Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Kusogea-karibu-na-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Kusogea-karibu-na-Mungu. Onyesha machapisho yote

Jumamosi, 22 Juni 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kuhusu Maisha ya Kawaida ya Kiroho

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kuhusu Maisha ya Kawaida ya Kiroho

Muumini lazima awe na maisha ya kawaida ya kiroho huu ni msingi wa kupitia maneno ya Mungu na kuingia katika hali halisi. Sasa hivi, je, maombi yote, kule kuja karibu na Mungu, kuimba, kusifu, kutafakari, na kule kujaribu kuelewa maneno ya Mungu ambayo mnatenda yanafikia viwango vya maisha ya kawaida ya kiroho? Hakuna kati yenu aliye wazi sana juu ya hili. Maisha ya kawaida ya kiroho hayakomi tukwa ombi, wimbo, maisha ya kanisa, kula na kunywa maneno ya Mungu, na matendo mengine kama haya, bali yana maana ya kuishi maisha ya kiroho yaliyo mapya na ya kusisimua. Siyo kuhusu mbinu, lakini matokeo. Watu wengi sana wanafikiri kwamba ili kuwa na maisha ya kawaida ya kiroho lazima mtu asali, aombe, ale na anywe maneno ya Mungu, au kujaribu kuelewa maneno ya Mungu. Bila kujali kama kuna matokeo yoyote, au kama kuna kuelewa kwa kweli, watu hawa hulenga tu kufanya mambo yasiyo ya dhati kwa nje, na hawalengi matokeo ni watu wanaoishi ndani ya mila za dini, na si watu wanaoishi ndani ya kanisa, na hata zaidi wao si watu wa ufalme. Sala za mtu wa aina hii, nyimbo zake, na kula na kunywa kwake maneno ya Mungu yote yanafuata amri, wanalazimika kufanya hayo, na yanafanyika katika kufuata mitindo, hayafanyiki kwa hiari wala kufanyika kutoka moyoni. Haijalishi ni kiasi gani watu hawa wanaomba au kuimba, hakutakuwa na matokeo kamwe, kwa sababu yote wanayofanya ni amri na mila za kidini, na wao hawatendi neno la Mungu. Kwa kulenga tu mbinu, na kuchukua maneno ya Mungu kama amri ya kuhifadhi, mtu wa aina hii hatendi neno la Mungu, bali tu anaridhisha mwili, na anafanya vitu ili kujionyesha kwa wengine. Aina hii ya matambiko ya dini na amri yanatoka kwa mwanadamu, si kwa Mungu. Mungu hahifadhi sheria, Hazingatii sheria yoyote; Anafanya mambo mapya kila siku na Anafanya kazi ya vitendo. Kama watu katika Kanisa la Nafsi Tatu ambao wamewekewa mipaka kwa ulinzi wa kila asubuhi, sala ya jioni, kutoa shukrani kabla ya kula, kuonyesha shukrani katika kila kitu, na matendo mengine kama haya, haijalishi ni kiasi gani watu hawa wanafanya, au muda wanatenda, hawatakuwa na kazi ya Roho Mtakatifu. Kama watu huishi ndani ya amri, na mioyo yao ikiwa katika vitendo, basi Roho Mtakatifu hana njia ya kufanya kazi, kwa sababu mioyo ya watu inachukuliwa na amri, inachukuliwa na dhana za kibinadamu; kwa hiyo Mungu hana njia ya kufanya kazi; watu daima watakuwa wakiishi tu chini ya utawala wa sheria, mtu wa aina hii kamwe hataweza kupokea sifa za Mungu.
Maisha ya kawaida ya kiroho ni kuishi maisha mbele ya Mungu. Wakati wa kuomba mtu anaweza kutuliza moyo wake mbele ya Mungu, na kwa njia ya sala anaweza kutafuta kupatiwa nuru na Roho Mtakatifu, kuelewa maneno ya Mungu, na anaweza kuelewa mapenzi ya Mungu. Wakati wa kula na kunywa maneno ya Mungu mtu anaweza kuelewa zaidi na kuwa udhahiri zaidi juu ya ni nini Mungu anataka kufanya sasa hivi, na mtu anaweza kuwa na njia mpya ya matendo na asiwe wa kushikilia ukale, ili matendo ya mtu yote ni kwa lengo la kufanikisha maendeleo katika maisha. Kwa mfano, sala ya mtu si kwa ajili ya kusema baadhi ya maneno mazuri, au kupiga kelele mbele ya Mungu kuonyesha deni ya mtu, bali ni kwa kufanya mazoezi ya kutumia roho ya mtu, kutuliza moyo wa mtu mbele ya Mungu, kufanya mazoezi ya kutafuta uongozi kwa vyote vile, kufanya moyo wa mtu uwe moyo wa kuvutiwa na mwanga mpya kila siku, kutokuwa wa kukaa tu wala mvivu, na kuingia kwenye njia sahihi ya kutenda maneno ya Mungu. Kwa sasa watu wengi wanalenga mbinu, na hawajaribu kufuata ukweli ili kufikia maendeleo katika maisha; hapa ndipo watu hupotoka. Pia kuna baadhi ya watu ambao, hata kama wao wana uwezo wa kupokea mwanga mpya, taratibu zao hazibadiliki, wao huunganisha fikra za dini za zamani ili kupokea neno la Mungu leo, na wanayoingiza bado ni kanuni ambayo hubeba fikra za dini kwa pamoja, na hawaingiziwi mwanga wa leo kabisa. Kwa hivyo, matendo yao ni machafu wanafanya matendo yale yale kwa jina jipya, na haijalishi matendo yao ni mazuri kiwango gani, bado ni ya unafiki. Mungu huongoza watu kufanya mambo mapya kila siku, na Anahitaji watu kuwa na umaizi mpya na ufahamu mpya kila siku, na si kuwa na mienendo ya zamani au wasiobadilika. Kama umemwamini Mungu kwa miaka mingi, ila mbinu zako hazijabadilika kamwe, kama bado wewe ni wa shauku na mwenye shughuli nyingi kwa nje, na wala huji mbele za Mungu kufurahia maneno Yake kwa moyo mtulivu, basi hutaweza kupata chochote. Wakati wa kupokea kazi mpya wa Mungu, kama hutaunda mpango mpya, kama hutatenda katika njia mpya, kama hutatafuta ufahamu mpya, lakini badala yake kushikilia mambo mazee ya zamani na kupokea kiasi kidogo tu cha mwanga mpya bila kubadili jinsi unavyotenda, basi mtu wa aina hii ingawa yu ndani ya mkondo huu kwa kawaida kwa kweli ni Mfarisayo wa dini nje ya mkondo wa Roho Mtakatifu.
Kama unataka kuishi maisha ya kawaida ya kiroho, unahitaji kupata mwanga mpya kila kuchao, kutafuta ufahamu wa kweli wa maneno ya Mungu, na kufikia udhahiri kuelekea ukweli. Unahitaji kuwa na njia ya kufanya matendo kwa vyote vile, na kwa kusoma maneno ya Mungu kila siku unaweza kupata maswali mapya na kugundua upungufu wako mwenyewe. Hili litaleta moyo ulio na kiu na unaotafuta, ambao utaweka nafsi yako yote katika mwendo, na wewe utakuwa na uwezo wa kuwa kimya mbele ya Mungu wakati wowote, na kuwa na hofu kubwa ya kuachwa nyuma. Kama mtu anaweza kuwa na huu moyo wa kiu, huu moyo wa kutafuta, na pia awe na nia ya kuingia ndani kwa kuendelea, basi yupo katika njia sahihi kwa ajili ya maisha ya kiroho. Wale wote ambao wanaweza kukubali kuongozwa na Roho Mtakatifu, ambao wanatamani kufanya maendeleo, ambao wako radhi kutafuta kukamilishwa na Mungu, wale ambao wanatamani kuelewa kwa undani maneno ya Mungu, na ambao hawatafuti vitu visivyo vya kawaida lakini wanalipa gharama ya vitendo, kuonyesha kwa vitendo kufikiria mapenzi ya Mungu, kuingia ndani kwa vitendo, kufanya uzoefu wao kuwa wa kweli zaidi na halisi zaidi, ambao hawatafuti maneno matupu ya kanuni, na ambao pia hawatafuti hisia isiyo ya kawaida, wala kumwabudu mtu yeyote mkubwa mtu wa aina hii ameingia katika maisha ya kawaida ya kiroho, na kila kitu anachofanya ni kwa lengo la kufanikisha maendeleo zaidi katika maisha, kufanya upya roho yake na wala si palepale, na daima awe na uwezo wa kuingia ndani kwa wema. Kwa mfano, aombapo kabla ya kula, halazimishwi kufanya hivyo, lakini badala yake anatuliza moyo wake mbele ya Mungu, kumshukuru Mungu katika moyo wake, yuko tayari kuishi kwa ajili ya Mungu, kuweka muda wake katika mikono ya Mungu, na yuko tayari kushirikiana na Mungu na kutumia rasilmali kwa ajili ya Mungu. Kama moyo wake hauwezi kuwa kimya mbele ya Mungu, ni afadhali asile bali azidi kutenda, basi hii si kufuata sheria, lakini ni kutenda neno la Mungu. Baadhi ya watu, wanapoomba kabla ya kula, kwa kujua wao hujifanya ili kuweka matendo ya kujionyesha, ambayo yanaweza kuonekana kama kumcha Mungu, lakini akili zao huwaza: "Kwa nini nahitaji kufanya matendo kwa njia hii? Si mambo ni mazuri bila kuomba? Mambo yangali vile baada ya kuomba, hivyo kwa nini kujisumbua?" Mtu wa aina hii hufuata amri, na ingawa maneno yake yanasema kwamba yuko tayari kumridhisha Mungu, moyo wake haujaja mbele za Mungu. Haombi namna hii ili afanye mazoezi ya kutuliza moyo wake mbele ya Mungu, bali hufanya hivyo ili kuwadanganya watu wengine na ili watu wengine waone. Mtu wa aina hii ni mnafiki kabisa, kama mchungaji wa dini ambaye anaweza kuombea tu wengine lakini hawezi mwenyewe kuingia ndani; mtu wa aina hii ni ofisa wa kidini, kabisa! Kila siku Mungu ananena mambo mapya, Anafanya mambo mapya, lakini wewe unafuata amri kila siku, ukijaribu kumdanganya Mungu, kushughulikia Mungu bila uangalifu, hivyo si wewe ni mtu ambaye anamwasi Mungu? Je, unaweza kupokea baraka wakati unazingatia amri na kumwasi Mungu? Si wewe utaadibiwa na Mungu?
Kazi ya Mungu kwa kasi inaendelea ikitupa vikundi vidogo mbalimbali vya watu wenye dini na "watu mashuhuri" wanaoshikilia misa ya kanisa kwa umbali sana, na pia kutawanya kwa pande zote nne wale "wataalamu" kati yenu ambao hasa hupenda kufuata kanuni. Kazi ya Mungu haisubiri, haitegemei kitu chochote nawala haizembei. Haivuti au kuburuta mtu yeyote; kama huwezi kustahimili basi utaachwa, bila kujali ni miaka ngapi umefuata. Haijalishi wewe ni mkongwe anayestahili kiasi kipi, kama wewe hufuata amri basi lazima uondolewe. Ninamshauri mtu wa aina hii kuwa na maarifa fulani ya kibinafsi, kwa hiari kuchukua kiti cha nyuma, na kutoshikilia kilicho cha kale; kuwalazimu wengine kutenda neno la Mungu kwa mujibu wa kanuni zako za vitendo si hii ni kujaribu kushinda mioyo ya watu? Utendaji wako ni kufuata sheria, kuwafundisha watu kufuata ibada ya kanisa, na mara zote kuwafanya watu wafanye mambo kulingana na matakwa yako, hivyo huku si kutengeneza vikundi? Hivyo huku si kugawanya kanisa? Basi wewe una ujasiri wa kusema kuwa unafikiria mapenzi ya Mungu vipi? Ni kipi kinakuwezesha kusema kwamba hili ni kuwakamilisha wengine? Ukiendelea kuongoza kwa njia hii, si hii ni kuwaongoza watu ndani ya matambiko ya kidini? Kama mtu ana maisha ya kawaida ya kiroho, kama anapata ufunguliaji na uhuru katika roho zao kila siku, basi anaweza kutenda maneno ya Mungu bila kuzuiwa kumridhisha na, hata anapoomba hapitii tu kanuni au kufuata mchakato, na anao uwezo wa kustahimili mwanga mpya kila siku. Wakati anafanya mazoezi ya kutuliza moyo wake mbele za Mungu, anaweza kufanya moyo wake kweli uwe tulivu mbele ya Mungu na hakuna mtu anayeweza kumvuruga, na hakuna mtu au kitu kinaweza kuzuia maisha yake ya kawaida ya kiroho. Aina hii ya matendo ni kwa lengo la kufanikisha matokeo, si tu kuwapa watu kanuni fulani za kuzingatia. Aina hii ya matendo si kufuata sheria, ila kuendeleza maendeleo ya watu katika maisha. Kama wewe ni mfuataji amri tu, basi maisha yako kamwe hayatabadilika, ingawa wengine wanaweza kufanya matendo kwa njia hii, kama wewe ufanyavyo, mwishowe, wengine wanaweza kustahimili kasi za kazi ya Roho Mtakatifu, wakati utaondolewa kutoka kwa mkondo wa Roho Mtakatifu. Hivyo basi je, hujidanganyi? Madhumuni ya maneno haya ni kuwaruhusu watu watulize mioyo yao mbele ya Mungu na kurejea kwa Mungu, kuruhusu kazi ya Mungu kutekelezwa kwa watu bila kizuizi, na ili itimize matokeo.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Jumamosi, 1 Juni 2019

Swahili Gospel Video "Kutoka kwa Enzi Hububujika Maji ya Uzima" (7) - Je, Kufanya Kazi Ngumu Kunamaanisha Tunafuata Mapenzi ya Baba wa Mbinguni?

Swahili Gospel Video "Kutoka kwa Enzi Hububujika Maji ya Uzima" (7) - Je, Kufanya Kazi Ngumu Kunamaanisha Tunafuata Mapenzi ya Baba wa Mbinguni?

