Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Jumapili, 10 Februari 2019

Ufahamu wa Kupata Mwili

Mwenyezi Mungu alisema | Sura ya 17. Ufahamu wa Kupata Mwili

Kumjua Mungu kunapaswa kufanywa kupitia kwa kusoma neno la Mungu na kulielewa neno la Mungu. Watu wengine husema: "Sijamwona Mungu mwenye mwili, hivyo nitawezaje kumjua Mungu?" Neno la Mungu kwa kweli ni maonyesho ya tabia ya Mungu. Kutoka kwa neno la Mungu unaweza kuuona upendo wa Mungu kwa wanadamu, wokovu Wake wa wanadamu, na jinsi Anavyowaokoa ... kwa sababu neno la Mungu linaonyeshwa na Mungu ikilinganishwa na Mungu kumtumia mwanadamu kuliandika. Linaonyeshwa na Mungu binafsi. Ni Mungu Mwenyewe Akielezea maneno Yake mwenyewe na sauti Yake ya ndani. Kwa nini tunayaita maneno ya dhati? Kwa sababu hayo hutolewa kutoka ndani kabisa, Akionyesha tabia Yake, mapenzi Yake, mawazo Yake, upendo Wake kwa wanadamu, wokovu Wake wa wanadamu, na matarajio Yake ya wanadamu. Miongoni mwa maneno ya Mungu kuna maneno makali, maneno ya upole na laini, maneno mengine yenye kuzingatia, na kuna maneno mengine ya ufunuo ambayo hayana utu. Ikiwa unayaangalia tu maneno ya ufunuo, unahisi kwamba Mungu ni mkali kabisa. Ikiwa unaangalia upande wa upole na laini tu, Mungu anaonekana kuwa hana mamlaka mengi. Kwa hiyo hupaswi kuelewa nje ya muktadha katika hili. Lazima uliangalie kutoka kila pembe. Wakati mwingine Mungu huzungumza kwa mtazamo mpole na wenye huruma, na watu wanauona upendo wa Mungu kwa wanadamu; wakati mwingine Yeye huzungumza kwa mtazamo mkali, na watu wanaona tabia ya Mungu isiyoweza kukosewa. Mwanadamu ni mchafu kwa njia ya kusikitisha na hastahili kuuona uso wa Mungu, na hastahili kuja mbele za Mungu. Watu kuja mbele za Mungu sasa ni kwa neema ya Mungu tu. Hekima ya Mungu inaweza kuonekana kutokana na jinsi Mungu anavyofanya kazi na maana ya kazi Yake. Hata kama watu hawajakutana na Mungu, bado wataweza kuona mambo haya katika neno la Mungu. Mtu ambaye ana ufahamu wa kweli anapokutana na Kristo, ufahamu wake unaweza kufanana na Wake, lakini wakati mtu ambaye ana ufahamu wa kinadharia tu anakuja katika mawasiliano na Mungu, hauwezi kufananishwa na Yeye. Kipengele hiki cha ukweli ni siri ya kina zaidi, ni ngumu kuelewa. Yafupishe maneno ambayo Mungu anasema juu ya siri ya kupata mwili, yaangalie kutoka pembe mbalimbali, kisha yajadili mambo haya miongoni mwenu. Unaweza kuomba, na kutafakari na kujadiliana sana kuhusu mambo haya. Labda Roho Mtakatifu huwaangazia na kukuwezesha kuyaelewa. Hii ni kwa sababu huna nafasi ya kuwasiliana na Mungu, na lazima utegemee uzoefu kwa njia hii ili kuihisi njia yako kidogo kidogo, ili kufikia ufahamu wa kweli wa Mungu.
Ukweli kuhusu kumjua Kristo na kumjua Mungu Mwenyewe ni wa kina zaidi. Ikiwa watu huweka mkazo juu ya kutafuta kipengele hiki cha ukweli, hata hivyo, ndani yao watakuwa waangavu na thabiti, na watakuwa na njia ya kutembea. Kipengele hiki cha ukweli kinafanana sana na moyo wa mwanadamu. Ikiwa mtu hana ukweli katika kipengele hiki, atakosa nguvu. Kadri mtu alivyo na maarifa zaidi ya kipengele hiki cha ukweli, ndivyo alivyo na nguvu zaidi. Sasa kuna watu wengine ambao husema: Katika uchambuzi wa mwisho, kupata mwili ni nini? Semi hizi zinaweza kuthibitisha kwamba Yeye ni Mungu mwenye mwili? Je! Maneno haya yanaweza kuthibitisha kwamba Yeye ni Mungu Mwenyewe? Ikiwa Hangesema maneno haya bado Angekuwa Mungu Mwenyewe? Au kama Angekuwa Amesema tu baadhi ya maneno, Angeweza kuwa Mungu bado? Ni nini kinachoamua kwamba Yeye ni Mungu? Je, inaamuliwa tu kwa maneno haya? Hili ni swali muhimu. Watu wengine hutambua maneno haya kwa njia visivyo sahihi kama agizo la Roho Mtakatifu, kwamba Alimaliza kutoa maagizo na kuondoka, kwamba Roho Mtakatifu aliacha kufanya kazi, kwamba mwili huu si zaidi ya mwili wa kawaida na mwili wa nyama, kwamba mwili huu hauwezi kuitwa Mungu, badala yake Anaweza kuitwa Mwana wa Adamu, na hawezi kuitwa Mungu. Watu wengine wanaielewa visivyo kwa njia hii. Basi, asili ya kutoelewa huku iko wapi? Ni kwamba watu hawajaelewa kupata mwili vizuri kabisa, na hawajafukua kwa undani. Watu wanaelewa kupata mwili kwa juu juu sana, na wanao ufahamu wa ujuzi kidogo tu. Ikiwa kusema maneno mengi ni sawa na Kwake kuwa Mungu, basi kusema maneno machache tu, badala ya mengi, pia kunamaanisha kwamba yeye ni Mungu? Kwa kweli kusema Kwake maneno machache pia ni maonyesho ya uungu. Je! Yeye ni Mungu? Kazi ambayo Mungu hufanya ina umuhimu mkubwa. Imeishinda mioyo ya wanadamu na kulipata kundi la watu. Je, kazi hiyo haingekuwa imemalizika, ingewezekana kumjua Yeye kama Mungu Mwenyewe? Hapo awali kulikuwa na watu ambao, wakati kazi ilikuwa imefanyika nusu, walifikiri hivi: Kama ninavyoona, kazi hii inapaswa kubadilika. Nani anayeweza kusema kupata mwili kweli ni nini! Je! Huku ni kuwa na mtazamo wa kutoamini kuhusiana na kupata mwili kwa Mungu? Kwamba unaweza kuwa na shaka kuhusu kupata mwili kwa Mungu kunaonyesha kwamba huamini katika kupata mwili, huamini kwamba Yeye ni Mungu, huamini kwamba Ana dutu ya Mungu, na huamini kwamba maneno Aliyosema yametoka kwa Mungu. Hata zaidi huamini kwamba maneno Aliyosema ni ufunuo wa tabia Yake Mwenyewe, na maonyesho ya dutu Yake. Watu wengine walizungumza kwa njia hii: Kama ninavyoona, njia ya Mungu ya kufanya kazi inapaswa kubadilika. Haijulikani kupata mwili ni nini hasa, na labda lazima kuwe na ufafanuzi mwingine kuuhusu. Kuna baadhi ya watu ambao husubiri na kuona, kuona kama kuna sauti yoyote kwa maneno yaliyonenwa na Mungu mwenye mwili Anayeketi pale, iwapo Anasema ukweli, na kama amesema chochote kipya. Ningekuwa na mashine ya eksirei ningeangalia na kuona ikiwa kuna ukweli wowote ndani ya tumbo Lake. Ikiwa hakuna ukweli, na kama Yeye ni mtu, basi nitatoroka kwa haraka, na sitaamini. Ningeangalia na kuona ikiwa Roho wa Mungu anafanya kazi ndani Yake, ikiwa Roho wa Mungu anamsaidia, na kumwongoza katika usemi Wake. Watu wengine wanashuku kwa njia hii, na daima wana wasiwasi kuhusu shida hii katika mioyo yao. Hali hii ipo kwa sababu gani? Si kwa sababu nyingine yoyote ila utambuzi wa juu juu ndani ya mwili. Hawaujui kikamilifu, na hawajafikia kiwango cha juu katika ufahamu wao. Kwa sasa, wanakubali tu kwamba mtu huyu ana Roho wa Mungu. Kusema, hata hivyo, kwamba ndani Yake kuna dutu ya Mungu, tabia ya Mungu, na kusema kwamba Yeye ana kile Mungu alicho na kile Alicho nacho, Ana Mungu mzima, na kusema kwamba Yeye si mwingine ila ni Mungu, ni vigumu kwa watu wengine kuelewa kikamilifu. Maneno hayanaonekani kufanana na mtu katika mambo kadhaa. Kile wanachoona watu na kile wanachoamini sio dutu ya Mungu. Kwa maneno mengine, kile watu wanachoona ni maneno hayo tu na kazi halisi. Watu hufikiri tu kwamba Mungu alifanya sehemu ya kazi, kwamba Mungu mwenye mwili Anaweza tu kufanya sehemu hii ya kazi. Hakuna mtu hata mmoja anayeamini kwamba ingawa kupata mwili sasa kunaonyesha sehemu hii ya kazi, Ana asili yote ya uungu. Hakuna mtu anayefikiria kwa njia hii. Sasa baadhi ya watu husema: "Kumjua Mungu mwenye mwili ni kugumu sana. Ingekuwa ni Roho wa Mungu anayefanya kazi moja kwa moja tungeweza kuelewa kwa urahisi. Tungeweza kuona moja kwa moja nguvu za Mungu na mamlaka ya Mungu katika kazi ya Roho. Kisha ingekuwa rahisi kumjua Mungu. "Je, neno hili linafaa? Sasa Nawauliza swali hivi: "Ni rahisi kumjua Mungu mwenye mwili au ni rahisi kumjua Roho? Ikiwa Mungu mwenye mwili Alifanya kazi kama Yehova, ni yupi Angekuwa rahisi kumwelewa? "Unaweza kusema Wao wote ni Wagumu kuelewa. Kama kungekuwa na njia, Wote wawili wangekuwa rahisi kuelewa. Kama hakungekuwa na ufahamu wa kiroho, wote wawili wangekuwa wagumu kuelewa. Je! Watu pia hawakuelewa kazi na maneno ya kupata mwili mwanzoni? Je! Wote waliyaelewa visivyo? Watu hawakujua kile ambacho Mungu alikuwa Anafanya; hakuna kitu kilichofanana na mawazo ya watu! Je! Watu wote waliibuka na mawazo? Hii inaonyesha kuwa watu hawamjui Mungu mwenye mwili kwa urahisi. Ni vigumu kama kumjua Roho, kwa sababu kazi ya kupata mwili ni maonyesho ya Roho, ni kwamba tu watu wanaweza kuona na kugusa kupata mwili. Ni nini maana ya ndani ya kupata mwili, hata hivyo, na ni nini kusudi la kazi Yake, inamaanisha nini, ni vipengele gani vya tabia Yake inavyowakilisha, na kwa nini Amefunuliwa kwa njia hii, watu huenda hawaelewi, sivyo? Kwamba huelewi inaonyesha kwamba hujui. Roho alikuja kufanya kazi, kusema seti ya maneno, na kisha Akaondoka. Kile ambacho watu wanafanya ni kuyatii na kuyafanya tu, lakini watu wanajua kwa kweli ni nini? Je! Watu wanaweza kujua tabia ya Yehova kutoka kwa maneno haya? Watu wengine husema kwamba Roho ni rahisi kumjua, kwamba Roho alikuja kufanya kazi Akibeba umbo la kweli la Mungu. Je, Yeye ni mgumu kumjua kivipi? Hakika unaijua picha Yake ya nje, lakini unaweza kujua kiini cha Mungu? Sasa Mungu mwenye mwili ni mtu wa kawaida ambaye unahisi ni rahisi kuwasiliana naye. Hata hivyo, wakati asili Yake na tabia Yake vinavyoonyeshwa, watu wanajua mambo hayo kwa urahisi? Je! Watu hukubali kwa urahisi maneno yale ambayo Alisema ambayo hayalingani na mawazo yao? Sasa watu wote wanasema kuwa kumjua Mungu mwenye mwili ni vigumu. Ikiwa Mungu baadaye Angegeuzwa, basi ingekuwa rahisi sana kumjua Mungu. Watu ambao husema hili huweka wajibu wote juu ya Mungu mwenye mwili. Je! Hiyo ndivyo ilivyo kwa kweli? Hata kama Roho angewasili hungeweza kumjua vile vile. Roho aliondoka mara tu baada ya kumaliza kuzungumza na watu, na hakuwaeleza mambo mengi sana, na hakushiriki na kuishi nao kwa njia ya kawaida. Watu hawakuwa na nafasi ya kumjua Mungu kwa namna ya utendaji zaidi. Faida ya kazi ya Mungu mwenye mwili kwa watu ni kubwa sana. Ukweli ambao huwaletea watu ni wa utendaji zaidi. Unawasaidia watu kumwona Mungu wa utendaji Mwenyewe. Hata hivyo, kujua kiini cha kupata mwili na kiini cha Roho ni vigumu vile vile. Hivi pia ni vigumu kujua.
Kumjua Mungu kunamaanisha nini? Kunamaanisha kwamba mtu anajua upeo wa hisia za Mungu, hii ndiyo maana ya kumjua Mungu. Unasema kwamba umemwona Mungu, ilhali huelewi upeo wa hisia za Mungu, huelewi tabia Yake, na wala hujui haki Yake. Huna ufahamu wa rehema Zake, wala hujui Anachokichukia. Hili haliwezi kuitwa ufahamu wa Mungu. Kwa hivyo, watu wengine wanaweza kumfuata Mungu, lakini hawamwamini Mungu hasa. Hii ndiyo tofauti. Ikiwa unamjua, unamwelewa, ikiwa unaweza kuelewa na kushika baadhi ya kile mapenzi Yake ni, na unaujua moyo Wake, basi unaweza kumwamini kwa kweli, unaweza kujisalimisha Kwake kwa kweli, kumpenda kwa kweli, na kumwabudu Yeye kwa kweli. Ikiwa huelewi mambo haya, basi unafuata tu, mtu anayefuata tu na kufuata umati. Hiyo haiwezi kuitwa kujisalimisha kwa kweli, na haiwezi kuitwa ibada ya kweli. Je! Ibada ya kweli inaweza kuzalishwaje? Hakuna watu wowote wanaomwona Mungu na kumjua Mungu ambao hawamwabudu Yeye, ambaye hawamheshimu. Mara tu wanapomwona Mungu wanaogopa. Kwa sasa watu wako katika wakati wa kazi ya Mungu mwenye mwili. Kadri watu wanavyokuwa na ufahamu wa tabia ya Mungu mwenye mwili na wa kile Alicho nacho na kile Alicho, ndivyo watu wengi watakavyovithamini, na ndivyo watakavyomheshimu Mungu. Mara nyingi, ufahamu mdogo unamaanisha kutokuwa waangalifu zaidi, kiasi kwamba Mungu anachukuliwa kama mwanadamu. Watu wataogopa na kutetemeka ikiwa wanamjua Mungu kwa kweli na kumwona kwa hakika. Kwa nini Yohana alisema, "Yeye anayekuja baada yangu, ambaye mimi sistahili kubeba viatu vyake"? Ijapokuwa ufahamu wake ndani ya moyo wake haukuwa wa kina kirefu sana, lakini alijua kwamba Mungu ni wa ajabu. Ni watu wangapi wanaoweza kumcha Mungu sasa? Bila kuijua tabia ya Mungu, mtu anawezaje kumheshimu? Ikiwa watu hawajui kiini cha Kristo, na hawaelewi tabia ya Mungu, hawawezi hata kumwabudu Mungu kwa kweli. Ikiwa watu wanaona tu kuonekana kwa nje kwa kawaida kwa Kristo na hawajui asili Yake, ni rahisi kwa watu kumchukulia Kristo kama mtu wa kawaida. Wanaweza kuchukua mtazamo usio wa heshima Kwake, wanaweza kumdanganya, kumkataa, kutomtii, kutoa hukumu Kwake, na kuwa na maoni. Wanaweza kuchukua neno Lake kama lisilo na maana, wanaweza kuutendea mwili Wake kama wanavyotaka, wanaweza kuwa na mawazo, na wanaweza kukufuru. Ili kutatua masuala haya mtu lazima ajue kiini cha Kristo, uungu wa Kristo. Hiki ndicho kipengele kikuu cha kumjua Mungu; ndicho watu wote wanaoamini katika Mungu wa utendaji wanapaswa kuingia na kufanikisha.
kutoka kwa Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Jumamosi, 9 Februari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Njia ya Huduma ya Kidini lazima Ipigwe Marufuku”

