Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Ushuhuda-wa-Kuipitia-Hukumu-ya-Kristo. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Ushuhuda-wa-Kuipitia-Hukumu-ya-Kristo. Onyesha machapisho yote
Jumamosi, 20 Oktoba 2018
Kanisa la Mwenyezi Mungu | Maneno ya Mungu Yameniamsha
Oktoba 20, 2018Hukumu-na-Kuadibu, maneno-ya-Mungu, Ushuhuda-wa-Kuipitia-Hukumu-ya-Kristo, VITABUNo comments
Miao Xiao Mji wa Jinan, Mkoa wa Shandong
Katika siku zilizopita, nilikuwa daima nikifikiri kuwa Mungu aliposema “ni kibaraka na msaliti anayekikimbia kiti kikuu cheupe cha enzi” Alikuwa anaashiria wale wanaoikubali hatua hii ya kazi lakini wanaishia kurudi nyuma kwa sababu hawako radhi kustahimili mateso ya kuadibu na hukumu Yake. Kwa hivyo, wakati wowote nilipoona ndugu wakijiondoa katika njia hii kwa sababu yoyote ile, moyo wangu ungejawa na dharau kwao. Huyo, kibaraka na msaliti mwingine anatoroka kutoka kwa kiti kikuu cheupe cha enzi ambaye atapokea adhabu ya Mungu. Wakati uo huo, nilijihisi nikiwa nikitenda ifaavyo kwa kukubali hukumu ya Mungu na nilikuwa siko mbali na kukubali ukombozi wake Mungu.
Siku moja, nilipokuwa nikitenda ibada ya kiroho, niliona maneno yafuatayo ya Mungu kwenye maandiko “Kristo Hufanya Kazi ya Hukumu kwa Ukweli”: “… kwa maana asili ya kazi ya aina hii hasa ni kazi ya kuweka wazi ukweli, njia, na uhai wa Mungu kwa wale wote walio na imani ndani Mwake. Kazi hii ni kazi ya hukumu inayofanywa na Mungu. Usipouchukulia ukweli huu kuwa muhimu na kila mara kufikiria kuuepuka au kutafuta njia nyingine isipokuwa ukweli, basi Ninasema kuwa wewe ni mtenda dhambi mkubwa. Iwapo una imani kwa Mungu, lakini hutafuti ukweli au mapenzi ya Mungu, wala hupendi njia inayokuleta karibu na Mungu, basi Nakwambia kuwa wewe ni yule anayejaribu kuepuka hukumu, na kwamba wewe ni kibaraka na msaliti anayekikimbia kiti kikuu cheupe cha enzi. Mungu hatawasamehe waasi wowote wanaotoroka machoni Pake. Wanadamu wa aina hii watapokea adhabu kali zaidi. Wale wanaokuja mbele za Mungu ili wahukumiwe, na zaidi ya hayo wametakaswa, wataishi milele katika ufalme wa Mungu.” Baada ya kutafakari maneno haya, hatimaye nilielewa kwamba: Inatukia kwamba vibaraka na wasaliti wanaotoroka kutoka kiti kikuu cheupe cha enzi hayazungumzii wale wanaorudi nyuma katika njia hii tu. La maana zaidi, ni kwamba yanarejelea wale wanaomfuata Mungu lakini hawaudhamini ukweli huu, watu ambao daima wanaukwepa ukweli huu, wanaotafuta njia mpya kando na njia ya kweli, na wasio tayari kujikabidhi kwa kuadibu na hukumu ya Mungu na kutafuta kutakaswa na Mungu. Chini ya nuru na mwongozo wa Mungu, nilianza kutafakari juu ya tabia yangu mwenyewe: Sasa Mungu anaonyesha maneno Yake kumhukumu mwanadamu, na kutakasa vitu kutoka kwa mwanadamu visivyolingana na Yeye kupitia mateso na usafishaji. Lakini nikikabiliwa na kuadibu na hukumu, mateso na usafishaji wa Mungu, mimi kila mara hujaribu kutoroka, nikitumaini kwamba Mungu ataondoa hali hizi upesi. Je, huku sio