Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana|”Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu”

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli. Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Alhamisi, 14 Februari 2019

Neno la Mungu | Sura ya 98

Neno la Mungu | Sura ya 98

Mambo yote yatakuja juu ya kila mmoja wenu, na yatawawezesha kujua zaidi juu Yangu na kuwa na uhakika zaidi juu Yangu. Yatawawezesha kunijua, Mungu mmoja Mwenyewe, kunijua Mimi Mwenye uweza, kunijua Mimi Mungu Mwenyewe mwenye mwili. Baadaye, Nitatoka katika mwili, Nirudi Sayuni, Nirudi katika nchi nzuri ya Kanaani, ambayo ni makazi Yangu, ndiyo hatima Yangu, na ndio msingi ambao niliumba vitu vyote. Sasa hakuna yeyote kati yenu anayeelewa maana ya maneno ambayo Ninasema, hakuna mtu hata mmoja ambaye anaweza kuelewa maana ya maneno haya. Ni wakati tu kila kitu kitafichuliwa kwenu ndipo mtaelewa kwa nini Ninasema maneno haya. Mimi si wa ulimwengu na Mimi sio hata wa ulimwengu kwa sababu Mimi ni Mungu Mwenyewe wa pekee. Ninashikilia ulimwengu dunia wote mkononi Mwangu, Mimi Mwenyewe Ninatawala, na watu wanaweza tu kutii mamlaka Yangu, kulitaja jina Langu takatifu, kunishangilia na kunisifu. Kila kitu kitafunuliwa kwenu hatua kwa hatua. Ingawa hakuna kitu kilichofichwa, ninyi bado hamwezi kuelewa njia Yangu ya kuzungumza, na sauti ya maneno Yangu. Bado hamwelewi mpango Wangu wa usimamizi unahusu nini. Kwa hiyo, Nitawaambia baadaye kuhusu mambo yote ambayo hamwelewi kwa yale Niliyoyasema kwa sababu, Kwangu Mimi, kila kitu ni rahisi na wazi wakati, kwenu, ni vigumu sana, hamwelewi tu kabisa. Kwa hiyo, Nitabadili njia Yangu ya kuzungumza, Sitaunganisha mambo pamoja Ninaponena lakini Nitafafanua kila hoja moja baada ya nyingine.
Kufufuka kutoka kwa wafu kunahusu nini? Je, ni kufa katika mwili na kisha kurudi kwenye mwili baada ya kifo? Je, huku kunaitwa kufufuka kutoka kwa wafu? Je, ni rahisi vile? Mimi ni mwenyezi Mungu, unajua nini kuhusu hili? Je, mnaelewaje hili? Je, kufufuka kutoka kwa wafu wakati wa kupata Kwangu mwili mara ya kwanza kwa kweli kunaweza kuchukuliwa neno kwa neno? Je, mchakato huo ulikuwa kama ulivyoelezwa katika maandiko? Nimesema kuwa kama Sizungumzi kwa uwazi, kama Sielezi wazi, hakuna mtu atakayeweza kuelewa maana ya maneno Yangu. Hakuna mtu hata mmoja katika enzi zote ambaye hakufikiri kwamba kufufuka kutoka kwa wafu kulikuwa vile. Tangu uumbaji wa dunia hakuna mtu aliyeelewa maana halisi ya hili. Je, nilipigwa misumari msalabani kwa kweli? Na, baada ya kifo, je, nilitoka kaburini? Ilikuwa namna hii kwa kweli? Je, hili linaezekana kweli? Hakuna mtu katika enzi zote ambaye ameweka jitihada yoyote katika hili, hakuna mtu ambaye amenijua kutoka kwa hili na hakuna mtu hata mmoja ambaye haamini, kila mtu anadhani kuwa hili ni kweli. Hawajui kwamba kila neno Langu lina maana ya ndani. Basi, kufufuka kutoka kwa wafu ni nini hasa? (Hivi karibuni, mtapitia jambo hili, kwa hivyo Nitawaambia kuhusu hilo mapema.) Kila kiumbe aliyeumbwa anataka kuishi kuliko kufa. Kutoka kwa mtazamo Wangu, kifo cha mwili sio kifo halisi. Wakati Roho Wangu anarudishwa kutoka kwa mtu, mtu huyo hufa. Kwa hiyo, Ninawaita wale mapepo wote waliopotoshwa na Shetani (wale ambao hawana imani, wasioamini wote) wafu. Tangu kuumbwa kwa dunia, Nimeongeza Roho Wangu kwa kila mtu Niliyemchagua. Hata hivyo, baada ya awamu iliyofuatia uumbaji, watu walimilikiwa na Shetani kwa kipindi cha muda. Kwa hiyo Niliondoka na watu wakaanza kuteseka (mateso Niliyovumilia Nilipopata mwili na kusulubishwa msalabani, kama ilivyoelezwa). Hata hivyo, kwa wakati uliopangiwa kabla na Mimi (wakati ambapo kuwaacha Kwangu watu kulimalizika), Niliwarejesha Kwangu watu Niliowaamulia kabla na Nikaweka tena Roho Wangu ndani yenu ili mpate kufufuka. Hii inaitwa “kufufuka kutoka kwa wafu.” Sasa, wale wanaoishi kwa kweli katika Roho Wangu wote wameshashinda uwezo wa binadamu, na wote wanaishi katika mwili. Hata hivyo, kabla ya muda mrefu, ninyi nyote mtaondoa fikira zenu, mtupe mawazo yenu, na kutupa mtego wote wa kidunia. Lakini, sivyo, kama watu wanavyofikiria, kufufuka kutoka kwa wafu baada ya mateso. Kwamba ninyi mnaishi sasa ni sharti la awali la kuishi katika mwili, ni njia muhimu ya kuingia katika ulimwengu wa kiroho. Kuzidi uwezo wa ubinadamu wa kawaida Ninaozungumza kuhusu kunamaanisha kutokuwa na familia, kutokuwa na mke, kutokuwa na watoto na mahitaji ya kibinadamu. Ni kuzingatia tu kuishi kwa kudhihirisha mfano Wangu, kuzingatia tu kuingia ndani Yangu na kutofikiria juu ya mambo mengine nje Yangu. Mahali popote unapoenda ni nyumbani kwako, huku ni kuvuka mipaka kwa ubinadamu wa kawaida. Ninyi mmeelewa visivyo kabisa maneno haya Yangu, ufahamu wenu ni wa kina kifupi sana. Je, Nitaonekanaje kwa mataifa yote na watu wote? Katika mwili leo? Hapana! Wakati utakapokuja, Nitaonekana katika mwili Wangu katika kila taifa la ulimwengu. Wakati ambapo wageni wanawahitaji muwachunge bado haujafika. Wakati huo ninyi mtahitaji kuja nje ya mwili na kuingia katika mwili ili muwalishe. Huu ni ukweli lakini sio “kufufuka kutoka kwa wafu” ambao watu wanafikiria. Wakati uliowekwa, mtatoka katika mwili bila kujua na kuingia katika ulimwengu wa kiroho na kutawala mataifa yote pamoja nami. Wakati haujafika bado. Ninapowahitaji kuwa katika mwili mtakuwa katika mwili (kulingana na mahitaji ya kazi Yangu, ninyi lazima muwe na fikira sasa, bado lazima muishi katika mwili, hivyo mnapaswa bado kufanya mambo ambayo mnapaswa kufanya katika mwili kulingana na hatua Zangu; msisubiri bila kufanya lolote kwa sababu hii itachelewesha mambo). Ninapowahitaji kutenda katika mwili kama wachungaji wa kanisa, ninyi mtatoka nje ya mwili, muache mawazo yenu, na kunitegemeana kabisa ili kuishi. Muwe na imani katika nguvu Zangu, muwe na imani katika hekima Yangu. Kila kitu kitafanywa na Mimi binafsi. Mnahitaji tu kusubiri kufurahia. Baraka zote zitawajia, na ninyi mtakuwa na ruzuku isiyoisha. Siku hiyo itakapokuja, mtaelewa kanuni ya jinsi Ninavyofanya hivi, mtajua matendo Yangu ya ajabu na kuelewa jinsi Ninavyoleta wana Wangu wazaliwa wa kwanza katika Sayuni. Hili sio gumu kama mnavyofikiria lakini pia si rahisi kama mnavyofikiria.
Najua Ninaposema hili hamwezi hata kwa kiwango cha chini kuelewa madhumuni Yangu katika hilo na huchanganyikiwa zaidi. Mtayachanganya na yale Niliyosema hapo awali ili msiweze kuelewa chochote, itaonekana kama kwamba hakuna njia nyingine. Hata hivyo, msijali, Nitawaambia kila kitu. Kila kitu Ninachosema kina maana. Nimesema kuwa Ninaweza kufanya vitu vilivyopo virudi kuwa bure na Ninaweza kufanya vitu viwe vingi kutoka kwa utupu. Katika mawazo ya binadamu, kuingia katika mwili kutoka kwa mwili, mtu lazima afufuliwe kutoka kwa wafu. Katika siku za nyuma, Nilitumia njia hii na Nikadhihirisha muujiza Wangu mkuu zaidi, lakini leo si kama zamani. Nitawachukua moja kwa moja kutoka kwa mwili hadi ndani ya mwili. Je, hii sio hata ishara kubwa zaidi na muujiza? Je, huu sio udhihirisho mkubwa zaidi wa kudura Yangu? Nina mpango Wangu, Nina nia Zangu. Nani asiye katika mikono Yangu? Ninafanya kazi na Ninajua. Njia Zangu za kufanya kazi leo ni, hata hivyo, tofauti na zilizopita. Ninabadilisha mbinu Zangu za kufanya kazi kulingana na mabadiliko ya enzi. Wakati Nilipigwa misumari msalabani, hiyo ilikuwa ni Enzi ya Neema, lakini sasa ni enzi ya mwisho. Kasi ya kazi Yangu inaongezeka, sio kasi sawa na ilivyokuwa hapo zamani, sembuse kuwa polepole kuliko siku za nyuma lakini, badala yake, ni haraka zaidi kuliko zamani. Hakuna njia ya kuielezea, hakuna haja ya michakato mingi migumu. Mimi Niko huru kufanya chochote; si kweli kwamba inachukua tu maneno machache ya mamlaka kutoka Kwangu kuamua jinsi mapenzi Yangu yatakamilishwa na jinsi Nitawakamilisha? Kila kitu Ninachosema hakika kitafanyika. Katika siku za nyuma, mara nyingi Nilisema kuwa nitateseka, na Sikuwaruhusu watu wataje mateso Niliyoyastahimili awali; kutaja hili kulikuwa kunikufuru. Hii ni kwa sababu Mimi ni Mungu Mwenyewe na Kwangu hakuna ugumu; unapotaja mateso haya unawafanya watu walie. Nimesema kuwa katika siku zijazo hakutakuwa na kutanafusi na hakutakuwa na machozi. Inapaswa kuelezwa kutoka kwa mtazamo huu, na kisha maana ya maneno Yangu yanaweza kueleweka. Maana ya “wanadamu hawawezi kustahimili mateso haya” ni kwamba Ninaweza kuondoka kutoka kwa dhana zote za binadamu na fikira, kuachana na hisia za mwili, kuacha mambo yote ya ulimwengu na kuondoka katika mwili, na bado Ninaweza kusimama wakati kila mtu ananikana Mimi. Hii inatosha kuthibitisha kuwa Mimi ni Mungu Mwenyewe wa pekee. Nimesema, “Kila mwana mzaliwa wa kwanza lazima aingie katika ulimwengu wa kiroho kutoka kwa mwili; hii ndiyo njia ambayo wanapaswa kuchukua ili kutawala pamoja nami kama wafalme.” Maana ya sentensi hii ni kwamba unapokumbana na kitu ambacho mnacho, zamani, mlifikiri, mtaondoka rasmi katika nyama na kuingia katika mwili ili muanze kuwahukumu rasmi wale wana wa wafalme na wafalme hao. Wao watahukumiwa kulingana na mambo yanayotokea wakati huu. Hata hivyo, sio ngumu kama mnavyofikiria, itafanyika papo hapo. Hamtahitaji kufufuka kutoka kwa wafu na hamtahitaji hata kuteseka (kwa sababu mateso na shida zenu duniani tayari zimekamilika na Nimekwisha kusema kuwa Sitashughulika tena na wanangu wazaliwa wa kwanza baada ya hapo). Hapa ndipo wazaliwa wa kwanza watafurahia baraka zao, kama ilivyoongelewa—mtaingia katika ulimwengu wa kiroho bila kujua. Kwa nini Nasema kuwa hii ni rehema Yangu na neema? Ikiwa mtu angeweza tu kuingia katika ulimwengu wa kiroho baada ya kufufuka kutoka kwa wafu, hii ingekuwa mbali na kuwa ya huruma na neema. Kwa hivyo haya ndiyo maonyesho ya dhahiri zaidi ya rehema Yangu na neema na, zaidi ya hayo, yanafichua uamuzi Wangu kabla na uteuzi Wangu wa watu. Inatosha kuonyesha jinsi amri Yangu ya utawala ilivyo kali. Nitakuwa mwenye huruma kwa yeyote Nitakayetaka na kuwa mwenye huruma kwa yeyote Nitakayetaka. Hakuna mtu atakayepinga au kupigana. Nitaamua yote haya.
Watu hawawezi kuelewa hilo na wanajiwekea shinikizo mpaka wasiweze kupumua na bado wanajifunga. Mawazo ya watu ni finyu sana, kwa hiyo ni lazima watupilie mbali mawazo na dhana za binadamu. Kwa hivyo, ni lazima Nitoke katika mwili na kuingia katika ulimwengu wa kiroho kuchukua udhibiti wa kila kitu, kusimamia kila kitu. Hii ndiyo njia pekee ya kutawala watu wote na mataifa yote na kutimiza mapenzi Yangu. Sio mbali sana. Hamna imani katika kudura Yangu, hamjui mwanadamu Niliye. Mnafikiri kwamba Mimi ni mtu tu, hamwezi kuona uungu Wangu hata kidogo. Mambo yatakuwa kamili wakati wowote Ninapotaka yawe kamili. Kinachohitajika tu ni neno kutoka katika kinywa Changu. Ninyi mmetilia maanani tu kipengele cha ubinadamu Wangu katika kile ambacho Nimesema hivi karibuni na kila Ninachofanya, lakini hamjatilia maanani kipengele cha uungu Wangu. Hiyo ni kusema kwamba mnadhani kwamba Mimi pia nina mawazo na dhana. Lakini Nimesema kuwa fikira Zangu, mawazo na akili, kila Ninachofanya, kila kitu Ninachotenda na kila kitu Ninachosema ni udhihirisho kamili wa Mungu Mwenyewe. Je, mmesahau yote haya? Ninyi nyote ni watu waliochanganyikiwa! Hamwelewi maana ya maneno Yangu. Nimewaruhusu kuona kipengele cha ubinadamu Wangu wa kawaida kutoka kwa kile Nilichosema (Nimewawezesha kuona ubinadamu Wangu wa kawaida katika maisha Yangu ya kila siku, kwa kweli, kwa sababu ninyi bado hamwelewi kipengele cha ubinadamu Wangu wa kawaida kutokana na kile Nilichosema wakati huu), ilhali hamwelewi ubinadamu Wangu wa kawaida, na mnajaribu kushikilia tu kitu ambacho kinaweza kutumiwa dhidi Yangu na mnakuwa bila nidhamu mbele Yangu. Ninyi ni vipofu! Ninyi ni wapumbavu! Hamnijui Mimi! Nimenena bure kwa muda mrefu, ninyi hamnijui Mimi kabisa, hamuchukulii ubinadamu Wangu wa kawaida kama sehemu ya Mungu Mwenyewe mkamilifu kabisa! Ninawezaje kukosa kuwa na hasira? Ninawezaje kuwa mwenye huruma tena? Ninaweza tu kuwajibu watoto hawa wa kutotii na hasira Yangu. Wenye kiburi sana, wasionijua sana! Mnafikiria kwa mwanadamu Niliye amefanya makosa! Naweza kufanya makosa? Ningechagua bila mpango kuuchukua mwili wowote? Ubinadamu Wangu na uungu Wangu ni sehemu mbili zisizoweza kutenganishwa ambazo zinajumuisha Mungu Mwenyewe mkamilifu. Sasa mnapaswa kuelewa vizuri kuhusu hili! Tayari Nimeshasema kila kitu Ninapaswa kusema. Sitalieleza zaidi!
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Jumatano, 13 Februari 2019

Kanuni Kuu za Jinsi Wafanyakazi Hufanya Kazi

Sura ya 37. Kanuni Kuu za Jinsi Wafanyakazi Hufanya Kazi

Katika kazi yao, wafanyakazi wanapaswa kuzingatia mambo mawili: Moja ni kufanya kazi kabisa kulingana na kanuni zilizowekwa masharti na mipangilio ya kazi. Wafanyakazi hawapaswi kukiuka kanuni hizi, wasifanye kazi kulingana na mawazo yao wenyewe, na siyo kulingana na mapenzi yao. Wanapaswa kuonyesha uhusiano kwa kazi ya familia ya Mungu, na kuweka maslahi ya familia ya Mungu kwanza katika kila kitu wakifanyacho. Jambo jingine pia ni muhimu, na ni kwamba, katika kila kitu wakifanyacho, kuzingatia kufuata mwongozo wa Roho Mtakatifu, na kufanya kila kitu kwa ukali kulingana na neno la Mungu. Usipotii mwongozo wa Roho Mtakatifu au ikiwa kwa ukaidi unafuata mawazo yako mwenyewe na kufanya mambo kulingana na fikira zako mwenyewe, hili linafanya upinzani mkali sana kwa Mungu. Mama kwa mara kutotii kupata nuru na mwongozo wa Roho Mtakatifu huelekeza kwa mwisho kabisa. Hakuna jinsi ya kuendelea na kazi kama mtu amepoteza kazi ya Roho Mtakatifu, na ingawa mtu hufanya kazi, hakuna kitu kinachotimizwa. Ni kanuni hizi kuu mbili za kuzingatia wakati ukiwa kazini: Moja ni kufanya kazi kabisa kulingana na mipangilio kutoka hapo juu, na kufanya kazi na kanuni zilizowekwa na hayo ya hapo juu. Jambo jingine ni kufuata mwongozo kutoka kwa Roho Mtakatifu karibu. Mara tu mambo haya mawili yanapofahamika, ni vigumu kwa kazi kukosa kufikia matarajio yake. Kwa nyinyi ambao uzoefu wenu katika eneo hili bado ni kidogo, ridhaa yenu wenyewe hughushi kazi yenu zaidi. Wakati mwingine, hamuwezi kuelewa kupata nuru au mwongozo kutoka kwa Roho Mtakatifu karibu; kwa wengine, mnaonekana kuielewa, lakini huenda mnaipuuza. Wewe daima hufikiria au kufikia hitimisho kwa njia ya kibinadamu, kufanya kama unavyofikiria kuwa sahihi, bila kujali kabisa juu ya nia ya Roho Mtakatifu. Wewe huendelea na kazi yako tu kulingana na mawazo yako mwenyewe, ukiweka kando upataji wa nuru kutoka kwa Roho Mtakatifu. Hali kama hizo hutokea mara kwa mara. Mwongozo wa ndani kutoka kwa Roho Mtakatifu si wa kupita uwezo wa binadamu kamwe. Kwa kweli ni wa kawaida sana: Mfiko wa ndani wa roho yako unajua hii ndiyo njia sahihi ya kufanya hivyo, na kwamba hii ndiyo njia bora zaidi. Wazo kama hilo ni wazi sana; si matokeo ya kutafakari, na wakati mwingine huwezi kuelewa kikamilifu ni kwa nini kuifanya kwa njia hii. Hii mara nyingi si kitu kingine bali kupata nuru kutoka kwa Roho Mtakatifu. Hali kama hiyo ndiyo hutokea kwa kawaida kwa watu wengi sana. Roho Mtakatifu hukuongoza utende kwa njia sahihi zaidi. Siyo matokeo ya fikira zako, badala yake una hisia moyoni mwako na unang'amua kwamba hii ndiyo njia bora zaidi ya kufanya hivyo. Pengine hili ni kutoka kwa Roho Mtakatifu. Mapenzi ya mtu mara nyingi ni matokeo ya mfanyiko tendani wa mawazo yake na yamepakwa rangi na mawazo yake: Mapato yangu ni nini, jinsi nitakavyofaidika—haya ni sehemu ya chochote ambacho watu huamua kukifanya wenyewe. Mwongozo kutoka kwa Roho Mtakatifu hauna ughushi kama huo hata kidogo. Ni muhimu kuzingatia kwa makini mwongozo au kupata nuru kutoka kwa Roho Mtakatifu; hasa katika masuala muhimu unapaswa kuwa makini ili ulielewe. Watu ambao hufikiria mengi sana, ambao hupenda kufuata mawazo yao huenda wakaukosa. Wafanyakazi wazuri, wafanyakazi waangavu, huzingatia kazi ya Roho Mtakatifu. Watu wanaomtii Roho Mtakatifu humwogopa Mungu na kutafuta ukweli bila kuchoka. Ili kumridhisha Mungu na kumshuhudia Yeye, mtu anapaswa kuchunguza kazi yake mwenyewe kwa dalili za ughushi na madhumuni, na kujaribu kuona ni kiasi gani kilichomotishwa na matakwa ya kibinafsi, ni kiasi gani kilichotokana na kupatiwa nuru na Roho Mtakatifu, na ni kiasi gani kilicho cha kuambatana na neno la Mungu. Ni lazima daima na katika hali zote uyakague maneno na matendo yako. Kutenda kwa njia hii daima kutakuweka kwenye njia sahihi ya kumtumikia Mungu. Ni muhimu kuwa na ukweli mwingi chini ya amri yako ili kutimiza huduma kwa Mungu ambayo ni ya kupendeza nafsi Yake. Watu wana uwezo wa kutofautisha baada tu ya kuelewa neno la Mungu, na wanaweza kutambua kinachotoka kwa mapenzi yao wenyewe na vitu vinavyoonyesha motisha yao. Wanaweza kutambua uchafu wa wanadamu, na maana ya kutenda kulingana na ukweli. Ni hapo tu utakapojua jinsi ya kutii zaidi kwa usafi. Bila ukweli haiwezekani kwa watu kutofautisha. Mtu mpumbavu anaweza kumwamini Mungu maisha yake yote bila kujua maana ya kufichua upotovu, wala hajui kumpinga Mungu ni nini, kwa sababu yeye hana ukweli, wazo hili halipo katika akili yake. Hili ni kama kukarabati kifaa cha umeme. Je, mtu anawezaje kukitengeneza ikiwa hajui ni mzunguko umeme upi una kosa? Ndani yenu pia kuna mizunguko mingi. Wakati mwingine hitilafu iko katika malengo yenu, au ambako mapenzi yenu wenyewe yanahusika. Wakati mwingine hitilafu ni upotovu wa ufahamu wenu au ujuzi. Ama inaweza kuwa kutokana na kufuata mapenzi yenu wenyewe au kwa kuamini na kupotoshwa na wengine. Wakati mwingine nyinyi hufuata mwili mnapojaribu kulinda sifa zenu au hadhi. Hitilafu kama hizi hutokea mara kwa mara, hivyo kupeleka kazi mrama na kuleta hasara kwa kazi ya familia ya Mungu na maisha ya ndugu. Thamani ya kazi ya aina hii ni nini? Ni katizo, usumbufu, na uharibifu tu. Ili kutimiza kazi ambayo Mungu huwapa ni muhimu kuelewa kanuni hizi mbili. Ni lazima mshike kabisa mipango ya kazi kama ilivyoelezwa hapo juu, na lazima mzingatie kuutii mwongozo kutoka kwa Roho Mtakatifu. Ni wakati tu kanuni hizi mbili zinapofahamika ndipo kazi inapoweza kuwa ya kufaa na mapenzi ya Mungu yaridhishwe.
Soma Zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu

Jumatatu, 11 Februari 2019

2018 Gospel Music "Mungu Kuwatawala na Kuwakimu Wanadamu na Vitu Vyote" (Swahili Subtitles)

2018 Gospel Music "Mungu Kuwatawala na Kuwakimu Wanadamu na Vitu Vyote" (Swahili Subtitles)

Chini ya mbingu, milima, mito, na maziwa vyote vina mipaka yavyo, na viumbe vyote huishi na kuzaana wakati wa misimu yote minne kulingana na sheria za maisha…. Ungependa kujua ni nani huwatawala na kuwakimu wanadamu na vitu v yote? Tazama dondoo hii ya filamu ya Kikristo ili kujua zaidi kuhusu mamlaka ya pekee ya Mungu.
Mwenyezi Mungu alisema, Mwanzoni, Mungu alikuwa anapumzika. Hakukuwa na binadamu ama kitu chochote kingine duniani wakati huo, na Mungu hakuwa amefanya kazi yoyote ile. Mungu alianza tu kazi Yake ya usimamizi baada ya binadamu kuwepo na baada ya binadamu kupotoshwa. Kutoka hapa kuendelea, Mungu hakupumzika tena lakini badala yake Alianza kufanya kazi miongoni mwa binadamu. Ilikuwa kwa sababu ya upotovu wa binadamu ndipo Mungu alichukuliwa kutoka kwa pumziko Lake, na ilikuwa pia kwa sababu ya uasi wa malaika mkuu ndipo Mungu alichukuliwa kutoka kwa pumziko Lake. Iwapo Mungu hatamshinda Shetani na kuokoa binadamu, ambao wamepotoshwa, Mungu hatawahi tena kuweza kuingia rahani. Mungu anakosa pumziko akosavyo mwanadamu. Wakati Mungu ataingia rahani tena, mwanadamu pia ataingia rahani. Maisha ya pumziko ni yale bila vita, bila uchafu, bila udhalimu unaoendelea. Hii ni kusema kwamba hayana unyanyasaji wa Shetani (hapa “Shetani” inamaanisha nguvu za uhasama), upotovu wa Shetani, na pia uvamizi wa nguvu yoyote inayompinga Mungu. Kila kitu kinafuata aina yake na kuabudu Bwana wa uumbaji. Mbingu na dunia ni shwari kabisa. Haya ni maisha matulivu ya binadamu. Mungu aingiapo rahani, hakuna udhalimu wowote utakaoendelea duniani, na hakutakuwa na uvamizi wowote wa nguvu za uhasama. Binadamu pia wataingia ulimwengu mpya; hawatakuwa tena binadamu waliopotoshwa na Shetani, lakini badala yake binadamu ambao wameokolewa baada ya kupotoshwa na Shetani. Siku ya pumziko ya binadamu pia ni siku ya pumziko ya Mungu. Mungu alipoteza pumziko Lake kwa sababu wanadamu hawakuweza kuingia rahani; haikuwa kwamba Hakuweza awali kupumzika. Kuingia rahani hakumaanishi kwamba mambo yote yatakoma kusonga, ama kwamba mambo yote yatakoma kuendelea, wala hakumaanishi kwamba Mungu atakoma kufanya kazi ama mwanadamu atakoma kuishi. Ishara ya kuingia rahani ni kama hii: Shetani ameangamizwa; wale watu waovu wanaomuunga mkono Shetani kwa kufanya maovu wameadhibiwa na kuondolewa; nguvu zote za uhasama kwa Mungu zimekoma kuwepo. Mungu kuingia rahani kunamaanisha kwamba Hatafanya tena kazi Yake ya wokovu wa binadamu. Binadamu kuingia rahani kunamaanisha kwamba binadamu wote wataishi ndani ya mwangaza wa Mungu na chini ya baraka Zake; hakutakuwa na upotovu wowote wa Shetani, wala maovu yoyote kutokea. Binadamu wataishi kama kawaida duniani, na wataishi chini ya ulinzi wa Mungu. Mungu na mwanadamu waingiapo rahani pamoja, kutamaanisha kwamba binadamu wameokolewa na kwamba Shetani ameangamizwa, kwamba kazi ya Mungu miongoni mwa mwanadamu imemalizika kabisa. Mungu hataendelea tena kufanya kazi miongoni mwa mwanadamu, na mwanadamu hataendelea tena kumilikiwa na Shetani. Kwa hivyo, Mungu hatakuwa shughulini tena, na mwanadamu hatakimbiakimbia tena; Mungu na mwanadamu wataingia rahani wakati huo huo. Mungu atarudia nafasi yake ya awali, na kila mtu atarudia nafasi yake husika. Hizi ndizo hatima ambazo Mungu na mwanadamu wataishi ndani kwa utaratibu huu baada ya mwisho wa usimamizi wote wa Mungu. Mungu ana hatima ya Mungu na mwanadamu ana hatima ya mwanadamu. Apumzikapo, Mungu ataendelea kuwaongoza binadamu wote kwa maisha yao duniani. Akiwa kwa mwangaza wa Mungu, mwanadamu atamwabudu Mungu wa kweli aliye mbinguni. Mungu hataishi tena miongoni mwa binadamu, na mwanadamu pia hataweza kuishi na Mungu katika hitimisho la Mungu. Mungu na mwanadamu hawawezi kuishi ndani ya ulimwengu sawa; badala yake, wote wawili wana njia zao binafsi za kuishi. Mungu ndiye anayeongoza binadamu wote, wakati binadamu wote ni matokeo ya kazi ya Mungu ya usimamizi. Ni binadamu wanaoongozwa; kuhusu kiini, binadamu si sawa na Mungu. Kuingia rahani kunamaanisha kurudi pahali pa awali pa mtu. Kwa hivyo, Mungu aingiapo rahani, kunamaanisha kwamba Mungu amerudi pahali Pake pa awali. Mungu hataishi tena duniani ama kushiriki kwa furaha na mateso ya binadamu wakati yupo miongoni mwa binadamu. Binadamu wanapoingia rahani, kunamaanisha kwamba mwanadamu amekuwa kiumbe halisi; binadamu watamwabudu Mungu wakiwa duniani na kuwa na maisha ya kawaida ya wanadamu. Watu hawatakuwa tena wasiomtii Mungu ama kumpinga Mungu; watarudia maisha asili ya Adamu na Hawa. Haya ndiyo maisha na hatima binafsi ya Mungu na binadamu baada ya kuingia rahani. Kushindwa kwa Shetani ni mwelekeo usioepukika katika vita kati ya Mungu na Shetani. Kwa njia hii, kuingia kwa Mungu rahani baada ya kukamilika kwa kazi Yake ya usimamizi na wokovu kamili wa mwanadamu na kuingia rahani pia kunakuwa mielekeo isiyoepukika. Pahali pa pumziko pa mwanadamu ni duniani, na pahali pa Mungu pa pumziko ni mbinguni. Mwanadamu anapomwabudu Mungu katika pumziko, ataishi duniani, na Mungu anapoongoza sehemu iliyobaki ya binadamu katika pumziko, Atawaongoza kutoka mbinguni, sio kutoka duniani. Mungu bado atakuwa Roho, wakati mwanadamu bado atakuwa mwili. Mungu na mwanadamu wote wawili wana njia zao tofauti za kupumzika. Mungu anapopumzika, Atakuja na kujitokeza miongoni mwa mwanadamu, mwanadamu anapopumzika, ataongozwa na Mungu kutembea mbinguni na pia kufurahia maisha mbinguni. Baada ya Mungu na mwanadamu kuingia rahani, Shetani hatakuweko tena, na kama Shetani, wale watu waovu pia hawatakuweko tena. Kabla ya Mungu na mwanadamu kuingia rahani, wale watu waovu waliomtesa Mungu wakati mmoja duniani na adui waliokuwa hawamtii duniani watakuwa tayari wameangamizwa; watakuwa wameangamizwa na majanga makubwa ya siku za mwisho. Baada ya hao watu waovu kuangamizwa kabisa, dunia haitajua tena unyanyasaji wa Shetani. Binadamu watapata wokovu kamili, na hapo tu ndipo kazi ya Mungu itaisha kabisa. Haya ndiyo masharti ya Mungu na mwanadamu kuingia rahani.
Kukaribia kwa mwisho wa kila kitu kunaonyesha mwisho wa kazi ya Mungu na kunaonyesha mwisho wa maendeleo ya binadamu. Hii inamaanisha kwamba binadamu kama walivyopotoshwa na Shetani wamefika mwisho wake wa maendeleo, na kwamba vizazi vya Adamu na Hawa vimeenea hadi mwisho wao binafsi, na pia inamaanisha kwamba haiwezekani kwa binadamu kama hawa, baada ya kupotoshwa na Shetani, kuendelea kustawi. Adamu na Hawa wa mwanzoni hawakuwa wamepotoshwa, lakini Adamu na Hawa waliofukuzwa kutoka Bustani ya Edeni walivurugwa na Shetani. Wakati Mungu na mwanadamu wanaingia rahani pamoja, Adamu na Hawa—waliofukuzwa kutoka Bustani ya Edeni—na vizazi vyao hatimaye watafika mwisho; binadamu wa baadaye bado watakuwa na vizazi vya Adamu na Hawa, lakini hawatakuwa watu wanaomilikiwa na Shetani. Badala yake, watakuwa watu waliookolewa na kutakaswa. Hawa watakuwa binadamu ambao wamehukumiwa na kuadibiwa, na walio watakatifu. Hawa watu hawatakuwa sawa na jamii ya binadamu kama ilivyokuwa awali; mtu anaweza kusema kwamba hao ni watu wa aina tofauti kabisa na Adamu na Hawa wa awali. Hawa watu watakuwa wamechaguliwa kutoka miongoni mwa wote waliopotoshwa na Shetani, na watakuwa ndio watu ambao hatimaye wamesimama imara wakati wa hukumu na kuadibu kwa Mungu, watakuwa kundi la mwisho la watu miongoni mwa wanadamu potovu. Kundi hili la watu ndilo tu litaweza kuingia katika raha ya mwisho pamoja na Mungu. Wanaoweza kusimama imara wakati wa kazi ya Mungu ya hukumu na kuadibu siku za mwisho—yaani, wakati wa kazi ya mwisho ya utakaso—watakuwa wale watakaoingia katika raha ya mwisho na Mungu; kwa hivyo, wanaoingia rahani wote watakuwa wametoka katika ushawishi wa shetani na kupokewa na Mungu baada tu ya kupitia kazi Yake ya mwisho ya utakaso. Hawa watu ambao hatimaye wamepokewa na Mungu wataingia katika raha ya mwisho. Kiini cha kazi ya Mungu ya kuadibu na hukumu ni kutakasa binadamu, na ni ya siku ya raha ya mwisho. Vinginevyo, binadamu wote hawataweza kufuata aina yao ama kuingia katika raha. Hii kazi ni njia ya pekee ya binadamu kuingia rahani. Kazi ya Mungu ya utakaso pekee ndiyo itatakasa udhalimu wa binadamu, na kazi Yake ya kuadibu na hukumu pekee ndiyo itadhihirisha hayo mambo yasiyotii miongoni mwa binadamu, hivyo kutenga wanaoweza kuokolewa kutoka wale wasioweza, na wale watakaobaki kutoka wale ambao hawatabaki. Kazi Yake itakapoisha, wale watu watakaobaki watatakaswa na kufurahia maisha ya pili ya binadamu ya ajabu zaidi duniani waingiapo ulimwengu wa juu wa binadamu; kwa maneno mengine, wataingia katika siku ya binadamu ya raha na kuishi pamoja na Mungu. Baada ya wasioweza kubaki kupitia kuadibu na hukumu, umbo zao halisi zitafichuliwa kabisa; baada ya haya wote wataangamizwa na, kama Shetani, hawatakubaliwa tena kuishi duniani. Binadamu wa baadaye hawatakuwa tena na aina yoyote ya watu hawa; watu hawa hawafai kuingia eneo la raha ya mwisho, wala hawafai kuingia siku ya raha ambayo Mungu na mwanadamu watashiriki, kwani ni walengwa wa adhabu na ni waovu, na si watu wenye haki. Walikuwa wamekombolewa wakati mmoja, na pia walikuwa wamehukumiwa na kuadibiwa; walikuwa pia wamemhudumia Mungu wakati mmoja, lakini siku ya mwisho itakapofika, bado wataondolewa na kuangamizwa kwa sababu ya uovu wao na kwa sababu ya kutotii na kutokombolewa kwao. Hawatakuwa tena katika ulimwengu wa baadaye, na hawatakuweko tena miongoni mwa jamii ya binadamu ya baadaye. Watenda maovu wote na yeyote na wote ambao hawajaokolewa wataangamizwa wakati watakatifu miongoni mwa binadamu wataingia rahani, bila kujali kama wao ni roho za wafu ama wale wanaoishi bado katika mwili. Bila kujali enzi ya hizi roho zitendazo maovu na watu watenda maovu, ama roho za watu wenye haki na watu wanaofanya haki wako, mtenda maovu yeyote ataangamizwa, na yeyote mwenye haki ataishi. Iwapo mtu ama roho inapokea wokovu haiamuliwi kabisa kulingana na kazi ya enzi ya mwisho, lakini inaamuliwa kulingana na iwapo wamempinga ama kutomtii Mungu. Kama watu wa enzi ya awali walifanya maovu na hawangeweza kuokolewa, bila shaka wangekuwa walengwa wa adhabu. Kama watu wa enzi hii wanafanya maovu na hawawezi kuokolewa, hakika wao pia ni walengwa wa adhabu. Watu wanatengwa kwa msingi wa mema na mabaya, sio kwa msingi wa enzi. Baada ya kutengwa kwa msingi wa mema na mabaya, watu hawaadhibiwi ama kutuzwa mara moja; badala yake, Mungu atafanya tu kazi Yake ya kuwaadhibu waovu na kuwatuza wema baada ya kufanya kazi Yake ya ushindi katika siku za mwisho. Kwa kweli, Amekuwa akitumia mema na mabaya kutenga binadamu tangu Afanye kazi Yake miongoni mwa binadamu. Atawatuza tu wenye haki na kuwaadhibu waovu baada ya kukamilika kwa kazi Yake, badala ya kuwatenga waovu na wenye haki baada ya kukamilika kwa kazi Yake mwishowe na kisha kufanya kazi Yake ya kuwaadhibu waovu na kuwatuza wazuri mara moja. Kazi Yake ya mwisho ya kuadhibu waovu na kuwatuza wazuri inafanywa kabisa ili kutakasa kabisa binadamu wote, ili Aweze kuleta binadamu watakatifu mno katika pumziko la milele. Hatua hii ya kazi Yake ni kazi Yake muhimu zaidi. Ni hatua ya mwisho ya kazi Yake yote ya usimamizi. Kama Mungu hangewaangamiza waovu lakini badala yake kuwaacha wabakie, basi binadamu wote bado hawangeweza kuingia rahani, na Mungu hangeweza kuleta binadamu katika ulimwengu bora. Kazi ya aina hii haingekuwa imekamilika kabisa. Atakapomaliza kazi Yake, binadamu wote watakuwa watakatifu kabisa. Mungu anaweza kuishi kwa amani rahani kwa namna hii pekee.
kutoka kwa Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja

Jumapili, 10 Februari 2019

Ufahamu wa Kupata Mwili

Mwenyezi Mungu alisema | Sura ya 17. Ufahamu wa Kupata Mwili

Kumjua Mungu kunapaswa kufanywa kupitia kwa kusoma neno la Mungu na kulielewa neno la Mungu. Watu wengine husema: "Sijamwona Mungu mwenye mwili, hivyo nitawezaje kumjua Mungu?" Neno la Mungu kwa kweli ni maonyesho ya tabia ya Mungu. Kutoka kwa neno la Mungu unaweza kuuona upendo wa Mungu kwa wanadamu, wokovu Wake wa wanadamu, na jinsi Anavyowaokoa ... kwa sababu neno la Mungu linaonyeshwa na Mungu ikilinganishwa na Mungu kumtumia mwanadamu kuliandika. Linaonyeshwa na Mungu binafsi. Ni Mungu Mwenyewe Akielezea maneno Yake mwenyewe na sauti Yake ya ndani. Kwa nini tunayaita maneno ya dhati? Kwa sababu hayo hutolewa kutoka ndani kabisa, Akionyesha tabia Yake, mapenzi Yake, mawazo Yake, upendo Wake kwa wanadamu, wokovu Wake wa wanadamu, na matarajio Yake ya wanadamu. Miongoni mwa maneno ya Mungu kuna maneno makali, maneno ya upole na laini, maneno mengine yenye kuzingatia, na kuna maneno mengine ya ufunuo ambayo hayana utu. Ikiwa unayaangalia tu maneno ya ufunuo, unahisi kwamba Mungu ni mkali kabisa. Ikiwa unaangalia upande wa upole na laini tu, Mungu anaonekana kuwa hana mamlaka mengi. Kwa hiyo hupaswi kuelewa nje ya muktadha katika hili. Lazima uliangalie kutoka kila pembe. Wakati mwingine Mungu huzungumza kwa mtazamo mpole na wenye huruma, na watu wanauona upendo wa Mungu kwa wanadamu; wakati mwingine Yeye huzungumza kwa mtazamo mkali, na watu wanaona tabia ya Mungu isiyoweza kukosewa. Mwanadamu ni mchafu kwa njia ya kusikitisha na hastahili kuuona uso wa Mungu, na hastahili kuja mbele za Mungu. Watu kuja mbele za Mungu sasa ni kwa neema ya Mungu tu. Hekima ya Mungu inaweza kuonekana kutokana na jinsi Mungu anavyofanya kazi na maana ya kazi Yake. Hata kama watu hawajakutana na Mungu, bado wataweza kuona mambo haya katika neno la Mungu. Mtu ambaye ana ufahamu wa kweli anapokutana na Kristo, ufahamu wake unaweza kufanana na Wake, lakini wakati mtu ambaye ana ufahamu wa kinadharia tu anakuja katika mawasiliano na Mungu, hauwezi kufananishwa na Yeye. Kipengele hiki cha ukweli ni siri ya kina zaidi, ni ngumu kuelewa. Yafupishe maneno ambayo Mungu anasema juu ya siri ya kupata mwili, yaangalie kutoka pembe mbalimbali, kisha yajadili mambo haya miongoni mwenu. Unaweza kuomba, na kutafakari na kujadiliana sana kuhusu mambo haya. Labda Roho Mtakatifu huwaangazia na kukuwezesha kuyaelewa. Hii ni kwa sababu huna nafasi ya kuwasiliana na Mungu, na lazima utegemee uzoefu kwa njia hii ili kuihisi njia yako kidogo kidogo, ili kufikia ufahamu wa kweli wa Mungu.
Ukweli kuhusu kumjua Kristo na kumjua Mungu Mwenyewe ni wa kina zaidi. Ikiwa watu huweka mkazo juu ya kutafuta kipengele hiki cha ukweli, hata hivyo, ndani yao watakuwa waangavu na thabiti, na watakuwa na njia ya kutembea. Kipengele hiki cha ukweli kinafanana sana na moyo wa mwanadamu. Ikiwa mtu hana ukweli katika kipengele hiki, atakosa nguvu. Kadri mtu alivyo na maarifa zaidi ya kipengele hiki cha ukweli, ndivyo alivyo na nguvu zaidi. Sasa kuna watu wengine ambao husema: Katika uchambuzi wa mwisho, kupata mwili ni nini? Semi hizi zinaweza kuthibitisha kwamba Yeye ni Mungu mwenye mwili? Je! Maneno haya yanaweza kuthibitisha kwamba Yeye ni Mungu Mwenyewe? Ikiwa Hangesema maneno haya bado Angekuwa Mungu Mwenyewe? Au kama Angekuwa Amesema tu baadhi ya maneno, Angeweza kuwa Mungu bado? Ni nini kinachoamua kwamba Yeye ni Mungu? Je, inaamuliwa tu kwa maneno haya? Hili ni swali muhimu. Watu wengine hutambua maneno haya kwa njia visivyo sahihi kama agizo la Roho Mtakatifu, kwamba Alimaliza kutoa maagizo na kuondoka, kwamba Roho Mtakatifu aliacha kufanya kazi, kwamba mwili huu si zaidi ya mwili wa kawaida na mwili wa nyama, kwamba mwili huu hauwezi kuitwa Mungu, badala yake Anaweza kuitwa Mwana wa Adamu, na hawezi kuitwa Mungu. Watu wengine wanaielewa visivyo kwa njia hii. Basi, asili ya kutoelewa huku iko wapi? Ni kwamba watu hawajaelewa kupata mwili vizuri kabisa, na hawajafukua kwa undani. Watu wanaelewa kupata mwili kwa juu juu sana, na wanao ufahamu wa ujuzi kidogo tu. Ikiwa kusema maneno mengi ni sawa na Kwake kuwa Mungu, basi kusema maneno machache tu, badala ya mengi, pia kunamaanisha kwamba yeye ni Mungu? Kwa kweli kusema Kwake maneno machache pia ni maonyesho ya uungu. Je! Yeye ni Mungu? Kazi ambayo Mungu hufanya ina umuhimu mkubwa. Imeishinda mioyo ya wanadamu na kulipata kundi la watu. Je, kazi hiyo haingekuwa imemalizika, ingewezekana kumjua Yeye kama Mungu Mwenyewe? Hapo awali kulikuwa na watu ambao, wakati kazi ilikuwa imefanyika nusu, walifikiri hivi: Kama ninavyoona, kazi hii inapaswa kubadilika. Nani anayeweza kusema kupata mwili kweli ni nini! Je! Huku ni kuwa na mtazamo wa kutoamini kuhusiana na kupata mwili kwa Mungu? Kwamba unaweza kuwa na shaka kuhusu kupata mwili kwa Mungu kunaonyesha kwamba huamini katika kupata mwili, huamini kwamba Yeye ni Mungu, huamini kwamba Ana dutu ya Mungu, na huamini kwamba maneno Aliyosema yametoka kwa Mungu. Hata zaidi huamini kwamba maneno Aliyosema ni ufunuo wa tabia Yake Mwenyewe, na maonyesho ya dutu Yake. Watu wengine walizungumza kwa njia hii: Kama ninavyoona, njia ya Mungu ya kufanya kazi inapaswa kubadilika. Haijulikani kupata mwili ni nini hasa, na labda lazima kuwe na ufafanuzi mwingine kuuhusu. Kuna baadhi ya watu ambao husubiri na kuona, kuona kama kuna sauti yoyote kwa maneno yaliyonenwa na Mungu mwenye mwili Anayeketi pale, iwapo Anasema ukweli, na kama amesema chochote kipya. Ningekuwa na mashine ya eksirei ningeangalia na kuona ikiwa kuna ukweli wowote ndani ya tumbo Lake. Ikiwa hakuna ukweli, na kama Yeye ni mtu, basi nitatoroka kwa haraka, na sitaamini. Ningeangalia na kuona ikiwa Roho wa Mungu anafanya kazi ndani Yake, ikiwa Roho wa Mungu anamsaidia, na kumwongoza katika usemi Wake. Watu wengine wanashuku kwa njia hii, na daima wana wasiwasi kuhusu shida hii katika mioyo yao. Hali hii ipo kwa sababu gani? Si kwa sababu nyingine yoyote ila utambuzi wa juu juu ndani ya mwili. Hawaujui kikamilifu, na hawajafikia kiwango cha juu katika ufahamu wao. Kwa sasa, wanakubali tu kwamba mtu huyu ana Roho wa Mungu. Kusema, hata hivyo, kwamba ndani Yake kuna dutu ya Mungu, tabia ya Mungu, na kusema kwamba Yeye ana kile Mungu alicho na kile Alicho nacho, Ana Mungu mzima, na kusema kwamba Yeye si mwingine ila ni Mungu, ni vigumu kwa watu wengine kuelewa kikamilifu. Maneno hayanaonekani kufanana na mtu katika mambo kadhaa. Kile wanachoona watu na kile wanachoamini sio dutu ya Mungu. Kwa maneno mengine, kile watu wanachoona ni maneno hayo tu na kazi halisi. Watu hufikiri tu kwamba Mungu alifanya sehemu ya kazi, kwamba Mungu mwenye mwili Anaweza tu kufanya sehemu hii ya kazi. Hakuna mtu hata mmoja anayeamini kwamba ingawa kupata mwili sasa kunaonyesha sehemu hii ya kazi, Ana asili yote ya uungu. Hakuna mtu anayefikiria kwa njia hii. Sasa baadhi ya watu husema: "Kumjua Mungu mwenye mwili ni kugumu sana. Ingekuwa ni Roho wa Mungu anayefanya kazi moja kwa moja tungeweza kuelewa kwa urahisi. Tungeweza kuona moja kwa moja nguvu za Mungu na mamlaka ya Mungu katika kazi ya Roho. Kisha ingekuwa rahisi kumjua Mungu. "Je, neno hili linafaa? Sasa Nawauliza swali hivi: "Ni rahisi kumjua Mungu mwenye mwili au ni rahisi kumjua Roho? Ikiwa Mungu mwenye mwili Alifanya kazi kama Yehova, ni yupi Angekuwa rahisi kumwelewa? "Unaweza kusema Wao wote ni Wagumu kuelewa. Kama kungekuwa na njia, Wote wawili wangekuwa rahisi kuelewa. Kama hakungekuwa na ufahamu wa kiroho, wote wawili wangekuwa wagumu kuelewa. Je! Watu pia hawakuelewa kazi na maneno ya kupata mwili mwanzoni? Je! Wote waliyaelewa visivyo? Watu hawakujua kile ambacho Mungu alikuwa Anafanya; hakuna kitu kilichofanana na mawazo ya watu! Je! Watu wote waliibuka na mawazo? Hii inaonyesha kuwa watu hawamjui Mungu mwenye mwili kwa urahisi. Ni vigumu kama kumjua Roho, kwa sababu kazi ya kupata mwili ni maonyesho ya Roho, ni kwamba tu watu wanaweza kuona na kugusa kupata mwili. Ni nini maana ya ndani ya kupata mwili, hata hivyo, na ni nini kusudi la kazi Yake, inamaanisha nini, ni vipengele gani vya tabia Yake inavyowakilisha, na kwa nini Amefunuliwa kwa njia hii, watu huenda hawaelewi, sivyo? Kwamba huelewi inaonyesha kwamba hujui. Roho alikuja kufanya kazi, kusema seti ya maneno, na kisha Akaondoka. Kile ambacho watu wanafanya ni kuyatii na kuyafanya tu, lakini watu wanajua kwa kweli ni nini? Je! Watu wanaweza kujua tabia ya Yehova kutoka kwa maneno haya? Watu wengine husema kwamba Roho ni rahisi kumjua, kwamba Roho alikuja kufanya kazi Akibeba umbo la kweli la Mungu. Je, Yeye ni mgumu kumjua kivipi? Hakika unaijua picha Yake ya nje, lakini unaweza kujua kiini cha Mungu? Sasa Mungu mwenye mwili ni mtu wa kawaida ambaye unahisi ni rahisi kuwasiliana naye. Hata hivyo, wakati asili Yake na tabia Yake vinavyoonyeshwa, watu wanajua mambo hayo kwa urahisi? Je! Watu hukubali kwa urahisi maneno yale ambayo Alisema ambayo hayalingani na mawazo yao? Sasa watu wote wanasema kuwa kumjua Mungu mwenye mwili ni vigumu. Ikiwa Mungu baadaye Angegeuzwa, basi ingekuwa rahisi sana kumjua Mungu. Watu ambao husema hili huweka wajibu wote juu ya Mungu mwenye mwili. Je! Hiyo ndivyo ilivyo kwa kweli? Hata kama Roho angewasili hungeweza kumjua vile vile. Roho aliondoka mara tu baada ya kumaliza kuzungumza na watu, na hakuwaeleza mambo mengi sana, na hakushiriki na kuishi nao kwa njia ya kawaida. Watu hawakuwa na nafasi ya kumjua Mungu kwa namna ya utendaji zaidi. Faida ya kazi ya Mungu mwenye mwili kwa watu ni kubwa sana. Ukweli ambao huwaletea watu ni wa utendaji zaidi. Unawasaidia watu kumwona Mungu wa utendaji Mwenyewe. Hata hivyo, kujua kiini cha kupata mwili na kiini cha Roho ni vigumu vile vile. Hivi pia ni vigumu kujua.
Kumjua Mungu kunamaanisha nini? Kunamaanisha kwamba mtu anajua upeo wa hisia za Mungu, hii ndiyo maana ya kumjua Mungu. Unasema kwamba umemwona Mungu, ilhali huelewi upeo wa hisia za Mungu, huelewi tabia Yake, na wala hujui haki Yake. Huna ufahamu wa rehema Zake, wala hujui Anachokichukia. Hili haliwezi kuitwa ufahamu wa Mungu. Kwa hivyo, watu wengine wanaweza kumfuata Mungu, lakini hawamwamini Mungu hasa. Hii ndiyo tofauti. Ikiwa unamjua, unamwelewa, ikiwa unaweza kuelewa na kushika baadhi ya kile mapenzi Yake ni, na unaujua moyo Wake, basi unaweza kumwamini kwa kweli, unaweza kujisalimisha Kwake kwa kweli, kumpenda kwa kweli, na kumwabudu Yeye kwa kweli. Ikiwa huelewi mambo haya, basi unafuata tu, mtu anayefuata tu na kufuata umati. Hiyo haiwezi kuitwa kujisalimisha kwa kweli, na haiwezi kuitwa ibada ya kweli. Je! Ibada ya kweli inaweza kuzalishwaje? Hakuna watu wowote wanaomwona Mungu na kumjua Mungu ambao hawamwabudu Yeye, ambaye hawamheshimu. Mara tu wanapomwona Mungu wanaogopa. Kwa sasa watu wako katika wakati wa kazi ya Mungu mwenye mwili. Kadri watu wanavyokuwa na ufahamu wa tabia ya Mungu mwenye mwili na wa kile Alicho nacho na kile Alicho, ndivyo watu wengi watakavyovithamini, na ndivyo watakavyomheshimu Mungu. Mara nyingi, ufahamu mdogo unamaanisha kutokuwa waangalifu zaidi, kiasi kwamba Mungu anachukuliwa kama mwanadamu. Watu wataogopa na kutetemeka ikiwa wanamjua Mungu kwa kweli na kumwona kwa hakika. Kwa nini Yohana alisema, "Yeye anayekuja baada yangu, ambaye mimi sistahili kubeba viatu vyake"? Ijapokuwa ufahamu wake ndani ya moyo wake haukuwa wa kina kirefu sana, lakini alijua kwamba Mungu ni wa ajabu. Ni watu wangapi wanaoweza kumcha Mungu sasa? Bila kuijua tabia ya Mungu, mtu anawezaje kumheshimu? Ikiwa watu hawajui kiini cha Kristo, na hawaelewi tabia ya Mungu, hawawezi hata kumwabudu Mungu kwa kweli. Ikiwa watu wanaona tu kuonekana kwa nje kwa kawaida kwa Kristo na hawajui asili Yake, ni rahisi kwa watu kumchukulia Kristo kama mtu wa kawaida. Wanaweza kuchukua mtazamo usio wa heshima Kwake, wanaweza kumdanganya, kumkataa, kutomtii, kutoa hukumu Kwake, na kuwa na maoni. Wanaweza kuchukua neno Lake kama lisilo na maana, wanaweza kuutendea mwili Wake kama wanavyotaka, wanaweza kuwa na mawazo, na wanaweza kukufuru. Ili kutatua masuala haya mtu lazima ajue kiini cha Kristo, uungu wa Kristo. Hiki ndicho kipengele kikuu cha kumjua Mungu; ndicho watu wote wanaoamini katika Mungu wa utendaji wanapaswa kuingia na kufanikisha.
kutoka kwa Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo

Jumamosi, 9 Februari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Njia ya Huduma ya Kidini lazima Ipigwe Marufuku”

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Njia ya Huduma ya Kidini lazima Ipigwe Marufuku”

Mwenyezi Mungu anasema, “Kuanzia leo, Mungu ataweza kuwafanya watu wasiokuwa na fikira za kidini kuwa watimilifu kwa njia rasmi, ambao wako tayari kuweka pembeni nafsi zao za kale, na ambao wanamtii tu Mungu, pamoja na kuwafanya kuwa watimilifu wale wanaotamani neno la Mungu. Watu hawa wanafaa kusimama na kumhudumia Mungu. Kwake Mungu kunayo na hekima nyingi na isiyoisha. Kazi yake ya kustaajabisha na matamshi yake yenye thamani ni vitu ambavyo vipo ili watu wengi zaidi kuweza kufurahia. Kama ilivyo sasa, vitu hivi vipya haviwezi kukubaliwa na wale walio na fikira za kidini, wanaochukua hali ya ukubwa, na wale ambao hawaweki pembeni nafsi zao za kale. Roho Mtakatifu hana fursa ya kuwafanya watu kama hao kuwa watimilifu. Kama mtu hana hamu ya kutii, na hana kiu cha neno la Mungu, basi mtu huyo hataweza kupokea mambo mapya. Wataendelea tu kuasi zaidi na zaidi, kuwa wajanja zaidi na zaidi, na hatimaye kujipata kwenye njia mbaya. Katika kazi ya Mungu ya sasa, Atawainua watu zaidi wanaompenda Yeye kwa kweli na wanaoweza kukubali mwangaza mpya. Na Atakatiza kabisa maafisa wa kidini wanaoonyesha ukubwa wao. Hataki mtu hata mmoja anayekataa mabadiliko.”

Ijumaa, 8 Februari 2019

Imani Tatu katika Mungu wa Vitendo

Sura ya 16. Imani Tatu katika Mungu wa Vitendo

Ndani ya familia ya Mungu, kuna imani kadhaa tofauti katika Mungu; imani hizi tofauti lazima zitambulishwe ili kuona wewe ni wa gani.
Na imani ya aina ya kwanza, ambayo pia ni aina bora zaidi, mtu huyo ana uwezo wa kuyaamini maneno ya Mungu katika vitu vyote; ana uwezo wa kukubali ufichuzi wote wa Mungu, ushugulikiaji, na upogoaji; yeye ni mwagalifu kwa mapenzi ya Mungu, hupenda, ni mwaminifu kwa, na humwabudu Mungu, na ako tayari kutenda ukweli. Imani kama hiyo huzaa maisha, na inawezesha mtu kupata mabadiliko katika tabia na kupatwa na Mungu.
Na imani ya aina ya pili, mtu huyo anamwamini Mungu kwa kiasi, lakini pia ni mwenye tuhumu kwa kiasi. Wakati kazi ya Mungu hairidhiani na yeye, angefanya ulinganishi katika moyo wake, akiwa na shaka kama Mungu Anapaswa kuwa akifanya vitu kama hivyo. Mara kwa mara anamtuhumu Mungu, kwa hivyo ana uwezo tu wa kumtii Mungu kwa kiasi, na hana uwezo wa kumtii Mungu katika vitu vingine; anaweza kulitii lile ambalo analiamini ni sawa, lakini ana mawazo yake mwenyewe anapokabiliwa na vitu ambavyo anahisi si sawa, na migongano katika moyo wake, na anakataa kuyatekeleza. Hili pia ni aina ya imani. Kimo cha watu siku hizi ni hasa kama hiki, wao wana uwezo tu wa kutii kile wanachohisi kuwa sawa, wao hawana uwezo wa kutii kile wanachohisi si sawa, na hawatatekeleza kile ambacho hawako tayari kufanya. Kadhalika, wakati mwingine hali ikiwa, wana shauku na Mungu, wakihisi kwamba wanapaswa kuwa waangalifu kwa mzigo wa Mungu, hivyo wanatimiza wajibu wao; au wakati mwingine wanashughulishwa na ushirika, wanapata Mungu kuwa wa kupendeka kabisa, na sasa tu ndio wenye imani katika Mungu kwa kiasi fulani. Hasa, imani yao katika Mungu ni tu kufuata umati; hawana upendo kwa Mungu, wala si waangalifu kwa Mungu, wakati bila shaka hawamtii na hawamwabudu Mungu kwa kweli. Kwa watu walio na imani kama hii katika Mungu, wako tu na kiasi cha wastani cha upendo, uangalifu, na utiifu kwa Mungu, kwa muda fulani, na inafanyika tu wakati Roho Mtakatifu hasa Anasonga, wakati Roho Mtakatifu anafanya kazi Yake. Wakati wako katika hali mbaya, au wakati wanachanganywa na wengine, wakati wao ni dhaifu na wamekata tamaa, vitu hivi vimeenda, vimetokomea, wakati wao wenyewe hawana habari jinsi hilo limekuja kupita. Hawana uwezo tena wa kumpenda Mungu hata wakitaka, hawana motisha ya kutenda maneno ya Mungu tena, na kisha wanaona kazi ya Mungu kama ya desturi sana, ya kawaida sana; hata kama wao hawana tuhuma tena, wao hawana ari yoyote tena. Kimo cha watu wengi zaidi kiko katika hatua hii, na hii ndiyo aina ya pili ya imani.
Na aina ya tatu ya imani, mtu hana uelewa wa Mungu mwenye mwili, kwake Yeye hujitokeza tu kama mtu wa kawaida, na hakuna tofauti kubwa inaweza kutambulishwa. Kwa hivyo, anamchukulia Mungu mwenye mwili kama tu mtu wa kawaida lakini mwenye cheo cha heshima, ana uwezo wa kufuatana na Mungu na kusema kitu kizuri, na pia ana uwezo wa kuandamana katika imani, lakini imani hii si imani halisi. Ana uwezo wa kufuatana na mambo ya upuuzi mara moja moja, lakini hakuna upendo kwa Mungu katika mtu wa aina hii—upendo si kujali kuhusu mwili lakini utiifu wa kweli katika kazi ya mtu na katika kutimiza wajibu wa mtu, kuwa mwangalifu kwa Mungu na kumcha Mungu. Upendo kwa Mungu ni kitu ambacho mtu aliye na uzoefu mkubwa tu anaweza kutangaza, si kitu ambacho mtu anaweza kusema kwa kupitia tu, kuona kwamba mtu ametekwa na hisia kali hivyo kusema kwamba huyu na huyu humpenda Mungu sana. Ama kusema kwamba watu kutoka dhehebu fulani humpenda Mungu kwa kweli. Huu ni upuuzi. Mtu kama huyu hawezi kukubali na kutii kwa urahisi kunapokuja kwa mambo ya upuuzi, na anapokabiliwa na mambo ya muhimu yanayohusiana na ukweli, hawezi kutii tu, na pia ana mawazo yake mwenyewe, hata anakuwa na tuhuma kuhusu Mungu. Watu kama hawa pia wako katika walio wengi. Wao ni wenye tuhuma kila wakati kuhusu Mungu: Je, huyu ni Mungu? Je, ni kwa nini Yeye hafanani na Mungu? Baadhi ya mambo Alivyosema labda yameelekezwa na Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu alimwelekeleza kusema mambo fulani, na kufanya vitu fulani. …Imani ya watu kama hawa ni ya kusikitisha zaidi.
Kiwango cha imani ya mtu katika Mungu, utiifu kwa Mungu, upendo, uangalifu, na uchaji kwa Mungu, kinatambulishwa hasa na yafuatayo:
Kwanza, kina msingi katika ikiwa mtu huyo hupenda ukweli. Kama unapenda ukweli basi unaweza kuendelea kuufuatilia zaidi, kisha unaweza kulenga kuwa na uelewa wa ukweli, wa maneno ya Mungu, wa kazi ya Mungu, wa umuhimu wa kupata mwili kwa Mungu, wa tabia ya Mungu, na uelewa wa Mungu una msingi hasa katika hiki kitu kimoja. Kadiri Unavyoweza kuelewa Mungu zaidi ndivyo unavyoweza kumtambua zaidi; kadiri unavyoweza kumwelewa Mungu zaidi ndivyo unavyoweza kumfuata bila kuyumbayumba. Hiyo ni, uelewa wa Mungu una msingi katika kufuatilia ukweli.
Pili, kina msingi katika uelewa wa mtu huyo wa Mungu mwenye mwili, hiyo ni muhimu. Bila uelewa wa Mungu wa vitendo, mazungumzo ya kumtii Mungu, kumpenda Mungu, kushuhudia Mungu, na kumhudumia Mungu yote ni maneno matupu. Vitu kama hivi haviwezi tu kufikiwa.
Tatu, kina msingi katika ubinadamu wa mtu huyo, lakini hili si halisi. Kwa sababu, baadhi ya watu wana ubinadamu mzuri, wao ni watu wazuri, lakini wao hawapendi ukweli. Kama wao hawana uelewa kabisa wa Mungu mwenye mwili, basi imani yao haiwezi kusiama, na wakati mwingine nia zao nzuri bila kujua husababisha madakizo. Je, unaweza kusema kwamba wao ni watu ambao wanamwamini Mungu kwa kweli? Wao ni wenye shauku, ni wa asili nzuri, na hufanya mambo fulani mazuri, lakini haya ni tabia nzuri tu ya nje, haya ni sura ya juu juu, haya hayaonyeshi kwamba imani yao ni halisi. Ukisema kwamba kwa kweli unamwamini Mungu, kweli unampenda Mungu, lazima uwe na uwezo wa kusema kwa nini unampenda Mungu, upendo wako kwa Mungu una msingi kwa nini, kwa nini unamwamini Yeye, kama wewe unaufuata umati tu ama unamwamini Yeye kwa sababu unaweza kumwona kwa kweli kama Mungu, imani na upendo wako kwa Mungu yana msingi katika ukweli upi: Haya lazima yategemezwe kwa misingi. Baadhi ya watu hupenda kusema kwamba wanamwamini Mungu kwa kweli na wanampenda Mungu, lakini wakati mtu anatamani kuwasiliana nao ukweli kwa uzito, hawana kitu cha kusema. Nimesikia watu wengi wakisema: “Mimi husikiza chochote ambacho Mungu husema, naamini yote ambayo Mungu husema, kwa njia yoyote ambayo Yeye huyasema. Sina mawazo yangu mwenyewe bila kujali kile Mungu husema, sina mawazo yangu mwenyewe bila kujali kile Mungu hufanya.” Je, wewe kweli ni mtu anayempenda Mungu kwa sababu tu umesema mambo kama haya? Lazima uwe na uzoefu halisi, lazima uwe na uwezo wa kuongea kuhusu uelewa halisi wa Mungu mwenye mwili. Pia, ni nini kiini cha Mungu, ni vitu vipi ambavyo watu huona vigumu kumtii Mungu katika, ni vitu vipi ambavyo watu wanaweza kumtii Mungu katika, wanamtii Mungu kwa kiasi gani, ni vitu vipi ambavyo huna uwezo wa kumtii Mungu katika, unatatua vipi mawazo yako kuhusu Mungu, unapanua vipi uelewa wako wa Mungu polepole? Kama unakosa uzoefu kama huo, basi huna mapenzi ya kweli kwa Mungu. Baadhi ya watu wana furaha hasa wanapoona kufika kwa Mungu, wanampokea kwa ukarimu, na kisha wanalia Mungu Anapoondoka. Watu wengine hufikiri kwamba hili ni onyesho la upendo wake kwa Mungu, lakini hili kweli linaweza kuonyesha kwamba anampenda Mungu? Hili linaweza kuonyesha tu kwamba anao moyo wenye ari, lakini mtu hawezi kusema kwamba matendo na maonyesho yake ni upendo kwa Mungu, kwamba ni imani ya kweli. Baadhi ya watu hutoa pesa kiasi, lakini hilo ni upendo kwa Mungu? Ama unaenda haraka kumwaga gilasi ya maji wakati unaambiwa, lakini hilo ni utiifu wa kweli? Kadhalika, watu wengine husema: “Nilimwamini Mungu baada ya mimi kusoma maneno ya Mungu, niliamini katika kupata mwili kwa Mungu, sina shaka baada ya mimi kumwona Mungu katika mwili wa kawaida.” Je, hili linaweza kuitwa imani ya kweli? Je, umekuwa na ushughulikaji na Mungu? Je, umejihusisha na Yeye? Je, unajua tabia Yake? Je, unajua ni nini Yeye hupenda? Je, unajua vitu unafanya ambavyo vinaikosea tabia Yake? Je, unajua upotovu ndani yako ambao Yeye huchukia? Je, unajua watu ambao Ameleta tabia Yake yenye haki kwao? Je, unajua ni watu wagani Yeye huchukia? Je, unajua ni masuala yapi unayo ambayo Yeye huchukia zaidi? Kama hujui vitu vyovyote kama hivi, linaonyesha kwamba kwa kweli huna uelewa wa Mungu. Huwezi kusema kwamba unamwamini Mungu kwa kweli, huwezi kusema kwamba unamtii Mungu kabisa, na bila shaka huwezi kusema kwamba unafanya vitu kulingana na mapenzi ya Mungu, kwamba unampenda Mungu, unamtii Mungu, ama unamwelewa Mungu. Unaweza kusema tu, kuhusu jambo hili, unayaelewa mapenzi Yake, unajua ni nini Yeye hupenda, kwamba unatenda kulingana na mapenzi ya Mungu katika jambo hili, kwamba unatenda kulingana na ukweli, kwamba unamtii katika jambo hili. Je, wewe ni mtu mtiifu kwa Mungu kwa sababu umemtii katika jambo hili tu? Huwezi kusema hilo, na kusema kwamba mtu humpenda Mungu kwa kuweka msingi tu kwa kitu cha juujuu, hilo ni kosa kubwa. Ukweli kwamba ulitenda kitu kizuri, ama kwamba umemjali Mungu hasa, huonyesha tu kwamba wewe ni mtu mwema, lakini hauonyeshi kwamba wewe ni mwangalifu kwa mapenzi ya Mungu. Bila shaka, upendo wa Mungu na kuwa mwangalifu kwa mapenzi ya Mungu yamejengwa juu ya msingi wa ubinadamu, na hakuwezi kuwa na upendo wa Mungu bila ubinadamu, kwa hivyo kila mmoja wenu lazima ajichunguze na aangalie mahali alipo. Baadhi ya watu hufikiri kwamba wao wako karibu hapo, lakini hili si lenye uhalisi; ilhali baadhi ya watu huenda kwa kiwangi kilichokithiri na hufikiri kwamba hakuna kitu kizuri kuwahusu, kwamba hawawezi kuachwa, na huu ni mtazamo hasi. Baadhi ya watu hufikiri kwamba hakuna mazuri ndani yao, na baadhi ya watu hujifafanua kama mtu anayempenda Mungu. Wao wako katika upande wa kushoto kabisa au katika upande wa kulia kabisa; huu ndio uhalisi wa watu hawa, ambao unaonyesha kwamba wao bado hawako katika njia sawa. Wao wanapaswa kuendelea kujitahidi kuwa dhahiri kuhusu ukweli, na kuingia katika uhalisi, ili kufuata mapenzi ya Mungu.
Soma Zaidi: Asili ya Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Alhamisi, 7 Februari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Ahadi kwa Wale Ambao Wamekamilishwa”

