote hawatauelewa ukweli au kumjua Mungu. Aina hizo za imani zinaweza kusemwa kuwa kuamini katika ubongo wao wenyewe na kuitembea njia yao wenyewe, na hawana uhusiano na Mungu wa vitendo.

kutoka katika Ushirika kutoka kwa Aliye Juu

Jumatatu, 6 Mei 2019

Unawezaje Kutofautisha Kati ya Viongozi wa Kweli na wa Uongo, na Wachungaji wa Kweli na wa Uongo

6. Unawezaje Kutofautisha Kati ya Viongozi wa Kweli na wa Uongo, na Wachungaji wa Kweli na wa Uongo?

Maneno Husika ya Mungu:
Wale wasiofuata kazi ya sasa ya Roho Mtakatifu hawajaingia katika kazi ya maneno ya Mungu, na haijalishi wanafanya kazi kiasi gani, au mateso yao ni makubwa vipi, au wanakimbia hapa na pale kiasi gani, hakuna linalomaanisha chochote kwa Mungu kati ya hayo, na Yeye hatawasifu. Leo, wale wote ambao hufuata maneno halisi ya Mungu wako ndani ya mkondo wa Roho Mtakatifu; wale ambao ni wageni kwa maneno halisi ya Mungu wako nje ya mkondo wa Roho Mtakatifu, na watu hao hawasifiwi na Mungu. Huduma ambayo imetenganishwa na matamshi halisi ya Roho Mtakatifu ni huduma ambayo ni ya mwili, na ya dhana, na haiwezi kuwa kwa mujibu wa mapenzi ya Mungu. Kama watu huishi miongoni mwa dhana za kidini, basi hawawezi kufanya lolote lenye kustahili kwa mapenzi ya Mungu, na hata ingawa wao humhudumia Mungu, wao huhudumu katikati ya mawazo na dhana zao, na hawawezi kabisa kuhudumu kwa mujibu wa mapenzi ya Mungu. Wale ambao hawawezi kuifuata kazi ya Roho Mtakatifu hawaelewi mapenzi ya Mungu, na wale ambao hawaelewi mapenzi ya Mungu hawawezi kumhudumia Mungu. Mungu hutaka huduma inayoupendeza moyo Wake mwenyewe; Hataki huduma ambayo ni ya dhana na mwili. Kama watu hawawezi kuzifuata hatua za kazi ya Roho Mtakatifu, basi wao huishi katikati ya dhana, na huduma ya watu hao hukatiza na huvuruga. Huduma hiyo huenda kinyume na Mungu, na hivyo wale ambao hawawezi kuzifuata nyayo za Mungu hawawezi kumhudumia Mungu; wale ambao hawawezi kuzifuata nyayo za Mungu humpinga Mungu bila shaka, na ni wasioweza kulingana na Mungu. "Kuifuata kazi ya Roho Mtakatifu" kuna maana ya kufahamu mapenzi ya Mungu leo, kuweza kutenda kwa mujibu wa masharti ya sasa ya Mungu, kuweza kutii na kumfuata Mungu wa leo, na kuingia kwa mujibu wa matamshi mapya zaidi ya Mungu. Huyu pekee ndiye mtu ambaye hufuata kazi ya Roho Mtakatifu na yuko ndani ya mkondo wa Roho Mtakatifu. Watu hao hawawezi tu kupokea sifa za Mungu na kumwona Mungu, lakini wanaweza pia kujua tabia ya Mungu kutoka kwa kazi ya karibuni zaidi ya Mungu, na wanaweza kujua dhana na ukaidi wa mwanadamu, na asili na kiini cha mwanadamu, kutoka kwa kazi Yake ya karibuni zaidi; pia, wanaweza kutimiza polepole mabadiliko katika tabia yao wakati wa huduma yao. Ni watu kama hawa pekee ndio wanaoweza kumpata Mungu, na ambao wamepata kwa halisi njia ya kweli. Wale ambao huondoshwa na kazi ya Roho Mtakatifu ni watu wasioweza kufuata kazi ya karibuni zaidi ya Mungu, na ambao huasi dhidi ya kazi ya karibuni zaidi ya Mungu. Kwamba watu hao humpinga Mungu waziwazi ni kwa sababu Mungu amefanya kazi mpya, na kwa sababu picha ya Mungu si sawa na ile iliyo ndani ya dhana zao—kutokana na hilo wao humpinga Mungu waziwazi na kumhukumu Mungu, kusababisha wao kuchukiwa na kukataliwa na Mungu.
kutoka kwa "Jua Kazi Mpya Zaidi ya Mungu na Fuata Nyayo za Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Mwenyezi Mungu alisema, Je, si watu wengi humpinga Mungu na kuzuia kazi ya Roho Mtakatifu kwa sababu hawajui kazi mbalimbali na tofautitofauti ya Mungu, na, zaidi ya hayo, kwa sababu wanamiliki maarifa na mafundisho duni ya kupima kazi ya Roho Mtakatifu? Ingawa uzoefu wa watu kama hawa ni wa juujuu tu, ni wenye majivuno na wadekezi katika asili yao, na wanatazama kazi ya Roho Mtakatifu kwa dharau, wanapuuza masomo ya Roho Mtakatifu na, hata zaidi, wanatumia hoja zao ndogo ndogo zee kudhibitisha kazi ya Roho Mtakatifu. Pia wanajifanya, na wanashawishika kabisa na elimu yao na maarifa yao, na kuwa wanaweza kusafiri duniani kote. Je, watu hawa si ni wale wanaochukiwa na kukataliwa na Roho Mtakatifu na je, si wataondolewa na enzi mpya? Je, si wale wanaokuja mbele ya Mungu na kumpinga waziwazi ni watu wadogo wasioona mbali, wanaojaribu kuonyesha tu jinsi walivyo werevu? Kwa maarifa haba ya Biblia, wanajaribu kupotosha "wasomi" wa dunia, kwa mafundisho duni ya dini ili kuwafunza watu, wanajaribu kurudisha nyuma kazi ya Roho Mtakatifu, na kujaribu kuifanya ihusu mchakato wao wanavyofikiria, na kwa kuwa hawaoni mbali, wanajaribu kuona kwa mtazamo mmoja miaka 6,000 ya kazi ya Mungu. Je, watu hawa wana mantiki yoyote ya kuzungumzia? Kwa kweli, maarifa ya watu kumhusu Mungu yanavyozidi kuwa mengi, ndivyo wanavyokuwa wagumu wa kuhukumu kazi Yake. Zaidi ya hayo, wanazungumzia tu machache kuhusu maarifa yao ya kazi ya Mungu leo, lakini si wepesi wa kuhukumu. Kadri watu wanavyojua machache kumhusu Mungu, ndivyo wanavyozidi kuwa wenye majivuno na wenye kujiamini sana, na ndivyo wanavyozidi kutangaza nafsi ya Mungu kwa utundu—ilhali wanazungumzia tu nadharia, na wala hawapeani ushahidi wowote halisi. Watu kama hawa hawana thamani yoyote kabisa. Wale wanaoona kazi ya Roho Mtakatifu kama mchezo ni wenye upuzi! Wale wasio waangalifu wanapokumbana na kazi mpya ya Roho Mtakatifu, wanaopayuka, ni wepesi wa kuhukumu wanaoruhusu silika yao ya kiasili kukana haki ya kazi ya Roho Mtakatifu, na pia kuitusi na kuikufuru—je, watu hawa wasio na heshima si ni wale wasiojua kazi ya Roho Mtakatifu? Je, si wao ndio, zaidi ya hayo, wale wasiojua, wenye majivuno ya asili na wasioweza kutawalwa? Hata ikiwa siku itakuja ambapo watu hawa watakubali kazi mpya ya Roho Mtakatifu, bado Mungu hatawavumilia. Hawadharau tu wale wanaofanya kazi ya Mungu, bali pia wanamkufuru Mungu Mwenyewe. Watu kama hawa jasiri pasi na hadhari hawatasamehewa, katika enzi hii ama enzi itakayokuja na wataangamia kuzimuni milele! Watu kama hawa wasio na heshima, wenye kujifurahisha, wanajifanya kuwa wanamwamini Mungu, na kadiri wanavyozidi kufanya vile, ndivyo wanavyozidi kukosea amri za utawala wa Mungu. Je, si hao mafidhuli ambao kiasili hawazuiliki, na hawajawahi kumtii yeyote, wote hupitia njia hii? Je, si wao humpinga Mungu siku baada ya siku, Yeye ambaye daima huwa mpya na wala hazeeki?
kutoka kwa "Kujua Hatua Tatu za Kazi ya Mungu Ndiyo Njia ya Kumjua Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Mtu kama huyu daima anakuwa na uadui dhidi ya kazi mpya ya Mungu, haonyeshi nia ya kujisalimisha, na hajawahi kutii ama kujinyenyekea kwa furaha. Anajisifu mbele ya wengine na kamwe hajisalimishi kwa mwingine. Mbele ya Mungu, anajiona kuwa hodari zaidi kuhubiri neno na mwenye ujuzi zaidi kwa kufanya kazi kwa wengine. Kamwe hatupi hazina anazomiliki, lakini anazichukua kama vitu vinavyorithiwa kwa familia vya kuabudiwa, vya kuhubiriwa kwa wengine, na kutumiwa kuhutubia wale wapumbavu wanaomwabudu. Hakika kuna baadhi ya watu kama hawa kanisani. Inaweza kusemwa kwamba wao ni "mashujaa wasioshindwa," kizazi baada ya kizazi kinakaa kwa muda mfupi ndani ya nyumba ya Mungu. Wanafikiria kuhubiri neno (mafundisho ya dini) ni wajibu wao wa juu zaidi. Mwaka baada ya mwaka na kizazi baada ya kizazi, wanatekeleza kwa nguvu wajibu wao "mtakatifu na usiokiukwa". Hakuna anayethubutu kuwaguza na hakuna anayethubutu kuwapinga kwa uwazi. Walikuwa "mfalme" kwa nyumba ya Mungu, wakitenda kama dikteta kupitia enzi nyingi.
kutoka kwa "Wale Wanaomtii Mungu kwa Moyo wa Kweli Hakika Watakubaliwa na Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Unamhudumia Mungu na hulka yako ya kiasili, na kulingana na mapendeleo yako ya kibinafsi; na zaidi , unaendelea kufikiria kwamba Mungu anapenda chochote kile unachopenda, na kwamba Mungu anachukia chochote kile ambacho hupendi, na kazi yako inaongozwa kabisa na mapendeleo yako binafsi. Je, huku kunaweza kuitwa kumhudumia Mungu? Hatimaye tabia yako ya maisha haitabadilishwa hata chembe. Kwa hakika, utakuwa msumbufu zaidi kwa sababu umekuwa ukimhudumia Mungu, na itafanya tabia yako potovu kukita mizizi zaidi. Kwa njia hii, utaendeleza kwa ndani sheria kuhusu huduma kwa Mungu zitokanazo kimsingi na hulka yako binafsi, na uzoefu unaotokana na kuhudumu kwako kulingana na tabia yako binafsi. Hii ni uzoefu na mafunzo ya kibinadamu. Ni filosofia ya maisha ya binadamu. Watu kama hawa wanapatikana miongoni mwa Mafarisayo na wale wajumbe wa kidini.
kutoka kwa "Sitisha Huduma ya Kidini" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kazi katika akili ya mwanadamu inafikiwa kwa urahisi sana na mwanadamu. Wachungaji na viongozi katika ulimwengu wa kidini, kwa mfano, wanategemea karama zao na nafasi zao katika kufanya kazi zao. Watu wanaowafuata kwa muda mrefu wataambukizwa na karama zao na kuvutwa na vile walivyo. Wanalenga karama za watu, uwezo na maarifa ya watu, na wanamakinikia mambo ya kimiujiza na mafundisho mengi yasiyokuwa na uhalisi (kimsingi, haya mafundisho hayawezi kutekelezeka). Hawalengi mabadiliko ya tabia za watu, badala yake wanalenga kuwafundisha watu uwezo wao wa kuhubiri na kufanya kazi, kuboresha maarifa ya watu na mafundisho makuu ya kidini. Hawalengi kuona ni kwa kiasi gani tabia ya watu imebadilika au ni kwa kiasi gani watu wanauelewa ukweli. Wala hawajali utu wa watu, wala kujua hali za watu za kawaida na zisizo za kawaida. Hawapingi mitazamo ya watu au kufunua mitazamo yao, achilia mbali kurekebisha hali yao ya dhambi. Watu wengi wanaowafuata wanahudumia kwa karama zao za asili, na kile wanachokidhihirisha ni maarifa na ukweli wa kidini usioeleweka, ambayo ni nje ya mguso wa uhalisia na kuwapatia watu uzima. Kimsingi, kiini cha kazi yao ni kulea talanta, kumlea mtu kuwa mhitimu mwenye talanta aliyemaliza mafunzo ya kidini ambaye baadaye anakwenda kufanya kazi na kuongoza.
kutoka kwa "Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Unaweza kuzungumza maarifa mengi kama mchanga wa bahari, lakini hakuna yaliyo na njia ya kweli. Katika hili, je huwadanganyi watu? Je, wewe si mtu wa maneno matupu bila vitendo? Kutenda kwa namna hii ni hatari kwa watu! Kadri nadharia inavyokuwa ya juu, ndivyo inavyokosa uhalisia, na ndivyo inavyokosa uwezo wa kuwapeleka watu katika uhalisia; kadri nadharia inavyokuwa ya juu, ndivyo inavyokufanya kumuasi na kumpinga Mungu. Usizichukulie nadharia za kiwango cha juu kama hazina ya thamani; zina madhara, na hazina kazi yoyote! Pengine baadhi ya watu wanaweza kuzungumza juu ya nadharia za juu sana—lakini nadharia hizo hazina kitu chochote cha uhalisia, maana watu hawa hawajawa na uzoefu binafsi nazo, na kwa hiyo hawana njia ya kutenda. Watu kama hao hawawezi kumwongoza mwanadamu katika njia nzuri, na watawapotosha tu watu. Je, hii si hatari kwa watu? Kwa kiwango cha chini kabisa, unapaswa uweze kutatua shida za sasa na kuwaruhusu watu kupata kuingia; hii tu ndiyo inahesabika kama ibada, na baada ya hapo ndipo utakuwa na sifa za kufaa kumfanyia Mungu kazi. Siku zote usizungumze maneno mazuri, ya kibunifu, na usiwalazimishe watu kukutii wewe pamoja na vitendo vyako visivyofaa. Kufanya hivyo hakutaleta matokeo mazuri, na kutaongeza tu mkanganyiko wa watu. Kuwaongoza watu namna hii kutazalisha taratibu nyingi, ambazo zitafanya watu wakuchukie. Huu ndio udhaifu wa mwanadamu, na kwa kweli hauvumiliki.
kutoka kwa "Sisitiza Zaidi Kwa Uhalisia" katika Neno Laonekana katika Mwili