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Njia ya Huduma ya Kidini lazima Ipigwe Marufuku”

Mwenyezi Mungu anasema, “Kuanzia leo, Mungu ataweza kuwafanya watu wasiokuwa na fikira za kidini kuwa watimilifu kwa njia rasmi, ambao wako tayari kuweka pembeni nafsi zao za kale, na ambao wanamtii tu Mungu, pamoja na kuwafanya kuwa watimilifu wale wanaotamani neno la Mungu. Watu hawa wanafaa kusimama na kumhudumia Mungu. Kwake Mungu kunayo na hekima nyingi na isiyoisha. Kazi yake ya kustaajabisha na matamshi yake yenye thamani ni vitu ambavyo vipo ili watu wengi zaidi kuweza kufurahia. Kama ilivyo sasa, vitu hivi vipya haviwezi kukubaliwa na wale walio na fikira za kidini, wanaochukua hali ya ukubwa, na wale ambao hawaweki pembeni nafsi zao za kale. Roho Mtakatifu hana fursa ya kuwafanya watu kama hao kuwa watimilifu. Kama mtu hana hamu ya kutii, na hana kiu cha neno la Mungu, basi mtu huyo hataweza kupokea mambo mapya. Wataendelea tu kuasi zaidi na zaidi, kuwa wajanja zaidi na zaidi, na hatimaye kujipata kwenye njia mbaya. Katika kazi ya Mungu ya sasa, Atawainua watu zaidi wanaompenda Yeye kwa kweli na wanaoweza kukubali mwangaza mpya. Na Atakatiza kabisa maafisa wa kidini wanaoonyesha ukubwa wao. Hataki mtu hata mmoja anayekataa mabadiliko.”