kuepuka ukweli na kutafuta njia ya kuuhepa ukweli? Wakati watu au maswala yanayoletewa na Mungu hayaambatani na dhana zangu binafsi, ama ninapojipata katika hali mbaya, hata kama mawasiliano ya ndugu zangu yanaweza kutatua matatizo yangu, yatatue kutoelewa kwangu kumhusu Mungu na kunisaidia kurejesha uhusiano wa kawaida na Mungu, mimi bado hupinga na kukataa kusikiliza. Je, hivi sivyo, Mungu asemavyo, kutotafuta ukweli na kutopenda njia inayonileta karibu na Mungu? Ninaposhughulikiwa na kupogolewa kwa sababu ya njia ya uzembe ambayo mimi hufanya kazi yangu, mimi kila mara huwa natafuta visingizio ili kujieleza. Je, hiki sio kiini kinachokataa kuukubali ukweli? Mara nyingi mimi hujikubali katika maisha halisi. Hata wakati najua kwamba ni ukweli, mimi hukataa kuusaliti mwili wangu ili nitende ukweli. Je, huku sio kutokubali hukumu tu, bali pia ni kutotafuta kutakaswa?...Sasa kwa kuwa natafakari kuhusu hili, nalielewa hata kwa wazi zaidi: Wale ambao Mungu husema hukimbia kutoka kwa kiti kikuu cheupe cha enzi haiashirii waliotoka kanisani tu. La muhimu hata zaidi, inarejelea mioyo yetu kukataa kukubali ukweli na kutokubali kujikabidhi kwa hukumu ya Mungu. Ni sasa tu ambapo ninaanza kuhisi wasiwasi na hofu. Japo sijaliwacha kanisa, moyo wangu kila mara ulikuwa unajaribu kuepuka hukumu ya Mungu. Je, mimi siye hasa yule kibaraka na msaliti anayekikimbia kiti cha hukumu ya Mungu? Ilhali nilikuwa nimesadiki kwamba wale wanaoiacha kanisa pekee ndio vibaraka na wasaliti wanaokikimbia kiti cha enzi cha Mungu, huku nilikuwa karibu sana kupokea wokovu wa Mungu. Ninaona kwamba kuelewa kwangu kwa neno la Mungu kuliegemea upande mmoja sana na ulikuwa wenye kina kifupi, na kwamba ufahamu wangu wa kazi ya Mungu ulikuwa umepungukiwa sana. Sasa, wale wanaokubali kwa dhati kuadibu na hukumu ya Mungu na wale ambao tabia zao zimefikia mabadiliko pekee ndio watakaopokea wokovu wa Mungu. Badala yake, nilikuwa ninaishi katika fikira zangu mwenyewe, bila kuwa na njaa ya ukweli, bila kuyawajibikia maisha yangu mwenyewe na kutokuwa na hisia ya hatari au haraka hata kidogo. Nikiendelea hivi, je, sitakuwa hasa kiumbe wa adhabu ya Mungu hasa.
Kwa sababu ya kutoa nuru kwa maneno ya Mungu, nimeamka kutoka kwa dhana na mawazo yangu, nikigundua kwamba mimi si mtu ambaye yuko tayari kukubali kuadibu na hukumu ya Mungu. Kumenifanya pia nione ya kwamba niko katika ukingo wa hatari. Kutoka sasa kuendelea, nitaupa moyo wangu wote kwa Mungu, nijikabidhi kwa kuadibu na hukumu Yake, na nifanye kila niwezalo kuutafuta ukweli na mabadiliko katika tabia, ili hivi karibuni niweze kutakaswa na nifanywe mkamilifu na Mungu.
kutoka kwa Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Vitabu
Jumapili, 23 Septemba 2018
Umeme wa Mashariki | Ni Nani Anayejua Moyo wa Kutunza wa Mungu?
Septemba 23, 2018Kiumbe-Aliyeumbwa, makusudi-ya-Mungu, Ushuhuda-wa-Kuipitia-Hukumu-ya-Kristo, VITABUNo comments
Umeme wa Mashariki | Ni Nani Anayejua Moyo wa Kutunza wa Mungu?
Ijumaa, 6 Julai 2018
Roho Mtakatifu Hufanya Kazi kwa Njia yenye Maadili
Julai 06, 2018Kazi-ya-Mungu, maneno-ya-Mungu, Ushuhuda-wa-Kuipitia-Hukumu-ya-Kristo, VITABUNo comments
26. Roho Mtakatifu Hufanya Kazi kwa Njia yenye Maadili
Qin Shuting Jijini Linyi, Mkoani Shandong
Kwa muda fulani, ingawa sikuwa nimeacha kula na kunywa manen0 ya Mungu, sikuhisi mwanga kamwe. Nilikuwa nimeomba kwa Mungu kwa ajili ya hili lakini, baadaye, bado sikuwa nimepata nuru. Hivyo niliwaza, “Nimekula na kunywa kile ambacho nilipaswa na Mungu hanipi nuru. Hakuna kile ninachoweza kufanya, na sina uwezo wa kupokea maneno ya Mungu. Kuna wakati wa Mungu kumpa kila mwanadamu nuru, kwa hivyo hakuna maana ya kuiharakisha.” Baadaye, nilishika amri na kula na kunywa maneno ya Mungu bila wasiwasi, nikingoja kwa “subira” kutoa nuru kwa Mungu.
Mpaka siku moja, nilisoma maneno haya ya Mungu: “Ni kama tu moyo wako uko na amani mbele za Mungu ndio kutafuta kwako ukweli na mabadiliko katika tabia yako kutazaa matunda. Kwa sababu unakuja ukiwa na mizigo mbele za Mungu na huwa unahisi kila mara kuwa unapungukiwa kiasi kikubwa, kwamba kuna ukweli mwingi ambao unahitaji kujua, uhalisi mwingi unaohitaji kupitia, na kwamba unapaswa kujali kikamilifu kuhusu mapenzi ya Mungu—mambo haya kila mara huwa mawazoni mwako, ni kana kwamba yamekufinyia chini sana kiasi kwamba huwezi kupumua, na hivyo unahisi mzito wa moyo (lakini sio kwa hali hasi). Ni watu wa aina hii pekee ndio wanastahili kukubali kupata nuru ya maneno ya Mungu na kuguswa na Roho wa Mungu. Ni kwa sababu ya mzigo wao, kwa sababu ni wenye moyo mzito, na, inaweza kusemwa, kwa sababu ya gharama ambayo wamelipa na mateso ambayo wamepitia mbele ya Mungu ndio wanapata nuru na mwangaza wa Mungu, kwa kuwa Mungu hamtendei yeyote kwa upendeleo. Yeye huwa mwenye haki kila mara katika kuwatendea watu, lakini Yeye sio holela katika kuwakimu watu, na hawapi bila masharti. Huu ni upande mmoja wa tabia Yake yenye haki” (“Ni Muhimu Sana Kuanzisha Uhusiano wa Kufaa na Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Katika kutafakari maneno haya ya Mungu, nilielewa: Mungu ni Mungu wa haki. Kamwe yeye Hayuko holela katika kumkidhi mwanadamu, na Hamtolei mwanadamu bila masharti. Kwa watu kupata nuru na mwangaza wa Mungu, lazima watulize mioyo yao mbele ya Mungu na wawe na moyo ambao unayatamani sana na kutafuta maneno ya Mungu. Lazima wabebe mzigo kwa ajili ya maisha yao wenyewe na kutafuta mapungufu yao wenyewe ndani ya maneno ya Mungu. Wakibeba mzigo wao, lazima kwa makusudi wale na kunywa maneno ya Mungu kujali mapenzi Yake na kwenda kwa kina zaidi katika ukweli. Ni kwa kulipa gharama kama hiyo kwa vitendo tu kufanya kazi na Mungu ndiyo mtu anaweza kupata nuru ya Mungu. Kwa kufikiria ya zamani, sikuwa nabeba mzigo wowote wala kuwa na moyo wowote wa kutamani sana hata kidogo kula na kunywa maneno ya Mungu. Kila mara nilipochukua kitabu cha neno la Mungu, ningepitia kwa haraka na kuona kwamba nilikuwa nimesoma kifungu hiki na kusoma kifungu kile, nikifikiri kuwa nilikuwa na wazo la juu juu kuhusu kila kifungu. Kisha ningepata chochote cha zamani, nikisome kwa haraka, na kisha ningekuwa nimemaliza. Nilipokula na kunywa maneno ya Mungu, ilikuwa inatosha tu kwangu kuelewa maana halisi ya maneno hayo, nikilenga tu kushika masharti machache na matendo. Bila shaka sikuona ukweli mwingi ambao nilipaswa kuingia ndani yake, wala sikuwa nauridhisha moyo wa Mungu. Sikuwa nabeba mzigo kwa ajili ya maisha yangu hata kidogo, wala sikuwa na wasiwasi kuhusu kutojiandaa na ukweli wa kutosha; nilikuwa nachukulia kula na kunywa kwangu maneno ya Mungu kwa kutojali tu. Na mwelekeo wa kifidhuli kwa maneno ya Mungu hivyo, ningewezaje kupata nuru na mwangaza Wake? Kwa kweli sikuwa nafanya kazi na Mungu, na nilikuwa natumia “Kuna wakati wa Mungu kumpa nuru kila mwanadamu” kama kisingizio kungoja kwa upofu kutoa nuru kwa Mungu. Kwa kweli nilikuwa mpumbavu sana! Ni sasa tu ndiyo natambua kwamba, ingawa kuna wakati wa Mungu kumpa nuru kila mwanadamu, hili ni kweli, kuna kanuni katika kazi ya Roho Mtakatifu kwa mwanadamu. Mwanadamu mwenyewe lazima awe na moyo wa tamaa kubwa, ya kutafuta ili kuweza kufanya kazi na Mungu kwa vitendo na kwa utendaji. Ni hapo tu ndipo Roho Mtakatifu anaweza kufanya kazi kwa mwanadamu na kutia nuru na kuangazia kuelewa kwa mwanadamu kwa mapenzi ya Mungu, kumfanya kuelewa ukweli katika maneno Yake.
Ee Mungu! Ninatoa shukrani kwa sababu ya kutoa nuru Kwako kwa muda ufaao ambako kuliniruhusu kuona mkengeuko katika uzoefu wangu mwenyewe. Sasa ninatamani kurudi katika kufanya kazi kwa moyo mwema na kiutendaji pamoja na Wewe, kuweka moyo unaotafuta na kutamani sana, kubeba mzigo wangu wa kula na kunywa maneno Yako, kufuatilia kupata nuru zaidi kunakopatikana kupitia katika maneno Yako, kujifanya kupenyeza zaidi katika ukweli, na kwa maisha yangu kua hata zaidi. Utukufu wote Uwe kwa Mwenyezi Mungu!
kutoka kwa Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo
Jumatano, 4 Aprili 2018
Roho Mtakatifu Hufanya Kazi kwa Njia yenye Maadili
Aprili 04, 2018Kanisa-la-Mwenyezi-Mungu, Kusogea-karibu-na-Mungu, Ushuhuda-wa-Kuipitia-Hukumu-ya-Kristo, VITABUNo comments
26. Roho Mtakatifu Hufanya Kazi kwa Njia yenye Maadili
Qin Shuting Jijini Linyi, Mkoani Shandong
Kwa muda fulani, ingawa sikuwa nimeacha kula na kunywa manen0 ya Mungu, sikuhisi mwanga kamwe. Nilikuwa nimeomba kwa Mungu kwa ajili ya hili lakini, baadaye, bado sikuwa nimepata nuru. Hivyo niliwaza, “Nimekula na kunywa kile ambacho nilipaswa na Mungu hanipi nuru.
Jumanne, 20 Februari 2018
Maneno ya Mungu Yameniamsha
Februari 20, 2018Kanisa-la-Mwenyezi-Mungu, Neno-la-Mungu, Ushuhuda-wa-Kuipitia-Hukumu-ya-Kristo, VITABUNo comments
22. Maneno ya Mungu Yameniamsha
Miao Xiao Mji wa Jinan, Mkoa wa Shandong
Katika siku zilizopita, nilikuwa daima nikifikiri kuwa Mungu aliposema “ni kibaraka na msaliti anayekikimbia kiti kikuu cheupe cha enzi” Alikuwa anaashiria wale wanaoikubali hatua hii ya kazi lakini wanaishia kurudi nyuma kwa sababu hawako radhi kustahimili mateso ya kuadibu na hukumu Yake.
Jumatatu, 19 Februari 2018
Ninaona njia ya kumjua Mungu
Februari 19, 2018Kanisa-la-Mwenyezi-Mungu, kumjua-Mungu, Ushuhuda-wa-Kuipitia-Hukumu-ya-Kristo, VITABUNo comments
9. Ninaona njia ya kumjua Mungu
Xiaocao Mji wa Changzhi, Mkoa wa Shanxi
Siku moja, niliona kifungu hiki kifuatacho cha neno la Mungu kwa maandishi “Namna Petro Alivyopata Kumjua Yesu”: “Kwenye kipindi kile alichomfuata Yesu, Petro alitazama na kutia moyoni kila kitu kuhusu maisha Yake: Matendo Yake, maneno Yake, mwendo Wake na maonyesho Yake. …
Jumanne, 13 Februari 2018
Umeme wa Mashariki | Kubagua dhidi ya Watu wa Nje ni Uovu Sana!
Februari 13, 2018Hukumu-na-Kuadibu, Umeme-wa-Mashariki, Ushuhuda-wa-Kuipitia-Hukumu-ya-Kristo, VITABU, VitendoNo comments
Umeme wa Mashariki | 42. Kubagua dhidi ya Watu wa Nje ni Uovu Sana!
Xiaojin Kaunti ya Pan’an , Mkoa wa Zhejiang
Katika mwezi wa Februari mwaka wa 2007, kanisa lilipokea mpango wa kazi uitwao "Nyunyizia na Uwape Waumini Wapya ili Kuwasaidia Kukita Mizizi Haraka Iwezekanavyo." Ulisisitiza kuwa "Ni muhimu kuwatumia wale wote wanaofaa na walio na tajriba katika kuwanyunyizia waumini wapya ili kukamilisha kazi hii.
Jumatano, 7 Februari 2018
Umeme wa Mashariki | Kwa Nini Nimetembea Njia ya Mafarisayo?
Februari 07, 2018Kanisa-la-Mwenyezi-Mungu, kumjua-Mungu, Siku-ya-Hukumu, Ushuhuda-wa-Kuipitia-Hukumu-ya-Kristo, VITABUNo comments
Umeme wa Mashariki | 73. Kwa Nini Nimetembea Njia ya Mafarisayo?
Suxing Mkoa wa Shanxi
Mimi ni mtu mwenye kiburi na majivuno, na cheo kimekuwa udhaifu wangu. Kwa miaka mingi, nimefungwa na sifa na cheo na sijaweza kujiweka huru kutoka kwazo. Mara kwa mara nimepandishwa cheo na kubadilishwa na mtu mwingine; nimekuwa na vizuizi vingi katika cheo changu na nimekumbwa na matuta mengi njiani.
Jumanne, 6 Februari 2018
Kukubali Ukweli kwa Hakika Ni Nini?
Jumamosi, 20 Januari 2018
Kanisa la Mwenyezi Mungu | 45. Kanuni Zangu za Maisha Ziliniacha Nikiwa Nimeharibika
Januari 20, 2018Hukumu-na-Kuadibu, Kanisa-la-Mwenyezi-Mungu, Ushuhuda-wa-Kuipitia-Hukumu-ya-Kristo, VITABUNo comments
45. Kanuni Zangu za Maisha Ziliniacha Nikiwa Nimeharibika
Changkai Mji wa Benxi, mkoa wa Liaoning
Maneno ya kawaida "Watu wazuri humaliza wakiwa wa mwisho" ni ambayo mimi binafsi ninayafahamu sana. Mimi na mume wangu sote tulikuwa hasa watu wasio na hatia: Wakati wa masuala yaliyohusisha faida au hasara yetu binafsi, hatukuwa aina ya watu wa kubishana na kusumbuana na wengine.