Waumini wengine wa Bwana hufikiria kwamba yote tunayohitaji kufanya ni kuteseka na kulipa gharama ya kueneza injili ya Bwana, kubeba msalaba ili kumfuata Bwana, na kutenda unyenyekevu, subira na uvumilivu, na kwamba kwa kufanya mambo haya yote tunafuata mapenzi ya Baba wa mbinguni, na pia wao huamini kwamba kila mara tukifuatilia imani yetu kwa njia hii, basi hatimaye tutaokolewa na Mungu na kuingia katika ufalme wa mbinguni na kupata uzima wa milele. Lakini je, ni sahihi kuwa na ufahamu wa aina hii na kutenda kwa njia hii? Bwana Yesu alisema, "Wengi wataniita siku hiyo, Bwana, Bwana, hatujafanya unabii kwa jina lako? na kwa jina lako kutoa pepo? na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Halafu nitasema wazi kwao, Sikuwajua nyinyi kamwe: ondokeni mbele yangu, nyinyi watenda maovu" (Mathayo 7:22-23). Kwa nini watu hawa ambao huhubiri na kufanya kazi kwa bidii kwa jina la Bwana hawataingia katika ufalme wa mbinguni pekee, lakini pia wataadhibiwa na Bwana?
Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Alhamisi, 28 Machi 2019

Jinsi ya Kuhudumu kwa Upatanifu na Mapenzi ya Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,

Jinsi ya Kuhudumu kwa Upatanifu na Mapenzi ya Mungu

Mwenyezi Mungu alisema, Leo, tutawasiliana hasa jinsi watu wanavyostahili kumhudumia Mungu katika imani yao kwa Mungu, masharti yanayopaswa kutimizwa na ukweli unaopaswa kufahamika na watu wanaomhudumia Mungu, na mikengeuko ipi iliyoko katika huduma yako. Unapaswa kufahamu haya yote. Masuala haya yanagusia jinsi unavyomwamini Mungu, jinsi unavyotembea katika njia ya kuongozwa na Roho Mtakatifu, na jinsi unatii mipango ya Mungu katika mambo yote, na yatakuwezesha kujua kila hatua ya kazi ya Mungu ndani yako. Ukifika mahali hapo utafurahia kujua imani katika Mungu ni nini, namna ya kumwamini Mungu vizuri, na kile unachopaswa kufanya ili kutenda mambo kwa upatanifu na mapenzi ya Mungu. Hili litakufanya utii kikamilifu kazi ya Mungu, na hutakuwa na malalamiko, hutahukumu, au kuchambua, sembuse kutafiti. Zaidi ya hayo, nyote mtakuwa na uwezo wa kumtii Mungu hadi kifo, mkimruhusu Mungu awaongoze na kuwachinja kama kondoo, ili nyote muweze kuwa akina Petro wa miaka ya tisini, na muweze kumpenda Mungu kwa hali ya juu sana hata msalabani, bila malalamiko yoyote. Hivyo ndivyo mtakavyoweza kuishi kama akina Petro wa miaka ya tisini.
Kila mtu ambaye ameamua anaweza kumhudumia Mungu—lakini ni lazima iwe kwamba wale tu ambao wanayashughulikia kwa makini mapenzi ya Mungu na kuyafahamu mapenzi ya Mungu ndio wanaohitimu na walio na haki ya kumhudumia Mungu. Nimegundua hili kati yenu: Watu wengi wanaamini ya kuwa bora tu wanaeneza injili kwa bidii kwa ajili ya Mungu, waende barabarani kwa ajili ya Mungu, wajitumie na kuacha vitu kwa ajili ya Mungu, na kadhalika, basi huku ni kumhudumia Mungu; hata zaidi, watu wa kidini huamini kwamba kumhudumia Mungu kuna maana ya kukimbia hapa na pale wakiwa na Biblia mikononi mwao, wakieneza injili ya ufalme wa mbinguni na kuwaokoa watu kwa kuwafanya watubu na kuungama; kuna wakuu wengi wa kidini wanaofikiri kwamba kumhudumia Mungu ni kuhubiri makanisani baada ya kusoma na kufunzwa katika chuo cha seminari, kuwafunza watu kwa kusoma sura za Biblia; pia kuna watu katika maeneo ya umaskini wanaoamini kwamba kumhudumia Mungu kuna maana ya kupokea uponyaji na kufukuza mapepo, au kuwaombea ndugu, au kuwahudumia; miongoni mwenu, kunao wengi wanaoamini kwamba kumhudumia Mungu kuna maana ya kula na kunywa maneno ya Mungu, kumwomba Mungu kila siku, na pia kutembelea na kufanya kazi katika makanisa kila mahali; kunao ndugu wengine wanaoamini kwamba kumhudumia Mungu kunamaanisha kutoolewa wala kulea familia kamwe, na kutoa nafsi zao zote kwa Mungu. Ilhali watu wachache wanajua maana ya kweli ya kumhudumia Mungu. Ingawa kunao wengi wanaomhudumia Mungu kama nyota angani, idadi ya wale wanaoweza kuhudumu moja kwa moja, na wanaoweza kutumikia kulingana na mapenzi ya Mungu, ni hafifu—ndogo isiyo na maana. Kwa nini Ninasema hivi? Ninasema hivi kwa sababu wewe hufahamu kiini cha fungu la maneno “huduma kwa Mungu,” na unafahamu machache sana kuhusu jinsi ya kutumikia kulingana na mapenzi ya Mungu. Leo, tunawasiliana hasa jinsi ya kuhudumu kulingana na mapenzi ya Mungu, jinsi ya kuhudumu ili kutosheleza mapenzi ya Mungu.
Ikiwa ungependa kutumikia kulingana na mapenzi ya Mungu, ni lazima kwanza ufahamu ni watu wa aina gani wanapendwa na Mungu, ni watu wa aina gani wanachukiwa na Mungu, ni watu wa aina gani wanafanywa kuwa kamili na Mungu, na ni watu wa aina gani wana sifa zinazostahili kumhudumia Mungu. Hiki ni kiasi kidogo zaidi unachopaswa kujiandaa nacho. Isitoshe, unapaswa kujua malengo ya kazi ya Mungu, na kazi ambayo Mungu Ataitenda hapa na wakati huu. Baada ya kufahamu haya, na kupitia kwa mwongozo wa maneno ya Mungu, kwanza unafaa kuingia, na kupokea agizo la Mungu kwanza. Unapopata uzoefu wa kweli kwa msingi wa maneno ya Mungu, na unapojua kweli kazi ya Mungu, utakuwa umehitimu kumhudumia Mungu. Na unapomhudumia ndipo Mungu hufungua macho yako ya kiroho, na kukuruhusu kuwa na ufahamu mkubwa zaidi wa kazi Yake na kuiona dhahiri zaidi. Ukiingia katika ukweli huu, uzoefu wako utakuwa wa kina zaidi na wa kweli, na wale wote ambao wamepata uzoefu wa aina hiyo wataweza kutembea miongoni mwa makanisa mengi na kuwatolea ndugu zako, ili muweze kutumia nguvu za kila mmoja kufidia upungufu wako na kupata maarifa mengi zaidi ndani ya roho zenu. Ni baada tu ya kutimiza matokeo haya ndipo utakapoweza kutumikia kulingana na mapenzi ya Mungu na kufanywa mkamilifu na Mungu wakati wa kufanya huduma yako.
Wanaomhudumia Mungu wanapaswa kuwa marafiki wema wa Mungu, wanapaswa kupendwa na Mungu, na kuwa na uaminifu wa hali ya juu kwa Mungu. Bila kujali iwapo unatenda bila kuonekana na watu, au mbele ya watu, unaweza kupata furaha ya Mungu mbele za Mungu, unaweza kusimama imara mbele za Mungu, na bila kujali jinsi watu wengine wanavyokutendea, wewe huifuata njia yako mwenyewe kila mara, na kuushughulikia kwa makini mzigo wa Mungu. Mtu wa aina hii pekee ndiye rafiki mwema wa Mungu. Marafiki wema wa Mungu wanaweza kumhudumia Yeye moja kwa moja kwa sababu wamepewa agizo kuu la Mungu, na mzigo wa Mungu, wao wanaweza kuuchukulia moyo wa Mungu kama moyo wao wenyewe, na mzigo wa Mungu kama mzigo wao wenyewe, na hawazingatii iwapo watafaidi au watapoteza matarajio: Hata wasipokuwa na matarajio, na hawatafaidi chochote, watamwamini Mungu daima kwa moyo wa upendo. Kwa hivyo, mtu wa aina hii ni rafiki mwema wa Mungu. Marafiki wema wa Mungu ni wasiri Wake pia; ni wasiri wa Mungu pekee ndio wanaoweza kushiriki katika kutotulia Kwake, matamanio Yake, na ingawa mwili wao una uchungu na ni mdhaifu, wanaweza kuvumilia uchungu na kuacha kile wanachokipenda ili kumridhisha Mungu. Mungu huwapa watu wa aina hii mizigo mingi, na kile ambacho Mungu atafanya hudhihirishwa kupitia kwa watu hawa. Yaani, watu hawa wanapendwa na Mungu, wao ni watumishi wa Mungu wanaoupendeza moyo Wake, na ni watu wa aina hii pekee ndio wanaoweza kutawala pamoja na Mungu. Ukishakuwa rafiki mwema wa Mungu ndipo utakapoweza kabisa kutawala pamoja na Mungu.
Yesu aliweza kukamilisha agizo la Mungu—kazi ya ukombozi wa wanadamu wote—kwa sababu alikabidhi kila tatizo kwa mapenzi ya Mungu, bila kufuata mipango na fikira Zake binafsi. Basi pia, Yeye Alikuwa rafiki mwema wa Mungu—Mungu Mwenyewe, jambo ambalo nyote mnalielewa vizuri sana. (Kwa kweli, alikuwa Mungu Mwenyewe aliyetolewa ushahidi na Mungu; Ninataja jambo hili hapa kwa kuutumia ukweli wa Yesu ili kuonyesha mfano wa suala hili.) Aliweza kuuweka mpango wa usimamizi wa Mungu katika kiini cha mambo yote, na kila mara alimwomba Baba wa mbinguni na kuyatafuta mapenzi ya Baba wa mbinguni. Aliomba, na kusema: “Mungu Baba! Timiza kile ambacho ni mapenzi Yako, na usitende kulingana na nia Zangu; ingekwa heri ukitenda kulingana na mpango Wako. Mwanadamu anaweza kuwa dhaifu, lakini kwa nini unapaswa kumshughulikia? Ni vipi ambavyo mwanadamu aliweza kuwa mhusika wa shughuli Zako, mwanadamu ambaye ni kama chungu mkononi Mwako? Ndani ya moyo Wangu, Ninatamani tu kutimiza mapenzi Yako, na Ninatamani Utende Unachotaka kutenda ndani Yangu kulingana na makusudio Yako mwenyewe.” Alipokuwa njiani kuelekea Yerusalemu, Yesu alihisi maumivu makali, kama kwamba kisu kilikuwa kimedungwa ndani ya moyo Wake, ilhali hakuwa na nia yoyote ya kwenda kinyume cha Neno lake; kila mara kulikuwa na nguvu zenye uwezo mkuu zilizomvutia Yeye kuelekea mahali ambapo Angesulubiwa. Mwishowe, alipigiliwa misumari juu ya msalaba na akawa mfano wa mwili wenye dhambi, akiikamilisha kazi hiyo ya ukombozi wa wanadamu, na kufufuka kutoka kwa pingu za kifo na Kuzimu. Mbele Yake, kifo, jehanamu, na Kuzimu vilipoteza nguvu zao, na vilishindwa Naye. Aliishi miaka thelathini na tatu, na katika miaka hiyo yote daima Alifanya kila Alichoweza kutimiza mapenzi ya Mungu kulingana na kazi ya Mungu wakati huo, bila kuzingatia atakachofaidi au kupoteza Yeye binafsi, na kila mara akiwaza kuhusu mapenzi ya Mungu Baba. Hivyo, baada ya Yeye kubatizwa, Mungu alisema: “Huyu ni Mwana wangu Mpendwa, ambaye Ninapendezwa naye.” Kwa sababu ya huduma Yake mbele ya Mungu, iliyokuwa na upatanifu na mapenzi ya Mungu, Mungu aliuweka mzigo mzito wa kuwakomboa wanadamu wote juu ya mabega yake na akamfanya ajitolee kuutimiza, na Alikuwa na ujuzi na ustahiki wa kuikamilisha kazi hii muhimu. Katika maisha Yake yote, alivumilia mateso yasiyokuwa na kipimo kwa ajili ya Mungu, na alijaribiwa na Shetani mara nyingi, lakini hakufa moyo. Mungu alimpa kazi ya aina hiyo kwa sababu Alimwamini Yeye, na kumpenda Yeye, na hivyo basi Mungu mwenyewe alisema: “Huyu ni Mwana wangu Mpendwa, ambaye Ninapendezwa naye.” Wakati huo, ni Yesu pekee ambaye angeweza kutimiza agizo hili, na hii ilikuwa sehemu moja ya Mungu kutimiza kazi Yake ya kuwakomboa wanadamu wote katika Enzi ya Neema.
Ikiwa, kama Yesu, unaweza kuushughulikia kwa makini mzigo wa Mungu, na kuyakataa mambo ya mwili wako, Mungu atakuaminia kazi Zake muhimu, ili uweze kufikia masharti ya kumhudumia Mungu. Ni katika hali hizo pekee ndipo utakapothubutu kusema kwamba unafanya mapenzi ya Mungu na kukamilisha agizo Lake, hapo ndipo utakapothubutu kusema unamhudumia Mungu kweli. Ukilinganishwa na mfano wa Yesu, unaweza kuthubutu kusema kwamba wewe ni mwandani wa Mungu? Je, unaweza kuthubutu kusema kwamba unatekeleza mapenzi ya Mungu? Je, unaweza kuthubutu kusema kwamba kweli unamhudumia Mungu? Iwapo, leo, hufahamu aina hii ya huduma kwa Mungu, unaweza kuthubutu kusema kwamba wewe ni rafiki mwema wa Mungu? Ukisema kwamba unamhudumia Mungu, humkufuru Yeye? Fikiria kuhusu hilo: Je, unamhudumia Mungu, au unajihudumia wewe mwenyewe? Unamhudumia Shetani, ilhali kwa ukaidi unasema kwamba unamhudumia Mungu—katika jambo hili humkufuru Mungu? Watu wengi walio nyuma Yangu wanatamani baraka ya cheo, wana ulafi wa chakula, wanapenda kulala na kuushughulikia mwili kwa makini, kila mara wakiogopa kwamba hakuna njia ya kuondoka ndani ya mwili. Hawaifanyi kazi yao ya kawaida kanisani, na kula chakula cha bure, au wanawaonya ndugu zao kwa maneno Yangu, wanasimama juu na kuwatawala wengine. Watu hawa huendelea kusema kwamba wanafanya mapenzi ya Mungu, wao husema kila mara kwamba ni marafiki wema wa Mungu—huu si upuuzi? Ikiwa una motisha iliyo sahihi, lakini huwezi kutumikia kulingana na mapenzi ya Mungu, basi wewe unakuwa mpumbavu; lakini ikiwa motisha yako si sahihi, na bado unasema kwamba unamhudumia Mungu, basi wewe ni mtu anayempinga Mungu, na unastahili kuadhibiwa na Mungu! Sina huruma kwa watu wa aina hiyo! Wao hula chakula cha bure katika nyumba ya Mungu, na kila mara wao hutamani raha za mwili, na hawazingatii mambo ambayo Mungu anayapenda; kila mara wao hutafuta mambo yaliyo mazuri kwao, wala hawatilii maanani mapenzi ya Mungu, mambo yote wanayoyafanya hayaongozwi na Roho wa Mungu, kila mara wao hufanya hila na njama dhidi ya ndugu zao, na kuwa ndumakuwili, kama mbweha ndani ya shamba la mizabibu, akiiba mizabibu kila mara na kulikanyaga na kuliharibu shamba la mizabibu. Je, watu wa aina hiyo wanaweza kuwa marafiki wema wa Mungu? Je, unastahili kupokea baraka za Mungu? Wewe huwajibiki kuhusu maisha yako na kanisa, unastahili kupokea agizo la Mungu? Ni nani anayeweza kuthubutu kumwamini mtu kama wewe? Unapohudumu kwa njia hii, je, Mungu anaweza kuthubutu kukuaminia kazi kubwa zaidi? Je, si wewe unachelewesha mambo?
Nasema hivi ili uweze kujua masharti yanayohitajika kutimizwa ili kuhudumu kwa upatanifu na mapenzi ya Mungu. Usipoutoa moyo wako kwa Mungu, usipoyashugulikia kwa makini mapenzi ya Mungu kama alivyofanya Yesu, basi huwezi kuaminiwa na Mungu, na mwishowe utahukumiwa na Mungu. Labda leo, katika huduma yako kwa Mungu, kila mara wewe huficha kusudi la kumdanganya Mungu—lakini bado Mungu atakugundua. Kwa kifupi, bila kujali mambo yote mengine, ukimdanganya Mungu hukumu isiyo na huruma itakujia. Unapaswa kutumia vizuri nafasi ya kuwa umeingia katika njia sahihi ya kumhudumia Mungu kwa kumpa Mungu moyo wako kwanza, bila kugawanya uaminifu wako. Bila kujali iwapo uko mbele za Mungu, au mbele ya watu wengine, moyo wako unapaswa kuelekezwa kwa Mungu kila wakati, na unapaswa kufanya uamuzi wa kumpenda Mungu kama Yesu. Kwa kufanya hivi, Mungu atakufanya uwe mkamilifu, ili uwe mtumishi wa Mungu anayempendeza Mungu. Ikiwa ungependa kweli kufanywa mkamilifu na Mungu, na huduma yako iwe katika upatanifu na mapenzi Yake, basi unapaswa kubadilisha maoni yako ya awali kuhusu imani kwa Mungu, na kubadilisha jinsi ulivyokuwa ukimhudumia Mungu, ili nafsi yako yote iweze kufanywa kuwa kamilifu na Mungu; kwa kufanya hivi, Mungu hatakuacha, na, kama Petro, utakuwa katika kikosi cha mbele cha wale wanaompenda Mungu. Ukibaki kuwa mtu asiyetubu, basi utakutana na mwisho kama wa Yuda. Hii inapaswa kufahamika na watu wote wanaomwamini Mungu.

Jumatano, 20 Februari 2019

Ni kwa Kupitia tu Majaribio ya Kuumiza Ndiyo Mnaweza Kujua Kupendeza kwa Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,

Ni kwa Kupitia tu Majaribio ya Kuumiza Ndiyo Mnaweza Kujua Kupendeza kwa Mungu

Mwenyezi Mungu  alisema, Unampenda Mungu kiasi gani hasa leo? Na unajua kiasi gani hasa kuhusu yote ambayo Mungu amefanya ndani yako? Haya ni mambo unayopaswa kujifunza. Mungu anapowasili duniani, yote ambayo Amefanya ndani ya mwanadamu na kumkubalia mwanadamu kuona ni ili mwanadamu atampenda na kumjua Yeye kweli. Kwamba mwanadamu anaweza kuteseka kwa ajili ya Mungu na ameweza kufikia umbali huu ni, kuhusiana na jambo moja, kwa sababu ya upendo wa Mungu, na kuhusiana na jambo lingine, ni kwa sababu ya wokovu wa Mungu; zaidi ya hayo, ni kwa sababu ya kazi ya hukumu na kuadibu ambayo Mungu ametekeleza ndani ya mwanadamu. Kama hamna hukumu, kuadibu, na majaribio ya Mungu, na kama Mungu hajawafanya mteseke, basi, kusema ukweli, ninyi hamumpendi Mungu kweli. Kadri kazi ya Mungu ilivyo kuu zaidi ndani ya mwanadamu, na kadri mateso ya mwanadamu yalivyo makuu zaidi, ndivyo inavyoweza kuonyesha zaidi hasa vile kazi ya Mungu ilivyo ya maana, na ndivyo moyo wa mwanadamu unavyoweza kumpenda Mungu kweli zaidi. Unajifunzaje jinsi ya kumpenda Mungu? Bila mateso makali na usafishaji, bila majaribio ya kuumiza—na kama, zaidi ya hayo, yote ambayo Mungu alimpa mwanadamu ingekuwa neema, upendo, na rehema—je, ungeweza kufikia upendo wa kweli kwa Mungu? Kwa upande mmoja, wakati wa majaribio ya Mungu mwanadamu huja kujua kasoro zake, na huona kwamba yeye ni mdogo, wa kudharauliwa, na duni, kwamba hana chochote, na si kitu; kwa upande mwingine, wakati wa majaribio Yake Mungu humuumbia mwanadamu mazingira tofauti yanayomfanya mwanadamu aweze zaidi kupitia kupendeza kwa Mungu. Ingawa maumivu ni makubwa, na wakati mwingine yasiyoshindika—na hata hufikia kiwango cha huzuni ya kuseta—baada ya kuyapitia, mwanadamu huona vile kazi ya Mungu ndani yake ni ya kupendeza, na ni juu ya msingi huu tu ndiyo ndani ya mwanadamu huzaliwa upendo wa kweli kwa Mungu. Leo mwanadamu huona kwamba na neema, upendo na rehema ya Mungu pekee, hana uwezo wa kujijua mwenyewe kweli, sembuse kuweza kujua kiini cha mwanadamu. Ni kupitia tu usafishaji na hukumu ya Mungu, ni wakati tu wa usafishaji kama huo ndiyo unaweza kujua kasoro zako, na kujua kwamba huna chochote. Hivyo, upendo wa mwanadamu kwa Mungu umejengwa juu ya msingi wa usafishaji na hukumu ya Mungu. Kama wewe hufurahia tu neema ya Mungu, na maisha ya familia yenye amani au baraka yakinifu, basi hujampata Mungu, na imani yako kwa Mungu haijafaulu. Mungu tayari ametekeleza hatua moja ya kazi ya neema katika mwili, na tayari amempa mwanadamu baraka yakinifu—lakini mwanadamu hawezi kufanywa mkamilifu na neema, upendo, na rehema pekee. Katika uzoefu wa mwanadamu yeye hukabiliwa na baadhi ya upendo wa Mungu, na huuona upendo na rehema ya Mungu, lakini baada ya kupitia kwa kipindi fulani cha wakati, yeye huona kwamba neema ya Mungu na upendo na rehema Yake hayawezi kumfanya mwanadamu awe mkamilifu, na hayana uwezo wa kufichua kile ambacho ni potovu ndani ya mwanadamu, wala hayawezi kumwondolea mwanadamu tabia yake potovu, au kufanya kuwa kamilifu upendo na imani yake. Kazi ya Mungu ya neema ilikuwa kazi ya kipindi kimoja, na mwanadamu hawezi kutegemea kufurahia neema ya Mungu ili kumjua Mungu.
Ni kupitia nini ndiyo ukamilishaji wa Mungu kwa mwanadamu hutimizwa? Kupitia tabia Yake yenye haki. Tabia ya Mungu hasa huwa na haki, ghadhabu, uadhama, hukumu, na laana, na ukamilishaji Wake wa mwanadamu hasa ni kupitia hukumu. Watu wengine hawaelewi, na huuliza ni kwa nini Mungu anaweza tu kumfanya mwanadamu kuwa mkamilifu kupitia hukumu na laana. Wao husema kwamba kama Mungu angemlaani mwanadamu, si mwanadamu angekufa? Kama Mungu angemhukumu mwanadamu, si mwanadamu angelaaniwa? Basi anawezaje hata hivyo kufanywa mkamilifu? Hayo ndiyo maneno ya watu wasioijua kazi ya Mungu. Kile ambacho Mungu hulaani ni uasi wa mwanadamu, na kile Anachohukumu ni dhambi za mwanadamu. Ingawa Yeye hunena kwa ukali, na bila kiwango cha hisi hata kidogo, Yeye hufichua yote yaliyo ndani ya mwanadamu, na kupitia maneno haya makali Yeye hufichua kile kilicho muhimu ndani ya mwanadamu, lakini kupitia hukumu kama hiyo, Yeye humpa mwanadamu ufahamu mkubwa wa kiini cha mwili, na hivyo mwanadamu hujitiisha chini ya utii mbele za Mungu. Mwili wa mwanadamu ni wa dhambi, na wa Shetani, ni wa kutotii, na chombo cha kuadibu kwa Mungu—na kwa hiyo, ili kumruhusu mwanadamu kujijua, maneno ya hukumu ya Mungu lazima yamfike na lazima kila aina ya usafishaji itumike; ni wakati huo tu ndiyo kazi ya Mungu inaweza kuwa ya kufaa.
Kutokana na maneno yaliyonenwa na Mungu inaweza kuonekana kwamba tayari Ameulaani mwili wa mwanadamu. Je, haya maneno, basi, ni maneno ya laana? Maneno yaliyonenwa na Mungu hufichua tabia halisi ya mwanadamu, na kupitia ufichuzi kama huo unahukumiwa, na unapoona kwamba huwezi kuyaridhisha mapenzi ya Mungu, ndani unahisi huzuni na majuto, unahisi kwamba unapaswa kumshukuru Mungu sana, na usiyetosha kwa ajili mapenzi ya Mungu. Kuna nyakati ambapo Roho wa Mungu hukufundisha nidhamu kutoka ndani, na nidhamu hii hutoka kwa hukumu ya Mungu; kuna nyakati ambapo Mungu hukushutumu na kuuficha uso Wake kutoka kwako, wakati ambapo hakusikilizi, na Hafanyi kazi ndani yako, akikuadibu bila sauti ili kukusafisha. Kazi ya Mungu ndani ya mwanadamu ni hasa ili kuweka wazi tabia Yake yenye haki. Ni ushuhuda gani ambao mwanadamu hatimaye huwa nao kwa Mungu? Yeye hushuhudia kwamba Mungu ni Mungu mwenye haki, kwamba tabia yake ni haki, ghadhabu, kuadibu, na hukumu; mwanadamu hushuhudia kwa tabia yenye haki ya Mungu. Mungu hutumia hukumu Yake kumfanya mwanadamu awe mkamilifu, Amekuwa Akimpenda mwanadamu, na kumwokoa mwanadamu—lakini ni kiasi gani kiko ndani ya upendo Wake? Kuna hukumu, uadhama, ghadhabu, na laana. Ingawa Mungu alimlaani mwanadamu katika wakati uliopita, Hakumtupa mwanadamu kabisa ndani ya shimo la kuzimu, lakini Alitumia njia hiyo kuisafisha imani ya mwanadamu; Hakumuua mwanadamu, lakini alitenda ili kumfanya mwanadamu awe mkamilifu. Kiini cha mwili ni kile ambacho ni cha Shetani—Mungu alikisema sahihi kabisa—lakini ukweli unaotekelezwa na Mungu haukamilishwi kufuatana na maneno Yake. Yeye hukulaani ili uweze kumpenda, na ili uweze kujua kiini cha mwili; Yeye hukuadibu ili uweze kuamshwa, kukuruhusu wewe ujue kasoro zilizo ndani yako, na kujua kutostahili kabisa kwa mwanadamu. Hivyo, laana za Mungu, hukumu Yake, na uadhama na ghadhabu Yake—yote ni kwa ajili ya kumfanya mwanadamu awe mkamilifu. Yote ambayo Mungu anafanya leo, na tabia yenye haki ambayo Yeye huifanya kuwa wazi ndani yenu—yote ni kwa ajili ya kumfanya mwanadamu awe mkamilifu, na huo ndio upendo wa Mungu.
Katika dhana za mwanadamu za kitamaduni, upendo wa Mungu ni neema Yake, fadhili, na huruma kwa udhaifu wa mwanadamu. Ingawa mambo haya pia ni upendo wa Mungu, yanaegemea upande mmoja sana, na si njia za msingi ambazo kwazo Mungu humfanya mwanadamu kuwa mkamilifu. Wakati ambapo watu wengine wameanza tu kumwamini Mungu, ni kwa sababu ya ugonjwa. Ugonjwa huu ni neema ya Mungu kwako; bila huo, hungemwamini Mungu, na kama hungemwamini Mungu basi hungefika umbali huu—na hivyo hata neema hii ni upendo wa Mungu. Katika wakati wa kumwamini Yesu, watu walifanya mengi ambayo hayakupendwa na Mungu kwa sababu hawakuelewa ukweli, lakini Mungu ana upendo na rehema, na Amemleta mwanadamu umbali huu, na ingawa mwanadamu haelewi chochote, bado Mungu humruhusu mwanadamu amfuate Yeye, na, zaidi ya hayo, Amemwongoza mwanadamu mpaka leo. Je, huu si upendo wa Mungu? Kile ambacho kinadhihirishwa katika tabia ya Mungu ni upendo wa Mungu—hili ni sahihi bila shaka. Wakati ambapo ujenzi wa kanisa ulifikia kilele chake, Mungu alifanya hatua ya kazi ya watendaji-huduma na akamtupa mwanadamu katika shimo la kuzimu. Maneno ya wakati wa watendaji-huduma yote yalikuwa laana: laana za mwili wako, laana za tabia yako potovu ya kishetani, na laana za mambo yanayokuhusu ambayo hayatimizi mapenzi ya Mungu. Kazi iliyofanywa na Mungu katika hatua hiyo ilidhihirishwa kama uadhama, karibukaribu sana baadaye Mungu alitekeleza hatua ya kazi ya kuadibu, na kisha kukaja majaribio ya kifo. Katika kazi kama hiyo, mwanadamu aliona ghadhabu, uadhama, hukumu, na kuadibu kwa Mungu, lakini aliona pia neema ya Mungu, na upendo na rehema Yake; yote aliyofanya Mungu, na yote yaliyodhihirishwa kama tabia Yake, ulikuwa upendo wa mwanadamu, na yote ambayo Mungu alifanya yaliweza kutimiza mahitaji ya mwanadamu. Aliyafanya ili kumfanya mwanadamu awe mkamilifu, na kutoa kwa kadri ya kimo cha mwanadamu. Kama Mungu hangefanya hili, mwanadamu hangekuwa na uwezo wa kuja mbele za Mungu, na hangekuwa na njia ya kuujua uso wa kweli wa Mungu. Tangu wakati ambapo mwanadamu alianza kwa mara ya kwanza kumwamini Mungu mpaka leo, Mungu amemkimu mwanadamu polepole kwa mujibu wa kimo chake, ili kwamba, ndani, mwanadamu amekuja kumjua Yeye polepole. Ni kwa kuweza kufika leo tu ndiyo mwanadamu ametambua hasa vile hukumu ya Mungu ni ya ajabu. Hatua ya kazi ya watendaji-huduma ilikuwa tokeo la kwanza la kazi ya laana tangu wakati wa uumbaji mpaka leo. Mwanadamu alilaaniwa kwenda katika shimo la kuzimu. Kama Mungu hangefanya hivyo, leo mwanadamu hangekuwa na ufahamu wa kweli wa Mungu; ni kupitia tu laana ya Mungu ndiyo mwanadamu hukutana kwa urasimu na tabia ya Mungu. Matukio hayo yalimwonyesha mwanadamu kwamba uaminifu wake haukukubalika, kwamba kimo chake kilikuwa kidogo sana, kwamba hakuwa na uwezo wa kuridhisha mapenzi ya Mungu, na kwamba madai yake ya kumridhisha Mungu wakati wote yalikuwa maneno matupu tu. Ingawa katika hatua ya kazi ya watendaji-huduma Mungu alimlaani mwanadamu, ikitazamwa kutoka leo hatua hiyo ya kazi ilikuwa ya ajabu: Ilileta mgeuzo mkubwa kwa mwanadamu, na kusababisha mabadiliko makuu katika tabia yake ya maisha. Kabla ya wakati wa watendaji-huduma, mwanadamu hakuelewa chochote kuhusu ukimbizaji wa maisha, ni nini maana ya kumwamini Mungu, au hekima ya kazi ya Mungu, wala hakufahamu kwamba kazi ya Mungu inaweza kumjaribu mwanadamu. Tangu wakati wa watendaji-huduma mpaka leo, mwanadamu huona vile kazi ya Mungu ni ya ajabu, haiwezi kueleweka kwa mwanadamu, na akitumia akili yake hawezi kufikiria jinsi Mungu hufanya kazi, na pia huona vile kimo chake ni kidogo na kwamba kiasi kikubwa chake ni cha kutotii. Mungu alipomlaani mwanadamu, ilikuwa ili Atimize athari, na Hakumuua mwanadamu. Ingawa Alimlaani mwanadamu, Alifanya hivyo kupitia maneno, na laana Zake hazikumwangukia mwanadamu kwa kweli, kwani kile ambacho Mungu alilaani kilikuwa kutotii kwa mwanadamu, na kwa hiyo maneno ya laana Zake pia yalikuwa kwa ajili ya kumfanya mwanadamu awe mkamilifu. Kama Mungu atamhukumu mwanadamu au kumlaani, yote mawili humfanya mwanadamu kuwa mkamilifu: Yote mawili ni kwa ajili ya kukifanya kamili kile ambacho ni kichafu ndani ya mwanadamu. Kupitia njia hii mwanadamu alisafishwa, na kile ambacho kilikuwa kinakosekana ndani ya mwanadamu kilifanywa kamilifu kupitia maneno na kazi Yake. Kila hatua ya kazi ya Mungu—kama ni maneno makali, au hukumu, au kuadibu—humfanya mwanadamu kuwa mkamilifu, na inafaa kwa uhalisi. Kotekote katika enzi zote Mungu hajawahi kufanya kazi kama hii; leo, Yeye hufanya kazi ndani yenu ili muweze kufahamu hekima Yake. Ingawa mmepitia maumivu fulani ndani yenu, mioyo yenu inajisikia thabiti, na kwa amani; ni baraka yenu kuweza kufurahia hatua hii ya kazi ya Mungu. Haijalishi kile mnachoweza kupata katika siku za baadaye, yote mnayoona kuhusu kazi ya Mungu ndani yenu leo ni upendo. Kama mwanadamu hapitii hukumu na kuadibu kwa Mungu, matendo yake na ari daima yatakuwa nje, na tabia yake daima itaendelea kutobadilika. Je, hii inahesabika kama kupatwa na Mungu? Leo, ingawa bado kuna mengi ndani ya mwanadamu ambayo ni yenye kiburi na yenye majivuno, tabia ya mwanadamu ni imara zaidi kuliko awali. Mungu kukushughulikia wewe ni ili kukuokoa, na ingawa unaweza kuhisi maumivu kidogo wakati huo, siku itafika ambapo kutatokea mabadiliko katika tabia yako. Wakati huo, utakumbuka ya nyuma na kuona vile kazi ya Mungu ni ya hekima, na huo utakuwa wakati ambao utaweza kufahamu kwa kweli mapenzi ya Mungu. Leo, kuna watu wengine ambao husema kwamba wanafahamu mapenzi ya Mungu—lakini hiyo si ya kweli kamwe, wao wanazungumza upuuzi, kwa sababu wakati huu bado hawajafahamu kama mapenzi ya Mungu ni kumwokoa mwanadamu au kumlaani mwanadamu. Labda huwezi kuliona kwa dhahiri sasa, lakini siku itafika ambapo utaona kwamba siku ya kutukuzwa kwa Mungu imefika, na uone jinsi ni ya maana kumpenda Mungu, ili utakuja kuyajua maisha ya binadamu, na mwili wako utaishi katika ulimwengu wa kumpenda Mungu, kwamba roho yako itawekwa huru, maisha yako yatajaa furaha, na kwamba daima utakuwa karibu na Mungu, na utamtegemea Mungu daima. Wakati huo, utajua kweli jinsi kazi ya Mungu ni ya thamani leo.
Leo, watu wengi sana hawana ufahamu huo. Wao huamini kwamba mateso hayana thamani, wao hukanwa na ulimwengu, maisha yao ya nyumbani yamesumbuliwa, wao si wapendwa wa Mungu, na matazamio yao ni matupu. Kuteseka kwa watu wengine hufikia kiwango fulani, na fikira zao hugeukia kifo. Huu si upendo wa kweli kwa Mungu; watu kama hao ni waoga, hawana ustahamilivu, wao ni wadhaifu na wasio na nguvu! Mungu ana hamu ya mwanadamu kumpenda Yeye, lakini kadri mwanadamu anavyompenda Yeye, ndivyo kuteseka kwa mwanadamu huwa kwingi zaidi, na kadri mwanadamu anavyompenda Yeye, ndivyo majaribio ya mwanadamu huwa makubwa zaidi. Ikiwa unampenda Yeye, basi kila aina ya mateso yatakufika—na ikiwa humpendi, basi labda kila kitu kitaendelea kwa urahisi kwako, na kila kitu kinachokuzunguka kitakuwa kitulivu kwako. Unapompenda Mungu, utahisi kwamba mengi kandokando yako hayawezi kushindikana, na kwa sababu kimo chako ni kidogo sana utasafishwa; aidha, huwezi kumridhisha Mungu, na daima utahisi kwamba mapenzi ya Mungu ni ya juu sana, kwamba hayawezi kufikiwa na mwanadamu. Kwa sababu ya haya yote utasafishwa—kwa sababu kuna udhaifu mwingi ndani yako, na mengi yasiyoweza kuridhisha mapenzi ya Mungu, utasafishwa ndani. Lakini lazima muone kwa dhahiri kwamba utakaso hutimizwa tu kupitia usafishaji. Hivyo, katika siku hizi za mwisho lazima muwe na ushuhuda kwa Mungu. Haijalishi mateso yenu ni makubwa vipi, mnapaswa kuendelea hadi mwisho kabisa, na hata wakati wa pumzi yenu ya mwisho, bado lazima muwe waaminifu kwa Mungu, na kudhibitiwa na Mungu; huku pekee ndiko kumpenda Mungu kweli, na huu pekee ndio ushuhuda thabiti na mkubwa sana. Unapojaribiwa, unapaswa kusema: “Moyo wangu ni wa Mungu, na Mungu tayari amenipata. Siwezi kukuridhisha wewe—lazima nitoe kila kitu changu ili kumridhisha Mungu.” Kadri unavyomridhisha Mungu, ndivyo Mungu hukubariki zaidi, na ndivyo nguvu za upendo wako kwa Mungu huwa kuu zaidi; kwa hiyo, vilevile, utakuwa na imani na azimio, na utahisi kwamba hakuna kilicho na thamani zaidi au cha maana kuliko kutumia maisha ukimpenda Mungu. Inaweza kusemwa kwamba mwanadamu anatakiwa tu kumpenda Mungu ili kuishi bila huzuni. Ingawa kuna nyakati ambazo mwili wako ni dhaifu na unazongwa na matatizo mengi ya kweli, katika nyakati hizi utamtegemea Mungu kweli, na ndani ya roho yako utafarijiwa, na utahisi hakika, na kwamba una kitu cha kutegemea. Kwa njia hii, utaweza kushinda hali nyingi, na kwa hiyo hutalalamika kuhusu Mungu kwa sababu ya uchungu unaopitia; utataka kuimba, kucheza, na kuomba, kukusanyika na kuwasiliana kwa karibu, kumfikiria Mungu, na utahisi kwamba watu wote, mambo, na vitu vilivyo kandokando yako ambavyo vimepangwa na Mungu vinafaa. Kama humpendi Mungu, yote ambayo unategemea yatakuwa yenye kero kwako, hakuna kitakachokuwa cha kufurahisha machoni mwako; ndani ya roho yako hutakuwa huru bali wa kudhulumiwa, moyo wako daima utalalamika kuhusu Mungu, na daima utahisi kwamba unapitia mateso mengi sana, na kwamba ni udhalimu sana. Kama hufuatilii kwa ajili ya furaha, bali ili umridhishe Mungu na kutoshtakiwa na Shetani, basi ukimbizaji kama huo utakupa nguvu nyingi za kumpenda Mungu. Mwanadamu anaweza kutekeleza yote yanayonenwa na Mungu, na yote ayafanyayo yanaweza kumridhisha Mungu—hii ndiyo maana ya kuwa na hakika. Kufuatilia ridhaa ya Mungu ni kuutumia upendo wa Mungu kutia maneno Yake katika vitendo; pasipo kutia maanani wakati—hata kama wengine hawana nguvu—ndani yako bado kuna moyo unaompenda Mungu, ambao unamtamani Mungu sana, na humkosa Mungu. Hiki ni kimo halisi. Jinsi ambavyo kimo chako ni kikubwa hasa hutegemea jinsi upendo wako kwa Mungu ulivyo mkuu, kama unaweza kusimama imara wakati unajaribiwa, kama wewe ni mdhaifu hali fulani inapokujia, na kama unaweza kusimama imara wakati ambapo ndugu zako wanakukataa; majilio ya ukweli yataonyesha hasa upendo wako kwa Mungu ukoje. Inaweza kuonekana kutoka kwa kazi nyingi ya Mungu kwamba Mungu kweli anampenda mwanadamu, ni hasa tu macho ya roho ya mwanadamu bado hayajafunguliwa kabisa, na hawezi kufahamu kazi nyingi ya Mungu, na mapenzi ya Mungu, na vitu vingi ambavyo ni vya kupendeza kuhusu Mungu; mwanadamu ana upendo kidogo sana wa kweli kwa Mungu. Umemwamini Mungu kotokote katika wakati huu wote, na leo Mungu amezuia njia zote za kutoroka. Kusema kwa kweli, huna chaguo lingine ila kuifuata njia sahihi, njia sahihi ambayo umeelekezwa kwayo kwa hukumu kali na wokovu mkubwa kabisa wa Mungu. Ni baada tu ya kupitia taabu na usafishaji ndiyo mwanadamu hujua kwamba Mungu ni wa kupendeza. Baada ya kupitia mpaka leo, inaweza kusemwa kwamba mwanadamu amekuja kujua sehemu ya kupendeza kwa Mungu—lakini hili bado halitoshi, kwa sababu mwanadamu amepungukiwa sana. Lazima apate uzoefu zaidi wa kazi ya Mungu ya ajabu, na zaidi ya usafishaji wote wa mateso uliowekwa na Mungu. Ni wakati huo tu ndiyo tabia ya maisha ya mwanadamu itaweza kubadilishwa.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Ijumaa, 8 Februari 2019

Imani Tatu katika Mungu wa Vitendo

Sura ya 16. Imani Tatu katika Mungu wa Vitendo

Ndani ya familia ya Mungu, kuna imani kadhaa tofauti katika Mungu; imani hizi tofauti lazima zitambulishwe ili kuona wewe ni wa gani.
Na imani ya aina ya kwanza, ambayo pia ni aina bora zaidi, mtu huyo ana uwezo wa kuyaamini maneno ya Mungu katika vitu vyote; ana uwezo wa kukubali ufichuzi wote wa Mungu, ushugulikiaji, na upogoaji; yeye ni mwagalifu kwa mapenzi ya Mungu, hupenda, ni mwaminifu kwa, na humwabudu Mungu, na ako tayari kutenda ukweli. Imani kama hiyo huzaa maisha, na inawezesha mtu kupata mabadiliko katika tabia na kupatwa na Mungu.
Na imani ya aina ya pili, mtu huyo anamwamini Mungu kwa kiasi, lakini pia ni mwenye tuhumu kwa kiasi. Wakati kazi ya Mungu hairidhiani na yeye, angefanya ulinganishi katika moyo wake, akiwa na shaka kama Mungu Anapaswa kuwa akifanya vitu kama hivyo. Mara kwa mara anamtuhumu Mungu, kwa hivyo ana uwezo tu wa kumtii Mungu kwa kiasi, na hana uwezo wa kumtii Mungu katika vitu vingine; anaweza kulitii lile ambalo analiamini ni sawa, lakini ana mawazo yake mwenyewe anapokabiliwa na vitu ambavyo anahisi si sawa, na migongano katika moyo wake, na anakataa kuyatekeleza. Hili pia ni aina ya imani. Kimo cha watu siku hizi ni hasa kama hiki, wao wana uwezo tu wa kutii kile wanachohisi kuwa sawa, wao hawana uwezo wa kutii kile wanachohisi si sawa, na hawatatekeleza kile ambacho hawako tayari kufanya. Kadhalika, wakati mwingine hali ikiwa, wana shauku na Mungu, wakihisi kwamba wanapaswa kuwa waangalifu kwa mzigo wa Mungu, hivyo wanatimiza wajibu wao; au wakati mwingine wanashughulishwa na ushirika, wanapata Mungu kuwa wa kupendeka kabisa, na sasa tu ndio wenye imani katika Mungu kwa kiasi fulani. Hasa, imani yao katika Mungu ni tu kufuata umati; hawana upendo kwa Mungu, wala si waangalifu kwa Mungu, wakati bila shaka hawamtii na hawamwabudu Mungu kwa kweli. Kwa watu walio na imani kama hii katika Mungu, wako tu na kiasi cha wastani cha upendo, uangalifu, na utiifu kwa Mungu, kwa muda fulani, na inafanyika tu wakati Roho Mtakatifu hasa Anasonga, wakati Roho Mtakatifu anafanya kazi Yake. Wakati wako katika hali mbaya, au wakati wanachanganywa na wengine, wakati wao ni dhaifu na wamekata tamaa, vitu hivi vimeenda, vimetokomea, wakati wao wenyewe hawana habari jinsi hilo limekuja kupita. Hawana uwezo tena wa kumpenda Mungu hata wakitaka, hawana motisha ya kutenda maneno ya Mungu tena, na kisha wanaona kazi ya Mungu kama ya desturi sana, ya kawaida sana; hata kama wao hawana tuhuma tena, wao hawana ari yoyote tena. Kimo cha watu wengi zaidi kiko katika hatua hii, na hii ndiyo aina ya pili ya imani.
Na aina ya tatu ya imani, mtu hana uelewa wa Mungu mwenye mwili, kwake Yeye hujitokeza tu kama mtu wa kawaida, na hakuna tofauti kubwa inaweza kutambulishwa. Kwa hivyo, anamchukulia Mungu mwenye mwili kama tu mtu wa kawaida lakini mwenye cheo cha heshima, ana uwezo wa kufuatana na Mungu na kusema kitu kizuri, na pia ana uwezo wa kuandamana katika imani, lakini imani hii si imani halisi. Ana uwezo wa kufuatana na mambo ya upuuzi mara moja moja, lakini hakuna upendo kwa Mungu katika mtu wa aina hii—upendo si kujali kuhusu mwili lakini utiifu wa kweli katika kazi ya mtu na katika kutimiza wajibu wa mtu, kuwa mwangalifu kwa Mungu na kumcha Mungu. Upendo kwa Mungu ni kitu ambacho mtu aliye na uzoefu mkubwa tu anaweza kutangaza, si kitu ambacho mtu anaweza kusema kwa kupitia tu, kuona kwamba mtu ametekwa na hisia kali hivyo kusema kwamba huyu na huyu humpenda Mungu sana. Ama kusema kwamba watu kutoka dhehebu fulani humpenda Mungu kwa kweli. Huu ni upuuzi. Mtu kama huyu hawezi kukubali na kutii kwa urahisi kunapokuja kwa mambo ya upuuzi, na anapokabiliwa na mambo ya muhimu yanayohusiana na ukweli, hawezi kutii tu, na pia ana mawazo yake mwenyewe, hata anakuwa na tuhuma kuhusu Mungu. Watu kama hawa pia wako katika walio wengi. Wao ni wenye tuhuma kila wakati kuhusu Mungu: Je, huyu ni Mungu? Je, ni kwa nini Yeye hafanani na Mungu? Baadhi ya mambo Alivyosema labda yameelekezwa na Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu alimwelekeleza kusema mambo fulani, na kufanya vitu fulani. …Imani ya watu kama hawa ni ya kusikitisha zaidi.
Kiwango cha imani ya mtu katika Mungu, utiifu kwa Mungu, upendo, uangalifu, na uchaji kwa Mungu, kinatambulishwa hasa na yafuatayo:
Kwanza, kina msingi katika ikiwa mtu huyo hupenda ukweli. Kama unapenda ukweli basi unaweza kuendelea kuufuatilia zaidi, kisha unaweza kulenga kuwa na uelewa wa ukweli, wa maneno ya Mungu, wa kazi ya Mungu, wa umuhimu wa kupata mwili kwa Mungu, wa tabia ya Mungu, na uelewa wa Mungu una msingi hasa katika hiki kitu kimoja. Kadiri Unavyoweza kuelewa Mungu zaidi ndivyo unavyoweza kumtambua zaidi; kadiri unavyoweza kumwelewa Mungu zaidi ndivyo unavyoweza kumfuata bila kuyumbayumba. Hiyo ni, uelewa wa Mungu una msingi katika kufuatilia ukweli.
Pili, kina msingi katika uelewa wa mtu huyo wa Mungu mwenye mwili, hiyo ni muhimu. Bila uelewa wa Mungu wa vitendo, mazungumzo ya kumtii Mungu, kumpenda Mungu, kushuhudia Mungu, na kumhudumia Mungu yote ni maneno matupu. Vitu kama hivi haviwezi tu kufikiwa.
Tatu, kina msingi katika ubinadamu wa mtu huyo, lakini hili si halisi. Kwa sababu, baadhi ya watu wana ubinadamu mzuri, wao ni watu wazuri, lakini wao hawapendi ukweli. Kama wao hawana uelewa kabisa wa Mungu mwenye mwili, basi imani yao haiwezi kusiama, na wakati mwingine nia zao nzuri bila kujua husababisha madakizo. Je, unaweza kusema kwamba wao ni watu ambao wanamwamini Mungu kwa kweli? Wao ni wenye shauku, ni wa asili nzuri, na hufanya mambo fulani mazuri, lakini haya ni tabia nzuri tu ya nje, haya ni sura ya juu juu, haya hayaonyeshi kwamba imani yao ni halisi. Ukisema kwamba kwa kweli unamwamini Mungu, kweli unampenda Mungu, lazima uwe na uwezo wa kusema kwa nini unampenda Mungu, upendo wako kwa Mungu una msingi kwa nini, kwa nini unamwamini Yeye, kama wewe unaufuata umati tu ama unamwamini Yeye kwa sababu unaweza kumwona kwa kweli kama Mungu, imani na upendo wako kwa Mungu yana msingi katika ukweli upi: Haya lazima yategemezwe kwa misingi. Baadhi ya watu hupenda kusema kwamba wanamwamini Mungu kwa kweli na wanampenda Mungu, lakini wakati mtu anatamani kuwasiliana nao ukweli kwa uzito, hawana kitu cha kusema. Nimesikia watu wengi wakisema: “Mimi husikiza chochote ambacho Mungu husema, naamini yote ambayo Mungu husema, kwa njia yoyote ambayo Yeye huyasema. Sina mawazo yangu mwenyewe bila kujali kile Mungu husema, sina mawazo yangu mwenyewe bila kujali kile Mungu hufanya.” Je, wewe kweli ni mtu anayempenda Mungu kwa sababu tu umesema mambo kama haya? Lazima uwe na uzoefu halisi, lazima uwe na uwezo wa kuongea kuhusu uelewa halisi wa Mungu mwenye mwili. Pia, ni nini kiini cha Mungu, ni vitu vipi ambavyo watu huona vigumu kumtii Mungu katika, ni vitu vipi ambavyo watu wanaweza kumtii Mungu katika, wanamtii Mungu kwa kiasi gani, ni vitu vipi ambavyo huna uwezo wa kumtii Mungu katika, unatatua vipi mawazo yako kuhusu Mungu, unapanua vipi uelewa wako wa Mungu polepole? Kama unakosa uzoefu kama huo, basi huna mapenzi ya kweli kwa Mungu. Baadhi ya watu wana furaha hasa wanapoona kufika kwa Mungu, wanampokea kwa ukarimu, na kisha wanalia Mungu Anapoondoka. Watu wengine hufikiri kwamba hili ni onyesho la upendo wake kwa Mungu, lakini hili kweli linaweza kuonyesha kwamba anampenda Mungu? Hili linaweza kuonyesha tu kwamba anao moyo wenye ari, lakini mtu hawezi kusema kwamba matendo na maonyesho yake ni upendo kwa Mungu, kwamba ni imani ya kweli. Baadhi ya watu hutoa pesa kiasi, lakini hilo ni upendo kwa Mungu? Ama unaenda haraka kumwaga gilasi ya maji wakati unaambiwa, lakini hilo ni utiifu wa kweli? Kadhalika, watu wengine husema: “Nilimwamini Mungu baada ya mimi kusoma maneno ya Mungu, niliamini katika kupata mwili kwa Mungu, sina shaka baada ya mimi kumwona Mungu katika mwili wa kawaida.” Je, hili linaweza kuitwa imani ya kweli? Je, umekuwa na ushughulikaji na Mungu? Je, umejihusisha na Yeye? Je, unajua tabia Yake? Je, unajua ni nini Yeye hupenda? Je, unajua vitu unafanya ambavyo vinaikosea tabia Yake? Je, unajua upotovu ndani yako ambao Yeye huchukia? Je, unajua watu ambao Ameleta tabia Yake yenye haki kwao? Je, unajua ni watu wagani Yeye huchukia? Je, unajua ni masuala yapi unayo ambayo Yeye huchukia zaidi? Kama hujui vitu vyovyote kama hivi, linaonyesha kwamba kwa kweli huna uelewa wa Mungu. Huwezi kusema kwamba unamwamini Mungu kwa kweli, huwezi kusema kwamba unamtii Mungu kabisa, na bila shaka huwezi kusema kwamba unafanya vitu kulingana na mapenzi ya Mungu, kwamba unampenda Mungu, unamtii Mungu, ama unamwelewa Mungu. Unaweza kusema tu, kuhusu jambo hili, unayaelewa mapenzi Yake, unajua ni nini Yeye hupenda, kwamba unatenda kulingana na mapenzi ya Mungu katika jambo hili, kwamba unatenda kulingana na ukweli, kwamba unamtii katika jambo hili. Je, wewe ni mtu mtiifu kwa Mungu kwa sababu umemtii katika jambo hili tu? Huwezi kusema hilo, na kusema kwamba mtu humpenda Mungu kwa kuweka msingi tu kwa kitu cha juujuu, hilo ni kosa kubwa. Ukweli kwamba ulitenda kitu kizuri, ama kwamba umemjali Mungu hasa, huonyesha tu kwamba wewe ni mtu mwema, lakini hauonyeshi kwamba wewe ni mwangalifu kwa mapenzi ya Mungu. Bila shaka, upendo wa Mungu na kuwa mwangalifu kwa mapenzi ya Mungu yamejengwa juu ya msingi wa ubinadamu, na hakuwezi kuwa na upendo wa Mungu bila ubinadamu, kwa hivyo kila mmoja wenu lazima ajichunguze na aangalie mahali alipo. Baadhi ya watu hufikiri kwamba wao wako karibu hapo, lakini hili si lenye uhalisi; ilhali baadhi ya watu huenda kwa kiwangi kilichokithiri na hufikiri kwamba hakuna kitu kizuri kuwahusu, kwamba hawawezi kuachwa, na huu ni mtazamo hasi. Baadhi ya watu hufikiri kwamba hakuna mazuri ndani yao, na baadhi ya watu hujifafanua kama mtu anayempenda Mungu. Wao wako katika upande wa kushoto kabisa au katika upande wa kulia kabisa; huu ndio uhalisi wa watu hawa, ambao unaonyesha kwamba wao bado hawako katika njia sawa. Wao wanapaswa kuendelea kujitahidi kuwa dhahiri kuhusu ukweli, na kuingia katika uhalisi, ili kufuata mapenzi ya Mungu.
Soma Zaidi: Asili ya Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumatatu, 28 Januari 2019

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Pili

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Pili

Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Pili Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”. Maudhui ya video hii: Awamu Sita katika Maisha ya Binadamu Kuzaliwa: Awamu ya Kwanza 1. Maisha Mapya Yanazaliwa Kulingana na Mipango ya Muumba 2. Kwa Nini Binadamu Tofauti Wanazaliwa Katika Hali Tofauti Kukua: Awamu ya Pili 1. Hali Ambazo Mtu Hukulia Ndani Zimepangwa na Muumba 2. Hali Mbalimbali Ambazo Watu Hukulia Ndani Husababisha Wajibu Tofauti
Mwenyezi Mungu alisema, Tangu unapoingia katika dunia hii ukilia, unaanza kutekeleza wajibu wako. Unachukua jukumu lako katika mpango wa Mungu na katika utaratibu wa Mungu. Unaanza safari ya maisha. Licha ya asili yako na licha ya safari iliyoko mbele yako, hakuna kitakachoepuka mpango na utaratibu ambao mbingu imeweka, na hakuna aliye na udhibiti wa hatima yake, kwa maana Anayetawala juu ya kila kitu ndiye tu Aliye na uwezo wa kazi hiyo. Tangu siku aliyoumbwa binadamu, Mungu amekuwa thabiti katika kazi Yake, kusimamia ulimwengu huu na kuelekeza mabadiliko na harakati ya mambo yote. Kama kila kiumbe, mwanadamu bila kujua anapata lishe ya utamu na mvua na umande kutoka kwa Mungu. Kama vitu vyote, mwanadamu bila kujua anaishi chini ya mpango wa mkono wa Mungu. Moyo na roho ya mwanadamu vimeshikwa katika mkono wa Mungu, na maisha yote ya mwanadamu yanatunzwa machoni mwa Mungu. Haijalishi kama unayaamini mambo haya au la, vitu vyote, vilivyo hai au vilivyokufa, vitahamishwa, vitabadilika, kufanywa vipya, na kutoweka kulingana na mawazo ya Mungu. Hivi ndivyo Mungu anavyotawala juu ya kila kitu.
kutoka kwa Mungu Ndiye Chanzo cha Uhai wa Mwanadamu