Ijumaa, 8 Februari 2019

Imani Tatu katika Mungu wa Vitendo

Sura ya 16. Imani Tatu katika Mungu wa Vitendo

Ndani ya familia ya Mungu, kuna imani kadhaa tofauti katika Mungu; imani hizi tofauti lazima zitambulishwe ili kuona wewe ni wa gani.
Na imani ya aina ya kwanza, ambayo pia ni aina bora zaidi, mtu huyo ana uwezo wa kuyaamini maneno ya Mungu katika vitu vyote; ana uwezo wa kukubali ufichuzi wote wa Mungu, ushugulikiaji, na upogoaji; yeye ni mwagalifu kwa mapenzi ya Mungu, hupenda, ni mwaminifu kwa, na humwabudu Mungu, na ako tayari kutenda ukweli. Imani kama hiyo huzaa maisha, na inawezesha mtu kupata mabadiliko katika tabia na kupatwa na Mungu.
Na imani ya aina ya pili, mtu huyo anamwamini Mungu kwa kiasi, lakini pia ni mwenye tuhumu kwa kiasi. Wakati kazi ya Mungu hairidhiani na yeye, angefanya ulinganishi katika moyo wake, akiwa na shaka kama Mungu Anapaswa kuwa akifanya vitu kama hivyo. Mara kwa mara anamtuhumu Mungu, kwa hivyo ana uwezo tu wa kumtii Mungu kwa kiasi, na hana uwezo wa kumtii Mungu katika vitu vingine; anaweza kulitii lile ambalo analiamini ni sawa, lakini ana mawazo yake mwenyewe anapokabiliwa na vitu ambavyo anahisi si sawa, na migongano katika moyo wake, na anakataa kuyatekeleza. Hili pia ni aina ya imani. Kimo cha watu siku hizi ni hasa kama hiki, wao wana uwezo tu wa kutii kile wanachohisi kuwa sawa, wao hawana uwezo wa kutii kile wanachohisi si sawa, na hawatatekeleza kile ambacho hawako tayari kufanya. Kadhalika, wakati mwingine hali ikiwa, wana shauku na Mungu, wakihisi kwamba wanapaswa kuwa waangalifu kwa mzigo wa Mungu, hivyo wanatimiza wajibu wao; au wakati mwingine wanashughulishwa na ushirika, wanapata Mungu kuwa wa kupendeka kabisa, na sasa tu ndio wenye imani katika Mungu kwa kiasi fulani. Hasa, imani yao katika Mungu ni tu kufuata umati; hawana upendo kwa Mungu, wala si waangalifu kwa Mungu, wakati bila shaka hawamtii na hawamwabudu Mungu kwa kweli. Kwa watu walio na imani kama hii katika Mungu, wako tu na kiasi cha wastani cha upendo, uangalifu, na utiifu kwa Mungu, kwa muda fulani, na inafanyika tu wakati Roho Mtakatifu hasa Anasonga, wakati Roho Mtakatifu anafanya kazi Yake. Wakati wako katika hali mbaya, au wakati wanachanganywa na wengine, wakati wao ni dhaifu na wamekata tamaa, vitu hivi vimeenda, vimetokomea, wakati wao wenyewe hawana habari jinsi hilo limekuja kupita. Hawana uwezo tena wa kumpenda Mungu hata wakitaka, hawana motisha ya kutenda maneno ya Mungu tena, na kisha wanaona kazi ya Mungu kama ya desturi sana, ya kawaida sana; hata kama wao hawana tuhuma tena, wao hawana ari yoyote tena. Kimo cha watu wengi zaidi kiko katika hatua hii, na hii ndiyo aina ya pili ya imani.
Na aina ya tatu ya imani, mtu hana uelewa wa Mungu mwenye mwili, kwake Yeye hujitokeza tu kama mtu wa kawaida, na hakuna tofauti kubwa inaweza kutambulishwa. Kwa hivyo, anamchukulia Mungu mwenye mwili kama tu mtu wa kawaida lakini mwenye cheo cha heshima, ana uwezo wa kufuatana na Mungu na kusema kitu kizuri, na pia ana uwezo wa kuandamana katika imani, lakini imani hii si imani halisi. Ana uwezo wa kufuatana na mambo ya upuuzi mara moja moja, lakini hakuna upendo kwa Mungu katika mtu wa aina hii—upendo si kujali kuhusu mwili lakini utiifu wa kweli katika kazi ya mtu na katika kutimiza wajibu wa mtu, kuwa mwangalifu kwa Mungu na kumcha Mungu. Upendo kwa Mungu ni kitu ambacho mtu aliye na uzoefu mkubwa tu anaweza kutangaza, si kitu ambacho mtu anaweza kusema kwa kupitia tu, kuona kwamba mtu ametekwa na hisia kali hivyo kusema kwamba huyu na huyu humpenda Mungu sana. Ama kusema kwamba watu kutoka dhehebu fulani humpenda Mungu kwa kweli. Huu ni upuuzi. Mtu kama huyu hawezi kukubali na kutii kwa urahisi kunapokuja kwa mambo ya upuuzi, na anapokabiliwa na mambo ya muhimu yanayohusiana na ukweli, hawezi kutii tu, na pia ana mawazo yake mwenyewe, hata anakuwa na tuhuma kuhusu Mungu. Watu kama hawa pia wako katika walio wengi. Wao ni wenye tuhuma kila wakati kuhusu Mungu: Je, huyu ni Mungu? Je, ni kwa nini Yeye hafanani na Mungu? Baadhi ya mambo Alivyosema labda yameelekezwa na Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu alimwelekeleza kusema mambo fulani, na kufanya vitu fulani. …Imani ya watu kama hawa ni ya kusikitisha zaidi.
Kiwango cha imani ya mtu katika Mungu, utiifu kwa Mungu, upendo, uangalifu, na uchaji kwa Mungu, kinatambulishwa hasa na yafuatayo:
Kwanza, kina msingi katika ikiwa mtu huyo hupenda ukweli. Kama unapenda ukweli basi unaweza kuendelea kuufuatilia zaidi, kisha unaweza kulenga kuwa na uelewa wa ukweli, wa maneno ya Mungu, wa kazi ya Mungu, wa umuhimu wa kupata mwili kwa Mungu, wa tabia ya Mungu, na uelewa wa Mungu una msingi hasa katika hiki kitu kimoja. Kadiri Unavyoweza kuelewa Mungu zaidi ndivyo unavyoweza kumtambua zaidi; kadiri unavyoweza kumwelewa Mungu zaidi ndivyo unavyoweza kumfuata bila kuyumbayumba. Hiyo ni, uelewa wa Mungu una msingi katika kufuatilia ukweli.
Pili, kina msingi katika uelewa wa mtu huyo wa Mungu mwenye mwili, hiyo ni muhimu. Bila uelewa wa Mungu wa vitendo, mazungumzo ya kumtii Mungu, kumpenda Mungu, kushuhudia Mungu, na kumhudumia Mungu yote ni maneno matupu. Vitu kama hivi haviwezi tu kufikiwa.
Tatu, kina msingi katika ubinadamu wa mtu huyo, lakini hili si halisi. Kwa sababu, baadhi ya watu wana ubinadamu mzuri, wao ni watu wazuri, lakini wao hawapendi ukweli. Kama wao hawana uelewa kabisa wa Mungu mwenye mwili, basi imani yao haiwezi kusiama, na wakati mwingine nia zao nzuri bila kujua husababisha madakizo. Je, unaweza kusema kwamba wao ni watu ambao wanamwamini Mungu kwa kweli? Wao ni wenye shauku, ni wa asili nzuri, na hufanya mambo fulani mazuri, lakini haya ni tabia nzuri tu ya nje, haya ni sura ya juu juu, haya hayaonyeshi kwamba imani yao ni halisi. Ukisema kwamba kwa kweli unamwamini Mungu, kweli unampenda Mungu, lazima uwe na uwezo wa kusema kwa nini unampenda Mungu, upendo wako kwa Mungu una msingi kwa nini, kwa nini unamwamini Yeye, kama wewe unaufuata umati tu ama unamwamini Yeye kwa sababu unaweza kumwona kwa kweli kama Mungu, imani na upendo wako kwa Mungu yana msingi katika ukweli upi: Haya lazima yategemezwe kwa misingi. Baadhi ya watu hupenda kusema kwamba wanamwamini Mungu kwa kweli na wanampenda Mungu, lakini wakati mtu anatamani kuwasiliana nao ukweli kwa uzito, hawana kitu cha kusema. Nimesikia watu wengi wakisema: “Mimi husikiza chochote ambacho Mungu husema, naamini yote ambayo Mungu husema, kwa njia yoyote ambayo Yeye huyasema. Sina mawazo yangu mwenyewe bila kujali kile Mungu husema, sina mawazo yangu mwenyewe bila kujali kile Mungu hufanya.” Je, wewe kweli ni mtu anayempenda Mungu kwa sababu tu umesema mambo kama haya? Lazima uwe na uzoefu halisi, lazima uwe na uwezo wa kuongea kuhusu uelewa halisi wa Mungu mwenye mwili. Pia, ni nini kiini cha Mungu, ni vitu vipi ambavyo watu huona vigumu kumtii Mungu katika, ni vitu vipi ambavyo watu wanaweza kumtii Mungu katika, wanamtii Mungu kwa kiasi gani, ni vitu vipi ambavyo huna uwezo wa kumtii Mungu katika, unatatua vipi mawazo yako kuhusu Mungu, unapanua vipi uelewa wako wa Mungu polepole? Kama unakosa uzoefu kama huo, basi huna mapenzi ya kweli kwa Mungu. Baadhi ya watu wana furaha hasa wanapoona kufika kwa Mungu, wanampokea kwa ukarimu, na kisha wanalia Mungu Anapoondoka. Watu wengine hufikiri kwamba hili ni onyesho la upendo wake kwa Mungu, lakini hili kweli linaweza kuonyesha kwamba anampenda Mungu? Hili linaweza kuonyesha tu kwamba anao moyo wenye ari, lakini mtu hawezi kusema kwamba matendo na maonyesho yake ni upendo kwa Mungu, kwamba ni imani ya kweli. Baadhi ya watu hutoa pesa kiasi, lakini hilo ni upendo kwa Mungu? Ama unaenda haraka kumwaga gilasi ya maji wakati unaambiwa, lakini hilo ni utiifu wa kweli? Kadhalika, watu wengine husema: “Nilimwamini Mungu baada ya mimi kusoma maneno ya Mungu, niliamini katika kupata mwili kwa Mungu, sina shaka baada ya mimi kumwona Mungu katika mwili wa kawaida.” Je, hili linaweza kuitwa imani ya kweli? Je, umekuwa na ushughulikaji na Mungu? Je, umejihusisha na Yeye? Je, unajua tabia Yake? Je, unajua ni nini Yeye hupenda? Je, unajua vitu unafanya ambavyo vinaikosea tabia Yake? Je, unajua upotovu ndani yako ambao Yeye huchukia? Je, unajua watu ambao Ameleta tabia Yake yenye haki kwao? Je, unajua ni watu wagani Yeye huchukia? Je, unajua ni masuala yapi unayo ambayo Yeye huchukia zaidi? Kama hujui vitu vyovyote kama hivi, linaonyesha kwamba kwa kweli huna uelewa wa Mungu. Huwezi kusema kwamba unamwamini Mungu kwa kweli, huwezi kusema kwamba unamtii Mungu kabisa, na bila shaka huwezi kusema kwamba unafanya vitu kulingana na mapenzi ya Mungu, kwamba unampenda Mungu, unamtii Mungu, ama unamwelewa Mungu. Unaweza kusema tu, kuhusu jambo hili, unayaelewa mapenzi Yake, unajua ni nini Yeye hupenda, kwamba unatenda kulingana na mapenzi ya Mungu katika jambo hili, kwamba unatenda kulingana na ukweli, kwamba unamtii katika jambo hili. Je, wewe ni mtu mtiifu kwa Mungu kwa sababu umemtii katika jambo hili tu? Huwezi kusema hilo, na kusema kwamba mtu humpenda Mungu kwa kuweka msingi tu kwa kitu cha juujuu, hilo ni kosa kubwa. Ukweli kwamba ulitenda kitu kizuri, ama kwamba umemjali Mungu hasa, huonyesha tu kwamba wewe ni mtu mwema, lakini hauonyeshi kwamba wewe ni mwangalifu kwa mapenzi ya Mungu. Bila shaka, upendo wa Mungu na kuwa mwangalifu kwa mapenzi ya Mungu yamejengwa juu ya msingi wa ubinadamu, na hakuwezi kuwa na upendo wa Mungu bila ubinadamu, kwa hivyo kila mmoja wenu lazima ajichunguze na aangalie mahali alipo. Baadhi ya watu hufikiri kwamba wao wako karibu hapo, lakini hili si lenye uhalisi; ilhali baadhi ya watu huenda kwa kiwangi kilichokithiri na hufikiri kwamba hakuna kitu kizuri kuwahusu, kwamba hawawezi kuachwa, na huu ni mtazamo hasi. Baadhi ya watu hufikiri kwamba hakuna mazuri ndani yao, na baadhi ya watu hujifafanua kama mtu anayempenda Mungu. Wao wako katika upande wa kushoto kabisa au katika upande wa kulia kabisa; huu ndio uhalisi wa watu hawa, ambao unaonyesha kwamba wao bado hawako katika njia sawa. Wao wanapaswa kuendelea kujitahidi kuwa dhahiri kuhusu ukweli, na kuingia katika uhalisi, ili kufuata mapenzi ya Mungu.
Soma Zaidi: Asili ya Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Alhamisi, 7 Februari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Ahadi kwa Wale Ambao Wamekamilishwa”

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Ahadi kwa Wale Ambao Wamekamilishwa”

Mwenyezi Mungu anasema, “Wale watakaokamilishwa na Mungu ni wale watakaopokea baraka za Mungu na urithi Wake. Yaani, wanasikia na kuelewa kile Mungu Alicho nacho na Alicho, ili kiwe kile ambacho walicho nacho ndani yao; wanayo maneno yote ya Mungu ndani yao; haijalishi ni vipi nafsi ya Mungu ilivyo, mnaweza kusikia na kuelewa kila kitu Anachokuambia vile kilivyo, na hivyo kuishi kwa kudhihirisha ukweli. Huyu ndiye aina ya binadamu aliyekamilishwa na Mungu na aliyepatwa na Mungu.”

Jumatano, 6 Februari 2019

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VII” Sehemu ya Pili

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VII” Sehemu ya Pili

Mwenyezi Mungu anasema, “Mungu ni Bwana wa kanuni zinazoudhibiti ulimwengu, Anadhibiti kanuni zinazoongoza kuishi kwa vitu vyote, na pia Anadhibiti ulimwengu na vitu vyote kiasi kwamba vinaweza kuishi pamoja; Anaifanya ili kwamba visikwishe au kutoweka ili kwamba binadamu aendelee kuishi, binadamu anaweza kuishi katika mazingira hayo kupitia uongozi wa Mungu. Kanuni hizi zinazoongoza vitu vyote zipo chini ya utawala wa Mungu, na binadamu hawawezi kuingilia na hawawezi kuzibadilisha; ni Mungu Mwenyewe pekee ndiye Anajua kanuni hizi na ni Yeye pekee ndiye anazisimamia.”

Jumanne, 5 Februari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa “Maonyo Matatu” | How to Be a Loyal Servant of God

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa “Maonyo Matatu” | How to Be a Loyal Servant of God

Mwenyezi Mungu anasema, “Kama muumini wa Mungu, hufai kuwa watiifu kwa yeyote mwingine isipokuwa Yeye katika mambo yote na mjilinganishe na moyo Wake katika mambo yote. Hata hivyo, ingawa wote huelewa mafundisho haya, ukweli huu wa kimsingi ulio wazi kabisa kwa binadamu hauwezi kuonekana kuwa kujumuishwa kwao kikamilifu, kutokana na ugumu wao, kama vile hali yao ya kutojua, upuzi, au ufisadi. Kwa hivyo, kabla ya kuuamua mwisho wenu, Ninafaa kuwaambia kwanza baadhi ya mambo, ambayo ni yenye umuhimu mkubwa sana kwenu. ... Katika maisha yenu, Naona mengi ambayo mnafanya ambayo hayana uhusiano na ukweli, kwa hivyo Nawaambia moja kwa moja muwe watumishi wa ukweli na wala si kutawaliwa na maovu na ubaya. Msikanyage ukweli na kuchafua sehemu yoyote ya nyumba ya Mungu. Hili ndilo onyo Langu kwenu.”

Jumatatu, 4 Februari 2019

Wale Wanaopenda Ukweli Wana Njia ya Kufuata

Sura ya 10. Wale Wanaopenda Ukweli Wana Njia ya Kufuata

1. Kama hali ya Watu Ni Ya Kawaida Inategemea na Kama Wanapenda Ukweli au La
Mwenyezi Mungu alisema, Watu wengi wameibua suala lifuatalo: Baada ya ushirika wa juu, wanahisi wazi kabisa, wanakuwa na nguvu zaidi, na hawana hisia hasi—lakini hali kama hiyo inabaki tu kwa karibu siku kumi, ambapo baadaye hawawezi kudumisha hali ya kawaida. Suala ni nini? Je mmewahi kujiuliza kinachosababisha hili? Mbona hali zenu ni nzuri sana katika siku hizo takriban kumi za kwanza? Wengine wanasema kuwa hili ni tokeo la kutolenga ukweli. Lakini hivyo ungeweza vipi kufikia kiwango hiki cha kawaida baada ya kusikia ushirika? Mbona ulikuwa na furaha sana baada ya kuusikia ukweli? Wengine wanasema ni kwa sababu ya kazi ya Roho Mtakatifu. Mbona basi kazi ya Roho Mtakatifu inakoma baada ya takriban siku kumi? Wengine husema ni kwa sababu wanakuwa wazembe na kuacha kusonga mbele na juu. Mbona basi hili linafanyika hata wakati watu wanapojaribu kufanya maendeleo? Mbona Roho Mtakatifu pia hafanyi kazi? Je, hukuwa unajaribu kusonga mbele na juu? Basi mbona Roho Mtakatifu hayuko kazini? Sababu ambazo watu hutoa haziko sambamba na hali ya kweli. Hapa, lazima tuibue hoja ifuatayo: Kama Roho Mtakatifu yuko kazini au la, ushirikiano wa watu binafsi hauwezi kupuuzwa. Watu walio wazi kuhusu ukweli na wanapenda ukweli kila wakati watakuwa na uwezo wa kubaki katika hali ya kawaida, bila kujali kama Roho Mtakatifu yuko kazini ama hapana. Kwa wale wasiopenda ukweli—hata kama ukweli hasa ni wazi kwao na hata kama Roho Mtakatifu anafanya kazi sana—kuna upeo kwa ukweli ambao wanaweza kuweka katika vitendo na kiwango cha muda ambao wanaweza kutenda. Mbali na wakati huo, hawafanyi chochote zaidi ya kudhihirisha asili yao wenyewe na maslahi yao wenyewe. Ipasavyo, kama hali ya mtu itafikia kiwango cha kawaida ama hapana na kama atauweka ukweli katika matendo ama hapana haitegemei tu kama Roho Mtakatifu yuko kazini au hapana, wala haiamuliwi tu na kama yuko wazi kuhusu ukweli ama hapana, ila hutegemea kama yuko tayari kuuweka ukweli katika matendo ama hapana na kama anapenda ukweli ama hapana.
Kwa kawaida, mtu husikia ukweli na, kwa muda, kila kitu huhisi kuwa kawaida kabisa kwake; katika muda huo wa kawaida, ukweli unaziinua hali zako kuwa kawaida. Unakufanya kujua asili yako potovu; moyo wako una furaha na unakuwa huru na hali yako inabadilika kuwa bora. Lakini baada ya muda, jambo laweza kukuchanganya; ukweli ulio ndani yako unakuwa usioonekana na bila kujua unaufanya ukweli huo kama jambo lisilo muhimu sana kwako; hujaribu kumtafuta Mungu katika matendo yako, unatenda kila kitu kwa mapenzi yako mwenyewe na huna nia ya kutenda ukweli kabisa. Wakati unapopita, unapoteza ukweli uliokuwa nao. Daima unadhihirisha asili yako mwenyewe, ukikosa kumpa Roho Mtakatifu nafasi ya kufanya kazi ndani mwako; hutafuti nia ya Mungu kamwe; hata unapomkaribia Mungu, unapitia tu katika mizunguko. Punde tu unapogundua ukweli wa ugonjwa wako, moyo wako uko mbali sana na Mungu; umemkataa Mungu kwa vitu vingi na kutamka kufuru nyingi. Bado kuna ukombozi kwa wale ambao hawajaenda mbali sana katika njia hii, lakini kwa wale ambao wameenda mbali sana hata kumkufuru Mungu na kujiweka wenyewe dhidi ya Mungu, wakipigania cheo, na chakula na mavazi, hakuna ukombozi. Kusudi la ushurika wazi kuhusu ukweli ni ili kuwafanya watu kutenda ukweli na kubadilisha tabia yao, sio tu kuwafanya wafurahi. Kama unaelewa ukweli lakini hauuweki katika matendo, basi ushirika kuhusu ukweli na ufahamu wa ukweli hautakuwa na maana yoyote. Iwapo unaelewa ukweli lakini hauuweki katika matendo, utapoteza nafasi yako ya kupata ukweli na kupoteza nafasizyote za kuokolewa. Ukiuweka ukweli unaoelewa katika matendo, utapata ukweli wa ndani zaidi; utapata wokovu wa Mungu; utapata kupata nuru, mwangaza na uongozi wa Roho Mtakatifu. Wengi hulalamika tu kuwa Roho Mtakatifu kamwe hawapi nuru, lakini hawagundui kuwa kimsingi hawauweki ukweli katika matendo. Kwa hivyo, hali zao hazitawahi kupata ukawaida na hawatawahi kuyaelewa mapenzi ya Mungu.
2. Unahitaji Tu Kutenda Ukweli na Njia Itafunguka Mbele Yako
Wengine husema kuwa shida zao hazitatatuliwa kwa kutenda ukweli. Wengine huamini kuwa ukweli hauwezi kutatua kikamilifu tabiapotovu za watu. Ukweli ni kwamba shida zote za watu zaweza kutatuliwa; cha muhimu ni kama watu wanaweza kutenda kulingana na ukweli au hapana. Shida zenu za sasa sio saratani ama magonjwa yasiotibika; kama mnaweza kuweka ukweli katika matendo, shida hizi zote zaweza kubadilishwa, ikitegemea kama unaweza kutenda kulingana na ukweli ama hapana. Kama unatembea katika njia sawa, utafanikiwa; kama unatembea katika njia mbaya, utakuwa umemalizika. Kwa mfano, watu wengine hufanya kazi zao bila kufikiria kuhusu jinsi ya kufanya vitu kwa njia ya faida kwa kazi ama kama jinsi wanavyofanya vitu inapatana na mapenzi ya Mungu; kama tokeo, wanafanya mabo mengi ambayo Mungu anachukia. Kama wangetenda kulingana na ukweli katika kila jambo, je hawangekuwa watu ambao wanaupendeza moyo wa Mungu? Watu wengine wanajua ukweli lakini hawauweki katika matendo, wakiamini kuwa ukweli ni hili tu na sio kitu kingine zaidi. Wanaamini kuwa hauwezi kutatua mapenzi yao wenyewe na upotovu wao. Je, mtu wa aina hii sio mmwenye mzaha? Je, yeye sio mpumbavu? Je hajioni mwenyewe kuwa werevu? Watu wakitenda kulingana na ukweli, tabia yao potovu itabadilishwa; watu wakimwamini na kumtumikia Mungu kulingana na tabia zao asili, hakuna kati yao atakayebadilishiwa tabia yake. Watu wengine wanajipata katika shughuli zao wenyewe siku nzima na wanakosa kuchunguza ama kutenda ukweli unaopatikana tayari. Utendaji huu ni wa kipumbavu sana; watu wa aina hii ni watesekaji kiasili, kuwa na baraka lakini hawaifurahii! Njia ipo, kinachofaa kufanywa tu ni wewe kuiweka katika matendo. Kama umeamua kuuweka ukweli katika matendo, unyonge wako na dosari mbaya zinaweza kubadilishwa, lakini lazima kila wakati uchukue tahadhari na kuwa makini na kupitia ugumu zaidi. Kumwamini Mungu kunahitaji moyo wenye busara—unaweza kumwamini Mungu vizuri ukichukua namna hii ya kawaida?
Watu wengine wanajihami tu na ukweli fulani kwa wakati wa dharura ama kujitelekeza wenyewe na kuwasaidia wengine, sio kutatua shida zao wenyewe; tunawaita “watu wasio na ubinafsi.” Wanawaona wengine kama vikaragosi wa ukweli na wenyewe kama mabwana wa ukweli, wakiwafunza wengine kuushikilia ukweli na wasiwe wasiojihususha, ilhali wao wenyewe ni watazamaji kando kando mwa uwanja—hao ni watu wa aina gani? Wakiwa wamejihami na baadhi ya maneno ya ukweli ili kuwahubiria wengine tu, wakikosa kufanya chochote kujizuia kutokana na kuangamia kwao wenyewe—inasikitishaje! Kama maneno yao yanaweza kuwasaidia wengine, mbona wasijisaidie wenyewe? Tunafaa kuwaita wanafiki wasio na ukweli. Wanatoa maneno ya ukweli kwa wengine na kuwaambia wengine wayaweke katika matendo, lakini hawafanyi juhudi yoyote kuyatenda wenyewe—je sio wa kudharauliwa? Kwa hakika hawawezi kulifanya wenyewe, ilhali wanawalazimisha wengine kuweka maneno ya ukweli katika matendo—hii ni njia ya ukatili iliyoje! Hawatumii ukweli kuwasaidia wengine; hawawatolei wengine kwa moyo wa upendo wa mama; wanawadanyanya tu watu na kuwapotosha watu. Hili likiendelea—na kila mtu akipitisha maneno ya ukweli kwa anayefuata—je kila mmoja mwishowe hatakuwa na uelewa tu wa maandishi ya ukweli wakikosa uwezo wa kuyatenda? Watu wa aina hii wanawezaje kubadilishwa? Hawazitambui shida zao wenyewe kabisa; kutaweza vipi kuwa na njia kwa ajili yao?
Kila tatizo lina njia ya kutatuliwa; kwa kila tatizo kila wakati kutakuwa na ukweli ufaao kushauri ili kukupa njia ya kuendelea mbele na kukuwezesha kubadilika. Hata kama mabadiliko hayatafanyika mara moja, sasa unaweza kuitambua hali yako. Kama kweli hizi hazingeweza kutatua matatizo ya watu, basi Mungu hatakuwa Amenena bure? Kwa hivyo, kama uko tayari kuuweka ukweli katika matendo, kila wakati utakua na njia ya kufuata.

Jumamosi, 2 Februari 2019

Namna ya Kumridhisha Mungu katikati ya Majaribu

Sura ya 59. Namna ya Kumridhisha Mungu katikati ya Majaribu

Ninaibua maswali machache kwa tafakari yenu: Tangu mara ya mwisho tuliposema kwamba kutakuwa na miaka saba mingine ya majaribu makubwa, iwe ni kwa dhiki au majanga, je, mmegundua kusudi la Mungu kupitia kwa hayo? Ni asili gani ya binadamu mnaweza kuona katika mijibizo na mitazamo ya watu kwa miaka hii saba ya majaribu? Hili litachanganuliwa vipi? Fikirieni hilo. Ninazungumzia asili ya binadamu katika kila ushirika, kufikia chanzo, kuchanganua asili ya binadamu, na kuchanganua kiini. Ni juu yenu basi kuwasiliana ufahamu wenu kuhusu hizi mada.

Mnapaswa kuelewa kusudi la Mungu na ni lazima muijue asili ya binadamu kupitia hii miaka saba ya majaribu. Kwa hakika, kila sentensi ya Mungu ina kusudi Lake, ambamo mmefichwa ukweli. Bila kujali ni suala gani linafanyiwa ushirika, au ni ukweli gani unaoenyeshwa, ndani yake mna njia ambayo watu wanapaswa kupitia, matakwa ya Mungu kwa watu, na kusudi la Mungu kwa wanaomtafuta. Katika haya mazungumzo ya majaribu, dhiki, na hatimaye mateso, matakwa kwa watu na kusudi la Mungu pia vimo ndani. Watu, bila shaka, wanaonyesha hisia kwa mitazamo yao, kwa kuwa watu hawajaundwa kwa mbao; wako hai, na wanaonyesha hisia kwa kila kitu. Je, kuna maana kuchanganua ni hali gani za asili ya binadamu zinawakilishwa katika hisia za watu? Ina maana kushiriki kuihusu? Uchanganuzi utasaidia watu kuliona hilo wazi, kulijua wao wenyewe, na kujua vyema kabisa mioyoni mwao ili kwamba hatimaye wawe na njia mwafaka ya kuchagua. Ikiwa mtu amekanganyikiwa na hajui kusudi la Mungu, haelewi ukweli, na ana ufahamu mdogo kuhusu matakwa ya Mungu kwake na wajibu anaopaswa kutekeleza, au njia gani anapaswa kutembea, pengine mtu wa aina hii hatasimama imara. Kwa hivyo, inapaswa kujulikana ni njia gani inapaswa kutumiwa baadaye wakati wa majaribu mbalimbali.

Kila wakati majaribu ya miaka saba yanapotajwa, kuna watu wengi wanaohisi vibaya sana na kuvunjika moyo kusiko kwa kawida, na kuna watu wengine ambao hulalamika, na kuna mchanganyiko wa hisia. Ni dhahiri kutokana na hizi hisia kwamba watu sasa wanahitaji majaribu haya, wanahitaji aina hii ya dhiki na utakasaji. Watu humwamini Mungu kwa nia ya kutaka kupata baraka siku zijazo. Watu wote wana kusudi na tumaini hili. Hata hivyo, upotovu ndani ya asili ya binadamu ni lazima uondolewe kupit majaribu. Katika hali yoyote usiyoipita, ni katika hizi hali ambamo ni lazima usafishwe—huu ni mpango wa Mungu. Mungu anakutengenezea mazingira, Akikulazimisha usafishwe hapo ili ujue upotovu wako mwenyewe. Hatimaye unafika hatua ambapo unaona heri kufa na kuziacha njama na tamaa zako, na kutii mamlaka na mipango ya Mungu.

Hivyo ikiwa watu hawana miaka kadhaa ya usafishaji, ikiwa hawana kiwango fulani cha mateso, hawataweza kuepuka utumwa wa upotovu wa mwili katika mawazo na mioyo yao. Katika hali zozote zile bado ungali mtumwa wa Shetani, katika hali zozote bado ungali na tamaa zako mwenyewe, matakwa yako mwenyewe—ni katika hali hizi ambamo unapaswa kuteseka. Mafunzo yanaweza kupatikana tu katika mateso, yaani, kuweza kupata ukweli, na kuelewa kusudi la Mungu. Kwa kweli, ukweli mwingi unafahamika katika uzoefu wa majaribu makali. Hakuna asemaye kuwa kusudi la Mungu linajulikana, kwamba uweza na busara Yake vinafahamika, kwamba tabia ya haki ya Mungu inaonekana katika mazingira ya utulivu au katika hali zinazofaa. Hilo haliwezekani!

Mungu ametayarisha mazingira mwafaka ambamo Anawafanya watu kuwa wakamilifu, ila haijulikani kwa yeyote ni kwa nini Mungu anaweza kutaka kuwajaribu watu, kuwatakasa. Nyinyi nyote mnasema, “Mungu anawependaje wanadamu kwamba Anaweza kutayarisha miaka saba ya majaribu kuwatakasa watu na kuwafanya safi! Ni mvumilivu kiasi gani! Ni mwenye kuonyesha huruma kiasi gani!” Haina haja uyaseme haya, kila mmoja anaelewa mafundisho, lakini kwa hakika hakuna yeyote anayeifahamu hali halisi Je, miaka saba ya Mungu ya majaribu, miaka saba ya kazi ni ya nini? Bila shaka, inahitajika ili kwamba kazi Yake ifanyike. Hata bila kukuokoa, bado kuna upendo, sawa? Anapokuokoa, unasema, “Haya ni mapenzi aliyonayo Mungu kwetu, hii ni huruma Yake.” Je, Asingekuwa ametayarisha hii miaka saba ya majaribu, na kukamilisha kazi mara moja, bado kusingekuwepo upendo? Je, ingelikuwa miaka miwili ya majaribu, au mwaka mmoja, au siku ingalifika mara moja, je, hayo yasingekuwa mapenzi na huruma? Si kama unavyodhani: Miaka saba ya majaribu ni utakaso wa Mungu kwetu, ni kiwango Anachotupenda: ni lazima tutii. Unasema haya wakati tu hakuna njia nyingine. Hili linadhihirisha nini? Linadhihirisha uhasi, linadhihirisha lawama, na linadhihirisha kukosa njia mbadala na kukata tamaa. Mungu alisema kwamba kutakuwa na miaka saba mingine. Wacha iwe miaka saba basi. Kisha unakurupuka na kusema maneno mazuri: Mungu, Unatupenda; Mungu, ni kwa ajili ya kututakasa. Bila miaka saba ya majaribu, je, huo usingelikuwa mwisho wetu? Kusingelikuwa na fursa. Watu wengine wanatamani kubarikiwa sasa hivi. Hiyo inaweza kuwa faida halisi! Mtu kama huyo hajali kitu kingine chochote kile. Mtu kama huyu hafai hata kwa senti moja. Kuna kazi ya vitendo katika hii miaka saba. Je, haijasemwa awali kwamba maneno mengine ni njia, lakini vilevile ni ukweli? Hakuna kipengele ambacho ni maneno tu bila matendo. Kila kipengele kina dhima. Aidha, kama aionavyo mwanadamu, takribani kila kipengele kina njia, lakini njia hii si ya kukurairai, si ya kukudanganya. Badala yake ni mazingira ya kweli, hali halisi Hakuna njia mwafaka kuliko hii. Baada ya kusikia maneno haya, watu wengine hufikiri: Ikiwa ni kama usemavyo, hii miaka saba inapoisha, ni nani anaweza kutambua umesalia muda kiasi gani! Kutokana na mijibizo ya watu inaonekana kuwa asili ya binadamu imewekwa kwa namna kwamba baada ya kukumbana na majaribu ya mateso, kupokea uchungu mwilini, anataka kuuepuka na kuukataa. Hakuna hata mtu mmoja hujitokeza na kuchukua hatua ya kudai: Mungu, nipe majaribu fulani ya kuteseka, nipatie dhiki fulani. Mungu, nipatie taabu zaidi. Hili linadhihirisha kuwa kiasilia watu hawapendi ukweli. Iwe ni kusudi la Mungu au la, au inafaidi watu vipi, haijalishi ni nzuri kiasi gani, watu wote hukataa hali yoyote inayoiletea miili yao machungu au ile isiyoafiki matamanio yao. Kuna watu wasemao: “Sipingi. Nilifanya uamuzi zamani kuyatoa maisha yangu yote kwa Mungu. Nina furaha kabisa haijalishi ni miaka mingapi, na nitamtumikia Mungu kwa moyo. Sina lawama. Haijalishi ninakumbana na majaribu gani, haijalishi ninakutana na mateso gani, iwe ni kutelekezwa na familia au maumivu ya ugonjwa, nitafuata hadi mwisho.” Huku kutokuwa na lawama kwako pia ni aina ya hali hasi, kwa sababu kila wakati unapokumbana na kitu chochote, kila wakati unaposemewa maneno, kwa hakika huelewi maana iliyo ndani. Hii “sina mjibizo” unayoisema kwa hivyo si kingine bali ni kutojali, njia wakati ambapo hakuna njia nyingine. Hakuna jingine la kufanya ila hili, kwa hivyo unajilazimisha kufuata hata wakati ambapo hauko radhi. Kwa vyovyote vile hakuna awezaye kufaulu kuepuka miaka saba ya majaribu. Hata hivyo, hii ni tofauti na wewe kutaka kutoroka. Ungetamani kuepuka lakini huwezi. Hili ni jambo la asili ya mwanadamu. Lifikirie. Je, ndivyo ilivyo? Watu wengine wanahisi: Nilipokumbana na tukio kama hili miaka kumi iliyopita, daima nilifuata, na niliteseka sana, kwa hivyo ninaweza kuendelea kuvumilia kwa miaka michache. Kutafuta kwenu kwa kusudi la Mungu kumekanganyikiwa na hamjakutilia maanani. Hivyo, ikiwa kwa ndani hujayatii mapenzi ya Mungu, basi umeyasaliti na kukana mapenzi ya Mungu. Ijapokuwa huna hali hii, na hujafanya jambo hili, hizi dalili, haya mambo yaliyo ndani yako, yanamkana Mungu, kwa sababu unachokifiria na kutarajia kwa ndani sicho Mungu anachokihitaji. Aidha kwa hakika humsifu Mungu kutoka ndani ya moyo wako kwa yote Anayohitaji kutoka kwako na yote Anayofanya, iwe ni njia, au kile ulichoambiwa.

Na kwa kila kitu Mungu ambacho anawataka watu wafanye, chochote Mungu alichowapangia watu kulingana na mahitaji yao, asili ya binadamu ni kukikataa, kukosa kukikubali. Haijalishi unautangaza vipi msimamo wako, au iwe una ufahamu kidogo, kwa vyovyote vile, ufahamu wako wa mafundisho hauwezi kutatua kilicho katika asili yako. Kwa hivyo ninasema kwamba watu wengi wanazungumzia vitu vizuri katika mafundisho, na kusema maneno ya juujuu kuyastahimili. Hatimaye, japo, katika maombi wanasema: Nimepitia kwa ufanisi miaka mingi sana. Miaka saba si miaka mingi na wala si miaka michache. Tazama ninavyozeeka, jinsi afya yangu ilivyoharibika, na kwamba sina familia nzuri. Nimeandamana na Wewe miaka hii yote, nifanya bidii hata bila malipo, nimechoka ijapokuwa sijafanya kazi kwa bidii. Hata kama Utaipunguza hata kwa miaka michache, nifanyie hisani mara hii moja! Unajua udahaifu wa watu… Kwa kuomba maneno haya, ni kama kuna utiifu kidogo. Wanaendelea kusema “Unajua udhaifu wa watu”; kuna maana nyingine ndani ya maneno haya, ambayo ni kusema, Unajua udhaifu wa binadamu, basi ni kwa nini inachukua muda mrefu kiasi hiki? Je, hii si hali iliyo ndani mwa watu? Kwa hivyo, mnahisi mnafahamu vitu vingi, tayari mmevikubali, na kuonekana mmefahamu ukweli, lakini kwa hakika bado mnaukataa ukweli, na kwenda kinyume cha ukweli. Vitu mnavyovifanya haviambatani na ukweli. Japo kijuujuu hamjafanya vitendo viovu, na hamjatamka kitu chochote kibaya, hii imejikita tu kwa kutovunja amri za utawala, kwa kutoikosea tabia ya Mungu. Hujaelewa kusudi Lake na hata hivyo hauko tayari kulipokea. Hukubaliani na Yeye kufanya mambo kwa njia hii. Unafikiri: Iwapo nitaifanya kazi hii, sitapoteza muda na nitaikamilisha kazi hii kwa muda mfupi iwezakanavyo, ili kwamba niwasaidie watu wa Mungu kuepuka mateso zaidi kutoka kwa joka kuu jekundu, kuzuia kupotea kwa watu wengi zaidi, kuepuka mateso yangu. Je, hili si wazo walilonalo watu? Watu mioyoni mwao wanatumaini kufika kwa ufalme wa Mungu, na kuangamia kwa haraka kwa ulimwengu wa Shetani. Ni neema kubwa ikiwa neno moja la Mungu litawabadilisha. Mitazamo ya ndani ya watu, matamanio yao makubwa kwa hakika hayatekelezi kusudi la Mungu, na kimsingi hakuna kiini cha kutii. Hili pia linagusa ule msemo: Asilimia mia moja ya kile kilicho ndani ya asili ya binadamu ni usaliti. Kwa hivyo, kwa kulichanganua hili au lile tukio lenu, kwa kulichanganua hili suala, lile wazo, au ile hisia, iwe unaikabili kwa njia hasi, au unalalamika, ikiwa hujali au umenyamaza bila kusema neno, kuna ukinzani katika haya yote. Haya yote ni usaliti. Je, huu uchanganuzi ni sahihi? Nisingalichanganua hili, kungekuwepo na watu wanaohisi: Ninaweza kudhaniwa kuwa mtu mzuri. Ningekumbana na jambo hili miaka michache iliyopita, bila shaka ningelalamika, ikiwezekana ningerudi nyuma, lakini sasa silalamiki. Hulalamiki, lakini je una uelewa? Je, uelewa wako mdogo unajumuisha uelewa wa kweli? Kuna ukweli ndani yake? Je, uelewa wako unalingana na kusudi la Mungu? Je, umepata kibali cha Mungu? Je, una kiini cha kumtii Mungu? Je, uko radhi na tayari kumtii Mungu? Kama sivyo, basi bila shaka unakinzana na Mungu. Inawezekana kwamba hali yako ya moyo sasa hivi ni nzuri, na hujihisi vibaya, au kwa sababu sasa hivi umewekwa katika kufanya kazi. Ikiwa siku moja utatumwa nyumbani, na utakapokuwa katika giza la hali mbaya ya moyo, hata hivyo, kilicho ndani ya moyo wako kitafichuliwa. Kuna watu wengine wenye kimo kidogo, wenye muda mfupi wa uzoefu ambao wanaweza kugeuka na kukimbia, kurudi ulimwenguni. Kwa hakika, katika uchanganuzi wa mwisho, mjibizo wowote ule ulionao, unakataa mazingira aliyokupangia Mungu. Asili ya watu ya kumsaliti Mungu inafichuliwa kila mahali. Ikiwa hili lisingechanganuliwa, watu wasingejijua kwa kina ipasavyo. Watu wakikumbana na kitu chochote, wote wanamsaliti Mungu na wanakosa kumtii. Mijibizo ya baadhi yenu ni kutotaka, au hisia za malalamiko, uhasi na huzuni, na mnasema: Kwa ndani, binadamu hapendi ukweli, na huku kutopenda si kingine bali ni usaliti. Bado haitoshi kama mnazungumza namna hii tu, na hamjachanganua hadi kwenye kina cha kiini. Mnasema kwamba kutopenda ukweli ni usaliti, lakini kwa kweli, hili si sahili hivyo Mmelichanganua vipi? Hamjielewi nyinyi wenyewe. Unaweza usijue hiyo ni hali gani uliyonayo, na huwezi kutofautisha mazuri na mabaya, ikiwa ni usaliti au la, na hujijui wazi wewe mwenyewe iwe umetii au la. Hamuwezi kuchanganua kabisa asili zenu wenyewe. Kila mara mnapokumbana na jambo fulani mnashindwa kujua namna ya kwenda mbele. Hatimaye, utakapokumbana na jaribu, je, utaweza kulitambua kusudi la Mungu? Utalifafanua hili vipi? Unapaswa kutembea katika njia gani? Ni mantiki gani au ni ukweli gani unapaswa kuwa nao ili kukidhi kusudi la Mungu? Kama kiwango cha chini zaidi, ni lazima uwe na mtazamo chanya. Je, mmeyawazia maswali haya?

Zamani watu wengine walikuwa na mawazo kuhusu anachokifanya Mungu mwenye mwili. Ushirika uliofuata ulisababisha kuwepo na ukweli usiohitaji uthibitisho. Ukweli huu usiohitaji uthibitisho ni: Binadamu wanapaswa kukiri kuwa yote anayofanya Mungu ni sahihi, kuwa yote ni muhimu. Kama binadamu hawataelewa wanapaswa hata hivyo kutii na si kupinga. Kama binadamu wana mawazo ni lazima wataaibika. Je, watu wanakumbuka maneno haya? Kila mara wanapokabiliana na kitu, wanajisemea wao wenyewe: Kwa namna yoyote usiwe na mawazo, kwa namna yoyote usiyahukumu. Kuna maana katika kila kitu anachokifanya Mungu. Ijapokuwa hatuwezi kuelewa kwa sasa, siku moja tutapata aibu. Wanazishikilia tu sheria kama hii. Sheria ya aina hii, hata hivyo, yaweza kusuluhisha matatizo kadhaa ya waumini ambao wamekanganyikiwa. Kwa mtu aliye na uelewa haya maneno yatasaidia kuelewa maana ya vitu vingi, na kutumia hii sheria kila mara hali inaposhuhudiwa yaweza kuweka wazi mambo mengi. Ni nini kinachofanyika kama hakuna umaizi? Mtu anaweza tu kutii sheria, na katika kufanya hivyo anaweza pia kulindwa na kuzuia kukiuka amri za utawala, si kueneza maafa. Sheria hii ina manufaa! Sio ati haina maana! Katika sehemu mbalimbali sheria hii imesomwa kwa moyo. Wengine huiandika madaftarini, au kuiandika kwenye jalada la kitabu, na kuisoma kila wakati wanapofungua kitabu, huku wakiikariri. Wanaikariri wanapoomba. Kufanya hivyo kuna manufaa kadhaa. Watu wengine hawathubutu kufanya mambo kwa kubahatisha, na wana uchaji mdogo mioyoni mwao. Ila kulingana na watu wengi, hawana uelewa wa kweli wa hali chanya, na kuna vitu vingi sana vilivyo hasi. Ijapokuwa inaonekana kuwa mnajihisi vyema kabisa na hamjaacha kufanya kazi, kuna vitu vingi hasi kwa kweli kati yenu, na hakuna vitu chanya. Kuna mijibizo mingi sana kanisani kuhusu mambo kama haya. Je, mmejaribu kujijumuishia nyinyi wenyewe? Kama vitu vya aina hii vingekabiliwa tena, mngemkataa Mungu au kumsaliti Mungu? Kuna baadhi ya watu ambao labda wametambua, "Binadamu hana uwezo wa kuielewa asili yake mwenyewe. Bila shaka sitajaribu kukataa tena, na lazima niwe makini. Lazima niombe kila siku!” Huu sio mpango wa uhakika. Nimegundua kuwa huwa mnapata aibu, na mara nyingi mnasema: "Ah, nitafanya nini kuhusu hii asili ya binadamu? Siwezi kuisuluhisha mimi mwenyewe, na siwezi kuielewa. Kwa kweli sina haki ya kujisimamia mimi mwenyewe. Sijui ninaweza kufanya nini siku moja. Ninaogopa sana. Kumwamini Mungu lazima kufanyike kwa makini mno. Uzembe wowote waweza kusababisha maafa, na hilo laweza kuwa jambo baya mno. Hata sijijui, siwezi kujitegemea..." Ingawa watu wanaosema haya mara kwa mara huwa wanajielewa kwa kiasi fulani, wana uelewa kidogo mno kuhusu ukweli. Wanachanganyikiwa kila mara wanapokumbana na kitu chochote. Wanapatwa na wasiwasi, wanahisi uoga, na hawana njia yoyote ile wanapopatwa na chochote kile. Wakati huu umeshinda miaka saba ya majaribu, na hujasababisha maafa, na hujakiuka amri za utawala, lakini je, waweza kuwa na uhakika kuhusu wakati ujao? Wawezaje kuyashinda haya yote bila kizuizi? Unaona kuwa umeyashinda masaibu kwa urahisi sana, kwa kujificha hapa na pale. Ulijificha kwa mwaka mmoja au nusu mwaka hadi yakaisha. Wanadamu wanaweza kujificha, lakini asili ya binadamu ni kitu ambacho hakiwezi kufichika. Je, hakupaswi kuwa na ukweli uisohitaji thibitisho unaohusiana na hili, pia? Katika kila majaribu ya Mungu kuna nia nzuri. Kwa kila tukio linaloshuhudiwa kuna ukweli ambao mtu anapaswa kuwa nao ili kusimama imara. Jiandaeni na ukweli ili kukabiliana na majaribu tofauti tofauti kwa sasa, na hamtaogopa bila kujali miaka ya majaribu hapo mbeleni. Lazima muwe na ujasiri. Kutii mipango ya Mungu kamwe hakuwezi kuwa na dosari. Njia daima itakuwa na matumaini. Mwawezaje kuwa wakamilifu bila majaribu kadhaa? Bila majaribu, hakuna shahidi. Ni vipi basi mtamridhisha Mungu? Majaribu yatawaletea baraka za Mungu. Ni kwa kumfuata tu Mungu hadi mwisho ndipo mtu aweza kuingia katika ufalme. Kumbuka: nyinyi nyote mna fungu katika dhiki, ufalme, na uvumilivu wa Kristo.


kutoka kwa Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Vitabu.

Ijumaa, 1 Februari 2019

Filamu za Injili | "Nimewahi Treni ya Mwisho" | Entering the Ark of the Last Days

Filamu za Injili | "Nimewahi Treni ya Mwisho" | Entering the Ark of the Last Days

Chen Peng alikuwa mchungaji katika kanisa la nyumba fulani. Alikuwa akimtumikia Bwana kwa bidii, na mara nyingi alifanya kazi kama mhubiri, akiwasaidia wafuasi wake, na kulibebea kanisa mizigo mizito. Lakini katika miaka ya hivi karibuni, kanisa lilizidi kuwa tupu zaidi na zaidi. Waumini walikuwa na roho dhaifu na wavivu, wakikosa mkutano baada ya mkutano. Na hivyo Mchungaji Chen aliona giza likiangukia nafsi yake, kana kwamba kisima cha roho yake kilikuwa kikavu, na hakuweza kuhisi uwepo wa Bwana. Katika mikutano, aligundua kwamba hakuwa na kitu alichoweza kuhubiri. ... Alifanya kila kitu alichoweza kufikiria ili kuimarisha kanisa, lakini jitihada zake zote zilikuwa bure. ... Chen Peng alikuwa amesitikika, amepotea, na hakuweza kuelewa kwa nini kanisa lake lilikuwa linajawa na ukiwa sana, na kwa nini walikuwa wamepoteza uwepo wa Bwana.
Hadi siku moja, kwa bahati, aliposikia injili ya ufalme wa Mwenyezi Mungu. Baada ya kupitia mjadala mkali, Chen Peng hatimaye aligundua sababu ya kanisa lake kuwa na ukiwa, na akaamini kwamba Mungu alikuwa tayari amekuwa mwili na kuwa Mwana wa Adamu: Mwenyezi Mungu, anayehukumiwa na kutelekezawa na ulimwengu wa kidini, ambaye anasema ukweli na kufanya kazi ya hukumu katika zile siku za mwisho! Ni wale tu ambao wanakubali kazi ya hukumu ya Mwenyezi Mungu, Kristo wa zile siku za mwisho, na kufuata nyayo za Mwana-Kondoo wataweza kunyakuliwa mbele ya kiti cha enzi cha Mungu na kufikia kunyunyuziwa na kupewa maji ya uzima. Kwa sababu ya hilo, Chen Peng aliwahi treni ya mwisho na kukubali kwa furaha kazi ya Mungu katika zile siku za mwisho.

Alhamisi, 31 Januari 2019

Swahili Christian Skit "Mipaka ya Meya wa Kijiji" | Why Is There No Religious Freedom in China?

Swahili Christian Skit "Mipaka ya Meya wa Kijiji" | Why Is There No Religious Freedom in China?

Mchezo mfupi Mipaka ya Meya wa Kijiji inaeleza hadithi ya kweli ya mume na mke Wakristo ambao wanalazimishwa kutoroka kwa sababu ya mateso ya serilaki ya CCP. Mkristo Liu Ming'en anahukumiwa na CCP miaka saba gerezani kwa kuamini katika Mungu. Hata baada ya kuachiliwa kutoka gerezani, anabakia kuwa wakulengwa na uchunguzi mkali wa CCP. Meya wa kijiji anatumia mfumo wa wajibu wa kaya-tano , kamera za usalama, ziara za nyumba, na njia nyingine kumzuia Liu Ming'en na mkewe kuamini katika Mungu, lakini hakuna inayoleta na matokeo yanayotakiwa. Wakati huu, meya anapokea taarifa za kipaumbele kutoka Kamati Kuu ya Chama, baada ya hapo anajaribu kutafuta njia za kumlazimisha Liu Ming'en na mkewe kuweka saini barua ya kuahidi kuacha kuamini katika Mungu. Baada ya hila yake kushindwa, polisi tena wanakuja kuwakamata waumini hawa wawili. Kuepuka kukamatwa na kuendelea kumfuata Mungu na kuamini katika Mungu, Liu Ming'en na mkewe wanalazimishwa kutoroka nyumbani kwao.
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumatano, 30 Januari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu | “Wale Ambao Hawalingani na Kristo Hakika Ni Wapinzani wa Mungu”

Maneno ya Roho Mtakatifu | “Wale Ambao Hawalingani na Kristo Hakika Ni Wapinzani wa Mungu”

Mwenyezi Mungu anasema, “Hata ingawa fikira za mwanadamu hakika haziwezi kupuuzwa, haikubaliki hata zaidi kwa mwanadamu kubadilisha kiini cha Kristo. Nyinyi mnamchukua Kristo kama asiyekufa au mhenga, lakini hakuna yeyote anayemchukua Kristo kama binadamu wa nyama na mwili aliye na kiini kitakatifu. Kwa hivyo, wengi wa wale ambao wanatamani usiku na mchana kumwona Mungu ni hasa maadui wa Mungu na hawapatani na Mungu. Je, haya si makosa kwa upande wa mwanadamu? Hata sasa bado mnadhani kwamba imani yenu na uaminifu umetosha kuwafanya mstahili kuona uso wa Kristo, lakini Mimi Nawasihi kujihami kwa mambo zaidi yaliyo na umuhimu! Hii ni kwa maana katika wakati uliopita, uliopo na ujao, wengi wa wale ambao hupatana na Kristo wameanguka au wataanguka; wao wote wamechukua jukumu la Mafarisayo. Sababu yenu ya kushindwa ni nini? Ni kwa sababu hasa katika fikra zenu kuna Mungu mkubwa, Atamanikaye. Lakini ukweli si kama vile mwanadamu atakavyo. Kristo si mkubwa tu, bali Yeye ni mdogo hasa; Yeye si mtu tu, bali ni mtu wa kawaida; Hana uwezo wa kupaa mbinguni tu, bali hana pia uhuru wa kuzunguka ardhini. Na kwa hivyo, watu humtendea kama mtu wa kawaida; wao hufanya wanavyopenda wanapokuwa pamoja naye, na kusema maneno kiholela Kwake, wakati huu wote wakingojea kurudi kwa "Kristo wa kweli." Mnamchukua Kristo aliyekuja tayari kama mtu wa kawaida na neno Lake kama lile la mtu wa kawaida. Kwa hivyo, hamjapata chochote kutoka kwa Kristo na badala yake mmeonyesha ubaya wenu kwenye mwangaza kabisa.”

Jumanne, 29 Januari 2019

Neno la Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee I Mamlaka ya Mungu (I)” Uendelezo wa Sehemu ya Pili

Neno la Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee I Mamlaka ya Mungu (I)” Uendelezo wa Sehemu ya Pili

Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”. Maudhui ya video hii: Kwenye Siku ya Nne, Misimu, Siku, na Miaka ya Mwanadamu Iliumbika Huku Mungu Akionyesha Mamlaka Yake kwa Mara Nyingine Tena Kwenye Siku ya Tano, Maisha ya Maumbo Tofauti na Pana Yaonyesha Mamlaka ya Muumba kwa Njia Tofauti Kwenye Siku ya Sita, Muumba Aongea, na Kila Aina ya Kiumbe Hai Akilini Mwake Chajitokeza, Kimoja Baada ya Kingine Katika Mamlaka ya Muumba, Viumbe Vyote ni Timilifu Hakuna Kiumbe Chochote Kati ya Vile Vilivyoumbwa na Vile Ambavyo Havikuumbwa Kinaweza Kubadilisha Utambulisho wa Muumba
Sikiliza zaidi: Kanisa la Mwenyezi Mungu video

Jumatatu, 28 Januari 2019

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Pili

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Pili

Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Pili Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”. Maudhui ya video hii: Awamu Sita katika Maisha ya Binadamu Kuzaliwa: Awamu ya Kwanza 1. Maisha Mapya Yanazaliwa Kulingana na Mipango ya Muumba 2. Kwa Nini Binadamu Tofauti Wanazaliwa Katika Hali Tofauti Kukua: Awamu ya Pili 1. Hali Ambazo Mtu Hukulia Ndani Zimepangwa na Muumba 2. Hali Mbalimbali Ambazo Watu Hukulia Ndani Husababisha Wajibu Tofauti
Mwenyezi Mungu alisema, Tangu unapoingia katika dunia hii ukilia, unaanza kutekeleza wajibu wako. Unachukua jukumu lako katika mpango wa Mungu na katika utaratibu wa Mungu. Unaanza safari ya maisha. Licha ya asili yako na licha ya safari iliyoko mbele yako, hakuna kitakachoepuka mpango na utaratibu ambao mbingu imeweka, na hakuna aliye na udhibiti wa hatima yake, kwa maana Anayetawala juu ya kila kitu ndiye tu Aliye na uwezo wa kazi hiyo. Tangu siku aliyoumbwa binadamu, Mungu amekuwa thabiti katika kazi Yake, kusimamia ulimwengu huu na kuelekeza mabadiliko na harakati ya mambo yote. Kama kila kiumbe, mwanadamu bila kujua anapata lishe ya utamu na mvua na umande kutoka kwa Mungu. Kama vitu vyote, mwanadamu bila kujua anaishi chini ya mpango wa mkono wa Mungu. Moyo na roho ya mwanadamu vimeshikwa katika mkono wa Mungu, na maisha yote ya mwanadamu yanatunzwa machoni mwa Mungu. Haijalishi kama unayaamini mambo haya au la, vitu vyote, vilivyo hai au vilivyokufa, vitahamishwa, vitabadilika, kufanywa vipya, na kutoweka kulingana na mawazo ya Mungu. Hivi ndivyo Mungu anavyotawala juu ya kila kitu.
kutoka kwa Mungu Ndiye Chanzo cha Uhai wa Mwanadamu

Jumapili, 27 Januari 2019

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Kumjua Mungu Ndiyo Njia ya Kumcha Mungu na Kuepuka Maovu”

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Kumjua Mungu Ndiyo Njia ya Kumcha Mungu na Kuepuka Maovu”

Mwenyezi Mungu anasema, “‘Kumwogopa Mungu na kuepuka maovu’ na kumjua Mungu ni uhusiano usiogawanyishwa na uliounganishwa kwa nyuzi zisizohesabika, na uhusiano kati yao ni dhahiri. Iwapo mtu anataka kupata uwezo wa kuepuka maovu, lazima kwanza amche Mungu kwa kweli; iwapo mtu anataka kupata uwezo wa kumcha Mungu kwa kweli, lazima awe na maarifa ya kweli kuhusu Mungu; Iwapo mtu anataka kupata maarifa ya Mungu, lazima kwanza ayapitie maneno ya Mungu, aingie katika ukweli wa maneno ya Mungu, apitie kuadibu na nidhamu ya Mungu, kuadibu Kwake na hukumu; iwapo mtu anataka kupitia maneno ya Mungu, lazima aje ana kwa ana na maneno ya Mungu, aje ana kwa ana na Mungu, na kumwomba Mungu Ampe fursa ya kupitia maneno ya Mungu katika hali ya aina yote ya mazingira inayowahusisha watu, matukio na vitu; iwapo mtu anataka kuja ana kwa ana na Mungu na maneno ya Mungu, lazima kwanza amiliki moyo wa kweli na mwaminifu, awe tayari kuukubali ukweli, kukubali kupitia mateso, uamuzi na ujasiri wa kuepuka uovu, na azimio la kuwa kiumbe halisi…Kwa njia hii, kuendelea mbele hatua kwa hatua, utamkaribia Mungu zaidi, moyo wako utakuwa safi zaidi, na maisha yako na thamani ya kuwa hai, pamoja na maarifa yako kumhusu Mungu, yatakuwa ya maana zaidi na yatakuwa hata ya kupevuka zaidi.”