Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Jumatatu, 25 Februari 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Umuhimu wa Kuukoa Uzao wa Moabu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Umuhimu wa Kuukoa Uzao wa Moabu

Katika miaka hii miwili hadi mitatu ya kazi, kile kilichopaswa kutimizwa katika kazi ya hukumu iliyofanyika juu yenu kimetimizwa kimsingi. Watu wengi wamesahau matarajio na kudura yao ya baadaye. Hata hivyo, inapotajwa kuwa ninyi ni uzao wa Moabu, wengi wenu huchukizwa sana—nyuso zenu hubadilika, vinywa vyenu hupinda, na macho yenu hukodolea. Hamuwezi kabisa kuamini kwamba ninyi ni uzao wa Moabu. Moabu ilifukuzwa hadi nchi hii baada ya kulaaniwa. Ukoo wa wana wa Moabu umerithishwa mpaka leo, na ninyi nyote ni uzao wake. Hakuna kitu ambacho Ninaweza kufanya—nani aliyekusababisha uzaliwe katika nyumba ya Moabu? Ninakuhurumia na Siko radhi uwe hivi, lakini ukweli hauwezi kubadilishwa na watu. Wewe ni uzao wa Moabu, na Siwezi kusema kuwa wewe ni uzao wa Daudi. Haijalishi wewe ni uzao wa nani, bado wewe ni mmoja wa viumbe. Ni kwamba tu wewe ni kiumbe wa cheo cha chini—wewe ni kiumbe wa kuzaliwa katika hali duni. Viumbe vyote lazima vipitie kazi yote ya Mungu, vyote ni vyombo vya kushinda Kwake, na lazima vyote viione tabia Yake yenye haki, na kupitia hekima na kudura Yake. Sasa wewe ni uzao wa Moabu na lazima uikubali hukumu hii na kuadibu, hivyo kama hungekuwa uzao wa Moabu, basi pia hungehitaji kukubali hukumu na kuadibu huku? Unapaswa kutambua hili! Kwa kweli, kufanya kazi kwa uzao wa Moabu kwa sasa ni kwa thamani sana na kwenye umuhimu sana. Maadam kazi imefanywa kwenu, ina umuhimu mkubwa mno. Kama kazi ingefanywa kwa uzao wa Hamu haingeweza kuwa muhimu kwa sababu wao hawajazaliwa katika hali duni kama hiyo na kuzaliwa kwao sio sawa na Moabu. Uzao wa mwana wa pili wa Nuhu Hamu umelaaniwa tu—hawakuja kutokana na uasherati. Ni kwamba tu wao ni wa hali ya chini, kwa sababu Nuhu aliwalaani na wao ni watumishi wa watumishi. Wanayo hali ya chini, lakini thamani yao ya asili haikuwa chini. Tukizungumza kuhusu Moabu, watu wanajua kwamba awali alikuwa na hali ya chini kwa sababu alizaliwa kutokana na uasherati. Ingawa nafasi ya Loti ilikuwa ya juu sana, Moabu alizaliwa na Lutu na binti yake. Ingawa Loti alikuwa mtu mwenye haki, Moabu bado alikuwa chombo cha laana. Moabu alikuwa wa thamani ya chini na alikuwa na cheo cha chini, na hata kama hakuwa amelaaniwa alikuwa wa uchafu, hivyo alikuwa tofauti na Hamu. Hakukubali na alipinga, aliasi dhidi ya Yehova, ndiyo sababu alianguka katika maeneo yenye giza zaidi. Kufanya kazi sasa kwa uzao wa Moabu ni kuwaokoa wale ambao wameanguka katika giza zaidi. Ingawa walikuwa wamelaaniwa, Mungu yuko tayari kupata utukufu kutoka kwao. Hii ni kwa sababu hapo awali, wote walikuwa watu waliomkosa Mungu mioyoni mwao—kuwafanya tu kuwa wale wanaomtii na kumpenda Yeye ni ushindi wa kweli, na matunda hayo ya kazi ni ya thamani sana na yenye kuridhisha zaidi. Huku tu ni kupata utukufu—huu ndio utukufu ambao Mungu anataka kuupata katika siku za mwisho. Ingawa watu hawa ni wa nafasi ya chini, sasa wanaweza kupata wokovu mkubwa mno, ambao kwa kweli ni kupandishwa hadhi na Mungu. Kazi hii ni ya maana sana, na ni kwa njia ya hukumu ndipo Anawapata watu hawa. Yeye hawaadhibu kwa makusudi, lakini Amekuja kuwaokoa. Kama bado angekuwa Anafanya kazi ya kushinda katika Israeli wakati wa siku za mwisho ingekuwa ni bure; hata kama ingezaa matunda, haingekuwa na thamani yoyote au umuhimu wowote mkubwa, na Yeye hangeweza kupata utukufu wote. Anafanya kazi kwenu, yaani, wale ambao wameanguka katika maeneo yenye giza zaidi, wao walio nyuma zaidi kimaendeleo. Watu hawa hawakiri kuwa kuna Mungu na kamwe hawajapata kujua kwamba kuna Mungu. Viumbe hawa wamepotoshwa na Shetani hadi kiwango ambapo wamemsahau Mungu. Wamepofushwa na Shetani na hawajui kabisa kwamba kuna Mungu mbinguni. Katika mioyo yenu nyote mnaabudu sanamu, mnamwabudu Shetani—je, si ninyi ni watu wa hali ya chini zaidi, watu walio nyuma zaidi kimaendeleo? Ninyi ni wa hali ya chini kabisa ya mwili, mnakosa uhuru wowote wa kibinafsi, na mnapitia shida pia. Ninyi pia ni watu mlio katika ngazi ya chini kabisa katika jamii hii, bila hata uhuru wa imani. Huu ni umuhimu wa kufanya kazi kwenu. Kufanya kazi kwenu sasa, uzao wa Moabu, sio kuwafedhehesha kwa makusudi, lakini ni kufichua umuhimu wa kazi. Ni kuwainua sana. Ikiwa mtu ana mantiki na utambuzi, atasema: “Mimi ni uzao wa Moabu. Kweli sistahili kuinuliwa kukuu huku na Mungu ambako nimepokea sasa, au baraka hizi nyingi. Kwa mujibu wa yale ninayofanya na kusema, na kulingana na hali na thamani yangu—sistahili kabisa hizo baraka nyingi kutoka kwa Mungu. Waisraeli wana upendo mkubwa kwa Mungu, na neema wanayoifurahia imefadhiliwa kwao na Yeye, lakini hali yao ni ya juu zaidi kuliko yetu. Abrahamu alijitolea sana kwa Yehova, na Petro alijitolea sana kwa Yesu—ibada yao ilishinda yetu kwa mara mia, na kwa msingi wa matendo yetu hatufai kabisa kufurahia neema ya Mungu.” Huduma ya watu hawa nchini China haiwezi kuletwa mbele za Mungu hata kidogo. Ni fujo kamili tu, na kwamba sasa mnafurahia neema nyingi za Mungu ni kuinuliwa na Mungu kabisa! Je, ni wakati upi mmeitafuta kazi ya Mungu? Je, mmeyatoa maisha yenu kwa Mungu lini? Ni wakati gani mmeiacha familia yako kwa urahisi, wazazi wenu, na watoto wenu? Hakuna hata mmoja wenu aliyelipa gharama kubwa! Kama haingekuwa kwa Roho Mtakatifu kukufanya uonekane, wangapi wenu wangeweza kutoa dhabihu kila kitu? Ni kwa sababu tu mmelazimishwa na kushurutishwa ndipo mmefuata hadi leo. Upendo wenu uko wapi? Utiifu wenu uko wapi? Kulingana na matendo vyenu, mngepaswa kuangamizwa muda mrefu uliopita—kufagiliwa mbali kungepaswa kufanywa kwenu. Mna haki gani ya kufurahia baraka nyingi mno—ninyi hamstahili kabisa! Nani kati yenu amebuni njia yake mwenyewe? Ni nani kati yenu ameipata njia ya ukweli mwenyewe? Ninyi nyote ni wavivu na walafi, fidhuli msio na maana ambao mnasherehekea katika faraja kwa tamaa! Mnafikiri ninyi ni wakubwa sana? Je, nini mlicho nacho cha kujivunia? Hata kama Singesema ninyi ni uzao wa Moabu, je, asili yenu, mahali penu pa kuzaliwa ni ya fahari sana? Hata kama Singesema ninyi ni uzao wake, je, si ninyi nyote ni uzao wa Moabu kwa kweli? Ukweli wa mambo unaweza kubadilishwa? Je, kufichua asili yenu sasa kunaenda dhidi ya ukweli wa mambo? Angalieni jinsi mlivyo wanyonge, maisha yenu, na tabia—je, hamjui kwamba ninyi ni wa chini kabisa kati ya walio chini miongoni mwa wanadamu? Nini mlicho nacho cha kujisifia? Angalia nafasi yenu katika jamii. Je, si mko katika kiwango cha chini kabisa? Je, mnadhani kwamba Nimenena vibaya? Ibrahimu alimtoa Isaka. Nini ambacho mmetoa? Ayubu ilitoa kila kitu. Nini ambacho mmetoa? Watu wengi sana wameyatoa maisha yao, wakafa, wakamwaga damu yao ili kutafuta njia ya kweli. Je, mmelipa gharama hiyo? Kwa kulinganisha, hamna sifa zinazostahili hata kidogo kufurahia neema hiyo kubwa, kwa hivyo ni sawa kusema leo kwamba ninyi ni uzao wa Moabu? Msijione kuwa wakuu sana. Huna chochote cha kujisifia. Wokovu mkubwa kama huo, neema hiyo kubwa imepewa kwenu bure. Hamjatoa chochote, lakini mmeifurahia neema bure. Je, hamuoni haya? Je, njia hii ya ukweli ni jambo ambalo ninyi wenyewe mlipata kupitia kutafuta? Je, si ni Roho Mtakatifu aliyewalazimisha kuikubali? Kamwe humkuwa na moyo wa kutafuta na hasa hamkuwa na mioyo ya kuutafuta ukweli, ya kuutamani ukweli. Mmekuwa tu mkistarehe na kuufurahia, na mmeupata ukweli huu bila jitihada kwa upande wenu. Mna haki gani ya kulalamika? Je, unadhani kuwa wewe ni wa thamani kubwa zaidi? Ikilinganishwa na wale ambao walitoa dhabihu maisha yao na kumwaga damu yao, nini mnachopaswa kulalamikia? Kuwaangamiza hivi sasa litakuwa ni jambo linalotarajiwa! Kando na kutii na kufuata, hamna chaguzi zingine. Ninyi hasa hamstahili! Wengi wa wale kati yenu waliitwa, lakini kama mazingira hayangewalazimisha au kama hamngeitwa, hamngekuwa tayari kabisa kutokea wazi. Nani yuko tayari kutelekeza mambo kwa namna hii? Ni nani yuko tayari kuacha anasa za mwili? Ninyi nyote ni watu ambao husherehekea kwa ulafi katika faraja na kutafuta maisha ya anasa! Mmepata baraka nyingi mno—nini kingine mnacho cha kusema? Mna malalamiko yapi? Mmefurahia baraka nyingi mno na neema kuu mno mbinguni, na kazi sasa imefichuliwa kwenu ambayo haikuwahi kufanywa duniani awali. Je, si hii ni baraka? Kwa sababu mmempinga na kuasi dhidi ya Mungu, sasa mmepitia kuadibu kiasi hiki. Kwa sababu ya kuadibu huku mmeziona rehema na upendo wa Mungu, na hata zaidi mmeziona haki na utakatifu Wake. Kwa sababu ya kuadibu huku na kwa sababu ya uchafu wa wanadamu, mmeiona nguvu kuu ya Mungu, na mmeuona utakatifu na ukuu Wake. Je, si huu ni ukweli adimu mno? Je! Si haya ni maisha yenye maana? Kazi ambayo Mungu hufanya ina maana tele! Hivyo nafasi yenu ilivyo chini zaidi, ndivyo inavyoonyesha zaidi kuinuliwa na Mungu, na ndivyo inavyothibitisha zaidi jinsi kazi Yake ilivyo na thamani kwenu leo. Ni hazina yenye thamani mno hasa! Haiwezi kupatikana popote pengine, na kwa muda mrefu hakuna mtu aliyefurahia wokovu mkubwa hivi. Ukweli kwamba nafasi yenu ni ya chini inaonyesha jinsi wokovu wa Mungu ulivyo mkuu, na inaonyesha kwamba Mungu ni mwaminifu kwa wanadamu—Yeye huokoa, sio kuangamiza.
Watu wa Uchina hawajawahi kumwamini Mungu na hawajawahi kumhudumia Yehova, hawajawahi kumhudumia Yesu. Yote wanayofanya ni kusujudu, kufukiza uvumba, kuchoma sanamu ya Mungu ya karatasi, na kumwabudu Buddha. Wao wanaabudu sanamu tu—wote ni waasi mno, hivyo jinsi nafasi ya watu ilivyo ya chini zaidi, ndivyo inavyoonyesha zaidi kwamba kile Mungu hupata kutoka kwenu ni utukufu hata zaidi. Kutoka kwa mtazamo wa watu fulani, wangesema: “Mungu, ni kazi gani Unayofanya? Wewe, Mungu mwenye fahari sana, Mungu mtakatifu mno, ulikuja katika nchi yenye uchafu? Je, Unajidharau sana hivyo? Sisi ni wachafu sana, lakini Uko radhi kuwa pamoja nasi? Uko tayari kuishi kati yetu? Sisi ni wa cheo cha chini sana, lakini Uko radhi kutufanya kuwa kamili? Na Ungetutumia sisi kama mifano na vielelezo? “Ninasema: Huelewi mapenzi Yangu! Huelewi kazi ambayo Nataka kufanya wala huelewi tabia Yangu. Huwezi kufikia umuhimu wa kazi ambayo Ninaenda kufanya. Je, kazi Yangu ingepatana na mawazo ya kibinadamu? Kulingana na mawazo ya kibinadamu, Ningelazimika kuzaliwa katika nchi nzuri ili kuonyesha kwamba mimi ni wa hali ya juu, kuonyesha kwamba Mimi ni wa thamani kubwa, na kuonyesha uheshimiwa, utakatifu, na ukuu Wangu. Kama Ningezaliwa mahali ambapo pananitambua, katika familia ya ngazi ya juu, na kama Ningekuwa wa cheo na hadhi ya juu, basi Ningetendewa vizuri sana. Hiyo haingekuwa na manufaa kwa kazi Yangu, hivyo je, wokovu mkuu mno bado ungeweza kufichuliwa? Wote wanaoniona Mimi wangenitii, na hawangenajisiwa na uchafu. Nilipaswa kuzaliwa katika mahali pa aina hii. Hivyo ndivyo ninyi mnaamini. Lakini litafakari: Je! Mungu alikuja duniani kwa ajili ya raha, au kwa ajili ya kazi? Kama Ningefanya kazi katika aina ya mahali hapo rahisi, mahali penye starehe, je, Ningepata utukufu Wangu kamili? Je, Ningeweza kuvishinda viumbe Vyangu vyote? Mungu alipokuja duniani Yeye hakuwa wa ulimwengu na Yeye hakuwa mwili ili apate kuufurahia ulimwengu. Mahali ambapo kufanya kazi kungefichua tabia Yake vizuri sana na pawe mahali pa maana zaidi ni mahali Alipozaliwa. Kama ni nchi takatifu au yenye uchafu, na bila kujali Anapofanya kazi, Yeye ni mtakatifu. Kila kitu duniani kiliumbwa na Yeye; Ni kwamba tu kila kitu kimepotoshwa na Shetani. Hata hivyo, vitu vyote bado ni Vyake; vyote viko mikononi Mwake. Kuja Kwake katika nchi yenye uchafu kufanya kazi ni kufichua utakatifu Wake; Yeye hufanya hivi kwa ajili ya kazi Yake, yaani, Yeye huvumilia aibu kubwa kufanya kazi kwa njia hii ili kuwaokoa watu wa nchi hii yenye uchafu. Hii ni kwa ajili ya ushuhuda na ni kwa ajili ya wanadamu wote. Kile aina hii ya kazi inawaruhusu watu kuona ni haki