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Ahadi kwa Wale Ambao Wamekamilishwa”

Mwenyezi Mungu anasema, “Wale watakaokamilishwa na Mungu ni wale watakaopokea baraka za Mungu na urithi Wake. Yaani, wanasikia na kuelewa kile Mungu Alicho nacho na Alicho, ili kiwe kile ambacho walicho nacho ndani yao; wanayo maneno yote ya Mungu ndani yao; haijalishi ni vipi nafsi ya Mungu ilivyo, mnaweza kusikia na kuelewa kila kitu Anachokuambia vile kilivyo, na hivyo kuishi kwa kudhihirisha ukweli. Huyu ndiye aina ya binadamu aliyekamilishwa na Mungu na aliyepatwa na Mungu.”

Jumatano, 6 Februari 2019

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VII” Sehemu ya Pili

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VII” Sehemu ya Pili

Mwenyezi Mungu anasema, “Mungu ni Bwana wa kanuni zinazoudhibiti ulimwengu, Anadhibiti kanuni zinazoongoza kuishi kwa vitu vyote, na pia Anadhibiti ulimwengu na vitu vyote kiasi kwamba vinaweza kuishi pamoja; Anaifanya ili kwamba visikwishe au kutoweka ili kwamba binadamu aendelee kuishi, binadamu anaweza kuishi katika mazingira hayo kupitia uongozi wa Mungu. Kanuni hizi zinazoongoza vitu vyote zipo chini ya utawala wa Mungu, na binadamu hawawezi kuingilia na hawawezi kuzibadilisha; ni Mungu Mwenyewe pekee ndiye Anajua kanuni hizi na ni Yeye pekee ndiye anazisimamia.”

Jumanne, 5 Februari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa “Maonyo Matatu” | How to Be a Loyal Servant of God

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa “Maonyo Matatu” | How to Be a Loyal Servant of God

Mwenyezi Mungu anasema, “Kama muumini wa Mungu, hufai kuwa watiifu kwa yeyote mwingine isipokuwa Yeye katika mambo yote na mjilinganishe na moyo Wake katika mambo yote. Hata hivyo, ingawa wote huelewa mafundisho haya, ukweli huu wa kimsingi ulio wazi kabisa kwa binadamu hauwezi kuonekana kuwa kujumuishwa kwao kikamilifu, kutokana na ugumu wao, kama vile hali yao ya kutojua, upuzi, au ufisadi. Kwa hivyo, kabla ya kuuamua mwisho wenu, Ninafaa kuwaambia kwanza baadhi ya mambo, ambayo ni yenye umuhimu mkubwa sana kwenu. ... Katika maisha yenu, Naona mengi ambayo mnafanya ambayo hayana uhusiano na ukweli, kwa hivyo Nawaambia moja kwa moja muwe watumishi wa ukweli na wala si kutawaliwa na maovu na ubaya. Msikanyage ukweli na kuchafua sehemu yoyote ya nyumba ya Mungu. Hili ndilo onyo Langu kwenu.”

Jumatatu, 4 Februari 2019

Wale Wanaopenda Ukweli Wana Njia ya Kufuata

Sura ya 10. Wale Wanaopenda Ukweli Wana Njia ya Kufuata

1. Kama hali ya Watu Ni Ya Kawaida Inategemea na Kama Wanapenda Ukweli au La
Mwenyezi Mungu alisema, Watu wengi wameibua suala lifuatalo: Baada ya ushirika wa juu, wanahisi wazi kabisa, wanakuwa na nguvu zaidi, na hawana hisia hasi—lakini hali kama hiyo inabaki tu kwa karibu siku kumi, ambapo baadaye hawawezi kudumisha hali ya kawaida. Suala ni nini? Je mmewahi kujiuliza kinachosababisha hili? Mbona hali zenu ni nzuri sana katika siku hizo takriban kumi za kwanza? Wengine wanasema kuwa hili ni tokeo la kutolenga ukweli. Lakini hivyo ungeweza vipi kufikia kiwango hiki cha kawaida baada ya kusikia ushirika? Mbona ulikuwa na furaha sana baada ya kuusikia ukweli? Wengine wanasema ni kwa sababu ya kazi ya Roho Mtakatifu. Mbona basi kazi ya Roho Mtakatifu inakoma baada ya takriban siku kumi? Wengine husema ni kwa sababu wanakuwa wazembe na kuacha kusonga mbele na juu. Mbona basi hili linafanyika hata wakati watu wanapojaribu kufanya maendeleo? Mbona Roho Mtakatifu pia hafanyi kazi? Je, hukuwa unajaribu kusonga mbele na juu? Basi mbona Roho Mtakatifu hayuko kazini? Sababu ambazo watu hutoa haziko sambamba na hali ya kweli. Hapa, lazima tuibue hoja ifuatayo: Kama Roho Mtakatifu yuko kazini au la, ushirikiano wa watu binafsi hauwezi kupuuzwa. Watu walio wazi kuhusu ukweli na wanapenda ukweli kila wakati watakuwa na uwezo wa kubaki katika hali ya kawaida, bila kujali kama Roho Mtakatifu yuko kazini ama hapana. Kwa wale wasiopenda ukweli—hata kama ukweli hasa ni wazi kwao na hata kama Roho Mtakatifu anafanya kazi sana—kuna upeo kwa ukweli ambao wanaweza kuweka katika vitendo na kiwango cha muda ambao wanaweza kutenda. Mbali na wakati huo, hawafanyi chochote zaidi ya kudhihirisha asili yao wenyewe na maslahi yao wenyewe. Ipasavyo, kama hali ya mtu itafikia kiwango cha kawaida ama hapana na kama atauweka ukweli katika matendo ama hapana haitegemei tu kama Roho Mtakatifu yuko kazini au hapana, wala haiamuliwi tu na kama yuko wazi kuhusu ukweli ama hapana, ila hutegemea kama yuko tayari kuuweka ukweli katika matendo ama hapana na kama anapenda ukweli ama hapana.
Kwa kawaida, mtu husikia ukweli na, kwa muda, kila kitu huhisi kuwa kawaida kabisa kwake; katika muda huo wa kawaida, ukweli unaziinua hali zako kuwa kawaida. Unakufanya kujua asili yako potovu; moyo wako una furaha na unakuwa huru na hali yako inabadilika kuwa bora. Lakini baada ya muda, jambo laweza kukuchanganya; ukweli ulio ndani yako unakuwa usioonekana na bila kujua unaufanya ukweli huo kama jambo lisilo muhimu sana kwako; hujaribu kumtafuta Mungu katika matendo yako, unatenda kila kitu kwa mapenzi yako mwenyewe na huna nia ya kutenda ukweli kabisa. Wakati unapopita, unapoteza ukweli uliokuwa nao. Daima unadhihirisha asili yako mwenyewe, ukikosa kumpa Roho Mtakatifu nafasi ya kufanya kazi ndani mwako; hutafuti nia ya Mungu kamwe; hata unapomkaribia Mungu, unapitia tu katika mizunguko. Punde tu unapogundua ukweli wa ugonjwa wako, moyo wako uko mbali sana na Mungu; umemkataa Mungu kwa vitu vingi na kutamka kufuru nyingi. Bado kuna ukombozi kwa wale ambao hawajaenda mbali sana katika njia hii, lakini kwa wale ambao wameenda mbali sana hata kumkufuru Mungu na kujiweka wenyewe dhidi ya Mungu, wakipigania cheo, na chakula na mavazi, hakuna ukombozi. Kusudi la ushurika wazi kuhusu ukweli ni ili kuwafanya watu kutenda ukweli na kubadilisha tabia yao, sio tu kuwafanya wafurahi. Kama unaelewa ukweli lakini hauuweki katika matendo, basi ushirika kuhusu ukweli na ufahamu wa ukweli hautakuwa na maana yoyote. Iwapo unaelewa ukweli lakini hauuweki katika matendo, utapoteza nafasi yako ya kupata ukweli na kupoteza nafasizyote za kuokolewa. Ukiuweka ukweli unaoelewa katika matendo, utapata ukweli wa ndani zaidi; utapata wokovu wa Mungu; utapata kupata nuru, mwangaza na uongozi wa Roho Mtakatifu. Wengi hulalamika tu kuwa Roho Mtakatifu kamwe hawapi nuru, lakini hawagundui kuwa kimsingi hawauweki ukweli katika matendo. Kwa hivyo, hali zao hazitawahi kupata ukawaida na hawatawahi kuyaelewa mapenzi ya Mungu.
2. Unahitaji Tu Kutenda Ukweli na Njia Itafunguka Mbele Yako
Wengine husema kuwa shida zao hazitatatuliwa kwa kutenda ukweli. Wengine huamini kuwa ukweli hauwezi kutatua kikamilifu tabiapotovu za watu. Ukweli ni kwamba shida zote za watu zaweza kutatuliwa; cha muhimu ni kama watu wanaweza kutenda kulingana na ukweli au hapana. Shida zenu za sasa sio saratani ama magonjwa yasiotibika; kama mnaweza kuweka ukweli katika matendo, shida hizi zote zaweza kubadilishwa, ikitegemea kama unaweza kutenda kulingana na ukweli ama hapana. Kama unatembea katika njia sawa, utafanikiwa; kama unatembea katika njia mbaya, utakuwa umemalizika. Kwa mfano, watu wengine hufanya kazi zao bila kufikiria kuhusu jinsi ya kufanya vitu kwa njia ya faida kwa kazi ama kama jinsi wanavyofanya vitu inapatana na mapenzi ya Mungu; kama tokeo, wanafanya mabo mengi ambayo Mungu anachukia. Kama wangetenda kulingana na ukweli katika kila jambo, je hawangekuwa watu ambao wanaupendeza moyo wa Mungu? Watu wengine wanajua ukweli lakini hawauweki katika matendo, wakiamini kuwa ukweli ni hili tu na sio kitu kingine zaidi. Wanaamini kuwa hauwezi kutatua mapenzi yao wenyewe na upotovu wao. Je, mtu wa aina hii sio mmwenye mzaha? Je, yeye sio mpumbavu? Je hajioni mwenyewe kuwa werevu? Watu wakitenda kulingana na ukweli, tabia yao potovu itabadilishwa; watu wakimwamini na kumtumikia Mungu kulingana na tabia zao asili, hakuna kati yao atakayebadilishiwa tabia yake. Watu wengine wanajipata katika shughuli zao wenyewe siku nzima na wanakosa kuchunguza ama kutenda ukweli unaopatikana tayari. Utendaji huu ni wa kipumbavu sana; watu wa aina hii ni watesekaji kiasili, kuwa na baraka lakini hawaifurahii! Njia ipo, kinachofaa kufanywa tu ni wewe kuiweka katika matendo. Kama umeamua kuuweka ukweli katika matendo, unyonge wako na dosari mbaya zinaweza kubadilishwa, lakini lazima kila wakati uchukue tahadhari na kuwa makini na kupitia ugumu zaidi. Kumwamini Mungu kunahitaji moyo wenye busara—unaweza kumwamini Mungu vizuri ukichukua namna hii ya kawaida?
Watu wengine wanajihami tu na ukweli fulani kwa wakati wa dharura ama kujitelekeza wenyewe na kuwasaidia wengine, sio kutatua shida zao wenyewe; tunawaita “watu wasio na ubinafsi.” Wanawaona wengine kama vikaragosi wa ukweli na wenyewe kama mabwana wa ukweli, wakiwafunza wengine kuushikilia ukweli na wasiwe wasiojihususha, ilhali wao wenyewe ni watazamaji kando kando mwa uwanja—hao ni watu wa aina gani? Wakiwa wamejihami na baadhi ya maneno ya ukweli ili kuwahubiria wengine tu, wakikosa kufanya chochote kujizuia kutokana na kuangamia kwao wenyewe—inasikitishaje! Kama maneno yao yanaweza kuwasaidia wengine, mbona wasijisaidie wenyewe? Tunafaa kuwaita wanafiki wasio na ukweli. Wanatoa maneno ya ukweli kwa wengine na kuwaambia wengine wayaweke katika matendo, lakini hawafanyi juhudi yoyote kuyatenda wenyewe—je sio wa kudharauliwa? Kwa hakika hawawezi kulifanya wenyewe, ilhali wanawalazimisha wengine kuweka maneno ya ukweli katika matendo—hii ni njia ya ukatili iliyoje! Hawatumii ukweli kuwasaidia wengine; hawawatolei wengine kwa moyo wa upendo wa mama; wanawadanyanya tu watu na kuwapotosha watu. Hili likiendelea—na kila mtu akipitisha maneno ya ukweli kwa anayefuata—je kila mmoja mwishowe hatakuwa na uelewa tu wa maandishi ya ukweli wakikosa uwezo wa kuyatenda? Watu wa aina hii wanawezaje kubadilishwa? Hawazitambui shida zao wenyewe kabisa; kutaweza vipi kuwa na njia kwa ajili yao?
Kila tatizo lina njia ya kutatuliwa; kwa kila tatizo kila wakati kutakuwa na ukweli ufaao kushauri ili kukupa njia ya kuendelea mbele na kukuwezesha kubadilika. Hata kama mabadiliko hayatafanyika mara moja, sasa unaweza kuitambua hali yako. Kama kweli hizi hazingeweza kutatua matatizo ya watu, basi Mungu hatakuwa Amenena bure? Kwa hivyo, kama uko tayari kuuweka ukweli katika matendo, kila wakati utakua na njia ya kufuata.

Jumamosi, 2 Februari 2019

Namna ya Kumridhisha Mungu katikati ya Majaribu

Sura ya 59. Namna ya Kumridhisha Mungu katikati ya Majaribu

Ninaibua maswali machache kwa tafakari yenu: Tangu mara ya mwisho tuliposema kwamba kutakuwa na miaka saba mingine ya majaribu makubwa, iwe ni kwa dhiki au majanga, je, mmegundua kusudi la Mungu kupitia kwa hayo? Ni asili gani ya binadamu mnaweza kuona katika mijibizo na mitazamo ya watu kwa miaka hii saba ya majaribu? Hili litachanganuliwa vipi? Fikirieni hilo. Ninazungumzia asili ya binadamu katika kila ushirika, kufikia chanzo, kuchanganua asili ya binadamu, na kuchanganua kiini. Ni juu yenu basi kuwasiliana ufahamu wenu kuhusu hizi mada.

Mnapaswa kuelewa kusudi la Mungu na ni lazima muijue asili ya binadamu kupitia hii miaka saba ya majaribu. Kwa hakika, kila sentensi ya Mungu ina kusudi Lake, ambamo mmefichwa ukweli. Bila kujali ni suala gani linafanyiwa ushirika, au ni ukweli gani unaoenyeshwa, ndani yake mna njia ambayo watu wanapaswa kupitia, matakwa ya Mungu kwa watu, na kusudi la Mungu kwa wanaomtafuta. Katika haya mazungumzo ya majaribu, dhiki, na hatimaye mateso, matakwa kwa watu na kusudi la Mungu pia vimo ndani. Watu, bila shaka, wanaonyesha hisia kwa mitazamo yao, kwa kuwa watu hawajaundwa kwa mbao; wako hai, na wanaonyesha hisia kwa kila kitu. Je, kuna maana kuchanganua ni hali gani za asili ya binadamu zinawakilishwa katika hisia za watu? Ina maana kushiriki kuihusu? Uchanganuzi utasaidia watu kuliona hilo wazi, kulijua wao wenyewe, na kujua vyema kabisa mioyoni mwao ili kwamba hatimaye wawe na njia mwafaka ya kuchagua. Ikiwa mtu amekanganyikiwa na hajui kusudi la Mungu, haelewi ukweli, na ana ufahamu mdogo kuhusu matakwa ya Mungu kwake na wajibu anaopaswa kutekeleza, au njia gani anapaswa kutembea, pengine mtu wa aina hii hatasimama imara. Kwa hivyo, inapaswa kujulikana ni njia gani inapaswa kutumiwa baadaye wakati wa majaribu mbalimbali.

Kila wakati majaribu ya miaka saba yanapotajwa, kuna watu wengi wanaohisi vibaya sana na kuvunjika moyo kusiko kwa kawida, na kuna watu wengine ambao hulalamika, na kuna mchanganyiko wa hisia. Ni dhahiri kutokana na hizi hisia kwamba watu sasa wanahitaji majaribu haya, wanahitaji aina hii ya dhiki na utakasaji. Watu humwamini Mungu kwa nia ya kutaka kupata baraka siku zijazo. Watu wote wana kusudi na tumaini hili. Hata hivyo, upotovu ndani ya asili ya binadamu ni lazima uondolewe kupit majaribu. Katika hali yoyote usiyoipita, ni katika hizi hali ambamo ni lazima usafishwe—huu ni mpango wa Mungu. Mungu anakutengenezea mazingira, Akikulazimisha usafishwe hapo ili ujue upotovu wako mwenyewe. Hatimaye unafika hatua ambapo unaona heri kufa na kuziacha njama na tamaa zako, na kutii mamlaka na mipango ya Mungu.

Hivyo ikiwa watu hawana miaka kadhaa ya usafishaji, ikiwa hawana kiwango fulani cha mateso, hawataweza kuepuka utumwa wa upotovu wa mwili katika mawazo na mioyo yao. Katika hali zozote zile bado ungali mtumwa wa Shetani, katika hali zozote bado ungali na tamaa zako mwenyewe, matakwa yako mwenyewe—ni katika hali hizi ambamo unapaswa kuteseka. Mafunzo yanaweza kupatikana tu katika mateso, yaani, kuweza kupata ukweli, na kuelewa kusudi la Mungu. Kwa kweli, ukweli mwingi unafahamika katika uzoefu wa majaribu makali. Hakuna asemaye kuwa kusudi la Mungu linajulikana, kwamba uweza na busara Yake vinafahamika, kwamba tabia ya haki ya Mungu inaonekana katika mazingira ya utulivu au katika hali zinazofaa. Hilo haliwezekani!

Mungu ametayarisha mazingira mwafaka ambamo Anawafanya watu kuwa wakamilifu, ila haijulikani kwa yeyote ni kwa nini Mungu anaweza kutaka kuwajaribu watu, kuwatakasa. Nyinyi nyote mnasema, “Mungu anawependaje wanadamu kwamba Anaweza kutayarisha miaka saba ya majaribu kuwatakasa watu na kuwafanya safi! Ni mvumilivu kiasi gani! Ni mwenye kuonyesha huruma kiasi gani!” Haina haja uyaseme haya, kila mmoja anaelewa mafundisho, lakini kwa hakika hakuna yeyote anayeifahamu hali halisi Je, miaka saba ya Mungu ya majaribu, miaka saba ya kazi ni ya nini? Bila shaka, inahitajika ili kwamba kazi Yake ifanyike. Hata bila kukuokoa, bado kuna upendo, sawa? Anapokuokoa, unasema, “Haya ni mapenzi aliyonayo Mungu kwetu, hii ni huruma Yake.” Je, Asingekuwa ametayarisha hii miaka saba ya majaribu, na kukamilisha kazi mara moja, bado kusingekuwepo upendo? Je, ingelikuwa miaka miwili ya majaribu, au mwaka mmoja, au siku ingalifika mara moja, je, hayo yasingekuwa mapenzi na huruma? Si kama unavyodhani: Miaka saba ya majaribu ni utakaso wa Mungu kwetu, ni kiwango Anachotupenda: ni lazima tutii. Unasema haya wakati tu hakuna njia nyingine. Hili linadhihirisha nini? Linadhihirisha uhasi, linadhihirisha lawama, na linadhihirisha kukosa njia mbadala na kukata tamaa. Mungu alisema kwamba kutakuwa na miaka saba mingine. Wacha iwe miaka saba basi. Kisha unakurupuka na kusema maneno mazuri: Mungu, Unatupenda; Mungu, ni kwa ajili ya kututakasa. Bila miaka saba ya majaribu, je, huo usingelikuwa mwisho wetu? Kusingelikuwa na fursa. Watu wengine wanatamani kubarikiwa sasa hivi. Hiyo inaweza kuwa faida halisi! Mtu kama huyo hajali kitu kingine chochote kile. Mtu kama huyu hafai hata kwa senti moja. Kuna kazi ya vitendo katika hii miaka saba. Je, haijasemwa awali kwamba maneno mengine ni njia, lakini vilevile ni ukweli? Hakuna kipengele ambacho ni maneno tu bila matendo. Kila kipengele kina dhima. Aidha, kama aionavyo mwanadamu, takribani kila kipengele kina njia, lakini njia hii si ya kukurairai, si ya kukudanganya. Badala yake ni mazingira ya kweli, hali halisi Hakuna njia mwafaka kuliko hii. Baada ya kusikia maneno haya, watu wengine hufikiri: Ikiwa ni kama usemavyo, hii miaka saba inapoisha, ni nani anaweza kutambua umesalia muda kiasi gani! Kutokana na mijibizo ya watu inaonekana kuwa asili ya binadamu imewekwa kwa namna kwamba baada ya kukumbana na majaribu ya mateso, kupokea uchungu mwilini, anataka kuuepuka na kuukataa. Hakuna hata mtu mmoja hujitokeza na kuchukua hatua ya kudai: Mungu, nipe majaribu fulani ya kuteseka, nipatie dhiki fulani. Mungu, nipatie taabu zaidi. Hili linadhihirisha kuwa kiasilia watu hawapendi ukweli. Iwe ni kusudi la Mungu au la, au inafaidi watu vipi, haijalishi ni nzuri kiasi gani, watu wote hukataa hali yoyote inayoiletea miili yao machungu au ile isiyoafiki matamanio yao. Kuna watu wasemao: “Sipingi. Nilifanya uamuzi zamani kuyatoa maisha yangu yote kwa Mungu. Nina furaha kabisa haijalishi ni miaka mingapi, na nitamtumikia Mungu kwa moyo. Sina lawama. Haijalishi ninakumbana na majaribu gani, haijalishi ninakutana na mateso gani, iwe ni kutelekezwa na familia au maumivu ya ugonjwa, nitafuata hadi mwisho.” Huku kutokuwa na lawama kwako pia ni aina ya hali hasi, kwa sababu kila wakati unapokumbana na kitu chochote, kila wakati unaposemewa maneno, kwa hakika huelewi maana iliyo ndani. Hii “sina mjibizo” unayoisema kwa hivyo si kingine bali ni kutojali, njia wakati ambapo hakuna njia nyingine. Hakuna jingine la kufanya ila hili, kwa hivyo unajilazimisha kufuata hata wakati ambapo hauko radhi. Kwa vyovyote vile hakuna awezaye kufaulu kuepuka miaka saba ya majaribu. Hata hivyo, hii ni tofauti na wewe kutaka kutoroka. Ungetamani kuepuka lakini huwezi. Hili ni jambo la asili ya mwanadamu. Lifikirie. Je, ndivyo ilivyo? Watu wengine wanahisi: Nilipokumbana na tukio kama hili miaka kumi iliyopita, daima nilifuata, na niliteseka sana, kwa hivyo ninaweza kuendelea kuvumilia kwa miaka michache. Kutafuta kwenu kwa kusudi la Mungu kumekanganyikiwa na hamjakutilia maanani. Hivyo, ikiwa kwa ndani hujayatii mapenzi ya Mungu, basi umeyasaliti na kukana mapenzi ya Mungu. Ijapokuwa huna hali hii, na hujafanya jambo hili, hizi dalili, haya mambo yaliyo ndani yako, yanamkana Mungu, kwa sababu unachokifiria na kutarajia kwa ndani sicho Mungu anachokihitaji. Aidha kwa hakika humsifu Mungu kutoka ndani ya moyo wako kwa yote Anayohitaji kutoka kwako na yote Anayofanya, iwe ni njia, au kile ulichoambiwa.

