Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Jumanne, 23 Oktoba 2018

Gospel Video "Rekodi ya Kazi ya Mungu ya Kuumba Ulimwengu na Kuwaongoza na Kuwakomboa Wanadamu"

Gospel Video "Rekodi ya Kazi ya Mungu ya Kuumba Ulimwengu na Kuwaongoza na Kuwakomboa Wanadamu"

Je, unataka kujua jinsi Mungu alivyouumba ulimwengu? Je, unataka kujua jinsi Mungu amewaongoza wanadamu hatua kwa hatua hadi leo? Sehemu hii ya ajabu kutoka kwa filamu ya Kikristo, "Yule Anayeshikilia Ukuu Juu Ya Kila Kitu", imerekodi kazi ya Mungu ya kuumba ulimwengu na kuwaongoza na kuwakomboa wanadamu. Itakufichulia majibu haya.
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, utukufu kwa Mungu

Jumatatu, 22 Oktoba 2018

kutoka kwa Ushuhuda wa Washindi | Upendo wa Mungu Ulikuwa Nami Katika Gereza la Giza la Ibilisi

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mateso ya Kidini

kutoka kwa Ushuhuda wa Washindi | 1. Upendo wa Mungu Ulikuwa Nami Katika Gereza la Giza la Ibilisi

Yang Yi, Mkoa wa Jiangsu
Mimi ni Mkristo wa Kanisa la Mwenyezi Mungu. Nimekuwa mfuasi wa Mwenyezi Mungu kwa zaidi ya miaka kumi. Katika wakati huu, kitu kimoja ambacho sitawahi kusahau ni taabu mbaya sana nilipokamatwa na polisi wa CCP muongo mmoja uliopita. Wakati huo, licha ya mimi kuteswa na kukandamizwa na ibilisi waovu, na kuwa ukingoni mwa kifo mara kadhaa, Mwenyezi Mungu alitumia mkono Wake wa nguvu kuniongoza na kunilinda, kunirudisha kwa uhai, na kunipeleka kwa usalama.... Kupitia hili, kwa kweli nilipitia uvukaji mipaka na ukuu wa nguvu ya uhai wa Mungu, na kupata utajiri wa thamani wa maisha niliyotunikiwa na Mungu.
Ilikuwa Januari 23, 2004 (siku ya pili ya Mwaka Mpya wa Kichina). Nilihitaji kuenda kumtembelea dada fulani kutoka kwa kanisa; alikuwa katika shida na alihitaji msaada kwa dharura. Kwa kuwa aliishi mbali sana, ilinibidi nirauke mapema ili kupata teksi ili niweze kurudi siku hiyo hiyo. Niliondoka nyumbani wakati tu mwanga ulichomoka. Kulikuwa na watu wachache sana barabarani, wafanyikazi wa kusafisha taka pekee. Kwa wasiwasi nilitafuta teksi, lakini hakukuwa na yoyote hapo. Nilienda kwa stesheni ya teksi kusubiri, na nikasongea kwa barabara kusimamisha moja nilipoiona ikija—lakini ikatokea kuwa gari la Shirika la Kulinda Mazingira. Waliniuliza mbona niliwasimamisha. “Naomba radhi, ilikuwa makosa, nilidhani mlikuwa teksi,” nilisema. “Tunafikiri ulikuwa ukitundika mabango yasiyo halali,” walijibu. “Je, mliniona? Yako wapi mabango niliyokuwa nikitundika?” nilisema. Bila kunipa fursa ya kujitetea, wao watatu walikimbia mbele na kwa nguvu walichunguza mfuko wangu. Walipekua kila kitu katika mfuko wangu—nakala ya mahubiri, kitabu cha kuandikia, pochi, simu ya rununu na bipa iliyoondolewa uwezo, na kadhalika. Kisha walichunguza kwa makini nakala hiyo ya mahubiri na kitabu cha kuandikia. Kwa kuona kwamba hakukuwa na mabango ndani ya mfuko wangu, waliinua nakala hiyo ya mahubiri na kusema: “Yaweza kuwa hukuwa ukitundika mabango yasiyo halali, lakini unamwamini Mwenyezi Mungu.” Kisha, walipigia simu Divisheni ya Dini ya Kikosi cha Usalama wa Taifa. Punde baadaye, watu wanne kutoka kwa Kikosi cha Usalama wa Taifa waliwasili. Walijua kwamba nilikuwa muumini wa Mwenyezi Mungu punde walipoona vitu ndani ya mfuko wangu. Bila kuniruhusu kusema lolote, walinitupa ovyo katika gari lao, kisha walifunga mlango kwa ufunguo ili kunikomesha kuhepa.
Tulipowasili katika Shirika la Usalama wa Umma, polisi waliniongoza kuingia katika chumba. Mmoja wao alichezacheza na bipa na simu yangu ya rununu, akitafuta dokezo. Aliwasha simu lakini ikaonyesha kwamba ilikuwa na betri ya chini, kisha ikasema betri ilikuwa tupu kabisa. Ingawa alijaribu sana, hangeweza kuiwasha. Akishika simu, alionekana kuwa na wasiwasi. Nilikanganywa pia—nilikuwa nimechaji simu hiyo asubuhi hiyo. Inawezekanaje iwe haina chaji? Ghafla nilitambua kwamba Mungu alikuwa amepanga hili kwa miujiza ili kuzuia polisi kupata taarifa yoyote kuhusu ndugu wengine. Pia nilielewa maneno yaliyonenwa na Mungu: “vitu vyote, vilivyo hai au vilivyokufa, vitahamishwa, vitabadilika, vitafanywa vipya, na kutoweka kulingana na mawazo ya Mungu. Hivi ndivyo Mungu anavyotawala juu ya kila kitu” (Kutoka kwa “Mungu Ndiye Chanzo cha Uhai wa Mwanadamu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Hili lilinipa ufahamu wa kweli wa ukuu na mpango wa Mungu wa mambo yote, na kuimarisha imani yangu katika ushirikiano wa baadaye. Akiashiria vitu ndani ya mfuko wangu, afisa wa polisi aliuliza kwa shutuma: “Haya yanaonyesha kwamba kwa kweli wewe si mshirika wa kawaida wa kanisa. Lazima uwe mmoja wa uongozi mkubwa, mtu ambaye ni muhimu. Kwa maana viongozi wadogo hawana bipa ama simu za rununu. Niko sahihi?” “Sielewi unachosema,” nilijibu. “Unajifanya huelewi!” alisema kwa sauti kubwa, kisha akaniamuru kuchuchumaa nilipozungumza. “Huku akiona kwamba singeshirikiana, walinizingira na kuanza kunipiga ngumu na kunipiga teke—kiasi cha kutosha kuniua. Uso wangu ukiwa umejaa damu na kuvimba, mwili wangu mzima ukiuma kiasi cha kutovumilika, nilianguka sakafuni. Nilikasirishwa. Nilitaka kuzungumza maana kwao, kutoa sababu ya kuthibitisha hali yangu: Nimekosea wapi? Mbona mlinichapa hivyo? Lakini sikuwa na njia ya kuongea maana nao, kwa sababu serikali ya CCP haiongei maana. Nilikanganyikiwa, lakini sikutaka kukubali vipigo vyao. Nilipokuwa tu sijui la kufanya, ghafla nilifikiri jinsi, kwa kuwa hawa maofisa waovu wa serikali ya CCP walikuwa wapuuzi sana, kwa kuwa hawakuwa wakiniruhusu kuzungumza maneno yoyote ya maana, sikuhitaji kuwaambia chochote. Ilikuwa ni heri nibaki kimya—kwa njia hiyo singekuwa na manufaa yoyote kwao. Nilipofikiri hili, niliacha kutia maanani walichokuwa wakisema.
Huku wakiona kuwa mtazamo huu haukuwa na athari yoyote kwangu, polisi hao waovu walikasirika sana na wakawa katili hata zaidi: Waligeukia mateso ili kutoa ili kunifanya nikiri. Walinitia pingu kwa kiti cha chuma kilichokazwa kwa skrubu sakafuni kwa njia ambayo singechuchumaa wala kusimama. Mmoja wao aliweka mkono wangu ambao hukuwa umetiwa pingu kwa kiti na kuupiga kwa kiatu, akikomesha tu wakati upande wa nyuma wa mkono wangu ulikuwa umegeuka rangi kuwa mweusi na samawati: mwingine aliponda vidole vyangu vya miguu chini ya kiatu chake cha ngozi. Ni hapo tu ndipo nilipitia kwamba uchungu katika vidole huenda moja kwa moja hadi moyoni. Baada ya hapo, polisi wasita ama saba walichukua zamu kwangu. Mmoja wao alilenga viungo vyangu, na kuvichuna kwa nguvu sana kiasi kwamba mwezi mmoja baadaye bado singeweza kuupinda mkono wangu. Mwingine alinyakua nywele zangu na kutingisha kichwa changu upande mmoja kuelekea upande mwingine, kisha akakivuta kwa ghafla nyuma ili nilikuwa nikiangalia juu. “Tazama anga na kuona iwapo kuna Mungu!” alisema kwa ukali. Waliendelea hadi usiku. Wakiona kwamba hawangepata chochote kutoka kwangu, na kwa sababu ilikuwa Mwaka Mpya wa Kichina, walinituma moja kwa moja hadi katika kituo cha kuzuia.
Nilipowasili katika kituo cha kuzuia, mlinzi alimwamuru mfungwa wa kike kunivua nguo zote na kuzirusha katika pipa la takataka. Kisha walinifanya nivae sare chafu ya gereza, iliyokuwa ikinuka vibaya. Walinzi waliniweka katika seli na kisha wakawadanganya wafungwa wengine, wakisema: “Yeye hasa alivunja familia za watu. Familia nyingi zimeharibiwa na yeye. Yeye ni mwongo, huwadanganya watu waaminifu, na kuvuruga utulivu wa umma....” “Mbona anafanana na punguani?” mmoja wa wafungwa aliuliza. Kwa hilo walinzi walijibu: “Anajifanya kuepuka kuhukumiwa. Ni nani kati yenu aliye mwerevu hivyo? Yeyote anayefikiri yeye ni mpumbavu ni mjinga kabisa kwa wote.” Hivyo wakiwa wamedanganywa na walinzi hao, wafungwa wengine wote walisema nilikuwa nikisamehewa kwa urahisi sana, na kwamba kitu kizuri pekee kwa mtu ambaye ni mbaya kama mimi kilikuwa kikosi cha wauaji! Kusikia hili kulinikasirisha—lakini hakukuwa na chochote ambacho ningeweza kufanya. Majaribio yangu ya upinzani yalikuwa bure, yalileta tu mateso na ukatili zaidi. Katika kituo cha kuzuia, walinzi waliwafanya wafungwa kukariri amri kila siku: “Kiri uhalifu wako na kutii sheria. Kuwashawishi wengine kutenda uhalifu hakukubaliwi. Kuunda magenge hakukubaliwi. Kupigana hakukubaliwi. Kuwadhulumu wengine hakukubaliwi. Kutoa mashtaka yasiyo kweli dhidi ya wengine hakukubaliwi. Kunyakua chakula ama mali ya wengine hakukubaliwi. Kufanya hila kwa wengine hakukubaliwi. Wadhalimu wa gerezani wanapaswa kuchukuliwa hatua kali. Ukiukaji wowote wa sheria unapaswa kuripotiwa kwa wasimamizi ama polisi wenye madaraka mara moja. Unapaswa kutoficha ukweli ama kujaribu kulinda wale wafungwa ambao wamekiuka sheria na kufuatia kunapaswa kuwa kwa kwenye huruma. ...” Kwa kweli, walinzi waliwatia moyo wafungwa wengine kunitesa, wakiwaruhusu kunitendea hila kila siku: Wakati ambapo halijoto ilikuwa digrii 8 ama 9 chini ya sufuri, walilowa viatu vyangu: kwa siri walimwaga maji kwenye chakula changu: jioni, nilipokuwa nikilala, walirowesha jaketi langu lililojazwa pamba: walinifanya nilale kando ya choo, mara kwa mara walivuta mfarishi wangu usiku, walivuta nywele zangu, ili kunizuia kulala; walininyang’anya andazi langu lilikopikwa kwa mvuke, walinilazimisha kusafisha choo, na kuingiza kwa nguvu dawa zao zilizosalia ndani ya mdomo wangu, hawakuniacha nikojoe.... Wakati sikufanya walichosema, wangechangia na kunipiga—na mara nyingi wakati kama huu wasimamizi ama polisi walio na mamlaka wangetoroka wasionekane ama kujifanya hawajaona chochote; wakati mwingine wangejificha mbali na kutazama. Iwapo wafungwa wangekaa siku chache bila kunitesa, wasimamizi na polisi wenye mamlaka wangewauliza: “Yule mwanamke mjinga ameerevuka siku hizi chache, siyo? Wakati huo, ninyi mmekuwa wajinga. Yeyote atakayembadilisha huyo mwanamke mjinga atapata msamaha.” Mateso ya kikatili ya hao walinzi yalinijaza na chuki kwao. Leo, iwapo singeona hili na macho yangu mwenyewe na kulipitia mimi binafsi, kamwe singeamini kwamba serikali ya CCP, ambayo inapaswa kuwa imejaa ukarimu na maadili, ingeweza kuwa ovu, ya kuogofya na mbaya—singewahi kuona sura yake ya kweli, sura ambayo ni danganyifu na yenye unafiki. Mazungumzo yake yote ya “kuhudumia watu, kutengeneza jamii iliyostaarabika na ya upatanifu”—huu ni uongo ulioundwa kuwadanganya na kuwahadaa watu, ilikuwa njia, hila, ya kujipendekeza na kupata heshima haifai kupata. Wakati huo, nilifikiri kuhusu maneno ya Mungu: “Haishangazi, basi, kwamba Mungu mwenye mwili abaki kuendelea kuwa Amefichwa: Katika jamii ya giza kama hii, ambapo mashetani hawana huruma na ni katili, inawezekanaje mfalme wa mashetani anayeua watu kwa kufumba na kufumbua, avumilie uwepo wa Mungu ambaye ni mwenye upendo, mpole, na mtakatifu? Anawezaje kushangilia na kufurahia ujio wa Mungu? Vikaragosi hawa! Wanalipa upole kwa chuki, wanamtweza Mungu kwa muda mrefu, wanamtukana Mungu, ni washenzi kupita kiasi, hawamjali Mungu hata kidogo, wanapora na kuteka nyara, wamepoteza dhamiri yote, na hawana hata chembe ya wema, na wanawajaribu watu wasiokuwa na hatia kuwa watu wasiokuwa na uwezo wa kuhisi. Wazazi wa kale? Viongozi Wapendwa? Wote wanampinga Mungu! Udukuzi wao umeacha wote walio chini ya mbingu katika hali ya giza na machafuko! Uhuru wa dini? Haki halali na matakwa ya wananchi? Zote hizo ni njama za kufunika dhambi!” (Kutoka kwa “Kazi na Kuingia (8)” katika Neno Laonekana katika Mwili). Nikilinganisha maneno ya CCP na uhalisi, niliona asili ovu na mbaya ya serikali ya CCP ya shetani kwa ubayana kamili. Kudumisha mamlaka yake ovu, inaweka mshiko uliobanwa kwa watu wake, na kufanya kila kitu kuwalaghai na kuwadanganya. Kwa juu juu, inadai kutoa uhuru wa dini—lakini kwa siri, inawakamata, kuwakandamiza, kuwatesa, na kuwaua watu kutoka kila pande zote za nchi ambao wanamwamini Mungu. Hata inajaribu kuwaua wote. Jinsi gani ibilisi alivyo mjanja, katili, na asiyependa maendeleo! Uhuru uko wapi? Haki za binadamu ziko wapi? Je, si zote ni hila za kutumia kuwadanganya watu? Je, watu wanaweza kuona mara moja matumaini ama mwanga wowote wakiishi chini ya utawala wake muovu? Wanawezaje kuwa huru kumwamini Mungu na kufuatilia ukweli? Hapo tu ndipo nilitambua kwamba Mungu alikuwa ameruhusu mateso na majaribu haya kunifikia, kwamba Alikuwa ameitumia kunionyesha ubaya na ukatili wa serikali ya CCP, ili kunionyesha asili yake ya shetani ambayo ina uadui na ukweli na ya uhasama kwa Mungu, na kunionyesha kwamba polisi wa watu, ambao serikali kwa nguvu huwajenga na kuwatangaza kama wanaoadhibu uovu, kutetea wema, na kukuza haki, ni washirika na watumishi imelea kwa uangalifu, kundi la wauaji ambao wana sura za wanaume lakini mioyo ya wanyama, na ambao wangeua kufumba kufumbua. Ili kujaribu kupiga marufuku na kukomesha kazi ya Mungu, na kunilazimisha kukataa na kumsaliti Mungu na kukubali nguvu yake ya dikteta, serikali ya CCP ilifanya kila kitu kunitesa na kuniangamiza—ilhali haikujua hata kidogo kwamba kadiri ilivyonitesa, ndivyo niliona sura yake ya ibilisi kwa wazi kabisa, na ndivyo nilivyoidharau na kuikataa zaidi kutoka kwa vina vya moyo wangu, kunifanya kumtamani sana Mungu kwa kweli na kumwamini Mungu. Hata zaidi, ilikuwa hasa kwa sababu ya mateso ya walinzi ndipo bila kutambua nilikuja kuelewa kinachomaanisha kweli kupenda anachopenda Mungu na kuchukia anachochukia Mungu, kinachomaanisha kumkwepa Shetani na kugeuza moyo wa mtu kwa Mungu, kinachomaanisha kuwa katili, nguvu za giza ni nini, na zaidi ya hayo, kinachomaanisha kuwa mbaya sana na mwenye kudhuru kwa siri, na mwongo na mdanganyifu. Nilimshukuru Mungu kwa kuniruhusu nipitie hali hii, kwa kuniruhusu kujua sahihi kutoka kwa isiyo sahihi na kuona njia sahihi ya maisha ambayo napaswa kuchukua. Moyo wangu—ambao ulikuwa umedanganywa na Shetani kwa muda mrefu sana—hatimaye uliamshwa na upendo wa Mungu. Nilihisi kwamba kulikuwa na maana kuu katika mimi kuwa na bahati ya kupitia jaribio na majaribu haya, kwamba kwa kweli nilikuwa nimeonyeshwa fadhili maalum.
Baada ya kujaribu kila kitu kingine, polisi waovu waliunda mpango mwingine: Walimpata mchungaji kutoka kwa kanisa la Nafsi Tatu ambaye alinijua kunifichua. Alisema nilimwamini Mwenyezi Mungu na wakati mmoja nilijaribu kueneza injili kwake—lakini alikuwa amekataa. Na pia alijaribu kunifanya nimkwepe Mungu. Kwa kuona huyu mtumishi mwovu ambaye alikuwa amewaripoti ndugu wengi ambao walieneza injili, na kwa kusikia maneno yote mabaya yaliyotoka mdomoni mwake—maneno yaliyosingizia, kukashifu, na kukufuru dhidi ya Mungu—moyo wangu ulijawa na ghadhabu. Nilitaka kumpigia kelele, kuuliza mbona alikuwa na uhasama kwa Mungu mno. Kwa nini iwe kwamba alifurahia sana neema ya Mungu, ilhali alikuwa ameshirikiana na ibilisi waovu kuwatesa wateule wa Mungu? Katika moyo wangu, kulikuwa na huzuni na uchungu usioelezeka. Nilihisi pia hisia kubwa ya huzuni na mwenye deni; kwa kweli nilijichukia kwa jinsi, zamani, sikuwa nimejaribu kufuatilia ukweli, na sikuwahi kujua lolote isipokuwa furaha ya neema na baraka za Mungu kama mtoto mjinga, nisitilie maanani uchungu na fedheha ambayo Mungu alikuwa amestahimili kwa ajili ya wokovu wetu. Ni sasa tu, nilipokuwa ndani sana ya pango la ibilisi, ndipo nilihisi jinsi ilivyokuwa vigumu kwa Mungu kufanya kazi katika nchi hii chafu, potovu, na jinsi uchungu Aliokuwa amepitia ulivyokuwa mkubwa! Kwa kweli, upendo wa Mungu kwa mwanadamu hubeba uchungu mkubwa. Anafanya kazi ya kumwokoa mwanadamu huku Akivumilia usaliti wa mwanadamu. Usaliti wa mwanadamu umemletea Yeye uchungu na maumivu pekee. Si ajabu Mungu alisema wakati mmoja: “Hata kama ni kwa muda wa usiku mmoja tu, wao watatoka katika hali ya tabasamu, watu wenye “mioyo mikunjufu” hadi wenye sura mbovu na wauaji wakatili, ghafla wakiwatendea wafadhili wao wa jana kana kwamba ni adui wa milele, bila chanzo wala sababu” (Kutoka kwa “Kazi ya Mungu na Utendaji wa Mwanadamu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Leo, ingawa nilikuwa nimetumbukia katika mishiko ya ibilisi, singemsaliti Mungu bila kujali chochote. Bila kujali taabu kubwa niliyopitia, singekuwa Yuda kwa ajili ya kujiokoa. Singemsababishia Mungu uchungu na huzuni. Kwa ajili ya mimi kusalitiwa na huyu mchungaji kutoka kwa jamii ya dini, polisi waovu waliongeza mateso yao. Yeye, wakati huo, alisimama upande mmoja na kusema: “Hujui kutofautisha mazuri kutoka kwa mabaya. Unastahili hili! Huthamini ukarimu wangu. Unastahili kuteswa hadi kufa!” Kusikia maneno haya mabaya, maovu kulinikasirisha—lakini pia nilihisi hisia isiyoelezeka ya huzuni. Nilitaka kulia, lakini nilijua haikunipasa kufanya hivyo. Moyoni mwangu, niliomba kwa siri: Ee Mungu! Ningependa upate moyo wangu. Ingawa siwezi kukufanyia lolote wakati huu, nataka kukutolea ushuhuda wa ushindi mbele ya Shetani na mtu huyu mwovu, kuwaaibisha kabisa, na kupitia hili kuleta faraja kwa moyo Wako. Ee Mungu! Ningependa ulinde moyo Wangu, na kunifanya kuwa mwenye nguvu zaidi. Iwapo nina machozi, naomba yatiririke kwa ndani—siwezi kuwaruhusu waone machozi yangu. Napaswa kuwa na furaha kwa sababu naelewa ukweli, kwani umeng’arisha macho yangu, Ukinipa uwezo wa kutofautisha, na kuona kwa dhahiri asili na kiini cha Shetani, ambacho ni kukupinga, kukusaliti, na kuvunja kazi Yako. Katikati ya usafishaji, nimeona pia jinsi mkono Wako wenye hekima hupanga yote. Nataka kuendelea kushirikiana na Wewe, hadi ushindi uwe Wako. Baada ya kuomba, moyoni mwangu kulikuwa na nguvu ya kutopumzika hadi nilipomaliza ushuhuda wangu kwa Mungu. Nilijua kwamba hili lilikuwa limepewa kwangu na Mungu, kwamba Mungu alikuwa amenipa ulinzi mkubwa na kunisisimua sana. Polisi waovu walitaka kutumia mtu mwovu kunifanya kumsaliti Mungu, lakini Mungu ni Mungu mwenye hekima, na Alitumia mtu huyo mwovu kama mfano unaopinga kunionyesha asili ya uasi ya wanadamu wapotovu, Akichangamsha azimio na imani yangu kumridhisha Mungu. Hata zaidi, nilikuwa na ufahamu fulani wa kazi ya hekima ya Mungu, niliona kwamba Mungu hutawala na kushawishi yote yaliyo katika huduma kukamilisha watu wa Mungu. Huu ni ukweli dhabiti wa utumizi wa Mungu wa hekima kumshinda Shetani.
Kwa kuona kuwa hawangeniruhusu kusema chochote nilichotaka, walitumia kila gharama—iwe ikama, ama vifaa na rasilmali za fedha—kufanya juu chini kuuliza dhibitisho kwamba nilikuwa muumini wa Mungu. Baada ya miezi mitatu, kuharakisha kote kwao huku na kule hakukuwa kumezaa matunda. Mwishowe, walijaribu kupiku: Walimpata mhojaji stadi. Ilisemekana kwamba kila mtu aliyeletwa kwake alipitia aina zake tatu za mateso, na hakuna mbaye hakuwahi kukiri. Siku moja, maafisa wanne wa polisi walikuja na kuniambia: “Leo, tunakupeleka nyumbani mpya.” Kisha, walinisukuma kwa gari la kusafirisha wafungwa, kufunga pingu mikono yangu nyuma ya mgongo wangu, na kuweka kifuniko kichwani mwangu. Hali ilinifanya nifikiri walikuwa wakinipeleka kuniua kwa siri. Moyoni mwangu, sikuweza kujizuia kuwa na hofu. Lakini baadaye, nilifikiri kuhusu wimbo ambao nilikuwa nikiimba nilipomwamini Yesu: “Tangu nyakati za awali kabisa za kanisa, wale ambao humfuata Bwana wamelazimika kulipa gharama ya juu. Makumi ya maelfu ya jamaa wa kiroho wamejitoa kwa injili, na hivyo wamepata uzima wa milele. Kifo cha kishahidi kwa ajili ya Bwana, niko tayari kufa shahidi kwa ajili ya Bwana.” Siku hiyo, hatimaye nilielewa wimbo huo: Wale wanaomfuata Bwana lazima walipe gharama ya juu. Mimi pia nilikuwa tayari kufa kwa ajili ya Mungu. Kustaajabika, baada ya kuingia kwa gari, bila kuwa mwangalifu nilisikia bila kusudia mazungumzo baina ya polisi waovu. Ilionekana walikuwa wakinipeleka mahali pengine kuhojiwa. Aa! Hawakuwa wakinipeleka kuuawa—na nilikuwa nimejitayarisha kufa shahidi kwa ajili ya Mungu! Nilipokuwa tu nikifikiria hili, kwa sababu fulani zisizojulikana mmoja wa polisi alikaza kamba za ukaya kichwani mwangu. Punde baadaye, nilianza kuhisi kutotulia–ilihisi kana kwamba nilikuwa nikisongwa. Nilijipata nikijiuliza iwapo kwa kweli wangenitesa hadi nife. Wakati huo, nilifikiri kuhusu jinsi wanafunzi wa Yesu walikuwa wamejitoa kueneza injili. Singekuwa mwoga. Hata iwapo ningekufa, singewasihi wailegeze, hata zaidi singekubali kushindwa. Lakini sikuweza kujidhibiti: Nilizirai na kuwaangukia. Huku wakiona kilichokuwa kikitendeka, polisi kwa haraka walilegeza kifuniko. Nilianza kutoa povu mdomoni, kisha sikuweza kuacha kutapika. Ilihisi kana kwamba ningetapika mpaka matumbo yangu yatoke nje. Nilihisi kizunguzungu, kichwa changu kilikuwa kitupu, na singeweza kufungua macho yangu. Sikuwa na nguvu popote mwilini mwangu kana kwamba nilikuwa nimepooza. Ilihisi kana kwamba kulikuwa na kitu cha kunata mdomoni mwangu ambacho singeweza kutoa. Daima nilikuwa dhaifu, na baada ya kuteswa namna hii nilihisi kwamba nilikuwa taabani, kwamba ningeacha kupumua wakati wowote. Katikati ya uchungu, nilimwomba Mungu: “Ee Mungu! Iwapo Unataka nishuhudie kifo Kwako, kwa furaha nakutii, na kwa furaha kutumia kifo kukuridhisha. Najua kwamba wale wanaokufa kwa jina la Mungu hawakufi, ila wanalala. Naamini kwamba chochote Unachofanya, ni cha haki, na ningependa kwamba Uulinde moyo wangu, ili kwamba niweze kustahi yote ambayo Unapanga na kuweka kwa utaratibu.” Wakati mwingine baadaye, gari liliwasili kwa hoteli fulani. Wakati huo, mwili wangu wote ulihisi mnyonge na singeweza kufungua macho yangu. Walinibeba hadi kwa chumba kilichofungwa kabisa. Yote ambayo ningesikia ilikuwa sauti ya watumishi wengi wa serikali ya CCP waliokuwa wamesimama wakinizingira wakinijadili, wakisema kwamba kuniona kulikuwa kama kuona jinsi Liu Hulan alivyokuwa. Ilikuwa kitu kilichozindua, cha kuvutia sana! Yeye hata ni sugu kuliko jinsi Liu Hulan alivyokuwa! Kwa kusikia hili, moyo wangu ulifura kwa msisimko. Niliona kwamba Mwenyezi Mungu alilazimika kuwa mshindi, kwamba Shetani alikuwa chini ya miguu ya Mungu! Nilimshukuru na kumsifu Mungu kwa kunipa imani na utiifu. Wakati huu, nilisahau uchungu. Nilihisi kufurahishwa pakubwa mno kutukuzwa na Mungu.
Punde baadaye, “mtaalamu wa mahojiano” ambaye polisi walimzungumzia aliwasili. Punde alipoingia, alipaza sauti: “Yuko wapi huyo mwanamke mjinga? Acha nimwone!” Alitembea mbele yangu na kunishika kwa nguvu. Bada ya kunizaba makofi mara kadhaa usoni, alinipiga ngumi za nguvu mara kadhaa kifuani na mgongoni, kisha akaondoa kiatu chake moja cha ngozi na kunipiga usoni nacho. Baada ya kuchapwa naye hivi, nilipoteza hisia kwamba kulikuwa na kitu ambacho singeondoa mdomoni ama tumboni mwangu. Kuchanganyikiwa kuliacha kichwa changu na ningeweza kufungua macho yangu. Hisia polepole ilirudi katika viungo vyangu, na nguvu ilianza kurudi mwilini mwangu. Kisha, kwa ukali alinyakua mabega yangu na kunisukuma nyuma dhidi ya ukuta, akiniamuru nimwangalie na kujibu maswali yake. Kuona kwamba sikuwa namzingatia hata kidogo kulimfanya akasirike sana, na alijaribu kupata mjibizo kutoka kwangu kupitia kutukana, kukashifu na kumkufuru Mungu. Alitumia mbinu duni, za kustahili dharau kabisa kuniambika, na kusema kwa kuogofya: “Kwa makusudi nakutesa kwa kutumia kile kisichovumilika na mwili na nafsi yako, ili kukufanya upitie uchungu ambao hakuna mtu wa kawaida angeweza kupitia—utatamani heri ufe. Mwishowe, utaniomba nikuache uende na hapo ndipo utazungumza maana, na kusema kwamba majaliwa yako hayako mikononi mwa Mungu—yako mikononi mwangu. Nikitaka ufe, itafanyika mara moja; nikitaka uishi, utaishi; na taabu yoyote nyingine ninayotaka upitie, hiyo ndiyo utapitia. Mwenyezi Mungu wako hawezi kukuokoa—utaishi tu ukituomba tukuokoe.” Nikiwa nimekabiliwa na hawa wauaji, wanyama mwitu, ibilisi waovu wenye kustahili dharau, wasio na aibu na walio duni, nilitaka sana kupigana nao. Wakati huo nilifikiri kuhusu wimbo wa uzoefu wa maisha: “Mbingu na dunia na kila kitu ndani yavyo viliumbwa na Mungu, na ni asili na haki kwa Mungu kuvifurahia. Mfalme wa ibilisi huvimiliki bila aibu; Shetani ana hatia ya uhalifu mbaya sana kabisa; makumi ya maelfu ya jamaa wa kiroho lazima waibuke” (“Kukimbia Kuelekea kwenye Njia Ng’avu” katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya). Nilikuwa nimefanya nini kuibuka? Kwa kutosema hata chochote kuwakanusha, kuwaacha tu wanitese kwa njia yoyote ambayo walitaka—katika hili, je, nilikuwa mnyonge sana? Moyo wangu ulijawa na ghadhabu. Nilihisi kana kwamba singeweza kuidhibiti, nilitaka kupiga yowe, kurudisha pigo, kuwatangazia: “Mwanadamu kamwe hawezi kuomba huruma kutoka kwa mbwa!” Niliamini kwamba hii ilikuwa hisia ya haki—lakini kwa mshangao wangu, kadiri nilivyofikiri zaidi kwa njia hii, ndivyo nilikuwa mwenye giza zaidi ndani. Nilijipata bila maneno ya maombi, nisiweze kufikiri nyimbo zozote. Mawazo yangu yalianza kukanganyikiwa, na sikujua cha kufanya, na wakati huo nilianza kuhisi mwenye woga kiasi. Kwa haraka nilijituliza mbele ya Mungu. Nilifikiri kujihusu, na kujaribu kujijua, na wakati huo maneno ya Mungu ya hukumu yalinijia: “Unachopendezwa nacho sio kujishusha kwa Kristo…. Haupendi wosia au kependeza kwa Kristo …” (Kutoka kwa “Je, Wewe ni Muumini wa Kweli wa Mungu?” katika Neno Laonekana katika Mwili). “Je, kufuata tamaa zako mwenyewe kunafichua mlingano Wangu? Je, hilo litaridhisha moyo Wangu? Je, wewe ni mtu ambaye kwa uaminifu amefuata dhamira Zangu? Je, wewe ni mtu ambaye kwa kweli amejaribu kuelewa moyo Wangu? Je, kwa hakika umejitoa Kwangu? Je, kwa kweli umejitumia kwa ajili Yangu. Je, umeyatafakari maneno Yangu?” (Matamshi na Ushuhuda wa Kristo Mwanzoni). Kila neno la hukumu ya Mungu liliudunga moyo wangu. Ndiyo—nilikuwa nimemwona Kristo kama mdogo sana, nilikuwa nimependa nguvu na uwezo, sio unyenyekevu wa Kristo, hata zaidi nilikuwa nimetamani hekima ya kazi fiche ya Mungu. Mungu hutumia hekima Yake kumshinda Shetani, Yeye hutumia unyenyekevu na ufiche Wake kufichua sura ya kweli ya Shetani, na kukusanya ushahidi kuwaadhibu waovu. Mimi, wakati huo, nilitegemea falsafa za kishetani kuheshimu kazi ya Kristo, daima nikijaribu kulipiza kisasi kuamini kwamba kuwa mzuri ni kudanganywa, kwamba watu wote huweka mizigo juu ya farasi aliye radhi. Mbona, wakati ambapo tunateswa, tunapaswa kuwaacha polisi waovu wafanye watakavyo? Je, ni bahati nasibu ya wale wanaomwamini Mungu kudhulumiwa, kandamizwa, na kutiwa uchungu? Kama matokeo ya asili yangu ya kiburi, sikuwa tayari kustahimili fedheha, sembuse dhuluma na ukandamizaji. Hili lilikuwa limenifanya niidharau kazi ya hekima ya Kristo na kutothamini unyenyekevu na ufiche wa Kristo. Badala yake, niliamini kwamba hisia ya haki, nguvu ya sifa, na heshima ilikuwa katika kupigana nao. Sikujua kabisa kwamba Shetani alitaka kunichochea ili nipigane dhidi yao, kunilazimisha kukiri ukweli wa imani yangu kwa Mungu ili kunitia hatiani. Iwapo kweli ningepigana nao na ujasiri wa msukumo, singeshikwa na njama zao danganyifu? Kwa kweli nilimshukuru Mungu kwa ajili ya kuadibu na hukumu Yake kwangu kwa wakati ufaao, ambayo ilinipa ulinzi katikati ya uasi wangu, ili kwamba nilibaini njama danganyifu za Shetani, na kutambua sumu za Shetani ndani yangu, na kupata maarifa kiasi ya kile alicho Mungu na asili ya uhai wa Mungu iliyo nyenyekevu na fiche. Nilifikiri juu ya jinsi Kristo alikabiliwa na kuteswa, kuwindwa, na kuuwawa na ibilisi CCP, na jinsi wanadamu wote walimhukumu, na kumshutumu, na kumkashifu, na kumwacha. Wakati huo wote, Alivumilia haya yote kwa ukimya, Akistahimili uchungu huu wote kutekeleza kazi Yake ya wokovu, kamwe kutopigana, na kamwe kutolalamika. Niliona jinsi tu tabia ya Mungu ilivyo karimu, na nzuri na ya heshima! Wakati huo, mimi—mtu mchafu, mpotovu—nilikuwa nimetaka kupigana nilipoteswa na ibilisi waovu, nilikuwa nimetaka kutumia ujasiri wangu wa msukumo kutetea heshima yangu ya kudhaniwa, kupigana kwa ajili ya haki yangu mwenyewe kulingana na mapenzi yangu mwenyewe. Hisia ya haki ilikuwa wapi ndani ya hili? Na nguvu ya sifa na heshima ilikuwa wapi? Katika hili, sikuwa nikionyesha sura yangu mbaya ya shetani? Sikuwa nikifichua asili yangu ya kiburi? Je, kulikuwa na ukweli wowote katika hili? Nikifikiri hili, moyo wangu ulijawa na huzuni. Niliamua kumwiga Kristo. Nilikuwa tayari kuvumilia hali hii na kujaribu kadri nilivyoweza kushirikiana na Mungu, nisimwachie Shetani fursa yoyote.
Moyo wangu ulianza kuwa mtulivu, na kwa kimya nilisubiri zamu iliyofuata ya mapambano haya na ibilisi. Kukataa kwangu kukiri kulikuwa kumemwaibisha sana huyo aliyedhaniwa mtaalamu. Kwa hasira alipinda mkono wangu mmoja nyuma ya mgongo wangu na kuvuta huo mwingine nyuma ya mabega yangu, kisha alitia pingu mikono yangu na kuibana pamoja. Baada ya chini ya nusu saa, matone makubwa ya jasho yalikuwa yakitiririka usoni pangu, yakinizuia kuweza kufungua macho yangu. Huku akiona kwamba bado singejibu maswali yake, alinirusha sakafuni, kisha aliniinua kwa pingu nyuma ya mgongo wangu. Mikono yangu mara moja ilihisi uchungu mwingi, kana kwamba ilikuwa imevunjwa. Ilitia uchungu sana kiasi kwamba nilipumua kwa shida. Kisha, alinirusha dhidi ya ukuta na kunifanya nisimame dhidi yake. Jasho ilikuwa ikitia waa macho yangu. Nilihisi uchungu sana kiasi kwamba mwili wangu wote ulijawa na jasho—hata viatu vyangu vililowa. Daima nilikuwa dhaifu, na wakati huu nilianguka. Yote ambayo ningefanya tu ilikuwa kuhema kupitia mdomo wangu. Ibilisi alisimama kwa upande mmoja akinitazama. Sikujua alichoona—pengine aliogopa angelaumiwa iwapo ningekufa—kwa haraka alichukua kiasi kidogo cha karatasi ya shashi na kupanguza jasho yangu, kisha akaninywesha kikombe cha maji. Alifanya hivi kila wakati chini ya nusu saa ilikuwa imepita. Sijui nilifanana vipi wakati huo. Nadhani lazima ilikuwa inaogofya sana, kwa sababu ningehema tu mdomo wangu ukiwa wazi: ilionekana nilikuwa nimepoteza uwezo wangu kupumua kupitia pua langu. Midomo yangu ilikuwa imekauka na kufanya upenyu na ilichukua nguvu yote niliyokuwa nayo kupumua tu. Nilihisi kifo kikikaribia tena—pengine wakati huu kwa kweli ningekufa. Lakini wakati huo, Roho Mtakatifu alinitia nuru. Nilimfikiria Luka, mmoja wa wanafunzi wa Mungu, na uzoefu wake wa kuangikwa akiwa hai. Moyoni mwangu, nilipata tena nguvu yangu kwa hiari, na kuendelea kusema kitu kile kile tena na tena kujikumbusha: “Luka alikufa kwa kuangikwa akiwa hai. Mimi, pia, lazima niwe Luka, lazima niwe Luka, niwe Luka ... Mungu atawasafisha watu kabisa; lakini mimi ni mnyonge sana, siwezi kushuhudia kabisa—na sasa niko karibu kufa. Hata nikifa kweli, kwa hiari ninatii utaratibu na mipango ya Mungu, nataka kuwa mwaminifu kwa Mungu hadi kufa kama Luka.” Wakati ule ule maumivu yalipokuwa hayawezi kuvumilika na nilikuwa ukingoni mwa kifo, ghafla nilisikia polisi mmoja mwovu kisema kwamba ndugu kadhaa waliomwamini Mwenyezi Mungu walikuwa wamekamatwa. Moyoni mwangu, nilishtuka: Ndugu wengine kadhaa watateswa. Lazima watakuwa wagumu hasa kwa kaka. Moyo wangu ulijawa na wasiwasi. Niliendelea kuwaombea kwa ukimya, nikimwomba Mungu awalinde na kuwaruhusu wawe na ushuhuda wa ushindi mbele ya Shetani na kutowahi kumsaliti Mungu, kwani sikutaka ndugu wowote wengine kuteseka kama nilivyoteseka. Pengine niliguswa na Roho Mtakatifu; niliomba bila kukoma, na kadiri nilivyoomba zaidi ndivyo nilivyotiwa moyo zaidi. Nilisahau uchungu wangu bila kufahamu. Nilijua vizuri sana kwamba hii ilikuwa mipango ya hekima ya Mungu; Mungu alijali udhaifu wangu, na alikuwa akiniongoza kupitia wakati wangu wa uchungu zaidi. Usiku huo, sikujali tena jinsi polisi waovu walivyonitendea, na sikutia maanani hata kidogo maswali yao. Huku wakiona kilichokuwa kikitendeka, polisi waovu walitumia ngumi zao kuupiga uso wangu kwa ukatili, kisha wakapinda nywele kwa panja langu vidoleni vyao na kuzivuta kwa ghafla. Masikio yangu yalikuwa yamevimba kwa ajili ya kupindwa, uso wangu ulikuwa usiotambulika, pande za juu na chini za miguu yangu zilikuwa zimeachwa na majeraha, na kuchunuka waliponichapa na kipande kinene cha mbao, na vidole vyangu vya miguu, pia, vilikuwa vimeachwa vyeusi na samawati baada ya kupondwa na kipande cha mbao. Baada ya kuniangika juu kwa pingu kwa saa sita, wakati polisi waovu walifungua pingu, zilikuwa zimeondoa nyama kutoka kwa kidole changu gumba cha kushoto—kulisalia tu safu nyembamba kabla ya mfupa. Pingu pia zilikuwa zimeacha vifundo vyangu vikiwa vimefunikwa na lengelenge ya njano, na hakukuwa na njia ya kuirudisha. Wakati huo, polisi wa kike aliyeonekana mwenye madaraka makubwa aliingia. Alinitazama juu na chini, kisha akawaambia: “Hamwezi kumchapa huyu tena—yuko karibu kufa.”
Polisi walinifungia katika chumba kimoja hotelini. Mapazia yake yalikuwa yamefungwa kwa kubanwa usiku kucha na mchana kutwa. Mtu fulani alipewa jukumu la kulinda mlango, na hakuna kati ya watumishi wa huduma aliyeruhusiwa kuingia, wala hakuna aliyeruhusiwa kuona matukio ya wao kunitesa na kunishambulia kikatili kule ndani. Walichukua zamu kunihoji bila pumziko. Kwa siku na usiku tano, hawakuniruhusu kulala, hawakuniruhusu kukaa wala kuchuchumaa, wala hawakuniruhusu kula chakula changu hadi kushiba. Niliruhusiwa tu kusimama nikiegemea dhidi ya ukuta. Siku moja, afisa mmoja alikuja kunihoji. Huku akiona kwamba nilikuwa nikimpuuza, alishikwa na hasira na kunipiga teke lililonirusha chini ya meza. Kisha, alinivuta kutoka hapo na kunipiga ngumi, akisababisha damu kububujika kutoka kwa kona ya mdomo wangu. Ili kuficha ukatili wake, kwa haraka alifunga mlango kuzuia yeyote kuingia. Kisha alirarua kiasi kidogo cha karatasi ya shashi na kupanguza damu yangu, akisafisha damu kutoka usoni pangu kwa maji na kusafisha damu kutoka kwenye sakafu. Niliacha damu kiasi kwa sweta yangu nyeupe kwa makusudi. Niliporudi katika kituo cha kuzuia, hata hivyo, polisi waovu waliwaambia wafungwa wengine kwamba damu kwenye mavazi yangu ilitokana na wakati nilipokuwa nikithibitishwa katika hospitali ya wagonjwa wa akili, na kusema kwamba hapo ndipo nilipokuwa siku kadhaa zilizopita. Majeraha na damu mwilini mwangu yalikuwa yamesababishwa na wagonjwa, wao, polisi, hawakuwa wamenigusa.... Ukweli huu katili ulinionyesha ukatili, ujanja wenye kudhuru kwa siri, na unyama wa “polisi wa watu,” na nilihisi kutojiweza na huzuni ya wale wanaoanguka mikononi mwao. Wakati huo huo, nilipata ufahamu wa kina wa haki, utakatifu, uchangamfu, na uzuri wa Mungu, na kuhisi kwamba kila kitu kinachotoka kwa Mungu ni upendo, ulinzi, nuru, ugavi, faraja, na msaada. Kila wakati uchungu wangu ulipofika kiwango mbaya kabisa, Mungu daima angeendelea kunitia nuru na kuniongoza, Akiongeza imani na nguvu yangu, Akiniruhusu kuiga roho ya watakatifu ambao walikuwa wamekufa shahidi kwa ajili ya Mungu kotekote katika enzi, kunipa ujasiri wa kutetea ukweli. Wakati ambapo ukatili wa polisi waovu uliniacha karibu na kifo, Mungu aliniruhusu kusikia habari ya kukamatwa kwa ndugu, kutumia hili kunisisimua zaidi kuwaombea, ili kwamba nilisahau uchungu wangu na bila kujua kushinda vikwazo vya kifo. Kwa sababu ya utumbuizo wa Shetani mwovu, mkatili, niliona kwamba Mungu pekee ndiye ukweli, njia, na uhai, na kwamba Mungu pekee ndiye ishara ya mamlaka ya juu, ya haki, na ishara ambayo haiwezi kushindwa ama kuingiliwa na uovu na nguvu yoyote ya uhasama. Mungu pekee ndiye hutawala vitu vyote, na hupanga kila kitu, na Yeye hutumia nguvu Yake kuu na hekima kuongoza kila hatua yangu katika kushinda mizinga ya umati wa ibilisi, katika kushinda udhaifu wa mwili na vikwazo vya kifo, kuniruhusu kwa kunata kuokoka katika pango hili ovu. Nilipokuwa nikifikiri kuhusu upendo na wokovu wa Mungu, nilihisi kutiwa moyo sana, na nikaamua kupigana na Shetani hadi mwisho kabisa. Hata ningedhoofika gerezani, ningesimama imara katika ushuhuda wangu na kumridhisha Mungu.
Siku moja, polisi wengi waovu ambao sikuwa nimewahi kuwaona awali walikuja kuniangalia na kujadili kesi yangu. Bila kutaka, nilisikia bila kusudia mtaalamu—akisema: “Kwa mahojiano yote ambayo nimefanya, sijawahi kuwa mgumu kwa mtu yeyote kama huyo mwanamke mjinga. Nilimfanya atundikwe kwa pingu kwa saa nane (kwa kweli ilikuwa saa sita, lakini alitaka kujionyesha, akiogopa kwamba wasimamizi wake wangesema alikuwa bure) na bado hakukiri.” Nilisikia sauti ya kike ikisema, “Mbona ulimchapa mwanamke huyo vibaya hivyo? Wewe ni mkatili.” Ilitukia kwamba miongoni mwa kila mtu ambaye alikuwa amekamatwa, nilikuwa nimeteseka zaidi. Mbona nilikuwa nimeteseka sana hivyo? Je, nilikuwa mpotovu kuliko watu wengine? Je, kile nilichopitia kilikuwa adhabu ya Mungu kwangu? Pengine kulikuwa na upotovu mwingi sana ndani yangu, na tayari nilikuwa nimefika kiwango cha adhabu? Nikifikiri hili, singeweza kuzuia machozi yangu. Nilijua kwamba lazima nisilie. Singeacha Shetani aone machozi yangu—kama angeona, angeamini kwamba nilikuwa nimeshindwa. Ilhali sikuweza kudhibiti hisia ya huzuni moyoni mwangu, na machozi yalitiririka kupita udhibiti wangu. Katikati ya kukata tamaa kwangu, ningemwita tu Mungu: “Ee Mungu! Wakati huu, nahisi kusikitika sana. Naendelea kutaka kulia. Tafadhali nilinde, nizuie dhidi ya kuinamisha kichwa changu mbele ya Shetani—siwezi ruhusu aone machozi yangu. Najua kwamba hali niliyomo si sahihi. Natoa madai Kwako, na kulalamika. Na najua kwamba bila kujali kile Ufanyacho, ni bora zaidi—lakini kimo changu ni kidogo sana, tabia yangu ya uasi ni kubwa sana, na sina uwezo wa kukubali ukweli huu kwa furaha, wala sijui kile ninachopaswa kufanya kutoka katika hali hii mbaya. Ningependa Uniongoze, na kuniruhusu kutii utaratibu na mipango Yako, na kutokufahamu visivyo tena ama kulalamika kuhusu Wewe.” Nilipokuwa nikiomba, fungu la maneno ya Mungu yalinijia akilini: “Lazima pia unywe kutoka kwenye kikombe kikali nilichonywea Mimi (hili ndilo alilomwambia baada ya kufufuka), lazima utembee njia niliyotembea Mimi, lazima uyapoteze maisha yako kwa ajili Yangu” (Kutoka kwa “Namna Petro Alivyopata Kumjua Yesu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Machozi yangu yalikoma mara moja. Mateso ya Kristo yalikuwa yasiyoweza kufananishwa na yale ya kiumbe yeyote aliyeumbwa, wala hayakuweza kuvumilika na kiumbe aliyeumbwa—ilhali nilikuwa hapa nikihisi nimekosewa na nikilalamika kwa Mungu kwamba haikuwa haki baada ya kupitia taabu kidogo. Dhamiri na mantiki ilikuwa wapi katika hili? Nilifaa vipi kuitwa binadamu? Baada ya hiyo, nilifikiri kuhusu kile Mungu alisema: “Hata hivyo, upotovu ndani ya asili ya binadamu ni lazima uondolewe kupit majaribu. Katika hali yoyote usiyoipita, ni katika hizi hali ambamo ni lazima usafishwe—huu ni mpango wa Mungu. Mungu anakutengenezea mazingira, Akikulazimisha usafishwe hapo ili ujue upotovu wako mwenyewe” (Kutoka kwa “Namna ya Kumridhisha Mungu katikati ya Majaribu” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo). Nikitafakari maneno ya Mungu na kufikiri kujihusu, nilielewa kwamba kile kilichopangwa na Mungu kililenga upotovu na upungufu wangu—na kilikuwa hasa kile ambacho maisha yangu yalihitaji. Kwa sababu nilikuwa nimepofishwa sana na kutiwa sumu na serikali ya CCP, moyo wangu daima ulikuwa umejaa imani na tegemeo mintaarafu yake, na hata ingawa nilikuwa nimeona makosa yake kiasi, hiyo haikuwa imebadili maoni yangu kuihusu. Leo, Mungu alikuwa ameunda hali hii maalum kwangu, Akiniruhusu kutofautisha kati ya Mungu na Shetani, kuweza kujua ni nani huniokoa na ni nani hunipotosha, nani ambaye napaswa kuabudu na nani ambaye napaswa kulaani, na ni kwa sababu ya hili tu ndipo niliona mwanga wa ukweli, na kumtazama Mungu wa kweli, na kuja kujua tofauti kati ya mwanga na giza. Iwapo singepitia taabu ambayo ilikuwa nyingi na kali ya kutosha, maarifa yangu na maoni ya serikali ya CCP hayangekuwa yamebadilika—wala, moyoni mwangu, singeutekeleza kwa kweli, na kwa kweli kumgeukia Mungu. Taabu hii ilikuwa upendo wa Mungu kwangu, ilikuwa baraka Yake maalum kwangu. Baada ya kuelewa mapenzi ya Mungu, moyo wangu mara moja ulihisi dhahiri na mchangamfu. Suitafahamu yangu ya Mungu ilitoweka. Nilihisi kulikuwa na thamani kubwa na maana katika mimi kuweza kupitia taabu hiyo siku!
Baada ya kujaribu kila kitu walichoweza, polisi waovu hawakuwa wamepata chochote kutoka kwangu. Mwishowe, walisema kwa kusadiki sana: “Wakomunisti wametengenezwa kwa chuma, lakini wale wanaomwamini Mwenyezi Mungu wametengenezwa kwa almasi—wako katika kiwango cha juu zaidi kuliko wakomunisti katika kila hali.” Baada ya kusikia maneno haya, moyoni mwangu singeweza kujizuia kufurahia na kumsifu Mungu: Ee Mungu, nakushukuru na kukusifu! Kwa uweza na hekima Yako Umemshinda Shetani na kushinda maadui Wako. Wewe ni mamlaka ya juu zaidi, na naomba utukufu uwe Wako! Ni wakati huu tu ndio niliona: Je, Chama cha Kikomunisti kina maana gani? Na je, utawala wote wa siasa duniani una maana gani? Vitu vyote mbinguni na duniani huja chini ya utawala wa Mungu. Lazima visiwe na chaguo lingine sembuse Shetani mdogo, asiye na maana ibilisi ambaye ni utumbuizo tu.
Siku moja, polisi waovu walikuja kunihoji mara nyingine tena. Wakati huu, wote walionekana kuwa wa ajabu kidogo. Waliniangalia walipozungumza, lakini haikuonekana kama walikuwa wakinizungumzia. Walionekana kujadili kitu. Kama nyakati za awali, mahojiano haya yaliishia katika kushindwa. Baadaye, polisi waovu walinirudisha kwa seli. Njiani, nilisikia ghafla wakisema kwamba ilionekana kuwa ningeachiliwa siku ya kwanza ya mwezi ujao. Kwa kusikia hili, moyo wangu karibu ulipasuka kwa msisimko: Hili inamaanisha nitaondoka katika siku tatu! Hatimaye naweza kuondoka katika jahanamu hii ya shetani! Kwa kukandamiza furaha iliyokuwa moyoni mwangu, nilitarajia na kusubiri kila sekunde ilipokuwa ikipita. Siku tatu zilihisi zaidi kama miaka mitatu. Mwishowe, siku ya kwanza ya mwezi iliwadia! Siku hiyo, niliendelea kukodolea mlango macho, nikisubiri mtu aite jina langu. Asubuhi ilipita, na hakuna kilichofanyika, niliweka matumaini yangu yote katika kuondoka alasiri—lakini jioni ilipofika, bado hakuna kilichofanyika. Wakati ambapo ilikuwa wakati wa chakula cha jioni, sikuhisi kula. Moyoni mwangu, nilikuwa na hisia ya hasara; wakati huo, ilikuwa kana kwamba moyo wangu ulikuwa umeanguka kutoka mbinguni hadi jahanamu. “Mbona hali?” mlinzi aliuliza wafungwa wengine. “Hajala sana tangu aliporudi kutoka kwa mahojiano siku ile,” mfungwa mmoja alijibu. “Gusa panja lake; je, yeye ni mgonjwa?” mlinzi alisema. Mfungwa alikuja na kugusa panja langu. Alisema lilikuwa na joto sana, kwamba nilikuwa na homa. Kwa kweli nilikuwa na homa. Ugonjwa huo ulikuwa umekuja ghafla sana, na ulikuwa mkali sana. Wakati huo, nilianguka. Kwa kipindi cha saa mbili, homa ikawa mbaya na mbaya zaidi. Nililia! Wote, akiwemo mlinzi, walinitazama nikilia. Wote waliduwaza: Maoni yao kunihusu yalikuwa kama mtu ambaye hakushawishika kwa kivutio wala kuogopeshwa kwa vitisho, ambaye hakuwahi kutoa chozi hata moja kila wakati alipokabiliwa na mateso ya kuhuzunisha, ambaye alikuwa ameangikwa juu kwa pingu kwa saa sita bila kupiga kite. Ilhali, leo, bila mateso yoyote, nililia. Hawakujua machozi yangu yalitoka wapi—walifikiri tu kwamba lazima niwe mgonjwa sana. Kwa kweli, mimi na Mungu tu ndio tulijua sababu. Haya yote yalikuwa kwa sababu ya uasi na kutotii kwangu. Machozi haya yalitiririka kwa sababu nilihisi kukata tamaa wakati ambapo matarajio yangu yaliambulia patupu na matumaini yangu yalikuwa yamevunjika. Yalikuwa machozi ya uasi na lalamiko. Wakati huo, sikutaka tena kuweka azimio langu kumshuhudia Mungu. Hata sikuwa na ujasiri kujaribiwa hivi tena. Jioni hiyo, nililia machozi ya taabu, kwa sababu nilikuwa nimechoshwa na maisha gerezani, niliwadharau pepo hawa—na hata zaidi ya hilo, nilichukia kuwa mahali hapa pa pepo. Sikutaka kukaa sekunde nyingine hapo. Kadiri nilivyofikiri kuhusu hilo, ndivyo nilivyovunjika moya zaidi, na ndivyo nilivyohisi hisia kubwa ya taabu, ya huzuni, na upweke zaidi. Nilihisi kana kwamba nilikuwa mashua pweke juu ya bahari, moja ambayo ingemezwa na maji wakati wowote; zaidi ya hayo, nilihisi wale walionizunguka walikuwa wenye kudhuru kwa siri sana na wabaya sana kiasi kwamba wangetoa hasira yao kwangu wakati wowote. Singeweza kujizuia kulia kwa sauti: “Ee Mungu! Nakuomba uniokoe. Niko karibu kuanguka, ninaweza kukusaliti wakati wowote na mahali popote. Ningependa uushike moyo wangu na uniwezeshe kurudi mbele Yako tena, ningependa Unihurumie mara moja nyingine, na kuniruhusu nikubali utaratibu na mipango Yako. Ingawa siwezi kuelewa kile Unachofanya sasa, najua kwamba yote Unayofanya ni mema, na ningetaka Uniokoe mara nyingine, na kuruhusu moyo wangu ukugeukie.” Baada ya kuomba, niliacha kuhisi kuogopa, nilianza kutulia na kufikiri kujihusu, na wakati huo maneno ya Mungu ya hukumu na ufunuo yalinijia: “Unataka mwili ama ukweli? Unataka hukumu, ama faraja? Baada ya kupitia na kuiona kazi nyingi ya Mungu, na baada ya kuuona utakatifu na haki ya Mungu, unafaa kumfuata vipi? Unapaswa kutembea vipi katika njia hii? Utahitajika kuweka mapenzi ya Mungu katika matendo kivipi? Je, adabu na hukumu ya Mungu zimekuwa na athari yoyote kwako? Kama una maarifa ya adabu na hukumu ya Mungu itategemea jinsi unavyoishi kwa kudhihirisha, na kiwango gani unapenda Mungu! Kinywa chako kinasema unampenda Mungu, ilhali unachoishi kwa kudhihirisha ni tabia nzee, zilizo potovu; humchi Mungu, na zaidi ya yote huna dhamiri. Je, watu wa aina hii wanampenda Mungu? Je, watu wa aina hii ni waaminifu kwa Mungu? … Mtu kama huyu anaweza kuwa Petro? Wale walio kama Petro wana maarifa, lakini je, wanaishi kulingana nayo?” (Kutoka kwa “Matukio Aliyopitia Petro: Ufahamu Wake wa Adabu na Hukumu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Kila neno la Mungu la hukumu lilikuwa kama upanga ukatao kuwili likiugonga udhaifu wangu, likirundika lawama juu yangu: Ndiyo, kulikuwa na nyakati nyingi ambapo nilitoa viapo vya dhati mbele ya Mungu, nikisema kwamba ningetelekeza kila kitu na kustahimili kila taabu kwa ajili ya ukweli. Ilhali leo, wakati ambapo Mungu alitumia ukweli kuniomba jambo, wakati Alinihitaji kwa kweli kuteseka na kulipa gharama ili kumridhisha, sikuwa nimechagua ukweli ama uzima, lakini kwa upofu nilikuwa nimejawa na wasiwasi, dhiki na masumbuko kwa sababu ya maslahi na matazamio ya mwili. Sikuwa hata na imani hata kidogo kwa Mungu. Katika hili, ningewezaje kuridhisha mapenzi ya Mungu? Mungu alitaka kile nilichoishi kwa kudhihirisha kuzaa matunda. Hakutaka viapo vya madoido, vitupu. Ilhali mbele ya Mungu nilikuwa na maarifa lakini sikuwa na uhalisi wowote, na kuelekea kwa Mungu, sikuwa na uaminifu ama upendo wa kweli, sembuse kuwa na utiifu wowote; sikuishi kwa kudhihirisha chochote ila udanganyifu, uasi, na upinzani. Katika hili, je, si nilikuwa mtu ambaye alimsaliti Mungu? Je, sikuwa mtu aliyeuvunja moyo wa Mungu? Wakati huo, nilifikiri kuhusu wakati Bwana Yesu alipokamatwa na kupigwa misumari msalabani. Mmoja baada ya mwingine, wale ambao mara nyingi walikuwa wamefurahia neema Yake walimwacha. Moyoni mwangu, singeweza kujizuia kujawa na majuto. Nilichukia uasi wangu, nilichukia ukosefu wangu wa ubinadamu, nilitaka kwa mara nyingine kusimama, kutumia vitendo vya ukweli kufanya ahadi zangu kwa Mungu kuwa uhalisi. Hata kama ningedhoofika gerezani, singeuumiza tena moyo wa Mungu. Singesaliti tena gharama ya damu ambayo Mungu alikuwa amelipa kwangu. Niliacha kulia, na moyoni mwangu nilimwomba Mungu kwa kimya: Ee Mungu, ahsante kwa kunitia nuru na kuniongoza, kuniruhusu kuelewa mapenzi Yako. Naona kwamba kimo changu ni kidogo sana, na kwamba sina upendo ama utiifu hata kidogo Kwako. Ee Mungu, sasa hivi nataka kujitoa kikamilifu Kwako. Hata nikiishi maisha yangu yote gerezani, kamwe singemkubali Shetani. Nataka tu kutumia vitendo vyangu vya ukweli kukuridhisha.
Baada ya muda, kulikuwa na uvumi zaidi kwamba ningeachiliwa. Walisema kwamba ingekuwa siku chache tu. Kwa sababu ya masomo niliyofunzwa wakati uliopita, wakati huu nilikuwa razini na mtulivu kiasi. Ingawa nilihisi mwenye kusisimka sana, nilitaka kuomba na kutafuta mbele ya Mungu, kutokuwa tena na chaguo langu mwenyewe. Ningemwomba Mungu tu anilinde ili niweze kutii utaratibu na mipango Yake yote. Baada ya siku chache, uvumi mara nyingine ulikuwa bure. Zaidi ya hayo, nilimsikia mlinzi akisema kwamba hata kama ningekufa gerezani, hawangeniachilia, sababu ikiwa kwamba singewaambia anwani yangu ya nyumbani na jina—hivyo ningetiwa gerezani milele. Kusikia hili kulikuwa kugumu sana, lakini nilijua kwamba huu ulikuwa uchungu niliopaswa kupitia. Mungu alitaka niwe na ushuhuda huu Kwake, na nilikuwa tayari kumtii Mungu, na kutii mapenzi ya Mungu, na niliamini kwamba mambo na vitu vyote vimo mikononi mwa Mungu. Hii ilikuwa neema maalum ya Mungu na kuniinua. Awali, ingawa nilikuwa nimesema ningedhoofika gerezani, hiyo ilikuwa tu hamu yangu na tamaa zangu—sikuwa na uhalisi huu. Leo, nilikuwa tayari kuwa na ushuhuda huu kupitia kuishi kwangu kulingana na matendo na kumruhusu Mungu kupata faraja kwangu. Wakati nilijawa na chuki kwa ajili ya Shetani, na nikaamua kufanya mapigano na Shetani hadi mwishoni kabisa, kwa kweli kuwa na ushuhuda wa kweli ya kudhoofikia gerezani, niliona kudura na matendo ya muujiza ya Mungu. Mnamo Desemba 6, 2005, gari la gerezani lilinichukua kutoka kituo cha kuzuia na kuniacha kando ya barabara. Kutoka wakati huo kuendelea, maisha yangu ya miaka miwili gerezani yaliisha.
Baada ya kupitia majaribu haya mabaya, ingawa mwili wangu ulikuwa umevumilia taabu kiasi, nilikuwa nimepata mara mia moja—mara elfu moja—zaidi: sikuwa tu nimekuza umaizi na utofautishaji, na kweli kuona kwamba serikali ya CCP ni mfano halisi wa Shetani ibilisi, kundi la wauaji ambao wangewaua watu kufumba kufumbua, lakini pia nilikuja kuelewa kudura na maarifa ya Mungu, na vilevile haki na utakatifu Wake, nilikuwa nimekuja kufahamu nia nzuri za Mungu katika kuniokoa, na utunzaji Wake na ulinzi Wake kwangu, Akiniruhusu, katika ukatili wa Shetani, kumshinda Shetani hatua kwa hatua, na kusimama imara katika ushuhuda wangu. Kutoka siku hiyo kuendelea, nilitaka kutoa nafsi yangu yote kwa Mungu kikamilifu. Kwa uthabiti ningemfuata Mungu, kwamba ningeweza kupatwa na Yeye mapema.
kutoka kwa kutoka kwa Ushuhuda wa Washindi

Jumapili, 21 Oktoba 2018

Swahili Gospel Video Clip "Kuibuka na Kuanguka kwa Falme ya Kirumi"

Swahili Gospel Video Clip "Kuibuka na Kuanguka kwa Falme ya Kirumi"

Milki ya kale ya Kirumi iliinuka na ilianzishwa kwa ajili ya kuenea kwa Ukristo. Kipindi chake cha heri na furaha kubwa kilikaribishwa na kuanzisha Ukristo kama dini yake ya kitaifa. Na ikaharibiwa kutokana na mateso yake ya Wakristo…. Tazama dondoo hii ya filamu ya Kikristo ili kutambua sababu za kuibuka na kuanguka kwa Milki ya Kirumi.
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumamosi, 20 Oktoba 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Maneno ya Mungu Yameniamsha

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, sauti ya Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu | 22. Maneno ya Mungu Yameniamsha

Miao Xiao Mji wa Jinan, Mkoa wa Shandong
Katika siku zilizopita, nilikuwa daima nikifikiri kuwa Mungu aliposema “ni kibaraka na msaliti anayekikimbia kiti kikuu cheupe cha enzi” Alikuwa anaashiria wale wanaoikubali hatua hii ya kazi lakini wanaishia kurudi nyuma kwa sababu hawako radhi kustahimili mateso ya kuadibu na hukumu Yake. Kwa hivyo, wakati wowote nilipoona ndugu wakijiondoa katika njia hii kwa sababu yoyote ile, moyo wangu ungejawa na dharau kwao. Huyo, kibaraka na msaliti mwingine anatoroka kutoka kwa kiti kikuu cheupe cha enzi ambaye atapokea adhabu ya Mungu. Wakati uo huo, nilijihisi nikiwa nikitenda ifaavyo kwa kukubali hukumu ya Mungu na nilikuwa siko mbali na kukubali ukombozi wake Mungu.
Siku moja, nilipokuwa nikitenda ibada ya kiroho, niliona maneno yafuatayo ya Mungu kwenye maandiko “Kristo Hufanya Kazi ya Hukumu kwa Ukweli”: “… kwa maana asili ya kazi ya aina hii hasa ni kazi ya kuweka wazi ukweli, njia, na uhai wa Mungu kwa wale wote walio na imani ndani Mwake. Kazi hii ni kazi ya hukumu inayofanywa na Mungu. Usipouchukulia ukweli huu kuwa muhimu na kila mara kufikiria kuuepuka au kutafuta njia nyingine isipokuwa ukweli, basi Ninasema kuwa wewe ni mtenda dhambi mkubwa. Iwapo una imani kwa Mungu, lakini hutafuti ukweli au mapenzi ya Mungu, wala hupendi njia inayokuleta karibu na Mungu, basi Nakwambia kuwa wewe ni yule anayejaribu kuepuka hukumu, na kwamba wewe ni kibaraka na msaliti anayekikimbia kiti kikuu cheupe cha enzi. Mungu hatawasamehe waasi wowote wanaotoroka machoni Pake. Wanadamu wa aina hii watapokea adhabu kali zaidi. Wale wanaokuja mbele za Mungu ili wahukumiwe, na zaidi ya hayo wametakaswa, wataishi milele katika ufalme wa Mungu.” Baada ya kutafakari maneno haya, hatimaye nilielewa kwamba: Inatukia kwamba vibaraka na wasaliti wanaotoroka kutoka kiti kikuu cheupe cha enzi hayazungumzii wale wanaorudi nyuma katika njia hii tu. La maana zaidi, ni kwamba yanarejelea wale wanaomfuata Mungu lakini hawaudhamini ukweli huu, watu ambao daima wanaukwepa ukweli huu, wanaotafuta njia mpya kando na njia ya kweli, na wasio tayari kujikabidhi kwa kuadibu na hukumu ya Mungu na kutafuta kutakaswa na Mungu. Chini ya nuru na mwongozo wa Mungu, nilianza kutafakari juu ya tabia yangu mwenyewe: Sasa Mungu anaonyesha maneno Yake kumhukumu mwanadamu, na kutakasa vitu kutoka kwa mwanadamu visivyolingana na Yeye kupitia mateso na usafishaji. Lakini nikikabiliwa na kuadibu na hukumu, mateso na usafishaji wa Mungu, mimi kila mara hujaribu kutoroka, nikitumaini kwamba Mungu ataondoa hali hizi upesi. Je, huku sio kuepuka ukweli na kutafuta njia ya kuuhepa ukweli? Wakati watu au maswala yanayoletewa na Mungu hayaambatani na dhana zangu binafsi, ama ninapojipata katika hali mbaya, hata kama mawasiliano ya ndugu zangu yanaweza kutatua matatizo yangu, yatatue kutoelewa kwangu kumhusu Mungu na kunisaidia kurejesha uhusiano wa kawaida na Mungu, mimi bado hupinga na kukataa kusikiliza. Je, hivi sivyo, Mungu asemavyo, kutotafuta ukweli na kutopenda njia inayonileta karibu na Mungu? Ninaposhughulikiwa na kupogolewa kwa sababu ya njia ya uzembe ambayo mimi hufanya kazi yangu, mimi kila mara huwa natafuta visingizio ili kujieleza. Je, hiki sio kiini kinachokataa kuukubali ukweli? Mara nyingi mimi hujikubali katika maisha halisi. Hata wakati najua kwamba ni ukweli, mimi hukataa kuusaliti mwili wangu ili nitende ukweli. Je, huku sio kutokubali hukumu tu, bali pia ni kutotafuta kutakaswa?...Sasa kwa kuwa natafakari kuhusu hili, nalielewa hata kwa wazi zaidi: Wale ambao Mungu husema hukimbia kutoka kwa kiti kikuu cheupe cha enzi haiashirii waliotoka kanisani tu. La muhimu hata zaidi, inarejelea mioyo yetu kukataa kukubali ukweli na kutokubali kujikabidhi kwa hukumu ya Mungu. Ni sasa tu ambapo ninaanza kuhisi wasiwasi na hofu. Japo sijaliwacha kanisa, moyo wangu kila mara ulikuwa unajaribu kuepuka hukumu ya Mungu. Je, mimi siye hasa yule kibaraka na msaliti anayekikimbia kiti cha hukumu ya Mungu? Ilhali nilikuwa nimesadiki kwamba wale wanaoiacha kanisa pekee ndio vibaraka na wasaliti wanaokikimbia kiti cha enzi cha Mungu, huku nilikuwa karibu sana kupokea wokovu wa Mungu. Ninaona kwamba kuelewa kwangu kwa neno la Mungu kuliegemea upande mmoja sana na ulikuwa wenye kina kifupi, na kwamba ufahamu wangu wa kazi ya Mungu ulikuwa umepungukiwa sana. Sasa, wale wanaokubali kwa dhati kuadibu na hukumu ya Mungu na wale ambao tabia zao zimefikia mabadiliko pekee ndio watakaopokea wokovu wa Mungu. Badala yake, nilikuwa ninaishi katika fikira zangu mwenyewe, bila kuwa na njaa ya ukweli, bila kuyawajibikia maisha yangu mwenyewe na kutokuwa na hisia ya hatari au haraka hata kidogo. Nikiendelea hivi, je, sitakuwa hasa kiumbe wa adhabu ya Mungu hasa.
Kwa sababu ya kutoa nuru kwa maneno ya Mungu, nimeamka kutoka kwa dhana na mawazo yangu, nikigundua kwamba mimi si mtu ambaye yuko tayari kukubali kuadibu na hukumu ya Mungu. Kumenifanya pia nione ya kwamba niko katika ukingo wa hatari. Kutoka sasa kuendelea, nitaupa moyo wangu wote kwa Mungu, nijikabidhi kwa kuadibu na hukumu Yake, na nifanye kila niwezalo kuutafuta ukweli na mabadiliko katika tabia, ili hivi karibuni niweze kutakaswa na nifanywe mkamilifu na Mungu.
kutoka kwa Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Vitabu

Ijumaa, 19 Oktoba 2018

2018 Gospel Music "Mungu Akiwaongoza Waisraeli Kutoka Misri" (Swahili Subtitles)

2018 Gospel Music "Mungu Akiwaongoza Waisraeli Kutoka Misri" (Swahili Subtitles)

Ili kuwaongoza Waisraeli kutoka Misri, Mungu alituma mapigo kumi Misri, akatumia mamlaka Yake kwa kutenganisha bahari, na kuwakomboa Waisraeli kutoka kwa maisha yao ya utumwa—yote ambayo yalidhihirisha uwezo Wake mkuu, na kueleza upendo Wake mkubwa na hangaiko Lake kwa wale wateule.
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Alhamisi, 18 Oktoba 2018

Swahili Gospel Video Clip "Maangamizi ya Mungu ya Sodoma na Gomora"

Swahili Gospel Video Clip "Maangamizi ya Mungu ya Sodoma na Gomora"

Ikifurika na uovu na uzinzi, miji hii miwili mikubwa ya Sodoma na Gomora iliichokoza tabia ya Mungu. Mungu alinyesha moto wa jahanamu kutoka mbinguni, akiiteketeza hiyo miji na watu ndani yayo hadi kuwa majivu, na kuwafanya watoweke katikati ya hasira Yake…. Tazama dondoo ya filamu ya Kikristo Maangamizo ya Mungu ya Sodoma na Gomora ili kujua zaidi juu ya tabia ya ghadhabu, isiyokiukwa ya Mungu na onyo Lake kwa vizazi vijavyo.
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Tabia ya Mungu

Jumatano, 17 Oktoba 2018

Swahili Gospel Video Clip "Ahadi ya Mungu kwa Waisraeli"

Swahili Gospel Video Clip "Ahadi ya Mungu kwa Waisraeli"

Baada ya mamia ya miaka ya kuwekwa chini ya sheria, Waisraeli hatimaye walikabiliwa na hatari ya kuhukumiwa na kuuawa na sheria kwa sababu ya dhambi zao. Walimwita Mungu kwa haraka, ambaye aliwapa ahadi—ahadi ambayo ingezibadilisha kudura zao na kuweko. Hivyo ahadi hii ilikuwa nini hasa? Jibu limefichuliwa katika dondo hii ya filamu ya kustaajabisha ya Kikristo, Ahadi ya Mungu kwa Waisraeli.
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, wafuasi wa Kristo

Jumanne, 16 Oktoba 2018

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Kuijua Kazi ya Mungu Leo"

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Kuijua Kazi ya Mungu Leo"

Mwenyezi Mungu anasema, "Kwa upande mmoja, Mungu katika mwili katika siku za mwisho Anaondoa nafasi iliyochukuliwa na Mungu asiye yakini katika dhana za mwanadamu, ili taswira ya Mungu asiye yakini isiwepo kabisa katika moyo wa mwanadamu. Kwa kutumia maneno Yake halisi na kazi Yake halisi, Anazunguka katika nchi zote, na kazi Anayoifanya miongoni mwa wanadamu ni halisi kabisa na ya kawaida, kana kwamba mwanadamu anakuja kujua uhalisia wa Mungu na Mungu asiye yakini Anapoteza nafasi Yake moyoni mwake. Kwa upande mwingine, Mungu Anatumia maneno yaliyozungumzwa na mwili Wake ili kumfanya mwanadamu mkamilifu, na kukamilisha vitu vyote. Hii ndiyo kazi ambayo Mungu Ataikamilisha wakati wa siku za mwisho."
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Video.
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kazi ya Mungu

Jumapili, 14 Oktoba 2018

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (5) - Je, Hukumu ya Mungu katika Siku za Mwisho ni Adhabu au Wokovu?

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (5) - Je, Hukumu ya Mungu katika Siku za Mwisho ni Adhabu au Wokovu?

Baadhi ya watu husoma maneno ya Mungu na kuona kwamba kunayo mambo makali ambayo ni hukumu ya wanadamu, na shutuma na laana. Wanafikiria kwamba kama Mungu huhukumu na kulaani watu, nao pia hawatashutumiwa na kuadhibiwa? Inawezaje kusemekana kwamba aina hii ya hukumu ni ya kutakasa na kuokoa wanadamu? Maneno ya Mungu yanasema: "Kile ambacho Mungu hulaani ni uasi wa mwanadamu, na kile Anachohukumu ni dhambi za mwanadamu." "Ufichuzi mkali wa neno ni kwa kusudi la kukuongoza kwenye njia sahihi" (Neno Laonekana katika Mwili). Ni njia gani nzuri ya kufahamu kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho?
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Video.

Jumamosi, 13 Oktoba 2018

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (4) - Je, Kusamehewa kwa Dhambi Zetu Ndiko Kweli Tiketi kuelekea Ufalme wa Mbinguni?

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (4) - Je, Kusamehewa kwa Dhambi Zetu Ndiko Kweli Tiketi kuelekea Ufalme wa Mbinguni?

Watu wengi katika dini wanafikiria kuwa wamezikiri dhambi zao na kuzitubu baada ya kumsadiki Bwana, hivyo wamekombolewa, na wameokolewa kwa neema. Wakati Bwana atakapokuja, atawainua moja kwa moja hadi kwenye ufalme wa mbinguni, na haiwezekani Yeye kufanya kazi ya utakaso na wokovu. Je, mtazamo huu unalingana na uhalisi wa kazi ya Mungu? Inasemekana kwenye Biblia: "Utakatifu, bila huu hakuna mwanadamu atakayemwona Bwana" (Waebrania 12:14). Mungu anasema: "Umepitwa na hatua moja katika imani yako kwa Mungu: umekombolewa tu, lakini haujabadilishwa. Ili uipendeze nafsi ya Mungu, lazima Mungu Mwenyewe afanye kazi ya kukubadilisha na kukutakasa; ikiwa umekombolewa tu, hautakuwa na uwezo wa kufikia utakatifu. Kwa njia hii hautahitimu kushiriki katika baraka nzuri za Mungu" (Neno Laonekana katika Mwili).
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, mapenzi ya Mungu

Ijumaa, 12 Oktoba 2018

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (3) - Je, Hakuna Maneno au Kazi ya Mungu Nje ya Biblia?

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (3) - Je, Hakuna Maneno au Kazi ya Mungu Nje ya Biblia?

Watu wengi katika ulimwengu wa kidini wanasadiki kwamba maneno yote ya Mungu yako ndani ya Biblia, na chochote kilicho nje ya Biblia hakina kazi Yake na maneno. Hawatafuti nje ya Biblia matamko Yake katika kurudi Kwake. Je, wataweza kukaribisha kurudi kwa Bwana kama wataendelea kushikilia wazo hili? Je, Mungu angeweza kuzuiliwa tu kwa kuongea maneno yaliyo ndani ya Biblia? Biblia inasema: "Na pia kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu alifanya, ambayo, yote yakiandikwa, ninafikiri kwamba hata dunia yenyewe haingetosha vitabu hivyo ambavyo vitaandikwa" (Yohana 21:25). Mungu anasema: "Yote yaliyoandikwa katika Biblia ni machache na hayawezi kuwakilisha kazi yote ya Mungu" (Neno Laonekana katika Mwili).
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Video.
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, maneno ya Mungu

Alhamisi, 11 Oktoba 2018

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (2) - Tunawezaje Kuwa na Uhakika kuwa Bwana Yesu Tayari Amerudi?

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (2) - Tunawezaje Kuwa na Uhakika kuwa Bwana Yesu Tayari Amerudi?

Tangu makanisa yalipoanza kukumbwa na ukiwa, ndugu wengi katika Bwana wamehisi kwa uwazi ukosefu wa kazi ya Roho Mtakatifu na uwepo wa Bwana, na wote wanatamani kurudi kwa Bwana. Lakini wakati tunaposikia habari ya kwamba Bwana Yesu tayari amerudi, tunawezaje kuwa na uhakika wa hili?
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Video.
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kazi ya Mungu

Jumatano, 10 Oktoba 2018

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (1) - Je, Ni Vipi Unabii wa Kurudi kwa Bwana Yesu Unatimia?

Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (1) - Je, Ni Vipi Unabii wa Kurudi kwa Bwana Yesu Unatimia?

Watu wengi katika ulimwengu wa kidini hufuata unabii unaosema kwamba Bwana atashuka akiwa juu ya wingu na wanamsubiria Yeye kuja kwa njia hiyo kisha kuwanyakua hadi kwenye ufalme wa mbinguni, lakini wanapuuza unabii mbalimbali wa Bwana kuhusu kuja kwa siri: "Tazama, mimi nakuja kama mwizi" (Ufunuo 16:15). "Na kukawa na kelele saa sita ya usiku, Tazama, anakuja bwana arusi; ondokeni nje ili kumkaribisha" (Mathayo 25:6). Hivyo unabii huu mbalimbali wa kurudi kwa Bwana unatimizwa vipi? Na tunafaa kuwa vipi wanawali wenye hekima ambao wanakaribisha kurudi kwa Bwana?
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, unabii wa Biblia

Jumanne, 9 Oktoba 2018

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Mungu Ndiye Bwana wa Viumbe Vyote

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki,

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Mungu Ndiye Bwana wa Viumbe Vyote

Hatua moja ya kazi ya enzi mbili za awali ilifanyika Israeli; nyingine ilifanyika Yudea. Kuzungumza kwa jumla, hakuna hatua ya kazi hii iliyoondoka Israeli; zilikuwa ni hatua za kazi zilizofanywa miongoni mwa wateule wa mwanzo. Hivyo, kwa mtazamo wa Waisraeli, Yehova Mungu ni Mungu wa Waisraeli pekee. Kwa sababu ya kazi ya Yesu huko Yudea, na kwa sababu ya kukamilisha Kwake kazi ya kusulubiwa, kwa mtazamo wa Wayahudi, Yesu ni Mkombozi wa watu wa Kiyahudi. Yeye ni Mfalme wa Wayahudi pekee, sio wa watu wengine wowote; Yeye si Bwana anayewakomboa Waingereza, wala Bwana anayewakomboa Wamarekani, lakini Yeye ni Bwana anayewakomboa Waisraeli, na katika Israeli ni Wayahudi ndio Anaowakomboa. Kwa kweli, Mungu ni Bwana wa mambo yote. Yeye ndiye Mungu wa viumbe vyote. Yeye si Mungu wa Waisraeli pekee, na Yeye si Mungu wa Wayahudi pekee; Yeye ni Mungu wa viumbe vyote. Hatua mbili za awali za kazi Yake zilifanyika Israeli, na kwa njia hii, dhana zingine zimejitokeza ndani ya watu. Watu wanafikiri kuwa Yehova alikuwa akifanya kazi Israeli na Yesu Mwenyewe alitekeleza kazi Yake Yudea—zaidi ya hayo, ilikuwa kupitia kupata mwili ambapo Alikuwa akifanya kazi Yudea—na kwa vyovyote, kazi hii haikuenea zaidi ya Israeli. Hakuwa akifanya kazi na Wamisri; Hakuwa akifanya kazi na Wahindi; Alikuwa tu akifanya kazi na Waisraeli. Watu basi wanaunda dhana mbalimbali; aidha, wanapanga kazi ya Mungu ndani ya eneo fulani. Wanasema kwamba wakati Mungu anafanya kazi, ni lazima ifanywe miongoni mwa wateule na ndani ya Israeli; mbali na Waisraeli, Mungu hana mpokeaji mwingine wa kazi Yake, wala Hana eneo lingine la kazi Yake; ni wakali hasa katika “kumfundisha nidhamu” Mungu mwenye mwili, kutomruhusu kuenda zaidi ya eneo la Israeli. Je, hizi zote si dhana za binadamu? Mungu aliunda mbingu na dunia yote na vitu vyote, na kuumba viumbe vyote; Angewezaje kuzuia kazi Yake ndani ya Israeli peke yake? Katika hali hiyo, kungekuwa na haja gani ya Yeye kuumba viumbe Vyake vyote? Aliiumba dunia nzima; Ametekeleza mpango Wake wa usimamizi wa miaka elfu sita sio tu ndani ya Israeli lakini pia na kila mtu ulimwenguni. Bila kujali kama anaishi Uchina, Amerika, Uingereza ama Urusi, kila mtu ni wa ukoo wa Adamu; wote wameumbwa na Mungu. Hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuondoka katika mawanda ya viumbe wa Mungu, na hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuepuka utambulisho wa “ukoo wa Adamu.” Wote ni viumbe wa Mungu, na wote ni wa ukoo wa Adamu; pia ni wazawa wapotovu wa Adamu na Hawa. Sio tu Waisraeli ambao ni viumbe wa Mungu, lakini ni watu wote; hata hivyo, wengine miongoni mwa viumbe wamelaaniwa, na wengine wamebarikiwa. Kuna mambo mengi ya kupendeza kuwahusu Waisraeli; Mungu awali alikuwa akifanya kazi nao kwa sababu walikuwa watu wapotovu kwa kiasi kidogo zaidi. Wachina ni dhaifu wakilinganishwa nao, na hawawezi hata kutumaini kulingana nao; hivyo, Mungu awali alifanya kazi miongoni mwa watu wa Israeli, na hatua ya pili ya kazi Yake ilifanywa tu Yudea. Kwa sababu hii, watu huunda dhana nyingi na kanuni nyingi. Kwa kweli, iwapo Angetenda kulingana na dhana za binadamu, Mungu angekuwa tu Mungu wa Waisraeli; kwa njia hii Asingeweza kupanua kazi Yake katika mataifa yasiyo ya Kiyahudi, kwa sababu Angekuwa tu Mungu wa Waisraeli badala ya Mungu wa viumbe vyote. Unabii ulisema kuwa jina la Yehova lingekuwa kubwa katika mataifa yasiyo ya Kiyahudi na kuwa jina la Yehova lingeenezwa kwa mataifa yasiyo ya Kiyahudi—mbona ulisema hivi? Iwapo Mungu angekuwa Mungu wa Waisraeli tu, basi Angefanya kazi tu Israeli. Zaidi ya hayo, Asingepanua kazi hii, na Asingefanya huu unabii. Kwa sababu Alifanya huu unabii, Angehitaji kuipanua kazi Yake hadi mataifa yasiyo ya Kiyahudi na hadi kila taifa na mahali. Kwa sababu Alisema hili, basi Angefanya hivyo. Huu ndio mpango Wake, kwani Yeye ndiye Bwana aliyeumba mbingu na dunia na vitu vyote, na Mungu wa viumbe vyote. Bila kujali iwapo Anafanya kazi na Waisraeli ama katika Yudea nzima, kazi Anayoifanya ni kazi ya ulimwengu mzima na kazi ya binadamu wote. Kazi Anayoifanya leo katika taifa la joka kubwa jekundu—katika taifa lisilo la Kiyahudi—bado ni kazi ya binadamu wote. Israeli inaweza kuwa kituo cha kazi Yake duniani; vivyo hivyo, Uchina pia inaweza kuwa kituo cha kazi Yake miongoni mwa mataifa yasiyo ya Kiyahudi. Je, sasa Hajatimiza unabii kwamba “jina la Yehova litakuwa kubwa katika mataifa yasiyo ya Kiyahudi”? Hatua ya kwanza ya kazi Yake miongoni mwa mataifa yasiyo ya Kiyahudi inahusu kazi hii Anayoifanya katika taifa la joka kuu jekundu. Kwa Mungu mwenye mwili kufanya kazi katika nchi hii na kufanya kazi miongoni mwa hawa watu waliolaaniwa hasa inaenda kinyume na dhana za binadamu; hawa watu ni wa chini zaidi na wasio na thamani yoyote. Hawa wote ni watu ambao Yehova alikuwa amewaacha mwanzoni. Watu wanaweza kuachwa na watu wengine, lakini wakiachwa na Mungu, hawa watu hawatakuwa na hadhi, na watakuwa na thamani ya kiwango cha chini zaidi. Kama sehemu ya viumbe, kumilikiwa na Shetani ama kuachwa na watu wengine yote mawili ni mambo machungu, lakini sehemu ya viumbe ikiachwa na Bwana wa viumbe, hii inaashiria kwamba hadhi yake iko katika kiwango cha chini kabisa. Wazawa wa Moabu walilaaniwa, na walizaliwa ndani ya nchi hii isiyo na maendeleo; bila shaka, wazawa wa Moabu ni watu walio na hadhi ya chini zaidi chini ya ushawishi wa giza. Kwa sababu hawa watu walimiliki hadhi ya chini zaidi zamani, kazi inayofanywa miongoni mwao inaweza kabisa kuzivunja dhana za binadamu, na pia ni kazi yenye faida kubwa zaidi kwa mpango Wake mzima wa usimamizi wa miaka elfu sita. Ili Afanye kazi miongoni mwa watu hawa ni kitendo kinachoweza zaidi kuzivunja dhana za binadamu; Akiwa na hili Anazindua enzi; na hili Anavunja dhana zote za binadamu; Akiwa na hili Anatamatisha kazi ya Enzi nzima ya Neema. Kazi Yake ya awali ilifanywa Yudea, ndani ya eneo la Israeli; katika mataifa yasiyo ya Kiyahudi Hakufanya kazi yoyote ya uzinduzi wa enzi hata kidogo. Hatua ya mwisho ya kazi Yake haifanywi tu miongoni mwa watu wa mataifa yasiyo ya Kiyahudi; hata zaidi ya hayo, inafanywa miongoni mwa watu waliolaaniwa. Jambo hili moja ndio ushahidi unaoweza zaidi kumwaibisha Shetani; hivyo, Mungu “anakuwa” Mungu wa viumbe vyote ulimwenguni na kuwa Bwana wa vitu vyote, Anayeabudiwa na kila kiumbe mwenye uhai.

      Kwa sasa bado kuna watu wengine wasioelewa ni aina gani ya kazi mpya ambayo Mungu amezindua. Mungu amefanya mwanzo mpya katika mataifa yasiyo ya Kiyahudi na Ameanza enzi nyingine na kuzindua kazi nyingine, na Anafanya kazi miongoni mwa ukoo wa Moabu. Je, hii si kazi Yake mpya kabisa? Hakuna yeyote katika enzi zote aliyeipitia kazi hii, wala hakuna aliyeisikia, sembuse kuithamini. Hekima ya Mungu, ajabu ya Mungu, kutoeleweka kwa Mungu, ukubwa wa Mungu, utakatifu wa Mungu vinategemea hatua hii ya kazi katika siku za mwisho, ili kuibuka wazi. Je, hii si kazi mpya inayovunja dhana za binadamu? Bado kuna wale wanaofikiria hivi: “Kwa sababu Mungu alimlaani Moabu na kusema kuwa Angewaacha wazawa wa Moabu, Angeweza kuwaokoaje sasa?” Hao ni wale watu kutoka mataifa yasiyo ya Kiyahudi waliolaaniwa na kulazimishwa nje ya Israeli; Waisraeli waliwaita “mbwa wasio wa Kiyahudi.” Kwa mtazamo wa kila mtu, wao sio mbwa wasio wa Kiyahudi pekee, lakini mbaya hata zaidi, ni wana wa maangamizi; kwa maneno mengine, wao si wateule wa Mungu. Ingawa awali walikuwa wamezaliwa ndani ya eneo la Israeli, wao siyo sehemu ya watu wa Israeli; wao pia walifukuzwa kwenda kwa mataifa yasiyo ya Kiyahudi. Wao ndio watu wa chini zaidi. Ni kwa sababu hasa wao ni watu wa chini zaidi miongoni mwa binadamu ndio Mungu anatekeleza kazi Yake ya kuzindua enzi mpya miongoni mwao. Kwa sababu wao ni wawakilishi wa binadamu wapotovu na kazi ya Mungu haikosi uchaguzi ama madhumuni, kazi Anayoifanya miongoni mwa watu hawa leo pia ni kazi inayofanywa miongoni mwa viumbe. Nuhu alikuwa sehemu ya viumbe, kama walivyo wazawa wake. Yeyote duniani aliye na mwili na damu ni sehemu ya viumbe. Kazi ya Mungu imeelekezwa kwa viumbe wote; haitekelezwi kulingana na kama mtu amelaaniwa baada ya kuumbwa. Kazi Yake ya usimamizi imeelekezwa kwa viumbe wote, sio wale wateule wasiolaaniwa. Kwa sababu Mungu anataka kutekeleza kazi Yake miongoni mwa viumbe Vyake, kwa hakika Ataifanya hadi kukamilika kwa mafanikio; Atafanya kazi miongoni mwa hao watu walio na manufaa kwa kazi Yake. Kwa hivyo, Anavunja mikataba yote ya kufanya kazi miongoni mwa watu; Kwake, maneno “kulaaniwa,” “kuadibu” na “kubarikiwa” hayana maana! Wayahudi ni wazuri hasa, na wateule wa Israeli sio wabaya pia; ni watu wenye ubora mzuri wa tabia na ubinadamu mzuri. Awali Yehova alizindua kazi Yake miongoni mwao na Akafanya kazi Yake ya awali, lakini ingekuwa bila maana kama Angewatumia kama wapokeaji wa kazi Yake ya ushindi sasa. Ingawa wao pia ni sehemu ya viumbe na wana vipengele vingi vyema, ingekuwa bila maana kutekeleza hatua hii ya kazi miongoni mwao. Asingeweza kumshinda yeyote, wala Asingeweza kushawishi viumbe wote. Huu ndio umuhimu wa uhamisho wa kazi Yake kwa watu hawa wa taifa la joka kubwa jekundu. Maana ya ndani zaidi hapa ni ya uzinduzi Wake wa enzi, ya kuvunja Kwake kwa kanuni zote na dhana zote za mwanadamu na pia kwa kumaliza Kwake kazi ya Enzi nzima ya Neema. Kama kazi Yake ya sasa ingefanywa miongoni mwa Waisraeli, ikifika wakati ambao mpango Wake wa usimamizi wa miaka elfu sita kukamilika, kila mtu angeamini kuwa Mungu ni Mungu tu wa Waisraeli, kuwa Waisraeli tu ndio wateule wa Mungu, kuwa Waisraeli tu ndio wanaostahili kurithi baraka na ahadi za Mungu. Katika siku za mwisho, Mungu anapata mwili katika taifa lisilo la Kiyahudi la joka kubwa jekundu; Ametimiza kazi ya Mungu kama Mungu wa viumbe wote; Amekamilisha kazi Yake yote ya usimamizi, na Atamaliza sehemu kuu ya kazi Yake kwa taifa la joka kubwa jekundu. Kiini cha hatua hizi tatu za kazi ni wokovu wa mwanadamu—ambao ni, kufanya viumbe wote vimwabudu Bwana wa viumbe. Hivyo basi, kila hatua ya kazi hii ni muhimu sana; Mungu hatafanya chochote kisicho na maana ama thamani. Kwa upande mmoja, hatua hii ya kazi inajumuisha kuzindua enzi na kukamilisha enzi mbili za awali; kwa upande mwingine inajumuisha kuvunja dhana zote za mwanadamu na njia ya zamani ya imani ya mwanadamu na maarifa. Kazi ya enzi mbili za awali ilifanywa kulingana na dhana tofauti za binadamu; hatua hii, hata hivyo, inafuta kabisa dhana za binadamu, na hivyo kuwashinda binadamu kikamilifu. Kwa kutumia ushindi wa ukoo wa Moabu na kutumia kazi iliyotekelezwa miongoni mwa ukoo wa Moabu, Mungu atawashinda binadamu wote katika ulimwengu mzima. Huu ndio umuhimu wa kina zaidi wa hatua hii ya kazi Yake, na ndicho kipengele cha thamani ya hatua hii ya kazi Yake. Hata kama sasa unajua kuwa hadhi yako ni ya chini na kuwa una thamani ya chini, bado utahisi kwamba umekutana na jambo linalofurahisha sana: Umerithi baraka kubwa, ukapata ahadi kubwa, na unaweza kamilisha hii kazi kubwa ya Mungu, na unaweza kuuona uso wa kweli wa Mungu, kujua tabia Yake ya asili, na kufanya mapenzi ya Mungu. Hatua mbili za awali za kazi ya Mungu zilifanywa Israeli. Iwapo hatua hii ya kazi Yake katika siku za mwisho bado ingefanywa miongoni mwa Waisraeli, viumbe wote havingeamini kwamba Waisraeli tu ndio waliokuwa wateule, lakini pia mpango wa usimamizi wa Mungu wote haungefikia athari iliyotaka. Wakati ambapo hatua hizi mbili za kazi Yake zilifanywa Israeli, hakuna kazi yoyote mpya iliyokuwa imefanywa na hakuna kazi yoyote ya Mungu ya kuzindua enzi ilikuwa imewahi kufanywa katika mataifa yasiyo ya Kiyahudi. Hatua hii ya kazi ya kuzindua enzi inafanywa kwanza katika mataifa yasiyo ya Kiyahudi, na zaidi ya hayo, inafanywa kwanza miongoni mwa ukoo wa Moabu; hii imezindua enzi mpya. Mungu amevunja maarifa yoyote yaliyo ndani ya dhana za binadamu na hajaruhusu yoyote yaendelee kuwa hai. Katika kazi Yake ya kushinda Amevunja dhana za binadamu, hiyo njia ya zamani, ya maarifa ya binadamu, Anaruhusu watu waone kuwa kwa Mungu hakuna kanuni, kwamba hakuna kitu kizee kumhusu Mungu, kwamba kazi Anayoifanya ni ya uhuru kabisa, ni huru kabisa, kwamba Yeye yuko sahihi katika chochote Anachofanya. Ni lazima utii kikamilifu kazi yoyote Anayoifanya miongoni mwa viumbe. Kazi yoyote Anayoifanya ni ya maana na inafanywa kulingana na mtazamo Wake na maarifa Yake na sio kulingana na chaguo za watu na dhana za watu. Anafanya yale mambo yaliyo na manufaa kwa kazi Yake; kama kitu hakina manufaa kwa kazi Yake, Hatakifanya, hata kiwe kizuri vipi! Anafanya kazi na kuchagua mpokeaji na eneo la kazi Yake kulingana na maana na madhumuni ya kazi Yake. Hafuati kanuni za zamani, wala Hafuati fomula nzee; badala yake, Anapanga kazi Yake kulingana na umuhimu wa kazi; mwishowe, Anataka kufikia matokeo yake ya kweli na madhumuni yanayotarajiwa. Iwapo huelewi mambo haya sasa, kazi hii haitatimiza matokeo yoyote kwako.
Sikiliza zaidi: Umeme wa Mashariki VITABU