Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Kiumbe-Aliyeumbwa. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Kiumbe-Aliyeumbwa. Onyesha machapisho yote

Jumatano, 24 Aprili 2019

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Kazi ya Kusimamia Mwanadamu ni Gani?

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Kazi ya Kusimamia Mwanadamu ni Gani?

Maneno Husika ya Mungu:
Kazi ya kumsimamia mwanadamu imegawanywa katika hatua tatu, na ina maana kuwa kazi ya kumwokoa mwanadamu imegawanywa katika hatua tatu. Hatua hizi tatu hazihusishi kazi ya kuuumba ulimwengu, ila ni hatua tatu za kazi ya Enzi ya Sheria, Enzi ya Neema, na Enzi ya Ufalme. Kazi ya kuiumba dunia ilikuwa kazi ya kusababisha uwepo wa wanadamu wote. Haikuwa kazi ya kumwokoa mwanadamu, na haina uhusiano na kazi ya kumwokoa mwanadamu, kwa kuwa dunia ilipoumbwa mwanadamu hakuwa amepotoshwa na Shetani, na hivyo hakukuwa na haja ya kutekeleza kazi ya kumwokoa mwanadamu. Kazi ya kumwokoa mwanadamu ilianza tu baada ya mwanadamu kupotoshwa, na kwa hivyo kazi ya kumsimamia mwanadamu pia ilianza tu punde mwanadamu alipopotoshwa. Kwa maneno mengine, usimamizi wa Mungu wa mwanadamu ulianza kutokana na kazi ya kumwokoa mwanadamu, na wala haukutokana na kazi ya kuiumba dunia. Hakungekuwa na kazi ya kumsimamia mwanadamu pasipo kuwepo na tabia potovu ya mwanadamu, na kwa hivyo kazi ya kumsimamia mwanadamu ina sehemu tatu, badala ya hatua nne, au enzi nne. Hii tu ndio njia sahihi ya kutaja kazi ya Mungu ya usimamizi wa mwanadamu. Enzi ya mwisho itakapofikia kikomo, kazi ya kusimamia mwanadamu itakuwa imekamilika. Hitimisho la kazi ya usimamizi lina maana kuwa kazi ya kuwaokoa wanadamu wote imemalizika kabisa, na kwamba mwanadamu amefika mwisho wa safari yake. Pasipo kazi ya kuwaokoa wanadamu wote, kazi ya usimamizi wa wanadamu haingekuwapo, wala hakungekuwa na hatua tatu za kazi. Ilikuwa ni hasa kwa ajili ya upotovu wa mwanadamu, na kwa sababu mwanadamu alihitaji wokovu kwa dharura, ndipo Yehova alikamilisha uumbaji wa dunia na kuanza kazi ya Enzi ya Sheria. Hapo tu ndipo kazi ya kumsimamia mwanadamu ilipoanza, kumaanisha kwamba hapo tu ndipo kazi ya kumwokoa mwanadamu ilipoanza. "Kumsimamia mwanadamu" haimaanishi kuongoza maisha ya mwanadamu aliyeumbwa upya duniani (ambapo ni kusema, mwanadamu ambaye bado hakuwa amepotoshwa). Badala yake, ni wokovu wa ubinadamu ambao umepotoshwa na Shetani, ambapo ni kusema kwamba, ni kubadilishwa kwa mwanadamu aliyepotoshwa. Hii ndiyo maana ya kumsimamia mwanadamu. Kazi ya kumwokoa mwanadamu haihusishi kazi ya kuiumba dunia, na kwa hivyo kazi ya kumsimamia mwanadamu haijumuishi kazi ya kuumba ulimwengu, na inahusisha tu hatua tatu za kazi zilizo tofauti na uumbaji wa ulimwengu. Ili kuelewa kazi ya kumsimamia mwanadamu, ni muhimu kuwa na ufahamu wa historia ya hatua tatu za kazi—hili ndilo kila mtu anapaswa kulifahamu ili kuokolewa. Kama viumbe wa Mungu, mnapaswa kutambua kuwa mwanadamu aliumbwa na Mungu, na kufahamu chanzo cha upotovu wa mwanadamu, na, vilevile, kufahamu mchakato wa wokovu wa mwanadamu. Iwapo mnafahamu tu jinsi ya kutenda kulingana na mafundisho ili kupata neema ya Mungu, lakini hamna fununu jinsi Mungu anavyomwokoa mwanadamu, au ya chanzo cha upotovu wa mwanadamu, basi hili ndilo mnalokosa kama viumbe wa Mungu. Hupaswi kutoshelezwa tu na kuelewa kwa ukweli unaoweza kuwekwa katika vitendo, huku ukibakia kutojua upeo mpana wa kazi ya usimamizi ya Mungu—kama hivi ndivyo ilivyo, basi wewe ni mwenye kulazimisha kauli sana. Hatua tatu za kazi ya Mungu ndizo hadithi ya ndani ya usimamizi wa Mungu wa mwanadamu, ujio wa injili ya dunia nzima, fumbo kubwa zaidi kati ya wanadamu, na pia ni msingi wa kueneza injili. Ukizingatia tu kuelewa ukweli sahili unaohusiana na maisha yako, na usijue lolote kuhusu hili, maajabu makuu zaidi na maono, basi maisha yako si ni sawa na bidhaa yenye kasoro, yasio na maana isipokuwa kuangaliwa?
kutoka kwa "Kujua Hatua Tatu za Kazi ya Mungu Ndiyo Njia ya Kumjua Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kazi ya usimamizi ilikuja tu kwa ajili ya wanadamu, yaani ilitolewa kwa ajili ya uwepo wa wanadamu. Usimamizi haukuwepo kabla ya uwepo wa wanadamu au mwanzo wakati mbingu na nchi na vilivyomo vilipoumbwa. Iwapo, katika kazi nzima ya Mungu, hakungekuwa na vitendo vinavyomfaidi mwanadamu, yaani kama Mungu asingeweka matakwa maalum kwa mwanadamu aliyepotoka (ikiwa kazi ifanywayo na Mungu haikuwa na njia nzuri ya vitendo vya mwanaadamu), basi kazi hii isingeitwa usimamizi wa Mungu. Iwapo kazi nzima ya Mungu ingehusisha tu kuwaambia wanadamu waliopotoka jinsi ya kuendeleza vitendo vyao, na Mungu hakuendeleza kazi yoyote ya mipango Yake, na Hakuonyesha uwepo wake wa daima au busara, basi bila kujali ni jinsi gani matakwa ya Mungu kwa mwanadamu yangewekwa juu, bila kujali Mungu aliishi muda mrefu kiasi gani miongoni mwa wanadamu, mwanadamu asingejua chochote juu ya tabia ya Mungu; kama ingekuwa hivyo, basi kazi hii isingeweza kukaribia kuitwa usimamizi wa Mungu. Kwa ufupi, kazi ya usimamizi wa Mungu ni kazi iliyofanywa na Mungu na kazi zote zilizofanywa chini ya uongozi wa Mungu na wale ambao wamepatikana na Mungu. Kazi kama hiyo inaweza kuchukuliwa kwa ufupisho kama usimamizi, na inaelezea kazi ya Mungu miongoni mwa wanadamu na vilevile ni ushirikiano Wake na wale wanaomfuata; kwa ujumla, hayo yote yanaweza kuitwa usimamizi. Hapa kazi ya Mungu inaitwa maono na ushirikianao wa mwanadamu unaitwa vitendo. Kadiri kazi ya Mungu ilivyo juu (yaani kadiri maono yalivyo juu), ndivyo tabia za Mungu zinakuwa wazi kwa mwanadamu, na kutoafikiana na mawazo ya mwanadamu, na ndivyo vitendo na ushirikiano wa mwanadamu huwa vya juu. Kadiri matakwa kwa mwanadamu yanavyokuwa ya juu, ndivyo kazi ya Mungu inavyotofautiana mawazo ya mwanadamu, matokeo yake yakiwa majaribu ya mwanadamu, na viwango anavyotarajiwa kuwa navyo, vilevile vinakuwa vya juu. Katika hatima ya kazi hii, maono yote yatakuwa yametimizwa, na yale yote mwanadamu anapaswa kuweka katika vitendo yatakuwa yamefikia kilele cha ukamilifu. Huu ndio wakati pia ambapo kila kitu kitawekwa katika kundi lake kwani kile kinachopaswa kufahamika na mwanadamu kitakuwa kimebainishwa kwake. Kwa hivyo maono yatakapofikia upeo wa juu, vivyo hivyo kazi nayo itakaribia hatima yake na vitendo vya mwanadamu vitakuwa vimefikia ufanisi wake. Vitendo vya mwanadamu vimekitwa katika kazi ya Mungu, na usimamizi wa Mungu unadhihirika tu kupitia vitendo na ushirikiano wa mwanadamu. Mwanadamu ni mfano wa kazi ya Mungu, na mlengwa wa kazi ya usimamizi mzima wa Mungu, na pia mazao ya kazi ya usimamizi wote wa Mungu. Iwapo Mungu angefanya kazi peke yake bila ushirika wa mwanadamu, basi pasingekuwepo na kitu cha kudhihirisha kazi Yake nzima na kwa hali hiyo kusingekuwa na umuhimu hata kidogo wa usimamizi wa Mungu. Ni kwa kuchagua tu chombo kifaacho kilicho nje ya kazi ya Mungu, na kinachoweza kudhihirisha kazi hii, na kuthibitisha kudura na busara zake, je, inawezekana kufikia dhumuni la usimamizi wa Mungu na kufikia dhumuni la kutumia kazi hii yote ili kumshinda kabisa Shetani. Na kwa hivyo mwanadamu ni sehemu muhimu katika kazi ya usimamizi ya Mungu, na mwanadamu ndiye pekee anayeweza kuifanya kazi ya usimamizi ya Mungu izae matunda na kufikia lengo Lake kuu; mbali na mwanadamu, hakuna kiumbe kingine chenye uhai kinachoweza kuchukua nafasi hiyo. Ikiwa mwanadamu atakuwa dhihirisho kamili la kazi ya usimamizi, basi uasi wa wanadamu wenye maovu lazima utokomezwe. Hii inahitaji kuwa mwanadamu apewe utendaji ufaao kwa kila muktadha, na kwamba Mungu afanye kazi inayotangamana miongoni mwa wanadamu. Ni kwa njia hii tu ndipo kutakuwa na kundi la watu waliokubaliwa ambao ni dhihirisho la kazi ya usimamizi. Kazi ya Mungu miongoni mwa wanadamu haiwezi kuwa ushuhuda kwa Mungu Mwenyewe kupitia kazi ya Mungu peke yake; ushuhuda huo vilevile unahitaji wanadamu ambao wanafaa ili kazi yake iafikiwe. Mwanzo Mungu atawatayarisha watu hawa ambao kupitia kwao kazi Yake itadhihirika na ushuhuda Wake utachukuliwa miongoni mwa viumbe. Kwa hili, Mungu atakuwa ameafiki lengo la kazi Yake. Mungu hafanyi kazi peke Yake kumshinda Shetani kwa sababu Mungu hawezi kujishuhudia Mwenyewe moja kwa moja miongoni mwa viumbe wote. Angefanya hivyo, ingekuwa vigumu kumshawishi mwanadamu, kwa hivyo Mungu lazima Afanye kazi kwa mwanadamu ili kumshinda na ndipo Atakapoweza kupata ushuhuda miongoni mwa viumbe vyote. Mungu angefanya kazi peke Yake bila kushirikiana na mwanadamu, au kama mwanadamu asingetakiwa kushirikiana, basi mwanadamu asingeitambua tabia ya Mungu na daima asingefahamu nia ya Mungu; na kwa hali hii haiwezi kuitwa usimamizi wa Mungu. Mwanadamu mwenyewe angejizatiti, na kutafuta, na kufanya bidii, bila kuifahamu kazi ya Mungu, basi mwanadamu angekuwa anafanya mizaha. Bila kazi ya Roho Mtakatifu, akifanyacho mwanadamu ni cha Shetani, ni muasi na mtenda maovu; Shetani anadhihirika katika yote yafanywayo na mwanadamu mwenye maovu na hamna kinachoafikiana na Mungu, na yote ni dalili ya Shetani. Hakuna kati ya vilivyozungumziwa kisichokuwa na maono na vitendo. Katika msingi wa maono, mwanadamu hupata vitendo, anapata njia ya utiifu, ili kwamba aweze kuweka kando mawazo yake ili apate vile ambavyo hajawahi kuwa navyo hapo awali. Mungu huhitaji mwanadamu ashirikiane naye, kwamba mwanadamu asikilize matakwa Yake, na mwanadamu ashikilie kazi ifanywayo na Mungu Mwenyewe na kuupitia uwezo mkubwa wa Mungu na kuifahamu tabia ya Mungu. Kwa kifupi, haya ndiyo usimamizi wa Mungu. Ushirika wa Mungu na mwanadamu ndio usimamizi, na ni usimamizi mkuu zaidi.
kutoka kwa "Kazi ya Mungu na Utendaji wa Mwanadamu" katika Neno Laonekana katika Mwili

Ijumaa, 8 Februari 2019

Imani Tatu katika Mungu wa Vitendo

Sura ya 16. Imani Tatu katika Mungu wa Vitendo

Ndani ya familia ya Mungu, kuna imani kadhaa tofauti katika Mungu; imani hizi tofauti lazima zitambulishwe ili kuona wewe ni wa gani.
Na imani ya aina ya kwanza, ambayo pia ni aina bora zaidi, mtu huyo ana uwezo wa kuyaamini maneno ya Mungu katika vitu vyote; ana uwezo wa kukubali ufichuzi wote wa Mungu, ushugulikiaji, na upogoaji; yeye ni mwagalifu kwa mapenzi ya Mungu, hupenda, ni mwaminifu kwa, na humwabudu Mungu, na ako tayari kutenda ukweli. Imani kama hiyo huzaa maisha, na inawezesha mtu kupata mabadiliko katika tabia na kupatwa na Mungu.
Na imani ya aina ya pili, mtu huyo anamwamini Mungu kwa kiasi, lakini pia ni mwenye tuhumu kwa kiasi. Wakati kazi ya Mungu hairidhiani na yeye, angefanya ulinganishi katika moyo wake, akiwa na shaka kama Mungu Anapaswa kuwa akifanya vitu kama hivyo. Mara kwa mara anamtuhumu Mungu, kwa hivyo ana uwezo tu wa kumtii Mungu kwa kiasi, na hana uwezo wa kumtii Mungu katika vitu vingine; anaweza kulitii lile ambalo analiamini ni sawa, lakini ana mawazo yake mwenyewe anapokabiliwa na vitu ambavyo anahisi si sawa, na migongano katika moyo wake, na anakataa kuyatekeleza. Hili pia ni aina ya imani. Kimo cha watu siku hizi ni hasa kama hiki, wao wana uwezo tu wa kutii kile wanachohisi kuwa sawa, wao hawana uwezo wa kutii kile wanachohisi si sawa, na hawatatekeleza kile ambacho hawako tayari kufanya. Kadhalika, wakati mwingine hali ikiwa, wana shauku na Mungu, wakihisi kwamba wanapaswa kuwa waangalifu kwa mzigo wa Mungu, hivyo wanatimiza wajibu wao; au wakati mwingine wanashughulishwa na ushirika, wanapata Mungu kuwa wa kupendeka kabisa, na sasa tu ndio wenye imani katika Mungu kwa kiasi fulani. Hasa, imani yao katika Mungu ni tu kufuata umati; hawana upendo kwa Mungu, wala si waangalifu kwa Mungu, wakati bila shaka hawamtii na hawamwabudu Mungu kwa kweli. Kwa watu walio na imani kama hii katika Mungu, wako tu na kiasi cha wastani cha upendo, uangalifu, na utiifu kwa Mungu, kwa muda fulani, na inafanyika tu wakati Roho Mtakatifu hasa Anasonga, wakati Roho Mtakatifu anafanya kazi Yake. Wakati wako katika hali mbaya, au wakati wanachanganywa na wengine, wakati wao ni dhaifu na wamekata tamaa, vitu hivi vimeenda, vimetokomea, wakati wao wenyewe hawana habari jinsi hilo limekuja kupita. Hawana uwezo tena wa kumpenda Mungu hata wakitaka, hawana motisha ya kutenda maneno ya Mungu tena, na kisha wanaona kazi ya Mungu kama ya desturi sana, ya kawaida sana; hata kama wao hawana tuhuma tena, wao hawana ari yoyote tena. Kimo cha watu wengi zaidi kiko katika hatua hii, na hii ndiyo aina ya pili ya imani.
Na aina ya tatu ya imani, mtu hana uelewa wa Mungu mwenye mwili, kwake Yeye hujitokeza tu kama mtu wa kawaida, na hakuna tofauti kubwa inaweza kutambulishwa. Kwa hivyo, anamchukulia Mungu mwenye mwili kama tu mtu wa kawaida lakini mwenye cheo cha heshima, ana uwezo wa kufuatana na Mungu na kusema kitu kizuri, na pia ana uwezo wa kuandamana katika imani, lakini imani hii si imani halisi. Ana uwezo wa kufuatana na mambo ya upuuzi mara moja moja, lakini hakuna upendo kwa Mungu katika mtu wa aina hii—upendo si kujali kuhusu mwili lakini utiifu wa kweli katika kazi ya mtu na katika kutimiza wajibu wa mtu, kuwa mwangalifu kwa Mungu na kumcha Mungu. Upendo kwa Mungu ni kitu ambacho mtu aliye na uzoefu mkubwa tu anaweza kutangaza, si kitu ambacho mtu anaweza kusema kwa kupitia tu, kuona kwamba mtu ametekwa na hisia kali hivyo kusema kwamba huyu na huyu humpenda Mungu sana. Ama kusema kwamba watu kutoka dhehebu fulani humpenda Mungu kwa kweli. Huu ni upuuzi. Mtu kama huyu hawezi kukubali na kutii kwa urahisi kunapokuja kwa mambo ya upuuzi, na anapokabiliwa na mambo ya muhimu yanayohusiana na ukweli, hawezi kutii tu, na pia ana mawazo yake mwenyewe, hata anakuwa na tuhuma kuhusu Mungu. Watu kama hawa pia wako katika walio wengi. Wao ni wenye tuhuma kila wakati kuhusu Mungu: Je, huyu ni Mungu? Je, ni kwa nini Yeye hafanani na Mungu? Baadhi ya mambo Alivyosema labda yameelekezwa na Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu alimwelekeleza kusema mambo fulani, na kufanya vitu fulani. …Imani ya watu kama hawa ni ya kusikitisha zaidi.
Kiwango cha imani ya mtu katika Mungu, utiifu kwa Mungu, upendo, uangalifu, na uchaji kwa Mungu, kinatambulishwa hasa na yafuatayo:
Kwanza, kina msingi katika ikiwa mtu huyo hupenda ukweli. Kama unapenda ukweli basi unaweza kuendelea kuufuatilia zaidi, kisha unaweza kulenga kuwa na uelewa wa ukweli, wa maneno ya Mungu, wa kazi ya Mungu, wa umuhimu wa kupata mwili kwa Mungu, wa tabia ya Mungu, na uelewa wa Mungu una msingi hasa katika hiki kitu kimoja. Kadiri Unavyoweza kuelewa Mungu zaidi ndivyo unavyoweza kumtambua zaidi; kadiri unavyoweza kumwelewa Mungu zaidi ndivyo unavyoweza kumfuata bila kuyumbayumba. Hiyo ni, uelewa wa Mungu una msingi katika kufuatilia ukweli.
Pili, kina msingi katika uelewa wa mtu huyo wa Mungu mwenye mwili, hiyo ni muhimu. Bila uelewa wa Mungu wa vitendo, mazungumzo ya kumtii Mungu, kumpenda Mungu, kushuhudia Mungu, na kumhudumia Mungu yote ni maneno matupu. Vitu kama hivi haviwezi tu kufikiwa.
Tatu, kina msingi katika ubinadamu wa mtu huyo, lakini hili si halisi. Kwa sababu, baadhi ya watu wana ubinadamu mzuri, wao ni watu wazuri, lakini wao hawapendi ukweli. Kama wao hawana uelewa kabisa wa Mungu mwenye mwili, basi imani yao haiwezi kusiama, na wakati mwingine nia zao nzuri bila kujua husababisha madakizo. Je, unaweza kusema kwamba wao ni watu ambao wanamwamini Mungu kwa kweli? Wao ni wenye shauku, ni wa asili nzuri, na hufanya mambo fulani mazuri, lakini haya ni tabia nzuri tu ya nje, haya ni sura ya juu juu, haya hayaonyeshi kwamba imani yao ni halisi. Ukisema kwamba kwa kweli unamwamini Mungu, kweli unampenda Mungu, lazima uwe na uwezo wa kusema kwa nini unampenda Mungu, upendo wako kwa Mungu una msingi kwa nini, kwa nini unamwamini Yeye, kama wewe unaufuata umati tu ama unamwamini Yeye kwa sababu unaweza kumwona kwa kweli kama Mungu, imani na upendo wako kwa Mungu yana msingi katika ukweli upi: Haya lazima yategemezwe kwa misingi. Baadhi ya watu hupenda kusema kwamba wanamwamini Mungu kwa kweli na wanampenda Mungu, lakini wakati mtu anatamani kuwasiliana nao ukweli kwa uzito, hawana kitu cha kusema. Nimesikia watu wengi wakisema: “Mimi husikiza chochote ambacho Mungu husema, naamini yote ambayo Mungu husema, kwa njia yoyote ambayo Yeye huyasema. Sina mawazo yangu mwenyewe bila kujali kile Mungu husema, sina mawazo yangu mwenyewe bila kujali kile Mungu hufanya.” Je, wewe kweli ni mtu anayempenda Mungu kwa sababu tu umesema mambo kama haya? Lazima uwe na uzoefu halisi, lazima uwe na uwezo wa kuongea kuhusu uelewa halisi wa Mungu mwenye mwili. Pia, ni nini kiini cha Mungu, ni vitu vipi ambavyo watu huona vigumu kumtii Mungu katika, ni vitu vipi ambavyo watu wanaweza kumtii Mungu katika, wanamtii Mungu kwa kiasi gani, ni vitu vipi ambavyo huna uwezo wa kumtii Mungu katika, unatatua vipi mawazo yako kuhusu Mungu, unapanua vipi uelewa wako wa Mungu polepole? Kama unakosa uzoefu kama huo, basi huna mapenzi ya kweli kwa Mungu. Baadhi ya watu wana furaha hasa wanapoona kufika kwa Mungu, wanampokea kwa ukarimu, na kisha wanalia Mungu Anapoondoka. Watu wengine hufikiri kwamba hili ni onyesho la upendo wake kwa Mungu, lakini hili kweli linaweza kuonyesha kwamba anampenda Mungu? Hili linaweza kuonyesha tu kwamba anao moyo wenye ari, lakini mtu hawezi kusema kwamba matendo na maonyesho yake ni upendo kwa Mungu, kwamba ni imani ya kweli. Baadhi ya watu hutoa pesa kiasi, lakini hilo ni upendo kwa Mungu? Ama unaenda haraka kumwaga gilasi ya maji wakati unaambiwa, lakini hilo ni utiifu wa kweli? Kadhalika, watu wengine husema: “Nilimwamini Mungu baada ya mimi kusoma maneno ya Mungu, niliamini katika kupata mwili kwa Mungu, sina shaka baada ya mimi kumwona Mungu katika mwili wa kawaida.” Je, hili linaweza kuitwa imani ya kweli? Je, umekuwa na ushughulikaji na Mungu? Je, umejihusisha na Yeye? Je, unajua tabia Yake? Je, unajua ni nini Yeye hupenda? Je, unajua vitu unafanya ambavyo vinaikosea tabia Yake? Je, unajua upotovu ndani yako ambao Yeye huchukia? Je, unajua watu ambao Ameleta tabia Yake yenye haki kwao? Je, unajua ni watu wagani Yeye huchukia? Je, unajua ni masuala yapi unayo ambayo Yeye huchukia zaidi? Kama hujui vitu vyovyote kama hivi, linaonyesha kwamba kwa kweli huna uelewa wa Mungu. Huwezi kusema kwamba unamwamini Mungu kwa kweli, huwezi kusema kwamba unamtii Mungu kabisa, na bila shaka huwezi kusema kwamba unafanya vitu kulingana na mapenzi ya Mungu, kwamba unampenda Mungu, unamtii Mungu, ama unamwelewa Mungu. Unaweza kusema tu, kuhusu jambo hili, unayaelewa mapenzi Yake, unajua ni nini Yeye hupenda, kwamba unatenda kulingana na mapenzi ya Mungu katika jambo hili, kwamba unatenda kulingana na ukweli, kwamba unamtii katika jambo hili. Je, wewe ni mtu mtiifu kwa Mungu kwa sababu umemtii katika jambo hili tu? Huwezi kusema hilo, na kusema kwamba mtu humpenda Mungu kwa kuweka msingi tu kwa kitu cha juujuu, hilo ni kosa kubwa. Ukweli kwamba ulitenda kitu kizuri, ama kwamba umemjali Mungu hasa, huonyesha tu kwamba wewe ni mtu mwema, lakini hauonyeshi kwamba wewe ni mwangalifu kwa mapenzi ya Mungu. Bila shaka, upendo wa Mungu na kuwa mwangalifu kwa mapenzi ya Mungu yamejengwa juu ya msingi wa ubinadamu, na hakuwezi kuwa na upendo wa Mungu bila ubinadamu, kwa hivyo kila mmoja wenu lazima ajichunguze na aangalie mahali alipo. Baadhi ya watu hufikiri kwamba wao wako karibu hapo, lakini hili si lenye uhalisi; ilhali baadhi ya watu huenda kwa kiwangi kilichokithiri na hufikiri kwamba hakuna kitu kizuri kuwahusu, kwamba hawawezi kuachwa, na huu ni mtazamo hasi. Baadhi ya watu hufikiri kwamba hakuna mazuri ndani yao, na baadhi ya watu hujifafanua kama mtu anayempenda Mungu. Wao wako katika upande wa kushoto kabisa au katika upande wa kulia kabisa; huu ndio uhalisi wa watu hawa, ambao unaonyesha kwamba wao bado hawako katika njia sawa. Wao wanapaswa kuendelea kujitahidi kuwa dhahiri kuhusu ukweli, na kuingia katika uhalisi, ili kufuata mapenzi ya Mungu.
Soma Zaidi: Asili ya Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumanne, 29 Januari 2019

Neno la Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee I Mamlaka ya Mungu (I)” Uendelezo wa Sehemu ya Pili

Neno la Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee I Mamlaka ya Mungu (I)” Uendelezo wa Sehemu ya Pili

Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”. Maudhui ya video hii: Kwenye Siku ya Nne, Misimu, Siku, na Miaka ya Mwanadamu Iliumbika Huku Mungu Akionyesha Mamlaka Yake kwa Mara Nyingine Tena Kwenye Siku ya Tano, Maisha ya Maumbo Tofauti na Pana Yaonyesha Mamlaka ya Muumba kwa Njia Tofauti Kwenye Siku ya Sita, Muumba Aongea, na Kila Aina ya Kiumbe Hai Akilini Mwake Chajitokeza, Kimoja Baada ya Kingine Katika Mamlaka ya Muumba, Viumbe Vyote ni Timilifu Hakuna Kiumbe Chochote Kati ya Vile Vilivyoumbwa na Vile Ambavyo Havikuumbwa Kinaweza Kubadilisha Utambulisho wa Muumba
Sikiliza zaidi: Kanisa la Mwenyezi Mungu video

Jumapili, 2 Desemba 2018

Neno la Mungu "Je, Kazi ya Mungu ni Rahisi Jinsi Mwanadamu Anavyodhania?" (Official Video)

Neno la Mungu "Je, Kazi ya Mungu ni Rahisi Jinsi Mwanadamu Anavyodhania?" (Official Video)

Mwenyezi Mungu anasema, "Unapaswa kuona kuwa mapenzi Yake na kazi Yake si rahisi kama ilivyokuwa katika kuumba mbingu na nchi na vyote vilivyomo. Kwa sababu kazi ya leo ni kubadilisha wale waliopotoshwa, wale waliokufa ganzi, na kutakasa walioumbwa kisha kushughulikiwa na Shetani, si kuumba Adamu na Hawa, ama hata kuumba mwanga, ama aina yote ya mimea na wanyama. Kazi Yake sasa ni kutakasa wote waliopotoshwa na Shetani ili kwamba wamrejelee, wawe miliki Yake na wawe utukufu wake. Kazi kama ile si rahisi jinsi mwanadamu anavyofikiria kuhusu kuumbwa kwa mbingu na nchi na vilivyomo, wala si sawa na kumkemea Shetani aende katika shimo lisilo na mwisho, kama anayvodhania mwanadamu. Bali, ni kumbadilisha mtu, kubadili kilicho hasi kuwa chanya na kufanya kuwa miliki Yake ambacho si chake."
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumapili, 23 Septemba 2018

Umeme wa Mashariki | Ni Nani Anayejua Moyo wa Kutunza wa Mungu?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, makusudi ya Mungu

Umeme wa Mashariki | Ni Nani Anayejua Moyo wa Kutunza wa Mungu?

Qingxin Mji wa Zhengzhou, Mkoa wa Henan
Kuhusu kipengele cha ukweli cha "Mungu ni mwenye haki ", siku zote nilikuwa na ufahamu wa upuuzi kwa kiasi fulani. Nilidhani kuwa almradi mtu fulani hufichua upotovu katika kazi yake au hufanya makosa ambayo huiharibu kazi ya kanisa,

Jumanne, 10 Julai 2018

Christian Music Video Swahili "Hadithi ya Xiaozhen"(1): Jiwe, Karatasi, Makasi

Christian Music Video Swahili "Hadithi ya Xiaozhen"(1): Jiwe, Karatasi, Makasi

Kikundi cha watoto wachangamfu, wanaopendeza kilikuwa kikicheza mchezo wakati, bila kufikiri, waliuliza swali lenye cha kali: "Wanadamu hutoka wapi?" Je, unalijua jibu la swali hili?
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, watu wa Mungu

Alhamisi, 5 Julai 2018

New Swahili Gospel Choir Full Album Documentary 2018 | "Yule Anayeshikilia Ukuu Juu ya Kila Kitu"

New Swahili Gospel Choir Full Album Documentary 2018 | "Yule Anayeshikilia Ukuu Juu ya Kila Kitu"

Throughout the vast universe, all celestial bodies move precisely within their own orbits. Under the heavens, mountains, rivers, and lakes all have their boundaries, and all creatures live and reproduce throughout the four seasons in accordance with the laws of life…. This is all so exquisitely designed—is there a Mighty One ruling and arranging all this? Since coming into this world crying we have begun playing different roles in life. We move from birth to old age to illness to death, we go between joy and sorrow…. Where does mankind really come from, and where will we really go? Who is ruling our fates? From ancient times to modern days, great nations have risen up, dynasties have come and gone, and countries and peoples have flourished and perished in the tides of history…. Just like the laws of nature, the laws of humanity's development contain infinite mysteries. Would you like to know the answers to them? The documentary The One Who Holds Sovereignty Over Everything will guide you to get to the root of this, to unveil all of these mysteries!

Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,

Jumanne, 26 Juni 2018

New Swahili Gospel Choir Full Album Documentary 2018 | "Yule Anayeshikilia Ukuu Juu ya Kila Kitu"

New Swahili Gospel Choir Full Album Documentary 2018 | "Yule Anayeshikilia Ukuu Juu ya Kila Kitu"

Throughout the vast universe, all celestial bodies move precisely within their own orbits. Under the heavens, mountains, rivers, and lakes all have their boundaries, and all creatures live and reproduce throughout the four seasons in accordance with the laws of life…. This is all so exquisitely designed—is there a Mighty One ruling and arranging all this? Since coming into this world crying we have begun playing different roles in life. We move from birth to old age to illness to death, we go between joy and sorrow…. Where does mankind really come from, and where will we really go? Who is ruling our fates? From ancient times to modern days, great nations have risen up, dynasties have come and gone, and countries and peoples have flourished and perished in the tides of history…. Just like the laws of nature, the laws of humanity's development contain infinite mysteries. Would you like to know the answers to them? The documentary The One Who Holds Sovereignty Over Everything will guide you to get to the root of this, to unveil all of these mysteries!
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,