Na kwa kila kitu Mungu ambacho anawataka watu wafanye, chochote Mungu alichowapangia watu kulingana na mahitaji yao, asili ya binadamu ni kukikataa, kukosa kukikubali. Haijalishi unautangaza vipi msimamo wako, au iwe una ufahamu kidogo, kwa vyovyote vile, ufahamu wako wa mafundisho hauwezi kutatua kilicho katika asili yako. Kwa hivyo ninasema kwamba watu wengi wanazungumzia vitu vizuri katika mafundisho, na kusema maneno ya juujuu kuyastahimili. Hatimaye, japo, katika maombi wanasema: Nimepitia kwa ufanisi miaka mingi sana. Miaka saba si miaka mingi na wala si miaka michache. Tazama ninavyozeeka, jinsi afya yangu ilivyoharibika, na kwamba sina familia nzuri. Nimeandamana na Wewe miaka hii yote, nifanya bidii hata bila malipo, nimechoka ijapokuwa sijafanya kazi kwa bidii. Hata kama Utaipunguza hata kwa miaka michache, nifanyie hisani mara hii moja! Unajua udahaifu wa watu… Kwa kuomba maneno haya, ni kama kuna utiifu kidogo. Wanaendelea kusema “Unajua udhaifu wa watu”; kuna maana nyingine ndani ya maneno haya, ambayo ni kusema, Unajua udhaifu wa binadamu, basi ni kwa nini inachukua muda mrefu kiasi hiki? Je, hii si hali iliyo ndani mwa watu? Kwa hivyo, mnahisi mnafahamu vitu vingi, tayari mmevikubali, na kuonekana mmefahamu ukweli, lakini kwa hakika bado mnaukataa ukweli, na kwenda kinyume cha ukweli. Vitu mnavyovifanya haviambatani na ukweli. Japo kijuujuu hamjafanya vitendo viovu, na hamjatamka kitu chochote kibaya, hii imejikita tu kwa kutovunja amri za utawala, kwa kutoikosea tabia ya Mungu. Hujaelewa kusudi Lake na hata hivyo hauko tayari kulipokea. Hukubaliani na Yeye kufanya mambo kwa njia hii. Unafikiri: Iwapo nitaifanya kazi hii, sitapoteza muda na nitaikamilisha kazi hii kwa muda mfupi iwezakanavyo, ili kwamba niwasaidie watu wa Mungu kuepuka mateso zaidi kutoka kwa joka kuu jekundu, kuzuia kupotea kwa watu wengi zaidi, kuepuka mateso yangu. Je, hili si wazo walilonalo watu? Watu mioyoni mwao wanatumaini kufika kwa ufalme wa Mungu, na kuangamia kwa haraka kwa ulimwengu wa Shetani. Ni neema kubwa ikiwa neno moja la Mungu litawabadilisha. Mitazamo ya ndani ya watu, matamanio yao makubwa kwa hakika hayatekelezi kusudi la Mungu, na kimsingi hakuna kiini cha kutii. Hili pia linagusa ule msemo: Asilimia mia moja ya kile kilicho ndani ya asili ya binadamu ni usaliti. Kwa hivyo, kwa kulichanganua hili au lile tukio lenu, kwa kulichanganua hili suala, lile wazo, au ile hisia, iwe unaikabili kwa njia hasi, au unalalamika, ikiwa hujali au umenyamaza bila kusema neno, kuna ukinzani katika haya yote. Haya yote ni usaliti. Je, huu uchanganuzi ni sahihi? Nisingalichanganua hili, kungekuwepo na watu wanaohisi: Ninaweza kudhaniwa kuwa mtu mzuri. Ningekumbana na jambo hili miaka michache iliyopita, bila shaka ningelalamika, ikiwezekana ningerudi nyuma, lakini sasa silalamiki. Hulalamiki, lakini je una uelewa? Je, uelewa wako mdogo unajumuisha uelewa wa kweli? Kuna ukweli ndani yake? Je, uelewa wako unalingana na kusudi la Mungu? Je, umepata kibali cha Mungu? Je, una kiini cha kumtii Mungu? Je, uko radhi na tayari kumtii Mungu? Kama sivyo, basi bila shaka unakinzana na Mungu. Inawezekana kwamba hali yako ya moyo sasa hivi ni nzuri, na hujihisi vibaya, au kwa sababu sasa hivi umewekwa katika kufanya kazi. Ikiwa siku moja utatumwa nyumbani, na utakapokuwa katika giza la hali mbaya ya moyo, hata hivyo, kilicho ndani ya moyo wako kitafichuliwa. Kuna watu wengine wenye kimo kidogo, wenye muda mfupi wa uzoefu ambao wanaweza kugeuka na kukimbia, kurudi ulimwenguni. Kwa hakika, katika uchanganuzi wa mwisho, mjibizo wowote ule ulionao, unakataa mazingira aliyokupangia Mungu. Asili ya watu ya kumsaliti Mungu inafichuliwa kila mahali. Ikiwa hili lisingechanganuliwa, watu wasingejijua kwa kina ipasavyo. Watu wakikumbana na kitu chochote, wote wanamsaliti Mungu na wanakosa kumtii. Mijibizo ya baadhi yenu ni kutotaka, au hisia za malalamiko, uhasi na huzuni, na mnasema: Kwa ndani, binadamu hapendi ukweli, na huku kutopenda si kingine bali ni usaliti. Bado haitoshi kama mnazungumza namna hii tu, na hamjachanganua hadi kwenye kina cha kiini. Mnasema kwamba kutopenda ukweli ni usaliti, lakini kwa kweli, hili si sahili hivyo Mmelichanganua vipi? Hamjielewi nyinyi wenyewe. Unaweza usijue hiyo ni hali gani uliyonayo, na huwezi kutofautisha mazuri na mabaya, ikiwa ni usaliti au la, na hujijui wazi wewe mwenyewe iwe umetii au la. Hamuwezi kuchanganua kabisa asili zenu wenyewe. Kila mara mnapokumbana na jambo fulani mnashindwa kujua namna ya kwenda mbele. Hatimaye, utakapokumbana na jaribu, je, utaweza kulitambua kusudi la Mungu? Utalifafanua hili vipi? Unapaswa kutembea katika njia gani? Ni mantiki gani au ni ukweli gani unapaswa kuwa nao ili kukidhi kusudi la Mungu? Kama kiwango cha chini zaidi, ni lazima uwe na mtazamo chanya. Je, mmeyawazia maswali haya?

Zamani watu wengine walikuwa na mawazo kuhusu anachokifanya Mungu mwenye mwili. Ushirika uliofuata ulisababisha kuwepo na ukweli usiohitaji uthibitisho. Ukweli huu usiohitaji uthibitisho ni: Binadamu wanapaswa kukiri kuwa yote anayofanya Mungu ni sahihi, kuwa yote ni muhimu. Kama binadamu hawataelewa wanapaswa hata hivyo kutii na si kupinga. Kama binadamu wana mawazo ni lazima wataaibika. Je, watu wanakumbuka maneno haya? Kila mara wanapokabiliana na kitu, wanajisemea wao wenyewe: Kwa namna yoyote usiwe na mawazo, kwa namna yoyote usiyahukumu. Kuna maana katika kila kitu anachokifanya Mungu. Ijapokuwa hatuwezi kuelewa kwa sasa, siku moja tutapata aibu. Wanazishikilia tu sheria kama hii. Sheria ya aina hii, hata hivyo, yaweza kusuluhisha matatizo kadhaa ya waumini ambao wamekanganyikiwa. Kwa mtu aliye na uelewa haya maneno yatasaidia kuelewa maana ya vitu vingi, na kutumia hii sheria kila mara hali inaposhuhudiwa yaweza kuweka wazi mambo mengi. Ni nini kinachofanyika kama hakuna umaizi? Mtu anaweza tu kutii sheria, na katika kufanya hivyo anaweza pia kulindwa na kuzuia kukiuka amri za utawala, si kueneza maafa. Sheria hii ina manufaa! Sio ati haina maana! Katika sehemu mbalimbali sheria hii imesomwa kwa moyo. Wengine huiandika madaftarini, au kuiandika kwenye jalada la kitabu, na kuisoma kila wakati wanapofungua kitabu, huku wakiikariri. Wanaikariri wanapoomba. Kufanya hivyo kuna manufaa kadhaa. Watu wengine hawathubutu kufanya mambo kwa kubahatisha, na wana uchaji mdogo mioyoni mwao. Ila kulingana na watu wengi, hawana uelewa wa kweli wa hali chanya, na kuna vitu vingi sana vilivyo hasi. Ijapokuwa inaonekana kuwa mnajihisi vyema kabisa na hamjaacha kufanya kazi, kuna vitu vingi hasi kwa kweli kati yenu, na hakuna vitu chanya. Kuna mijibizo mingi sana kanisani kuhusu mambo kama haya. Je, mmejaribu kujijumuishia nyinyi wenyewe? Kama vitu vya aina hii vingekabiliwa tena, mngemkataa Mungu au kumsaliti Mungu? Kuna baadhi ya watu ambao labda wametambua, "Binadamu hana uwezo wa kuielewa asili yake mwenyewe. Bila shaka sitajaribu kukataa tena, na lazima niwe makini. Lazima niombe kila siku!” Huu sio mpango wa uhakika. Nimegundua kuwa huwa mnapata aibu, na mara nyingi mnasema: "Ah, nitafanya nini kuhusu hii asili ya binadamu? Siwezi kuisuluhisha mimi mwenyewe, na siwezi kuielewa. Kwa kweli sina haki ya kujisimamia mimi mwenyewe. Sijui ninaweza kufanya nini siku moja. Ninaogopa sana. Kumwamini Mungu lazima kufanyike kwa makini mno. Uzembe wowote waweza kusababisha maafa, na hilo laweza kuwa jambo baya mno. Hata sijijui, siwezi kujitegemea..." Ingawa watu wanaosema haya mara kwa mara huwa wanajielewa kwa kiasi fulani, wana uelewa kidogo mno kuhusu ukweli. Wanachanganyikiwa kila mara wanapokumbana na kitu chochote. Wanapatwa na wasiwasi, wanahisi uoga, na hawana njia yoyote ile wanapopatwa na chochote kile. Wakati huu umeshinda miaka saba ya majaribu, na hujasababisha maafa, na hujakiuka amri za utawala, lakini je, waweza kuwa na uhakika kuhusu wakati ujao? Wawezaje kuyashinda haya yote bila kizuizi? Unaona kuwa umeyashinda masaibu kwa urahisi sana, kwa kujificha hapa na pale. Ulijificha kwa mwaka mmoja au nusu mwaka hadi yakaisha. Wanadamu wanaweza kujificha, lakini asili ya binadamu ni kitu ambacho hakiwezi kufichika. Je, hakupaswi kuwa na ukweli uisohitaji thibitisho unaohusiana na hili, pia? Katika kila majaribu ya Mungu kuna nia nzuri. Kwa kila tukio linaloshuhudiwa kuna ukweli ambao mtu anapaswa kuwa nao ili kusimama imara. Jiandaeni na ukweli ili kukabiliana na majaribu tofauti tofauti kwa sasa, na hamtaogopa bila kujali miaka ya majaribu hapo mbeleni. Lazima muwe na ujasiri. Kutii mipango ya Mungu kamwe hakuwezi kuwa na dosari. Njia daima itakuwa na matumaini. Mwawezaje kuwa wakamilifu bila majaribu kadhaa? Bila majaribu, hakuna shahidi. Ni vipi basi mtamridhisha Mungu? Majaribu yatawaletea baraka za Mungu. Ni kwa kumfuata tu Mungu hadi mwisho ndipo mtu aweza kuingia katika ufalme. Kumbuka: nyinyi nyote mna fungu katika dhiki, ufalme, na uvumilivu wa Kristo.


kutoka kwa Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo
Soma zaidi: Umeme wa Mashariki Vitabu.

Ijumaa, 1 Februari 2019

Filamu za Injili | "Nimewahi Treni ya Mwisho" | Entering the Ark of the Last Days

Filamu za Injili | "Nimewahi Treni ya Mwisho" | Entering the Ark of the Last Days

Chen Peng alikuwa mchungaji katika kanisa la nyumba fulani. Alikuwa akimtumikia Bwana kwa bidii, na mara nyingi alifanya kazi kama mhubiri, akiwasaidia wafuasi wake, na kulibebea kanisa mizigo mizito. Lakini katika miaka ya hivi karibuni, kanisa lilizidi kuwa tupu zaidi na zaidi. Waumini walikuwa na roho dhaifu na wavivu, wakikosa mkutano baada ya mkutano. Na hivyo Mchungaji Chen aliona giza likiangukia nafsi yake, kana kwamba kisima cha roho yake kilikuwa kikavu, na hakuweza kuhisi uwepo wa Bwana. Katika mikutano, aligundua kwamba hakuwa na kitu alichoweza kuhubiri. ... Alifanya kila kitu alichoweza kufikiria ili kuimarisha kanisa, lakini jitihada zake zote zilikuwa bure. ... Chen Peng alikuwa amesitikika, amepotea, na hakuweza kuelewa kwa nini kanisa lake lilikuwa linajawa na ukiwa sana, na kwa nini walikuwa wamepoteza uwepo wa Bwana.
Hadi siku moja, kwa bahati, aliposikia injili ya ufalme wa Mwenyezi Mungu. Baada ya kupitia mjadala mkali, Chen Peng hatimaye aligundua sababu ya kanisa lake kuwa na ukiwa, na akaamini kwamba Mungu alikuwa tayari amekuwa mwili na kuwa Mwana wa Adamu: Mwenyezi Mungu, anayehukumiwa na kutelekezawa na ulimwengu wa kidini, ambaye anasema ukweli na kufanya kazi ya hukumu katika zile siku za mwisho! Ni wale tu ambao wanakubali kazi ya hukumu ya Mwenyezi Mungu, Kristo wa zile siku za mwisho, na kufuata nyayo za Mwana-Kondoo wataweza kunyakuliwa mbele ya kiti cha enzi cha Mungu na kufikia kunyunyuziwa na kupewa maji ya uzima. Kwa sababu ya hilo, Chen Peng aliwahi treni ya mwisho na kukubali kwa furaha kazi ya Mungu katika zile siku za mwisho.