ya Mungu, na ina uwezo zaidi wa kuonyesha mamlaka ya juu kabisa ya Mungu. Ukuu na uadilifu Wake vinaonyeshwa kupitia wokovu wa kundi la watu wa hali ya chini ambao hakuna mtu anayewapenda. Kuzaliwa katika nchi yenye uchafu haimaanishi kabisa kuwa Yeye ni duni; inawaruhusu tu viumbe vyote kuuona utukufu Wake na upendo wake wa kweli kwa wanadamu. Zaidi Anavyofanya kwa njia hii, zaidi inavyofichua upendo Wake safi zaidi kwa mwanadamu, upendo wake usio na dosari. Mungu ni mtakatifu na mwenye haki. Hata ingawa Alizaliwa katika nchi yenye uchafu, na ingawa Anaishi na watu hao ambao wamejawa uchafu, kama vile Yesu alivyoishi na wenye dhambi katika Enzi ya Neema, si kazi Yake yote kwa ajili ya kuishi kwa wanadamu wote? Je, si yote ni ili mwanadamu aweze kuupata wokovu mkuu? Miaka elfu mbili iliyopita Aliishi na wenye dhambi kwa miaka kadhaa. Hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya ukombozi. Leo, Anaishi na kikundi cha watu wachafu, wa hali ya chini. Hii ni kwa ajili ya wokovu. Je, si kazi Yake yote ni kwa ajili yenu, wanadamu hawa? Kama haingekuwa ili kuwaokoa wanadamu, kwa nini Angeishi na kuteswa pamoja na wenye dhambi kwa miaka mingi sana baada ya kuzaliwa horini? Na kama haingekuwa ili kuwaokoa wanadamu, kwa nini Angeurudia mwili kwa mara ya pili, kuzaliwa katika nchi hii ambako mapepo hukusanyika, na kuishi na watu hawa ambao wamepotoshwa kwa kina na Shetani? Je, si Mungu ni mwaminifu? Ni aina gani ya kazi Yake ambayo haijakuwa kwa ajili ya wanadamu? Ni aina gani ambayo haijakuwa kwa ajili ya kudura yako? Mungu ni mtakatifu! Hili haliwezi kubadilika. Yeye hanajisiwi na uchafu, ingawa Amekuja katika nchi yenye uchafu; yote haya yanamaanisha tu kwamba upendo wa Mungu kwa wanadamu ni wenye kuwajali wengine sana, mateso na aibu Anayoyavumilia ni makubwa sana! Kwa ajili yenu nyote, na kwa ajili ya kudura yenu, Yeye hupitia aibu kubwa sana. Je, hamjui hivyo? Yeye hawaokoi watu wakuu au wana wa familia tajiri na zenye uwezo, lakini Yeye huwaokoa hasa wale ambao ni wa hali za chini na wanaodharauliwa na wengine. Je, si haya yote ni utakatifu Wake? Je, si haya yote ni haki Yake? Afadhali Azaliwe katika nchi yenye uchafu na kuteseka aibu yote kwa ajili ya kuishi kwa wanadamu wote. Mungu ni halisi sana—Hafanyi kazi ya uwongo. Je, si kila hatua ya kazi Yake imefanyika kwa utendaji hivi? Ingawa watu wote wanamkashifu na kusema kuwa Anakaa mezani pamoja na wenye dhambi, ingawa watu wote wanamdhihaki na kusema kuwa Anaishi na wana wa uchafu, na watu wa hali ya chini sana, bado Anajitolea bila ubinafsi, na bado Anakataliwa kwa njia hii kati ya wanadamu. Je, si mateso Anayoyahimili ni makubwa zaidi kuliko yenu? Je, si kazi Yake ni zaidi ya gharama ambayo mmelipa? Mlizaliwa katika nchi ya uchafu lakini mmepata utakatifu wa Mungu. Mlizaliwa katika nchi ambako mapepo hukusanyika lakini mmepokea ulinzi mkubwa. Je, mna uchaguzi gani mwingine? Ni malalamiko yapi mliyo nayo? Je, si mateso ambayo Amevumilia ni makubwa zaidi kuliko mateso ambayo mmevumilia? Amekuja duniani na hajawahi kufaidi furaha za ulimwengu wa kibinadamu. Anayachukia mambo hayo. Mungu hakuja duniani kufurahia manufaa ya kibinadamu kutoka kwa mwanadamu, wala haikuwa kufurahia mambo mazuri ya wanadamu kula na kuvalia. Hazingatii mambo haya; Alikuja duniani kuteseka kwa ajili ya mwanadamu, si kufurahia mambo mazuri ya kidunia. Alikuja kuteseka, Alikuja kufanya kazi, na kukamilisha mpango Wake wa usimamizi. Hakuchagua mahali pazuri, kuishi katika ubalozi au hoteli ghali mno, wala Hana watumishi kadhaa kumtumikia. Kutokana na kile mmeona, hamjui kama Alikuja kufanya kazi au kufurahia? Je, macho yenu hayafanyi kazi? Amewapa kiasi gani? Kama Angezaliwa katika mahali pazuri Angeweza kuupata utukufu? Je, Angeweza kufanya kazi? Je! Huko kungekuwa na umuhimu wowote? Angeweza kuwashinda kabisa wanadamu? Angeweza kuwaokoa watu kutoka katika nchi ya uchafu? Kulingana na mawazo ya kibinadamu, “Mungu, kwa kuwa Wewe ni mtakatifu, kwa nini Ulizaliwa katika mahali penye uchafu mno kama hapa? Unatuchukia na kutukirihi sisi wanadamu wachafu; Unachukia upinzani wetu na uasi wetu, hivyo kwa nini Unaishi nasi? Wewe ni Mungu mkuu sana—hungeweza kuzaliwa tu popote, lakini ilibidi uzaliwe katika nchi hii yenye uchafu? Unatuadibu na kutuhukumu kila siku na Unajua wazi kwamba sisi ni uzao wa Moabu, basi kwa nini bado Unaishi kati yetu? Kwa nini Ulizaliwa katika familia ya uzao wa Moabu? Kwa nini Ulifanya hivyo? “Aina hii ya ufahamu wenu inakosa mantiki! Ni aina hii ya kazi tu ambayo inawaruhusu watu kuuona ukuu Wake, unyenyekevu na kujificha Kwake. Yuko tayari kutoa kila kitu kwa ajili ya kazi Yake, na Amevumilia mateso yote kwa ajili ya kazi Yake. Anafanya kwa ajili ya wanadamu, na hata zaidi kumshinda Shetani ili viumbe vyote viweze kutii chini ya utawala Wake. Hii tu ni kazi ya maana, yenye thamani. Kama uzao wa Yakobo ungezaliwa nchini China, katika kipande hiki cha ardhi, na wote walikuwa ninyi nyote, basi umuhimu wa kazi iliyofanyika kwenu ingekuwa nini? Shetani angesema nini? Shetani angesema: “Walikuwa wakikuogopa Wewe, lakini hakuna mtu aliyeirithisha kwa muda mrefu. Hata hivyo, mababu zao walikuogopa; Walikutii tangu mwanzo na hawana historia ya kukusaliti. Ni kwamba tu baada ya kipindi cha muda hiyo haikurithishwa tena. Wao si wenye giza kabisa, wa hali ya chini kabisa, au walio nyuma zaidi kimaendeleo kati ya wanadamu. Walikukiri tangu mwanzo. Hakuna umuhimu wa kuifanya kwa njia hiyo! Ikiwa inafanyika hivi kwa kweli, nani atakayeridhishwa na kazi hii? “Kati ya ulimwengu wote, watu wa Kichina ni watu walio nyuma zaidi kimaendeleo. Wamezaliwa na hali ya chini na uadilifu duni, ni wapumbavu na wenye ganzi, nao ni watovu wa adabu na waliofifia. Wameloweshwa na tabia za kishetani, wachafu na waasherati. Mnayo haya yote. Kwa mintarafu ya tabia hizi potovu, baada ya kazi hii kukamilika watu watazitupilia mbali na wataweza kutii kikamilifu na kufanywa kuwa kamili. Tunda tu kutoka kwa aina hii ya kazi ndilo huitwa ushuhuda kati ya viumbe! Je, unaelewa kile kinachoitwa ushuhuda? Je, ushuhuda unapaswa kutolewaje? Aina hii ya kazi imewafanya kuwa foili[a] pamoja na vyombo vya huduma, na hata zaidi, mmekuwa vyombo vya wokovu. Leo ninyi ni watu wa Mungu na baadaye mtakuwa mifano na vielelezo. Katika kazi hii, mnajitwisha majukumu mbalimbali, na hatimaye mtakuwa vyombo vya wokovu. Watu wengi ni hasi kwa sababu ya hili; Je, si wao ni vipofu kabisa? Huwezi kuona chochote waziwazi! Je, cheo hiki tu kinakuzidi? Je, unaelewa kile kinachotajwa kama tabia ya Mungu yenye haki? Je, unaelewa wokovu ni nini? Je, unaelewa upendo wa Mungu ni nini? Huna uaminifu! Unapoona jina zuri unafurahi. Usipoona jina zuri hukubali nawe unarudi nyuma. Wewe ni nini? Hufuati njia ya kweli! Afadhali uache kutafuta mara moja. Ni jambo la aibu! Jambo dogo sana linakuzidi. Je, si hii ni ishara ya aibu?
Afadhali uweze kujijua kiasi. Usijione kuwa mkuu sana, wala usiwazie kwenda mbinguni. Tafuta tu kushindwa hapa duniani kwa kufanya wajibu ipasavyo! Usifikiri kuhusu ndoto hizo zisizo halisi ambazo hazipo. Mtu akisema jambo kama: “Ingawa mimi ni wa uzao wa Moabu, niko tayari kujitahidi kumpata Mungu, na katika siku zijazo nitamkana babu yangu wa zamani! Alinizaa na pia alinikandamiza, na hadi sasa nimekuwa nikiishi tu katika giza. Leo Mungu ameniachilia na hatimaye nimeiona mbingu. Kupitia kwa ufunuo wa Mungu hatimaye nimeona kwamba mimi ni wa uzao wa Moabu. Awali nilikuwa gizani, na sikujua kwamba Mungu amefanya kazi nyingi sana; yote ni kwa sababu nimepofushwa na Shetani huyu wa zamani. Nitamkana na kumuaibisha kabisa.” Haya ni maneno kutoka kwa mtu mwenye hamu ya kupata, mwenye ujasiri. Hivyo mna ujasiri? Licha ya ukweli kwamba mna mfano wa mwanadamu, mnashindwa kustahimili kasi zaidi kuliko mtu mwingine yeyote, nanyi ni wepesi zaidi wa kuathirika kuhusiana na suala hili. Mara tu inapotajwa kwamba ninyi ni uzao wa Moabu, midomo yenu inapinda kwa kuibibidua. Je! Si hii ni tabia ya nguruwe? Haina maana. Mko tayari kutoa dhabihu maisha yenu kwa ajili ya umaarufu na bahati yenu! Huko tayari kuwa uzao wa Moabu, lakini sivyo ulivyo? Ninasema leo kwamba wewe uko hivyo, na lazima ukiri jambo hilo. Siendi kinyume na ukweli. Watu wengine ni hasi kwa sababu ya jambo hili, lakini wewe ni hasi kuhusu nini? Je, si wewe pia ndiye mtoto wa joka kubwa jekundu? Je, ni udhalimu kusema kwamba wewe ni uzao wa Moabu? Angalia kile unachoishi kwa kudhihirisha, ndani na nje. Kutoka kichwani hadi mguuni, hakuna kitu cha kujisifia. Uasherati, uchafu, upofu, upinzani, uasi—si haya yote ni sehemu ya tabia yako? Daima wewe huishi ndani ya nchi ya uasherati nawe hufanya uovu wote. Unadhani kuwa wewe ni mtakatifu wa ajabu sana, lakini hebu yalinganishe mambo ambayo umeyafanya. Unafurahishwa sana na matokeo yako—nini ulicho nacho cha kujisifia? wewe ni kama wanyama, huna ubinadamu! Mnaafikiana na wanyama, mnaishi ndani ya uovu, dhana za kiasherati. Je! Mnakosa kiasi gani? Mnakubali kwamba ninyi ni watoto wa joka kubwa jekundu, na mko tayari kufanya huduma, lakini baadaye inaposemekana kuwa wewe ni uzao wa Moabu unakuwa hasi. Je! Si huu ni ukweli? Sawasawa na ulivyozaliwa na mama na baba yako, haijalishi jinsi walivyo wabaya, bado ulizaliwa na wao. Hata ukipata mama wa kambo na kuondoka katika nyumba hiyo, je, si wewe bado ni mtoto wa wazazi wako wa mwanzo? Je! Ukweli huo unaweza kubadilishwa? Je, nimekupachika tu jina kwa kubahatisha? Watu wengine wanasema: "Je! Si ungenipa tu jina lingine?” Ninasema: “Je, unaonaje Nikikupa jina la foili[a]?" Hawataki kuwa foili[a] pia. Basi unataka kuwa nini? Foili[a], watendaji huduma—si ninyi mko hivi? Ungechagua nini kingine? Je, si wewe ni mtu aliyezaliwa katika nchi ya joka kubwa jekundu? Haijalishi ni kiasi gani unasema kuwa wewe ni mwana wa Daudi, haikubaliani na ukweli. Je, hili ni jambo ambalo wewe mwenyewe ulichagua? Je, unaweza tu kutumia jina zuri kujitaja kwa kubahatisha? Je! Si watoto wa joka kubwa jekundu waliozungumziwa zamani ni nyinyi, kundi hili la watu waliopotoshwa? Watendaji huduma waliotajwa—je, si wao pia ni nyinyi, watu hawa waliopotoshwa? Vielelezo vilivyoshindwa, mifano iliyotajwa— si hivi pia ni nyinyi, watu hawa? Njia ya kukamilishwa—si hilo linasemwa kwa ajili yenu? Wale ambao wanaadibiwa na kuhukumiwa ni nyinyi, na si wale wanaokamilishwa baadaye watakuwa baadhi ya wale miongoni mwenu? Je, jina hili lina maana? Ninyi ni wapumbavu sana kiasi kwamba hamuwezi hata kuona kitu hicho kidogo kwa dhahiri? Hujui nani ni uzao wa nani, lakini Niko dhahiri kulihusu. Nawaambieni. Ikiwa unaweza kulitambua leo hivyo ni vizuri. Usijidhalilishe kila wakati. Zaidi unavyokuwa hasi na kurudi nyuma, ndivyo inavyoonyesha zaidi kwamba wewe ni uzao wa Shetani. Kuna mtu ambaye, unapomtaka asikilize wimbo, anasema: “Je, uzao wa Moabu hutumia vinasasauti? Sitausikiliza; Mimi sistahili!” Ukimtaka aimbe, anasema: “Ikiwa uzao wa Moabu unaimba, Je, Mungu yuko radhi kusikiliza? Mungu ananichukia. Nina aibu sana kwenda mbele za Mungu na siwezi kushuhudia Kwake. Sitaimba kabisa, Mungu asije akakasirika Anapousikia.” Je! Si hii ni njia hasi ya kulishughulikia? Kama mmoja wa viumbe, ulizaliwa katika nchi ya uasherati na wewe ni mtoto wa joka kubwa jekundu, uzao wa Moabu; unapaswa kumkana babu yako wa zamani na kumkana Shetani wa zamani. Huyu tu ndiye mtu anayemtaka Mungu kwa kweli.
