Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Jumatatu, 18 Februari 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Fumbo la Kupata Mwili (4)

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Yesu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Fumbo la Kupata Mwili (4)

Mnapaswa kujua kuhusu hadithi ya ndani na uumbaji wa Biblia. Ufahamu huu haushikiliwi na wale ambao hawajakubali kazi mpya ya Mungu. Wao hawajui. Waelezee mambo haya ya kiini, na hawatakuwa pamoja nawe wenye kushikilia sana elimu ya vitabuni na sheria kuhusu Biblia. Wao huchunguza kwa uthabiti kile ambacho kimetabiriwa: Kauli hii imeshatimia? Kauli ile imeshatimia? Kukubali kwao injili ni kwa mujibu wa Biblia; wao huhubiri injili kulingana na Biblia. Wao huyategemea maneno ya Biblia kumwamini Mungu; bila Biblia, wao hawatamwamini Mungu. Hii ndiyo njia ambayo wao huishi, kuichunguza Biblia hivyo. Wakati ambapo wao huchunguza Biblia tena na kukuuliza wewe kuhusu ufafanuzi, unaweza kusema, “Kwanza, hebu tusithibitishe kila kauli. Badala yake, hebu tuangalie vile Roho Mtakatifu hufanya kazi. Hebu tulinganishe dhidi ya ukweli ili tuone kama njia tunayotembea inakubaliana na kazi ya Roho Mtakatifu, na tutumie kazi ya Roho Mtakatifu kuangalia kwa makini kama njia hiyo ni sahihi. Kuhusu kama kauli hii au kauli ile imeshatimia, sisi binadamu hatupaswi kuingilia. Ni bora kwetu badala yake kuzungumza kuhusu kazi ya Roho Mtakatifu na kazi ya karibuni zaidi ambayo Mungu anafanya sasa. Biblia ina maneno ya Mungu yaliyonenwa na manabii na maneno yaliyoandikwa na wanadamu waliotumiwa na Mungu wakati huo; ni Mungu Mwenyewe tu ndiye anaweza kueleza maneno hayo, Roho Mtakatifu pekee ndiye anaweza kutambulisha maana ya maneno hayo, na Mungu Mwenyewe tu ndiye anaweza kuivunja mihuri saba na kukifungua kitabu. Wewe si Mungu, na wala Mimi si Mungu, kwa hiyo nani anathubutu kueleza kwa hiari maneno ya Mungu? Je, wewe unathubutu kueleza maneno hayo? Hata kama manabii Yeremia, Yohana na Eliya wangekuwa hapa, hawangethubutu, kwani wao si Mwanakondoo. Ni Mwanakondoo pekee ndiye anaweza kuivunja mihuri saba na kufungua kitabu, na hakuna mwingine awezaye kuyaeleza maneno Yake. Sithubutu kunyang’anya jina la Mungu, seuze kujaribu kuyaeleza maneno ya Mungu. Naweza tu kuwa yule ambaye humtii Mungu. Je, wewe ni Mungu? Hakuna viumbe wa Mungu ambao huthubutu kufungua kitabu au kuyafafanua maneno hayo, na hivyo Sithubutu kuyaeleza pia. Ni bora usijaribu kuyaeleza. Hakuna kati yetu atakayeeleza. Hebu tuzungumze kuhusu kazi ya Roho Mtakatifu; hili ndilo mwanadamu anaweza kufanya. Najua machache kuhusu kazi ya Yehova na Yesu, lakini kwa vile Sina uzoefu Wangu binafsi na kazi hiyo, Naweza tu kuizungumzia kwa kiasi kidogo. Kuhusu maneno yaliyonenwa na Isaya au Yesu wakati huo, Sitafanya ufafanuzi. Sijifunzi Biblia; badala yake, Mimi hufuata kazi ya sasa ya Mungu. Wewe kwa kweli unaichukulia Biblia kuwa kitabu kidogo, lakini siyo kweli kwamba kinaweza tu kufunguliwa na Mwanakondoo. Isipokuwa Mwanakondoo, nani mwingine anaweza kufanya hivyo? Wewe si Mwanakondoo, na wala Mimi sithubutu kudai kuwa Mungu Mwenyewe, kwa hiyo hebu tusichambue au kuichunguza Biblia. Bora kujadili kazi ambayo hufanywa na Roho Mtakatifu, yaani, kazi ya sasa ambayo hufanywa na Mungu Mwenyewe. Hebu tuangalie kanuni na kiini cha kazi ya Mungu, kisha tuyaangalie kwa makini dhidi ya hayo kuona kama njia tunayotembea siku hii ni ya kweli. Hebu tulinganishe na hili kama kiwango.” Kama ninyi huhubiri injili, hasa kwa wale walio katika ulimwengu wa kidini, lazima muelewe Biblia na muwe na ujuzi wa hadithi yake ya ndani, la sivyo, hutaweza kuhubiri injili. Mara tu unapopata utambuzi wa taswira kubwa, usiyachunguze maneno ya Biblia yaliyopitwa na wakati, na zungumza tu kuhusu kazi ya Mungu na ukweli wa maisha, kisha utaweza kuwapata wale wanaotafuta kwa roho ya kweli.
Mnafaa kuelewa kazi ya Yehova, sheria Alizoweka, na kanuni ambazo kwazo Aliyaongoza maisha ya mwanadamu, yaliyomo kwenye kazi Aliyofanya kwenye Enzi ya Sheria, kusudio lililomfanya Yeye kuweka wazi zile sheria, umuhimu wa kazi Yake katika Enzi ya Neema, na kazi anayofanya Mungu kwenye awamu hii ya mwisho. Hatua ya kwanza ni kazi ya Enzi ya Sheria, hatua ya pili ni kazi ya Enzi ya Neema, na hatua ya tatu ni kazi ya siku za mwisho. Lazima muelewe awamu hizi za kazi ya Mungu. Tangu mwanzo hadi mwisho, kuna hatua tatu kwa jumla. Ni nini kiini cha kila hatua ya kazi? Ni hatua ngapi hutekelezwa katika kazi ya mpango wa usimamizi wa miaka elfu sita? Kila hatua hutekelezwa vipi, na kwa nini kila mojawapo hutekelezwa kwa njia hii? Haya yote ni maswali ya maana sana. Kazi ya kila enzi ni wakilishi. Yehova alitekeleza kazi gani? Mbona Alifanya hivyo? Mbona Aliitwa Yehova? Yesu alitekeleza kazi gani katika Enzi ya Neema, na Alifanyaje hivyo? Ni hali gani za tabia ya Mungu huwakilishwa na kila hatua ya kazi na kila enzi? Ni hali zipi za tabia Yake zilijitokeza katika Enzi ya Sheria? Na katika Enzi ya Neema? Na kisha katika enzi ya mwisho? Haya maswali halisi ni yale ambayo ni lazima myaelewe. Tabia yote ya Mungu imefichuliwa katika mpango wote wa uongozi wa miaka elfu sita. Haikufichuliwa tu katika Enzi ya Neema, ni katika Enzi ya Sheria tu, na zaidi ya hayo, ni katika wakati huu wa siku za mwisho. Kazi iliyofanywa katika siku za mwisho inawakilisha hukumu, ghadhabu na kuadibu. Kazi ifanywayo katika siku za mwisho haiwezi kuwekwa mbadala wa kazi ya Enzi ya Sheria ama ile ya Enzi ya Neema. Ingawa, hatua zote tatu zinaungana kuwa kitu kimoja na yote ni kazi iliyofanywa na Mungu mmoja. Kawaida, utekelezaji wa kazi hizi umegawanyishwa katika enzi tofauti. Kazi iliyofanywa katika siku za mwisho inaleta kila kitu mpaka tamati; ile iliyofanywa katika Enzi ya Sheria ni ya mwanzo; na ile iliyofanywa katika Enzi ya Neema ni ya ukombozi. Na kuhusu maono ya kazi katika mpango wote wa usimamizi wa miaka elfu sita, hakuna anayeweza kupata ufahamu au kuelewa. Maono kama hayo yamebaki kuwa mafumbo kila wakati. Katika siku za mwisho, kazi ya neno pekee inafanyika ili kuukaribisha Wakati wa Ufalme lakini haiwakilishi enzi zile zingine. Siku za mwisho sio zaidi ya siku za mwisho na sio zaidi ya Enzi ya Ufalme, ambayo haiwakilishi Enzi ya Neema au Enzi ya Sheria. Siku za mwisho ni wakati ambapo kazi zote ndani ya mpango wa usimamizi wa miaka elfu sita inafichuliwa kwenu. Mafumbo kama hayo hayawezi kufichuliwa na mwanadamu yeyote. Haijalishi mwanadamu ana maarifa makubwa ya Biblia vipi, yanabaki tu kuwa maneno na si kitu zaidi, kwani mwanadamu haelewi kiini cha Biblia. Mwanadamu anaposoma Biblia, anaweza kupokea baadhi ya ukweli, kueleza baadhi ya maneno ama kuchunguza vifungu maarufu na nukuu, lakini hatawahi kuwa na uwezo wa kunasua maana iliyoko katika maneno hayo, kwani yote aonayo mwanadamu ni maneno yaliyokufa pekee, sio matendo ya kazi ya Yehova na Yesu, na mwanadamu hawezi kufumbua mafumbo ya kazi ya aina hiyo. Kwa hivyo, fumbo la mpango wa usimamizi wa miaka elfu sita ni fumbo kuu, iliyofichwa zaidi na isiyoshawishika kwa mwanadamu. Hakuna anayeweza kuelewa moja kwa moja mapenzi ya Mungu, ama, Yeye Mwenyewe Aeleze na kumfungulia mwanadamu, vinginevyo, yatabaki kuwa mafumbo milele kwa mwanadamu na kubaki mafumbo yaliyofungwa milele. Usiwajali wale walio katika ulimwengu wa kidini; kama hamngeambiwa leo, pia nyinyi hamngeweza kuelewa. Kazi hii ya miaka elfu sita ni ya fumbo zaidi kuliko unabii wote wa manabii. Ni fumbo kuu zaidi tangu uumbaji, na hakuna nabii wa awali ambaye amewahi kuweza kulielewa, kwani fumbo hili hufumbuliwa tu katika enzi ya mwisho na kamwe halijawahi kufichuliwa hapo awali. Mkielewa fumbo hili na muweze kulipokea kwa ukamilifu, wale watu wote wa kidini watashindwa kwa fumbo hili. Hili pekee ndilo kuu zaidi ya maono, lile ambalo mwanadamu hutamani sana kulielewa lakini pia lile ambalo si wazi zaidi kwake. Mlipokuwa katika Enzi ya Neema, hamkujua kazi ambayo ilifanywa na Yesu wala ile ambayo ilifanywa na Yehova. Watu hawakuelewa chochote kuhusu kwa nini Yehova alitangaza sheria, kwa nini Aliwaambia watu wazitii sheria au kwa nini ilikuwa lazima kwa hekalu kujengwa, na sembuse watu kuelewa kwa nini Waisraeli waliongozwa kutoka Misri hadi jangwani na kisha hadi Kanaani. Ni mpaka siku hii ndipo mambo haya yamefichuliwa.
Kazi katika siku za mwisho ni hatua ya mwisho kati ya hizo tatu. Ni kazi ya enzi nyingine mpya na haiwakilishi kazi ya usimamizi mzima. Mpango wa miaka elfu sita umegawa katika hatua tatu za kazi. Hakuna hatua moja pekee itakayowakilisha kazi ya enzi hizo tatu ila inaweza tu kuwakilisha sehemu moja ya yote. Jina Yehova haliwezi kuwakilisha tabia yote ya Mungu. Ukweli kuwa Alitekeleza kazi katika Enzi ya Sheria sio ushahidi kuwa Mungu Anaweza tu kuwa Mungu chini ya sheria. Yehova alitengeneza sheria kwa mwanadamu na kutoa amri, Akimuuliza mwanadamu ajenge hekalu na madhabahu; kazi Aliyofanya inawakilisha tu Enzi ya Sheria. Kazi Aliyoifanya haidhibitishi kuwa Mungu ni Mungu Anayemwamuru mwanadamu kufuata sheria, Mungu Aliye hekaluni, ama Mungu Aliye mbele ya madhabahu. Haya hayawezi kusemwa. Kazi chini ya sheria inaweza tu kuwakilisha enzi moja. Kwa hivyo, kama Mungu Alifanya kazi katika Enzi ya Sheria pekee, mwanadamu angemfafanua Mungu na kusema, “Mungu ni Mungu Aliye hekaluni. Ili kumtumikia Mungu, lazima tuvae mavazi ya kikuhani na tuingie hekaluni.” Iwapo kazi katika Enzi ya Neema haingetekelezwa na Enzi ya Sheria ingeendelea mpaka wakati huu wa sasa, mwanadamu hangefahamu kuwa Mungu pia ni mwenye huruma na upendo. Iwapo kazi katika Enzi ya Sheria haingefanywa, na badala yake kazi katika Enzi ya Neema pekee , basi yote ambayo mwanadamu angefahamu ni kwamba Mungu Anakomboa tu mwanadamu na kumsamehe dhambi zake. Wangefahamu tu kuwa Yeye ni mtakatifu na asiye na hatia, kwamba Anaweza kujitoa kafara na kusulubishwa kwa ajili ya mwanadamu. Mwanadamu angejua tu kuhusu haya na asiwe na ufahamu wa mambo mengine yoyote. Kwa hivyo kila enzi inawakilisha sehemu moja ya tabia ya Mungu. Enzi ya Sheria inawakilisha vipengele vingine, Enzi ya Neema vipengele vingine na enzi hii vipengele vingine. Tabia ya Mungu inaweza tu kuonekana kwa mchanganyiko wa hatua zote tatu. Ni wakati tu mwanadamu anajua hatua hizi tatu ndipo anaweza kuipokea kikamilifu. Hakuna hatua kati ya hizo tatu ambayo inaweza kuachwa. Utaiona tu tabia ya Mungu kwa ukamilifu wake mara tu utakapozijua hatua hizi tatu za kazi. Ukweli kamba Mungu alikamilisha kazi yake katika Enzi ya Sheria sio ushahidi kwamba Yeye ni Mungu chini ya sheria tu, na ukweli kamba alikamilisha kazi Yake ya ukombozi haimaanishi kuwa Mungu Atamkomboa mwanadamu milele. Hizi zote ni hitimisho zilizofanywa na mwanadamu kuhusu jambo hilo. Enzi ya Neema ikiwa imefika mwisho, huwezi basi kusema kuwa Mungu ni wa msalaba tu na kuwa msalaba pekee unawakilisha wokovu wa Mungu. Ukifanya hivyo, basi utakuwa unamfasili Mungu. Katika hatua hii, Mungu Anafanya zaidi kazi ya Neno, lakini huwezi kusema kuwa Mungu hajawahi kuwa Mwenye huruma kwa mwanadamu na kwamba yote Aliyoleta ni kuadibu na hukumu. Kazi katika siku za mwisho inaonyesha wazi kazi ya Yehova na ile ya Yesu na mafumbo yote yasioeleweka na mwanadamu. Hii inafanywa ili kuonyesha hatima na mwisho wa binadamu na kukamilisha kazi yote ya wokovu miongoni mwa wanadamu. Hatua hii ya kazi katika siku za mwisho huleta kila kitu kufika mwisho. Mafumbo yote yasiyoeleweka na mwanadamu lazima yaelezwe ili kumpa mwanadamu ufahamu na kuweza kuelewa kwa kina katika mioyo yao. Hapo tu ndipo wanadamu wataweza kugawanywa kulinga na aina zao. Baada tu ya mpango wa usimamizi wa miaka elfu sita kukamilishwa ndipo mwanadamu atapata kuelewa tabia ya Mungu kwa ukamilifu wake, kwani usimamizi Wake utakuwa umefika mwisho. Kwa kuwa mmeipitia kazi ya Mungu katika enzi ya mwisho, tabia ya Mungu ni gani? Je, wewe unathubutu kusema kwamba Mungu ni Mungu ambaye hunena maneno tu? Hungeweza kuthubutu kufanya uamuzi huu. Wengine husema kwamba Mungu ni Mungu ambaye hufumbua mafumbo, kwamba Mungu ni Mwanakondoo na Ambaye huvunja mihuri saba. Hakuna ambaye huthubutu kufanya uamuzi huu. Na kuna wengine ambao husema kwamba Mungu ni aliyepata mwili. Hili bado si sahihi. Wengine husema kwamba Mungu mwenye mwili hunena maneno tu na Hafanyi ishara na maajabu. Wala hungeweza kuthubutu kunena kwa njia hii, kwani Yesu alipata mwili na Alifanya ishara na maajabu, kwa hiyo wewe huthubutu kumfafanua Mungu kwa urahisi. Kazi yote iliyofanyika katika mpango wa usimamizi wa miaka elfu sita imefika mwisho sasa. Ni baada tu ya kazi hii kubainika wazi kwa mwanadamu na kutekelezwa miongoni mwa wanadamu ndipo watakapofahamu tabia Yake na mali Yake na uwepo. Kazi za enzi hizi zitakapokamilika, mafumbo yote yasiyoeleweka na mwanadamu yatakuwa yamebainika, ukweli wote ambao haukuwa unaeleweka utawekwa wazi, na mwanadamu atakuwa ameambiwa njia na hatima ya baadaye. Hii ndio kazi yote inayopaswa kufanyika katika hatua hii. Ingawa njia ambayo mwanadamu hutembea leo pia ni njia ya msalaba na ya kuteseka, kile ambacho mwanadamu wa leo hutenda, hula, hunywa na hufurahia ni tofauti zaidi na yale ya mwanadamu aliyekuwa chini ya sheria na katika Enzi ya Neema. Kinachohitajika kutoka kwa mwanadamu wakati huu sio kama ilivyokuwa kitambo na zaidi sio kama kilichohitajika kutoka kwake katika Enzi ya Sheria. Na ni kipi kilichoulizwa kwa mwanadamu chini ya Sheria kazi ilipofanya Israeli? Hawakuulizwa chochote zaidi ya kuiheshimu Sabato na Sheria za Yehova. Lakini si hivyo katika wakati huu. Siku ya Sabato, mwanadamu anafanya kazi, hukusanyika na kuomba kama kawaida, na hakuna vizuizi vinavyowekwa. Wale katika Enzi ya Neema ilibidi wabatizwe, na pia zaidi walitarajiwa kufunga, kuvunja mkate, kunywa divai, kufunika vichwa vyao na kuwaoshea wengine miguu yao. Sasa, sheria hizi zimefutwa na mahitaji makuu yanaulizwa kutoka kwa mwanadamu, kwani kazi ya Mungu inaendelea kuimarika na kuingia kwa mwanadamu kunafika kiwango cha juu. Zamani, Yesu Aliweka mikono Yake juu ya mwanadamu na kuomba, lakini sasa kwamba kila kitu kimesemwa, kuwekelea mikono kuna maana gani? Maneno pekee yanaweza kupata matokeo. Alipowekelea mikono Yake juu ya mwanadamu hapo awali, ilikuwa ni kwa ajili ya kumbariki na kumponya mwanadamu. Hivyo ndivyo Roho Mtakatifu Alivyofanya kazi wakati huo, lakini sio hivyo wakati huu. Wakati huu, Roho Mtakatifu Anatumia maneno katika kazi Yake ili kupata matokeo. Ameyafanya maneno Yake wazi kwenu, na mnapaswa tu kuyaweka katika matendo. Maneno Yake ni mapenzi Yake na yanaonyesha kazi Atakayofanya. Kupitia kwa maneno Yake, utaweza kuelewa mapenzi Yake na yale ambayo Anauliza upate. Unayaweka tu maneno Yake katika matendo moja kwa moja bila haja ya kuwekelea mikono. Wengine wanaweza kusema, “Wekelea mikono Yako juu yangu! Wekelea mikono yako juu yangu ili niweze kupokea baraka zako na kushiriki kwako.” Haya yote ni mazoezi yaliyopitwa na wakati na ambayo yanakataliwa katika wakati huu, kwani enzi zimebadilika. Roho Mtakatifu Anafanya kazi kulingana na enzi, sio tu katika mapenzi Yake ama kulingana na masharti. Enzi zimebadilika, na enzi mpya lazima ilete kazi mpya. Huu ni ukweli wa kila hatua ya kazi, na hivyo kazi Yake haiwezi kurudiwa. Katika Enzi ya Neema, Yesu Alifanya nyingi ya kazi hiyo, kama kuponya magonjwa, kukemea mapepo, kuwekelea mikono Yake juu ya wanadamu, na kumbariki mwanadamu. Hata hivyo, kuendelea kufanya hivyo hakutasaidia chochote katika wakati huu. Roho Mtakatifu Alifanya kazi hivyo katika huo wakati, kwani ilikuwa Enzi ya Neema, na mwanadamu alipewa neema ya kutosha ili afurahie. Mwanadamu hakuhitajika kulipa gharama yoyote na angepokea neema mradi tu angekuwa na imani. Kila mtu alitendewa kwa neema kubwa. Sasa, enzi imebadilika, na kazi ya Mungu imeendelea zaidi; kupitia kuadibu na hukumu Yake, uasi wa mwanadamu na vitu vichafu katika mwanadamu vitatupiliwa mbali. Jinsi ilivyokuwa hatua ya wokovu, ilimbidi Mungu kufanya kazi hiyo, Akimwonyesha mwanadamu neema ya kutosha ili mwanadamu afurahie, ili Amkomboe mwanadamu kutoka kwa dhambi, na kwa neema amsamehe mwanadamu dhambi zake. Hatua hii ya sasa ni ya kufichua udhalimu ulio ndani ya mwanadamu kwa njia ya kuadibu, hukumu, kupigwa na maneno, na vile vile nidhamu na ufunuo wa maneno, ili baadaye binadamu waweze kuokolewa. Hii ni kazi ya undani zaidi kuliko ukombozi. Katika Enzi ya Neema, mwanadamu alifurahia neema ya kutosha na amezoea neema hii, kwa hivyo sio ya kufurahiwa na mwanadamu tena. Kazi kama hii imepitwa na wakati sasa na haitafanyika tena. Sasa, mwanadamu anaokolewa kupitia hukumu ya neno. Baada ya mwanadamu kuhukumiwa, kuadibiwa na kusafishwa, tabia yake basi inabadilika. Je sio kwa sababu ya maneno ambayo Nimenena? Kila hatua ya kazi inafanywa kulingana na maendeleo ya binadamu wote na kwa enzi. Kazi yote ina umuhimu wake; inafanywa kwa ajili ya wokovu wa mwisho, ili binadamu awe na hatima nzuri baadaye, na kwa mwanadamu kugawanywa kulingana na aina Yake mwishowe.
Kazi katika siku za mwisho ni kunena maneno. Mabadiliko makuu yanaweza kusababishwa kwa watu kupitia katika maneno hayo. Mabadiliko yanayosababishwa sasa kwa watu hawa kwa sababu ya kukubali maneno haya ni makubwa kuliko yale ya watu katika Enzi ya Neema kwa kukubali ishara na maajabu hayo. Kwani, katika Enzi ya Neema, mapepo yaliondoka kutoka kwa mwanadamu kwa kuwekewa mikono na maombi, lakini tabia potovu ndani ya mwanadamu ilibaki. Mwanadamu aliponywa magonjwa na kusamehewa dhambi zake, lakini kazi ya jinsi tabia potovu za kishetani katika mwanadamu haikutupiliwa mbali na bado iko ndani yake. Mwanadamu aliokolewa na kusamehewa dhambi zake kwa imani yake, lakini asili ya dhambi ya mwanadamu haikuchukuliwa na ikabaki naye. Dhambi za mwanadamu zilisamehewa kupitia mwili wa Mungu mwenye mwili, lakini haimaanishi kuwa mwanadamu hana dhambi ndani yake. Dhambi za mwanadamu zingesamehewa kupitia sadaka ya dhambi, lakini mwanadamu hajaweza kutatua suala la vipi hangeweza kutenda dhambi na vile asili Yake ya dhambi ingetupiliwa mbali kabisa na kubadilishwa. Dhambi za mwanadamu zilisamehewa kwa sababu ya kazi ya Mungu ya kusulubiwa, lakini mwanadamu akaendelea kuishi katika tabia potovu za zamani za kishetani. Hivyo, mwanadamu lazima aokolewe kabisa kutoka kwa tabia potovu za kishetani ili asili ya dhambi ya mwanadamu itupiliwe mbali kabisa na isirudi tena, hivyo kukubali tabia ya mwanadamu kubadilika. Hii inampasa mwanadamu kuelewa njia ya kukua katika maisha, njia ya maisha, na jinsi ya kubadilisha tabia yake. Inamhitaji pia mwanadamu kutenda kulingana na njia hii ili tabia ya mwanadamu iweze kubadilika hatua kwa hatua na aishi chini ya nuru inayong’aa, na aweze kufanya mambo yote kulingana na mapenzi ya Mungu, atupilie mbali tabia potovu za kishetani, na kutoka kwa ushawishi wa Shetani wa giza, hivyo kutoka kabisa katika dhambi. Ni hapo tu ndipo mwanadamu atapokea wokovu kamili. Yesu Alipokuwa Akifanya kazi Yake, maarifa ya mwanadamu juu Yake yalikuwa bado hayakuwa bayana na hayakuwa wazi. Mwanadamu aliamini kila wakati kuwa Alikuwa Mwana wa Daudi na kumtangaza kuwa nabii mkuu na Bwana mwema Aliyezikomboa dhambi za mwanadamu. Wengine, wakiwa na msingi wa imani, wakaponywa tu kwa kugusa vazi Lake; vipofu wakaona na hata wafu kurejeshwa katika uhai. Hata hivyo, mwanadamu hangeweza kutambua tabia potovu za kishetani zilizokita mizizi ndani yake na pia mwanadamu hakujua jinsi ya kuitoa. Mwanadamu alipokea neema nyingi, kama amani na furaha ya mwili, baraka ya familia nzima juu ya imani ya mmoja, na kuponywa magonjwa, na mengine mengi. Yaliyobaki ni matendo mema ya mwanadamu na kuonekana kwa kiungu; kama mwanadamu angeishi katika huo msingi, alichukuliwa kama muumini mzuri. Waumini hao tu ndio wangeingia mbinguni baada ya kifo, hii ina maana kuwa walikuwa wameokolewa. Lakini katika maisha yao, hawakuelewa kamwe njia ya maisha. Walitenda tu dhambi, na kisha kukiri kila wakati bila njia ya kuielekea tabia iliyobadilika; hii ndiyo ilikuwa hali ya mwanadamu katika Enzi ya Neema. Je mwanadamu amepokea wokovu kamili? La! Kwa hivyo, hatua ilipokamilika, bado kuna kazi ya hukumu na kuadibu. Hatua hii inamfanya mwanadamu kuwa safi kupitia neno ili kumpatia mwanadamu njia ya kufuata. Hatua hii haingekuwa na matunda ama ya maana kama ingeendelea na kukemea mapepo, kwani msingi wa dhambi wa mwanadamu haungetupwa mbali na mwanadamu angekoma tu baada ya msamaha wa dhambi. Kupitia kwa sadaka ya dhambi, mwanadamu amesamehewa dhambi zake, kwani kazi ya kusulubisha imefika mwisho na Mungu Ametawala juu ya Shetani. Lakini tabia potovu ya wanadamu bado imebaki ndani yao na mwanadamu anaweza kutenda dhambi na kumpinga Mungu; Mungu hajampata mwanadamu. Hiyo ndio sababu katika hatua hii ya kazi Mungu Anatumia neno kutangaza tabia potovu ya mwanadamu na kumuuliza mwanadamu kutenda kulingana na njia sahihi. Hatua hii ni ya maana zaidi kuliko zile za awali na pia yenye mafanikio zaidi, kwani wakati huu ni neno ambalo linatoa maisha moja kwa moja kwa mwanadamu na linawezesha tabia ya mwanadamu kubadilishwa kabisa; ni hatua ya kazi ya uhakika kabisa. Kwa hivyo, Mungu kupata mwili katika siku za mwisho imekamilisha umuhimu wa Mungu kupata mwili wa Mungu na kukamilisha usimamizi wa Mungu katika mpango wa kuokoa mwanadamu.
Wokovu wa Mungu kwa mwanadamu haufanywi moja kwa moja kupitia njia ya Roho ama kama Roho, kwani Roho Wake hawezi kuguzwa ama kuonekana na mwanadamu, na hawezi kukaribiwa na mwanadamu. Kama Angejaribu kumwokoa mwanadamu moja kwa moja kwa njia ya Roho, mwanadamu hangeweza kupokea wokovu Wake. Na kama sio Mungu kuvalia umbo la nje la mwanadamu aliyeumbwa, mwanadamu hawangeweza kupokea wokovu huu. Kwani mwanadamu hawezi kumkaribia kwa njia yoyote ile, zaidi kama jinsi hakuna anayeweza kukaribia wingu la Yehova. Ni kwa kuwa mwanadamu wa kuumbwa tu, hivyo ni kusema, kuliweka neno Lake katika mwili Atakaogeukana kuwa, ndio ataweza kulifanya neno yeye Mwenyewe ndani ya wale wote wanaomfuata. Hapo ndipo mwanadamu atasikia mwenyewe neno Lake, kuona neno Lake, na kupokea neno Lake, kisha kupitia hili aokolewe kamili. Kama Mungu hangegeuka na kupata mwili, hakuna mwanadamu mwenye mwili ambaye angepokea wokovu huo mkuu, wala hakuna mwanadamu hata mmoja ambaye angeokolewa. Kama Roho wa Mungu angefanya kazi moja kwa moja kati ya mwanadamu, mwanadamu angepigwa ama kubebwa kabisa kama mfungwa na Shetani kwani mwanadamu hawezi kushirikiana na Mungu. Kupata mwili mara ya kwanza kulikuwa kumkomboa mwanadamu kutoka katika dhambi kupitia mwili wa Yesu, hivyo, Aliokoa mwanadamu kutoka kwa msalaba, lakini tabia potovu ya kishetani ilibaki ndani ya mwanadamu. Kupata mwili mara ya pili si kwa ajili ya kuhudumu tena kama sadaka ya dhambi ila ni kuwaokoa kamilifu wale waliokombolewa kutoka kwa dhambi. Hii inafanyika ili wale waliosamehewa wakombolewe kutoka kwa dhambi zao, na kufanywa safi kabisa, na kupata mabadiliko ya tabia, hivyo kujikwamua kutoka kwa ushawishi wa Shetani wa giza na kurudi mbele za kiti cha enzi cha Mungu. Hivyo tu ndivyo mwanadamu ataweza kutakaswa kikamilifu. Mungu Alianza kazi ya wokovu katika Enzi ya Neema baada ya Enzi ya Sheria kufika mwisho. Ni mpaka siku za mwisho tu ambapo Mungu Ametakasa binadamu kikamilifu kwa kufanya kazi ya hukumu na kuadibu mwanadamu kwa kuwa muasi, ndipo Mungu atakamilisha kazi Yake ya wokovu na kupumzika. Kwa hivyo, katika hatua tatu za kazi, ni mara mbili tu ndipo Mungu Alikuwa mwili ili kufanya kazi Yake kati ya mwanadamu Mwenyewe. Hiyo ni kwa sababu moja tu kati ya hatua tatu za kazi ni kuwaongoza wanadamu katika maisha yao, ilhali zingine mbili ni kazi ya wokovu. Mungu Anapokuwa mwili tu ndipo Atakapoishi pamoja na mwanadamu, kuzoea mateso ya dunia, na kuishi katika mwili wa kawaida. Katika hali hii tu ndipo Ataweza kumpatia mwanadamu wa uumbaji Wake neno la matendo wanalohitaji. Mwanadamu anapokea wokovu kamili kutoka kwa Mungu kwa sababu ya Mungu mwenye mwili, sio moja kwa moja kutoka kwa maombi yao kwenda mbinguni. Kwani mwanadamu ni mwenye mwili; mwanadamu hawezi kuona Roho wa Mungu na pia kutoweza kumkaribia. Kile tu mwanadamu anaweza kushiriki na mwili wa Mungu; kupitia Yeye tu ndipo mwanadamu ataweza kuelewa maneno yote, na ukweli wote, na kupokea wokovu kamili. Kupatikana kwa mwili mara ya pili kunatosha kumaliza dhambi za mwanadamu na kumtakasa mwanadamu. Hivyo, kupatikana kwa mwili mara ya pili kutafikisha tamati kazi yote ya Mungu mwenye mwili na kukamilisha umuhimu wa Mungu kupata mwili. Baada ya hapo, kazi ya Mungu mwenye mwili itakuwa imefika mwisho kabisa. Baada ya kupata mwili mara ya pili, hatakuwa mwili tena kwa kazi Yake. Kwani usimamizi Wake wote utakuwa umefika mwisho. Katika siku za mwisho, mwili Wake utakuwa umepata watu Wake teule kabisa, na yote mwanadamu katika siku za mwisho watakuwa wamegawanywa kulingana na aina yao. Hatafanya kazi ya wokovu tena, wala Hatarudi kuwa mwili ili kutekeleza kazi yoyote. Katika kazi ya siku za mwisho, neno ni kubwa zaidi ya udhihirisho wa ishara na maajabu, na mamlaka ya neno yanashinda yale ya ishara na maajabu. Neno linaweka wazi tabia zote potovu katika moyo wa mwanadamu. Huwezi kutambua binafsi wewe mwenyewe. Yatakapofunuliwa kwako kupitia kwa neno, utakuja kujua mwenyewe; hutaweza kuyakataa, na utashawishika kikamilifu. Je haya si mamlaka ya neno? Haya ndiyo matokeo yanayopatikana kwa kazi ya wakati huu ya neno. Kwa hivyo, mwanadamu hawezi kuokolewa kikamilifu kutoka kwa dhambi zake kwa kuponya magonjwa na kukemea mapepo na hawezi kufanywa mkamilifu kabisa kwa udhihirisho wa ishara na maajabu. Mamlaka ya kuponya na kukemea mapepo yanapatia mwanadamu neema tu, lakini mwili wa mwanadamu bado ni wa Shetani na tabia potovu za kishetani zitabaki ndani ya mwanadamu. Kwa maneno mengine, yale ambayo hayajatakaswa bado ni ya dhambi na uchafu. Ni baada tu ya mwanadamu kufanywa safi kupitia kwa maneno ndipo atakapotwaliwa na Mungu na kutakaswa. Wakati mapepo yalikemewa kutoka kwa mwanadamu na alikombolewa, hii ilimaanisha tu kwamba alipokonywa kutoka kwa mikono ya Shetani na kurudishwa kwa Mungu. Hata hivyo, hajafanywa msafi ama kubadilishwa na Mungu, anabaki mpotovu. Ndani ya mwanadamu bado kuna uchafu, pingamizi na uasi; mwanadamu amerudi tu kwa Mungu kupitia kwa ukombozi, lakini mwanadamu hana maarifa kumhusu na bado anamkataa na kumsaliti Mungu. Kabla ya mwanadamu kukombolewa, sumu nyingi ya Shetani ilikuwa imepandwa ndani yake tayari. Baada ya miaka mingi ya upotovu wa Shetani, mwanadamu tayari ana asili ndani yake inayompinga Mungu. Hivyo, mwanadamu atakapokombolewa, hakitakuwa kitu kingine ila ni ukombozi, ambapo mwanadamu ananunuliwa kwa gharama kuu, lakini asili ya sumu ndani yake haijaondolewa. Mwanadamu ambaye amechafuliwa lazima apitie mabadiliko kabla ya kuwa wa kustahili kumtumikia Mungu. Kupitia kazi hii ya kuadibu na hukumu, mwanadamu atakuja kujua hali yake kamili ya uchafu na upotovu ndani Yake, na ataweza kubadilika kabisa na kuwa msafi. Ni hivi tu ndivyo mwanadamu ataweza kustahili kurudi katika kiti cha enzi cha Mungu. Kazi yote ifanywayo siku hii ya leo ni ili mwanadamu afanywe msafi na kubadilika; kupitia hukumu na kuadibiwa na neno, na pia kutakaswa, mwanadamu anaweza kuutupa nje upotovu wake na kufanywa safi. Badala ya kuichukua hatua hii ya kazi kuwa ile ya wokovu, itafaa zaidi kusema kuwa ni kazi ya utakaso. Kwa kweli hatua hii ni ile ya ushindi na pia hatua ya pili ya wokovu. Mwanadamu anatwaliwa na Mungu kupitia hukumu na kuadibu na neno; kwa kutumia neno kusafisha, hukumu na kufichua, uchafu wote, fikira, nia, na matumaini ya mtu mwenyewe katika moyo wa mwanadamu zinafuliwa. Ingawa mwanadamu amekombolewa na kusamehewa dhambi zake, inachukuliwa kuwa Mungu hakumbuki makosa ya mwanadamu na kutomtendea mwanadamu kulingana na makosa yake. Hata hivyo, mwanadamu anapoishi katika mwili na hajaachiliwa huru kutoka kwa dhambi, ataendelea tu kutenda dhambi, akiendelea kufunua tabia yake potovu ya kishetani. Haya ndiyo maisha ambayo mwanadamu anaishi, mzunguko usiokoma wa dhambi na msamaha. Wengi wa wanadamu wanatenda dhambi mchana kisha wanakiri jioni. Hivyo, hata kama sadaka ya dhambi ni ya manufaa kwa binadamu milele, haitaweza kumwokoa mwanadamu kutoka kwenye dhambi. Ni nusu tu ya kazi ya wokovu ndiyo imemalizika, kwani mwanadamu bado yuko na tabia potovu. Kwa mfano, wakati ambapo watu walijua kwamba walitoka kwa Moabu, walitoa maneno ya malalamiko, hawakutafuta tena uzima, na wakawa baridi kabisa. Je, hili halionyeshi kwamba bado hawawezi kutii kwa ukamilifu kutawaliwa na Mungu? Je, hii siyo tabia ya kishetani ya upotovu kabisa? Ulipokuwa hupitii kuadibu, mikono yako iliinuliwa juu zaidi ya wengine wote, hata ile ya Yesu. Na ulilia kwa sauti kubwa: Kuwa mwana mpendwa wa Mungu! Kuwa mwandani wa Mungu! Ni heri tufe kuliko kumtii Shetani! Muasi Shetani wa zamani! Liasi joka kuu jekundu! Acha joka kuu jekundu lianguke kabisa kutoka mamlakani! Acha Mungu atufanye kamili! Vilio vyako vilikuwa vikubwa zaidi ya wengine. Lakini kisha zikaja nyakati za kuadibu na, mara tena, tabia ya upotovu ya watu ilifichuliwa. Kisha, vilio vyao vikakoma, na hawakuwa tena na azimio. Huu ni upotovu wa mwanadamu; unaingia ndani zaidi kuliko dhambi, ulipandwa na Shetani na umekita mizizi ndani zaidi ya mwanadamu. Sio rahisi kwa mwanadamu kuzifahamu dhambi zake; mwanadamu hawezi kufahamu asili yake iliyokita mizizi. Ni kupitia tu katika hukumu na neno ndipo mabadiliko haya yatatokea. Hapo tu ndipo mwanadamu ataendelea kubadilika kutoka hatua hiyo kuendelea. Mwanadamu alipiga kelele hivyo wakati uliopita kwa sababu mwanadamu hakuwa na ufahamu wa tabia yake potovu ya asili. Huo ndio uchafu ulio ndani ya mwanadamu. Kotekote katika kipindi kirefu hivyo cha hukumu na kuadibu, mwanadamu aliishi katika mazingira ya mvutano. Je, haya yote hayakutimizwa kupitia kwa neno? Wewe pia hukulia kwa sauti ya juu kabla ya majaribio ya watendaji huduma? Ingia katika ufalme! Wale wote ambao wanalikubali jina hili wataingia katika ufalme! Wote watashiriki Mungu! Wakati ambapo majaribio ya watendaji huduma yalikuja, hukulia tena. Mwanzoni, wote walilia, “Mungu! Popote Uniwekapo, nitatii kuongozwa na Wewe.” Baada ya kusoma maneno ya Mungu, “Nani atakuwa Paulo Wangu?” mwanadamu alisema, “Niko radhi!” Kisha akayaona maneno, “Na kuhusu imani ya Ayubu?” Kwa hiyo akasema, “Niko radhi kuichukua imani ya Ayubu. Mungu, tafadhali nijaribu!” Majaribio ya watendaji huduma yalipokuja, alizirai mara moja na nusura angekosa kusimama tena. Baada ya hilo, uchafu ndani ya moyo wa mwanadamu ulipungua polepole. Je, hili halikutimizwa kupitia kwa neno? Kwa hiyo, kile ambacho mmepitia wakati wa sasa ni matokeo ambayo hutimizwa kupitia kwa neno, hata makuu zaidi ya yale ambayo hutimizwa kupitia kwa Yesu kufanya ishara na maajabu. Utukufu wa Mungu na mamlaka ya Mungu Mwenyewe ambayo ninyi huona hayaonekani tu kupitia kwa usulubishaji, uponyaji wa magonjwa na ufukuzaji wa pepo, lakini zaidi kupitia kwa hukumu Yake kwa neno. Hili hukuonyesha wewe kwamba sio tu ufanyaji wa ishara, uponyaji wa magonjwa na ufukuzaji wa pepo ndiyo mamlaka na nguvu za Mungu, bali hukumu kwa neno unaweza kuwakilisha bora mamlaka ya Mungu na kufichua uweza Wake.
Kile ambacho mwanadamu amepata sasa—kimo cha mwanadamu leo, maarifa yao, upendo, uaminifu, utiifu, na pia kuona kwao—ni matokeo yanayopatikana kupitia hukumu kwa neno. Kwamba unaweza kuwa na uaminifu na kubaki umesimama mpaka siku hii ipatikane kwa kupita neno. Hivi sasa mwanadamu anaona kuwa kazi ya Mungu kupata mwili ni ya ajabu kweli. Kuna mengi ambayo hayawezi kupatikana na mwanadamu; ni mafumbo na maajabu. Kwa hivyo, wengi wamejiwasilisha. Wengine hawajawahi kujiwasilisha kwa mwanadamu yeyote kutoka siku za kuzaliwa kwao, ilhali wanapoyaona maneno ya Mungu siku hii, wanajiwasilisha kikamilifu bila kujua wamefanya vile, na hawajaribu kuchunguza au kusema chochote kingine. Binadamu wameanguka chini ya neno na wamesujudu chini ya hukumu kwa neno. Kama Roho wa Mungu angemwongelesha mwanadamu moja kwa moja, wote wangejiwasilisha kwa sauti hiyo, na kuanguka chini bila maneno ya ufunuo, vile Paulo alivyoanguka chini kukiwa na nuru alipokuwa akisafiri kwenda Damaski. Mungu angeendelea kufanya kazi kwa njia hii, mwanadamu hangeweza kutambua upotovu wake kupitia kwa hukumu katika neno na kupata wokovu. Ni kwa kupata mwili pekee ndiyo Ataweza kuwasilisha maneno Yake Mwenyewe kwa masikio ya wale wote ambao wana masikio waweze kuyasikia maneno Yake na kupokea kazi Yake ya hukumu kupitia kwa neno. Hayo tu ndio matokeo yanayopokewa na neno Lake, badala ya kutokea kwa Roho ikimtisha mwanadamu kuwasilisha. Ni kupitia tu kwa kazi ya vitendo na ya ajabu ndio tabia ya mwanadamu, iliyofichika ndani zaidi kwa enzi nyingi, ifichuliwe kabisa ili mwanadamu aitambue na kuibadilisha. Hili ndiyo kazi ya vitendo ya Mungu mwenye mwili wa Mungu; Ananena na kutekeleza hukumu juu ya mwanadamu kupitia kwa neno. Haya ndiyo mamlaka ya Mungu mwenye mwili na umuhimu wa Mungu kupata mwili. Inafanyika kuonyesha mamlaka ya Mungu mwenye mwili, matokeo yanayopatikana na kazi ya neno, na kwamba Roho Amekuja kwa mwili; Anaonyesha mamlaka Yake kupitia hukumu juu ya mwanadamu kwa neno. Ingawa mwili Wake ni hali ya nje ya mwanadamu wa kawaida, ni matokeo ambayo neno Lake linapokea ndiyo yanamwonyesha mwanadamu kuwa Amejaa mamlaka, kwama ni Mungu Mwenyewe na kwamba maneno Yake ni maonyesho ya Mungu Mwenyewe. Hii inaonyesha wanadamu wote kuwa Yeye ni Mungu Mwenyewe, Mungu Mwenyewe Aliyekuwa mwili, na kwamba Asikosewe na yeyote. Hakuna anayeweza kuepuka hukumu Yake kupitia kwa neno, na hakuna nguvu ya giza inayoweza kutamalaki juu ya mamlaka Yake. Mwanadamu anamtii Yeye kabisa kwa sababu Yeye ni Neno aliyepata mwili, kwa sababu ya mamlaka Yake, na kwa sababu ya hukumu Yake kwa neno. Kazi iliyoletwa na mwili Wake uliokuwa mwili ni mamlaka ambayo Anamiliki. Anakuwa mwili kwani mwili pia unaweza kuwa na mamlaka, na Anaweza kutekeleza kazi kati ya wanadamu katika halii ya njia halisi, inayoonekana na kuguswa na mwanadamu. Kazi kama hii ni ya ukweli kuliko kazi ingine yoyote ifanywayo moja kwa moja na Roho wa Mungu Aliye na mamlaka yote, na matokeo Yake ni dhahiri pia. Hii ni kwa sababu mwili Wake unaweza kuongea na kufanya kazi kwa njia halisi; hali ya nje ya mwili Wake haina mamlaka yoyote na inaweza kukaribiwa na mwanadamu. Dutu Yake inabeba mamlaka, lakini mamlaka Yake hayaonekani kwa yeyote. Anaponena na kufanya kazi, mwanadamu hana uwezo wa kutambua uwepo wa mamlaka Yake; hili ni nzuri kwa kazi Yake hata zaidi. Na kazi yote kama hiyo inaweza kupata matokeo. Ingawa hakuna mwanadamu anayefahamu kuwa Anayo mamlaka ama kuona kuwa Hastahili kukosewa ama kuona hasira Yake, kupitia mamlaka Yake yaliyofichika na hasira na hotuba ya uma, Anapata matokeo yaliyotarajiwa ya neno Lake. Kwa maneno mengine, kupitia kwa tani ya sauti Yake, ukali wa hotuba Yake, na hekima ya maneno Yake, mwanadamu anashawishika kabisa. Kwa njia hii, mwanadamu anawasilisha kwa neno la Mungu mwenye mwili wa Mungu, ambaye anaonekana kutokuwa na mamlaka, hivyo kufikia lengo Lake la wokovu kwa mwanadamu. Huu ndio umuhimu mwingine wa kuingia Kwake katika mwili: kuongea na ukweli zaidi na kukubali ukweli wa neno Lake kuwa na athari juu ya mwanadamu ili kushuhudia nguvu ya neno la Mungu. Kwa hivyo kazi hii, isipofanywa kupitia kupata mwili, haitakuwa na matokeo hata kidogo na haitaweza kuokoa watenda dhambi kikamilifu. Mungu Asipokuwa mwili, Atabaki kama Roho bila kuonekana au kuguswa na mwanadamu. Mwanadamu ni kiumbe wa mwili, na mwanadamu na Mungu ni wa dunia mbili tofauti na ni tofauti kwa asili. Roho wa Mungu hana uwiano na mwili wa mwanadamu, na hakuna uhusiano unaoweza kuwepo kati yao; pia, mwanadamu hawezi kuwa roho. Hivyo, Roho wa Mungu lazima ageuke mmoja wa viumbe na kufanya kazi yake ya asili. Mungu anaweza kujipandisha mahali pa juu zaidi na pia aweze kunyenyekea na kuwa mwanadamu aliyeumbwa, kufanya kazi na kuishi kati ya wanadamu, laikini mwanadamu hawezi kupanda juu na kuwa roho na pia kuteremka chini. Kwa hivyo, Mungu lazima awe mwili ili atekeleze kazi Yake. Kama ilivyokuwa wakati wa kuingia katika mwili mara ya kwanza, mwili wa Mungu mwenye mwili pekee ndio unaoweza kumkomboa mwanadamu kupitia kusulubiwa, ilhali hakuna uwezo wa Roho wa Mungu kusulubiwa kama sadaka ya dhambi kwa mwanadamu. Mungu Angekuwa mwili moja kwa moja ili kuwa sadaka ya dhambi kwa mwanadamu, lakini mwanadamu hangepanda mbinguni moja kwa moja kuchukua sadaka ambayo Mungu alikuwa amewaandalia. Hivyo, lazima Mungu asafiri kwenda na kurudi kati ya mbingu na nchi, badala ya kumwacha mwanadamu apande mbinguni kuchukua wokovu huu, kwani mwanadamu alikuwa ameanguka na hangepanda mbinguni, ama hata kupata sadaka ya dhambi. Kwa hivyo, ilikuwa lazima kwa Yesu kuja kati ya wanadamu na binafsi kufanya kazi ambayo mwanadamu hangeweza kukamilisha. Kila wakati ambapo Mungu aligeuka kuwa mwili, ilikuwa lazima kabisa Afanye hivyo. Iwapo hatua yoyote ingetekelezwa moja kwa moja na Roho wa Mungu, Hangevumilia ukosefu wa hadhi unaoambatana na kupata mwili.
Katika hatua hii ya mwisho ya kazi, matokeo yanapatikana kupitia kwa neno. Kupitia kwa neno, mwanadamu anaelewa mafumbo mengi na kazi ya Mungu katika vizazi vilivyopita; kupitia kwa neno, mwanadamu anapewa nuru na Roho Mtakatifu; kupitia kwa neno, mwanadamu anapata kuelewa mafumbo ambayo hayajawahi kuelezwa na vizazi vilivyopita, na pia kazi za manabii na, mitume wa enzi zilizopita, na kanuni ambazo walitumia kufanya kazi; kupitia kwa neno, mwanadamu anatambua tabia ya Mungu Mwenyewe, na pia uasi na pingamizi ya mwanadamu, na kujua dutu yao. Kupitia kwa hatua hizi za kazi na maneno yote yaliyonenwa, mwanadamu anatambua kazi ya Roho Mtakatifu, kazi ya mwili wa Mungu, na zaidi ya hayo, tabia Yake yote. Maarifa yako ya kazi ya usimamizi wa Mungu wa kupita miaka elfu sita ulitwaliwa kupitia kwa neno. Je, maarifa yako hayakuwa ya fikira zako za awali na mafanikio kwa kuyaweka kando pia yalipatikana kupitia neno? Katika hatua ya awali, Yesu Alifanya ishara na maajabu, lakini sio hivyo katika hatua hii. Je si kuelewa kwako kwa nini Hafanyi hivyo pia kulipatikana kupitia neno? Kwa hivyo, maneno yanenwayo katika hatua hii, yanashinda kazi iliyofanywa na mitume na manabii wa vizazi vilivyopita. Hata unabii uliotabiriwa na manabii haungeweza kupata matokeo haya. Manabii waliongelea unabii pekee, ya kile kitakachotendeka hapo baadaye, lakini sio kazi ambayo Mungu angefanya katika wakati huo. Hawakuongea kuongoza mwanadamu katika maisha yao, kuhifadhi ukweli juu ya mwanadamu ama kumfichulia mwanadamu mafumbo, ama hata kutawaza maisha. Kwa maneno yaliyonenwa katika hatua hii, kuna unabii na ukweli, lakini hasa yanafanya kazi ya kutawaza maisha juu ya mwanadamu. Maneno ya wakati huu sio kama unabii wa manabii. Hii ni hatua ya kazi isiyo ya unabii ila ya maisha ya mwanadamu, kubadili tabia ya maisha ya mwanadamu. Hatua ya kwanza ilikuwa kazi ya Yehova kutengeneza njia ya mwanadamu kuabudu Mungu duniani. Ilikuwa kazi ya kuanzisha kutafuta chanzo cha kazi duniani. Wakati huo, Yehova aliwafunza Waisraeli kuiheshimu Sabato, kuwaheshimu wazazi wao na kuishi kwa amani na wengine. Hii ilikuwa kwa sababu wanadamu wa wakati huo hawakuwa wanaelewa kiini cha mwanadamu, wala hawakuelewa wanavyopaswa kuishi duniani. Ilikuwa lazima Kwake katika hatua ya kwanza ya kazi kuwaongoza wanadamu katika maisha yao. Yote yale Yehova aliwazungumzia hayakuwa yamewahi kujulikana kwa binadamu ama kuwa katika umiliki wao. Wakati huo, manabii wengi walisimamishwa kuongelea unabii, yote kutengenezwa chini ya uongozi wa Yehova. Hii ilikuwa sehemu ya kazi hiyo. Katika hatua ya kwanza, Mungu hakuwa mwili, hivyo Alizungumza na makabila yote na mataifa kupitia kwa manabii. Yesu alipofanya kazi Yake katika huo wakati, Hakuzungumza sana kama wakati huu wa leo. Kazi hii ya neno katika siku za mwisho haijafanyika katika enzi na vizazi vilivyopita. Ingawa Isaya, Danieli na Yohana walitabiri utabiri mwingi, unabii huo ulikuwa tofauti kabisa na maneno yazungumzwayo sasa. Walichoongelea ulikuwa unabii pekee, lakini maneno ya sasa sio unabii. Iwapo Ningebadilisha Ninayoongea sasa yawe unabii, je mngeweza kuyaelewa? Iwapo ningezungumzia mambo baada ya Mimi kuondoka, utawezaje kupata kuelewa? Kazi ya neno haikuwahi kufanyika wakati wa Yesu ama Enzi ya Sheria. Labda wengine wanaweza kusema, “Je Yehova hakuzungumza maneno pia katika wakati wa kazi Yake? Juu yaa kuponya magonjwa, kukemea mapepo na kufanya ishara na maajabu, je Yesu hakuzungumza katika wakati huo?” Kuna tofauti katika vile maneno yananenwa. Ni nini ndiyo ilikuwa dutu ya maneno yaliyonenwa na Yehova? Alikuwa tu anawaongoza wanadamu katika maisha yao duniani, ambayo hayakuwa yanahusiana na mambo ya kiroho katika maisha. Ni kwa nini inasemekana kuwa maneno ya Yehova yalitangazwa katika sehemu zote? Neno “kufundisha” linamaanisha kuwaambia waziwazi na kuamrisha moja kwa moja. Hakupa mwanadamu maisha; ila, Alimchukua mwanadamu kwa mkono na kumfunza jinsi ya kumheshimu sana. Hakukuwa na mafumbo. Kazi ya Yehova katika Israeli haikuwa kushughulika na ama kumwadhibu mwanadamu ama kutoa hukumu na kuadibu; ilikuwa kuongoza. Yehova alimwambia Musa awaeleze watu Wake wakusanye mana jangwani. Kila asubuhi kabla ya jua kuchomoza, walikuwa wakusanye mana, iliyotosha tu kuliwa siku hiyo. Mana haingewekwa hadi siku inayofuata, kwani ingeoza. Hakuwafunza wanadamu kufichua asili zao, na Hakufichua mawazo yao na fikira. Hakuwabadilisha wanadamu ila tu aliwaongoza katika maisha yao. Katika wakati huo, mwanadamu alikuwa kama mtoto; mwanadamu hakuelewa chochote na angefanya hatua za kuelekezwa; kwa hivyo, Yehova aliamuru tu sheria kuongoza watu.
Iwapo unataka kueneza injili ili wale wote wanaotafuta kwa moyo wa kweli wapate maarifa ya kazi inayofanywa katika siku hii na kushawishika kabisa, lazima uielewe hadithi ya ndani, dutu na umuhimu wa kazi iliyofanywa katika kila hatua. Kwa kusikia ushirika wako, wataelewa kazi ya Yehova na kazi ya Yesu na, zaidi ya hayo, kazi yote ya Mungu wa leo, na vilevile uhusiano na tofauti kati ya hatua hizo tatu za kazi, ili kwamba, baada ya wao kusikiza, wataona kuwa hakuna hatua yoyote kati ya hizo tatu inahitilafiana na nyingine. Kwa hakika, yote yamefanywa na Roho mmoja. Ingawa Wanafanya kazi katika enzi tofauti , maudhui ya kazi Wanayotekeleza ni tofauti, na maneno Wanayozungumza pia ni tafauti, kanuni ambazo Wanafanya kazi nazo ni sawa. Haya ndiyo maono makuu zaidi ambayo watu wote wanapaswa kuelewa.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Jumapili, 17 Februari 2019

Jinsi Hatua ya Pili ya Kazi ya Ushindi Huzaa Matunda

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Jinsi Hatua ya Pili ya Kazi ya Ushindi Huzaa Matunda

Hatua ya kazi ya watenda-huduma ni hatua ya kwanza ya kazi ya ushindi; kwa sasa hii ni hatua ya pili ya kazi ya ushindi. Kwa nini ukamilifu unajadiliwa katika kazi ya ushindi? Ni kuujenga msingi kwa ajili ya siku za baadaye—kwa sasa hii ni hatua ya mwisho katika kazi ya kushinda, na baada ya hii, kazi ya kuwakamilisha watu itaanza rasmi wakati watakuwa wanapitia dhiki kuu. Jambo la msingi sasa ni ushindi; hata hivyo, hii pia ni hatua ya kwanza ya kukamilisha, kukamilisha ufahamu na utii wa watu, ambayo kwa kweli bado yanajenga msingi wa kazi ya kushinda. Kama unataka kukamilishwa, lazima uwe na uwezo wa kusimama imara katikati ya mateso ya siku za baadaye na uziweke nguvu zako zote katika kupanua hatua yenye kufuata ya kazi. Huku ni kukamilishwa, na huo ndio wakati ambao watu watakuwa wamepatwa na Mungu kabisa. Kile kinachojadiliwa hivi sasa ni kushindwa, ambako pia ni kukamilishwa; hata hivyo, kile kinachofanywa sasa ni msingi wa kukamilishwa katika siku za baadaye. Ili kufanywa mkamilifu, lazima watu wapitie mashaka, na lazima wayapitie juu ya msingi wa kushindwa. Kama watu hawana msingi huu wa sasa, kama hawajashindwa kikamilifu, basi itakuwa vigumu kwao kusimama hadi hatua inayofuata. Kushindwa tu si kufikia lengo la mwisho—ni kushuhudia kwa Mungu tu mbele ya Shetani. Kukamilishwa ni lengo la mwisho, na kama bado hujakamilishwa, basi utahesabiwa kama asiyefaa. Wanapokabiliwa na mashaka katika siku za baadaye, ndipo tu kimo halisi cha watu kitaonekana, yaani, usafi halisi wa upendo wako kwa Mungu utaonekana. Sasa, watu wote husema: “Haidhuru kile Mungu anachofanya sisi tutatii, nasi tuko tayari kuwa foili, kuchochea ukuu wa Mungu, tabia ya Mungu. Haidhuru kama Anaifadhili neema Yake juu yetu au la ama kama Anatulaani au Anatuhukumu, tutatoa shukrani Kwake.” Wewe kusema hili sasa ni ufahamu kiasi tu, lakini kama linaweza kutumika kwa hali halisi linategemea kama ufahamu wako kweli ni wa kweli. Kwamba watu sasa wameona na kueleweka mambo haya ni mafanikio ya kazi ya ushindi; kama unaweza kukamilishwa au la itaonekana hasa wakati mashaka yanakuja juu yako. Wakati huo itaonekana kama una upendo wa kweli kwa Mungu katika moyo wako au la, na kama kweli unao upendo safi kwa ajili Yake, utasema: “Sisi ni foili tu; sisi ni viumbe katika mikono ya Mungu.” Na wakati unapoieneza injili kwa mataifa mengine, utasema: “Mimi ni mtendaji-huduma tu na ni kwa sababu ya tabia zetu potovu ndiyo Mungu alinena sana kiasi kwamba tumeiona tabia Yake ya haki. Kama Mungu hangesema mambo hayo hatungeweza kumwona Yeye, hatungeweza kuionja hekima Yake, na hatungeweza kuupata wokovu mkuu mno, baraka kubwa mno. ”Kama kweli unayo maoni hayo, basi unafanya vizuri. Sasa umesema mambo mengi bila kufikiri na daima unasema wito kwa sauti kubwa: "Sisi ni foili na watenda-huduma; tuko tayari kushindwa na kuwa mashahidi wakubwa sana wa Mungu…” Huwezi tu kupaaza sauti na umalize bila kulifikiria tena, na uthibitishe kwamba wewe ni mtu mwenye kimo. Lazima uwe na ufahamu wa kweli, na ufahamu wako unapaswa kujaribiwa.
Tafakari uzoefu katika kipindi hiki cha wakati na uangalie tena mambo haya ambayo Nimeyasema, kisha uyalinganishe kile unachofanya. Ni kweli kabisa kwamba wewe ni foili kabisa! Ni kiwango gani cha ufahamu ulicho nacho sasa? Mawazo yako, fikra, tabia, maneno na matendo yako, kila kitu ambacho unaishi kwa kudhihirisha—si yot tu ni foili kwa haki na utakatifu wa Mungu? Si kila kitu ambacho kinafunuliwa kiko katika maneno ya sasa ya Mungu kuhusu tabia potovu ya wanadamu? Tabia ya Mungu yenye haki na utakatifu vinaonyesha kupitia mawazo yako na nia zako, na kupitia kwa yale unayoyafunua. Yeye, pia Akiishi katika nchi ya uchafu, hajatiwa waa na uchafu hata kidogo. Anaishi katika dunia ile ile chafu kama wewe, lakini Anamiliki mantiki na umaizi; Anachukia uchafu. Wewe mwenyewe huwezi kuona mambo machafu katika maneno na matendo yako mwenyewe lakini Yeye Anaweza—Anaweza kukuonyesha. Mambo hayo yako ya zamani—ukosefu wako wa kukuza, umaizi, na hisia, maisha yako ya kuelekea nyuma—yote yamefunuliwa kupitia kwa kufichua Kwake kwa mambo hayo sasa. Mungu Amekuja duniani kufanya kazi kwa namna hii, ili watu wauone utakatifu Wake na tabia Yake ya haki. Anakuhukumu na Kukuadibu na Kukufanya ujielewe. Wakati mwingine asili yako yenye pepo mbaya huonekana na Anaweza kukuonyesha. Anakijua kiini cha wanadamu sana. Anaishi kama wewe unavyoishi, Anakula chakula sawa na wewe, Anaishi katika aina ya nyumba kama wewe, lakini Anajua mengi zaidi kukuliko. Lakini kile Anachochukia hasa ni maisha ya filosofia ya watu na upotovu na udanganyifu wao. Anavichukia vitu hivi na Yeye hana nia ya kuvitambua. Yeye hasa anachukia maathiriano ya kimwili ya watu. Ingawa Haelewi kabisa baadhi ya maarifa ya jumla ya maathiriano wa binadamu, Anafahamu kikamilifu wakati ambapo watu wanafichua baadhi ya tabia zao potovu. Katika kazi Yake, Ananena na kuwafundisha watu kupitia mambo haya ndani yao, na kupitia haya Yeye huwahukumu watu na kufichua tabia yake yenye haki na takatifu. Hivi ndivyo watu wanakuwa foili kwa ajili ya kazi Yake. Ni Mungu mwenye mwili tu ambaye Anaweza kufichua kila aina ya tabia potovu za mwanadamu na nyuso zote mbaya za Shetani. Yeye hakuadhibu, Angeweza tu kukufanya wewe uwe foili kwa utakatifu wa Mungu. Huwezi kusimama imara mwenyewe kwa sababu wewe ni mchafu sana. Anaongea kupitia mambo yale ambayo watu wanadhihirisha na Yeye huyafunua ili watu waweze wajue jinsi Mungu ni mtakatifu. Hataacha uchafu hata kidogo ndani ya binadamu, sio hata wazo dogo zaidi chafu katika mioyo yao au maneno na matendo ambayo si sambamba na mapenzi Yake. Kupitia kwa maneno Yake, hakuna uchafu na hakuna kitu ndani ya mtu kitabaki—vyote vitawekwa wazi. Ni hapo tu ndipo utakapoona ya kwamba Yeye kweli yuko tofauti na watu. Anachukizwa kabisa na uchafu hata kidogo zaidi katika wanadamu. Wakati mwingine watu hata hawaelewi, na wanasema: “Kwa nini Wewe una hasira kila mara? Mungu, kwa nini Huujali udhaifu wa wanadamu? Kwa nini Huna msamaha kidogo kwa wanadamu? Kwa nini Hujali hisia za mwanadamu? Unajua jinsi watu walivyo wapotovu, hivyo kwa nini bado Unawatendea watu kwa njia hii?” Anachukizwa na dhambi; Anachukia dhambi. Yeye anachukizwa hasa na uasi wowote unaoweza kuwa ndani yako. Wakati ambapo unafichua tabia ya uasi Anachukizwa kupita kadiri. Ni kwa kupitia mambo haya ambapo tabia Yake na asili vinaweza kuonyeshwa. Unaipolinganisha na wewe mwenyewe, utaona kwamba ingawa Anakula chakula sawa, Anavaa mavazi sawa, na Ana starehe sawa na watu, ingawa Anaishi kandokando na pamoja na watu, Yeye si sawa. Je, hii si maana halisi ya kuwa foili? Ni kupitia mambo haya kwa watu ndiyo maana nguvu kuu ya Mungu inaonekana kwa urahisi sana; ni giza ambalo huchochea kuwepo kwa mwanga wa thamani.
Bila shaka Yeye hawatumii ninyi kwa makusudi kama foili, lakini wakati ambapo kazi hii inaonyesha matokeo, inaonyesha uasi wa wanadamu kama foili kwa ajili ya tabia ya Mungu yenye haki. Ni kwa sababu mmetenda kama foili ndiyo maana mna nafasi ya kujua maonyesho asili ya tabia ya Mungu yenye haki. Ni kwa sababu ya uasi wenu ndiyo maana mmepatwa na hukumu na kuadibu mara kwa mara; lakini pia ni kwa sababu ya uasi wenu ndiyo manaa mmetenda kama foili na mmepata neema kubwa sana ambayo Mungu amewakirimu. Ni uasi wenu ambao ni foili kwa uenyezi na hekima ya Mungu, na ni kwa sababu yake ndipo mmepata wokovu mkuu mno, baraka kubwa mno. Ingawa mmepokea hukumu Yangu mara kwa mara, pia mmepata wokovu mkuu ambao wale waliokuwa mbele yenu hawakuwahi kuupata. Kazi hii ni yenye maana ya ajabu sana kwenu. “Foili” hii kwa kweli ni yenye thamani sana kwenu—ni kwa sababu ya kutenda kama foili ndipo mmepata wokovu na neema. Je, si kuwa aina hii ya foili ya thamani sana? Je, si ni ya maana sana? Ni kwa sababu mnaishi katika ulimwengu sawa na Mungu, kwa sababu mnaishi naye katika nchi chafu ndipo mmekuwa foili Wake na mmepata wokovu wa ajabu sana. Kama Hangekuwa mwili, nani angekuwa na huruma kwenu, na nani angewatunza ninyi watu duni? Nani angewajali ninyi? Kama Mungu mwenye mwili hangekuwa anafanya kazi miongoni mwenu, ni wakati gani ambapo mngeweza kuupata wokovu huu ambao hakuna mtu yeyote amewahi kuupata awali? Kama Nisingekuwa mwili Niwajali na kuzihukumu dhambi zenu, si mgekuwa mmeanguka Kuzimuni muda mrefu uliopita? Kama Nisingekuwa mwili kujinyenyekeza miongoni mwenu, mngekuwa na haki gani kuwa foili kwa tabia ya Mungu yenye haki? Je, hamtendi kama foili kwa sababu Nimekuwa mwili kati yenu ili kwamba muweze kuupata wokovu mkuu mno? Si hiyo kabisa ni kwa sababu Nilikuwa mwili? Kama isingekuwa kwa ajili ya Mungu mwenye mwili akiishi miongoni mwenu, je, mngeweza kugundua kwamba mnaishi katika kuzimu duniani, vibaya zaidi kuliko nguruwe au mbwa? Je, si hukumu na kuadibu ambako mmepata kumekuwa kwa sababu ninyi ni foili kwa ajili ya kazi Yangu katika mwili? Kazi ya kuwa foili inafaa sana kwenu kwa kuwa mmeupata wokovu wa hukumu ya Mungu kwa sababu ya hii. Je, hamhisi kuwa ni baraka ya maisha yenu kuweza kutenda kama foili wenye sifa? Yote ambayo mmeyafanya ni kazi ya kuwa foili, lakini mmepata wokovu ambao hamjawahi kuupata au kufikiri kabla. Kuwa foili ni wajibu wenu sasa, na baraka za milele mtakazozifurahia wakati ujao zitakuwa zawadi mnayostahili. Wokovu mnaoupata si ufahamu wa mara moja au maarifa leo, lakini ni baraka zaidi, mwendelezo wa milele wa maisha. Ingawa ni kupitia kuwa foili ndiyo mnashindwa, mnapaswa kujua kwamba wokovu huu, baraka hii ni kuwapata ninyi kabisa; ni ushindi na pia ili kuwaokoa bora zaidi. Kuwa foili ni ukweli, lakini ni kwa sababu ya uasi wenu ndiyo ninyi ni foili na mmepata baraka ambazo hakuna aliyewahi kuzipata. Leo, mnaona na kusikia, na kesho mtapata, na mtapokea baraka kubwa hata zaidi. Hivyo si kuwa aina hii ya foili jambo muhimu sana? Ni kupitia kwa foili ya tabia zenu za uasi ndiyo kazi ya sasa ya kushinda huzaa matunda, ambayo ni, kilele cha kuadibu na hukumu ya pili ni kuufanya uchafu na uasi wenu kuwa foili ili muweze kuiona tabia ya haki ya Mungu. Wakati mtakapokuwa watiifu kwa mara nyingine tena katika kuadibu na hukumu ya pili, tabia Yake yenye haki yote itafunuliwa wazi kwenu. Hiyo ni, wakati ambapo kukubali kwenu kazi ya ushindi kumefika mwisho utakuwa wakati ambapo mmetimiza wajibu wenu wa kuwa foili. Si kuamua jambo kuwahusu bila kujali kuwajua, lakini ni kuikamilisha kazi ya kwanza ya kushinda kupitia kwa wajibu wenu kama watenda-huduma, ikifichua tabia yenye haki ya Mungu, isiyokosewa. Kupitia kwa kutenda kwenu kama foili, kupitia kwa uasi wenu kama foili, matunda ya kazi ya pili ya ushindi yamepatikana. Tabia Yake yenye haki ambayo haikuwa imefunuliwa kwenu kikamilifu mara ya kwanza sasa imefunguliwa yote juu yenu ili muweze kuiona tabia Yake yote yenye haki, muone yote ambayo Yeye aliye, ambayo ni ya hekima ya kazi Yake, ajabu, na utakatifu na usafi. Matunda haya ya kazi Yake yamefanikishwa kupitia kwa vipindi tofauti vya ushindi pamoja na hatua mbalimbali za hukumu. Kadri hukumu Yake inavyofikia kilele chake, ndivyo Yeye anavyoweza kufichua tabia za uasi za watu na ndivyo Yeye anaweza kufikia matokeo ya ushindi. Tabia Yake yote ya haki imedhihirishwa kutoka miongoni mwa aina hii ya kazi ya kushinda. Kazi ya ushindi imetengwa katika hatua mbili ambazo zinatekelezwa katika nyakati tofauti na ziko katika viwango mbalimbali. Na bila shaka matokeo yanayopatikana pia ni tofauti; ambayo ni, kiwango cha utii wa watu kinakuwa cha kina zaidi na zaidi. Tangu wakati huu kuendelea hatimaye itawezekana kuwaleta watu kwenye njia sahihi ya kukamilishwa. Baada ya kazi yote ya ushindi kukamilika (wakati ambapo hukumu ya pili imepata matokeo yake ya mwisho) hatimaye Mungu hatawahukumu wanadamu tena, lakini atawataka waingie katika njia sahihi ya kupitia maisha. Hii ni kwa sababu hukumu inawakilisha ushindi, na aina ya ushindi ni hukumu na kuadibu.
Ni kwa Mungu kuwa mwili tu katika mahali palipo nyuma mno kimaendeleo na pachafu mno ndiyo Yeye anaweza kudhihirisha ukamilifu wote wa tabia Yake takatifu na yenye haki. Na kupitia kwa nini ndiyo tabia Yake yenye haki inadhihirishwa? Kupitia kwa hukumu ya dhambi za watu, hukumu ya Shetani, karaha kuelekea dhambi, na chuki kwa maadui Zake ambao wanaasi dhidi Yake na kumpinga Yeye. Kile ambacho Nasema leo ni kuhukumu dhambi za watu na maovu yao; ni kulaani uasi wa watu. Udanganyifu na upotovu wao, na maneno na matendo yao, mambo yote ambayo hayako sambamba na mapenzi Yake yatapitia hukumu, na uasi wa watu unaamuliwa kuwa wenye dhambi. Ananena kulingana na kanuni za hukumu, naye anadhihirisha tabia Yake yenye haki kwa kuhukumu maovu yao, kulaani uasi wao, na kufichua nyuso zao zote mbaya. Utakatifu unawakilisha tabia Yake ya haki; utakatifu Wake kwa kweli ni tabia Yake ya haki. Msingi wa maneno Yangu leo ni kuzungumza, kuhukumu, na kufanya kazi ya ushindi kutokana na tabia zenu potovu. Hii pekee ni kazi halisi, na hii pekee ndiyo inaweza kabisa kuufanya utakatifu wa Mungu uonekane kwa urahisi sana. Kama hukuwa na tabia potovu hata kidogo, Mungu hangekuhukumu, pia hungeweza kuiona tabia Yake ya haki. Kwa kuwa una tabia potovu, Mungu hatakuachilia. Ni kupitia kwa hili ndiyo utakatifu wake unafunuliwa. Kama uchafu na uasi wa watu ni mkubwa mno na Aliuona lakini hakusema neno na wala Hakukuhumu wala kukuadibu kwa maovu yako, ingeonyesha kuwa Yeye hakuwa Mungu hata kidogo kwa sababu Yeye hangechukia dhambi, lakini angekuwa tu mchafu kama wanadamu walivyo. Hukumu Yangu kwako leo ni kwa sababu ya uchafu wako; kuadibu Kwangu kwako leo ni kwa sababu ya upotovu na uasi wako. Si kwa ajili ya kupata mamlaka na ufahari kati yenu wala kuwadhulumu kimakusudi, lakini ni kwa sababu ninyi mnaoishi katika nchi ya uchafu mmepakwa matope na uchafu mwingi sana. Mmepoteza tu uadilifu wenu, ubinadamu wenu, na hamko tofauti na nguruwe wanaoishi katika maeneo maovu mno. Ni kwa sababu ya mambo haya ndani yenu ndiyo mnahukumiwa na kwamba hasira Yake imepatiliziwa juu yenu. Ni kwa sababu ya hukumu hizi ndiyo mmeweza kuona kwamba Mungu ni Mungu mwenye haki, kwamba Mungu ni Mungu mtakatifu. Ni kwa sababu ya utakatifu na haki yake ndiyo Amewahukumu kuwapatilizia hasira Zake juu yenu. Kwa sababu Yeye anaweza kudhihirisha tabia yake ya haki anapotazama uasi wa wanadamu, na kwa sababu Anaweza kudhihirisha utakatifu Wake anapotazama uchafu wa wanadamu, hii inatosha kuonyesha kuwa Yeye ni Mungu Mwenyewe ambaye ni mtakatifu na bila doa, lakini pia Anaishi katika nchi ya uchafu. Kama Yeye angekuwa mtu Anayejitia matope pamoja na watu na kama Asingekuwa na dalili zozote za utakatifu au tabia ya haki, Asingekuwa na sifa kuhukumu uovu wa wanadamu au kuwa hakimu wa wanadamu. Kama mwanadamu angemhukumu mwanadamu, isingekuwa kama kuzaba kofi uso wake wenyewe? Mtu anawezaje kuwa na haki ya kuhukumu aina sawa ya mtu, ambaye ni mchafu tu kama yeye? Yule tu ambaye anaweza kuwahukumu wanadamu wote wachafu ni Mungu mtakatifu Mwenyewe, na mwanadamu angewezaje kuzihukumu dhambi za mwanadamu? Mwanadamu angewezaje kuona dhambi za mwanadamu, na angewezaje kuwa na sifa zinazostahili kumshutumu mwanadamu? Kama Mungu hangekuwa na haki ya kuzihukumu dhambi za mwanadamu, basi Angewezaje kuwa Mungu mwenye haki mwenyewe? Wakati ambapo tabia potovu za watu zinadhihirishwa, Yeye ananena kuwahukumu, na ni wakati huo tu ndipo wanaweza kuona kwamba Yeye ni mtakatifu. Hukumu, kuadibiwa, na mfichuo wa dhambi za wanadamu—hakuna mtu mmoja au kitu kinaweza kuepuka hukumu hii. Yote ambayo ni machafu yanahukumiwa na Yeye. Ni kwa kupitia hili tu ndiyo tabia Yake inasemekana kuwa yenye haki. Vinginevyo, inawezaje kusemwa kwamba ninyi mnastahili kuitwa foili?
Kazi iliyofanywa katika Israeli ni tofauti kabisa na kazi ya leo. Yehova aliyaongoza maisha yao lakini hakuwahukumu wala kuwaadibu almradi inavyofanyika sasa kwa sababu wakati huo, watu walielewa kidogo mno kuhusu mambo ya dunia na walikuwa na tabia chache potovu. Wakati huo, Waisraeli walikuwa wanyenyekevu kwa Yehova katika kila namna. Wakati Alipowaamuru kujenga madhabahu wangeharakisha kufanya hivyo, na Alipowaamuru kuvaa mavazi ya makuhani wangetii. Wakati huo Yehova alikuwa tu kama mchungaji wao akiliongoza kundi la kondoo duniani, na kondoo wote walifuata mahali mchungaji aliwaongoza kula nyasi katika malisho. Yehova Aliyaongoza maisha yao; Alikuwa mwongozo kwa ajili ya chakula chao, mavazi, malazi, na usafiri. Huo haukuwa wakati wa kufichua tabia ya Mungu kwa sababu watu wa wakati huo walikuwa watoto wachanga, na kisha kulikuwa na watu wachache sana ambao walikuwa waasi au wapinzani, nao hawakuwa wametiwa matope mno. Hivyo hawangeweza kuwa foili kwa ajili ya tabia ya Mungu. Utakatifu wa Mungu unafichuliwa kwa watu katika nchi ya uchafu. Na sasa ni uchafu unaofichuliwa na watu katika nchi ya uchafu ambao Mungu huuhukumu. Kwa njia hii, kile Alicho kinaonyeshwa chote katika hukumu Yake. Na kwa nini Yeye huhukumu? Ni kwa sababu Anachukizwa na dhambi, na hivyo Yeye ana uwezo wa kutoa maneno ya hukumu. Kama Yeye hangechukizwa na uasi wa mwanadamu, Angekuwa mwenye ghadhabu sana? Kama hakungekuwa na maudhi, hakuna chuki ndani Yake, ikiwa watu ni waasi lakini hakuwajali, hiyo ingeonyesha kwamba Yeye alikuwa mchafu tu kama wachafu kama wanadamu. Sababu amabyo Yeye ana uwezo wa kuhukumu na kuwaadibu wanadamu ni kwamba Anakuchukizwa na uchafu. Kila kitu ambacho Anachukizwa nacho ni kile Yeye mwenyewe hamiliki. Kama Yeye pia angekuwa na upinzani na uasi ndani ya nafsi Yake, hangechukizwa na watu wapinzani na waasi. Kama Kazi Yake katika siku za mwisho ingekuwa bado inafanywa katika Israeli haingekuwa na umuhimu hata kidogo. Kwa nini kazi ya siku za mwisho inafanywa nchini China, mahali penye giza sana, iliyo nyuma zaidi kimaendeleo? Ni kufichua utakatifu na haki ya Mungu. Kwa ufupi, jinsi mahali palivyo penye giza zaidi ndipo panapoweza kutoa mwanga bora kwa utakatifu Wake. Ukweli ni kwamba kufanya yote haya ni kwa ajili ya kazi ya Mungu. Mnajua tu sasa kwamba Mungu aliye mbinguni ameshuka duniani na anasimama katikati yenu, na Amepewa umuhimu dhidi ya uchafu na uasi wenu, ili muanze kuwa na ufahamu wa Mungu—je, si hili linatia moyo pakubwa? Ukweli ni kwamba ninyi ni kundi la watu nchini China ambao mmechaguliwa, na kwa sababu watu hawa wamechaguliwa na wamefurahia neema ya Mungu, na kwa sababu watu hawa hawafai kufurahia neema Yake nyingi, inaonyesha kwamba yote haya yanatia moyo pakubwa kwenu. Mungu Amejidhihirisha na tabia Yake yote takatifu kwenu, na Ametawaza yote hayo juu yenu, Akiwaruhusu kufurahia baraka tele. Hamjaonja tu tabia Yake yenye haki, lakini la muhimu zaidi, mmeonja wokovu Wake pamoja na ukombozi Wake na upendo usio na kikomo, ili ninyi, wachafu zaidi ya watu wote, mmepokea neema kuu mno—si huku ni kubarikiwa? Je, si huku ni kutiwa moyo na Mungu? Ninyi ni wa hadhi ya chini sana na hamkufaa baraka kuu kama hii, lakini Mungu alikuwa na nia ya kukutia moyo. Je, huoni aibu? Kama huwezi kutimiza wajibu wako, mwishowe utajionea aibu kabisa. Utajiadibu. Kwa sasa Yeye hakuchapi wala kukuadhibu; mwili yako uko salama salimini, lakini mwishowe maneno Yake yatakuletea aibu kwako mwenyewe. Hadi sasa Sijawahi kumwadibu mtu yeyote hadharani. Nimenena kwa ukali, lakini Nimekuwaje kuwaelekea watu? Nimekuwa mwenye faraja, Nimewahimiza, na pia Nimewaonya. Hii haijakuwa kwa lengo lingine zaidi ila kuwaokoa. Inawezekana kuwa kwamba hamueilewi nia Yangu kwa kweli? Ninaposema hivi nyote mnapaswa kuelewa na mnapaswa kutiwa moyo kwa maneno haya. Kunao wengi ambao hatimaye wameelewa hili sasa: Je, baraka hii si kutenda kama kama foili? Je, si kuwa foili jambo lenye baraka kuliko mambo yote? Mwishowe, mtaeneza injili ifuatayo: “Sisi ni foili wa mfano hasa. Watawauliza: “Ni nini maana ya kuwa na foili wa mfano hasa?” Na kisha mtasema: “Sisi ambao tunaikamilisha kazi ya Mungu na kutumika kama foili kwa nguvu za Mungu—ni kupitia kwa uasi wetu ndiyo tunatumika kama foili kwa ajili ya tabia Yake yote yenye haki. Sisi ni vyombo vya huduma na viungo kwa kazi ya mwisho ya Mungu—sisi ni vifaa. “Wanaposikia hivyo, watavutiwa sana. Kisha mtasema: “Sisi pia ni vielelezo na mifano kwa ajili ya kuikamilisha kazi ya ulimwengu mzima, na kuwashinda wanadamu wote. Bila kujali kama ninyi ni watakatifu au wachafu, tumebarikiwa zaidi kuwaliko, kwa sababu tumemwona Mungu. Nguvu ya Mungu imechochewa kupitia nafasi Yake kutushinda sisi, na ni kwa sababu ya uchafu wetu ndipo tabia yake yenye haki imechochewa. Je, mna uwezo wa hilo? Hamna haki! Hii kabisa ni sisi kutiwa moyo na Yeye! Ingawa sisi si wenye kiburi, tuna fahari ya kumtukuza Mungu kwa sababu hakuna mtu mwingine yeyote anaweza kushuhudia ahadi hiyo kubwa mno, na hakuna mtu mwingine yeyote anaweza kufurahia baraka kubwa kama hiyo. Ni ajabu kwamba watu wachafu jinsi hii kweli wanaweza kufanya kazi ya foili katika usimamizi wa Mungu, na kwa kweli tunashukuru zaidi ya maneno yanavyoweza kueleza. Watauliza: “Kwa hiyo basi, kielelezo na mfano ni nini?” Nanyi mtasema: “Sisi ni waasi zaidi miongoni mwa wanadamu wote pamoja na kuwa wachafu mno. Sisi ni wale walio wapotovu kwa undani zaidi na Shetani na wenye maendeleo kidogo mno na binadamu duni kabisa ambao ni wa mwili. Sisi ni wa mfano hasa wenye taswira ya kutumiwa na Shetani. Sasa tumechaguliwa na Mungu kuwa wale ambao wameshindwa kwanza kati ya wanadamu. Tumeiona tabia ya Mungu yenye haki, tumeirithi ahadi Yake, na Yeye atawashinda watu zaidi kupitia kwetu. Hii ndiyo sababu sisi ni vielelezo na mifano kwa wale ambao wameshindwa kati ya wanadamu.” Huu ni ushuhuda wenu bora kabisa, na huu ni uzoefu wenu bora kabisa.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Vitabu

Jumamosi, 16 Februari 2019

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (3)

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (3)

Mungu amewaaminia wanadamu vitu vingi sana na Amezungumza bila kikomo juu ya kuingia kwao. Lakini kwa sababu ubora wa tabia ya watu ni duni mno, maneno mengi ya Mungu yameshindwa kuanza kustawi. Kuna sababu mbalimbali za huu ubora duni wa tabia, kama vile uharibifu wa mawazo na maadili ya binadamu, na kutokuwa na malezi mazuri; imani za usihiri zilizojaa moyoni mwa mwanadamu; mitindo ya maisha iliyopotoka ambayo imeweka maovu mengi katika sehemu ya ndani kabisa ya moyo wa mwanadamu; maarifa ya juujuu ya utamaduni, na takribani asilimia tisini na nane ya watu ambao hawana elimu ya utamaduni na, aidha, watu wachache sana wanaopata viwango vya juu vya elimu ya utamaduni, hivyo kimsingi watu hawajui ni nini maana ya Mungu au Roho, bali wana taswira hafifu ya Mungu na isiyoeleweka vizuri kama iliyopatikana kutoka kwa imani ya usihiri; ushawishi wenye madhara ambao maelfu ya miaka ya “roho wa juu sana wa utaifa” umeacha ndani kabisa ya moyo wa mwanadamu pamoja na fikira za kikabaila ambazo watu wamefungwa nazo na kutiwa minyororo, bila uhuru wowote, na kusababisha watu kutokuwa na hamasa au ustahimilivu, hawana shauku ya kusonga mbele, lakini badala yake wanakuwa baridi na kurudi nyuma, wakiwa na akili ya utumwa ambayo ina nguvu sana. Na kadhalika. Sababu hizi zimetengeneza taswira chafu na mbaya kwa mitazamo ya njozi, mawazo, maadili, na tabia ya binadamu. Inaonekana, wanadamu wanaishi katika dunia ya giza la kutisha, na hakuna anayetafuta kusonga mbele miongoni mwao, hakuna anayefikiria kwenda katika ulimwengu ulio bora. badala yake, wanaridhika na waliyo nayo maishani,[1] kutumia siku zao kuzaa na kuwalea watoto, wakikazana, wakitoka jasho, wakifanya kazi zao, wakiwa na njozi ya kuwa na familia ya raha na yenye furaha, ya upendo wa ndoa, ya watoto wenye upendo, ya maisha yenye furaha katika miaka yao ya uzeeni wanapoishi kwa kudhihirisha maisha yao kwa amani. … Kwa makumi, maelfu, makumi ya maelfu ya miaka hadi sasa, watu wamekuwa wakipoteza muda wao kwa njia hii, hakuna anayetengeneza maisha makamilifu, wanapigana tu wenyewe kwa wenyewe katika ulimwengu huu wa giza, wakipambana kupata umaarufu na utajiri, na kufanyiana njama wao kwa wao. Nani amewahi kutafuta mapenzi ya Mungu? Kuna mtu yeyote aliyewahi kutilia maanani kazi ya Mungu? Sehemu hizi zote za binadamu zinazomilikiwa na ushawishi wa giza zimekuwa asili ya mwanadamu tangu zamani, kwa hiyo ni vigumu sana kutekeleza kazi ya Mungu na hata watu hawana moyo wa kuzingatia kile ambacho Mungu amewaaminia leo. Vyovyote vile, Ninaamini kwamba watu hawatajali Ninapotamka maneno haya kwa vile kile Ninachokisema ni historia ya maelfu ya miaka. Kuzungumza juu ya historia kuna maana ya ukweli na, zaidi ya hayo, kashfa zinazojulikana kwa wote, sasa kuna maana gani kuzungumza kitu ambacho ni kinyume na ukweli? Lakini pia Naamini kwamba watu wenye akili, wanapoona maneno haya, wataamka na kujitahidi kwa ajili ya kuendelea mbele. Mungu hutumaini kwamba wanadamu wanaweza kuishi na kufanya kazi kwa amani na kuridhika huku wakati ule ule wakiweza kumpenda Mungu. Ni mapenzi ya Mungu kwamba binadamu wote waweze kuingia katika raha; zaidi ya hili, kuijaza nchi yote na utukufu wa Mungu ni shauku kubwa ya Mungu. Ni aibu tu kwamba wanadamu husalia washenzi na wasiotambua mambo, waliopotoshwa vibaya sana na Shetani hivi kwamba leo hawafanani tena na binadamu. Kwa hiyo mawazo ya binadamu, uadilifu na elimu huunda kiungo muhimu, pamoja na mafunzo katika kujua kusoma na kuandika utamaduni yakiunda kiungo cha pili, bora zaidi ya kuinua ubora wa tabia wa utamadani wa binadamu na kubadilisha mtazamo wao wa kiroho.
Kwa kweli, Mungu hahitaji mengi kutoka kwa binadamu, lakini kwa sababu pengo kati ya uhodari wa watu na kiwango anachohitaji Mungu ni kikubwa sana, watu wengi sana hutazama tu upande wa matakwa ya Mungu lakini hukosa uwezo wa kuyatimiza. Kipaji cha watu cha asili, pamoja na kile wanachojiandaa nacho baada ya kuzaliwa, kiko mbali sana na kutimiza matakwa ya Mungu. Bali kutambua tu wazo hili si suluhisho la hakika kufanikiwa. Maji ya mbali hayawezi kukata kiu ya sasa hivi. Hata watu wakijifahamu kuwa duni kuliko vumbi, kama hawana azimio la kuuridhisha moyo wa Mungu, sembuse kuifuata njia iliyoko mbele ili kutimiza matakwa ya Mungu, basi maarifa ya aina hiyo yana thamani gani? Je, si kama kuchota maji na chungio—juhudi isiyo na maana? Kiini cha kile Nisemacho kinahusu kuingia; hiyo ndiyo mada kuu.
Wakati wa kuingia kwa mwanadamu, maisha huwa ya kuchosha daima, yaliyojaa sifa za lazima zisizobadilika za maisha ya kiroho, kama vile kufanya maombi, kula na kunywa maneno ya Mungu kiasi, au kufanya mikusanyiko, ili watu wahisi daima kwamba kumwamini Mungu hakuleti raha kuu. Shughuli za kiroho kama hizo kila mara hutekelezwa kwa msingi wa tabia ya asili ya binadamu, ambao wamepotoshwa na Shetani. Ingawa wakati mwingine watu wanaweza kupokea nuru ya Roho Mtakatifu, kufikiri kwao kwa asili, tabia, mitindo ya maisha na mienendo bado imekita mizizi, na kwa hiyo asili yao husalia isiyobadilika. Shughuli za kishirikina ambazo watu wanashughulika nazo ndizo Mungu anazichukia sana. lakini watu wengi bado hawawezi kuachana nazo, wakifikiri kwamba shughuli hizi za kishirikina zimeamriwa na Mungu, na hata leo bado hawajaziacha kabisa. Mambo kama mipango ambayo vijana hufanya kwa ajili ya sherehe za arusi au mahari, zawadi za pesa, dhifa, na maneno mengine na virai vinavyohusiana na matukio ya sherehe; maneno ya zamani ambayo yamerithishwa; shughuli zote za kishirikina zisizokuwa na maana zinazofanywa kwa niaba ya wafu na taratibu za mazishi; yote haya yanachukiwa sana na Mungu. Hata Jumapili (Sabato, kama inavoadhimishwa na Wayahudi) pia inachukiwa naye; mahusiano ya kijamii na mawasiliano ya kidunia kati ya mwanamme na mwanamme pia yanachukiwa na kukataliwa zaidi na Mungu. Hata Sikukuu ya Machipuko na Siku ya Krismasi, ambazo zinajulikana kwa kila mtu, haziamriwi na Mungu, sembuse wanasesere na mapambo (mashairi, keki ya Mwaka Mpya, mafataki, kandili, zawadi za Krismasi, sherehe za Krismasi, na Ushirika Matakatifu) ya sikukuu hizi—je, sio sanamu katika akili za wanadamu? Kumega mkate siku ya Sabato, mvinyo, na kitani nyembamba navyo ni sanamu zaidi. Siku zote za sherehe za kijadi ambazo ni maarufu sana nchini China, kama vile Siku ya kuinua Vichwa vya Joka, Sikukuu ya Mashua ya Joka, Sikukuu ya Majira ya Kati ya Kupukutika, Sikukuu ya Laba, na Siku ya Mwaka Mpya, na sikukuu zisizothibitika katika ulimwengu wa kidini, kama vile Pasaka, Siku ya Ubatizo, na Siku ya Krismasi, zote hizi zimepangwa na kurithishwa kwa watu wengi tangu zama za kale hadi leo, zote hazilingani kabisa na binadamu aliyeumbwa na Mungu. Ni uwezo mkubwa wa fikra za binadamu na dhana bunifu ambazo zimewaruhusu kurithishwa hadi leo. Zinaonekana kuwa hazina kasoro, lakini kwa kweli ni hila ambazo Shetani alifanya kwa binadamu. Kadri Shetani wanavyoishi katika eneo fulani, na kadri eneo hilo lilivyo nyuma kimaendeleo na kutofaa, ndivyo desturi zake za kikabaila zinakuwa nyingi zaidi. Vitu hivi vinawafunga watu kwa nguvu, bila kutoa nafasi kwa ajili ya maendeleo. Sikukuu nyingi katika ulimwengu wa kidini zinaonekana kuonyesha ubunifu mkubwa na zinaonekana kujenga daraja kwa kazi ya Mungu, lakini kweli ni vifungo visivyoshikika ambavyo Shetani hutumia kuwafunga watu ili wasije kumjua Mungu—hizi zote ni hila za ujanja za Shetani. Kwa kweli, hatua ya kazi ya Mungu inapomalizika, tayari Amekwishaharibu zana na mtindo wa wakati huo, bila kuacha alama yoyote. Hata hivyo, “waumini wasalihina” bado wanaabudu vitu hivyo vya kushikika; wakati huo huo wanaacha kile Alicho nacho Mungu, bila hata kukichunguza zaidi, wakionekana wamejawa na upendo wa Mungu lakini kwa uhalisi walimtoa ndani ya nyumba zamani sana na kumweka Shetani mezani kwa ajili ya kumwabudu. Sanamu ya Yesu, Msalaba, Maria, Ubatizo wa Yesu na Karamu ya Mwisho—watu wanavichukulia hivi kama Bwana wa Mbinguni, wanaviabudu wakati wote wakilia kwa sauti kwa kurudiarudia “Mungu Baba.” Je, huu sio utani? Hadi leo, misemo mingi ya kimapokeo kama hiyo iliyorithishwa miongoni mwa wanadamu ni chukizo kwa Mungu; inazuia kabisa njia ya kuendelea mbele kwa Mungu na, zaidi ya hayo, inasababisha vipingamizi vikubwa kwa kuingia kwa mwanadamu. Mbali na kiwango ambacho Shetani amemharibu mwanadamu, sheria ya Witness Lee, uzoefu wa Lawrence, uchunguzi wa Watchman Nee, na kazi ya Paulo, haya yote yameuteka moyo wa mwanadamu. Mungu hana namna ya kufanya kazi kwa wanadamu, kwa sababu ndani yao kuna ubinafsi mwingi, sheria, kanuni, taratibu na mifumo, na vitu kama hivi; vitu hivi, ukiongezea vitendo vya watu vya imani za kishirikina, vimewakamata na kuwaharibu wanadamu. Ni kana kwamba mawazo ya watu ni filamu ya ajabu ya kichimbakazi katika rangi kamili, ikiwa na watu wa ajabu wakiendesha mawingu, ya kubuni sana kiasi cha kuwastaajabisha watu, ikiwaacha watu wametunduwazwa na kupigwa butwaa. Kusema kweli, kazi ambayo Mungu huja kufanya leo ni hasa kushughulikia na kuondoa sifa za ushirikina za binadamu na kugeuza kabisa mtazamo wao wa akili. Kazi ya Mungu sio kile ambacho kimepitishwa kwa vizazi na kuhifadhiwa mpaka leo na binadamu; ni kazi kama ilivyoanzishwa na Yeye binafsi na kukamilishwa na Yeye, bila haja yoyote ya kuurithi urithi wa mwanadamu fulani mkuu wa kiroho, au kurithi kazi yoyote ya asili ya uwakilishi iliyofanywa na Mungu katika enzi nyingine fulani. Binadamu hawahitaji kujishughulisha na jambo lolote kati ya haya. Mungu ana mtindo mwingine leo wa kuzungumza na wa kufanya kazi, kwa hiyo mbona binadamu wajisumbue? Kama wanadamu watatembea njia ya leo katika mkondo wa sasa huku wakiendeleza urithi wa “babu” zao, hawatafikia hatima yao. Mungu huhisi kinyaa sana kwa hali hii hasa ya tabia ya mwanadamu, jinsi Anavyoichukia mno miaka, miezi na siku za ulimwengu wa binadamu.
Njia bora zaidi ya kubadilisha tabia ya mwanadamu ni kuondoa vitu hivi vyenye sumu kubwa katika mioyo ya wanadamu, kuwaruhusu watu kuanza kubadilisha fikira na maadili yao. Kwanza kabisa, watu wanatakiwa kuona waziwazi kwamba kaida zote hizi za kidini, shughuli za kidini, miaka na miezi, na sikukuu zote ni za kumchukiza Mungu. Wanatakiwa kuwa huru kutoka kwa vifungo hivi vya fikira za kishirikina na kuondoa kila alama ya kishirikina iliyozama kabisa ndani. Mambo haya yote ni sehemu ya kuingia kwa mwanadamu. Mnatakiwa kuelewa kwa nini Mungu huwatoa watu katika ulimwengu usiokuwa na dini, na pia kwa nini Huwatoa katika desturi na kanuni. Hili ndilo lango la kuingia kwenu, na ingawa halina uhusiano na uzoefu wenu wa kiroho, hivi ni vizuizi vikubwa vinavyowazuia kuingia, vinavyowazuia kumjua Mungu. Vinatengeza wavu unaowakamata watu. Watu wengi husoma Biblia sana na wanaweza hata kukariri mafungu mengi kutoka katika Biblia. Katika kuingia kwao leo, watu bila kujua wanaitumia Biblia kupima kazi ya Mungu, kana kwamba msingi wa hatua hii katika kazi ya Mungu ni Biblia na chanzo chake ni Biblia. Kazi ya Mungu inapokuwa sambamba na Biblia, watu huiunga mkono kazi ya Mungu kwa nguvu zote na kumwangalia Mungu kwa taadhima mpya; kazi ya Mungu inapokuwa haifanani na Biblia, watu huwa na dukuduku sana kiasi cha kuanza kutokwa jasho, wakitafuta ndani yake msingi wa kazi ya Mungu; kama kazi ya Mungu haikutajwa katika Biblia, watu watampuuza Mungu. Inaweza kusemwa kwamba, watu wengi wanaikubali kwa hadhari sana, wanatii kwa kusita, na hawajali kuhusu kuijua kazi ya Mungu; na kuhusu mambo yaliyopita, wanashikilia nusu moja na kuacha nusu nyingine. Je, huku kunaweza kuitwa kuingia? Kushikilia vitabu vya wengine kama hazina, na kuvichukulia kama ufunguo wa dhahabu wa kufungua lango la ufalme, watu hawaonyeshi kuvutiwa na matakwa ya Mungu ya leo. Aidha, “wataalamu wengi wenye akili” katika mkono wao wa kushoto wanashikilia maneno ya Mungu, huku katika mkono wa kulia wanashikilia “kazi kuu” za wengine, kana kwamba wanataka kutafuta msingi wa maneno ya Mungu kutoka kwa kazi hizi kuu ili kuthibitisha kwa ukamilifu kwamba maneno ya Mungu ni sahihi, na hata wanatoa ufafanuzi kwa wengine kwa kuunganisha na kazi kuu, kana kwamba walikuwa wanafanya kazi. Kusema kweli, kuna “watafiti wa kisayansi” wengi miongoni mwa wanadamu ambao hawajawahi heshimu mafanikio makubwa ya kisayansi ya leo, mafanikio ya kisayansi ambayo hayana kigezo (yaani, kazi ya Mungu, maneno ya Mungu, na njia ya kuingia uzimani), hivyo watu wote “wanajitegemea,” “wakihubiri” mbali sana wakitegemea sana ufasaha wao, wakiringia “jina zuri la Mungu.” Wakati huo huo, kuingia kwao kuko hatarini na umbali wa matakwa ya Mungu unaonekana kuwa mbali sana jinsi uumbaji ulivyo mbali na wakati huu. Ni rahisi kiasi gani kufanya kazi ya Mungu? Inaonekana kwamba watu wamekwishaamua kuacha nusu yao kwa mambo ya zamani na kuleta nusu yao kwa wakati wa leo, kuwasilisha nusu kwa Shetani na kukabidhi nusu kwa Mungu, kana kwamba hii ndiyo njia ya kutuliza dhamiri yao na kuweza kuwa na hisia ya utulivu fulani. Mioyo ya watu inadhuru sana kwa siri, wanaogopa sio tu kupoteza kesho bali pia wanahofia kupoteza jana, wanaogopa sana kumkosea Shetani na kumkosea Mungu wa leo, Anayeonekana kuwa na bado kutokuwa. Kwa sababu watu wameshindwa kukuza vizuri fikira na maadili yao, wanakosa utambuzi kabisa, na kimsingi hawajui kama kazi ya leo ni ile ya Mungu au siyo. Pengine ni kwa sababu fikra za kishirikina za watu zimekita mizizi sana kiasi kwamba ushirikina na ukweli, Mungu na sanamu, vimewekwa katika kundi moja; wala hawajali kuvibainisha vitu hivi, na inaonekana kama wametesa bongo zao lakini bado mambo hayo hayajawa wazi. Na hiyo ndio maana wanadamu wamesimama katika njia zao na hawasongi mbele tena. Haya yote yanatokea kwa sababu watu hawana elimu ya itikadi ambayo ni sahihi, kitu ambacho husababisha ugumu katika kuingia kwao. Na matokeo yake, watu wanapoteza mvuto kabisa katika kazi ya Mungu wa kweli, bali wanashikilia kwa kung’ang’ania[2] kazi ya mwanadamu (kama vile watu wanaotazamwa kuwa ni watu wakubwa) kana kwamba imepigwa muhuri. Je, hizi si mada mpya kabisa ambazo wanadamu wanapaswa kuingia ndani?
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Alhamisi, 14 Februari 2019

Neno la Mungu | Sura ya 98

Neno la Mungu | Sura ya 98

Mambo yote yatakuja juu ya kila mmoja wenu, na yatawawezesha kujua zaidi juu Yangu na kuwa na uhakika zaidi juu Yangu. Yatawawezesha kunijua, Mungu mmoja Mwenyewe, kunijua Mimi Mwenye uweza, kunijua Mimi Mungu Mwenyewe mwenye mwili. Baadaye, Nitatoka katika mwili, Nirudi Sayuni, Nirudi katika nchi nzuri ya Kanaani, ambayo ni makazi Yangu, ndiyo hatima Yangu, na ndio msingi ambao niliumba vitu vyote. Sasa hakuna yeyote kati yenu anayeelewa maana ya maneno ambayo Ninasema, hakuna mtu hata mmoja ambaye anaweza kuelewa maana ya maneno haya. Ni wakati tu kila kitu kitafichuliwa kwenu ndipo mtaelewa kwa nini Ninasema maneno haya. Mimi si wa ulimwengu na Mimi sio hata wa ulimwengu kwa sababu Mimi ni Mungu Mwenyewe wa pekee. Ninashikilia ulimwengu dunia wote mkononi Mwangu, Mimi Mwenyewe Ninatawala, na watu wanaweza tu kutii mamlaka Yangu, kulitaja jina Langu takatifu, kunishangilia na kunisifu. Kila kitu kitafunuliwa kwenu hatua kwa hatua. Ingawa hakuna kitu kilichofichwa, ninyi bado hamwezi kuelewa njia Yangu ya kuzungumza, na sauti ya maneno Yangu. Bado hamwelewi mpango Wangu wa usimamizi unahusu nini. Kwa hiyo, Nitawaambia baadaye kuhusu mambo yote ambayo hamwelewi kwa yale Niliyoyasema kwa sababu, Kwangu Mimi, kila kitu ni rahisi na wazi wakati, kwenu, ni vigumu sana, hamwelewi tu kabisa. Kwa hiyo, Nitabadili njia Yangu ya kuzungumza, Sitaunganisha mambo pamoja Ninaponena lakini Nitafafanua kila hoja moja baada ya nyingine.
Kufufuka kutoka kwa wafu kunahusu nini? Je, ni kufa katika mwili na kisha kurudi kwenye mwili baada ya kifo? Je, huku kunaitwa kufufuka kutoka kwa wafu? Je, ni rahisi vile? Mimi ni mwenyezi Mungu, unajua nini kuhusu hili? Je, mnaelewaje hili? Je, kufufuka kutoka kwa wafu wakati wa kupata Kwangu mwili mara ya kwanza kwa kweli kunaweza kuchukuliwa neno kwa neno? Je, mchakato huo ulikuwa kama ulivyoelezwa katika maandiko? Nimesema kuwa kama Sizungumzi kwa uwazi, kama Sielezi wazi, hakuna mtu atakayeweza kuelewa maana ya maneno Yangu. Hakuna mtu hata mmoja katika enzi zote ambaye hakufikiri kwamba kufufuka kutoka kwa wafu kulikuwa vile. Tangu uumbaji wa dunia hakuna mtu aliyeelewa maana halisi ya hili. Je, nilipigwa misumari msalabani kwa kweli? Na, baada ya kifo, je, nilitoka kaburini? Ilikuwa namna hii kwa kweli? Je, hili linaezekana kweli? Hakuna mtu katika enzi zote ambaye ameweka jitihada yoyote katika hili, hakuna mtu ambaye amenijua kutoka kwa hili na hakuna mtu hata mmoja ambaye haamini, kila mtu anadhani kuwa hili ni kweli. Hawajui kwamba kila neno Langu lina maana ya ndani. Basi, kufufuka kutoka kwa wafu ni nini hasa? (Hivi karibuni, mtapitia jambo hili, kwa hivyo Nitawaambia kuhusu hilo mapema.) Kila kiumbe aliyeumbwa anataka kuishi kuliko kufa. Kutoka kwa mtazamo Wangu, kifo cha mwili sio kifo halisi. Wakati Roho Wangu anarudishwa kutoka kwa mtu, mtu huyo hufa. Kwa hiyo, Ninawaita wale mapepo wote waliopotoshwa na Shetani (wale ambao hawana imani, wasioamini wote) wafu. Tangu kuumbwa kwa dunia, Nimeongeza Roho Wangu kwa kila mtu Niliyemchagua. Hata hivyo, baada ya awamu iliyofuatia uumbaji, watu walimilikiwa na Shetani kwa kipindi cha muda. Kwa hiyo Niliondoka na watu wakaanza kuteseka (mateso Niliyovumilia Nilipopata mwili na kusulubishwa msalabani, kama ilivyoelezwa). Hata hivyo, kwa wakati uliopangiwa kabla na Mimi (wakati ambapo kuwaacha Kwangu watu kulimalizika), Niliwarejesha Kwangu watu Niliowaamulia kabla na Nikaweka tena Roho Wangu ndani yenu ili mpate kufufuka. Hii inaitwa “kufufuka kutoka kwa wafu.” Sasa, wale wanaoishi kwa kweli katika Roho Wangu wote wameshashinda uwezo wa binadamu, na wote wanaishi katika mwili. Hata hivyo, kabla ya muda mrefu, ninyi nyote mtaondoa fikira zenu, mtupe mawazo yenu, na kutupa mtego wote wa kidunia. Lakini, sivyo, kama watu wanavyofikiria, kufufuka kutoka kwa wafu baada ya mateso. Kwamba ninyi mnaishi sasa ni sharti la awali la kuishi katika mwili, ni njia muhimu ya kuingia katika ulimwengu wa kiroho. Kuzidi uwezo wa ubinadamu wa kawaida Ninaozungumza kuhusu kunamaanisha kutokuwa na familia, kutokuwa na mke, kutokuwa na watoto na mahitaji ya kibinadamu. Ni kuzingatia tu kuishi kwa kudhihirisha mfano Wangu, kuzingatia tu kuingia ndani Yangu na kutofikiria juu ya mambo mengine nje Yangu. Mahali popote unapoenda ni nyumbani kwako, huku ni kuvuka mipaka kwa ubinadamu wa kawaida. Ninyi mmeelewa visivyo kabisa maneno haya Yangu, ufahamu wenu ni wa kina kifupi sana. Je, Nitaonekanaje kwa mataifa yote na watu wote? Katika mwili leo? Hapana! Wakati utakapokuja, Nitaonekana katika mwili Wangu katika kila taifa la ulimwengu. Wakati ambapo wageni wanawahitaji muwachunge bado haujafika. Wakati huo ninyi mtahitaji kuja nje ya mwili na kuingia katika mwili ili muwalishe. Huu ni ukweli lakini sio “kufufuka kutoka kwa wafu” ambao watu wanafikiria. Wakati uliowekwa, mtatoka katika mwili bila kujua na kuingia katika ulimwengu wa kiroho na kutawala mataifa yote pamoja nami. Wakati haujafika bado. Ninapowahitaji kuwa katika mwili mtakuwa katika mwili (kulingana na mahitaji ya kazi Yangu, ninyi lazima muwe na fikira sasa, bado lazima muishi katika mwili, hivyo mnapaswa bado kufanya mambo ambayo mnapaswa kufanya katika mwili kulingana na hatua Zangu; msisubiri bila kufanya lolote kwa sababu hii itachelewesha mambo). Ninapowahitaji kutenda katika mwili kama wachungaji wa kanisa, ninyi mtatoka nje ya mwili, muache mawazo yenu, na kunitegemeana kabisa ili kuishi. Muwe na imani katika nguvu Zangu, muwe na imani katika hekima Yangu. Kila kitu kitafanywa na Mimi binafsi. Mnahitaji tu kusubiri kufurahia. Baraka zote zitawajia, na ninyi mtakuwa na ruzuku isiyoisha. Siku hiyo itakapokuja, mtaelewa kanuni ya jinsi Ninavyofanya hivi, mtajua matendo Yangu ya ajabu na kuelewa jinsi Ninavyoleta wana Wangu wazaliwa wa kwanza katika Sayuni. Hili sio gumu kama mnavyofikiria lakini pia si rahisi kama mnavyofikiria.
Najua Ninaposema hili hamwezi hata kwa kiwango cha chini kuelewa madhumuni Yangu katika hilo na huchanganyikiwa zaidi. Mtayachanganya na yale Niliyosema hapo awali ili msiweze kuelewa chochote, itaonekana kama kwamba hakuna njia nyingine. Hata hivyo, msijali, Nitawaambia kila kitu. Kila kitu Ninachosema kina maana. Nimesema kuwa Ninaweza kufanya vitu vilivyopo virudi kuwa bure na Ninaweza kufanya vitu viwe vingi kutoka kwa utupu. Katika mawazo ya binadamu, kuingia katika mwili kutoka kwa mwili, mtu lazima afufuliwe kutoka kwa wafu. Katika siku za nyuma, Nilitumia njia hii na Nikadhihirisha muujiza Wangu mkuu zaidi, lakini leo si kama zamani. Nitawachukua moja kwa moja kutoka kwa mwili hadi ndani ya mwili. Je, hii sio hata ishara kubwa zaidi na muujiza? Je, huu sio udhihirisho mkubwa zaidi wa kudura Yangu? Nina mpango Wangu, Nina nia Zangu. Nani asiye katika mikono Yangu? Ninafanya kazi na Ninajua. Njia Zangu za kufanya kazi leo ni, hata hivyo, tofauti na zilizopita. Ninabadilisha mbinu Zangu za kufanya kazi kulingana na mabadiliko ya enzi. Wakati Nilipigwa misumari msalabani, hiyo ilikuwa ni Enzi ya Neema, lakini sasa ni enzi ya mwisho. Kasi ya kazi Yangu inaongezeka, sio kasi sawa na ilivyokuwa hapo zamani, sembuse kuwa polepole kuliko siku za nyuma lakini, badala yake, ni haraka zaidi kuliko zamani. Hakuna njia ya kuielezea, hakuna haja ya michakato mingi migumu. Mimi Niko huru kufanya chochote; si kweli kwamba inachukua tu maneno machache ya mamlaka kutoka Kwangu kuamua jinsi mapenzi Yangu yatakamilishwa na jinsi Nitawakamilisha? Kila kitu Ninachosema hakika kitafanyika. Katika siku za nyuma, mara nyingi Nilisema kuwa nitateseka, na Sikuwaruhusu watu wataje mateso Niliyoyastahimili awali; kutaja hili kulikuwa kunikufuru. Hii ni kwa sababu Mimi ni Mungu Mwenyewe na Kwangu hakuna ugumu; unapotaja mateso haya unawafanya watu walie. Nimesema kuwa katika siku zijazo hakutakuwa na kutanafusi na hakutakuwa na machozi. Inapaswa kuelezwa kutoka kwa mtazamo huu, na kisha maana ya maneno Yangu yanaweza kueleweka. Maana ya “wanadamu hawawezi kustahimili mateso haya” ni kwamba Ninaweza kuondoka kutoka kwa dhana zote za binadamu na fikira, kuachana na hisia za mwili, kuacha mambo yote ya ulimwengu na kuondoka katika mwili, na bado Ninaweza kusimama wakati kila mtu ananikana Mimi. Hii inatosha kuthibitisha kuwa Mimi ni Mungu Mwenyewe wa pekee. Nimesema, “Kila mwana mzaliwa wa kwanza lazima aingie katika ulimwengu wa kiroho kutoka kwa mwili; hii ndiyo njia ambayo wanapaswa kuchukua ili kutawala pamoja nami kama wafalme.” Maana ya sentensi hii ni kwamba unapokumbana na kitu ambacho mnacho, zamani, mlifikiri, mtaondoka rasmi katika nyama na kuingia katika mwili ili muanze kuwahukumu rasmi wale wana wa wafalme na wafalme hao. Wao watahukumiwa kulingana na mambo yanayotokea wakati huu. Hata hivyo, sio ngumu kama mnavyofikiria, itafanyika papo hapo. Hamtahitaji kufufuka kutoka kwa wafu na hamtahitaji hata kuteseka (kwa sababu mateso na shida zenu duniani tayari zimekamilika na Nimekwisha kusema kuwa Sitashughulika tena na wanangu wazaliwa wa kwanza baada ya hapo). Hapa ndipo wazaliwa wa kwanza watafurahia baraka zao, kama ilivyoongelewa—mtaingia katika ulimwengu wa kiroho bila kujua. Kwa nini Nasema kuwa hii ni rehema Yangu na neema? Ikiwa mtu angeweza tu kuingia katika ulimwengu wa kiroho baada ya kufufuka kutoka kwa wafu, hii ingekuwa mbali na kuwa ya huruma na neema. Kwa hivyo haya ndiyo maonyesho ya dhahiri zaidi ya rehema Yangu na neema na, zaidi ya hayo, yanafichua uamuzi Wangu kabla na uteuzi Wangu wa watu. Inatosha kuonyesha jinsi amri Yangu ya utawala ilivyo kali. Nitakuwa mwenye huruma kwa yeyote Nitakayetaka na kuwa mwenye huruma kwa yeyote Nitakayetaka. Hakuna mtu atakayepinga au kupigana. Nitaamua yote haya.
Watu hawawezi kuelewa hilo na wanajiwekea shinikizo mpaka wasiweze kupumua na bado wanajifunga. Mawazo ya watu ni finyu sana, kwa hiyo ni lazima watupilie mbali mawazo na dhana za binadamu. Kwa hivyo, ni lazima Nitoke katika mwili na kuingia katika ulimwengu wa kiroho kuchukua udhibiti wa kila kitu, kusimamia kila kitu. Hii ndiyo njia pekee ya kutawala watu wote na mataifa yote na kutimiza mapenzi Yangu. Sio mbali sana. Hamna imani katika kudura Yangu, hamjui mwanadamu Niliye. Mnafikiri kwamba Mimi ni mtu tu, hamwezi kuona uungu Wangu hata kidogo. Mambo yatakuwa kamili wakati wowote Ninapotaka yawe kamili. Kinachohitajika tu ni neno kutoka katika kinywa Changu. Ninyi mmetilia maanani tu kipengele cha ubinadamu Wangu katika kile ambacho Nimesema hivi karibuni na kila Ninachofanya, lakini hamjatilia maanani kipengele cha uungu Wangu. Hiyo ni kusema kwamba mnadhani kwamba Mimi pia nina mawazo na dhana. Lakini Nimesema kuwa fikira Zangu, mawazo na akili, kila Ninachofanya, kila kitu Ninachotenda na kila kitu Ninachosema ni udhihirisho kamili wa Mungu Mwenyewe. Je, mmesahau yote haya? Ninyi nyote ni watu waliochanganyikiwa! Hamwelewi maana ya maneno Yangu. Nimewaruhusu kuona kipengele cha ubinadamu Wangu wa kawaida kutoka kwa kile Nilichosema (Nimewawezesha kuona ubinadamu Wangu wa kawaida katika maisha Yangu ya kila siku, kwa kweli, kwa sababu ninyi bado hamwelewi kipengele cha ubinadamu Wangu wa kawaida kutokana na kile Nilichosema wakati huu), ilhali hamwelewi ubinadamu Wangu wa kawaida, na mnajaribu kushikilia tu kitu ambacho kinaweza kutumiwa dhidi Yangu na mnakuwa bila nidhamu mbele Yangu. Ninyi ni vipofu! Ninyi ni wapumbavu! Hamnijui Mimi! Nimenena bure kwa muda mrefu, ninyi hamnijui Mimi kabisa, hamuchukulii ubinadamu Wangu wa kawaida kama sehemu ya Mungu Mwenyewe mkamilifu kabisa! Ninawezaje kukosa kuwa na hasira? Ninawezaje kuwa mwenye huruma tena? Ninaweza tu kuwajibu watoto hawa wa kutotii na hasira Yangu. Wenye kiburi sana, wasionijua sana! Mnafikiria kwa mwanadamu Niliye amefanya makosa! Naweza kufanya makosa? Ningechagua bila mpango kuuchukua mwili wowote? Ubinadamu Wangu na uungu Wangu ni sehemu mbili zisizoweza kutenganishwa ambazo zinajumuisha Mungu Mwenyewe mkamilifu. Sasa mnapaswa kuelewa vizuri kuhusu hili! Tayari Nimeshasema kila kitu Ninapaswa kusema. Sitalieleza zaidi!
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Jumatano, 13 Februari 2019

Kanuni Kuu za Jinsi Wafanyakazi Hufanya Kazi

Sura ya 37. Kanuni Kuu za Jinsi Wafanyakazi Hufanya Kazi

Katika kazi yao, wafanyakazi wanapaswa kuzingatia mambo mawili: Moja ni kufanya kazi kabisa kulingana na kanuni zilizowekwa masharti na mipangilio ya kazi. Wafanyakazi hawapaswi kukiuka kanuni hizi, wasifanye kazi kulingana na mawazo yao wenyewe, na siyo kulingana na mapenzi yao. Wanapaswa kuonyesha uhusiano kwa kazi ya familia ya Mungu, na kuweka maslahi ya familia ya Mungu kwanza katika kila kitu wakifanyacho. Jambo jingine pia ni muhimu, na ni kwamba, katika kila kitu wakifanyacho, kuzingatia kufuata mwongozo wa Roho Mtakatifu, na kufanya kila kitu kwa ukali kulingana na neno la Mungu. Usipotii mwongozo wa Roho Mtakatifu au ikiwa kwa ukaidi unafuata mawazo yako mwenyewe na kufanya mambo kulingana na fikira zako mwenyewe, hili linafanya upinzani mkali sana kwa Mungu. Mama kwa mara kutotii kupata nuru na mwongozo wa Roho Mtakatifu huelekeza kwa mwisho kabisa. Hakuna jinsi ya kuendelea na kazi kama mtu amepoteza kazi ya Roho Mtakatifu, na ingawa mtu hufanya kazi, hakuna kitu kinachotimizwa. Ni kanuni hizi kuu mbili za kuzingatia wakati ukiwa kazini: Moja ni kufanya kazi kabisa kulingana na mipangilio kutoka hapo juu, na kufanya kazi na kanuni zilizowekwa na hayo ya hapo juu. Jambo jingine ni kufuata mwongozo kutoka kwa Roho Mtakatifu karibu. Mara tu mambo haya mawili yanapofahamika, ni vigumu kwa kazi kukosa kufikia matarajio yake. Kwa nyinyi ambao uzoefu wenu katika eneo hili bado ni kidogo, ridhaa yenu wenyewe hughushi kazi yenu zaidi. Wakati mwingine, hamuwezi kuelewa kupata nuru au mwongozo kutoka kwa Roho Mtakatifu karibu; kwa wengine, mnaonekana kuielewa, lakini huenda mnaipuuza. Wewe daima hufikiria au kufikia hitimisho kwa njia ya kibinadamu, kufanya kama unavyofikiria kuwa sahihi, bila kujali kabisa juu ya nia ya Roho Mtakatifu. Wewe huendelea na kazi yako tu kulingana na mawazo yako mwenyewe, ukiweka kando upataji wa nuru kutoka kwa Roho Mtakatifu. Hali kama hizo hutokea mara kwa mara. Mwongozo wa ndani kutoka kwa Roho Mtakatifu si wa kupita uwezo wa binadamu kamwe. Kwa kweli ni wa kawaida sana: Mfiko wa ndani wa roho yako unajua hii ndiyo njia sahihi ya kufanya hivyo, na kwamba hii ndiyo njia bora zaidi. Wazo kama hilo ni wazi sana; si matokeo ya kutafakari, na wakati mwingine huwezi kuelewa kikamilifu ni kwa nini kuifanya kwa njia hii. Hii mara nyingi si kitu kingine bali kupata nuru kutoka kwa Roho Mtakatifu. Hali kama hiyo ndiyo hutokea kwa kawaida kwa watu wengi sana. Roho Mtakatifu hukuongoza utende kwa njia sahihi zaidi. Siyo matokeo ya fikira zako, badala yake una hisia moyoni mwako na unang'amua kwamba hii ndiyo njia bora zaidi ya kufanya hivyo. Pengine hili ni kutoka kwa Roho Mtakatifu. Mapenzi ya mtu mara nyingi ni matokeo ya mfanyiko tendani wa mawazo yake na yamepakwa rangi na mawazo yake: Mapato yangu ni nini, jinsi nitakavyofaidika—haya ni sehemu ya chochote ambacho watu huamua kukifanya wenyewe. Mwongozo kutoka kwa Roho Mtakatifu hauna ughushi kama huo hata kidogo. Ni muhimu kuzingatia kwa makini mwongozo au kupata nuru kutoka kwa Roho Mtakatifu; hasa katika masuala muhimu unapaswa kuwa makini ili ulielewe. Watu ambao hufikiria mengi sana, ambao hupenda kufuata mawazo yao huenda wakaukosa. Wafanyakazi wazuri, wafanyakazi waangavu, huzingatia kazi ya Roho Mtakatifu. Watu wanaomtii Roho Mtakatifu humwogopa Mungu na kutafuta ukweli bila kuchoka. Ili kumridhisha Mungu na kumshuhudia Yeye, mtu anapaswa kuchunguza kazi yake mwenyewe kwa dalili za ughushi na madhumuni, na kujaribu kuona ni kiasi gani kilichomotishwa na matakwa ya kibinafsi, ni kiasi gani kilichotokana na kupatiwa nuru na Roho Mtakatifu, na ni kiasi gani kilicho cha kuambatana na neno la Mungu. Ni lazima daima na katika hali zote uyakague maneno na matendo yako. Kutenda kwa njia hii daima kutakuweka kwenye njia sahihi ya kumtumikia Mungu. Ni muhimu kuwa na ukweli mwingi chini ya amri yako ili kutimiza huduma kwa Mungu ambayo ni ya kupendeza nafsi Yake. Watu wana uwezo wa kutofautisha baada tu ya kuelewa neno la Mungu, na wanaweza kutambua kinachotoka kwa mapenzi yao wenyewe na vitu vinavyoonyesha motisha yao. Wanaweza kutambua uchafu wa wanadamu, na maana ya kutenda kulingana na ukweli. Ni hapo tu utakapojua jinsi ya kutii zaidi kwa usafi. Bila ukweli haiwezekani kwa watu kutofautisha. Mtu mpumbavu anaweza kumwamini Mungu maisha yake yote bila kujua maana ya kufichua upotovu, wala hajui kumpinga Mungu ni nini, kwa sababu yeye hana ukweli, wazo hili halipo katika akili yake. Hili ni kama kukarabati kifaa cha umeme. Je, mtu anawezaje kukitengeneza ikiwa hajui ni mzunguko umeme upi una kosa? Ndani yenu pia kuna mizunguko mingi. Wakati mwingine hitilafu iko katika malengo yenu, au ambako mapenzi yenu wenyewe yanahusika. Wakati mwingine hitilafu ni upotovu wa ufahamu wenu au ujuzi. Ama inaweza kuwa kutokana na kufuata mapenzi yenu wenyewe au kwa kuamini na kupotoshwa na wengine. Wakati mwingine nyinyi hufuata mwili mnapojaribu kulinda sifa zenu au hadhi. Hitilafu kama hizi hutokea mara kwa mara, hivyo kupeleka kazi mrama na kuleta hasara kwa kazi ya familia ya Mungu na maisha ya ndugu. Thamani ya kazi ya aina hii ni nini? Ni katizo, usumbufu, na uharibifu tu. Ili kutimiza kazi ambayo Mungu huwapa ni muhimu kuelewa kanuni hizi mbili. Ni lazima mshike kabisa mipango ya kazi kama ilivyoelezwa hapo juu, na lazima mzingatie kuutii mwongozo kutoka kwa Roho Mtakatifu. Ni wakati tu kanuni hizi mbili zinapofahamika ndipo kazi inapoweza kuwa ya kufaa na mapenzi ya Mungu yaridhishwe.
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu

Jumatatu, 11 Februari 2019

2018 Gospel Music "Mungu Kuwatawala na Kuwakimu Wanadamu na Vitu Vyote" (Swahili Subtitles)

2018 Gospel Music "Mungu Kuwatawala na Kuwakimu Wanadamu na Vitu Vyote" (Swahili Subtitles)

Chini ya mbingu, milima, mito, na maziwa vyote vina mipaka yavyo, na viumbe vyote huishi na kuzaana wakati wa misimu yote minne kulingana na sheria za maisha…. Ungependa kujua ni nani huwatawala na kuwakimu wanadamu na vitu v yote? Tazama dondoo hii ya filamu ya Kikristo ili kujua zaidi kuhusu mamlaka ya pekee ya Mungu.
Mwenyezi Mungu alisema, Mwanzoni, Mungu alikuwa anapumzika. Hakukuwa na binadamu ama kitu chochote kingine duniani wakati huo, na Mungu hakuwa amefanya kazi yoyote ile. Mungu alianza tu kazi Yake ya usimamizi baada ya binadamu kuwepo na baada ya binadamu kupotoshwa. Kutoka hapa kuendelea, Mungu hakupumzika tena lakini badala yake Alianza kufanya kazi miongoni mwa binadamu. Ilikuwa kwa sababu ya upotovu wa binadamu ndipo Mungu alichukuliwa kutoka kwa pumziko Lake, na ilikuwa pia kwa sababu ya uasi wa malaika mkuu ndipo Mungu alichukuliwa kutoka kwa pumziko Lake. Iwapo Mungu hatamshinda Shetani na kuokoa binadamu, ambao wamepotoshwa, Mungu hatawahi tena kuweza kuingia rahani. Mungu anakosa pumziko akosavyo mwanadamu. Wakati Mungu ataingia rahani tena, mwanadamu pia ataingia rahani. Maisha ya pumziko ni yale bila vita, bila uchafu, bila udhalimu unaoendelea. Hii ni kusema kwamba hayana unyanyasaji wa Shetani (hapa “Shetani” inamaanisha nguvu za uhasama), upotovu wa Shetani, na pia uvamizi wa nguvu yoyote inayompinga Mungu. Kila kitu kinafuata aina yake na kuabudu Bwana wa uumbaji. Mbingu na dunia ni shwari kabisa. Haya ni maisha matulivu ya binadamu. Mungu aingiapo rahani, hakuna udhalimu wowote utakaoendelea duniani, na hakutakuwa na uvamizi wowote wa nguvu za uhasama. Binadamu pia wataingia ulimwengu mpya; hawatakuwa tena binadamu waliopotoshwa na Shetani, lakini badala yake binadamu ambao wameokolewa baada ya kupotoshwa na Shetani. Siku ya pumziko ya binadamu pia ni siku ya pumziko ya Mungu. Mungu alipoteza pumziko Lake kwa sababu wanadamu hawakuweza kuingia rahani; haikuwa kwamba Hakuweza awali kupumzika. Kuingia rahani hakumaanishi kwamba mambo yote yatakoma kusonga, ama kwamba mambo yote yatakoma kuendelea, wala hakumaanishi kwamba Mungu atakoma kufanya kazi ama mwanadamu atakoma kuishi. Ishara ya kuingia rahani ni kama hii: Shetani ameangamizwa; wale watu waovu wanaomuunga mkono Shetani kwa kufanya maovu wameadhibiwa na kuondolewa; nguvu zote za uhasama kwa Mungu zimekoma kuwepo. Mungu kuingia rahani kunamaanisha kwamba Hatafanya tena kazi Yake ya wokovu wa binadamu. Binadamu kuingia rahani kunamaanisha kwamba binadamu wote wataishi ndani ya mwangaza wa Mungu na chini ya baraka Zake; hakutakuwa na upotovu wowote wa Shetani, wala maovu yoyote kutokea. Binadamu wataishi kama kawaida duniani, na wataishi chini ya ulinzi wa Mungu. Mungu na mwanadamu waingiapo rahani pamoja, kutamaanisha kwamba binadamu wameokolewa na kwamba Shetani ameangamizwa, kwamba kazi ya Mungu miongoni mwa mwanadamu imemalizika kabisa. Mungu hataendelea tena kufanya kazi miongoni mwa mwanadamu, na mwanadamu hataendelea tena kumilikiwa na Shetani. Kwa hivyo, Mungu hatakuwa shughulini tena, na mwanadamu hatakimbiakimbia tena; Mungu na mwanadamu wataingia rahani wakati huo huo. Mungu atarudia nafasi yake ya awali, na kila mtu atarudia nafasi yake husika. Hizi ndizo hatima ambazo Mungu na mwanadamu wataishi ndani kwa utaratibu huu baada ya mwisho wa usimamizi wote wa Mungu. Mungu ana hatima ya Mungu na mwanadamu ana hatima ya mwanadamu. Apumzikapo, Mungu ataendelea kuwaongoza binadamu wote kwa maisha yao duniani. Akiwa kwa mwangaza wa Mungu, mwanadamu atamwabudu Mungu wa kweli aliye mbinguni. Mungu hataishi tena miongoni mwa binadamu, na mwanadamu pia hataweza kuishi na Mungu katika hitimisho la Mungu. Mungu na mwanadamu hawawezi kuishi ndani ya ulimwengu sawa; badala yake, wote wawili wana njia zao binafsi za kuishi. Mungu ndiye anayeongoza binadamu wote, wakati binadamu wote ni matokeo ya kazi ya Mungu ya usimamizi. Ni binadamu wanaoongozwa; kuhusu kiini, binadamu si sawa na Mungu. Kuingia rahani kunamaanisha kurudi pahali pa awali pa mtu. Kwa hivyo, Mungu aingiapo rahani, kunamaanisha kwamba Mungu amerudi pahali Pake pa awali. Mungu hataishi tena duniani ama kushiriki kwa furaha na mateso ya binadamu wakati yupo miongoni mwa binadamu. Binadamu wanapoingia rahani, kunamaanisha kwamba mwanadamu amekuwa kiumbe halisi; binadamu watamwabudu Mungu wakiwa duniani na kuwa na maisha ya kawaida ya wanadamu. Watu hawatakuwa tena wasiomtii Mungu ama kumpinga Mungu; watarudia maisha asili ya Adamu na Hawa. Haya ndiyo maisha na hatima binafsi ya Mungu na binadamu baada ya kuingia rahani. Kushindwa kwa Shetani ni mwelekeo usioepukika katika vita kati ya Mungu na Shetani. Kwa njia hii, kuingia kwa Mungu rahani baada ya kukamilika kwa kazi Yake ya usimamizi na wokovu kamili wa mwanadamu na kuingia rahani pia kunakuwa mielekeo isiyoepukika. Pahali pa pumziko pa mwanadamu ni duniani, na pahali pa Mungu pa pumziko ni mbinguni. Mwanadamu anapomwabudu Mungu katika pumziko, ataishi duniani, na Mungu anapoongoza sehemu iliyobaki ya binadamu katika pumziko, Atawaongoza kutoka mbinguni, sio kutoka duniani. Mungu bado atakuwa Roho, wakati mwanadamu bado atakuwa mwili. Mungu na mwanadamu wote wawili wana njia zao tofauti za kupumzika. Mungu anapopumzika, Atakuja na kujitokeza miongoni mwa mwanadamu, mwanadamu anapopumzika, ataongozwa na Mungu kutembea mbinguni na pia kufurahia maisha mbinguni. Baada ya Mungu na mwanadamu kuingia rahani, Shetani hatakuweko tena, na kama Shetani, wale watu waovu pia hawatakuweko tena. Kabla ya Mungu na mwanadamu kuingia rahani, wale watu waovu waliomtesa Mungu wakati mmoja duniani na adui waliokuwa hawamtii duniani watakuwa tayari wameangamizwa; watakuwa wameangamizwa na majanga makubwa ya siku za mwisho. Baada ya hao watu waovu kuangamizwa kabisa, dunia haitajua tena unyanyasaji wa Shetani. Binadamu watapata wokovu kamili, na hapo tu ndipo kazi ya Mungu itaisha kabisa. Haya ndiyo masharti ya Mungu na mwanadamu kuingia rahani.
Kukaribia kwa mwisho wa kila kitu kunaonyesha mwisho wa kazi ya Mungu na kunaonyesha mwisho wa maendeleo ya binadamu. Hii inamaanisha kwamba binadamu kama walivyopotoshwa na Shetani wamefika mwisho wake wa maendeleo, na kwamba vizazi vya Adamu na Hawa vimeenea hadi mwisho wao binafsi, na pia inamaanisha kwamba haiwezekani kwa binadamu kama hawa, baada ya kupotoshwa na Shetani, kuendelea kustawi. Adamu na Hawa wa mwanzoni hawakuwa wamepotoshwa, lakini Adamu na Hawa waliofukuzwa kutoka Bustani ya Edeni walivurugwa na Shetani. Wakati Mungu na mwanadamu wanaingia rahani pamoja, Adamu na Hawa—waliofukuzwa kutoka Bustani ya Edeni—na vizazi vyao hatimaye watafika mwisho; binadamu wa baadaye bado watakuwa na vizazi vya Adamu na Hawa, lakini hawatakuwa watu wanaomilikiwa na Shetani. Badala yake, watakuwa watu waliookolewa na kutakaswa. Hawa watakuwa binadamu ambao wamehukumiwa na kuadibiwa, na walio watakatifu. Hawa watu hawatakuwa sawa na jamii ya binadamu kama ilivyokuwa awali; mtu anaweza kusema kwamba hao ni watu wa aina tofauti kabisa na Adamu na Hawa wa awali. Hawa watu watakuwa wamechaguliwa kutoka miongoni mwa wote waliopotoshwa na Shetani, na watakuwa ndio watu ambao hatimaye wamesimama imara wakati wa hukumu na kuadibu kwa Mungu, watakuwa kundi la mwisho la watu miongoni mwa wanadamu potovu. Kundi hili la watu ndilo tu litaweza kuingia katika raha ya mwisho pamoja na Mungu. Wanaoweza kusimama imara wakati wa kazi ya Mungu ya hukumu na kuadibu siku za mwisho—yaani, wakati wa kazi ya mwisho ya utakaso—watakuwa wale watakaoingia katika raha ya mwisho na Mungu; kwa hivyo, wanaoingia rahani wote watakuwa wametoka katika ushawishi wa shetani na kupokewa na Mungu baada tu ya kupitia kazi Yake ya mwisho ya utakaso. Hawa watu ambao hatimaye wamepokewa na Mungu wataingia katika raha ya mwisho. Kiini cha kazi ya Mungu ya kuadibu na hukumu ni kutakasa binadamu, na ni ya siku ya raha ya mwisho. Vinginevyo, binadamu wote hawataweza kufuata aina yao ama kuingia katika raha. Hii kazi ni njia ya pekee ya binadamu kuingia rahani. Kazi ya Mungu ya utakaso pekee ndiyo itatakasa udhalimu wa binadamu, na kazi Yake ya kuadibu na hukumu pekee ndiyo itadhihirisha hayo mambo yasiyotii miongoni mwa binadamu, hivyo kutenga wanaoweza kuokolewa kutoka wale wasioweza, na wale watakaobaki kutoka wale ambao hawatabaki. Kazi Yake itakapoisha, wale watu watakaobaki watatakaswa na kufurahia maisha ya pili ya binadamu ya ajabu zaidi duniani waingiapo ulimwengu wa juu wa binadamu; kwa maneno mengine, wataingia katika siku ya binadamu ya raha na kuishi pamoja na Mungu. Baada ya wasioweza kubaki kupitia kuadibu na hukumu, umbo zao halisi zitafichuliwa kabisa; baada ya haya wote wataangamizwa na, kama Shetani, hawatakubaliwa tena kuishi duniani. Binadamu wa baadaye hawatakuwa tena na aina yoyote ya watu hawa; watu hawa hawafai kuingia eneo la raha ya mwisho, wala hawafai kuingia siku ya raha ambayo Mungu na mwanadamu watashiriki, kwani ni walengwa wa adhabu na ni waovu, na si watu wenye haki. Walikuwa wamekombolewa wakati mmoja, na pia walikuwa wamehukumiwa na kuadibiwa; walikuwa pia wamemhudumia Mungu wakati mmoja, lakini siku ya mwisho itakapofika, bado wataondolewa na kuangamizwa kwa sababu ya uovu wao na kwa sababu ya kutotii na kutokombolewa kwao. Hawatakuwa tena katika ulimwengu wa baadaye, na hawatakuweko tena miongoni mwa jamii ya binadamu ya baadaye. Watenda maovu wote na yeyote na wote ambao hawajaokolewa wataangamizwa wakati watakatifu miongoni mwa binadamu wataingia rahani, bila kujali kama wao ni roho za wafu ama wale wanaoishi bado katika mwili. Bila kujali enzi ya hizi roho zitendazo maovu na watu watenda maovu, ama roho za watu wenye haki na watu wanaofanya haki wako, mtenda maovu yeyote ataangamizwa, na yeyote mwenye haki ataishi. Iwapo mtu ama roho inapokea wokovu haiamuliwi kabisa kulingana na kazi ya enzi ya mwisho, lakini inaamuliwa kulingana na iwapo wamempinga ama kutomtii Mungu. Kama watu wa enzi ya awali walifanya maovu na hawangeweza kuokolewa, bila shaka wangekuwa walengwa wa adhabu. Kama watu wa enzi hii wanafanya maovu na hawawezi kuokolewa, hakika wao pia ni walengwa wa adhabu. Watu wanatengwa kwa msingi wa mema na mabaya, sio kwa msingi wa enzi. Baada ya kutengwa kwa msingi wa mema na mabaya, watu hawaadhibiwi ama kutuzwa mara moja; badala yake, Mungu atafanya tu kazi Yake ya kuwaadhibu waovu na kuwatuza wema baada ya kufanya kazi Yake ya ushindi katika siku za mwisho. Kwa kweli, Amekuwa akitumia mema na mabaya kutenga binadamu tangu Afanye kazi Yake miongoni mwa binadamu. Atawatuza tu wenye haki na kuwaadhibu waovu baada ya kukamilika kwa kazi Yake, badala ya kuwatenga waovu na wenye haki baada ya kukamilika kwa kazi Yake mwishowe na kisha kufanya kazi Yake ya kuwaadhibu waovu na kuwatuza wazuri mara moja. Kazi Yake ya mwisho ya kuadhibu waovu na kuwatuza wazuri inafanywa kabisa ili kutakasa kabisa binadamu wote, ili Aweze kuleta binadamu watakatifu mno katika pumziko la milele. Hatua hii ya kazi Yake ni kazi Yake muhimu zaidi. Ni hatua ya mwisho ya kazi Yake yote ya usimamizi. Kama Mungu hangewaangamiza waovu lakini badala yake kuwaacha wabakie, basi binadamu wote bado hawangeweza kuingia rahani, na Mungu hangeweza kuleta binadamu katika ulimwengu bora. Kazi ya aina hii haingekuwa imekamilika kabisa. Atakapomaliza kazi Yake, binadamu wote watakuwa watakatifu kabisa. Mungu anaweza kuishi kwa amani rahani kwa namna hii pekee.
kutoka kwa Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja