Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo kumwamini-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo kumwamini-Mungu. Onyesha machapisho yote

Alhamisi, 6 Juni 2019

“Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VII Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (I)” Sehemu ya Tatu

“Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VII Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (I)” Sehemu ya Tatu

Mwenyezi Mungu anasema, “Mungu aliumba vitu vyote kuhusiana, kupatana na kutegemeana. Alitumia njia hii na kanuni hizi kudumisha kuendelea kuishi na uwepo wa vitu vyote na kwa njia hii binadamu ameishi kwa utulivu na kwa amani na amekua na kuzaliana kutoka kizazi kimoja hadi kingine katika mazingira haya hai hadi siku ya leo. Yaani, Mungu anaweka uwiano katika mazingira ya asili. Kama kusingekuwa na udhibiti na ukuu wa Mungu, hakuna mwanadamu ambaye angeweza kudumisha na kuweka wiano katika mazingira, hata kama yaliumbwa na Mungu kwanza.”
Mungu anamwacha mwanadamu kusimamia vitu vyote na kuwa na utawala juu yao, lakini mwanadamu anafanya kazi nzuri? (Hapana.) Ni kwa jinsi gani mwanadamu anafanya kazi mbaya? Mwanadamu ana tabia ya uharibifu; mwanadamu sio kwamba tu hawezi kutunza vitu kama Mungu alivyoviumba, kwa kweli ameviharibu. Binadamu ameifanya milima kuwa vifusi, ameijaza bahari kwa mchanga, na amezibadilisha tambarare kuwa majangwa ambapo hakuna kinachoweza kuishi. Halafu katika majangwa hayo mwanadamu amejenga viwanda na kujenga vinu vya nyuklia na uharibifu unaendelea katika pande zote. Mito si mito tena, bahari si bahari tena.... Binadamu anapovunja uwiano na kanuni za maumbile, siku yao ya maafa na kifo haipo mbali na haiepukiki. Maafa yanapokuja, watajua viumbe vya Mungu ni vya thamani kiasi gani jinsi vyote ni muhimu kwa binadamu. Mwanadamu kuishi katika mazingira yenye hali ya hewa nzuri ni sawa na kuwa peponi. Watu hawatambui baraka hii, lakini wakati ambapo wataipoteza yote ndipo watatambua ni jinsi gani yote ni adimu na ya thamani. Ni kwa jinsi gani mtu anaweza kuirudisha hii yote? Watu wangefanyaje ikiwa Mungu Asingekuwa tayari kuitengeneza tena? Mngefanyaje? (Tusingeweza kufanya chochote.) Kwa kweli, kuna kitu mnachoweza kufanya na ni rahisi sana na Nitakapowaambia ni nini, mara moja mtajua kwamba hiyo inawezekana. Kwa nini mwanadamu amejikuta katika mashaka yake ya kimazingira ya sasa? Je, ni kwa sababu ya tamaa na uharibifu wa mwanadamu? Ikiwa mwanadamu atasitisha uharibifu huu, je, mazingira ya kuishi hayatakuwa sawa taratibu yenyewe? Ikiwa Mungu hafanyi chochote, ikiwa Mungu hatamani tena kufanya kitu chochote kwa ajili ya binadamu—yaani, hataki kuingilia—njia bora zaidi ingekuwa ni binadamu kusitisha uharibifu huu na kurudisha vitu kuwa vile vilivyokuwa. Kusitisha uharibifu huu wote humaanisha kusitisha uporaji na uharibifu wa vitu ambavyo Mungu ameviumba. Hii itaruhusu mazingira ambamo mwanadamu anaishi kuboreka taratibu. Kushindwa kufanya hivyo kutasababisha uharibifu zaidi wa mazingira na hali itakuwa mbaya zaidi. Je, mbinu Yangu ni rahisi? (Ndiyo, ni rahisi.) Ni rahisi na inawezekana, siyo? Ni rahisi kweli, na inawezekana kwa baadhi ya watu, lakini je, hii inawezekana kwa watu walio wengi duniani? (Haiwezekani.) Kwenu nyinyi, angalau inawezekana? (Ndiyo.) Chanzo cha “ndiyo” yenu ni nini? Je, mtu anaweza kusema kuwa inahusisha kuanzisha msingi wa uelewa kuhusu matendo ya Mungu? Je, mtu anaweza kusema inahusisha kushikilia kanuni na mpango wa Mungu? (Ndiyo.) Kuna njia ya kubadilisha haya yote, lakini hiyo siyo mada tunayoijadili sasa. Mungu anawajibika kwa kila uhai wa binadamu na anawajibika hadi mwisho. Mungu Anawakimu, hata kama umeugua kutokana na mazingira yaliyoharibiwa na Shetani, au kuathiriwa na uchafuzi au kupata madhara mengine, haijalishi; Mungu Anakukimu na Atakuacha uendelee kuishi. Je, una imani katika hili? (Ndiyo.) Mungu hachukulii upotevu wa maisha ya binadamu kwa urahisi.
Mmehisi umuhimu wa kumtambua Mungu kama chanzo cha uhai kwa vitu vyote? (Ndiyo, tumehisi.) Mna hisia gani? Endelea, nitasikiliza. (Hapo awali, hatukufikiria kamwe kuhusisha milima, bahari na maziwa na matendo ya Mungu. Leo, kupitia ushirika wa Mungu, sasa tunaelewa kwamba haya yote siku zote yalikuwa ni matendo ya Mungu na yanatoka kwa hekima Yake, hivyo tunaona kwamba uumbaji wa Mungu wa vitu vyote ulioamuliwa kabla kuanzia mwanzoni kabisa na vyote vinakuwa na mapenzi mema ya Mungu. Vitu vyote vinahusiana na binadamu ndiye anayenufaika mwishowe. Tulichokisikia leo kinaonekana ni kipya na kigeni, na tumehisi jinsi ambavyo matendo ya Mungu ni halisi. Katika uhalisia na katika maisha yetu ya kila siku tunaona kwa kweli vitu kama vilivyo tunapokutana na viumbe hai.) Unaiona kabisa, sio? Mungu kumkimu binadamu sio bila msingi imara, hatamki tu maneno machache na kuishia hapo tu. Mungu anafanya mambo mengi, hata vitu ambavyo huvioni anafanya kwa manufaa yako. Mwanadamu anaishi katika mazingira haya, ulimwengu huu ambao Mungu Aliutengeneza, na ndani yake watu na vitu vingine vinategemeana, kama tu ambavyo gesi inayotoka kwenye mimea inaitakasa hewa na kuwanufaisha watu wanaoivuta. Hata hivyo, baadhi ya mimea ni sumu kwa watu, lakini hakuna mimea mingine ambayo ni kiuasumu kwao? Hili ni moja ya maajabu ya uumbaji wa Mungu! Hatukujadili mada hii leo, badala yake tumejadili kimsingi hali ya kutegemeana ya mwanadamu na vitu vingine, jinsi ambavyo mwanadamu hawezi kuishi bila vitu vingine. Ni nini umuhimu wa uumbaji wa Mungu wa vitu vyote? Mwanadamu hawezi kuishi bila vitu vingine, kama ambavyo mwanadamu anahitaji hewa kuweza kuishi na namna ambavyo kama ungewekwa kwenye ombwe ungekufa upesi. Hii ni kanuni ya msingi sana kukufanya kuona kwamba mwanadamu anahitaji vitu vingine. Hivyo ni aina gani ya mtazamo ambao mwanadamu anapaswa kuwa nao kwa vitu vyote? (Kuvithamini sana.) Vithamini sana, vitunze, vitumie kwa ufanisi, usiviharibu, usivipoteze, na usivibadilishe kwa ghafula, maana vitu vyote vinatoka kwa Mungu na vinatolewa kwa binadamu na binadamu anapaswa kuvichukulia kwa uangalifu. Leo tumejadili mada hizi mbili, na mtarudi na kuzitafakari kwa kina. Wakati ujao tutajadili vitu vingi zaidi kwa kina. Ushirika wetu utaishia hapa kwa leo. Kwa heri! (Kwa heri!)

Jumapili, 5 Mei 2019

Tofauti Kati Ya Matendo Mazuri ya Nje na Mabadiliko Katika Tabia

7. Tofauti Kati Ya Matendo Mazuri ya Nje na Mabadiliko Katika Tabia

Maneno Husika ya Mungu:
Mabadiliko katika tabia hasa huhusu mabadiliko katika asili ya watu. Mambo ya asili ya mtu hayawezi kuonekana kutoka kwa mienendo ya nje; yanahusisha moja kwa moja thamani na umuhimu wa kuwepo kwake. Yaani, yanahusisha moja kwa moja mitazamo ya mtu kuhusu maisha na maadili yake, mambo yaliyo ndani kabisa ya nafsi yake, na kiini chake. Mtu ambaye hawezi kukubali ukweli hatakuwa na mabadiliko katika hali hizi. Ni kwa kupitia kazi ya Mungu pekee, kuingia kikamilifu katika ukweli, kubadili maadili na mitazamo yake kuhusu kuwepo na maisha, kulinganisha msoni yake na ya Mungu, na kuwa na uwezo wa kutii na kujitoa kabisa kwa Mungu ndio tabia zake zinaweza kusemekana zimebadilika. Huenda ukaonekana kufanya juhudi fulani, unaweza ukawa thabiti unapokabiliwa na shida, huenda ukaweza kutekeleza utaratibu wa kazi kutoka walio juu, au huenda ukaweza kwenda popote unapoambiwa kwenda, lakini haya ni mabadiliko madogo tu katika mienendo yako, na hayatoshi kujumuisha mabadiliko katika tabia yako. Huenda ukaweza kukimbia katika njia nyingi, kuvumilia shida nyingi na kustahamili fedheha kuu; huenda ukajihisi karibu sana na Mungu, na Roho Mtakatifu anaweza kukufanyia kazi fulani. Hata hivyo, Mungu anapokuomba ufanye jambo fulani ambalo halipatani na fikira zako, huenda bado usitii, lakini utafute visababu, na kuasi na kumpinga Mungu, hata kufikia kiwango cha wewe kumhakiki Mungu na kumpinga Yeye. Hili ni tatizo kubwa! Hili linaonyesha kwamba bado una asili inayompinga Mungu na kwamba hujapitia mabadiliko yoyote kabisa.

kutoka katika “Unachopaswa Kujua Kuhusu Kuigeuza Tabia Yako” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Watu wanaweza kuwa na tabia nzuri, lakini hiyo haimaanishi kuwa wako na ukweli. Bidii ya watu inaweza tu kuwafanya wazingatie mafundisho na kufuata kanuni; watu wasio na ukweli hawana namna ya kutatua shida halisi, na mafundisho hayawezi kushikilia nafasi ya ukweli. Wale ambao wamepitia mabadiliko katika tabia zao ni tofauti. Wale ambao wamepitia mabadiliko katika tabia zao wameelewa ukweli, wanatambua masuala yote, wanajua jinsi ya kutenda kulingana na mapenzi ya Mungu, jinsi ya kutenda kulingana na kanuni za ukweli, jinsi ya kutenda ili kumridhisha Mungu, nao wanaelewa asili ya upotovu wanaoufichua. Mawazo na dhana zao wenyewe vinapofichuliwa, wanaweza kutambua na kuunyima mwili. Hivi ndivyo mabadiliko katika tabia yanavyoonyeshwa. Kitu cha muhimu kuhusu mabadiliko katika tabia ni kwamba wameelewa vyema ukweli, na wanapotekeleza mambo, wanauweka ukweli katika matendo kwa usahihi wa karibu na upotovu wao hauonekani mara nyingi. Kwa jumla, watu ambao tabia zao zimebadilika huonekana kuwa hasa wenye busara na wenye utambuzi, na kwa sababu ya kuelewa kwao ukweli, hawaonyeshi kujidai na kiburi sana. Wanaweza kubaini na kutambua upotovu mwingi unaofichuliwa, kwa hiyo hawana kiburi. Wanaweza kuwa na ufahamu wa taratibu kuhusu ni ipi nafasi ya mwanadamu, jinsi ya kutenda kwa busara, jinsi ya kuwa mtiifu, nini wanachofaa kusema na nini wasichofaa kusema, na nini cha kusema na nini cha kutenda kwa watu gani. Hii ndiyo sababu inasemwa kuwa watu wa aina hii ni wenye busara kiasi. Wale ambao wana mabadiliko katika tabia zao wanaishi kwa kudhihirisha sura ya binadamu kwa kweli, nao wanao ukweli. Daima wanaweza kuzungumza na kuona vitu kulingana na ukweli, na wana maadili katika kila kitu wanachokifanya; hawashawishiwi na mtu, kitu au jambo lolote, na wote wana maoni yao wenyewe na wanaweza kudumisha maadili ya ukweli. Tabia zao hazisitasiti, na haijalishi hali zao, wanaelewa jinsi ya kutimiza wajibu wao sawasawa na jinsi ya kufanya mambo ili kumridhisha Mungu. Wale ambao tabia zao zimebadilika hawalengi nini cha kufanya ili kujifanya waonekane wazuri katika kiwango cha juujuu—wanao uwazi wa ndani kuhusu kile cha kufanya ili kumridhisha Mungu. Kwa hivyo, kutoka nje wanaweza kukosa kuonekana wenye shauku sana ama kama wamefanya jambo lolote kubwa, lakini kila kitu wanachofanya kina maana, kina thamani, na kina matokeo ya kiutendaji. Wale ambao tabia zao zimebadilika wana uhakika kuwa na ukweli mwingi—hii inaweza kuthibitishwa kwa mitazamo yao kuhusu mambo na kanuni zao katika vitendo vyao. Wale wasio na ukweli hawajakuwa na mabadiliko katika tabia hata kidogo. Hiyo si kusema kwamba mtu aliyekomaa katika ubinadamu wake lazima atakuwa na mabadiliko katika tabia; labda hufanyika wakati baadhi ya sumu za kishetani katika asili ya mtu zinabadilika kwa sababu ya maarifa yao kuhusu Mungu na ufahamu wao wa ukweli. Hiyo ni kusema, sumu hizo za Shetani zinatakaswa na ukweli unaoonyeshwa na Mungu unaanza kustawi ndani ya mtu huyo, unakuwa maisha yake, nao unakuwa msingi wa kuwepo kwake. Hapo tu ndipo anakuwa mtu mpya, na hivyo tabia yake inabadilika. Hivi si kusema kwamba tabia yake ya nje ni ya upole kuliko hapo awali, kuwa alikuwa na kiburi lakini sasa maneno yake ni ya busara, kwamba hakuwa anamsikiza mtu yeyote lakini sasa anaweza kuwasikiza wengine—mabadiliko haya ya nje hayawezi kusemwa kuwa ni mabadiliko katika tabia. Bila shaka mabadiliko katika tabia yanajumuisha hali hizi, lakini jambo lililo muhimu zaidi ni kuwa maisha yake ya ndani yamebadilika. Ukweli unaoonyeshwa na Mungu unakuwa maisha yake hasa, baadhi ya sumu za kishetani zilizo ndani zimetolewa, mtazamo wa mtu huyo umebadilika kabisa, na hakuna chochote kati ya hali hizo kinachokubaliana yale ya dunia. Anaona waziwazi njama na sumu za joka kubwa jekundu; amefahamu kiini cha kweli cha maisha. Kwa hivyo maadili ya maisha yake yamebadilika—hili ndilo badiliko la muhimu zaidi na kiini cha mabadiliko katika tabia.

kutoka katika “Tofauti Kati Ya Mabadiliko Ya Nje Na Mabadiliko Katika Tabia” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Katika ulimwengu wa dini, watu wengi huteseka pakubwa maishani mwao mwote, kwa kuihini miili yao au kuubeba msalaba wao, au hata kuteseka na kustahimili hadi pumzi zao za mwisho! Wengine huwa wanafunga hadi siku ya kifo chao. Katika maisha yao yote wanajinyima chakula kizuri na mavazi mazuri, wakisisitiza mateso tu. Wanaweza kuihini miili yao na kuinyima miili yao. Uwezo wao wa kustahimili mateso unastahili sifa. Ila fikira zao, mawazo yao, mielekeo yao ya kiakili, na kwa hakika asili yao ya kale—hakuna kati yavyo kilichoshughulikiwa hata kidogo. Hawajifahamu. Picha ya Mungu akilini mwao ni ya kijadi na ya kidhahania, Mungu asiye yakini. Uamuzi wao wa kuteseka kwa ajili ya Mungu unaletwa na azma na asili yao chanya. Hata ikiwa wanamwamini Mungu, hawamfahamu Mungu wala kuyafahamu mapenzi Yake. Wanamfanyia Mungu kazi na kumtesekea Mungu kama vipofu. Hawawekei utambuzi thamani yoyote na hawajishughulishi na jinsi ambayo huduma yao inatimiza mapenzi ya Mungu kwa kweli. Aidha hawajui jinsi ya kutimiza ufahamu kuhusu Mungu. Mungu wanayemhudumia si Mungu katika sura Yake ya asili, ila ni Mungu waliyejifikiria, Mungu waliyemsikia, au Mungu wa kihadithi wanayemsoma katika maandiko. Kisha wanatumia mawazo yao dhahiri na mioyo yao ya kiungu kumtesekea Mungu na kuifanya kazi ambayo Mungu anapaswa kufanya. Huduma yao haiko sahihi, kiasi kwamba hakuna anayemhudumia Mungu kwa njia inayotimiza mapenzi Yake. Haijalishi wako radhi kiasi gani kuteseka, mitazamo yao asilia ya huduma na picha ya Mungu akilini mwao havibadiliki kwani hawajapitia hukumu ya Mungu na kuadibu na usafishaji Wake na ukamilifu, na kwa sababu hakuna yeyote aliyewaongoza na ukweli. Japo wanasadiki kwa Yesu Mwokozi, hamna kati yao aliyewahi kumwona Mwokozi. Wamemsikia tu kwa hadithi na uvumi. Hivyo huduma yao ni sawa na kuhudumu mara mojamoja macho yao yakiwa yamefungwa kama kipofu anayemhudumia baba yake. Ni nini kinaweza kupatikana kutokana na huduma kama hiyo? Na ni nani anaweza kuikubali? Huduma yao haibadiliki kamwe toka mwanzo hadi mwisho. Wanapokea mafunzo ya kibinadamu na kukita huduma yao katika uasili wao na kile wanachokipenda wao. Hili laweza kuzalisha faida gani? Hata Petro, aliyemwona Yesu, hakujua jinsi ya kumhudumia Mungu kwa njia inayotimiza mapenzi ya Mungu. Ni katika uzee wake ndipo alipopata ufahamu. Hili linaonyesha nini kuhusu wanadamu vipofu ambao hawajapitia ushughulikiaji na hawana upogoaji na ambao hawajawahi kupata yeyote wa kuwaongoza? Je, si huduma ya wengi miongoni mwenu leo ni kama ile ya vipofu? Wale wote ambao hawajapokea hukumu, hawajapokea upogoaji na ushughulikiaji, na hawana mabadiliko—je, wao si waliokosa kushindwa kabisa? Wana manufaa gani watu kama hao? Ikiwa fikira zako, ufahamu wako wa maisha, na ufahamu wako wa Mungu hauonyeshi mabadiliko mapya na hautoi faida hata kidogo, hutatimiza chochote kizuri katika huduma yako. Bila maono na bila ufahamu mpya wa kazi ya Mungu, huwezi kuwa mtu aliyeshindwa. Njia yako ya kumfuata Mungu itakuwa kama ile ya wale wanaoteseka na kufunga—itakuwa ya thamani ndogo! Hii ni kwa sababu kuna ushuhuda kidogo katika yale wayafanyayo ndipo Nasema huduma yao ni bure! Kotekote katika maisha yao, hao watu huteseka, hukaa gerezani kwa muda, na kwa kila wakati, hustahimili, husisitiza mapenzi na ukarimu, na kubeba msalaba wao. Wanatukanwa na kukataliwa na ulimwengu na hupitia kila ugumu. Wanatii hadi mwisho ila bado hawapati ushindi na hawawezi kutoa ushuhuda wa kutwaliwa. Wameteseka si haba, ila kwa ndani hawamfahamu Mungu kabisa. Hakuna fikira zao za zamani, mawazo ya zamani, vitendo vyao, uelewa wa wanadamu, na mawazo ya wanadamu yaliyoshughulikiwa. Kamwe hakuna uelewa mpya ndani yao. Hakuna hata chembe ya ufahamu wao wa Mungu ambao ni wa kweli au ni sahihi. Wamekosa kuyaelewa mapenzi ya Mungu. Je, huku kwaweza kuwa kumhudumia Mungu? Japo ulimfahamu Mungu zamani, tuseme umeudumisha ufahamu huo hadi leo na kuendelea kukita ufahamu wako kuhusu Mungu kwenye fikira na mawazo yako bila kujali Mungu anafanya nini. Yaani, ikiwa huna ufahamu mpya na wa kweli kuhusu Mungu na ukose kutambua sura na tabia ya kweli ya Mungu. Ikiwa ufahamu wako wa Mungu bado unaongozwa na fikira za uhasama na ushirikina na bado una mawazo na fikira za mwanadamu. Ikiwa hii ndiyo hali, basi hujashindwa. Lengo langu la kukwambia maneno haya yote sasa ni kukupa fursa ya kufahamu na kutumia utambuzi huu kukuongoza katika ufahamu sahihi na mpya. Aidha yanalengwa kukuondolea mawazo ya zamani na utambuzi wa zamani ulio nao ili uweze kuwa na ufahamu mpya. Ikiwa unakula na kunywa matamshi Yangu kweli, basi ufahamu wako utabadilika kwa kiwango kikubwa. Bora tu udumishe moyo mtiifu kwa kula na kunywa matamshi ya Mungu, mtazamo wako utabadilika. Bora tu unaweza kukubali kuadibu kwa kila mara, fikira zako za zamani zitabadilika taratibu. Bora tu fikira zako za zamani zimebadilishwa kabisa na kuwa mpya, vitendo vyako vitabadilika ipasavyo. Kwa njia hii, huduma yako itaendelea kuwa yenye malengo zaidi, na itaweza kutimiza mapenzi ya Mungu. Ukibadilisha maisha yako, ufahamu wako wa maisha, na mawazo yako mengi kuhusu Mungu, basi uasili wako utadidimia taratibu. Hili, na hakuna jingine ila hili, ndilo tokeo baada ya Mungu kumshinda mwanadamu; haya ndiyo mabadiliko yatakayoonekana ndani ya mwanadamu. Ikiwa katika kumwamini Mungu, yote ujuayo ni kuutiisha na kuuhini mwili wako na kustahimili na kuteseka, na hujui wazi ikiwa unachokifanya ni sawa au la, bila kujali unamfanyia nani kazi, basi vitendo kama hivi vitaletaje mabadiliko?

kutoka katika “Ukweli wa Ndani wa Kazi ya Kushinda (3)” katika Neno Laonekana katika Mwili

Kila mara watu wa kidini kama hao wanapokusanyika, wanauliza, “Dada, umeshinda vipi siku hizi?” Anajibu, “Nahisi kuwa mimi ni mdeni wa Mungu na siwezi kuridhisha matakwa ya moyo Wake.” Mwingine anasema, “Mimi, pia, ni mdeni wa Mungu na nimeshindwa kumkidhi.” Sentensi na maneno haya machache pekee yanaonyesha mambo maovu yaliyo ndani ya nyoyo zao. Maneno kama hayo ni ya kuchukiza zaidi na yenye makosa sana. Asili ya watu kama hao inampinga Mungu. Wale ambao huzingatia uhalisi huwasilisha vyovyote vilivyomo katika nyoyo zao na kufungua mioyo yao katika mawasiliano. Hakuna shughuli hata moja ya uongo, hakuna heshima ama salamu na mazungumzo matupu. Wao daima huwa na uwazi na hawafuati sheria za duniani. Kuna wale ambao wako na upendeleo wa kujionyesha kwa nje, hata bila maana yoyote. Wakati mwingine anaimba, yeye anaanza kukatika, bila hata kugundua kuwa wali katika sufuria yake umeshaungua. Watu wa aina hii si wacha Mungu au waheshimiwa, bali ni watu wa kijinga kupindukia. Hizi zote ni maonyesho ya ukosefu wa ukweli! Wakati watu wengine wanawasiliana kuhusu masuala ya maisha katika roho, ingawa hawasemi kuhusu kuwa wadeni wa Mungu, wao hubaki na upendo wa kweli kwa Mungu ndani ya mioyo yao. Kuwa kwako mdeni kwa Mungu hakuhusiani na watu wengine; wewe ni mdeni kwa Mungu, si kwa mwanadamu. Kwa hiyo ina maana gani wewe daima kuzungumzia haya kwa watu wengine? Lazima uweke umuhimu kwa kuingia katika uhalisi, si kwa bidii au maonyesho ya nje.

Je, matendo mazuri ya kijuujuu ya mwanadamu yanawakilisha nini? Hayo huwakilisha mwili, na hata matendo yaliyo bora zaidi ya nje hayawakilishi maisha, ila tabia yako tu mwenyewe. Matendo ya nje ya mwanadamu hayawezi kutimiza matakwa ya Mungu. Wewe daima huzungumza kuhusu udeni wako kwa Mungu, lakini huwezi kuyaruzuku maisha ya wengine au kuwafanya wengine kumpenda Mungu. Je, unaamini kwamba matendo kama hayo yatamridhisha Mungu? Unaamini kwamba hii ndiyo matakwa ya moyo wa Mungu, kwamba haya ni ya roho, lakini kwa kweli huu ni ujinga! Unaamini kwamba yale yanayokupendeza wewe na unayotaka ni yale yanayomfurahisha Mungu. Je, yanayokupendeza yanaweza kuwakilisha yanayompendeza Mungu? Je, tabia ya mwanadamu inaweza kumwakilisha Mungu? Yale yanayokupendeza wewe ndiyo hasa yale humchukiza Mungu, na mienendo yako ni ile ambayo Mungu huchukia na kukataa. Kama unahisi kuwa wewe ni mdeni, basi nenda na usali mbele za Mungu. Hakuna haja ya kuzungumzia jambo hilo kwa watu wengine. Usipoomba mbele za Mungu na badala yake mara kwa mara unajivuta nadhari kwako mbele ya wengine, jambo hili linaweza kutimiza matakwa ya moyo wa Mungu? Kama matendo yako daima yanaonekana tu, hii ina maana kuwa wewe ni mtu bure zaidi ya wote. Ni mtu wa aina gani yule aliye na matendo mazuri ya kijuujuu tu lakini hana uhalisi? Watu kama hao ni Mafarisayo wanafiki na watu wa dini! Msipoacha matendo yenu ya nje na hamuwezi kufanya mabadiliko, basi dalili za unafiki ndani yenu zitazidi kuimarika. Kadiri dalili za unafiki zinavyozidi, ndivyo upinzani kwa Mungu unavyozidi, na mwishowe, watu wa aina hii hakika watatupiliwa mbali!

kutoka katika “Kumwamini Mungu Kunapaswa Kulenge Uhalisi, Si Kaida za Kidini” katika Neno Laonekana katika Mwili

Madondoo ya Mahubiri na Ushirika kwa ajili ya Marejeo:

Katika ulimwengu wa kidini, kuna wacha Mungu wengi, wao husema, “Tumebadilika kwa sababu ya imani yetu katika Bwana Yesu. Tunaweza kujitahidi kwa ajili ya Bwana, kutenda kazi, kuvumilia gerezani kwa ajili ya Bwana, na hatulikatai jina Lake mbele yawengine. Tunaweza kuyatenda mambo mengi mema, kufadhili, kuchanga na kuwasaidia maskini. Haya ni mabadilikomakubwa! Tumebadilika, ndiyo sababu tunafaa kumngojea Bwana ili atulete katika ufalme wa mbinguni.” Je, mnafikiria nini juu ya maneno haya? Je, mna ufahamu wowote ijapo kwa maneno haya? Je, kutakaswa kunamaanisha nini? Je, unafikiria kwamba kama tabia yako imebadilika na unatenda matendo mema basi umetakaswa? Mtu mwingine husema, “Nimeacha kila kitu.” Hata Nimeiacha kazi yangu ulimwenguni, familia yangu na tamaa za mwili ili kujitahidi kwa ajili ya Mungu. Je, hii ni sawa na kutakaswa? Ingawa umeyatenda haya yote, huu si ushahidi thabiti kwamba umetakaswa. Hivyo, jambo muhimu ni lipi? Je, ni katika kipengele kipi unaweza kupata kutakaswa kunakoweza kuchukuliwa kama kutakaswa halisi? Kutakaswa kwa tabia ya kishetani ambayo humpinga Mungu. Sasa, udhihirisho wa tabia ya kishetani ambao humpinga Mungu ni upi? Je, udhihirisho ulio wazi zaidi ni upi? Kiburi cha mtu, majivuno, haki ya kibinafsi, na kujidai mwenyewe, pamoja na upotovu, hila, kusema uongo, udanganyifu na unafiki. Wakati mambo haya si sehemu ya mtu tena, basi kwa kweli ametakaswa. Kuna madhihirisho 12. Acheni tulitazame kila mojawapo ya haya madhihirisho 12: mtu mwenyewe kujiona kuwa mwenye kuheshimika zaidi; kuwaruhusu wale ambao hunitiiMimi kustawi na wale ambao hunipinga Mimikuangamia; kufikiria tu kuwa Mungu ndiye mkuu zaidi kukushinda, kutomnyenyekea mtuyeyote, kutowajali wengine; kufanyiza ufalme wa kibinafsi mara tu unapokuwa na uwezo; kutaka kuwa mtawala wa pekee na mjua yote na kuyaamua mambo wewe mwenyewe. Huu udhihirisho wote ni tabia za kishetani. Tabia hizi za kishetani lazima zitakaswe kabla ya mtu kuyapitia mabadiliko katika tabia ya maisha yake. Mabadiliko katika tabia ya maisha ya mtu ni kuzaliwa upya kwa sababu kiini chake kimebadilika. Awali, wakati alipopewa uwezo, aliweza kuunda ufalme wa kibinafsi. Sasa, wakati anapopewa uwezo, yeye humhudumia Mungu, humshuhudia Mungu na huwa mtumishi wa wateule wa Mungu. Je, haya siyo mabadiliko halisi? Awali, aliringa mwenyewe katika hali zote na aliwataka watu wengine wamheshimu na kumwabudu. Sasa, yeye humshuhudia Mungu kila mahali, hajishughulishi tena. Bila kujali wanavyonishughulikia watu, ni vyema. Bila kujali watu wanasema nini juu yangu, ni vyema. Sijali. Ninataka tu kumtukuza sana Mungu, kumshuhudia Mungu, kuwasaidia wengine wapate ufahamu wa Mungu, na kuwasaidia wengine watii mbele za uwepo wa Mungu. Je, haya si mabadiliko katika tabia ya maisha? “Nitawashughulikia ndugu kwa upendo. Nitawahurumia wengine katika hali zote. Katika mambo yote, sitajifikiria, nitawafikiria tu wengine. Nitawasaidia wengine kuyastawisha maisha yao na kuyatimiza majukumu yangu. Nitawasaidia wengine kuupata ukweli na kuufahamu ukweli.” Hii ndio maana ya kuwapenda watu, kuwapenda wengine kama mwenyewe! Kumhusu Shetani, unaweza kumtambua, kuwa na kanuni, kuwa na mipaka naye na kuyafunua maovu ya Shetani kabisa ili wateule wa Mungu wasipatwe na madhara yake. Huku ni kuwalinda wateule wa Mungu, na huku ni kuwapenda wengine zaidi kama mwenyewe. Zaidi ya hayo, unapaswa kukipenda ambacho Mungu hukipenda na kukichukia ambacho Mungu hukichukia. Je, basi, Mungu hukichukia nini? Yeye huwachukia wapinga Kristo, pepo waovu, na watu waovu. Hilo linamaanisha kuwa sisi pia tunapaswa kuwachukia wapinga Kristo, pepo waovu na watu waovu. Lazima tusimame upande wa Mungu. Hatuwezi kupatana nao. Mungu huwapenda wale ambao Yeye hutaka kuwaokoa na kuwabariki. Kuhusu watu hawa, lazima tuwajibike, tuwashughulikie kwa upendo, tuwasaidie, tuwaelekeze, tuwakimu na kuwahimili wao. Je, haya si mabadiliko katika tabia ya maisha ya mtu? Zaidi ya hayo, wakati umetenda dhambi au makosa fulani, au umetelekeza kanuni katika kulitenda jambo fulani, unaweza kukubali ukosoaji wa ndugu, kukaripia, kushughulikia na kupogoa; unaweza kuyapokea mambo haya yote kutoka kwa Mungu, usiwe na kinyongo, na uutafute ukweli ili kuusuluhisha upotovu wako. Je, haya si mabadiliko katika tabia yako ya maisha? Ndio, ni mabadiliko. …

Je, mabadiliko katika mwenendo ambao unazungumziwa katika ulimwengu wa kidini huwakilisha mabadiliko katika tabia ya maisha? (Hapana, hauwezi.) Kwa nini mabadiliko katika mwenendo wa mtu hayawezi kuwakilisha mabadiliko katika tabia yake ya maisha? Sababu muhimu ni kuwa bado anampinga Mungu. Unaweza kuyaona hayo kwa nje, Mafarisayo walikuwa wacha Mungu sana, waliomba, waliyaelezea maandiko na walizifuata kanuni za sheria vizuri sana. Ingeweza kusemwa kwamba kwa nje, hawakufedheheka. Watu hawakuweza kuyaona makosa. Hata hivyo, kwa nini bado waliweza kumpinga na kumshutumu Kristo? Je, hili linaonyesha nini? Hawakuwa na ukweli na hawakumjua Mungu. Kwa nje, walikuwa wazuri sana, lakini hawakuwa na ukweli, hii ndiyo sababu waliweza kumpimga Mungu. Kama walikuwa wazuri sana kwa nje, kwa nini hili halichukuliwi kama mabadiliko katika tabia ya maisha? Hii ni kwa sababu bado walikuwa wenye kiburi, wenye majivuno na hasa wenye unyoofu. Waliyaamini maarifa yao, nadharia na ufahamu wa maandiko. Waliamini kwamba walifahamu kila kitu na kwamba walikuwa bora kuliko watu wengine. Hii ndiyo sababu wakati ulimwengu wa kidini unasikia kwamba Kristo wa siku za mwisho ameuelezea ukweli wote, wanamshutumu Yeye ingawa wanajua kwamba ni ukweli.

kutoka katika Mahubiri na Ushirika Kuhusu Kuingia Katika Maisha, Juzuu ya 138

Jumanne, 5 Machi 2019

Uhusiano Wako Na Mungu Ukoje

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, wafuasi wa Kristo

Uhusiano Wako Na Mungu Ukoje

Mwenyezi Mungu alisema, Katika kuwa na imani kwa Mungu, ni lazima angalau utatue swala la kuwa na uhusiano wa kawaida na Mungu. Bila uhusiano wa kawaida na Mungu, basi umuhimu wa kumwamini Mungu unapotea. Kuunda uhusiano wa kawaida na Mungu kunapatikana kikamilifu kupitia kuutuliza moyo wako mbele ya Mungu. Uhusiano wa kawaida na Mungu unamaanisha kuweza kutoshuku au kukataa kazi yoyote ya Mungu na kutii, na zaidi ya hayo unamaanisha kuwa na nia sahihi mbele ya Mungu, sio kufikiria kujihusu, daima kuwa na maslahi ya familia ya Mungu kama jambo muhimu zaidi haijalishi kile unachofanya, kukubali kutazamiwa na Mungu, na kukubali mipangilio ya Mungu. Una uwezo wa kuutuliza moyo wako mbele ya Mungu kila unapofanya chochote; hata kama huelewi mapenzi ya Mungu, bado ni lazima utimize wajibu na majukumu yako kadri ya uwezo wako. Hujachelewa sana kusubiri mapenzi ya Mungu yafichuliwe kwako na kisha kuyaweka katika vitendo. Wakati uhusiano wako na Mungu umekuwa wa kawaida, basi pia utakuwa na uhusiano wa kawaida na watu. Kila kitu kimejengwa juu ya msingi wa maneno ya Mungu. Kupitia katika kula na kunywa maneno ya Mungu, tenda kulingana na mahitaji ya Mungu, weka sawa maoni yako, usitende mambo yanayompinga Mungu au kuingilia kati mambo ya kanisa. Usifanye vitu visivyo na manufaa kwa maisha ya ndugu, usiseme maneno yasiyosaidia wengine, usifanye vitu vya kufedhehesha. Kuwa mwadilifu na mwenye heshima unapofanya mambo yote na kuyafanya ya kupendeza mbele ya Mungu. Hata ingawa kutakuwa na nyakati ambazo mwili ni dhaifu, unaweza kushikiza umuhimu mkubwa kabisa kwa kufaidi familia ya Mungu, kutotamani faida yako mwenyewe, na kutekeleza haki. Ikiwa unaweza kutenda kwa njia hii, uhusiano wako na Mungu utakuwa wa kawaida.
Kila unapofanya chochote, lazima uchunguze iwapo motisha yako ni sahihi. Ikiwa unaweza kutenda kulingana na matakwa ya Mungu, basi uhusiano wako na Mungu utakuwa wa kawaida. Hiki ndicho kigezo cha chini zaidi. Iwapo, unapochunguza motisha yako, kunatokea zile zisizo sahihi, na iwapo unaweza kuzikwepa na kutenda kulingana na maneno ya Mungu, basi utakuwa mtu ambaye ni mwema mbele ya Mungu, kitu ambacho kitaonyesha kuwa uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida, na kwamba kila unachofanya ni kwa ajili ya Mungu, na sio kwa sababu yako binafsi. Ni lazima uuweke moyo wako sawa kila unapofanya ama kusema chochote, uwe mwenye haki katika matendo yako, na usiongozwe na hisia zako, au utende kulingana na mapenzi yako: Haya ndiyo maadili ambayo wale wanaoamini katika Mungu wanatenda kulingana nayo. Motisha za mtu na kimo chake vinaweza kufichuliwa katika kitu kidogo, na hivyo, kwa watu kuingia kwa njia ya kufanywa wakamilifu na Mungu, ni lazima kwanza wasuluhishe motisha yao wenyewe na uhusiano wao na Mungu. Ni pale ambapo tu uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida ndipo utaweza kufanywa mkamilifu na Mungu, na ni hapo tu ndipo ushughulikiaji, upogoaji, nidhamu, na usafishaji wa Mungu kwako utaweza kupata matokeo yanayotakiwa. Hiyo kusema, watu wanaweza kuwa na Mungu mioyoni mwao, wasitafute maslahi binafsi, wasifikirie kuhusu maisha yao binafsi ya baadaye (ikirejelea kufikiri juu ya mwili), lakini badala yake wanabeba mzigo wa kuingia katika maisha, wanajitahidi wawezavyo kutafuta ukweli, na kuitii kazi ya Mungu. Kwa namna hii, makusudi unayoyatafuta ni sahihi, na uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida. Inaweza kusemwa kwamba kuutengeneza uhusiano wako na Mungu ndiyo hatua ya kwanza ya kuingia katika safari yako ya kiroho. Ingawa kudura ya mtu iko mikononi mwa Mungu, na imeshaamuliwa kabla na Mungu, na haiwezi kubadilishwa na yeye mwenyewe, kwamba unaweza au huwezi kufanywa mkamilifu au kupatwa na Mungu kunategemea na kama uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida au la. Pengine kuna sehemu yako ambazo ni dhaifu au zenye kutotii—lakini bora tu mtazamo wako ni sawa na motisha zako ni sahihi, na bora tu umeuweka uhusiano wako na Mungu sawa na kuufanya wa kawaida, basi utastahili kufanywa mkamilifu na Mungu. Iwapo huna uhusiano sahihi na Mungu, na unatenda kwa ajili ya mwili, au familia yako, basi haijalishi unafanya kazi kwa bidii vipi, itakuwa bure. Iwapo uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida, basi kila kitu kingine kitakuwa sawa. Mungu haangalii chochote kingine, bali Anaangalia tu iwapo mitazamo yako kuhusu kuamini kwa Mungu ni sawa: unayemwamini, ni kwa ajili ya nani unaamini, na ni kwa nini unaamini. Iwapo unaweza kuona vitu hivi kwa udhahiri, na unaweza kuweka mitazamo yako na matendo, basi maisha yako yatapiga hatua, na una uhakika wa kuweza kuingia kwa njia sahihi. Iwapo uhusiano wako na Mungu sio wa kawaida, na mitazamo yako kuhusu kuamini katika Mungu inaacha maadili, basi haya yatazuia mengine yote. Haijalishi jinsi unavyoamini katika Mungu, hutafaidi chochote. Iwapo tu uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida ndipo utasifiwa na Mungu unapokwepa mwili, unapoomba, unapoteseka, unapostahimili, unapotii, unapowasaidia ndugu zako, unaweka juhudi zaidi kwa Mungu, na kadhalika. Hiyo kusema, watu wanaweza kuwa na Mungu mioyoni mwao, wasitafute maslahi binafsi, wasifikirie kuhusu maisha yao binafsi ya baadaye (ikirejelea kufikiri juu ya mwili), lakini badala yake wanabeba mzigo wa kuingia katika maisha, wanajitahidi wawezavyo kutafuta ukweli, na kuitii kazi ya Mungu. Kwa namna hii, makusudi unayoyatafuta ni sahihi, na uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida. Inaweza kusemwa kwamba kuutengeneza uhusiano wako na Mungu ndiyo hatua ya kwanza ya kuingia kwako katika safari ya kiroho. Ingawa hatima yako iko mikononi mwa Mungu, na imeshaamuliwa kabla na Mungu, na haiwezi kubadilishwa na wewe mwenyewe, kwamba unaweza au huwezi kufanywa mkamilifu au kupatwa na Mungu kunategemea na kama uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida au la. Pengine kuna sehemu ndani yako ambazo ni dhaifu au zenye kutotii—lakini bora tu mtazamo wako wa nje ni sawa na motisha yako ni sahihi, na bora tu umeuweka uhusiano wako na Mungu sawa na kuufanya wa kawaida, basi utafuzu kufanywa mkamilifu na Mungu. Iwapo huna uhusiano sahihi na Mungu, na unatenda kwa ajili ya mwili, au familia yako, basi haijalishi kiwango cha kazi unayofanya kwa bidii, itakuwa bure. Iwapo uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida, basi kila kitu kingine kitakuwa sawa. Mungu haangalii chochote kingine, bali anaangalia tu iwapo mitazamo yako kwa kuamini kwa Mungu ni sawa: unayemwamini, ni kwa ajili ya nani unaamini, na ni kwa nini unaamini. Iwapo unaweza kuona vitu hivi kwa udhahiri, na unaweza kuweka mitazamo yako iwe sawa na kuweza kutenda, basi maisha yako yatapiga hatua, na una uhakika wa kuweza kuingia kwenye njia sahihi. Iwapo uhusiano wako na Mungu sio wa kawaida, na mitazamo yako kwa kuamini katika Mungu inakiuka maadili, basi haya yatazuia mengine yote. Haijalishi jinsi unavyoamini katika Mungu, hutafaidi chochote. Iwapo tu uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida ndipo utasifiwa na Mungu unapoupa mwili kisogo, unapoomba, unapoteseka, unapostahimili, unapotii, unapowasaidia ndugu na dada zako, unaweka juhudi zaidi kwa Mungu, na kadhalika. Iwe kitu unachofanya kina thamani na umuhimu au hakina hutegemea iwapo makusudi yako ni sahihi na iwapo mitazamo yako ni sahihi. Siku hizi, imani ya watu wengi kwa Mungu ni kama kutazama saa kubwa huku vichwa vyao vikiwa vimeelekezwa upande mmoja—mitazamo yao imekengeuka. Kila kitu kitakuwa kizuri ikiwa mwelekeo mpya unaweza kufanyika hapa, kila kitu kitakuwa sawa ikiwa hili litatatuliwa, wakati hakutafanyika kitu ikiwa hili halitatatuliwa. Baadhi ya watu wanakuwa na tabia nzuri katika uwepo Wangu, lakini nyuma Yangu kile wanachofanya ni kupinga. Haya ni maonyesho yaliyopotoka na ya udanganyifu na aina hii ya mtu ni mtumwa wa Shetani, ni mfano halisi wa namna ile ile ya Shetani kumjaribu Mungu. Wewe ni mtu sahihi tu ikiwa unaweza kuitii kazi Yangu na maneno Yangu. Ilimradi unaweza kula na kunywa maneno ya Mungu, ilimradi kila kitu unachofanya kinapendeza mbele ya Mungu, ilimradi hufanyi mambo ya aibu, usifanye mambo ambayo yanaweza kuhatarisha maisha ya watu, ilimradi unaishi katika mwanga, hunyonywi na Shetani, basi uhusiano wako na Mungu utawekwa sawa.
Katika kumwamini Mungu, makusudi na mitazamo yako yanapaswa kuwekwa sawa; unapaswa kuwa na ufahamu sahihi na utendeaji sahihi wa maneno ya Mungu, kazi ya Mungu, mazingira yaliyopangwa na Mungu, mtu aliyeshuhudiwa na Mungu, na wa Mungu wa vitendo. Hupaswi kutenda kulingana na mawazo yako binafsi, au kufanya mipango yako midogo mwenyewe. Unapaswa kuweza kutafuta ukweli katika kila kitu na kusimama katika sehemu yako kama uumbaji wa Mungu na kuzitii kazi zote za Mungu. Kama unataka kutafuta kukamilishwa na Mungu na kuingia katika njia sahihi ya maisha, basi moyo wako siku zote unapaswa kuishi katika uwepo wa Mungu, usiwe fisadi, usimfuate Shetani, usimwachie Shetani fursa yoyote kufanya kazi yake, na usimruhusu Shetani kukutumia. Unapaswa kujitoa kikamilifu kwa Mungu na kumwacha Mungu akutawale.
Upo radhi kuwa mtumishi wa Shetani? Upo radhi kunyonywa na Shetani? Je, unamwamini Mungu na kumtafuta Mungu ili kwamba uweze kukamilishwa na Yeye, au ni ili uwe foili[a] katika kazi ya Mungu? Je, upo radhi kupatwa na Mungu na kuishi maisha ya maana, au upo radhi kuishi maisha tupu na yasiyo na thamani? Upo radhi kutumiwa na Mungu, au kunyonywa na Shetani? Upo radhi kuacha maneno ya Mungu na ukweli kukujaza, au kuacha dhambi na Shetani kukujaza? Litafakari na kulipima hili. Katika maisha yako ya kila siku, unapaswa kuyaelewa maneno hayo uyasemayo na mambo hayo uyafanyayo ambayo yatasababisha uhusiano wako na Mungu kuwa usio wa kawaida, halafu ujirekebishe na kuingia katika tabia sahihi. Yachunguze maneno yako, vitendo vyako, kila mwenendo wako, na fikra zako na mawazo wakati wote. Ielewe hali yako ya kweli na ingia katika njia ya kazi ya Roho Mtakatifu. Ni kwa njia hii tu ndipo unaweza kuwa na uhusiano wa kawaida na Mungu. Kwa kupima iwapo uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida, utaweza kurekebisha makusudi yako, kuielewa asili ya mwanadamu, na kujielewa mwenyewe; kupitia hili, utaweza kuingia katika uzoefu halisi, na kujinyima kwa kweli, na kupata utiifu wa makusudi. Katika masuala hayo kama unapokuwa unapitia iwapo uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida, utaweza kupata fursa za kukamilishwa na Mungu, utaweza kuelewa hali nyingi, ambazo kwazo Roho Mtakatifu Anafanya kazi, na utaweza kubaini mengi ya udanganyifu na njama za Shetani. Ni kupitia njia hii tu ndipo unaweza kukamilishwa na Mungu. Unaweka uhusiano wako na Mungu sawa ili kwamba ujisalimishe mwenyewe mipangilio yote ya Mungu. Ni ili utaingia kwa kina zaidi katika uzoefu halisi, na kupata kazi zaidi ya Roho Mtakatifu. Unafanya mazoezi ya kuwa na uhusianao wa kawaida na Mungu, muda mwingi, utapata huu kupitia kuunyima mwili na kupitia ushirikiano wako wa kweli na Mungu. Unapaswa kuelewa kwamba "bila moyo wa ushirikiano, ni vigumu kupokea kazi ya Mungu; ikiwa mwili haupati mateso, hakuna baraka kutoka kwa Mungu; ikiwa roho haihangaiki, Shetani hataaibishwa." Ikiwa unazitenda na kuzielewa vizuri kanuni hizi, mitazamo yako juu ya imani kwa Mungu itawekwa sawa. Katika matendo yenu ya sasa, mnapaswa kuacha mtazamo wa "kutafuta mkate ili kutuliza njaa," mnapaswa kuacha mtazamo wa "kila kitu kinafanywa na Roho Mtakatifu na watu hawawezi kuingilia." Watu wanaozungumza namna hii wote wanafikiri, "Watu wanaweza kufanya chochote kile ambacho wako radhi kukifanya, na muda utakapofika Roho Mtakatifu atafanya kazi na watu hawatakuwa na haja ya kuushinda mwili, hawatakuwa na haja ya kushirikiana, watakuwa wanahitaji tu Roho Mtakatifu kuwashawishi." Mitazamo hii yote ni ya kipuuzi. Katika mazingira haya, Roho Mtakatifu hawezi kufanya kazi. Ni mtazamo wa aina hii ndio unakuwa kizuizi kikubwa kwa kazi ya Roho Mtakatifu. Mara nyingi, kazi ya Roho Mtakatifu inapatikana kupitia ushirikiano wa watu. Bila ushirikiano na kudhamiria, basi kutaka kubadilisha tabia ya mtu, kupata kazi ya Roho Mtakatifu, na kupata mwangaza na nuru kutoka kwa Mungu zote ni fikra za kupita kiasi; hii inaitwa "kujifurahisha mwenyewe na kumsamehe Shetani." Watu kama hawa hawana uhusiano wa kawaida na Mungu. Umepata dalili nyingi za Shetani ndani yako, na katika matendo yako ya zamani, kuna mambo mengi ambayo yamepingana na matakwa ya sasa ya Mungu. Je, unaweza kuyatelekeza sasa? Pata uhusiano wa kawaida na Mungu, fanya kulingana na makusudi ya Mungu, kuwa mtu mpya na kuwa na maisha mapya, usitazame dhambi zako za zamani, usiwe mwenye majuto kupita kiasi, kuwa na uwezo wa kusimama na kushirikiana na Mungu, na kutimiza majukumu ambayo unapaswa kufanya. Kwa njia hii, uhusiano wako na Mungu utakuwa wa kawaida.
Ikiwa unakubali tu maneno haya kwa mdomo baada ya kuyasoma lakini hayajaingia moyoni mwako, na huko makini kuhusu kuwa na uhusiano wa kawaida na Mungu, basi inathibitisha kwamba huweki umuhimu mkubwa kwenye uhusiano wako na Mungu, mitazamo yako bado haijawekwa sawa, makusudi yako bado hayajaelekezwa kwa kumruhusu Mungu akupate, na kumkubalia Mungu utukufu, badala yake yameelekezwa kwa kuruhusu njama za Shetani kushinda na kwa kupata malengo yako binafsi. Watu wa aina hii wote wana makusudi na mitazamo isiyo sahihi. Bila kujali kile ambacho Mungu amesema au namna kilivyosemwa, hawajali na hakuna mabadiliko yanayoweza kuonekana. Mioyo yao haihisi woga wowote na hawaoni aibu. Mtu wa aina hii ni mtu aliyekanganyikiwa bila roho. Kwa kila tamshi la Mungu, baada ya kulisoma na kupata ufahamu, utaliweka katika vitendo. Bila kujali ulivyokuwa ukitenda kabla—pengine huko nyuma mwili wako ulikuwa dhaifu, ulikuwa muasi, na ulipinga—hili silo jambo kubwa, na haliwezi kuzuia maisha yako yasikue leo. Ilimradi unaweza kuwa na uhusiano wa kawaida na Mungu leo, basi kuna tumaini. Ikiwa kwa kila wakati unaposoma maneno ya Mungu, unakuwa na mbadiliko na kuruhusu watu wengine kuona kwamba maisha yako yamebadilika kuwa mazuri, inaonyesha kwamba una uhusiano wa kawaida na Mungu na kwamba umewekwa sawa. Mungu hashughulikii watu kulingana na dhambi zao. Ilimradi unaweza kutoasi tena na hupingi tena baada ya wewe kuelewa na kufahamu, basi Mungu atakuwa bado Ana huruma na wewe. Unapokuwa na ufahamu huu na nia ya kutafuta kukamilishwa na Mungu, basi hali yako katika uwepo wa Mungu itakuwa ya kawaida. Bila kujali unachofanya, zingatia: Mungu atafikiri nini ikiwa nitafanya hiki? Kitawaathiri vipi ndugu? Chunguza makusudi yako katika maombi, ushirika, usemi, kazi na kuhusiana na watu, na chunguza endapo uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida au si wa kawaida. Ikiwa huwezi kutofautisha makusudi yako na fikra zako, basi huna ubaguzi, kitu ambacho kinathibitisha kwamba unaelewa kidogo sana kuhusu ukweli. Kuwa na ufahamu ulio wazi wa kila kitu ambacho Mungu hufanya, vitazame vitu kulingana na neno la Mungu na vitazame vitu kwa kusimama katika upande wa Mungu. Kwa njia hii mitazamo yako itakuwa sahihi. Kwa hiyo, kujenga uhusiano mzuri na Mungu ni kipaumbele cha juu kwa mtu yeyote anayemwamini Mungu; kila mtu anapaswa kuichukulia kama kazi muhimu na kama tukio lao kubwa la maisha. Kila kitu unachofanya kinapaswa kipimwe dhidi ya iwapo una uhusiano wa kawaida na Mungu au la. Ikiwa uhusianao wako na Mungu ni wa kawaida na makusudi yako ni sahihi, basi kifanye. Ili kudumisha uhusiano wa kawaida na Mungu, hupaswi kuogopa kupoteza maslahi binafsi, hupaswi kumruhusu Shetani kushinda, hupaswi kumruhusu Shetani kupata kitu dhidi yako, na hupaswi kumruhusu Shetani kukufanya uwe kichekesho. Kusudi kama hili ni udhihirisho kwamba uhusiano wako na Mungu ni wa kawaida. Si kwa ajili ya mwili, badala yake ni kwa ajili ya amani ya roho, ni kwa ajili ya kupata kazi ya Roho Mtakatifu na kwa ajili ya kuyaridhisha mapenzi ya Mungu. Ili kuingia katika hali sahihi, unapaswa kujenga uhusiano mzuri na Mungu, unapaswa kuweka sawa mtazamo wako wa imani kwa Mungu. Ni kumruhusu Mungu kukupata, kumruhusu Mungu kufichua matunda ya maneno Yake kwako na kukuangazia na kukupatia nuru zaidi. Kwa namna hii utaingia katika tabia nzuri. Endelea kula na kunywa maneno ya Mungu ya sasa, ingia katika njia ya sasa ya kazi ya Roho Mtakatifu, fanya kulingana na matakwa ya Mungu ya sasa, usifuate mazoea ya kale, using'ang'anie njia za zamani za kufanya mambo, na haraka ingia katika namna ya kazi ya leo. Kwa njia hii uhusiano wako na Mungu utakuwa wa kawaida kabisa na utaingia katika njia sahihi ya kumwamini Mungu.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Ijumaa, 8 Februari 2019

Imani Tatu katika Mungu wa Vitendo

Sura ya 16. Imani Tatu katika Mungu wa Vitendo

Ndani ya familia ya Mungu, kuna imani kadhaa tofauti katika Mungu; imani hizi tofauti lazima zitambulishwe ili kuona wewe ni wa gani.
Na imani ya aina ya kwanza, ambayo pia ni aina bora zaidi, mtu huyo ana uwezo wa kuyaamini maneno ya Mungu katika vitu vyote; ana uwezo wa kukubali ufichuzi wote wa Mungu, ushugulikiaji, na upogoaji; yeye ni mwagalifu kwa mapenzi ya Mungu, hupenda, ni mwaminifu kwa, na humwabudu Mungu, na ako tayari kutenda ukweli. Imani kama hiyo huzaa maisha, na inawezesha mtu kupata mabadiliko katika tabia na kupatwa na Mungu.
Na imani ya aina ya pili, mtu huyo anamwamini Mungu kwa kiasi, lakini pia ni mwenye tuhumu kwa kiasi. Wakati kazi ya Mungu hairidhiani na yeye, angefanya ulinganishi katika moyo wake, akiwa na shaka kama Mungu Anapaswa kuwa akifanya vitu kama hivyo. Mara kwa mara anamtuhumu Mungu, kwa hivyo ana uwezo tu wa kumtii Mungu kwa kiasi, na hana uwezo wa kumtii Mungu katika vitu vingine; anaweza kulitii lile ambalo analiamini ni sawa, lakini ana mawazo yake mwenyewe anapokabiliwa na vitu ambavyo anahisi si sawa, na migongano katika moyo wake, na anakataa kuyatekeleza. Hili pia ni aina ya imani. Kimo cha watu siku hizi ni hasa kama hiki, wao wana uwezo tu wa kutii kile wanachohisi kuwa sawa, wao hawana uwezo wa kutii kile wanachohisi si sawa, na hawatatekeleza kile ambacho hawako tayari kufanya. Kadhalika, wakati mwingine hali ikiwa, wana shauku na Mungu, wakihisi kwamba wanapaswa kuwa waangalifu kwa mzigo wa Mungu, hivyo wanatimiza wajibu wao; au wakati mwingine wanashughulishwa na ushirika, wanapata Mungu kuwa wa kupendeka kabisa, na sasa tu ndio wenye imani katika Mungu kwa kiasi fulani. Hasa, imani yao katika Mungu ni tu kufuata umati; hawana upendo kwa Mungu, wala si waangalifu kwa Mungu, wakati bila shaka hawamtii na hawamwabudu Mungu kwa kweli. Kwa watu walio na imani kama hii katika Mungu, wako tu na kiasi cha wastani cha upendo, uangalifu, na utiifu kwa Mungu, kwa muda fulani, na inafanyika tu wakati Roho Mtakatifu hasa Anasonga, wakati Roho Mtakatifu anafanya kazi Yake. Wakati wako katika hali mbaya, au wakati wanachanganywa na wengine, wakati wao ni dhaifu na wamekata tamaa, vitu hivi vimeenda, vimetokomea, wakati wao wenyewe hawana habari jinsi hilo limekuja kupita. Hawana uwezo tena wa kumpenda Mungu hata wakitaka, hawana motisha ya kutenda maneno ya Mungu tena, na kisha wanaona kazi ya Mungu kama ya desturi sana, ya kawaida sana; hata kama wao hawana tuhuma tena, wao hawana ari yoyote tena. Kimo cha watu wengi zaidi kiko katika hatua hii, na hii ndiyo aina ya pili ya imani.
Na aina ya tatu ya imani, mtu hana uelewa wa Mungu mwenye mwili, kwake Yeye hujitokeza tu kama mtu wa kawaida, na hakuna tofauti kubwa inaweza kutambulishwa. Kwa hivyo, anamchukulia Mungu mwenye mwili kama tu mtu wa kawaida lakini mwenye cheo cha heshima, ana uwezo wa kufuatana na Mungu na kusema kitu kizuri, na pia ana uwezo wa kuandamana katika imani, lakini imani hii si imani halisi. Ana uwezo wa kufuatana na mambo ya upuuzi mara moja moja, lakini hakuna upendo kwa Mungu katika mtu wa aina hii—upendo si kujali kuhusu mwili lakini utiifu wa kweli katika kazi ya mtu na katika kutimiza wajibu wa mtu, kuwa mwangalifu kwa Mungu na kumcha Mungu. Upendo kwa Mungu ni kitu ambacho mtu aliye na uzoefu mkubwa tu anaweza kutangaza, si kitu ambacho mtu anaweza kusema kwa kupitia tu, kuona kwamba mtu ametekwa na hisia kali hivyo kusema kwamba huyu na huyu humpenda Mungu sana. Ama kusema kwamba watu kutoka dhehebu fulani humpenda Mungu kwa kweli. Huu ni upuuzi. Mtu kama huyu hawezi kukubali na kutii kwa urahisi kunapokuja kwa mambo ya upuuzi, na anapokabiliwa na mambo ya muhimu yanayohusiana na ukweli, hawezi kutii tu, na pia ana mawazo yake mwenyewe, hata anakuwa na tuhuma kuhusu Mungu. Watu kama hawa pia wako katika walio wengi. Wao ni wenye tuhuma kila wakati kuhusu Mungu: Je, huyu ni Mungu? Je, ni kwa nini Yeye hafanani na Mungu? Baadhi ya mambo Alivyosema labda yameelekezwa na Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu alimwelekeleza kusema mambo fulani, na kufanya vitu fulani. …Imani ya watu kama hawa ni ya kusikitisha zaidi.
Kiwango cha imani ya mtu katika Mungu, utiifu kwa Mungu, upendo, uangalifu, na uchaji kwa Mungu, kinatambulishwa hasa na yafuatayo:
Kwanza, kina msingi katika ikiwa mtu huyo hupenda ukweli. Kama unapenda ukweli basi unaweza kuendelea kuufuatilia zaidi, kisha unaweza kulenga kuwa na uelewa wa ukweli, wa maneno ya Mungu, wa kazi ya Mungu, wa umuhimu wa kupata mwili kwa Mungu, wa tabia ya Mungu, na uelewa wa Mungu una msingi hasa katika hiki kitu kimoja. Kadiri Unavyoweza kuelewa Mungu zaidi ndivyo unavyoweza kumtambua zaidi; kadiri unavyoweza kumwelewa Mungu zaidi ndivyo unavyoweza kumfuata bila kuyumbayumba. Hiyo ni, uelewa wa Mungu una msingi katika kufuatilia ukweli.
Pili, kina msingi katika uelewa wa mtu huyo wa Mungu mwenye mwili, hiyo ni muhimu. Bila uelewa wa Mungu wa vitendo, mazungumzo ya kumtii Mungu, kumpenda Mungu, kushuhudia Mungu, na kumhudumia Mungu yote ni maneno matupu. Vitu kama hivi haviwezi tu kufikiwa.
Tatu, kina msingi katika ubinadamu wa mtu huyo, lakini hili si halisi. Kwa sababu, baadhi ya watu wana ubinadamu mzuri, wao ni watu wazuri, lakini wao hawapendi ukweli. Kama wao hawana uelewa kabisa wa Mungu mwenye mwili, basi imani yao haiwezi kusiama, na wakati mwingine nia zao nzuri bila kujua husababisha madakizo. Je, unaweza kusema kwamba wao ni watu ambao wanamwamini Mungu kwa kweli? Wao ni wenye shauku, ni wa asili nzuri, na hufanya mambo fulani mazuri, lakini haya ni tabia nzuri tu ya nje, haya ni sura ya juu juu, haya hayaonyeshi kwamba imani yao ni halisi. Ukisema kwamba kwa kweli unamwamini Mungu, kweli unampenda Mungu, lazima uwe na uwezo wa kusema kwa nini unampenda Mungu, upendo wako kwa Mungu una msingi kwa nini, kwa nini unamwamini Yeye, kama wewe unaufuata umati tu ama unamwamini Yeye kwa sababu unaweza kumwona kwa kweli kama Mungu, imani na upendo wako kwa Mungu yana msingi katika ukweli upi: Haya lazima yategemezwe kwa misingi. Baadhi ya watu hupenda kusema kwamba wanamwamini Mungu kwa kweli na wanampenda Mungu, lakini wakati mtu anatamani kuwasiliana nao ukweli kwa uzito, hawana kitu cha kusema. Nimesikia watu wengi wakisema: “Mimi husikiza chochote ambacho Mungu husema, naamini yote ambayo Mungu husema, kwa njia yoyote ambayo Yeye huyasema. Sina mawazo yangu mwenyewe bila kujali kile Mungu husema, sina mawazo yangu mwenyewe bila kujali kile Mungu hufanya.” Je, wewe kweli ni mtu anayempenda Mungu kwa sababu tu umesema mambo kama haya? Lazima uwe na uzoefu halisi, lazima uwe na uwezo wa kuongea kuhusu uelewa halisi wa Mungu mwenye mwili. Pia, ni nini kiini cha Mungu, ni vitu vipi ambavyo watu huona vigumu kumtii Mungu katika, ni vitu vipi ambavyo watu wanaweza kumtii Mungu katika, wanamtii Mungu kwa kiasi gani, ni vitu vipi ambavyo huna uwezo wa kumtii Mungu katika, unatatua vipi mawazo yako kuhusu Mungu, unapanua vipi uelewa wako wa Mungu polepole? Kama unakosa uzoefu kama huo, basi huna mapenzi ya kweli kwa Mungu. Baadhi ya watu wana furaha hasa wanapoona kufika kwa Mungu, wanampokea kwa ukarimu, na kisha wanalia Mungu Anapoondoka. Watu wengine hufikiri kwamba hili ni onyesho la upendo wake kwa Mungu, lakini hili kweli linaweza kuonyesha kwamba anampenda Mungu? Hili linaweza kuonyesha tu kwamba anao moyo wenye ari, lakini mtu hawezi kusema kwamba matendo na maonyesho yake ni upendo kwa Mungu, kwamba ni imani ya kweli. Baadhi ya watu hutoa pesa kiasi, lakini hilo ni upendo kwa Mungu? Ama unaenda haraka kumwaga gilasi ya maji wakati unaambiwa, lakini hilo ni utiifu wa kweli? Kadhalika, watu wengine husema: “Nilimwamini Mungu baada ya mimi kusoma maneno ya Mungu, niliamini katika kupata mwili kwa Mungu, sina shaka baada ya mimi kumwona Mungu katika mwili wa kawaida.” Je, hili linaweza kuitwa imani ya kweli? Je, umekuwa na ushughulikaji na Mungu? Je, umejihusisha na Yeye? Je, unajua tabia Yake? Je, unajua ni nini Yeye hupenda? Je, unajua vitu unafanya ambavyo vinaikosea tabia Yake? Je, unajua upotovu ndani yako ambao Yeye huchukia? Je, unajua watu ambao Ameleta tabia Yake yenye haki kwao? Je, unajua ni watu wagani Yeye huchukia? Je, unajua ni masuala yapi unayo ambayo Yeye huchukia zaidi? Kama hujui vitu vyovyote kama hivi, linaonyesha kwamba kwa kweli huna uelewa wa Mungu. Huwezi kusema kwamba unamwamini Mungu kwa kweli, huwezi kusema kwamba unamtii Mungu kabisa, na bila shaka huwezi kusema kwamba unafanya vitu kulingana na mapenzi ya Mungu, kwamba unampenda Mungu, unamtii Mungu, ama unamwelewa Mungu. Unaweza kusema tu, kuhusu jambo hili, unayaelewa mapenzi Yake, unajua ni nini Yeye hupenda, kwamba unatenda kulingana na mapenzi ya Mungu katika jambo hili, kwamba unatenda kulingana na ukweli, kwamba unamtii katika jambo hili. Je, wewe ni mtu mtiifu kwa Mungu kwa sababu umemtii katika jambo hili tu? Huwezi kusema hilo, na kusema kwamba mtu humpenda Mungu kwa kuweka msingi tu kwa kitu cha juujuu, hilo ni kosa kubwa. Ukweli kwamba ulitenda kitu kizuri, ama kwamba umemjali Mungu hasa, huonyesha tu kwamba wewe ni mtu mwema, lakini hauonyeshi kwamba wewe ni mwangalifu kwa mapenzi ya Mungu. Bila shaka, upendo wa Mungu na kuwa mwangalifu kwa mapenzi ya Mungu yamejengwa juu ya msingi wa ubinadamu, na hakuwezi kuwa na upendo wa Mungu bila ubinadamu, kwa hivyo kila mmoja wenu lazima ajichunguze na aangalie mahali alipo. Baadhi ya watu hufikiri kwamba wao wako karibu hapo, lakini hili si lenye uhalisi; ilhali baadhi ya watu huenda kwa kiwangi kilichokithiri na hufikiri kwamba hakuna kitu kizuri kuwahusu, kwamba hawawezi kuachwa, na huu ni mtazamo hasi. Baadhi ya watu hufikiri kwamba hakuna mazuri ndani yao, na baadhi ya watu hujifafanua kama mtu anayempenda Mungu. Wao wako katika upande wa kushoto kabisa au katika upande wa kulia kabisa; huu ndio uhalisi wa watu hawa, ambao unaonyesha kwamba wao bado hawako katika njia sawa. Wao wanapaswa kuendelea kujitahidi kuwa dhahiri kuhusu ukweli, na kuingia katika uhalisi, ili kufuata mapenzi ya Mungu.
Soma Zaidi: Asili ya Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumanne, 5 Februari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa “Maonyo Matatu” | How to Be a Loyal Servant of God

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa “Maonyo Matatu” | How to Be a Loyal Servant of God

Mwenyezi Mungu anasema, “Kama muumini wa Mungu, hufai kuwa watiifu kwa yeyote mwingine isipokuwa Yeye katika mambo yote na mjilinganishe na moyo Wake katika mambo yote. Hata hivyo, ingawa wote huelewa mafundisho haya, ukweli huu wa kimsingi ulio wazi kabisa kwa binadamu hauwezi kuonekana kuwa kujumuishwa kwao kikamilifu, kutokana na ugumu wao, kama vile hali yao ya kutojua, upuzi, au ufisadi. Kwa hivyo, kabla ya kuuamua mwisho wenu, Ninafaa kuwaambia kwanza baadhi ya mambo, ambayo ni yenye umuhimu mkubwa sana kwenu. ... Katika maisha yenu, Naona mengi ambayo mnafanya ambayo hayana uhusiano na ukweli, kwa hivyo Nawaambia moja kwa moja muwe watumishi wa ukweli na wala si kutawaliwa na maovu na ubaya. Msikanyage ukweli na kuchafua sehemu yoyote ya nyumba ya Mungu. Hili ndilo onyo Langu kwenu.”

Jumanne, 22 Januari 2019

Kutupa mbali Jozi La Shetani Kunakomboa

Kutupa mbali Jozi La Shetani Kunakomboa

Momo Mji wa Hefei, Mkoa wa Anhui
Kabla ya kumwamini Mungu, bila kujali chochote nilichokuwa nikifanya, sikuwahi kutaka kubaki nyuma. Nilikuwa tayari kukubali shida yoyote ili mradi ingemaanisha ningeinuka juu ya kila mtu mwingine zaidi. Baada ya kumkubali Mungu, mtazamo wangu uliendelea kuwa sawa, kwa sababu niliamini kikamilifu msemo, “Hakuna maumivu, hakuna faida,” na kuona mtazamo wangu kama ushahidi wa msukumo wangu. Wakati Mungu alinifichulia ukweli, hatimaye niligundua kuwa nilikuwa nikiishi chini ya jozi la Shetani, nikiishi chini ya miliki yake.
Sio muda mrefu sana uliopita, kanisa lilifanya mipango ya kumtuma dada niliyeshiriki naye ili aweze kuhudumu katika nafasi ya uongozi. Niliposikia habari hizo, nilisononeka. Sisi sote tulikuwa tunahudumu katika majukumu ya uongozi hadi tulipoteuliwa tena kama wahariri. Sasa dada yangu angerudia nafasi ya uongozi na kumtumikia Mungu akiwa na uwezekano usio na kikomo wa ukuaji, lakini bado ningebakia nikifanya kazi kwa dawati, nikitekeleza kazi yangu bila kuonekana. Kunaweza kuwa na mategemeo gani ya baadaye katika hayo? Kwa kubadili mawazo, nilikumbushwa msemo wa kale, “Kuna njia milioni tofauti za mafanikio.” Ili mradi ningekamilisha kazi yangu vizuri, ningeweza pia kufanikiwa. Nilihitaji tu kuzidisha jitihada zangu katika kutafuatilia ukweli. Ikiwa ningelenga kuhariri mahubiri ili yawasilishe ukweli vizuri zaidi, labda siku moja viongozi wangeona kuwa nilielewa ukweli. Kisha wangenipandisha cheo na siku zangu za baadaye zingekuwa pia za kuchangamsha. Baada ya utambuzi huu, mawingu ya kijivu yalianza kurejea kwa ajili ya uamuzi mpya. Nilijitosa katika kazi yangu, na nikala na kunywa neno la Mungu wakati sikuwa na shughuli, bila kuthubutu kulegea hata kwa muda.
Siku moja, niliona kifungu kinachofuata katika Mahubiri na Ushirika Kuhusu Kuingia Katika Maisha: “Kila kitu kinachokuzuia kumtafuta Mungu na kutafuta ukweli ni mojawapo ya pingu za Shetani. Ukiwa umefungwa na moja kati ya minyororo ya Shetani, unaishi maisha yako chini ya miliki yake.” Baada ya kusikia haya, sikuweza kujizuia ila kuuliza, “Ni ipi kati ya jozi za shetani ninayoishi chini yake? Ni ipi kati ya sumu zake inayozuia utafutiliaji wangu wa ukweli?” Nilipojaribu kutafakari swali hili kwa kimya, nilikumbushwa hali yangu ya hivi karibuni. Baada ya dada yangu kupelekwa kwenye daraja lake jipya, sikuwa wa kutoonyesha hisia. Kwa kweli, nilijitolea zaidi kula na kunywa neno la Mungu, kumwomba Mungu, na kutekeleza kikamilifu kazi yangu. Kijuujuu, nilionekana kuwa na bidii zaidi katika kutafuta ukweli kuliko hapo awali, lakini ukifunua pazia na kuichambua, uwezo wangu wa kukubali kubaki nyuma ni kwa sababu nilikuwa na matamanio ya kuendelea siku moja. Tamaa yangu ya kuchochea kuwa bora zaidi ilikuwa ndiyo sababu sikuwa wa kutoonyesha hisia na badala yake nilifuatilia ukweli zaidi mno, lakini kunakodhaniwa kuwa ufuatiliaji wangu wa ukweli kulikuwa tu njonzi, ufuatiliaji ulio mchafu. Nilikuwa nikishiriki ufuatiliaji wa muda wa ukweli ili kutimiza madhumuni yangu ya kibinafsi. Nikifikiri nyuma kwa miaka yangu iliyotumika kufuata Mungu, nilitambua kuwa dhabihu zangu zote zilikuwa zimelipwa na sumu ya Shetani “Hakuna maumivu, hakuna faida.” Hivi ndivyo ilivyonifunga pingu isiyoonekana na kunitia kujitahidi kwa ubora. Nilipokuwa na cheo tayari, nilikuwa bado nikitafuta hata cha juu zaidi; Nilipopoteza cheo changu au niliposhindwa kujiendeleza, sikuwa wa kutoonyesha hisia; Mimi bado nilionekana kuwa na hiari ya kulipa bei ili kutafuta ukweli. Hata hivyo, hii haikuwa kwa sababu nilielewa ukweli na nilikuwa tayari kujitoa mhanga kwa ajili yake. Nilitaka tu kutumia kuonekana kwa kujitoa mhanga kwa jitihada za kufanikiwa. Hapo ndipo nilipobaini hatimaye kuwa msimamo wangu wa “Hakuna maumivu, hakuna faida,” ulikuwa kweli mojawapo wa sumu za Shetani zilizokuwa zikitiririka kupitia mishipa yangu. Nilikuwa nimetanganywa; sumu ilikuwa imeninyonya ubinadamu wangu wote. Nilikuwa na kiburi na mwenye tamaa bila hisia yoyote ya taswira yoyote. Mambo hayo yote yalifanyika kabisa chini ya pua langu. Kwa kweli nilifikiri kuwa matamanio yangu yalikuwa ushuhuda wa matarajio yangu. Nilidhani kuwa hali yangu ya kiburi ya kutotaka kubaki nyuma ilikuwa ishara ya motisha yangu. Niliabudu uongo wa Shetani kama ukweli na kuuona kama beji ya heshima badala ya alama ya fedheha. Nilikuwa mjinga kiasi kipi hadi kudanganyika na Shetani kiasi kile, kutojua kutofautisha kati mema na uovu? Hatimaye niliona jinsi nilivyokuwa ovyo. Nilijifunza pia jinsi Shetani ni mwenye kudhuru kwa siri na mwenye kuleta hizaya. Shetani hutumia udanganyifu spesheli kutudanganya na kutupotosha. Hutupotosha, na tunaapa uaminifu kwa mipango yake danganyifu. Hii yote hufanywa bila ujuzi wetu. Tunadhani tunatafuta ukweli na kujitolea kwa ajili ya kweli, lakini kwa kweli tunaishi katika kujidanganya. Sumu za Shetani zina nguvu kabisa! Ikiwa haingekuwa nuru yake Mungu, singewahi kamwe kuona ukweli kwamba nilikuwa nimepotoshwa na Shetani, na hakika singeweza kamwe kubaini mipango yake ya udanganyifu. Ikiwa haingekuwa nuru ya Mungu, ningeendelea kuishi chini ya jozi la Shetani, hadi wakati Shetani hatimaye anitumie mzima.
Wakati huo, nilifikiria kuhusu maneno ya Mungu: “Kama wewe unafurahia kuwa mtoa huduma katika nyumba ya Mungu, ukifanya kazi kwa bidii na kwa makini bila kuonekana, siku zote ukitoa na katu hupokei, basi Nasema kwamba wewe ni mtakatifu mtiifu, kwani hutafuti tuzo na unakuwa tu binadamu mwaminifu” (“Maonyo Matatu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mungu yalinionyesha njia ya kutenda: Kama mmoja wa viumbe wa Mungu, napaswa kumpenda na kumridhisha bila masharti na kutekeleza wajibu wangu kwa dhati. Hii ndiyo hisi ambayo kiumbe mmoja wa Mungu anapaswa kumiliki. Huu ni ufuatiliaji ambao unaambatana na mapenzi Yake. Kuanzia siku ya leo kwenda mbele, nitafanya liwezekanalo kufuatilia ukweli. Nitategemea ukweli ili kupenya udanganyifu wa Shetani na kutupa jozi lake. Sitafuatilia tena kitu chochote cha mwili. Badala yake, nitafanya kazi kwa bidii kwa kutoonekana, kutimiza wajibu wangu kumkidhi Mungu. Hata nikiachwa bila kitu chochote mwishowe, nitaendelea kwa hiari bila majuto yoyote, kwa sababu mimi ni moja tu wa viumbe duni wa Mungu. Kumridhisha Muumba ni nia yangu moja ya kweli maishani.
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Vitabu.

Ijumaa, 5 Oktoba 2018

Filamu za Injili | "Kupita Katika Mtego" | Je, Kuamini katika Biblia Kunaweza Kuwakilisha Kumwamini Mungu?

Filamu za Injili | "Kupita Katika Mtego" | Je, Kuamini katika Biblia Kunaweza Kuwakilisha Kumwamini Mungu?

Wachungaji na wazee wa ulimwengu wa dini hushikilia maneno ya Paulo katika Biblia yanayosema "Maandiko yote yametolewa kwa msukumo wa Mungu," wakiamini kwamba Biblia ni maneno ya Mungu kabisa na kufanya yote wanayoweza kuiinua Biblia na kuishuhudia, na kuifanya Biblia na Mungu kuwa visawe. Wanaamini kwamba Biblia inamwakilisha Bwana na kwamba imani katika Bwana ni imani katika Biblia. Je, Biblia nzima kweli imetolewa kwa msukumo wa Mungu? Je, Bwana, Mungu, yuko ndani ya Biblia? Je, ni kazi ya Mungu ambayo imetoa Biblia, au Biblia ambayo imetoa kazi ya Mungu? Je, Biblia inaweza kweli kumwakilisha Bwana? Video hii fupi itakuonyesha njia sahihi.
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, kumwamini Mungu

Jumatano, 7 Machi 2018

Kumwamini Mungu Lazima Kulenge Uhalisi, Si Tamaduni za Kidini

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,

Kumwamini Mungu Lazima Kulenge Uhalisi, Si Tamaduni za Kidini

Mwenyezi Mungu alisema, Je, ni desturi ngapi za kidini unazozizingatia? Ni mara ngapi wewe umeasi dhidi ya neno la Mungu na kwenda kwa njia yako mwenyewe? Ni mara ngapi wewe umetia katika vitendo neno la Mungu kwa sababu wewe kwa kweli unajali mizigo Aliyobeba na unatafuta kutimiza mapenzi Yake?

Jumatatu, 5 Machi 2018

Wale Wanaomjua Mungu Pekee Ndio Wanaoweza Kuwa na Ushuhuda Kwa Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu

Wale Wanaomjua Mungu Pekee Ndio Wanaoweza Kuwa na Ushuhuda Kwa Mungu

Mwenyezi Mungu alisema, Ni sheria ya Mbinguni na kanuni za duniani kumwamini Mungu na kumjua Mungu, na leo—wakati wa enzi ambapo Mungu mwenye mwili Anafanya kazi Yake mwenyewe—ndio wakati mwafaka hasa wa kumjua Mungu. Kumridhisha Mungu kunaafikiwa kwa msingi wa kufahamu mapenzi ya Mungu, na kuyafahamu mapenzi ya Mungu, ni muhimu kumjua Mungu. Ufahamu huu wa Mungu ni maono ambayo muumini anapaswa kuwa nayo; huu ndio msingi wa imani ya mwanadamu katika Mungu. Iwapo mwanadamu hana ufahamu huu, basi imani yake katika Mungu si dhahiri, na imejengwa juu ya nadharia tupu. Ingawa ni uamuzi wa watu kama hawa kumfuata Mungu, hawafaidi chochote. Wale wote wasiopata chochote kwenye mkondo huu ndio watakaoondolewa—wao wote hawana kazi. Haijalishi ni hatua gani ya kazi ya Mungu unayopitia, lazima uandamane na maono makuu. Bila maono kama haya, itakuwa vigumu kwako kukubali kila hatua ya kazi mpya, kwa maana mwanadamu hana uwezo wa kuwaza kuhusu kazi mpya ya Mungu, ni kuu kushinda mawazo ya mwanadamu. Kwa hivyo bila mchungaji kumlinda mwanadamu, bila mchungaji kushirikiana na mwanadamu kuhusu maono hayo, mwanadamu hana uwezo kukubali kazi hii mpya. Iwapo mwanadamu hawezi kupokea maono haya, basi hawezi kupata kazi mpya ya Mungu, na iwapo mwanadamu hawezi kutii kazi mpya ya Mungu, basi mwanadamu hana uwezo wa kuyaelewa mapenzi ya Mungu, na hivyo ufahamu wake wa Mungu ni bure. Kabla mwanadamu atimilize maneno ya Mungu, lazima ayajue maneno ya Mungu, hivyo ni kusema, aelewe mapenzi ya Mungu; ni kwa njia hii tu ndiyo maneno ya Mungu yanaweza kutekelezwa kwa usahihi na kulingana na moyo wa Mungu. Hili lazima liwe na kila mmoja anayetafuta ukweli, na ndiyo njia ambayo lazima kila mmoja anayejaribu kumjua Mungu aipitie. Njia ya kuyajua maneno ya Mungu ndiyo njia ya kumjua Mungu, na pia njia ya kuijua kazi ya Mungu. Na hivyo, kujua maono hakuashirii tu kuujua ubinadamu wa Mungu mwenye mwili, lakini pia kunajumuisha kujua maneno na kazi ya Mungu. Kutokana na maneno ya Mungu wanadamu wanapata kuelewa mapenzi ya Mungu, na kutokana na maneno ya Mungu wanapata kuelewa tabia ya Mungu na pia kujua kile Mungu alicho. Imani katika Mungu ndiyo hatua ya kwanza katika kumjua Mungu. Harakati ya kusonga kutoka katika imani ya mwanzo katika Mungu mpaka imani kuu kwa Mungu ndiyo njia ya kumjua Mungu, na harakati ya kuipitia kazi ya Mungu. Iwapo unaamini kwa Mungu kwa ajili tu ya kuamini kwa Mungu, na huamini kwa Mungu kwa ajili ya kumjua Mungu, basi hakuna ukweli katika imani yako, na haiwezi kuwa safi—kuhusu hili hakuna tashwishi. Iwapo, wakati wa harakati anapopata kumuonja Mungu, mwanadamu anapata kumjua Mungu polepole, basi hatua kwa hatua tabia yake itabadilika pia, na imani yake itaongezeka kuwa ya kweli zaidi. Kwa njia hii, wakati mwanadamu anafaulu katika imani yake kwa Mungu, ataweza kumpata Mungu kwa ukamilifu. Mungu alijitoa pakubwa kuingia katika mwili mara ya pili na kufanya kazi Yake binafsi ili mwanadamu apate kumjua Yeye, na ili mwanadamu aweze kumwona. Kumjua Mungu[a] ndiyo matokeo ya mwisho yanayofikiwa katika mwisho wa kazi ya Mungu; ndilo hitaji la mwisho la Mungu kwa mwanadamu. Anafanya hili kwa ajili ya ushuhuda Wake wa mwisho, na ili kwamba mwanadamu mwishowe na kwa kikamilifu aweze kumgeukia Yeye. Mwanadamu anaweza tu kumpenda Mungu kwa kumjua Mungu, na ili ampende Mungu lazima amjue Mungu. Haijalishi vile anavyotafuta, au kile anachotafuta kupata, lazima aweze kupata ufahamu wa Mungu. Ni kwa njia hii tu ndiyo mwanadamu anaweza kumridhisha Mungu. Ni kwa kumjua Mungu tu ndio mwanadamu anaweza kumwamini Mungu kwa ukweli, na ni kwa kumjua Mungu tu ndio anaweza kumwogopa na kumheshimu Mungu kwa kweli. Wale wasiomjua Mungu hawataweza kumwogopa na kumheshimu Mungu kwa kweli. Kumjua Mungu kunahusisha kujua tabia ya Mungu, kuelewa mapenzi ya Mungu, na kujua kile Mungu alicho. Na haijalishi ni kipengee gani cha kumjua Mungu, kila mojawapo kinamhitaji mwanadamu alipe gharama, na kinahitaji nia ya kutii, ambapo bila hivi hakuna atakayeweza kufuata mpaka mwisho. Kazi ya Mungu hailingani na mawazo ya mwanadamu hata kidogo, tabia ya Mungu na kile Mungu alicho ni vitu vigumu sana kwa mwanadamu kufahamu, na yote Anayosema na kufanya Mungu ni makuu sana yasiyoeleweka na mwanadamu; iwapo mwanadamu anatamani kumfuata Mungu, na hana nia ya kumtii Mungu, basi mwanadamu hatafaidi chochote. Tangu kuumbwa kwa dunia mpaka sasa, Mungu Amefanya kazi nyingi ambayo haieleweki na mwanadamu na ambayo mwanadamu amepata ugumu kuikubali, na Mungu amesema mengi yanayofanya mawazo ya mwanadamu magumu kupona. Ilhali Hajawahi kukomesha kazi Yake kwa sababu mwanadamu ana ugumu mwingi; Ameendelea kufanya kazi na kuzungumza, na hata ingawa idadi kubwa ya “wanajeshi” wameangamia njiani, Yeye bado Anaendelea na kazi Yake, na bado anateua kundi baada ya kundi la watu walio tayari kukubali kazi Yake mpya. Yeye hawahurumii wale “mashujaa” walioangamia, na badala yake anawathamini wale wanaoikubali kazi Yake mpya na maneno. Lakini ni kwa sababu gani ndiyo Anafanya kazi kwa njia hii, hatua kwa hatua? Ni kwa nini Yeye kila mara huwaondoa na kuchagua watu wengine? Ni kwa nini Yeye hutumia mbinu za aina hii kila mara? Kusudi la kazi Yake ni ile wanadamu wapate kumjua, na ili waweze kutwaliwa na Yeye. Kanuni ya kazi Yake ni kufanya kazi kwa wale wanaoweza kutii kazi Anayofanya leo, na sio kufanya kazi kwa wale wanaotii kazi Yake ya zamani, na wanaipinga kazi Yake ya leo. Hii ndiyo sababu hasa Amewafuta na kuwaangamiza watu wengi.

Matokeo ya funzo la kumjua Mungu haliwezi kufikiwa kwa siku moja au mbili:; Mwanadamu lazima apate uzoefu wa matukio mengi, apitie mateso, na awe na utiifu wa kweli. Kwanza kabisa, anza na kazi na maneno ya Mungu. Lazima uelewe kumjua Mungu kunajumuisha nini, jinsi ya kupata maarifa kuhusu Mungu, na jinsi ya kumwona Mungu katika matukio yako. Hili ndilo kila mtu lazima afanye wakiwa bado hawajamjua Mungu. Hakuna anayeweza kushika kazi na maneno ya Mungu kwa mara moja, na hakuna anayeweza kupata maarifa ya ukamilifu wa Mungu kwa muda mfupi. Kinachohitajika ni harakati mahususi ya matukio, na bila haya hakuna mwanadamu atakayeweza kumjua au kumfuata Mungu kwa kweli. Mungu Anapofanya kazi zaidi, ndivyo mwanadamu anavyozidi kumjua. Zaidi kazi ya Mungu inavyokinzana na mawazo ya mwanadamu, ndivyo ufahamu wa mwanadamu Kwake unavyofanywa upya na wenye kina kirefu. Iwapo kazi ya Mungu ingebaki milele bila kubadilika, basi mwanadamu angekuwa tu na ufahamu mdogo wa Mungu. Kati ya uumbaji na wakati wa sasa, vitu ambavyo Mungu alifanya wakati wa Enzi ya Sheria, Alichofanya wakati wa Enzi ya Neema, na kile Afanyacho wakati wa Enzi ya Ufalme: lazima ujue vizuri sana maono haya. Lazima mjue kazi ya Mungu. Ni baada tu ya kumfuata Yesu ndio Petro alipata kujua polepole kuhusu kazi ambayo Roho alifanya ndani ya Yesu. Alisema, “Kutegemea matukio ya mwanadamu hakutoshi kufukia ufahamu kamili wa Mungu; Lazima kuwe na mambo mengi kutoka kwa kazi ya Mungu ya kutusaidia kumjua Mungu.” Mwanzoni, Petro aliamini kuwa Yesu alitumwa na Mungu, kama mtume, na hakumwona Yesu kama Kristo. Wakati Petro aliitwa kumfuata[b] Yesu, Yesu Alimuuliza, “Simoni, mwana wa Yona, je, utanifuata?” Petro alisema, “Ni lazima nimfuate yule aliyetumwa na Baba wa mbinguni. Lazima nimtambue yule aliyechaguliwa na Roho Mtakatifu. Nitakufuata Wewe.” Kutoka kwa maneno Yake, inaonekana wazi kuwa Petro hakuwa na ufahamu kumhusu Yesu; alikuwa ameyapitia maneno ya Mungu, alikuwa amejikabili mwenyewe, na pia alikuwa amepitia ugumu kwa ajili ya Mungu, ilhali hakujua kazi ya Mungu. Baada ya muda wa uzoefu, Petro aliona ndani ya Yesu matendo mengi ya Mungu, aliona vile Mungu anavyopendeza, na aliona uwepo wa Mungu ndani ya Yesu. Vilevile, aliona kuwa maneno ya Yesu hayangeweza kuzungumzwa na mwanadamu, na kwamba kazi Aliyofanya Yesu haingefanyika na mwanadamu. Katika maneno ya Yesu na matendo Yake, zaidi ya hayo, Petro aliona wingi wa hekima ya Mungu, na kazi nyingi ya uungu. Wakati wa matukio yake, hakupata kujijua mwenyewe tu, ila alitilia maanani matendo ya Yesu, ambayo kutokana nayo aligundua mambo mengi mapya; kama vile, kwamba kulikuwa na maonyesho mengi ya Mungu wa matendo katika kazi ya Aliyofanya Mungu kupitia kwa Yesu, na kwamba maneno ya Yesu, matendo Yake, na jinsi Alivyoyachunga makanisa na kazi Aliyofanya ilitofautiana kabisa na mwanadamu wa kawaida. Hivyo, kutoka kwa Yesu alijifunza mafunzo mengi aliyopaswa kusoma, na kufikia wakati Yesu Alikuwa karibu kusulubiwa, alikuwa amepata ufahamu kiasi kuhusu Yesu—ufahamu ambao ulikuwa msingi wa uaminifu wake wa maisha katika Yesu, na kusulubiwa kwake kichwa chini kwa ajili ya Yesu. Yeye alikuwa na mawazo kadhaa, na hakuwa na ufahamu kamili kuhusu Yesu mwanzoni, lakini mambo kama haya bila shaka yanapatikana ndani ya wanadamu wapotovu. Alipokuwa karibu Anaondoka, Yesu Alimwambia Petro kwamba kusulubiwa Kwake ndiyo kazi Aliyokuja kufanya; Lazima Akataliwe na enzi hiyo, enzi hii nzee yenye uchafu lazima imsulubishe msalabani, na Alikuwa Amekuja kukamilisha kazi ya ukombozi, na, kwa kuwa Alikuwa ameikamilisha kazi hii, huduma Yake ilikuwa imekamilika. Aliposikia haya, Petro alipatwa na huzuni, na akampenda Yesu sana hata zaidi. Yesu Aliposulubiwa msalabani, Petro alilia kwa uchungu akiwa peke yake. Kabla ya hili, alikuwa amemuuliza Yesu, “Ee Bwana! Unasema kwamba unaenda kusulubiwa. Baada ya Wewe kwenda, tutakuona tena lini?” Je, hakuna mchanganyiko katika maneno Aliyozungumza? Je, hakuna mawazo yake pale ndani? Moyoni mwake, alijua kuwa Yesu Alikuja kukamilisha sehemu ya kazi ya Mungu, na kwamba baada ya Yesu kuondoka, Roho angekuwa pamoja naye; ingawa Angesulubiwa na Apae mbinguni, Roho wa Mungu Angekuwa pamoja naye. Wakati huo, alikuwa na ufahamu kiasi kumhusu Yesu, na kujua kwamba Alitumwa na Roho wa Mungu, kwamba Roho wa Mungu Alikuwa ndani Yake, na kwamba Yesu Alikuwa Mungu Mwenyewe, Alikuwa Kristo. Lakini kwa sababu ya upendo wake kwa Yesu, na kwa sababu ya udhaifu wa mwanadamu, bado Petro alisema maneno hayo. Ikiwa unaweza kutilia maanani na kupitia matukio ya hali ya juu katika kila hatua ya kazi ya Mungu, basi utaweza kuutambua uzuri wa Mungu hatua kwa hatua. Na maono ya Paulo yalikuwa yapi? Yesu Alipomwonekania, Paulo alisema, “Ee Bwana! Wewe ni nani?” Yesu Akasema, “Mimi ndimi Yesu, ambaye wewe unamtesa.” Haya ndiyo yalikuwa maono ya Paulo. Petro alitumia kufufuka kwa Yesu na kuonekana Kwake kwa siku arubaini, na mafunzo ya Yesu wakati wa maisha Yake, kama maono yake mpaka alipofika mwisho wa safari yake.

Mwanadamu humtambua Mungu, anapata kujijua mwenyewe, anajitoa katika tabia yake potovu, na kutafuta kukua katika maisha yote kwa ajili ya kumjua Mungu. Ukitafuta kujijua mwenyewe tu na kujishughulisha tu na tabia yako potovu, na huna ufahamu ni kazi gani Mungu Anafanya kwa mwanadamu, kuhusu jinsi wokovu Wake ulivyo mkuu, au jinsi unavyomjua Mungu na kushuhudia matendo ya Mungu, basi matukio yako hayana maana. Iwapo unafikiri kuwa kuweza kuuweka ukweli katika matendo, na kuwa na uwezo wa kuvumilia kunamaanisha maisha ya mtu yamekua, basi hii ina maana kuwa bado huelewi maana kamili ya maisha, na huelewi kusudi la Mungu la Kufanya kazi kwa mwanadamu. Siku moja, ukiwa katika makanisa ya kidini, miongoni mwa wanachama wa Kanisa la Toba au Kanisa la Uzima, utakutana na watu wengi wenye imani ambao maombi yao yana maono, na wanaohisi kuguzwa na walio na maneno ya kuwaongoza katika kuendelea kwao na maisha. La ziada, kwa mambo mengi wanaweza kuvumilia, na kujitelekeza wenyewe, bila kuongozwa na mwili. Wakati huo, huwezi kujua tofauti: Utaamini kuwa kila wanachofanya ni sawa, kuwa ni udhihirisho wa kawaida wa maisha, lakini ni jambo la kusikitisha kweli kuwa jina wanaloamini si sahihi. Je imani kama hizi si pumbavu? Ni kwa nini inasemekana kuwa watu wengi hawana maisha? Ni kwa sababu hawamjui Mungu, na hivyo inasemekana kuwa hawana Mungu, na hawana uhai. Iwapo imani yako kwa Mungu imefikia kiwango fulani ambapo unaweza kwa kikamilifu kuyafahamu matendo ya Mungu, ukweli wa Mungu, na kila hatua ya kazi ya Mungu, basi umejawa na ukweli. Iwapo hujui kazi na tabia ya Mungu, basi uzoefu wako bado ni wa chini. Jinsi Yesu Aliifanya hatua ile ya kazi Yake, jinsi hatua hii inavyoendelezwa, jinsi Mungu Alifanya kazi Yake katika enzi ya Neema na ni kazi ipi iliyofanywa, ni kazi ipi inafanyika katika hatua hii—iwapo huna ufahamu kamilifu wa mambo haya, basi hutawahi kuondokewa na wasiwasi na utakuwa na shaka. Iwapo, baada ya kipindi cha uzoefu, wewe unaweza kujua kazi inayofanywa na Mungu na kila hatua ya kazi ya Mungu, na unao ufahamu mkuu wa malengo ya maneno ya Mungu, na ni kwa nini maneno mengi yaliyozungumzwa na Yeye hayajatimika bado, basi unaweza kutulia na kuendelea katika safari iliyo mbele yako, ukiwa huru kutokana na wasiwasi na kusafishwa. Mnapaswa kuona kile Mungu anatumia wingi wa kazi Yake. Yeye hutumia maneno Anayozungumza, akimsafisha mwanadamu na kuyabadilisha mawazo ya mwanadamu kupitia maneno mengi tofauti. Mateso yote ambayo mmestahimili, kusafishwa kote ambako mmepitia, kushughulikiwa ambako mmekukubali ndani yenu, kupata nuru ambako mmeona—yote yamefanikishwa kutumia maneno Aliyozungumza Mungu. Ni kwa sababu ya nini ndio mwanadamu anamfuata Mungu. Ni kwa sababu ya maneno ya Mungu! Maneno ya Mungu ni yenye mafumbo makuu, na yanaweza kuuguza moyo wa mwanadamu, kufunua vitu vilivyo ndani ya moyo wa mwanadamu, yanaweza kumfanya ajue vitu vilivyotendeka zamani, na kumruhusu kuona katika siku za usoni. Na kwa hivyo mwanadamu anavumilia mateso kwa sababu ya maneno ya Mungu, na anafanywa mkamilifu kwa sababu ya maneno ya Mungu, na ni baada ya hapo tu ndipo mwanadamu anamfuata Mungu. Anachostahili kufanya mwanadamu katika hatua hii ni kukubali maneno ya Mungu, na haijalishi kama amefanywa mkamilifu, au kusafishwa, kilicho cha muhimu ni maneno ya Mungu; hii ni kazi ya Mungu, na ni maono ambayo mwanadamu lazima ayajue leo hii.
Mungu Anamfanyaje mwanadamu kuwa mkamilifu? Tabia ya Mungu ni gani? Na ni nini kilicho ndani ya tabia Yake? Haya yote lazima yaeleweke; hii ni kusambaza jina la Mungu, ni kuwa na ushuhuda kwa Mungu, na kumtukuza na kumsifu Mungu, na bila shaka mwanadamu atafikia mabadiliko katika tabia ya maisha yake kwa msingi wa kumjua Mungu. Zaidi mwanadamu anavyopitia kushughulikiwa na kusafishwa, ndivyo nguvu yake inavyoongezeka, na hatua za Mungu zinavyozidi kuwa nyingi, ndivyo mwanadamu anavyofanywa mkamilifu. Leo, katika uzoefu wa mwanadamu, kila hatua ya kazi ya Mungu inayagonga mawazo ya mwanadamu, na kila hatua haiwezi kuwazwa na akili ya mwanadamu, na kuzidi matarajio ya mwanadamu. Mungu Anakimu mahitaji yote ya mwanadamu, na kwa kila njia yote huwa yanakinzana na mawazo ya mwanadamu, na ukiwa mdhaifu, Mungu Ananena maneno Yake. Ni kwa njia hii tu ndio Anaweza kukupa uhai wako. Kwa kuzigonga fikira zako, unakuja kukubali kazi ya Mungu, na kwa njia hii pekee ndio unaweza kuondoa upotovu wako. Leo hii, kwa upande mmoja Mungu mwenye mwili Anafanya kazi katika uungu, na kwa upande mwingine Anafanya kazi katika ubinadamu wa kawaida. Unapoacha kuweza kukana kazi yoyote ya Mungu, unapoweza kutii bila kujali lolote Analosema Mungu au kufanya katika hali ya ubinadamu wa kawaida, unapoweza kutii na kuelewa bila kujali ni ukawaida wa aina gani Anadhihirisha: ni wakati huo tu ndio unaweza kuwa na uhakika kwamba Yeye ni Mungu, na ni hapo tu utakoma kuwa na dhana, na ni hapo tu ndio utaweza kumfuata mpaka mwisho. Kuna hekima katika kazi ya Mungu, na Anajua jinsi mwanadamu Anaweza kuwa na ushuhuda Kwake. Anajua pale ambapo udhaifu wa uhai wa mwanadamu upo, na maneno Anayozungumza yanaweza kukugonga pale penye udhaifu wako upo, lakini pia Anatumia maneno Yake makuu na yenye busara kukufanya uwe na ushuhuda Kwake. Hayo ndiyo matendo ya kimiujiza ya Mungu. Kazi inayofanywa na Mungu haiwezi kufikiriwa na akili ya mwanadamu. Hukumu ya Mungu inafunua aina za upotovu ambazo mwanadamu, kwa kuwa ni mwili, amejawa nao, na vitu vipi ndivyo umuhimu wa mwanadamu, na humwacha mwanadamu bila mahali pa kujificha aibu yake.
Mungu anafanya kazi ya hukumu na kuadibu ili kwamba mwanadamu amjue, na kwa ajili ya ushuhuda Wake. Bila hukumu Yake ya tabia potovu ya mwanadamu, basi mwanadamu hangeweza kujua tabia Yake ya haki isiyoruhusu kosa lolote, na hangeweza kubadili ufahamu Wake wa Mungu kuwa mpya. Kwa ajili ya ushuhuda Wake, na kwa ajili ya usimamizi Wake, Anafanya ukamilifu Wake kuwa wazi kwa kila mtu, hivyo kumwezesha mwanadamu kupata ufahamu wa Mungu, na kubadili tabia yake, na kuwa na ushuhuda mkuu kwa Mungu kupitia kuonekana kwa Mungu wa hadharani. Mabadiliko yanafanikishwa kwa tabia ya mwanadamu kupitia njia tofauti ya kazi ya Mungu; bila mabadiliko ya aina hii katika tabia ya mwanadamu, mwanadamu hangeweza kuwa na ushuhuda kwa Mungu, na hangekuwa wa kuupendeza moyo wa Mungu. Mabadiliko katika tabia ya mwanadamu yanaashiria kwamba mwanadamu amejiweka huru kutokana na minyororo ya Shetani, amejiweka huru kutokana na ushawishi wa giza, na kwa kweli amekuwa mfano na kifaa cha kujaribiwa cha kazi ya Mungu, amekuwa shahidi wa kweli wa Mungu na mtu aliye wa kuupendeza moyo wa Mungu. Leo hii, Mungu mwenye mwili Amekuja kufanya kazi Yake duniani, na Anahitaji kwamba mwanadamu apate ufahamu kumhusu, aweze kumtii, awe na ushuhuda Kwake—aweze kujua kazi Yake ya matendo na ya kawaida, atii maneno Yake yote na kazi ambayo haiambatani na mawazo ya mwanadamu, na kuwa na ushuhuda kwa kazi Yake yote ya kumwokoa mwanadamu, na matendo yote Anayofanya ya kumshinda mwanadamu. Wale walio na ushuhuda kwa Mungu lazima wawe na ufahamu wa Mungu; ni aina hii tu ya ushuhuda ndio ulio sahihi, na wa kweli, na ni aina hii tu ya ushuhuda ndio unaoweza kumpa Shetani aibu. Mungu Anawatumia wale waliomjua baada ya kupitia hukumu Yake na kuadibu, ushughulikiaji na upogoaji, kuwa na ushuhuda Kwake. Anawatumia wale waliopotoshwa na Shetani kumtolea Yeye ushuhuda, na vilevile Anawatumia wale ambao tabia yao imebadilika, na wale basi ambao wamepokea baraka Zake, kumtolea ushuhuda. Yeye hana haja na mwanadamu kumsifu kwa maneno tu, wala hana hitaji lolote la sifa na ushuhuda kutoka kwa namna ya Shetani, ambao hawajaokolewa na Yeye. Ni wale tu wanaomjua Mungu ndio wanaohitimu kumtolea Mungu ushuhuda, na ni wale tu ambao tabia zao zimebadilika ndio wanaofaa kumshuhudia Mungu, na Mungu hatamruhusu mwanadamu kwa makusudi aliletee jina Lake aibu.

kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili