Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Alhamisi, 31 Januari 2019

Swahili Christian Skit "Mipaka ya Meya wa Kijiji" | Why Is There No Religious Freedom in China?

Swahili Christian Skit "Mipaka ya Meya wa Kijiji" | Why Is There No Religious Freedom in China?

Mchezo mfupi Mipaka ya Meya wa Kijiji inaeleza hadithi ya kweli ya mume na mke Wakristo ambao wanalazimishwa kutoroka kwa sababu ya mateso ya serilaki ya CCP. Mkristo Liu Ming'en anahukumiwa na CCP miaka saba gerezani kwa kuamini katika Mungu. Hata baada ya kuachiliwa kutoka gerezani, anabakia kuwa wakulengwa na uchunguzi mkali wa CCP. Meya wa kijiji anatumia mfumo wa wajibu wa kaya-tano , kamera za usalama, ziara za nyumba, na njia nyingine kumzuia Liu Ming'en na mkewe kuamini katika Mungu, lakini hakuna inayoleta na matokeo yanayotakiwa. Wakati huu, meya anapokea taarifa za kipaumbele kutoka Kamati Kuu ya Chama, baada ya hapo anajaribu kutafuta njia za kumlazimisha Liu Ming'en na mkewe kuweka saini barua ya kuahidi kuacha kuamini katika Mungu. Baada ya hila yake kushindwa, polisi tena wanakuja kuwakamata waumini hawa wawili. Kuepuka kukamatwa na kuendelea kumfuata Mungu na kuamini katika Mungu, Liu Ming'en na mkewe wanalazimishwa kutoroka nyumbani kwao.
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumatano, 30 Januari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu | “Wale Ambao Hawalingani na Kristo Hakika Ni Wapinzani wa Mungu”

Maneno ya Roho Mtakatifu | “Wale Ambao Hawalingani na Kristo Hakika Ni Wapinzani wa Mungu”

Mwenyezi Mungu anasema, “Hata ingawa fikira za mwanadamu hakika haziwezi kupuuzwa, haikubaliki hata zaidi kwa mwanadamu kubadilisha kiini cha Kristo. Nyinyi mnamchukua Kristo kama asiyekufa au mhenga, lakini hakuna yeyote anayemchukua Kristo kama binadamu wa nyama na mwili aliye na kiini kitakatifu. Kwa hivyo, wengi wa wale ambao wanatamani usiku na mchana kumwona Mungu ni hasa maadui wa Mungu na hawapatani na Mungu. Je, haya si makosa kwa upande wa mwanadamu? Hata sasa bado mnadhani kwamba imani yenu na uaminifu umetosha kuwafanya mstahili kuona uso wa Kristo, lakini Mimi Nawasihi kujihami kwa mambo zaidi yaliyo na umuhimu! Hii ni kwa maana katika wakati uliopita, uliopo na ujao, wengi wa wale ambao hupatana na Kristo wameanguka au wataanguka; wao wote wamechukua jukumu la Mafarisayo. Sababu yenu ya kushindwa ni nini? Ni kwa sababu hasa katika fikra zenu kuna Mungu mkubwa, Atamanikaye. Lakini ukweli si kama vile mwanadamu atakavyo. Kristo si mkubwa tu, bali Yeye ni mdogo hasa; Yeye si mtu tu, bali ni mtu wa kawaida; Hana uwezo wa kupaa mbinguni tu, bali hana pia uhuru wa kuzunguka ardhini. Na kwa hivyo, watu humtendea kama mtu wa kawaida; wao hufanya wanavyopenda wanapokuwa pamoja naye, na kusema maneno kiholela Kwake, wakati huu wote wakingojea kurudi kwa "Kristo wa kweli." Mnamchukua Kristo aliyekuja tayari kama mtu wa kawaida na neno Lake kama lile la mtu wa kawaida. Kwa hivyo, hamjapata chochote kutoka kwa Kristo na badala yake mmeonyesha ubaya wenu kwenye mwangaza kabisa.”

Jumanne, 29 Januari 2019

Neno la Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee I Mamlaka ya Mungu (I)” Uendelezo wa Sehemu ya Pili

Neno la Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee I Mamlaka ya Mungu (I)” Uendelezo wa Sehemu ya Pili

Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”. Maudhui ya video hii: Kwenye Siku ya Nne, Misimu, Siku, na Miaka ya Mwanadamu Iliumbika Huku Mungu Akionyesha Mamlaka Yake kwa Mara Nyingine Tena Kwenye Siku ya Tano, Maisha ya Maumbo Tofauti na Pana Yaonyesha Mamlaka ya Muumba kwa Njia Tofauti Kwenye Siku ya Sita, Muumba Aongea, na Kila Aina ya Kiumbe Hai Akilini Mwake Chajitokeza, Kimoja Baada ya Kingine Katika Mamlaka ya Muumba, Viumbe Vyote ni Timilifu Hakuna Kiumbe Chochote Kati ya Vile Vilivyoumbwa na Vile Ambavyo Havikuumbwa Kinaweza Kubadilisha Utambulisho wa Muumba
Sikiliza zaidi: Kanisa la Mwenyezi Mungu video

Jumatatu, 28 Januari 2019

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Pili

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Pili

Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Pili Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”. Maudhui ya video hii: Awamu Sita katika Maisha ya Binadamu Kuzaliwa: Awamu ya Kwanza 1. Maisha Mapya Yanazaliwa Kulingana na Mipango ya Muumba 2. Kwa Nini Binadamu Tofauti Wanazaliwa Katika Hali Tofauti Kukua: Awamu ya Pili 1. Hali Ambazo Mtu Hukulia Ndani Zimepangwa na Muumba 2. Hali Mbalimbali Ambazo Watu Hukulia Ndani Husababisha Wajibu Tofauti
Mwenyezi Mungu alisema, Tangu unapoingia katika dunia hii ukilia, unaanza kutekeleza wajibu wako. Unachukua jukumu lako katika mpango wa Mungu na katika utaratibu wa Mungu. Unaanza safari ya maisha. Licha ya asili yako na licha ya safari iliyoko mbele yako, hakuna kitakachoepuka mpango na utaratibu ambao mbingu imeweka, na hakuna aliye na udhibiti wa hatima yake, kwa maana Anayetawala juu ya kila kitu ndiye tu Aliye na uwezo wa kazi hiyo. Tangu siku aliyoumbwa binadamu, Mungu amekuwa thabiti katika kazi Yake, kusimamia ulimwengu huu na kuelekeza mabadiliko na harakati ya mambo yote. Kama kila kiumbe, mwanadamu bila kujua anapata lishe ya utamu na mvua na umande kutoka kwa Mungu. Kama vitu vyote, mwanadamu bila kujua anaishi chini ya mpango wa mkono wa Mungu. Moyo na roho ya mwanadamu vimeshikwa katika mkono wa Mungu, na maisha yote ya mwanadamu yanatunzwa machoni mwa Mungu. Haijalishi kama unayaamini mambo haya au la, vitu vyote, vilivyo hai au vilivyokufa, vitahamishwa, vitabadilika, kufanywa vipya, na kutoweka kulingana na mawazo ya Mungu. Hivi ndivyo Mungu anavyotawala juu ya kila kitu.
kutoka kwa Mungu Ndiye Chanzo cha Uhai wa Mwanadamu

Jumapili, 27 Januari 2019

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Kumjua Mungu Ndiyo Njia ya Kumcha Mungu na Kuepuka Maovu”

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Kumjua Mungu Ndiyo Njia ya Kumcha Mungu na Kuepuka Maovu”

Mwenyezi Mungu anasema, “‘Kumwogopa Mungu na kuepuka maovu’ na kumjua Mungu ni uhusiano usiogawanyishwa na uliounganishwa kwa nyuzi zisizohesabika, na uhusiano kati yao ni dhahiri. Iwapo mtu anataka kupata uwezo wa kuepuka maovu, lazima kwanza amche Mungu kwa kweli; iwapo mtu anataka kupata uwezo wa kumcha Mungu kwa kweli, lazima awe na maarifa ya kweli kuhusu Mungu; Iwapo mtu anataka kupata maarifa ya Mungu, lazima kwanza ayapitie maneno ya Mungu, aingie katika ukweli wa maneno ya Mungu, apitie kuadibu na nidhamu ya Mungu, kuadibu Kwake na hukumu; iwapo mtu anataka kupitia maneno ya Mungu, lazima aje ana kwa ana na maneno ya Mungu, aje ana kwa ana na Mungu, na kumwomba Mungu Ampe fursa ya kupitia maneno ya Mungu katika hali ya aina yote ya mazingira inayowahusisha watu, matukio na vitu; iwapo mtu anataka kuja ana kwa ana na Mungu na maneno ya Mungu, lazima kwanza amiliki moyo wa kweli na mwaminifu, awe tayari kuukubali ukweli, kukubali kupitia mateso, uamuzi na ujasiri wa kuepuka uovu, na azimio la kuwa kiumbe halisi…Kwa njia hii, kuendelea mbele hatua kwa hatua, utamkaribia Mungu zaidi, moyo wako utakuwa safi zaidi, na maisha yako na thamani ya kuwa hai, pamoja na maarifa yako kumhusu Mungu, yatakuwa ya maana zaidi na yatakuwa hata ya kupevuka zaidi.”

Jumamosi, 26 Januari 2019

Je, Unauelewa Upendo wa Mungu kwa Binadamu?

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 56. Je, Unauelewa Upendo wa Mungu kwa Binadamu?

Upendo wa Mungu, ambaye alikuwa mwili, unajidhihirisha wapi kwa binadamu? Baada ya kupitia uzoefu wa kazi hatua kwa hatua, mnaweza kuona kwamba Mungu anapozungumza katika kila hatua ya kazi, anatumia ruwaza fulani, anazungumza unabii fulani, na anaonyesha ukweli fulani na tabia ya Mungu, na watu wote wana mijibizo. Mijibizo yao ni nini? Hawajinyenyekeshi kwa Mungu, hususan hawachukui hatua ya kutafuta ukweli, au hawapo radhi kukubali kazi ya Mungu. Wote wana mitazamo hasi na wabishi, na wanakanganyikiwa, wanakataa na hawakubali. Hata hivyo, toka mwanzo, Mungu hajabadilisha namna Anavyofanya kazi Yake, upendo Wake kwa binadamu haubadiliki. Bila kujali mtazamo wa watu, bila kujali kama wanakataa au wanakubali shingo upande, au wanabadilika kidogo, upendo wa Mungu haubadiliki. Kazi Yake haijawahi kuvurugwa katika hatua yoyote ile. Hiki ni kipengele kimojawapo ambapo upendo Wake unadhihirishwa. Aidha, baada ya kila hatua ya kazi kukamilika, bila kujali namna ambavyo watu wanajidhihirisha, upendo wa Mungu kwa watu haubadiliki. Siku zote Anafanya kazi na siku zote Anawaokoa watu. Katika hatua inayofuata Anapokuwa anafanya kazi Yake, maneno Yake ya hukumu na ufunuo yatakuwa ya kina, wazi zaidi, na kuelekezwa zaidi katika hali ya sasa ya watu. Anazungumza maneno fulani kuwaruhusu watu waweze kumuelewa na kumfahamu Yeye vizuri zaidi, na hususan ili kwamba waweze kuelewa mapenzi Yake na waweze kupata mapenzi Yake. Watu wataona kwamba Mungu bado Anawapenda binadamu. Bila kujali kama mijibizo ya watu siku zote kuwa ni hasi au inampinga Mungu, watu siku zote watakuwa na aina hii ya mijibizo katika kila hatua ya kazi. Hata hivyo, Mungu siku zote huzungumza na hufanya kazi, na Mungu kamwe hajawahi kubadili upendo Wake kwa binadamu. Kwa hiyo, kazi yote ya Mungu kwa binadamu ni upendo. Baadhi ya watu husema: "Kama yote ni upendo, basi kwa nini Anahukumu na kumwadibu mwanadamu? Kwa nini inaonekana ni chuki kwa watu? Hata anawajaribu watu na kuwaacha wafe!" Ni kweli, Mungu ana upendo tu kwa watu! Mungu huurudi na kuuhukumu uasi wa watu ili kuwafanya watu waelewe ukweli na kuwafanya watubu na kuanza upya, na kuwafanywa watu waielewe tabia ya Mungu, na hivyo kuwafanya watu kumheshimu Mungu na kujinyenyekesha Kwake. Baadhi ya watu akili zao zipo katika hali ya kupinga, lakini Mungu hakati tamaa hata kidogo katika kuwaokoa watu; hii huhitaji kiwango kikubwa cha upendo, sio? Wakati wa kipindi cha wafanya huduma, watu wengi wapo katika hali ya uhasi na maumivu kiasi kwamba wanalia na kuhangaika kwa kiasi ambacho wanaomboleza na kulalama kwa sauti, wakijiuliza wanawezaje kuwa wafanya huduma katika shida nyingi kiasi hicho. Kwa kweli hawako radhi! Hauko radhi na huelewi, lakini Mungu anakuelewa. Je, huu si upendo? Upendo Wake unajumuisha ufahamu wa watu, kuwaongoza watu wote, na uelewa wa kina wa watu. Upendo Wake haukanganywi, si wa kujifanya, si mtupu, bali ni wa kweli. Anauona upungufu na ujinga wako na Ana huruma juu yako, Anakupenda na siku zote Anakuamsha kihisia. Bila kujali kama upo tayari au haupo radhi kuwa mfanya huduma, siku zote Anazungumza na kukupatia miezi kadhaa ya utakasaji ili kufunua ufisadi wako na kukufanya uifahamu hali yako ya fedheha. Je, kunakuwa na upendo wakati wa kipindi hiki cha miezi mitatu? Kama Hakuwa na upendo, basi Angekupuuza; kwa kutazama mwenendo wako wa mambo wakati wa kipindi cha wanfanya huduma, Angekuwa amekusukumilia mbali mapema. Je, hauko radhi kuwa mfanya huduma? Hutoteswa na Mungu, lakini unarukaruka kwa furaha pale unapopata baraka. Ikiwa Mungu alikuwa na chuki pekee badala ya upendo, basi watu wangeangamizwa kwa sababu ya mijibizo yao miovu. Miezi mitatu ya utakasaji si muda mrefu. Kwa nini Nasema sio muda mrefu? Kwa sababu hiki ni kiasi tu cha muda ambao watu wanaweza kuvumilia. Kama ingekuwa kwa muda mrefu kidogo, basi wasingeweza kuvumilia. Ingawa siku zote wanaimba, wanakutana pamoja, na kushiriki, wanafurahia tu mambo hayo na hakika wasingeweza kuendelea kusimama; kwa hiyo, wanabadilishwa kuwa watu wa Mungu mapema Hii pia inahitaji upendo; Mungu anatumia moyo Wake na upendo kuwabadilisha watu na kuwashikilia watu. Huu pia ni udhihirishaji wa upendo. Unaweza kuona upendo wa Mungu katika kipindi cha muda huu; hachelewi hata kwa siku moja au mwezi mmoja. Siku itakapofika ambapo Atapaswa kuzungumza, basi huzungumza bila kuchelewa. Kama Angechelewa miezi mingine michache, basi hatua kwa hatua baadhi ya watu wangeondoka. Huku ni kufanya kazi kulingana na hali halisi za watu. Hachelewi kabisa au kupoteza muda, Anamzingatia kila mtu kwa umahususi. Kwa kuwa Anawaokoa watu, Anawajibika hadi mwisho. Lakini baadhi ya watu hawayaishi matarajio, wanateleza na kuanguka chini. Kabla ya watu hawajaondoka, Roho Mtakatifu kwa umahususi anawasukuma na kuwasihi wabaki. Baadhi ya watu kwa kweli wamebembelezwa kubaki lakini hawakubaki. Mungu kwa kweli anawapenda watu sana, lakini watu hawamruhusu Mungu kuwapenda. Ikiwa Mungu hawezi kuwapenda watu wanaojiondoa, basi itabadilika kuwa chuki, na Anaweza kumpuuza kabisa mtu wa aina hiyo. Kwa kuzingatia hatua na kiwango cha muda wa kazi, urefu wa hatua, kiasi cha maneno yaliyosemwa katika hatua, toni ya sauti, mbinu zilizotumika katika hatua, na ukweli unaoambatana nayo kukufanya uelewe, yote hujumuisha mawazo Yake makuu na tafakari na mpangilio na upangaji sahihi. Siku zote Anatumia hekima Yake kuwaongoza binadamu, kuwakimu, kuwahudumia, na kuwakuza kidogokidogo na kuwaleta katika siku hii. Kila mtu ambaye amepitia mambo haya sasa ana kiasi fulani cha ufahamu; hata kama Siijadili, watu wengi wanaweza; watu wanaweka mchakato wa hatua kwa hatua katika kumbukumbu zao. Hakuna maneno ya kuelezea upendo uliopo katika hili. Mungu anawapenda watu sana lakini watu hawataupitia upendo huo kwa kina; upendo huu ni wa kina sana na haiwezekani kuuelezea vizuri kwa maneno; haiwezekani kuuelezea kwa mtazamao wa wakati. Kwa mtazamo wa wakati, tunaweza kuona ni jinsi gani upendo Wake kwa binadamu ni wa kina sana; Anatoa uangalifu mkubwa kwa mambo madogomadogo na haruhusu muda kusonga hata kidogo. Anahofia kwamba ikiwa muda utasonga sana watu watajiondoa na kumwacha. Upendo Wake unawashikilia watu kwa nguvu na haukati tamaa kabisa. Aidha, kuna hatua za kurudi na hukumu pia ambazo Mungu Anazifahamu. Ikiwa kungekuwa na mbinu nyingine zaidi, watu wangehisi kwamba Mungu alikuwa Anawahadaa na kuwachezea. Vimo vya watu havijafikia kiwango na ni rahisi sana kwao kujitoa. Kwa hiyo, baada ya miezi mitatu ya utakasaji, Mungu alizungumza tena na kuwafanya wafanya huduma kuwa watu Wake na kila mtu alifurahi. Watu walitikiswa kihisia kiasi kwamba wakaangua kilio na wakaona kwamba hekima ya Mungu ni nzuri sana. "Wakati huo wote nilidhani nilikuwa mfanya huduma kweli, nilidhani sina hatima, na kwamba hii ilimaanisha kwamba Mungu hatutaki na tumekwisha kabisa." Wakati huo kama Ningesema kwamba nisingewaruhusu kufa, hakuna ambaye angeamini; mngedhani kwamba Mungu tayari amesema hivyo na kwamba ilikuwa ni kweli kabisa. Baada ya miezi mitatu, Nilizungumza kifungu kingine cha maneno na kuhitimisha hukumu ya wafanya huduma. Ingawa asili za watu zimepotoka, wakati mwingine watu wanakuwa hawana hatia hasa kama mtoto mdogo. Kwa nini inasemwa kwamba watu siku zote ni watoto wachanga mbele ya Mungu? Kila tendo wanalofanya ni kama la mtoto mchanga; watu wanawaangalia wengine kana kwamba wote wamepotoka na kuoza, lakini katika macho ya Mungu, watu siku zote ni watoto wachanga, wanyofu na wasio na hatia; kwa hiyo Mungu hawachukulii watu kama maadui, badala yake Anawaangalia kama walengwa Wake wa wokovu na upendo. Kwa hiyo upendo wa Mungu kwa watu si kama ambavyo watu wanafikiria, ambayo ni kusema tu mambo mazuri na heri. Wakati huu, kuna maneno fulani katika kazi ya Mungu ambayo kwa kweli hayakidhi matarajio ya watu, hadi kufikia hatua ya kuvunja mioyo ya watu na kuwasababishia maumivu. Baadhi ya maneno ya hukumu ni kama yanawachora na kuwakaripia watu, lakini kwa kweli yote yana muktadha wa kweli na yapo sambamba na uhakika na ukweli. Hayajaongezwa chumvi. Mungu anazungumza kulingana na dutu ya watu iliyopotoka na kwa kuwa watu watapitia uzoefu kwa kipindi fulani, basi wataelewa. Kusudi la Mungu kusema mambo haya ni kuwabadilisha na kuwaokoa watu. Ni kwa kuzungumza tu kwa namna hii ndiyo Anaweza kupata matokeo mazuri kabisa. Unapaswa kuona kwamba nia njema ya Mungu ni kwa ajili ya kuwaokoa watu na kila kitu kilichomo ndani yake ni upendo wa Mungu. Bila kujali kama unauangalia kwa mtazamo wa hekima katika kazi ya Mungu, kwa mtazamo wa hatua na ruwaza katika kazi ya Mungu, au kwa mtazamo wa wakaa wa kazi au mipangilio na mipango Yake sahihi—chote kilichomo ndani yake ni upendo Wake. Kwa mfano, watu wote wana upendo kwa wana na mabinti zao na ili kuwaruhusu watoto wao kutembea katika njia sahihi, wote wanaweka jitihada kubwa. Wanapogundua udhaifu wa watoto wao, wanahofia kwamba ikiwa watazungumza kwa sauti laini, watoto wao hawatasikia na hawataweza kubadilika, na wanahofia kwamba ikiwa watazungumza kwa ukali sana, wataumiza staha ya watoto wao na watoto wao hawataweza kuvumilia. Kwa hiyo, hii yote inafanyika chini ya ushawishi wa upendo na kiwango kikubwa cha jitihada kinatumika. Nyinyi ambao ni wana na mabinti mtakuwa mmeshawahi kupata upendo wa wazazi wenu. Sio tu upole na kujali ndio upendo, lakini hata zaidi, kuadibu sana ni upendo. Mungu yupo chini ya ushawishi wa upendo kwa binadamu na chini ya sharti la mwanzo la upendo. Kwa hiyo, Anafanya kwa kadri ya uwezo Wake wote kuwaokoa wanadamu waliopotoka. Hashughuliki nao kwa kutimiza wajibu tu, badala yake anafanya mipango sahihi, kulingana na hatua. Kwa kuzingatia wakati, eneo, toni ya sauti, mbinu ya kuzungumza, na kiwango cha jitihada kilichowekwa..., mnaweza kusema kwamba yote hii inafunua upendo Wake, na inaelezea vizuri kabisa kwamba upendo Wake kwa binadamu hauna mipaka na haupimiki. Na watu wengi wanasema maneno ya uasi wanapokuwa katikati ya kujaribiwa kwa mfanya huduma na wanatoa malalamiko. Lakini Mungu hagombanigombani juu ya mambo haya, na hakika hawaadhibu watu kwa hili. Kwa sababu Anawapenda watu, Anasamehe kila kitu. Ikiwa Angekuwa na chuki tu badala ya upendo, basi Angeweza kuwahukumu watu mapema kabisa. Kwa kuwa Mungu ana upendo, Hagombanigombani, bali Anavumilia, na Anaweza kuona shida za watu. Hii kabisa ni kufanya kila kitu chini ya ushawishi wa upendo. Mungu tu ndiye anawaelewa watu, wewe hata hujielewi. Hiyo si sahihi? Tafakari kuhusu hilo kwa makini, baadhi ya watu wanalalamika kuhusu hiki na kile; watu wanasababisha shida bila sababu, wanaishi kwenye baraka lakini hawahisi baraka. Hakuna Anayejua ni maumivu kiasi gani Mungu ambaye Alishuka duniani kutoka mbinguni atalazimika kuteseka kiasi gani. Mungu alikuwa mtu, Yeye ni mkuu sana na Aliweza kuwa mdogo hivyo, wa hali ya chini na Aliteswa hivyo. Ni maumivu kiasi gani Aliyopitia! Chukua mfano kutoka duniani: Mtawala mzuri huwapenda watu wake kama tu watoto wake, na ili kuelewa shida na mateso ya watu, yeye binafsi anatoka na kwenda kushuhudia. Kulinagana na nafasi yake, hapaswi kuteseka na maumivu haya, lakini ili kuondoa maumivu ya watu, anawatembelea kwa siri akiwa katika mavazi ya kawaida. Anakwenda miongoni mwa watu na kushuhudia na kuyaelewa maumivu ya watu kama mtu wa kawaida. Kulingana na nafasi yake, kujishusha hadhi kwenye hadhi ya mtu wa kawaida ni jambo la unyenyekevu; anapaswa kuishi kama mtu wa kawaida na watu hawaijui hadhi yake, na kwa kweli wanamchukulia kama mtu wa kawaida. Kuna hatari nyingi miongoni mwa watu, na kimsingi wanamchukulia kwa namna tofauti, na huanza kupata shida na mateso ya watu; huteseka kwa maumivu ambayo watu wanawayapata; analazimika kuwa mwangalifu na makini kila mahali. Anafanya hivi kwa ajili gani? Kuna lengo moja tu linalomsukuma. Mungu anaweza kufanya kazi kwa namna hii leo kwa sababu mpango Wake wa usimamizi umefikia kiwango hiki. Anawapenda binadamu hivyo Anawaokoa binadamu, Anaweza kufanya hili kwa sababu Anasukumwa na upendo na yupo ndani ya viunga vya upendo. Mungu alikuwa mwili na Aliteseka kwa mateso makubwa ili kuliokoa kundi hili la binadamu walioharibika. Hii kwa kutosheleza kabisa inathibitisha kwamba upendo Wake ni mkubwa sana. Kuna ushauri, faraja, tumaini, uvumilivu, na ustahimilivu katika maneno ambayo Mungu huzungumza, hata zaidi, kuna hukumu, adibu, laana, kufichuliwa hadharani, ahadi za kuvutia, n.k. katika maneno Yake. Bila kujali mbinu, yote hii imetawaliwa na upendo. Hii ni dutu ya kazi Yake, sio? Nyinyi nyote kwa sasa mna kiasi fulani cha uelewa, lakini sio wa kina kiasi hicho. Angalau mnaweza kuwa na kiasi fulani cha ufahamu, na baada ya kuwa na uzoefu wa miaka mitatu hadi mitano, mtaweza kuhisi kwamba upendo huu ni wa kina sana na ni mkubwa sana. Haiwezekani kutumia meneno ya binadamu kuelezea. Ikiwa watu hawana upendo, wanawezaje kurudisha upendo wa Mungu? Hata kama uliyatoa maisha yako kwa Mungu, usingeweza kumlipa. Baada ya nyinyi kupitia uzoefu wa mika mitatu hadi mitano, na kutafakari juu ya mafunuo na tabia zenu za sasa, mtakuwa na majuto kupita kiasi na mtapiga magoti chini na kusujudu vichwa vyenu kwenye ardhi. Kwa nini watu wengi wanafuatilia kwa karibu? Kwa nini watu wengi wamekuwa na shauku kubwa hivi? Wana uelewa wa upendo wa Mungu, na wanaona kwamba kazi ya Mungu ni kuwaokoa watu. Fikiria kuhusu hilo, je, kazi ya Mungu sio sahihi hususan kwa kuzingatia muda? Kiungo kimoja hufuata kiungo kingine bila kuchelewa hata kidogo. Kwa nini Hachelewi? Bado ni kwa ajili ya binadamu. Hayupo radhi kutoa sadaka au kupoteza roho hata moja. Watu hawajali kuhusu majaliwa yao wenyewe, kwa hiyo, ni nani katika dunia hii anakupenda sana? Hujipendi, hujui kutunza maisha yako mwenyewe, na hujui yana thamani kiasi gani. Ni Mungu Ndiye Anayewapenda sana binadamu. Ni Mungu pekee ndiye Anayewapenda sana binadamu. Watu wanaweza kuwa bado hawajaliona hili, wakidhani kwamba wanajipenda. Kwa kweli, ni upendo gani ambao watu wanao wao kwa wao? Ni upendo wa Mungu tu ndio upendo wa kweli; taratibu utaelewa upendo wa kweli ukoje. Ikiwa Mungu hangekuwa mwili na kufanya kazi na kuwaongoza watu uso kwa uso, ikiwa Hangekutana na watu na kuishi na watu wakati wote, basi kuuelewa upendo wa Mungu kwa kweli kisingekuwa kitu rahisi kwa watu kufanya.

Watu na Mungu kimsingi hawafanani na wanaishi katika dola mbili tofauti. Watu hawawezi kuielewa lugha ya Mungu, na zaidi hawawezi kuyaelewa mawazo ya Mungu. Ni Mungu pekee ndiye Anayewaelewa watu na haiwezekani kwa watu kumwelewa Mungu. Mungu ni lazima Awe mwili na Afanane na mwanadamu (kufanana kwa umbo la nje). Mungu anavumilia mateso na maumivu mengi ili kuwaokoa binadamu na kuwafanya watu kuielewa na kuifahamu kazi ya Mungu. Kwa nini Mungu siku zote Anawaokoa watu na hajawahi kukata tamaa? Hii si kwa sababu ya upendo Wake kwa watu? Anamwona binadamu akiharibiwa na Shetani na Hawezi kuvumilia kuacha au kukata tamaa. Kwa hivyo kuna mpango wa usimamizi. Ikiwa Angewaharibu binadamu Akipatwa na hasira kama watu walivyodhani, basi kusingekuwa na haja ya kuwaokoa watu waziwazi kwa namna Afanyavyo sasa. Na kwa kuwa Alikuwa mwili na Akateseka kwa maumivu, upendo Wake umedhihirishwa, upendo Wake unavumbuliwa kidogokidogo na watu na unafahamika kwa watu wote. Kama isingekuwa kwa kufanya kazi namna hii sasa, na ikiwa watu wangejua tu kwamba kuna Mungu mbinguni na kwamba Anawapenda binadamu, basi hili litakuwa ni fundisho tu, na watu kamwe wasingeweza kuuona upendo wa Mungu. Ni kwa Mungu tu kuwa mwili na kufanya kazi ndipo watu wanaweza kuwa na uelewa wa kweli juu Yake ambao si wa kufikirika au mtupu na wala sio maneno matupu, lakini badala yake ni ufahamu ambao ni wa kweli. Hii ni kwa sababu upendo ambao Mungu anawapatia watu ni wa manufaa yanayoonekana, kazi hii inaweza kufanywa tu kwa kuwa mwili na haiwezi kuchukuliwa nafasi na Roho Mtakatifu. Ni upendo mkubwa kiasi gani ambao Yesu aliwapa watu? Alihudumu kama sadaka ya dhambi kwa binadamu waliopotoka kwa kusulubiwa, Alikuja kukamilisha kazi ya ukombozi kwa ajili ya binadamu, hadi aliposulubiwa. Upendo huu hauna mipaka na kazi ambayo Mungu ameifanya ni ya muhimu sana. Kuna watu ambao wana dhana kuhusu Mungu kuwa mwili. Ni dhana gani hizi walizonazo? Bila Mungu kuwa mwili, imani ya watu kwa Mungu ingekuwa ni mfumo tupu na wakati wa mwisho wangeangamizwa. Upendo wa Mungu kwa binadamu hasa umedhihirishwa katika kazi Yake wakati akiwa katika mwili, Yeye binafsi Akiwaokoa watu, Akizungumza uso kwa uso na watu, na kuishi miongoni mwa watu bila kuwa mbali nao hata kwa hatua moja, bila kujifanya, lakini akifanya kweli. Huwaokoa watu kwa kiasi kwamba Aliweza kuwa mwili na kupita miaka mingi ya maumivu pamoja na watu duniani, yote hii ni kwa sababu ya upendo Wake na huruma kwa binadamu. Upendo wa Mungu kwa binadamu hauna masharti au matakwa. Anapata nini kutoka kwa binadamu? Watu hawamchangamkii Mungu. Nani anaweza kumchukulia Mungu kama Mungu? Watu hata hawampatii Mungu faraja, hata leo hii Mungu hajapokea upendo wa kweli kutoka kwa watu. Mungu Anatoa bila ubinafsi na Anakimu bila ubinafsi, lakini watu bado hawaridhiki na wanaendelea kuomba neema bila kukoma. Watu ni wagumu sana kushughulika nao na ni wasumbufu sana! Hata hivyo, siku moja siku itafika ambapo kazi ya Mungu itapata matokeo na idadi kubwa ya watu watatoa shukrani za kweli kutoka mioyoni mwao. Watu ambao wamepitia uzoefu wa miaka mingi wanaweza kuelewa kipengele hiki. Ingawa watu ni wazito, hata hivyo sio maroboti; si vitu visivyokuwa na uhai. Watu ambao hawajawahi kuwa na uzoefu na kazi ya Mungu wanaweza wasieweze kutambua mambo haya; wanakubali kwa kusema kwamba ukweli huu ni sahihi, lakini hawana uelewa wa kina sana.

Mungu alikuwa mwili na Amefanya kazi kwa miaka kadhaa na Amesema mambo yasiyoweza kuhesabika. Mungu anaanza kwa kutoa hukumu ya wafanya huduma, na baadaye Husema unabii na Huanza kazi ya hukumu na kurudi, kisha Hutumia kifo kuwatakasa watu. Baada ya hapo, Huwaongoza watu katika njia sahihi ya kumwamini Mungu, Akizungumza na kuwapatia watu ukweli wote na kupambana na dhana mbalimbali za mwanadamu. Baadaye, Humpatia mwandamu tumaini dogo kumruhusu kuona kuna tumaini mbele yake; yaani, Mungu na watu wanaingia katika mwisho mzuri wa safari kwa pamoja. Ingawa kazi hii inafanywa kulingana na mipango ya Mungu, yote inafanywa kulingana na mahitaji ya binadamu. Haifanywi kiholela na Yeye; Hutumia hekima Yake kufanya kazi yote hii. Kwa kuwa ana upendo, Anaweza kutumia hekima na kwa bidii kushughulika na watu hawa walioharibika. Hachezi na watu hata kidogo. Hebu angalia toni ya sauti na namna ya kutamka maneno katika maneno ya Mungu; wakati fulani inawapatia watu majaribu, wakati fulani meneno Yake huwafanya watu kutahayari, wakati fulani huwapatia watu maneno ambayo huwaokoa na hufanya wawe watulivu. Kwa kweli Anawafikiria sana na kuwajali watu. Ingawa watu ni viumbe wa Mungu, na wote wamepata uharibifu kutoka kwa Shetani, na ingawa watu hawana thamani, ni wazururaji, na asili zao ziko namna hii, Hashughuliki na watu kulingana na hulka zao, na Hashughuliki nao kulingana na adhabu ambayo wangestahili kuipata. Ingawa maneno Yake ni makali, siku zote Anashughulika na watu kwa ustahimilivu, uvumilivu, na huruma. Tafakari hili kwa taratibu na kwa makini! Ikiwa Mungu hakushughulika na watu kwa uvumilivu, huruma na neema, je, Angeweza kusema mambo haya yote ili kuwaokoa watu? Kwa nini Hakuwahukumu watu moja kwa moja? Watu ni wapumbavu sana na wajinga, watu hawana upendo katika dutu yao, na hawajui upendo ni nini, na hawajui kwa nini Mungu hufanya kazi namna hii. Watu wanapokuwa hawauoni upendo wa Mungu, basi wanahisi: Mungu hufanya kazi hii vizuri sana, ni faida kwa binadamu na inaweza kuwabadilisha watu. Hata hivyo, hakuna mtu hata mmoja ambaye huhisi kwamba Mungu Amefanya kazi Yake vizuri sana, kwa umuhimu mkubwa sana, na kwamba upendo Wake kwa binadamu ni wa kina sana, na kwamba kwa kweli hajawahi kushughulika na watu kama uchafu usioweza kuvumilika. Watu hawajawahi kumchukulia Mungu kama Mungu, lakini Mungu amewachukulia watu kama watu. Sivyo ilivyo? Mungu husema kwamba nyinyi ni wanyama, lakini Hajawahi kiwachukulia nyinyi kama wanyama. Ikiwa Angewachukulia kama wanyama, basi kwa nini Awapatie ukweli? Angekuwa Anakuokoa kwa ajili ya nini? Baadhi ya watu wanahisi wamekosewa sana na wanasema: "Mungu Alisema mimi ni mzururaji, nimeaibika sana siwezi kuendelea kuishi." Kwa kweli watu hawaelewi mapenzi ya Mungu. Mtu anaweza kusema kwamba unaweza kupitia uzoefu wa hekima na makusudi mema ya kazi ya Mungu katika maisha yako yote lakini hutaweza kuyaelewa kwa kina sana. Bila kujali kama uzoefu wako ni wa kina au la almradi mwishoni unaelewa na unajua kidogo, basi hiyo inatosha. Mungu anawaomba watu kuuelewa ukweli na kujikita katika kubadilisha tabia zao, ili polepole kuingia kwa kina katika kujitoa kwao na kujinyenyekeza vilevile katika upendo walio nao kwa Mungu katika mioyo yao. Watu wanapojitolea mhanga kidogo na kupata shida kidogo, basi wanafikiri kwamba michango yao ni mikubwa sana mbele ya Mungu, na kwamba wana ukuu. Wanapofanya mchango wao mdogo, wanakoga ukuu wao, na kama hawataji michango yao, basi hawahisi wapo imara au wametulia. Je, watu wana upendo? Watu wana upendo gani? Je, Mungu hupokea upendo wa kweli wa watu? Je, Mungu si mwenye kustahili upendo wa watu?
kutoka kwa Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Ijumaa, 25 Januari 2019

Bila Ukweli Ni Rahisi Kumkosea Mungu

Sura ya 28. Bila Ukweli Ni Rahisi Kumkosea Mungu

Mwenyezi Mungu alisema, Kutoa kwenu "muhtasari kuhusu ukweli" hakufanywi ili kuwawezesha watu kupata maisha au kupata mabadiliko katika tabia zao kutoka kwa ukweli. Badala yake, kunafanywa ili watu waweze kuwa weledi wa maarifa na mafundisho fulani kutoka kwa ukweli. Wao huonekana kana kwamba wanaelewa lengo lililokusudiwa katika kazi ya Mungu, wakati kwa kweli wamekuwa weledi wa baadhi ya maneno ya mafundisho tu. Hawaelewi maana iliyokusudiwa ya ukweli, na si tofauti na kusomea theolojia au kusoma Biblia. Wewe unakusanya vitabu hivi au vifaa hivyo, na hivyo unapata umiliki wa kipengele hiki cha mafundisho au kipengele kile cha ujuzi. Wewe ni msemaji wa kiwango cha juu wa mafundisho—lakini huwaje unapomaliza kusema? Watu basi hawana uwezo wa kupitia, hawana ufahamu wa kazi ya Mungu na hawana ufahamu wao wenyewe pia. Mwishowe, vitu vyote watakavyokuwa wamepata ni fomyula na sheria, na wanaweza kuzungumza juu ya mambo hayo lakini hakuna kitu kingine, hivyo kama Mungu akifanya jambo jipya, je, mafundisho yote unayoyajua yanaweza kufanana na kile Mungu anachofanya? Kwa hiyo, mambo hayo yako ni sheria tu na wewe unawafanya watu wajifunze theolojia tu: Wewe huwaruhusu kupitia neno la Mungu au kupitia ukweli. Vitabu hivi ambavyo watu hukusanya vinaweza kuwaletea teolojia na ujuzi tu, katika fomyula mpya na katika sheria na mila. Haviwezi kuwaleta watu mbele ya Mungu, au kuwaruhusu watu kuuelewa ukweli au kuyaelewa mapenzi ya Mungu. Kwa kuuliza swali baada ya swali kuhusu maneno hayo, kisha kujibu, kufanya muhtasari, unadhani kuwa wale walio chini wanaweza kuelewa kwa urahisi. Mbali na kuwa rahisi kukumbuka, wao wana uhakika juu ya maswali haya kwa tazamo la haraka, na unafikiri ni vizuri kufanya mambo kwa njia hii. Lakini kile wanachokielewa siyo maana iliyokusudiwa ya ukweli; inatofautiana na ukweli na ni maneno ya mafundisho tu. Hivyo ingekuwa bora zaidi kama wewe hungefanya mambo haya hata kidogo. Unafanya mambo haya kuwaongoza watu kuelewa ujuzi na weledi wa elimu. Wewe huwaleta wengine katika mafundisho, katika dini, na kuwafanya wamfuate Mungu na kumwamini Mungu ndani ya mafundisho ya dini. Je, si wewe ni sawa tu na Paulo? Ninyi hufikiri kwamba kupata weledi wa ujuzi wa ukweli ni muhimu hasa, na pia kujifunza kwa moyo mafungu mengi ya maneno ya Mungu. Lakini jinsi watu wanavyoelewa neno la Mungu si muhimu hata kidogo. Ninyi hudhani ni muhimu sana kwa watu kuweza kukariri mengi ya maneno ya Mungu, kuweza kuzungumza mafundisho mengi na kugundua fomyula nyingi ndani ya maneno ya Mungu. Kwa hiyo, siku zote ninyi hutaka kuweka katika mfumo vitu hivi ili kila mtu awe akiimba wimbo mmoja na kusema mambo hayo hayo, ili kila mtu aongee mafundisho sawa na wengine, awe na maarifa sawa na huweka sheria sawa—hili ndilo lengo lenu. Ninyi hufanya hivi kana kwamba kuwafanya watu waelewe vizuri zaidi, wakati kwa kinyume chake hamjui kwamba kwa kufanya hivi mnawaingiza watu katikati ya sheria ambazo ziko nje ya ukweli wa maneno ya Mungu. Ili kuwafanya watu wawe na ufahamu halisi wa ukweli, ni lazima ujiunge na uhalisi, jiunge na kazi, na uwalete watu mbele ya Mungu. Ni kwa njia hii tu ambapo watu wanaweza kuwa na weledi wa ukweli. Ikiwa jitihada zako zinaelekezwa tu kwa kutumia fomyula na sheria kwa maneno yaliyoandikwa, basi hutaweza kufikia ufahamu wa kweli, hutaweza kuwaongoza wengine kwa uhalisi, na seuze kuweza kuwaruhusu wengine kupitia mabadiliko zaidi au kujielewa wenyewe zaidi. Kama neno lililoandikwa lingekuwa badala ya watu, basi hamngehitaji kufanya chochote kamwe.
Nyinyi bado hamjagundua sheria za maneno ya Mungu, na watu wengi husema hivi: "Hakuna mantiki kwa maneno ya Mungu. Kila makala ina ya maudhui ya aina zote na kuna maana tofauti katika kila kifungu na kila sentensi hali inayofanya kuwa vigumu kwetu kukumbuka na vigumu kuelewa. Hata siyo rahisi kufupisha wazo la jumla la ibara." Neno la Mungu siyo riwaya, wala si nadhari au kazi ya fasihi. Ni ukweli; ni neno ambalo humpa mtu uzima. Neno silo jambo ambalo linaweza kueleweka kwa kufikiriwa kwa akili zenu, wala sheria zake haziwezi kufupishwa kwa juhudi kidogo. Kwa hiyo bila kujali ni kipengele kipi watu wana ufahamu mdogo wacho au wana ufahamu wa sheria zake, inaweza tu kuwa ufahamu wa upande mmoja, wa juu juu tu, kama tone moja tu katika bahari, na kimsingi hauwezi kufikia kile alichokusudia Mungu awali. Makala yoyote ya maneno ya Mungu itakuwa na vipengele kadhaa vya ukweli. Kwa mfano, makala kuhusu fumbo la Mungu kupata mwili itajumuisha umuhimu wa kupata mwili pamoja na kazi inayofanywa na upataji wa mwili. Na pia itakuwa na jinsi watu wanavyopaswa kuamini katika Mungu, na labda inaweza pia kuwa na jinsi watu wanavyopaswa kumwelewa na kumpenda Mungu; itajumuisha mambo mengi ya ukweli. Kama, kwa mujibu wa mawazo yako, umuhimu wa kupata mwili ulikuwa na vipengele vichache tu na unaweza kujumlishwa katika sentensi chache, ni matokeo yapi ambayo kazi ya Mungu kwa mtu yangeweza kufanikisha? Watu hufanywa kuelewa umuhimu wa kupata mwili ili kuwafanya wamwelewe Mungu. Baada ya mtu kumwelewa Mungu, kwa kawaida anakuwa na moyo ambao humcha Mungu, na hili sasa linahusisha matendo ya mtu. Hivyo hakuna kipengele cha maneno ya Mungu na hakuna kipengele cha ukweli kilicho rahisi kama unavyofikiria. Ikiwa wewe hutazama neno la Mungu na lugha ya Mungu kuwa rahisi, ukifikiri kwamba swali lolote linaweza kujibiwa kwa ibara ya maneno ya Mungu, basi huo si ukweli. Kila makala ina mitazamo mingi ambayo maneno ya Mungu huzungumzwa kwayo na hakuna njia ya watu kufupisha au ya kutoa muhtasari wa maneno Yake. Baada ya kufupisha maneno Yake, unafikiri fungu hili limejibu swali lililo hapo juu, lakini fungu hili pia linahusiana na maswali mengine. Kwa hiyo unasema nini kwa hilo? Ukweli una mambo mengi. Kwa nini husemwa kuwa ukweli ni uzima, kwamba unaweza kuleta starehe kwa mtu, kwamba hauwezi kupitiwa kwa ukamilifu wake kwa aushi kadhaa au miaka mia kadhaa? Kwa mfano ulikuwa uvitolee muhtasari baadhi ya vipengele vya ukweli au kifungu fulani cha maneno ya Mungu, halafu uulize swali kulihusu hilo. Kisha, kuzingatia swali hili, ulikuwa usome kifungu hiki, kisha ingekuwa dhahiri kuwa hiki kifungu kimesomwa kwa kulijibu swali hilo. Kwa hiyo kifungu hiki kimekuwa fomyula, kanuni na mafundisho, na si ukweli. Ingawa hakuna hata moja ya maneno ya awali limebadilika, hiki kwa dhahiri sana ni kipande cha mafundisho, na sio ukweli. Kwa nini? Kwa sababu swali ulilouliza uliliuliza vibaya. Liliwaongoza watu kupotea na kuwaingiza katika mafundisho, likawafanya kufikiri, kuwaza, kufikiria swali hili, na walisoma kifungu hiki kwa mujibu wa mafundisho yako, kukisoma wakitumia mtazamo wako wa mafundisho. Kisha wangekisoma tena na kurudia, wakiona swali moja pekee na bila kuona kitu kingine chochote. Mwishowe wao wangeletwa mahali ambapo hawawezi kupata ukweli na hawawezi kupitia neno la Mungu, mahali ambapo wanaweza kujiandaa tu na kujadili mafundisho na ni mahali ambapo hawawezi kumwelewa Mungu. Yote ambayo wangeweza kuzungumza yangekuwa mafundisho yenye kupendeza, mafundisho sahihi, lakini hakungekuwa na uhalisi ndani yao na hawangekuwa na njia ya kutembelea. Aina hii ya kuongoza kweli hufanya madhara makubwa!
Ni nini mwiko mkubwa katika huduma ya mtu kwa Mungu? Unajua? Wale miongoni mwenu ambao huhudumu kama viongozi daima hutaka kuwa na ubunifu mkubwa, kuwa wazuri kuliko wengine, kupata hila mpya ili Mungu aweze kuona jinsi kweli mlivyo na uwezo. Hata hivyo, nyinyi hamzingatii kufahamu ukweli na kuingia katika uhalisi wa neno la Mungu. Nyinyi daima hutaka kuringa; si huu ni ufunuo kwa usahihi wa asili ya kiburi? Wengine hata husema: "Kwa kufanya hivi nina uhakika kwamba Mungu atafurahi sana; Yeye kweli atapenda sana. Wakati huu nitaacha Mungu aone, kumpa Yeye mshangao mzuri." Kwa sababu yashangao huu unaondolewa! Usifanye tu chochote kijacho akilini mwako bila kufikiri. Je, inawezaje kuwa sawa kutozingatia matokeo hayo? Wakati wale kati yenu ambao huudhi tabia ya Mungu na kuziudhi amri Zake za utawala wataondolewa wakati huo, hakutakuwa na maneno mnayoweza kusema. Bila kujali dhamira yako, bila kujali kama wewe hufanya hivyo kwa makusudi au la, kama wewe huelewi tabia ya Mungu au huyaelewi mapenzi ya Mungu, kwa urahisi utamkosea Mungu na kwa urahisi utaziudhi amri Zake za utawala, hiki ni kitu ambacho kila mtu ni lazima ajichunge dhidi yake. Mara unapoziudhi amri za utawala za Mungu au kuiudhi tabia ya Mungu, Mungu hataangalia kama ulifanya hivyo makusudi au bila kukusudia; hiki ni kitu ambacho ni lazima uone kwa dhahiri. Ikiwa huwezi kuona ukweli halisi wa suala hili, basi unahakikishiwa kuwa na tatizo. Katika kumhudumia Mungu, watu wanataka kupiga hatua kubwa, kufanya mambo makubwa, kusema maneno makubwa, kufanya kazi kubwa, kuchapisha vitabu vikubwa, kufanya mikutano mikubwa na kuwa viongozi wakuu. Kama siku zote una matarajio makuu, basi utaziudhi amri kuu za utawala za Mungu; watu kama hawa watakufa haraka. Kama wewe si mwenye tabia njema, mwenye kumcha Mungu au mwenye busara katika kumhudumia Mungu, ipo siku utaziudhi amri za utawala za Mungu. Kama ukikosea tabia ya Mungu, kuziudhi amri Zake za kiutawala, na hivyo kutenda dhambi dhidi ya Mungu, basi Yeye hataangalia kuona ni kwa sababu gani ulitenda hivi, wala kuona nia zako. Kwa hivyo unafikiri Mungu hana busara? Je, Yeye amekosa huruma kwa mwanadamu? Hapana. Kwa nini Mimi Ninasema hapana? Kwa sababu watu si kiziwi, mjinga au kipofu. Nyote mnaweza kuona na kusikia, na bado mnasababisha kosa. Ni sababu gani unaweza kuizungumzia bado? Hata kama wewe huhifadhi nia zozote, mara unapokosea Mungu, lazima utaangamia na kupata adhabu. Kuna haja ya hali yoyote yako izingatiwe? Hakuna mtu yeyote anayelazimishwa kwa kisu kuzikosea amri za utawala za Mungu au tabia ya Mungu. Hili halifanyiki kamwe. Mtu alikuwekea kisu kooni na kukulazimisha, akisema: "Mlaani Mungu wenu. Baada ya kumlaani Yeye nitakupa pesa na sitakuua." Labda katika hali aina hii ungesema maneno ya kukufuru kwa sababu tu unaogopa kufa. Je, hali ya aina hii inaweza kutokea? Mambo huwa hayafiki kiwango hiki, ama hufika? Kwamba tabia ya Mungu haitaruhusu kosa ina maana yake iliyodokezwa. Hata hivyo adhabu za Mungu zinategemeza hali za watu na asili zao. Hali moja ni pale ambapo mtu hajui kuwa Yeye ni Mungu naye humkosea Yeye. Kujua kwamba Yeye ni Mungu na bado kumkosea Yeye kwa makusudi ni hali nyingine. Ikiwa mtu anafahamu kikamilifu kwamba Yeye ni Mungu na bado humkosea, basi mtu huyo ni lazima aadhibiwe. Mungu huonyesha kiasi cha tabia Yake katika kila hatua ya kazi Yake—watu wanafahamu chochote kwa hili? Katika siku za mwisho, Mungu amefanya kazi kwa miaka mingi, je, watu hawajui tabia Yake na ni vitu vipi ambavyo watu hufanya au kusema ambavyo vinaweza kumchukiza Mungu kwa urahisi? Na vitu ambavyo vimefafanuliwa na amri za utawala za Mungu—kile watu wanapaswa kufanya na kile hawapaswi kufanya—Je, watu hawajui hayo pia? Watu hawawezi kuelewa mambo fulani ambayo yanahusiana na ukweli au na kanuni. Hiyo ni kwa sababu hawajapitia kufikia kiwango hicho, na hivyo hawana njia ya kuelewa. Lakini amri za utawala za Mungu ziko ndani ya mawanda yaliyofafanuliwa na yanastahili kuwa ya sheria. Sio lazima kwa watu kuzielewa kwa njia yoyote, ni kwamba tu wafuate maana yazo halisi. Je, si hili ni jambo ambalo mtu sharti apambane nalo? Wewe huzingatii zaidi kitu chochote na humwogopi Mungu, kwa hiyo ni lazima upate adhabu!
kutoka kwa Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Alhamisi, 24 Januari 2019

Gospel Music | "Yule Anayeshikilia Ukuu Juu ya Kila Kitu" | Musical Documentary (Swahili Subtitles)

Gospel Music | "Yule Anayeshikilia Ukuu Juu ya Kila Kitu" | Musical Documentary (Swahili Subtitles)

Kote katika ulimwengu mkubwa mno, sayari zote ya mbingu husogea kwa usahihi katika mizunguko yazo zenyewe. Chini ya mbingu, milima, mito, na maziwa vyote vina mipaka yavyo, na viumbe vyote huishi na kuzaana wakati wa misimu yote minne kulingana na sheria za maisha…. Hili lote limepangwa vizuri sana—je, kuna Mwenye Uwezo Mmoja anayepanga na kutawala yote haya? Tangu tuje katika ulimwengu huu tukilia tumeanza kutekeleza majukumu tofauti katika maisha. Sisi husogea kutoka kuzaliwa mpaka uzee mpaka kuugua hadi kifo, sisi husogea kati ya furaha na huzuni…. Wanadamu kwa kweli hutoka wapi, na kwa kweli tutaenda wapi? Ni nani huitawala jaala yetu? Kutoka nyakati za kale hadi siku za kisasa, mataifa makubwa yameibuka, nasaba za wafalme zimekuja na kwenda, na nchi na watu wamesitawi na kuangamia katika mikondo ya historia…. Kama tu sheria za asili, sheria za maendeleo ya wanadamu zina mafumbo yasiyo na kikomo. Ungependa kujua majibu kuyahusu? Filamu iitwayo Yule Ambaye Hushikilia Ukuu Juu ya Kila Kitu itakuongoza kufikia kiini cha jambo hili, ili kufichua mafumbo yote haya!
Sikiliza zaidi: Kanisa la Mwenyezi Mungu video

Jumatano, 23 Januari 2019

Viumbe Wote Lazima Waje Chini ya Utawala wa Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,

 bhvViumbe Wote Lazima Waje Chini ya Utawala wa Mungu

I
Mungu aliumba vitu vyote, na hivyo Yeye hufanya viumbe vyote kuja chini ya amri Yake, na kutii utawala Wake. Anaamuru vitu vyote, akividhibiti katika mikono Yake. Vitu hai, milima, mito na mwanadamu lazima vyote vije chini ya amri Yake. Vitu angani na duniani lazima vyote vije chini ya utawala Wake. Vyote lazima vitii, bila uchaguzi wowote. Hii ni amri ya Mungu na mamlaka Yake.
II
Mungu aliumba vitu vyote, na hivyo Yeye hufanya viumbe vyote kuja chini ya amri Yake, na kutii utawala Wake. Kila kitu kinaamuriwa na Mungu. Anaamuru na kuvipanga vitu vyote, kila kuainishwa kulingana na aina na kwa mapenzi ya Mungu kupewa nafasi yake. Vitu angani na duniani lazima vyote vije chini ya utawala Wake. Vyote lazima vitii, bila uchaguzi wowote. Hii ni amri ya Mungu na mamlaka Yake.
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu

Jumanne, 22 Januari 2019

Kutupa mbali Jozi La Shetani Kunakomboa

Kutupa mbali Jozi La Shetani Kunakomboa

Momo Mji wa Hefei, Mkoa wa Anhui
Kabla ya kumwamini Mungu, bila kujali chochote nilichokuwa nikifanya, sikuwahi kutaka kubaki nyuma. Nilikuwa tayari kukubali shida yoyote ili mradi ingemaanisha ningeinuka juu ya kila mtu mwingine zaidi. Baada ya kumkubali Mungu, mtazamo wangu uliendelea kuwa sawa, kwa sababu niliamini kikamilifu msemo, “Hakuna maumivu, hakuna faida,” na kuona mtazamo wangu kama ushahidi wa msukumo wangu. Wakati Mungu alinifichulia ukweli, hatimaye niligundua kuwa nilikuwa nikiishi chini ya jozi la Shetani, nikiishi chini ya miliki yake.
Sio muda mrefu sana uliopita, kanisa lilifanya mipango ya kumtuma dada niliyeshiriki naye ili aweze kuhudumu katika nafasi ya uongozi. Niliposikia habari hizo, nilisononeka. Sisi sote tulikuwa tunahudumu katika majukumu ya uongozi hadi tulipoteuliwa tena kama wahariri. Sasa dada yangu angerudia nafasi ya uongozi na kumtumikia Mungu akiwa na uwezekano usio na kikomo wa ukuaji, lakini bado ningebakia nikifanya kazi kwa dawati, nikitekeleza kazi yangu bila kuonekana. Kunaweza kuwa na mategemeo gani ya baadaye katika hayo? Kwa kubadili mawazo, nilikumbushwa msemo wa kale, “Kuna njia milioni tofauti za mafanikio.” Ili mradi ningekamilisha kazi yangu vizuri, ningeweza pia kufanikiwa. Nilihitaji tu kuzidisha jitihada zangu katika kutafuatilia ukweli. Ikiwa ningelenga kuhariri mahubiri ili yawasilishe ukweli vizuri zaidi, labda siku moja viongozi wangeona kuwa nilielewa ukweli. Kisha wangenipandisha cheo na siku zangu za baadaye zingekuwa pia za kuchangamsha. Baada ya utambuzi huu, mawingu ya kijivu yalianza kurejea kwa ajili ya uamuzi mpya. Nilijitosa katika kazi yangu, na nikala na kunywa neno la Mungu wakati sikuwa na shughuli, bila kuthubutu kulegea hata kwa muda.
Siku moja, niliona kifungu kinachofuata katika Mahubiri na Ushirika Kuhusu Kuingia Katika Maisha: “Kila kitu kinachokuzuia kumtafuta Mungu na kutafuta ukweli ni mojawapo ya pingu za Shetani. Ukiwa umefungwa na moja kati ya minyororo ya Shetani, unaishi maisha yako chini ya miliki yake.” Baada ya kusikia haya, sikuweza kujizuia ila kuuliza, “Ni ipi kati ya jozi za shetani ninayoishi chini yake? Ni ipi kati ya sumu zake inayozuia utafutiliaji wangu wa ukweli?” Nilipojaribu kutafakari swali hili kwa kimya, nilikumbushwa hali yangu ya hivi karibuni. Baada ya dada yangu kupelekwa kwenye daraja lake jipya, sikuwa wa kutoonyesha hisia. Kwa kweli, nilijitolea zaidi kula na kunywa neno la Mungu, kumwomba Mungu, na kutekeleza kikamilifu kazi yangu. Kijuujuu, nilionekana kuwa na bidii zaidi katika kutafuta ukweli kuliko hapo awali, lakini ukifunua pazia na kuichambua, uwezo wangu wa kukubali kubaki nyuma ni kwa sababu nilikuwa na matamanio ya kuendelea siku moja. Tamaa yangu ya kuchochea kuwa bora zaidi ilikuwa ndiyo sababu sikuwa wa kutoonyesha hisia na badala yake nilifuatilia ukweli zaidi mno, lakini kunakodhaniwa kuwa ufuatiliaji wangu wa ukweli kulikuwa tu njonzi, ufuatiliaji ulio mchafu. Nilikuwa nikishiriki ufuatiliaji wa muda wa ukweli ili kutimiza madhumuni yangu ya kibinafsi. Nikifikiri nyuma kwa miaka yangu iliyotumika kufuata Mungu, nilitambua kuwa dhabihu zangu zote zilikuwa zimelipwa na sumu ya Shetani “Hakuna maumivu, hakuna faida.” Hivi ndivyo ilivyonifunga pingu isiyoonekana na kunitia kujitahidi kwa ubora. Nilipokuwa na cheo tayari, nilikuwa bado nikitafuta hata cha juu zaidi; Nilipopoteza cheo changu au niliposhindwa kujiendeleza, sikuwa wa kutoonyesha hisia; Mimi bado nilionekana kuwa na hiari ya kulipa bei ili kutafuta ukweli. Hata hivyo, hii haikuwa kwa sababu nilielewa ukweli na nilikuwa tayari kujitoa mhanga kwa ajili yake. Nilitaka tu kutumia kuonekana kwa kujitoa mhanga kwa jitihada za kufanikiwa. Hapo ndipo nilipobaini hatimaye kuwa msimamo wangu wa “Hakuna maumivu, hakuna faida,” ulikuwa kweli mojawapo wa sumu za Shetani zilizokuwa zikitiririka kupitia mishipa yangu. Nilikuwa nimetanganywa; sumu ilikuwa imeninyonya ubinadamu wangu wote. Nilikuwa na kiburi na mwenye tamaa bila hisia yoyote ya taswira yoyote. Mambo hayo yote yalifanyika kabisa chini ya pua langu. Kwa kweli nilifikiri kuwa matamanio yangu yalikuwa ushuhuda wa matarajio yangu. Nilidhani kuwa hali yangu ya kiburi ya kutotaka kubaki nyuma ilikuwa ishara ya motisha yangu. Niliabudu uongo wa Shetani kama ukweli na kuuona kama beji ya heshima badala ya alama ya fedheha. Nilikuwa mjinga kiasi kipi hadi kudanganyika na Shetani kiasi kile, kutojua kutofautisha kati mema na uovu? Hatimaye niliona jinsi nilivyokuwa ovyo. Nilijifunza pia jinsi Shetani ni mwenye kudhuru kwa siri na mwenye kuleta hizaya. Shetani hutumia udanganyifu spesheli kutudanganya na kutupotosha. Hutupotosha, na tunaapa uaminifu kwa mipango yake danganyifu. Hii yote hufanywa bila ujuzi wetu. Tunadhani tunatafuta ukweli na kujitolea kwa ajili ya kweli, lakini kwa kweli tunaishi katika kujidanganya. Sumu za Shetani zina nguvu kabisa! Ikiwa haingekuwa nuru yake Mungu, singewahi kamwe kuona ukweli kwamba nilikuwa nimepotoshwa na Shetani, na hakika singeweza kamwe kubaini mipango yake ya udanganyifu. Ikiwa haingekuwa nuru ya Mungu, ningeendelea kuishi chini ya jozi la Shetani, hadi wakati Shetani hatimaye anitumie mzima.
Wakati huo, nilifikiria kuhusu maneno ya Mungu: “Kama wewe unafurahia kuwa mtoa huduma katika nyumba ya Mungu, ukifanya kazi kwa bidii na kwa makini bila kuonekana, siku zote ukitoa na katu hupokei, basi Nasema kwamba wewe ni mtakatifu mtiifu, kwani hutafuti tuzo na unakuwa tu binadamu mwaminifu” (“Maonyo Matatu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mungu yalinionyesha njia ya kutenda: Kama mmoja wa viumbe wa Mungu, napaswa kumpenda na kumridhisha bila masharti na kutekeleza wajibu wangu kwa dhati. Hii ndiyo hisi ambayo kiumbe mmoja wa Mungu anapaswa kumiliki. Huu ni ufuatiliaji ambao unaambatana na mapenzi Yake. Kuanzia siku ya leo kwenda mbele, nitafanya liwezekanalo kufuatilia ukweli. Nitategemea ukweli ili kupenya udanganyifu wa Shetani na kutupa jozi lake. Sitafuatilia tena kitu chochote cha mwili. Badala yake, nitafanya kazi kwa bidii kwa kutoonekana, kutimiza wajibu wangu kumkidhi Mungu. Hata nikiachwa bila kitu chochote mwishowe, nitaendelea kwa hiari bila majuto yoyote, kwa sababu mimi ni moja tu wa viumbe duni wa Mungu. Kumridhisha Muumba ni nia yangu moja ya kweli maishani.
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Vitabu.

Jumatatu, 21 Januari 2019

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | "Kuhusu Majina na Utambulisho" Sehemu ya Kwanza

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | "Kuhusu Majina na Utambulisho" Sehemu ya Kwanza

Mwenyezi Mungu anasema, "Yesu aliwakilisha Roho wa Mungu, na Alikuwa Roho wa Mungu Akifanya kazi moja kwa moja. Alifanya kazi ya enzi mpya, kazi ambayo hakuna aliyekuwa amefanya mbeleni. Yeye Alifungua njia mpya, Alimwakilisha Yehova, na Alimwakilisha Mungu Mwenyewe. Ilhali kwa Petro, Paulo na Daudi, bila kujali walichoitwa, waliwakilisha tu utambulisho wa kiumbe wa Mungu, ama walitumwa na Yesu na Yehova. Kwa hivyo bila kujali kiasi cha kazi walichofanya, bila kujali jinsi walivyofanya miujiza kubwa, walikuwa bado tu viumbe wa Mungu, na hawakuweza kuwakilisha Roho Mtakatifu. Walifanya kazi kwa jina la Mungu ama baada ya kutumwa na Mungu; zaidi ya hayo, walifanya kazi katika enzi iliyoanzishwa na Yesu ama Yehova, na kazi waliyoifanya haikutengwa. Walikuwa, hatimaye, viumbe wa Mungu tu."

Jumapili, 20 Januari 2019

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | "Je, Wajua? Mungu Amefanya Jambo Kubwa Miongoni Mwa Wanadamu"


Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | "Je, Wajua? Mungu Amefanya Jambo Kubwa Miongoni Mwa Wanadamu"

Mwenyezi Mungu anasema, "Bila kazi ya Yesu, mwanadamu hangeweza kushuka chini kutoka msalabani, lakini bila kupata mwili siku hii, wale wanaoshuka chini kutoka msalabani hawangewahi kusifiwa na Mungu ama kuingia katika enzi mpya. Bila kuja kwa huyu mwanadamu wa kawaida, basi hamngeweza kuwa na hii fursa ama kustahiki kuona uso wa ukweli wa Mungu, kwani nyinyi nyote ni wale ambao wangepaswa kuangamizwa kitambo sana. Kwa sababu ya kuja kwa Mungu mwenye mwili kwa mara ya pili, Mungu amewasamehe na kuwaonyesha huruma. Bila kujali, maneno ambayo lazima Niwaachie mwishowe ni haya: Huyu mwanadamu wa kawaida, ambaye ni Mungu mwenye mwili, ni wa umuhimu sana kwenu. Hili ndilo jambo kubwa ambalo Mungu tayari Amefanya miongoni mwa wanadamu."

Jumamosi, 19 Januari 2019

Swahili Christian Video "Kutoroka Kizimba" (Crosstalk) | Christians Are Determined to Follow God

Swahili Christian Video "Kutoroka Kizimba" (Crosstalk) | Christians Are Determined to Follow God

Mazungumzo chekeshi Kutoroka Kizimbani yanaeleza hadithi ya jinsi Mkristo Xiaolan aliteswa na kufungiwa nyumbani mwao kwa mwezi mmoja na baba yake afisa wa Chama cha Kikomunisti, pale ambapo hakuweza kushiriki katika maisha ya kanisa, na uzoefu wake wa kutoroka nyumbani na kukimbia. Familia iliyokuwa na furaha ilitenganishwa, binti akamwacha mamake, na babake akawekea kisasi cha ndani dhidi yake. Ni nani aliyekuwa mbunifu mkuu? Na ni nani aliyempatia Xiaolan imani na nguvu, na kumwelekeza kutoroka kizimba na kutembea kwa njia sahihi ya maisha?
Sikiliza zaidi: Kanisa la Mwenyezi Mungu video

Ijumaa, 18 Januari 2019

Neno la Mungu | Kurejesha Maisha ya Kawaida ya Mwanadamu na Kumpeleka Kwenye Hatima ya Ajabu (Sehemu ya Kwanza)

Kurejesha Maisha ya Kawaida ya Mwanadamu na Kumpeleka Kwenye Hatima ya Ajabu (Sehemu ya Kwanza)

Mwenyezi Mungu anasema, "Punde tu kazi ya ushindi imekwisha kamilika, mwanadamu ataletwa katika dunia nzuri. Haya maisha, bila shaka, bado yatakuwa duniani, lakini yatakuwa tofauti kabisa na jinsi maisha ya mwanadamu yalivyo leo. Ni maisha ambayo mwanadamu atakuwa nayo baada ya wanadamu kwa ujumla kushindwa, itakuwa mwanzo mpya kwa mwanadamu hapa duniani, na kwa wanadamu kuwa na maisha kama hii ni ushahidi kwamba wanadamu wameingia katika milki jipya na nzuri. Itakuwa mwanzo wa maisha ya mwanadamu na Mungu duniani. Nguzo ya maisha mema kama haya ni lazima yawe kuwa, baada ya mwanadamu kutakaswa na kushindwa, anajiwasilisha mbele za Muumba. Na kwa hivyo, kazi ya ushindi ni awamu ya mwisho ya kazi ya Mungu kabla ya wanadamu kuingia katika hatima ya ajabu. Maisha kama haya ni maisha ya baadaye ya mwanadamu duniani, ni maisha yanayopendeza zaidi duniani, aina ya maisha ambayo mwanadamu ametamania, aina ambayo mwanadamu hajawahi kamwe kutimiza katika historia ya ulimwengu. Ni matukio ya mwisho ya miaka 6,000 ya kazi ya usimamizi, na ndicho wanadamu wanatamani sana, na pia ni ahadi ya Mungu kwa mwanadamu."
Soma Zaidi: Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Alhamisi, 17 Januari 2019

Wimbo wa Kuabudu | "Tabia ya Haki ya Mungu ni ya Pekee" | How to Know God

Wimbo wa Kuabudu | "Tabia ya Haki ya Mungu ni ya Pekee" | How to Know God

Mungu huonyesha tabia Yake ya haki kupitia mbinu na kanuni za kipekee, haidhibitiwi na watu, matukio au vitu. Na hakuna awezaye kubadili dhana au mawazo Yake, au kumshawishi Ajaribu njia tofauti. Hii ndiyo asili ya kipekee ya tabia ya haki ya Muumba! Tabia Yake ya haki!
Mungu huhuku matendo na mawazo yote ya viumbe kwa tabia Yake ya haki. Na kulingana na hili, Hutoa ghadhabu au kupeana rehema. Na hakuna awezaye kubadili rehema au ghadhabu Yake. Na ni kiini Chake tu kiwezacho kuamua njia hii. Hii ndiyo asili ya kipekee ya tabia ya haki ya Muumba! Tabia Yake ya haki!
Tabia ya haki ya Mungu, takatifu na ya kipekee; hakuna awezaye kiuka au kushuku hili. Hakuna awezaye kuimiliki, kiumbwacho au kisichoumbwa. Ghadhabu ya Mungu ni takatifu; haiwezi kukosewa. Rehema Yake pia yabeba asili hii. Hii ni asili ya kipekee ya tabia ya haki ya Muumba! Tabia Yake ya haki!
Hakuna mbadala wa Mungu katika Matendo Yake, kiumbwacho au kisichoumbwa. Wala hawezi kuuharibu Sodoma au kuuokoa Ninawi kama alivyofanya Mungu. Hii ndiyo asili ya kipekee ya tabia ya haki ya Muumba! Tabia Yake ya haki! Tabia Yake ya haki!
kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya
Sikiliza zaidi: Kanisa la Mwenyezi Mungu Nyimbo video

Jumatano, 16 Januari 2019

Uhusiano Kati ya Kila Moja ya Hatua Tatu za Kazi ya Mungu

3. Uhusiano Kati ya Kila Moja ya Hatua Tatu za Kazi ya Mungu

Maneno Husika ya Mungu:
Mwenyezi Mungu alisema, Kutoka kwa kazi ya Yehova mpaka ile ya Yesu, na kutoka kwa kazi ya Yesu hadi kwa kazi iliyoko kwa awamu hii ya sasa, awamu hizi tatu zinajumlisha upana wote wa usimamizi wa Mungu, na zote ni kazi za Roho mmoja. Kutoka Alipoumba ulimwengu, Mungu Amekuwa Akisimamia wanadamu. Yeye ndiye Mwanzo na ndiye Mwisho; Yeye ndiye wa Kwanza na wa Mwisho, na Yeye ndiye mwanzilishi wa enzi na Yeye ndiye huleta enzi kwenye kikomo. Awamu tatu za kazi, katika enzi tofauti na maeneo mbalimbali, hakika yanafanywa na Roho mmoja. Wote ambao wanatenganisha awamu hizi tatu wanampinga Mungu.
kutoka kwa "Maono ya Kazi ya Mungu (3)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Mnafaa kuelewa kazi ya Yehova, sheria Alizoweka, na kanuni ambazo kwazo Aliyaongoza maisha ya mwanadamu, yaliyomo kwenye kazi Aliyofanya kwenye Enzi ya Sheria, kusudio lililomfanya Yeye kuweka wazi zile sheria, umuhimu wa kazi Yake katika Enzi ya Neema, na kazi anayofanya Mungu kwenye awamu hii ya mwisho. Hatua ya kwanza ni kazi ya Enzi ya Sheria, hatua ya pili ni kazi ya Enzi ya Neema, na hatua ya tatu ni kazi ya siku za mwisho. Lazima muelewe awamu hizi za kazi ya Mungu. … Kazi ifanywayo katika siku za mwisho haiwezi kuwekwa mbadala wa kazi ya Enzi ya Sheria ama ile ya Enzi ya Neema. Ingawa, hatua zote tatu zinaungana kuwa kitu kimoja na yote ni kazi iliyofanywa na Mungu mmoja. Kawaida, utekelezaji wa kazi hizi umegawanyishwa katika enzi tofauti. Kazi iliyofanywa katika siku za mwisho inaleta kila kitu mpaka tamati; ile iliyofanywa katika Enzi ya Sheria ni ya mwanzo; na ile iliyofanywa katika Enzi ya Neema ni ya ukombozi. … Katika siku za mwisho, kazi ya neno pekee inafanyika ili kuukaribisha Wakati wa Ufalme lakini haiwakilishi enzi zile zingine. Siku za mwisho sio zaidi ya siku za mwisho na sio zaidi ya Enzi ya Ufalme, ambayo haiwakilishi Enzi ya Neema au Enzi ya Sheria. Siku za mwisho ni wakati ambapo kazi zote ndani ya mpango wa usimamizi wa miaka elfu sita inafuchuliwa kwenu. …
Kazi katika siku za mwisho ni hatua ya mwisho kati ya hizo tatu. Ni kazi ya enzi nyingine mpya na haiwakilishi kazi ya usimamizi mzima. Mpango wa miaka elfu sita umegawawa katika hatua tatu za kazi. Hakuna hatua moja pekee itakayowakilisha kazi ya enzi hizo tatu ila inaweza tu kuwakilisha sehemu moja ya yote. Jina Yehova haliwezi kuwakilisha tabia yote ya Mungu. Ukweli kuwa Alitekeleza kazi katika Enzi ya Sheria sio ushahidi kuwa Mungu Anaweza tu kuwa Mungu chini ya sheria. Yehova alitengeneza sheria kwa mwanadamu na kutoa amri, Akimuuliza mwanadamu ajenge hekalu na madhabahu; kazi Aliyofanya inawakilisha tu Enzi ya Sheria. Kazi Alioyoifanya haidhibitishi kuwa Mungu ni Mungu Anayemwamuru mwanadamu kufuata sheria, Mungu Aliye hekaluni, ama Mungu Aliye mbele ya madhabahu. Haya hayawezi kusemwa. Kazi chini ya sheria inaweza tu kuwakilisha enzi moja. Kwa hivyo, kama Mungu Alifanya kazi katika Enzi ya Sheria pekee, mwanadamu angemfafanua Mungu na kusema, "Mungu ni Mungu Aliye hekaluni. Ili kumtumikia Mungu, lazima tuvae mavazi ya kikuhani na tuingie hekaluni." Iwapo kazi katika Enzi ya Neema haingetekelezwa na Enzi ya Sheria ingeendelea mpaka wakati huu wa sasa, mwanadamu hangefahamu kuwa Mungu pia ni mwenye huruma na upendo. Iwapo kazi katika Enzi ya Sheria haingefanywa, na kwamba tu ile ya Enzi ya Neema ndiyo iliyofanywa, mwanadamu angefahamu tu kwamba Mungu Anakomboa mwanadamu na kumsamehe dhambi zake. Wangefahamu tu kuwa Yeye ni mtakatifu na asiye na hatia, kwamba Anaweza kujitoa kafara na kusulubishwa kwa ajili ya mwanadamu. Mwanadamu angejua tu kuhusu haya na asiwe na ufahamu wa mambo mengine yoyote. Kwa hivyo kila enzi inawakilisha sehemu moja ya tabia ya Mungu. Enzi ya Sheria inawakilisha vipengelele vingine, Enzi ya Neema vipengele vingine na enzi hii vipengele vingine. Tabia ya Mungu inaweza tu kuonekana kwa mchanganyiko wa hatua zote tatu. Ni wakati tu mwanadamu anajua hatua hizi tatu ndipo anaweza kuipokea kikamilifu. Hakuna hatua kati ya hizo tatu ambayo inaweza kuachwa. Utaiona tu tabia ya Mungu kwa ukamilifu wake mara tu utakapozijua hatua hizi tatu za kazi. Mungu kukamilisha kazi yake katika Enzi ya Sheria sio ushahidi kwamba Yeye ni Mungu chini ya sheria, na kukamilika kwa kazi Yake ya ukombozi haionyeshi kuwa Mungu Atamkomboa mwanadamu milele. Hizi zote ni hitimisho zilizofanywa na mwanadamu kuhusu jambo hilo. Enzi ya Neema imefika mwisho, lakini huwezi kusema kuwa Mungu ni wa msalaba tu na kuwa msalaba unawakilisha wokovu wa Mungu. Ukifanya hivyo, basi utakuwa unamfasili Mungu. Katika hatua hii, Mungu Anafanya zaidi kazi ya Neno, lakini huwezi kusema kuwa Mungu hajawahi kuwa Mwenye huruma kwa mwanadamu na kwamba yote Aliyoleta ni kuadibu na hukumu. Kazi katika siku za mwisho inaonyesha wazi kazi ya Yehova na ile ya Yesu na mafumbo yote yasioeleweka na mwanadamu. Hii inafanywa ili kuonyesha hatima na mwisho wa binadamu na kukamilisha kazi yote ya wokovu miongoni mwa wanadamu. Hatua hii ya kazi katika siku za mwisho huleta kila kitu kufika mwisho. Mafumbo yote yasiyoeleweka na mwanadamu lazima yaelezwe ili kumpa mwanadamu ufahamu na kuweza kuelewa kwa kina katika mioyo yao. Hapo tu ndipo wanadamu wataweza kugawanywa kulinga na aina zao. Baada tu ya mpango wa usimamizi wa miaka elfu sita kukamilishwa ndipo mwanadamu atapata kuelewa tabia ya Mungu kwa ukamilifu wake, kwani usimamizi Wake utakuwa umefika mwisho.
kutoka kwa "Fumbo la Kupata Mwili (4)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kazi inayofanywa kwa sasa imesukuma mbele kazi ya Enzi ya Neema; yaani, kazi katika mpango mzima wa usimamizi wa miaka elfu sita imesonga mbele. Ingawa Enzi ya Neema imekoma, kazi ya Mungu imeendelea sana. Kwa nini Ninazungumza mara kwa mara kwamba hatua hii ya kazi inajenga juu ya Enzi ya Neema na Enzi ya Sheria? Hii ina maana kwamba kazi ya wakati huu ni mwendelezo wa kazi iliyofanyika katika Enzi ya Neema na kuinua kazi ile iliyofanyika katika Enzi ya Sheria. Hatua hizi tatu zinaingiliana kwa karibu na kuunganika moja kwa inayofuata. Kwa nini pia Ninasema kwamba hatua hii ya kazi inajenga juu ya kile kilichofanywa na Yesu? Tuseme kwamba hatua hii haingeongezea juu ya kazi iliyofanywa na Yesu, ingebidi Asulubiwe tena katika hatua hii, na kazi ya ukombozi ya hatua iliyopita ingelazimika kufanywa upya tena. Hii isingekuwa na maana yoyote. Kwa hiyo, sio kwamba kazi imekamilika kabisa, bali ni kwamba enzi imesonga mbele, na kazi imekuwa ya juu kabisa kuliko ilivyokuwa kabla. Inaweza kusemwa kwamba hatua hii ya kazi imejengwa juu ya msingi wa Enzi ya Sheria na katika mwamba wa kazi ya Yesu. Kazi hii imejengwa hatua kwa hatua, na hatua hii sio mwanzo mpya. Ni muungano tu wa hatua tatu za kazi ndio unaweza kuchukuliwa kuwa mpango wa usimamizi wa miaka elfu sita.
kutoka kwa "Kupata Mwili Mara Mbili Kunakamilisha Umuhimu wa Kupata Mwili" katika Neno Laonekana katika Mwili
Hatua ya kazi ya mwisho haisimami peke yake, ila ni sehemu ya yote iliyounganishwa pamoja na hatua mbili za awali, ambayo ni kusema kwamba haiwezekani kukamilisha kazi nzima ya wokovu kwa kufanya kazi ya hatua moja pekee. Ingawa hatua ya mwisho ya kazi inaweza kumwokoa mwanadamu kabisa, hii haimaanishi kwamba ni muhimu tu kutekeleza hatua hii pekee, na kwamba hatua mbili za hapo awali hazihitajiki kumwokoa mwanadamu kutokana na ushawishi wa Shetani. Hakuna hatua moja kati ya zote tatu inayoweza kuwekwa kama maono ya kipekee ambayo lazima yajulishwe mwanadamu, kwa kuwa ukamilifu wa kazi ya wokovu ni hatua tatu za kazi, wala si hatua moja kati ya tatu. Ilimradi kazi ya wokovu bado haijakamilishwa, usimamizi wa Mungu utashindwa kufikia kikomo. Nafsi ya Mungu, tabia, na hekima zimeonyeshwa katika ukamilifu wa kazi ya wokovu, wala hazikufichuliwa kwa mwanadamu hapo mwanzo, lakini zimeonyeshwa hatua kwa hatua katika kazi ya wokovu. Kila hatua ya kazi ya wokovu huonyesha sehemu ya tabia ya Mungu, na sehemu ya nafsi Yake: si kila hatua ya kazi inayoweza moja kwa moja kuonyesha kabisa na kwa ukamilifu nafsi ya Mungu. Kwa hivyo, kazi ya wokovu inaweza tu kuhitimishwa hatua tatu za kazi zitakapokamilika, na kwa hivyo, maarifa ya mwanadamu ya ukamilifu wa Mungu hayawezi kutenganishwa na hatua tatu za kazi ya Mungu. Kile ambacho mwanadamu hupokea kutoka kwa hatua moja ya kazi ni tabia ya Mungu inayoonyeshwa katika sehemu moja ya kazi yake tu. Haiwezi kuwakilisha tabia na nafsi inayoonyeshwa katika hatua ya awali na ijayo. Hii ni kwa sababu kazi ya kumwokoa mwanadamu haiwezi kumalizika mara moja katika kipindi kimoja, ama katika eneo moja, lakini hukuwa kwa kina hatua kwa hatua kulingana na kiwango cha kukua kwa mwanadamu katika wakati na maeneo tofauti. Ni kazi inayofanywa hatua kwa hatua, na haikamilishwi katika hatua moja. Na kwa hiyo, hekima yote ya Mungu imejumuishwa katika hatua tatu, badala ya hatua moja. Nafsi yake yote na hekima yake yote zimewekwa wazi katika hatua hizi tatu, na kila hatua ina nafsi Yake, na ni rekodi ya hekima ya kazi Yake. … Kila moja ya hatua tatu za kazi huendelea juu ya msingi wa hatua iliyopita; haitekelezwi peke yake, tofauti na kazi ya wokovu. Ingawa kuna tofauti kubwa katika enzi na aina ya kazi ambayo inafanywa, katika kiini chake bado ni wokovu wa mwanadamu, na kila hatua ya kazi ya wokovu ina kina kuliko iliyopita.
kutoka kwa "Kujua Hatua Tatu za Kazi ya Mungu Ndiyo Njia ya Kumjua Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Usimamizi mzima wa Mungu umegawika kwa hatua tatu, na katika kila hatua, mahitaji yanayopatana yanatokana na mwanadamu. Aidha, kadri enzi zinavyopita na kuendelea, mahitaji ya Mungu kwa wanadamu huongezeka hata zaidi. Kwa hiyo, hatua kwa hatua, kazi hii ya usimamizi wa Mungu hufikia kilele chake, hadi mwanadamu aamini ukweli wa "kuonekana kwa Neno katika mwili," na hivyo mahitaji ya mwanadamu huongezeka hata zaidi, na mahitaji ya mwanadamu kutoa ushuhuda huongezeka hata zaidi. … Wakati wa kale, mwanadamu alihitajika kuzingatia sheria na amri, na alihitajika kuwa mpole na mnyenyekevu. Leo, mwanadamu anahitajika kutii mipango yote ya Mungu na awe na upendo mkuu wa Mungu, na zaidi bado anahitajika kumpenda Mungu katika mateso. Hatua hizi tatu ndizo Mungu anazozitazamia toka kwa mwanadamu, hatua kwa hatua, katika usimamizi Wake wote. Kila hatua ya kazi ya Mungu huzidisha kina kuliko iliyopita, na katika kila hatua, mahitaji ya mwanadamu ni makubwa kuliko yaliyopita, na kwa hali hii, umbo la usimamizi mzima wa Mungu huonekana. Ni hasa kwa sababu mahitaji ya mwanadamu kila mara huwa juu kuliko tabia yake inavyoweza kufikia viwango anavyovihitaji Mungu, na ni hapo ambapo wanadamu wataanza kujiondoa polepole kutoka kwa ushawishi wa Shetani, ndipo kazi ya Mungu itafikia kikomo, wanadamu wote watakuwa wameokolewa kutoka kwa ushawishi wa Shetani. Wakati huo utakapowadia, kazi ya Mungu itakuwa imefika mwisho, na ushirikiano wa mwanadamu na Mungu ili abadilishe tabia zake hautakuwepo, na wanadamu wote wataishi kwenye nuru ya Mungu, na kuanzia hapo kuendelea, hapatakuwa na uasi au upinzani wowote kwa Mungu. Aidha Mungu hatamwekea matakwa mwanadamu, na patakuwepo na ushirikiano mwema zaidi kati ya mwanadamu na Mungu, mojawapo ikiwa maisha ya mwanadamu na Mungu pamoja, maisha ambayo yatafuatia baada ya usimamizi wa Mungu kukamilishwa, na baada ya mwanadamu kuokolewa toka katika mafumbato ya Shetani.
kutoka kwa "Kazi ya Mungu na Utendaji wa Mwanadamu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kazi mzima ya mpangilio wa usimamizi wa Mungu inafanywa binafsi na Mungu mwenyewe. Awamu ya kwanza—uumbaji wa ulimwengu—ilifanywa binafsi na Mungu Mwenyewe, na kama haikuwa hivyo, basi hakuna yeyote ambaye angekuwa na uwezo wa kumuumba mwanadamu; awamu ya pili ilikuwa ukombozi wa wanadamu wote, na pia ilifanywa binafsi na Mungu Mwenyewe, awamu ya tatu inaenda bila kusemwa: Kuna haja kuu zaidi ya mwisho wa kazi ya Mungu kufanywa na Mungu Mwenyewe. Kazi ya ukombozi, ushindi, kumpata, na kumkamilisha wanadamu wote inafanywa binafsi na Mungu Mwenyewe. Kama hangefanya kazi hii Yeye binafsi, basi utambulisho wake hauwezi kuwakilishwa na mwanadamu, au kazi kufanywa na mwanadamu. Ili kumshinda Shetani, ili kumpata mwanadamu, na ili kumpa mwanadamu maisha ya kawaida duniani, Yeye binafsi humwongoza mwanadamu na hufanya kazi binafsi miongoni mwa wanadamu; kwa ajili ya mpangilio mzima wa usimamizi, na kwa kazi yake yote, ni lazima Yeye binafsi afanye kazi hii.
kutoka kwa "Kurejesha Maisha ya Kawaida ya Mwanadamu na Kumpeleka Kwenye Hatima ya Ajabu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Hatua tatu za kazi ambazo zilifanywa tangu mwanzo hadi leo zote zilitekelezwa na Mungu Mwenyewe, na zilitekelezwa na Mungu mmoja. Ukweli wa hatua tatu za kazi ni ukweli wa uongozi wa Mungu kwa wanadamu wote, ukweli ambao hakuna anayeweza kuupinga. Mwishoni mwa hatua tatu za kazi, vitu vyote vitaainishwa kulingana na aina na kurejea chini ya utawala wa Mungu, kwa kuwa duniani kote kuna Mungu mmoja tu, na hakuna dini nyingine.
kutoka kwa "Kujua Hatua Tatu za Kazi ya Mungu Ndiyo Njia ya Kumjua Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kama una maarifa wazi ya hatua tatu za kazi—ambapo ni kusema kwamba, ya mpango mzima wa usimamizi wa Mungu—na ikiwa utaweza kupatanisha hatua mbili za awali na hatua ya sasa, na unaweza kuona kwamba ni kazi iliyofanywa na Mungu Mmoja, basi utakuwa na msingi imara zaidi. Hatua tatu za kazi zilifanywa na Mungu mmoja; haya ndiyo maono makubwa zaidi, na ndiyo njia ya pekee ya kumjua Mungu. Hatua tatu za kazi zingefanywa tu na Mungu Mwenyewe, na hapana mwanadamu yeyote ambaye angeweza kufanya kazi kama hii kwa niaba Yake—ambayo ni kusema kuwa ni Mungu Mwenyewe pekee ambaye angeifanya kazi Yake toka mwanzo hadi leo.
kutoka kwa "Kujua Hatua Tatu za Kazi ya Mungu Ndiyo Njia ya Kumjua Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili

Jumanne, 15 Januari 2019

Ni vipi kazi ya hukumu ya Mungu katika siku za mwisho humtakasa na kumwokoa wanadamu?

3. Ni vipi kazi ya hukumu ya Mungu katika siku za mwisho humtakasa na kumwokoa wanadamu?

Aya za Biblia za Kurejelea:
"Na iwapo mtu yeyote atayasikia maneno yangu, na asiyaamini, Mimi sitamhukumu: kwa kuwa mimi sikuja ili niihukumu dunia, bali kuiokoa dunia. Yeye ambaye ananikataa mimi, na hayakubali maneno yangu, ana yule ambaye anamhukumu: neno hilo ambalo nimelisema, ndilo hilo ambalo litamhukumu katika siku ya mwisho" (YN. 12:47-48).
"Bado ningali nayo mengi ya kuwaambieni, lakini hivi sasa hamwezi kuyavumilia. Hata hivyo, wakati yeye, Roho wa ukweli, atakapokuja, atawaongoza hadi kwenye ukweli wote: kwa maana hatazungumza juu yake mwenyewe; bali chochote atakachosikia, atakinena: na atawaonyesha mambo yajayo" (YN. 16:12-13).
Maneno Husika ya Mungu:
Bila shaka, Mungu Anapopata mwili mara hii, kazi Yake ni kuonyesha tabia Yake, kimsingi kupitia kuadibu na hukumu. Akitumia haya kama msingi, Analeta ukweli zaidi kwa mwanadamu, kuonyesha njia zaidi za matendo, na hivyo Hufikia lengo Lake la kumshinda mwanadamu na kumwokoa mwanadamu kutokana na tabia yake potovu. Hili ndilo liko katika kazi ya Mungu katika Enzi ya Ufalme.
kutoka kwa "Dibaji" katika Neno Laonekana katika Mwili
Katika siku za mwisho, Kristo anatumia ukweli tofauti kumfunza mwanadamu, kufichua kiini cha mwanadamu, na kuyachangua maneno na matendo yake. Maneno haya yanajumuisha ukweli mbalimbali, kama vile wajibu wa mwanadamu, jinsi mwanadamu anavyofaa kumtii Mungu, jinsi mwanadamu anavyopaswa kuwa mwaminifu kwa Mungu, jinsi mwanadamu anavyostahili kuishi kwa kudhihirisha ubinadamu wa kawaida, na pia hekima na tabia ya Mungu, na kadhalika. Maneno haya yanalenga nafsi ya mwanadamu na tabia yake potovu. Hasa, maneno hayo yanayofichua vile mwanadamu humkataa Mungu kwa dharau yanazungumzwa kuhusiana na vile mwanadamu alivyo mfano halisi wa Shetani na nguvu ya adui dhidi ya Mungu. Mungu anapofanya kazi Yake ya hukumu, Haiweki wazi asili ya mwanadamu kwa maneno machache tu; Anaifunua, na kuishughulikia na kuipogoa kwa muda mrefu. Mbinu hizi za ufunuo, kushughulika, na kupogoa haziwezi kubadilishwa na maneno ya kawaida, ila kwa ukweli ambao mwanadamu hana hata kidogo. Mbinu kama hizi pekee ndizo huchukuliwa kama hukumu; ni kwa kupitia kwa hukumu ya aina hii pekee ndio mwanadamu anaweza kutiishwa na kushawishiwa kabisa kujisalimisha kwa Mungu, na zaidi ya hayo kufaidi ufahamu kamili wa Mungu. Kile ambacho kazi ya hukumu humletea mwanadamu ni ufahamu wa uso halisi wa Mungu na ukweli kuhusu uasi wake mwenyewe. Kazi ya hukumu humruhusu mwanadamu kupata ufahamu zaidi wa mapenzi ya Mungu, wa makusudi ya kazi ya Mungu, na wa mafumbo yasiyoweza kueleweka kwa mwanadamu. Pia inamruhusu mwanadamu kutambua na kujua asili yake potovu na asili ya upotovu wake, na pia kugundua ubaya wa mwanadamu. Matokeo haya yote huletwa na kazi ya hukumu, kwa maana asili ya kazi ya aina hii hasa ni kazi ya kuweka wazi ukweli, njia, na uhai wa Mungu kwa wale wote walio na imani ndani Mwake. Kazi hii ni kazi ya hukumu inayofanywa na Mungu.
kutoka kwa "Kristo Hufanya Kazi ya Hukumu kwa Ukweli" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kazi inayofanywa na Mungu katika enzi hii ni hasa ya kutoa maneno kwa ajili ya uzima wa mwanadamu, kuweka wazi hulka ya asili ya mwanadamu na tabia ya mwanadamu iliyoharibika, uondoaji wa dhana za kidini, fikra za kinjozi, mitazamo iliyopitwa na wakati, vilevile maarifa na utamaduni wa mwanadamu. Hii ni lazima iwekwe wazi na kusafishiwa kupitia maneno ya Mungu. Katika siku za mwisho, Mungu Anatumia maneno na siyo ishara na maajabu ili kumfanya mwanadamu kuwa mkamilifu. Anatumia maneno Yake kumweka wazi mwanadamu, kumhukumu mwanadamu, kumwadibu mwanadamu, na kumkamilisha mwanadamu, ili katika maneno ya Mungu, mwanadamu aje kuona hekima na wema wa Mungu, na aje kuelewa tabia ya Mungu, ili kupitia maneno ya Mungu, mwanadamu aone matendo ya Mungu.
kutoka kwa "Kuijua Kazi ya Mungu Leo" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kupitia kazi hii ya kuadibu na hukumu, mwanadamu atakuja kujua hali yake kamili ya uchafu na upotovu ndani Yake, na ataweza kubadilika kabisa na kuwa msafi. Ni hivi tu ndivyo mwanadamu ataweza kustahili kurudi katika kiti cha enzi cha Mungu. Kazi yote ifanywayo siku hii ya leo ni ili mwanadamu afanywe msafi na kubadilika; kupitia hukumu na kuadibiwa na neno, na pia kutakaswa, mwanadamu anaweza kuutupa nje upotovu wake na kufanywa safi. Badala ya kuichukua hatua hii ya kazi kuwa ile ya wokovu, itafaa zaidi kusema kuwa ni kazi ya utakaso. Kwa kweli hatua hii ni ile ya ushindi na pia hatua ya pili ya wokovu. Mwanadamu anatwaliwa na Mungu kupitia hukumu na kuadibu na neno; kwa kutumia neno kusafisha, hukumu na kufichua, uchafu wote, fikira, nia, na matumaini ya mtu mwenyewe katika moyo wa mwanadamu zinafuliwa.
kutoka kwa "Fumbo la Kupata Mwili (4)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Ni kupitia nini ndiyo ukamilishaji wa Mungu kwa mwanadamu hutimizwa? Kupitia tabia Yake yenye haki. Tabia ya Mungu hasa huwa na haki, ghadhabu, uadhama, hukumu, na laana, na ukamilishaji Wake wa mwanadamu hasa ni kupitia hukumu. Watu wengine hawaelewi, na huuliza ni kwa nini Mungu anaweza tu kumfanya mwanadamu kuwa mkamilifu kupitia hukumu na laana. Wao husema kwamba kama Mungu angemlaani mwanadamu, si mwanadamu angekufa? Kama Mungu angemhukumu mwanadamu, si mwanadamu angelaaniwa? Basi anawezaje hata hivyo kufanywa mkamilifu? Hayo ndiyo maneno ya watu wasioijua kazi ya Mungu. Kile ambacho Mungu hulaani ni uasi wa mwanadamu, na kile Anachohukumu ni dhambi za mwanadamu. Ingawa Yeye hunena kwa ukali, na bila kiwango cha hisi hata kidogo, Yeye hufichua yote yaliyo ndani ya mwanadamu, na kupitia maneno haya makali Yeye hufichua kile kilicho muhimu ndani ya mwanadamu, lakini kupitia hukumu kama hiyo, Yeye humpa mwanadamu ufahamu mkubwa wa kiini cha mwili, na hivyo mwanadamu hujitiisha chini ya utii mbele za Mungu. Mwili wa mwanadamu ni wa dhambi, na wa Shetani, ni wa kutotii, na chombo cha kuadibu kwa Mungu—na kwa hiyo, ili kumruhusu mwanadamu kujijua, maneno ya hukumu ya Mungu lazima yamfike na lazima kila aina ya usafishaji itumike; ni wakati huo tu ndiyo kazi ya Mungu inaweza kuwa ya kufaa.
kutoka kwa "Ni kwa Kupitia tu Majaribio ya Kuumiza Ndiyo Mnaweza Kujua Kupendeza kwa Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Mungu anazo mbinu nyingi za kumfanya binadamu kuwa mtimilifu. Yeye hutumia namna zote za mazingira ili kushughulikia tabia potovu ya mwanadamu, na hutumia mambo mbalimbali ya kumweka mwanadamu wazi; kwa njia moja Anamshughulikia binadamu, kwa njia nyingine Anamweka mwanadamu wazi, na kwa njia nyingine Anamfichua mwanadamu, Akichunguza na kufichua "siri" zilizomo katika kina cha moyo wa mwanadamu, na kumwonyesha mwanadamu asili yake kwa kufichua hali zake nyingi. Mungu humfanya mwanadamu kuwa mtimilifu kupitia mbinu nyingi—kupitia kwa ufunuo, kumshughulikia, utakasaji, na kuadibu—ili mwanadamu aweze kujua kwamba Mungu ni wa matendo.
kutoka kwa "Ni Wale tu Wanaolenga Vitendo Ndio Wanaweza Kufanywa kuwa Watimilifu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Majaribu haya yanailenga hali gani ya ndani ya watu? Yanalenga tabia ya uasi ndani ya watu ambayo haiwezi kumridhisha Mungu. Kuna mengi ambayo ni machafu ndani ya watu, na mengi ambayo ni ya unafiki, na kwa hivyo Mungu anawatia katika majaribu ili kuwasafisha. …
Ikiwa hujui tabia ya Mungu, bila shaka utaanguka wakati wa majaribu, kwa kuwa hufahamu jinsi Mungu anavyowafanya watu kuwa wakamilifu, na ni kwa njia gani Huwafanya wakamilifu, na majaribu ya Mungu yakikushukia na yasilingane na mawazo yako, utashindwa kusimama imara. Upendo wa kweli wa Mungu ni tabia Yake kamili, na tabia kamili ya Mungu ikionyeshwa kwako, hili linakuletea nini mwilini mwako? Tabia ya haki ya Mungu ikionyeshwa kwako, bila shaka mwili wako utapata uchungu mkubwa. Iwapo hutapata haya maumivu, basi huwezi kufanywa mkamilifu na Mungu, wala huwezi kumpa Mungu mapenzi ya kweli. Mungu akikufanya mkamilifu kwa hakika atakuonyesha tabia Yake kamili. Tangu uumbaji hadi leo, Mungu hajawahi kuonyesha tabia Yake kamili—ila katika siku za mwisho Anaifichua kwa hili kundi la watu ambao Aliwateua awali na kuwachagua, na kwa kuwafanya watu wakamilifu, Anaiweka wazi tabia Yake, na kupitia kwayo Analifanya kamili kundi la watu. Huo ndio upendo wa kweli wa Mungu kwa watu. Kuyapitia mapenzi ya kweli ya Mungu kunawapasa watu wastahimili uchungu mkali, na kulipa gharama kubwa. Ni baada tu ya hili ndipo watapatikana na Mungu na waweze kutoa tena mapenzi ya kweli kwa Mungu, na ni hapo tu ndipo Moyo wa Mungu utaridhishwa. Ikiwa watu wanataka wafanywe wakamilifu na Mungu, na kama wanataka kutenda kulingana na mapenzi Yake, na kumpa Mungu mapenzi yao ya dhati kikamilifu, ni sharti wapitie mateso mengi na maumivu makali kutokana na hali hizo, kupata uchungu mkali kuliko mauti, hatimaye watashurutishwa kuirejesha mioyo yao ya kweli kwa Mungu. Ikiwa mtu anampenda Mungu kwa dhati au la, itafichuliwa wakati wa shida na usafishaji. Mungu hutakasa mapenzi ya watu, na hili vilevile hupatikana tu ndani ya shida na usafishaji.
kutoka kwa "Kumpenda Mungu Tu Ndiko Kumwamini Mungu Kweli" katika Neno Laonekana katika Mwili
Hali moja ya kazi ya Mungu ni kuwashinda wanadamu wote na kuwapata watu waliochaguliwa kupitia kwa maneno Yake. Hali nyingine ni kuwashinda wana wote wa uasi kupitia kwa maafa mbalimbali. Hii ni sehemu moja ya kazi kubwa ya Mungu. Ni kwa njia hii tu ndio ufalme ulio hapa duniani ambao Mungu anataka unaweza kutimizwa kwa ukamilifu, na hii ni sehemu ya kazi ya Mungu ambayo ni kama dhahabu nzuri.
kutoka kwa "Fumbo la Kupata Mwili (4)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Leo hii, Sishuki tu juu ya taifa la joka kuu jekundu, Mimi pia Nageuza uso Wangu kuelekea ulimwengu mzima, mpaka kila kitu cha mbingu kinatetemeka. Kunayo sehemu hata moja isiyopitia hukumu Yangu? Kunayo sehemu isiyo chini ya mateso Ninayovurumisha kuelekea chini? Kila Ninapoenda Nimesambaza "mbegu za maafa" ya kila aina. Hii ni mojawapo ya njia ambazo Nafanya kazi, na bila shaka ni kitendo cha ukombozi kwa ajili ya mwanadamu, na kile Ninachompa bado ni aina ya upendo.
kutoka kwa "Tamko la Kumi" la Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima katika Neno Laonekana katika Mwili
Kushindwa na Mungu ni kama mashindano ya kareti.
Kila neno la Mungu hugonga eneo letu la ubinadamu, na hutuacha tukiwa tumejawa na huzuni na hofu. Yeye hufichua fikra zetu, hufichua mawazo yetu, na hufichua tabia zetu potovu. Kupitia kwa yale yote sisi husema na kuyatenda, na kila wazo na fikra zetu, asili na kiini zinafunuliwa kwa neno lake, na kutuacha na fedheha, tukitetemeka kwa hofu. Anatueleza kuhusu matendo yetu yote, malengo yetu na nia, na hata tabia potovu ambazo hatujawahi kugundua, na kutufanya tuhisi kwamba tumewekwa hadharani, na hata kuhisi tumeshawishika vikamilifu. Yeye hutuhukumu kwa ajili ya upinzani wetu Kwake, hutuadibu kwa ajili ya kufuru kwetu na kumshutumu kwetu, na kutufanya tuhisi kwamba hatuna thamani machoni pake, na kuwa sisi ni Shetani aishiye. Matumaini yetu yanakufa, na kamwe hatuwezi kumpa madai yasiyo na msingi au kumjaribu, na hata ndoto zetu kupotelea mara moja. Huu ni ukweli ambao hakuna kati yetu anaweza kufikiria, na kwamba hakuna yeyote kati yetu anayeweza kukubali. Kwa muda, akili zetu hukosa msimamo, na hatujui tutakavyoendelea na barabara iliyo mbele wala hatujui jinsi ambavyo tutaendelea katika imani zetu. Inaonekana kama imani yetu imerudi kama ilivyokuwa mwanzoni, na ya kuwa hatujawahi kumpata na kumtambua Yesu Kristo. Kila kitu machoni petu hutushangaza, na kutufanya tuhisi ni kama tumetupwa mbali. Tunasikitishwa, tunahuzunika, na ndani ya mioyo yetu kuna hasira ambayo haiwezi kufichika na pia kuna aibu. Tunajaribu kujieleza, kupata suluhisho, na, hali kadhalika, sisi hujaribu kuendelea kumsubiri Mwokozi Yesu, na kueleza mioyo yetu mbele yake. Ingawa kuna wakati mwingine ambao hatuna kiburi wala unyenyekevu kwa kutazamwa nje, mioyoni mwetu tunateseka na kuwa na hisia ya hasara kuliko vile tumewahi kuwa nayo. Ingawa wakati mwingine tunaonekana ni kama tuna utulivu kwa kutazamwa nje, ndani yetu tunavumilia bahari ya mateso inayopanda na kushuka. Hukumu yake na kuadibu Kwake zimechukua matumaini na ndoto zetu zote, na kutuacha bila tamaa zetu kuu na kutokuwa tayari kuamini kuwa Yeye ndiye Mwokozi wetu anayeweza kutuokoa. Hukumu Yake na kuadibu zimefungua ghuba kubwa kati yetu na Yeye na hakuna aliye tayari hata kuivuka. Hukumu na kuadibu Kwake ni mara ya kwanza kwamba sisi tunateseka kwa kupata shida kubwa hivi na udhalilishaji kiasi kikubwa hivyo. Hukumu na kuadibu Kwake vimetuwezesha kwa ukweli kuthamini heshima ya Mungu na kutovumilia kwake kwa makosa ya binadamu, ikilinganishwa na ambavyo sisi ni watu wa hadhi ya chini na najisi. Hukumu Yake na kuadibu vimetufanya sisi kutambua kwa mara ya kwanza, jinsi ambavyo tuna kiburi na wenye majivuno, na jinsi ambavyo mwanadamu kamwe hawezi kulingana na Mungu, ama kuwa sawa na Mungu. Hukumu Yake na kuadibu Kwake zimetufanya tutumaini kutoishi katika tabia potovu kama hiyo, na zimetufanya tutamani kuacha asili kama hiyo na kiini kama hicho haraka iwezekanavyo, na kamwe tusichukiwe Naye wala tusimchafue moyo. Hukumu na kuadibu kwake vimetufanya tufurahie kutii neno Lake, na hatumo tayari kamwe kwenda kinyume na matayarisho na mipangilio yake. Hukumu na kuadibu Kwake kwa mara nyingine, zimetuwezesha sisi tuwe na tamaa ya kutafuta uzima, na zimetuwezesha kufurahia kumkubali kama Mwokozi wetu.... Sisi tumetoka nje ya kazi ya ushindi, tumetoka kuzimu, tumetoka nje ya bonde la uvuli wa mauti.… Mwenyezi Mungu ametutamalaki, kundi hili la watu! Ameshinda dhidi ya Shetani, na kuwashinda adui zake!
kutoka kwa "Kutazama Kuonekana kwa Mungu katika Hukumu na Kuadibu Kwake" katika Neno Laonekana katika Mwili