Jumanne, 22 Januari 2019

Kutupa mbali Jozi La Shetani Kunakomboa

Kutupa mbali Jozi La Shetani Kunakomboa

Momo Mji wa Hefei, Mkoa wa Anhui
Kabla ya kumwamini Mungu, bila kujali chochote nilichokuwa nikifanya, sikuwahi kutaka kubaki nyuma. Nilikuwa tayari kukubali shida yoyote ili mradi ingemaanisha ningeinuka juu ya kila mtu mwingine zaidi. Baada ya kumkubali Mungu, mtazamo wangu uliendelea kuwa sawa, kwa sababu niliamini kikamilifu msemo, “Hakuna maumivu, hakuna faida,” na kuona mtazamo wangu kama ushahidi wa msukumo wangu. Wakati Mungu alinifichulia ukweli, hatimaye niligundua kuwa nilikuwa nikiishi chini ya jozi la Shetani, nikiishi chini ya miliki yake.
Sio muda mrefu sana uliopita, kanisa lilifanya mipango ya kumtuma dada niliyeshiriki naye ili aweze kuhudumu katika nafasi ya uongozi. Niliposikia habari hizo, nilisononeka. Sisi sote tulikuwa tunahudumu katika majukumu ya uongozi hadi tulipoteuliwa tena kama wahariri. Sasa dada yangu angerudia nafasi ya uongozi na kumtumikia Mungu akiwa na uwezekano usio na kikomo wa ukuaji, lakini bado ningebakia nikifanya kazi kwa dawati, nikitekeleza kazi yangu bila kuonekana. Kunaweza kuwa na mategemeo gani ya baadaye katika hayo? Kwa kubadili mawazo, nilikumbushwa msemo wa kale, “Kuna njia milioni tofauti za mafanikio.” Ili mradi ningekamilisha kazi yangu vizuri, ningeweza pia kufanikiwa. Nilihitaji tu kuzidisha jitihada zangu katika kutafuatilia ukweli. Ikiwa ningelenga kuhariri mahubiri ili yawasilishe ukweli vizuri zaidi, labda siku moja viongozi wangeona kuwa nilielewa ukweli. Kisha wangenipandisha cheo na siku zangu za baadaye zingekuwa pia za kuchangamsha. Baada ya utambuzi huu, mawingu ya kijivu yalianza kurejea kwa ajili ya uamuzi mpya. Nilijitosa katika kazi yangu, na nikala na kunywa neno la Mungu wakati sikuwa na shughuli, bila kuthubutu kulegea hata kwa muda.
Siku moja, niliona kifungu kinachofuata katika Mahubiri na Ushirika Kuhusu Kuingia Katika Maisha: “Kila kitu kinachokuzuia kumtafuta Mungu na kutafuta ukweli ni mojawapo ya pingu za Shetani. Ukiwa umefungwa na moja kati ya minyororo ya Shetani, unaishi maisha yako chini ya miliki yake.” Baada ya kusikia haya, sikuweza kujizuia ila kuuliza, “Ni ipi kati ya jozi za shetani ninayoishi chini yake? Ni ipi kati ya sumu zake inayozuia utafutiliaji wangu wa ukweli?” Nilipojaribu kutafakari swali hili kwa kimya, nilikumbushwa hali yangu ya hivi karibuni. Baada ya dada yangu kupelekwa kwenye daraja lake jipya, sikuwa wa kutoonyesha hisia. Kwa kweli, nilijitolea zaidi kula na kunywa neno la Mungu, kumwomba Mungu, na kutekeleza kikamilifu kazi yangu. Kijuujuu, nilionekana kuwa na bidii zaidi katika kutafuta ukweli kuliko hapo awali, lakini ukifunua pazia na kuichambua, uwezo wangu wa kukubali kubaki nyuma ni kwa sababu nilikuwa na matamanio ya kuendelea siku moja. Tamaa yangu ya kuchochea kuwa bora zaidi ilikuwa ndiyo sababu sikuwa wa kutoonyesha hisia na badala yake nilifuatilia ukweli zaidi mno, lakini kunakodhaniwa kuwa ufuatiliaji wangu wa ukweli kulikuwa tu njonzi, ufuatiliaji ulio mchafu. Nilikuwa nikishiriki ufuatiliaji wa muda wa ukweli ili kutimiza madhumuni yangu ya kibinafsi. Nikifikiri nyuma kwa miaka yangu iliyotumika kufuata Mungu, nilitambua kuwa dhabihu zangu zote zilikuwa zimelipwa na sumu ya Shetani “Hakuna maumivu, hakuna faida.” Hivi ndivyo ilivyonifunga pingu isiyoonekana na kunitia kujitahidi kwa ubora. Nilipokuwa na cheo tayari, nilikuwa bado nikitafuta hata cha juu zaidi; Nilipopoteza cheo changu au niliposhindwa kujiendeleza, sikuwa wa kutoonyesha hisia; Mimi bado nilionekana kuwa na hiari ya kulipa bei ili kutafuta ukweli. Hata hivyo, hii haikuwa kwa sababu nilielewa ukweli na nilikuwa tayari kujitoa mhanga kwa ajili yake. Nilitaka tu kutumia kuonekana kwa kujitoa mhanga kwa jitihada za kufanikiwa. Hapo ndipo nilipobaini hatimaye kuwa msimamo wangu wa “Hakuna maumivu, hakuna faida,” ulikuwa kweli mojawapo wa sumu za Shetani zilizokuwa zikitiririka kupitia mishipa yangu. Nilikuwa nimetanganywa; sumu ilikuwa imeninyonya ubinadamu wangu wote. Nilikuwa na kiburi na mwenye tamaa bila hisia yoyote ya taswira yoyote. Mambo hayo yote yalifanyika kabisa chini ya pua langu. Kwa kweli nilifikiri kuwa matamanio yangu yalikuwa ushuhuda wa matarajio yangu. Nilidhani kuwa hali yangu ya kiburi ya kutotaka kubaki nyuma ilikuwa ishara ya motisha yangu. Niliabudu uongo wa Shetani kama ukweli na kuuona kama beji ya heshima badala ya alama ya fedheha. Nilikuwa mjinga kiasi kipi hadi kudanganyika na Shetani kiasi kile, kutojua kutofautisha kati mema na uovu? Hatimaye niliona jinsi nilivyokuwa ovyo. Nilijifunza pia jinsi Shetani ni mwenye kudhuru kwa siri na mwenye kuleta hizaya. Shetani hutumia udanganyifu spesheli kutudanganya na kutupotosha. Hutupotosha, na tunaapa uaminifu kwa mipango yake danganyifu. Hii yote hufanywa bila ujuzi wetu. Tunadhani tunatafuta ukweli na kujitolea kwa ajili ya kweli, lakini kwa kweli tunaishi katika kujidanganya. Sumu za Shetani zina nguvu kabisa! Ikiwa haingekuwa nuru yake Mungu, singewahi kamwe kuona ukweli kwamba nilikuwa nimepotoshwa na Shetani, na hakika singeweza kamwe kubaini mipango yake ya udanganyifu. Ikiwa haingekuwa nuru ya Mungu, ningeendelea kuishi chini ya jozi la Shetani, hadi wakati Shetani hatimaye anitumie mzima.
Wakati huo, nilifikiria kuhusu maneno ya Mungu: “Kama wewe unafurahia kuwa mtoa huduma katika nyumba ya Mungu, ukifanya kazi kwa bidii na kwa makini bila kuonekana, siku zote ukitoa na katu hupokei, basi Nasema kwamba wewe ni mtakatifu mtiifu, kwani hutafuti tuzo na unakuwa tu binadamu mwaminifu” (“Maonyo Matatu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mungu yalinionyesha njia ya kutenda: Kama mmoja wa viumbe wa Mungu, napaswa kumpenda na kumridhisha bila masharti na kutekeleza wajibu wangu kwa dhati. Hii ndiyo hisi ambayo kiumbe mmoja wa Mungu anapaswa kumiliki. Huu ni ufuatiliaji ambao unaambatana na mapenzi Yake. Kuanzia siku ya leo kwenda mbele, nitafanya liwezekanalo kufuatilia ukweli. Nitategemea ukweli ili kupenya udanganyifu wa Shetani na kutupa jozi lake. Sitafuatilia tena kitu chochote cha mwili. Badala yake, nitafanya kazi kwa bidii kwa kutoonekana, kutimiza wajibu wangu kumkidhi Mungu. Hata nikiachwa bila kitu chochote mwishowe, nitaendelea kwa hiari bila majuto yoyote, kwa sababu mimi ni moja tu wa viumbe duni wa Mungu. Kumridhisha Muumba ni nia yangu moja ya kweli maishani.
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Vitabu.

Jumanne, 25 Desemba 2018

Namna ya Kumridhisha Mungu katikati ya Majaribu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki,  Hukumu na Kuadibu

Sura ya 59. Namna ya Kumridhisha Mungu katikati ya Majaribu

Ninaibua maswali machache kwa tafakari yenu: Tangu mara ya mwisho tuliposema kwamba kutakuwa na miaka saba mingine ya majaribu makubwa, iwe ni kwa dhiki au majanga, je, mmegundua kusudi la Mungu kupitia kwa hayo? Ni asili gani ya binadamu mnaweza kuona katika mijibizo na mitazamo ya watu kwa miaka hii saba ya majaribu? Hili litachanganuliwa vipi? Fikirieni hilo. Ninazungumzia asili ya binadamu katika kila ushirika, kufikia chanzo, kuchanganua asili ya binadamu, na kuchanganua kiini. Ni juu yenu basi kuwasiliana ufahamu wenu kuhusu hizi mada.
Mnapaswa kuelewa kusudi la Mungu na ni lazima muijue asili ya binadamu kupitia hii miaka saba ya majaribu. Kwa hakika, kila sentensi ya Mungu ina kusudi Lake, ambamo mmefichwa ukweli. Bila kujali ni suala gani linafanyiwa ushirika, au ni ukweli gani unaoenyeshwa, ndani yake mna njia ambayo watu wanapaswa kupitia, matakwa ya Mungu kwa watu, na kusudi la Mungu kwa wanaomtafuta. Katika haya mazungumzo ya majaribu, dhiki, na hatimaye mateso, matakwa kwa watu na kusudi la Mungu pia vimo ndani. Watu, bila shaka, wanaonyesha hisia kwa mitazamo yao, kwa kuwa watu hawajaundwa kwa mbao; wako hai, na wanaonyesha hisia kwa kila kitu. Je, kuna maana kuchanganua ni hali gani za asili ya binadamu zinawakilishwa katika hisia za watu? Ina maana kushiriki kuihusu? Uchanganuzi utasaidia watu kuliona hilo wazi, kulijua wao wenyewe, na kujua vyema kabisa mioyoni mwao ili kwamba hatimaye wawe na njia mwafaka ya kuchagua. Ikiwa mtu amekanganyikiwa na hajui kusudi la Mungu, haelewi ukweli, na ana ufahamu mdogo kuhusu matakwa ya Mungu kwake na wajibu anaopaswa kutekeleza, au njia gani anapaswa kutembea, pengine mtu wa aina hii hatasimama imara. Kwa hivyo, inapaswa kujulikana ni njia gani inapaswa kutumiwa baadaye wakati wa majaribu mbalimbali.
Kila wakati majaribu ya miaka saba yanapotajwa, kuna watu wengi wanaohisi vibaya sana na kuvunjika moyo kusiko kwa kawida, na kuna watu wengine ambao hulalamika, na kuna mchanganyiko wa hisia. Ni dhahiri kutokana na hizi hisia kwamba watu sasa wanahitaji majaribu haya, wanahitaji aina hii ya dhiki na utakasaji. Watu humwamini Mungu kwa nia ya kutaka kupata baraka siku zijazo. Watu wote wana kusudi na tumaini hili. Hata hivyo, upotovu ndani ya asili ya binadamu ni lazima uondolewe kupit majaribu. Katika hali yoyote usiyoipita, ni katika hizi hali ambamo ni lazima usafishwe—huu ni mpango wa Mungu. Mungu anakutengenezea mazingira, Akikulazimisha usafishwe hapo ili ujue upotovu wako mwenyewe. Hatimaye unafika hatua ambapo unaona heri kufa na kuziacha njama na tamaa zako, na kutii mamlaka na mipango ya Mungu.
Hivyo ikiwa watu hawana miaka kadhaa ya usafishaji, ikiwa hawana kiwango fulani cha mateso, hawataweza kuepuka utumwa wa upotovu wa mwili katika mawazo na mioyo yao. Katika hali zozote zile bado ungali mtumwa wa Shetani, katika hali zozote bado ungali na tamaa zako mwenyewe, matakwa yako mwenyewe—ni katika hali hizi ambamo unapaswa kuteseka. Mafunzo yanaweza kupatikana tu katika mateso, yaani, kuweza kupata ukweli, na kuelewa kusudi la Mungu. Kwa kweli, ukweli mwingi unafahamika katika uzoefu wa majaribu makali. Hakuna asemaye kuwa kusudi la Mungu linajulikana, kwamba uweza na busara Yake vinafahamika, kwamba tabia ya haki ya Mungu inaonekana katika mazingira ya utulivu au katika hali zinazofaa. Hilo haliwezekani!
Mungu ametayarisha mazingira mwafaka ambamo Anawafanya watu kuwa wakamilifu, ila haijulikani kwa yeyote ni kwa nini Mungu anaweza kutaka kuwajaribu watu, kuwatakasa. Nyinyi nyote mnasema, “Mungu anawependaje wanadamu kwamba Anaweza kutayarisha miaka saba ya majaribu kuwatakasa watu na kuwafanya safi! Ni mvumilivu kiasi gani! Ni mwenye kuonyesha huruma kiasi gani!” Haina haja uyaseme haya, kila mmoja anaelewa mafundisho, lakini kwa hakika hakuna yeyote anayeifahamu hali halisi Je, miaka saba ya Mungu ya majaribu, miaka saba ya kazi ni ya nini? Bila shaka, inahitajika ili kwamba kazi Yake ifanyike. Hata bila kukuokoa, bado kuna upendo, sawa? Anapokuokoa, unasema, “Haya ni mapenzi aliyonayo Mungu kwetu, hii ni huruma Yake.” Je, Asingekuwa ametayarisha hii miaka saba ya majaribu, na kukamilisha kazi mara moja, bado kusingekuwepo upendo? Je, ingelikuwa miaka miwili ya majaribu, au mwaka mmoja, au siku ingalifika mara moja, je, hayo yasingekuwa mapenzi na huruma? Si kama unavyodhani: Miaka saba ya majaribu ni utakaso wa Mungu kwetu, ni kiwango Anachotupenda: ni lazima tutii. Unasema haya wakati tu hakuna njia nyingine. Hili linadhihirisha nini? Linadhihirisha uhasi, linadhihirisha lawama, na linadhihirisha kukosa njia mbadala na kukata tamaa. Mungu alisema kwamba kutakuwa na miaka saba mingine. Wacha iwe miaka saba basi. Kisha unakurupuka na kusema maneno mazuri: Mungu, Unatupenda; Mungu, ni kwa ajili ya kututakasa. Bila miaka saba ya majaribu, je, huo usingelikuwa mwisho wetu? Kusingelikuwa na fursa. Watu wengine wanatamani kubarikiwa sasa hivi. Hiyo inaweza kuwa faida halisi! Mtu kama huyo hajali kitu kingine chochote kile. Mtu kama huyu hafai hata kwa senti moja. Kuna kazi ya vitendo katika hii miaka saba. Je, haijasemwa awali kwamba maneno mengine ni njia, lakini vilevile ni ukweli? Hakuna kipengele ambacho ni maneno tu bila matendo. Kila kipengele kina dhima. Aidha, kama aionavyo mwanadamu, takribani kila kipengele kina njia, lakini njia hii si ya kukurairai, si ya kukudanganya. Badala yake ni mazingira ya kweli, hali halisi Hakuna njia mwafaka kuliko hii. Baada ya kusikia maneno haya, watu wengine hufikiri: Ikiwa ni kama usemavyo, hii miaka saba inapoisha, ni nani anaweza kutambua umesalia muda kiasi gani! Kutokana na mijibizo ya watu inaonekana kuwa asili ya binadamu imewekwa kwa namna kwamba baada ya kukumbana na majaribu ya mateso, kupokea uchungu mwilini, anataka kuuepuka na kuukataa. Hakuna hata mtu mmoja hujitokeza na kuchukua hatua ya kudai: Mungu, nipe majaribu fulani ya kuteseka, nipatie dhiki fulani. Mungu, nipatie taabu zaidi. Hili linadhihirisha kuwa kiasilia watu hawapendi ukweli. Iwe ni kusudi la Mungu au la, au inafaidi watu vipi, haijalishi ni nzuri kiasi gani, watu wote hukataa hali yoyote inayoiletea miili yao machungu au ile isiyoafiki matamanio yao. Kuna watu wasemao: “Sipingi. Nilifanya uamuzi zamani kuyatoa maisha yangu yote kwa Mungu. Nina furaha kabisa haijalishi ni miaka mingapi, na nitamtumikia Mungu kwa moyo. Sina lawama. Haijalishi ninakumbana na majaribu gani, haijalishi ninakutana na mateso gani, iwe ni kutelekezwa na familia au maumivu ya ugonjwa, nitafuata hadi mwisho.” Huku kutokuwa na lawama kwako pia ni aina ya hali hasi, kwa sababu kila wakati unapokumbana na kitu chochote, kila wakati unaposemewa maneno, kwa hakika huelewi maana iliyo ndani. Hii “sina mjibizo” unayoisema kwa hivyo si kingine bali ni kutojali, njia wakati ambapo hakuna njia nyingine. Hakuna jingine la kufanya ila hili, kwa hivyo unajilazimisha kufuata hata wakati ambapo hauko radhi. Kwa vyovyote vile hakuna awezaye kufaulu kuepuka miaka saba ya majaribu. Hata hivyo, hii ni tofauti na wewe kutaka kutoroka. Ungetamani kuepuka lakini huwezi. Hili ni jambo la asili ya mwanadamu. Lifikirie. Je, ndivyo ilivyo? Watu wengine wanahisi: Nilipokumbana na tukio kama hili miaka kumi iliyopita, daima nilifuata, na niliteseka sana, kwa hivyo ninaweza kuendelea kuvumilia kwa miaka michache. Kutafuta kwenu kwa kusudi la Mungu kumekanganyikiwa na hamjakutilia maanani. Hivyo, ikiwa kwa ndani hujayatii mapenzi ya Mungu, basi umeyasaliti na kukana mapenzi ya Mungu. Ijapokuwa huna hali hii, na hujafanya jambo hili, hizi dalili, haya mambo yaliyo ndani yako, yanamkana Mungu, kwa sababu unachokifiria na kutarajia kwa ndani sicho Mungu anachokihitaji. Aidha kwa hakika humsifu Mungu kutoka ndani ya moyo wako kwa yote Anayohitaji kutoka kwako na yote Anayofanya, iwe ni njia, au kile ulichoambiwa.
Na kwa kila kitu Mungu ambacho anawataka watu wafanye, chochote Mungu alichowapangia watu kulingana na mahitaji yao, asili ya binadamu ni kukikataa, kukosa kukikubali. Haijalishi unautangaza vipi msimamo wako, au iwe una ufahamu kidogo, kwa vyovyote vile, ufahamu wako wa mafundisho hauwezi kutatua kilicho katika asili yako. Kwa hivyo ninasema kwamba watu wengi wanazungumzia vitu vizuri katika mafundisho, na kusema maneno ya juujuu kuyastahimili. Hatimaye, japo, katika maombi wanasema: Nimepitia kwa ufanisi miaka mingi sana. Miaka saba si miaka mingi na wala si miaka michache. Tazama ninavyozeeka, jinsi afya yangu ilivyoharibika, na kwamba sina familia nzuri. Nimeandamana na Wewe miaka hii yote, nifanya bidii hata bila malipo, nimechoka ijapokuwa sijafanya kazi kwa bidii. Hata kama Utaipunguza hata kwa miaka michache, nifanyie hisani mara hii moja! Unajua udahaifu wa watu… Kwa kuomba maneno haya, ni kama kuna utiifu kidogo. Wanaendelea kusema “Unajua udhaifu wa watu”; kuna maana nyingine ndani ya maneno haya, ambayo ni kusema, Unajua udhaifu wa binadamu, basi ni kwa nini inachukua muda mrefu kiasi hiki? Je, hii si hali iliyo ndani mwa watu? Kwa hivyo, mnahisi mnafahamu vitu vingi, tayari mmevikubali, na kuonekana mmefahamu ukweli, lakini kwa hakika bado mnaukataa ukweli, na kwenda kinyume cha ukweli. Vitu mnavyovifanya haviambatani na ukweli. Japo kijuujuu hamjafanya vitendo viovu, na hamjatamka kitu chochote kibaya, hii imejikita tu kwa kutovunja amri za utawala, kwa kutoikosea tabia ya Mungu. Hujaelewa kusudi Lake na hata hivyo hauko tayari kulipokea. Hukubaliani na Yeye kufanya mambo kwa njia hii. Unafikiri: Iwapo nitaifanya kazi hii, sitapoteza muda na nitaikamilisha kazi hii kwa muda mfupi iwezakanavyo, ili kwamba niwasaidie watu wa Mungu kuepuka mateso zaidi kutoka kwa joka kuu jekundu, kuzuia kupotea kwa watu wengi zaidi, kuepuka mateso yangu. Je, hili si wazo walilonalo watu? Watu mioyoni mwao wanatumaini kufika kwa ufalme wa Mungu, na kuangamia kwa haraka kwa ulimwengu wa Shetani. Ni neema kubwa ikiwa neno moja la Mungu litawabadilisha. Mitazamo ya ndani ya watu, matamanio yao makubwa kwa hakika hayatekelezi kusudi la Mungu, na kimsingi hakuna kiini cha kutii. Hili pia linagusa ule msemo: Asilimia mia moja ya kile kilicho ndani ya asili ya binadamu ni usaliti. Kwa hivyo, kwa kulichanganua hili au lile tukio lenu, kwa kulichanganua hili suala, lile wazo, au ile hisia, iwe unaikabili kwa njia hasi, au unalalamika, ikiwa hujali au umenyamaza bila kusema neno, kuna ukinzani katika haya yote. Haya yote ni usaliti. Je, huu uchanganuzi ni sahihi? Nisingalichanganua hili, kungekuwepo na watu wanaohisi: Ninaweza kudhaniwa kuwa mtu mzuri. Ningekumbana na jambo hili miaka michache iliyopita, bila shaka ningelalamika, ikiwezekana ningerudi nyuma, lakini sasa silalamiki. Hulalamiki, lakini je una uelewa? Je, uelewa wako mdogo unajumuisha uelewa wa kweli? Kuna ukweli ndani yake? Je, uelewa wako unalingana na kusudi la Mungu? Je, umepata kibali cha Mungu? Je, una kiini cha kumtii Mungu? Je, uko radhi na tayari kumtii Mungu? Kama sivyo, basi bila shaka unakinzana na Mungu. Inawezekana kwamba hali yako ya moyo sasa hivi ni nzuri, na hujihisi vibaya, au kwa sababu sasa hivi umewekwa katika kufanya kazi. Ikiwa siku moja utatumwa nyumbani, na utakapokuwa katika giza la hali mbaya ya moyo, hata hivyo, kilicho ndani ya moyo wako kitafichuliwa. Kuna watu wengine wenye kimo kidogo, wenye muda mfupi wa uzoefu ambao wanaweza kugeuka na kukimbia, kurudi ulimwenguni. Kwa hakika, katika uchanganuzi wa mwisho, mjibizo wowote ule ulionao, unakataa mazingira aliyokupangia Mungu. Asili ya watu ya kumsaliti Mungu inafichuliwa kila mahali. Ikiwa hili lisingechanganuliwa, watu wasingejijua kwa kina ipasavyo. Watu wakikumbana na kitu chochote, wote wanamsaliti Mungu na wanakosa kumtii. Mijibizo ya baadhi yenu ni kutotaka, au hisia za malalamiko, uhasi na huzuni, na mnasema: Kwa ndani, binadamu hapendi ukweli, na huku kutopenda si kingine bali ni usaliti. Bado haitoshi kama mnazungumza namna hii tu, na hamjachanganua hadi kwenye kina cha kiini. Mnasema kwamba kutopenda ukweli ni usaliti, lakini kwa kweli, hili si sahili hivyo Mmelichanganua vipi? Hamjielewi nyinyi wenyewe. Unaweza usijue hiyo ni hali gani uliyonayo, na huwezi kutofautisha mazuri na mabaya, ikiwa ni usaliti au la, na hujijui wazi wewe mwenyewe iwe umetii au la. Hamuwezi kuchanganua kabisa asili zenu wenyewe. Kila mara mnapokumbana na jambo fulani mnashindwa kujua namna ya kwenda mbele. Hatimaye, utakapokumbana na jaribu, je, utaweza kulitambua kusudi la Mungu? Utalifafanua hili vipi? Unapaswa kutembea katika njia gani? Ni mantiki gani au ni ukweli gani unapaswa kuwa nao ili kukidhi kusudi la Mungu? Kama kiwango cha chini zaidi, ni lazima uwe na mtazamo chanya. Je, mmeyawazia maswali haya?
Zamani watu wengine walikuwa na mawazo kuhusu anachokifanya Mungu mwenye mwili. Ushirika uliofuata ulisababisha kuwepo na ukweli usiohitaji uthibitisho. Ukweli huu usiohitaji uthibitisho ni: Binadamu wanapaswa kukiri kuwa yote anayofanya Mungu ni sahihi, kuwa yote ni muhimu. Kama binadamu hawataelewa wanapaswa hata hivyo kutii na si kupinga. Kama binadamu wana mawazo ni lazima wataaibika. Je, watu wanakumbuka maneno haya? Kila mara wanapokabiliana na kitu, wanajisemea wao wenyewe: Kwa namna yoyote usiwe na mawazo, kwa namna yoyote usiyahukumu. Kuna maana katika kila kitu anachokifanya Mungu. Ijapokuwa hatuwezi kuelewa kwa sasa, siku moja tutapata aibu. Wanazishikilia tu sheria kama hii. Sheria ya aina hii, hata hivyo, yaweza kusuluhisha matatizo kadhaa ya waumini ambao wamekanganyikiwa. Kwa mtu aliye na uelewa haya maneno yatasaidia kuelewa maana ya vitu vingi, na kutumia hii sheria kila mara hali inaposhuhudiwa yaweza kuweka wazi mambo mengi. Ni nini kinachofanyika kama hakuna umaizi? Mtu anaweza tu kutii sheria, na katika kufanya hivyo anaweza pia kulindwa na kuzuia kukiuka amri za utawala, si kueneza maafa. Sheria hii ina manufaa! Sio ati haina maana! Katika sehemu mbalimbali sheria hii imesomwa kwa moyo. Wengine huiandika madaftarini, au kuiandika kwenye jalada la kitabu, na kuisoma kila wakati wanapofungua kitabu, huku wakiikariri. Wanaikariri wanapoomba. Kufanya hivyo kuna manufaa kadhaa. Watu wengine hawathubutu kufanya mambo kwa kubahatisha, na wana uchaji mdogo mioyoni mwao. Ila kulingana na watu wengi, hawana uelewa wa kweli wa hali chanya, na kuna vitu vingi sana vilivyo hasi. Ijapokuwa inaonekana kuwa mnajihisi vyema kabisa na hamjaacha kufanya kazi, kuna vitu vingi hasi kwa kweli kati yenu, na hakuna vitu chanya. Kuna mijibizo mingi sana kanisani kuhusu mambo kama haya. Je, mmejaribu kujijumuishia nyinyi wenyewe? Kama vitu vya aina hii vingekabiliwa tena, mngemkataa Mungu au kumsaliti Mungu? Kuna baadhi ya watu ambao labda wametambua, "Binadamu hana uwezo wa kuielewa asili yake mwenyewe. Bila shaka sitajaribu kukataa tena, na lazima niwe makini. Lazima niombe kila siku!” Huu sio mpango wa uhakika. Nimegundua kuwa huwa mnapata aibu, na mara nyingi mnasema: "Ah, nitafanya nini kuhusu hii asili ya binadamu? Siwezi kuisuluhisha mimi mwenyewe, na siwezi kuielewa. Kwa kweli sina haki ya kujisimamia mimi mwenyewe. Sijui ninaweza kufanya nini siku moja. Ninaogopa sana. Kumwamini Mungu lazima kufanyike kwa makini mno. Uzembe wowote waweza kusababisha maafa, na hilo laweza kuwa jambo baya mno. Hata sijijui, siwezi kujitegemea..." Ingawa watu wanaosema haya mara kwa mara huwa wanajielewa kwa kiasi fulani, wana uelewa kidogo mno kuhusu ukweli. Wanachanganyikiwa kila mara wanapokumbana na kitu chochote. Wanapatwa na wasiwasi, wanahisi uoga, na hawana njia yoyote ile wanapopatwa na chochote kile. Wakati huu umeshinda miaka saba ya majaribu, na hujasababisha maafa, na hujakiuka amri za utawala, lakini je, waweza kuwa na uhakika kuhusu wakati ujao? Wawezaje kuyashinda haya yote bila kizuizi? Unaona kuwa umeyashinda masaibu kwa urahisi sana, kwa kujificha hapa na pale. Ulijificha kwa mwaka mmoja au nusu mwaka hadi yakaisha. Wanadamu wanaweza kujificha, lakini asili ya binadamu ni kitu ambacho hakiwezi kufichika. Je, hakupaswi kuwa na ukweli uisohitaji thibitisho unaohusiana na hili, pia? Katika kila majaribu ya Mungu kuna nia nzuri. Kwa kila tukio linaloshuhudiwa kuna ukweli ambao mtu anapaswa kuwa nao ili kusimama imara. Jiandaeni na ukweli ili kukabiliana na majaribu tofauti tofauti kwa sasa, na hamtaogopa bila kujali miaka ya majaribu hapo mbeleni. Lazima muwe na ujasiri. Kutii mipango ya Mungu kamwe hakuwezi kuwa na dosari. Njia daima itakuwa na matumaini. Mwawezaje kuwa wakamilifu bila majaribu kadhaa? Bila majaribu, hakuna shahidi. Ni vipi basi mtamridhisha Mungu? Majaribu yatawaletea baraka za Mungu. Ni kwa kumfuata tu Mungu hadi mwisho ndipo mtu aweza kuingia katika ufalme. Kumbuka: nyinyi nyote mna fungu katika dhiki, ufalme, na uvumilivu wa Kristo.
kutoka kwa Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Vitabu.

Jumamosi, 1 Desemba 2018

Mtu Ambaye Hupata Wokovu ni Yule Ambaye Yuko Radhi Kutenda Ukweli

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, sauti ya Mungu

Mtu Ambaye Hupata Wokovu ni Yule Ambaye Yuko Radhi Kutenda Ukweli

Hapo awali sana, umuhimu wa kuwa na maisha sahihi ya kanisa ulitajwa katika mahubiri. Kwa hivyo ni kwa nini maisha ya kanisa hayajaboreka bado, na bado ni kile kitu kimoja tu cha zamani? Mbona hakuna njia mpya na tofauti kabisa ya maisha? Je, inaweza kuwa sahihi kwa mtu wa miaka ya tisini kuishi kama mfalme wa enzi iliyopita? Ingawa chakula na vinywaji vinaweza kuwa vyakula vitamu vilivyoonjwa mara chache katika enzi zilizopita, hapajakuwa na mabadiliko makubwa katika hali kanisani. Imekuwa kama kuweka divai ya kale katika kiriba kipya. Je, kuna haja gani basi ya Mungu kusema sana? Makanisa katika maeneo mengi hayajabadilika kabisa. Mimi nimeliona kwa macho Yangu na ni wazi katika moyo Wangu; Hata kama sijapata uzoefu wa maisha ya kanisa Mimi Mwenyewe, Nazijua hali za mikusanyiko ya kanisa kama mgongo wa mkono Wangu. Hawajafanya maendeleo mengi. Inarejelea msemo—ni kama kutia divai ya kale katika kiriba kipya. Hakuna kilichobadilika, siyo hata kidogo! Wakati mtu anapowachunga wao huwaka kama moto, lakini wakati hakuna mtu hapo kuwafadhili, wao ni kama pande kubwa la barafu. Si wengi wanaoweza kuzungumza juu ya mambo ya vitendo, na ni mara chache mtu yeyote anaweza kushika usukani. Ingawa mahubiri ni ya juu, imekuwa nadra kwa mtu yeyote kupata kuingia. Watu wachache hutunza neno la Mungu. Wao hujawa na machozi wanapolikubali neno la Mungu na kuwa wachangamfu wanapoliweka kando; Wao husononeka na kuwa wenye huzuni wanapoliondokea. Kwa kusema kweli, nyinyi hamlitunzi neno la Mungu, na hamyaoni kamwe maneno kutoka kinywa Chake mwenyewe kama hazina. Nyinyi huwa na wasiwasi tu mnapolisoma neno Lake, na kuhisi ni lenye kuhitaji nguvu nyingi sana mnapolikariri, na inapofika kuliweka neno Lake katika matendo, ni kama kukabiliana na kazi isiyoweza kukamilika—hamjamotishwa, Nyinyi daima huwa mnachangamka mnaposoma neno la Mungu, lakini mnasahau mnapolitenda. Kwa hakika, maneno haya si lazima yazungumzwe kwa jitihada sana na kurudiwa kwa uvumilivu sana; watu husikiliza tu lakini hawayaweki katika matendo, kwa hiyo kimekuwa kizuizi kwa kazi ya Mungu. Mimi siwezi kukosa kulileta jambo hili kwa mjadala, Mimi siwezi kukosa kulizungumzia. Mimi ninalazimika kufanya hivyo; Siyo kwamba Mimi hufurahia kufunua udhaifu wa wengine. Mnafikiri kwamba matendo yenu yanafaa tu na mnadhani kwamba wakati ufunuo uko kileleni, kwamba mmeingia katika kilele pia? Je, ni rahisi hivyo? Hamchunguzi kamwe msingi ambao uzoefu wenu hatimaye umejengwa juu yake. Kwa wakati huu, mikusanyiko yenu haiwezi kuitwa maisha mazuri ya kanisa kabisa, wala kuwa maisha yafaayo ya kiroho kamwe. Ni mkusanyiko wa kundi la watu ambao hufurahia kuzungumza na kuimba. Kusema kweli, hakuna uhalisi mwingi ndani yake. Kulisema kwa dhahiri zaidi, kama hutendi, u wapi uhalisi? Je, huko siko kujigamba kusema kwamba una uhalisi? Wale ambao daima hufanya kazi ni wa kujigamba na wenye majivuno, wakati ambapo wale ambao hutii daima hutulia na kuinamisha vichwa vyao chini, bila nafasi yoyote ya kutenda. Watu ambao hufanya kazi huwa hawafanyi chochote ila kuzungumza, kuendelea zaidi na zaidi na mazungumzo yao yenye kuvutia, na wafuasi husikiliza tu. Hakuna mabadiliko ya kuzungumzia; Hizi ni njia tu za zamani! Leo, kuweza kwako kunyenyekea na kutothubutu kuingilia au kutenda makusudi ni kutokana na kuwasili kwa amri za kiutawala za Mungu; siyo mabadiliko uliyoyapata kupitia uzoefu. Ukweli kwamba kuna mambo mengi ambayo huwezi kuyafanya leo ambayo ungeweza kuyafanya jana ni kwa sababu kazi ya Mungu ni dhahiri kiasi kwamba imeshinda watu. Acha Nimuulize mtu fulani, ni kiasi gani cha ufanikishaji wako leo kilichopatikana kwa jasho la kazi ngumu yako mwenyewe? Ni kiasi gani ulichoambiwa moja kwa moja na Mungu? Ungejibu vipi? Je, ungepigwa na bumbuwazi na kutoweza kunena? Ungekosa adabu? Ni kwa nini wengine wanaweza kuzungumza juu ya mengi ya uzoefu wao ili kukuruzuku, wakati ambapo unafurahia tu chakula ambacho wengine wamepika? Je, huoni haya? Je, hutahayari?
Mnaweza kutekeleza uchunguzi wa kutafuta ukweli, kuchunguza wale walio katika viwango vya juu ambao yamkini ni bora zaidi: Unaelewa ukweli kiasi gani? Je, ni kiasi gani ambacho wewe hatimaye huweka katika mazoezi? Ni nani unayempenda zaidi, Mungu au wewe mwenyewe? Je, wewe hutoa mara nyingi zaidi, au hupokea mara nyingi zaidi? Je, ni mara ngapi wakati lengo lako lilikuwa lenye kosa umetelekeza nafsi yako ya zamani na kuyaridhisha mapenzi ya Mungu? Maswali haya machache tu yatawakanganya watu wengi. Kwa watu wengi sana, hata kama wakitambua kuwa nia yao si sahihi, bado hufanya makosa makusudi, nao hata hawajakaribia kuinyima miili yao wenyewe. Watu wengi sana huruhusu dhambi kuenea kote ndani yao, wakiruhusu hali ya dhambi kuongoza kila tendo lao. Hawawezi kushinda dhambi zao, na huendelea kuishi katika dhambi. Baada ya kufika kwenye hatua hii ya sasa, ni nani asiyejua ni matendo mangapi mabaya ameyafanya? Ukisema hujui, basi Mimi ningesema kwamba unasema uongo. Kusema ukweli, yote ni kutotaka kutelekeza nafsi yako ya zamani. Je, kuna maana gani ya kusema "maneno mengi kutoka kwa moyo" ya kutubu ambayo hayafai? Je, hili lingekusaidia kukua katika maisha yako? Kujijua mwenyewe ni kazi yako ya kudumu. Mimi huwafanya watu wakamilifu kupitia utii wao na kutenda kwao kwa maneno ya Mungu. Ukivaa tu neno la Mungu kama jinsi ungevaa nguo zako, ili kuwa tu nadhifu na maridadi, je, hujidanganyi mwenyewe na kuwadanganya wengine? Ikiwa yote uliyonayo ni kuongea na kamwe huyaweki katika matendo, ni kitu gani utakachokifikia?
Watu wengi wanaweza kuzungumza kidogo juu ya matendo na wanaweza kuzungumza kuhusu fikira zao za kibinafsi, lakini mengi yayo ni mwanga kutoka kwa maneno ya wengine. Haijumuishi chochote kutoka kwa matendo yao binafsi kamwe, wala kujumuisha kile wanachokiona kutokana na uzoefu wao. Nimechangua suala hili mapema; usifikiri kwamba sijui chochote. Wewe ni tishio la bure tu, na bado unaongea juu ya kumshinda Shetani, juu ya kutoa ushahidi wa ushindi, na kuishi kwa kudhihirisha mfano wa Mungu? Huu wote ni upuuzi! Je, unadhani kwamba maneno yote ambayo Mungu ameyasema leo ni yako kupendezwa nayo? Kinywa chako hunena juu ya kutelekeza nafsi yako ya zamani na kuweka ukweli katika matendo, lakini mikono yako inafanya vitendo vingine na moyo wako unapanga hila zingine—wewe ni mtu wa aina gani? Kwa nini moyo wako na mikono yako si kitu kimoja? Kuhubiri kwingi sana kumekuwa maneno matupu; si hili ni la kuvunja moyo? Ikiwa umeshindwa kuweka neno la Mungu katika matendo, inathibitisha kuwa bado hujaingia katika njia ambayo Roho Mtakatifu hufanya kazi, bado haujapata kuwa na kazi ya Roho Mtakatifu ndani yako, na bado haujapata mwongozo Wake. Ukisema kuwa unaweza tu kuelewa neno la Mungu lakini umeshindwa kuliweka katika matendo, basi wewe ni mtu asiyependa ukweli. Mungu huwa haji kumwokoa mtu wa aina hii. Yesu alipatwa na maumivu makubwa wakati Yeye aliposulubiwa ili kuwaokoa wenye dhambi, kuwaokoa maskini, kuwaokoa hao watu wanyenyekevu. Kusulubiwa Kwake kulileta sadaka ya dhambi. Ikiwa huwezi kutenda neno la Mungu, basi unapaswa kuondoka haraka unavyoweza; usijikalie pote katika nyumba ya Mungu kama doezi. Watu wengi hata huona vigumu kujizuia kufanya mambo ambayo humpinga Mungu kwa dhahiri. Je, si wanauliza kifo? Wanawezaje kuongea juu ya kuingia katika ufalme wa Mungu? Je, wangekuwa na ujasiri wa kuuona uso Wake? Kula chakula ambacho Yeye hukupa, kufanya mambo ya uhalifu ambayo humpinga Mungu, kuwa mwenye nia mbaya, mwenye kudhuru, na mwenye hila, hata wakati Mungu anakuruhusu kufurahia baraka ambazo Yeye amekupa—je, huzihisi zikiichoma mikono yako unapozipokea? Je, huuhisi uso wako ukigeuka kuwa mwekundu? Baada ya kufanya kitu kinyume na Mungu, baada ya kufanya hila ili "kuwa laghai," huhisi hofu? Kama huhisi chochote, unawezaje kuzungumza juu ya wakati wowote ujao? Kulikuwa tayari hakuna wakati ujao kwako zamani za kale, kwa hiyo ni matarajio yapi makubwa zaidi unaweza kuwa nayo bado? Ukisema kitu bila haya lakini huhisi hatia, na moyo wako hauna ufahamu, basi haimaanishi kwamba tayari umekataliwa na Mungu? Kuzungumza na kutenda kwa kujiachia na bila kuzuiwa imekuwa asili yako; Je, unawezaje kufanywa mkamilifu na Mungu hivi? Ungeweza kutembea ulimwenguni kote? Ni nani angethibitishiwa na wewe? Wale ambao wanaijua asili yako ya kweli watakaa mbali nawe. Je, si hii ni adhabu ya Mungu? Kwa jumla, ikiwa kuna mazungumzo tu bila matendo, hakuna ukuaji. Ingawa Roho Mtakatifu anaweza kuwa anafanya kazi kwako unapozungumza, kama hutendi, Roho Mtakatifu ataacha kufanya kazi. Ukizidi kuendelea kwa njia hii, kunawezaje kuwa na majadiliano yoyote ya wakati ujao au kutoa nafsi yako yote kwa kazi ya Mungu? Wewe husema tu juu ya kutoa nafsi yako yote, na bado humpi Mungu moyo wako ambao kwa hakika humpenda Yeye. Yote ambayo Mungu amepokea ni moyo wa maneno yako, na siyo moyo wa utendaji wako. Je, hiki kinaweza kuwa ndicho kimo chako cha kweli? Ikiwa ungeendelea kwa jinsi hii, ungefanywa mkamilifu na Mungu lini? Je, huhisi wasiwasi juu ya kesho yako ya giza na majonzi? Je, huhisi kwamba Mungu amepoteza tumaini kwako? Je, hujui kwamba Mungu hutamani kuwapa ukamilisho watu wengi na wapya? Je, vitu vya zamani vingeweza kukacha? Wewe huyazingatii maneno ya Mungu leo: Je, unasubiri kesho?
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili