Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Jumamosi, 22 Desemba 2018

Wale Ambao Wamepoteza Kazi ya Roho Mtakatifu Ndio Walio katika Hatari Kubwa Zaidi

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, sauti ya Mungu

Sura ya 47. Wale Ambao Wamepoteza Kazi ya Roho Mtakatifu Ndio Walio katika Hatari Kubwa Zaidi

Katika kazi ya kueneza injili ya Mungu ya siku za mwisho, watu walio wachache tu ndio wanaweza kuacha kila kitu na kuziacha familia zao, kufikia kiwango ambacho wanahisi hawatarudi nyumbani kwa miaka kumi au kwa maisha yao yote, na hawahisi mateso yoyote kwa sababu ya kufanya hivyo; hii ndiyo nguvu inayopewa watu na Roho Mtakatifu. Lakini kiwango hiki hakiwezi kufikiwa kupitia kwa kimo cha mtu, kwa sababu watu hawaumiliki ukweli, uaminifu fulani tu wa kutumia kwa ajili ya Mungu. Kama watu wanao uamuzi fulani wa kuutafuta ukweli, na Roho Mtakatifu kisha awape neema fulani, basi watahisi hasa kuwa na shukrani na watakuwa na nguvu za aina fulani, na hivyo wataweza kujitokeza na kutumia kwa ajili ya Mungu—hii ndiyo neema ya Mungu. Lakini wapo baadhi ya watu wasioifuata njia sahihi wakati wanapoutekeleza wajibu wao, hawautafuti ukweli hata kidogo na hata wanakosa adabu, na katika hali kama hiyo Roho Mtakatifu hafanyi kazi ndani yao. Yaani, mtu huyo hayuko sahihi, na hata kama Roho Mtakatifu aliwahi kufanya kazi ndani yake, kazi hiyo itaharibiwa na wao watafuata bila kukusudia njia ya kwenda chini. Kama unao uamuzi wa kuutafuta ukweli, basi Roho Mtakatifu atakupa neema ya kufurahiwa, na unaweza kusonga mbele ukifuata ya njia inayoongozwa na Roho Mtakatifu; ukweli utakuwa wazi zaidi na zaidi kwako wewe, uamuzi wako utakuwa thabiti zaidi na zaidi, na kazi ya Roho Mtakatifu inayofanya kazi ndani yako itakuwa rahisi zaidi na zaidi. Kama watu hawaitembelei njia sahihi basi Roho Mtakatifu, mwishowe, atawaondoa, na baada ya kuondolewa, uamuzi wao wa mwanzo, mapenzi ya mwanzo, na nguvu zao za kuacha na kutumia vyote vitatoweka, na hawataweza kujizuia dhidi ya kusema, "Kwa nini sikuwahi kumsadiki Mungu? Kama sikuwa nimemsadiki Mungu, ningekuwa ninakumbana na haya sasa?" Wakati majuto haya, malalamiko haya, na ubaya huu yanapojitokeza, Roho Mtakatifu atakuwa tayari ameacha kufanya kazi. Ingawa watu hawa wanaweza bado kutumika kuihubiri injili au kufanya kazi nyingine, kile watakachokuwa wakifanya hakitakuwa kazi ya Roho Mtakatifu, wala hakitapewa nuru au kuongozwa na Roho Mtakatifu. Kitafanywa tu kwa kutegemea akili kidogo na elimu waliyonayo. Ingawa wataweza kufanya mambo haya yote ya nje ambayo yanaweza kutimizwa kwa mwili, hayatawakilisha mwongozo wa Roho Mtakatifu, wala kuwakilisha akili ya Roho Mtakatifu. Kama tu mtoaji huduma, hata kama Roho Mtakatifu hafanyi kazi ndani yake, mtu anaweza bado kuitoa huduma kwa kipindi fulani. Hata hivyo, anayo mawazo ya mtu, ubongo wa mtu, kufikiria kwa mtu; yeye ni tofauti na ng’ombe, farasi, au punda—anako kufikiria kwa binadamu na ni wa kiwango cha juu zaidi cha mnyama, na anaweza angaa kufanya baadhi ya mambo ambayo mtu wa kawaida anaweza kufanya. Amefuata tu njia mbaya; hauutafuti ukweli, au wokovu au kuulipiza upendo wa Mungu, hivyo anapotembea, anagundua kwamba njia hii yaishia hapo, na hana chaguo ila kuenda nyumbani na kuishi maisha ya kawaida ya familia. Kwa sasa, watu wengi wanasema haya: "Najua kwamba Mimi ni mbaya kwa kawaida! Mimi ni mwepesi sana wa kuvutwa na huruma na nimeasi mno." Haijalishi ni nini wanachosema, hawajui asili yao binafsi, wala hawafahamu hali yoyote ya ukweli; haijalishi wanaweza kuongea vyema kwa njia gani kuhusu mafundisho na wanaonekana kufahamu kila kitu, hawawezi kuweka chochote katika vitendo, na haya yanatosha kuthibitisha kwamba kazi ya Roho Mtakatifu ndani yao tayari imetoweka. Hivyo basi, haijalishi ubinadamu wako uko vipi au unafahamu kiasi kipi cha mafundisho, umevumilia mateso kiasi kipi au ni mangapi ambayo umetelekeza, kama Roho Mtakatifu hafanyi kazi ndani yako basi kila kitu kitasitishwa. Bila kazi ya Roho Mtakatifu mtu ni mpumbavu; mtu anaweza kuwa na nguvu kiasi kipi basi? Imani kiasi kipi? Maarifa ya mtu yatakuwa na manufaa yapi? Chukulia kuwa gerezani kwa mfano: Tangu wakati ambapo watu walianza kumsadiki Mungu, watu wamekumbana na haya; mara nyingi wanateswa na kusakwa, wakitorokea kila pahali. Matukio haya yote yakitiwa, ndani ya fikira na moyo wa kila mmoja, mawazo yasiyofutika: "Siwezi kuwa Yuda, siwezi kuongea kabisa kuhusu masuala ya kanisa." Je, watu wengi zaidi hawajajitayarishia haya? Lakini wakati bahati mbaya inapokupata, unaweza kuchukua hatua bila kujua. Mtu hawi Yuda pindi mkanganyo unapompata. Imesemekana awali kwamba vile utakavyokuwa hatimaye lazima iamuliwe na kama umeidhinishwa na Mungu. Kuona kama unayo idhini ya Mungu ni kimsingi kuangalia mambo kama vile iwapo unaye Roho Mtakatifu akifanya kazi ndani yako, kama Roho Mtakatifu anakupa nuru na kukuongoza, na kama unaandamana na neema fulani.
Wakati baadhi ya watu walipotenda kwanza wajibu wao, walijaa nguvu, ni kana kwamba hawangewahi kuishiwa na nguvu hizo. Lakini inakuwaje kwa kadri wanapoendelea ndipo wanapoonekana kupoteza nguvu hizo? Mtu waliokuwa wakati huo na mtu waliye sasa ni sawa na watu wawili tofauti. Kwa nini walibadilika? Sababu ilikuwa gani? Ni kwa sababu imani yao kwa Mungu ilienda njia mbaya kabla ya kufikia njia sahihi. Waliichagua njia mbaya. Kulikuwa na jambo lililokuwa limefichwa ndani ya kufuatilia kwao kwa kwanza, na kwa wakati mwafaka jambo hilo likaibuka. Nini kilikuwa kimefichwa? Ni matarajio yanayokuwa ndani ya mioyo yao wakati wakimsadiki Mungu, matarajio kwamba siku ya Mungu inawadia hivi karibuni ili taabu yao itafika mwisho; matarajio kwamba Mungu atabadilika na kwamba mateso yao yote yataisha. Wote wanatarajia siku wanayoweza kurudi nyumbani ili kuungana tena na familia zao, wakati hakutakuwa na mateso tena, wakati watakuwa huru kabisa, wakati wanaweza kumsadiki Mungu kabisa bila ya vizuizi vyovyote kutoka kwa wengine, na kila mmoja anaweza kuishi katika mazingira mazuri pale wanapoweza kuvalia vizuri na kula vizuri. Je, hawana tumaini hili lote? Fikira hizi zipo katika kina cha mioyo yao kwa sababu mwili wa binadamu hauko radhi kuteseka na unatazamia siku bora zaidi kila unapopitia mateso. Mambo haya hayatafichuliwa bila ya hali sahihi[a]. Wakati hakuna hali yoyote kama hiyo, kila mmoja ataonekana kuwa sawa hasa, ataonekana hasa kuwa na kimo, kuufahamu ukweli kwa kiasi fulani, na kuonekana mwenye nguvu za kipekee. Siku moja, wakati hali fulani itakapoibuka, fikira hizi zote zitajitokeza. Akili zao zitaanza kung’ang’ana, na baadhi yao wataanza kuharibikiwa. Si kwamba Mungu haifungui njia kwa ajili yako, au kwamba Mungu hakupatii neema yake, na bila shaka si kwamba Mungu hakufikirii katika ugumu wako. Ni kwamba kuyavumilia maumivu haya sasa ndiyo baraka yako, kwa sababu lazima ustahimili mateso kama haya ili kuokolewa na kunusurika, na yote haya yamepangiliwa awali. Hivyo kwa mateso haya kukukumba wewe ni baraka kwako. Usifikirie kwamba jambo hili ni rahisi; hili si jambo tu la kuchezea watu na kuwafanya kuteseka; maana yake fiche ni ya kina sana, muhimu sana. Kama hutawahi kuoa katika maisha yako, au kutowahi kurudi nyumbani katika maisha yako yote, hayo yatakuwa mambo muhimu. Kama njia unayoifuata ni sahihi, kama kile unachotafuta ni sahihi, basi mwishowe kile utakachopata kitakuwa zaidi ya kile ambacho watakatifu wa enzi, na ahadi utakazorithi zitakuwa kubwa zaidi. Kwa sasa baadhi ya watu siku zote wanafikiria: "Kwa kweli Mungu atakumbuka mateso haya yote ninayoyavumilia? Kama kwa bahati yoyote hakuna mtu wa kunisaidia mwishowe, nitafanya nini? Ni nani atakayenitunza kama nitakuwa mgonjwa? Je, Mungu ana habari? Je, mateso haya yataisha lini? Je, mwangaza wa siku utawasili lini?" Siku zote watu wanayatarajia mambo haya ilhali hawafikirii ni nini umuhimu wa mateso yao. Siku zote wanatamani Mungu kuweza kubadilika ili waweze kujiondolea mateso. Kila mmoja anayo mipango yake ya kibinafsi, na mwishowe ni katika asili ya binadamu kumsaliti Mungu; hakuna watu ambao kwa kweli wanampenda Mungu, hakuna mtu anayemtamani Mungu, anayetaka kuishi pamoja na Mungu; hawawezi kumsubiri Mungu kuondoka ulimwenguni. "Haijalishi ni kwa kiasi kipi ambacho Mungu ameteseka, mradi tu Anaondoka na tunaweza kuyaondoa mateso haya, basi itakuwa sawa." Kwa nini watu husema hivyo? Siku hizi watu wengi wanalo tarajio hili: "Kama Mungu ataondoka, basi tutatawala kama wafalme na hatutawahi kupitia mateso haya; Joka Kuu Jekundu atakuwa pia amemalizika, na tunafaa kutumia fimbo ya chuma ili kuyatawala mataifa yote na watu wote, je, hatutauona basi mwangaza wa siku?" Baadhi ya watu hata hujifikiria: "Mume, watoto, jamaa, marafiki—nyinyi nyote ni mashetani mnaonitesa. Siku moja Mungu wetu atajitokeza hadharani na kuwaadhibu. Mtaona kwamba njia tu tunayoifuata ndiyo njia sahihi." Ingawa tumaini hili sio haki, kuna kitu kibaya na baadhi ya hali ndani ya watu. Hakuna anayepangilia kuifuata barabara hii kwa maisha yake yote, akiutafuta ukweli ili kuyapata maisha na kumfahamu Mungu, na kuishi maisha yenye maana kama Petero mwishowe. Hivyo basi, watu hupotoka katika njia yao, hawana nafasi ya Mungu mioyoni mwao wakiwa njiani, na Roho Mtakatifu hafanyi kazi tena ndani yao, na wanatembea kinyumenyume; bidii yao yote inayotokana na kusadiki katika kipindi cha miaka minane au tisa ya awali kunaharibika kabisa—hili ni jambo hatari sana! Kuteseka sana, kusikiliza mahubiri mengi sana, kuendelea vivyo hivyo kwa miaka mingi sana, yote haya ni bure; hii ni hatari sana! Ni rahisi kuuteremka mlima lakini ni vigumu kuupanda mlima na kuchagua barabara sahihi ambayo mtu anafaa kutembelea. Vichwa vya watu wengi havifikirii vizuri! Hawawezi kuchagua kwa usahihi ni barabara gani sahihi na ipi ni ya kupotosha. Baada ya kuyasikiliza mahubiri mengi na kuyasoma maneno mengi ya Mungu, wanajua kwamba Yeye ni Mungu, lakini bado hawaamini; wanajua ni njia ya kweli, lakini bado hawawezi kuitembelea; ni vigumu vipi kuwaokoa watu! Je, unawezaje kujua kwamba Yeye ni Mungu lakini kutoweza kumsadiki Yeye? Je, wewe si Shetani? Hatutaizungumzia asili yako, lakini wewe ni kitu cha aina gani, kwa nini wewe ni mjinga hivyo? Unajua kwamba ndiyo njia ya kweli ilhali huitafuti, unaufahamu ukweli lakini umeshindwa kuutenda hivyo, hivyo wewe si Shetani? Akilini mwako hakuna madhumuni ya maisha, mwelekeo wa maisha, wala mambo yoyote yale ya binadamu wa kweli; wewe ni sawa tu na mnyama. Hivyo basi, kwa baadhi ya watu, si kwamba Roho Mtakatifu hafanyi kazi ndani yao au kwa makusudi au huwafichua kwa makusudi, ni kwamba hakuna njia yake Yeye kufanya kazi ndani yao. Watu ni wapotovu sana, wagumu sana wa kuwashughulikia, na hawachagui njia sahihi, hivyo ni vipi Roho Mtakatifu atakavyofanya kazi ndani yao? Kila wakati Roho Mtakatifu anapofanya kazi anawapa watu nafasi ya kufanya uchaguzi wao binafsi na halazimishi kamwe yeyote. Lakini moyo wa binadamu ni mjinga sana; hawaupendi ukweli, hawako radhi kutembea njia ya mateso, na hawako radhi kuzitumia jitihada yoyote au kulipa gharama yoyote. Watu wanajali tu kile kilicho mbele yao, na ni wachoyo sana. Kama kuna kitu mbele yao ambacho wanaweza kuona na kufurahia, basi watakitafuta, kukifikia, na watapuuza yale mambo ambayo hawawezi kuyaona au yale wanayoyaona hayana maana; hii ndio hali ya watu wengi zaidi, na karibu hakuna nafasi yoyote kwa Roho Mtakatifu kufanya kazi ndani yao. Watu wengine husema: "Ninawezaje kuutatua ugumu huu? Pengine itakuwa vyema kama nitapata mtu anayefahamu namna ya kuzungumza nami." Baada ya mtu mwingine kumaliza kuzungumza nao, wanakubali kwamba hali iko hivyo, na wanafahamu kwa kiwango cha kimafunzo, lakini wanasema kwamba hawawezi kuweka hilo katika matendo. Kama huwezi kuliweka katika matendo, basi ni nini haja ya Mimi kukuambia kulihusu? Unafaa kukaa pembeni! Hustahili kuusikia ukweli! Hustahili kumsadiki Mungu! Unafaa kusubiri tu kuangamia! Kwa vile kile ulichochagua ni njia mbaya, inayostahili dharau, ya kishetani, haijalishi ni ukweli kiwango kipi utakaozungumziwa, hautaupenda, hivyo unafaa tu kukaa pembeni! Hakuna haja ya kusema chochote kwa mtu aina hii. Siku hizi mara nyingi kunasemekana: "Ninaelewa kila kitu, siwezi tu kukiweka katika matendo." Maneno haya ni ithibati kwamba mtu huyo ni Shetani na yeye ni wa namna ya Shetani kabisa. Mtu asiyeupenda ukweli ni mtu mwovu kwa kweli; kile ambacho mtu anapenda, anatumainia, anatamani na ana kiu nacho ni uwakilishi kamili wa asili ya mtu huyo. Kama huupendi ukweli basi wewe ni wa Shetani, wewe ni kitu cha maangamizo; kama unaupenda ukweli basi wewe ni mmojawapo wa wale waliopangiliwa kabla na kuchaguliwa na Mungu; je, haya si wazi?
Njia anayochagua mtu ni muhimu. Unaweza kutafakari kwa utulivu na makini, na hujachelewa kutubu. Kama unao uamuzi, basi hilo ni jambo zuri; wale wasiokuwa na uamuzi ndio wa chini zaidi ya wote. Angalau kabisa unahitaji kuwa na uamuzi; kuhusiana na namna ya kufikia kile ulichoamua kufanya, namna unavyoweza kukikamilisha kile ulichoamua kufanya, lazima kuwepo na njia kwa hili. Kwanza kabisa, lazima uuelewe ukweli, ujue hatima itakayofuata kwa wanadamu, ujue njia ambayo wanadamu wanafaa kutembelea na shabaha wanazofaa kufikia. Imesemekana, "Mambo na masuala yote yamo mikononi mwa Mungu." Unaweza kuyapitia maneno haya na kuyapima mambo yote dhidi yao. Kwa vile sasa unamsadiki Mungu, unafaa kuwa mtiifu kwa Mungu? Umuhimu wa imani kwa Mungu ni upi?? Je, imani kwa Mungu ni kuzipokea baraka tu? Unatembelea sasa katika njia hii, lakini utaweza kuvumilia mpaka mwisho? Utawezaje kuitembea katika siku za usoni? Wakati unapokumbana na ugumu, unafaa kuwa na baadhi ya kanuni za ukweli ili kujihimiza, ili usisite, kuwa mnyonge, usiwe mwenye mawazo mabaya, usilalamike kuhusu Mungu, na usitende dhambi dhidi ya Mungu—lazima uelewe na uwe wazi kuhusu mambo haya yote.
Watu wanapofurahi, wanasema: "Niko radhi kuitumia jitihada kwa ajili ya Mungu, nitaitumia kwa ajili ya Mungu kwa maisha yangu yote." Lakini pengine kwa wakati fulani wakati watakapokumbana na changamoto, watakuwa na mawazo mabaya na kujisemea wenyewe: "Mungu yupi? Mimi siwezi kumsadiki Yeye. Barabara hii ni ngumu sana!" Baada ya kuomba, kuna lawama: "Mimi napaswa kumshukuru Mungu!" Kujua kuwa unapaswa kumshukuru Mungu, hufai tena kutenda namna hivyo. Basi pengine siku moja itafika utakapokumbana na tukio baya na tena kuwa mwenye fikira mbaya, tena kulalamika kuhusu Mungu: "Mbona Mungu amepangilia hali hizi kwangu Mimi, kwa nini Yeye siku zote hunifanya Mimi kuteseka? Kwa nini hawezi kunizuia dhidi ya kuteseka?” Watu siku zote hulalamika, na pia husema kwamba wao wanapaswa kumshukuru Mungu. Siku zote hawabadiliki katu. Wakati wanapokumbana na changamoto au hata kitu kisichowapendeza kutakuwa na chuki na maudhi, na mbaya zaidi kutakuwa hata na baadhi ya watu wanaosema maneno ya kukufuru na hukumu; baadaye watahisi haikuwa vyema kuongea kwa njia hiyo, na watahisi vibaya kuhusu kufanya hivyo, na kujaribu haraka kutenda baadhi ya wajibu na kufanya baadhi ya mambo mazuri ili kuweza kufidia. Haya yote yanaonyesha nini? Asili ya binadamu ni mbaya, wao hawana akili na hisi. Sawa tu na kujihusisha katika mipango ya biashara, wakati wanapomhitaji Mungu watamvuta Yeye karibu, na wakati hawamhitaji Yeye watasonga mbali na Yeye na kumpinga Yeye, wakifanya kile kinachowafanya kufurahi. Binadamu ana kiburi na ni mwenye kujiamini mno, na hana uoga. Hana chuki ya kweli wala upendo wowote wa kweli ndani ya moyo wake, hakuna tofauti kati ya uhaki na kutokuwa na uhaki; hana mipaka. Hana shabaha, sembuse kuwa na kanuni zozote au ufahamu wa adabu anapofanya chochote. Moyo wa binadamu ni mbaya sana. Katika hali hii, watu wangali wanatazamia ahadi kuu wanazoweza kupokea, baraka nyingi wanazoweza kupata, namna watakavyopata umaarufu au anasa watakayopitia. Wanapofikiria tu kuhusu mambo haya ndipo wanapofikiri: "Namna Mungu alivyo mzuri! Lazima niufidie upendo wa Mungu!" Kwa nini wanasema "mzuri"? Wanatoa wapi msemo wa "fidia"? Unasemwa kwa nia? Hayo ni maneno ya wepesi wa kuvutwa na huruma yanayotamkwa katika hali ya kivutio na furaha ya mara moja, lakini je, yanachukuliwa kama ufahamu wa kweli? Huu ni upendo wa kweli? Je, unatoka ndani ya kina cha moyo wako? Kama una ufahamu huu kwa kweli, basi kwa nini bado unalalamika? Kama kweli unahisi unapaswa kumshukuru Mungu basi kwa nini unalalamika? "Mungu, Hujawa mwema kwangu Mimi, Umenipuuza, Hujawa mzuri kwangu Mimi, hivyo sitakumakinikia Wewe kwa vyovyote vile! Hunihitaji Mimi, hivyo sitakufanyia kazi Wewe tena!" Watu wanayo chuki nyingi sana ndani yao! Hatimaye, wangali wanafikiria: "Ninampenda Mungu! Ninampenda Mungu zaidi ya wengine wanavyompenda." Je, huu ni upendo wa kimatendo vipi kwa Mungu? Kwamba watu wanaweza kusema hivi kunathibitisha kwamba hawaijui asili yao binafsi, hawajui kile walicho wao, wameundwa na nini, na kwamba hawawezi kujikadiria wao binafsi. Kwa hakika ni katika asili ya kila mmoja kupinga na kumsaliti Mungu; hili ni jambo ambalo kila mmoja analo kwa pamoja na wote wanavyo vitu hivi ndani yao. Hakuna mtu anayependa kwa kweli kile ambacho kinastahili kupendwa, na hata zaidi hakuna mtu anayechukia kile kinachofaa kuchukiwa; hana mipaka yoyote sembuse maono yoyote, ndani yake hakuna tofauti kati ya haki na kutokuwa na haki, hakuna tofauti kati ya nyeusi na nyeupe, sembuse tofauti wowote kati ya ukweli na mafundisho au uvumi; hawezi kutambua kati ya mambo yoyote haya. Watu hawaelewi kuhusu kile kinachostahili upendo, kile kinachostahili kutafutwa, na kile kinachofaa kuchukiwa, na hawawezi kuchukuliwa kama wana utambuzi. Wakati watu wa ulimwengu wanapouimba wimbo, "Rudi Nyumbani Mara kwa Mara," baadhi ya watu wanashawishika kuwa mbali. Watu wana nini ndani yao? Wanao ukweli wowote? Baadhi ya watu hufikiri kwamba wanaweza kufanya kazi fulani, kwamba wana baadhi ya sifa zinazostahili, na wanaonekana kuwa na ukweli fulani. Kwa hakika, huna chochote, na wewe si chochote! Ingawa unaweza kuzungumzia mafundisho fulani kwa wengine sasa, pengine siku moja katika siku za usoni utaweza kubembelezwa na wengine, na utatetereka vibaya zaidi kuliko mtu yeyote mwingine, na utaathirika vikali zaidi na ubaya kuliko mtu mwingine yeyote. Je, unayaamini haya? Je, umeshawishika na suala hili? Pengine ungali bado hujapitia kuwa mbaya sana au kuanguka vibaya na kufikiria kuwa wewe ni mwenye nguvu sana. Bila ya uzoefu huo unafikiria kwamba unacho kimo kikuu, lakini pengine siku moja unapofichuliwa, utalia na kusema, "Nimepatikana, nimepatikana tu." Unaanza kusonga kutoka katika kipeo kimoja hadi kingine. Watu wengi walikuwa wamejaa nguvu walipomwamini Mungu mara ya kwanza, lakini pengine walikuja kukumbana na kitu kilichowafanya kuwa wanyonge ghafla, na hawakuweza katu kuinuka tena. Je, umewahi kugundua matatizo yoyote na watu hawa? Nguvu au unyonge wa kila mtu si jambo ambalo wanaweza kudhibiti wenyewe. Mambo yaliyofichwa ndani ya watu yanaweza kujitokeza wakati wowote na mahali popote. Hakuna kiwango chochote kidogo cha uchafu mbaya kilichoko ndani ya watu, na kinajitokeza kwa mtiririko usioisha! Hivyo basi, asili ya watu ni asili ya Shetani—hakuna tofauti kamwe—na ni tofauti kabisa na kiini cha Mungu.
Kitambo, Mungu alisema: "Ninaweza kumpenda binadamu milele, na ninaweza pia kumchukia binadamu milele." Yaani, Anavyo viwango, Anafikia hitimisho Zake mwenyewe, na anao msingi ambao Anafikia hitimisho hizo. Anazo hukumu Zake, vipimo na viwango vya kile Anachopenda na kuchukia, kinachomfanya Yeye kuwa na furaha na kile Anachochukia. Watu hawana vitu hivi hivyo watapotoka wakati wanapotembea, watakuwa vigeugeu na, bila mtu yeyote wa kuwaongoza, siku zote wataelekea upande usiofaa.
Baadhi ya watu wangali bado siku zote wanatumai: "Mungu anaondoka duniani lini? Harakisha na kuondoka. Baada ya kuipitia kazi Yake miaka hii michache, nafaa kuolewa lakini nagundua kuwa siwezi; waona, hili ndilo ninalopata kwa kumsadiki Mungu miaka yote hii!" Jukumu lote sasa linawekwa kwa Mungu. Hawajui kabisa kuhusu kile walichopata kwenye miaka hiyo, na thamani yake. Kama si kazi ya Mungu mwenye mwili, basi watu wa Kichina wangekuwa wametoweka kitambo; pengine hili ni jambo ambalo baadhi hawatasadiki. Kama hulisadiki, basi yamaanisha kwamba wewe huyaelewi mambo kabisa, lakini huu ndio ukweli. Watu hata hufikiria: "Bila ya Mungu kutuongoza, tunaweza bado kutembelea njia. Tumekisoma kitabu cha Neno Laonekana katika Mwili mara nyingi sana, kimeelezwa kwa muhtasari akilini mwetu, na tunazifahamu kanuni, ili tuweze kuichukua hatamu." Je, unaweza kweli kuichukua hatamu? Huwezi kuitembelea njia sahihi, na unapotoka baada ya kuitembelea kidogo, hivyo unaweza bado kuingia kuhalisia? Ungali wewe hujashawishika. Yaweza kusemekana kwamba yeyote atapotoka kama hana mwongozo wa aina hii kutoka kwa Mungu? Je, Roho Mtakatifu alikuwa akifanya katika Enzi ya Neema? Je, Roho Mtakatifu alifanya kazi? Ni madhehebu mangapi yalitenganishwa baadaye? Kulikuwepo na madhehebu yasiyofikirika ya kila aina, hata yale ambayo majina yao hayawezi kufikiriwa au kukumbukwa. Ni nini tatizo na hali hii? Mambo ya asili ya watu yaliyo ndani yao lazima yaeleweke kabisa, na lazima pia kuwepo na ufahamu wa kiini cha watu. Kufahamu na kuona kabisa hakumaanishi unafaa siku zote kukwama pale, lakini badala yake kunamaanisha kwamba kutoka pale, lazima uinuke na uutafute ukweli, yasome maneno ya Mungu uijue asili ya binadamu, ili kukifahamu kiini cha binadamu, na kutia jitihada na ukweli; kwa njia hii tu ndipo utakapotembea katika njia sahihi. Neno la Mungu lafunua na kuifichua asili ya binadamu, na kuwaruhusu watu kujua kiini chao ni kipi. Ni muhimu sana kuelewa kiini potovu cha binadamu. Waona, Shetani ni msiri kweli. Mungu alimwuliza: "Wewe watokea wapi?" naye Shetani akajibu: "Natoka katika kuzunguka huku na kule duniani, na katika kutembea huku na huku humo." Ukisikiza kwa makini kwa kauli hii ya Shetani, "Kutembea huku na kule duniani," utashangaa, alikuwa akienda au akitoka? Hivyo basi, kauli hii ni kauli ya siri, na kutoka katika kauli hii Shetani anaweza kuchukuliwa kuwa kiumbe cha siri. Baada ya watu kupotoshwa na Shetani wao pia huwa wasiri ndani yao; wakati wanapoyafanya mambo hawana kigezo, viwango, na kanuni, na hivyo basi kila mmoja anapotoshwa kwa urahisi. Wakati Shetani alipomjaribu Hawa, alisema: "Kwa nini usile tunda la mti ule?" Hawa akajibu, "Mungu alisema kwamba kama nitakula tunda la mti ule, nitakufa." Shetani kisha akasema, "Si lazima ufe kama utalila tunda la mti ule." Nia ya kauli hii ya Shetani ilikuwa ni kumjaribu; hakusema kwa hakika kwamba kwa kulila tunda lile kutoka katika mti binadamu asingekufa, alisema tu kwamba binadamu si lazima afe, na hivyo binadamu akafanywa kufikiria: "Kama si lazima nife, ni sawa nikilila." Binadamu hakuweza kulipinga jaribio la kulila tunda. Kwa njia hii, Shetani aliifikia shabaha yake ya kumjaribu binadamu hadi aitende dhambi; hakuchukua jukumu la hayo, kwa sababu hakulazimisha yeyote kulila. Sasa watu wote wanazo sumu za Shetani ndani yao ambazo humjaribu Mungu na kumjaribu binadamu. Wakati mwingine wakati watu wanapoongea wanaongea kwa sauti ya Shetani, kwa nia ya kupima na kujaribu. Fikira na mawazo yote yanayojaa ndani ya watu ni sumu za Shetani, tabia waliyo nayo ni jambo la Shetani, na wakati mwingine konyezo au ishara ya mkono huwa na dalili ya kupima na majaribu. Watu wengine husema: "Ninamsadiki Mungu na nafuata kwa njia hii, hivyo lazima kupata kitu. Siutafuti ukweli lakini ninaufuata hadi mwisho, na ninatumia nguvu zangu zote ili kuitumia jitihada na kuyaacha mambo yaliyo katika mkondo wa wajibu wangu. Hata kama nitatenda baadhi ya makosa, ninaweza bado kupata jambo." Hawajui kile wanachosema. Huku kukiwa na upotovu mwingi sana ndani ya watu, wanawezaje kubadilika kama hawautafuti ukweli? Kwa kiwango cha upotovu ambacho binadamu anacho, kama hakuna ulinzi kutoka kwa Mungu, basi mtu anaweza kutetereka na kumsaliti Mungu wakati wowote. Je, unayasadiki hayo? Hata kama utajilazimisha, huwezi bado kufaulu hadi mwisho kwa sababu hatua ya mwisho ni kuunda kundi la washindi; je, inaweza kuwa rahisi kama unavyofikiria? Mwishowe haihitajiki kwa watu kubadilika asilimia 100 au asilimia 80, lakini angaa kunafaa kuwa na badiliko la asilimia 30 au 40; angalau kabisa lazima uyachimbue mambo ambayo yamepachikwa ndani yako kabisa na kuyabadilisha; na unaweza kufikia hitaji la Mungu la asilimia 30 hadi 40, au bora zaidi kufikia badiliko la asilimia 60 hadi 70, kumaanisha kwamba unaumiliki ukweli fulani ndani yako, kwamba unayo mambo ambayo yanalingana na ya Mungu ndani yako, na kwamba unapokumbana na baadhi ya masuala haitakuwa rahisi kwako wewe kumpinga Mungu, na haitakuwa rahisi kuikosea tabia ya Mungu. Kwa njia hii, mwishowe, utafanywa kuwa mtimilifu, na kupongezwa.
Baadhi ya watu siku zote hufikiria: "Je, kumwamini Mungu ni kuhudhuria tu mikutano, kuimba nyimbo, kulisikiliza neno la Mungu, kuomba, kufanya baadhi ya wajibu? Je, hali haiko hivyo?" Haijalishi ni kwa muda gani mmekuwa waumini wa Mungu bado hamjaelewa kabisa umuhimu wa imani kwa Mungu. Kwa hakika, umuhimu wa imani kwa Mungu ni wa kina sana, na watu hawajaifikiria kabisa kuihusu. Mwishowe, mambo yaliyo ndani ya watu ambayo ni ya Shetani, na mambo ya asili yao lazima yabadilike, na lazima yalingane na mahitaji ya ukweli; kufanya hivi tu ndiko kuutimiza kwa kweli wokovu. Kama upo vile ulivyokuwa kwenye dini—kupiga kelele ukitaja baadhi ya maneno ya mafundisho tu au kupiga kelele ukitaja kaulimbiu fulani na kisha kutenda baadhi ya vitendo na tabia njema na kutotenda dhambi fulani, kutotenda dhambi za waziwazi—hii bado haimaanishi kwamba umeingia katika njia sahihi ya kumsadiki Mungu. Kwa sababu tu unaweza kuzitii sheria, hiyo inamaanisha kwamba unaitembelea njia sahihi? Je, inamaanisha kuwa umechagua kwa usahihi? Kama mambo ndani ya asili yako hayajabadilika na mwishowe ungali unampinga Mungu na kumkosea Mungu, basi haya ndiyo matatizo makubwa zaidi. Kama unamwamini Mungu lakini hulitatui tatizo hili, basi unaweza kuchukuliwa kuwa umeokolewa? Mimi kuyasema haya, kunamaanisha nini? Ni kuwafanya nyote kufahamu ndani ya mioyo yenu kwamba imani kwa Mungu haiwezi kutenganishwa na maneno ya Mungu, na Mungu au na ukweli. Lazima uichague njia yako vyema, utie jitihada katika ukweli na kutia jitihada ndani ya maneno ya Mungu. Usiwe tu na maarifa kiasi ya kijinga na kisha kujiona kuwa umemaliza, au kuyafahamu tu. Ukiyafanya mambo kwa njia ya haraka, utajidhuru tu mwenyewe. Mtu hafai kupotoka katika imani yake kwa Mungu; kama mwishowe hakuna Mungu ndani ya moyo wake, na anashikilia tu kitabu akikiangalia kidogo kana kwamba anatazama maua huku akienda shoti akiwa juu ya mgongo wa farasi, bila ya kuwa na nafasi ya Mungu ndani ya moyo wake, basi amepatikana. Je, "Imani ya binadamu kwa Mungu haiwezi kutenganishwa na maneno ya Mungu" inamaanisha nini? Unaelewa? Je, inakinzana na, "Imani katika Mungu haiwezi kutenganishwa na Mungu"? Unawezaje kuwa na Mungu ndani ya moyo wako kama maneno ya Mungu hayamo ndani ya moyo wako? Kama unamsadiki Mungu lakini Mungu hayumo ndani ya moyo wako, wala maneno ya Mungu hayako, wala mwongozo wa Mungu, basi umepatikana kabisa. Kama huwezi kufanya jambo dogo kulingana na hitaji la Mungu, basi ukikumbana na suala kubwa la kanuni utakuwa hata na uwezo mdogo zaidi kulitimiza hitaji la Mungu. Hii inamaanisha huna ushuhuda, na kwa hivyo kuna matatizo, na hivyo kuthibitisha kwamba huna chochote. Kunayo mambo mengi ambayo hayawezi kuelezewa kwa undani, na siku moja tu wakati Roho Mtakatifu atakupa nuru ndipo utakapofahamu kabisa. Sasa hivi ninaweza tu kutumia kauli kwamba watu watafikiria kuwa ni kawaida kabisa na pia haina mantiki sana kuonyesha. Je, wajua kwamba katika nchi hii, wakati unaweza kupitia mateso haya na kuifurahia kazi ya Mungu, wageni huwa wanawaonea wivu kabisa nyinyi wote? Matamanio ya wageni ni: Tunataka pia kupitia kazi ya Mungu, tutateseka kwa vyovyote vile kwa sababu ya hilo. Tunataka kuupata ukweli pia! Tunataka pia kupata umaizi fulani, kupata kimo fulani, lakini kwa bahati mbaya hatuna yale mazingira. Wanafikiria kwamba watu wa Kichina wamebarikiwa sana, lakini wewe unafikiria kwamba wao ndio waliobarikiwa, na unawaonea wivu; hii kwa kweli ni maana ya kuishi katika baraka lakini kutoweza kuihisi. Kulifanya kundi hili la watu kuwa kamili katika nchi ya joka kuu jekundu, kuwafanya kuvumilia mateso haya, kunaweza kusemekana kuwa utukuzaji mkubwa zaidi. Iliwahi kusemwa: "Nimeuleta utukufu Wangu kutoka Israeli hadi Mashariki kitambo." Je, nyinyi nyote mnaelewa maana ya kauli hii sasa? Mnafaa kuitembelea vipi njia iliyo mbele? Mnafaa kuutafuta vipi ukweli? Kama hamtautafuta ukweli basi mnawezaje kuipata kazi ya Roho Mtakatifu? Pindi utakapopoteza kazi ya Roho Mtakatifu, basi utakuwa katika hatari kubwa zaidi. Mateso ya sasa si muhimu. Je, wajua yatakufanyia nini?
kutoka kwa Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Ijumaa, 21 Desemba 2018

Maonyesho ya Mungu | "Mwanadamu Anaweza Kuokolewa tu Katikati ya Usimamizi wa Mungu"

Maonyesho ya Mungu | "Mwanadamu Anaweza Kuokolewa tu Katikati ya Usimamizi wa Mungu"

Mwenyezi Mungu anasema, "Mwanadamu hana ufahamu wa umuhimu wa Mungu kumwokoa na umuhimu wa kazi ya usimamizi wa Mungu, na hafahamu jinsi Mungu Anavyotamani zaidi wanadamu wawe. Je, ni wanadamu mfano wa Adamu na Hawa, wasiopotoshwa na Shetani? Hapana!

Jumatano, 19 Desemba 2018

Filamu za Injili | "Nimewahi Treni ya Mwisho" | Entering the Ark of the Last Days

Filamu za Injili | "Nimewahi Treni ya Mwisho" | Entering the Ark of the Last Days

Chen Peng alikuwa mchungaji katika kanisa la nyumba fulani. Alikuwa akimtumikia Bwana kwa bidii, na mara nyingi alifanya kazi kama mhubiri, akiwasaidia wafuasi wake, na kulibebea kanisa mizigo mizito. Lakini katika miaka ya hivi karibuni, kanisa lilizidi kuwa tupu zaidi na zaidi. Waumini walikuwa na roho dhaifu na wavivu, wakikosa mkutano baada ya mkutano. Na hivyo Mchungaji Chen aliona giza likiangukia nafsi yake, kana kwamba kisima cha roho yake kilikuwa kikavu, na hakuweza kuhisi uwepo wa Bwana. Katika mikutano, aligundua kwamba hakuwa na kitu alichoweza kuhubiri. ... Alifanya kila kitu alichoweza kufikiria ili kuimarisha kanisa, lakini jitihada zake zote zilikuwa bure. ... Chen Peng alikuwa amesitikika, amepotea, na hakuweza kuelewa kwa nini kanisa lake lilikuwa linajawa na ukiwa sana, na kwa nini walikuwa wamepoteza uwepo wa Bwana.
Hadi siku moja, kwa bahati, aliposikia injili ya ufalme wa Mwenyezi Mungu. Baada ya kupitia mjadala mkali, Chen Peng hatimaye aligundua sababu ya kanisa lake kuwa na ukiwa, na akaamini kwamba Mungu alikuwa tayari amekuwa mwili na kuwa Mwana wa Adamu: Mwenyezi Mungu, anayehukumiwa na kutelekezawa na ulimwengu wa kidini, ambaye anasema ukweli na kufanya kazi ya hukumu katika zile siku za mwisho! Ni wale tu ambao wanakubali kazi ya hukumu ya Mwenyezi Mungu, Kristo wa zile siku za mwisho, na kufuata nyayo za Mwana-Kondoo wataweza kunyakuliwa mbele ya kiti cha enzi cha Mungu na kufikia kunyunyuziwa na kupewa maji ya uzima. Kwa sababu ya hilo, Chen Peng aliwahi treni ya mwisho na kukubali kwa furaha kazi ya Mungu katika zile siku za mwisho.

Jumatatu, 17 Desemba 2018

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Kazi ya Mungu na Utendaji wa Mwanadamu" (Sehemu ya Pili)

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Kazi ya Mungu na Utendaji wa Mwanadamu" (Sehemu ya Pili)

Mwenyezi Mungu anasema, "Katika kila aina ya kazi ya Mungu kuna maono yanayofahamika na mwanadamu; maono yanayofuatwa na matarajio mwafaka ya Mungu kwa mwanadamu. Bila haya maono kama msingi, mwanadamu hawezi kuwa na uwezo wa utendaji na pia hangeweza kumfuata Mungu bila kuyumbayumba. Ikiwa mwanadamu hamjui Mungu au hayaelewi mapenzi ya Mungu, basi yote ayafanyayo ni bure na yasiyoweza kukubalika na Mungu. Hata mwanadamu awe na vipawa vingi kiasi gani, bado hawezi kujitenga na kazi ya Mungu na uongozi wa Mungu. Bila kujali uzuri na wingi wa matendo ya mwanadamu, bado hayawezi kuchukua nafasi ya kazi ya Mungu. Kwa hivyo basi, utendaji wa mwanadamu hauwezi kutenganishwa na maono katika hali yoyote ile. Wale ambao hawakubali maono mapya hawana vitendo vipya. Vitendo vyao havina uhusiano na ukweli kwani wanajifunga katika mafundisho ya dini na kufuata sheria zilizokufa; hawana maono mapya kabisa na kwa sababu hiyo hawatendi kulingana na enzi mpya. Wamepoteza maono na kwa kufanya hivyo wamepoteza kazi ya Roho Mtakatifu, hivyo basi kupoteza ukweli pia."

Jumapili, 16 Desemba 2018

Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu | "Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu"

Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu | "Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu"

Mwenyezi Mungu anasema, "Kama huelewi tabia ya Mungu, basi itakuwa haiwezekani kwako wewe kufanya kazi unayofaa kumfanyia. Kama hujui dutu ya Mungu, ndivyo pia haitawezekana kubakiza hali ya kumcha na kumwogopa Yeye, utakuwa ni uzembe na kuepuka kusema ukweli wote kwa kutojali, na zaidi, kukufuru kusikorekebishika. Kuelewa tabia ya Mungu kwa kweli ni muhimu sana, na maarifa ya dutu ya Mungu hayawezi kupuuzwa, ilhali hakuna yeyote amewahi kuchunguza kwa umakinifu au kudadisi suala hili. Ni wazi kuona kwamba nyote mmepuuzilia mbali amri za kiutawala Nilizozitoa. Kama hamuelewi tabia ya Mungu, basi mtaweza kukosea kwa urahisi sana tabia Yake. Kosa kama hilo ni sawa na kumkasirisha Mungu Mwenyewe, na tunda la msingi la tendo lako linakuwa ni uhalifu dhidi ya amri ya kiutawala. Sasa unafaa kutambua kwamba unaweza kuelewa tabia ya Mungu unapokuja kujua dutu Yake, na kuelewa tabia ya Mungu ni sawa na kuelewa amri za kiutawala. Bila shaka, wingi wa amri za kiutawala zinahusu tabia ya Mungu, lakini uzima wa tabia Yake bado haujaweza kuonyeshwa ndani yao. Hili linawahitaji kuzoea zaidi tabia ya Mungu."

Jumamosi, 15 Desemba 2018

Upendo wa Mungu Ulikuwa Nami Katika Gereza la Giza la Ibilisi

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Upendo wa Mungu

Upendo wa Mungu Ulikuwa Nami Katika Gereza la Giza la Ibilisi

Yang Yi, Mkoa wa Jiangsu
Mimi ni Mkristo wa Kanisa la Mwenyezi Mungu. Nimekuwa mfuasi wa Mwenyezi Mungu kwa zaidi ya miaka kumi. Katika wakati huu, kitu kimoja ambacho sitawahi kusahau ni taabu mbaya sana nilipokamatwa na polisi wa CCP muongo mmoja uliopita. Wakati huo, licha ya mimi kuteswa na kukandamizwa na ibilisi waovu, na kuwa ukingoni mwa kifo mara kadhaa, Mwenyezi Mungu alitumia mkono Wake wa nguvu kuniongoza na kunilinda, kunirudisha kwa uhai, na kunipeleka kwa usalama…. Kupitia hili, kwa kweli nilipitia uvukaji mipaka na ukuu wa nguvu ya uhai wa Mungu, na kupata utajiri wa thamani wa maisha niliyotunikiwa na Mungu.
Ilikuwa Januari 23, 2004 (siku ya pili ya Mwaka Mpya wa Kichina). Nilihitaji kuenda kumtembelea dada fulani kutoka kwa kanisa; alikuwa katika shida na alihitaji msaada kwa dharura. Kwa kuwa aliishi mbali sana, ilinibidi nirauke mapema ili kupata teksi ili niweze kurudi siku hiyo hiyo. Niliondoka nyumbani wakati tu mwanga ulichomoka. Kulikuwa na watu wachache sana barabarani, wafanyikazi wa kusafisha taka pekee. Kwa wasiwasi nilitafuta teksi, lakini hakukuwa na yoyote hapo. Nilienda kwa stesheni ya teksi kusubiri, na nikasongea kwa barabara kusimamisha moja nilipoiona ikija—lakini ikatokea kuwa gari la Shirika la Kulinda Mazingira. Waliniuliza mbona niliwasimamisha. “Naomba radhi, ilikuwa makosa, nilidhani mlikuwa teksi,” nilisema. “Tunafikiri ulikuwa ukitundika mabango yasiyo halali,” walijibu. “Je, mliniona? Yako wapi mabango niliyokuwa nikitundika?” nilisema. Bila kunipa fursa ya kujitetea, wao watatu walikimbia mbele na kwa nguvu walichunguza mfuko wangu. Walipekua kila kitu katika mfuko wangu—nakala ya mahubiri, kitabu cha kuandikia, pochi, simu ya rununu na bipa iliyoondolewa uwezo, na kadhalika. Kisha walichunguza kwa makini nakala hiyo ya mahubiri na kitabu cha kuandikia. Kwa kuona kwamba hakukuwa na mabango ndani ya mfuko wangu, waliinua nakala hiyo ya mahubiri na kusema: “Yaweza kuwa hukuwa ukitundika mabango yasiyo halali, lakini unamwamini Mwenyezi Mungu.” Kisha, walipigia simu Divisheni ya Dini ya Kikosi cha Usalama wa Taifa. Punde baadaye, watu wanne kutoka kwa Kikosi cha Usalama wa Taifa waliwasili. Walijua kwamba nilikuwa muumini wa Mwenyezi Mungu punde walipoona vitu ndani ya mfuko wangu. Bila kuniruhusu kusema lolote, walinitupa ovyo katika gari lao, kisha walifunga mlango kwa ufunguo ili kunikomesha kuhepa.
Tulipowasili katika Shirika la Usalama wa Umma, polisi waliniongoza kuingia katika chumba. Mmoja wao alichezacheza na bipa na simu yangu ya rununu, akitafuta dokezo. Aliwasha simu lakini ikaonyesha kwamba ilikuwa na betri ya chini, kisha ikasema betri ilikuwa tupu kabisa. Ingawa alijaribu sana, hangeweza kuiwasha. Akishika simu, alionekana kuwa na wasiwasi. Nilikanganywa pia—nilikuwa nimechaji simu hiyo asubuhi hiyo. Inawezekanaje iwe haina chaji? Ghafla nilitambua kwamba Mungu alikuwa amepanga hili kwa miujiza ili kuzuia polisi kupata taarifa yoyote kuhusu ndugu wengine. Pia nilielewa maneno yaliyonenwa na Mungu: “vitu vyote, vilivyo hai au vilivyokufa, vitahamishwa, vitabadilika, vitafanywa vipya, na kutoweka kulingana na mawazo ya Mungu. Hivi ndivyo Mungu anavyotawala juu ya kila kitu” (Kutoka kwa “Mungu Ndiye Chanzo cha Uhai wa Mwanadamu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Hili lilinipa ufahamu wa kweli wa ukuu na mpango wa Mungu wa mambo yote, na kuimarisha imani yangu katika ushirikiano wa baadaye. Akiashiria vitu ndani ya mfuko wangu, afisa wa polisi aliuliza kwa shutuma: “Haya yanaonyesha kwamba kwa kweli wewe si mshirika wa kawaida wa kanisa. Lazima uwe mmoja wa uongozi mkubwa, mtu ambaye ni muhimu. Kwa maana viongozi wadogo hawana bipa ama simu za rununu. Niko sahihi?” “Sielewi unachosema,” nilijibu. “Unajifanya huelewi!” alisema kwa sauti kubwa, kisha akaniamuru kuchuchumaa nilipozungumza. “Huku akiona kwamba singeshirikiana, walinizingira na kuanza kunipiga ngumu na kunipiga teke—kiasi cha kutosha kuniua. Uso wangu ukiwa umejaa damu na kuvimba, mwili wangu mzima ukiuma kiasi cha kutovumilika, nilianguka sakafuni. Nilikasirishwa. Nilitaka kuzungumza maana kwao, kutoa sababu ya kuthibitisha hali yangu: Nimekosea wapi? Mbona mlinichapa hivyo? Lakini sikuwa na njia ya kuongea maana nao, kwa sababu serikali ya CCP haiongei maana. Nilikanganyikiwa, lakini sikutaka kukubali vipigo vyao. Nilipokuwa tu sijui la kufanya, ghafla nilifikiri jinsi, kwa kuwa hawa maofisa waovu wa serikali ya CCP walikuwa wapuuzi sana, kwa kuwa hawakuwa wakiniruhusu kuzungumza maneno yoyote ya maana, sikuhitaji kuwaambia chochote. Ilikuwa ni heri nibaki kimya—kwa njia hiyo singekuwa na manufaa yoyote kwao. Nilipofikiri hili, niliacha kutia maanani walichokuwa wakisema.
Huku wakiona kuwa mtazamo huu haukuwa na athari yoyote kwangu, polisi hao waovu walikasirika sana na wakawa katili hata zaidi: Waligeukia mateso ili kutoa ili kunifanya nikiri. Walinitia pingu kwa kiti cha chuma kilichokazwa kwa skrubu sakafuni kwa njia ambayo singechuchumaa wala kusimama. Mmoja wao aliweka mkono wangu ambao hukuwa umetiwa pingu kwa kiti na kuupiga kwa kiatu, akikomesha tu wakati upande wa nyuma wa mkono wangu ulikuwa umegeuka rangi kuwa mweusi na samawati: mwingine aliponda vidole vyangu vya miguu chini ya kiatu chake cha ngozi. Ni hapo tu ndipo nilipitia kwamba uchungu katika vidole huenda moja kwa moja hadi moyoni. Baada ya hapo, polisi wasita ama saba walichukua zamu kwangu. Mmoja wao alilenga viungo vyangu, na kuvichuna kwa nguvu sana kiasi kwamba mwezi mmoja baadaye bado singeweza kuupinda mkono wangu. Mwingine alinyakua nywele zangu na kutingisha kichwa changu upande mmoja kuelekea upande mwingine, kisha akakivuta kwa ghafla nyuma ili nilikuwa nikiangalia juu. “Tazama anga na kuona iwapo kuna Mungu!” alisema kwa ukali. Waliendelea hadi usiku. Wakiona kwamba hawangepata chochote kutoka kwangu, na kwa sababu ilikuwa Mwaka Mpya wa Kichina, walinituma moja kwa moja hadi katika kituo cha kuzuia.
Nilipowasili katika kituo cha kuzuia, mlinzi alimwamuru mfungwa wa kike kunivua nguo zote na kuzirusha katika pipa la takataka. Kisha walinifanya nivae sare chafu ya gereza, iliyokuwa ikinuka vibaya. Walinzi waliniweka katika seli na kisha wakawadanganya wafungwa wengine, wakisema: “Yeye hasa alivunja familia za watu. Familia nyingi zimeharibiwa na yeye. Yeye ni mwongo, huwadanganya watu waaminifu, na kuvuruga utulivu wa umma….” “Mbona anafanana na punguani?” mmoja wa wafungwa aliuliza. Kwa hilo walinzi walijibu: “Anajifanya kuepuka kuhukumiwa. Ni nani kati yenu aliye mwerevu hivyo? Yeyote anayefikiri yeye ni mpumbavu ni mjinga kabisa kwa wote.” Hivyo wakiwa wamedanganywa na walinzi hao, wafungwa wengine wote walisema nilikuwa nikisamehewa kwa urahisi sana, na kwamba kitu kizuri pekee kwa mtu ambaye ni mbaya kama mimi kilikuwa kikosi cha wauaji! Kusikia hili kulinikasirisha—lakini hakukuwa na chochote ambacho ningeweza kufanya. Majaribio yangu ya upinzani yalikuwa bure, yalileta tu mateso na ukatili zaidi. Katika kituo cha kuzuia, walinzi waliwafanya wafungwa kukariri amri kila siku: “Kiri uhalifu wako na kutii sheria. Kuwashawishi wengine kutenda uhalifu hakukubaliwi. Kuunda magenge hakukubaliwi. Kupigana hakukubaliwi. Kuwadhulumu wengine hakukubaliwi. Kutoa mashtaka yasiyo kweli dhidi ya wengine hakukubaliwi. Kunyakua chakula ama mali ya wengine hakukubaliwi. Kufanya hila kwa wengine hakukubaliwi. Wadhalimu wa gerezani wanapaswa kuchukuliwa hatua kali. Ukiukaji wowote wa sheria unapaswa kuripotiwa kwa wasimamizi ama polisi wenye madaraka mara moja. Unapaswa kutoficha ukweli ama kujaribu kulinda wale wafungwa ambao wamekiuka sheria na kufuatia kunapaswa kuwa kwa kwenye huruma. …” Kwa kweli, walinzi waliwatia moyo wafungwa wengine kunitesa, wakiwaruhusu kunitendea hila kila siku: Wakati ambapo halijoto ilikuwa digrii 8 ama 9 chini ya sufuri, walilowa viatu vyangu: kwa siri walimwaga maji kwenye chakula changu: jioni, nilipokuwa nikilala, walirowesha jaketi langu lililojazwa pamba: walinifanya nilale kando ya choo, mara kwa mara walivuta mfarishi wangu usiku, walivuta nywele zangu, ili kunizuia kulala; walininyang’anya andazi langu lilikopikwa kwa mvuke, walinilazimisha kusafisha choo, na kuingiza kwa nguvu dawa zao zilizosalia ndani ya mdomo wangu, hawakuniacha nikojoe…. Wakati sikufanya walichosema, wangechangia na kunipiga—na mara nyingi wakati kama huu wasimamizi ama polisi walio na mamlaka wangetoroka wasionekane ama kujifanya hawajaona chochote; wakati mwingine wangejificha mbali na kutazama. Iwapo wafungwa wangekaa siku chache bila kunitesa, wasimamizi na polisi wenye mamlaka wangewauliza: “Yule mwanamke mjinga ameerevuka siku hizi chache, siyo? Wakati huo, ninyi mmekuwa wajinga. Yeyote atakayembadilisha huyo mwanamke mjinga atapata msamaha.” Mateso ya kikatili ya hao walinzi yalinijaza na chuki kwao. Leo, iwapo singeona hili na macho yangu mwenyewe na kulipitia mimi binafsi, kamwe singeamini kwamba serikali ya CCP, ambayo inapaswa kuwa imejaa ukarimu na maadili, ingeweza kuwa ovu, ya kuogofya na mbaya—singewahi kuona sura yake ya kweli, sura ambayo ni danganyifu na yenye unafiki. Mazungumzo yake yote ya “kuhudumia watu, kutengeneza jamii iliyostaarabika na ya upatanifu”—huu ni uongo ulioundwa kuwadanganya na kuwahadaa watu, ilikuwa njia, hila, ya kujipendekeza na kupata heshima haifai kupata. Wakati huo, nilifikiri kuhusu maneno ya Mungu: “Haishangazi, basi, kwamba Mungu mwenye mwili abaki kuendelea kuwa Amefichwa: Katika jamii ya giza kama hii, ambapo mashetani hawana huruma na ni katili, inawezekanaje mfalme wa mashetani anayeua watu kwa kufumba na kufumbua, avumilie uwepo wa Mungu ambaye ni mwenye upendo, mpole, na mtakatifu? Anawezaje kushangilia na kufurahia ujio wa Mungu? Vikaragosi hawa! Wanalipa upole kwa chuki, wanamtweza Mungu kwa muda mrefu, wanamtukana Mungu, ni washenzi kupita kiasi, hawamjali Mungu hata kidogo, wanapora na kuteka nyara, wamepoteza dhamiri yote, na hawana hata chembe ya wema, na wanawajaribu watu wasiokuwa na hatia kuwa watu wasiokuwa na uwezo wa kuhisi. Wazazi wa kale? Viongozi Wapendwa? Wote wanampinga Mungu! Udukuzi wao umeacha wote walio chini ya mbingu katika hali ya giza na machafuko! Uhuru wa dini? Haki halali na matakwa ya wananchi? Zote hizo ni njama za kufunika dhambi!” (Kutoka kwa “Kazi na Kuingia (8)” katika Neno Laonekana katika Mwili). Nikilinganisha maneno ya CCP na uhalisi, niliona asili ovu na mbaya ya serikali ya CCP ya shetani kwa ubayana kamili. Kudumisha mamlaka yake ovu, inaweka mshiko uliobanwa kwa watu wake, na kufanya kila kitu kuwalaghai na kuwadanganya. Kwa juu juu, inadai kutoa uhuru wa dini—lakini kwa siri, inawakamata, kuwakandamiza, kuwatesa, na kuwaua watu kutoka kila pande zote za nchi ambao wanamwamini Mungu. Hata inajaribu kuwaua wote. Jinsi gani ibilisi alivyo mjanja, katili, na asiyependa maendeleo! Uhuru uko wapi? Haki za binadamu ziko wapi? Je, si zote ni hila za kutumia kuwadanganya watu? Je, watu wanaweza kuona mara moja matumaini ama mwanga wowote wakiishi chini ya utawala wake muovu? Wanawezaje kuwa huru kumwamini Mungu na kufuatilia ukweli? Hapo tu ndipo nilitambua kwamba Mungu alikuwa ameruhusu mateso na majaribu haya kunifikia, kwamba Alikuwa ameitumia kunionyesha ubaya na ukatili wa serikali ya CCP, ili kunionyesha asili yake ya shetani ambayo ina uadui na ukweli na ya uhasama kwa Mungu, na kunionyesha kwamba polisi wa watu, ambao serikali kwa nguvu huwajenga na kuwatangaza kama wanaoadhibu uovu, kutetea wema, na kukuza haki, ni washirika na watumishi imelea kwa uangalifu, kundi la wauaji ambao wana sura za wanaume lakini mioyo ya wanyama, na ambao wangeua kufumba kufumbua. Ili kujaribu kupiga marufuku na kukomesha kazi ya Mungu, na kunilazimisha kukataa na kumsaliti Mungu na kukubali nguvu yake ya dikteta, serikali ya CCP ilifanya kila kitu kunitesa na kuniangamiza—ilhali haikujua hata kidogo kwamba kadiri ilivyonitesa, ndivyo niliona sura yake ya ibilisi kwa wazi kabisa, na ndivyo nilivyoidharau na kuikataa zaidi kutoka kwa vina vya moyo wangu, kunifanya kumtamani sana Mungu kwa kweli na kumwamini Mungu. Hata zaidi, ilikuwa hasa kwa sababu ya mateso ya walinzi ndipo bila kutambua nilikuja kuelewa kinachomaanisha kweli kupenda anachopenda Mungu na kuchukia anachochukia Mungu, kinachomaanisha kumkwepa Shetani na kugeuza moyo wa mtu kwa Mungu, kinachomaanisha kuwa katili, nguvu za giza ni nini, na zaidi ya hayo, kinachomaanisha kuwa mbaya sana na mwenye kudhuru kwa siri, na mwongo na mdanganyifu. Nilimshukuru Mungu kwa kuniruhusu nipitie hali hii, kwa kuniruhusu kujua sahihi kutoka kwa isiyo sahihi na kuona njia sahihi ya maisha ambayo napaswa kuchukua. Moyo wangu—ambao ulikuwa umedanganywa na Shetani kwa muda mrefu sana—hatimaye uliamshwa na upendo wa Mungu. Nilihisi kwamba kulikuwa na maana kuu katika mimi kuwa na bahati ya kupitia jaribio na majaribu haya, kwamba kwa kweli nilikuwa nimeonyeshwa fadhili maalum.
Baada ya kujaribu kila kitu kingine, polisi waovu waliunda mpango mwingine: Walimpata mchungaji kutoka kwa kanisa la Nafsi Tatu ambaye alinijua kunifichua. Alisema nilimwamini Mwenyezi Mungu na wakati mmoja nilijaribu kueneza injili kwake—lakini alikuwa amekataa. Na pia alijaribu kunifanya nimkwepe Mungu. Kwa kuona huyu mtumishi mwovu ambaye alikuwa amewaripoti ndugu wengi ambao walieneza injili, na kwa kusikia maneno yote mabaya yaliyotoka mdomoni mwake—maneno yaliyosingizia, kukashifu, na kukufuru dhidi ya Mungu—moyo wangu ulijawa na ghadhabu. Nilitaka kumpigia kelele, kuuliza mbona alikuwa na uhasama kwa Mungu mno. Kwa nini iwe kwamba alifurahia sana neema ya Mungu, ilhali alikuwa ameshirikiana na ibilisi waovu kuwatesa wateule wa Mungu? Katika moyo wangu, kulikuwa na huzuni na uchungu usioelezeka. Nilihisi pia hisia kubwa ya huzuni na mwenye deni; kwa kweli nilijichukia kwa jinsi, zamani, sikuwa nimejaribu kufuatilia ukweli, na sikuwahi kujua lolote isipokuwa furaha ya neema na baraka za Mungu kama mtoto mjinga, nisitilie maanani uchungu na fedheha ambayo Mungu alikuwa amestahimili kwa ajili ya wokovu wetu. Ni sasa tu, nilipokuwa ndani sana ya pango la ibilisi, ndipo nilihisi jinsi ilivyokuwa vigumu kwa Mungu kufanya kazi katika nchi hii chafu, potovu, na jinsi uchungu Aliokuwa amepitia ulivyokuwa mkubwa! Kwa kweli, upendo wa Mungu kwa mwanadamu hubeba uchungu mkubwa. Anafanya kazi ya kumwokoa mwanadamu huku Akivumilia usaliti wa mwanadamu. Usaliti wa mwanadamu umemletea Yeye uchungu na maumivu pekee. Si ajabu Mungu alisema wakati mmoja: “Hata kama ni kwa muda wa usiku mmoja tu, wao watatoka katika hali ya tabasamu, watu wenye “mioyo mikunjufu” hadi wenye sura mbovu na wauaji wakatili, ghafla wakiwatendea wafadhili wao wa jana kana kwamba ni adui wa milele, bila chanzo wala sababu” (Kutoka kwa “Kazi ya Mungu na Utendaji wa Mwanadamu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Leo, ingawa nilikuwa nimetumbukia katika mishiko ya ibilisi, singemsaliti Mungu bila kujali chochote. Bila kujali taabu kubwa niliyopitia, singekuwa Yuda kwa ajili ya kujiokoa. Singemsababishia Mungu uchungu na huzuni. Kwa ajili ya mimi kusalitiwa na huyu mchungaji kutoka kwa jamii ya dini, polisi waovu waliongeza mateso yao. Yeye, wakati huo, alisimama upande mmoja na kusema: “Hujui kutofautisha mazuri kutoka kwa mabaya. Unastahili hili! Huthamini ukarimu wangu. Unastahili kuteswa hadi kufa!” Kusikia maneno haya mabaya, maovu kulinikasirisha—lakini pia nilihisi hisia isiyoelezeka ya huzuni. Nilitaka kulia, lakini nilijua haikunipasa kufanya hivyo. Moyoni mwangu, niliomba kwa siri: Ee Mungu! Ningependa upate moyo wangu. Ingawa siwezi kukufanyia lolote wakati huu, nataka kukutolea ushuhuda wa ushindi mbele ya Shetani na mtu huyu mwovu, kuwaaibisha kabisa, na kupitia hili kuleta faraja kwa moyo Wako. Ee Mungu! Ningependa ulinde moyo Wangu, na kunifanya kuwa mwenye nguvu zaidi. Iwapo nina machozi, naomba yatiririke kwa ndani—siwezi kuwaruhusu waone machozi yangu. Napaswa kuwa na furaha kwa sababu naelewa ukweli, kwani umeng’arisha macho yangu, Ukinipa uwezo wa kutofautisha, na kuona kwa dhahiri asili na kiini cha Shetani, ambacho ni kukupinga, kukusaliti, na kuvunja kazi Yako. Katikati ya usafishaji, nimeona pia jinsi mkono Wako wenye hekima hupanga yote. Nataka kuendelea kushirikiana na Wewe, hadi ushindi uwe Wako. Baada ya kuomba, moyoni mwangu kulikuwa na nguvu ya kutopumzika hadi nilipomaliza ushuhuda wangu kwa Mungu. Nilijua kwamba hili lilikuwa limepewa kwangu na Mungu, kwamba Mungu alikuwa amenipa ulinzi mkubwa na kunisisimua sana. Polisi waovu walitaka kutumia mtu mwovu kunifanya kumsaliti Mungu, lakini Mungu ni Mungu mwenye hekima, na Alitumia mtu huyo mwovu kama mfano unaopinga kunionyesha asili ya uasi ya wanadamu wapotovu, Akichangamsha azimio na imani yangu kumridhisha Mungu. Hata zaidi, nilikuwa na ufahamu fulani wa kazi ya hekima ya Mungu, niliona kwamba Mungu hutawala na kushawishi yote yaliyo katika huduma kukamilisha watu wa Mungu. Huu ni ukweli dhabiti wa utumizi wa Mungu wa hekima kumshinda Shetani.
Kwa kuona kuwa hawangeniruhusu kusema chochote nilichotaka, walitumia kila gharama—iwe ikama, ama vifaa na rasilmali za fedha—kufanya juu chini kuuliza dhibitisho kwamba nilikuwa muumini wa Mungu. Baada ya miezi mitatu, kuharakisha kote kwao huku na kule hakukuwa kumezaa matunda. Mwishowe, walijaribu kupiku: Walimpata mhojaji stadi. Ilisemekana kwamba kila mtu aliyeletwa kwake alipitia aina zake tatu za mateso, na hakuna mbaye hakuwahi kukiri. Siku moja, maafisa wanne wa polisi walikuja na kuniambia: “Leo, tunakupeleka nyumbani mpya.” Kisha, walinisukuma kwa gari la kusafirisha wafungwa, kufunga pingu mikono yangu nyuma ya mgongo wangu, na kuweka kifuniko kichwani mwangu. Hali ilinifanya nifikiri walikuwa wakinipeleka kuniua kwa siri. Moyoni mwangu, sikuweza kujizuia kuwa na hofu. Lakini baadaye, nilifikiri kuhusu wimbo ambao nilikuwa nikiimba nilipomwamini Yesu: “Tangu nyakati za awali kabisa za kanisa, wale ambao humfuata Bwana wamelazimika kulipa gharama ya juu. Makumi ya maelfu ya jamaa wa kiroho wamejitoa kwa injili, na hivyo wamepata uzima wa milele. Kifo cha kishahidi kwa ajili ya Bwana, niko tayari kufa shahidi kwa ajili ya Bwana.” Siku hiyo, hatimaye nilielewa wimbo huo: Wale wanaomfuata Bwana lazima walipe gharama ya juu. Mimi pia nilikuwa tayari kufa kwa ajili ya Mungu. Kustaajabika, baada ya kuingia kwa gari, bila kuwa mwangalifu nilisikia bila kusudia mazungumzo baina ya polisi waovu. Ilionekana walikuwa wakinipeleka mahali pengine kuhojiwa. Aa! Hawakuwa wakinipeleka kuuawa—na nilikuwa nimejitayarisha kufa shahidi kwa ajili ya Mungu! Nilipokuwa tu nikifikiria hili, kwa sababu fulani zisizojulikana mmoja wa polisi alikaza kamba za ukaya kichwani mwangu. Punde baadaye, nilianza kuhisi kutotulia–ilihisi kana kwamba nilikuwa nikisongwa. Nilijipata nikijiuliza iwapo kwa kweli wangenitesa hadi nife. Wakati huo, nilifikiri kuhusu jinsi wanafunzi wa Yesu walikuwa wamejitoa kueneza injili. Singekuwa mwoga. Hata iwapo ningekufa, singewasihi wailegeze, hata zaidi singekubali kushindwa. Lakini sikuweza kujidhibiti: Nilizirai na kuwaangukia. Huku wakiona kilichokuwa kikitendeka, polisi kwa haraka walilegeza kifuniko. Nilianza kutoa povu mdomoni, kisha sikuweza kuacha kutapika. Ilihisi kana kwamba ningetapika mpaka matumbo yangu yatoke nje. Nilihisi kizunguzungu, kichwa changu kilikuwa kitupu, na singeweza kufungua macho yangu. Sikuwa na nguvu popote mwilini mwangu kana kwamba nilikuwa nimepooza. Ilihisi kana kwamba kulikuwa na kitu cha kunata mdomoni mwangu ambacho singeweza kutoa. Daima nilikuwa dhaifu, na baada ya kuteswa namna hii nilihisi kwamba nilikuwa taabani, kwamba ningeacha kupumua wakati wowote. Katikati ya uchungu, nilimwomba Mungu: “Ee Mungu! Iwapo Unataka nishuhudie kifo Kwako, kwa furaha nakutii, na kwa furaha kutumia kifo kukuridhisha. Najua kwamba wale wanaokufa kwa jina la Mungu hawakufi, ila wanalala. Naamini kwamba chochote Unachofanya, ni cha haki, na ningependa kwamba Uulinde moyo wangu, ili kwamba niweze kustahi yote ambayo Unapanga na kuweka kwa utaratibu.” Wakati mwingine baadaye, gari liliwasili kwa hoteli fulani. Wakati huo, mwili wangu wote ulihisi mnyonge na singeweza kufungua macho yangu. Walinibeba hadi kwa chumba kilichofungwa kabisa. Yote ambayo ningesikia ilikuwa sauti ya watumishi wengi wa serikali ya CCP waliokuwa wamesimama wakinizingira wakinijadili, wakisema kwamba kuniona kulikuwa kama kuona jinsi Liu Hulan alivyokuwa. Ilikuwa kitu kilichozindua, cha kuvutia sana! Yeye hata ni sugu kuliko jinsi Liu Hulan alivyokuwa! Kwa kusikia hili, moyo wangu ulifura kwa msisimko. Niliona kwamba Mwenyezi Mungu alilazimika kuwa mshindi, kwamba Shetani alikuwa chini ya miguu ya Mungu! Nilimshukuru na kumsifu Mungu kwa kunipa imani na utiifu. Wakati huu, nilisahau uchungu. Nilihisi kufurahishwa pakubwa mno kutukuzwa na Mungu.
Punde baadaye, “mtaalamu wa mahojiano” ambaye polisi walimzungumzia aliwasili. Punde alipoingia, alipaza sauti: “Yuko wapi huyo mwanamke mjinga? Acha nimwone!” Alitembea mbele yangu na kunishika kwa nguvu. Bada ya kunizaba makofi mara kadhaa usoni, alinipiga ngumi za nguvu mara kadhaa kifuani na mgongoni, kisha akaondoa kiatu chake moja cha ngozi na kunipiga usoni nacho. Baada ya kuchapwa naye hivi, nilipoteza hisia kwamba kulikuwa na kitu ambacho singeondoa mdomoni ama tumboni mwangu. Kuchanganyikiwa kuliacha kichwa changu na ningeweza kufungua macho yangu. Hisia polepole ilirudi katika viungo vyangu, na nguvu ilianza kurudi mwilini mwangu. Kisha, kwa ukali alinyakua mabega yangu na kunisukuma nyuma dhidi ya ukuta, akiniamuru nimwangalie na kujibu maswali yake. Kuona kwamba sikuwa namzingatia hata kidogo kulimfanya akasirike sana, na alijaribu kupata mjibizo kutoka kwangu kupitia kutukana, kukashifu na kumkufuru Mungu. Alitumia mbinu duni, za kustahili dharau kabisa kuniambika, na kusema kwa kuogofya: “Kwa makusudi nakutesa kwa kutumia kile kisichovumilika na mwili na nafsi yako, ili kukufanya upitie uchungu ambao hakuna mtu wa kawaida angeweza kupitia—utatamani heri ufe. Mwishowe, utaniomba nikuache uende na hapo ndipo utazungumza maana, na kusema kwamba majaliwa yako hayako mikononi mwa Mungu—yako mikononi mwangu. Nikitaka ufe, itafanyika mara moja; nikitaka uishi, utaishi; na taabu yoyote nyingine ninayotaka upitie, hiyo ndiyo utapitia. Mwenyezi Mungu wako hawezi kukuokoa—utaishi tu ukituomba tukuokoe.” Nikiwa nimekabiliwa na hawa wauaji, wanyama mwitu, ibilisi waovu wenye kustahili dharau, wasio na aibu na walio duni, nilitaka sana kupigana nao. Wakati huo nilifikiri kuhusu wimbo wa uzoefu wa maisha: “Mbingu na dunia na kila kitu ndani yavyo viliumbwa na Mungu, na ni asili na haki kwa Mungu kuvifurahia. Mfalme wa ibilisi huvimiliki bila aibu; Shetani ana hatia ya uhalifu mbaya sana kabisa; makumi ya maelfu ya jamaa wa kiroho lazima waibuke” (“Kukimbia Kuelekea kwenye Njia Ng’avu” katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Nilikuwa nimefanya nini kuibuka? Kwa kutosema hata chochote kuwakanusha, kuwaacha tu wanitese kwa njia yoyote ambayo walitaka—katika hili, je, nilikuwa mnyonge sana? Moyo wangu ulijawa na ghadhabu. Nilihisi kana kwamba singeweza kuidhibiti, nilitaka kupiga yowe, kurudisha pigo, kuwatangazia: “Mwanadamu kamwe hawezi kuomba huruma kutoka kwa mbwa!” Niliamini kwamba hii ilikuwa hisia ya haki—lakini kwa mshangao wangu, kadiri nilivyofikiri zaidi kwa njia hii, ndivyo nilikuwa mwenye giza zaidi ndani. Nilijipata bila maneno ya maombi, nisiweze kufikiri nyimbo zozote. Mawazo yangu yalianza kukanganyikiwa, na sikujua cha kufanya, na wakati huo nilianza kuhisi mwenye woga kiasi. Kwa haraka nilijituliza mbele ya Mungu. Nilifikiri kujihusu, na kujaribu kujijua, na wakati huo maneno ya Mungu ya hukumu yalinijia: “Unachopendezwa nacho sio kujishusha kwa Kristo…. Haupendi wosia au kependeza kwa Kristo …” (Kutoka kwa “Je, Wewe ni Muumini wa Kweli wa Mungu?” katika Neno Laonekana katika Mwili). “Je, kufuata tamaa zako mwenyewe kunafichua mlingano Wangu? Je, hilo litaridhisha moyo Wangu? Je, wewe ni mtu ambaye kwa uaminifu amefuata dhamira Zangu? Je, wewe ni mtu ambaye kwa kweli amejaribu kuelewa moyo Wangu? Je, kwa hakika umejitoa Kwangu? Je, kwa kweli umejitumia kwa ajili Yangu. Je, umeyatafakari maneno Yangu?” (Matamshi na Ushuhuda wa Kristo Mwanzoni). Kila neno la hukumu ya Mungu liliudunga moyo wangu. Ndiyo—nilikuwa nimemwona Kristo kama mdogo sana, nilikuwa nimependa nguvu na uwezo, sio unyenyekevu wa Kristo, hata zaidi nilikuwa nimetamani hekima ya kazi fiche ya Mungu. Mungu hutumia hekima Yake kumshinda Shetani, Yeye hutumia unyenyekevu na ufiche Wake kufichua sura ya kweli ya Shetani, na kukusanya ushahidi kuwaadhibu waovu. Mimi, wakati huo, nilitegemea falsafa za kishetani kuheshimu kazi ya Kristo, daima nikijaribu kulipiza kisasi kuamini kwamba kuwa mzuri ni kudanganywa, kwamba watu wote huweka mizigo juu ya farasi aliye radhi. Mbona, wakati ambapo tunateswa, tunapaswa kuwaacha polisi waovu wafanye watakavyo? Je, ni bahati nasibu ya wale wanaomwamini Mungu kudhulumiwa, kandamizwa, na kutiwa uchungu? Kama matokeo ya asili yangu ya kiburi, sikuwa tayari kustahimili fedheha, sembuse dhuluma na ukandamizaji. Hili lilikuwa limenifanya niidharau kazi ya hekima ya Kristo na kutothamini unyenyekevu na ufiche wa Kristo. Badala yake, niliamini kwamba hisia ya haki, nguvu ya sifa, na heshima ilikuwa katika kupigana nao. Sikujua kabisa kwamba Shetani alitaka kunichochea ili nipigane dhidi yao, kunilazimisha kukiri ukweli wa imani yangu kwa Mungu ili kunitia hatiani. Iwapo kweli ningepigana nao na ujasiri wa msukumo, singeshikwa na njama zao danganyifu? Kwa kweli nilimshukuru Mungu kwa ajili ya kuadibu na hukumu Yake kwangu kwa wakati ufaao, ambayo ilinipa ulinzi katikati ya uasi wangu, ili kwamba nilibaini njama danganyifu za Shetani, na kutambua sumu za Shetani ndani yangu, na kupata maarifa kiasi ya kile alicho Mungu na asili ya uhai wa Mungu iliyo nyenyekevu na fiche. Nilifikiri juu ya jinsi Kristo alikabiliwa na kuteswa, kuwindwa, na kuuwawa na ibilisi CCP, na jinsi wanadamu wote walimhukumu, na kumshutumu, na kumkashifu, na kumwacha. Wakati huo wote, Alivumilia haya yote kwa ukimya, Akistahimili uchungu huu wote kutekeleza kazi Yake ya wokovu, kamwe kutopigana, na kamwe kutolalamika. Niliona jinsi tu tabia ya Mungu ilivyo karimu, na nzuri na ya heshima! Wakati huo, mimi—mtu mchafu, mpotovu—nilikuwa nimetaka kupigana nilipoteswa na ibilisi waovu, nilikuwa nimetaka kutumia ujasiri wangu wa msukumo kutetea heshima yangu ya kudhaniwa, kupigana kwa ajili ya haki yangu mwenyewe kulingana na mapenzi yangu mwenyewe. Hisia ya haki ilikuwa wapi ndani ya hili? Na nguvu ya sifa na heshima ilikuwa wapi? Katika hili, sikuwa nikionyesha sura yangu mbaya ya shetani? Sikuwa nikifichua asili yangu ya kiburi? Je, kulikuwa na ukweli wowote katika hili? Nikifikiri hili, moyo wangu ulijawa na huzuni. Niliamua kumwiga Kristo. Nilikuwa tayari kuvumilia hali hii na kujaribu kadri nilivyoweza kushirikiana na Mungu, nisimwachie Shetani fursa yoyote.
Moyo wangu ulianza kuwa mtulivu, na kwa kimya nilisubiri zamu iliyofuata ya mapambano haya na ibilisi. Kukataa kwangu kukiri kulikuwa kumemwaibisha sana huyo aliyedhaniwa mtaalamu. Kwa hasira alipinda mkono wangu mmoja nyuma ya mgongo wangu na kuvuta huo mwingine nyuma ya mabega yangu, kisha alitia pingu mikono yangu na kuibana pamoja. Baada ya chini ya nusu saa, matone makubwa ya jasho yalikuwa yakitiririka usoni pangu, yakinizuia kuweza kufungua macho yangu. Huku akiona kwamba bado singejibu maswali yake, alinirusha sakafuni, kisha aliniinua kwa pingu nyuma ya mgongo wangu. Mikono yangu mara moja ilihisi uchungu mwingi, kana kwamba ilikuwa imevunjwa. Ilitia uchungu sana kiasi kwamba nilipumua kwa shida. Kisha, alinirusha dhidi ya ukuta na kunifanya nisimame dhidi yake. Jasho ilikuwa ikitia waa macho yangu. Nilihisi uchungu sana kiasi kwamba mwili wangu wote ulijawa na jasho—hata viatu vyangu vililowa. Daima nilikuwa dhaifu, na wakati huu nilianguka. Yote ambayo ningefanya tu ilikuwa kuhema kupitia mdomo wangu. Ibilisi alisimama kwa upande mmoja akinitazama. Sikujua alichoona—pengine aliogopa angelaumiwa iwapo ningekufa—kwa haraka alichukua kiasi kidogo cha karatasi ya shashi na kupanguza jasho yangu, kisha akaninywesha kikombe cha maji. Alifanya hivi kila wakati chini ya nusu saa ilikuwa imepita. Sijui nilifanana vipi wakati huo. Nadhani lazima ilikuwa inaogofya sana, kwa sababu ningehema tu mdomo wangu ukiwa wazi: ilionekana nilikuwa nimepoteza uwezo wangu kupumua kupitia pua langu. Midomo yangu ilikuwa imekauka na kufanya upenyu na ilichukua nguvu yote niliyokuwa nayo kupumua tu. Nilihisi kifo kikikaribia tena—pengine wakati huu kwa kweli ningekufa. Lakini wakati huo, Roho Mtakatifu alinitia nuru. Nilimfikiria Luka, mmoja wa wanafunzi wa Mungu, na uzoefu wake wa kuangikwa akiwa hai. Moyoni mwangu, nilipata tena nguvu yangu kwa hiari, na kuendelea kusema kitu kile kile tena na tena kujikumbusha: “Luka alikufa kwa kuangikwa akiwa hai. Mimi, pia, lazima niwe Luka, lazima niwe Luka, niwe Luka … Mungu atawasafisha watu kabisa; lakini mimi ni mnyonge sana, siwezi kushuhudia kabisa—na sasa niko karibu kufa. Hata nikifa kweli, kwa hiari ninatii utaratibu na mipango ya Mungu, nataka kuwa mwaminifu kwa Mungu hadi kufa kama Luka.” Wakati ule ule maumivu yalipokuwa hayawezi kuvumilika na nilikuwa ukingoni mwa kifo, ghafla nilisikia polisi mmoja mwovu kisema kwamba ndugu kadhaa waliomwamini Mwenyezi Mungu walikuwa wamekamatwa. Moyoni mwangu, nilishtuka: Ndugu wengine kadhaa watateswa. Lazima watakuwa wagumu hasa kwa kaka. Moyo wangu ulijawa na wasiwasi. Niliendelea kuwaombea kwa ukimya, nikimwomba Mungu awalinde na kuwaruhusu wawe na ushuhuda wa ushindi mbele ya Shetani na kutowahi kumsaliti Mungu, kwani sikutaka ndugu wowote wengine kuteseka kama nilivyoteseka. Pengine niliguswa na Roho Mtakatifu; niliomba bila kukoma, na kadiri nilivyoomba zaidi ndivyo nilivyotiwa moyo zaidi. Nilisahau uchungu wangu bila kufahamu. Nilijua vizuri sana kwamba hii ilikuwa mipango ya hekima ya Mungu; Mungu alijali udhaifu wangu, na alikuwa akiniongoza kupitia wakati wangu wa uchungu zaidi. Usiku huo, sikujali tena jinsi polisi waovu walivyonitendea, na sikutia maanani hata kidogo maswali yao. Huku wakiona kilichokuwa kikitendeka, polisi waovu walitumia ngumi zao kuupiga uso wangu kwa ukatili, kisha wakapinda nywele kwa panja langu vidoleni vyao na kuzivuta kwa ghafla. Masikio yangu yalikuwa yamevimba kwa ajili ya kupindwa, uso wangu ulikuwa usiotambulika, pande za juu na chini za miguu yangu zilikuwa zimeachwa na majeraha, na kuchunuka waliponichapa na kipande kinene cha mbao, na vidole vyangu vya miguu, pia, vilikuwa vimeachwa vyeusi na samawati baada ya kupondwa na kipande cha mbao. Baada ya kuniangika juu kwa pingu kwa saa sita, wakati polisi waovu walifungua pingu, zilikuwa zimeondoa nyama kutoka kwa kidole changu gumba cha kushoto—kulisalia tu safu nyembamba kabla ya mfupa. Pingu pia zilikuwa zimeacha vifundo vyangu vikiwa vimefunikwa na lengelenge ya njano, na hakukuwa na njia ya kuirudisha. Wakati huo, polisi wa kike aliyeonekana mwenye madaraka makubwa aliingia. Alinitazama juu na chini, kisha akawaambia: “Hamwezi kumchapa huyu tena—yuko karibu kufa.”
Polisi walinifungia katika chumba kimoja hotelini. Mapazia yake yalikuwa yamefungwa kwa kubanwa usiku kucha na mchana kutwa. Mtu fulani alipewa jukumu la kulinda mlango, na hakuna kati ya watumishi wa huduma aliyeruhusiwa kuingia, wala hakuna aliyeruhusiwa kuona matukio ya wao kunitesa na kunishambulia kikatili kule ndani. Walichukua zamu kunihoji bila pumziko. Kwa siku na usiku tano, hawakuniruhusu kulala, hawakuniruhusu kukaa wala kuchuchumaa, wala hawakuniruhusu kula chakula changu hadi kushiba. Niliruhusiwa tu kusimama nikiegemea dhidi ya ukuta. Siku moja, afisa mmoja alikuja kunihoji. Huku akiona kwamba nilikuwa nikimpuuza, alishikwa na hasira na kunipiga teke lililonirusha chini ya meza. Kisha, alinivuta kutoka hapo na kunipiga ngumi, akisababisha damu kububujika kutoka kwa kona ya mdomo wangu. Ili kuficha ukatili wake, kwa haraka alifunga mlango kuzuia yeyote kuingia. Kisha alirarua kiasi kidogo cha karatasi ya shashi na kupanguza damu yangu, akisafisha damu kutoka usoni pangu kwa maji na kusafisha damu kutoka kwenye sakafu. Niliacha damu kiasi kwa sweta yangu nyeupe kwa makusudi. Niliporudi katika kituo cha kuzuia, hata hivyo, polisi waovu waliwaambia wafungwa wengine kwamba damu kwenye mavazi yangu ilitokana na wakati nilipokuwa nikithibitishwa katika hospitali ya wagonjwa wa akili, na kusema kwamba hapo ndipo nilipokuwa siku kadhaa zilizopita. Majeraha na damu mwilini mwangu yalikuwa yamesababishwa na wagonjwa, wao, polisi, hawakuwa wamenigusa…. Ukweli huu katili ulinionyesha ukatili, ujanja wenye kudhuru kwa siri, na unyama wa “polisi wa watu,” na nilihisi kutojiweza na huzuni ya wale wanaoanguka mikononi mwao. Wakati huo huo, nilipata ufahamu wa kina wa haki, utakatifu, uchangamfu, na uzuri wa Mungu, na kuhisi kwamba kila kitu kinachotoka kwa Mungu ni upendo, ulinzi, nuru, ugavi, faraja, na msaada. Kila wakati uchungu wangu ulipofika kiwango mbaya kabisa, Mungu daima angeendelea kunitia nuru na kuniongoza, Akiongeza imani na nguvu yangu, Akiniruhusu kuiga roho ya watakatifu ambao walikuwa wamekufa shahidi kwa ajili ya Mungu kotekote katika enzi, kunipa ujasiri wa kutetea ukweli. Wakati ambapo ukatili wa polisi waovu uliniacha karibu na kifo, Mungu aliniruhusu kusikia habari ya kukamatwa kwa ndugu, kutumia hili kunisisimua zaidi kuwaombea, ili kwamba nilisahau uchungu wangu na bila kujua kushinda vikwazo vya kifo. Kwa sababu ya utumbuizo wa Shetani mwovu, mkatili, niliona kwamba Mungu pekee ndiye ukweli, njia, na uhai, na kwamba Mungu pekee ndiye ishara ya mamlaka ya juu, ya haki, na ishara ambayo haiwezi kushindwa ama kuingiliwa na uovu na nguvu yoyote ya uhasama. Mungu pekee ndiye hutawala vitu vyote, na hupanga kila kitu, na Yeye hutumia nguvu Yake kuu na hekima kuongoza kila hatua yangu katika kushinda mizinga ya umati wa ibilisi, katika kushinda udhaifu wa mwili na vikwazo vya kifo, kuniruhusu kwa kunata kuokoka katika pango hili ovu. Nilipokuwa nikifikiri kuhusu upendo na wokovu wa Mungu, nilihisi kutiwa moyo sana, na nikaamua kupigana na Shetani hadi mwisho kabisa. Hata ningedhoofika gerezani, ningesimama imara katika ushuhuda wangu na kumridhisha Mungu.
Siku moja, polisi wengi waovu ambao sikuwa nimewahi kuwaona awali walikuja kuniangalia na kujadili kesi yangu. Bila kutaka, nilisikia bila kusudia mtaalamu—akisema: “Kwa mahojiano yote ambayo nimefanya, sijawahi kuwa mgumu kwa mtu yeyote kama huyo mwanamke mjinga. Nilimfanya atundikwe kwa pingu kwa saa nane (kwa kweli ilikuwa saa sita, lakini alitaka kujionyesha, akiogopa kwamba wasimamizi wake wangesema alikuwa bure) na bado hakukiri.” Nilisikia sauti ya kike ikisema, “Mbona ulimchapa mwanamke huyo vibaya hivyo? Wewe ni mkatili.” Ilitukia kwamba miongoni mwa kila mtu ambaye alikuwa amekamatwa, nilikuwa nimeteseka zaidi. Mbona nilikuwa nimeteseka sana hivyo? Je, nilikuwa mpotovu kuliko watu wengine? Je, kile nilichopitia kilikuwa adhabu ya Mungu kwangu? Pengine kulikuwa na upotovu mwingi sana ndani yangu, na tayari nilikuwa nimefika kiwango cha adhabu? Nikifikiri hili, singeweza kuzuia machozi yangu. Nilijua kwamba lazima nisilie. Singeacha Shetani aone machozi yangu—kama angeona, angeamini kwamba nilikuwa nimeshindwa. Ilhali sikuweza kudhibiti hisia ya huzuni moyoni mwangu, na machozi yalitiririka kupita udhibiti wangu. Katikati ya kukata tamaa kwangu, ningemwita tu Mungu: “Ee Mungu! Wakati huu, nahisi kusikitika sana. Naendelea kutaka kulia. Tafadhali nilinde, nizuie dhidi ya kuinamisha kichwa changu mbele ya Shetani—siwezi ruhusu aone machozi yangu. Najua kwamba hali niliyomo si sahihi. Natoa madai Kwako, na kulalamika. Na najua kwamba bila kujali kile Ufanyacho, ni bora zaidi—lakini kimo changu ni kidogo sana, tabia yangu ya uasi ni kubwa sana, na sina uwezo wa kukubali ukweli huu kwa furaha, wala sijui kile ninachopaswa kufanya kutoka katika hali hii mbaya. Ningependa Uniongoze, na kuniruhusu kutii utaratibu na mipango Yako, na kutokufahamu visivyo tena ama kulalamika kuhusu Wewe.” Nilipokuwa nikiomba, fungu la maneno ya Mungu yalinijia akilini: “Lazima pia unywe kutoka kwenye kikombe kikali nilichonywea Mimi (hili ndilo alilomwambia baada ya kufufuka), lazima utembee njia niliyotembea Mimi, lazima uyapoteze maisha yako kwa ajili Yangu” (Kutoka kwa “Namna Petro Alivyopata Kumjua Yesu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Machozi yangu yalikoma mara moja. Mateso ya Kristo yalikuwa yasiyoweza kufananishwa na yale ya kiumbe yeyote aliyeumbwa, wala hayakuweza kuvumilika na kiumbe aliyeumbwa—ilhali nilikuwa hapa nikihisi nimekosewa na nikilalamika kwa Mungu kwamba haikuwa haki baada ya kupitia taabu kidogo. Dhamiri na mantiki ilikuwa wapi katika hili? Nilifaa vipi kuitwa binadamu? Baada ya hiyo, nilifikiri kuhusu kile Mungu alisema: “Hata hivyo, upotovu ndani ya asili ya binadamu ni lazima uondolewe kupit majaribu. Katika hali yoyote usiyoipita, ni katika hizi hali ambamo ni lazima usafishwe—huu ni mpango wa Mungu. Mungu anakutengenezea mazingira, Akikulazimisha usafishwe hapo ili ujue upotovu wako mwenyewe” (Kutoka kwa “Namna ya Kumridhisha Mungu katikati ya Majaribu” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo). Nikitafakari maneno ya Mungu na kufikiri kujihusu, nilielewa kwamba kile kilichopangwa na Mungu kililenga upotovu na upungufu wangu—na kilikuwa hasa kile ambacho maisha yangu yalihitaji. Kwa sababu nilikuwa nimepofishwa sana na kutiwa sumu na serikali ya CCP, moyo wangu daima ulikuwa umejaa imani na tegemeo mintaarafu yake, na hata ingawa nilikuwa nimeona makosa yake kiasi, hiyo haikuwa imebadili maoni yangu kuihusu. Leo, Mungu alikuwa ameunda hali hii maalum kwangu, Akiniruhusu kutofautisha kati ya Mungu na Shetani, kuweza kujua ni nani huniokoa na ni nani hunipotosha, nani ambaye napaswa kuabudu na nani ambaye napaswa kulaani, na ni kwa sababu ya hili tu ndipo niliona mwanga wa ukweli, na kumtazama Mungu wa kweli, na kuja kujua tofauti kati ya mwanga na giza. Iwapo singepitia taabu ambayo ilikuwa nyingi na kali ya kutosha, maarifa yangu na maoni ya serikali ya CCP hayangekuwa yamebadilika—wala, moyoni mwangu, singeutekeleza kwa kweli, na kwa kweli kumgeukia Mungu. Taabu hii ilikuwa upendo wa Mungu kwangu, ilikuwa baraka Yake maalum kwangu. Baada ya kuelewa mapenzi ya Mungu, moyo wangu mara moja ulihisi dhahiri na mchangamfu. Suitafahamu yangu ya Mungu ilitoweka. Nilihisi kulikuwa na thamani kubwa na maana katika mimi kuweza kupitia taabu hiyo siku!
Baada ya kujaribu kila kitu walichoweza, polisi waovu hawakuwa wamepata chochote kutoka kwangu. Mwishowe, walisema kwa kusadiki sana: “Wakomunisti wametengenezwa kwa chuma, lakini wale wanaomwamini Mwenyezi Mungu wametengenezwa kwa almasi—wako katika kiwango cha juu zaidi kuliko wakomunisti katika kila hali.” Baada ya kusikia maneno haya, moyoni mwangu singeweza kujizuia kufurahia na kumsifu Mungu: Ee Mungu, nakushukuru na kukusifu! Kwa uweza na hekima Yako Umemshinda Shetani na kushinda maadui Wako. Wewe ni mamlaka ya juu zaidi, na naomba utukufu uwe Wako! Ni wakati huu tu ndio niliona: Je, Chama cha Kikomunisti kina maana gani? Na je, utawala wote wa siasa duniani una maana gani? Vitu vyote mbinguni na duniani huja chini ya utawala wa Mungu. Lazima visiwe na chaguo lingine sembuse Shetani mdogo, asiye na maana ibilisi ambaye ni utumbuizo tu.
Siku moja, polisi waovu walikuja kunihoji mara nyingine tena. Wakati huu, wote walionekana kuwa wa ajabu kidogo. Waliniangalia walipozungumza, lakini haikuonekana kama walikuwa wakinizungumzia. Walionekana kujadili kitu. Kama nyakati za awali, mahojiano haya yaliishia katika kushindwa. Baadaye, polisi waovu walinirudisha kwa seli. Njiani, nilisikia ghafla wakisema kwamba ilionekana kuwa ningeachiliwa siku ya kwanza ya mwezi ujao. Kwa kusikia hili, moyo wangu karibu ulipasuka kwa msisimko: Hili inamaanisha nitaondoka katika siku tatu! Hatimaye naweza kuondoka katika jahanamu hii ya shetani! Kwa kukandamiza furaha iliyokuwa moyoni mwangu, nilitarajia na kusubiri kila sekunde ilipokuwa ikipita. Siku tatu zilihisi zaidi kama miaka mitatu. Mwishowe, siku ya kwanza ya mwezi iliwadia! Siku hiyo, niliendelea kukodolea mlango macho, nikisubiri mtu aite jina langu. Asubuhi ilipita, na hakuna kilichofanyika, niliweka matumaini yangu yote katika kuondoka alasiri—lakini jioni ilipofika, bado hakuna kilichofanyika. Wakati ambapo ilikuwa wakati wa chakula cha jioni, sikuhisi kula. Moyoni mwangu, nilikuwa na hisia ya hasara; wakati huo, ilikuwa kana kwamba moyo wangu ulikuwa umeanguka kutoka mbinguni hadi jahanamu. “Mbona hali?” mlinzi aliuliza wafungwa wengine. “Hajala sana tangu aliporudi kutoka kwa mahojiano siku ile,” mfungwa mmoja alijibu. “Gusa panja lake; je, yeye ni mgonjwa?” mlinzi alisema. Mfungwa alikuja na kugusa panja langu. Alisema lilikuwa na joto sana, kwamba nilikuwa na homa. Kwa kweli nilikuwa na homa. Ugonjwa huo ulikuwa umekuja ghafla sana, na ulikuwa mkali sana. Wakati huo, nilianguka. Kwa kipindi cha saa mbili, homa ikawa mbaya na mbaya zaidi. Nililia! Wote, akiwemo mlinzi, walinitazama nikilia. Wote waliduwaza: Maoni yao kunihusu yalikuwa kama mtu ambaye hakushawishika kwa kivutio wala kuogopeshwa kwa vitisho, ambaye hakuwahi kutoa chozi hata moja kila wakati alipokabiliwa na mateso ya kuhuzunisha, ambaye alikuwa ameangikwa juu kwa pingu kwa saa sita bila kupiga kite. Ilhali, leo, bila mateso yoyote, nililia. Hawakujua machozi yangu yalitoka wapi—walifikiri tu kwamba lazima niwe mgonjwa sana. Kwa kweli, mimi na Mungu tu ndio tulijua sababu. Haya yote yalikuwa kwa sababu ya uasi na kutotii kwangu. Machozi haya yalitiririka kwa sababu nilihisi kukata tamaa wakati ambapo matarajio yangu yaliambulia patupu na matumaini yangu yalikuwa yamevunjika. Yalikuwa machozi ya uasi na lalamiko. Wakati huo, sikutaka tena kuweka azimio langu kumshuhudia Mungu. Hata sikuwa na ujasiri kujaribiwa hivi tena. Jioni hiyo, nililia machozi ya taabu, kwa sababu nilikuwa nimechoshwa na maisha gerezani, niliwadharau pepo hawa—na hata zaidi ya hilo, nilichukia kuwa mahali hapa pa pepo. Sikutaka kukaa sekunde nyingine hapo. Kadiri nilivyofikiri kuhusu hilo, ndivyo nilivyovunjika moya zaidi, na ndivyo nilivyohisi hisia kubwa ya taabu, ya huzuni, na upweke zaidi. Nilihisi kana kwamba nilikuwa mashua pweke juu ya bahari, moja ambayo ingemezwa na maji wakati wowote; zaidi ya hayo, nilihisi wale walionizunguka walikuwa wenye kudhuru kwa siri sana na wabaya sana kiasi kwamba wangetoa hasira yao kwangu wakati wowote. Singeweza kujizuia kulia kwa sauti: “Ee Mungu! Nakuomba uniokoe. Niko karibu kuanguka, ninaweza kukusaliti wakati wowote na mahali popote. Ningependa uushike moyo wangu na uniwezeshe kurudi mbele Yako tena, ningependa Unihurumie mara moja nyingine, na kuniruhusu nikubali utaratibu na mipango Yako. Ingawa siwezi kuelewa kile Unachofanya sasa, najua kwamba yote Unayofanya ni mema, na ningetaka Uniokoe mara nyingine, na kuruhusu moyo wangu ukugeukie.” Baada ya kuomba, niliacha kuhisi kuogopa, nilianza kutulia na kufikiri kujihusu, na wakati huo maneno ya Mungu ya hukumu na ufunuo yalinijia: “Unataka mwili ama ukweli? Unataka hukumu, ama faraja? Baada ya kupitia na kuiona kazi nyingi ya Mungu, na baada ya kuuona utakatifu na haki ya Mungu, unafaa kumfuata vipi? Unapaswa kutembea vipi katika njia hii? Utahitajika kuweka mapenzi ya Mungu katika matendo kivipi? Je, adabu na hukumu ya Mungu zimekuwa na athari yoyote kwako? Kama una maarifa ya adabu na hukumu ya Mungu itategemea jinsi unavyoishi kwa kudhihirisha, na kiwango gani unapenda Mungu! Kinywa chako kinasema unampenda Mungu, ilhali unachoishi kwa kudhihirisha ni tabia nzee, zilizo potovu; humchi Mungu, na zaidi ya yote huna dhamiri. Je, watu wa aina hii wanampenda Mungu? Je, watu wa aina hii ni waaminifu kwa Mungu? … Mtu kama huyu anaweza kuwa Petro? Wale walio kama Petro wana maarifa, lakini je, wanaishi kulingana nayo?” (Kutoka kwa “Matukio Aliyopitia Petro: Ufahamu Wake wa Adabu na Hukumu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Kila neno la Mungu la hukumu lilikuwa kama upanga ukatao kuwili likiugonga udhaifu wangu, likirundika lawama juu yangu: Ndiyo, kulikuwa na nyakati nyingi ambapo nilitoa viapo vya dhati mbele ya Mungu, nikisema kwamba ningetelekeza kila kitu na kustahimili kila taabu kwa ajili ya ukweli. Ilhali leo, wakati ambapo Mungu alitumia ukweli kuniomba jambo, wakati Alinihitaji kwa kweli kuteseka na kulipa gharama ili kumridhisha, sikuwa nimechagua ukweli ama uzima, lakini kwa upofu nilikuwa nimejawa na wasiwasi, dhiki na masumbuko kwa sababu ya maslahi na matazamio ya mwili. Sikuwa hata na imani hata kidogo kwa Mungu. Katika hili, ningewezaje kuridhisha mapenzi ya Mungu? Mungu alitaka kile nilichoishi kwa kudhihirisha kuzaa matunda. Hakutaka viapo vya madoido, vitupu. Ilhali mbele ya Mungu nilikuwa na maarifa lakini sikuwa na uhalisi wowote, na kuelekea kwa Mungu, sikuwa na uaminifu ama upendo wa kweli, sembuse kuwa na utiifu wowote; sikuishi kwa kudhihirisha chochote ila udanganyifu, uasi, na upinzani. Katika hili, je, si nilikuwa mtu ambaye alimsaliti Mungu? Je, sikuwa mtu aliyeuvunja moyo wa Mungu? Wakati huo, nilifikiri kuhusu wakati Bwana Yesu alipokamatwa na kupigwa misumari msalabani. Mmoja baada ya mwingine, wale ambao mara nyingi walikuwa wamefurahia neema Yake walimwacha. Moyoni mwangu, singeweza kujizuia kujawa na majuto. Nilichukia uasi wangu, nilichukia ukosefu wangu wa ubinadamu, nilitaka kwa mara nyingine kusimama, kutumia vitendo vya ukweli kufanya ahadi zangu kwa Mungu kuwa uhalisi. Hata kama ningedhoofika gerezani, singeuumiza tena moyo wa Mungu. Singesaliti tena gharama ya damu ambayo Mungu alikuwa amelipa kwangu. Niliacha kulia, na moyoni mwangu nilimwomba Mungu kwa kimya: Ee Mungu, ahsante kwa kunitia nuru na kuniongoza, kuniruhusu kuelewa mapenzi Yako. Naona kwamba kimo changu ni kidogo sana, na kwamba sina upendo ama utiifu hata kidogo Kwako. Ee Mungu, sasa hivi nataka kujitoa kikamilifu Kwako. Hata nikiishi maisha yangu yote gerezani, kamwe singemkubali Shetani. Nataka tu kutumia vitendo vyangu vya ukweli kukuridhisha.
Baada ya muda, kulikuwa na uvumi zaidi kwamba ningeachiliwa. Walisema kwamba ingekuwa siku chache tu. Kwa sababu ya masomo niliyofunzwa wakati uliopita, wakati huu nilikuwa razini na mtulivu kiasi. Ingawa nilihisi mwenye kusisimka sana, nilitaka kuomba na kutafuta mbele ya Mungu, kutokuwa tena na chaguo langu mwenyewe. Ningemwomba Mungu tu anilinde ili niweze kutii utaratibu na mipango Yake yote. Baada ya siku chache, uvumi mara nyingine ulikuwa bure. Zaidi ya hayo, nilimsikia mlinzi akisema kwamba hata kama ningekufa gerezani, hawangeniachilia, sababu ikiwa kwamba singewaambia anwani yangu ya nyumbani na jina—hivyo ningetiwa gerezani milele. Kusikia hili kulikuwa kugumu sana, lakini nilijua kwamba huu ulikuwa uchungu niliopaswa kupitia. Mungu alitaka niwe na ushuhuda huu Kwake, na nilikuwa tayari kumtii Mungu, na kutii mapenzi ya Mungu, na niliamini kwamba mambo na vitu vyote vimo mikononi mwa Mungu. Hii ilikuwa neema maalum ya Mungu na kuniinua. Awali, ingawa nilikuwa nimesema ningedhoofika gerezani, hiyo ilikuwa tu hamu yangu na tamaa zangu—sikuwa na uhalisi huu. Leo, nilikuwa tayari kuwa na ushuhuda huu kupitia kuishi kwangu kulingana na matendo na kumruhusu Mungu kupata faraja kwangu. Wakati nilijawa na chuki kwa ajili ya Shetani, na nikaamua kufanya mapigano na Shetani hadi mwishoni kabisa, kwa kweli kuwa na ushuhuda wa kweli ya kudhoofikia gerezani, niliona kudura na matendo ya muujiza ya Mungu. Mnamo Desemba 6, 2005, gari la gerezani lilinichukua kutoka kituo cha kuzuia na kuniacha kando ya barabara. Kutoka wakati huo kuendelea, maisha yangu ya miaka miwili gerezani yaliisha.
Baada ya kupitia majaribu haya mabaya, ingawa mwili wangu ulikuwa umevumilia taabu kiasi, nilikuwa nimepata mara mia moja—mara elfu moja—zaidi: sikuwa tu nimekuza umaizi na utofautishaji, na kweli kuona kwamba serikali ya CCP ni mfano halisi wa Shetani ibilisi, kundi la wauaji ambao wangewaua watu kufumba kufumbua, lakini pia nilikuja kuelewa kudura na maarifa ya Mungu, na vilevile haki na utakatifu Wake, nilikuwa nimekuja kufahamu nia nzuri za Mungu katika kuniokoa, na utunzaji Wake na ulinzi Wake kwangu, Akiniruhusu, katika ukatili wa Shetani, kumshinda Shetani hatua kwa hatua, na kusimama imara katika ushuhuda wangu. Kutoka siku hiyo kuendelea, nilitaka kutoa nafsi yangu yote kwa Mungu kikamilifu. Kwa uthabiti ningemfuata Mungu, kwamba ningeweza kupatwa na Yeye mapema.
kutoka kwa Ushuhuda wa Washindi

Alhamisi, 13 Desemba 2018

Maonyesho ya Mungu | "Ni Wale tu Wanaomjua Mungu na Kazi Yake Ndio Wanaoweza Kumridhisha Mungu"

Maonyesho ya Mungu | "Ni Wale tu Wanaomjua Mungu na Kazi Yake Ndio Wanaoweza Kumridhisha Mungu"

Mwenyezi Mungu anasema, "Kuamini katika Mungu na kutafuta maarifa ya Mungu si jambo rahisi. Hayawezi kupatikana kwa kukusanyika pamoja na kusikiliza mahubiri, na huwezi kukamilishwa kwa kupenda tu. Lazima upitie uzoefu, na ujue, na kuongozwa na kanuni katika matendo yako, na kupata kazi za Roho Mtakatifu. Utakapopitia katika uzoefu, utakuwa na uwezo wa kutofautisha mambo mengi—utakuwa na uwezo wa kutofautisha kati ya jema na baya, kati ya haki na uovu, kati ya kile ambacho ni cha mwili na damu na kile ambacho ni cha kweli. Unapaswa kuwa na uwezo wa kutofautisha mambo haya yote, na kwa kufanya hivyo, haijalishi ni mazingira gani, hutapotea kamwe. Hiki ndicho kitakuwa kimo chako halisi.
Kuijua kazi ya Mungu si kazi rahisi: Unapaswa kuwa na viwango na malengo katika utafutaji wako, unapaswa kujua jinsi ya kutafuta njia ya kweli, na jinsi ya kupima kujua kama ni njia ya kweli au si ya kweli, na kama ni kazi ya Mungu au kinyume chake. Kanuni ya msingi kabisa katika kuutafuta ukweli ni nini? Unapaswa kuangalia kama kuna kazi ya Roho Mtakatifu au la, iwapo maneno haya ni maonyesho wa ukweli, yanamshuhudia nani, na ni kitu gani yanaweza kukupatia."

Jumatano, 12 Desemba 2018

II. Ni Lazima Mtu Ashuhudie Kipengele cha Ukweli Kuhusu Hatua Tatu za Kazi ya Wokovu wa Mungu kwa Wanadamu

II. Ni Lazima Mtu Ashuhudie Kipengele cha Ukweli Kuhusu Hatua Tatu za Kazi ya Wokovu wa Mungu kwa Wanadamu

3. Uhusiano Kati ya Kila Moja ya Hatua Tatu za Kazi ya Mungu
Maneno Husika ya Mungu:
Kutoka kwa kazi ya Yehova mpaka ile ya Yesu, na kutoka kwa kazi ya Yesu hadi kwa kazi iliyoko kwa awamu hii ya sasa, awamu hizi tatu zinajumlisha upana wote wa usimamizi wa Mungu, na zote ni kazi za Roho mmoja. Kutoka Alipoumba ulimwengu, Mungu Amekuwa Akisimamia wanadamu. Yeye ndiye Mwanzo na ndiye Mwisho; Yeye ndiye wa Kwanza na wa Mwisho, na Yeye ndiye mwanzilishi wa enzi na Yeye ndiye huleta enzi kwenye kikomo. Awamu tatu za kazi, katika enzi tofauti na maeneo mbalimbali, hakika yanafanywa na Roho mmoja. Wote ambao wanatenganisha awamu hizi tatu wanampinga Mungu.
kutoka kwa "Maono ya Kazi ya Mungu (3)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Mnafaa kuelewa kazi ya Yehova, sheria Alizoweka, na kanuni ambazo kwazo Aliyaongoza maisha ya mwanadamu, yaliyomo kwenye kazi Aliyofanya kwenye Enzi ya Sheria, kusudio lililomfanya Yeye kuweka wazi zile sheria, umuhimu wa kazi Yake katika Enzi ya Neema, na kazi anayofanya Mungu kwenye awamu hii ya mwisho. Hatua ya kwanza ni kazi ya Enzi ya Sheria, hatua ya pili ni kazi ya Enzi ya Neema, na hatua ya tatu ni kazi ya siku za mwisho. Lazima muelewe awamu hizi za kazi ya Mungu. … Kazi ifanywayo katika siku za mwisho haiwezi kuwekwa mbadala wa kazi ya Enzi ya Sheria ama ile ya Enzi ya Neema. Ingawa, hatua zote tatu zinaungana kuwa kitu kimoja na yote ni kazi iliyofanywa na Mungu mmoja. Kawaida, utekelezaji wa kazi hizi umegawanyishwa katika enzi tofauti. Kazi iliyofanywa katika siku za mwisho inaleta kila kitu mpaka tamati; ile iliyofanywa katika Enzi ya Sheria ni ya mwanzo; na ile iliyofanywa katika Enzi ya Neema ni ya ukombozi. … Katika siku za mwisho, kazi ya neno pekee inafanyika ili kuukaribisha Wakati wa Ufalme lakini haiwakilishi enzi zile zingine. Siku za mwisho sio zaidi ya siku za mwisho na sio zaidi ya Enzi ya Ufalme, ambayo haiwakilishi Enzi ya Neema au Enzi ya Sheria. Siku za mwisho ni wakati ambapo kazi zote ndani ya mpango wa usimamizi wa miaka elfu sita inafuchuliwa kwenu. …
Kazi katika siku za mwisho ni hatua ya mwisho kati ya hizo tatu. Ni kazi ya enzi nyingine mpya na haiwakilishi kazi ya usimamizi mzima. Mpango wa miaka elfu sita umegawawa katika hatua tatu za kazi. Hakuna hatua moja pekee itakayowakilisha kazi ya enzi hizo tatu ila inaweza tu kuwakilisha sehemu moja ya yote. Jina Yehova haliwezi kuwakilisha tabia yote ya Mungu. Ukweli kuwa Alitekeleza kazi katika Enzi ya Sheria sio ushahidi kuwa Mungu Anaweza tu kuwa Mungu chini ya sheria. Yehova alitengeneza sheria kwa mwanadamu na kutoa amri, Akimuuliza mwanadamu ajenge hekalu na madhabahu; kazi Aliyofanya inawakilisha tu Enzi ya Sheria. Kazi Alioyoifanya haidhibitishi kuwa Mungu ni Mungu Anayemwamuru mwanadamu kufuata sheria, Mungu Aliye hekaluni, ama Mungu Aliye mbele ya madhabahu. Haya hayawezi kusemwa. Kazi chini ya sheria inaweza tu kuwakilisha enzi moja. Kwa hivyo, kama Mungu Alifanya kazi katika Enzi ya Sheria pekee, mwanadamu angemfafanua Mungu na kusema, "Mungu ni Mungu Aliye hekaluni. Ili kumtumikia Mungu, lazima tuvae mavazi ya kikuhani na tuingie hekaluni." Iwapo kazi katika Enzi ya Neema haingetekelezwa na Enzi ya Sheria ingeendelea mpaka wakati huu wa sasa, mwanadamu hangefahamu kuwa Mungu pia ni mwenye huruma na upendo. Iwapo kazi katika Enzi ya Sheria haingefanywa, na kwamba tu ile ya Enzi ya Neema ndiyo iliyofanywa, mwanadamu angefahamu tu kwamba Mungu Anakomboa mwanadamu na kumsamehe dhambi zake. Wangefahamu tu kuwa Yeye ni mtakatifu na asiye na hatia, kwamba Anaweza kujitoa kafara na kusulubishwa kwa ajili ya mwanadamu. Mwanadamu angejua tu kuhusu haya na asiwe na ufahamu wa mambo mengine yoyote. Kwa hivyo kila enzi inawakilisha sehemu moja ya tabia ya Mungu. Enzi ya Sheria inawakilisha vipengelele vingine, Enzi ya Neema vipengele vingine na enzi hii vipengele vingine. Tabia ya Mungu inaweza tu kuonekana kwa mchanganyiko wa hatua zote tatu. Ni wakati tu mwanadamu anajua hatua hizi tatu ndipo anaweza kuipokea kikamilifu. Hakuna hatua kati ya hizo tatu ambayo inaweza kuachwa. Utaiona tu tabia ya Mungu kwa ukamilifu wake mara tu utakapozijua hatua hizi tatu za kazi. Mungu kukamilisha kazi yake katika Enzi ya Sheria sio ushahidi kwamba Yeye ni Mungu chini ya sheria, na kukamilika kwa kazi Yake ya ukombozi haionyeshi kuwa Mungu Atamkomboa mwanadamu milele. Hizi zote ni hitimisho zilizofanywa na mwanadamu kuhusu jambo hilo. Enzi ya Neema imefika mwisho, lakini huwezi kusema kuwa Mungu ni wa msalaba tu na kuwa msalaba unawakilisha wokovu wa Mungu. Ukifanya hivyo, basi utakuwa unamfasili Mungu. Katika hatua hii, Mungu Anafanya zaidi kazi ya Neno, lakini huwezi kusema kuwa Mungu hajawahi kuwa Mwenye huruma kwa mwanadamu na kwamba yote Aliyoleta ni kuadibu na hukumu. Kazi katika siku za mwisho inaonyesha wazi kazi ya Yehova na ile ya Yesu na mafumbo yote yasioeleweka na mwanadamu. Hii inafanywa ili kuonyesha hatima na mwisho wa binadamu na kukamilisha kazi yote ya wokovu miongoni mwa wanadamu. Hatua hii ya kazi katika siku za mwisho huleta kila kitu kufika mwisho. Mafumbo yote yasiyoeleweka na mwanadamu lazima yaelezwe ili kumpa mwanadamu ufahamu na kuweza kuelewa kwa kina katika mioyo yao. Hapo tu ndipo wanadamu wataweza kugawanywa kulinga na aina zao. Baada tu ya mpango wa usimamizi wa miaka elfu sita kukamilishwa ndipo mwanadamu atapata kuelewa tabia ya Mungu kwa ukamilifu wake, kwani usimamizi Wake utakuwa umefika mwisho.
kutoka kwa "Fumbo la Kupata Mwili (4)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kazi inayofanywa kwa sasa imesukuma mbele kazi ya Enzi ya Neema; yaani, kazi katika mpango mzima wa usimamizi wa miaka elfu sita imesonga mbele. Ingawa Enzi ya Neema imekoma, kazi ya Mungu imeendelea sana. Kwa nini Ninazungumza mara kwa mara kwamba hatua hii ya kazi inajenga juu ya Enzi ya Neema na Enzi ya Sheria? Hii ina maana kwamba kazi ya wakati huu ni mwendelezo wa kazi iliyofanyika katika Enzi ya Neema na kuinua kazi ile iliyofanyika katika Enzi ya Sheria. Hatua hizi tatu zinaingiliana kwa karibu na kuunganika moja kwa inayofuata. Kwa nini pia Ninasema kwamba hatua hii ya kazi inajenga juu ya kile kilichofanywa na Yesu? Tuseme kwamba hatua hii haingeongezea juu ya kazi iliyofanywa na Yesu, ingebidi Asulubiwe tena katika hatua hii, na kazi ya ukombozi ya hatua iliyopita ingelazimika kufanywa upya tena. Hii isingekuwa na maana yoyote. Kwa hiyo, sio kwamba kazi imekamilika kabisa, bali ni kwamba enzi imesonga mbele, na kazi imekuwa ya juu kabisa kuliko ilivyokuwa kabla. Inaweza kusemwa kwamba hatua hii ya kazi imejengwa juu ya msingi wa Enzi ya Sheria na katika mwamba wa kazi ya Yesu. Kazi hii imejengwa hatua kwa hatua, na hatua hii sio mwanzo mpya. Ni muungano tu wa hatua tatu za kazi ndio unaweza kuchukuliwa kuwa mpango wa usimamizi wa miaka elfu sita.
kutoka kwa "Kupata Mwili Mara Mbili Kunakamilisha Umuhimu wa Kupata Mwili" katika Neno Laonekana katika Mwili
Hatua ya kazi ya mwisho haisimami peke yake, ila ni sehemu ya yote iliyounganishwa pamoja na hatua mbili za awali, ambayo ni kusema kwamba haiwezekani kukamilisha kazi nzima ya wokovu kwa kufanya kazi ya hatua moja pekee. Ingawa hatua ya mwisho ya kazi inaweza kumwokoa mwanadamu kabisa, hii haimaanishi kwamba ni muhimu tu kutekeleza hatua hii pekee, na kwamba hatua mbili za hapo awali hazihitajiki kumwokoa mwanadamu kutokana na ushawishi wa Shetani. Hakuna hatua moja kati ya zote tatu inayoweza kuwekwa kama maono ya kipekee ambayo lazima yajulishwe mwanadamu, kwa kuwa ukamilifu wa kazi ya wokovu ni hatua tatu za kazi, wala si hatua moja kati ya tatu. Ilimradi kazi ya wokovu bado haijakamilishwa, usimamizi wa Mungu utashindwa kufikia kikomo. Nafsi ya Mungu, tabia, na hekima zimeonyeshwa katika ukamilifu wa kazi ya wokovu, wala hazikufichuliwa kwa mwanadamu hapo mwanzo, lakini zimeonyeshwa hatua kwa hatua katika kazi ya wokovu. Kila hatua ya kazi ya wokovu huonyesha sehemu ya tabia ya Mungu, na sehemu ya nafsi Yake: si kila hatua ya kazi inayoweza moja kwa moja kuonyesha kabisa na kwa ukamilifu nafsi ya Mungu. Kwa hivyo, kazi ya wokovu inaweza tu kuhitimishwa hatua tatu za kazi zitakapokamilika, na kwa hivyo, maarifa ya mwanadamu ya ukamilifu wa Mungu hayawezi kutenganishwa na hatua tatu za kazi ya Mungu. Kile ambacho mwanadamu hupokea kutoka kwa hatua moja ya kazi ni tabia ya Mungu inayoonyeshwa katika sehemu moja ya kazi yake tu. Haiwezi kuwakilisha tabia na nafsi inayoonyeshwa katika hatua ya awali na ijayo. Hii ni kwa sababu kazi ya kumwokoa mwanadamu haiwezi kumalizika mara moja katika kipindi kimoja, ama katika eneo moja, lakini hukuwa kwa kina hatua kwa hatua kulingana na kiwango cha kukua kwa mwanadamu katika wakati na maeneo tofauti. Ni kazi inayofanywa hatua kwa hatua, na haikamilishwi katika hatua moja. Na kwa hiyo, hekima yote ya Mungu imejumuishwa katika hatua tatu, badala ya hatua moja. Nafsi yake yote na hekima yake yote zimewekwa wazi katika hatua hizi tatu, na kila hatua ina nafsi Yake, na ni rekodi ya hekima ya kazi Yake. … Kila moja ya hatua tatu za kazi huendelea juu ya msingi wa hatua iliyopita; haitekelezwi peke yake, tofauti na kazi ya wokovu. Ingawa kuna tofauti kubwa katika enzi na aina ya kazi ambayo inafanywa, katika kiini chake bado ni wokovu wa mwanadamu, na kila hatua ya kazi ya wokovu ina kina kuliko iliyopita.
kutoka kwa "Kujua Hatua Tatu za Kazi ya Mungu Ndiyo Njia ya Kumjua Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Usimamizi mzima wa Mungu umegawika kwa hatua tatu, na katika kila hatua, mahitaji yanayopatana yanatokana na mwanadamu. Aidha, kadri enzi zinavyopita na kuendelea, mahitaji ya Mungu kwa wanadamu huongezeka hata zaidi. Kwa hiyo, hatua kwa hatua, kazi hii ya usimamizi wa Mungu hufikia kilele chake, hadi mwanadamu aamini ukweli wa "kuonekana kwa Neno katika mwili," na hivyo mahitaji ya mwanadamu huongezeka hata zaidi, na mahitaji ya mwanadamu kutoa ushuhuda huongezeka hata zaidi. … Wakati wa kale, mwanadamu alihitajika kuzingatia sheria na amri, na alihitajika kuwa mpole na mnyenyekevu. Leo, mwanadamu anahitajika kutii mipango yote ya Mungu na awe na upendo mkuu wa Mungu, na zaidi bado anahitajika kumpenda Mungu katika mateso. Hatua hizi tatu ndizo Mungu anazozitazamia toka kwa mwanadamu, hatua kwa hatua, katika usimamizi Wake wote. Kila hatua ya kazi ya Mungu huzidisha kina kuliko iliyopita, na katika kila hatua, mahitaji ya mwanadamu ni makubwa kuliko yaliyopita, na kwa hali hii, umbo la usimamizi mzima wa Mungu huonekana. Ni hasa kwa sababu mahitaji ya mwanadamu kila mara huwa juu kuliko tabia yake inavyoweza kufikia viwango anavyovihitaji Mungu, na ni hapo ambapo wanadamu wataanza kujiondoa polepole kutoka kwa ushawishi wa Shetani, ndipo kazi ya Mungu itafikia kikomo, wanadamu wote watakuwa wameokolewa kutoka kwa ushawishi wa Shetani. Wakati huo utakapowadia, kazi ya Mungu itakuwa imefika mwisho, na ushirikiano wa mwanadamu na Mungu ili abadilishe tabia zake hautakuwepo, na wanadamu wote wataishi kwenye nuru ya Mungu, na kuanzia hapo kuendelea, hapatakuwa na uasi au upinzani wowote kwa Mungu. Aidha Mungu hatamwekea matakwa mwanadamu, na patakuwepo na ushirikiano mwema zaidi kati ya mwanadamu na Mungu, mojawapo ikiwa maisha ya mwanadamu na Mungu pamoja, maisha ambayo yatafuatia baada ya usimamizi wa Mungu kukamilishwa, na baada ya mwanadamu kuokolewa toka katika mafumbato ya Shetani.
kutoka kwa "Kazi ya Mungu na Utendaji wa Mwanadamu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kazi mzima ya mpangilio wa usimamizi wa Mungu inafanywa binafsi na Mungu mwenyewe. Awamu ya kwanza—uumbaji wa ulimwengu—ilifanywa binafsi na Mungu Mwenyewe, na kama haikuwa hivyo, basi hakuna yeyote ambaye angekuwa na uwezo wa kumuumba mwanadamu; awamu ya pili ilikuwa ukombozi wa wanadamu wote, na pia ilifanywa binafsi na Mungu Mwenyewe, awamu ya tatu inaenda bila kusemwa: Kuna haja kuu zaidi ya mwisho wa kazi ya Mungu kufanywa na Mungu Mwenyewe. Kazi ya ukombozi, ushindi, kumpata, na kumkamilisha wanadamu wote inafanywa binafsi na Mungu Mwenyewe. Kama hangefanya kazi hii Yeye binafsi, basi utambulisho wake hauwezi kuwakilishwa na mwanadamu, au kazi kufanywa na mwanadamu. Ili kumshinda Shetani, ili kumpata mwanadamu, na ili kumpa mwanadamu maisha ya kawaida duniani, Yeye binafsi humwongoza mwanadamu na hufanya kazi binafsi miongoni mwa wanadamu; kwa ajili ya mpangilio mzima wa usimamizi, na kwa kazi yake yote, ni lazima Yeye binafsi afanye kazi hii.
kutoka kwa "Kurejesha Maisha ya Kawaida ya Mwanadamu na Kumpeleka Kwenye Hatima ya Ajabu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Hatua tatu za kazi ambazo zilifanywa tangu mwanzo hadi leo zote zilitekelezwa na Mungu Mwenyewe, na zilitekelezwa na Mungu mmoja. Ukweli wa hatua tatu za kazi ni ukweli wa uongozi wa Mungu kwa wanadamu wote, ukweli ambao hakuna anayeweza kuupinga. Mwishoni mwa hatua tatu za kazi, vitu vyote vitaainishwa kulingana na aina na kurejea chini ya utawala wa Mungu, kwa kuwa duniani kote kuna Mungu mmoja tu, na hakuna dini nyingine.
kutoka kwa "Kujua Hatua Tatu za Kazi ya Mungu Ndiyo Njia ya Kumjua Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kama una maarifa wazi ya hatua tatu za kazi—ambapo ni kusema kwamba, ya mpango mzima wa usimamizi wa Mungu—na ikiwa utaweza kupatanisha hatua mbili za awali na hatua ya sasa, na unaweza kuona kwamba ni kazi iliyofanywa na Mungu Mmoja, basi utakuwa na msingi imara zaidi. Hatua tatu za kazi zilifanywa na Mungu mmoja; haya ndiyo maono makubwa zaidi, na ndiyo njia ya pekee ya kumjua Mungu. Hatua tatu za kazi zingefanywa tu na Mungu Mwenyewe, na hapana mwanadamu yeyote ambaye angeweza kufanya kazi kama hii kwa niaba Yake—ambayo ni kusema kuwa ni Mungu Mwenyewe pekee ambaye angeifanya kazi Yake toka mwanzo hadi leo.
kutoka kwa "Kujua Hatua Tatu za Kazi ya Mungu Ndiyo Njia ya Kumjua Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
    Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Vitabu.