Mwanzoni nilipowapa nafasi ya watu wa Mungu mlikuwa mnaruka juu chini—mliruka kwa furaha zaidi kuliko mtu yeyote. Lakini ilikuwaje mara Niliposema kuwa ninyi ni uzao wa Moabu? Ninyi nyote mlishindwa kustahimili! Ungesema kimo chenu kipo wapi? Dhana yenu ya nafasi ni nzito sana! Wengi hawawezi kujiinua. Wengine huenda kufanya biashara, na wengine huenda kazini. Mara tu Ninaposema kwamba ninyi ni uzao wa Moabu nyote mnataka kukimbia. Je, huku ndiko kushuhudia kwa Mungu ambako huwa mnapigia kelele wakati wote? Je! Shetani ataridhishwa kwa njia hii? Si hii ni alama ya aibu? Ni faida gani kuwa na nyinyi? Ninyi nyote ni taka! Ni mateso ya namna gani ambayo mmestahimili, lakini mnahisi kuwa mmetendewa mabaya sana? Mnafikiri kwamba mara tu Mungu amewatesa hadi kiwango fulani Atafurahi, kana kwamba Mungu alikuja kuwahukumu kimakusudi, na baada ya kuwahukumu na kuwaangamiza, kazi Yake itakuwa imekamilika. Je, ni hivyo ndivyo Nimesema? Je, si hii ni kwa sababu ya upofu wenu? Je! Ni kwamba ninyi wenyewe hamjitahidi kufanya vizuri au kwamba Ninawahukumu kwa makusudi? Sijawahi kufanya hivyo—hilo ni jambo ambalo mlilifikiria wenyewe. Sijafanya kazi kwa njia hiyo kabisa, wala Sina nia hiyo. Kama Ningetaka kuwaangamiza kwa kweli, je, Ningehitaji kuteseka sana hivyo? Ningetaka kuwaangamiza kwa kweli, Ningehitaji kuzungumza nanyi kwa dhati? Mapenzi Yangu ni haya: wakati ambapo Nimewaokoa ndipo Nitakapoweza kupumzika. Zaidi mtu alivyo wa hali ya chini, ndivyo alivyo chombo cha wokovu wangu zaidi. Zaidi mwezavyo kuingia kiutendaji, ndivyo Nitakavyofurahia zaidi. Zaidi mnavyoshindwa kustahimili ndivyo Ninavyofadhaika zaidi. Daima mnataka kuingia kwa mwendo wa furaha kuelekea kiti cha enzi, lakini Nitawaambieni, hiyo sio njia ya kuwaokoa kutokana na uchafu. Njozi ya kukaa kwa kiti cha enzi haiwezi kukufanya kuwa mkamilifu; hiyo si kweli. Nasema kuwa wewe ni uzao wa Moabu, kisha unakuwa na huzuni. Unasema: “Unataka niende kuzimu. Sitakuwa na ushuhuda Kwako au kuteswa kwa ajili Yako.” Je, si kufanya kwako hivi ni kunipinga Mimi? Je, hili ni la manufaa kwako? Nimekupa neema nyingi sana—umesahau? Moyo wa Mungu ambao ni kama tu mama mwenye upendo umegeuka kuwa maji baridi kwa sababu yako na kuwa barafu. Je! Shetani atakuachilia huru? Ikiwa hushuhudii Kwangu Sitakuhimiza lakini unapaswa kujua kwamba hatimaye utakuwa lengo la maangamizo. Ikiwa Siwezi kupata ushuhuda ndani yako, Nitaupata kwa watu wengine. Hilo halina maana Kwangu, lakini mwishowe utalijutia, na wakati huo utakuwa umeanguka gizani muda mrefu uliopita. Basi nani atakayeweza kukuokoa? Usifikiri kwamba kazi haiwezi kufanyika bila wewe. Hakungekuwa na wengi sana pamoja na wewe, na hakungekuwa na wachache sana bila wewe. Usijione kuwa mheshimiwa sana. Ikiwa hutaki kunifuata, hiyo inaonyesha tu kwamba wewe ni muasi, na hakuna kitu cha kutamanisha ndani yako. Ikiwa wewe ni msemaji mzuri, si hivyo ni kwa sababu tu umejiandaa na maneno Niliyoyaleta kupitia kwa kazi Yangu? Nini ulicho nacho cha kujisifia? Usiruhusu mawazo yako yafikie hitimisho lisilo la msingi! Ikiwa Siwezi kupata utukufu kutoka kwenu, uzao huu wa Moabu, Nitachagua kikundi cha pili, na cha tatu cha uzao wa Moabu kufanya kazi mpaka Nipate utukufu. Ikiwa huko radhi kuwa na ushuhuda Wangu, basi toka nje! Sitakulazimisha! Usifikiri kwamba Nitashindwa kusonga hatua bila ninyi. Kupata vyombo vinavyofaa kwa kazi Yangu katika nchi hii ya China hakuhitaji jitihada. Hakuna kitu kingine chochote kinachoweza kupatikana katika nchi hii—watu wachafu, wapotovu bila shaka wako kila mahali na kazi Yangu inaweza kufanyika popote. Usiwe na kiburi sana! Bila kujali wewe ni mwenye kiburi vipi, je, si bado wewe ni mtoto aliyezaliwa kutokana na uzinzi? Angalia thamani yako, na ni chaguo gani lingine ulilo nalo? Kukukubali tu kuishi ni kuinuliwa kukubwa, kwa hivyo ni nini unajivunia? Kama haingekuwa kwa ajili ya kazi Yangu kukomesha enzi, je, si ungekuwa umeanguka katika majanga ya kawaida na maafa ya kibinadamu zamani sana? Je! Unaweza bado kuishi kwa raha sana? Bado daima unabishana kuhusu suala hili. Tangu Niliponena kuhusu uzao wa Moabu umekuwa ukibibidua midomo wakati wote. Hufanyi uchunguzi, husomi, na unamchukia kila mtu. Unapowaona watu wengine wakifanya uchunguzi unawavuruga na kusema mambo ya kuwavunja moyo. Una ujasiri! Unasema: “Uzao wa Moabu unajifunza nini? Sitajifunza kwa ajili Yake. "Je, si hili ni jambo ambalo mnyama angesema? Je, hata unafikiriwa kuwa mwanadamu? Nimesema mambo mengi kwako, lakini haijafanikisha chochote. Je, Nimefanya kazi hii yote bure? Je, Nimesema maneno haya yote bure? Kama ungekuwa mbwa bado ungeutikisa mkia wako; mtu wa aina hiyo siye hata sawa na mbwa! Wakati mwingine unabibidua midomo, wakati mwingine unatazama kwa shaka—je, kazi hii yote iliyofanyika kwako ilikuwa ya bure? Mara tu Ninaponena kuhusu uzao wa Moabu, watu wengine hujishusha hadhi kimakusudi. Wanavaa tofauti kuliko hapo awali nao ni wachafu sana kisai kwamba hawaonekani kama watu, nao hunung’unika: “Mimi ni uzao wa Moabu, sifai kitu. Hata hivyo hakuna kitu kizuri ndani yangu na sitaki kupata baraka zozote. Kwa vyovyote, hivi ndivyo ilivyo. Je, uzao wa Moabu unaweza kufanywa kuwa mkamilifu? "Mara tu Ninaponena kuhusu uzao wa Moabu, watu wengi hawana matumaini tena, na kusema: “Mungu anasema kwamba sisi ni uzao wa Moabu—hii inaonyesha nini? Kwa kuchunguza toni ya sauti Yake, hakuna uwezekano wa ukombozi! Hakuna upendo katika maneno Yake. Je! Si sisi ni malengo ya maangamizo? “Je! Umesahau kile kilichosemwa hapo awali? Leo neno “uzao wa Moabu” ni jambo pekee ambalo umekumbuka? Kwa kweli, maneno mengi ni kwa ajili ya kufikia kitu, lakini pia yanafichua ukweli wa mambo. Watu wengi hawaliamini. Huko tayari kuteseka kwa njia hiyo kwa ajili Yangu. Unaogopa kifo na daima unataka kutoroka. Ikiwa unataka kwenda Sitakulazimisha kukaa, lakini ni lazima Nikweleze wazi jambo moja: Usiishi maisha yote bure, na usisahau mambo yote Nilivyokwambia zamani. Kama mmoja wa viumbe unapaswa kutekeleza wajibu wa mmoja wa viumbe. Usifanye mambo dhidi ya dhamiri yako; unachopaswa kufanya ni kujitolea kwa Bwana wa uumbaji. Uzao wa Moabu pia ni sehemu tu ya uumbaji, ni kwamba tu wamelaaniwa. Chochote kitokeacho, bado wewe ni mmoja wa viumbe. Ikiwa unasema: “Ingawa mimi ni uzao wa Moabu, nimefurahia neema nyingi ya Mungu mbeleni, hivyo ni lazima niwe na dhamiri. Nitakiri tu lakini sitafikiri sana kulihusu. Hata kama nitateseka ndani ya mkondo huu, nitateseka mpaka mwisho. Kama mimi ni wa uzao wa Moabu basi iwe hivyo! Bado nitafuata hadi mwisho. “Ikiwa unasema hivi, basi huko mbali sana. Lazima ufuate mpaka mwisho. Ukikimbia kwa kweli huna matumaini ya baadaye — umeingia kwenye barabara ya maangamizo.
Ni vizuri kuwafanya muelewe asili yenu, na kuwafanya muuelewe ukweli wa mambo ni wenye manufaa kwa kazi. Vinginevyo, matokeo ambayo yanapaswa kufanikishwa hayatafanikishwa. Hii ni sehemu ya kazi ya kushinda, na ni hatua muhimu katika kazi. Huo ni ukweli. Kufanya kazi hii ni kuziamsha roho za watu, kuamsha hisia za dhamiri zao na kuwaruhusu watu kupata wokovu huu mkubwa. Ikiwa mtu ana dhamiri, anapoona kwamba yeye ni wa hali ya chini anapaswa hasa kumshukuru Mungu. Anayashika maneno Yake kwa nguvu, anaishika kwa nguvu neema ambayo Amempa, na hata kulia kwa uchungu na kusema: “Nafasi yetu ni ya chini sana na hatujapata chochote duniani. Hakuna mtu kutuheshimu, watu hawa wa hali ya chini. Tunateswa katika mazingira yetu ya nyumbani, waume zetu hutukana, wake zetu hutushutumu, watoto wetu hutudharau, na tunapokuwa wazee, binti zetu wakwe pia hututesa. Hakika hatujateseka kidogo, na kwamba sasa tunafurahia upendo mkuu wa Mungu ni furaha sana! Kama haungekuwa wokovu wa Mungu kwetu, tungewezaje kung’amua mateso ya kibinadamu? Je, si bado tungekuwa tumepakazwa matope katika dhambi hii? Je, huku si Mungu kutuinua? Mimi ni mmoja wa watu duni kabisa na Mungu ameniinua juu sana. Hata kama nitaangamia bado lazima niulipize upendo Wake. Mungu anaweza kutuheshimu na kunena uso kwa uso nasi, watu duni mno, na hata kama Yeye huniadibu—ninaweza kusema nini? Je, si kuadibu pia ni kuinua Kwake? Hata ikiwa ninaadibiwa bado naweza kuiona nguvu Yake kuu. Siwezi kuwa bila dhamiri—lazima niulipize upendo Wake. Siwezi kuwa muasi sana dhidi ya Mungu. Yeye hunena nami uso kwa uso na Hunifundisha kwa kuushika mkono wangu. Yeye huniandalia kila kitu, Huishi pamoja nami, na Huteseka pamoja nami.” Nafasi ya Mungu na hadhi Yake si sawa na ya watu, lakini mateso Yake ni sawa, na kile Anachokula na kuvaa ni sawa, ni watu wote tu humheshimu—hii ndiyo tofauti pekee. Je, si kila kitu kingine ambacho kinafurahiwa ni sawa? Hivyo mna haki gani kuwa na mengi ya kusema kulihusu? Mungu amevumilia mateso makubwa mno na kufanya kazi kubwa sana, na nyinyi—mlio chini kuliko mchwa, kuliko wadudu—mmepata kuinuliwa pakubwa leo. Ikiwa huwezi kuulipiza upendo wa Mungu, dhamiri yako iko wapi? Watu wengine hunena kutoka mioyoni mwao na kusema: “Kila wakati nikifikiri kuondoka kutoka kwa Mungu macho yangu yanajawa na machozi nami nahisi kuhukumiwa na dhamiri yangu. Mimi ni mwenye kuwiwa kwa Mungu. Siwezi kufanya hivi. Siwezi kuwa namna hiyo Kwake. Ningekufa na kufa kwangu kuipe kazi Yake utukufu, nitaridhika kupita kiasi. Vinginevyo, hata nikiishi sitahisi amani. “Sikiliza maneno haya—huu ndio wajibu ambao kiumbe anapaswa kutimiza. Ikiwa mtu anakuwa na maono haya ndani yake kila mara, atahisi kuwa dhahiri na starehe ndani yake; atakuwa na uhakika wa mambo haya. Utasema: “Mungu haniumizi na Hanifedheheshi kimakusudi wala Haniaibishi. Ingawa Ananena kwa ukali kwa kiasi fulani na huuchoma moyo, ni kwa ajili yangu mwenyewe. Ingawa Ananena kwa ukali namna hiyo, bado Ananiokoa, na Yeye bado ni mwenye huruma kwa udhaifu wangu. Hanihukumu na ukweli. Naamini kwamba Mungu ni wokovu.” Ikiwa kweli una maono haya, hutafikia kiwango cha kukimbia. Katika dhamiri yako, unaweza kuhisi kuwa umekosea, unaweza kuhisi shutuma, kwamba hupaswi kumtendea Mungu kwa namna hiyo. Unafikiri kuhusu neema yote uliyoipata, maneno yote ambayo umeyasikia—je, unaweza kuyasikiliza bure? Haijalishi ni nani anakimbia, wewe huwezi. Watu wengine hawaamini, lakini lazima wewe uamini. Watu wengine wanamtelekeza Mungu, lakini lazima wewe umtetee Mungu na kushuhudia Kwake. Wengine humkashifu Mungu, lakini wewe huwezi. Haijalishi jinsi Mungu asivyo na huruma kwako, bado unapaswa kumtendea vyema. Unapaswa kuulipiza upendo Wake na lazima uwe na dhamiri, kwa sababu Mungu hana hatia. Kuja Kwake duniani kutoka mbinguni kufanya kazi miongoni mwa wanadamu kulikuwa aibu kubwa tayari. Yeye ni mtakatifu bila uchafu hata kidogo. Kuja kwenye nchi ya uchafu—ni fedheha kiasi gani ambayo Amevumilia? Kufanya kazi ndani yenu ni kwa ajili yenu. Ikiwa huna dhamiri katika kumtendea Yeye, ingekuwa bora kufa kifo cha mapema!
Hivi sasa, watu wengi wanakosa kipengele hiki cha maono na hawawezi kabisa kuielewa kazi hii na hawajui nini Mungu anataka hasa kukamilisha kupitia kazi hii. Hasa wale waliokanganyika—ni kama wameingia katika matata mengi na kutunduwazwa baada ya zamu chache. Ukifafanua kikamilifu lengo la mpango wa usimamizi wa Mungu kwao, basi hiyo haingekuwa hivyo. Watu wengi hawawezi kulielewa, na wanaamini kwamba kazi ya Mungu ni kuwatesa watu. Hawaelewi hekima na maajabu ya kazi Yake, na hawaelewi kwamba kazi Yake ni kufichua nguvu Yake kuu, na hata zaidi ni kuwaokoa wanadamu. Hawaoni yote hayo, wao huona tu kama wana matumaini yoyote, na kama wataweza kuingia mbinguni. Wanasema: Kazi ya Mungu daima ni ya mzunguko; kama ungetufanya tu tuione hekima Yako moja kwa moja hiyo ingekuwa vizuri. Hupaswi kututesa kwa njia hii. Tunakosa sana katika ubora wa tabia na hatuyafahamu mapenzi Yako. Ingekuwa vizuri sana kama Ungenena na kutenda tu moja kwa moja. Unatufanya tukisie, lakini hatuwezi. Ingekuwa vizuri kama Ungeharakisha na kuturuhusu tuuone utukufu Wako. Nini haja ya kufanya mambo kwa njia ya mzunguko? “Kile mnachokosa sana sasa ni dhamiri. Zingatieni hili zaidi na fungueni macho yenu wazi kabisa ili muone nani hasa anayefanya hatua kwa hatua kwa kazi. Msifikie uamuzi upesi bila kutafakari. Sasa umeelewa zaidi kwa juujuu njia ya maisha unayopaswa kupitia. Bado kuna kiasi kikubwa cha ukweli ambacho unapaswa kupitia, na siku inapokuja ambapo unaweza kuuelewa kikamilifu, hutasema hivyo tena, wala hutalalamika. Wala hutaufafanua bila uzito. Utasema: "Mungu ni mwenye busara sana, mtakatifu sana. Yeye ni mwenye nguvu sana!"
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Jumapili, 24 Februari 2019

Unapaswa Kutafuta Njia ya Uwiano na Kristo

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,

Unapaswa Kutafuta Njia ya Uwiano na Kristo

Mwenyezi Mungu alisema, Nimefanya kazi kubwa miongoni mwa binadamu, na maneno ambayo Nimeeleza wakati huu yamekuwa mengi. Maneno haya ni kwa ajili ya wokovu wa mwanadamu, na yalikuwa yanaeleza ili binadamu aweze kulingana na Mimi. Ilhali Nimewapokea watu wachache tu duniani ambao wanalingana na Mimi, na hivyo Nimesema kwamba binadamu hathamini maneno Yangu, kwa kuwa binadamu halingani na Mimi. Kwa njia hii, kazi ambayo Naifanya sio tu kwa ajili ya mwanadamu aweze kuniabudu; muhimu zaidi, ni kwa ajili ya mwanadamu aweze kulingana na Mimi. Watu, ambao wamepotoshwa, wote huishi katika mtego wa Shetani, wao kuishi katika mwili, kuishi katika tamaa za ubinafsi, na hakuna hata mmoja kati yao anayelingana na Mimi. Kuna wale ambao wanasema kwamba wao wanalingana na Mimi, lakini ambao wote huabudu sanamu zisizo yakini. Ingawa wanakubali jina Langu kama takatifu, wao hutembea kwenye njia ambazo huenda kinyume na Yangu, na maneno yao yamejaa kiburi na kujiamini, kwa sababu, katika mizizi, wote wananipinga na hawalingani Nami. Kila siku wao hutafuta dalili Yangu katika Biblia, na kupata vifungu "vinavyofaa" hapa na pale wanavyovisoma bila kukoma, na ambavyo wao hukariri kama maandiko. Hawajui jinsi ya kulingana na Mimi, hawajui maana ya kuwa katika uadui na Mimi, na wanasoma tu maandiko kwa upofu. Wao huzuia ndani ya Biblia na Mungu asiye yakini ambaye hawajawahi kumwona, na hawana uwezo wa kumwona, na wao huitoa tu na kuiangazia wakati wao wa ziada. Wao wanaamini kuwepo Kwangu tu ndani ya eneo la Biblia. Kwa fikira zao, Mimi ni sawa na Biblia; bila Biblia Mimi sipo, na bila Mimi hakuna Biblia. Wao hawatilii maanani kuwepo Kwangu au matendo, lakini badala yake hujishughulisha na umakini mno na maalum kwa kila neno la Maandiko, na wengi wao hata huamini kwamba Mimi sipaswikufanya jambo lolote Nipendalo kufanya ila tu kama lilitabiriwa na Maandiko. Wao hutia umuhimu mwingi sana kwa Maandiko. Inaweza kusemwa kwamba wao huona maneno na maonyesho yakiwa muhimu mno, kwa kiasi kwamba wao hutumia mistari ya Biblia kupima kila neno Ninalolisema, na kunilaani Mimi. Wanalotafuta si njia ya uwiano na Mimi, au njia ya uwiano na ukweli, lakini njia ya uwiano na maneno ya Biblia, na wanaamini kwamba chochote ambacho hakiambatani na Biblia, bila ubaguzi, si kazi Yangu. Je, si watu wa namna hiyo ni wazawa watiifu wa Mafarisayo? Mafarisayo Wayahudi walitumia sheria ya Musa kumhukumu Yesu. Hawakutafuta uwiano na Yesu wa wakati huo, bali waliifuata sheria kwa makini, kwa kiasi kwamba wao hatimaye walimpiga misumari Yesu asiye na hatia juu ya msalaba, baada ya kumshitaki Yeye kwa kukosa kufuata sheria za Agano la Kale na kutokuwa Masihi. Kiini chao kilikuwa ni nini? Haikuwa kwamba hawakutafuta njia ya uwiano na ukweli? Walitamani na kutilia maanani mawazo yao na kila neno la Maandiko, bila kuyajali mapenzi Yangu na hatua na mbinu za kazi Yangu. Hawakuwa watu waliotafuta ukweli, ila walikuwa watu waliofuata maneno ya Maandiko kwa uimara; hawakuwa watu walioamini katika Mungu, bali walikuwa watu walioamini katika Biblia. Kimsingi, walikuwa walinzi wa Biblia. Ili kulinda maslahi ya Biblia, na kuzingatia hadhi ya Biblia, na kulinda sifa za Biblia, wao walitenda kiasi kwamba walimsulubisha Yesu mwenye huruma msalabani. Haya walifanya tu kwa ajili ya kuitetea Biblia, na kwa ajili ya kudumisha hali ya kila neno la Biblia katika mioyo ya watu. Hivyo waliona ni heri kuyaacha maisha yao ya baadaye na sadaka ya dhambi kwa sababu ya kumhukumu Yesu, ambaye hakuwa Anazingatia kanuni za Maandiko, mpaka kifo. Je hawakuwa watumishi kwa kila mojawapo ya maneno ya Maandiko?
Na je watu leo? Kristo amekuja kutoa ukweli, lakini wanaona ni afadhali wao kumfukuza Yeye kutoka kati ya wanadamu ili wapate kuingia mbinguni na kupokea neema. Wanaona ni afadhali kabisa kukataa kuja kwa ukweli, ili kulinda maslahi ya Biblia, na ni afadhali kumtundika Kristo ambaye Alirudi kwa mwili kwa misumari msalabani tena ili kuhakikisha kuwepo kwa Biblia milele. Jinsi gani mwanadamu anaweza kupokea wokovu Wangu, wakati moyo wake una nia mbaya namna hiyo, na asili yake inanipinga Mimi? Mimi huishi miongoni mwa wanadamu, ilhali bado wanadamu hawajui kuhusu kuwepo Kwangu. Ninapoangaza mwanga Wangu juu ya wanadamu, bado yeye hana ufahamu kuhusu kuwepo Kwangu. Wakati Ninatoa ghadhabu Yangu juu ya wanadamu, wao hukanusha kuwepo Kwangu kwa nguvu kubwa zaidi. Binadamu hutafuta uwiano na maneno, na Biblia, ilhali bado hakuna mwanadamu hata mmoja huja Kwangu kutafuta njia ya uwiano na ukweli. Binadamu huniheshimu sana Nikiwa mbinguni, na kujishughulisha hasa na kuwepo Kwangu mbinguni, ilhali hakuna anayenijali Nikiwa katika mwili, kwa maana Mimi Ninayeishi miongoni mwa wanadamu sina umuhimu kwao hata kidogo. Wale ambao hutafuta tu uwiano na maneno ya Biblia, na ambao hutafuta tu uwiano na Mungu asiye yakini, mbele Yangu ni fidhuli. Hiyo ni kwa sababu wanachokiabudu ni maneno yaliyokufa, na Mungu Aliye na uwezo wa kuwapa hazina isiyoambilika. Wanachoabudu ni mungu anayedhibitiwa na mtu, na ambaye hayuko. Ni nini, basi, ambacho watu wa namna hiyo wanaweza kupokea kutoka Kwangu? Mwanadamu ni kiumbe duni sana kiasi kwamba maneno hayawezi kueleza hali yake. Wale wanaonipinga, wanaofanya madai yasiyo na kipimo dhidi Yangu, wasio na upendo kwa ukweli, wanaoniasi—wangewezaje kulingana na Mimi?
Wale wanaonipinga ni wale ambao hawalingani na Mimi. Vile vile wale wasiopenda ukweli, na wale wanaoniasi ndio walio wapinzani Wangu zaidi na hawalingani na Mimi. Wale wote ambao hawalingani na Mimi Nawawasilisha mikononi mwa yule mwovu. Ninawaacha wao kwa upotovu wa yule mwovu, Nawaachilia huru ili wafichue maovu yao, na hatimaye kuwakabidhi kwa yule mwovu ili waliwe. Mimi Sijali ni watu wangapi wananiabudu, ambayo ni kusema, Sijali ni watu wangapi wanaamini ndani Yangu. Kinachonijalisha ni watu wangapi wanalingana na Mimi. Hiyo ni kwa sababu wote wasiolingana na Mimi ni wale waovu wanaonisaliti; wao ni adui Zangu, Nami "Sitawatunza" adui Zangu katika nyumba Yangu. Wale ambao wanalingana na Mimi watanitumikia milele katika nyumba Yangu, na wale wanaojiweka katika uadui na Mimi watateseka milele katika adhabu Yangu. Wale wanaojali tu kuhusu maneno ya Biblia, wasiojali kuhusu ukweli au kutafuta nyayo Zangu—wao wananipinga, kwa kuwa wao wananizuilia Mimi kulingana na Biblia, na kuniwekea vizuizi ndani ya na Biblia, na hivyo ni wa kukufuru pakubwa dhidi Yangu. Jinsi gani watu wa aina hii wanaweza kuja mbele Zangu? Wao hawatilii maanani matendo Yangu, au mapenzi Yangu, au ukweli, badala yake wanashikilia maneno, maneno yanayoua. Jinsi gani watu kama hao wanaweza kulingana na Mimi?
Nimeeleza maneno mengi sana, na pia nimeeleza mapenzi Yangu na tabia, lakini hata hivyo, bado watu hawana uwezo wa kunijua Mimi na kuniamini. Au, inaweza kusemwa, bado hawana uwezo wa kunitii. Wale wanaoishi katika Biblia, wale wanaoishi katika sheria, wale wanaoishi juu ya msalaba, wale ambao wanaishi kwa mujibu wa mafundisho, wale wanaoishi miongoni mwa kazi Ninayofanya leo—yupi kati yao analingana na Mimi? Ninyi mnafikiria tu kupokea baraka na tuzo, na hamjawahi kamwe kufikiria jinsi ya kulingana na Mimi, au jinsi ya kujizuia wenyewe kutoka katika uadui na Mimi. Nimeaibishwa sana na nyinyi, kwa kuwa Nimewapa mengi sana, ilhali Mimi Nimepokea kidogo sana kutoka kwenu. Udanganyifu wenu, kiburi chenu, tamaa yenu, tamaa yenu yenye fujo, usaliti wenu, kuasi—lipi kati ya haya linaweza kujificha kutoka kwa macho Yangu? Mnafanya mzaha na Mimi, mnanidanganya Mimi, mnanitusi, mnanilaghai, mnanilazimisha, mnapata sadaka kutoka Kwangu kwa nguvu—ni jinsi gani tabia ya kudhuru kama hii itaepuka ghadhabu Yangu? Udhalimu wenu ni thibitisho la uadui wako Kwangu, na ni thibitisho la uwiano wenu na Mimi. Kila mmoja wenu anaamini mwenyewe akilingana na Mimi, lakini ikiwa ni hivyo, basi ni kwa nani ushahidi huu dhahiri unatumika? Mnaamini wenyewe kwamba mnao ukweli wa juu sana na uaminifu Kwangu. Mnafikiri kwamba nyinyi ni wema sana, wenye huruma sana, na mmetoa sana Kwangu. Mnafikiri kwamba mmefanya vya kutosha kwa ajili Yangu. Bado hamjawahi kulinganisha imani hizi dhidi ya tabia zenu wenyewe? Nasema mmejaa mengi ya kiburi, tamaa nyingi, wingi wa uzembe; hila mnayotumia kunidanganya ni janja sana, na mna mengi ya nia ya kudharau na mbinu ya kudharau. Uaminifu wenu pia ni mdogo, bidii yenu pia ni ndogo, na dhamiri yako hata haipo zaidi. Kuna mabaya mengi sana katika nyoyo zenu, na hakuna mtu atakayesamehewa kutoka kwa hayo, hata Mimi mwenyewe. Mnanifungia nje kwa ajili ya watoto wenu, au waume wenu, au kwa ajili ya hifadhi zenu wenyewe. Badala ya kunijali, mnajali familia zenu, watoto wenu, hali yenu, maisha yenu ya baadaye, na kujitosheleza wenyewe. Ni lini mmewahi kuniwaza Mimi mnapozungumza au kutenda? Wakati hali ya hewa ni baridi, mawazo yenu hurejea kwa watoto wenu, waume wenu, wake wenu, au wazazi wenu. Wakati hali ya hewa ni ya joto, hata Siwezi kupata nafasi katika mawazo yenu pia. Unapotekeleza wajibu wako, wewe huwaza tu kuhusu maslahi yako mwenyewe, ya usalama wako mwenyewe binafsi, ya watu wa familia yako. Ni nini umewahi kufanya kwa ajili Yangu? Ni lini umeweza kuwaza kunihusu Mimi? Ni lini umewahi kujitoa mwenyewe, kwa gharama yoyote, kwa ajili Yangu na kazi Yangu? Uko wapi ushahidi wa uwiano wako na Mimi? Uko wapi ukweli wa uaminifu wako kwa ajili Yangu? Uko wapi ukweli wa utiifu wako Kwangu? Ni lini mujibu wako hujakuwa kwa sababu ya kupokea baraka Zangu? Mnanilaghai na kunidanganya Mimi, mnacheza na ukweli na kuficha kuwepo kwa kweli, na kuisaliti dutu ya ukweli, na mnajiweka wenyewe kwa uadui kama huu na Mimi. Basi, ni nini kinawangoja katika siku za usoni? Ninyi mnatafuta tu uwiano na Mungu asiye yakini, na kutafuta tu imani zisizo yakini ilhali ninyi hulingani na Kristo. Si uovu wenu utapata adhabu kama ile wanayostahili waovu? Wakati uo huo, mtagundua kuwa hakuna mtu yeyote asiyelingana na Kristo atakayeepuka siku ya ghadhabu, na mtagundua ni aina gani ya adhabu italetwa juu ya wale walio katika uadui na Kristo. Siku hiyo itakapofika, ndoto yenu ya kubarikiwa kwa imani yenu katika Mungu na kupata kuingia mbinguni, yote itakatizwa. Lakini, hata hivyo, si hivyo kwa wale ambao wanalingana na Kristo. Ingawa wao wamepoteza sana, ingawa wamekabiliwa na mengi ya ugumu wa maisha, watapokea urithi wote ambao Nimeutoa kwa ajili ya mwanadamu. Hatimaye, mtaelewa kwamba Mimi tu ndiye Mungu mwenye haki, na kwamba ni Mimi tu Niliye na uwezo wa kuwachukua binadamu mpaka kwenye hatima yao yenye kupendeza.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Jumamosi, 23 Februari 2019

Matamshi ya Mungu | “Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II" Sehemu ya Pili

Matamshi ya Mungu | “Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II" Sehemu ya Pili

Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”. Maudhui ya video hii: Kuhusu Ayubu Katika Maisha ya Kila Siku ya Ayubu Tunaona Utimilifu, Unyofu, Kumcha Mungu, na Kujiepusha na Maovu Kwake Maonyesho ya Ubinadamu wa Ayubu Wakati wa Majaribio Yake (Kuelewa Utimilifu wa Ayubu, Unyofu, Kumcha Mungu na Kujiepusha na Maovu Wakati wa Majaribio Yake) Urazini wa Ayubu Asili Halisi ya Ayubu: Mkweli, Aliyetakaswa, na Asiye na Uongo Utenganisho wa Ayubu kati ya Upendo na Chuki Ukarimu na Uaminifu wa Ayubu Uhusiano Kati ya Mungu kumpa Shetani Ayubu na Malengo ya Kazi ya Mungu Kubali Mitihani ya Mungu, Shinda Majaribio ya Shetani, na Mruhusu Mungu Kupata Nafsi Yako Nzima Onyo na Nuru Iliyotolewa kwa Vizazi vya Baadaye Na Ushuhuda wa Ayubu
Mwenyezi Mungu alisema, Maudhui ya ushirika wetu wa mwisho kuhusu kazi ya Mungu yaliweza kuangazia mambo yaliyofanyika kitambo kwenye Biblia. Maudhui hayo yote yalikuwa hadithi kuhusu binadamu na Mungu, na yalimfanyikia binadamu na wakati huohuo yakahusisha kushiriki na maonyesho ya Mungu, hivyo basi hadithi hizi zinashikilia thamani na umuhimu mkubwa katika kujua Mungu. Baada tu ya kuumba ubinadamu, Mungu Alianza kujihusisha na binadamu na kuzungumza na binadamu, na tabia yake ikaanza kuonyeshwa kwa binadamu. Kwa maneno mengine, tangu Mungu alipojihusisha kwanza na mwanadamu, Alianza kuujuza umma kuhusu binadamu, bila kusita, kiini Chake halisi na kile Anacho na alicho. Licha ya kama watu wa awali au watu wa leo wanaweza kuona au kuelewa kiini hicho, kwa ufupi Mungu anamzungumzia mwanadamu na kufanya kazi miongoni mwa binadamu, Akifichua tabia Yake na Akionyesha kiini Chake—jambo ambalo ni ukweli, na lisilopingika na mtu yeyote. Hii inamaanisha pia kwamba tabia ya Mungu, kiini cha Mungu, na kile Anacho na alicho vyote vinatolewa daima na kufichuliwa huku naye Akifanya kazi na kujihusisha na binadamu. Hajawahi kusetiri au kumfichia binadamu chochote, lakini badala yake anatangaza kwa umma na kuachilia tabia Yake binafsi bila ya kuficha chochote. Hivyo basi, Mungu anatumai kwamba binadamu anaweza kumjua Yeye na kuielewa tabia Yake na kiini chake. Hapendi binadamu kuchukulia tabia Yake na kiini Chake kuwa mafumbo ya milele, wala Hataki mwanadamu kumchukulia Mungu kama fumbo lisiloweza kutatuliwa. Mpaka tu pale ambapo mwanadamu atakapomjua Mungu ndipo binadamu atakapojua njia ya kufuata na kuweza kuukubali mwongozo wa Mungu, na mwanadamu tu kama huyu ndiye anayeweza kuishi kwa kweli katika utawala wa Mungu, na kuishi katika mwangaza, na kuishi katikati ya baraka za Mungu.
Maneno na tabia iliyowasilishwa mbele na kufichuliwa na Mungu inawakilisha mapenzi Yake, na pia inawakilisha kiini Chake halisi. Wakati Mungu anapojihusisha na binadamu, haijalishi ni nini Anachosema au kufanya, au tabia gani Anayofichua, na haijalishi ni nini binadamu anaona kuhusu kiini cha Mungu na kile Anacho na alicho, vyote vinawasilisha mapenzi ya Mungu kwa binadamu. Licha ya kiwango ambacho binadamu anaweza kutambua, kufahamu, au kuelewa, vyote hivi vinawakilisha mapenzi ya Mungu—mapenzi ya Mungu kwa binadamu. Hii ni zaidi ya shaka! Mapenzi ya Mungu kwa binadamu ni vile Anavyohitaji watu kuwa, kile Anachohitaji wao kufanya, namna Anavyohitaji wao kuishi, na vile Anavyowahitaji kuweza kukamilisha kutimia kwa mapenzi ya Mungu. Je, mambo haya hayawezi kutenganishwa na kiini cha Mungu? Kwa maneno mengine, Mungu huwasilisha mbele tabia Yake na vyote Alivyo navyo na kile ambacho Mungu ni wakati huohuo Akimtolea madai binadamu. Hakuna uongo, hakuna kusingizia, hakuna ufichaji, na wala hakuna kupiga chuku. Ilhali kwa nini binadamu hawezi kujua na kwa nini hajawahi kuweza kutambua waziwazi tabia ya Mungu? Na kwa nini hajawahi kutambua mapenzi ya Mungu? Kile ambacho kimefichuliwa na kuwasilishwa mbele na Mungu ndicho kile Mungu anacho Mwenyewe na maana yake, na kinaonyesha kila kipengele cha tabia Yake ya kweli—hivyo kwa nini binadamu hawezi kuona? Kwa nini binadamu hana uwezo wa kuwa na maarifa ya kina? Kunayo sababu muhimu ya haya. Na sababu yenyewe ni ipi? Tangu wakati wa uumbaji, binadamu hajawahi kumchukulia Mungu kama Mungu. Kwenye nyakati zile za mwanzo kabisa, haikujalisha ni nini Mungu alifanya kuhusiana na binadamu, yule binadamu ambaye ndiye tu alikuwa ameumbwa, binadamu alimchukulia yeye kuwa mwandani wake tu na wala si zaidi ya hapo, kama mtu wa kutegemewa, na hakuwa na maarifa yoyote wala uelewa wa Mungu. Hivi ni kusema, hakujua kwamba kile kilichowasilishwa mbele na Kiumbe huyu—Kiumbe huyu ambaye yeye alitegemea na kumwona kuwa mwandani wake—alikuwa kiini cha Mungu, na wala hakujua kwamba Kiumbe huyu ndiye anayetawala viumbe wote. Nikisema kwa urahisi, watu wa wakati huo hawakuwa na maarifa hata kidogo kumhusu Mungu. Hawakujua kwamba mbingu na nchi na mambo yote yalikuwa yameumbwa na Yeye na wala hawakujua ni wapi Alipotokea, na, zaidi hawakujua Yeye Alikuwa nani. Bila shaka, wakati huo Mungu hakumhitaji binadamu kumjua Yeye au kumfahamu Yeye au kuelewa kila kitu Alichofanya, au kufahamishwa kuhusu mapenzi Yake, kwani hizi zilikuwa nyakati za mapema zaidi baada ya uumbwaji wa mwanadamu. Wakati Mungu alipoanza matayarisho ya kazi ya Enzi ya Sheria, Mungu alifanya mambo fulani kwa binadamu na pia Akaanza kutolea binadamu madai fulani, Akimwambia namna ya kutolea Mungu sadaka na namna ya kumwabudu. Ni wakati huo ndipo binadamu alipopata mawazo machache mepesi kuhusu Mungu, ni hapo tu ndipo alipojua tofauti kati ya binadamu na Mungu na kwamba Mungu Ndiye aliyewaumba wanadamu. Wakati binadamu alipojua kwamba Mungu alikuwa Mungu na binadamu alikuwa binadamu kukawa umbali fulani kati ya Yeye na Mungu, bado Mungu hakuhitaji kwamba binadamu awe na maarifa makuu au uelewa wa kina kumhusu Yeye. Hivyo basi, Mungu anayatoa mahitaji tofauti kwa binadamu kutokana na awamu na hali za kazi Yake. Mnaona nini katika haya? Ni kipengele kipi cha tabia ya Mungu unayoitambua? Je, Mungu ni wa kweli? Yale mahitaji ambayo Mungu anampa binadamu yanastahili? Kwenye nyakati za mapema kabisa kufuatia uumbaji wa wanadamu na Mungu, wakati ambao Mungu alikuwa bado hajatekeleza kazi ya ushindi na utimilifu wa binadamu, na Alikuwa hata bado hajaongea yale maneno mengi sana kwake, Alihitaji kidogo sana kutoka kwa binadamu. Licha ya kile ambacho binadamu alifanya na namna alivyotenda—hata kama alifanya mambo fulani yaliyomkosea Mungu—Mungu alimsamehe hayo yote, na akayapuuza. Kwa sababu Mungu Alijua kile Alichokuwa Amempa binadamu, na Alijua kile kilichokuwa ndani ya binadamu, basi Alijua kiwango cha mahitaji ambayo anafaa kudai kutoka kwa binadamu. Ingawaje kiwango cha mahitaji Yake kilikuwa cha chini sana wakati huo, hii haimaanishi kwamba tabia Yake haikuwa kuu, au kwamba hekima na uweza Wake yalikuwa si yoyote ila maneno matupu. Kwa binadamu, kunayo njia moja tu ya kujua tabia ya Mungu na Mungu Mwenyewe: kwa kufuata hatua za kazi ya usimamizi ya Mungu na wokovu wa mwanadamu, na kuyakubali maneno ambayo Mungu anaongea akiyaelekeza kwa mwanadamu. Kujua kile Mungu anacho na alicho, na kujua tabia ya Mungu, bado binadamu angemuuliza Mungu kumwonyesha ubinafsi Wake halisi? Binadamu hatafanya hivyo, na hathubutu kufanya hivyo, kwa kuweza kuifahamu tabia ya Mungu na kile Anacho na alicho, tayari binadamu atakuwa amemwona Mungu Mwenyewe wa kweli, na atakuwa tayari ameona ubinafsi Wake halisi. Haya ndiyo matokeo yasiyoepukika.
Kazi na mpango wa Mungu ulipokuwa ukiendelea mbele bila kusia, na baada ya Mungu kuanzisha agano la upinde wa mvua na binadamu kama ishara kwamba Hangewahi tena kuuangamiza ulimwengu kwa kutumia gharika, Mungu alikuwa na tamanio lililokuwa likiongezeka na kumsukuma kuwapata wale ambao wangeweza kuwa katika akili moja na Yeye. Hivyo, pia, Alikuwa na tamanio lenye udharura zaidi wa kupata wale waliokuwa na uwezo wa kutekeleza mapenzi Yake duniani, na, isitoshe, kupata kundi la watu ambao wangeweza kuwa huru dhidi ya nguvu za giza, na kutoweza kuwa watumwa wa Shetani, na kuweza kuwa na ushuhuda kwake Yeye duniani. Kupata kundi la watu kama hawa kulikuwa ni tamanio la Mungu kwa muda mrefu, Alichokuwa akisubiria tangu wakati wa uumbaji. Hivyo basi, licha ya matumizi ya gharika na Mungu ili kuuangamiza ulimwengu, au agano Lake na binadamu, mapenzi ya Mungu, hali yake ya akili, mpango, na matumaini yote yalibakia yaleyale. Kile Alichotaka kufanya, ambacho Alikuwa ametamani kwa muda mrefu kabla ya uumbaji, kilikuwa kupata wale walio miongoni mwa wanadamu ambao Alitamani kuwapata—Kupata watu wa kundi hili ambao walioweza kufahamu na kujua tabia Yake, na kuyaelewa mapenzi Yake, kundi ambalo lingeweza kumwabudu Yeye. Watu kwenye kundi kama hili wanaweza kweli kuwa na ushuhuda kwake, na wao ndio, yaweza kusemekana, wasiri Wake.

Ijumaa, 22 Februari 2019

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Jinsi ya Kuhudumu kwa Upatanifu na Mapenzi ya Mungu”

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Jinsi ya Kuhudumu kwa Upatanifu na Mapenzi ya Mungu”

Mwenyezi Mungu anasema, “Ikiwa ungependa kutumikia mapenzi ya Mungu, ni lazima kwanza ufahamu ni watu wa aina gani wanapendwa na Mungu, ni watu wa aina gani wanachukiwa na Mungu, ni watu wa aina gani wanafanywa kuwa kamili na Mungu, na ni watu wa aina gani wana sifa zinazostahili kumhudumia Mungu. Hiki ni kiasi kidogo zaidi unachopaswa kujiandaa nacho. Isitoshe, unapaswa kujua malengo ya kazi ya Mungu, na kazi ambayo Mungu Ataitenda hapa na wakati huu. Baada ya kufahamu haya, na kupitia kwa mwongozo wa maneno ya Mungu, kwanza utaingia, na kupokea agizo la Mungu kwanza. Unapopata uzoefu wa kweli kwa msingi wa maneno ya Mungu, na unapojua kweli kazi ya Mungu, utakuwa umehitimu kumhudumia Mungu. Na unapomhudumia ndipo Mungu atayapa nuru macho yako ya kiroho, na kukuruhusu kuwa na ufahamu mkubwa zaidi wa kazi Yake na kuiona dhahiri zaidi. Ukiingia katika ukweli huu, uzoefu wako utakuwa wa kina zaidi na wa kweli, na wale wote ambao wamepata uzoefu wa aina hiyo wataweza kutembea miongoni mwa makanisa mengi na kuwatolea ndugu zao, kila upande ukipokea kutoka kwa uwezo wa wengine ili upungufu wao wenyewe, na kupata maarifa mengi zaidi ndani ya roho zao. Ni baada tu ya kutimiza matokeo haya ndipo utakapoweza kutumikia mapenzi ya Mungu na kufanywa mkamilifu na Mungu wakati wa kufanya huduma yako.”

Alhamisi, 21 Februari 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sisitiza Uhalisi Zaidi

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sisitiza Uhalisi Zaidi

Kila mtu ana uwezekano wa kukamilishwa na Mungu, kwa hiyo kila mtu anapaswa kuelewa ni huduma gani kwa Mungu inayofaa zaidi makusudi ya Mungu. Watu wengi hawajui kumwamini Mungu humaanisha nini na hawajui kwa nini wanapaswa kumwamini Mungu. Yaani, watu wengi zaidi hawana ufahamu wa kazi ya Mungu au lengo la mpango wa usimamizi wa Mungu. Hadi leo, watu wengi zaidi bado wanadhani kumwamini Mungu kunahusu kwenda mbinguni na roho zao kuokolewa. Bado hawajui chochote kuhusu umuhimu mahususi wa kumwamini Mungu, na aidha hawana ufahamu wowote wa kazi muhimu kabisa ya Mungu katika mpango Wake wa usimamizi. Kwa aina zote za sababu zao binafsi, watu hawavutiwi kabisa na kazi ya Mungu na hawatafakari juu ya makusudi ya Mungu au mpango wa Mungu wa usimamizi. Kama mtu binafsi katika mkondo huu, kila mtu anapaswa kujua lengo la mpango mzima wa usimamizi wa Mungu ni nini, ukweli ambao Mungu tayari ametimiza, kwa nini Mungu amelichagua kundi hili la watu, malengo yake na umuhimu wake ni upi, na kile ambacho Mungu anataka kufanikisha katika kundi hili. Katika nchi ya joka kuu jekundu, Mungu ameweza kuinua kundi kama hilo la watu wasioonekana kwa urahisi, na Ameendelea kufanya kazi hadi sasa, Akijaribu na kuwakamilisha kwa kila namna, Akizungumza maneno yasiyohesabika, Akifanya kazi kubwa na kutuma vitu vingi vya kuhudumu. Kutokana na Mungu kukamilisha kazi kubwa kiasi hicho, inaweza kuonekana kwamba umuhimu wa kazi ya Mungu ni mkubwa sana. Bado hamuwezi kuielewa kabisa. Kwa hiyo, msiichukulie kazi ambayo Mungu amefanya kwenu kama suala dogo; hiki si kitu kidogo. Kile tu ambacho Mungu amewaonyesha leo kinawatosha kutafakari na kukielewa. Mkielewa tu kwa kweli na kwa kina ndipo mtaweza kupata uzoefu wa kina zaidi na kupiga hatua katika maisha yenu. Kile ambacho watu wanakielewa na kukifanya sasa ni kidogo sana na hakiwezi kukidhi kikamilifu makusudi ya Mungu. Huu ndio upungufu wa wanadamu na kushindwa kutimiza wajibu wao. Hii ndiyo maana matokeo ambayo yangepaswa kufikiwa bado hayajafikiwa. Roho Mtakatifu hana njia ya kufanya kazi kwa watu wengi kwa sababu wana ufahamu wa chini wa kazi ya Mungu na hawako tayari kuichukulia kazi ya nyumba ya Mungu kama kitu fulani cha thamani. Siku zote wanafanya vitu kwa namna isiyo ya dhati ili kuishi, au kuiga kile ambacho watu wengi zaidi wanafanya, au kuwaonyesha watu tu kwamba na wao “wanafanya kazi.” Leo, kila mtu katika mkondo huu atakumbuka iwapo kile ambacho umefanya ndicho kila ambacho ungeweza kufanya, na iwapo umetia bidii zako zote. Watu hawajatimiza wajibu wao kabisa. Si kwamba Roho Mtakatifu hafanyi kazi Yake bali ni kwamba watu hawafanyi kazi yao, wakifanya isiwezekane kwa Roho Mtakatifu kufanya kazi Yake. Mungu amemaliza kuonyesha maneno Yake, lakini hawajaenda kwa kasi sawa kabisa, na wamebaki nyuma kabisa, wasiweze kukaa karibu na kila hatua, wasiweze kuzifuata nyayo za Mwana Kondoo kwa karibu. Kile ambacho walipaswa kukitii hawajakitii; kile ambacho walipaswa kukitenda hawajakitia katika vitendo; kile ambacho walipaswa kukiomba hawajakiomba; kile ambacho walipaswa kukiacha hawajakiacha. Bado hawajafanya kitu chochote kati ya hivi. Kwa hiyo, mazungumzo haya ya kwenda kwenye dhifa ni maneno matupu na hayana maana kabisa. Yamo katika fikira za watu tu. Inaweza kusemwa kwamba hadi sasa watu hawajatimiza majukumu yao kabisa. Kila kitu kinategemea Mungu kufanya na kusema vitu Yeye Mwenyewe, wakati kazi ya watu kwa kweli imekuwa ndogo sana. Wote ni taka isiyokuwa na maana ambao hawajui jinsi ya kupatana na Mungu. Mungu amezungumza mamia ya maelfu ya maneno, lakini watu hawajayaweka katika vitendo kabisa, kuanzia kunyima mwili, kuacha dhana, kuwa watiifu katika mambo yote, kukuza ufahamu na kupata umaizi wakati uo huo, hadi kwa kuachilia hadhi za watu katika mioyo yao, kuondoa sanamu ambazo zinamiliki mioyo yao, kuasi dhidi ya makusudi binafsi ambayo si sahihi, kutotenda kwa msingi wa mihemko yao, kufanya mambo kwa haki bila ubaguzi, kufikiri zaidi juu ya maslahi ya Mungu na ushawishi wao kwa wengine wanapozungumza, kufanya mambo zaidi yanayonufaisha kazi ya Mungu, kukumbuka kunufaisha nyumba ya Mungu katika yote wanayofanya, kutoruhusu mihemko yao kuamua tabia yao, kuacha yale ambayo yanapendeza miili yao wenyewe, kuondoa dhana za zamani za ubinafsi, na kadhalika. Kwa kweli watu wanafahamu baadhi ya mambo katika maneno haya yote juu ya kile ambacho Mungu anahitaji kutoka kwao, lakini hawako tayari kuyaweka katika vitendo. Ni kwa namna gani nyingine ambayo Mungu anaweza kufanya kazi na kuwashawishi? Waasi machoni pa Mungu wanawezaje bado kuwa na ujasiri wa kuchukua maneno ya Mungu na kuyastahi? Wanawezaje kuwa na ujasiri wa kula chakula cha Mungu? Dhamiri ya mwanadamu ipo wapi? Hawajatimiza wajibu mdogo kabisa waliopaswa kutimiza, kwa hiyo kuzungumza juu ya kufanya yote wawezayo ni hoja isiyokuwa na maana. Je, wao si watu wa njozi tu? Hakuwezi kuwa na mazungumzo ya uhalisi bila matendo. Huo ni ukweli wa wazi!
Mnapaswa kuwa mkijifunza masomo zaidi ya uhalisi sasa. Hakuna haja ya hayo mazungumzo matupu, yenye kuvutia na ambayo watu wanayastahi. Linapokuja suala la kuzungumza kuhusu maarifa, ya kila mtu ni ya juu kuliko ya aliyetangulia, lakini bado hawana njia ya kutenda. Ni wangapi wameweka kitu chochote katika vitendo? Ni wangapi wamejifunza masomo halisi? Ni nani anayeweza kufanya ushirika kuhusu uhalisi? Kuweza kuzungumza juu ya maarifa ya maneno ya Mungu si sawa na kimo chako halisi. Hilo linaishia konyesha tu kuwa ulizaliwa ukiwa na akili na wewe ni mwenye karama. Bado haina maana ikiwa huwezi kuonyesha njia, na wewe ni taka tu isiyokuwa na maana! Je, hujifanyi tu ikiwa huwezi kusema chochote kuhusu njia halisi ya kufanya vitendo? Je hujifanyi ikiwa huwezi kutoa uzoefu wako mwenyewe halisi kwa wengine, na hivyo kuwapa masomo ambayo wanaweza kujifunza kwayo au njia ya kufanya vitendo? Je, wewe si bandia tu? Una thamani gani? Mtu kama huyo angeweza tu kushikilia sehemu ya kuwa “mvumbuzi wa nadharia ya ujamaa,” si “mchangiaji wa kuleta ujamaa.” Kutokuwa na uhalisi ni kutokuwa na ukweli. Kutokuwa na uhalisi ni kutokuwa na thamani. Kutokuwa na uhalisi ni kukosa uhai. Kutokuwa na uhalisi ni “kuwa na fikira za Umaksi na Ulenini,” bila thamani kama marejeo. Ninamsihi kila mtu kufunga mdomo kuhusu nadharia na kuzungumzia kitu ambacho ni halisi, kitu ambacho ni cha kweli na thabiti, kujifunza baadhi ya “sanaa za kisasa,” kuzungumza juu ya kitu ambacho ni halisi, kuchangia uhalisi kiasi, na kuwa na roho ya kujitoa. Uukabili uhalisi unapozungumza na usijiingize katika mazungumzo yasiyokuwa na uhalisi na yaliyotiwa chumvi ili kuwafurahisha watu au ili waweze kukufikiria kwa namna tofauti. Thamani yake ni nini? Kuna maana gani katika kuamsha shauku za watu kwa ajili yako? Kuwa “stadi” katika usemi wako, tenda haki katika matendo yako, kuwa mwenye busara katika kazi yako, kuwa mwenye uhalisi katika kuzungumza na watu, kumbuka kuinufaisha nyumba ya Mungu katika kila tendo, wacha dhamiri yako iongoze hisia zako, usilipize wema kwa chuki, au kutokuwa na shukrani kwa wema, na usiwe mnafiki, usije ukawa na “ushawishi mbaya.” Unapokula na kunywa maneno ya Mungu, yahusishe zaidi na uhalisi, na unapowasiliana, zungumza zaidi kuhusu mambo ya uhalisi na usijikweze—Mungu hukataa hilo. Kuwa mvumilivu na mstahimilivu zaidi, fanya mazoezi zaidi ya kukubali, kuwa mkarimu na wazi kwa watu, na jifunze kutoka kwa “roho ya waziri mkuu.”[a] Unapokuwa na mawazo ambayo si mazuri, fanya mazoezi zaidi ya kunyima mwili zaidi. Unapofanya kazi, zungumza zaidi kuhusu njia halisi na usiwe na majivuno sana vinginevyo itakuwa zaidi ya upeo wa watu. Starehe kidogo, mchango zaidi—onyesha roho yako ya kujitolea isiyo ya ubinafsi. Fikirieni zaidi makusudi ya Mungu, sikilizeni zaidi dhamiri zenu, na kumbukeni zaidi na msisahau jinsi ambavyo Mungu huwaonya kila siku kwa kuwajali. Soma “shajara ya mwaka ya zamani” mara kwa mara. Omba zaidi na shiriki mara kwa mara. Usiendelee kuwa mtu aliyekanganyika sana, bali onyesha busara zaidi na upate umaizi fulani. Mkono wa dhambi unaponyooka, urudishe nyuma na usiuache utandae zaidi. Haina maana! Mnachokipata kutoka kwa Mungu si chochote bali laana; kuweni waangalifu. Wacheni mioyo yenu iwe na huruma kwa wengine na siku zote msiwapige kwa silaha mkononi. Toeni zaidi na mzungumze zaidi kuhusu maisha, mkiwa na roho ya kuwasaidia wengine. Tendeni zaidi na kusema kidogo. Tieni zaidi katika vitendo na kidogo katika utafiti na uchambuzi. Gusweni zaidi na Roho Mtakatifu, na mpeni Mungu fursa zaidi ya kuwakamilisha. Ondoeni zaidi sifa za kibinadamu—bado kuna namna nyingi za kibinadamu za kufanya mambo. Matendo na tabia za juujuu bado zinachukiza kabisa. Ziondoeni zaidi. Hali zenu za akili bado zinachukiza sana. Zisahihisheni zaidi. Hadhi ambayo watu wanamiliki katika mioyo yenu bado ni kubwa sana. Mpatie Mungu hadhi zaidi na usiwe mtu usiyekuwa na akili. “Hekalu” kwanza ni la Mungu na halipaswi kumilikiwa na watu. Kwa ujumla, sisitiza zaidi haki na kidogo katika mihemko, na ni bora zaidi kuuondoa mwili; zungumza zaidi kuhusu uhalisi na kidogo kuhusu maarifa, na ni bora zaidi kuwa kimya; zungumza zaidi juu ya njia ya vitendo na kwa kiasi kidogo mazungumzo ya kiburi yasiyokuwa na maana, na ni bora zaidi kuanza kutenda kuanzia sasa.
Matakwa ya Mungu kwa watu si ya juu sana. Ikiwa watu wataweka jitihada kidogo wataweza kupata “alama ya kufaulu.” Kwa kweli, kufahamu, kujua, na kuukubali ukweli kunatatiza sana kuliko kuutenda ukweli; kuujua na kuukubali ukweli kunakuja baada ya kuutenda ukweli kwanza. Hii ndiyo hatua na njia ya kazi ya Roho Mtakatifu. Unawezaje kutoitii? Je, utaweza kuwa na kazi ya Roho Mtakatifu kwa kufanya mambo kwa namna yako? Je, Mungu hufanya kazi kwa kuzingatia matakwa yako, au baada ya wewe kulinganisha dhidi ya maneno ya Mungu? Haina maana ikiwa huwezi kuliona hili kwa uwazi. Kwa nini watu wengi zaidi wametumia jitihada nyingi kusoma maneno ya Mungu lakini wana na maarifa tu na hawawezi kusema kitu chochote kuhusu njia halisi baada ya hapo? Unadhani kwamba kuwa na maarifa ni sawa na kuwa na ukweli? Je, huo si mtazamo uliokanganywa? Unaweza kuzungumza maarifa mengi kama mchanga ulivyo ufuoni, lakini hakuna yaliyo na njia ya kweli. Katika hili, je huwadanganyi watu? Je, wewe si mtu wa maneno matupu bila vitendo? Kutenda kwa namna hii ni kwa madhara kwa watu! Kadiri nadharia inavyokuwa ya juu, ndivyo inavyokosa uhalisi zaidi, na ndivyo inavyokosa zaidi uwezo wa kuwapeleka watu katika uhalisi; kadiri nadharia inavyokuwa ya juu, ndivyo inavyokufanya umuasi na kumpinga Mungu. Usizichukulie nadharia za kiwango cha juu kama hazina ya thamani; zina madhara, na hazina kazi yoyote! Pengine baadhi ya watu wanaweza kuzungumza juu ya nadharia za juu sana—lakini nadharia hizo hazina kitu chochote cha uhalisi, maana watu hawajazipitia wao binafsi , na kwa hiyo hawana njia ya kutenda. Watu kama hao hawawezi kumwongoza mwanadamu katika njia nzuri, na watawapotosha tu watu. Je, hii haileti madhara kwa watu? Angalau kabisa, unapaswa kuweza kutatua shida za sasa na kuwaruhusu watu kupata kuingia; hii tu ndiyo inachukuliwa kama ibada, na baada ya hapo ndipo utakuwa na sifa za kufaa kumfanyia Mungu kazi. Siku zote usizungumze maneno ya kifahari, ya ajabu, na usiwalazimishe watu kukutii wewe pamoja na vitendo vyako visivyofaa. Kufanya hivyo hakutaleta matokeo, na kunaweza kuongeza tu mkanganyiko wa watu. Kuwaongoza watu kwa namna hii kutaleta taratibu nyingi, ambazo zitafanya watu wakuchukie. Huu ni udhaifu wa mwanadamu, na kwa kweli hauvumiliki. Kwa hiyo, zungumza zaidi juu ya matatizo yaliyopo sasa. Usichukulie uzoefu wa watu wengine kama mali binafsi na kuuleta kwa wengine ili wautambue. Wewe binafsi unapaswa kutafuta suluhisho. Hiki ndicho ambacho kila mtu anapaswa kuweka katika vitendo.
Ikiwa kile unachosema kinaweza kuwapatia watu njia ya kutembelea, basi hiyo ni sawa na wewe kuwa na uhalisi. Haijalishi kile unachosema, ni lazima uwalete watu katika vitendo na kuwapatia njia wanayoweza kuifuata. Si tu kuhusu kuifanya ili watu wapate maarifa, lakini muhimu zaidi, ni kuhusu kuwa na njia ya kutembea. Ili watu wamwamini Mungu, wanapaswa kutembea njia ambayo kwayo Mungu huwaongoza. Yaani, mchakato wa kumwamini Mungu ni mchakato wa kutembea kwenye njia ambayo Roho Mtakatifu anakuongoza kwayo. Vivyo hivyo, unapaswa kuwa na njia ambayo unaweza kuitembea kwa vyovyote vile, na unapaswa kutembea kwenye njia ya kukamilishwa na Mungu. Usilitumie zaidi ya kiasi, na usijihusishe nayo sana. Ikiwa tu unatembea kwenye njia ambayo Mungu hukuongoza kwayo bila kusababisha mwingiliano ndipo unaweza kupokea kazi ya Roho Mtakatifu na kuwa na njia ya kuingia. Hili tu ndilo linachukuliwa kama la kufaa makusudi ya Mungu na kutimiza wajibu wa mwanadamu. Kama mtu binafsi katika mkondo huu, kila mtu anapaswa kutimiza wajibu wake kikamilifu, fanya zaidi yale ambayo watu wanapaswa kuyafanya, na usitende kwa lengo la kudhuru. Watu wanaotekeleza kazi wanapaswa kuweka maneno yao wazi, watu wanaofuata wanapaswa kusisitiza zaidi kuhimili ugumu na kutii, na kila mtu anapaswa kutunza nafasi yake na kutotoka nje ya mstari. Linapaswa lieleweke wazi katika moyo wa kila mtu namna ambavyo wanapaswa kutenda na ni kazi gani wanapaswa kutimiza. Chukua njia ambayo kwayo Roho Mtakatifu huongoza; usipotoke au kukosea. Lazima muione kazi ya leo waziwazi. Kuingia katika mbinu ya kazi ya leo ndicho mnachopaswa kutenda. Ni kitu cha kwanza mnachopaswa kuingia. Msipoteze maneno yoyote zaidi kwenye mambo mengine. Kufanya kazi ya nyumba ya Mungu leo ni jukumu lenu, kuingia katika mbinu ya kazi ya leo ni wajibu wenu, na kutenda ukweli wa leo ni mzigo wenu.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Jumatano, 20 Februari 2019