Maarifa yenu yanaweza kuwakimu watu kwa muda tu. Wakati unapoendelea, ukiendelea kusema kitu kile kile, watu kadhaa wataweza kutambua; watasema wewe ni mtu wa juu juu sana, aliyekosa kina sana. Hutakuwa na budi ila kujaribu kuwadanganya watu kwa kuongea mafundisho, na kama wewe daima huendelea hivi, wale walio chini yako watafuata namna yako, nyayo, na mfano wa kumwamini Mungu na kupitia, na watatia maneno na mafundisho hayo katika vitendo, na hatimaye, unapoongea katika njia hii, watakutumia kama mfano. Unachukua mwongozo kuongea mafundisho, na wale walio chini yako watajifunza mafundisho kutoka kwako, na vitu vinapoendelea utakuwa umechukua njia ambayo si sawa. Wale walio chini yako wanafuata njia yako … Tazama viongozi wa kila madhehebu na faraka. Wote ni wa kujigamba na kujisifu, na wanafafanua Biblia nje ya muktadha na kulingana na ubunifu wao wenyewe. Wote wanategemea zawadi na maarifa kufanya kazi yao. Kama hawangekuwa na uwezo wa kuhubiri chochote, wale watu wangewafuata? Wao, hata hivyo, wanamiliki ujuzi fulani, na wanaweza kuongea mafundisho kiasi, au wanajua jinsi ya kuwashawishi wengine na jinsi ya kutumia ustadi kadhaa, ambao kupitia kwake wamewaleta watu mbele yao wenyewe na kuwadanganya. Kwa jina, watu hao humwamini Mungu—lakini katika uhalisi wanafuata viongozi wao. Wakikutana na wale wanaohubiri njia ya kweli, baadhi yao wangesema, "Lazima tutafute ushauri kwake kuhusu imani yetu katika Mungu." Tazama jinsi wanavyohitaji ridhaa ya mtu ili kumwamini Mungu; hilo si tatizo? Viongozi hao wamekuwa nini, basi? Hawajakuwa Mafarisayo, wachungaji waongo, wapinga Kristo, na vikwazo kwa kukubali kwa watu njia ya kweli?
kutoka kwa "Ukimbizaji Ukweli Tu Ndiyo Imani ya Kweli katika Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kutoa kwenu "muhtasari kuhusu ukweli" hakufanywi ili kuwawezesha watu kupata maisha au kupata mabadiliko katika tabia zao kutoka kwa ukweli. Badala yake, kunafanywa ili watu waweze kuwa weledi wa maarifa na mafundisho fulani kutoka kwa ukweli. Wao huonekana kana kwamba wanaelewa lengo lililokusudiwa katika kazi ya Mungu, wakati kwa kweli wamekuwa weledi wa baadhi ya maneno ya mafundisho tu. Hawaelewi maana iliyokusudiwa ya ukweli, na si tofauti na kusomea theolojia au kusoma Biblia. Wewe unakusanya vitabu hivi au vifaa hivyo, na hivyo unapata umiliki wa kipengele hiki cha mafundisho au kipengele kile cha ujuzi. Wewe ni msemaji wa kiwango cha juu wa mafundisho—lakini huwaje unapomaliza kusema? Watu basi hawana uwezo wa kupitia, hawana ufahamu wa kazi ya Mungu na hawana ufahamu wao wenyewe pia. Mwishowe, vitu vyote watakavyokuwa wamepata ni fomyula na sheria … Kwa kuuliza swali baada ya swali kuhusu maneno hayo, kisha kujibu, kufanya muhtasari, unadhani kuwa wale walio chini wanaweza kuelewa kwa urahisi. Mbali na kuwa rahisi kukumbuka, wao wana uhakika juu ya maswali haya kwa tazamo la haraka, na unafikiri ni vizuri kufanya mambo kwa njia hii. Lakini kile wanachokielewa siyo maana iliyokusudiwa ya ukweli; inatofautiana na ukweli na ni maneno ya mafundisho tu. Hivyo ingekuwa bora zaidi kama wewe hungefanya mambo haya hata kidogo. Unafanya mambo haya kuwaongoza watu kuelewa ujuzi na weledi wa elimu. Wewe huwaleta wengine katika mafundisho, katika dini, na kuwafanya wamfuate Mungu na kumwamini Mungu ndani ya mafundisho ya dini. Je, si wewe ni sawa tu na Paulo? … Mwishowe wao wangeletwa mahali ambapo hawawezi kupata ukweli na hawawezi kupitia neno la Mungu, mahali ambapo wanaweza kujiandaa tu na kujadili mafundisho na ni mahali ambapo hawawezi kumwelewa Mungu. Yote ambayo wangeweza kuzungumza yangekuwa mafundisho yenye kupendeza, mafundisho sahihi, lakini hakungekuwa na uhalisi ndani yao na hawangekuwa na njia ya kutembelea. Aina hii ya kuongoza kweli hufanya madhara makubwa!
kutoka kwa "Bila Ukweli Ni Rahisi Kumkosea Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Watu wengine wanajihami tu na ukweli fulani kwa wakati wa dharura ama kujitelekeza wenyewe na kuwasaidia wengine, sio kutatua shida zao wenyewe; tunawaita "watu wasio na ubinafsi." Wanawaona wengine kama vikaragosi wa ukweli na wenyewe kama mabwana wa ukweli, wakiwafunza wengine kuushikilia ukweli na wasiwe wasiojihususha, ilhali wao wenyewe ni watazamaji kando kando mwa uwanja—hao ni watu wa aina gani? Wakiwa wamejihami na baadhi ya maneno ya ukweli ili kuwahubiria wengine tu, wakikosa kufanya chochote kujizuia kutokana na kuangamia kwao wenyewe—inasikitishaje! Kama maneno yao yanaweza kuwasaidia wengine, mbona wasijisaidie wenyewe? Tunafaa kuwaita wanafiki wasio na ukweli. Wanatoa maneno ya ukweli kwa wengine na kuwaambia wengine wayaweke katika matendo, lakini hawafanyi juhudi yoyote kuyatenda wenyewe—je sio wa kudharauliwa? Kwa hakika hawawezi kulifanya wenyewe, ilhali wanawalazimisha wengine kuweka maneno ya ukweli katika matendo—hii ni njia ya ukatili iliyoje! Hawatumii ukweli kuwasaidia wengine; hawawatolei wengine kwa moyo wa upendo wa mama; wanawadanyanya tu watu na kuwapotosha watu. Hili likiendelea—na kila mtu akipitisha maneno ya ukweli kwa anayefuata—je kila mmoja mwishowe hatakuwa na uelewa tu wa maandishi ya ukweli wakikosa uwezo wa kuyatenda?
kutoka kwa "Wale Wanaopenda Ukweli Wana Njia ya Kufuata" katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo
Wale wanaosoma Biblia kwa makanisa makubwa hukariri Biblia kila siku, lakini hakuna yeyote anayeelewa madhumuni ya kazi ya Mungu. Hakuna hata mmoja anayeweza kumwelewa Mungu; juu ya hayo, hakuna yeyote anayekubaliana na moyo wa Mungu. Wote hawana thamani, wanadamu wabovu, kila mmoja akisimama juu kumfundisha Mungu. Ingawa wanalionyesha hadharani jina la Mungu, wanampinga makusudi. Ingawa wanajiita waumini wa Mungu, wao ni wale wanaokula mwili na kunywa damu ya mwanadamu. Wanadamu wote kama hao ni mashetani wanaoteketeza nafsi ya mwanadamu, mapepo yanaowasumbua kimakusudi wanaojaribu kutembea katika njia iliyo sawa, na vizuizi vinavyozuia njia ya wanaomtafuta Mungu. Ingawa wenye "mwili imara," wafuasi wao watajuaje kwamba wao ni maadui wa Kristo wanaomwongoza mwanadamu katika upinzani kwa Mungu? Watajuaje kwamba hao ni mashetani hai wanaotafuta hasa nafsi za kuteketeza?
kutoka kwa "Wote Wasiomjua Mungu Ndio Wanaompinga Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Mbona Nasema wale walio katika dunia ya kidini hawaamini katika Mungu na ni waovu, walio sawa na ibilisi? Ninaposema ni watenda maovu, ni kwa sababu hawaelewi matakwa ya Mungu, wala kuona hekima Yake. Hakuna wakati ambao Mungu anadhihirisha kazi Yake kwao; ni vipofu, wasioona matendo ya Mungu. Wao ndio walioachwa na Mungu na hawamiliki kabisa utunzaji na ulinzi wa Mungu, sembuse kazi ya Roho Mtakatifu. Wale walio bila kazi ya Mungu ni watenda maovu na humpinga Mungu.
kutoka kwa "Wote Wasiomjua Mungu Ndio Wanaompinga Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Ushirika wa Mtu:
Wajibu wa wafanyakazi ni kutenda kazi yao na kuyaongoza makanisa kulingana na mapenzi ya Mungu na kwa mujibu wa mahitaji na mipango ya Mungu. Kazi kama hii hubarikiwa na Mungu. Ikiwa wafanyakazi hawana urazini kama huo, na hukiuka mapenzi ya Mungu kwa kufanya mambo kwa njia yao wenyewe, wakichukua nafasi ya mchungaji na kuwafundisha watu jinsi wanavyopenda, wakitoa dhana zao, mawazo, na mafundisho na kuwafanya wengine kuyakubali, basi wafanyakazi kama hawa wamekuwa wachungaji wa uongo. Kuna mifano mingi ya wafanyakazi kuwa wachungaji wa uongo, na idadi kubwa wameondoshwa na Mungu katika kila hatua ya kazi Yake. Mungu wakati mmoja Alisema kuwa katika kila enzi kuna watu wengi wanaomtumikia Mungu na bado pia humpinga, hata hatimaye huwafanya wengine wawatii na kuwaabudu kama wao ni Mungu. Hili ni dhihirisho la "wachungaji wa uongo." Sote tunapaswa kuchukua hili kama onyo; wafanyakazi wanapaswa kuzingatia mabadiliko katika tabia, na ikiwa watazembea na kutokuwa waangalifu kwa hili, basi ni rahisi mno kwao kuwa wachungaji wa uongo. Kazi ya wachungaji wa uongo ina mkazo maalum juu ya kuwaongoza watu kulingana na maana ya wachungaji wa uongo wenyewe. Yote wanayofanya, kusema, na kutafuta ni ya mpango wao wenyewe, na hulichukulia hili kama ukweli safi mno kuliko ukweli wote, na wao hudhani kuwa wanaweza kuwafundisha watu kuwa wanadamu na kuwaruhusu watu kupata ukweli kulingana na mpango wao wenyewe. Haya ni maonyesho ya kiburi cha juu kabisa na hali ya kujidai ya wachungaji wa uwongo. Kwa wale ambao kweli ni wa busara, wanapoamini kuwa wako sahihi hasa wangetafuta na kuwasiliana ukweli kwa karibu , na kutenga uangalifu wao kwa kusikia maoni na maarifa tofauti ya wengine ili kuthibitisha kama yote waliyoyaelewa ni sahihi. Wale wote ambao wamepitia kupogolewa na kushughulikiwa kwa Mungu wanapaswa kuweza kuweka kando baadhi ya hali zao za kujidai na majisifu. Wanapofanya kazi, wao ni waangalifu katika hatua zao ili kuepuka kukiuka mapenzi ya Mungu na kuchukua njia mbaya. Matokeo yao kuwa wachungaji wa uongo hayawezi kufikiriwa. Kila mfanyakazi ana matendo yake mwenyewe, wote wana nadharia zao wenyewe ambazo wao hutumia kunyunyizia watu; kwa kweli, hakuna yeyote anayeweza kufahamu kabisa ni kiasi gani cha ukweli au thamani njia yao wenyewe inacho. Watu wamekosa hali ya kujitambua, hawana bidii au tafakari ya kina sana katika maarifa yao ya ukweli, na wao huchukua kiholela vitu visivyo na maana na kuvichukulia kama hazina za kutolewa kwa wengine. Si matendo kama hayo yanaashiria mchungaji wa uwongo? Si hili linawadhuru wengine pamoja na wao wenyewe? Bila kujali ni kazi kiasi gani wachungaji wa uwongo hufanya, hawana uwezo kabisa wa kuwaleta watu mbele ya Mungu na kuwaruhusu wamjue na kumtii Mungu. Yote yanayofunguliwa na wachungaji wa uongo ni maneno na mafundisho tu, na mawazo na fikra, na hakuna kitu ambacho huzuia kazi ya Mungu au kumpinga Yeye zaidi.
kutoka kwa "Maana ya 'Wachungaji Kondoo wa Uongo'" katika Ushirikiano Kutoka kwa wa Juu
Huduma kulingana na mbinu za kidini inamaanisha kufanya kila kitu kulingana na njia za desturi za dini na utaratibu wa huduma, kuzingatia kwa imara sherehe mbalimbali za kidini, na kuwaongoza watu tu kulingana na maarifa ya Biblia. Kwa kuonekana, yaelekea kuwa yenye bidii na nguvu, inaashiria dini, inafaa barabara kwa mawazo ya watu, na hawana vipingamizi. Lakini haina kabisa kazi ya Roho Mtakatifu, kinachohubiriwa si kitu ila mafundisho ya kidini na elimu ya Biblia, imejaa mawazo ya kidini, haina chochote kuhusu upataji wa nuru ya Roho Mtakatifu, na mikutano imetuama na kukosa uhai. Kwa huduma kama hii, miaka inavyoendelea watu waliochaguliwa wa Mungu bado wanabaki bila ukweli, hawana maarifa ya Mungu au utii kwa Mungu, na hawajaingia kwenye njia sahihi ya imani kwa Mungu–kwa kuwa kile watu hufuatilia sio wokovu bali ni neema na baraka, kiasi kwamba hakuna dalili za mabadiliko katika tabia ya maisha yao. Baada ya kuhudumu kwa miaka kadhaa, hawa watu bado wako mikono mitupu, bila ushahidi wa kitu walichopata wenyewe. Haya ndiyo matokeo ya huduma kulingana na mbinu za kidini. Ni dhahiri kuwa, watu kama hawa wanaomtumikia Mungu hawajui kazi ya Mungu, hawaelewi mapenzi ya Mungu, na hawajui maana ya kushirikiana na kazi ya Roho Mtakatifu. Ni jambo dhahiri la vipofu wakiwaongoza vipofu, huwapotosha watu waliochaguliwa wa Mungu , kama Mafarisayo humwamini Mungu na bado humpinga Mungu, hawamjui Mungu, na kimsingi hawawezi kufanikisha wokovu wa Mungu.
kutoka kwa "Wale tu Wanaoingia Kwenye Njia Sahihi ya Imani katika Mungu Ndio Wanaweza Kuchukua njia Sahihi ya Huduma kwa Mungu" katika Kumbukumbu za Kihistoria za Ushirika na Mipangilio ya Kazi ya Kanisa (I)
Wachungaji wa jamii ya kidini hutumia kila fursa ya kutangaza kiwango cha maarifa yao na kutoa sura ya uchaji Mungu. Lengo lao ni kuwafanya watu wawastahi na kuwaabudu, na wao hutumia taswira yao wenyewe kuwavuta watu kwao ili wawatii na kuwafuata, matokeo yakiwa ni wao kuwaongoza watu kuabudu maarifa ya Biblia, kuabudu hadhi na nguvu, na kuabudu ustadi katika kuhubiri. Kwa njia hii, kwa kila hatua huwaongoza watu katika njia ya kumpinga Mungu. Wale wanaoongozwa na wapinga Kristo humwamini Mungu asiye yakini, wao ni wazuri kwa kuzungumzia mafundisho matupu na yasiyo na maana, na wenye ujuzi katika unafiki, na wao wote humwamini Mungu na bado humpinga na kumwasi Mungu. Hakuna shaka kwamba njia ambayo viongozi wa uongo na wapinga Kristo hufanyia kazi–ile ambayo wao hutumia kumtumikia Mungu na bado kumpinga Yeye–ni ya kuwadhuru watu sana.
kutoka kwa "Kulinda Dhidi ya Wapinga Kristo na Njia ya Wapinga Kristo Ni ya Umuhimu Mkuu" katika Kumbukumbu za Kihistoria za Ushirika na Mipangilio ya Kazi ya Kanisa (II)

Jumapili, 5 Mei 2019

Tofauti Kati Ya Matendo Mazuri ya Nje na Mabadiliko Katika Tabia

7. Tofauti Kati Ya Matendo Mazuri ya Nje na Mabadiliko Katika Tabia

Maneno Husika ya Mungu:
Mabadiliko katika tabia hasa huhusu mabadiliko katika asili ya watu. Mambo ya asili ya mtu hayawezi kuonekana kutoka kwa mienendo ya nje; yanahusisha moja kwa moja thamani na umuhimu wa kuwepo kwake. Yaani, yanahusisha moja kwa moja mitazamo ya mtu kuhusu maisha na maadili yake, mambo yaliyo ndani kabisa ya nafsi yake, na kiini chake. Mtu ambaye hawezi kukubali ukweli hatakuwa na mabadiliko katika hali hizi. Ni kwa kupitia kazi ya Mungu pekee, kuingia kikamilifu katika ukweli, kubadili maadili na mitazamo yake kuhusu kuwepo na maisha, kulinganisha msoni yake na ya Mungu, na kuwa na uwezo wa kutii na kujitoa kabisa kwa Mungu ndio tabia zake zinaweza kusemekana zimebadilika. Huenda ukaonekana kufanya juhudi fulani, unaweza ukawa thabiti unapokabiliwa na shida, huenda ukaweza kutekeleza utaratibu wa kazi kutoka walio juu, au huenda ukaweza kwenda popote unapoambiwa kwenda, lakini haya ni mabadiliko madogo tu katika mienendo yako, na hayatoshi kujumuisha mabadiliko katika tabia yako. Huenda ukaweza kukimbia katika njia nyingi, kuvumilia shida nyingi na kustahamili fedheha kuu; huenda ukajihisi karibu sana na Mungu, na Roho Mtakatifu anaweza kukufanyia kazi fulani. Hata hivyo, Mungu anapokuomba ufanye jambo fulani ambalo halipatani na fikira zako, huenda bado usitii, lakini utafute visababu, na kuasi na kumpinga Mungu, hata kufikia kiwango cha wewe kumhakiki Mungu na kumpinga Yeye. Hili ni tatizo kubwa! Hili linaonyesha kwamba bado una asili inayompinga Mungu na kwamba hujapitia mabadiliko yoyote kabisa.

kutoka katika “Unachopaswa Kujua Kuhusu Kuigeuza Tabia Yako” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Watu wanaweza kuwa na tabia nzuri, lakini hiyo haimaanishi kuwa wako na ukweli. Bidii ya watu inaweza tu kuwafanya wazingatie mafundisho na kufuata kanuni; watu wasio na ukweli hawana namna ya kutatua shida halisi, na mafundisho hayawezi kushikilia nafasi ya ukweli. Wale ambao wamepitia mabadiliko katika tabia zao ni tofauti. Wale ambao wamepitia mabadiliko katika tabia zao wameelewa ukweli, wanatambua masuala yote, wanajua jinsi ya kutenda kulingana na mapenzi ya Mungu, jinsi ya kutenda kulingana na kanuni za ukweli, jinsi ya kutenda ili kumridhisha Mungu, nao wanaelewa asili ya upotovu wanaoufichua. Mawazo na dhana zao wenyewe vinapofichuliwa, wanaweza kutambua na kuunyima mwili. Hivi ndivyo mabadiliko katika tabia yanavyoonyeshwa. Kitu cha muhimu kuhusu mabadiliko katika tabia ni kwamba wameelewa vyema ukweli, na wanapotekeleza mambo, wanauweka ukweli katika matendo kwa usahihi wa karibu na upotovu wao hauonekani mara nyingi. Kwa jumla, watu ambao tabia zao zimebadilika huonekana kuwa hasa wenye busara na wenye utambuzi, na kwa sababu ya kuelewa kwao ukweli, hawaonyeshi kujidai na kiburi sana. Wanaweza kubaini na kutambua upotovu mwingi unaofichuliwa, kwa hiyo hawana kiburi. Wanaweza kuwa na ufahamu wa taratibu kuhusu ni ipi nafasi ya mwanadamu, jinsi ya kutenda kwa busara, jinsi ya kuwa mtiifu, nini wanachofaa kusema na nini wasichofaa kusema, na nini cha kusema na nini cha kutenda kwa watu gani. Hii ndiyo sababu inasemwa kuwa watu wa aina hii ni wenye busara kiasi. Wale ambao wana mabadiliko katika tabia zao wanaishi kwa kudhihirisha sura ya binadamu kwa kweli, nao wanao ukweli. Daima wanaweza kuzungumza na kuona vitu kulingana na ukweli, na wana maadili katika kila kitu wanachokifanya; hawashawishiwi na mtu, kitu au jambo lolote, na wote wana maoni yao wenyewe na wanaweza kudumisha maadili ya ukweli. Tabia zao hazisitasiti, na haijalishi hali zao, wanaelewa jinsi ya kutimiza wajibu wao sawasawa na jinsi ya kufanya mambo ili kumridhisha Mungu. Wale ambao tabia zao zimebadilika hawalengi nini cha kufanya ili kujifanya waonekane wazuri katika kiwango cha juujuu—wanao uwazi wa ndani kuhusu kile cha kufanya ili kumridhisha Mungu. Kwa hivyo, kutoka nje wanaweza kukosa kuonekana wenye shauku sana ama kama wamefanya jambo lolote kubwa, lakini kila kitu wanachofanya kina maana, kina thamani, na kina matokeo ya kiutendaji. Wale ambao tabia zao zimebadilika wana uhakika kuwa na ukweli mwingi—hii inaweza kuthibitishwa kwa mitazamo yao kuhusu mambo na kanuni zao katika vitendo vyao. Wale wasio na ukweli hawajakuwa na mabadiliko katika tabia hata kidogo. Hiyo si kusema kwamba mtu aliyekomaa katika ubinadamu wake lazima atakuwa na mabadiliko katika tabia; labda hufanyika wakati baadhi ya sumu za kishetani katika asili ya mtu zinabadilika kwa sababu ya maarifa yao kuhusu Mungu na ufahamu wao wa ukweli. Hiyo ni kusema, sumu hizo za Shetani zinatakaswa na ukweli unaoonyeshwa na Mungu unaanza kustawi ndani ya mtu huyo, unakuwa maisha yake, nao unakuwa msingi wa kuwepo kwake. Hapo tu ndipo anakuwa mtu mpya, na hivyo tabia yake inabadilika. Hivi si kusema kwamba tabia yake ya nje ni ya upole kuliko hapo awali, kuwa alikuwa na kiburi lakini sasa maneno yake ni ya busara, kwamba hakuwa anamsikiza mtu yeyote lakini sasa anaweza kuwasikiza wengine—mabadiliko haya ya nje hayawezi kusemwa kuwa ni mabadiliko katika tabia. Bila shaka mabadiliko katika tabia yanajumuisha hali hizi, lakini jambo lililo muhimu zaidi ni kuwa maisha yake ya ndani yamebadilika. Ukweli unaoonyeshwa na Mungu unakuwa maisha yake hasa, baadhi ya sumu za kishetani zilizo ndani zimetolewa, mtazamo wa mtu huyo umebadilika kabisa, na hakuna chochote kati ya hali hizo kinachokubaliana yale ya dunia. Anaona waziwazi njama na sumu za joka kubwa jekundu; amefahamu kiini cha kweli cha maisha. Kwa hivyo maadili ya maisha yake yamebadilika—hili ndilo badiliko la muhimu zaidi na kiini cha mabadiliko katika tabia.

kutoka katika “Tofauti Kati Ya Mabadiliko Ya Nje Na Mabadiliko Katika Tabia” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Katika ulimwengu wa dini, watu wengi huteseka pakubwa maishani mwao mwote, kwa kuihini miili yao au kuubeba msalaba wao, au hata kuteseka na kustahimili hadi pumzi zao za mwisho! Wengine huwa wanafunga hadi siku ya kifo chao. Katika maisha yao yote wanajinyima chakula kizuri na mavazi mazuri, wakisisitiza mateso tu. Wanaweza kuihini miili yao na kuinyima miili yao. Uwezo wao wa kustahimili mateso unastahili sifa. Ila fikira zao, mawazo yao, mielekeo yao ya kiakili, na kwa hakika asili yao ya kale—hakuna kati yavyo kilichoshughulikiwa hata kidogo. Hawajifahamu. Picha ya Mungu akilini mwao ni ya kijadi na ya kidhahania, Mungu asiye yakini. Uamuzi wao wa kuteseka kwa ajili ya Mungu unaletwa na azma na asili yao chanya. Hata ikiwa wanamwamini Mungu, hawamfahamu Mungu wala kuyafahamu mapenzi Yake. Wanamfanyia Mungu kazi na kumtesekea Mungu kama vipofu. Hawawekei utambuzi thamani yoyote na hawajishughulishi na jinsi ambayo huduma yao inatimiza mapenzi ya Mungu kwa kweli. Aidha hawajui jinsi ya kutimiza ufahamu kuhusu Mungu. Mungu wanayemhudumia si Mungu katika sura Yake ya asili, ila ni Mungu waliyejifikiria, Mungu waliyemsikia, au Mungu wa kihadithi wanayemsoma katika maandiko. Kisha wanatumia mawazo yao dhahiri na mioyo yao ya kiungu kumtesekea Mungu na kuifanya kazi ambayo Mungu anapaswa kufanya. Huduma yao haiko sahihi, kiasi kwamba hakuna anayemhudumia Mungu kwa njia inayotimiza mapenzi Yake. Haijalishi wako radhi kiasi gani kuteseka, mitazamo yao asilia ya huduma na picha ya Mungu akilini mwao havibadiliki kwani hawajapitia hukumu ya Mungu na kuadibu na usafishaji Wake na ukamilifu, na kwa sababu hakuna yeyote aliyewaongoza na ukweli. Japo wanasadiki kwa Yesu Mwokozi, hamna kati yao aliyewahi kumwona Mwokozi. Wamemsikia tu kwa hadithi na uvumi. Hivyo huduma yao ni sawa na kuhudumu mara mojamoja macho yao yakiwa yamefungwa kama kipofu anayemhudumia baba yake. Ni nini kinaweza kupatikana kutokana na huduma kama hiyo? Na ni nani anaweza kuikubali? Huduma yao haibadiliki kamwe toka mwanzo hadi mwisho. Wanapokea mafunzo ya kibinadamu na kukita huduma yao katika uasili wao na kile wanachokipenda wao. Hili laweza kuzalisha faida gani? Hata Petro, aliyemwona Yesu, hakujua jinsi ya kumhudumia Mungu kwa njia inayotimiza mapenzi ya Mungu. Ni katika uzee wake ndipo alipopata ufahamu. Hili linaonyesha nini kuhusu wanadamu vipofu ambao hawajapitia ushughulikiaji na hawana upogoaji na ambao hawajawahi kupata yeyote wa kuwaongoza? Je, si huduma ya wengi miongoni mwenu leo ni kama ile ya vipofu? Wale wote ambao hawajapokea hukumu, hawajapokea upogoaji na ushughulikiaji, na hawana mabadiliko—je, wao si waliokosa kushindwa kabisa? Wana manufaa gani watu kama hao? Ikiwa fikira zako, ufahamu wako wa maisha, na ufahamu wako wa Mungu hauonyeshi mabadiliko mapya na hautoi faida hata kidogo, hutatimiza chochote kizuri katika huduma yako. Bila maono na bila ufahamu mpya wa kazi ya Mungu, huwezi kuwa mtu aliyeshindwa. Njia yako ya kumfuata Mungu itakuwa kama ile ya wale wanaoteseka na kufunga—itakuwa ya thamani ndogo! Hii ni kwa sababu kuna ushuhuda kidogo katika yale wayafanyayo ndipo Nasema huduma yao ni bure! Kotekote katika maisha yao, hao watu huteseka, hukaa gerezani kwa muda, na kwa kila wakati, hustahimili, husisitiza mapenzi na ukarimu, na kubeba msalaba wao. Wanatukanwa na kukataliwa na ulimwengu na hupitia kila ugumu. Wanatii hadi mwisho ila bado hawapati ushindi na hawawezi kutoa ushuhuda wa kutwaliwa. Wameteseka si haba, ila kwa ndani hawamfahamu Mungu kabisa. Hakuna fikira zao za zamani, mawazo ya zamani, vitendo vyao, uelewa wa wanadamu, na mawazo ya wanadamu yaliyoshughulikiwa. Kamwe hakuna uelewa mpya ndani yao. Hakuna hata chembe ya ufahamu wao wa Mungu ambao ni wa kweli au ni sahihi. Wamekosa kuyaelewa mapenzi ya Mungu. Je, huku kwaweza kuwa kumhudumia Mungu? Japo ulimfahamu Mungu zamani, tuseme umeudumisha ufahamu huo hadi leo na kuendelea kukita ufahamu wako kuhusu Mungu kwenye fikira na mawazo yako bila kujali Mungu anafanya nini. Yaani, ikiwa huna ufahamu mpya na wa kweli kuhusu Mungu na ukose kutambua sura na tabia ya kweli ya Mungu. Ikiwa ufahamu wako wa Mungu bado unaongozwa na fikira za uhasama na ushirikina na bado una mawazo na fikira za mwanadamu. Ikiwa hii ndiyo hali, basi hujashindwa. Lengo langu la kukwambia maneno haya yote sasa ni kukupa fursa ya kufahamu na kutumia utambuzi huu kukuongoza katika ufahamu sahihi na mpya. Aidha yanalengwa kukuondolea mawazo ya zamani na utambuzi wa zamani ulio nao ili uweze kuwa na ufahamu mpya. Ikiwa unakula na kunywa matamshi Yangu kweli, basi ufahamu wako utabadilika kwa kiwango kikubwa. Bora tu udumishe moyo mtiifu kwa kula na kunywa matamshi ya Mungu, mtazamo wako utabadilika. Bora tu unaweza kukubali kuadibu kwa kila mara, fikira zako za zamani zitabadilika taratibu. Bora tu fikira zako za zamani zimebadilishwa kabisa na kuwa mpya, vitendo vyako vitabadilika ipasavyo. Kwa njia hii, huduma yako itaendelea kuwa yenye malengo zaidi, na itaweza kutimiza mapenzi ya Mungu. Ukibadilisha maisha yako, ufahamu wako wa maisha, na mawazo yako mengi kuhusu Mungu, basi uasili wako utadidimia taratibu. Hili, na hakuna jingine ila hili, ndilo tokeo baada ya Mungu kumshinda mwanadamu; haya ndiyo mabadiliko yatakayoonekana ndani ya mwanadamu. Ikiwa katika kumwamini Mungu, yote ujuayo ni kuutiisha na kuuhini mwili wako na kustahimili na kuteseka, na hujui wazi ikiwa unachokifanya ni sawa au la, bila kujali unamfanyia nani kazi, basi vitendo kama hivi vitaletaje mabadiliko?

kutoka katika “Ukweli wa Ndani wa Kazi ya Kushinda (3)” katika Neno Laonekana katika Mwili

Kila mara watu wa kidini kama hao wanapokusanyika, wanauliza, “Dada, umeshinda vipi siku hizi?” Anajibu, “Nahisi kuwa mimi ni mdeni wa Mungu na siwezi kuridhisha matakwa ya moyo Wake.” Mwingine anasema, “Mimi, pia, ni mdeni wa Mungu na nimeshindwa kumkidhi.” Sentensi na maneno haya machache pekee yanaonyesha mambo maovu yaliyo ndani ya nyoyo zao. Maneno kama hayo ni ya kuchukiza zaidi na yenye makosa sana. Asili ya watu kama hao inampinga Mungu. Wale ambao huzingatia uhalisi huwasilisha vyovyote vilivyomo katika nyoyo zao na kufungua mioyo yao katika mawasiliano. Hakuna shughuli hata moja ya uongo, hakuna heshima ama salamu na mazungumzo matupu. Wao daima huwa na uwazi na hawafuati sheria za duniani. Kuna wale ambao wako na upendeleo wa kujionyesha kwa nje, hata bila maana yoyote. Wakati mwingine anaimba, yeye anaanza kukatika, bila hata kugundua kuwa wali katika sufuria yake umeshaungua. Watu wa aina hii si wacha Mungu au waheshimiwa, bali ni watu wa kijinga kupindukia. Hizi zote ni maonyesho ya ukosefu wa ukweli! Wakati watu wengine wanawasiliana kuhusu masuala ya maisha katika roho, ingawa hawasemi kuhusu kuwa wadeni wa Mungu, wao hubaki na upendo wa kweli kwa Mungu ndani ya mioyo yao. Kuwa kwako mdeni kwa Mungu hakuhusiani na watu wengine; wewe ni mdeni kwa Mungu, si kwa mwanadamu. Kwa hiyo ina maana gani wewe daima kuzungumzia haya kwa watu wengine? Lazima uweke umuhimu kwa kuingia katika uhalisi, si kwa bidii au maonyesho ya nje.

Je, matendo mazuri ya kijuujuu ya mwanadamu yanawakilisha nini? Hayo huwakilisha mwili, na hata matendo yaliyo bora zaidi ya nje hayawakilishi maisha, ila tabia yako tu mwenyewe. Matendo ya nje ya mwanadamu hayawezi kutimiza matakwa ya Mungu. Wewe daima huzungumza kuhusu udeni wako kwa Mungu, lakini huwezi kuyaruzuku maisha ya wengine au kuwafanya wengine kumpenda Mungu. Je, unaamini kwamba matendo kama hayo yatamridhisha Mungu? Unaamini kwamba hii ndiyo matakwa ya moyo wa Mungu, kwamba haya ni ya roho, lakini kwa kweli huu ni ujinga! Unaamini kwamba yale yanayokupendeza wewe na unayotaka ni yale yanayomfurahisha Mungu. Je, yanayokupendeza yanaweza kuwakilisha yanayompendeza Mungu? Je, tabia ya mwanadamu inaweza kumwakilisha Mungu? Yale yanayokupendeza wewe ndiyo hasa yale humchukiza Mungu, na mienendo yako ni ile ambayo Mungu huchukia na kukataa. Kama unahisi kuwa wewe ni mdeni, basi nenda na usali mbele za Mungu. Hakuna haja ya kuzungumzia jambo hilo kwa watu wengine. Usipoomba mbele za Mungu na badala yake mara kwa mara unajivuta nadhari kwako mbele ya wengine, jambo hili linaweza kutimiza matakwa ya moyo wa Mungu? Kama matendo yako daima yanaonekana tu, hii ina maana kuwa wewe ni mtu bure zaidi ya wote. Ni mtu wa aina gani yule aliye na matendo mazuri ya kijuujuu tu lakini hana uhalisi? Watu kama hao ni Mafarisayo wanafiki na watu wa dini! Msipoacha matendo yenu ya nje na hamuwezi kufanya mabadiliko, basi dalili za unafiki ndani yenu zitazidi kuimarika. Kadiri dalili za unafiki zinavyozidi, ndivyo upinzani kwa Mungu unavyozidi, na mwishowe, watu wa aina hii hakika watatupiliwa mbali!

kutoka katika “Kumwamini Mungu Kunapaswa Kulenge Uhalisi, Si Kaida za Kidini” katika Neno Laonekana katika Mwili

Madondoo ya Mahubiri na Ushirika kwa ajili ya Marejeo:

Katika ulimwengu wa kidini, kuna wacha Mungu wengi, wao husema, “Tumebadilika kwa sababu ya imani yetu katika Bwana Yesu. Tunaweza kujitahidi kwa ajili ya Bwana, kutenda kazi, kuvumilia gerezani kwa ajili ya Bwana, na hatulikatai jina Lake mbele yawengine. Tunaweza kuyatenda mambo mengi mema, kufadhili, kuchanga na kuwasaidia maskini. Haya ni mabadilikomakubwa! Tumebadilika, ndiyo sababu tunafaa kumngojea Bwana ili atulete katika ufalme wa mbinguni.” Je, mnafikiria nini juu ya maneno haya? Je, mna ufahamu wowote ijapo kwa maneno haya? Je, kutakaswa kunamaanisha nini? Je, unafikiria kwamba kama tabia yako imebadilika na unatenda matendo mema basi umetakaswa? Mtu mwingine husema, “Nimeacha kila kitu.” Hata Nimeiacha kazi yangu ulimwenguni, familia yangu na tamaa za mwili ili kujitahidi kwa ajili ya Mungu. Je, hii ni sawa na kutakaswa? Ingawa umeyatenda haya yote, huu si ushahidi thabiti kwamba umetakaswa. Hivyo, jambo muhimu ni lipi? Je, ni katika kipengele kipi unaweza kupata kutakaswa kunakoweza kuchukuliwa kama kutakaswa halisi? Kutakaswa kwa tabia ya kishetani ambayo humpinga Mungu. Sasa, udhihirisho wa tabia ya kishetani ambao humpinga Mungu ni upi? Je, udhihirisho ulio wazi zaidi ni upi? Kiburi cha mtu, majivuno, haki ya kibinafsi, na kujidai mwenyewe, pamoja na upotovu, hila, kusema uongo, udanganyifu na unafiki. Wakati mambo haya si sehemu ya mtu tena, basi kwa kweli ametakaswa. Kuna madhihirisho 12. Acheni tulitazame kila mojawapo ya haya madhihirisho 12: mtu mwenyewe kujiona kuwa mwenye kuheshimika zaidi; kuwaruhusu wale ambao hunitiiMimi kustawi na wale ambao hunipinga Mimikuangamia; kufikiria tu kuwa Mungu ndiye mkuu zaidi kukushinda, kutomnyenyekea mtuyeyote, kutowajali wengine; kufanyiza ufalme wa kibinafsi mara tu unapokuwa na uwezo; kutaka kuwa mtawala wa pekee na mjua yote na kuyaamua mambo wewe mwenyewe. Huu udhihirisho wote ni tabia za kishetani. Tabia hizi za kishetani lazima zitakaswe kabla ya mtu kuyapitia mabadiliko katika tabia ya maisha yake. Mabadiliko katika tabia ya maisha ya mtu ni kuzaliwa upya kwa sababu kiini chake kimebadilika. Awali, wakati alipopewa uwezo, aliweza kuunda ufalme wa kibinafsi. Sasa, wakati anapopewa uwezo, yeye humhudumia Mungu, humshuhudia Mungu na huwa mtumishi wa wateule wa Mungu. Je, haya siyo mabadiliko halisi? Awali, aliringa mwenyewe katika hali zote na aliwataka watu wengine wamheshimu na kumwabudu. Sasa, yeye humshuhudia Mungu kila mahali, hajishughulishi tena. Bila kujali wanavyonishughulikia watu, ni vyema. Bila kujali watu wanasema nini juu yangu, ni vyema. Sijali. Ninataka tu kumtukuza sana Mungu, kumshuhudia Mungu, kuwasaidia wengine wapate ufahamu wa Mungu, na kuwasaidia wengine watii mbele za uwepo wa Mungu. Je, haya si mabadiliko katika tabia ya maisha? “Nitawashughulikia ndugu kwa upendo. Nitawahurumia wengine katika hali zote. Katika mambo yote, sitajifikiria, nitawafikiria tu wengine. Nitawasaidia wengine kuyastawisha maisha yao na kuyatimiza majukumu yangu. Nitawasaidia wengine kuupata ukweli na kuufahamu ukweli.” Hii ndio maana ya kuwapenda watu, kuwapenda wengine kama mwenyewe! Kumhusu Shetani, unaweza kumtambua, kuwa na kanuni, kuwa na mipaka naye na kuyafunua maovu ya Shetani kabisa ili wateule wa Mungu wasipatwe na madhara yake. Huku ni kuwalinda wateule wa Mungu, na huku ni kuwapenda wengine zaidi kama mwenyewe. Zaidi ya hayo, unapaswa kukipenda ambacho Mungu hukipenda na kukichukia ambacho Mungu hukichukia. Je, basi, Mungu hukichukia nini? Yeye huwachukia wapinga Kristo, pepo waovu, na watu waovu. Hilo linamaanisha kuwa sisi pia tunapaswa kuwachukia wapinga Kristo, pepo waovu na watu waovu. Lazima tusimame upande wa Mungu. Hatuwezi kupatana nao. Mungu huwapenda wale ambao Yeye hutaka kuwaokoa na kuwabariki. Kuhusu watu hawa, lazima tuwajibike, tuwashughulikie kwa upendo, tuwasaidie, tuwaelekeze, tuwakimu na kuwahimili wao. Je, haya si mabadiliko katika tabia ya maisha ya mtu? Zaidi ya hayo, wakati umetenda dhambi au makosa fulani, au umetelekeza kanuni katika kulitenda jambo fulani, unaweza kukubali ukosoaji wa ndugu, kukaripia, kushughulikia na kupogoa; unaweza kuyapokea mambo haya yote kutoka kwa Mungu, usiwe na kinyongo, na uutafute ukweli ili kuusuluhisha upotovu wako. Je, haya si mabadiliko katika tabia yako ya maisha? Ndio, ni mabadiliko. …

Je, mabadiliko katika mwenendo ambao unazungumziwa katika ulimwengu wa kidini huwakilisha mabadiliko katika tabia ya maisha? (Hapana, hauwezi.) Kwa nini mabadiliko katika mwenendo wa mtu hayawezi kuwakilisha mabadiliko katika tabia yake ya maisha? Sababu muhimu ni kuwa bado anampinga Mungu. Unaweza kuyaona hayo kwa nje, Mafarisayo walikuwa wacha Mungu sana, waliomba, waliyaelezea maandiko na walizifuata kanuni za sheria vizuri sana. Ingeweza kusemwa kwamba kwa nje, hawakufedheheka. Watu hawakuweza kuyaona makosa. Hata hivyo, kwa nini bado waliweza kumpinga na kumshutumu Kristo? Je, hili linaonyesha nini? Hawakuwa na ukweli na hawakumjua Mungu. Kwa nje, walikuwa wazuri sana, lakini hawakuwa na ukweli, hii ndiyo sababu waliweza kumpimga Mungu. Kama walikuwa wazuri sana kwa nje, kwa nini hili halichukuliwi kama mabadiliko katika tabia ya maisha? Hii ni kwa sababu bado walikuwa wenye kiburi, wenye majivuno na hasa wenye unyoofu. Waliyaamini maarifa yao, nadharia na ufahamu wa maandiko. Waliamini kwamba walifahamu kila kitu na kwamba walikuwa bora kuliko watu wengine. Hii ndiyo sababu wakati ulimwengu wa kidini unasikia kwamba Kristo wa siku za mwisho ameuelezea ukweli wote, wanamshutumu Yeye ingawa wanajua kwamba ni ukweli.

kutoka katika Mahubiri na Ushirika Kuhusu Kuingia Katika Maisha, Juzuu ya 138

Jumamosi, 4 Mei 2019

1. Kujua Chanzo cha Upinzani wa Watu kwa Kazi Mpya ya Mungu katika Imani Yao kwa Mungu

1. Kujua Chanzo cha Upinzani wa Watu kwa Kazi Mpya ya Mungu katika Imani Yao kwa Mungu

Maneno Husika ya Mungu:
Sababu kwamba mwanadamu humpinga Mungu inatoka, kwa upande mmoja, katika tabia potovu ya mwanadamu, na kwa upande mwingine, kutokana na kutomfahamu Mungu na kutoelewa kanuni za kazi ya Mungu na mapenzi Yake kwa mwanadamu. Vipengele hivi viwili vinaunganishwa katika historia ya upinzani wa mwanadamu kwa Mungu. Wanafunzi katika imani wanampinga Mungu kwa sababu upinzani kama huu uko ndani ya asili yao, ilhali upinzani dhidi ya Mungu wa wale walio na miaka mingi katika imani unatokana na kutomfahamu Mungu, kuongeza kwa tabia yao potovu.
kutoka katika “Wote Wasiomjua Mungu Ndio Wanaompinga Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili
Kazi ya Mungu inaendelea kusonga mbele, na ingawa madhumuni ya kazi Yake bado hayajabadilika, njia anazozitumia kufanya kazi zinabadilika mara kwa mara, na hivyo pia wale wanaomfuata Mungu. Zaidi iwapo kazi ya Mungu, zaidi mwanadamu anakuja kumjua kwa kina Mungu, na tabia ya mwanadamu inabadilika ipasavyo pamoja na kazi Yake. Hata hivyo, ni kwa sababu kazi ya Mungu milele inabadilika ndio wale wasiojua kazi ya Roho Mtakatifu na wale wanadamu wajinga wasiojua ukweli wanakuwa wapinzani wa Mungu. Kazi ya Mungu kamwe haifuati dhana za mwanadamu, kwani kazi Yake daima ni mpya na siyo nzee. Kamwe Hairudii kazi ya zamani lakini badala Anasonga mbele na kazi ambayo haijafanywa hapo awali. Kwa sababu Mungu harudii kazi Yake na mwanadamu daima anahukumu kazi ya Mungu leo kulingana na kazi Yake ya zamani, ni vigumu sana kwa Mungu kutekeleza kila hatua ya kazi ya enzi mpya. Mwanadamu ana vizuizi vingi sana! Kufikiria kwa mwanadamu ni kwa akili finyu! Hakuna mwanadamu anayeijua kazi ya Mungu, lakini bado wote wanafafanua kazi hiyo. Mbali na Mungu, mwanadamu anapoteza uhai, ukweli na baraka za Mungu, lakini bado mwanadamu hajapokea uhai wala ukweli, na hata baraka kubwa Mungu anazowapa wanadamu. Wanadamu wote wanataka kumpata Mungu lakini bado hawawezi kuvumilia mabadiliko yoyote kwa kazi ya Mungu. Wale wasiokubali kazi mpya ya Mungu wanaamini kwamba kazi ya Mungu haibadiliki, na kwamba kazi ya Mungu milele inabakia kusimama. Kwa imani yao, yote yanayohitajika kupata wokovu wa milele kutoka kwa Mungu ni kuhifadhi sheria, na iwapo watatubu na kukiri dhambi zao, dhamira ya Mungu milele itaridhika. Wana maoni kwamba Mungu anaweza tu kuwa Mungu chini ya sheria na Mungu aliyesulubiwa kwa sababu ya mwanadamu; pia ni maoni yao kwamba Mungu hastahili na Hawezi kuzidi kiwango cha Biblia. Ni hasa maoni haya yaliyowafunga imara kwa sheria ya zamani na kuendelea kuwafumba kwa kanuni ngumu. Hata zaidi wanaamini kwamba kazi yoyote ile mpya ya Mungu, ni lazima ithibitishwe na unabii, na kwamba katika kila hatua ya hiyo kazi, wote wanaomfuata na roho ya kweli lazima pia waonyeshwe ufunuo, vinginevyo kazi hiyo haiwezi kuwa ya Mungu. Tayari si kazi rahisi kwa mwanadamu kuja kumjua Mungu. Ikichukuliwa pamoja na moyo wa ujinga wa mwanadamu na asili yake ya kuasi ya kujiona muhimu na kujivunia, basi ni vigumu zaidi kwa mwanadamu kukubali kazi mpya ya Mungu. Mwanadamu haitafiti kazi mpya ya Mungu kwa utunzaji wala haikubali na unyenyekevu; badala yake, mwanadamu anachukua mtazamo wa dharau, kusubiri ufunuo na mwongozo wa Mungu. Hii siyo tabia ya mwanadamu anayeasi dhidi ya na kumpinga Mungu? Ni jinsi gani wanadamu kama hawa wanaweza kupata idhini ya Mungu?
kutoka katika “Ni Jinsi Gani Mwanadamu Ambaye Amemfafanua Mungu katika Dhana Zake Anaweza Kupokea Ufunuo wa Mungu?” katika Neno Laonekana katika Mwili
Kwa sababu kazi ya Mungu mara zote huwa na masuala mapya, hivyo pana kazi mpya, na hivyo basi kuwepo na kazi iliyopitwa na wakati. Hapana ukinzani kati ya kazi mpya na ya zamani, ila zinatoshelezana, kila hatua ikifuata iliyotangulia. Kwa kuwa kuna kazi mpya, mambo ya zamani, kwa hakika, ni sharti yaondolewe. Kwa mfano, baadhi ya vitendo vilivyokita mizizi na misemo ya mwanadamu iliyozoeleka, kuongeza juu miaka mingi ya mazoea na mafundisho ya mwanadamu, ilimuumbia mwanadamu kila aina ya dhana. Maelezo ya mwanadamu kuhusu dhana kama hizi ni kwamba bado Mungu hajafichua uso Wake halisi na tabia Yake asili kwa mwanadamu, pamoja na kuenea kwa nadharia za kale kwa miaka mingi. Ni haki kusema kuwa katika kipindi cha imani ya mwanadamu kwa Mungu, ushawishi wa dhana mbalimbali umesababisha kutengenezwa na kubadilika kwa ufahamu kwa mwanadamu ambapo mwanadamu ana kila aina ya dhana kumhusu Mungu—na matokeo yake ni kuwa wengi wa watu wa kidini wanaomhudumia Mungu wamegeuka kuwa adui Zake. Kwa hivyo, kadiri dhana za watu ya kidini zinavyokuwa thabiti, ndivyo wanavyozidi kumpinga Mungu, na ndivyo wanavyozidi kuwa maadui wa Mungu. Kazi ya Mungu daima huwa mpya, si kongwe na huwa haitengenezi mafundisho ya kidini na badala yake inabadilika kila mara na kuwa mpya kwa kiwango fulani. Kazi hii ni onyesho la tabia ya asili ya Mungu Mwenyewe. Vilevile ni kanuni ya asili ya kazi ya Mungu na mojawapo ya njia ambazo Mungu hutimiza usimamizi Wake. Iwapo Mungu asingefanya kazi kwa njia hii, mwanadamu asingebadilika au kuweza kumfahamu Mungu, na Shetani asingeshindwa. Hivyo basi, kila mara katika kazi Yake, kunatokea mabadiliko ambayo yanaonekana hayatabiriki, ila ambayo, kwa hakika, yana kipindi chake. Njia mwanadamu anavyomwamini Mungu hata hivyo ni tofauti. Anashikilia mifumo ya zamani ya kidini na kadiri yalivyo ya zamani, ndivyo yanavyokuwa ya kupendeza kwake. Akili ya kipumbavu ya mwanadamu, akili isiyobadilika kama mawe inawezaje kukubali kazi nyingi isiyoeleweka mpya na maneno ya Mungu? Mwanadamu anamchukia Mungu ambaye ni mpya kila siku na si wa zamani; anampenda Mungu wa zamani ambaye Amejaa mvi na Asiyepiga hatua. Hivyo, kwa sababu Mungu na mwanadamu kila mmoja analo alipendalo, mwanadamu amekuwa adui wa Mungu. Kwa kiwango kikubwa, huu utata upo hata leo, wakati ambao Mungu amekuwa akifanya kazi mpya kwa takribani miaka 6000. Hawawezi kusaidika. … Madhumuni ya Mungu mara zote ni kuona kazi Yake ikiwa mpya na hai, si kongwe na iliyokufa, na kile Anachotaka mwanadamu ashikilie kwa nguvu kinabadilika kulingana na enzi na kipindi, na si cha kudumu milele na kisichobadilika. Hii ni kwa sababu Yeye ni Mungu ambaye husababisha mwanadamu kuishi na kuwa mpya, tofauti na ibilisi anayemsababishia mwanadamu kufa na kuwa mzee. Je, bado hamlielewi hili? Una dhana kuhusu Mungu na umeshindwa kuziacha kwa kuwa hutafakari. Si kwamba kuna maana kidogo sana katika kazi ya Mungu, au kwa sababu kazi ya Mungu hailingani na matakwa ya binadamu—wala kwamba Mungu mara zote ni “mzembe katika wajibu Wake.” Huwezi kuacha dhana zako kwa kuwa umepungukiwa na utiifu, na huna sifa hata kidogo za kiumbe wa Mungu, na si kwamba Mungu anakufanyia mambo kuwa magumu. Yote haya umejisababishia na hayana uhusiano na Mungu; mateso na misukosuko yote husababishwa na mwanadamu. Dhamira za Mungu mara zote huwa nzuri: hakusudii kukufanya uzitoe dhana, ila angependa ubadilike na uwe mpya kadiri enzi zinavyopita. Ila bado huwezi kutofautisha chokaa na jibini na kila mara ama unachunguza au unachanganua. Si kwamba Mungu anakufanyia mambo kuwa magumu, ila ni kuwa humheshimu Mungu na uasi wako umezidi. Kiumbe mdogo anathubutu kuchukua sehemu ndogo ya kile alichopewa mwanzo na Mungu na kukitumia ili kumvamia Mungu—je, huu si uasi wa mwanadamu? Ni haki kusema kuwa mwanadamu hana sifa kabisa za kutoa maoni yake mbele za Mungu, sembuse kubuni apendavyo kanuni zozote zile zisizo na thamani, za kuchukiza na zilizooza—bila kutaja chochote kuhusu hizo dhana zilizooza. Haina maana?
kutoka katika “Ni Wale tu Wanaoijua Kazi ya Mungu Leo Wanaoweza Kumhudumia Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili
Fahamuni kuwa mnapinga kazi ya Mungu, ama mnatumia dhana zenu kupima kazi ya leo, kwa sababu hamjui kanuni za kazi ya Mungu, na kwa sababu hamchukulii kazi ya Roho Mtakatifu kwa makini kutosha. Upinzani wenu kwa Mungu na kuzuia kazi ya Roho Mtakatifu kumetokana na dhana zenu na upumbavu wenu wa kiasili. Si kwa sababu kazi ya Mungu si sawa, lakini ni kwa sababu mna tabia ya kiasili ya kutotii. Baada ya kupata imani yao katika Mungu, watu wengine hawawezi hata kusema kwa uhakika mwanadamu alikotoka, ilhali wanathubutu kuzungumza hadharani wakitathmini haki na makosa ya kazi ya Roho Mtakatifu. Na pia wanawakemea mitume ambao wana kazi mpya ya Roho Mtakatifu, wakitoa maoni huku wakizungumza kwa zamu; ubinadamu wao uko chini sana, na hawana hisia zozote. Je, si siku itawadia ambapo watu kama hawa watakataliwa na kazi ya Roho Mtakatifu, na kuchomwa katika moto wa kuzimu? Hawafahamu kazi ya Mungu, lakini badala yake wanakosoa kazi Yake, na pia wanajaribu kumwagiza Mungu jinsi atakavyofanya kazi. Je, ni kwa namna gani watu hawa wasio na busara watamjua Mungu? Mwanadamu huja kumjua Mungu wakati anapomtafuta na anapokuwa na uzoefu naye; si katika kumkosoa kwa ghafla ndipo anapokuja kumjua Mungu kwa kupitia kutiwa nuru na Roho Mtakatifu. Kadiri maarifa ya watu kuhusu Mungu yanavyozidi kuwa sahihi, ndivyo upinzani wao Kwake unavyopungua. Kinyume na hayo, kadri watu wanavyomjua Mungu kwa kiasi kidogo, ndivyo wanavyokuwa na uwezekano wa kumpinga. Dhana zako, ubinadamu wako wa zamani, na utu wako, tabia na maadili ndiyo “mtaji” ambao unampingia Mungu, na kadri unavyokuwa mpotovu, ama ulivyoshushwa heshima na ulivyo duni, ndivyo unavyozidi kuwa adui wa Mungu. Wale waliomilikiwa na dhana kali na wenye tabia ya unafiki wamo hata zaidi katika uadui wa Mungu mwenye mwili, na watu kama hawa ni wapinga Kristo. Ikiwa dhana zako hazitarekebishwa, basi daima zitakuwa kinyume na Mungu; daima hutalingana na Mungu, na daima utakuwa mbali na Yeye.
kutoka katika “Kujua Hatua Tatu za Kazi ya Mungu Ndiyo Njia ya Kumjua Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili
Je, mngependa kujua kiini cha sababu ya Mafarisayo kumpinga Yesu? Je, mnataka kujua dutu ya Mafarisayo? Walikuwa wamejawa na mawazo makuu kuhusu Masiha. Kilicho zaidi, waliamini tu kuwa Masiha angekuja, ilhali hawakutafuta ukweli wa uzima. Na hivyo, hata leo bado wanamngoja Masiha, kwani hawana maarifa ya njia ya uzima, na hawajui ukweli ni nini. Ni vipi, hebu nielezeni, watu wapumbavu, wakaidi na washenzi kama hawa wangeweza kupata baraka za Mungu? Wangewezaje kumwona Masiha? Walimpinga Yesu kwa sababu hawakujua mwelekeo wa kazi ya Roho Mtakatifu, kwa sababu hawakuijua njia ya ukweli uliozungumziwa na Yesu, na zaidi, kwa sababu hawakumwelewa Masiha. Na kwa kuwa hawakuwa wamewahi kumwona Masiha, na hawakuwa wamewahi kuwa pamoja na Masiha, walifanya kosa la kuonyesha heshima tupu kwa jina la Masiha huku wakipinga dutu ya Masiha kwa kila njia. Mafarisayo hawa kwa dutu walikuwa wakaidi, wenye kiburi na hawakutii ukweli. Kanuni ya imani yao kwa Mungu ni: Haijalishi mahubiri Yako ni makubwa vipi, haijalishi mamlaka Yako ni makubwa vipi, Wewe si Kristo iwapo Huitwi Masiha. Je, maoni haya si ya upuuzi na ya kudhihaki? Nawauliza tena: Je, si rahisi sana kwenu kufanya makosa ya Mafarisayo wa mbeleni zaidi, kwa kuwa hamna ufahamu hata kidogo kumhusu Yesu? Je, unaweza kuitambua njia ya ukweli? Je, unaweza kutoa uhakika kweli kuwa hutampinga Kristo? Je, una uwezo wa kuifuata kazi ya Roho Mtakatifu? Kama hujui iwapo utampinga Kristo, basi Nasema kuwa tayari unaishi kwenye ukingo wa kifo. Wale wote ambao hawakumfahamu Masiha walikuwa na uwezo wa kumpinga Yesu, wa kumkataa Yesu, wa kumpaka Yeye tope. Watu wote wasiomwelewa Yesu wako na uwezo wa kumkana, na kumtusi. Zaidi, wako na uwezo wa kuona kurejea kwa Yesu kama uwongo wa Shetani, na watu zaidi watamshutumu Yesu aliyerudi kwa mwili. Je, haya yote hayawafanyi muogope? Mtakachokumbana nacho kitakuwa kumkufuru Roho Mtakatifu, kuharibiwa kwa maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa, na kukataliwa kwa dharau ya yale yote ambayo yamedhihirishwa na Yesu. Mnaweza kupata nini kutoka kwa Yesu kama mmetatizwa kwa namna hii? Mtaielewaje kazi ya Yesu atakaporudi kwa mwili kwa wingu jeupe, kama mnakataa katakata kuona makosa yenu? Nawaambieni hili: Watu wasioukubali ukweli, ilhali wanangoja kufika kwa Yesu juu ya wingu jeupe kwa upofu, kwa hakika watamkufuru Roho Mtakatifu, na ni kundi ambalo litaangamizwa. Mnatamani tu neema ya Yesu, na kutaka tu kufurahia ulimwengu wa mbinguni wenye raha, ilhali hamjawahi kutii maneno yaliyonenwa na Yesu, na hamjawahi kupokea ukweli utakaoonyeshwa na Yesu atakaporudi katika mwili. Mtashikilia nini badala ya ukweli wa kurejea kwa Yesu juu ya wingu jeupe? Je, ni ukweli ambao ndani yake mnashinda mkitenda dhambi, na kisha kuzikiri, tena na tena? Mtatoa nini kama kafara kwa Yesu Anayerejea juu ya wingu jeupe? Je, ni miaka ya kazi ambayo mnajiinua nayo? Ni nini mtakachoinua kumfanya Yesu Anayerejea kuwaamini? Je, ni hiyo asili yenu ya kiburi, ambayo haitii ukweli wowote?
kutoka katika “Utakapouona Mwili wa Kiroho wa Yesu Ndio Utakuwa Wakati Ambao Mungu Ametengeneza Upya Mbingu na Dunia” katika Neno Laonekana katika Mwili
Chanzo cha upinzani wa mwanadamu na uasi dhidi ya Mungu ni kupotoshwa kwake na Shetani. Kwa sababu amepotoshwa na Shetani, dhamiri ya mwanadamu imekuwa bila hisia, yeye ni mwovu, mawazo yake yamepotoka, na ana mtazamo duni. Kabla ya kupotoshwa na Shetani, mwanadamu kawaida alimfuata Mungu na alitii maneno Yake baada ya kuyasikia. Alikuwa kawaida mwenye akili timamu na dhamiri, na wa ubinadamu wa kawaida. Baada ya kupotoshwa na Shetani, hali yake ya awali, dhamiri, na ubinadamu vilidhoofika sana na viliharibiwa na shetani. Hivyo, yeye amepoteza utii wake na upendo kwa Mungu. Akili ya mwanadamu imekuwa potovu, tabia yake imekuwa sawa na ile ya mnyama, na uasi wake kwa Mungu kabisa umekuwa wa mara kwa mara na wa kuhuzunisha zaidi. Hata hivyo mwanadamu bado hajui wala kutambua hili, na kwa upofu anapinga na kuasi. Ufunuo wa tabia ya mwanadamu ni udhihirisho wa hisia zake, utambuzi na dhamiri, na kwa sababu hisia yake na utambuzi si timamu, na dhamiri yake imezidi kuwa ndogo zaidi, hivyo tabia yake ni ya uasi dhidi ya Mungu. …
Chanzo cha ufunuo wa upotovu wa tabia ya mwanadamu ni dhamiri yake iliyofifia, asili yake mbovu na akili yake isiyo timamu; kama dhamiri ya mwanadamu na hisia vinaweza kurudi kawaida, basi atafaa kwa matumizi mbele ya Mungu. Ni kwa sababu tu kuwa dhamiri ya mwanadamu daima imekuwa isiyosikia, akili ya mwanadamu haijawahi kuwa timamu, na inazidi kuwa hafifu ndio mwanadamu amezidisha uasi wake kwa Mungu, hata akampiga Yesu misumari juu ya msalaba na kumkataa Mungu mwenye mwili wa siku za mwisho kuingia katika nyumba yake, na analaani mwili wa Mungu, na anaona mwili wa Mungu kuwa ya kuchukiza na wa hali ya chini. Kama mwanadamu angekuwa na ubinadamu kidogo, hangekuwa mkatili kiasi hicho katika utendeaji wake wa mwili wa Mungu mwenye mwili; kama angekuwa na akili hata kidogo tu, hangekuwa hivyo katika utendeaji wake wa mwili wa Mungu mwenye mwili; kama angekuwa na dhamiri hata kidogo, hangekuwa mwenye “shukrani” kwa Mungu mwenye mwili kwa njia hii. Mwanadamu anaishi katika enzi ya Mungu kuwa katika mwili, lakini yeye hawezi kumshukuru Mungu kwa kumpatia nafasi nzuri kiasi hicho, na badala yake analaani kuja kwa Mungu, au kupuuza kabisa ukweli wa Mungu aliyepata mwili, na inaonekana anapinga hali hii na anachoshwa nayo. Haijalishi jinsi mwanadamu anachukua kuja kwa Mungu, Mungu, kwa ufupi, daima ameendeleza kazi yake bila kujali—hata kama mwanadamu hajawahi kumkaribisha, na bila kujua yeye hufanya maombi kwa Mungu. Tabia ya mwanadamu imekuwa mbaya zaidi, akili yake imekuwa hafifu zaidi, na dhamiri yake imekanyagwa kabisa na yule muovu na kwa muda mrefu imekoma kuwa dhamiri ya awali ya mwanadamu.
kutoka katika “Kuwa na Tabia Isiyobadilika Ni Kuwa katika Uadui na Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili

Soma Zaidi: Je, Mwenyezi Mungu na Bwana Yesu ni Mungu Mmoja?

Ijumaa, 3 Mei 2019

Katika Kumwamini Mungu, Unapaswa Kuweka Uhusiano wa Kawaida na Mungu

3. Katika Kumwamini Mungu, Unapaswa Kuweka Uhusiano wa Kawaida na Mungu

Maneno Husika ya Mungu:
Katika kuwa na imani kwa Mungu, ni lazima angalau utatue swala la kuwa na uhusiano wa kawaida na Mungu. Bila uhusiano wa kawaida na Mungu, basi umuhimu wa kumwamini Mungu unapotea. Kuunda uhusiano wa kawaida na Mungu kunapatikana kikamilifu kupitia kuutuliza moyo wako mbele ya Mungu. Uhusiano wa kawaida na Mungu unamaanisha kuweza kutoshuku au kukataa kazi yoyote ya Mungu na kutii, na zaidi ya hayo unamaanisha kuwa na nia sahihi mbele ya Mungu, sio kufikiria kujihusu, daima kuwa na maslahi ya familia ya Mungu kama jambo muhimu zaidi haijalishi kile unachofanya, kukubali kutazamiwa na Mungu, na kukubali mipangilio ya Mungu. Una uwezo wa kuutuliza moyo wako mbele ya Mungu kila unapofanya chochote; hata kama huelewi mapenzi ya Mungu, bado ni lazima utimize wajibu na majukumu yako kadri ya uwezo wako. Hujachelewa sana kusubiri mapenzi ya Mungu yafichuliwe kwako na kisha kuyaweka katika vitendo. Wakati uhusiano wako na Mungu umekuwa wa kawaida, basi pia utakuwa na uhusiano wa kawaida na watu. Kila kitu kimejengwa juu ya msingi wa maneno ya Mungu. Kupitia katika kula na kunywa maneno ya Mungu, tenda kulingana na mahitaji ya Mungu, weka sawa maoni yako, usitende mambo yanayompinga Mungu au kuingilia kati mambo ya kanisa. Usifanye vitu visivyo na manufaa kwa maisha ya ndugu, usiseme maneno yasiyosaidia wengine, usifanye vitu vya kufedhehesha. Kuwa mwadilifu na mwenye heshima unapofanya mambo yote na kuyafanya ya kupendeza mbele ya Mungu. Hata ingawa kutakuwa na nyakati ambazo mwili ni dhaifu, unaweza kushikiza umuhimu mkubwa kabisa kwa kufaidi familia ya Mungu, kutotamani faida yako mwenyewe, na kutekeleza haki. Ikiwa unaweza kutenda kwa njia hii, uhusiano wako na Mungu utakuwa wa kawaida.
kutoka katika “Uhusiano Wako Na Mungu Ukoje?” katika Neno Laonekana katika Mwili
Kila unapofanya chochote, lazima uchunguze iwapo motisha yako ni sahihi. Ikiwa unaweza kutenda kulingana na matakwa ya Mungu, basi uhusiano wako na Mungu utakuwa wa kawaida. Hiki ndicho kigezo cha chini zaidi. Iwapo, unapochunguza motisha yako, kunatokea zile zisizo sahihi, na iwapo unaweza kuzikwepa na kutenda kulingana na maneno ya Mungu, basi utakuwa mtu ambaye ni mwema mbele ya Mungu, kitu ambacho kitaonyesha kuwa uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida, na kwamba kila unachofanya ni kwa ajili ya Mungu, na sio kwa sababu yako binafsi. Ni lazima uuweke moyo wako sawa kila unapofanya ama kusema chochote, uwe mwenye haki katika matendo yako, na usiongozwe na hisia zako, au utende kulingana na mapenzi yako: Haya ndiyo maadili ambayo wale wanaoamini katika Mungu wanatenda kulingana nayo. Motisha za mtu na kimo chake vinaweza kufichuliwa katika kitu kidogo, na hivyo, kwa watu kuingia kwa njia ya kufanywa wakamilifu na Mungu, ni lazima kwanza wasuluhishe motisha yao wenyewe na uhusiano wao na Mungu. Ni pale ambapo tu uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida ndipo utaweza kufanywa mkamilifu na Mungu, na ni hapo tu ndipo ushughulikiaji, upogoaji, nidhamu, na usafishaji wa Mungu kwako utaweza kupata matokeo yanayotakiwa. Hiyo kusema, watu wanaweza kuwa na Mungu mioyoni mwao, wasitafute maslahi binafsi, wasifikirie kuhusu maisha yao binafsi ya baadaye (ikirejelea kufikiri juu ya mwili), lakini badala yake wanabeba mzigo wa kuingia katika maisha, wanajitahidi wawezavyo kufuatilia ukweli, na kuitii kazi ya Mungu. Kwa namna hii, makusudi unayoyatafuta ni sahihi, na uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida. Inaweza kusemwa kwamba kuutengeneza uhusiano wako na Mungu ndiyo hatua ya kwanza ya kuingia kwako katika safari ya kiroho. Ingawa hatima yako iko mikononi mwa Mungu, na imeshaamuliwa kabla na Mungu, na haiwezi kubadilishwa na wewe mwenyewe, kwamba unaweza au huwezi kufanywa mkamilifu au kupatwa na Mungu kunategemea na kama uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida au la. Pengine kuna sehemu ndani yako ambazo ni dhaifu au zenye kutotii—lakini bora tu mtazamo wako wa nje ni sawa na motisha yako ni sahihi, na bora tu umeuweka uhusiano wako na Mungu sawa na kuufanya wa kawaida, basi utafuzu kufanywa mkamilifu na Mungu. Iwapo huna uhusiano sahihi na Mungu, na unatenda kwa ajili ya mwili, au familia yako, basi haijalishi kiwango cha kazi unayofanya kwa bidii, itakuwa bure. Iwapo uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida, basi kila kitu kingine kitakuwa sawa. Mungu haangalii chochote kingine, bali anaangalia tu iwapo mitazamo yako kwa kuamini kwa Mungu ni sawa: unayemwamini, ni kwa ajili ya nani unaamini, na ni kwa nini unaamini. Iwapo unaweza kuona vitu hivi kwa udhahiri, na unaweza kuweka mitazamo yako iwe sawa na kuweza kutenda, basi maisha yako yatapiga hatua, na una uhakika wa kuweza kuingia kwenye njia sahihi. Iwapo uhusiano wako na Mungu sio wa kawaida, na mitazamo yako kwa kuamini katika Mungu inakiuka maadili, basi haya yatazuia mengine yote. Haijalishi jinsi unavyoamini katika Mungu, hutafaidi chochote. Iwapo tu uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida ndipo utasifiwa na Mungu unapoupa mwili kisogo, unapoomba, unapoteseka, unapostahimili, unapotii, unapowasaidia ndugu na dada zako, unaweka juhudi zaidi kwa Mungu, na kadhalika.
kutoka katika “Uhusiano Wako Na Mungu Ukoje?” katika Neno Laonekana katika Mwili
Watu wanaamini katika Mungu, wanampenda Mungu, na kumkidhi Mungu kwa kugusa Roho wa Mungu kwa moyo wao, hivyo kupata ridhaa ya Mungu; na wakati wanajihusisha na maneno ya Mungu kwa moyo wao, kwa hivyo wanasisimuliwa na Roho wa Mungu. Ikiwa unataka kufikia maisha ya kawaida ya kiroho na kuanzisha uhusiano wa kawaida na Mungu, lazima kwanza uutoe moyo wako kwa Mungu, na uuweke moyo wako uwe mtulivu mbele za Mungu. Baada tu ya kuutoa moyo wako mzima katika Mungu ndipo utaweza kuwa na maisha ya kawaida ya kiroho hatua kwa hatua. Kama, kwa imani yao katika Mungu, watu hawautoi moyo wao kwa Mungu, ikiwa moyo wao hauko katika Mungu, na wala hawauchukulii mzigo wa Mungu kama wao wenyewe, basi kila kitu wanachofanya ni kumdanganya Mungu, nayo ni matendo ya watu wa kidini, wasioweza kuipokea sifa ya Mungu. Mungu hawezi kupata kitu chochote kutoka kwa aina hii ya mtu; aina hii ya mtu anaweza tu kutumika kama foili[a] kwa kazi ya Mungu, kama pambo katika nyumba ya Mungu, kuchukua nafasi, naye hana manufaa—Mungu hamtumii aina hii ya mtu. Katika mtu kama huyo, sio tu kwamba hakuna nafasi kwa ajili ya kazi ya Roho Mtakatifu, hata zaidi hakuna thamani ya ukamilifu; aina hii ya mtu ni “mfu atembeaye” halisi—hana sehemu ambazo zinaweza kutumika na Roho Mtakatifu—wao wote wametwaliwa na Shetani, kupotoshwa kwa kiwango kilichokithiri na Shetani, ambao ni chombo cha kuondolewa na Mungu. Kwa sasa Roho Mtakatifu hawatumii tu watu kwa kuyaweka maadili yao katika matumizi, lakini pia kuwakamilisha na kubadilisha dosari zao. Kama moyo wako unaweza kumiminwa ndani ya Mungu, na kukaa kimya mbele za Mungu, basi utakuwa na nafasi na sifa za kuhitimu ili kutumiwa na Roho Mtakatifu, kupokea nuru na mwangaza wa Roho Mtakatifu, na hata zaidi, utakuwa na nafasi kwa Roho Mtakatifu kufidia dosari zako. Unapoutoa moyo wako kwa Mungu, unaweza kuingia kwa undani zaidi kwenye upande mzuri na kuwa kwenye kiwango cha juu zaidi cha uelewaji; katika upande hasi, utakuwa na uelewa zaidi wa makosa na dosari zako mwenyewe, utakuwa na hamu zaidi ya kutafuta kuyakidhi mapenzi ya Mungu, na hutakuwa katika hali ya kukaa tu, utaingia ndani kwa utendaji. Hii itamaanisha kuwa wewe ni mtu sahihi.
kutoka katika “Ni Muhimu Sana Kuanzisha Uhusiano wa Kufaa na Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili
Ikiwa unataka kuwa na uhusiano wa kufaa na Mungu, lazima moyo wako umgeukie Mungu, na juu ya msingi huu, pia utakuwa na uhusiano wa kufaa na watu wengine. Iwapo huna uhusiano unaofaa na Mungu, haijalishi unachofanya kudumisha uhusiano wako na watu wengine, haijalishi jinsi gani unafanya kazi kwa bidii au ni nguvu kiasi gani unaweka ndani yake, bado ni ya falsafa ya mwanadamu ya maisha. Unadumisha nafasi yako miongoni mwa watu kupitia mtazamo wa mwanadamu na falsafa ya mwanadamu ili kwamba wakupe wewe sifa. Hauundi uhusiano unaofaa na watu kulingana na neno la Mungu. Iwapo hutilii maanani uhusiano wako na watu lakini unadumisha uhusiano unaofaa na Mungu, ikiwa uko tayari kumpa Mungu moyo wako na ujifunze kumtii, kwa kawaida sana, uhusiano wako na watu wote utakuwa unaofaa. Kwa njia hii, uhusiano huu haujengwi kwa mwili, bali juu ya msingi wa upendo wa Mungu. Kwa kiasi kikubwa hakuna ushirikiano uliojengwa juu ya mwili, lakini katika roho kuna ushirikiano na vilevile upendo, starehe, na kutoleana kwa wenza. Haya yote yanafanywa kwa msingi wa moyo unaomridhisha Mungu. Uhusiano huu haudumishwi kwa kutegemea falsafa ya mwanadamu ya maisha, bali unaundwa kwa kawaida kupitia mzigo wa Mungu. Hauhitaji jitihada za binadamu—unawekwa katika matendo kupitia maadili ya neno la Mungu. Je, unayo hiari ya kuwa mwenye kufikiria mapenzi ya Mungu? Je, uko tayari kuwa mtu “bila mantiki” mbele za Mungu? Je, uko tayari kuutoa moyo wako kwa Mungu kabisa, na kutofikiri kuhusu msimamo wako kati ya watu? Kati ya watu wote ambao una mawasiliano nao, ni gani ambao kati yao unayo mahusiano bora zaidi? Wepi kati yao ambao unayo mahusiano mabaya zaidi nao? Je, mahusiano yako na watu ni ya kufaa? Je, unawachukulia watu wote kwa usawa? Je, uhusiano wako na wengine umeimarishwa kwa mujibu wa falsafa yako ya maisha, ama umejengwa kwenye msingi wa upendo wa Mungu? Wakati mtu hautoi moyo wake kwa Mungu, basi roho yake inakuwa butu, inakufa ganzi na kutofahamu. Aina hii ya mtu kamwe hataelewa maneno ya Mungu na kamwe hatakuwa na uhusiano wa kufaa na Mungu; aina hii ya mtu kamwe hatabadilisha tabia yake. Kubadilisha tabia ya mtu ni mchakato wa mtu kuutoa kabisa moyo wake kwa Mungu, na wa kupokea nuru na mwangaza kutoka kwa maneno ya Mungu. Kazi ya Mungu inaweza, kumruhusu mtu kuingia kwa utendaji, na pia kumwezesha kuepuka masuala yake hasi baada ya kupata maarifa. Unapoweza kuutoa moyo wako kwa Mungu, utaweza kuhisi kila harakati yenye hila ndani ya roho yako, nawe utajua kila nuru na mwangaza upokelewao kutoka kwa Mungu. Shikilia hili, nawe utaingia katika njia ya kukamilishwa na Roho Mtakatifu hatua kwa hatua. Kadri moyo wako unavyoweza kuwa mtulivu mbele za Mungu, ndivyo roho yako itakavyokuwa makini zaidi na wa kutaka uangalifu mkubwa, na kadri roho yako itakavyoweza kutambua kuchochewa na Roho Mtakatifu, kisha uhusiano wako na Mungu utakuwa wa kufaa zaidi na zaidi. Uhusiano unaofaa kati ya watu unaundwa juu ya msingi wa kumpa Mungu moyo wako; haufanikishwi kupitia jitihada za binadamu. Bila Mungu mioyoni mwao, uhusiano kati ya watu ni uhusiano wa mwili tu. Sio uhusiano unaofaa, bali ni kujiingiza katika tamaa za mwili—ni uhusiano ambao Mungu anachukia, Asioupenda. Ukisema kuwa roho yako imeguzwa, lakini daima unataka kuwa na ushirika na watu wanaokupendeza, na wale unaowachukulia kwa hali ya juu, na iwapo kuna mtafutaji mwingine ambaye hakupendezi, ambaye huna upendeleo kwake na huwezi kujihusisha naye, huu ni ushahidi zaidi kuwa wewe ni mtu mwenye hisia na kuwa huna uhusiano unaofaa na Mungu kamwe. Unajaribu kumdanganya Mungu na kuficha ubaya wako mwenyewe. Hata ingawa unaweza kushirikisha uelewano kiasi lakini unabeba ubaya moyoni mwako, kila kitu unachofanya ni kizuri tu kwa kiwango cha mwanadamu. Mungu hatakusifu—unatenda kulingana na mwili, sio kulingana na mzigo wa Mungu. Iwapo unaweza kuutuliza moyo wako mbele ya Mungu na kuwa na ushirikiano wa kufaa na wale wote wanaompenda Mungu, ni hapo tu ndipo utakuwa uko tayari kwa matumizi ya Mungu. Kwa njia hii, haijalishi jinsi unavyopatana na wengine, haitakuwa kulingana na falsafa ya maisha, lakini itakuwa kuishi mbele ya Mungu, kuufikiria mzigo Wake.
kutoka katika “Ni Muhimu Sana Kuanzisha Uhusiano wa Kufaa na Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili
Kwa kila tamshi la Mungu, baada ya kulisoma na kupata ufahamu, utaliweka katika vitendo. Bila kujali ulivyokuwa ukitenda kabla—pengine huko nyuma mwili wako ulikuwa dhaifu, ulikuwa muasi, na ulipinga—hili silo jambo kubwa, na haliwezi kuzuia maisha yako yasikue leo. Ilimradi unaweza kuwa na uhusiano wa kawaida na Mungu leo, basi kuna tumaini. Ikiwa kwa kila wakati unaposoma maneno ya Mungu, unakuwa na mbadiliko na kuruhusu watu wengine kuona kwamba maisha yako yamebadilika kuwa mazuri, inaonyesha kwamba una uhusiano wa kawaida na Mungu na kwamba umewekwa sawa. Mungu hashughulikii watu kulingana na dhambi zao. Ilimradi unaweza kutoasi tena na hupingi tena baada ya wewe kuelewa na kufahamu, basi Mungu atakuwa bado Ana huruma na wewe. Unapokuwa na ufahamu huu na nia ya kutafuta kukamilishwa na Mungu, basi hali yako katika uwepo wa Mungu itakuwa ya kawaida. Bila kujali unachofanya, zingatia: Mungu atafikiri nini ikiwa nitafanya hiki? Je, kitawafaidi ndugu? Je, kitakuwa cha faida kwa kazi ya nyumba ya Mungu? Chunguza makusudi yako katika maombi, ushirika, usemi, kazi na kuhusiana na watu, na chunguza endapo uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida au si wa kawaida. Ikiwa huwezi kutofautisha makusudi yako na fikra zako, basi huna ubaguzi, kitu ambacho kinathibitisha kwamba unaelewa kidogo sana kuhusu ukweli. Ikiwa unaweza kuwa na ufahamu ulio wazi wa kila kitu ambacho Mungu hufanya, vitazame vitu kulingana na neno la Mungu na vitazame vitu kwa kusimama katika upande wa Mungu, basi mitazamo yako itakuwa sahihi. Kwa hiyo, kujenga uhusiano mzuri na Mungu ni kipaumbele cha juu kwa mtu yeyote anayemwamini Mungu; kila mtu anapaswa kuichukulia kama kazi muhimu na kama tukio lao kubwa la maisha. Kila kitu unachofanya kinapaswa kipimwe dhidi ya iwapo una uhusiano wa kawaida na Mungu au la. Ikiwa uhusianao wako na Mungu ni wa kawaida na makusudi yako ni sahihi, basi kifanye. Ili kudumisha uhusiano wa kawaida na Mungu, hupaswi kuogopa kupoteza maslahi binafsi, hupaswi kumruhusu Shetani kushinda, hupaswi kumruhusu Shetani kupata kitu dhidi yako, na hupaswi kumruhusu Shetani kukufanya uwe kichekesho. Kusudi kama hili ni udhihirisho kwamba uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida. Si kwa ajili ya mwili, badala yake ni kwa ajili ya amani ya roho, ni kwa ajili ya kupata kazi ya Roho Mtakatifu na kwa ajili ya kuyaridhisha mapenzi ya Mungu. Ili kuingia katika hali sahihi, unapaswa kujenga uhusiano mzuri na Mungu, unapaswa kuweka sawa mtazamo wako wa imani kwa Mungu. Ni kumruhusu Mungu kukupata, kumruhusu Mungu kufichua matunda ya maneno Yake kwako na kukuangazia na kukupatia nuru zaidi. Kwa namna hii utaingia katika tabia nzuri. Endelea kula na kunywa maneno ya Mungu ya sasa, ingia katika njia ya sasa ya kazi ya Roho Mtakatifu, fanya kulingana na matakwa ya Mungu ya sasa, usifuate mazoea ya kale, using’ang’anie njia za zamani za kufanya mambo, na haraka ingia katika namna ya kazi ya leo. Kwa njia hii uhusiano wako na Mungu utakuwa wa kawaida kabisa na utaingia katika njia sahihi ya kumwamini Mungu.
kutoka katika “Uhusiano Wako Na Mungu Ukoje?” katika Neno Laonekana katika Mwili