Ni kwa Kupitia tu Majaribio ya Kuumiza Ndiyo Mnaweza Kujua Kupendeza kwa Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,

Ni kwa Kupitia tu Majaribio ya Kuumiza Ndiyo Mnaweza Kujua Kupendeza kwa Mungu

Mwenyezi Mungu  alisema, Unampenda Mungu kiasi gani hasa leo? Na unajua kiasi gani hasa kuhusu yote ambayo Mungu amefanya ndani yako? Haya ni mambo unayopaswa kujifunza. Mungu anapowasili duniani, yote ambayo Amefanya ndani ya mwanadamu na kumkubalia mwanadamu kuona ni ili mwanadamu atampenda na kumjua Yeye kweli. Kwamba mwanadamu anaweza kuteseka kwa ajili ya Mungu na ameweza kufikia umbali huu ni, kuhusiana na jambo moja, kwa sababu ya upendo wa Mungu, na kuhusiana na jambo lingine, ni kwa sababu ya wokovu wa Mungu; zaidi ya hayo, ni kwa sababu ya kazi ya hukumu na kuadibu ambayo Mungu ametekeleza ndani ya mwanadamu. Kama hamna hukumu, kuadibu, na majaribio ya Mungu, na kama Mungu hajawafanya mteseke, basi, kusema ukweli, ninyi hamumpendi Mungu kweli. Kadri kazi ya Mungu ilivyo kuu zaidi ndani ya mwanadamu, na kadri mateso ya mwanadamu yalivyo makuu zaidi, ndivyo inavyoweza kuonyesha zaidi hasa vile kazi ya Mungu ilivyo ya maana, na ndivyo moyo wa mwanadamu unavyoweza kumpenda Mungu kweli zaidi. Unajifunzaje jinsi ya kumpenda Mungu? Bila mateso makali na usafishaji, bila majaribio ya kuumiza—na kama, zaidi ya hayo, yote ambayo Mungu alimpa mwanadamu ingekuwa neema, upendo, na rehema—je, ungeweza kufikia upendo wa kweli kwa Mungu? Kwa upande mmoja, wakati wa majaribio ya Mungu mwanadamu huja kujua kasoro zake, na huona kwamba yeye ni mdogo, wa kudharauliwa, na duni, kwamba hana chochote, na si kitu; kwa upande mwingine, wakati wa majaribio Yake Mungu humuumbia mwanadamu mazingira tofauti yanayomfanya mwanadamu aweze zaidi kupitia kupendeza kwa Mungu. Ingawa maumivu ni makubwa, na wakati mwingine yasiyoshindika—na hata hufikia kiwango cha huzuni ya kuseta—baada ya kuyapitia, mwanadamu huona vile kazi ya Mungu ndani yake ni ya kupendeza, na ni juu ya msingi huu tu ndiyo ndani ya mwanadamu huzaliwa upendo wa kweli kwa Mungu. Leo mwanadamu huona kwamba na neema, upendo na rehema ya Mungu pekee, hana uwezo wa kujijua mwenyewe kweli, sembuse kuweza kujua kiini cha mwanadamu. Ni kupitia tu usafishaji na hukumu ya Mungu, ni wakati tu wa usafishaji kama huo ndiyo unaweza kujua kasoro zako, na kujua kwamba huna chochote. Hivyo, upendo wa mwanadamu kwa Mungu umejengwa juu ya msingi wa usafishaji na hukumu ya Mungu. Kama wewe hufurahia tu neema ya Mungu, na maisha ya familia yenye amani au baraka yakinifu, basi hujampata Mungu, na imani yako kwa Mungu haijafaulu. Mungu tayari ametekeleza hatua moja ya kazi ya neema katika mwili, na tayari amempa mwanadamu baraka yakinifu—lakini mwanadamu hawezi kufanywa mkamilifu na neema, upendo, na rehema pekee. Katika uzoefu wa mwanadamu yeye hukabiliwa na baadhi ya upendo wa Mungu, na huuona upendo na rehema ya Mungu, lakini baada ya kupitia kwa kipindi fulani cha wakati, yeye huona kwamba neema ya Mungu na upendo na rehema Yake hayawezi kumfanya mwanadamu awe mkamilifu, na hayana uwezo wa kufichua kile ambacho ni potovu ndani ya mwanadamu, wala hayawezi kumwondolea mwanadamu tabia yake potovu, au kufanya kuwa kamilifu upendo na imani yake. Kazi ya Mungu ya neema ilikuwa kazi ya kipindi kimoja, na mwanadamu hawezi kutegemea kufurahia neema ya Mungu ili kumjua Mungu.
Ni kupitia nini ndiyo ukamilishaji wa Mungu kwa mwanadamu hutimizwa? Kupitia tabia Yake yenye haki. Tabia ya Mungu hasa huwa na haki, ghadhabu, uadhama, hukumu, na laana, na ukamilishaji Wake wa mwanadamu hasa ni kupitia hukumu. Watu wengine hawaelewi, na huuliza ni kwa nini Mungu anaweza tu kumfanya mwanadamu kuwa mkamilifu kupitia hukumu na laana. Wao husema kwamba kama Mungu angemlaani mwanadamu, si mwanadamu angekufa? Kama Mungu angemhukumu mwanadamu, si mwanadamu angelaaniwa? Basi anawezaje hata hivyo kufanywa mkamilifu? Hayo ndiyo maneno ya watu wasioijua kazi ya Mungu. Kile ambacho Mungu hulaani ni uasi wa mwanadamu, na kile Anachohukumu ni dhambi za mwanadamu. Ingawa Yeye hunena kwa ukali, na bila kiwango cha hisi hata kidogo, Yeye hufichua yote yaliyo ndani ya mwanadamu, na kupitia maneno haya makali Yeye hufichua kile kilicho muhimu ndani ya mwanadamu, lakini kupitia hukumu kama hiyo, Yeye humpa mwanadamu ufahamu mkubwa wa kiini cha mwili, na hivyo mwanadamu hujitiisha chini ya utii mbele za Mungu. Mwili wa mwanadamu ni wa dhambi, na wa Shetani, ni wa kutotii, na chombo cha kuadibu kwa Mungu—na kwa hiyo, ili kumruhusu mwanadamu kujijua, maneno ya hukumu ya Mungu lazima yamfike na lazima kila aina ya usafishaji itumike; ni wakati huo tu ndiyo kazi ya Mungu inaweza kuwa ya kufaa.
Kutokana na maneno yaliyonenwa na Mungu inaweza kuonekana kwamba tayari Ameulaani mwili wa mwanadamu. Je, haya maneno, basi, ni maneno ya laana? Maneno yaliyonenwa na Mungu hufichua tabia halisi ya mwanadamu, na kupitia ufichuzi kama huo unahukumiwa, na unapoona kwamba huwezi kuyaridhisha mapenzi ya Mungu, ndani unahisi huzuni na majuto, unahisi kwamba unapaswa kumshukuru Mungu sana, na usiyetosha kwa ajili mapenzi ya Mungu. Kuna nyakati ambapo Roho wa Mungu hukufundisha nidhamu kutoka ndani, na nidhamu hii hutoka kwa hukumu ya Mungu; kuna nyakati ambapo Mungu hukushutumu na kuuficha uso Wake kutoka kwako, wakati ambapo hakusikilizi, na Hafanyi kazi ndani yako, akikuadibu bila sauti ili kukusafisha. Kazi ya Mungu ndani ya mwanadamu ni hasa ili kuweka wazi tabia Yake yenye haki. Ni ushuhuda gani ambao mwanadamu hatimaye huwa nao kwa Mungu? Yeye hushuhudia kwamba Mungu ni Mungu mwenye haki, kwamba tabia yake ni haki, ghadhabu, kuadibu, na hukumu; mwanadamu hushuhudia kwa tabia yenye haki ya Mungu. Mungu hutumia hukumu Yake kumfanya mwanadamu awe mkamilifu, Amekuwa Akimpenda mwanadamu, na kumwokoa mwanadamu—lakini ni kiasi gani kiko ndani ya upendo Wake? Kuna hukumu, uadhama, ghadhabu, na laana. Ingawa Mungu alimlaani mwanadamu katika wakati uliopita, Hakumtupa mwanadamu kabisa ndani ya shimo la kuzimu, lakini Alitumia njia hiyo kuisafisha imani ya mwanadamu; Hakumuua mwanadamu, lakini alitenda ili kumfanya mwanadamu awe mkamilifu. Kiini cha mwili ni kile ambacho ni cha Shetani—Mungu alikisema sahihi kabisa—lakini ukweli unaotekelezwa na Mungu haukamilishwi kufuatana na maneno Yake. Yeye hukulaani ili uweze kumpenda, na ili uweze kujua kiini cha mwili; Yeye hukuadibu ili uweze kuamshwa, kukuruhusu wewe ujue kasoro zilizo ndani yako, na kujua kutostahili kabisa kwa mwanadamu. Hivyo, laana za Mungu, hukumu Yake, na uadhama na ghadhabu Yake—yote ni kwa ajili ya kumfanya mwanadamu awe mkamilifu. Yote ambayo Mungu anafanya leo, na tabia yenye haki ambayo Yeye huifanya kuwa wazi ndani yenu—yote ni kwa ajili ya kumfanya mwanadamu awe mkamilifu, na huo ndio upendo wa Mungu.
Katika dhana za mwanadamu za kitamaduni, upendo wa Mungu ni neema Yake, fadhili, na huruma kwa udhaifu wa mwanadamu. Ingawa mambo haya pia ni upendo wa Mungu, yanaegemea upande mmoja sana, na si njia za msingi ambazo kwazo Mungu humfanya mwanadamu kuwa mkamilifu. Wakati ambapo watu wengine wameanza tu kumwamini Mungu, ni kwa sababu ya ugonjwa. Ugonjwa huu ni neema ya Mungu kwako; bila huo, hungemwamini Mungu, na kama hungemwamini Mungu basi hungefika umbali huu—na hivyo hata neema hii ni upendo wa Mungu. Katika wakati wa kumwamini Yesu, watu walifanya mengi ambayo hayakupendwa na Mungu kwa sababu hawakuelewa ukweli, lakini Mungu ana upendo na rehema, na Amemleta mwanadamu umbali huu, na ingawa mwanadamu haelewi chochote, bado Mungu humruhusu mwanadamu amfuate Yeye, na, zaidi ya hayo, Amemwongoza mwanadamu mpaka leo. Je, huu si upendo wa Mungu? Kile ambacho kinadhihirishwa katika tabia ya Mungu ni upendo wa Mungu—hili ni sahihi bila shaka. Wakati ambapo ujenzi wa kanisa ulifikia kilele chake, Mungu alifanya hatua ya kazi ya watendaji-huduma na akamtupa mwanadamu katika shimo la kuzimu. Maneno ya wakati wa watendaji-huduma yote yalikuwa laana: laana za mwili wako, laana za tabia yako potovu ya kishetani, na laana za mambo yanayokuhusu ambayo hayatimizi mapenzi ya Mungu. Kazi iliyofanywa na Mungu katika hatua hiyo ilidhihirishwa kama uadhama, karibukaribu sana baadaye Mungu alitekeleza hatua ya kazi ya kuadibu, na kisha kukaja majaribio ya kifo. Katika kazi kama hiyo, mwanadamu aliona ghadhabu, uadhama, hukumu, na kuadibu kwa Mungu, lakini aliona pia neema ya Mungu, na upendo na rehema Yake; yote aliyofanya Mungu, na yote yaliyodhihirishwa kama tabia Yake, ulikuwa upendo wa mwanadamu, na yote ambayo Mungu alifanya yaliweza kutimiza mahitaji ya mwanadamu. Aliyafanya ili kumfanya mwanadamu awe mkamilifu, na kutoa kwa kadri ya kimo cha mwanadamu. Kama Mungu hangefanya hili, mwanadamu hangekuwa na uwezo wa kuja mbele za Mungu, na hangekuwa na njia ya kuujua uso wa kweli wa Mungu. Tangu wakati ambapo mwanadamu alianza kwa mara ya kwanza kumwamini Mungu mpaka leo, Mungu amemkimu mwanadamu polepole kwa mujibu wa kimo chake, ili kwamba, ndani, mwanadamu amekuja kumjua Yeye polepole. Ni kwa kuweza kufika leo tu ndiyo mwanadamu ametambua hasa vile hukumu ya Mungu ni ya ajabu. Hatua ya kazi ya watendaji-huduma ilikuwa tokeo la kwanza la kazi ya laana tangu wakati wa uumbaji mpaka leo. Mwanadamu alilaaniwa kwenda katika shimo la kuzimu. Kama Mungu hangefanya hivyo, leo mwanadamu hangekuwa na ufahamu wa kweli wa Mungu; ni kupitia tu laana ya Mungu ndiyo mwanadamu hukutana kwa urasimu na tabia ya Mungu. Matukio hayo yalimwonyesha mwanadamu kwamba uaminifu wake haukukubalika, kwamba kimo chake kilikuwa kidogo sana, kwamba hakuwa na uwezo wa kuridhisha mapenzi ya Mungu, na kwamba madai yake ya kumridhisha Mungu wakati wote yalikuwa maneno matupu tu. Ingawa katika hatua ya kazi ya watendaji-huduma Mungu alimlaani mwanadamu, ikitazamwa kutoka leo hatua hiyo ya kazi ilikuwa ya ajabu: Ilileta mgeuzo mkubwa kwa mwanadamu, na kusababisha mabadiliko makuu katika tabia yake ya maisha. Kabla ya wakati wa watendaji-huduma, mwanadamu hakuelewa chochote kuhusu ukimbizaji wa maisha, ni nini maana ya kumwamini Mungu, au hekima ya kazi ya Mungu, wala hakufahamu kwamba kazi ya Mungu inaweza kumjaribu mwanadamu. Tangu wakati wa watendaji-huduma mpaka leo, mwanadamu huona vile kazi ya Mungu ni ya ajabu, haiwezi kueleweka kwa mwanadamu, na akitumia akili yake hawezi kufikiria jinsi Mungu hufanya kazi, na pia huona vile kimo chake ni kidogo na kwamba kiasi kikubwa chake ni cha kutotii. Mungu alipomlaani mwanadamu, ilikuwa ili Atimize athari, na Hakumuua mwanadamu. Ingawa Alimlaani mwanadamu, Alifanya hivyo kupitia maneno, na laana Zake hazikumwangukia mwanadamu kwa kweli, kwani kile ambacho Mungu alilaani kilikuwa kutotii kwa mwanadamu, na kwa hiyo maneno ya laana Zake pia yalikuwa kwa ajili ya kumfanya mwanadamu awe mkamilifu. Kama Mungu atamhukumu mwanadamu au kumlaani, yote mawili humfanya mwanadamu kuwa mkamilifu: Yote mawili ni kwa ajili ya kukifanya kamili kile ambacho ni kichafu ndani ya mwanadamu. Kupitia njia hii mwanadamu alisafishwa, na kile ambacho kilikuwa kinakosekana ndani ya mwanadamu kilifanywa kamilifu kupitia maneno na kazi Yake. Kila hatua ya kazi ya Mungu—kama ni maneno makali, au hukumu, au kuadibu—humfanya mwanadamu kuwa mkamilifu, na inafaa kwa uhalisi. Kotekote katika enzi zote Mungu hajawahi kufanya kazi kama hii; leo, Yeye hufanya kazi ndani yenu ili muweze kufahamu hekima Yake. Ingawa mmepitia maumivu fulani ndani yenu, mioyo yenu inajisikia thabiti, na kwa amani; ni baraka yenu kuweza kufurahia hatua hii ya kazi ya Mungu. Haijalishi kile mnachoweza kupata katika siku za baadaye, yote mnayoona kuhusu kazi ya Mungu ndani yenu leo ni upendo. Kama mwanadamu hapitii hukumu na kuadibu kwa Mungu, matendo yake na ari daima yatakuwa nje, na tabia yake daima itaendelea kutobadilika. Je, hii inahesabika kama kupatwa na Mungu? Leo, ingawa bado kuna mengi ndani ya mwanadamu ambayo ni yenye kiburi na yenye majivuno, tabia ya mwanadamu ni imara zaidi kuliko awali. Mungu kukushughulikia wewe ni ili kukuokoa, na ingawa unaweza kuhisi maumivu kidogo wakati huo, siku itafika ambapo kutatokea mabadiliko katika tabia yako. Wakati huo, utakumbuka ya nyuma na kuona vile kazi ya Mungu ni ya hekima, na huo utakuwa wakati ambao utaweza kufahamu kwa kweli mapenzi ya Mungu. Leo, kuna watu wengine ambao husema kwamba wanafahamu mapenzi ya Mungu—lakini hiyo si ya kweli kamwe, wao wanazungumza upuuzi, kwa sababu wakati huu bado hawajafahamu kama mapenzi ya Mungu ni kumwokoa mwanadamu au kumlaani mwanadamu. Labda huwezi kuliona kwa dhahiri sasa, lakini siku itafika ambapo utaona kwamba siku ya kutukuzwa kwa Mungu imefika, na uone jinsi ni ya maana kumpenda Mungu, ili utakuja kuyajua maisha ya binadamu, na mwili wako utaishi katika ulimwengu wa kumpenda Mungu, kwamba roho yako itawekwa huru, maisha yako yatajaa furaha, na kwamba daima utakuwa karibu na Mungu, na utamtegemea Mungu daima. Wakati huo, utajua kweli jinsi kazi ya Mungu ni ya thamani leo.
Leo, watu wengi sana hawana ufahamu huo. Wao huamini kwamba mateso hayana thamani, wao hukanwa na ulimwengu, maisha yao ya nyumbani yamesumbuliwa, wao si wapendwa wa Mungu, na matazamio yao ni matupu. Kuteseka kwa watu wengine hufikia kiwango fulani, na fikira zao hugeukia kifo. Huu si upendo wa kweli kwa Mungu; watu kama hao ni waoga, hawana ustahamilivu, wao ni wadhaifu na wasio na nguvu! Mungu ana hamu ya mwanadamu kumpenda Yeye, lakini kadri mwanadamu anavyompenda Yeye, ndivyo kuteseka kwa mwanadamu huwa kwingi zaidi, na kadri mwanadamu anavyompenda Yeye, ndivyo majaribio ya mwanadamu huwa makubwa zaidi. Ikiwa unampenda Yeye, basi kila aina ya mateso yatakufika—na ikiwa humpendi, basi labda kila kitu kitaendelea kwa urahisi kwako, na kila kitu kinachokuzunguka kitakuwa kitulivu kwako. Unapompenda Mungu, utahisi kwamba mengi kandokando yako hayawezi kushindikana, na kwa sababu kimo chako ni kidogo sana utasafishwa; aidha, huwezi kumridhisha Mungu, na daima utahisi kwamba mapenzi ya Mungu ni ya juu sana, kwamba hayawezi kufikiwa na mwanadamu. Kwa sababu ya haya yote utasafishwa—kwa sababu kuna udhaifu mwingi ndani yako, na mengi yasiyoweza kuridhisha mapenzi ya Mungu, utasafishwa ndani. Lakini lazima muone kwa dhahiri kwamba utakaso hutimizwa tu kupitia usafishaji. Hivyo, katika siku hizi za mwisho lazima muwe na ushuhuda kwa Mungu. Haijalishi mateso yenu ni makubwa vipi, mnapaswa kuendelea hadi mwisho kabisa, na hata wakati wa pumzi yenu ya mwisho, bado lazima muwe waaminifu kwa Mungu, na kudhibitiwa na Mungu; huku pekee ndiko kumpenda Mungu kweli, na huu pekee ndio ushuhuda thabiti na mkubwa sana. Unapojaribiwa, unapaswa kusema: “Moyo wangu ni wa Mungu, na Mungu tayari amenipata. Siwezi kukuridhisha wewe—lazima nitoe kila kitu changu ili kumridhisha Mungu.” Kadri unavyomridhisha Mungu, ndivyo Mungu hukubariki zaidi, na ndivyo nguvu za upendo wako kwa Mungu huwa kuu zaidi; kwa hiyo, vilevile, utakuwa na imani na azimio, na utahisi kwamba hakuna kilicho na thamani zaidi au cha maana kuliko kutumia maisha ukimpenda Mungu. Inaweza kusemwa kwamba mwanadamu anatakiwa tu kumpenda Mungu ili kuishi bila huzuni. Ingawa kuna nyakati ambazo mwili wako ni dhaifu na unazongwa na matatizo mengi ya kweli, katika nyakati hizi utamtegemea Mungu kweli, na ndani ya roho yako utafarijiwa, na utahisi hakika, na kwamba una kitu cha kutegemea. Kwa njia hii, utaweza kushinda hali nyingi, na kwa hiyo hutalalamika kuhusu Mungu kwa sababu ya uchungu unaopitia; utataka kuimba, kucheza, na kuomba, kukusanyika na kuwasiliana kwa karibu, kumfikiria Mungu, na utahisi kwamba watu wote, mambo, na vitu vilivyo kandokando yako ambavyo vimepangwa na Mungu vinafaa. Kama humpendi Mungu, yote ambayo unategemea yatakuwa yenye kero kwako, hakuna kitakachokuwa cha kufurahisha machoni mwako; ndani ya roho yako hutakuwa huru bali wa kudhulumiwa, moyo wako daima utalalamika kuhusu Mungu, na daima utahisi kwamba unapitia mateso mengi sana, na kwamba ni udhalimu sana. Kama hufuatilii kwa ajili ya furaha, bali ili umridhishe Mungu na kutoshtakiwa na Shetani, basi ukimbizaji kama huo utakupa nguvu nyingi za kumpenda Mungu. Mwanadamu anaweza kutekeleza yote yanayonenwa na Mungu, na yote ayafanyayo yanaweza kumridhisha Mungu—hii ndiyo maana ya kuwa na hakika. Kufuatilia ridhaa ya Mungu ni kuutumia upendo wa Mungu kutia maneno Yake katika vitendo; pasipo kutia maanani wakati—hata kama wengine hawana nguvu—ndani yako bado kuna moyo unaompenda Mungu, ambao unamtamani Mungu sana, na humkosa Mungu. Hiki ni kimo halisi. Jinsi ambavyo kimo chako ni kikubwa hasa hutegemea jinsi upendo wako kwa Mungu ulivyo mkuu, kama unaweza kusimama imara wakati unajaribiwa, kama wewe ni mdhaifu hali fulani inapokujia, na kama unaweza kusimama imara wakati ambapo ndugu zako wanakukataa; majilio ya ukweli yataonyesha hasa upendo wako kwa Mungu ukoje. Inaweza kuonekana kutoka kwa kazi nyingi ya Mungu kwamba Mungu kweli anampenda mwanadamu, ni hasa tu macho ya roho ya mwanadamu bado hayajafunguliwa kabisa, na hawezi kufahamu kazi nyingi ya Mungu, na mapenzi ya Mungu, na vitu vingi ambavyo ni vya kupendeza kuhusu Mungu; mwanadamu ana upendo kidogo sana wa kweli kwa Mungu. Umemwamini Mungu kotokote katika wakati huu wote, na leo Mungu amezuia njia zote za kutoroka. Kusema kwa kweli, huna chaguo lingine ila kuifuata njia sahihi, njia sahihi ambayo umeelekezwa kwayo kwa hukumu kali na wokovu mkubwa kabisa wa Mungu. Ni baada tu ya kupitia taabu na usafishaji ndiyo mwanadamu hujua kwamba Mungu ni wa kupendeza. Baada ya kupitia mpaka leo, inaweza kusemwa kwamba mwanadamu amekuja kujua sehemu ya kupendeza kwa Mungu—lakini hili bado halitoshi, kwa sababu mwanadamu amepungukiwa sana. Lazima apate uzoefu zaidi wa kazi ya Mungu ya ajabu, na zaidi ya usafishaji wote wa mateso uliowekwa na Mungu. Ni wakati huo tu ndiyo tabia ya maisha ya mwanadamu itaweza kubadilishwa.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Jumanne, 19 Februari 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Utendaji (2)

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Utendaji (2)

Katika nyakati zilizopita, watu walijifundisha wenyewe kuwa na Mungu na kuishi katikati ya roho kila wakati, ambao, ukilinganishwa na utendaji wa leo, ni mafundisho rahisi ya kiroho tu. Utendaji kama huu huja kabla ya kuingia kwa watu katika njia sahihi ya maisha, na ni mbinu ya juujuu zaidi na rahisi zaidi kati ya mbinu zote za utendaji. Ni utendaji wa hatua za mwanzoni kabisa za imani ya watu kwa Mungu. Ikiwa watu wataishi kila mara kwa utendaji huu, watakuwa na hisia nyingi sana, na hawataweza kuingia katika uzoefu ambao ni wa kina na wa kweli. Wataweza tu kuzifundisha roho zao, kuifanya mioyo yao iweze kusonga kwa kawaida karibu na Mungu, na kupata kila mara furaha nyingi mno katika kuwa na Mungu. Watakuwa wamejiwekea mipaka kwa ulimwengu mdogo wa kuwa na mshikamano na Mungu, wasiweze kuelewa kile kilicho katika vina vya ndani kabisa. Watu ambao huishi katika mipaka hii pekee hawana uwezo wa kupiga hatua yoyote kubwa. Wakati wowote, wanaweza kulia, “Aa! Bwana Yesu. Amina!” Wanapokula, wao hulia, “Ee Mungu! Nala na Wewe unakula....” Na ni hivi karibu kila siku. Huu ni utendaji wa nyakati zilizopita, ni utendaji wa kuishi ndani ya roho kila wakati. Huo sio utovu wa adabu? Leo, kama ni wakati wa kutafakari juu ya maneno ya Mungu, unapaswa kuyatafakari, kama ni wakati wa kutia ukweli katika vitendo unapaswa kuuweka katika vitendo, na wakati ni muda wa kutekeleza wajibu wako, unapaswa kuutekeleza. Kufanya utendaji hivyo ni huru kabisa, kunakufungua wewe. Sio kama vile wazee wa dini huomba na kusema neema. Bila shaka, hapo awali, hivi ndivyo watu walioamini katika Mungu walitakiwa kutenda—lakini kutenda kwa njia hii kila mara ni kuliko nyuma kimaendeleo kabisa. Utendaji wa wakati uliopita ni msingi wa utendaji wa leo. Ikiwa kungekuwa na njia kwa utendaji wa nyakati zilizopita, utendaji wa leo utakuwa rahisi zaidi. Kwa hiyo, leo, tunapozungumza juu ya “kumleta Mungu katika maisha halisi,” ni hali gani ya utendaji inatajwa? “Maisha halisi” hasa yanahitaji watu wawe na ubinadamu wa kawaida; kile ambacho watu wanapaswa kuwa nacho ni kile ambacho Mungu anataka kutoka kwao leo. Kuyaleta maneno ya Mungu katika maisha halisi ndiyo maana halisi ya “kumleta Mungu katika maisha halisi.” Leo, watu wanapaswa hasa kujiandaa wenyewe na yafuatayo: Kuhusu suala moja, lazima waendeleze uhodari wao, wafunzwe, waongeze msamiati wao, na kuendeleza ustadi wao wa kusoma; na katika lingine, lazima waishi maisha ya watu wa kawaida. Umerudi tu mbele ya Mungu kutoka ulimwenguni, na lazima kwanza uifunze roho yako, kuufunza moyo wako kuwa na amani mbele ya Mungu. Hili ndilo la msingi kabisa, na pia ni hatua ya kwanza katika kutimiza mabadiliko. Watu wengine ni wepesi kubadilika katika utendaji wao; wao hutafakari ukweli huku wakifua nguo zao, wakielewa ukweli wanaopaswa kuelewa na kanuni wanazopaswa kuweka katika vitendo kwa uhalisi. Katika suala moja, lazima uwe na maisha ya kawaida ya ubinadamu, na katika lingine lazima kuwe na kuingia katika ukweli. Huu ni utendaji bora zaidi kwa maisha halisi.
Zamani, watu walipitia magumu mengi sana, lakini mengine yalikuwa yasiohitajika kwa kweli, kwani mengine yalikuwa mambo ambayo hayakuhitajika kutendwa na mwanadamu. Wanapomleta Mungu katika maisha yao halisi, Mungu kimsingi anahitaji kwamba watu wamwabudu Mungu, wafuatilie ufahamu wa Mungu, na kutekeleza wajibu wa kiumbe wa Mungu katikati ya ubinadamu wa kawaida. Hawahitajiki kumwomba Mungu mara tu wanapoanza kufagia sakafu, wakihisi ni wadeni Wake wasipofanya hivyo. Utendaji wa leo sio hivyo; ni uliolegezwa na rahisi! Watu hawaambiwi watii mafundisho ya dini. Kila mmoja anapaswa kutenda kulingana na kimo chake mwenyewe: Ikiwa mume wako haamini, mchukulie kama mtu asiyemwamini Mungu, na ikiwa yeye huamini mchukulie kama muumini. Usisisitize kuhusu upendo na uvumilivu, bali kuhusu hekima. Watu wengine huenda kununua mboga, na wanapokuwa wakitembea wao hunong’ona: Ee Mungu! Ni mboga gani ambazo unanikubalia ninunue leo? Naomba usaidizi Wako. Je, nichague ninaponunua? Kisha wao hufikiria: Sitachagua; Mungu ananiambia kwamba nimtukuze Yeye, kwamba nilitukuze jina Lake katika mambo yote, na kwamba watu wote wawe na ushuhuda, kwa hiyo muuzaji akinipa kitu fulani cha kitambo na kilichokauka, bado nitampa Mungu shukrani—nitavumilia! Sisi tuaminio katika Mungu hatuchagui ni mboga gani za kununua. Unafikiri kwamba kufanya hivi ni kuwa na ushuhuda kwa Mungu, na baada ya kutumia yuan[a] moja kununua mboga ya kitambo iliyo na kuvu, bado unaomba na kusema: Ee Mungu! Bado nitaila mboga hii iliyooza—maadamu Unikubali, nitaila. Je, utendaji kama huu sio wa kipumbavu? Je, huko sio kufuata mafundisho ya dini? Hapo awali, watu walizifundisha roho zao na waliishi ndani ya roho kila wakati, na hili lilihusiana na kazi iliyofanywa katika Enzi ya Neema. Uchaji Mungu, unyenyekevu, upendo, uvumilivu, kutoa shukrani kwa mambo yote—haya ndiyo yaliyotakiwa kutoka kwa kila muumini katika Enzi ya Neema. Wakati huo, watu walimwomba Mungu katika mambo yote; wangeomba waliponunua nguo, na walipofahamishwa juu ya mkutano, pia wangeomba na kusema: Ee Mungu! Je, Unanikubalia niende au la? Ikiwa unanikubalia kwenda, basi nitayarishie njia iliyonyooka, acha kila kitu kifanyike kwa urahisi. Na ikiwa hunikubalii kwenda, basi nifanye nianguke chini. Walipoomba, walimsihi Mungu. Baada ya kuomba walihisi wasio na utulivu, na hawakuenda. Pia kulikuwa na dada ambao, kwa vile waliogopa kupigwa na waume wao wasiomwamini Mungu wakati ambapo wangerudi, walihisi wasio na utulivu walipoomba—na kwa vile walihisi wasio na utulivu, hawakuenda kwa mkutano. Waliamini hayo yalikuwa mapenzi ya Mungu, ilhali kweli ni kwamba, iwapo wangeenda, hakuna chochote ambacho kingefanyika. Matokeo ni kwamba walikosa mkutano. Haya yote yalisababishwa na ujinga wa watu wenyewe. Watu wanaofanya utendaji kwa njia hii huishi kwa hisia zao wenyewe. Njia hii ya utendaji ina kosa na ni ya kipumbavu, haina udhahiri, na hisia na mawazo yao wenyewe kwa wingi sana. Ukiambiwa kuhusu mkutano, basi nenda, na usipoambiwa, basi usiende; unapoambiwa kuuhusu, hakuna haja ya kumwomba Mungu. Je, hili si rahisi? Ikiwa, leo, unahitaji kununua kipande fulani cha mavazi, basi nenda ukafanye hivyo. Usimwombe Mungu na kusema: Ee Mungu! Leo napaswa kununua kipande fulani cha mavazi, je, Unanikubalia niende au la? Ni aina gani ya mavazi ninayopaswa kununua? Je dada mmoja akija hapa nikiwa nimeenda? Kwa kuomba na kutafakari, unajiambia mwenyewe: “Sitaki kwenda leo, huenda dada fulani akaja hapa.” Ilhali matokeo ni kwamba, kufikia jioni, hakuna aliyekuja hapo, na umekosa mengi. Hata katika Enzi ya Neema, njia hii ya utendaji ilikuwa na makosa na isiyo sahihi. Kwa hiyo, ikiwa watu watafanya utendaji kama katika nyakati zilizopita, hakutakuwa na mabadiliko katika maisha yao. Watakuwa tu watiifu, na hawatatilia maanani upambanuzi, na hawatafanya lolote ila kutii na kuvumilia pasipo kufikiria. Katika wakati huo, watu walisisitiza kuhusu kumtukuza Mungu—lakini Mungu hakupata utukufu wowote kutoka kwao, kwani hawakuwa wameishi kwa kudhihirisha lolote, na hawakuwa wamebadilika. Walijitiisha tu na kujiwekea mipaka wenyewe kulingana na dhana zao wenyewe, na hata miaka mingi ya utendaji haikuleta mabadiliko katika maisha yao; walijua tu kuvumilia, kuwa wanyenyekevu, kupenda, na kusamehe, na hawakupata nuru hata kidogo kutoka kwa Roho Mtakatifu. Wangemjuaje Mungu?
Watu wataingia tu kwa njia sahihi ya imani katika Mungu ikiwa watamleta Mungu ndani ya maisha yao halisi, na katika maisha yao ya kawaida ya ubinadamu. Leo, maneno ya Mungu yanawaongoza ninyi, na hakuna haja ya kutafuta na kupapasa kama nyakati zilizopita. Wakati ambapo unaweza kutenda kulingana na maneno haya, na unaweza kujichunguza na kujitathmini mwenyewe kulingana na hali ambazo Nimetaja, basi utaweza kubadilika. Haya siyo mafundisho ya dini, lakini kile ambacho Mungu anamtaka mwanadamu afanye. Leo, Nakwambia kiini cha jambo: Jishughulishe tu na kutenda kulingana na maneno Yangu. Matakwa Yangu kwako ni kulingana na mahitaji ya watu wa kawaida, na Nimekwambia hilo tayari; ikiwa unasisitiza kabisa kutenda kwa njia hii, utaweza kuufurahisha moyo wa Mungu. Siku hii ndio wakati wa kuishi katika maneno ya Mungu: Maneno ya Mungu yameeleza yote, yote yamefafanuliwa wazi, na maadamu unaishi kwa maneno ya Mungu, utaishi maisha yaliyo huru kabisa na yaliyokombolewa. Hapo awali, ulipomleta Mungu katika maisha yako halisi, ulipitia mafundisho ya dini na sherehe nyingi sana, ulimwomba Mungu hata katika mambo madogo sana, uliyaweka maneno dhahiri upande mmoja, kutoyasoma, na ukajitolea juhudi zako zote kwa kutafuta—na matokeo kwamba hakukuwa na athari. Chukua mfano wa, kile ulichovaa: Wakati ambapo uliomba, uliliweka jambo hili mikononi mwa Mungu, ukiomba kwamba Mungu achague kitu kinachofaa kwa wewe kuvaa. Mungu aliyasikia maneno haya na kusema: “Unaniomba Nijishughulishe Mimi na tondoti hafifu kama hizi? Ubinadamu wa kawaida na urazini Nilivyokuumbia vimeenda wapi?” Wakati mwingine, mtu fulani atafanya makosa katika matendo yake, na ataamini kwamba amemkosea Mungu, naye huanza kufungwa. Hali za watu wengine ni nzuri sana, lakini wanapofanya kitu fulani kidogo kwa njia isiyo sahihi wao huamini kwamba Mungu anawaadibu. Kwa kweli, hii si kazi ya Mungu, lakini ya akili za watu wenyewe. Wakati mwingine, huwa hakuna kosa lolote na vile unavyopitia tukio, laini wengine husema kwamba unapitia tukio kwa njia isiyo sahihi, na hivyo unategwa—unakuwa mbaya, na mwenye giza ndani. Mara kwa mara, watu wakiwa baridi kwa njia hii, wao huamini kwamba wanaadibiwa na Mungu, lakini Mungu husema: “Sifanyi kazi ya kuadibu ndani yako, ungenilaumuje Mimi hivyo?” Watu ni wabaya sana. Wao pia ni wepesi kuhisi sana mara kwa mara na wao hulalamika kuhusu Mungu mara kwa mara. Mungu hakutaki wewe uteseke, ilhali wewe unajiacha uingie katika hali hiyo. Hakuna thamani katika kuteseka kwa aina hii. Kwa sababu watu hawajui kazi inayofanywa na Mungu, katika mambo mengi wao ni wajinga, na hawawezi kuona kwa dhahiri. Katika nyakati kama hizo, wao hunaswa katika mawazo yao wenyewe, wakiendelea kutegwa zaidi milele. Watu wengine husema kwamba vitu vyote na mambo yote yamo mikononi mwa Mungu—kwa hiyo Mungu hangejua watu wanapokuwa wabaya? bila shaka Mungu hujua. Wakati ambapo unategwa katika dhana za binadamu, Roho Mtakatifu hana njia ya kufanya kazi ndani yako. Wakati mwingi, watu wengine hutegwa katika hali mbaya, lakini Mimi bado huendelea na kazi Yangu. Kama wewe ni mbaya au mtendaji, Mimi sizuiliwi na wewe—lakini unapaswa kujua kwamba maneno mengi Ninenayo, na kiasi kikubwa sana cha kazi Nifanyayo, huja kwa wingi na haraka kulingana na hali ya watu. Wakati ambapo wewe ni mbaya, hili halizuii kazi ya Roho Mtakatifu. Katika nyakati za kuadibu na kifo, watu wote walitegwa ndani ya hali mbaya, lakini hili halikuizuia kazi Yangu; ulipokuwa mbaya, Roho Mtakatifu aliendelea kufanya kilichohitajika kufanywa ndani ya wengine. Unaweza kuendelea kusimama kwa mwezi mmoja, lakini Naendelea kufanya kazi—chochote ufanyacho katika siku za baadaye au sasa, hakiwezi kuizuia kazi ya Roho Mtakatifu. Hali nyingine mbaya hutokana na udhaifu wa binadamu; wakati ambapo watu hawawezi kweli kufanya jambo au kulielewa, wao huwa wabaya. Kwa mfano, katika nyakati za kuadibu, maneno ya Mungu yalizungumza kuhusu kumpenda Mungu kwa kiwango fulani wakati wa kuadibu—lakini wewe uliamini kwamba huwezi. Wakati wa hali hii watu walihisi hasa wenye huzuni na wakaomboleza, walisikitika kwamba miili yao ilikuwa imepotoshwa vikali na Shetani, na kwamba uhodari wao ulikuwa mbaya sana, walihisi kwamba ilisikitisha kuwa walizaliwa katika mazingira haya. Watu wengine walihisi kwamba wakati ulikuwa umepita sana wa kuamini katika Mungu na kumjua Mungu, na kwamba walikuwa hawastahili kufanywa wakamilifu. Hizi zote ni hali za kawaida.
Mwili wa mwanadamu ni wa Shetani, umejaa tabia za kutotii, ni mchafu ya kusikitisha, ni kitu kichafu. Watu hutamani raha ya mwili kupita kiasi, kuna maonyesho mengi sana ya mwili, na kwa hiyo Mungu hudharau mwili kwa kiwango fulani. Watu wanapoacha uchafu, mambo potovu ya Shetani, wao hupata wokovu wa Mungu. Lakini wakibaki bila kuweza kuachana na uchafu na upotovu, basi bado watamilikiwa na Shetani. Kula njama, udanganyifu, na uhalifu wa watu ni mambo ya Shetani; kwa kukuokoa wewe, Mungu hukutenganisha na mambo haya na kazi ya Mungu haiwezi kuwa na kosa, na yote ni kwa sababu ya kuwaokoa watu kutoka gizani. Wakati ambapo umeamini kwa kiwango fulani na unaweza kuachana na upotovu wa mwili, na hufungwi tena na upotovu huu, je, hutakuwa umeokolewa? Wakati ambapo unaishi ukimilikiwa na Shetani huwezi kumdhihirisha Mungu, wewe ni kitu kichafu, na hutapokea urithi wa Mungu. Mara tu umetakaswa na kufanywa kamili, utakuwa mtakatifu, na utakuwa wa kawaida, na utabarikiwa na Mungu na wa kufurahisha kwa Mungu. Kazi inayofanywa na Mungu leo ni wokovu, na, zaidi ya hayo, ni hukumu, kuadibu, na laana. Ina hali nyingi. Je, maneno mengine ya Mungu sio hukumu na kuadibu tu, bali pia laana? Nazungumza ili kutimiza athari fulani, kuwafanya watu wajijue wenyewe, na sio kuwafisha watu; Moyo Wangu ni kwa ajili yenu. Kuzungumza ni mbinu mmojawapo ambayo Mimi hufanyia kazi, Natumia maneno kuonyesha tabia ya Mungu, na kukuruhusu wewe kuelewa mapenzi ya Mungu. Mwili wako waweze kufa, lakini una roho na nafsi. Kama watu wangekuwa na mwili tu, basi hakungekuwa na maana ya wao kuamini katika Mungu, wala hakungekuwa na maana kwa kazi hii yote ambayo Nimefanya. Leo, Nazungumza juu ya jambo moja na kisha lingine, wakati mmoja Ninachukia mno watu, na wakati mwingine Ninapenda kwa hali ya juu; Nafanya hili kuzibadilisha tabia zako, na kuzigeuza dhana zako.
Siku za mwisho zimefika, na nchi nyingi kutoka upande mmoja wa ulimwengu hadi mwingine ziko katika machafuko, kuna vurugu ya kisiasa, njaa, ndwele, mafuriko, na ukame unaonekana kila mahali, kuna maangamizi katika ulimwengu wa mwanadamu, na Mbingu imetuma msiba hapa chini. Hizi ni ishara za siku za mwisho. Lakini kwa watu, unaonekana kama ulimwengu wa uchangamfu na fahari, ambao unaendelea kuwa hivyo zaidi na zaidi. Watu wanapotazama ulimwengu, mioyo yao inavutiwa nao, na wengine hawawezi kujinasua kutoka kwa ulimwengu; idadi kubwa itadanganywa na wale wanaoshiriki katika hila na uchawi. Usipojitahidi ili kuendelea mbele, na huna maadili, utapeperushwa na wimbi hili lenye dhambi. China ni nchi iliyo nyuma sana kimaendeleo kuliko zote, ni nchi ambayo joka kuu jekundu limelala likiwa limejiviringisha, ina watu wengi zaidi wanaoabudu sanamu na kushiriki katika uchawi, hekalu nyingi zaidi, na ni mahali ambapo pepo wachafu huishi. Ulizaliwa ndani yake, unafurahia manufaa yake, na unapotoshwa na kuteswa nalo, lakini baada ya kupitia kujichungua unaachana nalo na unapatwa kabisa na Mungu. Huu ni utukufu wa Mungu, na kwa hiyo hatua hii ya kazi ina umuhimu mkubwa. Mungu amefanya kazi ya kiwango kikubwa hivi, amenena maneno mengi sana, na hatimaye Atawapata ninyi kabisa—hii ni sehemu moja ya kazi ya usimamizi wa Mungu, na ni “mateka ya ushindi” ya vita dhidi ya Shetani. Kadri watu hawa wanavyokuwa bora na kadri maisha ya kanisa yanavyokuwa thabiti, ndivyo joka kuu jekundu linavyotiishwa. Haya ni mambo ya ulimwengu wa kiroho, ni vita vya ulimwengu wa kiroho, na Mungu anapokuwa mshindi, Shetani ataaibishwa na kuanguka chini. Hatua hii ya kazi ya Mungu ina umuhimu wa ajabu. Kazi ya kiwango kikubwa hivyo huokoa kabisa kikundi hiki cha watu; unaponyoka kutoka kwa ushawishi wa Shetani, unaishi katika nchi takatifu, unaishi katika nuru ya Mungu, na hapo kuna uongozi na mwongozo wa nuru, na kisha kuna maana katika kuwa kwako hai. Mnachokula na kuvaa ni tofauti na wao; mnafurahia maneno ya Mungu, na kuishi maisha yenye maana—na wao hufurahia nini? Wao hufurahia tu urithi wa babu zao na “roho ya kitaifa.” Hawana hata dalili ndogo kabisa ya ubinadamu! Mavazi, maneno, na matendo yenu vyote ni tofauti na vyao. Hatimaye, mtaacha kabisa uchafu, hamtategwa tena na ushawishi wa Shetani, na mtapata upaji wa Mungu wa kila siku. Mnapaswa kila mara kuwa waangalifu. Ingawa mnaishi mahali pachafu hamjawekwa mawaa na uchafu na mnaweza kuishi ubavuni mwa Mungu, mkipokea ulinzi Wake mkuu. Mmechaguliwa miongoni mwa wote walio katika nchi hii ya manjano. Je, ninyi sio watu waliobarikiwa zaidi? Kama kiumbe aliyeumbwa, unapaswa bila shaka kumwabudu Mungu na kufuatilia maisha yenye maana. Usipomwabudu Mungu na uishi katika mwili mchafu, basi wewe siye mnyama tu aliye ndani ya vazi la mwanadamu? Kama binadamu, unapaswa kutumia rasilmali kwa ajili ya Mungu na kuvumilia kila mateso. Unapaswa kukubali kwa furaha na kwa hakika mateso kidogo unayopitia leo na kuishi maisha yenye maana, kama Ayubu, kama Petro. Katika ulimwengu huu, mwanadamu huvaa mavazi ya ibilisi, hula chakula kinachotolewa na ibilisi, na hufanya kazi na kutumika chini ya Shetani, na kukanyagiwa ndani ya uchafu wake. Usipoelewa maana ya maisha au njia ya kweli, basi ni nini maana ya maisha yako? Ninyi ni watu mnaofuatilia njia sahihi, wale wanaotafuta maendeleo. Ninyi ni watu ambao huinuka katika nchi ya joka kuu jekundu, wale ambao Mungu huwaita wenye haki. Je, hayo si maisha yenye maana zaidi?
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili
Soma Zaidi: Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?